Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104795 articles
Browse latest View live

Marekani Yalaani Mauaji ya Kiongozi wa CHADEMA, Daniel John na Majeraha Aliyopatiwa Reginald Mallya.

$
0
0
Marekani imesikitishwa sana na taarifa za kutekwa na utumiaji nguvu kikatili uliosababisha kifo cha Daniel John na majeraha kwa Reginald Mallya.


Tunatuma salamu zetu za rambirambi kwa familia na marafiki wa marehemu kwa msiba huu. Kuongezeka kwa makabiliano ya kihasama na vitendo vya kikatili ni jambo linalotutia wasiwasi na kutusikitisha sana. Tunatoa wito kwa vyama vyote kulinda amani na usalama wa mchakato wa kidemokrasia, taifa na wa watu wa Tanzania.

Aidha, tunaungana na Watanzania katika kutoa wito wa kufanyika kwa uchunguzi wenye uwazi ili kuwawajibisha wale wote wanaohusika na vitendo hivi vya kikatili kwa mujibu wa sheria za Tanzania



Mwanaharakati Mange Kimambi Ana Nguvu Sawa na Chama Kikuu cha Upinzani nchini

$
0
0
Kwa kweli mwanaharakati huyu ana ujasiri wa kupigiwa mfano. Sitaki kumtolea mfano wa akina- Assange na Snowden lakini Mange ana nguvu kubwa kama chama kikuu cha upinzani.

Mimi naona ni mwanamke mwenye akili kubwa na uwezo wa kufikiri mkubwa kwani kila nyanja anaweza akaisemea vizuri.

Huyu ana faida kwetu lakini tumsaidie kwa kumpa taarifa zenye ukweli na manufaa ya taifa letu. Mfano mpenyesheeni majina na kikundi cha wasiojulikana angalau tuishi kwa amani mtaani kwetu, ufisadi... n.k.

Hongera Mange Kimambi.

Viongozi wa CHADEMA wakiongozwa na Mbowe, waenda NEC kuwasilisha malalamiko kuhusu Uchaguzi ubunge Jimbo la Kinondoni

$
0
0
Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA Freeman Mbowe, mgombea Ubunge Jimbo la Kinondoni kupitia chama hicho Salum Mwalimu na baadhi ya wabunge wa chama hicho, muda huu wapo ofisi za Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) Wakitaka kuonana na Mkurugenzi wa tume hiyo.

Lengo la kuwasilisha malalamiko yao kuhusu mchakato wa uchaguzi mdogo wa ubunge katika jimbo la Kinondoni Dar es Salaam.

Mkurugenzi wa NEC hawajamkuta, ila wameweza kuongea kwa simu kwa kutumia simu ya mmoja wa Maofisa wa NEC baada ya kutopokea simu ya Mbowe. Wamekubaliana kwamba Malalamiko yote waliyo yawasilisha yatatatuliwa leo hadi kufikia jioni.

 Mwenyekiti wa Taifa wa (Chadema) Mhe Freeman Mbowe na viongozi wengine wa chama hicho wamekwenda ofisi ya NEC, kushinikiza wapewe viapo vya mawakala wao ambavyo mpaka sasa hawajapewa huku wakidai mawakala wa CCM wameshapewa.

Msafara huo wa viongozi hao ulipofika ofisi hizo kwa lengo la kukutana na Mkurugenzi wa Tume hiyo, Ramadhan Kairima waligonga mwamba baada ya watumishi wa NEC kudai kuwa Mkurugenzi huyo hayupo ofisini, viongozi hao waligoma kuondoka katika ofisi hiyo mpaka baadae Mbowe aliongea kwa simu na Mkurugenzi huyo na kukubaliana.

Zifuatazao zilikuwa kauli za viongozi hao wakiwa kwenye ofisi hiyo ya NEC
Mbunge wa Kawe Mhe Halima Mdee "Mnadhani tumekuja kunywa soda hapa sisi tumeacha shughuli muhimu kuliko hata nyinyi mnaokula ugali hapa, wewe tuma mtu aende pale amcheki Mkurugenzi ilo ndiyo jambo la mbolea ila hapa hatutoki, piga simu mtume mtu aulize kama Mkurugenzi yuko pale tunagawa timu wengine wanakwenda wengine tunabaki hapa"

Kwa upande wa Mhe John Heche alikuwa na haya ya kusema "Kailima huyu kwenye Uchaguzi Mkuu nimempigia simu huyu madiwani wameondolewa nje ya utaratibu akarudisha leo kuongea na sisi moja kwa moja anashindwa nini? Na simu hapokei pia hata tulikuwa hatuna haja ya kuja hapa tunapiga simu hapokei, sisi tunamkutano jioni turuhusu tuingie tuonane naye twende kwenye mkutano, nyinyi mshaanza kusema tumevamia ofisi zenu kwa nguvu"

Mbali na huyo Mbunge wa Bunda mjini Mhe Ester Bulaya naye alifunguka na kusema kuwa tayari mawakala wa Chama Cha Mapinduzi "CCM viapo wameshapewa wengine hamtaki kuwapa kama mnawaogopa watu mnaowagopa wa nini, sisi tusishiriki uchaguzi nyinyi mtapata faida gani"

Aidha Mbunge wa Iringa Mjini Mchungaji Peter Msigwa naye alihoji "Au ndugu zetu mmeshapanga kutangaza matokeo mnavyotaka nyinyi"

Baada ya vuta vutana hiyo ya maneno baadaye Mhe Mbowe aliweza kuingia ndani na alipotoka alikuwa na haya ya kusema kwa viongozi wengine wa Chadema waliofika hapo

"Nimemwambia kwamba sisi tumekuja kwa sababu hapokei simu zetu na maandishi yetu hayajibiwa kwa wakati na uchaguzi umekaribia na kuna mambo chungu nzima ya kurekebishwa kabla ya uchaguzi kwa hiyo tumekubaliana kwamba yeye naye lazima aitishe kikao chake na Tume ya Uchaguzi tukubaliane nao malalamiko gani ambayo tunayo halafu tupate muafaka kisha baadaye mchana awe amefanya mawasiliano, kama tutakutana tena mchana kuelekea jioni ili ratiba zingine ziendelee kwa hiyo mimi nimeridhika na hilo sioni kama kuna tatizo kwa hiyo cha msingi Waheshimu ninataka watu watatu wanne tukae sehemu tujadili mambo yetu halafu tumpigie simu maana anasubiri simu yetu jambo hilo" alisema Mhe Mbowe. VIDEO:

Humphrey Polepole Awaomba Polisi, CHADEMA Wasilinde Kura Sio Kazi Yao

$
0
0
Katibu wa Itikadi na Uenezi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Humphrey Polepole amefunguka na kulitaka jeshi la polisi kuhakikisha Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) hakilindi kura kwani hilo si jukumu lao.
[​IMG]
Polepole amesema hayo leo Februari 15, 2018 wakati akiongea na waandishi wa habari kuelekea uchaguzi mdogo wa Ubunge na nafasi za udiwani ambao unatarajia kufanyika Februari 17 2018 na kudai kuwa mpaka sasa wamepata taarifa kuwa CHADEMA wanachukua watu kutoka mikoani kuja kulinda kura kitu ambacho hakikubaliki.

"Zipo nyumba kadhaa hapa Dar es Salaam ambazo zimehifadhi watu wasio wakazi wametoka mikoa mbalimbali kuja hapa kwa kigezo cha kulinda kura, sisi hatufanyi siasa za matukio wala kutafuta kiki baada ya kujua hili tumewajulisha jeshi la polisi juu ya nyumba hizo na watu hao, kitakachofuata ni kushugulika na watu hao ambao hawapendi utaratibu mzuri na desturi yetu nzuri ya uchaguzi"

Polepole aliendelea kusema kuwa

"Kura hazilindwi na watu wanaoletwa kwa makundi bali kura kwa mujibu wa Katiba, Sheria ya uchaguzi na kanuni mbalimbali za uchaguzi zimewekewa utaratibu wa kisheria kuhakikisha mwenye yake na anaipata hiyo, upo utaratibu wa mawakala kila chama kina wakala huyo ndiye atakayeshiriki kuhesabu, kujua hii kura yangu au si yangu sasa unapoanza kuandaa watu wasiojulikana na kuwaleta Dar es Salaam ni kuleta taharuki na mpango huo msingi wake ni kutisha wakina mama, vijana na wazee wasijitokeze kwenda kupiga kura, tumesema jeshi la polisi tafadhali tena tafadhali sana watu wasiohusika na usimamizi wa zoezi la uchaguzi ni sheria hawapaswi kuwepo wanatakiwa kuwepo kwenye maeneo yao wakafanye kazi zao za kujiletea kipato, uchaguzi haulindwi na mabaunsa, kura hailindwi bali dola ina vyombo vyake ambavyo sisi wote vyama vya siasa tumekubaliana" alisisitiza Polepole

Jamii Forums

Habari Njema: Tunatibu Busha, Korodani Kuvimba, Ngiri, Miguu Kufa Ganzi Pamoja na Matatizo ya Nguvu za Kiume

$
0
0

Ni dawa ya nguvu za kiume inayorefusha na kunenepesha uume saizi uipendayo (Inch 1-7) kwa muda wa siku 6 tu.Dozi hii itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa muda wa dakika 30, utarudia tendo la ndoa zaidi ya mara 4 bila hamu kuisha bila kujali umri na garantee ni miaka 60 baada ya kutibu tatizo.

Pia tunatibu Busha bila kufanyiwa Oparesheni, korodani moja kuvimba, ngiri, tumbo kujaa gesi na kuunguruma, kutopata choo vizuri, miguu kuwaka moto na kufa ganzi, chango la wanawake, kisukari na kutokwa na kinyama sehemu ya haja kubwa.

MIHAYO:
Inarudisha mke, mchumba, hawara na atakutimizia kila kitu unachotaka kutoka kwake ndani ya  saa 2 tu hata kama yupo mbali. atarudi na kumfunga asiwe na mwingine zaidi yako.

Umefukuzwa kazini? unataka kupandishwa cheo? Umepoteza pesa zako kwenye biashara bila kujua umepandikizwa chuma ulete? Njoo urudishe pesa zako. Unauza mali yako haiendi?


Wasiliana na mtaalam Challo kwa; 0714006521 

Huyu Hapa Ndio Mpenzi wa Mwanamuziki FID Q, Watazame Wakieleza Walivyokutana..Hakika ni Kama Movies

$
0
0
Unaambiwa kitabu ndio chanzo cha yote haya Fid Q na mpenzi wake wa sasa walikutana kwenye mazingira ambayo ni kama movie..Tazama Hapa Chini wakielezea Mkanda Mzima:

Mtoto wa Miaka 2 Amerudishwa Nchini, Baada ya Wazazi Wake Kukamatwa na Dawa za Kulevya China

$
0
0
Taarifa tuliyoipokea kutoka Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya ni kuhusu Watanzania wawili wamekamatwa nchini China January 19, 2018 wakiwa wamemeza dawa za kulevya tumboni kwenye uwanja wa ndege wa Baiyun Guangzhou

Bunge Lamchagua Cyril Ramaphosa Kuwa Rais wa Afrika Kusini

$
0
0
BUNGE la Afrika Kusini limemchagua Mwenyekiti wa chama tawala cha ANC Cyril  Ramaphosa, kuwa Rais wa mpito wa nchi hiyo, mpaka pale uchaguzi utakapofanyika baada ya rais wa taifa hilo Jacob Zuma kujiuzulu.

Zuma alikuwa akikabiliwa na tuhuma nyingi, moja ikiwa ni kumhusisha na vitendo vya rushwa japokuwa mwenyewe amekanusha kuhusishwa na tuhuma hizo.

Alijiuzulu mara moja jana jioni licha ya kusema hakubaliani na uamuzi wa chama.

CCM wajiandaa kutangazwa washindi uchaguzi mdogo wa ubunge na udiwani

$
0
0
Chama Cha Mapinduzi (CCM) kimeanza maandalizi ya kusheherekea ushindi wa kishindo na kihistoria kitakaoupata katika uchaguzi mdogo wa ubunge na madiwani utakaofanyika Februari 17, 2018.

Pia, chama hicho tawala kimelitaka Jeshi la Polisi kuhakikisha linalinda amani wakati wote wa uchaguzi huo ili wananchi wakawachague viongozi wanaowapenda na wasiruhusu hila zozote.

Hayo yamesemwa leo Februari 15,2018 na Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, lepHumphrey Poole alipozungumza na waandishi wa habari ofisi ndogo za chama hicho, Lumumba jijini Dar es Salaam.

"CCM inawachama wasiopungua milioni 12. Tanzania ina wananchi wasiopungua milioni 50 na wapiga kura wa Taifa zima ni milioni 25. Tunapokwenda katika uchaguzi, wenzetu wanapaswa kulitambua hili," amesema Polepole,

"Ushindi ni sayansi, ukiondoa wanachama wetu na kazi ya siasa ambayo tunaifanya, tumefanya kampeni jimbo zima, kata nzima, mtaa wote, kaya, kitanda kwa kitanda na mtu kwa mtu. Baada ya haya tunakamilisha kuandaa sherehe ya kusheherekea ushindi."

Kwa msisitizo, Polepole amesema: "Kwa namba hii CCM itakuwa na ushindi mkubwa na wa kishindo na hii tutakuwa tunatesti mitambo kwa uchaguzi mkuu 2020 na ule wa serikali za mitaa."

Amewasihi vyama vya upinzani kuwa tayari kushindwa akisema, “kwa hiyo wawe tayari kushindwa kwani wamezoea kushindwa na kwa hesabu hizo hapo juu tushashinda."

Kuhusu wagombea katika uchaguzi huo, Polepole amesema: "Wagombea hawa 12, wawili wa majimbo na 10 wa Kata. Kinondoni - Maulid Mtulia na Dk Godwin Mollel kule Siha na madiwani ni makini kwelikweli ambao watashughulika na matatizo ya wananchi na hawa ndio wataibuka washindi."

"Uteuzi wa wagombea hawa haukufanyika kiholela, unazingatia Katiba na kanuni za Chama. Wagombea wote wamepitishwa katika matanuru ya kupimwa kwa hatua mbalimbali na hakika ni watu waadilifu, wachapa kazi."

Polepole amesema kuna taarifa wamezipata kwamba kuna mkakati unaandaliwa na wapinzani wa kutoa watu mikoani ili waje kuharibu uchaguzi huo ambao hawatakubali hilo litokee.

"Tumelijulisha Jeshi la Polisi juu ya nyumba hizo na watu hao. Sisi tumefanya yetu tumemaliza. Kura hazilindwi na watu, kwa mujibu wa taratibu za kisheria uko utaratibu," amesema Polepole na kuongeza:

"Uchaguzi ni sehemu ya wananchi kuchagua. Vyombo vyenye mamlaka ya kuhakikisha amani inakuwapo na wananchi wawachague viongozi wanaowapenda. Hatuliagizi Jeshi la Polisi, lakini sisi ndio chama kinachoongoza nchi."

Mbowe na Viongozi Wengine Wavamia Ofisi za NEC Kushinikiza Haya

$
0
0
Mwenyekiti CHADEMA Freeman Mbowe na viongozi wengine wa chama wamekwenda ofisi ya NEC kushinikiza wapewe viapo na vitambulisho vya mawakala wao, huku wakidai mawakala wa CCM wameshapewa
-
Msafara huo wa viongozi ulipofika ofisi hizo kwa lengo la kukutana na Mkurugenzi wa Tume hiyo, Ramadhan Kailima waligonga mwamba baada ya watumishi wa NEC kudai kuwa Mkurugenzi huyo hayupo ofisini
-
Viongozi hao waligoma kuondoka katika ofisi hiyo mpaka baadae Mbowe alipoongea na Mkurugenzi huyo kwa simu na kukubaliana mambo kadhaa
-
Mbowe alisema amefika ofisini hapo kutokana na kuwa na mawasiliano madogo na NEC. Kailima ameahidi kuzungumza na wenzake katika Tume kuona watafanya nini na kuwajibu CHADEMA leo jioni kwa njia ya simu na maandishi
-
Miongoni mwa viongozi waliokuwepo ni Halima Mdee, Esther Bulaya, John Heche, Peter Msigwa, John Mnyika na mgombea wa Jimbo la Kinondoni, Salim Mwalim

Soma Nafasi za Ajira Zilizotangazwa Siku ya Leo

$
0
0

Rais Magufuli Ampangia Ubalozi wa Sweden Dk. Slaa Kumwapisha Leo Ikulu

$
0
0
Rais Magufuli Ampangia Kuwa Balozi wa Sweden Dk. Slaa Kumwapisha Leo Ikulu
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli leo Februari 16, 2018 saa 3 asubuhi atawaapisha Dkt. Wilbrod Peter Slaa ambaye ameteuliwa kuwa Balozi wa Tanzania nchini Sweden na Muhidin Ally Mboweto kuwa Balozi wa Tanzania nchini Nigeria.

Mapya Yaibuka Afisa Aliyeanguka Ghafla Baada ya Kutumbuliwa na Makonda

$
0
0
Mapya Yaibuka Afisa Aliyeanguka Ghafla Baada ya Kutumbuliwa na Makonda
Mapya zaidi yanayomhusu yule Mkuu wa Idara ya Ardhi, Wilaya ya Ilala jijini Dar es Salaam, Paul Mbembela ambaye mwishoni mwa wiki alianguka baada ya kubanwa maswali na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda yameibuka ambapo siri imefichuka safari yake ya kupelekwa Hospitali ya Rufaa ya Amana imedaiwa iliishia njiani.



Amani lilizungumza na mfanyakazi mwenzake ambaye aliomba jina lake lihifadhiwe ambapo alidai kuwa, Paul baada ya kuanguka na kuwekwa kwenye gari la wagonjwa akipelekwa Amana, njiani aliomba kushushwa ili aendelee na hamsini zake.



Mfanyakazi huyo alidai kuwa, wao wameshindwa kuamini kama Paul kweli alipata mshtuko au aliamua kuua soo la kuendelea kuhojiwa maswali na Makonda.

“Mbona Paul hakufikishwa huko Hospitali ya Amana alishukia njiani na anaendelea na maisha yake kama kawaida.


Paul Mbembela akiwa mahtuti.



“Unajua kiukweli tunashindwa kuelewa kama kweli alipata mshtuko au laa, maana alipoingia tu kwenye gari la wagonjwa, akaomba kushuka bila hata kupewa huduma yoyote,” alisema mfanyakazi huyo.

Baada ya habari hizo, Amani liliingia kazini kufuatilia suala hilo ambapo lilianzia Hospitali ya Amana na kufanikiwa kuzungumza na baadhi ya madaktari ambao waliweka wazi kuwa hawajampokea mgonjwa wa aina hiyo.



“Huyo mgonjwa hatujampokea kabisa hapa na hata kama angefikishwa kwa ishu ya kuanguka angeondoka haraka tu si wa kulazwa sana hospitali,” alisema daktari mmoja.

Baada ya daktari kuongea hayo, Amani lilienda Halmashauri ya Wilaya ya Ilala kwa ajili ya kumtafuta Paul ili kuongea naye ambapo ilielezwa kuwa hakufika kazini lakini waandishi wetu walifanikiwa kupata namba yake na kuzungumza naye.

Hata hivyo, baada ya kupokea simu, aliitikia vizuri salamu lakini alipoambiwa kwamba unazungumza na mwandishi wa habari, alijibu kwa kifupi na kukata simu.



Amani: Halo nazungumza na Mr Mbembela?

Mbembela: Yeah, nani mwenzangu.

Amani: Naitwa (jina la mwandishi).

Mbembela: Ndiyo bwana niambie.



Amani: Bwana pole sana kwa matatizo yaliyotokea.

Mbembela: Asante bwana kwani wewe umesema ni (anataja jina moja la mwandishi) nani?

Amani: (Mwandishi anarudia kutaja jina lake kamili na kujitambulisha chombo anachotoka) nilitaka kujua unaendeleaje na…

Mbembela: Bwana mimi bado naumwa, niko hospitali na daktari wangu amenikataza kuzungumza kwa sasa.



Amani: Lakini tulitaka kuju…

Mbembela alikata simu na hata alipopigiwa mara kadhaa tena, hakupokea.

Mbembela alizua gumzo la aina yake baada ya kuulizwa maswali na Makonda katika mkutano wake wa kutatua kero mbalimbali za wananchi uliowakutanisha wakuu wa idara zote za Jiji la Dar pamoja na wanasheria katika Ukumbi wa Diamond Jubilee.

Kwenye mkutano huo, Mbembela alipokuwa akielezea kesi za migogoro ya ardhi zilizopo katika wilaya yake alisema zipo 139 wakati Makonda alisema taarifa aliyonayo yeye ni kesi 1503 na alipobanwa zaidi, ghafla Mbembela alianguka.

Marekani Yatoa Neno Kuhusu Mauaji Yanaoendelea kwa Viongozi wa Chadema

$
0
0
Marekani Yatoa Neno Kuhusu Mauaji Yanaoendelea kwa Viongozi wa Chadema
Ubalozi wa Marekani nchini Tanzania umeweka wazi kusikitishwa na taarifa za kutekwa na utumiaji nguvu kikatili uliosababisha kifo cha Katibu wa CHADEMA kata ya Hananasifu Daniel John.


Taarifa hiyo kutoka ubalozi wa Marekani kwa vyombo vya habari  imesema kwamba tukio hilo la mauaji la makabiliano ya kihasama na vitendo vya kikatili ni jambo linalotia wasiwasi na kusikitisha sana.

‘’Tunatuma salamu zetu za rambirambi kwa familia na marafiki wa marehemu kwa msiba huu. Tunatoa wito kwa vyama vyote kulinda amani na usalama wa mchakato wa kidemokrasia, taifa na wa watu wa Tanzania’ ’imesema taarifa hiyo.

Aidha taarifa hiyo imeongeza kwamba  ‘’Tunaungana na Watanzania katika kutoa wito wa kufanyika kwa uchunguzi wenye uwazi ili kuwawajibisha wale wote wanaohusika na vitendo hivi vya kikatili kwa mujibu wa sheria za Tanzania".

Kiongozi wa CHADEMA kata ya Hananasif Kinondoni, Daniel John ameuawa kwa kukatwa mapanga baada ya kuamriwa kuingia kwenye gari na baadaye mwili wake kuokotwa kwenye ufukwe wa ,Coco Beach' ukiwa umekatwa mapanga sehemu mbalimbali.

Julius Mtatilo Aiponda Kazi ya Polepole

$
0
0
Julius Mtatilo Aiponda Kazi ya Polepole
Mwenyekiti Kamati ya muda ya uongozi wa CUF, Julius Mtatiro amesema hata kama angelikuwa ni miongoni mwa wanachama wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) asingeweza kukubali kukitumikia cheo cha Humphrey Polepole kwa madai sio kazi sahihi.


Mtatiro ametoa kauli hiyo mapema leo asubuhi katika ukurasa wake wa kijamii baada ya kupita masaa kadhaa tokea Katibu wa Itikadi na Uenezi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Humphrey Polepole kuongea na waandishi wa habari na kuwataka vyama vya upinzani viwe na uvumilivu katika uchaguzi unaotarajiwa kufanyika kesho (Jumamosi) kwa sababu ni kawaida yao kushindwa katika chaguzi zote.

"Hata kama ningelikuwa mwana CCM, ningeikataa kazi ya usemaji wa CCM. Ina hukumu nyingi sana mbeleni, si kazi sahihi", ameandika Mtatiro.

Kwa upande mwingine, Kesho (Jumamosi) Wananchi wa Jimbo la Kinondoni, Siha wanatarajia kuingia katika zoezi la kupiga kura ili waweze kumpata muwakilishi mmoja katika jimbo lao aweze kwenda kuwatetea maslahi yao ndani ya Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania linalotarajiwa kuanza Aprili 03 mwaka 2018.

Kwa Mara ya Kwanza Caira Aonyesha Sura ya Mtoto Wake

$
0
0
Kwa Mara ya Kwanza Caira Aonyesha Sura ya Mtoto Wake
Msanii wa muziki wa RnB, Ciara ameachia picha zinazoonyesha sura ya mtoto wake Sienna Princess Wilson aliyezaliwa mwezi wanne mwaka 2017 kwa mara ya kwanza.

Picha za mtoto huyo wa Ciara na Russell Wilson, zimeachiwa kupitia app ya TraceMe ya mume wake huyo aliyiozundua.

“She’s The Sweetest Angel! Read my letter to Sienna and see more photos of Baby SiSi and I Shot By Daddy on my TraceMe App. ❤” ameandika Ciara ambaye ni mama wa watoto wawili kupitia mtandao wa kijamii wa Instagram


Fuvu la Miaka 100 Lakutwa Ofisi za Mawakili IMMMA

$
0
0
Fuvu la Miaka 100 Lakutwa Ofisi za Mawakili IMMMA
WAJENZI wa jengo la ofisi ya kampuni ya uwakili jijini Dar es Salaam, wamekuta fuvu la binadamu linalosadikiwa kuwa la miaka 100 iliyopita.

Jengo linalojengwa upya ni mali ya Kampuni ya uwakili ya IMMMA, baada ya la awali kuharibiwa na mlipuko mwaka jana.

Mmoja wa mawakili wa kampuni hiyo, Fatuma Karume, aliiambia Nipashe jana kuwa baada ya jengo la ofisi hiyo kuharibiwa, walivunja jengo la nyuma yake kwa ajili ya ujenzi wa jengo jipya.

“Wakati mkandarasi anachimba chini ndipo walipokuta fuvu, inasemekana limezikwa kama miaka 100, nafikiri lilikuwa ni kaburi la mtu binafsi,” alisema.

Karume alisema kaburi lolote kulihamisha inabidi itolewa amri ya mahakama na mamlaka ya kushughulikia suala hilo ni polisi.

“Polisi watafanya kazi hiyo, sio kazi yetu kwa sababu hili kaburi linaonyesha ni la muda mrefu, tulichokuta ni fuvu,” alisema Karume.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Ilala, Salum Hamdani, alithibitisha kuwapo kwa tukio hilo na kueleza kuwa kichwa kinachodhaniwa cha binadamu kilikutwa urefu wa futi tatu hadi nne na mafundi hao.

“Tunafanya uchunguzi kubaini kama hivyo viungo ni vya binadamu na pia kuangalia historia ya eneo hilo,” alisema Hamdani.

“Tutakapojiridhisha kama ni viungo vya binadamu tutafuata taratibu za kisheria,” aliongeza Kamanda Hamdani bila kudokeza ni hatua zipi za kisheria.

Trafiki Alierekodiwa Akipewa Rushwa Ashughulikiwa

$
0
0
Trafiki Alierekodiwa Akipewa Rushwa Atimuliwa
ASKARI wa Kikosi cha Usalama Barabarani, ambaye video yake ilisambaa kwenye mitandao ya kijamii jana ikimwonyesha akipokea rushwa ya Sh. 5,000, amefukuzwa kazi kwa fedheha na Jeshi la Polisi.


Video hiyo ambayo ilianza kusambaa kwenye makundi mbalimbali ya kijamii ya WhatsApp na Facebook jana mchana, inamwonyesha askari huyo akipokea kiasi hicho cha fedha iliyoambatanishwa na leseni eneo la Mwenge, jijini Dar es Salaam, pengine mapema wiki hii.

Katika tukio hilo, dereva mmoja aliyeombwa rushwa alimrekodi askari huyo kupitia simu yake ya mkononi wakati akimpatia rushwa hiyo iliyowekwa chini ya leseni.

Dereva huyo akiwa ametegesha kamera yake kwenye gari, askari huyo alifika kwenye kioo cha mlango wa dereva na kumrudishia leseni yake ambayo alikuwa nayo tayari, kisha askari huyo kumwomba ampatie leseni hiyo kwa mara nyingine ikiwa na rushwa.

Baada ya dereva kurudishiwa leseni, aliiunganisha na Sh. 5,000 aliyoiweka kwa chini na kumrudishia askari ambaye naye alikuwa akijifanya kama anatoa risiti kwenye mashine yake kielektroniki aliyokuwa ameishika mkononi.

Baada ya kupokea leseni iliyokuwa ikiwa imeambatanishwa na fedha hizo, trafiki huyo alichukua fedha na kumrudishia leseni dereva huyo kisha kuondoka.

Akizungumza na Nipashe jana jijini Dar es Salaam,  Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Kinondoni, Kamishna Msaidizi wa Polisi Jumanne Murilo, alisema tayari askari huyo ameshachukuliwa hatua kwa kufukuzwa kazi tangu Jumanne.

Kamanda Murilo alisema askari huyo hadi anafukuzwa kazi ndani ya Jeshi la Polisi alikuwa amefanya kazi kwa muda wa mwaka mmoja na nusu.

"Tukio hili lilifanyika eneo la Mwenge na baada ya kulibaini tulianza uchunguzi wetu ambao juzi (Jumanne) ulikamilika na kubaini tukio hilo lilikuwa la kweli (kwamba) amepokea rushwa. Hivyo tumemuondoa kazini," alisema.

Kamanda Murilo ambaye hakumtaja jina askari huyo aliwakumbusha trafiki kuzingatia maadili ya kazi na taratibu za kijeshi zilizowekwa.

Vitendo vya kuwachukua video trafiki wanaopokea rushwa vimekuwa vikijitokeza mara kwa mara ambapo tukio lingine linalofanana na hilo lilitokea mkoani Tanga mwaka 2015.

Katika tukio hilo, aliyekuwa askari wa Kikosi cha Usalama Barabarani, Koplo Anthon Temu, mwenye namba F785 alifukuzwa kazi kwa tuhuma za kuomba na kupokea rushwa.

Tukio hilo lilithibitishwa na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tanga, Zuberi Mwombeji ambaye alisema lilitokea barabara kuu ya Chalinze-Segera.

Alisema kupitia mitandao ya kijamii, askari huyo alionekana akipokea rushwa kutoka kwa dereva wa gari alilokuwa amelisimamisha kwa ajili ya kukagua makosa yanayoweza kuhatarisha usalama barabarani.

Tukio lingine ni lile lililotokea visiwani Zanzibar mwaka uliopita, baada ya Sajini Hamad Kassim wa Kituo cha Mkokotoni visiwani humo, kuonekana kwenye video akipokea rushwa ya Sh. 10,000.

Rushwa hiyo aliiomba kutoka kwa raia wa kigeni baada ya kumkamata akiwa hajafunga mkanda wakati akiendesha gari.

Miujiza ya Sharifu Seif Mohamed..JE Umeachwa na Mme/Mke au Mpenzi, Umesongwa na Mitihani ya Maisha..Piga Simu Upate Muujiza Wako

$
0
0
SHARIFU SEIF MOHAMED ANAWASHUKURU WALE WOTE WANAOENDELEA KUPIGA SIMU, WENYE MATATIZO NA WALE WANAOTOA  SHUKRANI NA SHUHUDA JINSI TIBA ZAKE ZINAVYO WASAIDIA,

(Rudisha mahusiano yako ndani ya masaa 72 tu)

SHARIFU MOHAMED Ni  mtaalam na mnajimu maarufu wa nyota na kubashiri mambo yanayo watesa binadamu duniani kote na kupata ufumbuzi, Anatumia kitabu cha QUR'AN, Dawa za Asili, Dawa za Kiarabu na majini kwa kumtuliza mke/mme, mchumba au mpenzi ndani ya masaa 72 tu, na kutatua matatizo yote ya kimaisha,

Je Umeachwa na UMPENDAE awe Mme/Mke na bado unampenda? Je Umekimbiwa na Mmeo/ Mkeo n anaishi na mtu mwingine? Je Umejaribu sehemu nyingi bila mafanikio? Mpigie simu SHARIFU SEIF sasa hivi ujionee Muujiza wa Papo kwa Papo, Anauwezo wa hali ya juu wa kusambaratisha mahusiano yao na kumrejesha kwako haraka sana na Kumfanya Atimize Ahadi zote Ndani ya Muda Mfupi Endapo Utafwata Atakacho Kuelekeza

ANAZO DAWA ZA MAPENZI, NGUVU ZA KIUME, CHANGO NGIRI MAJI NA N.K, ZINDIKO LA NYUMBA NA BIASHARA, PETE ZA BAHATI, HUMALIZA KABISA TATIZO LA NGUVU ZA KIUME NA KUREFUSHA UUME KWA SAIZI UNAYOTAKA, HUZUIA CHUMA ULETE KWENYE BIASHARA, HURUDISHA MALI ZILIZOPOTEA, MAGONJWA SUGU, MIGUU KUWAKA MOTO AU KUFA GANZI, HUTIBU BUSHA BILA KUPASUA, ANAO UWEZO WA KUMRUDISHA ALIE MBALI AU ALIECHUKULIWA MSUKULE, KUPANDISHA NYOTA NA KUSHINDA BAHATI NA SIBU, KASAFISHA NYOTA NA KUKUPA MVUTO WA AJABU, KUTOA NUKSI NA VIFUNGO MBALIMBALI,  MAFANIKIO YA MAISHA NA UTAJIRI BILA MASHARI, NA MENGINE MENGI YA SIRI,

JE UMAHANGAIKA KUPATA MTOTO BILA MAFANIKIO? WASILIANA NA MTAALAMU HUYU KWANI YEYE HUFAULU PALE WOTE WALIPOSHINDWA, PIA UMALIZA KAZI ZILIZO SHINDIKANA NA WATAALAM WENGINE NDANI YA MASAA 24 TU,

(NA ANATIBU KWA NJIA YA SIMU UKIWA NCHI YOYOTE AU MKOA WOWOTE ENDAPO UTAFWATA MAELEKEZO YAKE)

Kwa ushauri na mawasiliano  zaidi Piga SIMU No:

Mobile +255 654-836970
WhatsApp +255 756-033670

Azam Ugenini Leo Kuvaana na Lipuli FC

$
0
0
Azam Leo Ipo Ugenini Kuvaana na Lipuli FC
Ligi kuu soka Tanzania Bara inaendelea leo kwa mchezo mmoja ambapo Azam FC watakuwa ugenini mkoani Iringa kucheza na wenyeji wao Lipuli FC kwenye uwanja wa Samora mjini humo.


Azam FC leo watakuwa wanasaka ushindi wa kwanza ndani ya mechi tatu, baada ya Februari 7 kufungwa 1-0 na Simba SC Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam kabla ya kutoa sare ya 1-1 na wenyeji, Kagera Sugar Uwanja wa Kaitaba mjini Bukoba.

Kwa upande wao Lipuli FC inayofundishwa na nyota wa zamani wa Simba SC, Amri Said na Suleiman Matola, wametoka kushinda mechi moja kati ya 10 zilizopita, wakifungwa tano na sare nne hivyo nao watakuwa wanataka kuutumia uwanja wa nyumbani vizuri.

Kikosi cha Azam FC kimepata nguvu mpya kuelekea mchezo wake wa leo baada ya wachezaji wake wawili waliokosa mechi mbili zilizopita, Nahodha msaidizi Aggrey Moris, aliyekuwa akitumikia adhabu ya kadi tatu za njano na mshambuliaji Yahya Zayd wote kurejea kikosini.

Mchezo huo ni wa raundi ya 19 ambapo Azam FC inashika nafasi ya tatu kwa pointi 34 nyuma ya Yanga yenye alama 37 katika nafasi ya pili na vinara Simba wakiwa kileleni kwa pointi 42. Lipuli FC inashika nafasi ya 9 na alama 19.
Viewing all 104795 articles
Browse latest View live




Latest Images