Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104789 articles
Browse latest View live

Tuzo za Sinema Zetu Zampa Dili Nono Wema Sepetu

$
0
0
Tuzo za Sinema Zetu Zampa Dili Nono Wema Sepetu
MWIGIZAJI bora wa kike katika tasnia ya filamu nchini Tanzania Wema Sepetu amesaini mkataba mnono na Kampuni ya Auguster kwa ajili ya usambazaji wa filamu yake ya Heaven Sent.

Mkataba huo umesainiwa leo katika mkutano uliofanyika ndani ya studio za Azam TV jijini Dar es Salaam, ambapo kampuni hiyo imewakilishwa na Ofisa Uhusiano wake Nembris Soka.

Tukio pia limeshuhudiwa na mwandishi na muongozaji wa filamu hiyo, Neema Ndepanya.

Kwa upande wa Wema amesema tangu kutolewa rasmi kwa filamu hiyo, wapenzi wake wamekuwa wakiipata kupitia ‘Application’ ya Wema Sepetu, na hapakuwa na DVD zozote ambazo zilikuwa zikisambazwa kwa watu.

Amesema kampuni hiyo imeamua kufanya kazi hiyo baada ya filamu hiyo kushinda tuzo mbili katika Tuzo za Kimataifa za Filamu (SZIFF) zilizofanyika Aprili  MOSI, mwaka huu katika Ukumbi wa Mlimani City.

Soka yeye amesema Kampuni ya Auguster wamevutiwa na kiwango cha filamu hiyo na wameona jinsi mashabiki wa filamu nchini walivyo na kiu ya kuitazama filamu hiyo, na ndiyo maana wameamua kuifanya kazi hiyo ya usambazaji ili iwafikie watu.


TCRA Yatoa Hukumu kwa Times Fm Kisa Daimond... Clouds Nayo Yapewa Onyo Kali

$
0
0
TCRA Yatoa Hukumu kwa Times Fm Kisa Daimond... Clouds Nayo Yapewa Onyo Kali
KAMATI ya Maudhui ya Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA),imetoa hukumu kwa vituo viwili vya radio vya Times FM na Clouds FM kwa makosa ya ukiukwaji wa kanuni za utangazaji za mwaka 2018.

Taarifa iliyotolewa leo jijini Dar es Salaam imesema kuwa Radio ya Times FM walitangaza mahojiano na mwanamziki Nasib Abdul a.k.a Diamond Platinum.

Imeelezwa kwenye mahojiano hayo mwanamuziki huyo alitamka maneno yasiyofaa kimaudhui akimshambulia Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Juliana Shonza.
"Times FM wamepewa onyo na kutakiwa kumuomba radhi Naibu Waziri Shonza na jamii kwa ukiukwaji huo wa maadili ya utangazaji,"imesema sehemu ya taarifa hiyo.

Kuhusu Radio ya Clouds FM ni kwamba imepewa onyo kwa kutozingatia mizania ya utoaji wa habari uliohusu pande mbili ya mwanamuziki Ibrahim Musa a.k.a Roma mkatoliki na Naibu Waziri Shonza.

Kamati ya Rufaa TFF Yaridhia Wambura Kufungiwa Maisha Kujihusisha na Soka

$
0
0
Kamati ya Rufaa TFF Yaridhia Wambura Kufungiwa Maisha Kujihusisha na Soka
KAMATI ya Rufaa ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania(TFF) imeridhia uamuzi wa Kamati ya Maadili ya Shirikisho hilo kumfungia maisha, aliyekuwa Makamu wa Rais wa shirikisho hilo Michael Wambura.

Taarifa iliyotolewa muda huu inaeleza Kamati ya Rufaa ya Shirikisho hilo imeridhia na uamuzi wa kufungiwa kwa Wambura.

"Kamati ya Rufaa ya Shirikisho la Kabumbu nchini  (TFF) imeridhia maamuzi ya Kamati ya Maadili ya Shirikisho hilo kumfungia maisha, aliyekuwa Makamu wa Rais(TFF), Michael Richard Wambura"imesema taarifa hiyo ambayo pia imesambaa kwenye mitandao mbalimbali ya kijamii.Hata hivyo taarifa zaidi zitakujia muda wowote kuanzia sasa.

Awali kamati ya maadili ya TFF ilikutana Machi 14 mwaka huu kupitia shauri linalomhusu Wambura aliyekuwa anashtakiwa na Sekretarieti ya TFF kwa makosa matatu ya kimaadili.

Sekretarieti ya TFF iliwasilisha mbele ya Kamati mashtaka matatu (3) ambayo ni kupokea /kuchukua fedha za  TFF za malipo ambayo hayakuwa halali ikiwa ni kinyume na kifungu cha 73(1) cha Kanuni za Maadili za TFF Toleo la 2013.

Pia anatuhumiwa kughushi barua ya kuelekeza alipwe malipo ya kampuni ya JEKC SYSTEMS LIMITED huku akijua malipo hayo si halali ikiwa ni kinyume na kifungu cha 73(7) cha Kanuni za Maadili za TFF Toleo la 2013.

Hivyo kufanya vitendo vinavyoshusha hadhi ya Shirikisho ikiwa ni kinyume na ibara ya 50(1) ya Katiba ya TFF (kama ilivyorekebishwa 2015).

Kutokana na tuhuma hizo Wambura alipelekewa mwito wa kufika mbele ya Kamati Machi 14 mwaka huu ili awasilishe utetezi kuhusu tuhuma zinazomkabili.

Wambura alipewa hiari ya kutoa utetezi huo kwa mdomo, kutuma kwa maandishi, kuleta mashahidi au kutuma mwakilishi kama kifungu cha 58 cha Kanuni za Maadili za TFF toleo la 2013 kinavyoelekeza.

Hivyo Wambura alimtuma mwakilishi wake, Wakili Emanuel Muga, aliyefika na kuthibitisha ametumwa na mteja wake (Wambura) kuwasilisha utetezi wake mbele ya Kamati.

Baada ya kuelezwa mashtaka yanayomkabili mteja wake, Wakili Muga aliiomba Kamati kuwa mteja wake anaomba kupewa muda wa kupitia shauri hilo ili aandae utetezi, vielelezo, na mashahidi.

Mbunge CCM Ahoji Mwanamke Kuvaa Wigi Kwenye Nembo Ya Taifa

$
0
0
Mbunge CCM Ahoji Bibi Kuvaa Wigi Kwenye Nembo Ya Taifa
Mbunge wa Ulanga, Goodluck Mlinga (CCM), ameiomba Serikali ipige marufuku matumizi ya nembo ya Taifa yenye picha ya ya mwanamke na mwanamume (Bibi na Bwana) kwa sababu mwanamke huyo amevaa wigi hivyo kutoakisi maisha ya Mtanzania.

Mbunge huyo ameomba mwongozo wa Spika leo Ijumaa Aprili 6, kwa Mwenyekiti wa Bunge, Andrew Chenge ambapo amedai katika nembo hiyo kuna bwana amevaa lubega ambaye anaakisi maisha ya Mtanzania.

“Bibi aliyevaa wigi haakisi maisha halisi ya Mtanzania hivyo naiomba Serikali isitishe matumizi ya nembo hiyo na izuie isitumike hadi ifanyiwe marekebisho kwani bibi amevaa wigi ambalo haliakisi maisha ya Mtanzania,” amesema Mlinga.

Akijibu mwongozo huo Chenge alihoji iwapo tukio hilo limetokea leo hadi Mbunge huyo anauliza.

“Narudi kwenye kanuni je, suala hili limetokea leo na kama halijatokea leo halipo kwenye kanuni,” amesema.

Amesema kwa sasa wanatakiwa kuheshimu sheria inayosimamia nembo

Aliyegundua Madini ya Tanzanite Amshukuru Rais Magufuli kwa Kutambua Mchango Wake na Kumpa Milioni 100

$
0
0
Mgunduzi wa madini ya Tanzanite, Jumanne Ngoma ametoa ya moyoni baada ya Rais John Magufuli kusema Serikali inautambua mchango wake na kumpa Sh 100 milioni.

Akizungumza leo Aprili 6, wakati wa uzinduzi wa ukuta kuzungumza mgodi wa Tanzanite, Magufuli amesema atampa barua Mzee Ngoma ya kutambua mchango wake katika ugunduzi wa madini hayo yanayopatikana Tanzania pekee.

Mzee Ngoma alimshukuru Rais Magufuli na kusema alibaini kuwa kiongozi huyo amechaguliwa na Mungu tangu wakati wa kampeni za urais mwaka 2015.

“Ninakushukuru sana Rais, kwa heshima hii na kunitambua mimi kama mgunduzi wa madini, ni heshima kubwa kwangu na niseme kuwa wewe umechaguliwa na Mungu,” amesema na kuongeza:

“Wananchi wa Mirerani huyu ni Rais wa wanyonge, mimi nisingejulikana leo hii, hii ni furaha kubwa.”

 Mtoto wa Mzee Ngoma, Asha Ngoma naye ametoa neno katika hafla hiyo na kumshukuru Rais kwa kuusoma na kuufanyia kazi ujumbe wake wa simu aliomtumia Rais leo asubuhi saa 12 kasoro.

“Nikushukuru sana kwa sababu sikutegemea kama utausoma na kuufanyia kazi ujumbe wangu wa simu niliokutumia leo asubuhi. Naomba uendelee kuuthamini mchango wa mzee Ngoma na kuhakikisha madini ya Tanzanite yanaendelea kuwa na thamani,” amesema.

Mwanamume Atolewa Mswaki Tumboni Uliokwama kwa Siku Sita

$
0
0
Mwanamume Atolewa Mswaki Tumboni Uliokwama kwa Siku Sita
Madaktari katika Hospitali Kuu ya Mkoa ya Pwani (CPGH) mjini Mombasa, Kenya wamefanikiwa kuutoa mswaki ambao ulikuwa umekwama tumboni mwa mwanamume mmoja kwa siku sita.

David Charo alikuwa akipiga mswaki alipoumeza kimakosa Jumapili wiki iliyopita apokuwa anajiandaa kwenda kazini Bamba, Kilifi.

Kufikia jana, alikuwa ameanza kupata matatizo ya kupumua.

Awali, madaktari walikuwa wamedokeza kwamba angehitaji kufanyiwa upasuaji kuutoa.

Lakini Ijumaa asubuhi, madaktari wakiondozwa na Ramadhan Omar wamefanikiwa kuutoa mswaki huo bila kumfanyia upasuaji wa kawaida.

Badala yake, wamemfanyia upasuaji wa kutumia matundu madogo.

Jumapili, Charo alipokuwa alipoumeza mswaki huo kimakosa, awali ulikwama ndani ya koo kabla ya kutumbukia ndani tumboni.

Juhudi za nduguye mdogo Julius Charo za kuutoa hazikufanikiwa na ikalazimu wamkimbize hospitali iliyokuwa karibu.

"Tulipompeleka kwenye hospitali hiyo, madaktari walitushauri kumleta katika hospitali hii ya Pwani ambapo alipigwa picha ya x-ray, lakini kwa muda hakufanyiwa matibabu yoyote," Bw Julius aliambia gazeti la Nation.

"Ninaweza tu kulala au kusimama. Siwezi kujikunja au kuinama. Ninapojaribu kujipinda, nausikia mswaki ukinibana," alisema awali alipokuwa anahojiwa na gazeti la Nation.

Akizungumza na gazeti la kibinafsi la Star awali, Bw Charo alikuwa amesema amekuwa akiutumia mswaki huo kupiga mswaki kwa miaka 20.

"Ni makosa tu kwamba uliteleza kutoka mikononi mwangu Jumapili. Lakini hali yangu ni nzuri," alisema.

Serikali Iwafukuze Wabunge Wenye Elimu ya Darasa la Saba- Mbunge Msukuma

$
0
0
 Serikali Iwafukuze  Wabunge Wenye Elimu ya Darasa la Saba- Mbunge Msukuma
Mbunge wa Geita Vijijini Joseph msukuma ameitaka serikali iwafukuze wabunge wenye elimu ya darasa la 7, iwapo haitawarudisha kazini walimu na watendaji wa serikali waliokuwa na elimu ya darasa la saba.


Msukuma ameyasema hayo Bungeni leo alipokuwa akichangia hotuba ya ofisi ya Waziri Mkuu, na kwamba wakishaondolewa warudishwe kama wabunge  wa viti maalum ili wawatetee darasa la saba wenzao.

“Wabunge wenzangu wa CCM tutoe tamko la kuwarudisha hawa watendaji na sio kuwalipa, na kama serikali itakaidi, na humu ndani kuna wabunge darasa la saba zaidi ya mia, na sio la saba tu, hata waliofeli form four, wenye vyeti havieleweki wapo humu ndani, ninaomba sana serikali kama hamuwezi kuwarudisha hawa watendaji, na sisi wabunge wa darasa la saba humu ndani mtufukuze, sioni sababu hata ya wabunge wa darasa la saba kuwa humu ndani, ni bora katiba ikatuondoa humu, mturudishe kwa viti maalum kwa sababu na sisi tuko wengi wa darasa la saba”, amesema Mbunge Msukuma.

Mbunge Msukuma ameendelea kwa kusema kwamba kitendo cha serikali kufukuza watendaji wa serikali ambao wana elimu ya darasa la saba sio sahihi na sio haki, kwani wao ndio watendaji wazuri wa kazi kuliko wale wenye elimu kubwa.

“Nashangaa ni kwa nini wamewafukuza watendaji wa vijiji wa darasa la saba, wanataka hizi nafasi za watu wa darasa la saba wapewe watu wa vyuo vikuu, ni kijiji gani mmepeleka mtendaji 'graduate' aliyeweza kufanya kazi akawazidi darasa la saba, tumefukuza madereva, mnataka watoto wenu wanaosoma nje mpaka vyo vikuu ndio wakawe madereva, mnamfukuza mtu amebakiza miaka miwili ya ustaafu, hamfanyi haki”, amesema Mbunge Joseph Msukuma.

Rais Magufuli Atengua Uteuzi wa Mkurugenzi Mpwapwa

$
0
0
Rais Magufuli atengua uteuzi wa mkurugenzi Mpwapwa
Rais John Magufuli ametengua uteuzi wa Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mpwapwa Mohamed Maje kuanzia leo kwa kilichoelezwa kushindwa kutimiza majukumu yake.

Taarifa iliyotolewa na Katibu Mkuu wa Tamisemi Mussa Iyombe inasema Maje amesababishia hasara serikali ikiwamo kushindwa hata kukusanya mapato ya serikali.

"Hata makusanyo ya mwaka huu hatuhjui anapeleka wapi hadi leo amekusanya asilimia 24 tu katika halmashari ya kongwa na Mpwapwa licha ya kuwa na vyazo vingi vya mapato.

Iyombe amesema Mkurugebnzi huyo kwa sasa yupo chini ya uchunguzi.


Punguza Unene Unaokusumbua Katika Mwili Kwa Kutumia Bidhaa za Edmark

$
0
0
Tumia Dawa za Edmark za Kupunguza uzito uliozidi Mwilini Mwako, Edmark ni Vurutubisho na Chakula Mbadala na Zimehakikiwa na TFDA...

Ni uhakika kwa afya yako,👉 kupunguza uzito na sumu mwilini, Mafuta Sehemu Mbaya, Kitambi na nyama uzembe na kutibu MAGONJWA Mbalimbali kwa msaada wako mfuate instagram: @my_health_my_wealth @my_health_my_wealth


Au Mtafute WhatsApp Huyu Dada kwa kutumia Namba +255783 566844

Pia Dawa za Edmark Zinaweza kupa Fursa ya Biashara Uweze pata Kipato Kirahisi kwa Kuwasaidia watu Kuimarisha Afya zao

Dada wa Kazi Anavaa Hivi...Mama Mwenye Nyumba Upo Unaangalia tu...Unategemea nini?

$
0
0
Wapo watu ambao bado hawajajua madhara ya mavazi, mavazi yanaweza kuharibu nyumba, dada wa kazi akijiachia namna hii na mwenye nyumba unaangalia tu madhara ni makubwa labda kama mnaishi wawili tu hapo ndani ila kama unaishi na mumeo kazi unayooo..!!

SOMA PIA: Soma Nafasi za Ajira 221 Zilizotangazwa Leo Ijumaa

Bashe Ataka Serikali Iunde Chombo Kuchunguza Mauaji Ya Muuza Machungwa Mbeya

$
0
0
Mbunge wa Nzega Mjini, Hussein Bashe (CCM), ameitaka Ofisi ya Waziri Mkuu na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, kuunda chombo maalumu kuchunguza mauaji ya muuza machungwa Allen Mapunda (20), anayedaiwa kuuawa mkoani Mbeya kwa kupigwa na polisi.

Akichangia hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Ofisi ya Waziri Mkuu bungeni leo Ijumaa aprili 6, Bashe amesema chombo hicho kitaondoa utata uliopo sasa ambapo wazazi wa marehemu wadai mtoto wao alipigwa na polisi huku jeshi hilo likikanusha kuhusika.

“Yapo mambo ambayo yanaanza kutokea ambayo yanaashiria kuanza kuwepo kwa migawanyiko katika taifa letu na mambo haya tukiendelea kuyatizama kwa macho, hayaleti taswira njema huko mbele na wala hayataweza kulifanya taifa hili kuwa moja wala kupambana na adui mkubwa ambaye ni umaskini.

“Yanatokea matukio ya kusikitisha katika nchi yetu, ambayo ukitazama huoni chombo chochote kikichukua jitihada za makusudi ambayo itawajengea Watanzania imani kwamba hata mimi mdogo nikiwa mkubwa yupo anayenilinda.

“Yamekuwa yakitokea matukio mengi na kukosa majibu katika nchi yetu, lipo tukio la kijana anaitwa Allan ambaye ni muuza machungwa pale Mbeya.

“Naiomba serikali kwa heshima kabisa, matukio ya namna hii yakiendelea kujengeka katika nchi yetu yataanzisha utamaduni wa kutowajibika, yanaharibu amani iliyo katika taifa letu.

“Kijana huyu amefariki, ripoti ya Mganga Mkuu wa Hospitali ya Rufaa ya Mbeya, inasema kijana huyu kafariki kwa majeraha ya ndani ya mwili wake.

“Familia yake inasema waliompiga ni jeshi la polisi, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya anasema hawahusiki, matokeo yake serikali imeenda kutoa rambirambi ya Sh 200,000,” amesema Bashe.

“Hii ndiyo sababu matukio ya namna hiyo yameendelea kuwepo, mimi ningeiomba Wizara ya Mambo ya Ndani na Ofisi ya Waziri Mkuu, waagize kuundwa kwa chombo rasmi huru ifanye uchunguzi ya haya mambo.

“Hatuwezi kuacha hii hali ya utamaduni wa kutojali ikaendelea katika nchi yetu, inahuzunisha na inaharibu taswira na hii ndiyo inatumika na watu wasiopenda nchi yetu kuendelea kuharibu heshima ya taifa letu. Naiomba serikali ichukue hatua katika jambo hili, hili ni jambo la msingi sana,” amesema Bashe.

Nataka Kupenda Kama Mjinga, Nizame Nipotee! Kama limbwata ni Kweli Lipo Basi Nilishwe Hata

$
0
0
It may sound strange but this has been my major wish for a while,

Nataka kupenda kama mjinga, yaani niwe zombiee, nizame mapenzini nipotelee huko. Kila nachoambiwa nione sawa niwe mjinga mjinga no reasoning.

Yale mapenzi usipowasiliana ama kumwona mtu wako for a day unajisikia mgonjwa, mapenzi ambayo unaongea na mtu wako for two or three hrs and you feel like its just 5 minutes na haujui mlikuwa mnaongea nini.

Yaani mapenzi ambapo nikiachwa au nililazimika kuacha basi nichanganyikiwe, nishindwe kula, nikose usingizi, nipungue uzito, nione kama dunia imekwisha shughuli zangu nishindwe kufanya, kichwa kigome kufukiri

Kama limbwata ni kweli lipo basi nilishwe hata hilo, haya mapenzi ya kupenda robo robo with a lot of reasoning sio nayotaka.

Natamani kupenda with all my heart, soul, mind, body and my everything, nataka kupenda kamili kamili, kwa kila kitu, mpenzi wangu awe kila kitu, awe ndio dunia na maisha yangu.

Trust me I want to love like nothing else

Jovin

SOMA PIA: Nimechanganyikiwa Nimegundua Mke wangu na Dada wa Kazi Wanasagana

Jenerali Mabeyo Ampa Ahadi Nzito Rais Magufuli

$
0
0
Mkuu wa Majeshi nchini ampa ahadi nzito Rais Magufuli
Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Tanzania, Jenerali Venance Mabeyo amesema kuwa kwa kuzingatia kiapo chao wataendelea kumuunga mkono Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambaye pia ni Amiri Jeshi Mkuu, Dk. John Pombe Magufuli katika jitihada za kuleta maendeleo.



Akizungumza leo wakati Rais Magufuli azinduzi wa ukuta wa Tanzanite Mirerani Mkoani Manyara, Mobeyo amesema kuwa uhodari wao ndio nguzo kubwa ya Jeshi hilo.

“Tutazingatia kiapo chetu, uaminifu wetu, utii wetu na uhodari ambayo ndio nguzo kubwa kwa jeshi letu, tutaendelea kukuunga mkono katika jitihada zako za kuliletea maendeleo Taifa letu Mh. Rais na Amiri Jeshi Mkuu sisi tuko tayari kwa Watanzania wenzangu nawasihi sana tujivunie Tanzania yetu na tuilinde jukumu la ulinzi wa Taifa letu ni letu sote na jukumu la kuleta maendeleo kwenye Taifa hili ni la Watanzania wote,” amesema Mobeyo.

“Tuutunze ukuta huu na ibakie kuwa alama ya umoja wetu kulinda rasilimali zetu tufanye kazi kwa manufaa ya Taifa letu , Tanzania ndio Tunu tuliopewa na Mwenyezi Mungu tuilinde amani yetu na kuidumisha kwa gharama yoyote ile, Jeshi la Wananchi wa Tanzania liko imara kwa umoja wetu tutafanikiwa,” ameongeza.

Magufuli Awataja Wanaochonganisha Nchi

$
0
0
Magufuli Awataja Wanaochonganisha Nchi
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli, ameweka wazi kuwa hatua inazopiga serikali kudhibiti uchumi, waliokuwa na tabia za kutuibia rasilimali hawawezi kufurahia, hivyo watatumia njia yoyote kukwamisha ikiwemo kuchonganisha.


Rais Magufuli ametoa kauli hiyo leo alipokuwa akihutubia umma wakati wa uzinduzi wa ukuta uliojengwa kuzunguka eneo lenye madini ya Tanzanite, ambayo yanapatikana Tanzania pekee .

Rais Magufuli amesema watu hao wakiwemo wale waliokuwa wanaiba wanyama na kuwasafirisha kwa ndege ili miaka ya baadaye wasiwe na sababu ya kuja Tanzania kutalii, watatumia mbinu yoyote kuhakikisha Tanzania haifanikiwi kujikwamua kiuchumi, ili waje watawale tena.

“Awamu ya tano inapambana vita ya uchumi, vita ya uchumi ni ngumu, inapambana na mabeberu ya kila aina, tunaowazuia wizi hawawezi wakafurahi, tunapowazuia wizi wa dhahabu hawawezi wakafurahi, waliokuwa wanasafirisha wanyama wetu kwenye ndege wakiwa hai ili miaka ijayo wasije hapa kutalii, hawawezi wakafurahi. Na ni watu wenye uwezo mkubwa, mengine ni mataifa makubwa kutoka nje, wataleta vitimbwi vya kila aina, watawachonganisha kwa kila aina, kwa sababu ukitaka watu uwatawale ni kuwachonganisha”, amesema Rais Magufuli.

Rais Magufuli ameendelea kwa kusema ...”wapo waliokuwa wanataka nchi yetu isiendelee, unanunua ndege, wanatumiwa watu wanashangilia kukamatwa ndege yao, ni ushetani kweli kweli, ndege ni yenu, mtapanda wote lakini mtu anasimama pale anasema afadhali imeshikwa, ibaki huko huko, mnajiulizaje mtu wa aina hiyo, mali ni yenu, imeshikwa ni mali yenu lakini wanashangilia.

Sambamba na hilo Rais Magufuli amewataka watanzania kuwa wazalendo na kuzingatia uchumi wa nchi, na sio kushangilia pale panapotokea tatizo.

Bashe Ataka Serikali Iunde Chombo Kuchunguza Mauaji Ya Muuza Machungwa Mbeya

$
0
0
Bashe Ataka Serikali Iunde Chombo Kuchunguza Mauaji Ya Muuza Machungwa Mbeya
Mbunge wa Nzega Mjini, Hussein Bashe (CCM), ameitaka Ofisi ya Waziri Mkuu na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, kuunda chombo maalumu kuchunguza mauaji ya muuza machungwa Allen Mapunda (20), anayedaiwa kuuawa mkoani Mbeya kwa kupigwa na polisi.

Akichangia hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Ofisi ya Waziri Mkuu bungeni leo Ijumaa aprili 6, Bashe amesema chombo hicho kitaondoa utata uliopo sasa ambapo wazazi wa marehemu wadai mtoto wao alipigwa na polisi huku jeshi hilo likikanusha kuhusika.

SOMA PIA: Mume wa Mtu Sumu, Look at What Happened to This Cute Lady

“Yapo mambo ambayo yanaanza kutokea ambayo yanaashiria kuanza kuwepo kwa migawanyiko katika taifa letu na mambo haya tukiendelea kuyatizama kwa macho, hayaleti taswira njema huko mbele na wala hayataweza kulifanya taifa hili kuwa moja wala kupambana na adui mkubwa ambaye ni umaskini.

“Yanatokea matukio ya kusikitisha katika nchi yetu, ambayo ukitazama huoni chombo chochote kikichukua jitihada za makusudi ambayo itawajengea Watanzania imani kwamba hata mimi mdogo nikiwa mkubwa yupo anayenilinda.

“Yamekuwa yakitokea matukio mengi na kukosa majibu katika nchi yetu, lipo tukio la kijana anaitwa Allan ambaye ni muuza machungwa pale Mbeya.

“Naiomba serikali kwa heshima kabisa, matukio ya namna hii yakiendelea kujengeka katika nchi yetu yataanzisha utamaduni wa kutowajibika, yanaharibu amani iliyo katika taifa letu.

“Kijana huyu amefariki, ripoti ya Mganga Mkuu wa Hospitali ya Rufaa ya Mbeya, inasema kijana huyu kafariki kwa majeraha ya ndani ya mwili wake.

“Familia yake inasema waliompiga ni jeshi la polisi, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya anasema hawahusiki, matokeo yake serikali imeenda kutoa rambirambi ya Sh 200,000,” amesema Bashe.

“Hii ndiyo sababu matukio ya namna hiyo yameendelea kuwepo, mimi ningeiomba Wizara ya Mambo ya Ndani na Ofisi ya Waziri Mkuu, waagize kuundwa kwa chombo rasmi huru ifanye uchunguzi ya haya mambo.

“Hatuwezi kuacha hii hali ya utamaduni wa kutojali ikaendelea katika nchi yetu, inahuzunisha na inaharibu taswira na hii ndiyo inatumika na watu wasiopenda nchi yetu kuendelea kuharibu heshima ya taifa letu. Naiomba serikali ichukue hatua katika jambo hili, hili ni jambo la msingi sana,” amesema Bashe.

Polisi Wamshikilia Kijana Mmoja Aliyeweka Mwili wa Mama Yake Kwenye Friji kwa Miaka Mitatu

$
0
0
 Polisi nchini India wameeleza kuwa wanamshikilia mwanaume mmoja ambaye aliweka mwili wa mama yake mzazi aliyekufa kwenye freezer na kuishi nao kwa miaka 3.  Mtuhumiwa huyo Subhabrata Majumdar anaelezwa kuwa aliweza kutunza mwili huo kwenye freezer kwa kutumia kemikali za kuuchoma mwili wa marehemu.  Uchunguzi juu ya tukio hili unaendelea huku polisi wakieleza kuwa wanahisi alitunza mwili huo ili apate mafao ya mama yake na pia alikuwa akiamini kuwa mama yake atazaliwa upya kama mwili wake utatunzwa.  Kesi ya Uhujumu Uchumi ‘Ifikie mahali washtakiwa wajulikane wanafungwa ama lah” Hakimu
Polisi nchini India wameeleza kuwa wanamshikilia mwanaume mmoja ambaye aliweka mwili wa mama yake mzazi aliyekufa kwenye freezer na kuishi nao kwa miaka 3.

Mtuhumiwa huyo Subhabrata Majumdar anaelezwa kuwa aliweza kutunza mwili huo kwenye freezer kwa kutumia kemikali za kuuchoma mwili wa marehemu.

Uchunguzi juu ya tukio hili unaendelea huku polisi wakieleza kuwa wanahisi alitunza mwili huo ili apate mafao ya mama yake na pia alikuwa akiamini kuwa mama yake atazaliwa upya kama mwili wake utatunzwa.

Kesi ya Uhujumu Uchumi ‘Ifikie mahali washtakiwa wajulikane wanafungwa ama lah” Hakimu

SOMA PIA: Ndoa Nyingi za Kizazi Hiki Zinavunjika Kwa Sababu za Kijinga, Nguvu ya Mwanamke Katika Ndoa

SOMA PIA: KUFIKA KILELENI KWA MWANAMKE NDIO KUKOJE?

Rufaa ya Wambura yagonga mwamba.......Ataendelea na Kifungo

$
0
0
Kamati ya Rufaa ya Maadili ya TFF imetupilia mbali rufaa ya aliyekuwa makamu wa Rais wa shirikisho hilo Ndg. Michael Wambura aliyefungiwa maisha kutojihusisha na soka mapema mwezi Machi.

Taarifa ya TFF leo, imeeleza kuwa baada ya kupitia hoja zake za kukata rufaa kamati imejiridhisha na maamuzi ya awali yaliyotolewa na Kamati ya Maadili ya kumfungia Maisha.‬

Machi 14 Wambura akiwa Makamu wa Rais wa TFF alifikishwa kwenye kamati hiyo kwa masuala ya kimaadili, akikabiliwa na makosa matatu kupokea fedha za shirikisho malipo yasiyo halali, kugushi barua na kushusha hadhi ya Shirikisho.

Machi 15 Kamati ya Maadili ya TFF ilimfungia Michael Wambura kifungo cha kutojihusisha na mpira wa Miguu maisha kwa mujibu wa kifungu cha 73(1) (c) cha Kanuni za Maadili ya TFF Toleo la 2013. Baada ya kupatikana na makosa matatu.

Mara kadhaa Wambura amekuwa akijitokeza hadharani na kuweka wazi kuwa hakubaliani na maamuzi hayo kwani hakupewa nafasi

PIA SOMA: JE, NI KWELI KUWA KILA MWANAMKE ANAJIUZA NA SIO WALE TU WANAOSIMAMA BUGURUNI??

Makosa Wanayofanya Wanandoa Wawapo Chumbani na Wenzi Wao

$
0
0

Ni matumaini yangu kwamba u mzima wa afya na unaendelea vyema na majukumu yako ya kila siku.

Leo ningependa kujadiliana na wewe msomaji wangu kuhusu makosa ambayo watu wengi huwa wanayafanya wawapo chumbani na wenzi wao, hususan wanandoa au wapenzi wanaoishi pamoja.

Wapenzi wengi wanaishi kwa mazoea, hawajui nini wafanye na nini wasifanye kwa ajili ya kupalilia mapenzi yao na matokeo yake, inakuwa rahisi mume kumchoka mke au mke kumchoka mume kwa sababu ya vitu ambavyo wahusika wenyewe ndiyo wamevikaribisha.

Yapo makosa ambayo watu wengi wamekuwa wakiyafanya wawapo chumbani na wenzi wao, iwe ni kwa kujua au kwa kutokujua.

Hakuna muda wa muhimu kwa wanandoa au wapenzi wanaoishi pamoja, kama ule muda kabla hamjapitiwa na usingizi. Ukiwa makini, utayafurahia mapenzi lakini ukikosa umakini na kuyafanya makosa yafuatayo, utakuwa unaiua ndoa yako kwa mikono yako mwenyewe.

Yafuatayo ni makosa ambayo wapenzi wengi huyafanya kila siku na kusababisha mapenzi yapungue taratibu:

•KWENDA KULALA MUDA TOFAUTI
Yawezekana watu wengi wanalichukulia suala la kila mmoja kwenda kulala kwa wakati wake kama jambo la kawaida. Kwamba wanandoa au wapenzi wanaishi pamoja lakini kila mtu ana ratiba yake ya kwenda kulala, huyu akiwahi leo kupanda kitandani, yule anachelewa, yule akichelewa huyu anawahi, ilimradi tu mnapishana.

Wataalamu wa uhusiano wanaeleza suala hili kuwa sumu kali kwa wapendanao kwa sababu kisaikolojia, unapopanda peke yako kitandani kulala, nafsi inajihisi upweke na taratibu inaanza kujitenga na ya umpendaye.

Mkiendelea hivi kwa muda mrefu, hisia zinapungua na baadaye unaanza kumchukulia mwenzi wako kama mtu wa kawaida tu, ambaye hata asipokuwepo au ukikosa ukaribu wake maisha yako yanaendelea kama kawaida.

Kama na wewe ni miongoni mwa watu wenye tabia hii, badilika mara moja. Hutakiwi kuwa na visingizio katika hili, muda wa kulala ukifika, hakikisha unaambatana na mwenzi wako kupanda kitandani.

Faida nyingine ya kuongozana pamoja kwenda kulala, hata kama kulitokea mikwaruzano ya hapa na pale kutwa nzima, huu ndiyo muda mzuri ambao kila mmoja anaweza kueleza dukuduku lake na kumaliza tofauti kati yenu.

Nandy: Huwa Napuuza kwa Kumuonesha Anachofanya ni cha Kijinga

$
0
0
Hitmaker wa ngoma ‘Kivuruge’, Nandy a.k.a African Princess amesema moja ya vitu asivyovipenda katika muziki wake ni kuingia katika beef na msanii mwingine.

Muimbaji huyu ameiambia Clouds TV kuwa yeye sio msanii wa kupenda ugomvi na yeyote anayetaka ugomvi kwake huwa anampuuzia.

“Mimi sio mtu wa ugomvi wa mara kwa mara kwa hiyo sitamani kuingia kwenye ugomvi na mtu.

" Huwa napuuzia kwa kumuonyesha kuwa anachokifanya ni cha kijinga sifuatili, yaani Simuonyeshi kuwa nimeshtushwa na kitu ambacho anakifanya au labda nakifuatilia,” amesema Nandy.

Utakumbuku kumekuwa na stori zinazodai kuwa Nandy na Ruby wana beef, hata hivyo wote wawili wamekuwa wakikanusha hilo kila wanapoulizwa na vyombo vya habari.

Punguza Unene Unaokusumbua Katika Mwili Kwa Kutumia Bidhaa za Edmark

$
0
0
Tumia Dawa za Edmark za Kupunguza uzito uliozidi Mwilini Mwako, Edmark ni Vurutubisho na Chakula Mbadala na Zimehakikiwa na TFDA...

Ni uhakika kwa afya yako,👉 kupunguza uzito na sumu mwilini, Mafuta Sehemu Mbaya, Kitambi na nyama uzembe na kutibu MAGONJWA Mbalimbali kwa msaada wako mfuate instagram: @my_health_my_wealth @my_health_my_wealth


Au Mtafute WhatsApp Huyu Dada kwa kutumia Namba +255783 566844

Pia Dawa za Edmark Zinaweza kupa Fursa ya Biashara Uweze pata Kipato Kirahisi kwa Kuwasaidia watu Kuimarisha Afya zao

Viewing all 104789 articles
Browse latest View live




Latest Images