Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104799 articles
Browse latest View live

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Ijumaa ya June 1

$
0
0


Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Ijumaa ya June 1

Kauli ya Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Kuhusu Mwalimu Aliyewanajisi Wanafunzi wa St. Florence

$
0
0
Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Salum Hapi ameliagiza Jeshi la Polisi kufanya uchunguzi wa kina kuhusu tuhuma za mwalimu wa kiume katika Shule ya St Florence ya jijini Dar es Salaam kudaiwa kuwanajisi wanafunzi.

Ameagiza kutafutwa na kukamatwa kwa mwalimu huyo   anayetuhumiwa kufanya vitendo hivyo ambaye tangu Machi 16, 2018 haonekani shuleni hapo.

Tangu jana jioni kumekuwa na taarifa za mwalimu mmoja wa shule hiyo kuwanajisi watoto wanne wa darasa la saba, jambo lililozua taharuki.

Mkuu huyo wa wilaya alipowasili shuleni hapo alipokewa na mwalimu mkuu,  Wilson Mwabuka huku baadhi ya walimu wakitimua mbio na kujifungia wakihofia kupigwa picha.

Akizungumza baada ya kutembelea shule hiyo, Hapi aliwataka wazazi na jamii kuwa watulivu wakati polisi wakiendelea na uchunguzi.

"Walimu, wanafunzi na watumishi wa shule ni binadamu na kila binadamu ana hulka zake ndio maana tunazo sheria kwa kuwa makosa hayawezi kutotokea. Makosa ya walimu yasichanganywe na makosa ya taasisi, tuiache taasisi iendelee kutoa elimu," amesema.

Awali,  Mwabuka alisema tayari Jeshi la Polisi linaendelea na upelelezi hivyo hataweza kuzungumzia jambo hilo.

Amesema tangu Machi16, 2018 mwalimu huyo hajaonekana shuleni.

"Kwa hiyo kwa sababu mimi siyo mwanasheria siwezi kuzungumza, nawaomba wazazi na jamii kusubiri polisi kwa sababu wanaendelea kufanya uchunguzi na wameshatuhoji," amesema.

Bado Lulu ‘anamchanganya’ Bahati kutoka Kenya

$
0
0

Kitendo cha Elizabeth Michael ‘Lulu’ kumuweka msanii Bahati kutokea Kenya hotelini kinyume na makubaliano yao, bado hakimtoki kichwani muimbaji huo wa gospel.

Kwa mujibu wa Bahari mwaka 2016 alikuja Tanzania kwa ajili ya kufanya video ya wimbo wake ‘Maria’ na alipanga kumtumia Lulu kama video vixen, hata hivyo mrembo huyo hakutokea katika kikao walichopanga kingefanyika hotelini.

Kwa sasa Bahati amerudi tena Tanzania kwa ajili ya kufanya kazi na msanii wa WCB, Mbosso, hata hivyo bado anakumbuka alichofanyiwa na Lulu.

“Ilikuwa meeting ya video vixen, kama alinifanyia hivyo je anayempenda inakuwaje?, na mimi nilikuwa nimeweka shilingi kidogo, naongea kwa uchungu,” amesema Bahati hapo jana mara alipowasili Bongo.

Soma Pia; Bahati asimulia kilichomtokea kwa Lulu

Hata hivyo baada ya kutompata Lulu, Bahati alikuja kufanya video hiyo na Jokate Mwegelo.

Kabla ya tukio hilo kutokea, hapo awali muimbaji huyo aliwahi kueleza hisia zake kwa Lulu kupitia vyombo vya habari kwa kueleza kuwa iwapo atampata mrembo huyo atakuwa ametulia kabisa.

Dawa Bora za Nguvu za Kiume na Kukosa Hamu ya Tendo la Ndoa

$
0
0

Baada ya utafiti wa muda mrefu juu ya matatizo ya upungufu wa nguvu za kiume na ukosaji wa hamu ya tendo la ndoa ama kushindwa kurudia tendo kwa haraka sasa

MWASELE HERBAL CLINIC. inakuletea suluhu juu ya matatizo haya kwa kutumia dawa za

FULL POWER .ni dawa asili ya vidonge inayotibu tatizo la upungufu au ukosefu wa nguvu zakiume. dawa hii ina mchanganyiko wa kutosha kuzalisha vichocheo vingi vya hormone za gestrogen ziwemo vitamin B6&B1, vitamini E pamoja madini aina ya zinc vitakufanya kuwa na nguvu na muzunguko mzuri wa damu na kuongeza hamu na uwezo wa kufanya tendo la ndoa zaidi ya hatua nne au zaidi na kuchelewa kufika kileleni zaidi ya dakika 20-30. ZAT 50 inarudisha maumbile ya uume yaani kurefusha na kunenepesha ulefu nchi 3-7, upana cm, 3-4 standard kiafya haijalishi umri wako hata kwa wazee ukitumia maumbile yatabaki kuwa hivyo siku zote . pia tunatibu matatizo mengine kama presha, kisukari , ngiri ,chango la tumbo,tumbo kujaa gesi, kutokupata choo vizuri,miguu kuwaka moto,matatizo ya uzazi, bawasili namagonjwa yazinaa kama kisonono nakaswende.

Tunapatikana DAR ES SALAAM. SHINYANGA NA ZANZIBAR. kwa wakazi wa dar es salaam utaletewa huduma hii popote ulipo . wa mikoani tunawatumia kwanjia ya mabasi .

Wasiliana nasi kwa sim no 0717702227 au 0754568767.DR . SAGUDA nyote mnakaribishwa

Mbunge Ataka Wanaokamatwa Na Na Madini ya Tanzanite Wauawe

$
0
0
Mbunge wa Mtwara Mjini, Maftah Nachuma (CUF), ameitaka serikali kuwaua watu watakaokamatwa na madini ya Tanzanite.

Amesema pamoja na serikali kuzungushia ukuta machimbo ya madini hayo Mirerani, mkoani Arusha njia pekee ya kukabiliana na watoroshaji hao ni kuyaweka katika orodha ya nyara za serikali ili watakaokamatwa nao wauawe.

Nachuma ameyasema hayo jana Mei 31, bungeni jijini Dodoma, alipokuwa akichangia bajeti ya Wizara ya Madini kwa mwaka wa fedha 2018/19.

“Lakini pia serikali inunue mashine za kuchakata madini ya Tanzanite nchini badala ya uchakataji huo kufanyika nje ya nchi ikiwamo India ambako madini hayo yamesababisha ajira laki sita,” alisema.

Katika hatua nyingine, Mbunge wa Viti Maalumu Catherine Magige aliitaka serikali ifanye kila linalowezekana katika kudhibiti utoroshwaji wa madini ya Tanzanite kwa kuwa bado yanatoroshwa nchini ijapokuwa kuna ukuta umejengwa.

Kinyume na ilivyotegemewa na Wengi...Kocha Zidane Ajiuzulu Real Madrid

$
0
0
HISPANIA: Kocha wa Real Madrid, Mfaransa Zinedine Zidane leo Mei 31, 2018 ametangaza kujiuzulu kufundisha klabu hiyo kwa msimu ujao ikiwa ni siku tano baada ya kuipa ubingwa wa UEFA Champions League mara ya 3 mfululizo.

Zidane anaondoka klabuni hapo kwa heshima baada ya kuitumikia kwa miaka miwili. Mfaransa huyo ametangaza kujiuzulu nafasi hiyo katika mkutano wake na waandishi wa habari leo.

Mkongwe huyo wa soka mwenye miaka 45, baada ya kutwaa ubingwa wa Uefa ilikuwa inatabiriwa angeongezewa mkataba hadi mwaka 2020. Hata hivyo awali kulikuwa na presha kubwa kutoka uongozi wa Madrid kutokana na kutofanya vyema kwenye La Liga msimu huu ulioisha.

Makocha Arsene Wenger na Antonio Conte ni miongoni mwa wanaotajwa kumrithi Zidane, huku Conte akipewa nafasi kubwa Zaidi.

Zidane alimrithi kocha Rafael Banitez Januari 2016 na msimu huo huo aliipa taji la Ligi ya Mabingwa timu hiyo.

Zidane ameitumikia Madrid tangu (2016-18)
UEFA Champions League🏆🏆🏆
UEFA Super Cup🏆🏆
Club World Cup🏆🏆
Spanish Super Cup🏆
Liga🏆

Siri Gari Mpya ya Diamond Yafichuka

$
0
0
DAR ES SALAAM: Lile gari jipya la staa wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond’ aina ya Land Cruiser, ambalo limedaiwa ni toleo jipya la 2018 kuzua gumzo mitandaoni, siri imefichuka kuwa si jipya bali ni la zamani lakini limebadilishwa muundo na Kampuni ya TTTR Auto Up Grades. Co. Ltd iliyopo Mikocheni B jijini Dar.



Chanzo makini kililieleza Amani kuwa tangu awali mzazi mwenziye na mwanamuziki huyo, Zarinah Hassan ‘Zari The Boss Lady’ alipoanika ndinga lake jipya ilionekana wazi kwamba msanii huyo aliamua kulipiza kisasi kwa kutupia Land Cruiser hilo.

Diamond kwa mara ya kwanza alianika gari hilo kwenye ukurasa wake wa Instagram ambapo watu wengi walikuwa wakimpongeza kwa hatua hiyo ya kununua gari hilo jipya la mwaka 2018.

SIRI YAFICHUKA

Baada ya Diamond kuanika gari hilo, Amani lilidodosa mmoja wa wamiliki wa kampuni iliyomtengenezea gari hilo ambaye alikiri kuwa ni la zamani lakini wamelifanyia matengenezo na kuonekana jipya huku akigoma kutaja gharama yake.


“Sisi ndiyo tumelitengeneza hilo gari na kulibadilisha kama kutoka katika gari la zamani lakini hatuna mamlaka ya kusema ni kiasi gani mteja wetu katumia kwenye matengenezo hayo mpaka mwenyewe aruhusu,” alisema mmiliki huyo aliyeomba hifadhi ya jina.


Kumekuwa na ushindani mkubwa kati ya timu Zari na timu Diamond baada ya msanii huyo kulionyesha gari hilo kwa mara ya kwanza kwenye mitandao ya kijamii na kuzua mjadala huku kila mtu akimsifia mtu wake.

Stori: Imelda Mtema, Amani

Makanga 3 Power; Dawa Bora Nguvu Za Kiume

$
0
0

Kutibu nguvu za kiume dakika(10) na kupona muda wa siku tatu tuu. Kuimarisha misuli ya uume uliolegea, pia ipo Dawa ya kurefusha uume mfupi inchi NNE hadi saba na kunenepesha uume mfupi sentimita NNE.

Tiba ya kudumu kutibu maumivu ya mgongo,kiuno, tumbo kuunguruma na kujaa gesi, kupata choo vizuri, na kutibu uzazi, kutibu busha bila operesheni, kisukari, presha ,miguu kuuma, uzazi, fangas sugu, vidonda vya tumbo.

Ni docta bingwa wa kutibu magonjwa sugu, kutoa ndagu za utajiri kwa kutumia Pete, kazi ,cheni, mikufu maalumu ya bahati, una kesi umedhulumiwa Mali au pesa? Zitarudi muda wa Masaa matatu tuu.

Onana na Dr shilindes shida zako zote zitakwisha, anatoa Dawa za utajiri kwa wafanyakazi, wakulima, na wafugaji, wafanyabiashara na wachimba madini kwa kutumia pete, kazi kwa yeyote anaetaka kuwa na pesa nyingi.

Pia anaboresha akili kwa wanafunzi darasani, masomo na kufaulu mitihani pia kushinda bahati nasibu yeyote.

Pia tunatoa Dawa kumrudisha Mume, mke, mpenzi, hawara, kwa muda wa SAA moja tuu, na kuomba msamaha kwa kukupigia magoti na yeyote yule, unaemtaka kimapenzi au kuoana, utampata na kumfunga asitoke nje ya ndoa daima na kutekeleza shida zako zote. Kupunguza unene, kupunguza matiti makubwa, tumbo na nyama uzembe muda wa siku sita unapata saizi uipendayo.

Kutoa makovu mwilini, chunusi, upele na mabaka, pia tunayo Dawa ya kuongeza hipsi, makalio, mguu wa bia na kupata shepu safi kwa muda wa siku saba tuu.

Wa mikoani mtapata huduma popote mlipo.
Tupo dar es salam mbagala rangi tatu.

Mawasiliano simu namba: 0784 460 348. Au 0659 103 360.


PICHA: Kinana Akabidhi Ofisi Kwa Katibu Mpya wa CCM

$
0
0
Katibu Mkuu mstaafu wa CCM, Abdulrahman Kinana leo Alhamisi Mei 31, 2018 amemkabidhi ofisi mrithi wake, Dk Bashiru Ally katika ofisi ndogo za chama hicho tawala, Lumumba jijini Dar es Salaam.

Baada ya makabidhiano hayo, wawili hao waliingia katika kikao cha ndani na wafanyakazi wa chama hicho.

Dk Bashiru anakuwa Katibu Mkuu wa nane wa CCM baada ya kujiuzulu kwa Kinana aliyemuandikia barua mwenyekiti wa chama hicho, Rais John Magufuli aridhie ombi lake hilo.

Mei 29, 2018 Halmashauri Kuu, ambayo ni chombo cha pili kwa ukubwa cha CCM na ambayo ilikutana kwa siku mbili Ikulu jijini Dar es Salaam, ilimpitisha Dk Bashiru ambaye aliongoza kamati iliyohakiki mali za chama hicho kwa miezi mitano kuwa katibu mkuu mpya wa chama hicho.

Habari Njema..Mo Salah Rasmi Kushiriki Kombe la Dunia Urusi

$
0
0

Uongozi wa timu ya Taifa ya Misri umethibitisha kuwa mshambuliaji wao hatari amabye anacheza kwenye klabu ya Liverpool, Mohamed Salah atashiriki kwenye michuano ya Kombe la Dunia nchini Urusi itakayoanaza kufanyika Juni mwaka huu.



Salah ambaye aliumia bega la kushoto wakati wa fainali ya klabu bingwa ya Ulaya Jumamosi iliyopita baada ya kuchezewa vibaya na Sergio Ramos na kutoka nje yauwanja dakika ya 24.


Sergio Ramos akimchezea rafu mbaya Mohamed Salah

Kutokana na majeraha hayo yalileta wasiwasi kwa mashabiki na kuhusu kushiriki kwake kwenye michuano hiyo mikuba ya dunia.

Wakati huo huo Mwanasheria wa Misri, Bassam Wahba amesema amepeleka kesi kwenye shirikisho la soka duniani (FIFA) kumshtaki Ramos atoe kiasi cha Euro billion moja kwa kumuumiza makusudi Salah.

Sasha 'Nitaendelea Kupiga Picha za Nusu Utupu Baada ya Kupumzika Kwa Muda'

$
0
0
LICHA ya Naibu Waziri wa Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo, Juliana Shonza kuwafungia na kuwaita na kuwakanya wasanii ambao wamekuwa wakijianika nusu utupu, muuza nyago kwenye video mbalimbali za wanamuziki Bongo, Sasha Kassim amefunguka kuendelea kupiga picha za nusu utupu.

Akizungumza na Gazeti la Amani, Sasha alisema kuwa anajiandaa kupiga picha nyingine ambazo kama ni nguo za ndani zitaonekana nadhifu na zenye kuvutia na pia zitapungua ‘ukali’.

 “Nilipotea kwa sababu niliibiwa akaunti yangu ya Instagram, si unajua ilikuwa na picha nyingi sana ila sasa hivi najiandaa kupiga picha nyingine mpya zitakuwa zikinionyesha sehemu zangu za mwili lakini zitakuwa zenye kujistiri kidogo,” alisema Sasha

Stori: Imelda Mtema

Bia iliyotengenezwa Kwa Kutumia Majitaka

$
0
0
Katika juhudi za kuongeza ufahamu juu ya uwezekano wa kuyabadilisha Majitaka kuwa maji salama kampuni moja inayozalisha bia jijini Stockholm nchini Swaeden imetengeneza bia iliyobatizwa jina la PU: REST kwa kutumia Majitaka yaliyotibiwa (recycled sewage water).

Kampuni hiyo ambayo katika uzalishaji wa bia hiyo wameshirikiana na Taasisi ya Utafiti wa Mazingira nchini Sweden imedhamiria kupitia kinywaji hicho kuwashawishi wakazi wa nchi hiyo kuwa ‘Maji taka yaliyotibiwa (recycled sewage water)’ ni maji safi na salama kama yanayotoka kwenye mabomba.

Kwa mujibu wa Taasisi ya Utafiti wa Mazingira nchini Sweden wamesema kuwa changamoto ya watu kutoyaamini majitaka yaliyotibiwa sio ya kiufundi bali ni changamoto ya kisaikolojia na ndio maana wametengeneza bia ili kuwashawishi watu kuyatumia Majitaka yaliyotibiwa.

Kwa sasa PU:REST bia inapatikana pekee katika mgahawa wa New Camegie Brewery’s jijini Stockholm na July 2 itauzwa kwenye migahawa na kwenye matamasha yote nchini Sweden.

Katibu Mkuu Mpya CCM: Nitakuwa Mtendaji Zaidi Kuliko Kufanya Siasa za Majukwaani

$
0
0
Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Dk. Bashiru Ally amesema hataonekana katika majukwaa ya siasa kwa sababu yeye ameteuliwa kuwa mtendaji  na si mwanasiasa wa chama hicho hivyo atatekeleza yale tu yanayoamriwa katika vikao vya Halmashauri Kuu.

Dk. Bashiru amesema hayo jana alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari baada ya kukabidhiwa ofisi na kutambulishwa kwa watendaji wa chama hicho, na Katibu Mkuu mstaafu, Abdulrhaman Kinana katika Ofisi kuu za chama hicho Lumumba jijini Dar es Salaam.

“Mimi nimeteuliwa kuwa mtendaji wa chama kazi niliyopewa si ya jukwaaani, ni marufuku kwa watendaji kujihusisha na siasa hivyo watu wasitarajie kuniona katika majukwaa.

“Jukumu langu kubwa ni kutekeleza maazimio ya vikao, kutoa taarifa pamoja na kusimamia maagizo ya chama haya ni masuala ya mezani si ya jukwaani wapo waliopewa dhamana ya kukaa katika majukwaa,” alisema Dk. Bashiru.

Aidha, alisema atalipa kipaumbele suala la serikali kuhamia Dodoma ambapo katika miaka iliyopita walishindwa, hivyo ataanzia hapo na kuhakikisha wanafanikiwa na ataendelea pale walipoanzia.

Binti wa Kiganda Aeleza Sababu za Kujiteka

$
0
0
Nakusogezea hii kuhusu Jeshi la Polisi ambapo limemkamata mtoto wa miaka 15 baada ya kufeki kutekwa na kubakwa ili ajipatie fedha kwa baba yake nchini Uganda.

Msichana huyo alimpigia simu baba yake David Kazibwe, akimwambia kuwa ametekwa na wanaume wanne ambao wanahitaji Shilingi Milioni 30 za kiganda ambazo ni sawa na zaidi ya Milioni 18 za kitanzania ili aachiwe huru jumamosi iliyopita.

Afisa wa kituo cha polisi cha Bujuuko Emmy Nuwagira amesema kuwa Kazibwe aliwaarifu polisi baada ya mtoto wake huyo kurudi nyumbani na baada ya kumuuliza alikuwa wapi alidai kuwa amefanikiwa kuwatoroka watekaji.

Kazibwe aliwaambia polisi pia baada ya kurudi nyumbani alikuwa akilalamika kuwa anasikia maumivu makali  yaliyosababishwa na kubakwa na kundi hilo la wabakaji.

Baada ya kumpeleka kituo cha polisi kwa ajili ya kuandika maelezo na punde polisi kuanza kumhoji waligundua kuwa maelezo yake yanakinzana na ndipo walipoamua kumpeleka katika kituo cha afya cha Nyange ili akafanyiwe vipimo.

Kwa mujibu wa ripoti ya daktari ni kuwa mtoto huyo ni bikira yaani hajawahi kufanya tendo la ndoa katika maisha yake yote  na wala  hakuwa na majeraha yoyote kwenye mwili wake.

Hata hivyo mtoto huyo alikubali baadae mwenyewe kuwa alifeki kutekwa ili apate fedha kutoka kwa baba yake ili aanzishe biashara yake.

“Nilikuwa nimechoka kukaa nyumbani hivyo nilikuwa nataka baba anipe hela nikaanzishe maisha yangu mapya sehemu nyingine” alisema mtoto huyo.

Kwa sasa mtoto huyo anashikiliwa katika kituo cha polisi cha Bujuuko kwa kutoa taarifa za uongo na kufeki kutekwa.

Matuta ya Barabarani Rukwa na Tunduma yawa Kero, Waziri ataka yaondolewe

$
0
0

Moja ya mbinu za kupunguza Mwendokasi kwa madereva wanaoendesha vyombo vya moto barabarani ni kuweka 'humps' maarufu kama matuta kwa wengi. Lakini matuta hayo yanapozidi inakuwa kero

Barabara inayounganisha Wilaya ya Sumbawanga mkoani Rukwa na Tunduma iliyopo mkoani Songwe yenye urefu wa Kilometa 220 ina idadi ya matuta takribani 115, karibia wastani wa tuta moja kila baada ya Kilometa 1

Katika barabara hiyo Kijiji cha Tamasenga kilichopo katika Manispaa ya Sumbawanga peke yake kina idadi ya matuta 10.

Wadau wengi akiwemo Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Mhandisi Atashasta Nditiye wameonyeshwa kukerwa na matuta hayo na kutaka yaondolewe

Naibu Waziri alisema kuweka matuta kunachangia kuharibu miundombinu ya barabara, pamoja na magari hasa pale magari yapokuwa yakipunguza mwendo ili kupita katika matuta hayo. Mkuu wa wilaya ya Sumbawanga, Dk. Halfan Haule amewahi kunukuliwa kuwa wanatumia muda mrefu wa saa 5 hadi 7 kutoka Sumbawanga hadi Tunduma

Nini mtazamo au maoni yako kuhusu utumiaji huu matuta mengi barabarani ili kupunguza Mwendokasi?

Pata Tiba ya Tatizo la Nguvu Za Kiume, Inasaidia Kukufanya Urudie Mara 5 na kuchelewa kwa Dakika 20

$
0
0
TATIZO LA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME NA MAUMBILE MADOGO LINATIBIKA.Baada ya utafiti wa mda mrefu juu ya matatizo ya upungufu wa nguvu za kiume na ukosaji wa hamu ya tendo la ndoa ama kushindwa kurudia tendo kwa haraka DR Magise imekuletea tiba ya matatizo hayo kwa kutumia dawa za:

GUMBA POWER:Ni dawa asili ya vidonge inayotibu tatizo la upungufu au ukosefu wa nguvu za kiume,dawa hii inamchanganyiko wakutosha wenyekuzalisha vichocheo vingi vya Hemone za Gestrogen vikiwemo vitamin B6&B1,vitamini E,pamoja na madini aina ya zinc vitakufanya kuwa na nguvu na mzunguko mzuri wa damu na kuongeza hamu na uwezo wa kufanya tendo la ndoa zaidi ya hatua nne au zaidi,na kuchelewa kufika kileleni zaidi dakka 20-30.

NTINJE:Inarutubisha maumbile ya uume yani kurefusha na kunenepesha nchi 4-7 upana cm3-4 standard kiafya haijalishi umri wako hata kwa wazee ukiitumia maumbile yako yatabaki kuwa hivyo siku zote,Pia tunatibu Presha,kisukari siku7,ngiri,chango la tumbo tumbo kujaa gesi,kutopata choo vizuri

 TUPO TZ DAR ES SALAAM   MBAGALA RANGI TATU.HUDUMA HII UTALETEWA POPOTE ULIPO .WASILIANA NAMI 0754741788, 0715741788, 0783741788

-DR MAGESA

Kutana na Baba Mwenye Nyumba Asiyedai Kodi, Anayewahudumia Wapangaji

$
0
0
Katika Instagram ya Millardayo jana alikuwekea short story ya Baba mwenye nyumba asiyedai kodi na anawahudumia wapangaji wake sasa leo May 31, 2018  nakusogezea full story juu ya Baba mwenye nyumba mmoja nchini Uganda anayeitwa Kenneth Mubiru amewashangaza wengi jinsi ambavyo anaishi na wapangaji wake.

Mpangaji mmoja wa Mubiru anasimulia kuwa bwana huyo hajawahi kuwafuata akidai kodi ya nyumba bali wao wapangaji ndio huwa wanampigia simu na kumuomba aende akachukue fedha hizo.

“Na ukimpigia simu anaweza kuja kuchukua fedha hizo mwezi unaofata na tena mpaka umtishie kwamba utazitumia fedha na cha ajabu atakwambia tumia kidogo tu unayoweza kurudisha” alisema mpangaji huyo.

Anaendelea kusimulia kuwa kuna kipindi aliwahi kukaa miezi mitatu hajalipa kodi na alitegemea Mubiru kumpigia simu akimdai kodi lakini mambo yalikuwa tofauti. Mubiru alinisubiria mpaka nilipopata fedha ndipo nikalipa na alinishukuru sana badala ya kunilalamikia kuwa nimechelewesha kodi.

Mpangaji huyo anasema kuwa baba mwenye nyumba ana mashamba hivyo huwaletea mazao kila mpangaji wake bure kabisa na kama kuna kitu kimeharibika kwenye nyumba basi atakirekebisha bila kulalamika.

Aidha Mubiru akijua mpangaji wake anaumwa basi atakuwa anamjulia hali yake kila siku na atakuwa akimpelekea chakula mpaka atakapojisikia vizuri.

Hata hivyo Mubiru hapendi mambo yasiyokuwa na maadili katika nyumba yake ijapokuwa hajawapangia sheria za namna ya kuishi katika nyumba yake.

Unaambiwa hivi wapangaji huondoka kwenye nyumba ya bwana Mubiru wakiwa wanahamia kwenye nyumba zao na si vinginevyo.

Nahitaji Ushauri, Mke Amebadilika Sana Tangu Mimi Niondoke..

$
0
0
Wadau hamjambo,

Naomba msaada, niko South Africa since last week, niliondoka Tz mpaka South Africa baada ya kupata mchongo kwa rafiki yangu ambaye alinitafutia mchongo wa kazi.

Namshukuru Mungu nilifika salama na maisha yanaendelea vyema kabisa.
suala kubwa lililopo ni kuhusu wife wangu, kipindi naondoka nilimshirikisha lakini alionekana kuwa na hasira sana juu ya uamuzi wangu wakuja South,

Nilijaribu sana kumsihi yakuwa nakuja kuangalia namna mambo au upepo ulivyo kisha nitageuza lakini alishindwa kunielewepa kabisa na kuwa mtu mwenye hasira kiasi ambacho hata unyumba alininyima.

Nikafikiri sana namna gani yakufanya, sikuona namna, maana nilikuwa tayari nishakatiwa ticket ya kuja na kurudi(Go and Return) yaani kama mambo yakiwa mabaya niko huru kurudi. Basi kiukweli nilichukua uamuzi mgumu nikafwatilia kila kitu na safari ikaiva yakuja South, nikaondoka na kufika salama.

Lakini kabla sijaondoka wife alinitumia sms na kuniambia nisimshirikishe lolote wala kumpigia wala kuhangaika na yeye.

Sasa tangu nimefika nimejaribu kumtumia sms, kutaka kujua hali ya maendeleo na nilimwomba hata akaunt ya bank ili nimtumie pesa kwa ajili ya matumizi, lakini wadau huyu mwanamke alinitukana na kunitumia sms za ajabu sana, oooh, wewe mwanaume gani, tena kwa taarifa yako nimeshapata baba wa mtoto na maneno mengine mengi ya ajabu.

Kweli najisikia vibaya sana na majuto kuwa na mwanamke mwenye hasira na asiye na kipimo cha maneno kwangu kwa heshima. Japo alinitukana vya kutosha lakini sijaacha kumtumia sms za kutaka kujua hali yake na mtoto, ila cha ajabu hajibu chochote.

Niko njiapanda, nishaurini nifanye nini, kwa wadau naombeni ushauri wenye hekima ili niuchukue maana niko mbali na ninahisi kuumia sana.

Please ushauri sio kejeli.

Thanks wadau.

Nawasilisha

Hapa kuna Mbuzi na Kuku Lazima Tuheshimiane- Steve Nyerere

$
0
0
Msanii wa filamu bongo ambaye pia ni mchekeshaji maarufu Steve Nyerere, ameingilia kati ugomvi baina ya Duma na Gabo Zigamba huku akimtaka Duma kuachana na masuala hayo kwa kuwa anaetaka kushindana naye yupo juu yake zaidi kwa kila kitu.


Steve ametoa kauli hiyo wakati akizungumza kwenye kipindi cha eNewz kutoka EATV huku akionekana kukerwa na kitendo hicho ambacho kimedumu kwa muda mrefu kwa wawili hao na kupelekea Steve kuwafananisha na wanyama aina ya mbuzi na kuku kutokana na tabia zao.

"Hapa katikati kuna mbuzi na kuku, lazima tuheshimiane kutokana na urefu na hata jinsi mbuzi anapochinjwa kilo zake huwa kubwa na kilo za kuku ni ndogo. Kwa hiyo lazima waheshimiane hata kwa kilo, ukuaji. Wasifikilie kwamba ugomvi wanapokuwa wanagombana ulaya basi nasi Afrika tufanye ili tuuze sokoni maana wengine wanasema kugombana ni kiki, na kataa hilo muda mwingine ni kudhalilishana tu", amesema Steve.

Pamoja na hayo, Steve Nyerere ameendelea kwa kusema "heshima sio lazima uwe umetokanayo nyumbani kwenu hata unapokuwa heshima unakuwa nayo ili upate kumuheshimu kila mmoja upate connection na maisha ya kesho na kesho kutwa".

UKUTA Waongeza Mapato ya Tanzanite Maradufu kwa Miezi Mitatu

$
0
0
Mikakati ya serikali kudhibiti utoroshwaji wa madini ya tanzanite imefanikisha mapato ya madini hayo kuongezeka, ikielezwa kuwa mapato ya miezi mitatu (Januari hadi Machi, mwaka huu) yamezidi ya miaka mitatu iliyopita.

Imeelezwa kuwa mafanikio hayo ni matokeo ya uamuzi wa Rais John Magufuli alioutoa Septemba 20, mwaka jana, wa kujengwa ukuta kuzunguka eneo la migodi ya tanzanite iliyoko Mirerani, Simanjiro mkoani Manyara.

Agizo hilo la Rais lilitekelezwa na Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) kwa kujenga ukuta huo kuanzia Novemba Mosi hadi Februari 15, mwaka huu.

Akiwasilisha hotuba bungeni jijini Dodoma jana kuhusu makadirio ya wizara yake kwa mwaka ujao wa fedha, Wizara ya Madini, Angellah Kairuki, alisema mafanikio makubwa yamepatikana kutokana na udhibiti wa tanzanite.

Alisema katika kipindi cha miezi mitatu kuanzia Januari hadi Machi, mwaka huu, wizara yake imekusanya mrabaha wa Sh. milioni 714.6.

Kairuki alibainisha kuwa kati yake, Sh. milioni 614.6 zinatokana na makusanyo kutoka kwa wachimbaji wadogo.

"Kiasi hicho kilichokusanywa kinazidi jumla ya makusanyo ya mrabaha wa miaka mitatu iliyopita kutoka kwa wachimbaji wadogo," alisema na kueleza zaidi:

"Pia Bunge lako tukufu litapendezwa kufahamu kwamba katika mwaka 2015 tulikusanya mrabaha wa Sh. milioni 166.8, mwaka 2016 Sh. milioni 71.8 na mwaka 2017, Sh. milioni 147.1 kutoka kwa wachimbaji wadogo."

Waziri huyo pia alisema wizara inaendelea kufanya ukaguzi wa uzalishaji wa madini kwenye migodi mbalimbali kuhakikisha inapata takwimu sahihi za madini yanayozalishwa na kuuzwa ndani na nje ya nchi.

Alisema ukaguzi huo hususan kwenye migodi na mitambo ya uchenjuaji, umekuwa ukifanyika kwa kushirikiana na vyombo vya ulinzi na usalama.

"Kutokana na jitihada hizo, makusanyo ya mrabaha yameongezeka. Hadi kufikia Machi mwaka huu, Ofisi ya Madini iliyopo Chunya ilikuwa imekusanya Sh. milioni 718.6 na Ofisi ya Madini Mwanza ilikuwa imekusanya Sh. bilioni 9.8 ikilinganishwa na Sh. milioni 416.9 na Sh. bilioni 6.1 zilizokusanywa na ofisi hizo kwa mwaka wa fedha wa 2016/17 kwa mfuatano huo," alisema.
Viewing all 104799 articles
Browse latest View live




Latest Images