Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104793 articles
Browse latest View live

Haji Manara Afunguka Baada ya Simba Kupigwa Out “Tunarudi Nyumbani Tukiacha Heshma Kubwa ya Klabu na Nchi”

$
0
0
Baada ya wekundu wa msimbazi Simba kutolewa katika mashindano ya Kombe la Shirikisho Barani Afrika na timu ya Al Masry huku wakitoka sare ya 0 – 0 nchini Misri, afisa habari wa klabu hiyo, Haji Manara amesema kuwa timu yake imefanya kila kitu lakini mwisho wa siku mpangaji ni Mungu hata hivyo wanarejea nyumbani wakiwa wameacha heshima kubwa.

Tumefanya tuliyojaaliwa lakini mpangaji wa kila kitu ni Manani…jitihada hazishindi kudra..tunarudi nyumbani tukiacha heshma kubwa ya klabu na nchi kwa ujumla Misri…sasa nguvu yetu ipo ktk VPL…..Asante kwa dua na Sala zenu..Bravo SSC

Mnyama Simba SC atolewa kiume na Waarabu wa Misri



Simba SC imeyaaga mashindano hayo kwa jumla ya mabao 2 – 2 waliyofungwa hapa nyumbani katika uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.


Kupunguza Uzito na Miiko Yake, Pata Dawa Zitakazo Saidia Upungue Mwili Kwa Haraka Bila Madhara

$
0
0

Kama ilivyo katika shughuli nyingine za kibinadamu zenye mpangilio maalum, kupunguza uzito uliozidi lazima uende sambamba na do’s na dont’s zake yaani fanywa na siofanywa. Fanywa/do’s

Jitambue na kubali kwamba unaugua unene na ili kujitibu ni lazima kuwa na adabu katika matibabu hayo. Tambua kwamba vyakula vyoote ni vizuri ILA kula vilivyo rafiki na salama kwa zoezi lako la kupunguza uzito. Tambua kiwango cha chakula unachokihitaji na ule kwa usahihi Tambua muda sahihi unaotakiwa kula na ule kwa wakati

MUHIMU(DONT’S/VISIVYOFANYWA)

Unapopunguza uzito ni kuwa unapunguza mafuta na tindikali ya ziada vilivyorundikana mwilini mwako kwahiyo ni lazima kula milo sahihi inayokuepusha kuongeza mafuta zaidi lakini pia kutouongezea mwili vyakula vyenye kuutengenezea asidi au tindikali nyingi. Hivyo ni vyema kuzingatia kiasi cha chakula kwasababu kuwa mnene unamaanisha unanguvu mwili nyingi usizozihitaji zimejirundika mwilini na mwili umezigeuza mafuta ndio hayo manyama uzembe.

Unatakiwa kupangilia ulaji ili uruhusu mwili kusaga kidogo ulichokula, lakini nguvu nyingine (kalori au calories) uzipate kutoka kwenye mafuta yaleee manyama uzembe. Kana utakula kwa kiwango kikubwa, mwili utakitumia hicho ulichokula tu na kama kitakuwa kingi kuliko kinachohitajika, kitageuzwa mafuta na kuongeza manyama uzembe.

Ni lazima kula kwa muda maalum kwa sababu tunakula ili mwili upate nguvu ya kujiendesha baada ya kukisaga chakula hicho. Ikiwa utakula chakula kingi na kutulia au kulala muda mfupi baadae, unajiumiza kwasababu mwili unapo’relax hauhitaji nguvu nyingi kwahiyo utakigeuza chakula hicho mafuta na hapo tunamaanisha tunapata tena nyongeza ya manyama uzembe. KWAHIYO? Tujitahidi kula milo sahihi, kwa wakati sahihi na kiwango sawia.

KWANINI UNAHITAJI BIDHAA ZETU?

Bidhaa zetu zinavirutubishwa vyoote muhimu vinavyozingatia mlo sahihi, muda muafaka na kiwango sawia. Zaidi huwezi kuzilinganisha bidhaa zetu na hizo nyingine za kichina unazozisikia huko mitaani kwasababu:-

Za kwetu hazina kemikali kwahiyo hizi sio “weka mbali na watoto” maana ni salama kwa watu wote katika familia hata wa kundi dhaifu la watoto, wazee, wajawazito na wanaonyonyesha. Zimethibitishwa na zimeruhusiwa kuwa salama na shirika la viwango duniani ISO, zinatambuliwa kuwa zinafaa kwa dini zote na kupewa ubora wa viwango na HALAL, na hapa kwetu vina kibali cha TFDA.

Sio zile zinazoingizwa kimyakimya kwenye mabegi hatimaye zinawaumiza na kuwatia ubovu na madhara ya kudumu ya miili. Bidhaa zetu huingizwa bila kificho na zinalipiwa kodi zote na zina vibali.

Wa Dar es salaam unaweza kufika ofisini Masaki, au ukituma pesa kabla ya saa 8 mchana utaletewa ulipo. Wateja wa mikoani unatuma pesa kabla ya saa kumi unatumiwa mzigo kwenye basi utakayoelekeza wewe, na wa Zanzibar unatumiwa kwenye boti zenye uhakika, wa nje ya Tanzania tunajadiliana juu courier unayoiamini.



Nipo active muda na saa yoyote kukuhudumia, karibu.

Piga au WhatsApp +255783566844
M
na kutufuata @afyayanguutajiriwangu_ayuw

Facebook: Kwambiwa Nelly Machenje


Youtube : afyayanguutajiriwangu

Hii ndiyo Chocolate ya Gharama zaidi Duniani

$
0
0
Basi jana March 16, 2018 chocolate inayodaiwa kuwa ya gharama ya juu zaidi duniani ilipelekwa kwenye maonyesho ya biashara kwenye Mji wa Obidos nchini Ureno.

Chocolate hiyo ambayo ni ya gharama ya Euro 7,728 ambayo ni sawa na Fedha za Kitanzania Shilingi Milioni 20.7, imefunikwa na dhahabu inayoweza kuliwa, na imetengenezwa na vitu vingine ikiwa ni pamoja na truffle nyeupe, nyuzinyuzi za saffron, na vanilla kutoka Visiwa vya Madagascar.

Mtengenezaji wa chocolate hiyo Daniel Gomes ambaye ni raia wa Ureno ameeleza kuwa chocolate hiyo ambayo ina umbo la fedha imepewa cheti cha kutambuliwa kama Chocolate ya gharama ya juu zaidi duniani na Kitabu cha Kumbukumbu cha Guiness mwaka 2017.

Dalili 6 Zitakazokuonyesha Kuwa Mwenzi Wako Ana Mtu mwingine Katika Mahusiano

$
0
0
Mahusiano yoyote yale huhitaji mtu mwenye uvumilivu, imara, mkweli na muwazi lakini hivi vyote vikishindikana basi, mahusiano hayo huingia doa.

Watu kuwa na wapenzi wawili wawili huenda ikawa sijambo geni, lakini ni jambo geni pale mwezi wako akilifanya.

Matatizo haya yamekuwepo kwa miaka mingi, lakini sidhani kama yatakuja kuzoeleka, maana kila mmoja hapa anahitaji upendo wa dhati na wakwake tuu, usio na kugawana na mtu mwingine.

Vitabu vya dini vinasisitiza upendo ulio mmoja katika mahusiano yaliyohalalishwa na Mwenyezi Mungu mwenyewe, 'tuliheshimu hili'.

Katika makala hii inayolenga kukuonyesha dalili za mwenzi wako kutoka nje ya mahusiano, kwa kiasi kikubwa itakusaidia wewe kuwa sehemu sahihi.

Dalili 6 zitakazokuonyesha kuwa mpenzi wako anamahusiano nje ya ndoa au urafiki wenu.

1. Mmekuwa wawazi kwa muda sasa, yani mwenzi wako amekuwa akishea na wewe mambo mbalimbali ya siku nzima, ghafla anaanza kuchelewa kurudi kutoka kazini, na akirudi hakuambii alikuwa wapi.

2. Umekuwa ukikaribishwa kumtembelea kazini kwake, lakini siku hizi anatengeneza sababu nyingi za kukuweka mbali na maeneo ya kazini kwake kabisaa.

3. Siku moja unapanda katika gari ya mkeo au mmeo alafu unataka kufungua kile kibox kilichopo pale mbele ambacho huwa kinatumika kuhifadhia vitu mbali mbali, mara unakuta kimefungwa kabisa na mwenzi wako anagoma kukifungua.

4. Ghafla mkeo/mme anaanza kujifungia bafuni anapokwenda kuoga, na hakuwa anafanya hivyo, je huenda akawa anatumia muda huo kuwasiliana na mtu mwingine kwa njia ya maandishi?

5. Mke/mme wako ana mikutano au mitoko na marafiki na kumbuka kukuhusu sehemu wanayokwenda inautata, mfano disco, bar usiku alafu hakuambii n.k.

6. Mpenzi wako anageuka kuwa msiri katika mambo yake, yani anakuficha nywila/passwod ya simu au laptop yake, tofauti na mwanzoni alikuwa anakuweka wazi.

Hayo na mengine mengi yanaweza kukufanya ukaona kuwa ni sehemu kubwa ya kuwa mumeo/mkeo anamahusiano na mtu mwingine nje ya mahusiano yenu.

Angalizo: Dalili zote hizo 6 huenda mpenzi wako akawanazo baadhi tu, kwa mfano kuchelewa kazini, usiri wa kazini n.k hii aimaanishi tu ni msaliti wa mapenzi, hapana wakati mwingine ziko sababu za msingi zinazo msababisha yeye kufanya hivyo na sio kuchepuka

Download Application ya Udaku Special kwenye Simu yako Kama Bado Hujadownload

$
0
0
Download Application ya Udaku Special kwenye Simu yako Kama Bado Hujadownload


DOWNLOAD HAPA
 


UPDATE HAPA

Shkamoo Tshishimbi....Miguu iliyofunga Ndoa na Mpira

$
0
0
Fundi wa mpira. Mpaka rangi bora wa soka kwa muda huu. Kichaa wa soka kwenye kumiliki. Mkongo mwenye miguu iliyofunga ndoa na mpira. Akili kubwa kwenye dunia ya soka letu la afrika mashariki na kati.

Endelea kubishana kwa sababu hujamshuhudia au una kiburi . Ni mara chache sana mwanasoka kupendwa au kukubalika na pande mbili zote yaani Simba na Yanga.



Iliwatokea wachache sana. Kama Said Mwamba ‘Kizota’. Alipendwa na wana Yanga. Akakubalika kwa wana Simba. Kwamba huyu mtu ni fundi. Said alikuwa kama Juma Nature wa soka kwa wakati ule.



Ndivyo ilivyokuwa kwa kina Method Mogela. Hamis Gaga. Edibily Lunyamila na Juma Kaseja. Achana na Sunday Manara. Pamoja na upinzani mkali uliopo kwa timu hizi mbili. Marehemu Ben Luoga alikubalika kote kote. Simba walimpenda. Yanga wakamuhusudu.



Uchawi na ustaarabu kama siyo uhuni wa miguu yao. Ilikuwa chanzo cha kupendwa na kukubalika na kila pande za mashabiki wa timu hizi za Kariakoo. Walikuwa zaidi ya viingilio vilivyotolewa pale shamba la bibi.



‘Boban Mawela’ Haruna Moshi. Jibu utakalopewa na mashabiki wa Simba kuhusu uwezo wake. Litakuwa Kulwa. Na jibu utakalopewa na mashabiki wa Yanga kuhusu ufundi wake litakuwa Doto.



Yatafanana tu kwa kila kitu. Kuna uwezo wa soka wa mtu unamfanya hata shabiki wa timu pinzani ahusudu. Aheshimu na kumkubali mchezaji husika. Hakuna shabiki wa Manchester United aliyepinga uwezo wa Thierry Henry wa Arsenal katika ubora wake.



Kwa sasa hivi kuna mtu mmoja tu kwenye ligi kuu Tamzania Bara. Papy Kabamba Tshishimbi. Mkongomani huyu. Fundi wa mpira. Wakili halisi wa soka. Shahidi namba moja wa nini anatakiwa kufanya kiungo uwanjani.



Achana na blabla za wasemaji wa timu hizi. Huyu Tshishimbi siyo wa dunia hii. Ukimuangalia ni muunganiko wa Kizota Method na Gaga. Utaona robo ya ufundi wa Kizota. Robo ya ufundi wa Gaga na robo ya ufundi wa Method. Anajua sana huyu raia wa Kongo.



Ogopa sana mchezaji ambaye mashabiki wa timu pinzani wanatamani ashike mpira ili wafaidi ufundi wake. Anavutia kumtazama akichezea mpira kuliko ushindi wa timu yako.

Wakati Yanga wanaogopa Okwi asimiliki mpira kwa sababu atawaumiza muda wowote. Kuna kundi la mashabiki wa Simba litatamani Tshishimbi achukue mpira ili wafaidi kipaji halisi cha soka.



Haji Manara anakiri kuwa Tshishimbi ni mashine. Ndivyo ambavyo mashabiki wa simba sura zao zinadhihirisha kukubaliana na uwezo wa Tshishimbi. Jamaa anajua mpaka anakera.

Yanga wanaweza kuelemewa timu nzima. Lakini utamuona Tshishimbi tu uwanjani. Akipora mipira. Akigawa mpira. Akiomba pasi. Akiziba nafasi.



Hii siyo Bongo tu. Hata Ulaya mashabiki hukubali uwezo wa mchezaji wa timu pinzani. 2003 Old Trafford yote ilisimama kumpigia makofi mkongwe katika soka Ronaldo Nazario Luis De Lima.

Baada ya guu lake la kulia kutupia kambani goli tatu ndani ya dakika chache. Akimuacha Bathez na upara wake akilambalamba midomo kama zuzu. Ferguson akipata kigugumizi cha kutafuna jojo zake.



Ndivyo ilivyokuwa kwa Ronaldinho pale Saintiago Bernabue. Baada ya kuwalaza na viatu mastaa wenye ustaa halisi wa Real Madrid. Wakati akitoka uwanjani majukwaa yote yalisikika makofi.

Heshima hii ya mashabiki kusimama majukwaani na kumpigia makofi mchezaji wa timu pinzani. Kwa hapa Bongo huo utamaduni umetuacha mbali sana. Haiwezi kutokea. Ila moyoni wataishia kukubaliana na hali halisi.



Kuna wakati unamtazama Tshishimbi. Unaona kama anawaonea wenzake au amelazimishwa kucheza nao. Anatuliza mpira tofauti na wenzake. Anapiga pasi tofauti na wenzake. Na hata namna anavyogeuka kutazama wapi apeleke mpira ni tofauti sana.

Ufundi huu ulikuwepo nyakati za kina Hussein Aman Masha. Marehemu James Tungaraza na kina Steven Mussa. Hawa ndiyo waliyokuwa wakifanya anayoyafanya Tshishimbi wa leo.



Lakini hawa wengine wanaopambwa kwenye vyombo vya habari. Ni wachezaji sawa. Lakini kwa Tshishimbi wa sasa ni kama mtende kuota katika ya Jangwa. Anaonekana peke yake uwanja mzima.

Naam hayo yalikuwa mawazo ya dk Levy

Mrembo Tunda Atema Cheche, Skendo ya Kuchoropoa Mimba Nane za Wanaume Tofaut

$
0
0
Baada ya kusambaa kwa skendo ya kudaiwa kuchoropoa mimba takriban nane, muuza nyago maarufu Bongo, Tunda Sabasita amezungumza na Risasi Jumamosi na kuanika ukweli wa mambo.

Mrembo huyo ambaye amekuwa gumzo siku za hivi karibuni kutokana na kudaiwa kuwa na msururu wa wanaume, ameibuliwa skendo hiyo ya kuchoropoa mimba baada ya kusambaa kwa picha yake mpya inayomuonesha kama ni mjamzito.



ETI NI NDANI YA MIAKA MICHACHE TU
Madai hayo mazito yaliyoporomoshwa mtandaoni, mbali na kutaja idadi hiyo ya kutisha, yalizidi kumtafuna mrembo huyo kwa kudai amefanya matukio hayo yote ndani ya miaka michache iliyopita.


HUYU HAPA TUNDA
Akizungumza na Risasi Jumamosi katika mahojiano hayo maalum, Tunda alisema anashangazwa na madai hayo kwa sababu katika hali ya kawaida mtu huwezi kuchoropoa idadi hiyo ya mimba na bado ukaendelea kufanya shughuli zako kama kawaida.
Alisema katika hali ya kawaida, si rahisi kabisa kwani kama kweli angefanya hivyo, lazima angepata madhara na hata afya yake ingezorota.

“Jamani kweli mtu unaweza kuchoropoa mimba nane tena ndani ya kipindi kifupi? Sidhani kama unaweza ukawa binadamu sahihi kabisa na binafsi sijawahi kutoa mimba kama watu wanavyodai,” alisema Tunda.

 TUMBO LAKE NDO LILIVYO
Mrembo huyo aliendelea kusema kuwa watu wanaweza kumsema hivyo kutokana na tumbo lake lilivyo kwani mara nyingi akifanya mazoezi linapungua, akiacha linakuwa kubwa na watu kudhani ana mimba.

“Hili tumbo wanaweza kulishangaa lakini ni kwamba liko hivyo siku zote kama sijafanya mazoezi muda mrefu na pia sijinyimi kwenye kula chakula kabisa, linakuwa kubwa utadhani nina mimba kumbe walaa,” alisema Tunda ambaye ameuza nyago kwenye video ya Wimbo wa Why Me ya Amini Mwinyimkuu na Elias Barnaba.

Tunda aliongeza kuwa, watu wengi wanamtabiria ana ujauzito kitu ambacho sio kweli kwani hajawahi kushika mimba hata ya kusingiziwa.
“Mimi napenda tu watu wafahamu kuwa sijawahi kushika mimba ya mtu yeyote kama wanavyosema siku zote na wala sijawahi kutoa maana tumbo langu ndivyo lilivyo,” alisema Tunda.

AMTEMA DIAMOND
Alipoulizwa kuhusu uhusiano wake na mkali wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ na kama ana mpango wa kuzaa naye, Tunda alisema kwa sasa hataki kumuongelea kabisa staa huyo.
“Huyo Diamond naomba nisimuongelee kabisa. Sitaki kuhusishwa naye kwa namna yoyote ile,” alisema Tunda.


Young D na Tunda.
AGUSIA MSURURU WAKE
Mbali na Diamond, kwenye mahojiano hayo, Tunda pia aliugusia msururu wa wanaume anaotajwa kubanjuka nao penzini akiwemo David Genzi ‘Young D’ na Kinjekitile Mwiru ‘Kinje’.
“Wengine wote ni zilipendwa. Na kwenye maisha kila mtu anapitia mambo mbalimbali ila kwa sasa wote siko nao,” alisema Tunda.



AMUANIKA MTU WAKE
Kama hiyo haitoshi, katika kuonesha kwamba kwa sasa yupo ‘serious’ katika mahusiano, Tunda alimuanika mtu anayetembea naye kwa sasa akidai ni mtangazaji wa Clouds TV, Casto Dickson.
“Kwa sasa mtu wangu ni Cast na hayo maneno mengine sitaki kabisa kuyasikia jamani. Huyu ndiye ninayetarajia kuzaa naye. Nipo na maisha mengine kabisa kwa sasa,” alisema Tunda.

Diamond 'Wema Sepetu Ndio Mwanamke Pekee Aliyekuwa Akiniliza Wengine Nilipita tu'

$
0
0

Diamond amesema hayo alivyokua anafanyiwa interview huko Kenya alipoenda Kuzindua album yake ya 'A boy from Tandale'

Kua amethibitisha Zari amemuacha tarehe 14 February 2018 ila mwanamke aliyempenda haswaaa na kufanya alie ni Wema haswa pale alipokua anamfanyia vituko na visa ktk mahusiano yao.

Kuna muda alikua akiwa na wema anahis yuko peponi haswaaa!!japo kwa sasa they are not together anymore zaidi ya urafiki tu na kabla ya kuachana na Wema hakutegemea kama angeweza kuishi bila Wema Sepetu na ilimchukua muda kumsahau Wema so kwa muda wa miaka minne waliyoachana wala hana mapenzi na Wema zaidi ya urafiki na atakua host wa Wasafi Media.

Kwa sasa yuko busy kutangaza album yake mapenzi baadae!

Hayo ndo ya Diamond na Zari,Diamond na Wema (wote wapo single)mliokua mnammendea Zarina the time is now sasa Dogo kashatemwa nendeni mkamlee mama watano!       


Wakili wa Mwanafunzi Abdul Nondo, anayeendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Afunguka Tena Kunyimwa Kuonana na Mteja Wake

$
0
0

Wakili wa Mwanafunzi Abdul Nondo, anayeendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi kwa upelelezi kufuatia madai ya kutekwa, amesema mpaka sasa amefanya kila jitihada za kumuona mteja wake pasipo mafanikio.

"Kwa jitihada nilizofanya hadi sasa kumuona Abdul Nondo hazijazaa matunda. Hayupo vituo vikuu vyote, tukutane Mahakama Kuu kupitia Habeus Corpus watamleta wenyewe!" amesema Wakili Jebra Kambole.

Kauli hii ameitoa tena kufuatia Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dar, Lazaro Mambosasa kusema taarifa za Wakili huyo kuwa amezuiwa kumuona kijana huyo ni za uongo.

Nafasi za Ajira Serikalini

Mkapa Ashangazwa na Shule za Serikali Kufanya Vibaya Katika Matokeo ya Mitihani ya Kitaifa

$
0
0

DODOMA: Rais Mstaafu, Benjamin Mkapa amesema ni muhimu kuitishwa mjadala wa kitaifa ili kujadili hali ya elimu nchini

Amefafanua kuwa ni lazima taifa litafakari kwanini shule za serikali zinaendelea kufanya vibaya katika matokeo ya mitihani ya kitaifa kila mwaka

Aidha, Mkapa ameshauri mjadala huo uhusishe makundi yote ya jamii wakiwemo wadau kutoka sekta binafsi, wasomi pamoja na wananchi wa kawaida ili kutafuta suluhu ya kudumu ya tatizo hilo

Mkapa ambaye ni Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM), ameyasema hayo wakati wa tukio la kumkaribisha Makamu Mkuu mpya wa Chuo Kikuu hicho, Profesa Egid Mubofu na kumuaga aliyekuwa Makamu Mkuu wa chuo aliyemaliza muda wake, Profesa Idrisa Kikula.

Miujiza ya Sharifu Seif Mohamed..JE Umeachwa na Mme/Mke au Mpenzi, Umesongwa na Mitihani ya Maisha

$
0
0
SHARIFU SEIF MOHAMED ANAWASHUKURU WALE WOTE WANAOENDELEA KUPIGA SIMU, WENYE MATATIZO NA WALE WANAOTOA  SHUKRANI NA SHUHUDA JINSI TIBA ZAKE ZINAVYO WASAIDIA,

(Rudisha mahusiano yako ndani ya masaa 72 tu)

SHARIFU MOHAMED Ni  mtaalam na mnajimu maarufu wa nyota na kubashiri mambo yanayo watesa binadamu duniani kote na kupata ufumbuzi, Anatumia kitabu cha QUR'AN na Nyota

Je Umeachwa na UMPENDAE awe Mme/Mke na bado unampenda? Je Umekimbiwa na Mmeo/ Mkeo n anaishi na mtu mwingine? Je Umejaribu sehemu nyingi bila mafanikio? Mpigie simu SHARIFU SEIF sasa hivi ujionee Muujiza wa Papo kwa Papo, Anauwezo wa hali ya juu wa kusambaratisha mahusiano yao na kumrejesha kwako haraka sana na Kumfanya Atimize Ahadi zote Ndani ya Muda Mfupi Endapo Utafwata Atakacho Kuelekeza

 ZINDIKO LA NYUMBA NA BIASHARA, PETE ZA BAHATI, HUMALIZA KABISA TATIZO   HUZUIA CHUMA ULETE KWENYE BIASHARA, HURUDISHA MALI ZILIZOPOTEA, NA KUPONYA MAGONJWA SUGU ANAO UWEZO WA KUMRUDISHA ALIE MBALI AU ALIECHUKULIWA MSUKULE, KUPANDISHA NYOTA NA KUSHINDA BAHATI NA SIBU, KASAFISHA NYOTA NA KUKUPA MVUTO WA AJABU, KUTOA NUKSI NA VIFUNGO MBALIMBALI,  MAFANIKIO YA MAISHA NA UTAJIRI BILA MASHARI, NA MENGINE MENGI YA SIRI,

JE UMAHANGAIKA KUPATA MTOTO BILA MAFANIKIO? WASILIANA NA MTAALAMU HUYU KWANI YEYE HUFAULU PALE WOTE WALIPOSHINDWA, PIA UMALIZA KAZI ZILIZO SHINDIKANA NA WATAALAM WENGINE NDANI YA MASAA 24 TU,

(NA ANATIBU KWA NJIA YA SIMU UKIWA NCHI YOYOTE AU MKOA WOWOTE ENDAPO UTAFWATA MAELEKEZO YAKE)

Kwa ushauri na mawasiliano  zaidi Piga SIMU No:

Mobile +255 654-836970
WhatsApp 0622766715 

Diamond Platnumz moving to Kenya? Acquires a huge mansion in Nairobi

$
0
0
Diamond Platnumz has bought a beautiful home in Nairobi, Kenya. The singer bought the house recently during his visit to Kenya, where he also made deals with Safaricom Diamond Platnumz’s Kenyan fans are excited with the news, hoping the star will relocate to Kenya soon

Celebrated Bongo Flava crooner Diamond Platnumz has sparked excitement among his Kenyan fans after acquiring a new home in Nairobi.

Known for his singing talent and riches, Diamond recently flew to Kenya and splashed serious money on an apartment that sits in one of Nairobi’s leafy suburbs.

Wananchi wamuomba Rais Magufuli kuingilia kati vitendo vya udhalilishaji vinavyofanya na Jeshi la polisi

$
0
0
Baadhi ya Wakazi wa Mtaa wa Kambarage Kata ya Buhalahala wilayani Geita katika Mkoa wa Geita wanaomba msaada kutoka kwa Rais Dk. John Magufuli kutokana na vitendo vya unyanyasaji na udhalilishaji vinavyofanywa na askari wa Jeshi la Polisi.

Wakizungumza katika mahojiano maalum na Muungwana Blog, walieleza Mwaka 2003, wananchi kushirikiana na wafadhili Mradi wa Plan walifanikisha kujenga kisima cha maji kwa ajili ya matumizi ya wakazi hao, ambapo kila Kaya ilichangia  kiasi cha shilingi 1000/= , jambo lililopelekea kupungua kwa kero ya maji.

Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa wa Kambarage Bw. Mfaume Habali, alifafanua kuwa uongozi wa Shule binafsi ya sekondari ya Waja uliunganisha mabomba kutoka shuleni hadi kisimani kwa ajili ya kuvuta bila kutoa taarifa kwenye uongozi wa serikali, jambo lililopelekea wananchi kugomea zoezi hilo.

Habali, alisema baada ya kuibuka mgogoro kati ya Shule ya Waja na wananchi taarifa zilimfikia Mkuu wa Wilaya na kuitisha ambapo aliitisha Mkutano wa Hadhara wakawa wamemaliza tofauti, lakini baada siku kadhaa wakandarasi wa mabomba walifika tena kuendeleza zoezi la kuvuta maji kutoka kisimani hapo, jambo lililopelekea wananchi kupiga mwano bila msaada.

"Mnamo Februari 22, mwaka huu polisi walivamia hapa mtaani na kuanza kuwapiga wananchi ovyo huku baadhi ya wakina mama walijikuta walinyanyaswa  kudhalilishwa, ambapo wengine waliacha miji yao na kukimbia kutafuta sehemu yenye usalama zaidi," alisema.

Mwenyekiti huyo alimpigia simu Mkuu wa Wilaya kumueleza juu ya vitendo vinavyofanywa na askari hao, ambapo mkuu wa wilaya alimpa jibu kwa njia ya ujumbe mfupi katika simu yake uliosomeka "Hakuna Hati Miliki ya Mitaa, nimewatuma mimi mwenyewe na yeyote atakayepinga hata kama ni wewe watakukamata. Agizo la Halmashauri haliwezi kupingwa na mtaa na wewe ni chanzo cha kuvuruga zoezi hilo".

Bw. Habali  aliwataja baadhi ya  wahanga katika tukio hilo, kwa wanawake ni Justa Fungameza na Fidelina Petro, baada ya kupigwa kuvulishwa nguo kisha kushikwa kifuani wakiwa hawana mavazi, huku kwa upande wa wanaume ni Msika Stima aliyepigwa na kitako cha bunduki kichwani kisha kuzimia, Reonard Lutama, Daud Stephano, Ephraim Odelo wao walipigwa na kushikiliwa kisha kupangiwa siku ya kuripoti mpaka Ijumaa iliopita waliambiwa warudi kituoni mpaka watakapowapatia sababu huku anaye washtaki hafiki na kutojulikana.

Kocha wa Simba: Yanga kutufikia kipointi kwetu wala halijatupa hofu yoyote

$
0
0
BAADA ya Simba kutoka suluhu na Al Masry kwenye mchezo wa Kombe la Shirikisho Afrika jana na kutupwa nje ya michuano hiyo, hatimaye wamesema kuwa sasa ligi ndiyo itakuwa tamu. Simba jana walikuwa wanatakiwa kupata ushindi au sare ya zaidi ya mabao 2-2, lakini waliambulia suluhu kwenye mchezo ambao walionyesha kiwango cha juu sana nchini Misri.

Pamoja na kuondolewa kwenye michuano hiyo, pia Simba wamekuwa na hasira zaidi baada ya kulingana kwa pointi na watani wao wa jadi Yanga ambapo kila moja ina pointi 46, hivyo wamesema kuwa hasira zao sasa ni kwenye ligi. Benchi la ufundi la Simba chini ya kocha wake mkuu, Pierre Lechantre limeweka wazi kuwa halina hofu hata kidogo na kwamba sasa mambo ndiyo yameanza kunoga.

Simba kwa muda mrefu walikuwa ndiyo vinara wa ligi kabla ya Yanga kuwafikia na timu zote kwa sasa kuwa na pointi 46, lakini Simba wenyewe wameendelea kuwa kileleni kutokana na tofauti ya mabao ya kufunga ambayo wao wanayo mengi 11 zaidi ya wapinzani wao hao.

Kocha msaidizi wa Simba, Masoud Djuma ameliambia Spoti Xtra, kuwa; “Yanga kutufikia kipointi kwetu wala halijatupa hofu yoyote ile zaidi ya kwamba wametuongezea changamoto ya kupambana zaidi kwenye kila mchezo wetu ili kupata matokeo mazuri kutafuta nafasi ya kuwatoka na kuendelea kuongoza ligi.”

“Kwa kitendo ambacho wamekifanya Yanga kwa sasa ni kunogesha tu ligi yaani limekuwa tamu zaidi kwa sababu tunalingana pointi na hivi ndivyo inavyotakiwa kuwa, lakini ikumbukwe wao wapo mbele yetu kwa mechi moja zaidi jambo ambalo utaona linatubeba sisi,” alisema Djuma.

Katika mchezo huo uliochezwa mjini Port Said nchini Misri, Simba kama wangepata ushindi dhidi ya Al Masry walikuwa wanapewa kila mchezaji shilingi milioni 5, hivyo wamepoteza dodo nono.

VIDEO:Zitto Kuishauri Zanzibar iishtaki Tanzania, Ayataja Maandamano

$
0
0
Kiongozi Mkuu wa Chama Cha ACT Wazalendo, Zitto Kabwe amesema hafahamu kuhusu maandamano yanayotajwa na viongozi wakubwa Serikalini huku akisema kuwa amedhamiria kuishauri Zanzibar iishtaki Tanzania kwenye mahakama ya Afrika Mashariki kama Serikali ya Muungano itashindwa kumaliza tofauti iliyopo kuhusu uuzwaji wa sukari ya Zanzibar upande wa bara.

TAZAMA FULL VIDEO HAPA CHINI

Shinda Gari la Bure Kabisa Mwezi Huu Kutoka Japan

$
0
0
Jee!! Katika Maisha yako umewahi kuwa na ndoto ya kumiliki Gari lako?  Kama jibu ni Ndio Basi Kampuni ya Kijapan inakupa Fasi ya kushinda Gari Buree yani Buree bila kulipa chochote..

Chakufanya ni kubofiya neno SHINDA GARI  hapo chini na kisha Bonyeza Neno APPLY NOW kwa kujisajili...

Kumbuka huduma hii ni ya Bure kabisaaaaa...


>> SHINDA GARI <<


>> SHINDA GARI <<

Polepole: Zitto Kabwe atafute kazi nyingine ya kufanya

$
0
0
Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Ndg. Humphrey Polepole amefunguka na kusema Mbunge wa Kigoma mjini kwa tiketi ya ACT Wazalendo, Zitto Kabwe mwaka 2020 atafute kazi nyingine ya kufanya kwa sababu jimbo hili litarudi kwenye Chama Cha Mapinduzi (CCM)

Polepole amesema hayo Machi 17, 2018 wakati akifanya ukaguzi wa mradi wa kusambaza maji mkoa wa Kigoma ambapo amesema kuwa wanataka kuhakikisha kuwa mkoa huo unapata maji safi kabla ya mwaka 2020.

"Mkandarasi ameniahidi mpaka mwezi wa tano maji yataanza kutolewa kwa karibia asilimia mia moja katika mji wote wa Kigoma Ujiji na maeneo ya pembezoni na mimi nimezungumza na viongozi wenzangu wa CCM wafike hapa mwezi mmoja kutoka leo kujiridhisha juu ya maendeleo ya kukamilisha mradi huu na kupeleka maji katika mji wetu wa Kigoma , sisi tunafanya hivi sababu tunao mkataba na wananchi na tunataka kuukamilishe mapema kabisa kabla ya 2020 ili ifikapo 2020 basi mbunge wa hapa atafaute kazi nyingine" alisisitiza Polepole

Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Ndg. Humphrey Polepole yupo mkoani Kigoma katika ziara ya Kukagua na kufuatilia utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM Mwaka 2015 - 2020.

TRA yawasimamisha kazi watumishi wawili

$
0
0
Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) imewasimamisha kazi watumishi wake wawili mkoani Lindi, kwa kile kilichodaiwa kwenda kinyume na kanuni na miongozo ya kazi inavyowaelekeza na kutumia lugha isiyo rafiki na wateja wao {wafanyabiashara}.

Uamuzi huo,umechukuliwa na Kamishina kodi ya Mapato za ndani nchini, Elijah Mwandumbya, wakati wa kikao cha pamoja kati yake na wafanyabiashara wa mkoa huo,kilichofanyika Manispaa ya Lindi baada ya kusikiliza malalamiko mbalimbali kutoka kwa wafanyabiashara hao.

Mwandumbya amesema Taifa wamekuwa wakipata taarifa kwamba hakuna mahusiano mazuri kati watumishi hao na wafanyabiashara, hali iliyohustua uongozi na kumtuma Kamishina huyo kufika mkoani humo kupata maelezo ya kina.

Kamishina huyo wa kodi za ndani amesema {TRA}  inapitia kipindi ambacho kinahitaji kuwapatia huduma bora wateja wao ili waweze kumsaidia Rais wa nchi katika utekelezaji wake wa maendeleo kwa kuhakikisha wanazingatia Sheria, kanuni, taratibu na miongozo,kuhakikisha wanatoa huduma iliyo bora kwa walipa kodi.

VIDEO: EXCLUSIVE: LIPUMBA Aibuka Leo Na Kumtupia Dongo Maalim Seif

$
0
0
Mwenyekiti wa Chama cha Wananchi CUF ambaye anatambulika na Msajili wa vyama vya siasa, Profesa Ibrahim Lipumba ameibuka leo katika mkutano wa chama hicho na kumtupia dongo Katibu Mkuu wake, Maalim Seif Hamad akimuita mbinafsi huku akisema chama hicho kimemdekeza sana.

TAZAMA FULL VIDEO HAPA CHINI

Viewing all 104793 articles
Browse latest View live




Latest Images