Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104789 articles
Browse latest View live

Waziri Mwakyembe Asikia Kilio cha Roma Aamua Kumfutia Adhabu ya Kufungiwa

$
0
0
Waziri Mwakyembe Asikia Kilio cha Roma Aamua Kumfutia Adhabu ya Kufungiwa
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Harisson Mwakyembe leo Machi29, 2018 ametangaza kufuta adhabu ya kufungiwa kwa msanii wa muziki Roma Mkatoliki.

Akizungumza na Waandishi wa Habari katika Ofisi ya Wizara hiyo jijini Dar es salaam Waziri Mwakyembe amesema kuwa muda wowote kuanzia sasa Roma Mkatoliki atakuwa huru kufanya shughuli zake za muziki kama ilivyokuwa awali kwa sharti moja la kukamilisha taratibu za kujisajili BASATA.

Kwa upande mwingine, Roma Mkatoliki ambaye naye aliongozana na Waziri Mwakyembe amesema kuwa hata kama ameachiwa huru lakini wimbo wake wa kibamia ameviomba vituo vya redio na runinga kutocheza wimbo huo baada ya kufutiwa adhabu yake.

Mwanzoni mwa mwezi Machi serikali kupitia Wizara ya Habari ilitangaza kumfungia miezi sita msanii Roma Mkatoliki kutojihusisha na masuala ya muziki kwa kukaidi amri ya kubadilisha baadhi ya mashairi ya wimbo wake wa Kiba100.

Haji Manara Amuwashia Moto Abdi Banda “Alikuwa Afukuzwe Timu Kitambo”

$
0
0
Haji Manara Amuwashia Moto Abdi Banda “Alikuwa Afukuzwe Timu Kitambo”
Baada ya kusambaa kwa interview ya beki wa zamani wa Simba Abdi Banda anayeichezea Baroka FC ya Afrika Kusini akifanya mahojiano na muandishi wa habari za michezo wa gazeti la Champions Saleh Jembe na kuelezea kusikitishwa na baadhi ya viongozi wa soka Bongo kupenda kulalamika katika vyombo vya habari.

Mahojiano ya Abdi Banda na Saleh Jembe yanaonekana kumgusa Haji Manara kiasi cha kufikia kuandika waraka wazi kupitia ukurasa wake wa instagram kuoneshwa kusikitishwa kwake kwa kile alichokizungumza Abdi Banda.

Hiki ndicho alichokiandika Haji Manara kuhusiana na Abdi Banda

Huku Panapoelekea Ndoto ya Baba Daimond kwa Wema Zitatimia

$
0
0
Huku Panapoelekea Ndoto ya Baba Daimond kwa Wema Zitatimia
AWALI ya yote nikiri tu kwamba, mimi ni kati ya watu ambao walitokea kuipenda sana ‘kapo’ ya mwanamuziki Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ na Wema Sepetu. Nilitokea kuwapenda tu. Nilisikia raha sana nilipokuwa nikisikia wakiitana majina mazuri kama vile baby…honey…sweet heart na nikatamani sana kusikia siku moja wamekuwa mke na mume.



Bahati mbaya sana ni kwamba, si kila anachotaka binadamu kitokee, kinatokea na hii inatokana na ukweli kwamba, kila jambo linapangwa na Mungu. Kama Mungu akisema hili ‘no’, hata ufanyeje haliwezi kutokea. Ila akisema liwe, basi linakuwa.



Lakini niwakumbushe tu kwamba, siyo mimi peke yangu niliyekuwa nikitaka siku moja Wema na Diamond waoane. Wapo mashabiki wengi tu ambao nao walikuwa wakitamani iwe hivyo.


Diamond na Zari.

Kama wewe ni mfuatiliaji wa mitandao, utakubaliana na mimi kwamba, kila picha ya Diamond na Wema ilipokuwa ikitupiwa, wengi walikuwa wakikomenti kuonesha kuwa, wanawapenda na wanatamani wawe mwili mmoja.



Achana na mimi na hao mashabiki wengine wa mastaa hao, hata baba mzazi wa Diamond, Mzee Abdul Juma naye aliwahi kukiri kuwa anampenda sana Wema na moyo wake ungefarijika sana kama siku moja angemuita Wema mkwe wake. Kwa bahati mbaya sana uhusiano wa wawili hao ukawa mara unang’ara, mara unazimika.



Mtakumbuka Wema na Diamond wameachana na kurudiana zaidi ya mara moja. Hata hivyo, mara ya mwisho walivyoachana kasha Diamond akajiweka kwa Zarina Hassan ‘Zari’ kisha wakazaa watoto wawili, kila mmoja alijisemea kuwa, Diamond na Wema imebaki stori na hawawezi kurudiana tena.


Baba Diamond akiwa amembeba mjukuu wake.

Ghafl a mambo yamebadilika, tumeona Zari ameamua kubwaga manyanga baada ya kuona Wema amerudisha majeshi kiaina. Hata hivyo, hakuna anayeweza kuthibitisha kwamba Wema na Diamond wamerudiana lakini kuna kila dalili kwamba, wawili hao wameamua ‘kama mbwai iwe mbwai tu’. Vijana wa mjini wanasema; ‘kama kusoma huwezi hata picha nayo huoni?



Sasa kwa nini nasema ‘soon’ ndoto za Baba Diamond ‘Baba D’ zitatimia? Iko hivi, Diamond amewahi kuwa kwenye uhusiano wa kimapenzi na mademu kibao. Kwa kifupi mtungo wa huyo dogo unawafunika mastaa wote wa kiume.



Naweza kusema Diamond ndiye staa wa kiume aliyetembea na mastaa wengi wa kike hapa Bongo. Kajiachia na Irene Uwoya, Wema Sepetu, Penniel Mungilwa ‘Penny’, Jokate Mwegelo, Hamisa Mobeto na wengineo.


Diamond.

Lakini sasa katika listi hiyo, hakuna hata mmoja aliyewahi kutambulishwa kwa wazazi wote wa Diamond isipokuwa Wema na Mobeto.



Ndiyo maana hata kwa picha tu tanaona kwamba zipo picha ambazo Wema amepiga na baba Diamond na mama Diamond, Mobeto naye kapiga akiwa na wazazi wote lakini sasa kuwahakikishia kuwa, Wema ndiyo chagua la baba D, yeye tu ndiye aliyefanikiwa kupiga picha ya pamoja akiwa na Baba D na Diamond.



Niambie wewe msomaji, uliwahi kumuona Diamond na demu gani wakiwa wamepiga picha na baba Diamond? Kwa kifupi hakuna! Lakini pia kama hujui basi leo ndiyo ujue kwamba, hakuna hata picha moja inayomuonesha baba Diamond akiwa na Diamond isipokuwa picha hiyo moja tu ambayo yupo Wema, Baba D na Diamond.



Hii ina maana gan



Inaonesha kwamba Diamond alimpenda sana Wema hadi akafi kia hatua ya kumpeleka kwa ‘mdingi’ wake na kwa bahati nzuri baba naye akabariki ndoa lakini haikuwa hivyo.



Sasa Wema na Diamond wamekuwa ndiyo habari ya mjini na watu wa karibu na baba D wanasema kuwa, anaomba usiku na mchana warudiane na wafunge ndoa.



Sisi yetu macho tu ila kwa maoni yangu mimi, Wema ana kila kigezo cha kuwa mke wa Diamond, kwanza wote dini moja, wamekuwa pamoja kwa muda mrefu, wanajuana vizuri hivyo ni rahisi ‘kushikiana madhaifu’ yao na wakadumu kwenye ndoa yao. Ila yote kwa yote ni wao na maisha yao!.

Kajala Afunguka Kuhusu Mahusiano Yake ya Kimapenzi na Chege

$
0
0
Kajala Afunguka Kuhusu Mahusiano Yake ya Kimapenzi na Chege
Msanii wa filamu nchini Kajala Masanja amefunguka na kuweka wazi kuhusu tetesi zinazosambaa kuwa sasa anatoka kimapenzi na msanii wa muziki wa Bongo fleva kutoka kiumeni Chege Chigunda.


Kajala akipiga stori na Big Chawa kwenye kipindi cha Planet bongo ya East Africa Radio amekana kuhusu kutoka kimapenzi na msanii huyo na kudai kuwa hakuna jambo kama hilo na

"Mama yangu mzazi hakuna kitu kama hicho si mmeona Chege kapata mtoto juzi tu hapa, yaani mimi sina hata namba yake ya simu na haiwezi kutokea kitu kama hicho"alisisitiza Kajala

Mbali na hilo Kajala amewatakia kheri wanawake wote maarufu ambao wanakaribia kuolewa siku za karibuni na kusema kwake yeye badobado kwani anaamini mume mwema anatoka kwa Mungu hivyo atakapompata huenda na yeye ndiyo akafanya maamuzi hayo ya kuolewa sasa.

Waziri Mwakyembe Ampa Onyo Kali Nay wa Mitego

$
0
0
Waziri Mwakyembe Ampa Onyo Kali Nay wa Mitego
Waziri wa Habari Dk Mwakyembe amefunguka na kumuonya msanii Nay wa Mitego kuhusu kuwadanganya wasanii wenzake na kusema ataendelea kufanya muziki ambao amekuwa akifanya miaka yote ili hali msanii huyo sasa amekuwa mstali wa mbele kufuata sheria.


Mwakyembe amesema hayo leo Machi 29, 2018 wakati waliokutana na msanii Roma Mkatoliki na waandishi wa habari na kutoa msamaha kwa msanii huyo kufuatia adhabu yake ya kufungiwa miezi sita kutojihusisha na sanaa.

"Nay wa Mitego alivyoongea na wenzake akawa anatamba kule mimi sibadilishi kitu akawa anawadanganya wenzake, Nay wa Mitego acha tabia ya kuwadanganya wenzako wakati wewe umebadilisha kila kitu na kupeleka BASATA halafu huku anatamba kwenye mitandao kwamba sibadilishi kitu, ujanja wa namna hiyo siyo mzuri anawadanganya wenzake wamuone ngangari kumbe hakuna lolote" alisema Mwakyembe

Msanii Nay wa Mitego kupitia mtandao wake wa Instgtram aliweka wazi kuwa katika wimbo wake mpya 'Mikono juu' hajabadilisha jambo lolote na kusema yeye ataendelea kufanya muziki wake kama ambavyo watu wamekuwa wakimjua kwa kuwa muziki huo wa kuchana watu ndiyo ulimtambulisha kwa jamii.

Mbowe, Viongozi Chadema Kula Pasaka Mahabusu

$
0
0
Mbowe, Viongozi Chadema Kula Pasaka Mahabusu
Hakimu Mkazi Mkuu wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Wilbard Mashauri amesema baada ya kusikiliza hoja zilizowasilishwa na upande wa Serikali na utetezi katika kesi inayowakabili viongozi wa Chadema, akiwemo mwenyekiti wa chama hicho, Freeman Mbowe washtakiwa hao wafikishwe mahakamani hapo Aprili 3, 2018.

Amesema siku hiyo washtakiwa watasaini bondi ya Sh20 milioni na wakiwa huru ndipo utaratibu wa kukata rufaa wa upande wa mashtaka utafanyika.

Kufuatia uamuzi huo, viongozi hao watakula Sikukuu ya Pasaka wakiwa mahabusu. Sikukuu hiyo inasherehekewa kuanzia kesho hadi Jumatatu.

Awali, Hakimu Mashauri alieleza dhamana kwa washtakiwa hao iko wazi, jambo ambalo lilipingwa na upande wa Serikali.

Washtakiwa hao walitakiwa kila mmoja kuwa na wadhamini wawili ambao watasaini hati ya dhamana ya Sh20 milioni na kuwa na barua kutoka kwa viongozi wao ama wa vijiji au mtaa, ambao watapaswa kuwa na nakala za vitambulisho vyao.

Pia, walitakiwa kuripoti katika Kituo Kikuu cha Polisi, Dar es Salaam.

Hakimu alisema kwa asiyeridhika na uamuzi huo ana haki ya kukata rufaa.

Katika mvutano wa kisheria, mmoja wa mawakili wa viongozi hao, Peter Kibatala alipinga taarifa ya rufaa iliyotolewa na wakili wa Serikali.

Kibatala aliiomba mahakama kutekeleza amri yake ya dhamana kwa kuwasainisha washtakiwa bondi ya Sh20 milioni kila mmoja katika tarehe ambayo inaona inafaa na baada ya hapo ndipo ipokee taarifa ya Serikali ya kukata rufaa.

Wakili wa Serikali, Faraja Nchimbi alidai kuwa hilo ni suala la kisheria kwa kuwa taarifa ya rufaa ikishawasilishwa mahakamani na kupokewa, mahakama husika itakuwa imefungwa mikono kuongea chochote kuhusiana na taarifa hiyo kwa maelezo kuwa itakuwa imeingia katika kumbukumbu za mahakama.

Dili Alilosaini Zali Lawavuruga Mastaa wa Bongo

$
0
0
Dili Alilosaini Zali Lawavuruga Wabongo
Mkataba alioingia jana mpenzi wa zamani wa mwanamuziki Diamond Platnumz, Zarina Hassan maarufu Zari umewagawa wasanii nchini kila mmoja akiwa na mtazamo wake.

Mjadala huo umekuja kufuatia baadhi ya watu kuhoji uhalali wa Zari ambaye ni Mganda kupata dili hilo nchini wakati  hapa nchini kuna mastaa wengi wenye sifa kama zake.

Miongoni mwa watu maarufu waliolalamikia hatua hiyo ni mwanadada Faiza Ally akisema amesikitishwa na kitendo hicho akihoji kwa nini hakupewa Mtanzania.

Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Faiza alihoji kwa nini kampuni zinawapa kipaumbele wageni na kuwaacha wazawa.

“Mastaa wote Watanzania, watu wote hamkuona hata mmoja anaye stahili kupata dili zaidi ya Zari ? Kwa nini tunawapa kipa umbele wageni tunajidharau sisi?” amehoji.

Maoni hayo ya Faiza yalizua mjadala mkali mtandaoni, mashabiki ambao wengine walimuunga mkono na wapo waliompinga huku wakimuuliza kama anaona anastahili kupewa ubalozi kutokana na namna anavyolibeba jina lake.

 Wakati Faiza akilalamikia hilo, Shamsa Ford amesema mastaa wenyewe hawajiweki katika hadhi ya kupewa ubalozi wa bidhaa.

“Naona tu watu wanalalamika kwa nini ‘madili’ yanawapita mastaa wa Bongo na wageni ndio wanapata nafasi hiyo. Mimi nina mtazamo tofauti kabisa. Kabla ya kuanza kumtafuta mchawi ni nani ni bora kwanza tukajikagua wenyewe kwanza. Nina uhakika kila biashara ina taratibu zake na kila biashara inahitaji faida,” amesema Shamsa.

“Hakuna mfanyabiashara atakayekubali kumchukua staa wa Bongo kisa uzalendo tu halafu apate hasara. Tusipinge ukweli sisi wenyewe baadhi ya wasanii tumevunja uaminifu kwa wafanyabiashara wakubwa kutokana na matendo yetu. Suala sio kujulikana tu ila unajulikana vipi?.”

Mastaa wengine waliompongeza Zari ni washindi wa Miss Tanzania kwa miaka tofauti Millen Magese na Hoyce Temu.

Baada ya Kufutiwa Kifungo na Waziri Roma Atangaza Kuufuta Wimbo wa “Kibamia”

$
0
0
 Baada ya Kufutiwa Kifungo na Waziri Roma Atangaza Kuufuta Wimbo wa “Kibamia”
Waziri wa habari,utamaduni, sanaa na michezo Dkt Harrison Mwakyembe akiambatana na Naibu waziri Juliana Shonza, katibu mtendaji wa BASATA Geofrey Mngeleza, Mwakilishi wa bodi ya filamu Tanzania na Katibu wa chama cha muziki wa kizazi kipya wameamua kukutana na wasanii ambao ni Roma Mkatoliki na Pretty Kind

 Moja kati ya vitu ambavyo wamejadili ni maombi yao ya kusamehewa adhabu zao za kufungiwa na kujishugulisha kwenye sanaa ya muziki kwa kipindi cha miezi sita kwa upande wa Roma baada ya kutangaza kusamehewa alitangaza kuufuta wimbo wake wa “Kibamia” .

Roma Mkatoliki alisema……..>>>“Mimi kama Roma au kama mtu niliotoa bidhaa kuna maamuzi ambayo tumefikia  ni kwamba ile bidhaa ina ukakasi na mimi nasema kama mwenye bidhaa vyombo ama mamlaka na taasisi ambazo zinasimamia hizi bidhaa kuingia sokoni ziweze kuiondoa hiyo bidhaa mara moja”

Kwanini Wanawake Wengi Warembo Wanaishia Kuwa Michepuko ?

$
0
0
Kwanini Wanawake Wengi Warembo Wanaishia Kuwa Michepuko ?
Ni ukweli kwamba wako wanawake wengi sana ambao wanahesabu kuwa ni baraka na jambo la kumshukuru Mungu kwa kuwaumba wenye sura nzuri na wenye mvuto. Pamoja na ukweli huu, ni wazi na imethibitika kwamba wako wanawake ambao wanahesabu kuzaliwa warembo ni mojawapo ya laana au mkosi kwasababu ya zile hali ambazo wamezipitia hususani katika mahusiano yao ya kila siku na wanaume.

Mara kwa mara kumekuwepo na tabia ya wanaume kutamani sana kuwa kwenye mahusiano na wanawake warembo, na hupenda kuwatongoza hao mara kwa mara ingawa moyoni mwao wanawaangalia warembo hawa kama wasichana wa kula nao raha tu “good time girls” na wala sio wake wakuoa.

Utakubaliana na mimi labda umewahi kuona mwanaume anakuwa kwenye mahusiano na binti mzuri sana kisura na kiumbo tena wanakuwa kwenye mapenzi kwa muda mrefu tu huku huyu binti akijua mbeleni kuna ndoa, ghafla ukija kusikia huyu kaka anaona unapigwa mshangao kuona wala sio yule binti mrembo anayeolewa.

Hii imewaacha mabinti wa aina hii katika maumivu makali sana ya moyo, na wengine wamekata tama na kuamua kujirahisisha ili mraadi maisha yaende. Wengine wameamua kukaa wakitunzwa na waume za watu kwasababu wao wamejithibitishia kwamba kuolewa hakupo.Tafiti zinaonyesha kwamba ukiona mwanaume aliyeamua kukaa muda mrefu na mwanamke mrembo, mara ningi unakuta ni wale wanaume wenye tabia za kisanii “players” ambao hata wao huwatumia mabinti hawa na kuwatelekeza hapo baadae.

Inasemekana imani au mtazamo huu hauko tu kwa wanaume bali hata wanawake wale wenye uzuri au urembo wa kati au wasio warembo kabisa wanajua na kuamini hivyo na mara nyingine huwarushia vijembe wale wanawake warembo kuwa “utachezewa tu na utaachwa na wataolewa wengine”. Na pale inapotokea kwenye mahusiano binti wa kawaida akagundua mpenzi wake wa kiume ametembea au husiana kinyemela na binti mrembo zaidi kuliko yeye, utakuta wakikutana kwenye kupashana au hata kwenye ugomvi wa kuandikiana ujumbe wa maneo, huyu binti wa kawaida humwambia yule mrembo kwamba “we jifurahishe tu ila usiamini kwamba utaolewa, huyu mwenzako anakuchezea tu anajuwa nani wa kuoa”. Unadhani imani hii wameitoa wapi?

Wakati mfumo au mtazamo huu unapoenea au kujirudia zaidi, wanawake hawa warembo au wazuri wa sura na umbo huamini kwamba wanaume wote ndivyo walivyo, wanaamini kwamba wanaume wote huwasogelea ili kujifurahisha kimapenzi tu na baada ya hapo kuwakimbia. Wakati huu wa kusubiria kumpata mwanaume wa kuoa “Mr. Right” ukizidi wanawake hawa huchoka na kukata tama, na hivyo wao sasa huamua kukimbizana na kutafuta mwanaume wa kuwapenda na kutulizana nao.

Tabia hii ya kuwafukuzia wanaume kwa bahati mbaya kuwagharimu sana wanawake hawa kwasababu wanaume wengi wanamtazamo hasi kwa wanawake wa jinsi hii. Wanaume wengi wanaamini wao ndio wanatakiwa kuwa wa kwanza kumtongoza mwanamke na sio mwanamke kuwa wa kwanza kuwatongoza wao, na mbaya zaidi anapokuwa mwanamke mzuri ndio shida huongezeka, wengine wakianza kuambiana “huyu lazima atakuwa mgonjwa anataka kuambukiza wengine”. Hapa unaweza kuelewa ni kwa kiasi gani hali huwa ya kutatiza.

Kwa upande mwingine, wanawake hawa wanaoonekana wazuri wa umbo na sura, sio halisi kama wanavyoonekana. Kwa mbali ni kweli mwanaume yeyote atavutiwa nao lakini jinsi unavyowakaribia na kuwafahamu unagundua mengi yanayohuzunisha na kuogopesha kuishi nao. Unagundua kuwa uzuri mwingine umeongezewa kutoka madukani zaidi na sio ulio halisi. Mara nyingine uzuri huu na ile hali ya kuonekana ni wagharama sana huwaogopesha wanaume wasio na kipato kikubwa na kwahiyo wanaume hawa wakishapata kabahati ka kufaidi penzi mara moja au mbili wanakimbia tena kwa kasi wakihofia kukamuliwa kiuchumi, ingawa mara nyingine hofu yao hii huwa sio ya kweli. Inasemekana baadhi ya wanawake wa aina hii huwekeza zaidi kwenye kuonekana wazuri na walimbwende ili kuficha au kufunika baadhi ya mapungufu yao.

Wanaume wengi walioulizwa sababu za kuwatumia na kuwatelekeza wanawake wa jinsi hii walisema kuwa, kwa kutembea, kuonekana nao au kufanya nao mapenzi, wanaume hawa hujihisi sifa sana, hususani wanapoonekana na wanaume wenzao, yani ni kama vile timu ndogo iliyopata nafasi kucheza katika kombe la dunia. Unajua tena wanaume wanavyopenda kujionyesha wanapokuwa na wanawake wazuri mbele ya macho ya wanaume wenzao.

Wamesema kwamba wanapowaza kuishi na wanawake hawa kama mume na mke, huwa wanazidiwa na hofu ya kuelemewa au kujihisi kutokuwa salama “sense of insecurity”. Mioyoni mwao wanahisi kwamba kama wanaume wenye hela wamekuwa wanamfuatilia kwa kasi kubwa hivi mwanamke huyu, vipi nikishaoana naye?? Si ndiyo kila siku kusuguana na kukorofishana vishawishi vinapozidi? Je nitaweza kustahimili?

Wanaume wengine walioulizwa walijibu kwamba, wanawake wa jinsi hii ni wa gharama sana, sio rahisi kuwaweka mjini na kuhakikisha wanaishi maisha yao ya kawaida kama hauna fedha ya kutosha. Hata wale wanaume wachache waliokuwa na hao wanawake kwa muda wa maswali haya wameeleza jinsi wanavyohisi wanatumia fedha nyingi na yamkini zaidi ya wanavyojiweza.

Wanawake wa aina hii watahitaji mitoko ya nje ya mji, sehemu zilizojitenga, sehemu za faragha ambazo ni za bei ghali, wanataka zawadi za gharama, ukitaka kuwapa zawadi za kushtukiza “surprise” basi ujipange, sio vitu vya kitoto vitakavyomsisimua aweze kukwambia “waoooooow…this is wonderful” hapo lazima ujipinde mfukoni haswa.

Ukitaka kuwatoa nje kwa ajili ya chakula cha jioni basi lazima kwenda maeneo wanayoenda watu maarufu, mkitaka kwenda kupumzika kidogo nje ya nyumbani basi uwaambie wachague wao wapi pa kwenda, na hapo utakapotajiwa ni pa gharama kubwa sana, na imeelezwa kwamba pamoja na mambo yote haya ya gharama kubwa bado huko wapenzi hawa wanapoenda msichana huyu anaishia kuonekana ni mwanafunzi asiyejua tendo la ndoa kabisa tofauti na hali aliyoionyesha “poor perfomer”, wanaume wengine wanasema inaonekana kama kupoteza tu pesa, unaishia kutokufurahia penzi lenyewe.

Na wengine wameenda mbali zaidi kueleza kwamba hata unapotaka kuzaa na mwanamke wa jinsi hii basi yeye anataka mtoto mmoja au wawili tu akiogopa asije kuliharibu umbo lake, tofauti na kiu ya mwanaume ya kupata watoto zaidi ya wawili. Imeelezwa kuwa hata ujuzi wa kupika kwao ni shida maana kutwa kucha wako “bize” na sura zao, na hata ukikaa nao sio watu wakufurahisha zaidi ya kutumia tu hela zako “they are boring”.

Pamoja na uchunguzi huu na ukiangalia hali halisi ya maisha yetu ya kila siku tena katika jamii tofauti utagundua kwamba wanaume kiu yao sio kuoa wanawake wenye umaarufu, au wenye kujulikana sana, au walio warembo kupindukia, bali wanaume wanapotaka kutafuta mke wa kuoa wanaangalia tabia na haiba zilizojificha, wanauliza tabia ya huyo msichana, wanataka kujua anavyohusiana na watu, wataangalia nyendo zake kuanzia wakati anasoma.

Ni ngumu kuwakuta wamenaswa na aina ya wanawake ambao wanataka kuonekana wakati wote, wanataka wajulikane kuwa wao nao wapo kwenye makundi ya watu, la hasha. Kiu zao ni kuwa na mwanamke ambaye atakuwa mke anaye leta furaha nyumbani, anaye sikiliza, anaye weza kushauri na kushaurika, aliyeko tayari kufundishika sio kuwa mwalimu kwenye kila kitu, anayeweza kuandaa mapishi mazuri yatakayo wafurahisha watoto na mume wake, sio kila siku kuelekeza kipikwe nini wakati yeye analinda kucha zake zisiharibike.

Hivi umewahi kujiuliza kwanini watu wengi waliooa wakiwa na michepuko, hiyo michepuko ni mabinti warembo na walimbwende ila hawajaolewa, hivi hujajiuliza kwanini hawajaolewa? Na hata wengine wakiolewa hizo ndoa kila siku tia maji tia maji, wataachika leo na kuolewa kesho na kuachika kesho kutwa nakuolewa tena mtondogoo.

Unadhani hawa wanaume wanaoenda kwa hao wanawake ni kwamba hawajui wanachokitaka? utashangaa hata umpe mapenzi gani bado hawezi kukwambia atakuoa, ingawa yuko tayari akupangishie nyumba au hata akujengee lakini ulale huko mwenyewe, yeye anaenda kulala na mke wake. Ushauri wangu wa bure kwa wanawake wa jinsi hii; badilikeni tabia zenu, jitihada mnazotumia kwenye kucha na sura zenu ziwekeni kwenye kushuhulikia tabia na haiba zenu, la sivyo mtasubiri sana tu.

JE Unafahamu Laana ya Kutembea na Mume wa Mtu na Madhara Yake ?

$
0
0
JE Unafahamu Laana ya Kutembea na Mume wa Mtu na Madhara Yake ?
Kutembea na mume wa mtu sio jambo zuri japo wanawake wengi wanaona ni kawaida bila kujua wanajilimbikizia laana itakayofanya maisha yao kuwa magumu mbeleni.

Machozi ya uchungu ya mwanamke mwenzio juu ya mume wake hayafutiki haraka.. Ni kama zigo la kinyesi mgongoni linavutiwa na inzi pekeake.

Huyo mwanaume unaemuona Leo ana mke, Pesa na mali na kuona ndo fursa kwako kumpata kwasababu anajua kujali na anapesa za kutosha kukugharamia.... Ukirudi nyuma miaka 10-15-20 mwanaume huyo huyo alikuwa kama huyu unae mkataa leo

Unaye muona hajui kuvaa.... Hana pesa za kutosha.. Hana mali kwahiyo hakufai.

Wanaume wengi wanaanzia chini... Jitihada za wake zao zinawafikisha walipo Leo. Heshimu jitihada hizo.

Heshimu siku walizofunga kwa ajili ya waume zao.
Heshimu machozi waliomlilia Mungu awafikishe walipo...
Heshimu muda na jasho walilolitoa kuhakikisha waume zao wanaonekana watu mbele za watu.

Muombe Mungu akupe wa kwako hata kama masikini mpate utajiri pamoja. Na wewe ubige magoti , ulie na kufunga.

Wanawake wengi wanalalamika hawaolewi au Wachumba wanawaacha bila sababu za msingi. Wanasahau zigo la kinyesi walilobeba mgongoni. Mwanamke piga magoti muombe Mungu akusamehe kwa kumliza mwanamke mwenzio.

Tuwaombee watoto wetu na kuwaonyesha njia iliyo bora. Kuwafundisha dini ili wawe na mahusiano mazuri na Mungu... wasikumbwe na laana hii.

Ewe mama elimisha watoto wako. Ewe dada elimisha wadogo zako.

Tukishirikiana kwa pamoja tutayafuta machozi ya wanawake .

Daunguro Kubwa Zaidi' la Makahaba Barani Asia Lapata Sura Mpya

$
0
0
Daunguro Kubwa Zaidi' la Makahaba Barani Asia Lapata Sura Mpya
Wasanii wa michoro wasiokubali jinsia ya maumbile yao wamekuwa wakiipatia sura mpya ya michoro ya rangi za kuvutia wilaya yenye idadi kubwa ya makahaba ya Sonagachi iliyopo katika jiji lililopo mashariki mwa India la Kolkata (zamani likiitwa Calcutta).

Picha hiyo juu inaonyesha mchoro uliochorwa kwenye jengo la chama cha ushirika cha makahaba.

Ikisemekana kuwa wilaya yenye idadi kubwa zaidi ya mahahaba bara Asia, Sonagachi ni wilaya yenye mitaa yenye barabara nyingi nyembamba na njia za uchochoroni kati kati mwa jiji la Kolkata, ikiwa ni makazi ya makahaba takriban 11,000.

Indian commuters walk past a painted building at Sonagachi red light district in Kolkata,Haki miliki ya pichaEPA
Wakifanya kazi kwa ushirikiano na wasanii wenye makao yao Bangalore, wasanii wa michoro wasiokubali maumbile yao ya jinsia (transgender) walichora michoro kwenye michoro ya rangi za kuvutia kwenye baadhi ya majengo kama sehemu ya kampeni ya kuhamasisha umma kuhusu haki za makahaba na pia kujaribu kuzuia unyanyasaji dhidi ya wanawake.

Uchoroji wa michoro hii ulichukua muda wa wiki nzima
Mengi kati ya madanguro haya yamechakaa.

Wapitanjia katika mtaa wa makahaba katika wilaya Sonagachi jijini KolkataHaki miliki ya pichaEPA
Image caption
Wapitanjia wa Kihindi wakipita kwenye mtaa wa madanguro ya makahaba yenye michoro katika wilaya ya Sonangachi jijini Kolkata
Kuta katika mtaa wenye majengo yaliyosongamana pia zilipakwa rangi.

Wapitanjia katika mtaa wa makahaba katika wilaya SonagachiHaki miliki ya pichaEPA
Hapa wapitanjia na wafanyabiashara wanaonekana kwenye moja ya jengo lililopigwa rangi.

Kuna mipango ya kuyapaka rangi majengo zaidi katika wilaya ya Sonangachi.

Indian commuters walk past a painted wall at Sonagachi red light district in KolkataHaki miliki ya pichaEPA
Ukahaba umesalia kuwa tatizo kubwa kwa India, ambako wanawake milioni tatu wanaaminiwa kufanya biashara ya ukahaba.

Afungwa Maisha Jela kwa Kubaka Mtoto

$
0
0
Afungwa Maisha Jela kwa Kubaka Mtoto
Moja ya stori ambayo ningependa ikufikie leo March 30, 2018 ni kumhusu Mwanaume aliefahamika kwa jina Shadrack Majimbo mwenye miaka 42 mkazi wa Nakuru Kenya, amehukumiwa kifungo cha maisha jela, kwa kumbaka binti wa miaka 9 na kumuambukiza magonjwa ya zinaa.

Hakimu wa Mahakama hiyo Judicaster Nthuku amesema ushahidi unaonyesha kuwa mtuhumiwa huyo alifanya vitendo hivyo vya ubakaji, ripoti ya daktari imethibitisha hilo huku akimuambukiza ugonjwa wa zinaa.

Imeelezwa kwamba mtuhumiwa alikuwa ni rafiki wa karibu wa familia ya binti huyo, ambapo siku ya tukio alimuita na kumtaka kumsaidia kazi za nyumbani, ndipo alipomfanyia kitendo hicho.

‘Bajeti Binafsi Chanzo cha Msongo wa Akili

$
0
0
‘Bajeti Binafsi Chanzo cha Msongo wa Akili
Kutokuwa na bajeti binafsi au ya familia imebainika ni chanzo cha mambo maovu katika jamii, maradhi ya akili na msongo wa mawazo kwa watu.

Hayo yalisemwa na mkurugenzi mtendaji wa kampuni ya Iscot inayojihusisha na masuala ya ushauri wa mambo mbalimbali, Patrobas Mazara kwenye kongamano la kuwajengea uwezo wa matumizi ya fedha wafanyabiashara wanawake lililoandaliwa na Tanzania Women Chamber of Commerce. “Usipokuwa na utawala sahihi wa fedha yako unayoipata kama malipo ya shughuli unayofanya, utaishia kulalamika kila siku fedha haitoshi,” alisema Mazara.

Mmoja wa washiriki, Irene Kasubi alisema licha ya jitihada kubwa alizokuwa akizitumia kuhakikisha anafanikiwa alishindwa kufikka malengo.

Silaha Iliyomgusa Akwilina Haijajulikana – Kamanda Mambosasa

$
0
0
Silaha Iliyomgusa Akwilina Haijajulikana – Kamanda Mambosasa
Kamanda Polisi Kanda Maalum ya Dar es salaam, Lazaro Mambosasa amesema askari polisi waliotuhumiwa kifo cha Mwanafunzi wa chuo cha NIT, Akwina Akwiline bado uchunguzi unaendelea na haijajulikana ni silaha ipi iliyomgusa.



Akizungumza na waandishi wa habari leo, Kamanda Mambosasa amesema kuwa kama walivyotoa taarifa kutuhumiwa kwao na hata upelelezi utakapo kamilika wataeleza.

“Askari waliokuwa wametuhumiwa kuhusu kifo cha Akwilina ikumbukwe kwamba walivyokamatwa tulieleze bayana kwamba upelelezi unafanyika ili kujua ni nani ambaye ametenda kosa lile. Kwahiyo bado suala la upepelezi unaendelea yapo maelekezo ambayo yaliyotolewa.Ikumbukwe silaha moja ambayo haijajulikana ni ipi ndiyo iliyokwenda ikamgusa Akwilina lakini askari wale kama mnavyojua walikuwa ni wengi lakini pia kulikuwa hakuna ushahidi ni yupi alikuwa ametenda kwahiyo upepelezi bado unaendelea,“ amesema Mambosasa.

Idadi ya Waliofariki Katika Ajari Mkoani Tabora Yaongezeka

$
0
0
Idadi ya Waliofariki Katika Ajari Mkoani Tabora Yaongezeka
Idadi ya watu waliofariki kwenye ajali ya basi mkoani Kagera imeongezeka na kufikia saba, ambapo wengine wawili walifariki wakiwa hospitali.

Akizungumza na www.eatv.tv, Kamanda wa Polisi mkoa wa Kagera Agustino Olomi amesema mpaka jana jioni ilivyotokea ajali watu watano ndio walikuwa wamefariki, lakini mpaka sasa wengine wawili wameongezeka na kufanya idadi kufikia saba.

Ajali hiyo imetokea katika kijiji cha Kasharazi wilayani Ngara mkoani Kagera, ambapo moja ya basi kati ya mabasi manane yaliyokuwa yamebeba wakimbizi yakiwa kwenye msafara sambamba na magari mengine madogo, kufeli breki na kugonga basi lingine, na kusababisha kumgonga muendesha baiskeli na kufariki papo hapo, kisha basi hilo kupinduka na kusababisha vifo vya watu wanne hapo hapo.

Kamando Olomi amesema mpaka sasa hawajajua idadi ya majeruhi kwani wakimbizi hao ambao walikuwa wakitokea kwenye kambi ya Nduta Wilayani Kibondo mkoani Kigoma na kuelekea Burundi, kupelekwa kwenye kambi ya wakimbizi karibu na eneo hilo, na wahusika wa kambi ndio wanahusika na taarifa zao.

Mwwakyembe, Basata Watoa Baraka kwa Waandaaji wa Shindano la Miss Tanzania

$
0
0
Mwwakyembe, Basata Watoa Baraka kwa Waandaaji wa Shindano la Miss Tanzania
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo,  Harisson Mwakyembe pamoja na Baraza la Sanaa(BASATA) wametoa baraka  kwa waandaji wa shindano la Miss Tanzania linalosimamiwa na The Look Company Limited, iliyopo chini ya Mkurugenzi wake, Basilla Mwanukuzi aliyewahi kuwa Miss Tanzania mwaka 1998.

Baraka hizo zimetolewa katika ofisi ya Waziri ambapo alikutana na Mkurugenzi wa Kampuni ya Look Limited, Mwanukuzi ambaye amebeba dhamana ya shindalo hilo baada ya Mkurugenzi wa Kampuni wa Lino International Agency LTD Hashim Lundenga kutangaza rasmi kuacha shughuli za kuendesha mashindano hayo.

Miss Tanzania 2018 itazinduliwa rasmi  April 7, mwaka huu na Mikoa 26 itahusika katika shindano hilo ambayo ni:- Arusha, Dodoma, Geita, Iringa, Kagera, Katavi, Kigoma, Kirimanjaro, Lindi, Mara, Mbeya, Morogora, Mtawara, Mwanza, Njombe, Rukwa, Ruvuma, Shinyanga, Simiyu, Singida, Tabora, Tanga, Ilala, Kigamboni, Kinondoni na Temeke.

Febuari 28 mwaka huu, aliyekuwa Mkurungezi wa shindano hilo Hashimu Lundenga alitangaza kuacahana na shughuli za kuandaa shindano na kusimamia shindano la Miss Tanzania na alimpa kijiti cha kusimamamia na kuongoza kazi hiyo aliyekuwa Miss Tanzania 1998, Basila Mwanukuzi.

Bombardier Iliyozuiliwa Canada Yaachiwa.... Kutua Nchini Muda Wowote

$
0
0
Bombardier Iliyozuiliwa Canada Yaachiwa.... Kutua Nchini Muda Wowote
SERIKALI ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imewathibitishia wananchi kuwa ndege yake aina Bombardier Q400 iliyokuwa imezuiliwa nchini Canada imearuhusiwa kuondoka nchini humo na muda wowote kutoka sasa itawasili hapa Tanzania.

Taarifa hiyo imetolewa na Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, Ikulu, Gerson Msigwa leo Machi 30, 2018 kupitia ukurasa wake wa Twitter huku akiweka picha zilizokuwa zikionesha ndege hiyo wakati wa matengenezo ya mwisho kabla ya kuruhusiwa kuondoka.

“Ndege yetu aina ya Bombardier Q400, iliyokuwa imezuiliwa nchini Canada ilikwishaondoka Canada kuja Tanzania. Pia ndege kubwa nyingine tatu (2 Bombardier CS300 kutoka Canada na  1 Boeing 787-8 Dreamliner) kutoka Marekani, zitawasili baadaye mwaka huu. Nawatakia Ijumaa Kuu njema”, amesema Msigwa.

Aidha, Msigwa amesema hawajajua tarehe maalumu ya kutua ndege hiyo katika ardhi ya Tanzania kutokana na baadhi ya vitu kuwa vinamaliziwa.

Dah… Ningekuwa na Mtoto Wangu Ningekuwa Nampost All the Time- Wema Sepetu

$
0
0
Dah… Ningekuwa na Mtoto Wangu Ningekuwa Nampost All the Time- Wema Sepetu
Mrembo Wema Sepetu ametoa sababu ni kwanini kila mara anapenda kuposti picha za watoto tofauti tofauti katika ukurasa wake wa Instagram.

Ameeleza hayo baada ya kufanya hivyo na baadae mugizaji Idris Sultan kumwambia; si uanzishe tu nursery.

Mrembo huyo aliyekuwa Miss Tanzania mwaka 2006 hakukawia kujibu comment hiyo ya Idriss, ni kama alichokozwa alivyoijibu kwa haraka;

Dah… mbona ningekuwa nae wa kwangu ningekuwa nampost all the time… ni kwasababu tu sina wangu… so i post every baby dat melts my heart…
Since i don’t have one to call my owm… ila ningekuwa nae mbona ungeni-unfollow… Smh…

Utakumbuka mwaka 2016 Idris na Wema walikuwa katika mahusiano ya kimapenzi na ilifikia hatua wakaeleza kuwa wanatarajia kupata watoto mapacha, hata hivyo baadae ilikuja kuripotiwa kuwa ujauzito huo kuharibika.

Kamanda Mambosasa Atoa Tahadhari kwa Wananchi Msimu Huu wa Sikukuu

$
0
0
Kamanda Mambosasa Atoa Tahadhari kwa Wananchi Msimu Huu wa Sikukuu
Kamanda wa Jeshi la Polisi kanda maalum Dar es salaam, Lazaro Mambosasa amesema wamejipanga vizuri katika kuimarisha hali ya usalama nchini katika sikukuu hii ya Pasaka na kudai atakayethubutu kufanya vitendo vya kiharifu atachukuliwa hatua kali.

Kamanda Mambosasa ameeleza hayo leo (Machi 30, 2018) wakati alipokuwa anazungumza na waandishi wa habari Jijini Dar es Salaam na kusema kulingana na uzoefu waliokuwa nao wamejipanga kuimarisha usalama kwa hali ya juu ili wananchi waweze kusherehekea kwa amani na utulivu.

"Jeshi la Polisi litahakikisha wananchi wa Dsm wanasherehekea sikukuu hii kwa amani na utulivu na kwa kuwa uzoefu unaonesha kwamba mara nyingi katika sherehe kama hizi watu wenye nia ovu wanajiandaa kufanya vitendo vya kiharifu ikiwa na pamoja na kufanya ujambazi ili kujipatia vipato kwaajili ya kusherehekea sikukuu", amesema Mambosasa.

Pamoja na hayo, Mambosasa ameendelea kwa kusema "baada ya kulijua hilo Jeshi la Polisi tumejipanga vizuri, kwamba hakuna mtu yeyote atakayeweza kupata fursa ya kufanya lolote katika uvunjifu wa sheria, tumeimarisha doria lakini tunaendelea na misako maeneo yote ya jiji la Dar es Salaam katika mikoa yote mitatu na wilaya zote za kipolisi 11".

Kwa upande mwingine, Kamanda Mambosasa amesema hayo yote yanafanyika kwa lengo la kuimarisha hali ya usalama katika siku kama hizi za sikukuuu.

Miujiza ya Sharifu Seif Mohamed..JE Umeachwa na Mme/Mke au Mpenzi, Umesongwa na Mitihani ya Maisha

$
0
0

SHARIFU SEIF MOHAMED ANAWASHUKURU WALE WOTE WANAOENDELEA KUPIGA SIMU, WENYE MATATIZO NA WALE WANAOTOA  SHUKRANI NA SHUHUDA JINSI TIBA ZAKE ZINAVYO WASAIDIA,

(Rudisha mahusiano yako ndani ya masaa 72 tu)

SHARIFU MOHAMED Ni  mtaalam na mnajimu maarufu wa nyota na kubashiri mambo yanayo watesa binadamu duniani kote na kupata ufumbuzi, Anatumia kitabu cha QUR'AN na Nyota

Je Umeachwa na UMPENDAE awe Mme/Mke na bado unampenda? Je Umekimbiwa na Mmeo/ Mkeo n anaishi na mtu mwingine? Je Umejaribu sehemu nyingi bila mafanikio? Mpigie simu SHARIFU SEIF sasa hivi ujionee Muujiza wa Papo kwa Papo, Anauwezo wa hali ya juu wa kusambaratisha mahusiano yao na kumrejesha kwako haraka sana na Kumfanya Atimize Ahadi zote Ndani ya Muda Mfupi Endapo Utafwata Atakacho Kuelekeza

 ZINDIKO LA NYUMBA NA BIASHARA, PETE ZA BAHATI, HUMALIZA KABISA TATIZO   HUZUIA CHUMA ULETE KWENYE BIASHARA, HURUDISHA MALI ZILIZOPOTEA, NA KUPONYA MAGONJWA SUGU ANAO UWEZO WA KUMRUDISHA ALIE MBALI AU ALIECHUKULIWA MSUKULE, KUPANDISHA NYOTA NA KUSHINDA BAHATI NA SIBU, KASAFISHA NYOTA NA KUKUPA MVUTO WA AJABU, KUTOA NUKSI NA VIFUNGO MBALIMBALI,  MAFANIKIO YA MAISHA NA UTAJIRI BILA MASHARI, NA MENGINE MENGI YA SIRI,

JE UMAHANGAIKA KUPATA MTOTO BILA MAFANIKIO? WASILIANA NA MTAALAMU HUYU KWANI YEYE HUFAULU PALE WOTE WALIPOSHINDWA, PIA UMALIZA KAZI ZILIZO SHINDIKANA NA WATAALAM WENGINE NDANI YA MASAA 24 TU,

(NA ANATIBU KWA NJIA YA SIMU UKIWA NCHI YOYOTE AU MKOA WOWOTE ENDAPO UTAFWATA MAELEKEZO YAKE)

Kwa ushauri na mawasiliano  zaidi Piga SIMU No:

Mobile +255 654-836970
WhatsApp 0756033670
Viewing all 104789 articles
Browse latest View live




Latest Images