Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104808 articles
Browse latest View live

Halima Mdee Kufikishwa Mahakamani Jumanne Aprili 3

$
0
0
Mbunge wa Kawe, Halima Mdee, anatarajia kufikishwa mahakamani Jumanne Aprili 3, kuungana viongozi wengine wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), akiwamo Mwenyekiti wake Freeman Mbowe, wanaoshtakiwa kwa makosa manane yakiwamo uchochezi, kuhamasisha maandamano na uasi.

Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Lazaro Mambosasa amesema hayo leo na kuongeza kuwa mbunge huyo amekiuka masharti yaliyomtaka kuripoti kituo cha polisi pamoja na viongozi wengine saba wa chama hicho kabla ya kufikishwa mahakamani.

Halima alikamatwa leo Jumapili Aprili Mosi, saa tisa alfajiri katika Uwanja wa Ndege wa Mwalimu Julius Nyerere (JNIA), alipokuwa akirejea nchini akitokea Afrika Kusini alipokuwa akipatiwa matibabu.

Aidha, alipoulizwa ni kwanini Halima amekamatwa wakati mawakili wake walikuwa wakitoa taarifa zake, Mambosasa amesema: “hayo ni maneno tu, anafahamu taratibu zikoje, anafahamau sheria zinasemaje kwa sababu wanatunga wenyewe huko bungeni hilo si suala la kujadili na mimi, asubiri atajibu hayo mahakamani.

Mambosasa amesema hayo muda mchache baada ya Chadema kulitaka Jeshi la Polisi kumpatia dhamana Mbunge ili aweze kuendelea na matibabu.

Mkurugenzi wa Itifaki, Mawasiliano na Mambo ya Nje ya chama hicho, John Mrema amesema licha ya kwamba Mbunge huyo kuwa mgonjwa ambaye hivi punde ametoka hospitali, lakini pia dhamana ni haki yake na lawama zote zitakuwa juu yao endapo afya ya mbunge huyo itatetereka.

“Hadi mchana wa leo Aprili Mosi, Jeshi la Polisi limeendelea kumshikilia Katika Kituo Kikuu cha Polisi Dar es Salaam na hajapatiwa dhamana pamoja na daktari wake kuwathibitishia polisi kuwa Mheshimiwa Halima ni mgonjwa.

“Tunasikitishwa na kulaani kitendo hiki cha polisi kuendelea, kumshikilia mgonjwa ambaye alikuwa amelazwa hospitalini, , tumetuma mawakili daktari wake lakini hawajafanikiwa mwisho, Jeshi la Polisi litawajibika kwa Watanzania endapo afya ya Halima Mdee ikitetereka au ikidhoofu zaidi na lawama zote zitakuwa juu yao,” amesema Mrema

Askofu Masangwa Akerwa Na Manabii Wa Uongo Wanaotoza Waumini Fedha Kuwaombea

$
0
0
Askofu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Dayosisi ya Kaskazini Kati, Dk. Solomon Masangwa amewataka waumini wa kanisa hilo kusimama katika imani zao wasidanganywe na manabii wa uongo wanaotoza waumini fedha.

Aidha amewataka waumini wa kikristo nchini kuishi kwa kuzingatia imani ya dini hiyo ili kuishi maisha yanayompendeza Mungu.

Dk. Masangwa ameyasema hayo leo Jumapili Aprili Mosi, mjini hapa alipokuwa akihubiri katika Ibada ya Pasaka iliyofanyika katika Usharika wa Mjini Kati Arusha na kuongeza kuwa kuna baadhi ya waumini ambao amewataka kuacha tabia ya kutanga tanga katika dini ambapo wamekuwa wakidanganywa na watu wanaojiita manabii na mitume.

“Kwanini mnakubali kudanganywa, siku hizi kuna watu wanajiita manabii, mitume na mnaenda kwao tena kwingine mnalipa kiingilio hata laki moja ili kumuona nabii au mtume,kwanini mdanganywe na mnasahau kusimama katika imani zenu,mnasahau ukombozi umepatikana kwa kifo na kufufuka kwa Yesu,” amesema.

Pamoja na mambo mengine, Askofu Masangwa amekemea vitendo vya uovu vinavyoendelea nchini ikiwamo mauaji ya watu wenye ulemavu wa ngozi na wizi.

“Baadhi ya waumini wamekuwa wakitaka kuishi maisha mazuri, biashara zao kukua kwa kasi ambapo wengine wanajihusisha na imani za kishirikina zinazowafanya kujiingiza katika vitendo viovu.

“Kwanini mnakwenda kukata viungo vya albino au kumrusha mwenzao au kuiba, unakwenda kutafuta hirizi ili biashara ishamiriili maisha yawe mazuri mnasahau Yesu ni  bwana wa mabwana, Mungu ndiye anayetoa uwezo na nguvu za kuwa tajiri, mtegemeeni si waganga,” amesema.

Download Upya Application Yetu Ya Udaku Special .....Ile Ya Zamani Tutaifuta

Askofu Banzi: Tuwaheshimu Marehemu, Tusiwafunge Kwenye Viroba

$
0
0
Askofu wa Kanisa Katoliki Jimbo la Tanga, Mhashamu Anthony Banzi ameitaka jamii kuiheshimu miili ya marehemu kwa kuwapa maziko ya heshima badala ya kuwafunga kwenye viroba na kuwatupa kwenye maji.

Amesema jambo ambalo si zuri machoni kwa wanadamu na kwa Mwenyezi Mungu na pia inakiuka utamaduni wetu kama Watanzania ambapo ameitaka jamii kubadilika kwa vitendo vya namna kwani vinaondoa utu wao.

Ameyasema hayo leo Jumapili Aprili Mosi, wakati akitoa salamu za Pasaka kwa waumini wa kanisa hilo kwenye misa iliyofanyika katika Kanisa la Mtakatifu Anthony wa Padua, Chumbageni Jijini Tanga.

“Lazima tuwaheshimu marehemu katika nchi yetu, pengine tunataka kuwa na utamaduni tofauti wafu wengi tunaambiwa wameokotwa ndani ya viroba kwenye maji na kuzikwa, je hali hii inatupeleka wapi kama taifa” Tujitafakari kwa jambo hilo.

“Kama unavyoheshimika ukiwa mzima, marehemu pia wanapaswa kuheshimika hata wanapokuwa wamefariki kwa kuhifadhiwa mahali ambapo hawawezi kuonekana tena,” amesema.

Aidha, amewataka viongozi ambao wanajukumu la kulinda usalama wa nchi, kuhakikisha wananchi wanaishi kwa amani na utulivu ambayo ni tunu tulioachiwa na waasisi wa taifa hili.

“Mara nyingi tumesikia raia wema wametoa taarifa ya kukamatwa wahalifu hivyo ni jukumu la waliochaguliwa kutazama usalama wao kwa lengo la kuwawezesha kutimiza majukumu mengine ya kimaendeleo,” amesema Askofu Banzi.

Askofu Manase: Kila Kanisa Likitoa Waraka Wake Taifa Halitakalika

$
0
0
Askofu Mkuu wa Makanisa ya Babtisti Tanzania, Mchungaji Arnold Manase amewataka viongozi wa dini kushauri kwa namna njema bila kutabiria nchi mambo mabaya kwani ubaya huenea haraka kuliko wema.

Aidha, amesema kila dhehebu nchini likisimama na kutoa waraka wake taifa halitakalika.

Askofu Manase ameyasema hayo leo Jumapili Aprili Mosi, jijini Arusha wakati akitoa salam kwenye Ibada ya Pasaka katika Kanisa la Jerusalem Babtisti lilipo Ngarenaro mjini Arusha.

Kupitia Ibada hiyo, Askofu Manase amewaomba wadau wa amani nchini, ikiwamo Serikali kukaa na wadau ili kujadili mustabali wa taifa.

“Tunahitaji kuomba amani ya Mungu itawale, kama ambavyo Yesu Kristo alivyotuachia amani yake.

“Tukiwa kama viongozi wa dini kama kuna mambo tunaweza kushauri basi tuyashauri kwa namna njema tusitabirie nchi mambo mabaya Kwani ubaya unaenea haraka kuliko wema, nawasihi tuhubiri amani,” amesema Askofu Manase.

Pamoja na mambo mengine, Askofu Manase katika Ibada hiyo ameongoza maombi kuomba hekima kwa viongozi wa Serikali, madhehebu yote nchono ili hekima ya Yesu Kristo ikatawale kwenye mioyo yao.

Hongera Wasafi Kwa Kuwasha TV Yenu

$
0
0
Naiona wasafi Tv kupitia Azam decoder Chanell # 122. Ki ukweli mmeanza vizuri, Quality ya picha ni mzuri.
Mmechagua vyema kuweka ktk decoder ya Azam kwani kwa sasa hakina mpinzani kwa Tz.

Nawatabiri makubwa zaidi!

HONGERA DIAMOND na Uongozi wako!

Mpenzi wa Cristiano Ronaldo Aandika kwa Kiswahili Kwenye Post yake

$
0
0
Georgina Rodríguez ni mwanamitindo na ndio mpenzi wa sasa wa Ronaldo na wamefanikiwa kupata mtoto mmoja anayejulikana kwa jina la Alana Martina, hivyo katika insta story yake amepost picha yake na Ronaldo na kuandika ‘Hakuna Matata’

Msemo wa hakuna matata ni msemo wa Kiswahili ambao umeonekana kupendwa na umekuwa msemo maarufu sana kwa wageni wanaopenda kujua lugha ya Kiswahili, huo huwa ni msemo wao wa kwanza kujifunza lakini haijajulkana bado Georgina Rodríguez ameujulia wapi msemo huo.



Baada ya Kudanga Sana...Vera Sidika Aamua Kupata Ujauzito

$
0
0

Mlimbwende kutoka Kenya ambaye pia ni maarufu kwenye mitandao Vera Sidika, amethibitisha tetesi za kuwa mjamzito, na kusema kwamba ni kitu alichokuwa anakitamani sana.

Kwenye ukurasa wake wa instagram Vera Sidika ameandika Ujumbe akisema kuwa amejitahidi kuficha suala hilo kwa muda mrefu, lakini ameona ni vyema kuujulisha umma kwani mimba sio jambo la kuweza kuficha muda mrefu bila watu kuweza kukushtukia.

Kwenye post hiyo Vera amesema siku zote alikuwa akitamani kabla hajafikisha miaka 30 awe mama, na anashukuru Mungu kwa baraka alizompa za kuweza kupata ujauzito na hatimaye kusubiria mtoto wake wa kwanza kwa furaha akiwa ndani ya miaka 29 tu.


Hii Ndio Hotel ya Kifahari Aliyofikia Zari Dubai Kujiliwaza Baada ya Kumtema Diamond...Gharama zake Hizi Hapa

$
0
0
Zari The Boss Lady ametua nchini Dubai kwa ajili ya kula bata na kufurahia wikiendi ikiwa ni siku chache zimepita tangu aliposaini dili la mamilioni ya fedha na kampuni moja ya nepi za watato hapa Bongo.

Kupitia mtandao wa Instagram, mrembo huyo ameweka picha kadhaa akionyesha akiwa ameongozana na watoto wake wawili akiwemo Raphael G na Lil Q.

Zari na familia yake hiyo wamefikia kwenye moja ya hoteli maarufu Dubai inayofahamika kama Dusit Residence Dubai Marina. Gharama za Kulala kwenye hoteli hiyo kwa usiku mmoja kwa bei ya chini ni takribani 385,000 hadi 1,010,000.

Hata hivyo inadaiwa kuwa ex huyo wa Diamond hivi karibuni atarudi tena Tanzania kwa ajili ya kusaini mkataba mwingine na kampuni ambayo bado haijafahamika.

Nimekuta Picha za Utupu za Girlfriend Wangu Kwenye Simu yake...Ushauri Please

$
0
0
Jamani Wapendwa Sikukuu ya Pasaka imenikalia Pabaya leo yaani, My girl kaja kulala kwangu ili leo tusherekee wote hii siku kuna mahali tunaenda out of Town, ila sasa asubuhi ya leo wakati tunajiandaa nikachukua simu yake nikawa nampiga picha alivyopendeza baada ya kuvaaa sasa katika kuziangalia zile picha nikakutana na picha zingine za utupu alizopiga like one week ago, Sasa najiuliza hizo picha alipiga kwa ajili ya nani je alimtumia mtu maana kama ni mimi hakunitumia, nimemuuliza anasema alijipiga kujifurahisha, yaani hapa niko nae ila kama simwamini tena jamani naombeni ushauri.

By Lewis

Wema Sepetu Kaamua Kuvunja Kabati...Huo ndio Muonekano Wake Usiku wa Sinema Zetu Film Festival 2018

$
0
0

Wema Sepetu Kaamua Kuvunja Kabati...Huo ndio Muonekano Wake Usiku wa Sinema Zetu Film Festival 2018

Meli ya abiria ya Uingereza iliyozamishwa mwaka 1942 yaondolewa baharini

$
0
0
Meli ya abiria ya Uingereza iliyozamishwa wakati ilishambuliwa kwa bomu na ndege za Japan wakati wa vita vya pili vya dunia, imeinuliwa kutoka baharini pwani mwa Sri Lanka baada ya miaka 75.

SS Sagain, ambayo abiria wake wengi na mizigo iliokolewa mwaka 1942, imeinuliwa na kundi la wapiga mbizi kutoka kwa jeshi la wanaji wa Sri Lanka, Ilikuwa karibu umbali wa futi 35 chini ya bahari katika bandari ya Trincomalee.

Shughuli ya kuiinua meli hiyo ilichukua miezi kadhaa na ilifanywa na kikosi cha wanamaji cha Mashariki mwa Sri Lanka.



Mchungaji Lwakatare: Mwisho wa matatizo umekaribia

$
0
0
Waumini wa Kanisa la Mikocheni B Assemblies of God jijini Dar es Salaam leo wameadhimisha Sikukuu ya Pasaka ambayo ni kumbukumbu ya kufufuka kwa Mkombozi wao Yesu Kristo, huku wakiondoka na ujumbe wa amani na matumaini katika maisha yao.

Katika mahubiri na salamu zake za Pasaka, Mchungaji Kiongozi Dkt Getrude Lwakatare amewasihi watanzania kupendana na kudumisha amani, huku wakiamini kuwa kifo na hatimaye kufufuka kwa Yesu Kristo, ni ishara tosha kwamba mwisho wa matatizo yanayomkabili kila mtu katika maisha yake umekaribia.

Akifafanua salamu zake hizo, Dkt Lwakatare amesema kama ilivyotokea kwa Yesu Kristo, watanzania na hususani waumini wa dini ya Kikristo wanapaswa kuwa na imani kuwa matatizo pamoja na shida mbali mbali zinazowakabili mwisho wake umekaribia.

Maaskofu Hawajapoa...Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumatatu ya April 2

$
0
0


Maaskofu Hawajapoa...Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumatatu ya April 2

MBELE YA WEMA! Diamond na Mobeto Wakumbatiana Live!..Wema Anuna

$
0
0
Zile tuzo zilizokuwa zikiwaniwa kwa muda mrefu za 'Sinema Zetu International Film Festival' zilizoandaliwa na kituo cha Azam Tv, hatimaye zimefikia tamati na wasanii mbalimbali wa filamu wamejitokeza katika ukumbi wa Mlimani City, kwa ajili ya kushuhudia nani ataibuka kidedea na kujinyakulia tuzo katika vipengele tofauti tofauti.

Katika usiku huo wa ugawaji wa tuzo za SZIFF, watu maarufu kutoka katika tasnia mbalimbali na viongozi wa serikali walijitokeza, akiwemo mkali wa Bongo Fleva, Diamond Platnumz na mzazi mwenziye Hamisa Mobeto, ambao waliitwa jukwaani kwa ajili ya kutoa tuzo kwa mshindi.

Baada ya kupanda jukwaani Hapo Diamond na Mobeto walikumbatiana na mbongo fleva huyo akatoa maneno matamu ya mahaba kwa mama mtoto wake huyo, huku Malkia wa Bongo Muvi, Wema Sepetu, akishuhudia tukio hilo live, hali iliyozua minongo'no kwa wageni waalikwa waliofika ukumbini hapo.

VIDEO:


Download Upya Application Yetu Ya Udaku Special .....Ile Ya Zamani Tutaifuta

Tatua Matatizo yako Kwa Mtaalam wa Dua na Dawa za Kiarabu Pamoja na Mitishamba...

$
0
0
YULE MTAHALAM WA DUA NA DAWA ZA KIARABU NA ZA KIASILI YANI MITI SHAMBA SHARIFU LUKUMANI SASA YUPO HEWANI WENYE SHIDA ZITUATAZO CHEO KAZINI,KUONGEZEWA MSHAHARA KAZINI,MWENYE TATIZO LA NGUVU ZA KIUME,ALIEPOTELEWA NA HAMU YA KUFANYA TENDO LA NDOA, MWENYE KIFAFA,KISUKARI,FANGASI SEHEMU ZA SIRI KWA WALE WENYE MIILI MINENE MTOTO WA JICHO PAMOJA NA WALE WAKINA MAMA WANAOSUMBULIA NA CHANGO LA UZAZI PUMU YA MUDA MREFU WANAWAKE KUJAA MAJI SEHEMU ZA SIRI MWANAUME KUWAI KUFIKA KILELENI AU KUTOA MANII MFANO WA MAJIMAJI YAKIWA MEPESI AUTOWEZA KUMPA MKEO UJAUZITO JAMBO HILI LINAWASUMBUA WANAUME WALIO WENGI DUNIANI KWA KAWAIDA WANAUME ASIE NA TATIZO HILI UTOA MANII MAZITO NDIO YENYEUWEZO WA KUMPA MWANAMKE MIMBA.MWANAUME KUPATA MPENZI KWA ULAISI PASIPO NA GHARAMA YOYOTE YANI KWA WALE MADOMO ZEGE KUWA NA UWEZO WA KUSIKILIZWA HATAKAMA RAIA WA INCHI GANI NA UWEZO WA KURUDISHA MPENZI ALIE POTEA NA KUMFANYA AWE WAKO KWA WALE WASIO TAKA MITALA PIA UFANYA KAZI YA KUNG'ALISHA NYOTA SASA MATATIZO YAKO YAMEPATA SULUHISHO

 ANAPATIKA KWA MASAA ISHIRINI NA NNE WASILIANA NAE KWA NAMBA
 0762899488
0656145170
WhatsApp namba +255620665635

Dini Kuingiliwa na Siasa ndo Mwanzo wa Kutokomea Kabisa

$
0
0
Najaribu kutafakari mwenendo wa Siasa za matusi na kejeli,mwenendo wa Siasa za kutishana na Mwenendo wa siasa zisizokuwa na amani kabisa uhuru kuminywa bila sababu za msingi.Wakati nawaza haya pia nahisi tupo wengi ambao tushafikiria haya.

Kati ya vitu ambavyo Wananchi huamini zaidi basi ni Dini pengine kuliko hata kingine chochote kile.Wananchi huamini viongozi wa dini kuliko wa vyama vya siasa au wanasiasa kabisa hii ni kutokana na uwoga juu ya nguvu zisizokuwa na kikomo kabisa (MUNGU)

Kiungo ambacho kinatumiwa kuunganisha watu wa rika zote,wa dini tofauti na daraja tofauti basi ni Dini.Dini ndo inawafanya watu wawe wamoja na kuzika tofauti zingine kwa sababu wote ni zao la Adam lkn leo kunatumika tofauti kabisa

Dini imeingiliwa na Siasa zisizokuwa na ukweli ndani yake.Siasa za chuki lengo kubwa ni kuwa nani achukue kundi kubwa la watu mwingine akose.Maaskofu wanaonekana wazalendo huku waislamu chini ya BAKWATA wanaoenakana kuunga mkono chama Tawala wala sio Wazalendo.Umeona shida hiyo?Tofauti za waziwazi kabisa.

Dini daima kama sehemu nyeti ya kulinda amani basi haifai kuingiliwa na Siasa kwa namna moja au nyingine.Inafaa iwe ni sehemu inayojitegemea peke yake wala haifai kuingiliwa

Tunaona Syria , Afghanistan,Iraq jinsi mambo yalivyowageukia kisa uingiliwaji wa Siasa na dini.Hata vita vya Eslael na Palestina ni hii ni kutokana na sintofahamu za Kidini ya Siasa kwa pamoja.Ni sababu zipi zinapelekea haya? Kwann yatokee?

Nawatakia Wakristo wote Pasaka Njema

Je Kunadalili ya Kuanza Kufunga ndoa na ROBOT?

$
0
0
Ulimwenguni sayansi na technolojia imeendelea kukuwa kwa kasi sana kupelekea tishio sasa la watu kuanza kufunga ndoa na Marobot kama wake au waume na kuishi maisha ya kimapenzi.


Wakati wasiwasi ukiendele kutanda kuwa Roboti anaweza kuchukua nafasi ya kimapenzi kwa mwenza wako na akafanya vizuri zaidi, Maumbile ya marobiti yameendelea kuboreshwa hatakufikia kuwa na mvuto kama binadamu wa kawaida.

Wataalamu wa tekinolojia wameendela kueleza kuwa marobot wanaendelea kuboreshwa zaidi na kufanana zaidi na binadamu ilikuweza kuamsha hisia za kimapenzi.

Dr Kevin Curran, mshirika mkogwe wa Institute of Electronic napia ni  ‘Electrical Engineer’ na ni ‘computer scientist’ wa chuo kikuu cha Ulster, amezidi sema ujio wa ‘cloud computing’ unaweza ongeza ubora zaidi wa robot hao kuwa natabia na mienendo itakayo fanana zaidi na binadamu wa kawaida.

Lulu Diva Adaiwa Kutupiwa Jina na Mke wa Mtu....

$
0
0
JAMANI wapenda ubuyu mtamu mpo? Basi kwa taarifa yenu ubuyu wa motomoto Pasaka hii unamhusu mwanamuziki wa kike anayefanya poa kwa sasa kwenye Bongo Fleva, Lulu Abbas ‘Lulu Diva’.

Kwa mujibu wa mtoa ubuyu wetu ambaye ni mtu wa karibu wa Lulu Diva, mwanadada huyo anadaiwa kutupiwa jini na mke wa mtu baada ya kumchukulia mumewe miaka kadhaa iliyopita.

Inasemekana kwamba, jini huyo kazi yake ni kumharibia Lulu Diva ili asipate mwanaume wa kumuoa badala yake awe anahangaika na wanaume tu hadi uzeeni kwake.

“Ninyi muulizeni kama baada ya tukio hilo la kutupiwa jini, kuna mwanaume yeyote ambaye amewahi kutulia naye?

MAHARI YARUDISHWA

“Kila mwanaume aliyempata aliingia mitini. Kama ni kuolewa, basi Lulu Diva angeolewa mwaka jana mwishoni, lakini mchumba huyo alipobaini anatoka kimapenzi na mwanamuziki mwenzake, akaomba mahari yake irudishwe maana alikuwa ameshatoa kabisa mahari,” kilisema chanzo.

HUYU HAPA LULU DIVA

Baada ya kuumung’unya ubuyu huo, Ijumaa Wikienda lilimtafuta Lulu Diva na kumuuliza juu ya jambo hiyo ambapo mambo yalikuwa hivi;

Ijumaa Wikienda: Mambo vipi Lulu Diva?

Lulu Diva: Poa tu, naona leo kuna ishu.

Ijumaa Wikienda: Ni kweli kuna ishu kwelikweli maana hapa kuna ubuyu kuwa uliwahi kutupiwa jini na mke wa mtu ndiyo maana huwa hutulii na mpenzi mmoja au huolewi. Je, hii ishu ikoje?

Lulu Diva: Kwanza niseme, huyo aliyewaambia nimeshamjua maana ni mimi mwenyewe niliamua kumwambia ishu hiyo.

Isitoshe mimi nilitoa siri hiyo kwa sababu kila mipango yangu ya ndoa ikikamilika, kunatokea jambo na mwanaume anasema ana mambo yake mengine.

Hapo kama siyo kupigwa juju ni nini? Hilo la kwamba aliyenipiga juju ni mume wa mtu ni siri yangu.

Ijumaa Wikienda: Je, utaishi hivyo hadi lini?

Lulu Diva: Ninamuomba Mungu aniondolee huyo jini ili siku moja na mimi nimpate wangu wa kufa na kuzikana, tudumu hadi kifo kitutenganishe.

Viewing all 104808 articles
Browse latest View live


Latest Images