Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104789 articles
Browse latest View live

Hii Hapa Ndinga Analomiliki Samatta Huko Ubelgiji

$
0
0
Hii Hapa Ndinga Analomiliki Samatta Huko Ubelgiji
Moja kati ya majina makubwa katika soka kutokea ukanda wa Afrika Mashariki basi huwezi kuacha kutaja jina la nadhoa wa timu ya taifa ya Tanzania Taifa Stars anayecheza soka la kulipwa katika club ya KRC Genk ya Ubelgiji Mbwana Samatta.

Samatta ni moja kati ya mastaa wa soka ambao hawapendi kuweka mali zao hadharani mara kwa mara lakini leo amepost picha ya gari nyeupe lakini kwa mujibu wa maneno yake aliyoyaandika May 26 2015 katika picha ya Range Rover yake aliyoipost instagram, gari ya leo pia inatajwa kuwa ni lake.

Majaliwa Awapiga Stop Wakandalasi Kuagiza Mabomba Nje ya Nchi Atawa Watumie ya Ndani

$
0
0
Majaliwa Awapiga Stop Wakandalasi Kuagiza Mabomba Nje ya Nchi Atawa Watumie ya Ndani
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amesema hakuna sababu ya wakandarasi wa miradi ya maji kuagiza mabomba nje ya nchi wakati kuna mabomba yanayozalishwa hapa nchi tena kwa ubora hivyo kuwataka watumie ya ndani .

Ameyasema hayo Februari 20  wakati akiweka jiwe la msingi katika kiwanda cha kuzalisha mabomba cha Mwanza Plstics eneo la Nyamhongolo wilayn Ilemela Mwanza.

"Niwatake wakandarasi tuendelee kutumia mabomba ya ndani ili kuendelea kutoa sapoti kwa wawekezaji hawa,"amesema

Kwa kusimamia hilo ameagiza miradi yote ya maji inayotekelezwa katika halamshauri za mkoa huo kuhakikisha mabomba ya maji yananunuliwa katika kiwanda hicho cha mzawa ilmradi kiwango cha mabomba hayo yawe yanapatikana hapo.

"Kuna mradi wa kusambaza maji katikati ya mji wa Sh14 bilion ambao upo hatua za manunuzi, mkurugenzi wa Mwauwasa simamia hilo wakandarasi wanunue mabomba kiwanda hiki," amesema  Waziri

Mkurugenzi Mtendaji wa kiwanda hicho John Charles alisema kiwanda hicho chenye wafanyakazi 15 wazawa wenye ajira za kudumu na watatu kutoka nje ya nchi, kilianza mwaka 2008 kwa kutengeneza plastiki na vikombe.

Amesema wanakabiliwa na uhaba wa umeme wa kutosha kwani unakuwa wakati mwingine unakosa nguvu na miundombinu ya barabara hivyo kuonheza gharama za uzalishaji.

Kutokana na hayo waziri alimwagiza mkurugenzi wa manispaa ya Ilemela John Wanga kuhakikisha maeneo yote ya uwekezaji kuhakikisha miundiombinu yote muhimmu inafika.

Madona Ataka Mwanaye Kuwa Rais wa Malawi

$
0
0
Madona Ataka Mwanaye Kuwa Rais wa Malawi
Nyota wa muziki wa pop nchini Marekani Madonna amesema kuwa mwanawe David Banda atakuwa rais wa Malawi siku zijazo katika ujumbe aliouchapisha katika mtandao wa Twitter akimsifu mvulana huyo mwenye umri wa miaka 12.

Mwanamuziki huyo wa Marekani ana watoto sita ,wanne akiwa aliwahasili kutoka Malawi. Madonna amekuwa na uhusiano mbaya na mamlaka ya taifa hilo la kusini mashariki mwa Afrika.

Mwaka 2013 Malawi ilimshutumu Madonna kwa kutumia ushawishi wake kuwatishia maafisa wa serikali akisisitiza mchango wake kwa taifa hilo mbali na kutaka kupewa heshima.

Meneja wa Madonna aliishutumu serikali ya Malawi kwa kiuwa na chuki dhidi ya shirika la hisani la nyota huyo la Raising Malawi ambalo alilianzisha 2006 mwaka huohuo aliomuasili David.

David Banda ndio mkubwa kati ya watoto hao wanne. Uasili wake ulizua hisia kali miongoni mwa raia kwa kuwa sheria ya Malawi inawataka wazazi waliomchukua mtoto kuishi ndani ya taifa hilo mwaka mmoja kabla ya kuasili mtoto.

Kikwazo hicho kiliondolewa kwa nyota huyo wa muziki ambaye alimwambia Oprah Winfrey wakati huo kwamba hakuna sheria za kuasili ambazo zilikuwa zinadhibiti uasili wa kigeni.

Baada ya kukata rufaa mahakama ya juu ilimpatia haki za kuasili mwanawe wa pili kutoka Malawi Mercy Jame
Baada ya kukata rufaa mahakama ya juu ilimpatia haki za kuasili mwanawe wa pili kutoka Malawi Mercy James.
Mwaka 2009, mahakama ya taifa hilo ilikataa ombi la Madonna la kuasili msichana chini ya sheria kwamba hajaishi katika taifa hilo la Afrika kwa miezi 18 ili kuweza kuasili.

Baada ya kukata rufaa mahakama ya juu ilimpatia haki za kuasili mwanawe wa pili kutoka Malawi Mercy James.

Mwaka uliopita ,Malawi ilimpatia nyota huyo ruhusa nyengine ya kuasili tena na akawa mama wa pacha wa kike Esther na Stella Mwale.

Okwi Aikutanisha Simba na Waarabu Baada ya Kufanikiwa Hatua ya Kwanza

$
0
0
Okwi Aikutanisha Simba na Waarabu Baada ya Kufanikiwa Hatua ya Kwanza
SIMBA imefanikiwa kutinga hatua ya kwanza ya michuano ya Kombe la Shirikisho barani Afrika baada ya jana kupata ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Gendarmarie nchini Djibouti.

Mshambuliaji raia wa Uganda, Emmanuel Okwi, aliifungia Simba bao hilo pekee katika dakika ya 53 na kuifanya Simba sasa kukutana na 'Waarabu' wa Al Masry.

Simba imesonga mbele kwa jumla ya mabao 5-0 kufuatia ushindi wa bao 4-0 walioupata kwenye mchezo wa kwanza uliochezwa jijini Dar es Salaam wiki iliyopita.

Al Masry yenyewe pia imesonga mbele kwa jumla ya mabao 5-1 baada ya jana kubanwa na Green Buffaloes na kutoka sare ya bao 1-1 nchini Zambia.

Katika mchezo wa kwanza uliochezwa Misri, wenyeji walishinda kwa mabao 4-0.

Simba sasa itakuwa na kibarua mbele ya Waarabu hao, katika kuwania kutinga hatua ya makundi ya michuano hiyo.Timu hizo zitakutana kati ya Machi 6, 7 mwaka huu, huku Simba wakianzia nyumbani kabla ya kuwafuata Al Masry wiki mbili baadaye. 

Yanga Leo Ina Kibarua Kigumu Mbele ya St Louis ya Shelisheli

$
0
0
Yanga Leo Ina Kibarua Kigumu Mbele ya St Louis ya Shelisheli
WAWAKILISHI wa Tanzania kwenye michuano ya ligi ya mabingwa Afrika, Yanga leo ina kibarua kigumu mbele ya St Louis ya Shelisheli kwenye mchezo wa marudiano wa michuano hiyo hatua ya awali.

Yanga inawakabili wapinzani wao hao huku wakiwa mbele kwa bao 1-0 kufuatia ushindi walioupata kwenye mchezo wa kwanza jijini Dar es Salaam.

Kocha msaidizi wa Yanga, George Lwandamina, aliiambia Nipashe kutoka Shelisheli kuwa mchezo huo wa leo hautakuwa rahisi lakini wamejipanga na kuwashukia kivingine wapinzani wao hao.

"Tunahitaji ushindi, ndio kitu pekee tulichokifuata huku, hautakuwa mchezo mwepesi kwa sababu kwa namna nilivyowaona wapinzani wetu, si timu ya kuidharau," alisema Lwandamina.

Alisema watajitahidi kucheza soka la kasi ndani ya dakika 20 za kwanza kujaribu kutafuta bao la kuongoza hili kuwapa presha wapinzani wao hao.

Yanga leo haitakuwa na mshambuliaji wake nyota, Obbrey Chirwa, lakini itawategemea nyota wengine, Ibrahim Ajibu na Papy Tshishimbi kuzamisha  jahazi la St Louis.

Meneja wa timu hiyo, Hafidh Saleh, aliambia Nipashe kutoka nchini humo kuwa wachezaji wote walioongozana na timu wapo katika hali nzuri.

Ili kusonga mbele, Yanga inahitaji ushindi wa aina yoyote au sare kwenye mchezo huo wa leo.

Kwenye mchezo wa kwanza kwenye uwanja wa taifa, goli pekee la Yanga lilifungwa na kiungo Juma Mahadhi huku pia mashabiki wakishuhudia Chirwa akikosa penalti. 

Soma Nafasi za Ajira Zilizotangazwa Leo Jumatano

$
0
0

Rais Magufuli Aondoka Leo Kuelekea Uganda kwa Ziara

$
0
0
Rais Magufuli Aondoka Leo Kuelekea Uganda kwa Ziara
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli ameondoka nchini leo kuelekea Uganda kushiriki Mkutano wa siku mbili wa wakuu wa nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki unaofanyika jijini Kampala.


Rais Magufuli ameagana na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda na Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Tanzania (CDF ), Jenerali Venance Mabeyo.

Watu 18 Wapoteza Maisha kwa Ugonjwa wa Kipindupindu Dodoma

$
0
0
Watu 18 Wapoteza Maisha kwa Ugonjwa wa Kipindupindu Dodoma
Watu 18 wamepoteza maisha kutokana na ugonjwa wa kipindupindu mkoani Dodoma ndani ya miezi minne huku zaidi ya watu 470 wakiugua ndani ya muda huo.


Hayo yamethibitishwa na Mganga Mkuu wa Mkoa huo, Dkt. James Kiologwe na kusema ugonjwa huo tangu uingie Dodoma Oktoba mwaka 2017, hadi sasa umesababisha vifo hivyo na idadi hiyo ya wagonjwa.

"Wagonjwa wengi wanatoka katika wilaya za Mpwapwa na Chamwino na miongoni mwa sababu za kuenea kwa ugonjwa huo ni unywaji wa maji ya kwenye madimbwi ambayo si safi na salama. Ugonjwa huu ulianza Oktoba, mwaka jana, katika wilaya zote za mkoa wa Dodoma lakini zaidi katika wilaya hizo mbili", amesema Dkt Kiologwe.

Pamoja na hayo, Dkt. Kilogwe ameendelea kwa kusema "kuna wakati ulipungua, lakini umerudi tena na umekuja kwa kasi sana mwezi huu wa pili hadi juzi kulikuwa na wagonjwa wapya 26 na 22 kati yao waliruhusiwa kurudi nyumbani na wanatoka Mpwapwa na Chamwino".

Kwa upande mwingine, Dkt. Kiologwe amesema wanaendelea na jitihada za kukabiliana na ugonjwa huo kwa kugawa ‘Water Guard’ vidogo 250,000 kwa ajili ya kusafisha maji na kuweka katika vyanzo vya maji huku akiwata wakazi wa mkoa huo kuhakikisha wanachemsha maji ya kunywa na kuzingatia kanuni zote za usafi, ili kuepukana na ugonjwa huo.

Polisi Yapata Kigugumizi Upekuzi Ofisi za Chadema

$
0
0
Polisi Yapata Kigugumizi Upekuzi Ofisi za Chadema
Viongozi wa Jeshi la Polisi wametupitia mpira juu ya taarifa za askari wake kwenda ofisi za makao makuu ya Chadema Mtaa wa Ufipa, Kinondoni jijini Dar es Salaam kwa lengo la kufanya upekuzi.

Wakati Chadema wakidai kuwa askari wa jeshi hilo walikwenda ofisini hapo juzi saa moja usiku kwa lengo la kufanya upekuzi, si Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai (DCI) Robert Boaz; Msemaji wa Jeshi la Polisi, Barnabas Mwakalukwa; wala Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Lazaro Mambosasa aliyekuwa tayari kulizungumzia.

Juzi usiku, Chadema ilitoa taarifa kuhusu tukio hilo ikisema polisi walifika katika ofisi zao wakiwa na magari matano wakijitambulisha kuwa ni kutoka ofisi za upelelezi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam.

Taarifa hiyo ya mkurugenzi wa itifaki, mawasiliano na mambo ya nje, John Mrema ilisema polisi waliwajulisha walinzi kuwa wanataka kufanya upekuzi kwenye ofisi lakini hawakuwa na hati ya upekuzi na hawakufuatana na viongozi wa serikali ya mtaa kama sheria inavyotaka.

“Walinzi wetu waliwakatalia kwa kuwa hawakufuata utaratibu na wala hawakueleza wanataka kupekua nini ndani ya ofisi zetu. Tunalaani kitendo hiki na tunajiuliza ni kwa nini wamekuja usiku na ikiwa ni siku moja tu baada ya polisi kufanya uvamizi kama huo kwa CUF Zanzibar na kufanya upekuzi,” alihoji Mrema.

Alipotafutwa ili kuzungumzia ukweli wa taarifa hiyo ya Chadema, Kamanda Mambosasa alisema, “Sijaletewa taarifa za waliokwenda kwani waliokwenda ni makao makuu wale.”

Msemaji wa jeshi hilo, Mwakalukwa alisema asingeweza kulizungumzia kwa kuwa alikuwa safarini akitokea Kigoma kuelekea Dar es Salaam.

“Ofisi ni taasisi, kuna IGP, DCI na kuna msemaji wa Jeshi la Polisi ambaye ni mimi ila nipo safarini natoka Kigoma na kesho (leo) nitakuwa ofisini. Watafute IGP au DCI,” alisema Mwakalukwa.

DCI Boaz alipopigiwa simu na kuelezwa kuhusu suala hilo alisema apewe muda aulize kwa kuwa halifahamu.

Baada ya muda alipiga simu mwenyewe na kusema, “Masuala ya mikoani yanashughulikiwa na makamanda wa mikoa yao. Jitahidi umpate Mambosasa atakupa taarifa kwa maandishi. Makao makuu tunashughulika na sera na mambo makubwa si madogo madogo kama hayo.”

Waachiwa kwa dhamana

Jana mchana, viongozi wanne kati ya saba wa chama hicho waliripoti Kituo Kikuu cha Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam kuitikia wito wa jeshi hilo, huku wakitoa sababu ya mwenyekiti, Freeman Mbowe; katibu mkuu, Dk Vincent Mashinji; na naibu katibu mkuu (Zanzibar), Salum Mwalimu kushindwa kuripoti.

Walioripoti jana kituoni hapo saa 6:10 mchana na kuachiwa kwa dhamana saa 7:45 mchana kwa dhamana ni, naibu katibu mkuu-Bara, John Mnyika; mwenyekiti wa Baraza la Wanawake la Chadema (Bawacha), Halima Mdee; mwenyekiti wa Kanda ya Serengeti, John Heche; na Esther Matiko ambaye ni mweka hazina wa Bawacha.

Mnyika ambaye pia ni mbunge wa Kibamba akizungumza kwa niaba ya wenzake alisema kupitia wakili wao, Peter Kibatala walipewa dhamana na kutakiwa kuripoti kituoni hapo Februari 27.

Wito wa Polisi kwa viongozi hao, ulitolewa juzi ikiwa ni siku nne kupita tangu kutokea kwa kifo cha Akwilina Akwiline, mwanafunzi wa mwaka wa kwanza wa Chuo cha Taifa cha Usafirishaji (NIT).

Kifo cha Akwilina kinadaiwa kuwa kimetokana na kupigwa risasi na polisi Februari 16 akiwa ndani ya daladala eneo la Mkwajuni, Kinondoni jijini Dar es Salaam wakati polisi wakiwatawanya wafuasi wa Chadema waliokuwa wakienda ofisi za mkurugenzi wa Halmashauri ya Kinondoni kudai viapo vya mawakala wao.

Sababu za Mbowe, Dk Mashinji

Mbowe, Dk Mashinji na Mwalimu hawakufika kuripoti polisi ikielezwa na Mrema ni kutokana na kuwa nje ya Dar es Salaam.

“Mfano, Salum Mwalimu jana alitangulia Mafinga (Iringa) kwa ajili ya kuongoza mazishi ya kiongozi wetu Daniel John hivyo kwa wito tuliopokea asingeweza kufika sawa na mwenyekiti (Mbowe) alikuwa nje ya Dar es Salaam,” alisema Mrema.

Alisema Dk Mashinji wakati wito wa kuripoti polisi ukitolewa alikuwa safarini kwenda Marekani.

Somo la Sumaye kwa viongozi

Mbali na matukio hayo, katika Kanisa Katoliki la Mtakatifu Anna lililoko Hananasif jijini Dar es Salaam, kulifanyika ibada ya kumwombea Daniel John (37) aliyekuwa katibu wa Chadema, Kata ya Hananasif, ambaye mwili wake uliokotwa Coco Beach baada ya kutokweka Februari 11.

John aliyezaliwa Desemba 26, 1980 ameacha watoto wawili na mjane mmoja, Paulina Vitalis na jana mwili wake ulisafirishwa kwenda Mafinga mkoani Iringa kwa mazishi yatakayofanyika leo.

Katika ibada iliyohudhuriwa na viongozi wa Chadema, wanachama na waombolezaji wengine, mwenyekiti wa Kanda ya Pwani wa Chadema na Waziri Mkuu mstaafu, Frederick Sumaye alitoa wito kwa viongozi wa Serikali na dini kuhakikisha wanajenga umoja na kukemea uvunjifu wa amani.

“Haki haitendeki, maumivu yanatokea na tunanyamaza, tunapaswa kutupwa nje na kukanyagwa, Daniel amekuwa chumvi hivyo ametupwa nje. Mungu alitoa na Mungu ametwaa lakini sisi binadamu tunafanya mambo yasiyostahili kama hili lililotokea kwa Daniel,” alisema.

Sumaye alisema, “Katika kupigania haki, kuna wachache watamwaga damu, Daniel ni miongoni mwao na hao hawatarudi, hakuna historia hiyo popote ila damu hiyo itadai siku zote.”

Kuhusu viongozi wa kiroho alisema, “Viongozi wa dini kemeeni, mnapoona kuna ubaya halafu hamsemi, mnabaki kusema hii si siasa, kemeeni ni jukumu letu sote na msipokemea taifa hili linakwenda kubaya.”

Vanessa Mdee Afata Nyayo za Alikiba, Ommy Dimpoz na Ben Pol Naye Abadirisha Rangi ya Nywele

$
0
0
Vanessa Mdee Afata Nyayo za Alikiba, Ommy Dimpoz na Ben Pol
Ben Pol ameonekana kuwavutia wasanii wa Bongo Flava kwa mwaka huu katika staili ya kuweka rangi nywele (breach). Baada ya Alikiba na Ommy Dimpoz kufanya hivyo, Vanessa Mdee ameamua kufuata nyayo hizo.

Vanessa amepost picha tatu katika mtandao wake wa Instagram ambazo zinamuonyesha akiwa katika muonekano wake mpya wa nywele zikiwa na rangi ya karoti.

New Hair Who Dis? @iambenpol najua umefarijika sana 🤣📸 ,” ameandika Vee kwenye moja ya picha alizoziweka kwenye mtandao huo.

Naye Ben Pol amemjibu Vanessa kupitia mtandao huo kwa kuandika, “Happy Faraja Week, naendelea kufarijika tu 😀 @vanessamdee 😍🧡.”

Kocha wa Azam: Michuano Hii ni Migumu Hatutaki Kufanya Makosa

$
0
0
Kocha wa Azam: Michuano Hii ni Migumu Hatutaki Kufanya Makosa

Kocha wa Azam FC  Aristica Cioaba, amesema hataki timu yake ifanye makosa kwenye mchezo wa raundi ya 16 bora ya kombe la shirikisho nchini dhidi ya timu iliyopanda ligi kuu ya KMC.

Mchezo huo ambao unatarajiwa kupigwa jumamosi hii kwenye uwanja wa Azam Complex, Cioaba ameueleza kuwa ni mchezo muhimu kwa timu yake kutokana na timu hiyo kutaka kusonga mbele ya michuano hiyo.

“Hatutaki kufanya makosa na wachezaji wanafahamu michuano hii kuwa ni migumu kama huweki umakini wa kushinda mchezo basi utapata tatizo kwa kuwa ni mchezo mmoja tu na sio kama ligi'', amesema.

Azam FC inayoshika nafasi ya tatu kwenye msimamo wa ligi ilitinga katika hatua hii baada ya kuifunga Shupavu ya Morogoro mabao 5-0. Wakati KMC  iliichapa Toto Africans ya Mwanza mabao 7-0.

KMC ni timu iliyopo chini ya Manispaa ya Kinondoni ya kuanzia msimu ujao itaanza kucheza ligi kuu baada ya kufanikiwa kupanda kutoka ligi daraja la kwanza.

Madiwani Wengine Wawili Wa Chadema Wajiunga na CCM .... Wamtumia Ujumbe Huu Lema

$
0
0
Madiwani Wengine Wawili Wa Chadema Wajiunga na CCM .... Wamtumia Ujumbe Huu Lema

Katibu wa CCM wilaya ya Arusha, Musa Matoroka amewapokea madiwani Prosper Msofe na Obed Meng’oriki wa CHADEMA ambao walitangaza kujivua uanachama jana.

Wawili hao walitoa tangazo jana kwa waandishi wa habari la kujivua uanachama wa CHADEMA na kujiunga na CCM kwa madai kuwa wanataka kuunga mkono jitihada za uongozi wa Rais John Magufuli.

Matoroka ametoa ujumbe kwa Mbunge wa Arusha Mjini Godbless Lema kuwa wamejiandaa kuchukua jimbo hilo hivyo aanze kutafuta kazi nyingine.

Upande wa Mashtaka Watakiwwa Kufuatilia Jalada la Kesi ya Mhasibu Mkuu wa Takukuru

$
0
0
Upande wa Mashtaka Watakiwwa Kufuatilia Jalada la Kesi ya Mhasibu Mkuu wa Takukuru

Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu imeutaka upande wa mashtaka kufuatilia jalada la kesi inayomkabili Mhasibu Mkuu wa (TAKUKURU), Godfrey Gugai anayedaiwa kuwa na utajiri wa mali zenye thamani ya Bilioni 3 ambazo haziendani na kipato chake kwa Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP).

Wakili wa serikali Vitalis Peter amemueleza Hakimu Mkazi Mkuu, Thomas Simba kuwa kesi hiyo imeitishwa kwa ajili ya kutajwa na kwamba jalada bado lipo kwa (DPP) kwa ajili ya kulipitia na kulitolea maamuzi.

Baada ya kusema hayo Hakimu Simba amesema kesi hiyo sio suala la upande wa mashtaka kuamua wanavyotaka na kwamba hataki kesi hiyo ifike miaka mitatu kama kesi nyingine zilizopo.

“Hakikisheni upelelezi unakamilika haraka kesi hii isichukue muda mrefu kama nyingine kwani jamii inajua Mahakama ndio inachelewesha kesi” -Hakimu Simba

Hakimu Simba aliutaka upande wa mashtaka wakati ujao wawe na lugha inayoeleweka la sivyo kuna kitu atakifanya na wakae wakijua washtakiwa wapo ndani.

Naye Wakili wa utetezi Alex Mgongolwa amedai hawajaenda mahakamani kutembea na kuiomba mahakama iamuru upande wa mashtaka kutekeleza majukumu yao na haki iweze kutendeka.

Awali  jalada hilo lilipelekwa kwa DPP ambapo alilipitia na kulirejesha TAKUKURU na kuelekeza baadhi ya maeneo yafanyiwe uchunguzi zaidi.

Hakimu Simba aliiahirisha kesi hiyo hadi March 6,2018 na kuutaka upande wa mashtaka uhakikishe wanalifanyia kazi jalada hilo.

Mbali na Gugai, washtakiwa wengine katika kesi hiyo ni George Makaranga, Leonard Aloys na Yasini Katera.

Washtakiwa hao wanaokabiliwa na mashtaka 43 yakiwemo 20 ya utakatishaji fedha haramu, kumiliki mali zisizoendana na kipato na kughushi mikataba ya mauziano ya viwanja katika maeneo mbalimbali.

Mtanzania Akamatwa Nairobi na Dhahabu ya Dola Milioni Moja

$
0
0
Mtanzania Akamatwa Nairobi na Dhahabu ya Dola Milioni Moja

Maafisa wa forodha nchini Kenya wamemkamata mwanamume anayedaiwa kuwa raia wa Tanzania katika uwanja wa kimataifa wa ndege wa Jomo Kenyatta, Nairobi akisafirisha dhahabu ya thamani ya dola milioni moja, taarifa zinasema.

Mwanamume huyo mwenye umri wa miaka 46 anadaiwa kuwasili kutoka Mwanza, Tanzania kupitia uwanja wa Kilimanjaro na alikuwa safarini kuelekea Dubai.

Mahakama Yamfutia Kesi ya Madai Uhuru Kenyatta

$
0
0
Mahakama Yamfutia Kesi ya Madai Uhuru Kenyatta
Mahakama Kuu Jumanne iliamua kwamba mashtaka ya uhalifu au madai hayawezi kufunguliwa dhidi ya Rais juu ya utendaji wake wa kazi katika kipindi ambacho alikuwa madarakani.

Kutokana na msingi huo wa kisheria Jaji Chacha Mwita aliliondoa jina la Rais Uhuru Kenyatta kutoka kwenye kesi iliyofunguliwa na mwanaharakati Okiya Omtatah akipinga uamuzi wake wa kuteua makatibu wakuu na makatibu tawala.

Ingawa Jaji Mwita hakutoa sababu za kuliondoa jina la Rais Kenyatta kutoka kwenye kesi, kwa namna fulani ni kama alikubaliana na maoni ya Mwanasheria Mkuu kwamba Rais ana kinga ya kutoshtakiwa.

"Kwa maoni yangu, jina la Rais halipaswi kuwemo katika ombi hili. Nitaeleza sababu katika hukumu ya mwisho," alisema kwa ufupi.

Mwanasheria mkuu kupitia mwanasheria mwandamizi Jennifer Gitiri, aliomba mashtaka hayo yafutwe na kuondolewa kwa jina la Rais Kenyatta katika suala linalojadiliwa kwamba ni kinyume cha katiba kuanzisha mashtaka yoyote dhidi ya Mkuu wa Serikali.

"Tunasisitiza kwamba rais hawezi kushtakiwa kwani anafurahia kinga ya rais," aliongeza.

Gitiri alimwambia Jaji Chacha kuwa hakuna ulazima kwa Rais Kenyatta kuingizwa katika suala hili kwa kuwa AG ana uwezo wa kuiwakilisha serikali ya kitaifa katika madai yoyote.

"Maombi hayatapata pigo lolote ikiwa jina la Rais Kenyatta litaondolewa katika kesi hii," aliongeza.

Bunge kupitia kwa mwanasheria Mbarak Awadh Ahmed alijihusisha na mjibu maombi mwanasheria mkuu kwamba amewasilisha maombi ya kutafuta kupinga mamlaka ya mahakama kusikiliza kesi iliyofunguliwa na Omtatah.

Kikundi cha vijana, kilichodai kina maslahi katika kesi hiyo kilimwambia Jaji Mwita kuwa chini ya sheria ya kimataifa, rais aliyeko madarakani, wakuu wa serikali na mabalozi wana kinga ya kutoshtakiwa.

Katika kesi hiyo, Omtatah aliwashtaki Rais Kenyatta, Tume ya Utumishi wa Umma, Mwanasheria Mkuu na Spika wa Bunge juu ya uteuzi wa Baraza la Mawaziri.

Maskini Mguu wa Mtoto Wanasa Kwenye Ngazi za Umeme Airport

$
0
0
Maskini Mguu wa Mtoto Wanasa Kwenye Ngazi za Umeme Airport
Mtoto Julian ambaye mguu wake ulinaswa kwenye ngazi za umeme kwenye uwanja wa ndege wa Vancouver, Canada. Mama yake, Andrea Diaczok, ametoa wito kwa wazazi kuwa macho na watoto wao katika sehemu hizo.

MTOTO Julian mwenye umri wa miaka miwili alijikuta akivunjwa mifupa ya mguu wake uliponasa kwenye ngazi za umeme katika kiwanja cha ndege cha Vancouver, Canada.


Kiatu cha Julian kikiwa katika mashine za ngazi za umeme kilipokuwa kimenasa.

Julian alikuwa na wazazi wake, Andrea Diaczok, mama yake,  na baba yake, Jeff Lee walikuwa wakirejea mjini Calgary wiki iliyopita kutokea Vancouver.  Mguu wa mtoto huyo ulikwama pembeni kati ya ngazi na vyuma vinavyozungusha mikanda inayopandisha abiria.


Julian akiwa amelazwa hospitali akipatiwa matibabu, kinyume na woga wa wazazi wake ambao walifikiri huenda mguu wake ungekatwa.

“Mguu wake ulipotea kabisa kwenye mkanda unaozunguka,” Diaczok, alisema na kuongeza kwamba kuona hivyo alipiga kelele kwa nguvu.


Wazazi wa Julian wakifurahi naye baada ya matibabu ya mguu wake ambayo yalichukua wiki kadhaa.

“Mtambo huo uliukunja mguu wake na kuvunja mifupa ya mguu ambapo kiatu chake kilipotelea ndani ya mkanda huo wenye kuzunguka,” alisema.

Kiatu cha Julian kilikuwa kimebanwa kwenye mkanda huo na ilibidi wafanyakazi wa uwanjani hapo na wapita njia kumng’oa mahali hapo aliponasa.

Diaczok na Lee ambao ni wafanyakazi katika fani ya afya, walikuwa wamejitayarisha kwamba mwanao angekatwa mguu. Hata hivyo, madhara hayakuwa makubwa sana, kwani mbali na mifupa iliyokuwa imevunjika na miteguko kadhaa, madaktari waliweza kuhakikisha mtoto huyo anapata matibabu ambayo hayakuwalazimisha kuukata mguu huo.

Kutana na Mtabibu Mwenye KUBRI kutoka kwa ALLAH issa simba Mtabibu wa Nyota za Binadamu na Kutumia Vitabu vya QUR-AN

$
0
0
Kutana na Mtabibu Mwenye KUBRI kutoka kwa ALLAH issa simba said Mtabibu wa Nyota za Binadamu   Africa Mwenye UWEZO Kubaini tatizo lako Pindi tu Utakapo Fanya Mawasilino Kupitia Wasaa Husika..

JE UNASUMBULIWA NA Mapenzi? (Umeachwa na Umpendae,Awe Mume,Mke na Bado unampenda?Na Umejaribu Sehemu nyingi Bila Mafanikio?Wasilina na Maalim Hussein Ujione muujiza wa Papo kwa Papo.. anauwezo WA KURUDISHA MAHUSIANO NA KUIMARISHA NDOA YAKO . Umekimbiwa na Mumeo,mkeo au Mpenzi na anaishi na mtu mwingine? Muone akutatulie Anauwezo wa Hali ya Juu wa Kusambalatisha Mahusiano yao Endapo utafata Atakacho kuelekeza.
Atamfanya Atimize Ahadi zote kwa Muda Mfupi.

Issa simba said Anatumia Jina la Muhusika au Picha Kumaliza Tatizo lako..
Anatibu kwa Kutumia Vitabu vya QUR-AN .Anatafsiri Ndoto. Kushinda BAHATI NASIBU, KUSAFISHA NYOTA. Mvuto wa Mwili na BIASHARA, Kinga ya Mwili,ZINDIKO za Nyumba.MIGUU Kufa GANZI.Kufungua KIZAZI kwa wale walio fungwa kwa njia za KISHIRIKINA.

Anakupa Jini la Mali kwa yule anaehitaji Utajiri BILA MASHARTI.  Humaliza Kesi zilishindika ndani ya siku 14 tu..na mengi zaidi

+255 622588038au 0679119679 au +255 764318107

Rais Magufuli Awasili Uganda Afanya Mazungumzo na Museveni

$
0
0
Rais Magufuli Awasili Uganda Afanya Mazungumzo na Museveni
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana na mwenyeji wake Rais wa Uganda Mheshimiwa Yoweri Museveni mara baada ya kuwasili katika Ikulu ya Entebe nchini Uganda.


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na mwenyeji wake Rais wa Uganda Mheshimiwa Yoweri Museveni kabla ya kuanza mazungumzo yao katika Ikulu ya Entebe nchini Uganda.


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na ujumbe wake katika Mazungumzo na Rais wa Uganda Mheshimiwa Yoweri Museveni katika Ikulu ya Entebe nchini Uganda.


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiwasili katika Uwanja wa Ndege wa Entebe nchini Uganda ambapo pamoja na mambo mengine atahudhuria vikao vya Wakuu wa nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki vitakavyoanza kesho jijini Kampala nchini Uganda.

Rais Magufuli leo amewasili nchini Uganda kushiriki mkutano wa siku 2 wa wakuu wa nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki utaofanyika tarehe 23/02/2018

Kesho atahudhuria mkutano maalumu katika ngazi ya wakuu wa nchi unaohusu maswala ya miundombinu na afya

Kibenteni cha Kenya Chajitokeza Kumfuta Machozi Zari Baada ya Kutangaza Kumwacha Diamond

$
0
0
Kibenteni cha Kenya Chajitokeza Kumfuta Machozi Zari Baada ya Kutangaza Kumwacha Diamond
Msanii wa muziki wa Injili kutoka nchini Kenya, Ringtone Apoko ameweka wasi mipango yake ya kutoka kuwa katika mahusiano na Zari The Boss Lady.

Maamuzi ya msanii huyo yanakuja ikiwa ni siku kadhaa zimepita tangu Zari kutangaza kuachana na Diamond. Kupitia mtandao wa Instagram Ringtone Apoko ameeleza kuwa Diamond hawezi kumuhudumia Zari kwani mrembo huyo anamuhitaji mtu kama yeye.

“Zari Hassan needs a man to lead her to church and to Christ. Diamond can’t offer such. Naomba namba yake Zari inbox me asap if you have it. MWANAMME NI YULE ANAJUA YESU NA MALI ANAYO NA WAKO WENGI HAPA KENYA. By the way wakisii hawananga shida bibi akija na watoto” ameandika.

Bajeti ya Mazishi ya Akwilina Yakubaliwa na Serikali Lakini si Kutoa Fedha

$
0
0
Bajeti ya Mazishi ya Akwilina Yakubaliwa na Serikali Lakini si Kutoa Fedha
Familia ya marehemu  Akwilina Akwiline inaendelea na maandalizi ya mazishi, huku ikielezwa kuwa Serikali imekubali kuyagharimia lakini si kutoa fedha.

Serikali imefikia hatua hiyo baada ya jana Februari 20,2018 familia ya Akwilina kueleza kuwa bajeti ya mazishi ni Sh80 milioni.

Katibu wa kamati ya mazishi Moi Kiyeyeu, ambaye ni kaka wa Akwilina amesema Serikali imewajibu kuwa haitawapa fedha taslim bali itagharimia vitu vilioorodheshwa katika bajeti ya mazishi hayo.

"Tulipotoa bajeti hatukuwa na maana kuishinikiza Serikali itoe fedha zote bali ilikuwa mahitaji ya msiba hadi pale utakapoisha. Tunashukuru Mungu kwa Serikali kuridhia kugharimia," amesema Kiyeyeu.

Kuhusu hilo, Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia katika taarifa iliyotolewa leo Februari 21,2018  imesema kupitia kwa Katibu Mkuu wake, Dk Leonard Akwilapo ilipokea makisio ya gharama za mazishi ya Sh80 milioni kutoka kwa msemaji wa familia, Festo Kavishe.

Mkuu wa kitengo cha mawasiliano cha wizara hiyo, Mwasu Sware alisema baada ya kupokea makisio hayo Dk Akwilapo alitahadharisha kuwa kuna baadhi ya matumizi hayatakubaliwa kwa kuwa kisheria hayagharamiwi na Serikali.

Pia, katika makisio hayo kuna gharama ambazo zilikuwa zimepewa makadirio ya juu.

Alisema katibu mkuu aliagiza kuwe na kikao kati ya wizara na ndugu wa marehemu ili kuweka sawa changamoto hizo na kuwa na bajeti ya pamoja ambacho kilifanyika jana jioni Februari 20,2018 na kufikia muafaka.

“Wizara inapenda kuufahamisha umma kuwa taratibu nyingine za maandalizi ya mazishi zinaendelea vizuri,” amesema.

Wakati huohuo, Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dk Harrison Mwakyembe amefika nyumbani kwa dada wa marehemu Mbezi Luis kuhani msiba.

Dk Mwakyembe amesema tukio la kifo cha Akwilina ni la kusikitisha.

Viewing all 104789 articles
Browse latest View live




Latest Images