Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104795 articles
Browse latest View live

Picha za Zari Akila Bata Dubai Baada ya Kupiga Bonge la Deal Tanzania

$
0
0
MPENZI wa zamani wa mwanamuziki Diamond Platnumz, Zarinah Hassan ‘Zari The Boss Lady’ baada ya kusaini mkataba na kuwa balozi wa Kampuni ya Keds Tanzania inayojishughulisha na utengenezaji wa taulo za watoto.

Hafla iliyofanyika kwenye Hoteli ya New Africa jinini Dar es Salaam. Baada ya kuondoka Tanzania ameamua kwenda kula bata na watoto wake kwa upande wa marehemu Ivan Ssemwanga.




Wakina Dada Mnaohudumia Saloon za Kiume Punguzeni Kidogo...Wengine Tuna Wake Nyumbani

$
0
0
Hakika nawaambieni sisi wanaume kwa hizi Barbershop kuzikimbia inataka kama kuwa ngumu hivi?

Kwanza hawa kina dada wa Saloon za kiume wameteka sana soko then wanapenda sana Tip. Yaani imekuwa kama lazima kumbe ni hiari ya mtolewa huduma.

Halafu hawa Dada wajanja sana akitaka kukuhudumia mfano scrub anakufungua vishkizo vya juu then anapitisha mikono yake kifuani huku anakuburuzia na kucha zake ndefu kwa Nippon zako aise seriously lazima unyegeke tuu, then anamalizia kwenye masikio then anakuulizia vipi Una- Enjoy?

Huwa wanamikono lainiiiiiii hatari sana akikushika lazima utoe pesa tuu hata 30,000/= walahi. Kuna Barbershop hapo Sinza nilienda nikanyoa fresh baada ya kumaliza kuna huyo Sister akaniuliza unahitaji scrub? Nikakubali akasema twende ndani nimekaa tu kwenye kiti anarembua hatari, kanisugua masikioni, shingoni, akaniambia nitoe shati litachafuka daah nikatoa basi kanisuguaa hadi kifuani huku mmmmh nikaanza kama kusahau shida, baada ya hapo ananiuliza do u need extra service plz ni nzuri nitakuonesha aisee nilimpa pesa nikakurupuka ndukiii kubwa.

Nawaonea huruma wanawake waliiolewa wanaibiwa sana duuuh jifunzeni kuwafanyia scrub waume zenu nyumbani mnaibiwaa sana huku..

Zari Amkomesha Diamond, Atua Bongo na Kuondoka Bila Kukanyaga Madale...Diamond Abaki Mdomo Wazi

$
0
0
Zarinah Hassan ‘Zari The Boss lady’, aliyekuwa baby mama wa staa wa Bongo Fleva, Nasibu abdul ‘Diamond Platnumz’, amekinukisha ile mbaya baada ya kutua Bongo na kutokwenda nyumbani kwa jamaa huyo, Madale-Tegeta jijini Dar, risasi Jumamosi limenyetishiwa.

 ATUA USIKU WA MANANE, AFIKIA HOTELINI

Zari alitua Dar usiku wa manane wa Jumanne iliyopita na kufikia katika Hoteli ya Hyatt Regency The Kilimanjaro, zamani Kempinski iliyopo Posta, Dar na mapema kesho yake (Jumatano iliyopita), alisaini dili nono na Kampuni ya Softcare. Zari alisaini dili hilo la mamilioni, tukio lililofanyika mbele ya vyombo vya habari kwenye ukumbi wa hoteli hiyohiyo na sasa akawa ndiye balozi mkuu wa pampers za watoto zinazosambazwa na kampuni hiyo.


AULIZWA KUHUSU DIAMOND

Katika zoezi hilo la kusaini dili hilo, ulipofika muda wa maswali, Zari aliulizwa juu ya uhusiano wake na Diamond ambapo ‘aliwaka’ na kusema kwamba, kilichomleta Bongo ni dili hilo tu na asingependa kuzungumzia mambo ya Diamond.

AWA BENETI NA NOEL, ATIMKA BONGO

Tofauti na alivyozoeleka kuwa na Diamond, safari hii Zari alionekana akiwa beneti na jamaa ambaye ni mbunifu wa mavazi Bongo aliyetajwa kwa jina moja la Noel kabla ya kutimka Bongo mara tu baada ya kukamilisha kilichomleta.


TAARIFA ZILIVYOTUFIKIA

Tukirudi nyuma, usiku uleule wa Jumanne, mara tu baada kutua kwa mwanamama huyo, taarifa za uwepo wake Dar zilienea, nasi zikatufikia.

Tulipomtembelea kwenye kurasa zake za kijamii ndipo tukakutana na ujumbe wake kwenye Snapchat akithibitisha kuwepo Bongo kwa shughuli hiyo maalum. Usiku huohuo, pia baadhi ya watu walikosa usingizi huku wakivipa vidole vyao kazi ya kuandika na kuposti kwenye mitandao ya kijamii juu ya ujio wa Zari ambaye aliishia hotelini.

NI WIKI KADHAA TANGU AMMWAGE DIAMOND

Zari alilifanya jambo hilo ikiwa ni wiki kadhaa tangu alipotangaza kummwaga rasmi Diamond ambaye kwa sasa makazi yake, mama na ndugu zake ni Madale-Tegeta jijini Dar.

 FAMILIA YA DIAMOND

Taarifa za kijasusi kutoka ndani ya familia ya Diamond huko Madale-Tegeta, nje kidogo ya Jiji la Dar, zilidai kwamba, familia hiyo ilikumbwa na sintofahamu na kujikuta ikiparanganyika na kila mmoja kusema lake kutokana na kutokuamini kama kweli Zari anaweza kuwa Dar, lakini asikanyage nyumbani hapo kuwasalimu. “Achilia mbali kuwasalimu, lakini bado chumba chake hakina mrithi pale Madale na hata yeye mwenyewe alisema ameachana na Diamond, lakini undugu utaendelea kuwepo kwa sababu amezaa naye watoto wawili, Tiffah na Nillan.

 MAMA DIAMOND ATIBUKA

“Kiukweli jambo hilo limetuumiza sana sisi kama familia, yaani kila mtu ana mtazamo wake, lakini Zari ametutibua sana,” alisema memba huyo wa familia ya Diamond na kuongeza: “Unaambiwa bi mkubwa (mama Diamond) ametibuka balaa maana anaona kama Zari hathamini wala hajali kama amezaa na mwanaye. “Bi mdanga (mama Diamond) anahoji kama Zari amegombana na Diamond ndiyo awachunie wote?”

 MAWIFI WATOA YA MOYONI

Wakizungumza na mwandishi wetu kwa nyakati tofauti, dada zake Diamond au mawifi wa Zari, Esma Khan ‘Esma Platnumz’ na Mwanaisha Abdul ‘Queen Darleen’, walitoa ya moyoni; esMa PlaTNUMZ “Mimi ninachojua Zari hawezi kuja Madale kwa sababu amegombana na Diamond. Kwanza mimi sina ukaribu naye kwa sababu kama una wifi, alafu

akawa anakufanyia vitu vizuri, anakujali na kukunyenyekea, lazima uwe karibu naye, mi’ sina ukaribu naye,” alisema Esma Platnumz ambaye kwa muda mrefu alidaiwa kutoivana na Zari kwa kuwa anampenda zaidi Wema Sepetu aliyekuwa mpenzi wa Diamond kabla ya Zari.

QEEN DARLEEN “Mi’ sina cha kusema, lakini watu wajue tu ninampenda sana Zari, tena sana,” alisema Queen Darleen ambaye tangu zamani alijipambanua kuwa anamkubali Zari.

Anthony Joshua Noma Ashinda Pambano Lake na Joseph Parker Kwa Kishindo

$
0
0
Usiku wa April 1 2018 mashabiki wa mchezo wa ngumi duniani walikuwa wanasubiria kwa hamu pambano la mabondia Anthony Joshua na Joseph Parker kupanda ulingoni kila mmoja akitarajiwa kulinda rekodi yake.

Bondia Anthony Joshua leo amefanikiwa kumpiga Joseph Parker kwa ‘Unanimous Decision’ hilo likiwa ni pambano lake la 21 kwa Athony Joshua kushinda kati ya mapambano yake 21 ila ni pambano lake la kwanza kushinda kwa point ila yote 20 yaliyosalia amekuwa akishinda kwa‘Knock Out’

Kwa upande wa Joseph Parker mwenye umri wa miaka 26 akizidiwa na Anthony Joshua miaka miwili, yeye anapoteza pambano lake la kwanza kati ya mapambano yake 25 akiwa kashinda 18 kwa Knock Out, 6 kwa point, Joshua anazidi kudhihirisha ubora wake katika mchezo huo baada ya ushindi huo kumpa Ubingwa wa WBO

Punguza Unene Unaokusumbua Katika Mwili Kwa Kutumia Bidhaa za Edmark

$
0
0
"Tumia Dawa za Edmark za Kupunguza uzito uliozidi Mwilini Mwako, Edmark ni Vurutubisho na Chakula Mbadala na Zimehakikiwa na TFDA...

Ni uhakika kwa afya yako,👉 kupunguza uzito na sumu mwilini, Mafuta Sehemu Mbaya, Kitambi na nyama uzembe na kutibu MAGONJWA Mbalimbali kwa msaada wako mfuate instagram: @my_health_my_wealth @my_health_my_wealth


Au Mtafute WhatsApp Huyu Dada kwa kutumia Namba +255783 566844

Pia Dawa za Edmark Zinaweza kupa Fursa ya Biashara Uweze pata Kipato Kirahisi kwa Kuwasaidia watu Kuimarisha Afya zao

Kamata Kamata ya Wapinzani Yaendelea...Halima Mdee akamatwa Airport Akitokea Kwenye Matibabu

$
0
0
Mbunge Jimbo la Kawe kupitia tiketi ya CHADEMA, Halima Mdee amekamatwa na Jeshi la Polisi leo asubuhi kwenye uwanja wa ndege wa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere Jijini Dar es Salaam akiwa anatokea nchini Afrika Kusini kwaajili ya kupatiwa matitabu.

Hayo yamethibitishwa na Mbunge wa Jimbo la Ubungo kupitia Chadema Saed Kubenea na kusema ni kweli Halima Mdee amekamatwa leo na Jeshi la Polisi kutokana na yeye kutoripoti katika kesi iliyofunguliwa japokuwa alitoa taarifa ya udhuru.

"Ni kweli Halima Mdee amekamatwa leo asubuhi akiwa Airport Jijini Dar es Salaam na Jeshi la Polisi, inafahamika kuwa Mdee ni miongoni mwa viongozi wa Chadema wanaoshtakiwa kwenye kesi ambayo ipo Mahakamani ambapo Mwenyekiti Freeman Mbowe akiwa mmoja wao", amesema Kubenea.

Pamoja na hayo, Kubenea ameendelea kwa kusema "walikuwa nje kwa dhamana kabla ya kesi kupelekwa Mahakamani, kwa hiyo Halima alikuwa hajaenda kuripoti Polisi siku waliyoambiwa waende kuripoti Polisi kwa maana yeye alikuwa nje ya nchi. Sasa amerejea nchini leo asubuhi ndipo walipomkamata Airport".

Kwa upande mwingine, Kubenea amesema kukamatwa kwa Halima Mdee bila shaka Jeshi la Polisi linataka kumuunganisha na viongozi wengine waliokuwa gerezani mpaka muda huu lisha ya kwamba wamepatiwa dhamana ya Mahakama.

Ray C Alia na Bongo Flava..'Nahisi Kuna Jini Mmoja Kwenye Hii Industry Anayesababisha Wasanii Wajihisi Hawawezi tena'

$
0
0

Muimbaji Ray C amefunguka mazito kwa kile anachoona kinaenda ndivyo sivyo katika muziki wa Bongo Flava kwa sasa.

Ray C amefikia hata hatua ya kutumia maneno makali kueleza hisia zake kwa yale ambavyo hakubaliani nayo kwenye tasnia hiyo. Kupitia ukurasa wake wa Instagram ameandika;

Kuna muda huwa nafikiria mambo mengi sana! kuna muda najiskia kuamua kutiwa mimba, nizae niwe tu mama wa nyumbani! maana kuna muda nikiangalia wasanii wenye maendeleo kwenye Bongo Flava ni wachache saaaaana! na sijiongelei mimi maana mimi mwenyewe kuna wakati nilivurunda mwenyewe!

Nakubali nilibugi na nikagundua nimebugi haswa na ndio maana nimepambana mpaka hapa niliko baada ya kugundua baraka tele nilizozawadiwa na Mungu ni kubwa mno kuliko starehe za muda za ndogo na za kibwege!!! Ila huwa nakaa najiuliza miaka kama sita ambayo nilipotea kwenye industry! kuna wasanii nilianza nao na wana vipaji vya ajabu maskini lakini wengi wao wamezimwa kama taa!!!

Namkumbuka Nature, Joseline, Bushoke, Z Anto, Matonya, Makamua, Marlow, Domokaya n.k😢 majina ni mengi siwezi maliza!!!!!Wengi sana ni wasanii wakubwa sana na wana uwezo mkubwa mno. Najiuliza kitu gani kinachowakatisha tamaa hadi leo wamekuwa hadimu!!!???Mi nilikuwa kimya kutokana na sehemu.niliyokuwepo!!NAMAANISHA!? Jehanam!! na hawa niliowaacha je??? Kuna nini kwenye bongo flava???

Wasanii wapya ni wengi yes nalijua hilo lakini ukweli ni kuwa nchi yoyote hapa Afrika Mashariki nikienda naskia tu nyimbo za zamani nyingi na mpya pia!! mimi mwenyewe pamoja na mahanjumat ya pepo ya ahera yote lakini bado sauti ipo na nyie je???Nahisi kuna jini mmoja kwenye hii industry anaesababisha wasanii wengi wajione kama ndo basi tena! point yake ni moja! Na uwezo wa kukujenga na kukumaliza mara moja!!!maana yake nini sasa???.

Mungu anisamehe nianze kwenda kabla ya huyu jini!Pesa!! pesa!Pesa!Pesa!Ingekuwa pesa ndo uhai wallah hata Michael Jaclson asingekufa!!!!.

Nimeitumia hiyo picha sababu roho imeniuma siku ya mwisho kabisa ndo venue inabadilishwa!!!!Kuna karoho tu kamenikasirisha nimehisi kama kuna upuuzi wa kisengwile umefanywa ili mradi tu waharibu shughuli ya dada wa watu! Roho ya ndani huongea ukweli na ndo ninachohisi siku ya leo.

Wasanii mna kazi kubwa ya kuanza kujiamini kwanza kabla ya kuamini mtu mwingine! Mkishajua aliewapa vipaji naamini Mtasimama tena, Mtaingia studio tena! Maana mashabiki wenu bado wapo!!! Kinachohitajika ni kipaji sio promota anaefikiria tumbo lake na mpaka leo anazidi kukondeana!! ziba lakini tutakutana kaburini!.

Aliyezaa na Casto! "Tunda Hana Lolote, Casto ni Mchafu Simpendi Tena"

$
0
0
Aliyezaa na Casto! "Tunda Hana Lolote, Casto ni Mchafu Simpendi Tena"

Kufuatia 'Couple' mpya inayotikisa jiji kwa sasa ya mtangazaji wa Clouds, Casto Dickson na Video queen, Tunda, mwanamke mmoja ambaye ni mzazi mwenza wa mtangazaji huyo anayefahamika kwa jina la Don Posh, ameibuka na kuweka bayana kuwa wawili hao hawawezi kuwa na uhusiano kamwe ila ni kiki tu.

Posh amesema kuwa bado anampenda mzazi mwenziye huyo, na kusema kuwa hakuna mwanamke atakayetokea kupendwa na Casto kama yeye kwani alichompatia hawezi kupatiwa na mwanamke mwingine yeyote.

Posh ameongeza kuwa Casto ni mlevi sana, na kuwa hapendi vile ambavyo Casto anashikana shikana na Tunda na kuachia video zao mitandaoni, huku akichanganya maelezo yake baada ya kusema pia kuwa hampendi tena kutokana na uchafu wake wa kutembea na wanawake hovyo hadi mahausigeli.


Isome HAPA Barua ya Profesa Kitila Mkumbo Kwenda kwa Mkuu wa Kanisa la KKKT Ikipinga Waraka Wao

$
0
0


Baba Askofu Dkt. Fredrick Shoo,
Mkuu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT)
S. L. P. 3033
ARUSHA.

Mheshimiwa Baba Askofu, Shalom!

YAH: MAMBO MATANO AMBAYO HAYAPONYI KATIKA WARAKA WA MAASKOFU WA KKKT

Jina langu ni Kitila Mkumbo, muumini katika Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), ambalo wewe ndiye mkuu wake. Kikazi, mimi ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Maji na Umwagiliaji, Dodoma. Kitaaluma, mimi ni mhadhiri mwandamizi katika Saikolojia na Elimu nikiwa na cheo cha Profesa mshiriki katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.

Mheshimiwa Baba Askofu, kwa unyenyekevu mkubwa nimeamua kukuandika barua hii ili kutoa maoni yangu binafsi kwa kanisa unaloliongoza kupitia kwako kuhusu maudhui ya waraka uliotolewa na waheshimiwa maaskofu wa KKKT siku ya Jumamosi tarehe 24 Machi 2018. Waraka huo ulitarajiwa kusomwa katika makanisa siku ya Jumapili tarehe 25 Machi 2018. Katika kutoa maoni yangu kuhusu waraka huo, ninalenga mambo makubwa mawili ambayo ni pongezi kwenu, na pili ni mtazamo wangu juu ya baadhi ya masuala yaliyomo katika waraka huo.

Mheshimiwa Baba Askofu, kwa dhati kabisa ninawapongeza sana kwa kujali na kwa utayari wenu katika kuzungumzia na kuchambua kwa kina mambo muhimu ya kijamii, kisiasa na kiuchumi yanayogusa moja kwa moja uhai na haki za kibinadamu za waumini wa KKKT na Watanzania kwa ujumla.

Aidha, ninawapongeza sana kwa ujasiri na kwa kutumia vizuri nafasi zenu katika kanisa na jamii ya Watanzania katika kuyatolea kauli mambo yanayogusa masilahi mapana ya nchi yetu.

Kupitia waraka huo, mmetimiza ipasavyo majukumu yenu ya msingi kwa jamii. Binafsi ninaamini kuwa pamoja na kwamba ninyi ni viongozi wa kiroho, bado mnayo nafasi kubwa katika kuchangia maendeleo ya nchi yetu kisiasa, kijamii na kiuchumi kwani mambo yote hayo yana uhusiano wa moja kwa moja na afya ya kiroho.

Mheshimiwa Baba Askofu, mbali ya pongezi hizo, nina maoni kwenu ninyi viongozi wetu wa kiroho katika mambo kadhaa yaliyobainishwa kwenye waraka, ambayo ninaona kuwa maudhui yake hayaakisi hadhi na wajibu wa msingi wa kanisa.

Kama ambavyo mmekuwa mkitufundisha siku zote, na vile tusomavyo katika Biblia Takatifu, ninafahamu kuwa kazi za msingi za kanisa ni zile ambazo Bwana Yesu Kristo alizifanya alipokuwa duniani. Kazi hizo ni kuhubiri habari njema (injili), kufundisha waumini ambao ni sehemu ya jamii na kuponya wenye shida mbalimbali kijamii, kimwili na kiroho.

 Ninaamini kuwa ninyi viongozi wetu wa kanisa ni warithi wa kazi hizo wenye wajibu wa kuziendeleza hapa duniani. Inatarajiwa kuwa maneno na matendo yenu ndani na nje ya kanisa yatakuwa yenye mwelekeo wa kutekeleza kazi hizo ambazo matokeo yake ni uponyaji wa jamii na kuleta matumaini ya kimaisha, kiroho na kimwili.

Mheshimiwa Baba Askofu, katika waraka wenu mmetoa maoni katika maeneo 18 ambayo mmeyagawanya katika maeneo makuu matatu (jamii na uchumi; maisha ya siasa na masuala mtambuka). Kwa ujumla, ninakubaliana na mengi mliyogusia katika waraka huo na ninaamini yamefundisha na kuponya roho zetu kwa kiasi kikubwa, hasa kipingele cha tano (v) mnapozungumzia masula mtambuka pale mnaposema: “Uhai wa mtu una thamani isiyopimika. Ni wajibu usiokwepeka kuulinda na kuutunza uhai kwa vitendo halisi. Endapo uhai umepotea katika mazingira yoyote, uchunguzi huru na wa haki ufanyike na taarifa zitolewe kwa wakati muafaka ili kujenga jamii yenye imani kwa Serikali na vyombo vyake”.

Hata hivyo, yapo maeneo matano (5) muhimu mliyoyatolea kauli ambayo, kwa maoni yangu, hayaponyi bali yanaleta mkanganyiko zaidi kwa jamii kwa kuwa hayakujengwa katika msingi wa mantiki na ushahidi wa neno la Mungu, wala kuzingatia mantiki na ushahidi wa kisayansi, ambayo siku zote yamekuwa ni msingi wa hoja za KKKT.

Mheshimiwa Baba Askofu, baada ya maelezo hayo ya utangulizi, naomba sasa niyabainishe maeneo hayo matano ambayo ninaamini kuwa mngejipa nafasi ya kutafakari kwa kina zaidi msingeyatolea kauli au mngeyatolea kauli kwa namna nyingine.

1.Kuhusu uhuru wa Bunge, Mahakama na Tume ya Uchaguzi
Mheshimiwa Baba Askofu, katika kujadili maisha ya siasa, katika hoja yenu ya nne (4), mmeeleza kwamba kuna “kubanwa na hatimaye kuelekea kupungua kwa uhuru wa Bunge, Mahakama na Tume ya Uchaguzi”.

Maoni haya siyo mageni na yamesambaa mtaani na hasa miongoni mwa viongozi wa vyama vya siasa vya upinzani. Hata hivyo, maoni kama haya yanapotolewa na ninyi viongozi wetu wakuu wa kiroho yanakuwa na mwangwi tofauti katika jamii.

Suala hili la uhuru wa Bunge na Mahakama ni mjadala wa kudumu katika siasa duniani kote. Hii inatokana na ukweli kwamba hakuna kigezo kimoja kilichokubalika duniani kote cha kupima uhuru wa Bunge na Mahakama. Kila jamii au upande una tafsiri yake kutokana na muktadha wa nchi husika.

Mheshimiwa Baba Askofu, labda nifafanue hoja yangu kwa kutumia mfano wa Bunge. Katiba yetu ipo wazi kwamba Bunge ndicho chombo cha mamlaka ya juu (supreme) katika mihimili mitatu ya dola nchini mwetu.

Aidha, katika mfumo wa vyama vingi, Bunge huongozwa kwa msingi wa demokrasia ya wachache wasikilizwe lakini wengi waamue. Katika Bunge letu la sasa, idadi ya wabunge wa chama kinachounda Serikali yaani CCM, ni zaidi ya theluthi mbili ya idadi ya wabunge wote.

Hii inamaanisha kuwa, kwa mujibu wa Katiba yetu na sheria zake, kwa Bunge hili wabunge wa CCM ndiyo wenye haki ya maamuzi kutokana na idadi yao. Kwa sababu hii, kama kuna tatizo katika mfumo wa maamuzi wa Bunge letu, tatizo la msingi haliwezi kuwa kukosekana kwa uhuru wa Bunge kwa kuwa Katiba yetu imetoa uhuru wa kutosha kabisa kwa chombo hiki. Ingekuwa ni tatizo kama kuna siku Bunge lingekuwa limeamua kinyume cha matakwa na maamuzi ya walio wengi ndani ya Bunge.

2.Kuhusu wanasiasa kuhama vyama
Mheshimiwa Baba Askofu, eneo la pili ambalo nina maoni tofauti ni katika hoja yenu ya saba linalohusu maisha ya siasa. Katika eneo hili hoja yenu ya msingi ni kwamba kuna udhalilishaji wa kauli njema isemayo “maendeleo hayana chama”. Waheshimiwa Maaskofu mnadai kuwa “udhalilishaji huu unafanyika kwa njia ya kutumia fedha nyingi katika chaguzi ndogo zinazotokana na watu wanaobadili vyama ili kuleta maendeleo”. Mmeendelea kujenga hoja kwa kujiuliza, “kama maendeleo hayana chama, kwa nini mtu anajiuzulu chama fulani eti kwenda kingine?”

Mheshimiwa Baba Askofu, katika utangulizi wa waraka wenu, mmeeleza vizuri sana kuhusu umuhimu wa kudumisha mfumo wa vyama vingi. Hata hivyo, kwa maoni yangu, kauli yenu niliyoinukuu hapo juu haikuzingatia ipasavyo utamaduni unaoambatana na mfumo wa vyama vingi.

Duniani kote, pamoja na mambo mengine, utamaduni wa mfumo wa vyama vingi huambatana na watu kuhama vyama kila wanapojisikia kufanya hivyo. Vyama vya siasa ni taasisi ambazo wanachama wake wapo huru kuingia na kutoka bila kutakiwa kujieleza kwa mtu yeyote yule ilimradi katika kufanya hivyo hawavunji sheria za nchi.

Labda nikupeni mifano michache katika kupanua uelewa wa jambo hili. Katika nchi ya jirani Kenya viongozi wote wakuu katika siasa za Kenya wamewahi kuhama vyama mara nyingi. Rais wa sasa wa Kenya ameshahama na kubadili vyama mara nne. Kiongozi nguli wa upinzani Raila Odinga ameshahama na kubadilisha vyama mara sita. Huko nchini Uganda kiongozi maarufu wa upinzani nchini humo Kiiza Besigye alikuwa katika chama kimoja na Rais Museveni, lakini alihama na kuanzisha chama chake.

Pengine unaweza ukasema tabia za kuhama vyama zipo Afrika tu. Hapana. Muasisi wa kuhama vyama duniani ni Winston Churchil, ambaye ndiye anayeshikilia rekodi ya kuwa waziri mkuu bora nchini Uingereza. Huyu alihama kutoka chama cha Conservative na kujiunga na chama cha Liberal. Baadaye tena alirudi katika chama cha Conservative na hatimaye kuchaguliwa kuwa waziri mkuu.

Ukienda nchini Marekani wapo wanasiasa maarufu 21 waliowahi kuhama vyama vyao. Kwa mfano, rais wa zamani wa Marekani Ronald Reagan alikuwa mwanachama wa chama cha Democrat, lakini alihamia chama cha Republican na baadaye akaja kuwa rais wa nchi hiyo.

Alipoulizwa kwa nini alihama alijibu kuwa “I didnt leave the Democratic Party. The party left me” (Sikukiacha Chama cha Democrat. Chama ndicho kilichoniacha). Wanasiasa wengine maarufu waliowahi kuhama vyama vyao nchini Marekani ni pamoja na Condoleeza Rice, Elizabeth Warren, Hillary Clinton na Theodore Roosevelt. Rais wa sasa wa Marekani, Donald Trump alishahama vyama mara tatu na hadi mwaka 2001 alikuwa mwanachama wa chama cha Democrat.

Mheshimiwa Baba Askofu, nimetoa mifano yote hii katika kujaribu kupanua uelewa wenu kuhusu tabia za wanasiasa katika mfumo wa vyama vingi duniani kote. Hata hivyo, jambo hili halipo katika siasa tu. Wewe unafahamu vizuri kuwa hata katika dini watu hubadili dini na madhehebu yao. Sembuse vyama vya siasa?

Aidha, katika nchi yetu tumeshakuwa na chaguzi ndogo nyingi zinazotokana na wabunge na madiwani ama kuhama vyama vyao au kufukuzwa katika vyama vyao tangu mfumo wa vyama ulipoanza, na chaguzi zote hizo husababisha gharama kubwa. Sasa ninajiuliza kwa nini Kanisa limeumia sana na chaguzi za kipindi hiki? Kuna nini?

3.Kuhusu mikopo kwa wanafunzi wa elimu ya juu
Mheshimiwa Baba Askofu, hoja ya tatu ambayo nayo pia ningependa kuitolea maoni ipo katika eneo la tatu la waraka wenu, ambayo ni kuhusu upatikanaji wa mikopo ya elimu ya juu. Katika hoja hiyo mmeeleza kwamba, “uwezeshwaji wa vijana kupata mikopo ya elimu ya juu uwe shirikishi na usiokuwa na ubaguzi kati ya wanafunzi wa vyuo binafsi na wale wa serikali; sayansi na sanaa; wazazi maskini na wenye nafasi; waliosoma shule binafsi na wale wa shule za Serikali”.

Kwa ufahamu wangu ni kwamba kimsingi kila mkopo lazima uwe na vigezo. Msingi mkubwa wa mikopo inayotolewa kwa wanafunzi wa elimu ya juu hapa nchini ni kile kinachofahamika kama means testing, ambapo Bodi ya Mikopo huchambua maombi ya mikopo kwa kuzingatia, pamoja na mambo mengine, uwezo wa wazazi wa wanafunzi. Hivyo, mnaposema pasiwe na tofauti katika utoaji wa mikopo, mlitaka kumaanisha nini hasa?

Ni vizuri kukumbushana kuwa kuanzishwa kwa mikopo kwa wanafunzi wa elimu ya juu kulitokana na Serikali kushindwa kugharamia wanafunzi wote wanaodahiliwa katika elimu ya juu. Kwa sababu hii, njia pekee ilikuwa ni kuja na vigezo ambavyo vingewaondoa wale ambao wana uwezo wa kujilipia.

Katika mazingira haya, sio sahihi, kwa mfano, kusema kuwa hata mtoto wa mzazi mwenye wadhifa kama wangu naye apate mkopo. Aidha, kanisa haliwezi kueleweka linapotaka mtoto aliyesomeshwa na mzazi wake katika Shule ya Sekondari Feza au International School of Tanganyika naye apate mkopo wa serikali.

Aidha, kila nchi duniani ina vipaumbele vyake vya mahitaji kutokana na wakati na mazingira. Kwa wakati na mazingira ya nchi yetu kwa sasa tunahitaji zaidi wataalamu katika fani za sayansi kuliko sanaa.

Ni kwa sababu hii Serikali inawekeza zaidi katika kusomesha wanafunzi katika fani za sayansi kuliko sanaa. Huu ndiyo msingi wa Serikali kuwapa kipaumbele wanafunzi wanaosoma masomo ya sayansi kuliko wale wanaosoma masomo ya sanaa.

Kwa maoni yangu, jukumu la kanisa katika suala hili lingekuwa ni kuiasa serikali kuepuka ubaguzi katika mikopo kwa misingi ya dini, itikadi za siasa na ukabila ambapo bahati nzuri ubaguzi huo haupo.

Ubaguzi katika mikopo ya elimu ya juu kwa misingi ya uwezo wa wazazi na aina ya shule ambayo mtoto alisoma (binafsi au umma) hauepukiki. Kwa maoni yangu, kuna haja pia kuangalia kama bado ni muhimu kutoa kipaumbele kilicho sawa kati ya wanafunzi wanaodahiliwa katika vyuo vikuu vya umma na wale wanaodahiliwa katika vyuo vikuu vya binafsi.

Huo pia unaweza ukawa aina nyingine ya ubaguzi unaokubalika katika utoaji wa mikopo kwa wanafunzi wa elimu ya juu, hasa katika mazingira ambayo vyuo vya umma vina nafasi ya kutosha ya kudahili wanafunzi wote wenye sifa za kujiunga na elimu ya juu.

4.Katiba Mpya
Mheshimiwa Baba Askofu, katika waraka wenu mmetoa pia maoni kuhusu umuhimu na uharaka wa kupatikana kwa Katiba mpya. Hii ni hoja kubwa inayogusa Taifa letu kwa muda mrefu. Sote tunatambua utashi na ujasiri aliouonyesha Mheshimiwa Rais wa Awamu ya Nne wa kuruhusu mchakato huu uanze, pamoja na kwamba haikuwa ajenda ya msingi na kipaumbele katika chama chake. Kwa hiyo, ninaunga mkono kanisa kulitolea kauli jambo hili kubwa na muhimu kwa Taifa letu.

Hata hivyo, baadhi ya hoja zenu na lugha iliyotumika katika kuwakilisha hoja hiyo haiponyi bali inaligawa kanisa na nchi kwa ujumla. Kwa mfano, mnaposema kuwa “tunaisihi Serikali ya Awamu ya Tano kurejea mchakato wa upatikanaji wa KATIBA MPYA ya wananchi iliyopendekezwa na wananchi kupitia Tume ya Warioba”, mlitaka kumaanisha nini hasa?

Ninauliza hivi kwa sababu ninafahamu kuwa mchakato wa kuunda Katiba mpya ulikuwa umevuka ngazi ya Tume ya Warioba na kufikia ngazi ya Bunge la Katiba, ambapo Bunge lilipitisha kwa kura ya wengi.

Kilichokwama katika mchakato huo ni kura ya maoni ya wananchi kutokana na kukosekana kwa maridhiano mapana ya kijamii baada ya baadhi ya wawakilishi katika Bunge la Katiba kususa kuhudhuria vikao vya Bunge hilo.

Ninafahamu pia kuwa kanisa na dini zingine ziliwakilishwa kikamilifu katika Bunge hilo. Wawakilishi wa kanisa sio miongoni mwa wabunge waliosusia Bunge la Katiba, ikimaanisha kuwa kanisa liliridhia mchakato hadi mwisho na ni sehemu ya jamii waliokubaliana na rasimu iliyopitishwa na Bunge hilo.

Sababu za msingi za mchakato wa Katiba kukwama ni kutokana na kukosekana kwa mwafaka na maridhiano ya kitaifa. Kwa sababu hii mchakato wa Katiba mpya umebaki ukielea. Sasa katika mazingira haya ni hatari sana kwa ninyi viongozi wetu wakuu wa kiroho kuchukua upande mmojawapo katika mgawanyiko huo uliotokea.

Kwa maoni yangu, kwa upande wenu kama kanisa ingetosha kutoa wito wa kurejewa kwa mchakato wa Katiba mpya na kutoa wito wa mchakato huo kuzingatia maridhiano ya kitaifa.

Kwa mujibu wa matokeo ya utafiti wa Sauti za Wananchi yaliyotolewa mwezi Oktoba 2017, maoni ya wananchi yamegawanyika katika makundi manne kuhusu upatikanaji wa Katiba mpya. Kuna kundi la Watanzania linalotaka mchakato uanze upya. Kuna kundi jingine linalotaka turejee kwa Tume ya Warioba.

Lipo kundi linalotaka tumalizie mchakato kwa kwenda katika kura ya maoni. Lakini pia wapo Watanzania wanaosema hakuna haja tena ya Katiba mpya. Makundi yote haya ni ya Watanzania na bila shaka miongoni mwao ni waumini wa KKKT. Hivyo, ninyi viongozi wetu mnapoongelea suala hili kwa namna ya kuhimitisha (conclusive) mnajiweka katika mazingira ya kuchochea mgawanyiko badala ya kuleta umoja na uponyaji.

5.Kuhusu Serikali kutoendeshwa kwa ilani ya vyama
Hoja yenu nyingine katika eneo la maisha ya siasa ni kuhusu nafasi ya ilani ya vyama katika kuendesha nchi na Serikali. Katika hoja yenu hii mmenena ya kuwa, “Taifa haliongozwi na ilani za vyama. Serikali haiongozwi na ilani za vyama. Serikali huongozwa na Katiba, sheria, kanuni na mapokeo mema (misingi na tunu za Taifa)”.

Baba Askofu, niruhusu nikupeni elimu ya siasa kidogo kuhusu jambo hili. Duniani kote inajulikana kuwa chama kinachopata ridhaa ya kuunda serikali hupewa dhamana ya kutekeleza ahadi ambazo chama hicho kilizitoa katika uchaguzi.

Ndiyo kusema, vyama vinapoingia kushindana katika uchaguzi hushindania fursa ya kuunda serikali ili vitekeleze yale ambayo vinaamini ni muhimu kwa maendeleo ya Taifa husika. Kwa hivyo, msingi wa sera za serikali iliyopo madarakani ni ilani ya chama tawala iliyosheheni ahadi za chama hicho wakati wa uchaguzi.

Ndiyo kusema mara chama kinaposhinda uchaguzi na kuunda serikali ahadi zake zilizopo ndani ya ilani hugeuka kuwa ajenda za maendeleo za Taifa hilo. Ndiyo maana ahadi za CCM za uchaguzi wa mwaka 2015 ni sehemu muhimu ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa wa Miaka Mitano.

Kwa hiyo serikali huongozwa na vyombo vikubwa viwili katika kuendesha nchi. Chombo cha kwanza ni ilani ya chama tawala ambayo hutekelezwa kama sehemu ya ajenda za maendeleo ya Taifa husika.

Chombo cha pili ni Katiba, sheria, kanuni na miongozo mbalimbali ambayo hutolewa na vyombo mbalimbali vya dola. Katiba, sheria na kanuni ni nyenzo za utekelezaji wa mipango ya maendeleo ya Taifa, ikiwemo ilani ya chama tawala.

Hadi hapo utaona kuwa hamkuwa sahihi hata kidogo kuwahubiria waumini wa KKKT na Watanzania kwa ujumla kuwa Serikali haiendeshwi kwa ilani za vyama. Ukweli ni kuwa ilani ya chama tawala ni nyenzo na ajenda muhimu ya kuendesha serikali katika nchi zote zinaendeshwa kidemokrasia na kwa kufuata utawala wa sheria.

Marekani, kwa mfano, leo wanajenga ukuta wa kuitenga Marekani na Mexico ili kudhibiti wahamiaji kutoka Mexico. Hii ilikuwa ni moja ya ahadi kubwa za Rais Donald Trump na chama chake cha Republican wakati wa kampeni za uchaguzi mkuu wa mwaka 2016. Baada ya Donald Trump kushinda uchaguzi na kuunda serikali ahadi hii sasa ni ajenda ya Taifa la Marekani.

Mheshimiwa Baba Askofu, nihitimishe barua yangu kwa kurudia tena pongezi za dhati kwa kuandaa Waraka ambao umegusa masuala nyeti yanayohusu nchi yetu. Hata hivyo, upo umuhimu kwa kanisa kujiepusha kadri inavyowezekana kuonekana lipo upande fulani kwenye mijadala ya kitaifa inayogusa jamii pana yenye mitazamo kinzani.

Kwa kufanya hivyo, mtaepusha migawanyiko isiyo ya lazima kwa waumini ndani ya kanisa na wananchi kwa ujumla. Ushauri wangu ni kwamba ili kanisa lionekane linaendeleza kazi za msingi zilizoanzishwa na Bwana wetu Yesu Kristo, ni muhimu sana kufanya utafiti na uchambuzi wa kina wa jambo lolote kabla ya kulitolea kauli hadharani.

Aidha, ni muhimu kwa kanisa kupima kwa umakini mkubwa uzito wa kila neno kabla ya kutoa kauli katika umma. Ni hatari kwa kanisa kutoa kauli inayosababisha maumivu na mifarakano badala ya kuponya. Ili kuepuka kauli za namna hii, ni vizuri kila mara kanisa na viongozi wetu mkajenga hoja zenu kwa kuzingatia mantiki na ushahidi wa kiinjili unaopatikana ndani ya Biblia Takatifu, na/au mantiki na ushahidi wa kisayansi unaopatikana kupitia tafiti na tafakuri pana na shirikishi.

Mheshimiwa Baba Askofu, Bwana Yesu Asifiwe.
Kwa heshima na taadhima ninaomba kuwasilisha.
Dodoma
Alhamisi 29 Machi 2018.

Download Upya Application Yetu Ya Udaku Special .....Ile Ya Zamani Tutaifuta

Ni Kweli Wanawake Wamewazidi Wanaume Kwa Mambo Haya Kumi?

$
0
0
1. Wana Nguo Nyingi Kuliko Wanaume.
2. Wanafahamu Nani Ni Baba Halisi Wa Watoto Wao.
3. Ni Wepesi Kupenda Na Wakipenda Hupenda Kweli.
4. Wanaoga Mara Nyingi Zaidi Kwa Siku.
5. Wana Huruma Sana Ingawa Mara Nyingi Huwa Inawaponza.
6. Wana Uwezo Wa Kubadilisha Tabia Ya Mwanaume Muda Wowote.
7. Wana Uwezo Wa Kuishi Na Kupendeza Bila Kuwa Na Kazi Wala Biashara Yoyote.
8. Kwao Nywele Na Kucha Ndo Vitu Vya Kwanza Kufikiria Wakitaka Kutoka.
9. Wana Uwezo Wa Ku-Pretend Kwa Muda Mrefu Zaidi Hasa Kwenye Mapenzi.
10.Tupia Nyingine Unayodhani Nimeisahau...

Rafiki wa Kike wa Mchumba Wangu Ana Shida..Je Nimsaidie?

$
0
0

Waadau habari za wkend....

Jana meshindwa kumjibu mdada ambae ni rafiki wa karibu na girlfriend wangu,alinipigia simu na kuniomba nimsaidie kiasi flani cha fedha amtoe kuna rafiki yake yupo polisi.
nilimwambia kuna kazi nafanya ntamjibu baadae....
kuna maswali nimejiuliza.

1. Kwanini asipitie kwa rafiki yake ambae ni mchumba wangu?
2. Nikimsaidia je gf wangu akija kujua si atajua tulikuwa na mahusiano kabla?
3. Nikimwambia gf wangu si ndo anaweza kuzua ugomvui kati yao?
4. Niuchune tuuu.

Ungekuwa wewe ungefanyaje?anajua kuwa uwezo wa kumsaidia unao.

Hali ya Upinzania Bongo Yazidi Kuwa Tata...Viongozi Wengine wa Upinzani Wadakwa na Polisi

$
0
0
Mjumbe wa Kamati Kuu, na Mwenyekiti wa Kamati ya Taifa ya Sheria ya ACT Wazalendo, Wakili Thomas Msasa amekamatwa na polisi mjini Kigoma.

Tarifa ya kukamatwa kwake imetolewa na Mbunge wa Kigoma Ujiji Zitto Kabwe, na kusema kwamba sababu ya kukamatwa ni  kuwatetea Madiwani, viongozi na wanachama wa chama hicho waliokuwa wamekamatwa na Jeshi la Polisi hapo jana.

Zitto Kabwe amesema wakili Msasa alikwenda polisi kama wakili wa Madiwani wawili wa ACT Wazalendo, diwani wa kata ya Kipampa, ndugu Mussa Mgongolwa, pamoja na diwani wa kata ya Kigoma, ndugu Hussein Kalyango, aliyekuwa mgombea udiwani kata ya Mwanga, ndugu Winston Mogha, katibu wa ngome ya vijana ya ACT Wazalendo mkoa, ndugu Masabo, pamoja na wanachama na wafuasi mbalimbali wa ACT Wazalendo wa mkoa wa Kigoma, ambao walikamatwa hapo jana.

Kwa upande wa msemaji wa chama hiko Ado Shaibu amesema mpaka sasa upande wa jeshi la Polisi hawajatoa taarifa rasmi juu ya sababu ya kukamatwa kwa watu hao, na kwamba wanasheria wao wanashughulikia suala hilo na utaratibu wa dhamana.

Isome hapa taarifa yote aliyoandika Zitto Kabwe.


Chadema Yazungumzia Hali ya Halima, Yapeleka Daktari Kudhibitisha Kuwa ni Mgonjwa

$
0
0
Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kimesema kimeamua kumpelekea daktari wa Mbunge wa Kawe, Halima Mdee ili aweze kumcheki na kuwathibitishia Jeshi la Polisi kuwa Halima ni mgonjwa na wala hakuwa na nia ya kukimbia kuripoti Polisi.

Hayo yamebainishwa na Mkurugenzi wa Itifaki na Mawasiliano ya Mambo ya Nje wa Chadema, John Mrema wakati alipokuwa anazungumza na mwandishi wa habari hii muda mchache alipokamatwa Halima Mdee na Jeshi la Polisi katika uwanja wa ndege wa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere Jijini Dar es Salaam leo (Aprili Mosi, 2018).

"Halima Mdee bado anashikiliwa na Jeshi la Polisi wa kituo cha 'Centro' Jijini Dar es Salaam mpaka hivi sasa japokuwa amewaeleza ukweli kwamba ametoka kwenye matibabu na kuwaonesha vyeti vyote vya hospitali lakini bado wanaendelea kumshikiria", amesema Mrema

Pamoja na hayo, Mrema ameendelea kwa kusema "mpaka sasa hivi hatua tulizozichukua ni kumpeleka daktari wake ili aende kumcheki na kuwathibitishia Polisi kuwa Halima kweli ni mgonjwa pia wanasheria wa chama wataelekea kituoni hapo muda si mrefu".

Halima Mdee ni miongoni mwa viongozi wa Chadema wanaotuhumiwa na Jeshi la Polisi kufanya maandamano yasiyokuwa na kibali kipindi cha uchaguzi mdogo wa marudio katika jimbo la Kinondoni.

Askofu Shoo: Wanaopotosha Ukweli Waraka Wa Maaskofu KKKT Ni Wajinga

$
0
0
Mkuu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Dk. Fredrick Shoo, amesema wale wote wanaojaribu kupotosha ukweli wa waraka wa maskofu kwa kuupaka matope ni wajinga.

Askofu Shoo ametoa kauli hiyo leo katika Usharika wa Moshi Mjini Dayosisi ya kaskazini, mkoani Kilimanjaro wakati akitoa salamu za Pasaka katika ibada maalumu ya kusherekea sikukuu hiyo.

Amesema kumekuwa na baadhi ya watu wakiwamo wanasiasa ambao wamekuwa wakitumia nguvu nyingi kupotosha waraka  wa maaskofu hao na kulipaka kanisa matope kwa malengo yao binafsi jambo ambalo halipendezi na kwamba watu hao ni wajinga.

“Wapo wanaotumia nguvu nyingi kutaka kupotosha ujumbe wa waraka wa maaskofu na wamekuwa wakilipaka kanisa matope ili waweze kurejea katika waraka ule, watu hawa naweza kuwaita ni wajinga lakini pamoja na hilo nataka wakayatafakari na kama wanaona kuna hatua za kuchukua wachukue.

“Kanisa limekuwa linapata kejeli za aina mbalimbali kutoka kwa watu hao na kuwatuhumu kuwa maskofu walifikia maamuzi ya kuandika waraka huo kutokana na sababu za kimaslahi kwa maana ya sadaka makanisani kupungua jambo ambalo si la kweli.

“Kanisa linasitikika sana, tunaposema jambo la kweli na jambo linalohusu maisha ya Watanzania wote, halafu kunatokea watu chache ambao naweza kuwaita wajinga wanakebehi na kusema eti kwa sababu sadaka zimepungua kanisani sisi sadaka hazijapungua kwani wakristo wanajitoa sana na hatujapungukiwa na kitu ila tunasema yale tunayoyaamini,” amesema.

Askofu Shoo amesema anafahamu kuwa kupitia waraka ule maaskofu wa kanisa hilo watabatizwa majina ya aina mbalimbali na kwamba hizo ni jitihada za kujaribu kuuzima ukweli ulipo katika wataka huo na wao hawajali kuhusu hilo bali watasimamia ukweli zaidi.

“Najua tutaitwa majina mengi maaskofu na hizo ni jitihada za upotoshaji wa ule ukweli ulipo katika waraka na tukumbuke hili si jambo la hivi hivi tu…. kwani kwa wakati mmoja mabaraza ya  maaskofu wa makinsa makubwa mawili nchini kukaa na kutoa waraka ambao una ujumbe ulioshabihiana si kitu cha kawaida mimi nasema kuna kitu Mungu anataka kutuambia kupitia ujumbe ule tutafakari hili kama taifa,” amesema.


Mpenzi Wangu Anakosa ute Wakati wa Tendo Ushauri Wako Tafadhali

$
0
0
Tuna mwaka na miezi 3 toka tuanze uhusiano. Mwanzo nilikua namuandaa anatoa ute wakutosha kabisa ,ila kadri siku zinapozidi kusonga hata nimuandae vipi ute unatoka lakini wakulazimisha mno!!

Hali hiyo ilivyoanza tulijua labda ni hali ya mpito lakini hakuna mabadiliko yoyote... nikimuuliza anadai yeye mwenyewe haelewi na inamuumiza kuwa hivyo na hajui tatizo nini..

Nimeona nilete jamvini maana naamini hapa hakishindikani kitu....

Miujiza ya Sharifu Seif Mohamed..JE Umeachwa na Mme/Mke au Mpenzi, Umesongwa na Mitihani ya Maisha

$
0
0
SHARIFU SEIF MOHAMED ANAWASHUKURU WALE WOTE WANAOENDELEA KUPIGA SIMU, WENYE MATATIZO NA WALE WANAOTOA  SHUKRANI NA SHUHUDA JINSI TIBA ZAKE ZINAVYO WASAIDIA,

(Rudisha mahusiano yako ndani ya masaa 72 tu)

SHARIFU MOHAMED Ni  mtaalam na mnajimu maarufu wa nyota na kubashiri mambo yanayo watesa binadamu duniani kote na kupata ufumbuzi, Anatumia kitabu cha QUR'AN na Nyota

Je Umeachwa na UMPENDAE awe Mme/Mke na bado unampenda? Je Umekimbiwa na Mmeo/ Mkeo n anaishi na mtu mwingine? Je Umejaribu sehemu nyingi bila mafanikio? Mpigie simu SHARIFU SEIF sasa hivi ujionee Muujiza wa Papo kwa Papo, Anauwezo wa hali ya juu wa kusambaratisha mahusiano yao na kumrejesha kwako haraka sana na Kumfanya Atimize Ahadi zote Ndani ya Muda Mfupi Endapo Utafwata Atakacho Kuelekeza

 ZINDIKO LA NYUMBA NA BIASHARA, PETE ZA BAHATI, HUMALIZA KABISA TATIZO   HUZUIA CHUMA ULETE KWENYE BIASHARA, HURUDISHA MALI ZILIZOPOTEA, NA KUPONYA MAGONJWA SUGU ANAO UWEZO WA KUMRUDISHA ALIE MBALI AU ALIECHUKULIWA MSUKULE, KUPANDISHA NYOTA NA KUSHINDA BAHATI NA SIBU, KASAFISHA NYOTA NA KUKUPA MVUTO WA AJABU, KUTOA NUKSI NA VIFUNGO MBALIMBALI,  MAFANIKIO YA MAISHA NA UTAJIRI BILA MASHARI, NA MENGINE MENGI YA SIRI,

JE UMAHANGAIKA KUPATA MTOTO BILA MAFANIKIO? WASILIANA NA MTAALAMU HUYU KWANI YEYE HUFAULU PALE WOTE WALIPOSHINDWA, PIA UMALIZA KAZI ZILIZO SHINDIKANA NA WATAALAM WENGINE NDANI YA MASAA 24 TU,

(NA ANATIBU KWA NJIA YA SIMU UKIWA NCHI YOYOTE AU MKOA WOWOTE ENDAPO UTAFWATA MAELEKEZO YAKE)

Kwa ushauri na mawasiliano  zaidi Piga SIMU No:

Mobile +255 654-836970
WhatsApp 0756033670

Wakili wa ACT Wazalendo amekamatwa na Polisi kwa kuwatetea Madiwani

$
0
0
Leo April 1, 2018 Mjumbe wa Kamati Kuu, na Mwenyekiti wa Kamati ya Taifa ya Sheria ya ACT Wazalendo, Wakili Thomas Msasa amekamatwa na polisi jana mjini Kigoma kwa sababu ya kuwatetea Madiwani, Viongozi na Wanachama wa Chama hicho waliokuwa wamekamatwa na Jeshi la Polisi.

Taarifa iliyotolewa na Mwenyekiti wa ACT Wazalendo Kigoma, Sendwe Ibrahimu Mbaruku imesema Wakili Msasa alikwenda polisi kama Wakili wa Madiwani wawili wa ACT Wazalendo, Diwani wa Kata ya Kipampa, Mussa Mgongolwa, pamoja na Diwani wa Kata ya Kigoma, Hussein Kalyango, aliyekuwa mgombea Udiwani Kata ya Mwanga Winston Mogha, Katibu wa Ngome ya Vijana ya ACT Wazalendo Mkoa, Masabo, pamoja na wanachama na wafuasi mbalimbali wa ACT Wazalendo wa Mkoa wa Kigoma.

“Kukamatwa huku ni sehemu ya mpango wa CCM na Jeshi la Polisi wa kukamata Viongozi na Wafuasi wa Vyama vya Upinzani unaoendelea nchi nzima, na kuhakikisha kuwa wanawaweka ndani kwa muda mrefu kwa uonevu tu.” –Mwenyekiti Mbaruku

“Chama ngazi ya Mkoa, pamoja na Taifa tunashirikiana kuhakikisha wote waliokamatwa wanaachiwa au wanafikishwa mahakamani.” -Mwenyekiti Mbaruku

Dalali afunguka Simba kutwaa ubingwa msimu huu

$
0
0
Mwenyekiti wa zamani wa klabu ya Simba, Hassan Dalali, anaimani timu yake itatwaa ubingwa wa ligi msimu huu baada ya kuukosa kwa muda wa takribani miaka mitano.

Dalali ambaye aliwahi kufanya vizuri wakati akiwa Mwenyekiti wa Simba, amesema kikosi walichonacho hivi sasa kina morali ya juu na si kama kadhaa nyuma.

"Simba hii iko vizuri, hauwezi ukailinganisha na timu zingine katika ligi, uwezekano wa kubeba kombe upo kwa asilimia 100" alisema Dalali wakati akizungumza na kipindi cha Michezo, kupitia Radio One jana.

Aidha Dalali ametamba kwa kusema Simba ni lazima ishinde mchezo wa Jumanne dhidi ya Njombe Mji ili kuendelea kujitengenezea mazingira ya kuwa kileleni. Mchezo huo utapigwa Uwanja wa Sabasaba mjini Njombe.

Dalali ameeleza mchezo huo utakuwa mgumu kutokana na kila timu kuwa na uhitaji

Yanga Mdebwedo...Yachapwa na Watoto wa Singida United

$
0
0

Mechi iliyokuwa ikisubiriwa kwa hamu zaidi katika Azam Sports Federation Cup imemalizika Uwanja wa Namfua kwa wenyeji kuibuka na ushindi wa mabao 4-2 kwa njia ya matuta dhidi ya Yanga.

Mchezo huo wa hatua ya robo fainali ya mashindano hayo ulianza kwa kasi huku timu zote mbili zikipambana kupata bao la mapema.

Yanga ndiyo ilikuwa ya kwanza kujipatia bao lililofungwa na Yusuph Mhilu kufuatia mpira wa kona uliopigwa na Ibrahim Ajib kwenye dakika ya 24.

Bao hilo lilifanya dakika 45 za kwanza kumalizika huku Yanga wakiwa kifua mbele kwa goli moja.

Kipindi cha pili kilianza huku Singida wakionekana kulikamia zaidi lango la Yanga, ambapo katika dakika ya 47, Ken Ally, alisaawazishia Singida United kwa bao safi lililofanya mpaka dakika 90 zinamalizika matokeo yakiwa 1-1.

Baada ya dakika 90 kumalizika, hatua ya matuta ilifuata na Singida wakaweza kuibuka kidedea kwa ushindi wa penati 4-2 dhidi ya Yanga hivyo kuwafanya kuingia moja kwa moja katika hatua ya nusu fainali ya Kombe la FA.

Matokeo hayo yanaifanya Yanga iungane na Njombe Mji FC, Tanzania Prisons pamoja na Azam FC zilizoondolewa kwenye hatua hiyo ya robo fainali huku Singida ikiungana na JKT Tanzania, Mtibwa Sugar pamoja na Azam FC zilizotinga kuingia hatua ya nusu fainali.
Viewing all 104795 articles
Browse latest View live




Latest Images