Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104809 articles
Browse latest View live

Zitto Akataa Katu Katu Kumpa Pole Sugu Baada ya Kutoka Jela

$
0
0

Mbunge wa Kigoma Mjini, Mhe. Zitto Kabwe amesema kuwa amefurahi kuona Mbunge mwenzake wa Mbeya Mjini kupitia tiketi ya CHADEMA, Joseph Mbilinyi maarufu kwa jina la Sugu pamoja na mwenzie Emmanuel Masonga wakitoka gerezani lakini amekataa kuwapa pole kwa kile alichodai kuwa viongozi wote wa upinzani kwa sasa ni wafungwa watarajiwa.


Zitto amesema kuwa anaamini kukaa kwao gerezani kumewaongezea zaidi ari ya kupambania Demokrasia pana ya nchi yetu. “Nafurahi kuwa Mbunge Mbeya Mjini Ndg. Joseph Mbilinyi (Sugu) na mdogo wangu Emmanuel Masonga wametoka Gerezani! siwapi pole, maana katika nyakati za Udikteta wapinzani wote ni wafungwa watarajiwa.

Naamini kukaa kwao gerezani kumewaongezea zaidi ari ya kupambania Demokrasia pana ya Nchi yetu.Watawala mjue sasa kuwa vifungo vya Uonevu, kututishia Maisha na hata kutupiga risasi havita turudisha nyuma kwenye kupigania demokrasi ya nchi yetu.“ameandika Zitto Kabwe kwenye ukurasa wake wa Twitter.
Mhe.

Joseph Mbilinyi ‘Sugu’ ameachiwa huru leo Mei 10, 2018 kutoka gereza la Ruanda, Mbeya alipokuwa akitumikia kifungo cha miezi mitano kwa makosa ya uchochezi.

Rais Magufuli Awaapisha Balozi Kidata na Makungu

$
0
0
Rais Magufuli Awaapisha Balozi Kidata na Makungu
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli leo amewaapisha Mhe. Alphayo Kidata kuwa balozi wa Tanzania nchini Canada pamoja na Bw. Msalika Robert Makungu kuwa katibu Tawala wa mkoa wa Tabora  kwenye hafla ndogo iliyofanyika Ikulu jijini Dar es salaam leo Mei 10, 2018.

Serikali Yaagiza Bomberdier 10 Kuboresha Usafiri wa Anga

$
0
0
Serikali Yaagiza Bomberdier 10 Kuboresha Usafiri wa Anga
Wakati Tanzania ikipiga hatua ya ununuzi wa ndege tatu aina ya Bombardier Q400 kutoka Canada, tayari nchi ya Ethiopia nayo imeagiza ndege nyingine  10 aina hiyo ili kuimarisha usafiri wa anga nchini humo.



Taarifa iliyotolewa na mtandao wa kampuni hiyo mnamo Aprili 27, 2018 imeonesha kuwa nchi hiyo nimeshaweka oda ya ndege 10 ambapo oda hiyo inakadiliwa kuwa na gharama ya kiasi cha dola milioni 332 zaidi ya tsh bilioni 736.

Shirika la ndege la Ethiopia ndio shirika la ndege la kwanza barani Afrika kuagiza kwa wingi ndege za Bombardier ambapo hadi sasa inamiliki ndege 22 za Bombardier Q400.

Shirika hilo pia linatumia ndege hizo za Bombadier Q400 kwenye nchi za Togo na Malawi hii ni baada ya kuingia ubia na mashirika ya Asky na Malawi Airline.

Maneno ya Nape baada ya Sugu kutoka Gerezani

$
0
0
Maneno ya Nape baada ya Sugu kutoka Gerezani
Mbunge wa Jimbo la Mtama, Nape Nnauye amemkaribisha uraini Mbunge wa Mbeya Mjini,Joseph Mbilinyi ‘Sugu’ baada ya kutoka gereza la Ruanda alipokuwa akitumikia kifungo chake .

Nape amesema kuwa anakumbuka Mbunge huyo ambaye pia ni msanii aliwahi kuimba juu yake wakat alipoanza siasa.

“Karibu tena Uraini brother!{nakumbuka uliwahi kuimba juu yangu wakati huo nilipoanza siasa},” ameandika Nape kupitia ukurasa wake Twitter.

Sugu na katibu wa Chadema kanda ya Nyasa, Emmanuel Masonga walitiwa hatiani na kuhukumiwa kifungo cha miezi mitano jela February 26, 2018 kwa kutoa lugha ya fedhea dhidi ya Rais John Magufuli kwenye mkutano wa hadhara walioufanya Desember 30, 2017 katika uwanja wa shule ya msingi Mwenge, Mbeya

Mzee wa Miaka 104 Aliyeomba Kujiua, Hatimaye Afanikiwa Kujiua

$
0
0
Mzee wa Miaka 104 Aliyeomba Kujiua, Hatimaye Afanikiwa  Kujiua
Mwanasayansi David Goodall amehitimisha safari yake ya hapa duniani baada ya kujichoma sindano mwenyewe ya sumu iliyochukua dakika moja kuchukua uhai wake.

Mwanasayansi huyo mwenye miaka 104 aliyehitimisha maisha yake ya kuishi hapa duniani alizaliwa jijini London Aprili mwaka 1914 ikiwa ni mwezi mmoja kabla ya kuanza vita ya kwanza ya dunia.

Mwanasayansi huyo mkongwe  alisafiri kutoka Australia mpaka Basel, Uswis kwa ajili ya kujitoa uhai kwa hiari, ingawa alisema anachukizwa na kitendo hicho.

Goodall alishika bomba la sindano yenye sumu na kusukuma kwenye mwili wake, na  ilitumia dakika moja sumu ikaenea mwili na kupoteza uhai wake.

Sindano ambayo aliitumia kujichoma ilikuwa na sumu aina ya Sodium pentobarbital ambayo iliingia kwenye mishipa ya mwanasayansi huyo.

Wasamaria wema walimchangia Dola 20,000  za Marekani ambazo ni sawa na Sh45milioni ili kumsaidia kutimiza azma yake hiyo.

Kabla ya kifo chake alisema kwamba kinachomfanya  aharakishe kufa ni kutokana na kupungua kwa  uhuru unaosababishwa na  umri.

Hata hivyo mwili wake utachomwa moto nchini Uswisi na kisha majivu yatapelekwa nchini Australia.


Zamaradi Afunguka Steve Nyerere Kutafuna Michango ya Masogange

$
0
0
Zamaradi Afunguka Steve Nyerere Kutafuna Michango ya Masogange
Siku moja baada ya msanii Steve Nyerere, kudaiwa kutafuna michango ya msiba wa Agnes Masogoange, aliyekuwa mweka hazina Zamaradi Mketema amesema hakuna ukweli wowote katika madai hayo.

Akizungumzana na MCL Digital leo Mei  10, amesema fedha hizo Sh2.1 milioni, anazo yeye na wanachosubiri ni kupata taarifa sahihi za mtoto wake Sania Sabri, kutoka kwa familia ili wamhifadhie benki.

“Jamani wanamuonea tu Steve wa watu, mbona hela ninazo mpaka sasa, kilichopo hapa ni mawasiliano na familia ili kutupa taarifa kamili za mtoto kwa ajili ya kutusaidia mchakato wa kumfungulia akaunti.

“Pia ieleweke uamuzi wa kufungua akaunti ya mtoto haukutolewa na Steve bali na kamati iliyokuwa ikisimamia shughuli zote za mazishi,” amesema.

Juzi akihojiwa katika moja ya kituo cha redio, ndugu wa baba wa mtoto aliyejitambulisha kwa jina la Sada, alisema mpaka sasa hawajapata michango hiyo na wala hawana mawasiliano na kina Steve, jambo lilizua gumzo mitandaoni.

Hata hivyo, Steve aliyekuwa mwenyekiti wa kamati hiyo alipohojiwa kuhusiana na suala hilo alisisitiza kuwa fedha hizo hatopewa mtu mkononi bali atafunguliwa mtoto akaunti ili zimfae wakati akianza kidato cha kwanza mwakani.

Masongane alifariki Aprili 20, mwaka huu, akiwa anapatiwa matibabu katika hospitali ya Mama Ngoma, na kuzikwa Aprili 23 kijijini kwa baba yake Utengule, mkoani Mbeya.

Mahakama Yapokea Vielelezo vya Mtandao Kesi ya Abdul Nondo

$
0
0

Mahakama Yapokea Vielelezo vya Mtandao Kesi ya Abdul Nondo
Mahakama ya Hakimu Mkazi, Iringa, imepokea vielelezo vya kimtandao vilivyoletwa na upande wa mashtaka dhidi ya Mwanafunzi wa mwaka wa tatu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, (UDSM) Abdul Nondo.

Akizungumza Mahakamani hapo, leo Mei 10, Hakimu Mkazi, wa mahakama hiyo, John Mpitanjia amesema amepokea vielelezo hivyo baada ya kupitia sheria mbalimbali za mitandao ya kijamii.

Mpitanjia amesema, mahakama inawajibu wa kupokea kila kielelezo kinachokuja mbele yake.

Baada ya uamuzi huo upande wa utetezi chini Wakili Chance Luoga uliridhia maamuzi hayo na kuomba kesi hiyo  iendelee tena Mei 14

Nondo ambaye pia ni Mwenyekiti wa Mtandao wa Wanafunzi wa Vyuo Vikuu,(TSN) anakabiliwa  anakabiliwa na mashtaka mawili shtaka la kwanza ni kusambaza taarifa za uongo akiwa jijini Dar es Salaam kuwa ametekwa na kosa la pili ni kutoa taarifa za uongo akiwa mjini Mafinga kwa askari Polisi kituo cha Mafinga Wilayani Mufindi.

Wasiliana na Mtaalam wa Dua na Dawa za Kiarabu na Asili Dr Sharifu Lukumani

$
0
0

YULE MTAHALAM WA DUA NA DAWA ZA KIARABU NA ZA KIASILI YANI MITI SHAMBA SHARIFU LUKUMANI SASA YUPO HEWANI WENYE SHIDA ZITUATAZO CHEO KAZINI,KUONGEZEWA MSHAHARA KAZINI,MWENYE TATIZO LA NGUVU ZA KIUME,ALIEPOTELEWA NA HAMU YA KUFANYA TENDO LA NDOA, MWENYE KIFAFA,KISUKARI,FANGASI SEHEMU ZA SIRI KWA WALE WENYE MIILI MINENE MTOTO WA JICHO PAMOJA NA WALE WAKINA MAMA WANAOSUMBULIA NA CHANGO LA UZAZI PUMU YA MUDA MREFU WANAWAKE KUJAA MAJI SEHEMU ZA SIRI MWANAUME KUWAI KUFIKA KILELENI AU KUTOA MANII MFANO WA MAJIMAJI YAKIWA MEPESI AUTOWEZA KUMPA MKEO UJAUZITO JAMBO HILI LINAWASUMBUA WANAUME WALIO WENGI DUNIANI KWA KAWAIDA WANAUME ASIE NA TATIZO HILI UTOA MANII MAZITO NDIO YENYEUWEZO WA KUMPA MWANAMKE MIMBA.MWANAUME KUPATA MPENZI KWA ULAISI PASIPO NA GHARAMA YOYOTE YANI KWA WALE MADOMO ZEGE KUWA NA UWEZO WA KUSIKILIZWA HATAKAMA RAIA WA INCHI GANI NA UWEZO WA KURUDISHA MPENZI ALIE POTEA NA KUMFANYA AWE WAKO KWA WALE WASIO TAKA MITALA PIA UFANYA KAZI YA KUNG'ALISHA NYOTA SASA MATATIZO YAKO YAMEPATA SULUHISHO ANAPATIKA KWA MASAA ISHIRINI NA NNE

WASILIANA NAE KWA NAMBA 0762899488-0656145170

WhatsApp namba +255620665635

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Ijumaa ya May 11

$
0
0


Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Ijumaa ya May 11

Rais Magufuli: Kuteuliwa sio tatizo, ukishindwa tunakurudisha

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli amesema kuwa amesikitishwa na vitendo vya Mabalozi kushindwa kutekeleza maagizo yake aliyowapa ya kumpa taarifa juu ya utendaji kazi wao na manufaa ambayo Tanzania imeyapata kwa uwepo wa kila Balozi katika nchi aliyopangiwa kila robo mwaka.

Ameyasema hayo Ikulu Jijini Dar es salaam mara baada ya kumaliza kumuapisha, Alphayo Kidata kuwa Balozi wa Tanzania nchini Canada na Msalika Robert Makungu kuwa Katibu Tawala wa Mkoa wa T abora.

Amewataka viongozi hao kwenda kuchapa kazi kwa juhudi na maarifa na kwa manufaa ya Taifa na sio kufanya mambo ndivyo sivyo.

“Balozi ameteuliwa kuiwakilisha Tanzania katika nchi fulani, nchi imenufaikaje na uwepo wake kwenye nchi ile?. Kuteuliwa sawa lakini sio lazima ukae katika ubalozi huo kwa kipindi chote ulichopangiwa, ukishindwa kuleta manufaa unarudishwa na huko anapangiwa mtu mwingine atakayeleta manufaa kwa nchi,”amesema Rais Dkt. Magufuli

Hata hivyo,Rais Dkt. Magufuli ameipongeza Wizara ya Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) kwa kufanya kazi nzuri katika sekta ya Elimu na Afya

Spika ataka Mawaziri wasafiri, awapa kazi wabunge

$
0
0

Spika wa Bunge, Job Ndugai amesema kuna haja ya wabunge kuwaombea mawaziri kwenye mamlaka husika ili wapate fursa kusafiri nje ya nchi.

KauIi hiyo ya Spika imekuja kufuatia hoja ya Mbunge wa Kigoma Mjini, Zitto Kabwe, wakati akichangia hotuba ya bajeti ya Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji ambapo alisema ni muhimu Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Charles Mwijage asafiri nje ya nchi, ili kujenga uhusiano ya kidiplomasia na kutafuta masoko ya bidhaa za mbaazi, choroko na giligilani.

Spika Ndugai ambaye alikiri kukubaliana na mchango wa Zitto Kabwe amesema ni kweli mawaziri inabidi wasafiri na wabunge wanapaswa kuwaombea kutoka kwenye mamlaka.

“Waziri wa Biashara hawezi kukaa na sisi hapa, lazima aende, tumuombee popote pale kwenye mamlaka lazima asafiri, maana bidhaa zetu tutauza Kongwa, kuna soko huko?

“Waziri wa utalii lazima asafiri ‘apige mawingu’ huko na wengine huko, ndiyo ukweli jamani, sisi wabunge lazima tuwasemee,” amesisitiza Ndugai.

Warembo Wazichapa Kavu Kavu Kumgombea Baba Diamond...

$
0
0
DARESSAL AA M: Warembo wawili ambao walifahamika kwa majina ya Ashura na Zubeda, wamedaiwa kuzichapa kavukavu chanzo kikitajwa kuwa ni kumgombea baba wa msanii wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’, Abdul Juma.

Tukio hilo lililokusanya watu lilitokea hivi karibuni katika baa moja maarufu kwa jina la Suma iliyopo maeneo ya Magomeni-Kagera jijini Dar ambayo baba wa msanii huyo anadaiwa kuwa anakwenda mara kwa mara kupata ‘kinywaji’.

 Mtoa ubuyu wetu aliyelipigia simu Amani alisema kuwa, warembo hao walitangulia kufika katika baa hiyo na kupiga stori pamoja huku wakipata kilevi lakini baadaye alipotokea baba Diamond na kujumuika nao, kila mmoja alianza kujitapa kuwa ni wake. “Yani walianza kubishana. Ghafla wakaanza kushikana na ndipo watu walipowawahi na kuwaamua. Baba Diamond kukwepa soo akaamua kutoweka eneo hilo,” kilidai chanzo chetu.

 Baada ya kuunasa ubuyu huo, Amani lilimvutia waya baba Diamond ambaye alishtuka kusikia habari zimetua gazetini na kusema: “Ni kweli lakini please naomba upotezee maana wale wote sio watu wangu wewe si unajua mimi nina mke wangu, mambo ya kilabuni hayo babu

Mwandishi Wetu, Amani

Zari , Mwanaume Haachwi , Ulicheza Faulo Kumwacha Diamond Kirahisi Rahisi

$
0
0
Tatizo wadada wa mjini mnapenda kuoelewa/ kudate mastaa Ila hamtaki kulipa gharama, ku date na staa sio mchezo, mamillion ya watu wanatamani kulala na mastaa, mastaa huwa wanasumbuliwa kila kukicha, ebu fikiria mtu kama Rihanna, unadhani hakuna mtu wa kumuoa? , tatizo watu wanajua ni stress kumdate rihanna , mtu kila siku anazunguka duniani kufanya shoo, unajua anakutana na watu wangapi? , Hana muda na mpenzi wala familia, uko tayar kuvumilia ku date mtu kama huyo , uko tayar ku cope? , mastaa hawana muda wa kutosha wa ku enjoy na familia zao.

Sasa Dada yetu zari wakati unakutana na diamond ulimkuta akiwa staa tayar , alikua na msululu kibao wa wanawake aliodate nao au kulala nao , ulijua fika kuwa mtu wako anawindwa na wadada wa mujini, Ila wewe ukabahatika, na mkazaa , tena mtoto wa watu alikua anakuheshimu na kukupost instagram juu, Diamond ni malaya hilo liko Wazi, Ila kwa kuwa iliamua kumzalia tena watoto wawili, we ni bora tu ungemvumilia upuuzi wake mkalea watoto vizuri , maana tunajua kama usingetangaza kuachana na diamond sidhan kama yeye angekuacha, hyo jeuri Hana , Diamond anakupenda Ila kuna watu tu wanamchezeya tu akili kuaribu familia yako, sasa na wewe ulivyokua na moyo mwepesi na kujifanya bosslady ukaamua kumuacha, wenzio wakambeba maana walikua wanammendea toka alivyokua kwako, Ila tunajua tu soon atarudi kwako kwa magoti maana now sio akili zake, Ila ulicheza faulo kumuacha baba watoto wako

By Warumi/JF

Maxence Melo: Utambulisho wa Majina Mitandaoni Utaua Habari za Kiuchunguzi

$
0
0
Wadau wa majukwaa ya habari za mitandaoni, nchini Tanzania wameitaka Serikali kutafakari juu ya kasoro zilizoko katika Kanuni za Maudhui ya kimtandao.

Wakati wa mdahalo huo uliofanyika Jumamosi, Dar es Salaam, wadau hao walijadili mchango wa mitandao ya kijamii katika kuhamasisha utawala bora.

Mkurugenzi Mtendaji wa mtandao wa Jamii Forums, Maxence Melo alisema kipengele kinachotaka utambulisho wa majina ya washiriki katika mitandao ya kijamii kinalenga kuuwa upatikanaji wa taarifa nyingi za kiuchunguzi.

“Athari zake ni kwamba, utapata watu wachache watakaotoa taarifa za ufisadi ndani ya Serikali, hatuoni sababu za kutambua majina ya washiriki katika mitandao, itakuwa ni mwisho wa watu wengi kusema ukweli,” alisema Melo aliyesimulia harakati za kuanzisha jukwaa hilo takribani miaka 15 iliyopita.

Washiriki wengine katika mdahalo huo ulioandaliwa na Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC), ni makundi ya vijana mbalimbali ya wafuasi wa vyama vya siasa, wanahabari na wanasheria. Pia walikuwepo watoa huduma na wamiliki wa majukwaa ya habari za mitandaoni, wasomi na watumiaji wa mitandao.

Mwanafunzi wa Shahada ya Uzamivu Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM), Rachel Yusuph alisema kanuni zenye adhabu kali siyo suluhusho la kurejesha nidhamu na uhuru wenye mipaka katika matumizi ya mitandao nchini.

Alisema elimu bado inahitajika kwa watumiaji wake ili kuwaondoa katika utamaduni wa matumizi mabaya ya mitandao hiyo.

Prof. Mwandosya: Hongera Mhe.Joseph Mbilinyi (Sugu) Kwa Kuhitimu Chuo cha Uanasiasa

$
0
0
Nikimpa hongera Mbunge wangu wa Mbeya Mjini (Mhe. Joseph Mbilinyi, MB-kulia) kwa kuhitimu Chuo cha Uanasiasa, Gereza la Ruanda, Mbeya, leo tarehe 10 Mei 2018. Somo: Kutofautiana vyama, itikadi na misimamo isiwe msingi uhasama na uadui. Mwenyezi Mungu, Mwingi wa Rehema, Ibariki Tanzania.

Congratulating my Member of Parliament for Mbeya Urban (Hon. Joseph Mbilinyi, MP-right) after graduating from Ruanda Penitentiary (Prison), the ultimate college for politicians all over the world. Lesson: Differences of opinion, outlook, political party affiliation or ideology should not be a basis for division, hatred or disunity. May Almighty God Bless Tanzania.

Download Hapa Application Mpya ya Udaku Special Uweze Soma Vimbwanga na Udaku Mtaani Kila Siku

$
0
0
Mpendwa msomaji wetu, tunakukumbusha Kuidownload Upya Application yetu ya UDAKU SPECIAL Maana ile ya Zamani Tutaifuta.

Kuna Marekebisho Makubwa tumeyafanya ikiwa na tatizo la Notification kutatuliwa

NB: App mpya ina Icon Nyekundu

 Bonyeza Hapa Chini Kuinstall Upya:


==>>Unaweza Kuidownload << kwa Kubofya Hapa>>  
 

Hii Hapa Dawa Bora ya Nguvu za Kiume na Maumbile Madogo ya Uume

$
0
0
Tatizo hili limekuwa likiwaadhiri watu wengi sana kisaikolojia hasa baada ya kujiona wapo tofauti sana na wengine kwa kawaida mwanaume anatakiwa awe na uume kuanzia nchi 6-8 kwanza upungufu wa vichocheo hivi huchochea ukuaji wa uume chongo ambalo hushambulia nerve ambayo uharibu kabisa ukuaji wa uume, ngiri, punyeto, ambayo huathili misuli ya uume, ngiri huleta maumivu, tumbo kuunguruma na kujaa gesi, korodani moja kuvimba, kutopata choo vizuri, sababu hizi hufanya uume kulegea na kusinyaa na kuwa mfupi na mwembamba na mara nyingi hata nguvu za kiume ( hamu ya tendo la ndoa) hupungua na kwisha kabisa

GEMBE :Ni dawa inayozalisha na kukufanya uume kukua na kuongezeka
NGEMO : Ni dawa bora ya kuongeza nguvu za kiume

Hukutia hamu ya kuludia tendo la ndoa zaidi mara4 nne bila kukinai au kuchoka pia itakufanya uchelewe kufika kileleni zaidi ya dk30-45 kwa mtumiaji pia tunatibu kisukari, bp, ngiri, miguu kuwaka moto KAMA HUNAMDA WA KUFIKA OFISINI KWETU UTALETEWA POPOTE TUPO MBAGALA RANGI TATU

 0753471612/ 0715249530
0623 386 305

DR KUZENZA

Wolpe Akubali Kumaliza Bifu lake na Harmonize

$
0
0
Wolpe Akubali Kumaliza Bifu lake na Harmonize
Malkia wa filamu, Jacqueline Wolper ameamua kunyamaza na kusitisha malumbano yaliyoanza kwenye mitandao kati yake na aliyekuwa mpenzi wake wa zamani, Harmonize.


Malumbano hao yasiokuwa ya kawaida yameanza Jumanne hii baada ya Harmonize kupost list ya wanaume aliodai wamewahi kutembea na mpenzi wake huyo wazamani, Jacqueline Wolper.

Hatua hiyo ilimfanya Wolper kuibuka na kuanza kuandika mambo mbalimbali mabaya akimtuhumu muimbaji huyo wa wimbo, DM Chick, huku akidai ndiye aliyesababisha alumbane na Sarah.

Alhamisi hii Wolper aameamua kuwa mpole kwa kufunga malumbano hayo baada ya Harmonize kudai ataandaa list C ya wanaume aliotembea na mrembo huyo kutoka katika kiwanda cha filamu.

“Mungu nifundishe kunyamaza, we ndio unaujua ukweli 🙏#Najifunzakuheshimkilangaziiliyonifikishanilipo
#NdiomaanataupambanesiwezkushukaatanishushaMungupekee #jifunzekuheshimkilangaziiliyokufishaulipokamweutoteterekakwajarbulolote
#MunguwanguwaushindiwewenijbuToshaNimekukabidhiwewekilaktu🙌🙏,”

Baadhi ya mashabiki katika mitandao ya kijamii wanadai Harmonize anamchokoza Wolper ili apate kiki za project yake mpya.

Muimbaji huyo siku ya leo ameachia kolabo yake ya wimbo ‘Pull Up’ akiwa ameshirikiana na Eddy Kenzo

Sugu Ajifananisha na Mandela" Najisikia Furaha Kuingia Kundi la Wafungwa wa Kisiasa"

$
0
0
Sugu Ajifananisha na Mandela" Najisikia Furaha Kuingia Kundi la Wafungwa wa Kisiasa"
Mbunge wa Mbeya Mjini (CHADEMA) Joseph Mbilinyi maarufu kama Sugu amesema anajiona shujaa baada ya kufanikiwa kutoka gerezani na kusema kuwa amepata hisia walizopitia viongozi waliofungwa kisiasa duniani.


Sugu amesema hayo leo Mei 10, 2018, wakati akiongea na vyombo vya habari nyumbani kwake Mjini Mbeya muda mfupi baada ya kuachiwa huru, na kusema kuwa yeye alifungwa kisiasa na ndiyo maana anajiona shujaa kwasabau ameingia katika kundi moja la vingozi wa zamani kama Hayati Nelson Mandela wa Afrika Kusini.

"Najisikia shujaa kuingia kundi la wafungwa wa kisiasa duniani, Mandela, Obasanjo, ingawa ni kwa muda mfupi lakini zile hisia alichokua anajisikia Mandela wakati yupo ndani, katikati ya usiku haupo na familia hizo hisia ninazo" amesema Sugu.

Sugu alitumia muda huo kuwapa pole wakazi wa jimbo la Mbeya mjini kwa sababu muda mrefu walimkosa Mbunge huyo na kudai kuwa yeye alifungwa kimwili ila wakazi wa jimbo hilo walifungwa mioyo.

Mbunge Sugu na Katibu wa Chadema kanda ya nyanda za juu kusini Emmanuel Masonga, waliachiwa huru mapema leo Mei 10, 2018 baada ya kuhudumu katika Gereza la Ruanda mkoani mbeya kwa siku 73 ambapo taarifa ya Gereza hilo imedai wawili hao walitolewa kwa msamaha wa Rais John Magufuli alioutoa katika sherehe za siku ya muungano April 26, 2018.

February 26, 2018 Mahakama ya Hakimu mkazi Mbeya iliwatia hatiani Sugu na Masonga na kuhukumiwa kifungo cha miezi mitano jela kwa kosa la kutumia lugha ya fedheha dhidi ya Rais John Magufuli katika mkutano wa hadhara uliofanyika Disemba 30, 2017

Magufuli Awataka Watendaji Idara za Maji, Ardhi Kuripoti Wizarani

$
0
0
Magufuli Awataka Watendaji Idara za Maji, Ardhi Kuripoti Wizarani
Rais John Magufuli ameagiza watendaji wa idara za maji na ardhi kuwajibika moja kwa moja Serikali Kuu kupitia wizara husika badala ya halmashauri.

Rais Magufuli alitoa agizo hilo jana, Ikulu jijini Dar es Salaam alipowaapisha balozi wa Tanzania nchini Cuba, Alphayo Kidata na katibu tawala wa Mkoa wa Tabora, Msalika Makungu. Hotuba yake ilitangazwa moja kwa moja na kituo cha televisheni cha TBC1.

Alisema Serikali imewaacha watalaamu hao kwa muda mrefu wakitumia nafasi zao kuhujumu miradi ya umma, hatua inayochelewesha maendeleo ya wananchi na upatikanaji wa huduma za maji.

Rais alisema asilimia 75 ya miji wakazi wake wamejenga bila utaratibu wa mipango miji na changamoto hiyo imeendelea kuongezeka kutokana na udhaifu wa watendaji wa ardhi katika halmashauri.

Kuhusu changamoto ya utekelezaji wa miradi ya maji, alisema kuanzia mwaka 2010 hadi sasa Serikali ina miradi yenye thamani ya Sh109 bilioni, lakini imetekelezwa kwa Sh17 bilioni.

“Wameleta miradi yenye thamani ya Sh109 bilioni, lakini value for money (thamani ya fedha) ya hiyo miradi mpaka leo kwamba kama kuna mradi unatakiwa kulipwa ni Sh17 bilioni, miradi inasomeka Sh109 bilioni, lakini thamani ya kazi zilizofanyika for ten years (kwa miaka kumi) ni Sh17 bilioni ambayo ndiyo inaweza ikalipwa, miradi mingine imekaa zaidi ya miaka minane haikamiliki,” alisema.

“Miradi mingine ni forgery (ya kughushi) tu, kinapelekwa kifaa tu na hayupo mtu wa kumbana kule kwa sababu hawa (Wizara ya Maji) hawako ‘connected’ (hawajaunganishwa) na watalaamu wenzao, sasa nimeamua wataalamu wote wanaohusika na maji kuanzia kwenye halmashauri watawajibika direct (moja kwa moja) na Wizara ya Maji ili injinia wa maji akifanya ujinga wilayani afukuzwe moja kwa moja na katibu mkuu.”

Rais alisema endapo wataalamu hao wakiendelea kusimamiwa na madiwani watabaki kuwa huru na changamoto hazitamalizika.

Pia, alimuagiza waziri wa wizara hiyo kutengeneza mabadiliko ya kimfumo ili kila bajeti ya maji itakapopelekwa katika halmashauri, waziri akasimamie mwenyewe na si halmashauri kama ilivyokuwa awali.

“Na katibu mkuu kiongozi kama kuna instruments (nyenzo) za kubadilisha, zibadilishe. Nataka hawa wasimamiwe moja kwa moja na wizara inayohusika, hatuwezi kupeleka miradi haitekelezwi. Hata wabunge wamezungumza sana kuhusu miradi kutotekelezwa yaani fedha inapelekwa lakini miradi hai-move (haiendelei) vizuri,” alisema.

Kama ilivyo katika sekta ya maji, Rais Magufuli alisema hali si nzuri katika sekta ya ardhi kwa wataalamu waliopo kwenye halmashauri mbalimbali.

“Maofisa ardhi, ma-planners, wataalamu wa mipango miji walioko kwenye halmashauri nao hawako answerable (hawawajibiki) wizarani, ‘connection’ haipo. Nakumbuka nikiwa waziri wa ardhi niliwaomba hawa watu, kwamba ‘nipeni niwanyoshe’ lakini nikakataliwa kwa sababu wana kiburi, wanatoa ‘double allocation’, wanafanya mambo ya hovyo hawashughulikiwi. Kwenye mkutano wa madiwani atazungumza hiki kinatakiwa hivi, anaweka na maneno ya Kiingereza madiwani wanaona huu ndiyo utaratibu,” alisema.

Alisisitiza kuwa katika vikao vya mabaraza ya madiwani wataalamu hao hufikia hatua ya kunukuu vipengele vya sheria zinazosimamiwa na wizara husika akitoa mfano wa zile zinazohusika na usimamizi wa ardhi.

Rais alisema wataalamu hao wako huru, wanafanya wanachotaka na hakuna wa kuwahoji na kuwawajibisha. Alitoa mfano wa utaratibu wa mwananchi kuomba kibali cha ujenzi akisema usumbufu unaotokana na mizunguko ya vikao kutumia muda mrefu imekuwa ikiwakatisha tamaa hatua inayochangia wajenge bila vibali. “Ukiwauliza wanasema kibali labda ukilipie, kikao kitakaa, wamekaa jana watakaa miezi miwili ijayo sasa umekopa benki unataka kuanza kujenga kesho, unasubiri kikao wakati mwingine kikao huko ukawape pesa, sasa hili nimeliona, nimepata malalamiko mengine ndiyo maana 75 ‘percent’ ya miji imejengwa kwenye unplanned areas (maeneo yasiyopangwa),” alisema Rais Magufuli.

Aliongeza kuwa wataalamu hao pia wataanza kusimamiwa moja kwa moja na Wizara ya Ardhi ili mtaalamu yeyote atakayeharibu afukuzwe siku hiyohiyo na katibu au waziri bila kusubiri kikao cha madiwani.

Viewing all 104809 articles
Browse latest View live




Latest Images