Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104795 articles
Browse latest View live

Mmh Wema naye Afunguka Mazito Kuhusu Kifo Chake... Atakwa Azikwe Hivi

$
0
0
Mmh Wema naye Afunguka Mazito Kuhusu Kifo Chake... Atakwa Azikwe Hivi
HII ni kali! Ndivyo unavyoweza kusema baada ya staa wa filamu Bongo, Wema Isac Sepetu, kutoa kali ya aina yake kwa kueleza namna mazishi yake yatakavyokuwa punde tu Mungu atakapoutwaa uhai wake.

Kauli hiyo imekuja ikiwa ni siku chache baada ya msanii mwingine wa Bongo Fleva na Bongo Movie, Zuwena Mohamed ‘Shilole’ kusema siku akifa, aagiwe msikitini na si kwingineko.

Akizungumza na Ijumaa Wikienda, Wema alisema yeye angependa kwenye mazishi yake wahudhuriaji wapendeza, wafurahie maisha aliyokuwa akiishi na katika nyumba itakayokuwa na msiba wake, papambwe rangi ya pinki.



“Napenda sana siku ya mazishi yangu waombolezaji wawe kwenye muonekanao mzuri na pia sehemu ambayo mwili wangu utafikia pawe pamepambwa vizuri kwa maua ya pinki yanayovutia,” alisema Wema.

Staa huyo alifunguka zaidi kuwa kwenye mazishi yake hayo baada ya familia, mtu mwingine ambaye anataka awe mstari wa mbele kwenye mazishi yake ni staa mwenziye, Aunt Ezekiel na kudai kuwa yeye ndio ataweka ua wa kwanza kwenye kaburi lake kabla ya staa mwingine yeyote.



Wema alienda mbele zaidi na kusema kuwa kwa vile yeye ni mtoto wa Kiislam hatoruhusiwa kuagwa lakini jeneza lake lipambwe maua mengi ambapo watu watakuwa wamelizunguka na kuliombea.

“Ningependa sana baada ya familia yangu Aunt awe mstari wa mbele zaidi kuliko staa yeyote na yeye ndio aanze kuweka ua wa kwanza kwenye kaburi langu kabla ya staa yeyote yule na jeneza langu lipambwe maua mengi maana najua watu hawatoniaga,” alisema Wema.

Alikiba Kiboko Azindua Kinywaji Chake Siku ya Harusi Yake

$
0
0
Alikiba Kiboko Azindua Kinywaji Chake Siku ya Harusi Yake
Msanii wa Bongo Fleva, Alikiba ametumia sherehe ya harusi yake kuzindua rasmi kinywaji chake kinachofahamika kwa jina la Mofaya katika ukumbi wa Hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam ambako harusi hiyo ilikuwa ikifanyika usiku wa kuamkia leo Jumatatu.



Kinywaji hicho cha Mofaya hakina kilevi.

Buhari Kuwa Kiongozi wa Kwanza wa Afrika Kulakiwa na Donald Trump

$
0
0
 Buhari Kuwa Kiongozi wa Kwanza wa Afrika Kulakiwa na Donald Trump
Rais wa Nigeria Muhammadu Buhari atakuwa kiongozi wa kwanza wa taifa la kutoka bara Afrika kulakiwa na Rais wa Marekani Donald Trump White House atakapokutana na kiongozi huo kwa mashauriano rasmi mjini Washington baadaye leo.

Marais wengine wa Afrika wamewahi kukutana na Bw Trump akiwa rais, wakiwemo Paul Kagame wa Rwanda na Uhuru Kenyatta wa Kenya, lakini nje ya Marekani.

Rais Kenyatta alikutana na Trump pambizoni mwa mkutano wa G7 nchini Italia mwezi Mei mwaka jana, naye Rais Kagame akakutana na kiongozi huyo wa Marekani Januari mwaka huu mjini Davos, Uswizi pambizoni mwa mkutano mkuu kuhusu uchumi wa dunia.

Septemba mwaka jana, Rais wa Uganda Yoweri Museveni pia alikutana na kupigwa picha na Rais Trump kwenye dhifa iliyoandaliwa wakati wa mkutano wa viongozi wa nchi wanachama wa Umoja wa Mataifa jijini New York. Hakukuwa na mazungumzo yoyote hata hivyo na haikuwa ziara ya kikazi kwa Bw Museveni.

Wawili hao wanatarajiwa kujadiliana kuhusu masuala ya kiuchumi na kiusalama watakapokutana leo.

Lakini wengi watafuatilia kwa karibu mazungumzo hayo hasa baada ya Bw Trump kushutumiwa vikali kutokana na kuyaeleza mataifa ya Afrika kama ''machafu" au ya "mabwege" mapema mwaka huu.


Haji Manara Afunguka Kipigo Walichokipata Yanga Jana "Hata 'Corner' Wenzetu"

$
0
0
Haji Manara Afunguka Kipigo Walichokipata Yanga Jana "Hata 'Corner' Wenzetu"
Afisa Habari wa vinara wa Ligi Kuu Tanzania Bara Simba SC, Haji Manara amefunguka na kudai kipigo walichokipata Yanga jana Aprili 29, 2018 cha bao 1-0 ni cha heshima kutokana na wao kuwa mabingwa watetezi hivyo isingekuwa vizuri kuwadharaulisha mbele ya umati wa mashabiki.


Manara ametoa kauli hiyo mara baada ya 'Kariakoo Derby' kumalizika katika uwanja vya Taifa Jijini Dar es Salaam huku timu yake ikiwa imetoka na ushindi wa bao 1 lililofungwa mnamo mwa dakika 38 kupitia Erasto Nyoni kwa kutumia kichwa akiunganisha krosi ya Kichuya.

"Tunamshukuru Mwenyezi Mungu tumepata matokeo ila hatujaridhika bado mpaka tuwe mabingwa, 'perfomance' yetu kwa ujumla ilikuwa nzuri ndio maana hata 'corner' moja wenzetu hawakuweza kupata lakini sisi vilevile tulicheza kwa heshima", amesema Manara.

Pamoja na hayo, Manara ameendelea kwa kusema "kipindi cha kwanza kilipomalizika nilishuka chini nikazungumza na wachezaji wangu kuwa waende wakawafunge Yanga kwa heshima kwasababu wao ni mabingwa watetezi na msiende kuwafunga kwa dharau kwa hiyo niliwapa maelekezo madhuri vinginevyo tungewadharaulisha kwa kuwafunga mabao 5, 6 kwa hiyo tumewafunga kwa heshima kutokana ni wakubwa wenzetu".

Kutoka na ushindi walioupata jana Simba sasa wamekuwa wamefikisha alama 62 kwenye mechi 26 huku ikiwa haijapoteza mchezo hata mmoja kwenye ligi kuu msimu huu. Simba inabakiza alama 4 pekee ili iweze kuwa bingwa msimu huu.

Harusi ya Alikiba Kiboko Viongozi wa Serikali Wamiminika Ukumbini ..... Mama Salma Kikwete Ummy Mwalimu Waudhuria Kigwangala Atoa Zawadi Hii

$
0
0
Harusi ya Alikiba Kiboko Viongozi wa Serikali Wamiminika Ukumbini ..... Mama Salma Kikwete Ummy Mwalimu Waudhuria Kigwangala Atoa Zawadi Hii
Usiku wa jana imefanyika sherehe nyingine ya harusi ya Alikiba na mkewe Aminah Rikesh Ahmed na mdogo wake Abdu Kiba na Ruwayda katika ukumbi wa Serena Hotel jijini Dar es Salaam.

Sherehe hiyo ilifaana zaidi baada ya kuhudhuriwa na watu lukuki wakiwemo wazazi wa wana ndoa wote na watu maarufu pamoja na viongozi wa serikali akiwemo mke wa rais wa awamu ya nne, Mama Salma Kikwete, Waziri wa Àfya, Ummy Mwalimu, Naibu Waziri wa Kazi, Anthony Mavunde, Waziri wa Maliasili na Utalii Dkt. Hamis Kigwangalla na Gavana wa mji wa Mombosa, Hassan Joho ambaye pia ni mtu wa karibu wa msanii Kiba.


Mama Salma KKikwete (kushoto) akiwa na Waziri wa Àfya, Ummy Mwalimu

Katika sherehe hiyo Waziri Kigwangala amewataka maharusi wote kuchagua sehemu yoyote ya kitalii ndani ya Tanzania kwenda kufanyia fungate yao na yeye atagharamia kila kitu.



Wamiliki wa Sober Houses Wajibu Tuhuma za Serikali

$
0
0
Wamiliki wa Sober Houses Wajibu Tuhuma za Serikali
Wamiliki wa nyumba zinazosaidia waathirika wa dawa za kulevya nchini yaani 'Sober Houses' wamekanusha tuhuma za serikali kwamba wanatumia nyumba hizo kwa maslahi binafsi


Akiongea na waandishi wa habari Jiji Dar es Salaam Katibu wa Umoja wa Wamiliki wa Sober Houses, Pili Missanah, amekanusha vikali tuhuma zilizotolewa na baadhi ya Wabunge mnamo April 25, 2018 kwamba baadhi ya wamiliki wa nyumba hizo huwachoma sindano za dawa za kulevya baadhi ya waathirika pindi wanapokaribia kupona ili wazazi au walezi waendelee kuchangia fedha kwenye nyumba hizo.

Aidha, Pili Missanah amesema kwamba wapo tayari kutoa ushirikiano na pia wameiomba serikali kupitia Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya kufanya uchunguzi na kwamba, hawajapata malalamiko yoyote kutoka kwa wazazi au walezi wa waathirika hao kuhusu ya tuhuma hizo.

Pili amesisitizia kuwa kuna nyumba 22 pekee Tanzania na hadi sasa zina waathirika 737 wanaopatiwa matibabu wakiwemo wanawake 21 na wanaume 726 na wamefanikiwa kuokoa watu zaidi ya 4,000 ambao wameachana na matumizi ya dawa za kulevya na wanaendelea na shughuli nyingine za kimaendeleo.

Simba Yasubiri Point Tano Kuwapokonya Yanga Ubingwa VPL

$
0
0
Simba Yasubiri Point Tano Kuwapokonya Yanga  Ubingwa VPL
Ushindi wa Simba wa goli 1-0 dhidi ya Yanga unaifanya Simba ambayo imecheza michezo 26 ya Ligi na kusaliwa na michezo minne, ili iwe Bingwa bila ya kujali matokeo ya timu nyingine Simba inahitaji point tano yaani ishinde mchezo mmoja na itoke sare mchezo mmoja.

Kwa upande wa Yanga wao ili kutetea Ubingwa wao kunategemeana na Simba apoteze mechi tatu huku yeye akipata matokeo chanya, baada ya ushindi huo kocha wa Simba Pierre Lechantre amewaambiwa wachezaji wake kuwa sasa wanahitaji ushindi game moja na sare moja.

Rais JPM Awajibu Wabunge Wanaobeza Serikali Kukopa

$
0
0
Rais JPM Awajibu Wabunge Wanaobeza Serikali Kukopa
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli amewataka Watanzania kutowasikiliza Wabunge wanaosema serikali inadaiwa madeni ilhali wao wanapita katika barabara hizo kuelekea bungeni.



Rais Magufuli amesema kuwa hata katika ukopaji unaweza ukakopa leo na ukalipa baada ya miaka 40 au 50 huku akieleza kuwa madeni anayokopa yeye huenda yakalipwa yeye hayupo duniani.

Rais Magufuli ameyasema hayo mjini Iringa alipofungua barabara ya Lami ya Iringa – Migoli- Fufu inayounganisha mikoa ya Iringa na Dodoma.

“Kwahiyo mimi nataka niwaeleze ukweli ndugu zangu, lile deni walilokopa wakoloni waingereza kwa kujenga ile barabara ya Morogoro Road kule Dar es salaam deni lake limemalizika mwaka juzi amelimaliza Kikwete, deni lilikopwa kwaajili ya uhuru kile kipande na si barabara yote kwahiyo unaweza ukakopa leo ukalipa baada ya miaka labda 40 hata miaka 50 madeni tunayolipa sasa hivi yanayolipwa yamekopwa katika awamu hizo zote,“ amesema Rais Magufuli.

“Inawezekana awamu ya madeni ninayo kopa yatalipwa wala mimi sipo duniani na ndio maana huwa mnawasikia wengine wanazungumza serikali inadaiwa madeni na huwa wanasahau wengine wanatoka huku Iringa wanaitumia hiyo hiyo barabara kwenda Bungeni, wanaitumia barabara hiyo hiyo kwa magari yao waliyoyapata waliyokopeshwa lakini wakiisha fika kule wanasema serikali inadaiwa madeni wanasahau kuwa hayo madeni ni pamoja na barabara waliyoipitia wakati wanaenda Bungeni.“

Soma Nafasi za Kazi Zilizotangazwa Leo

Breaking News:Mahakama Yatoa Amri Hans Pop wa Simba Akamatwe

$
0
0
Breaking News:Mahakama Yatoa Amri  Hans Pop wa Simba Akamatwe
Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu imetoa amri kwamba mwenyekiti wa usajili wa Simba SC, Zacharia Hans Poppe na Franklin Lauwo wakamatwe na wafikishwe mahakamani kuunganishwa katika kesi inayomkabili Rais wa Klabu hiyo, Evans Aveva na Makamu wake Kaburu.

Amri hiyo imetolewa na Hakimu Mkazi Mkuu Thomas Simba baada ya Wakili wa TAKUKURU, Leonard Swai kubadilisha hati ya mashtaka na kuwaongeza watuhumiwa hao.

Swai amedai amewatafuta washtakiwa hao toka mwezi wa tatu bila mafanikio na kuomba hati ya kuwakamata washtakiwa hao ambao hawakuepo mahakamani.

Washtakiwa hao wameongezwa katika kesi ya utakatishaji fedha na kugushi inayomkabili Rais wa Simba, Evans Aveva na makamu wake, Geofrey Nyange ‘Kaburu’ .

Okoa Ndoa yako Sasa...Umepungukiwa na Nguvu za Kiume na Unashindwa Kupanda Mlima Vizuri

$
0
0
OKOA NDOA YAKO SASA : JE UMEPUNGUKIWA NA NGUVU ZA KIUME AU UUME WAKO MDOGO AU MPENZI WAKO HAKUTIMIZII UTAKACHO:


Acha kujiona mpweke pale ukutanapo na mpenzi au mke wako kwa sababu ya kutokuwa na nguvu za kiume au Uume wako mdogo

Dawa YA MAPRO POWERA ndio dawa sahihi na tiba tosha kwa sasa Kutibu tatizo na kuponesha kabisa tatizo LA KUWAI KUFIKA KILELENI KABLA MWENZI WAKO BADO AJAKOJOA

KUSHINDWA KURUDIA TENDO LA NDOA NA MWILI KUCHOKA

UUME KUSINYAA NA KUWA LEGELEGE

KUUMWA NA TUMBO WAKATI UNAPOMALIZA KUFANYA TENDO

Dawa hii utumiwa ata na wazee wenye umri mkubwa na haina madhara yoyote

MAKAKANUA HII NI dawa ya maumbili madogo urefusha na kunenepesha saizi upendayo saiz 5-6-7-8 na unene sm 3-4-5 kwa mini huabiki kwa kuwa na UUME mdogo wai sasa upate tiba sahihi kabisa na ni tofauti na ulizowai kutumia :

Tunarudisha mke au mpenzi ndani ya masaa matatu tu zipo dawa za presha kisukali vidonda vya tumbo korodani iliyovimba dawa za uzazi tunapunguza matiti makubwa kitambi na mwili mkubwa dawa zipo FIKA OFISINI KWANGU MBAGALA ZAKHEMU KWA WATEJA AMBAO AMTAKUWA NA NAFASI YA KUJA OFISINI AU MLIO MKOANI MTALETEWA p

Piga simu 0743362017 au 0789234653

DR AGU

Utani wa RC Makonda: Nasikia Wana Yanga Wanauliza Lini Tunaanza Kuwapima Tezi Dume!

$
0
0
Utani wa RC Makonda: Nasikia Wana Yanga Wanauliza Lini Tunaanza Kuwapima Tezi Dume!
Baada ya klabu ya Simba SC Jumapili na jana kuibuka na ushindi wa goli moja bila dhidi ya watani wao wa jadi, Yanga SC, mashabiki wa timu ya Simba ambayo ipo katika mbio za ubingwa, wamekuwa wakituma mtandaoni vitu vya utani kwa mashabiki wa Simba.


Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam,Paul Makonda ambaye ni shabiki wa Simba, ametupia mtandaoni video inayomuonyesha msemaji wa Simba, Haji Manara akishangilia ushindi wa jana na kuandika ujumbe ambao umeonekana kuwaumiza mashabiki wa Yanga.

“Nasikia wana Yanga wanauliza lini tunaanza kuwapima tezi dume!,” aliandika RC Makonda kama kuwadhihaki mashabiki wa Yanga.

Mama Salma Kikwete Ampa Wosia Mzito Alikiba "“Simu Mtihani na ni Hatari"

$
0
0
Mama Salma Kikwete Ampa Wosia Mzito Alikiba "“Simu Mtihani na ni Hatari"
Mke wa Rais Mstaafu wa awamu ya nne, Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete, Mama Salma Kikwete amewaasa wasanii wawili wa muziki wa Bongo Fleva, Alikiba na mdogo wake Abdu Kiba kuwa wawe waaminifu kwenye maisha yao ya ndoa hasa hasa kwenye masuala ya simu.

Mama Salma ametoa wosia huo jana Aprili 29, 2018 katika hoteli ya Serena  jijini Dar es salaam kwenye sherehe za harusi ya Alikiba na mdogo wake Abdukiba ambao wote wamefunga ndoa wiki mbili zilizopita.

“Simu mtihani na ni hatari, mkiendekeza simu mnachukua mnaangalia mtaaachana kabla ya siku si nyingi. Aminianeni mkiaminiana  maisha yatakuwa mazuri, laikini kila dakika ukirudi basi umerudi unaanza kupakua nani ametuma meseji, hapana. Wakati mwingine simu inalia ikishalia ile simu unakosa amani ya moyo unatoka nje au unaingia chooni kuongea,“amesema Mama Salma Kikwete.

Kwa upande mwingine Mama Salma Kikwete amesema yeye tangu afunge ndoa na Mzee Kikwete wamekuwa wakichangia simu na mara nyingine hata kupokeleana pale inapokuwa inaita.

Alikiba na mdogo wake Abdukiba wamefunga ndoa wiki mbili zilizopita ambapo Alikiba alifunga ndoa na mchumba wake Aminah Khalef jijini Mombasa.

Manara Aliamsha Dude Kisa Beki wa Yanga Kumtemea Mate Kwasi " Huyu ni Bwege na Hastahili Kuachwa"

$
0
0
Manara Aliamsha Dude Kisa Beki wa Yanga  Kumtemea Mate Kwasi " Huyu ni Bwege na Hastahili Kuachwa"
Soka ni burudani na siyo vita. Mkuu wa kitengo cha Habari na Mawasiliano Simba, Haji Manara ametoa povu zito kutokana na kitendo cha beki wa Yanga Kevin Yondani kudaiwa kumtemea mate Asante Kwasi kwenye mchezo uliochezwa jana (Jumapili) katika uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.

Yondani ameonekana kwenye vipande vya video akimtemea mate Kwasi wakati alipokuwa akimzuia kwenye goli la Yanga wakisubiri kupigwa kwa mpira wa kona.

Kupitia mtandao wa Instagram, Manara ameonyesha kukerwa zaidi na tukio hilo kitendo ambacho amemuahidi mchezaji wao Kwasi watalifanyia kazi kuhakikisha mambo kama hayo hayajirudii tena.

Huyu jamaa ni mshamba.mtu asiye na ustaarabu. bwege na hastahili kuachwa hv hv..ni tukio la hovyo zaid nchini kwa mwaka huu..nilikuwa namheshimu kama senior player ila kwa sasa namuona ni zaidi ya takataka..usela wa kihayawani..chuki hyo ya nn?nyie mmeshinda mara ngapi mbona hamjatemewa makohozi ?vtendo hv lazma vilaaniwe na kila mmoja…..kwasi nakuahidi hili jambo tutalisimamia kwa nguvu kubwa..na hongera kwa nidhamu wachezaji wetu…na lazma apimwe kama hana maradhi sugu ya kuambukiza huyu jamaa..na tunangoja kauli ya Yanga kwa ushenzi huu wa kipumbavu..samahani watu wangu kwa lugha kali..ila sina maneno laini ya kuelezea upumbav kama huu….bullshit!!!!!



Mbunge Selasini Aibana Serikali Kuhusu Viti Bungeni "Kiti Nilichokalia Kimenifinya Makalio"

$
0
0
Mbunge Selasini Aibana Serikali Kuhusu Viti Bungeni "Kiti Nilichokalia Kimenifinya Makalio"
Mbunge wa Rombo, Joseph Selasini (Chadema) ameomba mwongozo bungeni akitaka viti vya bungeni kukarabatiwa kwa kuwa viti hivyo ni vibovu.

“Ni lini serikali itakarabati viti hivi, hiki nilichokalia leo asubuhi kimenifinya makalio,“ alihoji.

Salasini ameyasema hayo leo Bungeni mjini Dodoma, wakati wa kipindi cha Maswali na majibu huku akiitaka serikali itoe majibu ni lini viti hivyo vitakarabatiwa.

Aidha Mbunge huyo amesema kuwa kiti hicho alichokalia leo katika bunge hilo kimemfinya makalio. Sambamba na kuomba muongozo huo Spika Ngudai amesema kuwa suala hilo limepokea na litatolewa ufafanuzi.

Binti Aliyetumia YouTube Kujizalisha Mwenyewe Hotelini

$
0
0
Binti aliyetumia YouTube kujizalisha mwenyewe hotelini
Kwenye dunia ya sasa, teknolojia imekuja na faida na hasara zake. Kutoka nchini Marekani binti mmoja wa miaka 22 ameeleza jinsi gani teknolojia imeokoa maisha yake pamoja na ya mtoto wake.

Binti huyo ajulikanaye kama Tia Freeman, kutoka Nashville ameeleza kuwa alikuwa hajui jinsi kama ni mjamzito. Alikuwa anasafiri kwenda Ujerumani na Uturuki kwa ajili ya mapumziko.

Anaeleza kuwa hakuwa amegundua mabadiliko yoyote mwilini mwake tofauti na kuongezeka uzito kidogo hivyo hakuhisi kuwa anaweza kuwa mjamzito.

Alipokuwa kwenye ndege kuelekea Ujerumani anasema alikuwa anahisi maumivu makali ya tumbo, safari nzima na hata walipofika Ujerumani na kwenda hoteli bado tumbo liliendelea kumuuma sana.

Tia anaeleza kuwa alihisi labda alikula chakula chenye sumu na kupelekea kuumwa tumbo kiasi hicho, hivyo aliamua kutafuta kwenye mtandao wa google kujua ni nini kinaweza kuwa kinamsumbua.

Kutokana na maelezo aliyoandika ya anavyojisikia, aligundua kupitia google kwamba ulikuwa ni uchungu wa kujifungua, kutokana na hilo hakutaka kupiga simu kuomba msaada hivyo alianza kutafuta kwenye YouTube jinsi ya kujifungua.

Alichemsha maji na kuyaweka kwenye beseni kisha kuyapoza na kuingia kwenye beseni hilo na kuanza kujizalisha mwenyewe hadi akafanikiwa na kuchukua kamba yake ya kiatu na kuitumia kufunga kitovu.

Kwa bahati nzuri, Tian anasema alifanikiwa kujifungua mwenye tena haraka sana na kesho yake alijiandaa na kwenda uwanja wa ndege kupanda ndege ili aende Uturuki.

Wahudumu wa Uwanja wa ndege walishangaa kuona jana yake alipita akiwa na mtoto na kesho yake tu alikuwa na mtoto na wakahisi kuwa pengine alikuwa amemuiba mtoto huyo.

Alipojielezea ilikuwaje akajifungua, Kampuni ya ndege ya Turkish Airline ilimlipia hoteli kwa wiki mbili mjini Istanbul ambapo alikuwa akiangaliwa na maafisa wa matibabu pamoja na mtoto wake.

Mkasa huu wa binti huyu wa miaka 22 kutumia video ya youtube na kuweza kuzaa akiwa peke yake kwenye chumba cha hoteli imesisimua watu wengi na kuzua mijadala kwenye mitandao ya kijamii.

Harusi ya Kiba Yawavuruga Bilnass, Christian Bella

$
0
0
Harusi ya Kiba yawachanganya Bilnass, Christian Bella
Sherehe ya harusi ya msanii Ali Kiba, iliyofanyika jana katika Ukumbi wa Hoteli ya Serena, imewachanganya watu mbalimbali wakiwemo wasanii Bilnas na Christian Bella.

MCL Digital iliyopata mwaliko katika sherehe hizo ilizungumza na wasanii mbalimbali ambao wamesema Kiba kawadhihirishia kuwa msanii ukiamua kuoa au kuolewa inawezekana.

Bilnas amesema kwake harusi hiyo imezidi kumchanganya zaidi baada ya kuona Kiba ameweza kuoa wazazi wake wote wakiwa bado hai, jambo ambalo ni la kumshukuru Mwenyezi Mungu.

“Kiukweli hii harusi wengi imetuchanganya na kutuamsha kuwa ukitaka kufanya jambo kama hili inawezekana tena inakuwa vizuri na wazazi wakalishuhudia kama alivyofanya mwenzetu Kiba.

“Amenitamanisha kiukweli na mimi niingie katika kundi la wanandoa, na ninaahidi nitafanya hivyo muda si mrefu,” amesema Bilnas mkali wa kibao cha Mazoea.

Kwa upande wake Christiana Bella, amesema harusi ya Kiba imempa fundisho naye sasa kuangalia namna ya kuanza kutoka kwenye maisha ya ‘ubachela’.

“Unajua si jambo dogo kwa msanii kijana kuamua kuoa akiwa katika umri mdogo, tunapitia vishawishi vingi ambavyo kama hutakuwa makini unaweza ukajikuta kila siku hutaki kuitwa mume wa mtu,” amesema.

Harusi hiyo ya Kiba imekuwa gumzo baada ya sherehe yake kufanyika mara mbili na kurushwa mubashara na kituo cha televisheni cha Azam huku ikifuatiliwa na mamilioni ya watu.

Prof Jay Apewa Ahadi Hii na Waziri

$
0
0
Prof Jay Apewa Ahadi Hii na Waziri
Wizara ya Nishati kupitia Naibu Waziri wake Subira Mgalu imemuahidi Mbunge wa Mikumi Joseph Haule  (Prof Jay) kwamba itapeleka umeme katika jimbo lake la Mikumi kupitia Mradi wa Umeme wa Vijijini, (Rea) awamu ya tatu, katika mzunguko wa kwanza.


Ahadi ya Wizara hiyo imekuja leo baada ya Mbunge huyo ni lini serikali itapeleka umeme katika jimbo lake la Mikumi ambalo limebarikiwa kuwa na mbuga za wanyama zilizosheheni vivutio mbalimbali.

Mh. Mgalu amesema kuwa jimbo hilo lina jumla ya vijiji 57 na kati ya hivyo vijiji 16 tayari vina umeme wakati vijiji vinane umeme utapelekwa mapema zaidi.

Naibu Waziri amesema kazi ya kupeleka umeme kwa vijiji vinane kwa kuanzia, itahusisha ujenzi wa kilomita 26 za njia ya msongo wa kilovoti 33 na kilomita 32 njia ya umeme wa msongo wa kilovoti 0.4

Utani wa Spika: Wabunge Ambao ni Wapenzi wa Yanga Wameshindwa Kufika Bungeni

$
0
0
Utani wa Spika: Wabunge Ambao ni Wapenzi wa Yanga Wameshindwa Kufika Bungeni
Wakati mashabiki wa Simba SC wakiendelea kusherekea ushindi walioupata jana dhidi ya watani wao, Yanga SC, leo bungeni Dodoma Spika wa Bunge, Job Ndugai amesema ana taarifa za baadhi ya wabunge ambao ni wapenzi wa Yanga kutofika bungeni.

Akizungumza katika hali ya utani, Spika Ndugai amesema wabunge hao wameshindwa kufika kutokana kipigo cha hapo jana, huku akiwataja miongoni mwao ni Dkt. Mwigulu na Mkuchika.

“Habari nilizonazo ni kwamba wabunge ambao wapenzi wa Yanga hawajaweza kufika Bungeni, naskia baadhi yao wamelala na viatu vitandani maana hawakukumbuka hata kuvua viatu,” amesema Spika Ndugai.

Baada ya Kukamilisha Matibabu Lissu Kutua Dar Siku Hii

$
0
0
Baada ya Kukamilisha Matibabu Lissu Kutua Dar Siku Hii
MBUNGE wa Singida Mashariki (Chadema), Tundu Lissu (50) aliyelazwa nchini Ubelgiji anatarajiwa kurejea nyumbani siku yoyote kuanzia juzi, baada ya madaktari kumaliza kumpatia matibabu, amesema.



Lissu ambaye amekuwa hospitalini tangu Septemba 7, mwaka jana aliposhambuliwa kwa risasi nyumbani kwake Area D, mjini Dodoma, aliliambia Shirika la Utangazaji la BBC juzi, kuwa kwa sasa hana tena kidonda cha risasi na yupo tayari kurudi nyumbani.



“Sina tena kidonda cha risasi, nilipigwa mara 16, sina tena kiungo kilichovunjwa. Nilikuwa nimevunjwa mguu mmoja mara tatu, mikono yote ilikuwa imevunjwa, nilikuwa na risasi nyingi mwilini, na vidonda vingi,” alisema Lissu.



Lissu alisema analazimika kurundi nchini kwa kuwa yeye ni Mbunge, Kiongoziwa Upinzani Bungeni naWaziri kivuli wa Sheria na Katiba. Alisema kwa majukumu hayo hawezi kwenda mafichoni. “Siwezi kwenda mafichoni, siwezi kuikimbia nchi yangu,nitarudi Tanzania,” alisema.

“Mimi ni mbunge, mimi ni kiongozi bungeni, ni Mnadhimu Mkuu wa Kambi Rasmi ya Upinzani bungeni, mimi ni msemaji wa sheria na katiba wa chama changu,” aliongeza Lissu.



Hata hivyo, akizungumza na Nipashe jana kaka wa Lissu, wakili Alute Mughwai alisema familia bado haijapokea taarifa ya siku anayotarajia kurudi. Alisema familiainachofahamu ni kuwa Lissu amefanyiwaoperesheni ya 19 wiki chache zilizopita, hivyo kutakuwa na uangalizi wa afya yake.



“Hayo mahojiano aliyofanya juzi sijayaona, nitawasiliana naye leo jioni (jana) nimsikilize, lakini sisi kama familia hatujapata taarifa yoyote lini atarudi, wala hatuwezi kujua haditupewe taarifa na hospitali,” alisema wakili Mughwai.

Lissu alipoulizwa na BBC endapo amepata msaadawa matibabu kutokaserikalini, alisema chombo pekee chenye wajibu wa kumgharamia matibabuyake ni Bunge na “siyo serikali, wala Ikulu, wala mtu yeyote.”

Credit: Nipashe April 30, 2018.
Viewing all 104795 articles
Browse latest View live




Latest Images