Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104789 articles
Browse latest View live

Kiongozi wa ACT-Wazalendo Aliyepinga Waraka wa Maaskofu Avuliwa Uanachama

$
0
0
Kiongozi wa ACT-Wazalendo Aliyepinga Waraka wa Maaskofu Avuliwa Uanachama KioKiKKKKKKngozi wa Ngome ya Vijana ambaye ni Mratibu wa Masuala ya Elimu wa chama cha ACT-Wazalendo, Philipo Mwakibinga amevuliwa uanachama na chama hicho kutokana kupinga tamko la Maaskofu wa KKKT ambalo chama hicho kinaunga mkono.


Chama hicho kimesema amekuwa akitoa taarifa zinazokinzana na misimamo ya chama na kutolea mfano pia wakati wa kifo cha mwanafunzi wa Chuo cha Taifa cha Usafirishaji (NIT), Akwilina Akwilin ambapo chama kimesema alitoa tamko ambalo lilikuwa kinyume na msimamo wa chama.

Mwakibinga ambaye pia ni Mkurugenzi wa Utafiti wa Tasisi ya Watetezi wa Rasilimali wasio na Mipaka WARAMI, aliupinga waraka huo kwa madai kuwa ulikuwa wa kisiasa wenye lengo la kukososa utendaji wa serikali na kuleta hofu kwa jamii.

ACT Wazalendo kupitia kwa Katibu Uenezi wa Ngome ya Vijana, Karama Kaila kimesema kuwa kama hajaridhika na uamuzi huo anaweza kupeleka suala lake katika kamati ya maadili ya chama hicho ili liweze kushungulikiwa zaidi

Kiongozi wa Mtandao wa Kuiba Fedha Kwenye Mabenki Duniani Atiwa Mbaroni

$
0
0
Kiongozi wa Mtandao wa Kuiba Fedha Kwenye Mabenki Duniani Atiwa Mbaroni
Leo March 26, 2018 Nguli wa kuiba kwa kutumia mtandao duniani amekamatwa na Jeshi la Polisi nchini Hispania kwa kutuhumiwa kuiba Paundi milioni 870 ambayo ni sawa na Shilingi trilioni 2.49.

Mtu huyo anasemekana kuwa kiongozi wa kundi kubwa la wezi hao wa mtandao duniani ambao walikuwa wanaendesha kampeni za software za Carbanak na Colbat ambazo zilikuwa zinaibia mabenki.

Mamlaka zinaeleza kuwa kundi hilo lilianza mwaka 2013 na liliibia benki takribani 100 kwa wakati huo. Pesa hizo ziliibwa kwa kupitia njia za benki za kuhamisha fedha ambazo zinatolewa moja kwa moja kwenye mashine za kutolea fedha (ATM).

Vurugu Zaibuka Mbeya Mauaji ya Kijana Anayedaiwa Kuuliwa na Polisi

$
0
0
Vurugu Zatanda  Mbeya Mauaji ya Kijana Anayedaiwa Kuuliwa na Polisi
KIFO cha kutatanisha cha kijana anayejishughulisha na uuzaji wa machungwa jijini Mbeya, kimeibua vurugu kubwa za vijana wenzake kutokana na kuhusishwa na Jeshi la Polisi.

Kijana huyo aliyefahamika kwa jina la Allen Mapunda (20), alifariki dunia, siku moja baada ya kukamatwa na kukaa mahabusu kisha kupelekwa hospitali.

Alifia hospitali alikopelekwa kupatiwa matibabu ya majereha baada ya kukamatwa kwa tuhuma za uhalifu ambazo hazijawekwa wazi.

Mapunda alifariki dunia katika Hospitali ya Rufani ya Kanda ya Mbeya, baada ya kukaa kituo cha polisi kwa siku moja.

Inadaiwa kuwa kijana huyo mkazi wa Mtaa wa Iyela II anayefanya shughuli zake za ujasiriamali katika Soko la Sido jijini Mbeya,  kabla ya mauti kumkuta alikamatwa Machi 24,  mwaka huu majira ya saa nne usiku katika eneo la kucheza ‘pool’ Mtaa wa Maendeleo na kumpeleka hadi Kituo Kikuu cha Polisi.

Inadaiwa Mapunda alikuwa na vijana wenzake wakicheza mchezo huo na baada ya kuwaona polisi aliwaambia wenzake wakimbie, lakini wote walitiwa mbaroni.

Habari zaidi zinaeleza kuwa Mapunda alikaa kwa siku moja na kesho yake alidhaminiwa na ndugu ambao waliamua kumpeleka hospitali kwa ajili ya matibabu kutokana na majeraha aliyoyapata.

Kwa mujibu wa mama yake mlezi, Alice Mapunda, marehemu alionekana na majeraha mkononi na kichwani ambako alikuwa akivuja damu huku akilalamikia maumivu.

Baada ya hali ya marehemu kuwa mbaya katika Hospitali ya Rufani ya Mkoa, walimpa rufani ambapo alihamishiwa Hospitali ya Rufani ya Kanda ya Mbeya ambapo, alifariki dunia muda mfupi wakati akiendelea kupatiwa matibabu.

VURUGU ZAIBUKA

Kufuatia kifo cha kijana huyo, baadhi ya vijana wa Iyela waliamua kuandamana kupinga tukio hilo, wakidai kuwa linahusishwa na polisi, hivyo walianza kuwatafuta polisi wanaoishi eneo la kata hiyo na viongozi wa mtaa kwa nia ya kulipa kisasi.

Miongoni mwa viongozi walikumbwa na kadhia hiyo ni Mwenyekiti wa Iyela II, Boaz Kyejo, ambaye alivunjiwa dirisha la nyumba yake wakimtuhumu kuhusika  kuwaita polisi kwa ajili ya kufanya doria ya kuwakamata vijana  wa kata hiyo baada ya kifo cha Mapunda.

Hata hivyo, Kyejo alisema hahusiki na tukio la kuwaita polisi wala doria na hata kifo cha kijana huyo hakuwa na taarifa nacho.

“Vijana wameharibu mali nyingi za mtaa huu, ikiwamo kuvunjwa kwa meza za soko na mali nyingine zilizokuwa sokoni hapo,” alisema Kyejo.

Kutokana na vurugu hizo, polisi wanadaiwa kuingilia kati kutumia nguvu ikiwamo kulipua mabomu.

Kwa upande wake mama mdogo wa marehemu, Justina Kilasa, alisema marehemu hakuwa na tabia mbaya, hivyo kitendo cha kukamatwa kwa madai ya kuhusika na uhalifu sio cha kweli, kutokana na marehemu kuwa na tabia njema.

“Mwanangu hakuwa mgomvi, alikuwa hajihusisha na tabia zozote mbaya, akitoka kwenye kibarua chake cha kuuza machungwa kule Sido anaenda ibadani na kurudi nyumbani,” alisema na kuongeza:

“Kwa kweli kifo hiki kimetushtua, mbaya zaidi Jeshi la Polisi limepiga mabomu ya machozi hapa msibani.”

Kilasa alisema kuwa mwili wa marehemu unahifadhiwa hospitali na wanasubiri kukabidhiwa kwa ajili ya maziko.

Mtendaji wa Kata ya Iyela, Anna Supalika, alisema amesikitishwa na uharibifu uliofanywa na vijana hao na kwamba hasara iliyopatikana haijabainika na kwamba shughuli za kiofisi zimesimama.

KAULI YA POLISI

Alipoulizwa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya, Mohammed Mpinga, alikiri kutokea kwa tukio hilo na kwamba taarifa rasmi ataitoa baada ya uchunguzi kukamilika.

Colabo za Baraka The Prince, Sauti Sol na Cassper Zaota Mbawa

$
0
0
Colabo za Baraka The Prince, Sauti Sol  na Cassper Zaota Mbawa
Ulikuwa unahamu ya kuzisikia kolabo za Barakah The Prince alizofanya na Sauti Sol na Cassper Nyovest? Hilo unatakiwa kusahau tena

Barakaha aliwahi kusema kuwa tayari ameshafanya kolabo kibao na mastaa wakubwa Afrika na kutuhakikishia kuwa ngoma hizo zitapatikana kwenye albamu yake, lakini kwa sasa ameonyesha ni vigumu kuzisikia tena ngoma hizo.

Akiongea na mtangazaji wa Jembe FM, JJ amesema, “Hizo zilikua ni project ambazo zilikuwa under Rockstar kipindi ambacho nilikuwa yao. Ni nyimbo ambazo wanazishikilia wao, walinilipia kila kitu kutoka hapa na kwenda Kenya na kila kitu Production, Producer na kila kitu. Sauti Sol makubaliano yao mikataba. Tulisaini mkataba kabla hatujarekodi, kwa hiyo ilikuwa ni product ya kwao kina Seven.”

“Nimejaribu kuongea nao kupatiwa hizo nyimbo, kulikuwa na ngoma ya Cassper kuna Sauti Sol, wamezing’ang’ania kwa sababu zao wao,” ameongeza.

Baada ya Kuumia Mazoezini Jana Jonas Mkude Haya Hapa Majibu ya Daktari

$
0
0
Baada ya Kuumia Mazoezini Jana Jonas Mkude Haya Hapa Majibu ya Daktari
Kiungo mchezaji wa Simba, Jonas Mkude, aliumia jana wakati kikosi hicho kikijiandaa na mazoezi kuelekea mchezo ujao wa ligi dhidi ya Njombe.

Mkude aliumia wakati akiwania mpira na kiungo mshambuliaji, Mzamiru Yassin na kuepelekea kuanguka chini kisha kutolewa nje ya Uwanja wa Boko Vetarani.

Kufuatia kuumia huko, kwa mujibu wa Afisa Habari wa Simba, Haji Manara, Daktari wa timu hiyo, Yassin Gembe, alisema Mkude hajapata maumivu makali, na anaweza akarejea baada ya siku mbili mpaka tatu.

Wakati Simba inajiandaa kuivaa Njombe Mji, Aprili 3 2018, kumekuwa na hofu kubwa kwa mashabiki kama ataweza kurejea mapema, japo majibu ya Daktrari yameeleza hatachukua muda mrefu.

Augustine Mrema Akunwa na Muziki wa Daimond "Nampenda sana Daimond Huyu Mtoto Anajua Kuimba"

$
0
0
Augustine Mrema Akunwa na Muziki wa Daimond "Nampenda sana Daimond Huyu Mtoto Anajua Kuimba"
Mwenyekiti wa Chama cha TLP, Augustine Mrema amesema yeye ni miongoni kwa watu ambao wamekuwa wakifuatilia muziki wa wasanii wa hapa nchini na kati ya watu ambao wanamkuna ni Naseeb Abdul maarufu kama Diamond.

Mrema amesema kwamba anapenda sana nyimbo za mwanamuzi huyo na kwa muda mrefu amekuwa akizifuatilia.

“Nampenda sana Diamond si ndiyo yule aliyeimba ‘zilipendwa huku akitutaja mimi na Lipumba? Huyu mtoto anajua kuimba,”anasisitiza.

Mrema amesema kuwa wimbo huo ametokea kuupenda kwa kwa sababu unaonyesha hali halisi ya maisha yake sasa kwa kuwa ni ukweli usiopingika kwamba yeye na Lipumba sasa ni zilipendwa.

“Kweli tumekuwa wazeee, wakati wetu umefika na sasa tunatakiwa kuwapisha vijana waendeleze gurudumu lakini usifikirie mimi mzee ukajua sisikilizi muziki wa kizazi kipya nasikiliza zote na ninafurahi sana wanafanya kazi nzuri,”ameongeza.

Wolper: Sitoi Kiki Kuhusiana na Ishu ya Brown na Nisha

$
0
0
Wolper: Sitoi Kiki Kuhusiana na Ishu ya Brown na Nisha
Muigizaji wa Bongo movie na mfanyabiashara maarufu Jacqueline Wolper ameibuka na kuweka wazi hana mpango wa kuwapa kiki Nisha na Brown walioanika penzi lao hivi karibuni.

Wiki iliyopita msanii Salma Jabu ‘Nisha’ alianika Hadharani Penzi lake na Ex boyfriend wa Wolper anayejulikana kama Brown jambo lililowashangaza watu wengi hasa kwa sababu ya urafiki wa Wolper na Nisha.

Gazeti la Ijumaa Wikienda linaripoti kuwa Nisha na Brown walianza kunyemeleana tangu Brown akiwa na Wolper Lakini pia inasemekana wawili hao walikuwa wanawasiliana kwa siri siri Jambo lililosababisha migogoro na Wolper.

Baada ya stori hizi kutrend sana Wolper alitafutwa ili kutaka kujua kama alikuwa ana taarifa kuwa alinyakuliwa na Nisha:

"Jamani mimi sijui lolote, niko bize na cherehani yangu na mambo mengine hayanihusu kabisa lakini Sasa hivi sitoi kiki kwa mtu yoyote, niko bize na mambo yangu, mimi mambo ya watu hayanihusu kabisa”.

Nisha na Brown wamekuwa waki posti video na picha Kwenye mitandao ya kijamii kuonyeshana mahaba na hata Brown kafuta tatoo ya Wolper Kifuani kwake na kumuweka Nisha.

Breaking News: Rais Magufuli Awatumbua Wakurugenzi Wawili

$
0
0
Rais Magufuli Amuagiza Waziri  Kuwasimamishwa Kazi Mkurugenzi wa Kigoma Ujiji na Pangani
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dr,John Pombe Magufuli amemuagiza Waziri wa TAMISEMI Seleman Jafo kuwasimamisha kazi Wakurugenzi wawili wa Kigoma Ujiji na Pangani kwa sababu ya kupata hati chafu katika ripoti ya CAG iliyowasilishwa leo.

“Kuna Wilaya mbili, Halmashauri Mbili zina hati chafu, Mimi nafikiri Kigoma Ujiji na Pangani, Mimi nafikiri saa nyingine tuchukue hatua kwa vile Waziri wa TAMISEMI upo hapa WAKURUGENZI wa Wilaya hizo WASIMAMISHWE kazi leo” -Rais Magufuli

Kutana na Mtabibu Mwenye KUBRI kutoka kwa ALLAH issa simba said Mtabibu wa Nyota za Binadamu na Dawa za Asili

$
0
0
Kutana na Mtabibu Mwenye KUBRI kutoka kwa ALLAH issa simba said Mtabibu wa Nyota za Binadamu na Dawa za Asili ya Africa Mwenye UWEZO Kubaini tatizo lako Pindi tu Utakapo Fanya Mawasilino Kupitia Wasaa Husika..JE UNASUMBULIWA NA Mapenzi? (Umeachwa na Umpendae,Awe Mume,Mke na Bado unampenda?Na Umejaribu Sehemu nyingi Bila Mafanikio?Wasilina na Maalim Hussein Ujione muujiza wa Papo kwa Papo.. anauwezo WA KURUDISHA MAHUSIANO NA KUIMARISHA NDOA YAKO NDANI YA SAA 12 TU. Umekimbiwa na Mumeo,mkeo au Mpenzi na anaishi na mtu mwingine? Muone akutatulie Anauwezo wa Hali ya Juu wa Kusambalatisha Mahusiano yao Endapo utafata Atakacho kuelekeza.
Atamfanya Atimize Ahadi zote kwa Muda Mfupi.

Issa simba said Anatumia Jina la Muhusika au Picha Kumaliza Tatizo lako..
Anatibu kwa Kutumia Vitabu vya QUR-AN Dawa za Asili za Africa,Dawa za Kiarabu na Majini.Anatafsiri Ndoto. Kushinda BAHATI NASIBU, KUSAFISHA NYOTA. Mvuto wa Mwili na BIASHARA, Kinga ya Mwili,ZINDIKO za Nyumba.MIGUU Kufa GANZI.Kufungua KIZAZI kwa wale walio fungwa kwa njia za KISHIRIKINA. Anakupa Jini la Mali kwa yule anaehitaji Utajiri BILA MASHARTI. Nguvu za KIUME, Humaliza Kesi zilishindika ndani ya siku 14 tu..na mengi zaidi

+255 622588038au 0679119679 au +255 764318107

NB: TIBA KWA DINI ZOTE NA IMANI ZOTE...

Mwenyekiti UVCCM Amvaa Waziri Shonza "Mnawafungia Kina Roma, Daimond Mtaimba Nyie"

$
0
0
Mwenyekiti UVCCM Amvaa Waziri Shonza "Mnawafungia Kina Roma, Daimond Mtaimba Nyie"
Kufuatia sakata la kufungiwa kwa baadhi ya wasanii na nyimbo zao, akiwemo Roma Mkatoliki, Diamond Platnumz, Snura na wengine, Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM), Kheri James, amekerwa na maamuzi hayo yaliyofanywa na Basata na Wizara ya Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo, kupitia kwa Naibu wake, Juliana Shonza.



Akizungumza jana Mjini Dodoma, Kheri James alieleza masikitiko yake na kusema kuwa wizara hiyo inarudisha nyuma maendeleo ya wasanii ambao wengi wao ni vijana wanaojitafutia kipato kupitia tasnia hiyo.



“Mmemfungia Roma, mmemfungia Diamond na wengine, kila anaenyanyuka mamkata mguu, hivi mnavyowafungia mtaimba nyie?



“Kama wizara itendelea na tabia hiyo ya kuwafungia wasanii, na wao ndio viongozi wa sanaa je watamsimamia nani wakishawafungia wote?” alihoji Kheri.

Timbulo Awapa Makavu Wanaoshobokea Mali Zake

$
0
0
Timbulo Awapa Makavu Wanaoshobokea Mali Zake
Msanii wa BongoFleva anayetamba na kibao chake kipya cha 'Post', Timbulo amefunguka na kuwataka watu wasipagawe na vitu anavyokuwa anaviweka katika mitandao ya kijamii hasa hasa magari kwa madai sio ya kwake huwa anaazima ili apigie picha.


Timbulo amebainisha hayo kupitia kipindi cha eNewz inayorushwa na tinga namba moja kwa vijana EATV baada ya watu wengi kujiuliza maswali mengi kuwa anapata wapi jeuri ya kubadilisha magari ya kifahari kila uchao wakati haonekani hata kufanya 'show' msanii huyo.

"Mimi ni msanii tu, halafu yale magari watu wasipagawane nayo ninayoyaweka instagram, ni magari ya ma-boss wakina Chief Kiumbe. Kwa hiyo wasipagawe na kila wanachokiona ukurasa wangu wa kijamii maana vingine vinakuwaga ni ku-entertain tu, ndio maana hatupendi hata kuweka wazi magari ya watu", amesema Timbulo.

Idriss, Vanessa Mdee Watajwa Katika Tuzo za Mitindo Nigeria

$
0
0
Idriss, Vanessa Mdee Watajwa Katika Tuzo za Mitindo Nigeria
Msanii wa muziki wa Bongo Fleva, Vanessa Mdee na Mchekeshaji Idris Sultan ni miongoni mwa Watanzania waliofanikiwa kutajwa kwenye tuzo za mitindo nchini Nigeria za Nigeria Icons Fashion Awards – African Diaspora 2018.

Tokeo la picha la vanessa Mdee idris sultan
Idris Sultan na Vanessa Mdee

Watanzania wengine watakaopeperusha bendera ya Tanzania kwenye tuzo hizo ni Wanamitindo Hamissa Mobetto, Sheria Ngowi,  Ben Breaker, Richard George Maliti na  Shawn Kieffer.

Vanessa Mdee ametajwa kwenye kipengele cha Most Stylish Female Artiste of the Year ambapo atapambana na Yemi Alade, Tiwa Savage, Nadia Nakai na Nsoki Neto.

Kwa upande wa Idris Sultan yeye atachuana na Wanaijeria wanne kwenye kipengele cha Most Stylish/Dressed Celebrity of the Year (Male).

Upigaji wa kura wa tuzo hizo utaanza Aprili 10, 2018 ambapo njia ya kupiga kura itatanjwa baadaye .

TAZAMA ORODHA KAMILI YA TUZO HIZO NA VIPENGELE VYOTE VILIVYO ORODHESHWA.

BEST DRESSED MALE MEDIA PERSONALITY OF THE YEAR – African Diaspora

1. Katleho Sinivasan (South Africa)
2. Uti Nwachukwu (Nigeria)
3. jamal Gaddafi (Kenya)
4. George Ndirangu (Rwanda)
5. Denola Grey (Nigeria)

MALE FASHIONISTA OF THE YEAR – African Diaspora

1. Eddie Kirindo (Kenya)
2. Noble Igwe (Nigeria)
3. Prince Thabiso Mkhize (South Africa)
4. Josef Adamu (Nigeria)
5. Sir Abner (South Africa)

FEMALE FASHIONISTA OF THE YEAR – African Diaspora

1. Stefani Roma (Kenya)
2. Sharon Ojong (Nigeria)
3. Antonia Shinana (Namibia)
4. Didi Olomide (Congo)
5. Hamisa Mobeto (Tanzania)

MOST STYLISH /DRESSED ACTRESS OF THE YEAR – African Diaspora

1. Mercy Aigbe (Nigeria)
2. Juliet Ibrahim (Ghana)
3. Genevieve Nnaji (Nigeria)
4. Yvonne Nelson (Ghana)
5. Rita Dominic (Nigeria)
6. Omotola Jalade Ekeinde (Nigeria)

MOST STYLISH /DRESSED ACTOR OF THE YEAR – African Diaspora

1. Jim Iyke (Nigeria)
2. Sama Ndango (Cameroon)
3. John Dumelo (Ghana)
4. Mike Ezuruonye (Nigeria)
5. Ken Erics (Nigeria)

FASHION ICONS OF THE YEAR : African Diaspora

1. Soares Anthony (Nigeria)
2. Frank Oshodi (Nigeria)
3. Yomi Casual (Nigeria)
4. Yemi Osunkoya (Nigeria)
5. Lola Faturoti (Nigeria)
6. Ohima Atafo (Nigeria)

MALE FASHION ENTREPRENEUR OF THE YEAR – African Diaspora

1. Mark Essien (Nigeria)
2. Isaac Oboth (Uganda)
3. Tonye Rex Idaminabo (Nigeria)
4. Voule Yaovi Akpedze (Togo)
5. Adii Pienaar (South Africa)
6. Nick Kaoma (South Africa)
7. Stephen Sembuya (Uganda)
8. Edose Ohen (Nigeria)

FEMALE FASHION ENTREPRENEUR OF THE YEAR – African Diaspora

1. Uche Pedro (Nigeria)
2. Clarisse Iribagiza (Rwanda)
3. Catherine Mahugu (Kenya)
4. Elizabeth Kperrum (Nigeria)
5. Isoken Ogiemwonyi (Nigeria)
6. Banke Kuku (Nigeria)
7. Eseoghene Odiete (Nigeria)
8. Kunmi Otitoju (Nigeria)
9. Jordan Smith (Nigeria)

FASHION BEAUTY QUEEN OF THE YEAR – African Diaspora

1.) Ntombifuthi Gumede (South Africa)
2.) Emmanuella Undie (Nigeria)
3.) Modesta Okeke (Nigeria)
4.) Florence Mantey (London)

SPECIAL AWARDS CATEGORIES

1.) NiFA – African Diaspora Patron
2.) NiFA – African Diaspora Merton
3.) NiFA – African Diaspora Ambassador
4.) NiFA – African Diaspora Hall Of Fame
5.) NiFA – African Diaspora Achiever
6.) NiFA – African Diaspora Special Recognition Honors

★ ABOUT NIGERIA ICONS FASHION AWARDS

NiFAwards honors and recognizes people in the business of fashion in their career, being promising for the future, for exceptional contributions in creativity and development supporting the department of fashion and its mission to advance the fashion world, economic and encourage fashion in the world.

★ THE OBJECTIVE OF THE NIGERIA ICONS FASHION AWARDS

* To Encourage Excellence In The Business Of Fashion.

* To Inspire People Of All Ages Through The Example Of Entrepreneurship.

* To Highlight For The General Public The Accomplishments Of The Fashion Practitioners Of The African Diaspora Community

LHRC Wampinga Waziri Nchemba Matumizi ya Viboko Shuleni

$
0
0
LHRC Wampinga Waziri Nchemba Matumizi ya Viboko Shuleni
Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC), kimetofautiana na kauli ya Waziri wa Mambo ya Ndani, Dk. Mwigulu Nchemba ya kutaka walimu kutumia adhabu ya fimbo kuweka nidhamu kwa wanafunzi shuleni

Akizungumza katika harambee ya ujenzi wa mabweni ya Shule ya Sekondari Lulumba Wilaya ya Iramba mkoani Singida, Dk. Nchemba alisema walimu wanatumia fimbo kunyoosha nidhamu za wanafunzi, ili kutengeneza hatima ya nchi.

Alisema wakati walimu wakitekeleza majukumu yao ikiwamo kunyoosha nidhamu kwa wanafunzi kwa kutumia fimbo, wapo baadhi ya watu wamekuwa wakiwalalamikia na kuwataka wawaache watekeleze majukumu yao.

“Wakati walimu wananyoosha nidhamu za wanafunzi, wapo watu wengine huwalalamikia tu, na hawajui kwamba kinachofanyika ni kwa manufaa yetu.

"Niwaombe kwenye kutumia mifano tumieni mifano na kwenye kutumia fimbo fanyeni hivyo, ili kutengeneza taswira ya nchi yetu,” alisema Dk. Mwigulu.

Akizungumzia kauli hiyo, Mkurugenzi Mtendaji wa LHRC, Dk. Hellen Kijo Bisimba, amesema kutumia fimbo kwa mwanafunzi hakuwezi kusaidia kumjengea nidhamu.

Pia, amesema kutumia adhabu hiyo kunaweza kuwa chanzo cha kurudisha nyuma maendeleo yao kielimu.

“Ni kweli kwamba walimu wanapaswa kuachwa watekeleze majukumu yao bila kuingiliwa, lakini linapokuja jambo la adhabu au kujenga nidhamu kwa wanafunzi lazima uangaliwe mfumo unaotumika,” alisema Dk. Kijo Bisimba na kuongeza:

“Zipo adhabu ambazo mwanafunzi anaweza kupewa akikosa, lakini si kwa kuchapwa fimbo. Unaweza ukafikiri ukimchapa ndio unamjenga, lakini kumbe ndio unambomoa zaidi.

"Nasema hivyo kwa sababu unapoanza kumchapa mwanafunzi hawezi kufanya vizuri tena darasani. Mimi namuomba waziri a-deal (ashughulike) na mambo ya wizara yake, ya elimu ayaache.”

Kim Jong-un Amefanya Ziara ya Kushtukiza China

$
0
0
Kim Jong-un Amefanya Ziara ya Kushtukiza China
Kuna tetesi ambazo zinaendelea kushika kasi kwamba afisa wa ngazi ya juu wa serikali ya Korea Kaskazini ambaye amefanya ziara ya ghafla nchini China ni kiongozi wa Korea Kaskazini Kim Jong-un.

Vyombo vya habari Japan vilikuwa vya kwanza kuibuka na taarifa kwamba afisa wa ngazi ya juu mno kutoka Korea Kaskazinia alikuwa amewasili Beijing kwa kutumia treni maalum ya kidiplomasia.

Korea Kusini imesema haifahamu ni nani huyo aliyefanya ziara hiyo lakini inafuatilia tukio hilo kwa makini sana.

Ikithibitishwa kwamba aliyefanya safari hiyo alikuwa Bw Kim, basi itakuwa mara yake ya kwanza kufanya ziara nje ya nchi yake tangu alipochukua madaraka mwaka 2011.

Bado hakujakuwa na taarifa yoyote rasmi kutoka China wala Korea Kaskazini, lakini tukio kama hilo litakuwa kubwa.

Mwezi jana, Rais wa Marekani Donald Trump alikubali mwaliko usio wa kawaida wa kukutana na Bw Kim.
Maafisa wa Marekani wanadaiwa kushughulika sana kuhakikisha taratibu zote zinawekwa sawa kidiplomasia kuhakikisha mkutano huo unafanyika na kuwa wa kufana.

Polisi wa China wakiwa wamefunga barabara kuruhusu msafara wa magari yanayodaiwa kuwa na maafisa wa Korea Kaskazini kupita karibu na ikulu ndogo ya rais ya Diaoyutai, Beijing
Picha za video za treni hiyo ambazo zimepeperushwa na kituo cha habari cha Nippon News Network chenye makao yake Tokyo zimeonesha treni hiyo ina mistari ya mlazo ya rangi ya manjano.

Kituo hicho cha runinga kimesema treni hiyo inafanana sana na aliyoitumia babake Bw Kim, mtangulizi wake Kim Jong-il alipozuru Beijing mwaka 2011.

"Kulikuwa na maafisa wengi wa polisi nje na kwenye barabara upande wa mbele wa kituo. Kituo hicho kilikuwa kimefungwa ndani," ameambia AFP.

Polisi pia waliwaelekeza watalii hadi nje ya uwanja maarufu wa Tiananmen, Beijing kwa mujibu wa Reuters jambo linaloashiria kwamba kulikuwa na mkutano wa ngazi ya juu sana katika ukumbi maarufu wa mikutano ulio hapo karibu wa Great Hall of the People.

Msafara wa magari uliosindikizwa na maafisa wa polisi ulionekana ukiondoka eneo hilo, Reuters wanasema.

Katika jiji la mpakani kati ya China an Korea Kaskazini la Dandong, ambapo kuna reli inayounganisha China na Korea Kaskazini, matukio yasiyo ya kawaida yalishuhudiwa pia.

Shirika la habari za Korea Kaskazini NK News limesema limepata picha zinazoonesha vibao vya muda vikitumiwa kuziba njia moja ya kuingia eneo hilo, ingawa kuna uwezekano kwamba pengine kulikuwa na kazi ya ukarabati.

Wachambuzi waliozungumza na kituo cha habari cha Korea Kusini Yonhap wanasema aliyezuru huenda pia akawa dada mdogo wa Bw Kim, Kim Yo-jong, ambaye majuzi alihudhuria Michezo ya Olimpiki ya majira ya baridi nchini Korea Kusini, au iwe ni afisa mkuu wa kijeshi Choe Ryong-hae.

Waandamanaji Seoul 5 Novemba, 2017 wakiitisha amani kati ya Marekani na Korea Kaskazini
Mikutano mingi

Mapema mwezi huu wa Machi, waziri wa mambo ya nje wa Korea Kaskazini alihudhuria mazungumzo na waziri mkuu wa Sweden mjini Stockholm Stefan Lofven, kabla ya mkutano huo wa Bw Trump na Bw Kim mbao bado unapangwa.

Wakifanikiwa kukutana kama ilivyotarajiwa mwezi Mei, itakuwa ni mara ya kwanza kwa viongozi wa Marekani na Korea Kaskazini kukutana.

Bw Kim pia anatarajiwa kukutana na mwenzake wa Korea Kusini Moon Jae-in mwezi ujao.

Serikali Yatoa Kauli Hii Kuhusu Waraka wa Maaskofu

$
0
0
Serikali Yatoa Kauli Hii Kuhusu Waraka wa Maaskofu
Waraka uliotolewa na Baraza la maaskofu wa kanisa la Kiinjili la Kilutheri chini Tanzania (KKKT) mwishoni mwa wiki iliyopita umeendelea kuibua mjadala mkubwa nchini.

Katika waraka wa ujumbe wa pasaka, baraza hilo limeorodhesha mambo kadhaa ambayo wameyataja kuwa ndio tishio la umoja na amani ya nchi.
Mambo hayo kwa mujibu wa waraka huo ni Utekwaji wa watu ,utesaji, kupotea kwa watu, mauaji yenye mwelekeo wa kiitikadi, vitisho, ubambikiziaji wa kesi, na matumizi mabaya ya vyombo vya dola.

Mkurugenzi wa Idara ya Habari MAELEZO, ambaye pia ni Msemaji Mkuu wa Serikali, Dkt. Hassan Abbas, alipoulizwa msimamo wa serikali kuhusu waraka na matamko mbalimbali ya viongozi wa dini  alijibu kuwa   kwa sasa serikali haioni cha kujibu na kwamba inawatakia tu waumini kheri ya Pasaka.


RC Makonda Atoa Kauli Nzito kwa Waliotoa Waraka wa Kuikosoa Serikali

$
0
0
RC Makonda Atoa Kauli Nzito kwa Waliotoa Waraka wa Kuikosoa Serikali
Ni vigumu sana Kusimama Katika HAKI Kwenye Dunia iliyojaa Uovu , Kwamaana Unapigwa Katika Kila Upande  na Hata Waliotakiwa Kuzama Katika Maombi nao Wamekengeuka .

Ninapoitazama Kazi ya Msalaba Naelewa Kwanini Yesu Kristo alibaki Peke Yake .

Umepigana VITA ya Madini sikuona Waraka , Umejenga Ukuta Mkubwa Mererani Kulinda Rasilimali Yetu ya Tanzanite , Sikuona Waraka ,Umepigana Vita ya Rushwa,Umeanzisha Mahakama za Mafisadi sikuona Waraka Umepambana na Wazembe Maofisini sikuona Waraka, Umetoa Elimu BURE Sikuona Waraka , Umefufua Shirika la NDEGE, Unajenga  Treni ya Mwendo Kasi (SGR) Sikuona Waraka. Umeanzisha Mchakato wa Ujenzi wa Vyanzo Vipya Vya Umeme (Stigglers Gorge), Hatujaona Waraka.

Lakini Kama Haitoshi Umekomesha Mauaji ya Kutisha Ya Rai wasiokuwa Na Hatia kule Kibiti , Hatujaona Waraka ,Umekomesha Tabia Ya Askari kuvamiwa Na kuuwawa Vituoni wakiwa wanatimiza  Majukumu yao Ya Kulinda Raia , Hatujaona Waraka.Nakumbuka Kulikuwa na Tabia Ya kutorosha Wanyama kwa Kuwapandisha Ndege, Leo Umekomesha , Hatujaona Waraka .

Lakini Niwakumbushe , Umeongeza Bajeti ya Ununuzi wa Madawa Na Vifaa Tiba Kutoka Bilioni 31 Mpaka kufika Bilioni 260 , sijawai Kuona Waraka .

Tangu Umeingia Madaraka Umeongeza Vivuko katika Maeneo Yote Yanayohitaji Vivuko vya Majini , pamoja Na Madaraja Ya Kupitia Juu kwa wananchi Kuvuka , Pamoja Na Ununuzi wa Meli Kubwa Za Mizigo Na kubeba Abiria, Sijaona Waraka.

Umeamisha Makao Makuu ya Nchi Kupeleka Dodoma ,Unaongeza Uzalishaji wa Umeme Huku Ukiwapelekea Wananchi Mpaka Vijijini , Umeongeza Nidhamu Serikalini Unaongeza AJIRA Kupitia Viwanda , Yote haya na Mengine Mengi  Sijaona Waraka .

Leo Hii wananchi wa Mkoa wa Dar es salaam Wanaunganishiwa Maji Mpaka kwa Mkopo , Sijaona Waraka.

Leo Hii Mtulia Kuhama Chama Ambapo Ni Haki yake Kikatiba Ndio Nimeona Waraka .Ninakusihi na Kukuomba nikiwa  Mtumishi wa Mungu Ninae TAMKA  mambo na Kutokea.

Ninaye Yaona Mambo Yasiyo ONEKANA kwa  macho ya Mwili, Naiona Tanzania Mpya katika Uongozi wako.Shupavu.
Usifadhaike wala usihuzunike  kwa Sababu Unayoyasikia LEO na Kuyaona Hutayasikia tena kwa jina la Yesu Krsito Mwana wa Mungu aliye Hai.

Nakwasababu Wamebadili Kusudi la Kufa kwa Yesu Kristo , na kupoteza maana ya Pasaka.Bwana wa Majeshi anakwenda Kupindua Meza zao Kama ilivyotokea YERUSALEM.. Endelea.

Ujumbe huu Ukawatie Moyo Watu Wote Wanaoipenda Nchi na Kukuombea   kwa Roho na KWELI

 Ni mimi Mtumishi Wenu
 Paul Makonda
 Niliyepewa kipande cha Dar es salaam

Deni la Serikali Latia Wasiwasi Lafikia Trilioni 46 .... CAG Aonya Ukuaji wa Deni Hilo

$
0
0
Deni la Serikali Latia Wasiwasi Lafikia Trilioni 46 .... CAG Aonya Ukuaji wa Deni Hilo
Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali  (CAG), Profesa Mussa Assad amesema deni la Taifa linatia wasiwasi hivyo Serikali inatakiwa kuchukua hatua kupunguza ukubwa wa deni hilo.

Profesa Assad ametoa kauli hiyo leo Jumanne Machi 27, 2018 na kubainisha kuwa  deni hilo ni Sh46 trilioni kutoka Sh41 trilioni la mwaka uliopita, kwamba ni ongezeko la asilimia 12.

Ametoa kauli hiyo leo Ikulu jijini Dar es Salaam wakati wa uwasilishaji wa ripoti yake ya ukaguzi mwaka 2016/17 iliyobaini madudu Serikali za Mitaa na Mashirika ya Umma.

“Tulichosema hapa kwa kweli ukuaji wa deni tunasema ni himilivu lakini jinsi linavyoongezeka tunakaribia maeneo ya wasiwasi. Asilimia 72 ya GDP (Pato la Taifa) siyo mbaya lakini ikifika asilimia 76 nchi nyingine zimepata shida, inabidi tuangalie sasa namna gani tunaweza  ku-control ukuaji wa deni hilo,” amesema.

Nafasi za Ajira Zilizotangazwa Leo

Breaking News: Freeman Mbowe na Viongozi Wengine wa Chadema Wafikishwa Mahakamani

$
0
0
Breaking News: Freeman Mbowe  na Viongozi Wengine wa Chadema Wafikishwa Mahakamani
 Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Freeman Mbowe na viongozi wengine wa chama hicho, wamefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kwa ajili ya kusomewa mashtaka yanayowakabili.

Viongozi wa CHADEMA wengine waliofikishwa Mahakamani ni Katibu Mkuu Dr. Vincent Mashinji, Mbunge wa Kibamba John Mnyika, Naibu Katibu Mkuu Zanzibar Salum Mwalim, Mbunge wa Iringa Mjini Peter Msigwa na Ester Matiko Mbunge.

Miujiza ya Sharifu Seif Mohamed..JE Umeachwa na Mme/Mke au Mpenzi, Umesongwa na Mitihani ya Maisha

$
0
0
SHARIFU SEIF MOHAMED ANAWASHUKURU WALE WOTE WANAOENDELEA KUPIGA SIMU, WENYE MATATIZO NA WALE WANAOTOA  SHUKRANI NA SHUHUDA JINSI TIBA ZAKE ZINAVYO WASAIDIA,

(Rudisha mahusiano yako ndani ya masaa 72 tu)

SHARIFU MOHAMED Ni  mtaalam na mnajimu maarufu wa nyota na kubashiri mambo yanayo watesa binadamu duniani kote na kupata ufumbuzi, Anatumia kitabu cha QUR'AN na Nyota

Je Umeachwa na UMPENDAE awe Mme/Mke na bado unampenda? Je Umekimbiwa na Mmeo/ Mkeo n anaishi na mtu mwingine? Je Umejaribu sehemu nyingi bila mafanikio? Mpigie simu SHARIFU SEIF sasa hivi ujionee Muujiza wa Papo kwa Papo, Anauwezo wa hali ya juu wa kusambaratisha mahusiano yao na kumrejesha kwako haraka sana na Kumfanya Atimize Ahadi zote Ndani ya Muda Mfupi Endapo Utafwata Atakacho Kuelekeza

 ZINDIKO LA NYUMBA NA BIASHARA, PETE ZA BAHATI, HUMALIZA KABISA TATIZO   HUZUIA CHUMA ULETE KWENYE BIASHARA, HURUDISHA MALI ZILIZOPOTEA, NA KUPONYA MAGONJWA SUGU ANAO UWEZO WA KUMRUDISHA ALIE MBALI AU ALIECHUKULIWA MSUKULE, KUPANDISHA NYOTA NA KUSHINDA BAHATI NA SIBU, KASAFISHA NYOTA NA KUKUPA MVUTO WA AJABU, KUTOA NUKSI NA VIFUNGO MBALIMBALI,  MAFANIKIO YA MAISHA NA UTAJIRI BILA MASHARI, NA MENGINE MENGI YA SIRI,

JE UMAHANGAIKA KUPATA MTOTO BILA MAFANIKIO? WASILIANA NA MTAALAMU HUYU KWANI YEYE HUFAULU PALE WOTE WALIPOSHINDWA, PIA UMALIZA KAZI ZILIZO SHINDIKANA NA WATAALAM WENGINE NDANI YA MASAA 24 TU,

(NA ANATIBU KWA NJIA YA SIMU UKIWA NCHI YOYOTE AU MKOA WOWOTE ENDAPO UTAFWATA MAELEKEZO YAKE)

Kwa ushauri na mawasiliano  zaidi Piga SIMU No:

Mobile +255 654-836970
WhatsApp 0622766715

Viewing all 104789 articles
Browse latest View live




Latest Images