Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104789 articles
Browse latest View live

Bila cheti cha kuzaliwa ndoa hakuna

$
0
0

BARAZA la Madiwani wa  Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga, limepitisha sheria ndogo itakayomlazimu binti anayetaka kuolewa kuonyesha cheti cha kuzaliwa kwanza kitakachomwezesha mwenyekiti wa kijiji kutoa kibali au la.

Uamuzi wa kupitisha sheria hiyo ulitolewa juzi na Mwenyekiti wa halmashauri hiyo, Ngassa Mboje, kwenye mkutano wa Shirika la

Agape la kutetea haki za watoto mkoani Shinyanga, uliohusisha madiwani wa Manispaa ya Shinyanga, vijiji, maofisa maendeleo ya jamii na wakuu wa shule, uliokuwa na lengo la kujadili namna ya kumkomboa mtoto wa kike kielimu.

Alisema baada ya kuona tatizo la ndoa na mimba za utotoni linaendelea kushamiri kwenye wilaya hiyo, wakaona ni vyema kutunga na kupitisha sheria ndogo ambayo itawabana wazazi kushindwa kuozesha mabinti zao walio chini ya umri wa miaka 18 kwa tamaa ya mifugo na mali.

“Sheria ya Ndoa ya mwaka (1971) siyo rafiki kabisa kumlinda mtoto wa kike, ina ruhusu kuolewa akiwa chini ya umri wa miaka 18 kwa ridhaa ya wazazi wake au mahakama, na hivyo kusababisha kuendelea kuwepo kwa ndoa nyingi za utotoni, na kukatisha ndoto za wanafunzi wa kike,” alisema Mboje.

“Baada ya kuona sheria hiyo ni tatizo, sisi baraza letu ikabidi tutunge sheria na kuipitisha na inafanya kazi sasa, kuwa hakuna mzazi kuozesha binti yake bila ya kutoa taarifa kwa uongozi wa serikali ya kijiji, pamoja na kuonyesha cheti chake cha kuzaliwa ili kujiridhisha kama hayupo chini ya umri miaka 18 na hasomi,” aliongeza.

Ofisa Mradi wa kutokomeza mimba na ndoa za utotoni kutoka Shirika la Agape mkoani hapa, Mustapha Isabuda, alisema wameamua kukutana na madiwani hao kuonyesha ukubwa wa tatizo ulivyo, ili wapate kuguswa na kutunga sheria ndogo za kubana wazazi kuozesha watoto.

Aidha, aliwataka madiwani wanapokuwa wanapitisha bajeti zao la kila mwaka wa fedha, wahakikishe suala la elimu wanalipatia kipaumbele kwa kulitengea bajeti kubwa, ili kuondoa upungufu wa ujenzi wa matundu ya vyoo na vyumba vya kujisitiri hedhi na vitaulo vya kujihifadhi wanafunzi wa kike.

Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga, Geofrey Mwangulumbi, alilipongeza Shirika hilo kwa kumpigania mtoto wa kike apate kusoma, na kuahidi watatunga sheria hizo ndogo kupitia Mwanasheria wao. 

Wolper Aamua Kumuachia Mungu Sakata la Harmonize Kutoa List ya Wanaume Waliompitia

$
0
0

Baada ya Harmonize kusema kuwa yupo mbioni kutoa list nyingine ya wanaume aliotoka nao Wolper. Actress huyo amesema ameamua kumpotezea Harmonize kuacha kulumbana nae badala yake ameamuachia Mungu

Yanga Hali Bado Tete, Yaambulia Kipigo cha Tatu Mfululizo

$
0
0
Klabu ya Yanga bado ipo kwenye kipindi kigumu katika mapambano ya Ligi kuu vodacom Tanzania Bara kwani leo tena imeambulia kipigo cha goli 1-0 dhidi ya Mtibwa Sugar.

Kipigo hicho ni cha tatu mfululizo kwa klabu hiyo baada ya kuadabishwa na Simba na klabu ya Mbeya City.

Goli la mtibwa sugar limefungwa na Hassan Dilunga kunako dakika ya 82 na kwa matokeo hayo Yanga itasalia nafasi ya tatu ikiwa na alama 48 nyuma ya Simba na Azam. Tazama goli hilo la Mtibwa Sugar video by Azam TV

Mtanzania Anusurika Kifo Baada ya Kujifungia Kwenye Kontena Bandarini kwa Masaa 23 (+video)

$
0
0
Mwanaume mmoja aliyetambulika kwa jina la Hassani Mkazi wa Miembeni mjini Unguja amenusurika kifo baada ya kutolewa ndani ya kontena ambapo alidaiwa kujifungia.

Kwa mujibu wa maelezo aliyoyatoa Msimamizi wa makontena katika Bandari ya Malindi, Ibrahim Abdallah kwenye mahojiano yake na gazeti la mwananchi leo Mei 13, 2018 amesema bado sababu ya mtu huyo anayekadiriwa kuwa na miaka 30 kujifungia kwenye kontena haijajulikana na kwa sasa amepelekwa katika hospitali ya Mnazi Mmoja mjini humo.

Akielezea jinsi tukio hilo lilivyotokea, Abdallah amesema wakiwa katika eneo hilo la kazi saa moja asubuhi walisikia sauti ikisema “Nakufaaaa” ikitoka ndani ya kontena na walipouliza wewe ni nani walijibiwa “Hassani”.

“Baada ya kutaja jina tulifungua kontena ambalo alikuwa amelifunga na kumtoa akiwa na hali mbaya kiafya na tulimpeleka Hospitali ya Mnazi Mmoja ili kupatiwa huduma ya kwanza,” amesema Abdallah kwenye mahojiano yake na Gazeti la Mwananchi.

Hata hivyo mashuhuda wa tukio hilo ambao wengi ni wafanyakazi bandarini hapo wamesema haijawahi kutokea tukio kama hilo la mtu kujifungia katika Kontena na makontena hayo yamepangwa tangu jana asubuhi .Tazama video ya tukio hilo la kuokolewa kwa Hassani.(Video na Mtandao)

VIDEO:

Video ya ‘Mvumo wa Radi’ ya Alikiba yafanyiwa zengwe YouTube, mwenyewe atoa tamko

$
0
0
Video ya wimbo wa ‘Mvumo wa Radi’ ya Msanii wa Bongo Fleva, Alikiba imeelezwa kuwa imefanyiwa figisu figisu hususani kwenye suala la Watazamaji (Views) kwa kile kilichoelezwa kuwa hawaongezeki toka itoke video hiyo siku ya Ijumaa.

Alikiba amesema amepokea malalamiko hayo na hata hao wenyewe wamelitambua tatizo hilo na tayari wametuma malalamiko hayo makao makuu ya YouTube Afrika kuweza kutatua changamoto hiyo, na kuwaomba mashabiki wake waendelee kutazama kichupa hicho.

“Tunafahamu tatizo la kutokuongezeka kwa views kwenye akaunti ya YouTube ya ALIKIBA, na tupo kwenye mawasiliano ya moja kwa moja na makao makuu ya YouTube Africa ambao wanafanya kila jitihada kutatua tatizo hili kwa haraka iwezekanavyo. Shukrani kwa uvumilivu wenu na support mnayoendelea kutupa! Endeleeni kuangalia video ya Mvumo wa Radi,“ameeleza Alikiba kwenye taarifa yake kwa umma.

Video ya Mvumo wa Radi tangu jana Mei 12, 2018 imekuwa namba moja kwenye Trending ya video zinazotazamwa zaidi Tanzania na mpaka sasa bado ipo namba moja lakini tangu jana licha ya kuwa namba moja bado views wanaongezeka taratibu sana ukilinganisha na siku ya Ijumaa.

Kwa siku ya Jana hadi leo wameongezeka watazamaji chini ya 70+k ile hali kwa siku ya Ijumaa hadi Jana Jumamosi video hiyo ilikuwa imetazamwa na watu 690+k .

Hii sio mara ya kwanza kwa msanii wa Bongo Fleva kuhusu figisu figisu za views kwenye mtandao wa YouTube kwani Baraka The Prince alishawahi kukiri kuwa kuna watu wanamfanyia mchezo huo.

Haji Manara Aweka nia ya Kuisaidia Yanga

$
0
0
Afisa Habari wa timu ya Mabingwa Tanzania Bara, Haji Manara ameweka nia yake ya kutaka kuandaliwa mechi kati ya Simba  na watani zao wa jadi Yanga ili waweze kuwasaidia kiuchumi kwa kuwapatia mapato yatakayokusanywa katika mchezo huo.

Manara ameyasema hayo ikiwa ni katika kuendeleza utani wake kwa klabu hiyo ambayo imeshindwa kutetea ubingwa wake katika msimu huu huku ikidhaniwa kwamba ni kutokana na hali ngumu ya kiuchumiinayopitia klabu hiyo.

Manara kupitia ukurasa wake wa Instagram leo ameweka picha ya gari la klabu ya Yanga ambalo likionekana limepata hitilafu  na kusema kwamba kati mechi hiyo sharti wanalotoa kwa watani zao ni kuwapa shikamoo Simba.

"Nnajaribu kuongea na wenzangu klabuni tuone namna ya kucheza mechi ya kirafiki na hawa jamaa ili wachukue mapato yote ya uwanjani kuwanusuru na swaumu yao..hata sijui kama bima imelipiwa hii gari" Manara.

Ameongeza "Sharti la hiyo mechi Gongowazi wote watuamkie..Shikamoo Simba.

VIDEO "Tunampongeza Rais Kukiri Hali ni Mbaya, Kauli Zake Zipimwe"

$
0
0
Chama cha ACT Wazalendo kimempongeza Rais Magufuli kwa kusema ukweli kuwa hatoongeza kima cha mishahara ya wafanyakazi kwa kuwa kwa sasa anafanya miradi mikubwa ya maendeleo kuliko angewapa ahadi hewa kama ambavyo ilifanyika kwenye sikukuu za nyuma za mei mosi. Chama hicho pia kimetaka kauli na matamko yanayotolewa na Rais kuangaliwa upya.

TAZAMA FULL VIDEO

Kapombe Afafanua Style ya Kushangilia, Niyonzima Kafunguka

$
0
0
Shomari Kapombe ndiye aliifungia Simba goli pekee lililoamua matokeo ya mchezo dhidi ya Singida United.

Kapombe alishangilia kwa style iliyoashiria analea, baada ya mchezo alisema mkewake amejifungua mtoto wa kike ndiyo sababu iliyomfanya ashangilie kama anabembeleza mtoto.

“Zawadi ya goli hili kama mlivyoona nilipofunga nilishangilia kwa sababu nimepata mtoto wa kike, nashukuru Mungu kwa kunipa zawadi hii”-Shomari Kapombe.

Wakati huohuo kiungo wa Simba Haruna Niyonzima ambaye hajaonekana mara nyingi kwenye mechi za ligi amesema lengo la Simba ni kumaliza ligi bila kupoteza mchezo.

“Tumeshachukua ubingwa lakini malengo ya Simba ni kumaliza ligi bila kufungwa, hatuta poteza mchezo wowote licha kwamba kupoteza ni sehemu ya mchezo wa mpira”
VIDEO

Hamisa Mobetto 'Wema Sepetu Anaroho Nzuri Sana, Siku Shangaa Alivyobariki Diamond Anioe

$
0
0
Mrembo Hamisa Mobetto amehojiwa na Wasafi TV kuhusu kauli ya Wema Sepetu ya Kubariki Diamond Kumuoa na amefunguka hivi

"Ni Kitu ambacho kutoka kwa Dada Wema is not a suprise coz unajua nini Dada Wema ana roho safi hawezi kusema kitu ambacho hamanishi coz namjua alivyo na hana tatizo na couple yetu ni kama ametupa baraka" Hamisa

Wasiliana na Mtaalam wa Dua na Dawa za Kiarabu na Asili Dr Sharifu Lukumani

$
0
0
YULE MTAHALAM WA DUA NA DAWA ZA KIARABU NA ZA KIASILI YANI MITI SHAMBA SHARIFU LUKUMANI SASA YUPO HEWANI WENYE SHIDA ZITUATAZO CHEO KAZINI,KUONGEZEWA MSHAHARA KAZINI,MWENYE TATIZO LA NGUVU ZA KIUME,ALIEPOTELEWA NA HAMU YA KUFANYA TENDO LA NDOA, MWENYE KIFAFA,KISUKARI,FANGASI SEHEMU ZA SIRI KWA WALE WENYE MIILI MINENE MTOTO WA JICHO PAMOJA NA WALE WAKINA MAMA WANAOSUMBULIA NA CHANGO LA UZAZI PUMU YA MUDA MREFU WANAWAKE KUJAA MAJI SEHEMU ZA SIRI MWANAUME KUWAI KUFIKA KILELENI AU KUTOA MANII MFANO WA MAJIMAJI YAKIWA MEPESI AUTOWEZA KUMPA MKEO UJAUZITO JAMBO HILI LINAWASUMBUA WANAUME WALIO WENGI DUNIANI KWA KAWAIDA WANAUME ASIE NA TATIZO HILI UTOA MANII MAZITO NDIO YENYEUWEZO WA KUMPA MWANAMKE MIMBA.MWANAUME KUPATA MPENZI KWA ULAISI PASIPO NA GHARAMA YOYOTE YANI KWA WALE MADOMO ZEGE KUWA NA UWEZO WA KUSIKILIZWA HATAKAMA RAIA WA INCHI GANI NA UWEZO WA KURUDISHA MPENZI ALIE POTEA NA KUMFANYA AWE WAKO KWA WALE WASIO TAKA MITALA PIA UFANYA KAZI YA KUNG'ALISHA NYOTA SASA MATATIZO YAKO YAMEPATA SULUHISHO ANAPATIKA KWA MASAA ISHIRINI NA NNE

WASILIANA NAE KWA NAMBA 0762899488-0656145170

WhatsApp namba +255620665635

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumatatu ya May 14

$
0
0


Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumatatu ya May 14

Mbunge: ''Serikali imeshindwa Kuzuia Bidhaa Feki''

$
0
0
Mbunge wa Wawi (CUF), Ahmed Ngwali ameitaka serikali kukiri wazi kwamba imeshindwa kuzuia uingizwaji wa bidhaa bandia nchini licha ya jitihada ambazo serikali inatangaza kuzifanya lakini bado bidhaa hizo zimeeendela kuingia  nchini.

Mbunge huyo amesema hayo Bungeni Mei 11, 2018 wakati wa kuchangia hoja bajeti ya Wizara ya viwanda, biashara na uwekezaji kwa mwaka wa fedha 2018/2019 na kuongeza kuwa polisi ndiyo watuhumiwa wakubwa katika uingizwaji wa bidhaa hizo.

“Serikali iseme tu kama imeshindwa kuzuia bidhaa bandia nchini,  lakini polisi ambao unasema katika kitabu chako,  mnataka kutumia mpaka Interpol katika kuzuia bidhaa feki, polisi hao wenyewe ndiyo wanashiriki katika mambo hayo ya kuingiza bidhaa feki, sasa hiyo Interpol gani mnataka kutumia? Mheshimiwa Mwijage hilo mlirekebishe” alisema Ngwali.

Mbunge huyo ameongeza kwamba serikali imekua inatumia mifumo mbalimbali ikiwemo ukaguzi wa mizigo bandarini lakini tatizo la uingizwaji wa bidhaa bandia umeendelea kuwa mkubwa.

Kwa upande mwingine Mbunge Ngwali amesema mahitaji ya gypsum nchini ni makubwa kuliko uwezo wa uzalishaji wa viwanda vya ndani ambavyo vipo vinne tu na vinauweo wa kuzalisha gypsum milioni tano tu wakati mahitaji ya gypsum nchini ni zaidi ya milioni 10 hadi 12.

Waziri wa Afya: Upimaji UKIMWI Baa sio Lazima

$
0
0
Waziri  wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu amesema upimaji wa Kifua Kikuu (TB) na Ukimwi kwenye baa hautakuwa wa lazima.

Akizungumza wakati wa maadhimisho wa miaka 30 ya Mpango wa Taifa wa Kudhibiti Ukimwi (NACP), Mwalimu alisema baada ya kutolewa taarifa ya kuwapo mpango huo watu wengi wamekuwa na hofu.

“Tutatekeleza mpango wa kusogeza huduma za upimaji TB na ukimwi kwenye baa, ila hautakuwa wa lazima, tutachofanya ni kuwashawishi wananchi kutumia fursa ya kusogezewa huduma hiyo,”alisema.

Aidha, alisema kwa sasa wizara yake iko katika mkakati wa kufanyia marekebisho ya Sheria ya Ukimwi kwa lengo la kuruhusu watu kujipima mwenyewe, kutoa fursa kwa vijana kuanzia miaka 15 kwenda kupima ukimwi bila kupata ridhaa ya wazazi au walezi.

“Haya ni maeneo ambayo kama tutayafanyia marekebisho tutaweza kusaidia kuongeza kasi ya kudhibiti maambukizi ya Ukimwi,” alisema.

Katika hatua nyingine, Mwalimu aliagiza kuanzia Julai mosi mwaka huu, watu wanaoishi wa virusi vya Ukimwi kupewa dawa za miezi mitatu badala ya sasa ya kupewa kwa miezi mwili.

Agizo alilitoa kutokana na Mwenyekiti wa Baraza la Watu wanaoishi na Virusi vya Ukimwi, Justin Mwinuka kudai kuwa utaratibu wa kupewa dawa za miezi miwili umekuwa ukiongezea gharama, kwani wamekuwa wakitakiwa kupima afya zao kila baada ya miezi mitatu.

Waziri huyo alisema utaratibu huo wa kuwapa dawa kwa miezi mitatu mitatu uanze haraka isipokuwa kwa wale ambao wanaonekana hawataweza kutunza dawa hizo au ambao ndio kwanza wanaanza kutumia dawa hizo.

ACT Wazalendo Yataka Wanafunzi Waruhusiwe Kufanya Siasa Vyuoni

$
0
0
Chama cha ACT Wazalendo kimeitaka Serikali kuwaruhusu wanafunzi wa vyuo vikuu wafanye siasa vyuoni kwa taratibu zilizowekwa kwa sababu vyuo ni kitovu cha mabadiliko ya jamii.

Wito huo umetolewa jana Mei 13 na Katibu wa Itikadi, Mawasiliano na Uenezi wa chama hicho, Ado Shaibu ambaye anapinga kauli ya Rais John Magufuli aliyoitoa alipotembelea Chuo cha Kilimo cha Sokoine (Sua) kuwataka wanafunzi wasifanye siasa vyuoni.

Shaibu alisema historia inaonyesha kwamba viongozi wengi wa taifa hili walishawahi kuwa viongozi wa serikali za wanafunzi walipokuwa vyuoni. Amesisitiza kwamba maisha ya siasa wakiwa vyuoni ndiyo yaliwapa ujasiri wa kuingia kwenye ulingo wa siasa.

"Kupiga marufuku siasa vyuoni ni kujenga taifa la vijana waoga, wasiokuwa na uwezo wa kuhoji. Vijana msiache kuhoji mambo ya msingi kwa jamii zenu, hiyo ndiyo maana ya usomi," alisema Shaibu.

Katibu huyo alitoa mifano ya baadhi ya viongozi waliokuwa viongozi vyuoni kuwa ni pamoja na Waziri Mkuu wa zamani, Joseph Warioba ambaye amesema mwaka 1965 alikuwa mwenyekiti wa jumuiya ya wanafunzi wa vyuo vikuu hapa nchini.

Alimtaja pia Spika wa zamani, Samuel Sitta ambaye pamoja na wenziwe walifukuzwa chuo mwaka 1966 kwa kufanya mgomo kupinga matabaka hapa nchini, ajenda ambayo Mwalimu Nyerere aliibeba kwenye Azimio la Arusha.

"Siasa za vyuo vikuu zimewekewa utarabitu wake, sasa tukianza kuwadhibiti hata vijana walio vyuoni tunatengeneza taifa la namna gani?" Alihoji Shaibu na kusisitiza kwamba serikali ina wajibu wa kuhamasisha vijana kujitosa kwenye siasa ili Taifa lipate viongozi bora siku zijazo.

Fisi Avamia Wapenzi na Kuua Mmoja......Mwingine Kajeruhiwa Vibaya

$
0
0
Mkazi wa wilayani Igunga, mkoani Tabora ameuawa na fisi na mwingine kujeruhiwa baada ya kushambuliwa na mnyama huyo katika Kata ya Ziba, wakati wakirejea nyumbani kutoka kwenye klabu ya pombe.

Azizi Kombe, Ofisa Mtendaji wa Kijiji cha Ziba, alimtaja aliyeuawa ni Mwajuma Masanja (37), mkazi wa Kijiji cha Iduguta wilayani Nzega na Shija Maneno (35), mkazi wa Kitongoji cha Ipuli Kijiji cha Igumila Kata ya Ziba ambaye amelazwa katika Hospitali ya Rufani Nkinga na hali yake ni mbaya.

Mtendaji huyo alifafanua watu hao walikuwa ni mtu na mpenzi wake ambao walikuwa wakinywa pombe za kienyeji kwenye klabu iliyopo Kata ya Ziba na kuongeza kuwa baada ya kufika saa 3 usiku waliamua kuondoka kurudi nyumbani.

Hata hivyo, Kombe alibainisha wakati wakiwa njiani kurejea nyumbani walishambuliwa na fisi eneo la vichaka ambapo alimng’ata Mwajuma sehemu za makalio na tumboni, hali iliyomlazimu Shija amsaidie huku akipiga kelele za kuomba msaada.

Mtendaji huyo alisema wakati mwanaume huyo akitoa msaada kwa mpenzi wake, ndipo fisi alimng’ata usoni na ndipo aliposhindwa kutoa msaada na fisi huyo aliendelea kumshambulia mwanamke huyo hadi alipopoteza maisha papo hapo.

Kwa mujibu wa mtendaji huyo, muda mfupi wananchi walifika eneo hilo wakiwa na baadhi ya askari wa kituo kidogo cha polisi Ziba kisha kufanikiwa kumuua fisi huyo.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tabora, Kamishna Msaidizi wa Polisi, Willibrod Mutafungwa, alithibitisha kuuawa kwa mwanamke huyo kwa kushambuliwa na fisi na kwamba fisi huyo aliuawa.

Kwa mujibu wa Kamanda Mutafungwa, majeruhi alikimbizwa Hospitali ya Rufani ya Nkinga ambako alilazwa na kutoa wito kwa wananchi mkoani Tabora kuwa makini na wanyama hatari kwa kutotembea usiku kwenye maeneo hatarishi kwa ajili ya usalama wao.


Hii Hapa Dawa Bora ya Nguvu za Kiume na Maumbile Madogo ya Uume

$
0
0
Tatizo hili limekuwa likiwaadhiri watu wengi sana kisaikolojia hasa baada ya kujiona wapo tofauti sana na wengine kwa kawaida mwanaume anatakiwa awe na uume kuanzia nchi 6-8 kwanza upungufu wa vichocheo hivi huchochea ukuaji wa uume chongo ambalo hushambulia nerve ambayo uharibu kabisa ukuaji wa uume, ngiri, punyeto, ambayo huathili misuli ya uume, ngiri huleta maumivu, tumbo kuunguruma na kujaa gesi, korodani moja kuvimba, kutopata choo vizuri, sababu hizi hufanya uume kulegea na kusinyaa na kuwa mfupi na mwembamba na mara nyingi hata nguvu za kiume ( hamu ya tendo la ndoa) hupungua na kwisha kabisa

GEMBE :Ni dawa inayozalisha na kukufanya uume kukua na kuongezeka
NGEMO : Ni dawa bora ya kuongeza nguvu za kiume

Hukutia hamu ya kuludia tendo la ndoa zaidi mara4 nne bila kukinai au kuchoka pia itakufanya uchelewe kufika kileleni zaidi ya dk30-45 kwa mtumiaji pia tunatibu kisukari, bp, ngiri, miguu kuwaka moto KAMA HUNAMDA WA KUFIKA OFISINI KWETU UTALETEWA POPOTE TUPO MBAGALA RANGI TATU

 0753471612/ 0715249530
0623 386 305

DR KUZENZA

PICHA: Zari, Vera Sidika Wakutana Live Baada ya Bifu la Muda Mrefu

$
0
0
Masista duu wanaosumbua kwenye mitandao ya kijamii, zari the bosslady (Uganda) , pamoja na Vera Sidika(Kenya) wamekutana na kupiga picha ya pa moja  baada ya muda mrefu kudaiwa kuwa kwenye bifu la chini kwa chini huku kila mmoja akidai yeye ndo Bosslady wa East Africa...

Kigwangalla amteua mlimbwende wa Miss Tanzania kuwa balozi wa utalii wa Pori la Akiba Selous

$
0
0
Na Hamza Temba-WMU-Dodoma

Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla amemteua mshindi wa taji la Miss Journalism Tanzania, 2018, Witness Teddy Kavumo (21) kuwa balozi wa utalii wa Pori la Akiba Selous.

Amefanya uteuzi huo mwishoni mwa wiki Jijini Dodoma baada ya mazungumzo na mwanamitindo huyo aliyemtembelea ofisini kwake kwa ajili ya kuomba ufadhili wa kuandaa  mradi wa kijamii ambao ni sehemu ya shindano atakaloshiriki la taji la Dunia la Miss Journalism 2018 litakalofanyika Oktoba 27 Jijini Arusha.

Kufuatia uteuzi huo, Dk. Kigwangalla amemuagiza Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Utalii Tanzania, Devotha Mdachi kuandika barua ya uteuzi kwa balozi huyo mpya sambamba na kumkabidhi hati ya uteuzi ili pamoja na mambo mengine aweze kunadi vivutio vya utalii vya pori hilo.

Wakati huo huo, Dk. Kigwangalla amemuagiza Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania TAWA, Dk. James Wakibara kuandaa safari maalum ya balozi huyo mteule aweze kutembelea Pori la Akiba Selous kwa ajili ya kuona na kujifunza mambo mbalimbali yanayohusu hifadhi hiyo kwa ajili ya utangazaji.

Sambamba na pori hilo atatembelea pia mapori mengine ikiwemo BBK (Burigi, Biharamulo na Kimisi) mkoani Kagera na Mpanga Kipengele mkoani Njombe ambapo  atatumia fursa hiyo kufanya mahojiano na wasichana wa vijiji jirani na hifadhi hizo kwa ajili ya mradi wa kijamii wa kuwainua ikiwa ni sehemu yenye alama muhimu kwenye shindano hilo la Dunia la Miss Journalism 2018.

Awali akiwasilisha ombi lake kwa Waziri Kigwangalla la ufadhili wa safari yake ya ushiriki wa mashindano hayo, Witness pia aliomba kupewa fursa ya kuwa balozi wa Tanzania kwenye moja ya sekta ikiwemo Misitu, Nyuki au Utalii.

Mbali na kushikilia taji la Miss Journalism Tanzania 2018, Witness amesema amewahi kushinda mataji mengine manne makubwa ya kimataifa ya ulimbwende nchini Afrika ya Kusini anakosomea urubani kwa sasa.

Anasema, "Miongoni mwa mataji hayo ni Miss Garden Route 2017, ambalo ni taji la kitaifa la kuhamasisha na kukuza sekta ya Maliasili na Utalii nchini humo, licha ya kuwa ugenini nilitumia fursa hiyo kunadi vivutio vya utalii vya Tanzania.

"Mashindano haya yalihusisha washiriki 600 na wote walikuwa na asili ya kizungu, mimi peke yangu nilikuwa na asili ya kiafrika na niliibuka mshindi".

Aliyataja mataji mengine kuwa ni Miss Bees Cape Town 2017 kwa ajili kuhamasisha uhifadhi wa sekta ya nyuki na mataji mawili ya kimkoa ambayo ni Miss Asla Capetown 2017 na Miss Carnival Mosselbay 2017.

Mataji mengine ya kitaifa aliyowahi kushinda Witness hapa nchini ni pamoja na Miss Arusha Higher Learning 2014 na Miss Northern Zone 2014.

Mashindano hayo ya Dunia ya Miss Journalism 2018 yanahusisha pia uhamasishaji wa maendeleo ya utalii, utamaduni wa amani, uandishi wa habari na kupiga vita ugonjwa wa ukimwi na Malaria.

Pori la akiba Selous ndio hifadhi kubwa kuliko zote nchini ikiwa na ukubwa wa kilomita za mraba takriban 50,000 katika mikoa ya Pwani, Morogoro, Lindi, Mtwara na Ruvuma. Mwaka 1982, Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (Uneso) lilitangaza eneo hilo kuwa moja ya eneo la Urithi wa Dunia na kuanza kuhifadhiwa.

Picha: Hatimaye Jack Wolper Stylish Amvalisha Wema sepetu..

$
0
0
Katika hali isiyotegemewa na wengi especially kwa mastaa mafahari wawili, namzungumzia wema sepetu pamoja na jackline wolper ambapo wawili hao walikua hawaivi chungu kimoja , Ila sasa hivi unaambiwa ubest wao umerudi kwa kasi ya 4G ambapo imefikia stage ya wasanii hao kusapotiana kwenye kazi zao

Wolper ambaye anamiliki kampuni ya Home of stylish, kampuni inayojihusisha na uanamitindo na ushonaji wa mavazi mbali mbali, hivi sasa amepiga hatua kwa kufanikiwa kumvalisha msanii nyota wema sepetu , ambapo inaonekana wema kuvaa nguo za wolper itakua kiki wa kampuni ya wolper na kusababisha watu kibao kujazana kwa mrembo huyo

Kwa mujibu wa warumi , nahisi pia hii ni moja ya project ya kuua soko la hamisa mobeto ambaye hivi karibuni na yeye amefungua duka lake la nguo ambapo pia anashona na kuuza nguo za kike, huenda mastaa hao wameamua kujiunga kuua soko la hamisa( hayo mawazo ya warumi) , nini maoni yako?

Serikali Yaagiza Tani 70,354.35 za Sukari Kutoka Nje ya Nchi.....Tizeba Asema Hakutakuwa na Upungufu

$
0
0
Na Bashiri Salum, Dodoma
Serikali imeagiza sukari kiasi cha tani 70,354.35 kutoka nchi za nje lengo likiwa ni kujipanga ili kuhakikisha kuwa hapatokei upungufu wa bidhaa hiyo hapa nchini.

Akizungumza na vyombo vya habari hivi karibuni waziri  wa kilimo Mhe. Dkt. Charles Tizeba amesema kuwa tani 60,539.35 ya sukari itaanza kuingia hapa nchini katikati ya mwezi Mei 2018 ambapo kiasi kilichobaki cha tani 9,815 kitaingia mwezi  June mwaka 2018.

Aidha  Dkt. Tizeba amefafanua kwamba hakutarajiwi kuwa na upungufu wa sukari hapa nchini  kwa sababu hadi kufikia tarehe 10 mei 2018 katika maghala ya wazalishaji na wafanyabiashara kulikuwa na tani 78,147.67 za sukari na kiasi kingine  tani 25,441.25 kipo Bandarini .

Kwa kiasi cha sukari ambacho tayari kipo hapa nchini kikijumlishwa na kiasi ambacho kitaingia hivi karibuni kutoka nje ya nchi ni dhahiri kwamba  nchi haiwezi kupata upungufu wa bidhaa hiyo, alisema Mhe.Waziri.

Awali Dkt.Tizeba  alisema kwamba mahitaji ya sukari nchi nzima ni tani 630,000 ambapo kati ya hizo, tani 145,000 ni kwa ajili ya matumizi ya viwandani na tani 485,000 ni kwajili ya matumizi ya kawaida.

Hata hivyo mapitio yanaonesha kwamba  msimu wa mwaka 2017/18  viwanda vya ndani vilizalisha tani 306,226  za sukari kwa matumizi ya kawaida  ambapo mwisho wa msimu huu uzalishaji umefikia tani 307,481.76 aliongezea Dkt. Tizeba.

Akimalizia taarifa yake Mhe. Tizeba amebainisha kuwa kwa kiasi ambacho sukari imeagizwa kutoka nje Pamoja na viwanda vya ndani inadhihirisha kwamba hakutakuwa na upungufu wa aina yeyote ya sukari hapa nchini na ikizingatiwa  kuwa viwanda vitaanza uzalishaji mwingine mwezi mei ambapo ukarabati (services ) itakuwa imekamilika .
Viewing all 104789 articles
Browse latest View live




Latest Images