Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104795 articles
Browse latest View live

Download Application ya MCHAMBUZI HURU Kwenye Simu yako Kusoma Habari za Siasa Kila Baada ya Lisaa Limoja

$
0
0

Maswala ya Siasa na Matamko ya kila siku ya Wanasiasa Hakikisha Umedownload App ya Mchambuzi Huru Kwenye simu yako

Kama we ni Mpenzi wa Habari za Siasa Usipitwe na Hii Application ya Mchambuzi..... 

Bonyeza HAPA Kudownload kwenye Simu yako



Malisa: Polisi ni Sehemu ya Watuhumiwa Hawapaswi Kuhusika Kuchunguza Kifo cha Akwilina

$
0
0
Malisa: Polisi ni Sehemu ya Watuhumiwa Hawapaswi Kuhusika Kuchunguza Kifo cha Akwilina

Aliyekuwa mgombea ubunge Kinondoni kupitia Chama cha Tanzania Labour (TLP) katika uchaguzi uliofanyika Februari 17, 2018, Dk Godfrey Malisa amesema polisi hawapaswi kuhusika katika uchunguzi wa kifo cha mwanafunzi wa Chuo cha Usafirishaji cha Taifa (NIT), Akwilina Akwiline.

Akizungumza leo Februari 19, 2018 na MCL Digital, Malisa amesema polisi ni sehemu ya watuhumiwa, hivyo hawawezi kujichunguza wenyewe.

Akwilina aliuawa Februari 16, 2018 kwa kupigwa risasi na polisi eneo la Mkwajuni wakati askari wakiwatawanya wafuasi wa Chadema wakiongozwa na Mwenyekiti wa chama hicho, Freeman Mbowe waliokuwa wakielekea katika ofisi ya Msimamizi wa Uchaguzi Jimbo la Kinondoni, Aron Kagurumjuli kudai hati ya viapo vya mawakala wao.

Tayari Jeshi la Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam linawashikilia askari wake sita kwa uchunguzi pamoja na silaha zao huku Kamanda wa kKanda hiyo, Lazaro Mambosasa akisema hawajathibitisha kama risasi iliyompata Akwilina ilipigwa na askari na kwamba, watuhumiwa 40 wanachunguzwa ili kubaini kama miongoni mwao walikuwa na silaha za moto.

“Namuomba sana Rais (John Magufuli) kuingilia kati uchunguzi huru wa tukio la kifo cha mwanafunzi. Polisi hawatakiwi kujichunguza wenyewe kwa sababu ni sehemu ya watuhumiwa, inawezekaje mtuhumiwa kujichunguza?” amehoji Malisa.

“Tena wanasema tutachunguza kama risasi ilikuwa ya polisi au waandamaji. Namuomba Rais aingilie kati ili  iundwe tume huru ya uchunguzi.”

Tohara kwa Wanaume Yapigwa Marufuku

$
0
0
Tohara kwa Wanaume Yapigwa Marufuku
Wakati Serikali ya Tanzania na nchi nyingine barani Afrika zikihimiza ulazima wa tohara kwa wanaume, hii ni tofauti kabisa na nchi ya Iceland ambapo limetangaza kupiga marufuku tohara kwa wanaume na kuwa taifa la kwanza barani Ulaya kufanya hivyo.


Hata hivyo mvutano wa kupitisha muswada huo bado unajadiliwa bungeni huku kukiwa na mvutano wa kidini kati ya Wayahudi na Waislamu ambao ndio wachache kwenye bunge hilo.

Kwa mujibu wa gazeti la Times Of Israel limeeleza kuwa Muswada huo unaojadiliwa na Bunge la Iceland unapendekeza kwa mtu yeyote atakayekutwa amefanyiwa tohara afungwe hadi miaka sita jela la sivyo awe na sababu maalumu za kufanyiwa tohara.

Kwa upande mwingine Wanaharakati na Wanadiplomasia duniani wamesema kuwa hatua hiyo itazua hisia kali kwa viongozi wa kidini barani Ulaya huku wakieleza kuwa Wayahudi na Waislamu ambao ni zaidi ya 2,000+ nchini Iceland watakuwa katika hali ngumu ya maisha.

Wabunge wengi wanaounga mkono muswada huo Muswada huo wanasema kuwa tohara ya wavulana wadogo inakiuka haki yao ya kibinaadamu na ni kinyume na azimio la Umoja wa Mataifa kuhusu haki ya mtoto.

Ingawaje kwenye muswada huo kuna kipengele kinachoruhusu mwanaume kufanyiwa tohara kwa sababu za kidini au afya kwa masharti ya hadi afikie miaka 18, Waislamu na Wayahudi wanapinga vikali hatua hiyo kwani inakiuka tamaduni yao ya kuwafanyia tohara watoto wadogo.

Jux Ashukuru Shangwe la Burundi "Sitokuja Kusahau Upendo Wenu Kwenye Maisha Yangu"

$
0
0
Jux Ashukuru Shangwe la Burundi "Sitokuja Kusahau Upendo Wenu Kwenye Maisha Yangu"
Siku ya February 14,2018 staa wa muziki nchini Juma Jux aliwasili Burundi kwa ajili ya kufanya show ikiwa ndio mara yake ya kwanza nchini humo ambapo alipokelewa kwa shangwe na baadhi ya mashabiki.

Kupitia instagram akaunti ya Jux ameonyesha kufurahishwa na mashabiki walijitokeza kum-support kwa  kuhudhuria show ambayo aliifanya nchini humo na wakati akiwa kwenye stage waliimba pia wimbo wa Taifa wa nchi hiyo.



“Asanteni sana burundi sitaweza kuja kusahau upendo wenu kwenye Maisha yangu japo Mvua kubwa kunyesha bado mkakubali mnyeshewe nakuja kwa wingi sana kwenye show.”

“We made a history nashukuru kwa heshima yenu ya kuniimbia wimbo wa taifa 🙌🏾🙌🏾 kama heshima yenu kwangu na hii haijawahi kutokea kwa Msanii yoyote yani yote aliyeshawahi kuja burundi Asanteni sana sana #love #burundi #history#music #power #africanboyworldwide”

Ukiacha nchi za jirani kama Kenya, Uganda, Burundi ndio taifa lingine la jirani na Tanzania linalocheza nyimbo za Bongofleva Redioni na kwenye Tv

Serikali Kumfikisha Mahakamani Mkandarasi wa Uwanja wa Ndege wa Songwe

$
0
0
Serikali Kumfikisha Mahakamani Mkandarasi wa Uwanja wa Ndege wa Songwe
Serikali imeagiza Mkandarasi jengo la abiria uwanja wa ndege wa kimataifa wa Songwe uliopo katika Mkoa wa Mbeya, afikishwe Mahakamani kwa kushindwa kukamilisha kwa wakati ujenzi wa jengo la abiria katika uwanja huo.


Maagizo hayo yametolewa na Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Mhandisi Atashasta Ndikiye wakati akifuatilia utekelezaji wa agizo la Waziri wa Wizara hiyo Prof. Makame Mbarawa ambapo aliagiza kampuni ya kiazalendo ya DB Shapriya ikamilike ujenzi kabla ya Januari 31 mwaka huu.

"Tunahitaji miradi ya serikali ambayo inawagusa wananchi ifanyike na imalizike. Tunataka awamu hii tuoneshe kwa vitendo kwamba tunataka kufanya kazi za nchi", amesema Mhandisi Atashasta.

Kwa upande wake, Kaimu Mkurugenzi wa viwanja vya ndege vya mikoa, Joseph Nyahende amemweleza Naibu Waziri Ndikiye kuwa mradi huo ambao pia unahusisha ujenzi wa maegesho ya ndege na barabara, ulikuwa na thamani ya zaidi ya shilingi bilioni 11 na kwamba hadi sasa serikali haidaiwi na mkandarasi, huku mhandisi mshauri wa mradi huo Silanda Dustan akiishauri serikali kutafuta njia mbadala ya kukamilisha kazi hiyo kwa vile mkandarasi wa sasa hana uwezo.

Msikilize hapa chini  Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Mhandisi Atashasta Ndikiye akifafanua baadhi ya mambo.

Mwili wa Mwanafunzi Aliyepigwa Risasi Wapelekwa Muhimbili kwa Uchunguzi

$
0
0
Mwili wa Mwanafunzi Aliyepigwa Risasi Wapelekwa Muhimbili kwa Uchunguzi
Mwili wa mwanafunzi wa Chuo cha Taifa cha Usafirishaji (NIT), Akwilina Akwiline umepelekwa Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) leo Jumatatu Februari 19,2018 asubuhi.

Mwili wa Akwilina umehamishiwa Muhimbili ukitokea Hospitali ya Mwananyamala kwa ajili ya kufanyiwa uchunguzi.

Ndugu wa marehemu wamekusanyika Muhimbili katika eneo la chumba cha kuhifadhia maiti, wakisubiri uchunguzi ukamilike ili kujua hatima ya kuusafirisha kwa ajili ya mazishi yatakayofanyika wilayani Rombo mkoani Kilimanjaro.

Akwilina alifariki dunia Februari 16,2018 baada ya kupigwa risasi kichwani akiwa kwenye daladala na polisi walipokuwa wakiwatawanya waandamanaji ambao ni wafuasi wa Chadema.

Akizungumza na MCL Digital hospitalini Muhimbili leo Februari 19,2018, Moses Kiyeyeu aliyejitambulisha kuwa ni kaka wa marehemu amesema madaktari na wahusika wengine wanaendelea na utaratibu wa uchunguzi wa mwili.

"Mwili umefikishwa hapa tangu asubuhi na kule ndani kuna kaka yetu ndiye anashuhudia uchunguzi huo, wametwambia tutoke kwanza ndani watatuita baadaye ili kupewa taarifa nini kinafuata kuhusu mwili wa ndugu yetu," amesema.

Kiyeyeu amesema familia inasubiri uchunguzi ukamilike ili waruhusiwe kuuchukua mwili kwa kuwa wazazi wa Akwilina wanausubiri.

Trump Awatoa Hofu Wafuasi Wake Amchimba Mkwara Oprah

$
0
0
Trump Awatoa Hofu Wafuasi Wake Amchimba Mkwara Oprah
Rais wa Marekani, Donald Trump amewatoa hofu wafuasi wake  baada ya tetesi kuwa huenda mwanamke Mjasiriamali, Oprah Winfrey atajitupa kwenye kinyang’anyiro cha urais wa nchi hiyo mwaka 2020.

Trump amesema anamfahamu sana Mwanamama huyo na ni moja ya watu ambao huwa anafuatilia viindi vyake ingawaje huwa anaboreka na namna ya uuliza maswali yake kwa wageni anaowaalika kwenye show zake huku akipindisha baadhi ya ukweli wa mambo.

“Nimemtazama Oprah Winfrey mtu asiyekuwa madhubuti, ambaye kwa upande mmoja namfahamu vizuri, nimekuwa nikimtazama akifanya mahojiano na watu wengi kwa dakika 60. Maswali yake yamekuwa ya upendeleo, yamekosa mwelekeo na amekuwa akipindisha ukweli, natumaini Oprah anaweza akajitokeza na kugombea urais na nitamshinda kama nilivyowafanyia wenzake,“ameandika Trump kwenye ukurasa wake wa Twitter.

Mwishoni mwa mwaka jana Oprah wakati akitoa hotuba yake katika ugawaji wa tuzo za Golden Globe aliushitua ulimwengu baada ya kutangaza kuwa  anaweza akagombea Urais wa Marekani mwaka 2020.

Hata hivyo, baadaye Oprah kupitia kipindi chake cha ‘Daytime Talk Show’  alikuja kukanusha uvumi huo kwa kusema kuwa alitania tu ili kunogesha hotuba kwani kazi hiyo haipo kwenye damu yake.

Wafanyakazi Wawaponza Wakurugenzi Wao Wafikishwa Mahakamani

$
0
0
Wafanyakazi Wawaponza Wakurugenzi Wao Wafikishwa Mahakamani
Leo February 19, 2018 Wakurugenzi  Watendaji wa Kampuni nne wamefikishwa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu wakikabiliwa na makosa ya kutojisajili na kupeleka taarifa za wafanyakazi wao katika Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi ( WCF).

Wakurugenzi hao ni Abshir Gure na Farhiya Wrsame (Kampuni ya Lasar Logistic Limited), Joseph Alexander (Kamanda Security Guards Co.Ltd).

Pia Riziki Shemdoe na Deusdedit Kibassa (Kampuni ya ENCC Consultants) na Mallakhara Semis na Shafeek Purayil (Kampuni ya Spash International Co.Ltd).

Washtakiwa hao wamesomewa mashtaka yao mbele ya Hakimu Mfawidhi, Victoria Nongwa na Mawakili tofauti akiwemo Emmil Kilia.

Akisomewa mashtaka yake, Joseph wa Kampuni ya Kamanda Security Guards Co.Ltd anadaiwa kuwa January ,26,2018 walishindwa kujisajili na kutoa taarifa muhimu za shughuli zake kwa WCF.

Kilia amedai katika kesi hiyo namba 34 ya 2018 mshtakiwa huyo alishindwa kutoa taarifa muhimu za wafanyakazi wake kwa afisa aliyeteuliwa na Mkurugenzi Mkuu wa WCF.

Ilidaiwa January 11,2018 mshtakiwa huyo alishindwa kutoa taarifa muhimu za waajiriwa wake ikiwamo majina na mishahara ya wafanyakazi.

Mshtakiwa Malakhara Semis na Shafeek Purayil wa kampuni ya Spash International Co.Ltd
wamesomewa mashtaka yao na Wakili wa Serikali Mwandamizi, Benson Mangowi ambapo amedaili December 25,2017 washtakiwa walishindwa kusajili.

Pia walishindwa kutoa taarifa muhimu za wafanyakazi wao kwa Afisa aliyeteuliwa na Mkurugenzi Mkuu wa WCF ambapo September 6,2017  washtakiwa hao walishindwa kutoa taarifa muhimu za wafanyakazi ikiwamo majina na mishahara.

Mshtakiwa mwingine Abshir Gure na Farhiya Warsame wamesomewa mashtaka yao na wakili wa Serikali, Emma Msofe ambapo amedai November 3,2017 walishindwa kusajili na kupelekwa taarifa muhimu kwa Mfuko wa WCF.

Amedai kuwa October 19,2017 walishindwa kutoa taarifa muhimu zikiwamo majina na mishahara.

Hata hivyo, mshtakiwa Riziki Shemdoe na Deusdedit Kibassa wa kampuni ya ENCC wameshindwa kusomewa mashtaka yao kwa sababu hawakuwepo mahakamani kutokana na kupata udhuru.

Katika kesi hizo, upande wa mashtaka umeeleza kuwa upelelezi wa kesi hizo umekamilika.

Hakimu Nongwa alimtaka kila mshtakiwa kuwa na wadhamini wawili ambapo kila mdhamini atasaini ahadi ya Shilingi Milioni 50.

Washtakiwa hao walitimiza masharti ya dhamana na kuachiwa.

Familia ya Wanandoa Waliokamatwa China naDawa za Kulevya Wafikiana Matunzo ya Mtoto

$
0
0
Familia ya Wanandoa Waliokamatwa China naDawa za Kulevya Wafikiana Matunzo ya Mtoto
Kamishna Msaidizi wa Ustawi wa Jamii, Daniel Masunzu amesema familia mbili za wanandoa Baraka Malali na Ashura Mussa zimekubaliana mtoto atunzwe na babu yake Hashim Mbarouk.

Wanandoa Baraka na Ashura walikamatwa Januari 19,2018 nchini China wakiwa na mtoto wao mwenye umri wa miaka miwili na miezi tisa wakituhumiwa kupatikana na dawa za kulevya.

Mbarouk ni babu upande wa mama aliyempokea mtoto huyo aliporejeshwa nchini Februari 14,2018.

Masunzu akizungumza na waandishi wa habari leo Februari 19, 2018 baada ya majadiliano na pande hizo mbili, amesema muafaka umepatikana mtoto kuwa chini ya familia ya Mbarouk na Zuhura Nyangasa ambaye ni bibi yake upande wa mama.

“Familia zote mbili zimekubaliana kuhusu hatua hii. Mtoto kukaa upande wa Mbarouk haina maana kwamba matunzo watayatoa wao peke yao, bali ndugu wengine wana jukumu la kuendelea kufanya mawasiliano na mtoto kwa ajili ya matunzo,” amesema Masunzu.

Akizungumza kwa niaba ya familia hizo mbili, Wile Stanford ambaye ni kaka wa Malali amezishukuru Serikali za Tanzania na China kwa kumrejesha salama mtoto huyo.

Amesema wazazi wa pande zote mbili wamefikia makubaliano mazuri kuhusu matunzo.

Fainali za Mataifa ya Afrika (Afcon) Mwakani Kupigwa Uwanja wa Uhuru

$
0
0
Fainali za Mataifa ya Afrika (Afcon)  Mwakani Kupigwa Uwanja wa Uhuru
Waziri wa Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo, Dk Harrison Mwakyembe ametaja viwanja vitakavyotumika katika mashindano ya vijana chini ya miaka 17 katika fainali za Mataifa ya Afrika (Afcon) mwakani.

Waziri Mwakyembe alisema Uwanja wa Taifa utatumika kwaajili ya ufunguzi na kufungukia mashindano hayo, huku viwanja vingine vya Uhuru na Azam Complex Chamazi vikitumika katika mechi za mashindano hayo.

"Tunataka tufanye mabadiliko katika hizi nyasi bandia za uhuru tuweke mpya, lakini uwanja wa Gymkhana utatumika kwa mazoezi, bado kuna viwanja vingine tunaendelea kuvichagua ili timu zipate sehemu ya kufanyia mazoezi kwa urahisi," alisema Mwakyembe.

Waziri Mwakyembe alisema wanajua wingi wa timu nane zinazokuja zitakuwa na viongozi, wachezaji na mashabiki hivyo wanajiandaa kuhakikisha wageni hao wanapata mahitaji yao mapema.

"Magari yanahitajika kwaajili ya kuwabeba wageni wetu hivyo inabidi yapatikane na kuandaliwa mapema, lakini pia tunajupanga juu ya suala la foleni wasiweze kukutana nalo,'' alisema.

Mwakyembe aliongeza kwamba wanaendelea na maandalizi, wapo katika hatua nzuri kwa ajili ya mashindano hayo.

utana na Mtabibu Mwenye KUBRI kutoka kwa ALLAH issa simba Mtabibu wa Nyota za Binadamu na Kutumia Vitabu vya QUR-AN

$
0
0
Kutana na Mtabibu Mwenye KUBRI kutoka kwa ALLAH issa simba said Mtabibu wa Nyota za Binadamu   Africa Mwenye UWEZO Kubaini tatizo lako Pindi tu Utakapo Fanya Mawasilino Kupitia Wasaa Husika..

JE UNASUMBULIWA NA Mapenzi? (Umeachwa na Umpendae,Awe Mume,Mke na Bado unampenda?Na Umejaribu Sehemu nyingi Bila Mafanikio?Wasilina na Maalim Hussein Ujione muujiza wa Papo kwa Papo.. anauwezo WA KURUDISHA MAHUSIANO NA KUIMARISHA NDOA YAKO . Umekimbiwa na Mumeo,mkeo au Mpenzi na anaishi na mtu mwingine? Muone akutatulie Anauwezo wa Hali ya Juu wa Kusambalatisha Mahusiano yao Endapo utafata Atakacho kuelekeza.
Atamfanya Atimize Ahadi zote kwa Muda Mfupi.

Issa simba said Anatumia Jina la Muhusika au Picha Kumaliza Tatizo lako..
Anatibu kwa Kutumia Vitabu vya QUR-AN .Anatafsiri Ndoto. Kushinda BAHATI NASIBU, KUSAFISHA NYOTA. Mvuto wa Mwili na BIASHARA, Kinga ya Mwili,ZINDIKO za Nyumba.MIGUU Kufa GANZI.Kufungua KIZAZI kwa wale walio fungwa kwa njia za KISHIRIKINA.

Anakupa Jini la Mali kwa yule anaehitaji Utajiri BILA MASHARTI.  Humaliza Kesi zilishindika ndani ya siku 14 tu..na mengi zaidi

+255 622588038au 0679119679 au +255 764318107

Ndugu Wagoma Kuchukua Mwili wa Akwilina

$
0
0
 Ndugu Wagoma Kuchukua Mwili wa Akwilina
Dada wa mwanafunzi wa Chuo Kikuu cha Taifa cha Usafirishaji (NIT), Akwilina Akwiline aliyeuawa kwa kupigwa risasi na polisi, Tegolena Uiso amesema hawatapokea mwili wa mwanafunzi huyo bila kuelezwa nini kilichomuua ndugu yao.

Mwili wa Akwilina umehamishiwa Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) ukitokea Hospitali ya Mwananyamala kwa ajili ya kufanyiwa uchunguzi.

Akizungumza leo Februari 19, 2018 na MCL Digital akiwa MNH, Tegolena amesema ni vyema wakapewa ripoti kuhusu kilichogundulika baada ya ndugu kuelezwa kuwa mochuari ya  Muhimbili kwamba watatoa ripoti ya uchunguzi baada ya siku 14.

"Sisi tumekuja kwa ajili ya kujua hasa ndugu yetu nini kimemkuta hatuwezi kupokea mwili bila ripoti. Wanatuambia  ni baada ya wiki mbili sina hakika kama hawajabaini kitu chochote, hatuwezi kuuchukua mwili mpaka tupewe sababu," amesema Tegolena.

Amesema mpaka sasa wamezungumza na Mkuu wa Chuo cha Usafirishaji NIT, Profesa Zakaria Mhanilwa ambaye bado anawasiliana na madaktari ndani na hawajajua iwapo atakuja na majibu sahihi.

Awali, Profesa Mhanilwa amesema amefika hospitalini hapo kufuatilia uchunguzi huo akiwa ni miongoni mwa wafiwa.

Akwilina alifariki dunia Februari 16, 2018 baada ya kupigwa risasi kichwani akiwa kwenye daladala wakati polisi wakiwatawanya waandamani ambao ni wafuasi wa Chadema.

Serikali Yapiga Marufuku Matangazo ya Kuongeza Makalio

$
0
0
Serikali Yapiga Marufuku Matangazo ya Kuongeza Makalio
Serikali kupitia Mamlaka ya Chakula na Dawa nchini Tanzania (TFDA) kwa kushirikiana na Jeshi la Polisi nchini, imepiga marufuku matangazo ya biashara za vipodozi na dawa za kuongeza maumbile kwenye mitandao ya kijamii kama vile Instagram, Facebook, Twitter na kwenye blogs.

Akizungumza na waandishi wa habari jana Februari 18, 2018 jijini Dar es Salaam, Kaimu Mkurugenzi wa TFDA, Agnes Kijo amesema matangazo hayo yanatakiwa kukoma mara moja na wahusika wanastahili kufika katika mamlaka hizo kuomba kibali.

Bi Kijo amesema kumekuwepo na wimbi la watu mbalimbali wanaotangaza vipodozi kwa lengo la kujichubua na dawa za kuongeza maumbile kwenye mitandao hiyo ya kijamii wakifanya kinyume na Sheria ya Mamlaka ya Chakula, Dawa na Vipodozi sura ya 219.

Amesisitiza kuwa matangazo ya vipodozi na dawa hizo yamekuwa na madai mbalimbali kama vile kuongeza makalio, kuongeza nyonga, sehemu za siri za mwanaume, kurudisha bikira kwa wanawake na kuondoa mabaka sugu na tiba hizo kwenye mfumo wa vidonge, jeli, losheni, mafuta, krimu na dawa za kunywa. Kijo alisema baadhi ya watu wamekuwa wakipotosha umma kuwa bidhaa zao zimethibitishwa na TFDA kitu ambacho si kweli.

Simba Yatimbiza Ndoto za Mtoto Kipenzi cha Okwi

$
0
0
Simba Yatimbiza Ndoto za Mtoto Kipenzi cha Okwi
Soka la Tanzania linazidi kukuwa na kujenga mapenzi kwa watu mbalimbali wazidi kuupenda mchezo huo hususani watoto, tumeona kwa sasa haishangazi kuona watoto wamechora t-shirt zao majina ya wachezaji bongo wanaowapenda tofauti na zamani walikuwa wakiandika majina ya wachezaji wa nje.

Ilianzia Dodoma pale ambapo alipatika mtoto aliyejulikana kwa jina la Ajib wa Dodoma kuandika tshirt yake kwa peni jina la Ajib na namba lakini wakati huu ni wakati wa Okwi wa Bukoba ambaye leo amekabidhiwa jezi za shujaa wake Emmanuel Okwi.

Leo mtoto Shabani Okwi ambaye ni shabiki wa mchezaji wa Simba Emmanuel Okwi ambaye picha zake zilisambaa akihojiwa na Azam TV akiwa ameandika jina la Okwi kwenye nguo yake, amekabidhiwa jezi ya shujaa wake Okwi na  kiongozi wa Makundi ya Simba mtandaoni Jose Munyama.

Mastaa wa soka Bongo Niyonzima, Kaseja, Okwi, Manula na Himid wakiwa na wake zao

Godzilla Auponda Wimbo Mpya wa Nay wa Mitego "Wimbo Mbaya"

$
0
0
Godzilla Auponda Wimbo Mpya wa Nay wa Mitego "Wimbo Mbaya"
Msanii kutoka Bongoflevani Nay wa Mitego amechia Video ya wimbo wake mpya leo February 19, 2018 ambapo kupitia ukurasa wake wa istagram February 18 Nay wa Mitego aliweka caption iliyosomeka…>>>“Video Ya #MikonoJuu Inatoka Kesho J3 Subscribe Kwenye YouTube Channel Yangu #MrNay Uwe Wa Kwanza Kutizama Full Video Ya #MikonoJuu” – Nay wa Mitego

Baada ya Post hiyo ya Nay wa Mitego, msanii wa Hip Hop Godzilla aka-comment chini na kusema wimbo huo wa Nay ni mbaya…>>>”Wimbo mbaya Emanuel” – Godzilla



Hii Hapa Ratiba ya Mazishi Iliyotolewa na Chadema

$
0
0
Hii Hapa Ratiba ya Mazishi Iliyotolewa na Chadema
Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), kimesema kinatarajia kuongoza shughuli za utoaji wa heshima za mwisho kwa mwili wa aliyekuwa Katibu wa chama hicho Kata ya Hananasif Jimbo la Kinondoni, Daniely John siku ya kesho (Jumanne).


Hayo yamebainishwa na taarifa zilizotolewa na Mkuu wa Idara ya Habari na Mawasiliano, Tumaini Makene jioni ya leo (Jumatatu) na kudai mwili wa marehemu Daniel unatarajiwa kufika nyumbani kwake Hananasif ukiwa unatokea hospitali ya Taifa Muhimbili majira ya saa 4 asubuhi na kisa kupelekwa katika Kanisa la Katoliki kwa ajili ya misa ya kumuombea marehemu itakayoanza saa 5 asubuhi kanisani hapo.

Baada ya ibada hiyo, waombolezaji watatoa heshima zao za mwisho kwa Daniel kabla ya mwili wake kusafirishwa kwenda mkoani Iringa ambako atazikwa siku ya Jumatano, katika kijiji cha Chikelewatu wilayani Mafinga.

Binti wa Miaka 7 Kutoka Afrika Apata Shavu Hollywood

$
0
0
Binti wa Miaka 7 Kutoka Afrika Apata Shavu Hollywood
Fani ya uchekeshaji katika mitandao imekuwa ikishika kasi kila kukicha huku wengi wao wakitumia nafasi ya mitandao kuuza kazi zao. Kijana wa miaka saba kutoka Nigeria, Emanuella Ella Angel amefanikiwa kupata dili la kuigiza na kufanya kazi na kampuni kubwa dunia ya utengenezaji filamu ya Disney Studios.

Binti huyo Emanuella ameshafanya kazi vyingi za uchekeshaji ikiwemo ya “My Real Face” ambayo ilimfanya apata tuzo ya G Influence Niger Delta Special Talent Award mwaka 2015, ametumia ukursa wake wa mtandao wa kijamii wa Instagram kujuza mashabuki zake na umma kuhusu dili hilo pia kuwashukuru kwa ushirikiano wao kwake.

“Thanks @disneystudios God bless everyone whose support has added to bringing us here. I never dreamed of being here so soon. I miss Success. I love you all, ameandika Emanuela.

Download Application ya MCHAMBUZI HURU Kwenye Simu yako Kusoma Habari za Siasa Kila Baada ya Lisaa Limoja

$
0
0
Maswala ya Siasa na Matamko ya kila siku ya Wanasiasa Hakikisha Umedownload App ya Mchambuzi Huru Kwenye simu yako

Kama we ni Mpenzi wa Habari za Siasa Usipitwe na Hii Application ya Mchambuzi..... 

Bonyeza HAPA Kudownload kwenye Simu yako


Hatimaye Ndugu Wamekubali Kuuchukua Mwili wa Mwanafunzi Aliyepigwa Risasi Baada ya Kugoma

$
0
0
Ndugu wa mwanafunzi wa Chuo Kikuu cha Taifa cha Usafirishaji (NIT), Akwilina Akwiline aliyepigwa risasi na Polisi Februari 16, 2018 wameeleza ndugu yao alifariki dunia baada ya kupigwa risasi kichwani.

Wametoa ufafanuzi huo leo Februari 19, 2018 muda mfupi baada ya kususa kupokea mwili wa mwanafunzi huyo uliokuwa ukifanyiwa uchunguzi Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) bila kuelezwa nini kilichomuua.

Wakizungumza mara baada ya maafikiano baina yao na madaktari, wamesema wamepewa sehemu ya ripoti ya uchunguzi ambayo wameridhika nayo na sasa wanakwenda kufanya kikao cha ndugu kujadili namna gani watampumzisha Akwilina.

Shemeji wa mwanafunzi huyo, Festo Kavishe amesema uchunguzi wa mwili huo, umeonyesha kwamba Akwilina alijeruhiwa vibaya kichwani.

"Ripoti ambayo tumepewa imeonyesha kwamba kichwa cha marehemu kilipasuliwa vibaya na risasi ambayo iliingilia upande wa kushoto kwa kichwa chake na kutokea upande wa kulia  ambao umefumuka vibaya," amesema.

Kwa mujibu wa Kavishe, iwapo madaktari wasingewapatia majibu hayo wasingethubutu kuuchukua mwili huo kwa mazishi, kwa sababu walihitaji kupata picha kamili ya nini kilimuua Akwilina.

"Sasa tumeshafahamu nini hasa kimemuua ndugu yetu kwa mujibu wa ripoti iliyotolewa na madaktari baada ya uchunguzi, hivi sasa tunakwenda kujadiliana kuhusu mazishi yake," amesema Kavishe.

Akwilina alifariki dunia Februari 16, 2018 baada ya kupigwa risasi kichwani akiwa kwenye daladala wakati polisi wakiwatawanya waandamanaji ambao ni wafuasi wa Chadema.

Ali Kiba Aamua Kufuata Nyayo za Ben Pol...Atupia Marangi Rangi Kichwani

$
0
0
Imekuwa ni kawaida kwa mastaa mbalimbali Duniani kupenda kubadili mionenakano yao, inawezekana ukawa ni muonekano wa style za mavazi au wakati mwingine inaweza ikawa style za nywele ili tu kuwa tofauti.

Kuna mitindo ya nywele kwa baadhi ya mastaa inayo-trend  ambapo kwa sasa kila mtu anakuja na mtindo wake mwenyewe ili kuleta upekee wa muonekano wake kama ilivyo kwa Ben Pol alikuja na mtindo wa rangi ya nywele za kijani kibichi na imempa dili kibao kutokana na mtindo huo wa rangi.

Staa wa Bongofleva Ali Kiba leo nae ameonekana akiwa miongoni mwa mastaa wa Bongo waliokuja na style mpya wa nywele ambapo ameamua kuweka rangi ya kwenye nywele zake na kuubadili muonekano wake kichwani tofauti na tulivyomzoea.
Viewing all 104795 articles
Browse latest View live




Latest Images