Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104809 articles
Browse latest View live

Pata Tiba ya Tatizo la Nguvu Za Kiume, Inasaidia Kukufanya Urudie Mara 5 na kuchelewa kwa Dakika 20

$
0
0
TATIZO LA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME NA MAUMBILE MADOGO LINATIBIKA.Baada ya utafiti wa mda mrefu juu ya matatizo ya upungufu wa nguvu za kiume na ukosaji wa hamu ya tendo la ndoa ama kushindwa kurudia tendo kwa haraka DR Magise imekuletea tiba ya matatizo hayo kwa kutumia dawa za:

GUMBA POWER:Ni dawa asili ya vidonge inayotibu tatizo la upungufu au ukosefu wa nguvu za kiume,dawa hii inamchanganyiko wakutosha wenyekuzalisha vichocheo vingi vya Hemone za Gestrogen vikiwemo vitamin B6&B1,vitamini E,pamoja na madini aina ya zinc vitakufanya kuwa na nguvu na mzunguko mzuri wa damu na kuongeza hamu na uwezo wa kufanya tendo la ndoa zaidi ya hatua nne au zaidi,na kuchelewa kufika kileleni zaidi dakka 20-30.

NTINJE:Inarutubisha maumbile ya uume yani kurefusha na kunenepesha nchi 4-7 upana cm3-4 standard kiafya haijalishi umri wako hata kwa wazee ukiitumia maumbile yako yatabaki kuwa hivyo siku zote,Pia tunatibu Presha,kisukari siku7,ngiri,chango la tumbo tumbo kujaa gesi,kutopata choo vizuri

 TUPO TZ DAR ES SALAAM   MBAGALA RANGI TATU.HUDUMA HII UTALETEWA POPOTE ULIPO .WASILIANA NAMI 0754741788, 0715741788, 0783741788

-DR MAGESA

Nasikitika Kuona Kizazi cha 'Wife Material' Kinazidi Kupotea Duniani

$
0
0

Natumai mko wazima wa afya, wakuu nimekuwa katika tafiti zangu juu ya wanawake kwa muda wa miaka minne.

Jambo nililogundua ni kuwa binti wengi wanaanza mapenzi wakiwa na umri mdogo tena na watu walio wazidi umri. Yani kisa kilichonimaliza nguvu ni binti wa form one tena kiongozi wa dini, kwa macho ni katulivu, kapole lakini baba mzima ndo anafanya nae mapenzi bila aibu.

Huyo ni mmoja wapo kati ya sample 100 nilizozitumia za mabinti umri wa miaka 10 - 14.Tena wengine hawana aibu wanapost na boyfriend zao fb.

Sasa ninachojiuliza hivi mama zao hawana utaratibu wa kuwakagua bikra kila weekend kama bado zipo? Pia katika utafiti wangu nimegundua 96% ya wanawake wameolewa bila bikra.


Mwisho: NASIKITIKA SANA KUONA KIZAZI CHENYE BIKRA KINAZIDI KUPOTEA KWENYE USO WA DUNIA KAMA DINASOUR

By Emok Jr

Kutana na Mtabibu Mwenye KUBRI kutoka kwa ALLAH Mzee sulutani Mtabibu wa Nyota za Binadamu

$
0
0
Kutana na Mtabibu Mwenye KUBRI kutoka kwa ALLAH Mzee sulutani Mtabibu wa Nyota za Binadamu na Dawa za Asili ya Africa Mwenye UWEZO Kubaini tatizo lako Pindi tu Utakapo Fanya Mawasilino Kupitia Wasaa Husika..JE UNASUMBULIWA NA Mapenzi? (Umeachwa na Umpendae,Awe Mume,Mke na Bado unampenda?Na Umejaribu Sehemu nyingi Bila Mafanikio?Wasilina na Mzee sulutani Ujione muujiza wa Papo kwa Papo.. anauwezo WA KURUDISHA MAHUSIANO NA KUIMARISHA NDOA YAKO NDANI YA SAA 12 TU.

Umekimbiwa na Mumeo,mkeo au Mpenzi na anaishi na mtu mwingine? Muone akutatulie Anauwezo wa Hali ya Juu wa Kusambalatisha Mahusiano yao Endapo utafata Atakacho kuelekeza.
Atamfanya Atimize Ahadi zote kwa Muda Mfupi.
Mzee sulutani Anatumia Jina la Muhusika au Picha Kumaliza Tatizo lako..

Anatibu kwa Kutumia Vitabu vya QUR-AN Dawa za Asili za Africa,Dawa za Kiarabu na Majini.Anatafsiri Ndoto. Kushinda BAHATI NASIBU, KUSAFISHA NYOTA. Mvuto wa Mwili na BIASHARA, Kinga ya Mwili,ZINDIKO za Nyumba.MIGUU Kufa GANZI.

Kufungua KIZAZI kwa wale walio fungwa kwa njia za KISHIRIKINA. Anakupa Jini la Mali kwa yule anaehitaji Utajiri BILA MASHARTI. Nguvu za KIUME, Humaliza Kesi zilishindika ndani ya siku 14 tu..

Na Mengi zaidi +255) 623448511 au (+255) 783636592

NB: TIBA KWA DINI ZOTE NA IMANI ZOTE...

Mbwana Samatta Atua Mecca Kufanya Umrah

$
0
0
Mbwana Samatta atua Mecca kufanya Umrah
Mbali na soka lakini mchezaji wa Taifa Stars na Klabu ya KRC Genk ya Ubelgiji, Mbwana Samatta ni mtu wa ibada.

Mchezaji huyo baada ya kumalizika kwa ligi kuu ya Ubelgiji ametua mjini Mecca nchini Saudia Arabia kwa ajili ya kufanya ibada ya Umrah.


Mbwana Samatta (kushoto) akiwa na mchezaji mwenzake wa Genk, Omar Colley

Kwenye ziara hiyo, Samatta ameambatana na mchezaji mwenzake wa Genk, Omar Colley ambaye ni raia wa nchini Gambia.

Samatta anatarajiwa kurejea hapa nchini muda sio mrefu kwa ajili ya kujiandaa na mchezo wa hisani wa kuchangia elimu kati yake na timu ya Alikiba kwenye mchezo ambao unatarajiwa kuchezwa Juni 9, mwaka huu.

Serikali Yakiri Ubovu Mashine Za EFD

$
0
0
Serikali Yakiri Ubovu Mashine Za EFD
Serikali imesema mashine za kielektroniki za (EFD) hazifanyi kazi kwa sasa nchi nzima ambapo imesambaza wataalamu nchi nzima kutatua ttaizo hilo.

Kauli hiyo imetolewa na Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Dk. Ashatu Kijaji alipokuwa akijibu mwongozo wa spika ulioombwa na Mbunge wa Sumve, Richard Ndassa aliyetaka kujua serikali imejipangaje kwa kuwa uharibifu wa mashine hizo unalipotezea taifa mapato na kwamba linaweza kuwa ni tatizo lililotengenezwa na baadhi ya watu kwa ajili ya kuhujumu mapato ya serikali.

Akijibu swali hilo Dk. Kijaji amesema mashine hizo zilianza kutofanya kazi kuanzia Mei 11, mwaka huu na baadaye likatatuliwa.

“Wiki moja baada ya kutatuliwa tatizo likajirudia hadi leo, lakini serikali imepeleka wataalamu wa ICT katika Ofisi za Mamlaka ya Mapato (TRA) kwa ajili ya kutatua tatizo hilo ambalo naamini litatatuliwa ndani ya muda mfupi ujao,” amesema.

Baada ya Kuteuliwa na Rais Dk Bashiru Atinga UDSM

$
0
0
Baada ya Kuteuliwa na Rais Dk Bashiru Atinga UDSM
Katibu Mkuu Mteule wa CCM, Dk Bashiru Ali amewasili katika viunga vya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) alikokuwa akifundisha.

Dk Bashiru ameonekana leo Mei 30, katika chuo hicho, akisalimiana na kupongezwa na wahadhiri wenzake pamoja na wanafunzi, ikiwa ni siku moja baada ya kuteuliwa kushika nafasi hiyo.

Dk Bashiru ametuliwa jana na Halmashauri Kuu ya CCM, kushika nafasi hiyo, akimrithi Abdulahman Kinana.

Awali baada ya kiongozi huyo kufika chuoni aliingia katika jengo la Utawala na baadaye kuelekea Idara ya Sayansi ya Sanaa na Utawala alikokuwa akifanyia kazi.

Akiwa kwenye idara hiyo, Dk Bashiru alizungumza na Mkuu wa Idara hiyo, Rasul Ahmed Minja ambaye pia alimlaki kwa shangwe na kumpongeza kwa uteuzi.

Kijana Aliyemuokoa Mtoto Toka Ghorofani Aanza Kazi Katika Jeshi la Zimamoto

$
0
0
Kijana Aliyemuokoa Mtoto Toka Ghorofani Aanza Kazi  Katika Jeshi la Zimamoto
Hadi mwishoni mwa wiki iliyopita maisha ya Mamoudou Gassama, kijana wa Mali mwenye umri wa miaka 22 yalikuwa sawa na ya maelfu ya wahamiaji wanaohaha huku na kule barani Ulaya wakitafuta maisha bora.

Ghafla Jumapili nyota ya bahati ilimwangazia Gassama, mambo yalibadilika na kuwa shujaa wa Ufaransa leo. Tukio moja tu la kuokoa maisha ya mtoto limemfungulia bahati na sifa sasa amepewa jina la "Spiderman wa Paris", hadhi kisheria ya kuishi Ufaransa na kufanya kazi katika Jeshi la Zimamoto.

Tukio lililomfanya Gassama, ambaye hadi mwishoni mwa wiki alikuwa mhamiaji haramu lisingefikiriwa kumbadili haraka hivi. Hata hivyo, kuanzia wikiendi hiyo, kijana huyo anaishi maisha ya ndoto yake tangu kumwokoa mtoto wa miaka minne aliyekuwa ananing’inia kwenye kibaraza cha ghorofa ya nne ya jengo.

Kitendo hicho cha kishujaa kimepongezwa nchini kwake Mali na Ufaransa. Jumatatu kijana huyo alipokewa na Rais wa Ufaransa Emmanuel Macron na akaahidiwa kupewa uraia ambao Uhamiaji wamekuwa wakishughulikia kuanzia Jumanne. Gassama atapewa kadi ya kibali cha kuishi Ufaransa kwa miaka 10 kabla ya kupewa uraia kamili.

Halafu alikwenda katika Jeshi la Zimamoto la Paris Fire Brigade ambako alitia saini mkataba wa miezi 10. Jumatano alianza mafunzo ya kazi itakayomwezesha kulipwa karibu euro 600 kwa mwezi sawa na shilingi za Tanzania 1,588,990.70

Msanii mashuhuri Rihanna amesema kupitia Instagram: "Nimefurahishwa sana."  Rais wa Mali Ibrahim Boubacar Keïta, mbali ya kumpigia simu kumpongeza ameandika kupitia akaunti ya Twitter: “Mwana mzuri na shujaa wa Mali".

Mwanaume Ajinyonga kwa Chandalua Baada ya Mkewe Kufariki

$
0
0
Mwanaume Ajinyonga kwa Chandalua Baada ya Mkewe Kufariki
Charles Monene Nyatete miaka 42 amekutwa amejinyonga kwa kutumia chandarua kwenye mti wa mparachichi baada ya mke wake kufariki.

Kwa mujibu wa Chifu wa kijiji cha Nyankami jimbo la Nyamira, Cosmas Mocha amesema kuwa marehemu alitoweka baada ya kupata taarifa za mke wake , Carren Kwamboka Monene  kuaga dunia May 27 akiwa hospitalini.

Mke wa marehemu inadaiwa kuwa alikuwa amelazwa hospitalini kwa kipindi cha wiki mbili kabla hajafariki.

Aidha taarifa ya familia ya marehemu inasema kuwa walianza kumtafuta marehemu huyo baada ya kutoweka May 27 kabla ya kumkuta May 28 akiwa ananing’inia kwenye mti wa mparachichi akiwa tayari amekufa kwa kujinyonga kwa kutumia chandarua.

Baadaye mwili huyo wa marehemu waliuchukua na kuupeleka mochwari kwa ajili ya uchunguzi zaidi wa kipolisi.

"Mimi Sipendi Kutumia Kondomu" - Chemical

$
0
0
"Mimi sipendi kutumia kondomu" - Chemical
Mwanamuziki anayefanya poa na ngoma zake , Chemical ameweka wazi kuwa yeye siyo muumini wa kutumia kinga (kondomu) ndiyo maana mara nyingi anapenda kuwa kwenye mahusiani na mtu ambaye ni muaminifu.


Kupitia kipindi cha Kikaangoni  kinachorushwa kila Jumatano kupitia ukurasa wa Facebook EATV, Chemical amesema hayo wakati alipoulizwa na mtangazaji wa kipindi hicho mara yake ya mwisho kutumia kinga.

"Mara ya mwisho kutumia kinga wakati nafanya mapenzi ni muda kidogo, ila kiukweli mimi sio shabiki wa kinga kabisa. Mambo ya kinga kinga mimi hapana ndiyo maana napenda sana kuwa na mtu aliyetulia. Chemical"

Pamoja na hayo Msanii ameweka wazi kwa sasa hayupo kwenye mahusiano na mtu yoyote kwa kuwa ameamua kuchagua kutengeneza maisha yake na kuhofia kuumizwa moyo wake.

Waziri Mkuu: Nitazindua Kampeni Ya Kupima VVU .....Lengo Ni Kuhamasisha Wanaume Wapime Afya Zao, Wajue Hali Zao

$
0
0

WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema mwezi ujao, atazindua kampeni maalum ya upimaji wa virusi vya UKIMWI (VVU) ambayo imelenga kuwahamasisha wanaume wapime afya zao na kutambua hali zao.

“Serikali tumeandaa kampeni maalum ya kuhamasisha upimaji wa VVU na kuanza matumizi ya dawa za kufubaza VVU mara moja (Test and Treat), hasa kwa wanaume. Kampeni hii itazinduliwa rasmi na mimi mwenyewe jijini Dodoma tarehe 19 Juni 2018,” amesema.

Ametoa kauli hiyo leo (Jumatano, Mei 30, 2018) wakati akizindua maadhimisho ya miaka 15 tangu kuanzishwa kwa Mfuko wa Dharura wa Rais wa Marekani wa Kupambana na Kudhibiti Maambukizi ya Virusi vya UKIMWI (PEPFAR) kwenye ukumbi wa Mwalimu Nyerere, jijini Dar es Salaam.

“Takwimu zinaonyesha watu ambao wako tayari kupima kwa hiyari yao siku zote ni wanawake. Akinababa wakiambiwa hutoa sababu mara hiki, mara kile. Nitoe wito kwa wanaume wote, tubadilike! Ni vema tushiriki kampeni ya wanaume kujitambua na kupima ili tujue hali zetu,” amesema.

Amewataka wadau wote wanaohusika na masuala ya UKIMWI washiriki kikamilifu katika kampeni hiyo baada ya uzinduzi, na pia akawataka Wakuu wa Mikoa mikoa yote nchini wasimamie kampeni hizo muhimu katika mikoa yao hadi ngazi ya vijiji.

Waziri Mkuu amesema ujio wa PEPFAR umeleta mafanikio makubwa katika vita dhidi ya UKIMWI na kupitia shughuli zake, elimu ya kinga na ufahamu kuhusu UKIMWI ilitolewa kwa watu wa rika na makundi mbalimbali ya jamii.

Hata hivyo, Waziri Mkuu amesema Tanzania bado inakabiliwa na changamoto kadhaa zikiwemo ukubwa wa viwango vya maambukizi na kuongezeka kwa idadi ya watu wanaoambukizwa VVU katika baadhi ya mikoa nchini.

Amesema kuna mikoa 14 ambayo kiwango cha maambukizi kiko juu ya wastani wa kitaifa wa asilimia 4.7 na akaitaja mikoa hiyo kuwa ni Njombe wenye asilimia 11.4, Iringa (asilimia 11.3), Mbeya (asilimia 9.3), Mwanza (asilimia 7.2), Kagera (asilimia 6.5) na Katavi (asilimia 5.9). Mikoa mingine ni Shinyanga (asilimia 5.9), Songwe (asilimia 5.8) Ruvuma (asilimia 5.6) Pwani (asilimia 5.5) Tabora (asilimia 5.1) pamoja na Tanga, Dodoma na Geita ambayo yote ina asilimia 5.0 ya maambukizi.

Waziri Mkuu ameitaja mikoa mingine sita ambayo ina ongezeko kubwa la watu wanaoishi na VVU kuwa ni Iringa (asilimia 11.3), Mwanza (asilimia 7.2), Kagera (asilimia 6.5), Tanga (asilimia 5.0), Dodoma (asilimia 5.0) na Manyara (asilimia 2.3).

Amesema takwimu hizo zinaonesha kuwa nguvu na jitihada zaidi zinahitajika katika kuzuia maambukizi mapya ya VVU kwa kuweka utaratibu thabiti na endelevu wa kutoa elimu na hamasa ya kutumia huduma zilizopo za kupambana na UKIMWI nchini. “Kwa hiyo, programu za kinga zinapaswa kuwa endelevu kwenye mikoa yote nchini, hususan mikoa yenye kiwango cha juu cha maambukizi. Pia huduma za ARVs ziendelee kupewa kipaumbele katika mipango yetu,” amesisitiza.

Mapema, akimkaribisha Waziri Mkuu kuzungumza na washiriki wa hafla hiyo, Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Bi. Ummy Mwalimu alisema Tanzania kwa sasa ina watu karibu milioni moja ambao wako kwenye matibabu ya kufubaza VVU.

“Kutokana na mpango wa PEPFAR, Tanzania imekwishapokea sh. trilioni 10 tangu mfuko huu uanzishwe mwaka 2003 na matumizi ya dawa za kufubaza VVU yamesaidia kupunguza idadi ya vifo vitokanavyo na UKIMWI kwa asilimia 70, yaani kutoka vifo 110,000 mwaka 2003 hadi kufikia 33,000 mwaka 2016,” alisema.

Alisema kutokana na matumizi ya dawa hizo, maambukizi mapya kutoka kwa mama kwenda kwa mtoto nayo pia yamepungua kutoka asilimia 12 na kufikia asilimia 4.9 hivi sasa.

Kwa upande wake, Kaimu Balozi wa Marekani, Bi Inmi Patterson alisema kati ya sasa na Septemba 2019, PEPFAR inatarajia kutumia zaidi ya sh. trilioni moja (dola za Marekani milioni 512) katika kuboresha huduma za kuzuia maambukizi ya VVU, upimaji na matibabu hapa nchini.

Alisema wanapoendelea na utekelezaji wa kazi za mfuko huo na maadhimisho ya miaka 15 ya PEPFAR, kampeni yao itaendelea kwa mwaka wote wa 2018 na imelenga kupunguza unyanyapaa na tabia ya kuwatenga watu wanaoishi na virusi vya UKIMWI.

“Kampeni ya PEPFAR15 inalenga kupunguza unyanyapaa, kuongeza upatikanaji na matumizi ya huduma zitolewazo za kukabiliana na VVU. Kila mtu atakayepimwa na kugundulika kuwa ana maambukizi ya VVU, ataanzishiwa matibabu mara moja. Tutafanya kazi na watu wanaoishi na VVU nchini kote ili kusimulia habari nzuri (positive stories) za watu wanaoishi na VVU ambao waliwahi kuwa dhaifu ama wagonjwa lakini sasa wana nguvu na afya; habari za akinamama wanaoishi na VVU na wanapata matibabu ili kuwalinda watoto wao,” alisema.

IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,

Kutana na Mtabibu Mwenye KUBRI kutoka kwa ALLAH Mzee sulutani Mtabibu wa Nyota za Binadamu

$
0
0



Kutana na Mtabibu Mwenye KUBRI kutoka kwa ALLAH Mzee sulutani Mtabibu wa Nyota za Binadamu na Dawa za Asili ya Africa Mwenye UWEZO Kubaini tatizo lako Pindi tu Utakapo Fanya Mawasilino Kupitia Wasaa Husika..JE UNASUMBULIWA NA Mapenzi? (Umeachwa na Umpendae,Awe Mume,Mke na Bado unampenda?Na Umejaribu Sehemu nyingi Bila Mafanikio?Wasilina na Mzee sulutani Ujione muujiza wa Papo kwa Papo.. anauwezo WA KURUDISHA MAHUSIANO NA KUIMARISHA NDOA YAKO NDANI YA SAA 12 TU.

Umekimbiwa na Mumeo,mkeo au Mpenzi na anaishi na mtu mwingine? Muone akutatulie Anauwezo wa Hali ya Juu wa Kusambalatisha Mahusiano yao Endapo utafata Atakacho kuelekeza.
Atamfanya Atimize Ahadi zote kwa Muda Mfupi.
Mzee sulutani Anatumia Jina la Muhusika au Picha Kumaliza Tatizo lako..

Anatibu kwa Kutumia Vitabu vya QUR-AN Dawa za Asili za Africa,Dawa za Kiarabu na Majini.Anatafsiri Ndoto. Kushinda BAHATI NASIBU, KUSAFISHA NYOTA. Mvuto wa Mwili na BIASHARA, Kinga ya Mwili,ZINDIKO za Nyumba.MIGUU Kufa GANZI.

Kufungua KIZAZI kwa wale walio fungwa kwa njia za KISHIRIKINA. Anakupa Jini la Mali kwa yule anaehitaji Utajiri BILA MASHARTI. Nguvu za KIUME, Humaliza Kesi zilishindika ndani ya siku 14 tu..

Na Mengi zaidi +255) 623448511 au (+255) 783636592

NB: TIBA KWA DINI ZOTE NA IMANI ZOTE...

Bushiri Aibua Utata CCM, Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Alhamisi ya May 31

$
0
0



Bushiri Aibua Utata CCM, Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Alhamisi ya May 31

Zitto Kabwe Atangaza Ushirikiano na Chadema Jimbo la Buyungu

$
0
0
Jana Jumatano Mei 30, 2018, Zitto kupitia mitandao mbalimbali ya kijamii ameeleza kuwa yeye na mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe wamekubaliana kuwa watashawishi kuwepo na ushirikiano wa vyama vya upinzani katika uchaguzi huo.

Uchaguzi wa Buyungu utafanyika baadaye mwaka huu baada ya aliyekuwa mbunge wa jimbo hilo, Kasuku Bilago kufariki dunia Mei 26, 2018.

“Kwa heshima ya mwalimu Bilago mimi na Mbowe tumekubaliana kuwa tutashawishi kuwepo na democratic front (ushirikiano wa kidemokrasia) katika Jimbo la Buyungu,”amesema Zitto.

“Ama ACT itaunga mkono mgombea wa Chadema au Chadema itaunga mkono mgombea wa ACT Wazalendo. Tunataka kuweka mgombea mmoja anayekubalika na wananchi wa Buyungu na kufanya kampeni kwa pamoja mpaka ushindi.”

Amesema huo ni mwanzo wa harakati za kuwa na ushirikiano imara wa kidemokrasia dhidi ya ukandamizaji wa demokrasia nchini na hali mbaya ya maisha ya wananchi.

“Umoja wa zaidi ya vyama vya siasa ukihusisha vyama vya wafanyakazi, vyama vya wakulima, vyama vya wafanyabiashara na wananchi wengine,” amesisitiza mbunge huyo.

Hatimaye Mrisho Ngassa Amerudi Yanga

$
0
0
Baada ya kuenea kwa tetesi mbaimbali zikidai kuwa club ya Yanga SC sasa wameyumba kiuchumia kiasi cha kushindwa kufanya usajili wa nafasi tatu za wachezaji watakaoongeza nguvu katika kikosi cha Kombe la shirikisho Afrika.

Jumatano ya May 30 2018 kutoka mtandao wa habari za michezo wa shaffihdauda.com zimeripotiwa taarifa za kufanya usajili wa mshambuliaji wao wa zamani Mrisho Khalfan Ngassa, Yanga imemsajili Mrisho Ngassa kwa ajili ya kuongeza nguvu.

Kama utakuwa unakumbuka vizuri Mrisho Khalfan Ngassa aliwahi kuichezea Yanga kwa miaka kadhaa kabla ya kuamua kwenda Free State ya Afrika Kusini, Fanja FC ya Oman, Mbeya City ya Mbeya na baadae akajiunga na Ndanda FC kabla ya leo hii kutangazwa kurudi Yanga.

Amber Lulu Ametaja List ya Mastaa wote Bongo Aliowahi Kutoka nao

$
0
0
Muimbaji wa Bongofleva Amber Lulu leo kupitia mahojiano yake na kipindi cha Break cha Clouds TV amekuwa gumzo mitandaoni baada ya kukubali kuweka wazi orodha ya mastaa wa Bongo ambaye amewahi kutoka nao kimapenzi.

Amber Lulu akihojiwa na Simple The Boy aliulizwa vipi anatoka kimapenzi na Nuh Mziwanda na alikanusha  lakini alipoulizwa  ni mastaa gani wa bongo ambao amewahi kuingia nao katika mahusiano ya kimapenzi alikuwa radhi kusema.

“Mimi na Nuh  ni marafiki tu na tumefanya kazi pamoja list ya mastaa ambao nimewahi kulala nao ni Barnaba, Aslay, Rammy Garis ila Young Dee sio sana lakini Prezoo ni mume wangu unajua nampenda tu naomba anisamehe tu” Amber Lulu

Mbunge wa Morogoro Alia na JWTZ Migogoro ya Ardhi na Wananchi, Wazri Mwinyi Amtuliza

$
0
0
Mbunge wa Morogoro Mjini (CCM), Abdulaziz Mohamed Abood ameiomba Serikali kutumia ramani ya mwaka 1970 kuwapatia haki yao ya ardhi wananchi wa Kata ya Kauzeni na Luhogo mkoani Morogoro ambao maeneo yao yameingiliwa na mipaka ya kambi ya Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ).

Abood ametoa kauli hiyo bungeni mjini Dodoma leo Jumatano Mei 30, 2018 wakati akiuliza swali la nyongeza kufuatia  majibu ya Serikali kuwa wananchi wa eneo hilo hawana mgogoro na JWTZ baada ya upimaji wa mwaka 2002.

“Wananchi wa maeneo hayo walianza kuishi hapo mwaka 1969 na ilipofika mwaka 1970 Serikali iliwapimia eneo hilo lakini cha kushangaza kila wakati wanaambiwa wamevamia ni kwa nini mipaka ya mwaka 1970 isitumike ili wabaki na maeneo yao,” amehoji Abood.

Katika swali lake la msingi, mbunge huyo amesema ni lini Serikali itawarudishia wananchi maeneo yao ya kilimo, kuhoji kwanini isichukue hatua kwa kuruhusu wananchi wamiliki maeneo hayo kwa kuwa  JWTZ imewakuta.

Katika majibu yake, Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa (JKT), Dk Hussein Mwinyi amesema ufumbuzi  wa mgogoro wa mipaka ulishafanyika kwa kushirikiana na halmashauri ya Manispaa ya Morogoro hivyo jeshi  halina mgogoro na wananchi wa maeneo hayo.

Amesema manung’uniko yaliyopo yanatokana na uamuzi wa JWTZ kusitisha utaratibu wa kuwaruhusu kwa muda baadhi ya wananchi kulima mashamba ndani ya mipaka yake kwa sababu za kiulinzi na usalama.

“Haitakuwa vyema kwa JWTZ kuondoka katika maeneo yaliyochaguliwa kistratejia za ulinzi, kuondoka katika maeneo haya kutaligharimu Taifa hivyo wananchi waelimishwe juu ya jambo hili,” amesema Mwinyi.

MSAMI “Nilivyoachana na Uwoya Nilikuwa Bado Nampenda”

$
0
0
Jana May 30, 2018 kupitia kipindi cha XXL cha Clouds Fm dancer na pia msanii wa Bongofleva  Msami alifanya mahojiano na kuongea vitu kibao ikiwemo mahusiano yake na muigizaji Irene Uwoya ambaye kwa sasa ni mke halali wa Dogo Janja.

Msami amefunguka na kusema kuwa Godzilla aliwahi kumpigia simu aliyekuwa mpenzi wake Irene Uwoya na kumzungumzia vibaya juu yake na hakujua lengo halisi la Godzilla kufanya hivyo ilikuwa ni nini hasa.

“Wakati nikiwa na mahusiano na Irene Uwoya Godzilla alimpigia simu uwoya na kunipondea sana”

Msami ameongezea pia na kusema kuwa wakati anaachana na Irene Uwoya alikuwa bado anampenda.

Muone Ustadhi Ashrafu Atimize ndoto yako..Anatumia Nyota na Nguvu za Asili Kutibu

$
0
0
Muone Ustadhi Ashrafu Atimize ndoto yako. yawezekana ulizaliwa nanyota yakitajiri ila watu wabaya wameikalia mpaka sasa ikawa hufahamu chochote. Mtafute ust Ashrafu Airudishe nyota yako yakitajiri kwakupitia pete inayoendana na nyota yako. Ust Ashrafu Ananguvu zamajini katika utendaji wake.

Anauwezo wakutoa Mali kwakupitia pete nakwakupitia majini wake. Na anauwezo wakuzirudisha Mali zilizopotea kwanjia zakichawi kwakupitia Pete yakifalme Ambayo inayong'aa muda wowote nakubadilikabadilika rangi. Ust Ashrafu Ametembea baadhi ya nchi kwakuwapatia watu huduma mbalimbali. Kama vile maradhi yakisukari, presha, ukimwi, bawasiri, tezidume, mwiliwote kupooza nakutetemeka, NK. Navilevile Amewapatia wengi huduma yamvuto wa kibiashara, nayamvuto wakimapenzi.

Nawengi wametoa shukrani zao kwa ust Ashrafu namna Alivyozirudisha Ndoa zao zilizo sambaratika kwamuda mrefu. Mtafute ust Ashrafu ili akusaidie juu yamambo yako. Nahuyu ust anasaidia matatizo yauzazi, nguvu zakiume, kuwashwa mwilini, kutokwa namapere usoni nasehemu za siri, NK. Na anadawa yakumtuliza mume asiesikia nakutulia inayoitwa limbwata. Na anadawa yakumrudisha mpenzi ktk mahusiano kwamda mchache.

Na amezipatanisha familia nyingi zilizogombana. Na anauwezo wakufarakanisha maadui waliokua pamoja. Mtafute Ustadhi Ashrafu kwa no. 0768486717-0627423037 Au Mtafute kwa whasapp 0659438578

Hizi ndio namba zake mpigie muda wowote usiogope yupo kwaajili yako. Mpigie hupate muongozo wa bure naushri. Ustadhi Ashrafu huduma zake hupatikana mahala popote utakapo muhitaji, ila sehemu kuu anapatikana Bagamoyo.

Mhubiri Awaomba Waumini Wake Wamnunulie Ndege ya nne

$
0
0
Mhubiri mmoja wa Kiinjilisti nchini Marekani amewaomba waumini wake kuchanga pesa za kumsaidia kununua ndege yake ya nne.

Amesema hata kama Yesu angekuwepo siku hizi, "hangekuwa anapanda punda".

Jesse Duplantis amesema Mungu amemwambia anunue ndege aina ya Falcoln 7X ambayo inagharimu $54m (£41m).

Ameongeza kwamba alikuwa na shaka pia kuhusu kuendelea na ununuzi huo mwanzoni, lakini Mungu alimwambia: "Sikukwambia uilipie. Nilikwambia uamini na utaipata."

Ingawa si jambo nadra kwa wahubiri kumiliki ndege zao binafsi, ombi lake kwa waumini kuchangia limezua shutuma.

Watu kwenye Twitter wamepokea ombi hilo kwa mshangao, wengi wakinukuu aya kwenye Biblia zinazotahadharisha dhidi ya ulafi na "manabii wa uongo".

Wengine wanasema pesa hizo zingetumika vyema kuwasaidia maskini.

Kwenye ujumbe wa video ambayo imepakiwa kwenye mtandao wake, Duplantis mwenye umri wa miaka 68 alisema: "Mwajua, nimemiliki ndege tatu maishani mwangu, na nimezitumia na kuchoma mafuta kwa ajili ya Bwana Yesu Kristo.

"Sasa, baadhi ya watu wanaamini kwamba wahubiri hawafai kuwa na ndege. Ninaamini kwamba wahubiri wanafaa kwenda kwenye kila redio (au kipaza sauti), kwenye kila chombo (cha habari), kuwezesha Injili kuenezwa kote duniani."

Huku akiwa amesimama karibu na picha za ndege zake anazozimiliki sasa, mhubiri huyo alisema ndege aliyoinunua miaka 12 iliyopita kwa sasa haitoshi kwa utumishi na matumizi ya kanisa lake.

Alisema ni kwa sababu ndege hiyo haiwezi kusafiri mbali bila kutua, hiyo ikiwa na maana kwamba hulazimika kulipa pesa nyingi kutua ili kuiongeza mafuta.

Picha nyingine iliyooneshwa kwenye video hiyo ilimuonyesha mhubiri huyo akiwa amesimama na ndege hizo tatu, na juu ya picha hiyo maelezo: "Si kuhusu vitu unavyomiliki, bali vitu unavyovipa kipaumbele."

Bw Duplantis ametetea ombi lake la kutaka kununuliwa ndege akisema Yesu aliwaambia wafuasi wake "nendeni kote duniani na mkahubiri Injili kwa kila kiumbe, sasa tutawezaje kutimiza hilo? Siwezi kuishi muda mrefu wa kutosha kusafiri kote kwa kutumia gari au meli au treni, lakini ninaweza kusafiri mbali kwa kutumia ndege."

Mwaka 2015, Bw Duplantis alitokea kwenye video na mhubiri mwingine Kenneth Copeland, ambapo Bw Copeland alieleza kusafiri kwenye ndege za kibiashara, pamoja na watu wengine wa kawaida, kama kusafiri "katika mkebe mkubwa uliojaa mashetani."

Hii Ndiyo Huduma ya Kwanza kwa mtu Aliyegongwa na Nyoka

$
0
0
Huduma ya kwanza ni matibabu ya awali anayopata mgonjwa mara tu au muda mfupi baada ya kugongwa na nyoka kabla hajafikishwa kwenye kituo cha afya. Inaweza kufanywa na muathirika mwenyewe au mtu yeyote mwenye ujuzi wa kutoa huduma ya kwanza aliyepo karibu.

Malengo ya huduma ya kwanza

Kujaribu kuzuia kusambaa kwa sumu
Kulinda uhai na kuzuia madhara kabla mgonjwa hajapata matibabu
Kudhibiti dalili hatarishi za sumu
Kuandaa usafiri wa kumpeleka mgonjwa kwenye kituo cha tiba
Muhimu zaidi, Ni kuepuka kusababisha madhara zaidi.


Hatua za Huduma ya Kwanza
1. Mtie moyo mgonjwa (mara nyingi anakuwa na hofu).

2. Mlaze mgonjwa katika hali ya utilivu, hakikisha viungo havichezi . Viungo vikicheza huchangia sumu kusambaa mwilini.

3. Epuka kugusa sehemu iliyogongwa. Unapogusa sehemu iliyogongwa unasababisha sumu kusambaa kwa urahisi, kuingiza vimelea vya bakteria na damu kuvuja.

KUMBUKA : Iwapo nyoka ameuwawa unaweza kwenda nae katika kituo cha afya.
Viewing all 104809 articles
Browse latest View live


Latest Images