Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104789 articles
Browse latest View live

Ngorongoro Heroes yaipiga Msumbiji 2-1

$
0
0
Kikosi cha Timu ya Taifa ya Vijana chini ya miaka ishirini, Ngorongoro Heroes, kimeibuka na ushindi wa mabao 2-1 katika mchezo wa kirafiki dhidi ya Msumbiji jioni hii.

Ushindi huu umekuwa wa pili mfululizo, baada ya kuifunga pia Morocco katika mchezo uliochezwa Machi 18 2018 jijini Dar es Salaam.

Mabao ya Ngorongoro yamefungwa na Abdul Suleimani katika dakika ya 35 na Saidi Mussa akifunga kwenye dakika ya 71, bao la kufutia machozi upande wa Msumbiji limefungwa na Leonel Victor katika dakika ya 13.

Matokeo haya yanaipa nafasi nzuri Ngorngoro kuelekea mchezo wake wa kuwania kufuzu kushiriki Kombe la Mataifa ya Afrika kwa Vijana (AFCON U20) dhidi ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, mechi itapigwa Machi 31 2018 kwenye uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Baada ya Mahojiano na Diamond, Times FM Wawekwa Kikaangoni na Kamati ya Maudhui ya TCRA

$
0
0
Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) imesema kamati yake ya maudhui inafuatilia mahojiano ya mwanamuziki Nasseb Abdul maarufu Diamond aliyoyafanya katika kituo cha Redio cha Times jijini Dar es Salaam.

Mkuu Idara ya Utangazaji ya mamlaka hiyo, Andrew Kisaka amesema wamechukua uamuzi huo kwa kuwa mahojiano hayo yamefanyika katika kituo wanachokisimamia.

JF

Diamond Platnumz Aeleza Bifu yake na Ali Kiba ilivyosukwa ‘Kumuua Kimuziki’ Adai Walikutana

$
0
0
Diamond Platinumz amedai kuwa uhasama kati yake na Ali Kiba ulipikwa na chombo kimoja cha habari kwa lengo la kumuondoa kwenye ramani ya muziki.

Bosi huyo wa WCB amefunguka katika mahojiano na Lil Ommy wa Times FM, ambapo amedai kuwa uhasama huo ulikuwa miongoni mwa mbinu za muda mrefu zilizoshindwa za kutaka kumuua kimuziki.

Amesema kuwa baada ya kugundua mbinu hiyo, alikutana na Ali Kiba jijini Nairobi na akazungumza naye kuhusu hilo na wakakubaliana hakuna tofauti kati yao.

Diamond ambaye anapromoti albam yake mpya ya ‘A Boy From Tandale’ alisema kuwa tofauti kati yake na Ali Kiba haiko kiuhalisia kwani inatengenezwa na watu wasiomtakia mema na kukuzwa na mashabiki.

Aliongeza kuwa njama na jitihada za kutaka kumuangusha kimuziki zilianza miaka minne iliyopita lakini haziwezi kufanikiwa. Alisisitiza kuwa hakuna anayeweza kumuua kimuziki akiwa hai, “labda unitoe uhai, lakini kuniua kimuziki haiwezekani.”

Lil Ommy alitaka kujua kama nyimbo za Ali Kiba zitachezwa kwenye vituo vya Wasafi Radio na Wasafi TV.

“Bro nisikudanganye, pale atachezwa kila msanii na yeyote mwenye talent (kipaji). Hadi sasa pale watu wanabishana kuhusu slogan (kauli mbiu), kuna wanaosema ‘Welcome Home’ na ‘Hii ni Yetu Sote’. Kwa hiyo hii ni ya wasanii na haipo kwasababu ya matabaka,” alijibu.

Chibu alisema kuwa ushikirikiano wa wasanii ndio utakaoendelea kuukuza muziki wa Bongo Fleva na sio uhasama na ushindani usiokuwa na lengo zuri.

Jifunze Kupika Karanga za Mayai kwa Ajili ya Kula au Kuuza

$
0
0

Mahitaji

Karanga kilo 1
Yai moja
Mafuta ya kula ( ya maji ) mls 750
Sukari vijiko 6 vya chakula
Unga wa ngano kikombe kimoja cha kahawa( coffee cup)
Chumvi ya unga nusu kijiko cha chai.
Jiko
Chombo –Sufuria/bakuli
Mwiko /kijiko kikubwa

Maelekezo

Chukua  yai,  pasua  na  koroga  kwenye  chombo  kisafi.
Chukua  karanga,mimina kwenye chombo ulicho koroga yai ,changanya kwa kutumia mikono.
Weka chumvikidogo, changanya vizuri, weka sukari changanya, mimina unga wa ngano, changanyavizuri.
Weka mafuta jikoni hadi yapate moto.
Chota karanga kwa kutumia kijiko  kikubwa  na  weka  kwenye  mafuta  kisha  zigeuze  bila  kuacha  hadi utakapoona karanga zimebadilika rangi kua kahawia.
Tumia  kijiko  kikubwa  kuziepua  na  weka  kwenye  chombo  kisafi  cha  wazi  ilizipoe.
Funga kwenye vifuko vidogo na zihifadhi mahali pasafi tayari kwa kula au kuuza.

Jifunze Jinsi ya Kuwa Mzungumzaji Bora

$
0
0

Wapo baadhi ya wasomaji wangu walikuwa wakiniuliza "eti nifanye nini ili kuwa mzungumzaji mzuri mbele ya watu wengine?  Swali hili kiukweli limekuwa likiwatatiza watu wengi sana kwa namna moja ama nyingine.  Na kutokana na hali hiyo kumewafanya watu hao hao kuwa katika hali unyonge,  kwani huisi watachekwa na sababu nyingine kama hizo.

Lakini ukweli ni kwamba endapo utazijua siri hizi kuwa mzungumzaji bora zitakwenda kukusaidia kutoka katika hali uliyonayo hatimaye kuwa mzungumzaji mzuri.

Zifuatazo ndizo mbinu kuwa mzungumaj bora:

1.Kuwa na Taarifa za Uhakika na Kutosha.

Moja ya  njia bora ya kuwa mzungumzaji mzuri ni kuwa na utajiri wa vitu vingi katika kibubu cha ubongo wako . Watu wengi wanajiona hawawezi kuchangia maada yeyote ile mbele ya wengine hii ni kwa sababu wamekuwa hawana taarifa sahihi na za uhakika za kuweza kuzungumza. Hivyo Kama endapo nia yako ni kutaka kuzungumza mambo mbalimbali katika jamii yako ni lazima ujue vitu hivyo kwa undani zaidi.

Kama unataka kuwa mzungumzaji juu ya masuala ya michezo ni lazima uweze kufutilia taarifa mbalimbali za michezo kutoka vyanzo mbalimbali ambavyo hutoa taarifa za michezo. Kutokuwa na taarifa nyingi za kutosha zimefanya watu mbalimbali kufanya vitu vile vile kila wakati.

Watazame wasanii mbalimbali katika nchi wameshindwa kuwa wabunifu katika kazi zao kwa sababu waliyonayo wanahisi yanatosha.  Ila ukweli ni kwamba kujifunza vitu vipya hakuna mwisho. Na daima kumbuka ule usemi usemao "no research no right to speak" kama hauna utafiti wa kutosha huna haki ya kuzungumza, hivyo ukitaka kuwa mzungumzaji mzuri ni lazima ufanye utafiti wa kutosha juu ya jambo hilo.

2. Lazima uwe msikilizaji mzuri.

Hii pia ni siri mojawapo ya kuwa mzungumzaji mzuri mbele ya watu wengine. Huwezi kutaka kuwa mzungumzaji bora kama hujui kusikiliza. Matokeo ya kuzungumza chanzo chake hutokana na kusikiliza vizuri anachokizungumza mtu mwingine.

Pia tatizo hili la kutojua kusikiliza limekuwa likiwaathiri watu wengi sana.  Kwa tafiti zinaonyesha ya kwamba msikilizaji ndiye ambaye hutumia nguvu nyingi katika kuelewa kuliko mzungumzaji.  Kama ndivyo hivyo hakikisha unatumia nguvu nyingi sana katika kusimamia akili yako katika kusikiliza, kama kweli unahitajj kuwa mzungumzaji mzuri.

3. Kujiamini

Suala kubwa ambalo limekuwa likiwaathiri watu wengi katika kuzungumza ni kushindwa kujiamini. Wengi wamejenga na hofu ambayo imekuwa haiwasaidii.  Wengi huona ya kwamba Watachekwa, watazomewa na vitu vingine vingi kama hivyo. Lakini hali hii imekuwa ikizuka kwa baadhi ya watu ambao kwa asilimia kubwa imejengeka tangu wakiwa wadogo.

Na hofu hiyo umekufanya ujione mnyonge sana,  hata wakati mwingine umekuwa ikihisi huna thamani mbele ya watu wengine. Ila nichotaka kukwambia njia bora ya kuondokana na hofu hiyo uliyonayo ni kufanya kitu ambacho unakiogopa.  Kama umekuwa unashindwa kuzungumza mbele za watu anza leo. Kwani kama nilivyosema hapo awali njia bora ya Kuwa mtu mwenye mafanikio ni kufanya kitu ambacho unakiogopa.

4. Anza kufanya mazoezi ya kuzungumza.

Jambo la nne na la mwisho ambalo nilipanga kuzungumza nawe siku ya leo ni kuanza kufanya mazoezi ya kuzungumza .  Huwezi kuwa mzungumzaji bora kama hutaki kufanya mazoezi ya kuwa hivyo inavyokata. Hivyo mazoezi ni chanzo cha ushindi. Kama ilivyo kwa wachezaji wa mpira kama hawajaanza kucheza mechi ni lazima wafanye mazoezi. Hivyo hata wewe unahitaji kutenga  walau nusu saa ya kuzungumza.  Unaweza ukachugua maada fulani na ukafanya mazoezi angalau nusu saa ya kuzungumza maada hiyo ukiwa peke yako.

Endapo utafanya hivyo kutakusaidia kujenga uwezo wa kukufanya uwe mzungumzaji mzuri kwa watu wengine.

Yawezekana kabisa suala hili la kutokuwa mzungumzaji linakuhusu wewe ambaye unasoma makala haya,  nichotaka kukwambia kila kitu kinawezekana na utakwenda kuwa mzungumzaji mzuri mbele ya watu wengine endapo tu yote ambayo nimeyaeleza utaamua kuyafanyia kazi.

Mbinu Zitazokusaidia Kufikia Malengo ya Mafanikio

$
0
0

Umbali uliopo kati ya malengo yako na mafanikio ni mrefu sana, na una vikwazo vingi sana, nafahamu fika ya kwamba hilo unalitambua vizuri sana.Umbali huo ambao upo baadhi ya watu ambao wana Mafanikio wameweka mikakati thabiti ambayo imewafanya wameweza kufanikiwa.

Pia kwa upande watu ambao hawajafanikiwa kwa kiwango cha juu na wao katika malengo yao wameweka mikakati, ila wengi wao hukata tamaa njiani katika utekelezaji wa mambo mbalimbali yatayowalete mafanikio.

Hali hiyo hutokea kwa sababu wengi wao hushidwa kuhimili changamoto ambazo hujitokeza katika safari hiyo ya kutoka katika malengo hadi Mafanikio.

Kama na wewe ni miongoni mwa watu ambao hukata tamaa katika safari yako ya kuelekea mafanikio, naomba nichukue nafasi hii kuweza kukaribisha katika makala haya ambapo tutazungumzia masuala ya kupanga malengo yako hadi kufikia mafanikio.

Kwani Wengi hujikuta wakishindwa wakiishia njiani katika safari yao ya mafanikio hii ni kutokana kutokujua namna ya kuzitambua mbinu za kukuza malengo hadi mafanikio.

1. Malengo ni lazima yaandikwe.

Malengo lazima uyaandike sehemu ambayo inaonekana, hapa ni maana ya kwamba uandike sehemu ambayo inaonekana, kufanya hivi kutakuwa kuna kutakufanya malengo hayo uwe unayakumbuka na kujua namna ya kuayatekeleza.

Unaweza ukayaandika malengo hayo kuyaweka katika simu yako katika (screen saver), kioo ambacho unakitumia kujitazama asubuhi na sehemu nyingine ambayo utayaona malengo hayo.

2. Weka vipaumbele katika malengo yako.

Inawezekana fika ukawa na malengo mengi, yaandike malengo hayo katika makundi matatu.
Kundi la kwanza jua yapi ni malengo ya muhimu yapi si malengo ya muhimu, yapi ni malengo ya haraka na yapi sio malengo, na tatu andika malengo ambayo sio ya muhimu sana.

Endapo utagawa malengo hayo utajua ni kipi kinatakiwa kuanza na kipi kinatakiwa kufuata na kwa muda gani.

3. Anza kwa kuanza na hatua ndogo.

Siku zote kama ilivyo ukuaji Wa kiumbe chochote chenye uhai huanza ukuaji wake katika hali ya chini. Kama ilivyo kwa kiumbe yeyote katika ukuaji hata katika ukuaji wa mafanikio yako huanza katika ngazi za chini.

Kitu cha msingi ni kuweza kupanua wigo mpana kwa ajili ya kupata mafanikio zaidi kwa kila jambo ambalo unalifanya. Na kwa kuwa mafanikio hayana ukomo hakikisha ya kwamba kila iitwayo leo unapata kiu ya kutaka kufanikiwa zaidi.

4. Malengo ni lazima yawe chanya.

Mara kadha watu huwa na ndoto nzuri sana, na pia wengi wao hupanga mambo mazuri kwa ajili ya utekelezaji wa ndoto hizo, ila changamoto kubwa ambayo huwa inakuja ni pale ambapo linakuja suala la utekelezaji wa jambo hilo.

Hapo sasa ndipo utakapoanza kumsikia mtu anasema aaah hivi nitaweza kweli, inatakiwa uondokane na kukata tamaa, vinginevyo kufanikiwa utaendelea kusikia kwa akina Donald Trump.

5.Malengo lazima yawe katika muda maalumu.

Ni lazima uweke muda kamili kwa ajili ya kutekeleza malengo yako, ifike mahali Malengo yako yafananishe na makampuni yanayohusika ujenzi kwani wao kabla ya kuanza kwa mradi huwa wanafanya mahesabu ili kujua mradi huo wa ujenzi utachukua muda gani mpaka ukamilike.

Ukiishi katika utaratibu Wa kuweka mbinu hiyo itakuwa ni rahisi kwako kutekeleza mambo ambayo unataka kutekeza. Kwa mfano lengo lako ni kujenga nyumba unaweza ukaandika katika lengo lako ya kwamba baada ya muda fulani inabidi uwe umekamilisha ujenzi huo.

Kupanga malengo bila kujua muda Wa kutekeleza malengo ni sawa na bure. Hivyo ni vyema ukajua ya kwamba muda ni mali katika kufanikisha malengo yako kwa wakati sahihi.

6. Malengo ni lazima yawe na mbinu za utekelezaji.

Watu wengi wana malengo ya kusema kwa mdomo tu. Lakini nikwambie ya kwamba ukitaka kufa maskini basi endelea na utaratibu huo Wa kuweka malengo mdomoni.

Kama kweli unataka kufanikiwa hakikisha ya kwamba malengo ambayo umejipangia umeyaandika na kuandika mbinu au njia kwa ajili ya utekelezaji wa malengo hayo.

Kufanya hivi kutakusaidia kujua jinsi ambavyo utayatekeleza malengo hayo ili kupata mafanikio. Kwa mfano kama malengo yako ni kujenga nyumba basi huna budi kuandika mbinu ambazo zitakusaidia kutengeza nyumba hiyo, pia hapa huenda sambamba na bajeti ya utekelezaji wa malengo yako.

7. Malengo ni lazima yapimike.

Kila malengo ambayo umejipangia Ni lazima yaweze kupimika. Kama nilivyoeleza hapo awali ya kwamba malengo ni lazima yawe na muda maalum kwa ajili ya utekelezaji.

Hivyo ni lazima upime malengo yako ni wapi ambapo umefikia? Katika muda ambao umepanga kuyatekeza malengo hayo je unahisi utafikia malengo hayo?

Pia uchunguzi yakinifu juu ya malengo yako ni lazima ufanyike ili kujua fursa na changamoto ambazo zimejitokeza katika kutekeleza malengo yako.

Mpaka kufikia hapa sina la ziada, tukutane siku nyingine.

Jinsi ya Kutafuta Masoko

$
0
0

UTANGULIZI
Kuwafundisha washiriki kufikiri ki- masoko na kuelewa baadhi ya mbinu za masoko kitu ambacho kitawafanya waelewwe maana ya maneno “soko na masoko” pia utafiti wa soko na kuyafanyia kazi  katika biashara/miradi yao.

Soko ni nini?
Soko ni utaratibu au mtindo  uliowekwa kwa mujibu wa kanuni /sheria  kumwezesha mfanya biashara kuuza bidhaa zake kwa wateja/walaji. Husaidia kupanga nini uuze,nani umuuzie au jinsi gani watu wanavyoweza kujuakitu gani unauza,hivyo kukuwezesha kuzalisha kile ambacho kinahitajika  katika soko sahihi.

Mafanikio katika biashara hutokana na mwonekano wa kipekee  wa bidhaa au bidhaa unayozalisha kukidhi matakwa ya walaji au wateja pia, kuweza kutambua  aina fulani ya watu ambao wangependa kununua bidhaa yako na kuweza kueleza  bayana ni kitu gani, watu wategemee kunufaika kwa kunua bidhaa zako kati ya kundi hili la walengwa.

Kwa kifupi soko ni MTEJA Wa bidhaa na huduma uayozalisha

Soko lako ni;

Wateja wako ulionao kwasasa
Wateja uaotarajia kuwapata baadae
Wateja uliopoteza na untarajia watakurudia tena

Masoko ni nini?
Masoko ni shughuli yoyote ile anayofanya mfanyabiashara ili kuimarisha biashara yake.

Haitoshelezi tu kukaa kungojea oda.

Mfano wa shughuli hizo ni;

Kuelewa matakwa ya wateja wa bidhaa yako
Kupanga bei ambayo wateja  watakuwa tayari kulipa na itakupa faida
Usambazaji wa bidhaa au huduma kwa wateja wako
Kuwavutia wateja wanaume bidhaa au huduma yako

UTAFITI WA SOKO
1. Kwa nini tujifunze kuhusu soko?
a)  Mahitaji (demand)

Waswahili husema ‘unaweza kumlazimisha punda aende mtoni lakini huwezi kumlazimisha anywe maji’inamaana bidhaa zako kuwa wakati soko halihitaji bidhaa zako huwezi kulazimisha bidhaa yako inunuliwe

b)  Bidhaa sahihi – usijaribu kumuuzia kitana mtu mwenye kipara bali muuzie kofia

c)  Kufuata mkumbo-ni vema kutofautisha bidhaa za kuuza kwa wateja

2. Unahitaji kufahamu nini kutokana na soko lako?
Maswali yafuatayo ndio yakusaidia kufanya utafiti wa soko lako

Wateja wako ni akina nani?

Wako wapi
Mahitaji yao ni nini?
Wanapendelea nini kutokana na bidhaa zako
Ni mara ngapi na kiasi gani a wanacho nunua?
Wana nunua wakati gani?
Ni kiasi gani cha pesa wako tayari kutoa?
Ni jinsi gani bidhaa zitawafikia wateja
Washindani wako ni wapi?
Ubora wa bidhaa zao na bei zao vikoje

NB; kutafuta majibu ya maswali haya kunaitwa utafiti wa masoko

3. Jinsi ya kufanya utafiti a soko
Mbinu zifuatazo zinaeza kutumika kufanya utafiti wa soko la bidhaa au huduma unazozalisha:-

Kupitia Kwa wateja (kusikiliza maoni yao, kuachunguza na kuwauliza maswali).
Kuwauliza maswali watumiaji mbali mbali wa bidhaa zako ( nini wanachohitaji na wasicho kihitaji, mapendekezo na nini kiongezwe)
Kwa marafiki na ndugu
Kusoma kwenye vitabu, magazeti, kusikiliza radio na kuangalia televisheni
Kupeleka bidhaa zako katika maonesho ya biashara
Kuangalia biashara za washindani wako: bei, ubora, tofauti za bidhaa,, kuonesha bidhaa, na huduma zinazoambatana na bidhaa zako
Onesha sampuli ya bidhaaa au tembezasampuli ya bidhaa na waulize watu maoni juu ya bidhaa zako

4. Jumuisho la masuala ya masoko

B-Nne  katika masoko
Bidhaa
Bei
Banda
Bango

a)  BIDHAA- Bidhaa ni kitu chochote kinachozalishwa kwa ajili ya kuuza au kutumia.

Sifa za bidhaa
Bidhaa nzuri ni ile inayoridhisha na inakidhi matakwa ya soko. Kwa mfano:-

Ubora(muda, malighafi nzuri, iliyotengenezwa vizuri)
Yenye kuvutia ( rangi,mapambo,usafi, utengenezaji mzuri)
Mtindo (umbile zuri, inahusiana na thamani,saizi)
Ya kisasa (Inayoendana matumizi ya mtindo uliopo- fassion)
Tofauti na bidhaa za ashindani

b) BEI- Bei nithamani ya bidhaa au huduma ambayo mteja yuko tayari kumudu au kulipia. Kwa hiyo bei hujumuisha Gharama zote na faida au Bei huiumuisha gharama za ununuzi, gharama za uendeshaji na faida.

Mambo muhimu ya kuzingatia wakati wa kupanga bei.
Ghrama zote ka jumla (gharama halisi)
Bei za wapinzani
Mahali ulipo 9 kiasi ambacho wwateja wwako radhi kulipia kwa kutegemea uezo wao kifedha)
Msimu (kwa mfano bei kubwa za vinyago msimu wa watalii au bei ndogo za feniture wakati wa mvua )
Kupata faida ya kutosha kuendesha shughuli bila matatizo

c) Banda au mahali pa kufanyia biashara
Banda ni mahali muhimu sana  katika kuuza bidhaa au huduma. Mahali pa kufanyia biashara  panatakiwa pae na sifa zifuatazo:-

Rahisi kufikiwa na wateja
Usalama, usafi
Sehemu ya maegesho
Kuwa karibu na huduma nyingine muhimu kama vile usafiri wa daladala, sehemu za vinywaji, vyakula,umeme n.k
Yenye mwanga wa kutosha
Rahisi kuonekana
Huduma hutolewa saa zote

5. Upangaji mzuri wa bidhaa mahali pa biashara.

Bidhaa zipangwe kwa seti
Mahali pa wazi panapoonekana kiurahisi
Weka bidhaa chache katika makundi madogo madogo
Weka bidhaa za aina mbalimbali
Panga sehemu yenye mwanga wa kutosha
Sehemu safi
Tumia picha au katalogi

6. BANGO AU UVUMISHAJI

Uvumishaji unajumuisha shughuli kadhaa  ikiwa ni pamoja na uvumishaji  wa mauzo,utangazaji,uhusiano wa jumuia na mbinu za kuuza. Shughuli hizo zinasaidia kuwavitia wateja, lakini hasahasa zinawapa wateja imani na bidhaa zako kuhakikisha kuwa hawanunui kwa mtu mwingine.Jambo muhimu la kuzingatia katika uvumishaji wa bidhaa ni lazima uwe mchangamfu na kuwa macho kuvutia wateja.

Kuvumisha mauzo (sales promotion)
Punguza bei yako kidogo ili wateja waone kuwa ni ndogo. Mfano:-  shs 999.00 badala ya 1000.00
Weka bei maalum wakati wa sikukuu mbalimbali
Panga bidhaa madirishani ilizionekane kwa nje (display)
Uza bidhaa zinazoendana. Mfano muuza maandazi anaweza kuuza chai au muuza sukari anaweza kuuza majani ya chai
Utangazaji

Radio, magazeti,tv,sinema,mabango,kadi za biashara za mwenye biashara9business card)na sifa zinazotolewa kwa njia yam domo na watu watu waliokwisha kutumia bidhaa hizo.

Mahusiano
Kuchangia huduma za jamii Kama vile elimu, afya mazingira n.k

Mbinu za uuzaji

Jinsi ya kutambulisha bidhaa, eleza faida za bidhaa na ubora ake
Kumthamini mteja
Eleza faida ya bidhaa yako kabla hujataja bei
Jaribu kuuliza juu ya mahitaji ya mteja ili uweze kumwelekeza kwenye bidhaa itakayomfaa.
Kama mteja akiuliza bidhaa ambayo huuzi , unamwekeza zinapoatikana.

MKAKATI WA MASOKO

Kuwa na mkakati wa soko utakusaidia kufiki malengo yako kupitia kuweka lengo kuu/kubuni bidhaa/huduma mchanganyiko na kuchukua SWOT ANALYSIS(maeneo tunayofanya vizuri,maeneo ambayo hatufanyi vizuri,fursa tulizonazo, na changamoto zinazotukabili) katika bidhaa /huduma.

MAELEZO YA MALENGO YAKO

Maelezo ya malengo ni nini? Ni maelezo ya jumla  juu ya kila unachotarajia kufikia,au lengo kuu la shirika. Hujulikana pia kama dira ya shirika . hivyo ni vema kuwa na wazo ambalo unaweza kuliweka kama kitovu cha kukuwezesha kuona unapoelekea  kibiashara. Kulingana na kukua kwa biashara yako waweza kuendeleza malengo yako kuipa nguvu dira yako

Lengo lako lazima liwe dhahiri / bayana
Ni nini unataka kutimiza?
Kwa nini/ sababu gani ya kutimiza?
Nani atafanya nini?
Ni wapi utafanyia kile unachotarajia?
Kipi kinatakiwa kufikia lengo lako?
Malengo yako lazima yaweze kupimika.

Kwa kiasi gani?
Vingapi?
Malengo yako lazimayawe ya kufikiwa.
Ya juu Sana kisi cha kushindwa kufikia malengo yako?
Ya chini Sana kisi kwamba malengo yako hayaleti maana?
Ni muhimu kuweka malengo yanayokubalika lakini yenye kutamanisha.
Malengo yako yawe na uhusiano na kile unachotaka kufanya

Tuzo nitakayoipata baada ya kufikia malengo itazidi gharama (faida)
Tuzo nitakaipata baada ya kufikia malengo itafikia maezo ya malengo yako ya awaliKufikiwa kwa malengo yako kutakusaidia  kufikia mipango yako?

Malengo yako lazima yaende na wakati

Ni lini litaanza?
Itachua muda gani kufikia malengo yako?Naweza kufanya nini kila juma,Mwezi juu ya bidhaa nyingine iliyopo ambayo ina matumizi sawa na ile anayohitaji, mteja

Faida 5 za Kuendesha Baiskeli

$
0
0

Najua fika utakuwa umeshangazwa na kichwa ya mada hapo juu, ya kwamba hivi ni kweli kuna faida yeyote ya kuendesha baiskeli kiafya, ukiachana na dhana ya kwamba baiskeli ni chombo cha usafiriambacho hutumika kukufikisha sehemu unayotaka kwenda? Majibu ya swali hilo yapo katika Makala haya kwamba ndiyo zipo faida ambazo utazipata endapo utaendesha baiskeli mara kwa mara.

Miongoni mwa faida hizo ni;

1. Kuendesha baiskeli kunasaidia kupunguza kwa kiwango kikubwa  mafuta  mwilini, kwasababu hupunguza calori  mwilini.

2. Baskeli ni usafiri rahisi unaoweza kujichanga ukanunua na ukaokoa bajeti ya nauli za kilasiku uendapo katika shughuli zako kama si mbali sana na maeneo unayoishi.

3. Hukufanya uwe karibu na watu wanaotembea kwa miguu, kwa mfano ukiwa njiani utasalimiana na watu mbalimbali, tofauti ilivyo gari.

4. Ukitumia baskeli hukupa nafasi ya kuona kupita sehemu ambazo kwa gari usingefika, hivyo hutumia njia fupi.

5. Kuendesha baiskeli husaidia kuimarisha misuli ya mwili hivyo kwa maneno mengine tunaweza tukasema licha ya baiskeli kutumika kama usafiri lakini vilevile ni chombo cha mazoezi, hivyo endesha baiskeli   mara kwa mara ili kuuweka mwili wako sawa.


Soda ni SUMU

$
0
0

AFYA za mamilioni ya Watanzania wanaotumia vinywaji vya aina ya soda ipo hatarini, baada ya kugunduliwa uwepo wa chembechembe zenye kemikali za sumu ndani ya vinywaji hivyo, MTANZANIA Jumatano linaripoti.

Utafiti uliofanywa na Muungano wa Waandishi wa Habari za Uchunguzi Tanzania (Investigative Journalists Union of Tanzania- IJUTA) pamoja na tafiti zilizofanywa na wataalamu waliobobea katika afya ya umma duniani, umebaini kuwa vinywaji baridi aina ya soda ni hatari kuliko utumiaji wa sigara inayosababisha maradhi ya kansa katika mwili wa binadamu.

Kwa mujibu wa utafiti wa wanasayansi mbalimbali duniani, yapo madhara makubwa ya utumiaji wa vinywaji vya aina ya soda katika mwili wa binadamu.

Utafiti huo unaonyesha kuwa zipo sababu nane kuu zinazokiweka kinywaji aina ya soda kwenye kundi la vinywaji vyenye sumu ambavyo havifai kwa matumizi ya binadamu.

IJUTA imebaini kuwa makampuni makubwa yanayotengeneza vinywaji baridi aina ya soda yanatumia mabilioni ya dola kila mwaka kujitangaza na kutoa misaada ya kijamii kutokana na mauzo yake, bila kutaja madhara ya vinywaji hivyo kwa binadamu.

Kwamba matangazo hayo yanayogharimu mamilioni ya fedha ndiyo yanayokifanya kinywaji hicho kuwa maarufu zaidi duniani, licha ya kuwa na madhara makubwa katika mwili wa binadamu.

Aidha, utafiti huo unaonyesha kuwa umaarufu mwingine wa kinywaji aina ya soda ni utamu wa kupindukia ulio ndani ya soda.

Utafiti wa IJUTA unaonyesha kuwa utamu wa kupindukia iliomo ndani ya soda unawapumbaza wanywaji ili wasisikie ladha kali ya asidi iliyomo ndani ya soda.

IJUTA imegundua kuwa kiwango cha asidi kilicho ndani ya soda hakiwekwi wazi kwa walaji kwa sababu ya kuhofia kuwa wakibaini wataacha kikutumia kinywaji hicho.

Inaelezwa pia kuwa madini ya cola yaliyo ndani ya soda yana kilevi aina kafein kinachomteka mnywaji kuwa teja wa kinywaji hicho.

Tafiti za kitaalamu zimeonyesha kuwa soda inahusishwa na matatizo mengi ya kiafya kwa watoto na watu wazima, yakiwemo matatizo ya kuongezeka unene kupita kiasi, ugonjwa wa ini na mengineyo.

Utafiti uliofanywa nchini Marekani unaonyesha kuwa soda huwekewa ‘fructose’ (sukari) nyingi kupitia mfumo wa sirapu (fructose corn syrup) ambayo inaongoza kwa kusababisha magonjwa ya unene, kisukari, ugonjwa wa moyo na magonjwa mengine sugu yanayowakabili Wamarekani wengi hivi sasa na dunia kwa ujumla.

Dk. Mercola, ambaye ni mtaalamu wa masuala ya lishe asilia na tiba mbadala nchini Marekani, amekaririwa na tafiti mbalimbali zilizofanyika nchini humo akieleza kuwa kinywaji aina ya soda ni hatari kwa binadamu, sawa na mtu anayevuta sigara au zaidi, jambo alilosisitiza kuwa siyo la kutia chumvi, bali ukweli halisi.

Watumiaji wa vinywaji aina ya soda wanaelezwa kuwa wamekuwa wakinywa kiasi kikubwa cha kaboni, kafeini (dawa ya kulevya), sukari ya kupundukia na asidi kali ambayo huvuruga afya ya mtumiaji kwa kiwango cha juu.

Soda pia imebainika kutokuwa na lishe ya aina yoyote zaidi ya maji na sukari.

Uchunguzi wa IJUTA na utafiti ya wanasayansi mbalimbali duniani, umeonyesha kuwa watu wengi hawajui kuwa unywaji wa soda huwaongezea kiasi kikubwa cha madini joto.

Chupa moja ya soda yenye ujazo wa mililita 330 husababisha unene kwa kiwango cha paundi moja kwa mwezi.

Mkurugenzi wa Taasisi ya Kisukari Tanzania (TDA), Ramadhan Mongi, amepata kukaririwa na vyombo vya habari hapa nchini akieleza kuwa ugonjwa wa kisukari Tanzania umeongezeka mara sita katika siku za hivi karibuni.

Alisema miaka kumi iliyopita, hali ya kisukari ilikuwa asilimia tatu (3), lakini katika miaka ya karibuni umeongezeka mara sita.

“Tunastahili kuongeza jitihada ya kupambana na gonjwa hili la kisukari kwa gharama zote kwa sababu kisukari ni moja ya magonjwa manne yanayomaliza Watanzania,” alisema.

Utafiti uliofanyika Mkoa wa Dar es Salaam ulibaini kwamba kati ya watu watano waathirika wa kisukari, mmoja tu ndiyo hupata matibabu ya serikali.

Unywaji kwa mpigo wa kabohaidrets iliyo na sukari nyingi kwenye soda hudhoofisha seli zinazozalisha vimeng’enya tofauti na vyakula vingine na pia imebainika kuwa sukari ikiingia kwa wepesi kwenye mzunguko wa damu husababisha kongosho kuzalisha vimeng’enya vingi mwilini.

Uchunguzi wa kitabibu katika Hospitali ya wanawake ya Boston nchini Marekani na katika Chuo cha Kitabibu cha Harvard umeonyesha wanawake 51,000 hawakuwa na kisukari mwanzoni mwaka wa 1991, lakini miezi minane baadaye wanawake 741 waligundulika na kisukari.

Ripoti ya utafiti huo ilionyesha kuwa wanawake waliokuwa wakitumia kinywaji aina ya soda moja ama mbili kwa siku waliongezeka uzito maradufu na walikuwa hatarini kupata ugonjwa wa kisukari.

Pia ilionyesha kuwa soda hudhoofisha mifupa na husababisha hali ya mifupa kupuputika, hali inayomuweka mtumiaji kuwa katika hatari ya kuvunjika mifupa kirahisi.

Madhara mengine yaliyobainika kusababishwa na unywaji soda ni kupukutika kwa meno na ama kuoza. Pia soda husababisha matatizo ya figo.

Soda yenye chembe ya cola husababisha figo kuwa na mawe kwa sababu ya asidi na kemikali mbalimbali zinazofichwa vipimo vyake kwa walaji.

Madaktari bingwa wa wanamichezo wanaeleza madhara yanayosababishwa na soda mwilini kuwa ni pamoja na shinikizo la damu, uharibifu wa ini, huvurugu mfumo wa kumeng’enya chakula tumboni kutokana asidi ya kiwango cha juu iliyo kwenye soda.

Wanashauri kuwa soda haistahili kutumika kama kishawishi kwenye mchezo, kwa sababu ina madhara makubwa kwa wanamichezo kwa sababu hunyonya maji kwenye mwili na kudhoofisha mwili.

Wakati utafiti huo ukidhihirisha hayo, Taasisi ya Chakula na Dawa Tanzania (TFDA) imeshindwa kutoa tamko lolote kuhusu utafiti huo, hata baada ya kupelekewa maswali kwa maandishi yanayoomba ufafanuzi wa ubora wa vinywaji vya soda katika mwili wa binadamu.

Soda yapigwa marufuku Ughaibuni
Jumatano, Mei 15, 2013 05:22 Na Fred Okoth

Yakatazwa shuleni, watoto chini ya miaka 12
Sasa yabainika kuwa ina sumu inayoua taratibu
Yagundulika kupumbaza na kusababisha uteja


SIKU chache baada ya gazeti hili kuripoti madhara yanayosababishwa na kinywaji aina ya soda, katika utafiti wake gazeti hili limebaini mengine mapya.

Kwa mujibu wa utafiti huo, imebainika kuwa soda imepigwa marufuku kutumiwa na watoto walio na umri chini ya miaka 12 na walio shuleni katika baadhi ya mataifa ya Ulaya na Marekani, kutokana na madhara ya kiafya yanayosababishwa na kinywaji hicho.

Taarifa zilizotolewa na Shirika la Habari la The Press Television Technology Advertising and Branding (Adweek) zinazonukuu taarifa ya kampuni moja kubwa duniani inayozalisha kinywaji aina ya soda, imeamua kupambana na unene (obesity), unaosababishwa na unywaji wa soda kwa kuondoa matangazo ya vinywaji vyake kwenye vyombo vya habari.

Kampuni hiyo kupitia taarifa yake hiyo iliyotolewa katika moja ya sherehe zake, ilieleza kuwa lengo la kuondoa matangazo hayo ni kuwanusuru watoto wadogo na matumizi ya vinywaji aina ya soda vilivyobainika kuwa na madhara katika mwili wa binadamu.

Nchini Marekani, tayari imekwishapitishwa sheria inayokataza watoto walio na umri wa chini ya miaka 12, kunywa kinywaji aina ya soda.

Mwenyekiti wa Kampuni hiyo, alieleza kuwa mipango ya mbeleni ya kampuni yake ni kutengeneza kinywaji hicho kikiwa na kiwango kidogo cha Kalori na kubuni kinywaji cha aina hiyo ambacho kitakuwa hakina Kalori.

Alisema mipango hiyo itatekelezwa duniani kote ambako kinywaji cha aina ya soda kinatengenezwa na nchini Marekani tayari imekwishaanza kutekelezwa.

Aidha, Kampuni hiyo imeahidi kuweka wazi virutubisho vyote vinavyotumika kutengeneza bidhaa zake na kuahidi kutoa misaada ya hali na mali kwa nchi zote 200 duniani ambako kinywaji cha soda kinauzwa.

Mbali na Marekani, kinywaji cha aina ya Soda kimekwishapigwa marufuku shuleni katika nchi za Uingereza, Ufaransa na katika majimbo ya Los Angeles, Philadelphia na Miami nchini Marekani na kwa watu wazima matumizi yake yanaelekezwa kuwa ya kiwango kidogo sana.

Vyombo vya habari vya nchini New Zealand, mwezi Machi mwaka huu viliripoti kuwa mwanamke mmoja aliyefahamika kwa jina la Natasha Harris (31), alifariki kutokana na unywaji wa soda nyingi.

Shirika la habari la AFP la Ufaransa, liliripoti tukio hilo kwa kueleza kuwa Natasha alikuwa akinywa soda nyingi kila siku, jambo ambalo liligeuka kuwa sehemu ya maisha yake kwa kipindi cha miaka mingi.

Kwamba familia ilikuwa ikimuita teja wa soda, baada ya meno yake kuoza kwa sababu ya kunywa soda, alijifungua mtoto ambaye hakuwa na fizi jambo ambalo liligundulika baadaye kuwa lilisababishwa na matumizi makubwa ya kinywaji hicho.

“Tumegundua kwamba, kwa kuzingatia ushahidi uliopo, kama sio unywaji wa soda uliopitiliza, Natasha Harris asingekufa katika muda ule na katika hali alivyokufa

“Ripoti ya Daktari aliyechunguza maiti yake (Pathologia), iligundua kwamba ini lake lilipanuka sana, likawa na mrundiko mkubwa wa mafuta kutokana na kula sukari kwa wingi. Kuwepo kwa madini aina ya ‘potasiam’ kwa kiwango kidogo sana kwenye damu yake, pia kulitokana na unywaji wa soda.” Taarifa ya kitabibu katika Hospitali aliyofia nchini New Zealand ilieleza.

Kwa mujibu wa tafiti mbalimbali za kisayansi zilizo kwenye mitandao ya wanasayansi waliobobea duniani, unywaji wa soda humpumbaza mtumiaji na kumsahaulisha kula vyakula vyenye madini muhimu mwilini.

Moja ya andishi linalotahadharisha utumiaji wa kinywaji cha soda na kukitaja kuwa cha hatari kwa matumuzi ya binadamu, ni Jack Winkler, Profesa wa sera za lishe katika Chuo Kikuu cha Metropolitan nchini London, linaloeleza kuwa Soda ni bidhaa ya kishetani inayoua binadamu taratibu baada ya kinywaji hicho kumzalishia magonjwa mengi mwilini yanayomfanya kuwa tegemezi wa dawa.

Wakati msomi huyo akieleza hayo katika utafiti wake, Mkurugenzi wa Mamlaka ya Chakula na Dawa (TFDA) Dk. Raymond Wigenge, amelieleza gazeti hili soda siyo kinywaji hatari kwa matumizi ya binadamu kwa sababu kinatumiwa na mamilioni ya watu duniani kote.

Akizungumza na MTANZANIA Jumatano ofisini kwake wiki iliyopita baada ya kutoa ufafanuzi kuhusu madhara yanayosababishwa na kinywaji aina ya soda katika mwili wa binadamu, Dk. Wigenge alisema pamoja na changamoto zilizopo katika kinywaji hicho, taasisi yake haipingi uwepo wa kinywaji hicho sokoni.

“Soda haina shida kwa binadamu na hata mkiendelea kuandika suala hili, sisi tutaendelea kuueleza umma kwamba waendelee kupata kinywaji, hivyo kama ambavyo tumekuwa tukifanya,” alisema.

Alipoulizwa kama anakubaliana na tafiti za wanasayansi bingwa wa magonjwa ya binadamu walioeleza katika tafiti zao kuwa unywaji wa soda una madhara katika mwili wa binadamu, alisema hizo ni changamoto za kawaida, kwa sababu madhara yaliyomo kwenye soda hayamuathiri mtu mara moja bali huchukua muda mrefu.

Wakati Dk. Wigenge akieleza msimamo wake kuhusu kinywaji aina ya soda, nchini Mexico, taasisi ya El Poder del Consumidor inayojihusisha na kutetea walaji, inashinikiza Serikali ya nchi hiyo kuzilazimisha kampuni za soda kuorodhesha madini na chembechembe zote za kemikali zinazotumika kutengeneza kinywaji hicho.

Mkurugenzi wa taasisi hiyo, Alejandro Calvillo, amekaririwa na vyombo vya habari vya nchi hiyo akieleza kuwa unywaji wa soda ni hatari na hilo limethibitishwa na wataalamu wa afya duniani kuwa soda ni sumu mbaya, inauwa taratibu.

Tafiti mbalimbali za wanasayansi zinaeleza kuwa soda ina asidi aina ya ‘phosphoric’ yenye uwezo wa kuvuruga madini ya ‘calcium’ yaliyoko mwilini na kusababisha mifupa na meno kudhoofika.

Aidha, asidi aina ya ‘phosphoric’ huvuruga asidi aina ya ‘hydrochloric’ iliyo tumboni mwa binadamu na hivyo kuharibu mfumo wa kusaga chakula.

Viwanda vya soda ndio watumiaji wakubwa wa sukari na wanasayansi wanasema sukari hupandisha kiwango cha ‘insulin’ ambayo husababisha kasi ya mzunguko wa damu, ugonjwa wa moyo, kupanda kwa ‘Cholesterol, kisukari, kuzeeka mapema, ongezeko la uzito na maradhi mengine.

Aidha inadaiwa kuwa viwanda vya soda pia hutumia dawa ya kulevya aina ya kafeini. Wataalamu wanasema vinywaji vyenye kafeini, husababisha kupanda kwa mapigo ya moyo, kasi ya mzunguko wa damu na matatizo ya kizazi.

Wawili Mbaroni Maandamano ya Mange Kimambi...Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Alhamisi yya Marchh 22

Waziri Ummy Awashauri Wananchi Kwenda Vituo Vya Tiba Haraka Pindi Wanapogundua Dalili Za Ugonjwa Wa Dengue

$
0
0


WAZIRI wa Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu amewashauri wananchi kwenda vituo vya tiba haraka mara baada ya kugundua kuwa wana dalili za ugonjwa wa dengue.

Hayo ameyasema wakati alipotoa tamko juu ya kuingia kwa ugonjwa wa dengue hapa nchini mara baada ya kufunga Mkutano wa 65 wa Jumuiya ya Mawaziri wa Afya wa Nchi za Afrika Mashariki, Kati na Kusini ECSA jana  jijini Dar es salaam.

“Kuna dalili za Ugonjwa Dengue zikiwemo homa ya ghafla, kuumwa kichwa hususan sehemu za macho, maumivu ya viungo na uchovu. Dalili hizi huanza kujitokeza kati ya siku 3 hadi 14 tangu mtu alipoambukizwa virusi vya homa ya Dengue hivyo Wizara inashauri kuwa wananchi wasiwe na hofu, bali mara tu wanapoona dalili za ugonjwa waende katika vituo vya tiba " alisema Waziri Ummy.

Aidha Waziri Ummy amesema kuwa Wakati mwingine dalili za ugonjwa huu zinaweza kufanana sana na dalili za malaria hivyo basi wananchi wanaaswa kuwa, wakipata homa wahakikishe kuwa wanapima ili kugundua kama wana vimelea vya malaria au Dengue, au sababu nyingine, ili hatua stahiki zichukuliwe.

Waziri Ummy amesema kuwa ili kujikinga na ugonjwa huo ni lazima Kuangamiza mazalio ya mbu kwa kufukia madimbwi ya maji yaliyotuama au nyunyuzia dawa ya kuua viluwiluwi vya mbu kwenye madimbwi hayo pamoja na Kujikinga na kuumwa na mbu kwa  kuvaa nguo ndefu muda wote hasa nyakati za mchana.

Aidha Waziri Ummy amesema kuwa Wizara itaendelea Kuimarisha ufuatiliaji wa magonjwa nchi nzima kwa kutumia mfumo uliopo wa ukusanyaji wa taarifa (IDSR), ambapo tunaendelea kupata taarifa za kila siku juu ya mwenendo wa ugonjwa huu na Kutoa elimu kwa jamii kupitia vyombo vya habari.

Mbali na hayo Waziri Ummy amesisitiza kuwa  hakuna vikwazo vyovyote vilivyowekwa kwa ajili ya wasafiri wanaoingia na wanaotoka nchini na  Wizara itaendelea kushirikiana na wadau na sekta mbalimbali katika kufuatilia na kudhibiti ugonjwa huo.

Homa ya Dengue ni ugonjwa unaosababishwa na virusi vinavyoenezwa na mbu wa aina ya Aedes ambao ni weusi wenye madoa madoa meupe yenye kung’aa.

Mfanyakazi wa Balozi Akamatwa na Polisi

$
0
0

Polisi Mkoa wa Kinondoni wanamshikilia mfanyakazi wa ubalozi wa Syria  nchini kwa tuhuma za kumjeruhi usoni mhasibu wa ubalozi huo,  Hassan Alfaouri na kumpora Euro 93,000 (Sh237milioni).

Akizungumza leo Jumatano Machi 21, 2018 kamanda wa polisi mkoani humo, Jumanne Muliro amesema tukio hilo lilitokea Machi 19, 2018 saa nane mchana eneo la Shule ya Msingi Oysterbay, jijini Dar es Salaam.

Amesema siku hiyo, mhasibu huyo akiwa katika gari na dereva wake wakielekea Benki ya Azania tawi la Mazdu House lililopo mtaa wa Samora wakipeleka fedha hizo, walipofika mtaa wa Zambia dereva huyo alianza kuendesha gari taratibu.

Amesema baada ya kupunguza mwendo, alisimama  na kuzima gari ghafla walitokea watu watatu; mmoja kati yao alikuwa na kipande cha nondo mkononi  na kuingia katika gari hilo na kumtaka mhasibu huyo awape fedha.

Muliro amebainisha kuwa uchunguzi wa awali unaonyesha kuwa tukio hilo lilipangwa na baadhi ya wafanyakazi wa ubalozi wasio waaminifu, akiwamo dereva huyo ambaye wakati uporaji ukiendelea, hakutoa msaada wowote.

"Walivyoona anakawia kutoa fedha walimjeruhi usoni kwa kipande cha nondo, walimshusha dereva kwa nguvu na kuondoka na gari hilo,” amesema.

Amesema baada ya tukio hilo, polisi walianza msako  na kuikuta gari hiyo ikiwa imetelekezwa Msasani Bonde la Mpunga.

Kutana na Mtatibu Mongwa Anayesafisha Nyota na Kutoa Pete za Bahati

$
0
0
KWA WALE WENYE KUHITAJI TIBA

Husafisha nyota na kutoa Pete za bahati na kwawale walio sumbuka kwaajili ya matibabu na hawakufanikiwa chochote sasa njoo ujionee miujiza hapo kwahapo bila malipo yoyote malipo baada yakazi napia humpa mtu jini la mali kwayule anaye taka kumiliki bila mashariti yoyote
Tunatibu magonjwa mbalimbali yaliyo shindikana mpenzi aliye kukimbia nakumrudisha kwa masaa 24 tu napia natoa dawa za nguvu za kiume kuurefusha uume paka pale unapotaka .

Natoa dawa za biashara na mvuto ==tunatoa dawa zauzazi kwa wale kina mama wenye matatizoya uzazi walio angaika kwa muda mrefu bila kupata mafanikio yoyote njoo umalize tatizo lako sasa
Natoa mazindiko yanyumba na mwili biashara na mvuto kazini

Kupandisha nyota ili kungaa kupandishwa cheo kazini kurudisha mali zilizo pote zilizo ibiwa kuzulumiwa
Kesi zilizo shindikana uzimaliza mara moja namengine mengi ya siri piga simu

+255 764291657

Label ya Young Dee Yalia na BASATA Kwa Kufungia Wimbo wa Bongo Bahati Mbaya

$
0
0

Label ya King Cash ambayo inafanya kazi na rapa, Young Dee imeandika barua ya wazi kwa Baraza la Sanaa Taifa BASATA baada ya wimbo ‘Bongo Bahati Mbaya’ wa msanii wao huyo kufungiwe kwa kigezo cha kukosa uzalendo.

Uongozi wa label hiyo umetoa taarifa hii

Kama mwekezaji kupitia tasnia ya muziki wa Bongo Fleva napenda kufikisha kilio hiki kwenu BASATA kwa sababu pale muziki wa msanii wa King Cash unapofungiwa inamaanisha biashara ya King Cash imefungiwa, Hii inamaanisha nini? kama ikifungiwa miziki zaidi ya 100 kuna familia nyingi zitaathirika kupitia mnyororo huo.

Ukiangalia upande wa biashara ya King Cash, kampuni ya kitanzania inayoongeza ajira, kwa kujiari na kuajiri wengi zaidi ili kuunga mkono sera ya serikali ya ‘hapa kazi tuu’ baada yake mnaona kama ni kitu kidogo cha kukosoa tu kwa juu juu na kufungia bila kuangalia ni ubunifu wa namna gani ulitumika katika utunzi wa nyimbo ya moja ya msanii, tena mmefungia kwa kigezo cha wimbo haiendani na uzalendo, kweli jamani tutafika kwa namna hii.

Kama hamjui kila nyimbo tunayotoa ina bajeti yake ya kuizalisha na kuitangaza, na matarajio ya kipato kitakacho zalishwa na nyimbo hiyo ambapo faida itatutumika kuendesha maisha ya msanii na kutengeneza nyimbo nyingine. Sasa mnapo fungia nyimbo zetu inamaana tuache hii kazi ya muziki na familia zetu ziishi vipi?, kingine hebu tujifunze kupitia nchi jirani tunaweza kuwa na busara katika hili na ushirikiano ni jambo katika kukuza ustawi wa sanaa zetu.

Asante sana.
King Cash
Dar es salaam.

VIDEO: Ebitoke na Bwana Mjeshi Kufuata Nyayo za Diamond

$
0
0

Kundi la Timamu ambalo lina wakali kibao kwa upande wa uchekeshaji kama Ebitoke na Bwana Mjeshi wanatarajia kuachia filamu yao mpya inayokwenda kwa jina la Sema nchini Kenya. Uzinduzi huo utafanyika mwanzoni mwa June mwaka huu.

Wasikilize hapa.



TCRA Kufuatilia Maudhui ya Mahijiano ya Diamond na Kituo cha Times FM

$
0
0

Baada ya Waziri wa Habari , Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dkt. Harrison Mwakyembe kusema kwamba amesikitishwa na kauli za Diamond alizozitoa kupitia kipindi The Playlist cha Times Fm dhidi ya Naibu Waziri wake, Juliana Shonza, Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) imesema kamati yake ya maudhui inafuatilia mahojiano ya mwanamuziki huyo aliyoyafanya katika kituo hicho.

Akiongea na mtandao wa gazeti la Mwananchi leo, Ofisa Mkuu Idara ya Utangazaji ya mamlaka hiyo, Andrew Kisaka amesema wamechukua uamuzi huo kwa kuwa mahojiano hayo yamefanyika katika kituo wanachokisimamia.

Katika mahojiano hayo, Diamond alimjibu Naibu Waziri wa Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo, Juliana Shonza kutokana na Serikali kuzifungia nyimbo 15 mwezi uliopita, zikiwemo mbili za mwanamuziki huyo.

Kisaka amefafanua kuwa kiutaratibu wao wanaangalia zaidi chombo ambacho wamekipa leseni na kwamba, masuala mengine yatashughulikiwa na mamlaka nyingine.

Amesema suala hilo kwa sasa linafanyiwa kazi na kamati ya maudhui na kuahidi kulitolea ufafanuzi siku za hivi karibuni akiwataka wananchi kuwa na subira.

Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo DKt. Harrison Mwakyembe amesema si busara kwa Diamond kushindana na serikali endapo ana ushauri wowote ni vema akauwasilisha kwa njia sahihi na si kumshambulia Naibu Waziri kwa dharua na kejeli.

Roma Aipigia Magoti BASATA “Mtaniua Njaa Jamani!”

$
0
0

Msanii wa muziki wa hip hop, Roma Mkatoliki amefunguka kwa mara ya kwanza ikiwa ni mwezi mmoja toka afungiwe na Baraza la Sanaa la Taifa kujihusisha na shughuli za sanaa kutokana na kudaiwa kutoa wimbo ‘Kibamia’ ambao hauna maadili.


Basata wamesema walimfungia msanii huyo baada ya kutakiwa na baraza hilo kubadili wimbo huo lakini hakufanya hivyo na kila alivyoita hakuweza kutokea.

Akiongea katika kipindi cha XXL cha Clouds FM Jumatato hii, Roma akiwa na mwanae, Ivan amesema anawaomba BASATA kumpungia adhabu kwani hali yake ya kiuchumi siyo nzuri.

“Haya yote yanaongeleka, lengo ni Roma aendelee kufanya muziki wake kwa sababu muziki unamsaidia kama ajira, nyuma ya Roma kuna watu ambao anawasaidia. Kwahiyo wakati mwingine naomba ieleweke kwamba tufanye tu Roma aendelee na muziki wake ili maisha yake yaendelee,” alisema Roma.

Aliongeza,”Tena nikitoka hapa nitawasiliana na Katibu mkuu wa Basata najua atanisikiliza, pia nimesikia Jumatatu kuna mkutano wa wasanii wote na BASATA utafanyikia pale BASATA, zote ni katika njia ya kwenda kuyaongelea haya mambo, lengo tuwe chombo kimoja,

Akiwa katika mahojiano hayo na mtoto wake, Ivan aliulizwa na matangazaji wakipindi hicho kwanini hakwenda shule, na mtoto alisema hajaenda shule kutokana na tatizo la ada.

“Sijakwenda shule leo baba hana ada,” alisema Ivan mb

Amber Lulu Afunguka Anavyomchukia Baba Yake

$
0
0

Video vixen maarufu aliyegeukia sanaa ya Bongo fleva Amber Lulu amekiri kuwa amemtosa Baba yake mzazi na hataki hata kumuona.

Amber Lulu amefunguka hayo wakati anaelezea changamoto alizozipitia katika maisha yake baada ya Baba yake mzazi kuwakimbia na kumuacha yeye kama mtu pekee ambaye alitakiwa kuiangalia familia yake hasa mama yake ambaye alikuwa mgonjwa.

Amber Lulu ameongelea uhusiano aliokuwa nao na Baba yake mzazi ambapo amekiri katika umri mdogo alianza kushika majukumu mazito ya kuielea familia yake hivyo ilimbidi ajiingize katika biashara mbali mbali ili aweze kupata pesa.

Kwenye mahojiano aliyofanya na Clouds Fm, Amber Lulu aliongea haya kuhusiana na changamoto alizozipitia:

"Kipindi hiko nilikuwa bado niko shule lakini ilikuwa likizo hata ya wiki mbili nilikuwa nakuja Dar kufanya kazi maana tulikuwa tunahitaji pesa na mama Yangu alikuwa mgonjwa na ndio baba alikuwa kashatukimbia, nakumbuka msanii alikuwa anaitwa Pasha alinitumia kwenye video yake akanilipa shilingi elfu hamsini ambayo sikutumia hata senti nikaenda kumpa Mama yangu ambaye alikuwa anahitaji lakin moja na nusu ya matibabu”.

Lakini Pia Amber Lulu ameongelea uhusiano wake na Baba yake mzazi ambaye alimkimbia:

"Wanasema mzazi ni mzazi lakini mimi Baba yangu alinitelekeza kaja kunitafuta nilivyotoa wimbo wangu wa Watakoma alafu ananiomba hela kusema kweli aliniumiza kwa sababu hajanitafuta kama miaka kumi halafu anakuja kunitafuta kwa sababu anataka hela , dah kusema ukweli simpendi baba yangu hata kidogo na sitaki hata kumuona”

Maboresho Katika Application ya Udaku Special.... Download Upya Kwenye Simu yako Kupata Habari Zetu Haraka

$
0
0
  
Kuna Maboresho Mapya Yamefanyika Hatika Application Yetu ya UDAKU SPECIAL. Maboresho hayo yamelenga kukufanya upate habari zetu kwa wepesi zaidi kama vile Magazeti kuliko ilivyo sasa.

Chakufanya, Ingia PlayStore, Download Upya Application yetu

Tumekurahisishia;

==>>Unaweza Kuidownload << kwa Kubofya Hapa>>  

Nafasi za Ajira Zilizotangazwa Leo

Viewing all 104789 articles
Browse latest View live




Latest Images