Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104795 articles
Browse latest View live

Waziri wa Elimu Profesa Ndalichako alivyomwaga machozi msiba Maria na Consolata

$
0
0
Waziri wa Elimu Profesa Ndalichako alivyomwaga machozi msiba Maria na Consolata
Miili ya mapacha Maria na Consolata Mwakikuti (20) waliofariki dunia Jumamosi iliyopita katika Hospitali ya Mkoa wa Iringa, imeagwa katika viwanja vya Chuo Kikuu cha Ruaha (RUCU) kabla ya kuzikwa katika makaburi ya viongozi wa dini yaliyopo Tosamaganga mkoani humo leo Jumatano, Juni 6, 2018.

Maria na Consolata ambao enzi za uhai wao walikataa kutenganishwa, watazikwa kwenye jeneza moja litakalokuwa na misalaba miwili.

Familia za baba na mama wa mapacha hao kutoka Tukuyu, Mbeya na Bukoba, Kagera, waliokuwa walezi wa mapacha hao, masista wa Consolata wa Iringa, na waombolezaji wengine,  wameungana katika kuwasindikiza mapacha hao katika safari yao ya mwisho duniani.

Pia viongozi mbalimbali wa kimkoa na wa kitaifa wameungana na waombolezaji  kwa ajili ya kutoa heshima za mwisho kwa pacha hao, Maria na Consolata Mwakikuti.

Miongoni mwa waliofika ni pamoja na Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Joyce Ndalichako na mkuu wa wilaya ya Mufindi Jamhuri Willium.


Wafugaji Holela wa Mifugo Kutozwa Adhabu ya Milioni Moja na Kifungo Miezi Sita Jela

$
0
0
Wafugaji Holela wa Mifugo Kutozwa Adhabu ya Milioni Moja na Kifungo Miezi Sita Jela
Ufugaji mifugo holela ni kosa la jinai katika Halmashauri ya Wilaya ya Ilemela ambapo kima cha chini cha adhabu iwapo utakutwa na kosa hilo ni shilingi milioni moja au kutumikia kifungo cha miezi sita jela.

Hayo yamesemwa katika Kilele cha Maadhimisho ya Siku ya Mazingira Duniani na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela John Wanga  kwa niaba ya Mgeni Rasmi Mkuu wa Mkoa wa Mwanza John Mongella, ambapo kiwilaya yamefanyika Kata ya Kawekamo na kuwataka wananchi kusimamia na kuitunza miti iliyopandwa kutoka eneo la Kona ya Malaika mpaka Misheni Makongoro.

"Tumepanda miti ya miembe pembezoni mwa barabara kuu ya Uwanja wa ndege naomba wananchi wazingatie utunzaji wa mazingira, ukihitaji kukata mti lazima uwe na kibari. Ujenzi holela haurusiwi kwani ni chanzo cha uharibifu wa mazingira pia lazima upate kibari kabla hujajenga kutoka Idara ya mpango Mji," alisema Wanga.

Wanga alieleza kaulimbiu ya Maadhimisho hayo kuwa  ni "Mkaa ni gharama tumia nishati mbadala" ambapo amewaomba wananchi kutumia nishati ya gesi kwa ajili ya matumizi ya nyumbani badala ya matumizi ya mkaa kwani yana gharama kubwa.

Kwa upande wake Afisa Mazingira katika Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela Simon Nzagi alisema kuwa lengo la kupanda miti ya miembe ni kuweka kivuli pembezoni mwa barabara na  miti hiyo inatoa matunda pia ni pendekezo la Mkuu wa Mkoa, ambapo lengo ni upandaji wa miti 340 na zoezi hilo litakuwa endelevu.

Aidha Nzagi alitoa wito kwa wananchi kuepuka watu wasikate miti kwa ajili ya utengenezaji wa mkaa kwani wanasababisha ukame katika nchi sambamba na vifo vya wanyama kwani maji na vyakula vitapungua.

Hiki Hapa Kinachosababisha Mapacha Kuungana

$
0
0
Hiki Hapa Kinachosababisha Mapacha Kuungana
Imeelezwa kuwa hali ya watoto kuungana hutokea wakati wa mgawanyiko wa seli ingawa si mara zote na chanzo kikuu ni makosa ya taarifa za vinasaba katika mfumo wa uzazi.

Hayo yameelezwa na Dk. Festo Dugange wakati akizungumza na eatv.tv katika mahojiano maalum ambapo amesema kuwa makosa ya taarifa za ‘DNA’ hushindwa kugawanya yai na ndipo hutokea mapacha hao.

"Mbegu ya baba ikikutana na yai la mama ili kutengeneza mtoto, huwa kunatokea mgawanyiko wa seli mara 18 sasa iwapo seli hizo hazikugawanyika na kuachana ikiwa mimba hiyo ni ya watoto pacha basi huzaliwa wakiwa wameungana baadhi ya viungo vyao,” amesema Dk. Dugange.

Ameongeza kuwa  hali hiyo inapotokea wakati mwingine mtoto mmoja hukutwa akiwa amekamilika viungo vyote huku mwenzake akiwa na kasoro kadhaa.

Wamiliki wa Magari Wapewa Onyo Kali na Jeshi la Polisi

$
0
0
Wamiliki wa Magari Wapewa Onyo Kali na Jeshi la Polisi
Kamanda wa Kikosi cha Usalama Barabarani nchini Fortunatus Muslim amefunguka na kuwataka wananchi kuacha tabia ya kuwapa magari yao madereva wasiokuwa na leseni kwani endapo watabainika watakuwa wamejiingiza katika kosa la uvunjifu wa sheria za barabarani.


Muslim ametoa kauli hiyo wakati alipokuwa anazungumza kwenye kipindi cha East Africa Drive kilichorushwa jana jioni Juni 05, 2018 kutoka East Africa Radio baada ya kuwepo kadhia hiyo kwa watu wengi kupenda kuendesha magari ya watu bila ya kuwa na leseni inayowaruhusu kufanya hivyo huku wengine kutumia kigezo hicho kutenda uhalifu.

"Ni kosa kumpa gari dereva kuendesha wakati unajua kwamba hana leseni na hili kosa huwa linakuja mpaka kwa mmiliki wa gari kwa hiyo wote wawili watakuwa watuhumiwa kwaajili ya mujibu wa sheria", amesema Kamanda Muslim.

Rais Magufuli Aguswa na Msiba wa Watu 10 Ajali ya Treni Atuma Salamu za Rambirambi

$
0
0
Rais Magufuli Aguswa na Msiba wa Watu 10 Ajali ya Treni Atuma Salamu za Rambirambi
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli ametuma salam za rambirambi kufuatia vifo vya watu 10 baada ya basi walilokuwa wanasafiria kugonga Treni la mizigo Mkoani Kigoma.

Soma taarifa kamili:

Wasiliana na Dr Mabula Anatibu Upungufu wa Nguvu za Kiume, Busha na Matatizo ya Maumbile Madogo kwa Mwanaume

$
0
0


TUNATIBU NA KUPONESHA KABISA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME UUME MDOGO BUSHA BILA KUPASUA PRESHA VIDONDA VYA TUMBO
Asilimia kubwa ya wanadamu wanasumbuliwa na magonjwa mbalimbali na wapo waliongahika sehemu mbalimbali bira MAFANIKIO MABULA CLINIC ni kituo cha tiba asilia kilichopo mbagara zakhemu njia kuu ya JESHINI JE HUNAUPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME AU UUME WAKO MDOGO NA MWEMBAMBA?

MAPRO PAWER NO 2 ndio Tiba kwa sasa utibu matatizo matatu kwa pamoja 1hitakufanya uchelewe kufika kilekeni dikika 15-20 kwa tendo la kwanza 2 uhimalisha misuli iliyoregea na kusinyaa hasa kwa wale walio hasirika na upigaji punyeto 3 itakufanya upate amu ya kurudia tendo zaidi ya Mara tatu

KWA NINI UJIONE MPWEKE PALE UKUTANAPO NA MPENZI AU MKE WAKO kisa unawai kukojoa au unakomea bao moja tu na huku dawa zipo MAKAKANUA mix ni dawa iliyochanganywa na miti Shamba 9 na Kuwa na uwezo wa kuongeza uume saizi upendayo inchi 5-8 Kwa Urefu na unene sentimita 1-5 dawa hizi hazina madhara yoyote kwa mtumiaji ata wazee wenye umri mkubwa wanapona? zipo dawa za mvuto wa mpenzi mme au mke Kwa masaa matatu tu na kukupigia simu yeye mwenyewe mvuto wa biashara kutengeneza mwonekano mzuri wa mwili kwa wanawake yani shepu tunatibu ngiri miguu mgongo na kiuno kuumwa kupunguza kitambi minyama uzembe matiti na mwili mkubwa

TIBA NA USHAULI MUONE DR MABULA AU PIGA SIMU NO 0752348593 UDUMA ZANGU UTAZIPATA POPOTE ULIPO KAMA UWEZI KUFIKA OFISINI

Waziri Ndalichako : “Maria na Consolata ni Mashujaa wa Taifa”

$
0
0
Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Joyce Ndalichako ameongoza waombolezaji  kutoa heshima za mwisho kwa Mapacha walioungana Maria na Consolata mkoani Iringa amabapo alizungumza na waandishi wa habari na kusema mapacha hao  Maria na Consolata  ni  mashujaa wa Taifa  na kwamba wameliacha taifa katika simanzi nzito.

"Mara ya mwisho niliwaona pale Mwaisela wakiwa wodi ya wagonjwa mahututi, inaniumiza mno lakini mapenzi ya Mungu yatimizwe," amesema.

Amesema wizara hiyo imepoteza watu muhimu waliokuwa wakipigania elimu bila kujali ulemavu na namna walivyo.

Mange Kimambi Aichana Familia ya Diamond Kwa Kumdhalilisha Hamisa Mobetto Mwezi Mtukufu

$
0
0

From @mangekimambi_ - Unapoona familia ya kiislam hata mwezi wa Ramadhan hawana uwoga nao. Yani hata mwezi wa Ramadhan bado wanaendelea na visa, matusi, kejeli, chuki, husda, fitna, roho mbaya, dharau basi mtu inabidi uelewe unadili na watu wa aina gani.
.
.
Seriously mwezi wa Ramadhan wale bado wanachamba na kumdhalilisha mwanamke mwenzao. Yani hawana hofu ya Mungu hata mwezi huu ambao hata sisi tulioshindikana tumekituliza..Yani nashindwa hata kuwasema the way natamani niwaseme
.
.
Kutwa kuwapambanisha watoto wa wenzao huyu anajua kupika, huyu hajui, huyu mchafu, huyu msafi wao wanajua kupika? Wao wasafi? Mbona wao hawanyanyaswi au kudhalilishwa na ndugu za waume zao? Ila Mungu ni mkali sana @mama_mobetto siku hizi zilizobaki za mwezi mtukufu kazana na dua, mlilie Allah siku hizi zilizobaki. Wakabidhi kwake!! Usiwaombeee mabaya ila wakabidhi tu. Hizi dharau zote kwa wanawake wenzao sababu tu Allah kamwonyesha Neema ndugu yao?? Allah asingempa mafanikio ndugu yao je wangekuwa na dharau hizi? Hawa wanamletea nuksi ndugu yao. .
.
Pia Mungu keshaanza kujibu, Esma yuko busy na mahusiano ya kakake alafu mume wake laki moja hana mpaka anaweka passport rehani. Hizo zote ni fimbo Mungu anawachapa. Imagine kutwa mtoto wa mwenzenu yuko mdomoni alafu waume zenu laki hawana huo muda si mngeutumia kwa waume zenu ili wasiathirike? Kama nilivyosema nifimbo ya Mungu. Wao si wamemdhalilisha Hamisa sasa wao wanadhalilika mara mbili ya Hamisa.
.
.
Ila wale jamani sijui waislamu wa wapi wale. Yani hawana woga na mwezi mtukufu. Wengine hata kuandika shenzi hatuwezi ila wale wakavuuuuuuuu tena kwenye macamera, yani hawajali. Ndio sisi wote ni watenda dhambi so we cant judge each other ila muislam ambae hata mwezi mtukufu anaendelea na matendo yake ya kila siku huyo sio mzima.

Maria na Consolata Watakumbukwa kwa Haya

$
0
0
Maria na Consolata Watakumbukwa kwa Haya
Watoto mapacha Maria na Consolata Mwakikuti (20) waliofariki mwishoni mwa wiki iliyoisha wataendelea kukumbukwa na mamia ya walimwengu nchini kwa kuweza kuyakubali maumbile yao waliyokuwa nayo na kujikubali mpaka kufikia hatua ya kufariki wakiwa katika mwili mmoja.


Miaka 22 iliyopita, familia ya Alfred Mwakiuki na Naomi Mshumbusi ilifanikiwa kupata watoto mapacha ambao ni Maria na Consolata lakini hawakuwa pacha wa kawaida kama jamii ya kitanzania ilivyozoea kuziona au kujaliwa nazo kwa kuwa wao walikuwa wameungana na kwa wakati huo hapakuwepo na uwezekano wa kuwatenganisha.

Akizungumza wakati wa kutoa salamu za kuaga miili ya mapacha hao Askofu Jimbo Katoliki Njombe, Alfred Maluma amesema vifo vya pacha hao vinafaa kutumiwa na watanzania kukumbushana wajibu wao kwa watu wenye ulemavu.

Mbali na Askofu Maluma, naye Mkuu wa mkoa wa Iringa Amina Masenza amesema mkoa wa Iringa umepata pigo kubwa la kuondokewa na pacha hao waliokuwa na upendo wa dhati na wenye kujitambua.

"Katika mkoa wa Iringa tumepata mtihani wa kuondokewa na watoto waliokuwa na upendo sana, najua kwa jinsi gani tulivyokuwa tunawapenda lakini Mungu amewapenda zaidi. Maria na Consolata walijitambua na wakakubali maumbile waliokuwa nayo halafu wakajiamini ndio maana waliweza kusoma kwa bidii na kufiki hatua ya chuo kikuu", amesema Masenza.

Pamoja na hayo, Masenza ameendelea kwa kusema "niwaombe wazazi kwamba serikali ipo tayari kuwasaidia watoto wenye ulemavu hakuna haja ya kuwaficha, waacheni watoto waje maana neema yao ipo. Kuwaficha huko ni kutenda dhambi".

Maria na Consolata walizaliwa Novemba 19, mwaka 1997 ambao enzi za uhai wao walikataa kutenganishwa miili yao na kupelekea leo hii kuzikwa kwenye jeneza moja litakalokuwa na misalaba miwili  katika makaburi ya viongozi wa dini yaliyopo Tosamaganga mkoani humo.

Akutana na Mwanaye Miaka 30 Baada ya Kuitoa Mimba

$
0
0
Akutana na mwanaye miaka 30 baada ya kuitoa mimba
Akiwa na miaka 14, Melissa Ohden was 14 aliijuwa siri kubwa - mamake alijaribu kumuua akiwa angali tumboni.

Aliokolewa na mhudumu wa afya aliyemsikia akilia katika taka taka za hospitali nchini Marekani.

Hii ni hadithi ya uhai wake, na kuhusu mamake aliyedhani kwamba amekufa.

"Nili inukia nikijua kwamba nilizaliwa kabla ya kutimiza miezi 9, na kuwa niliasiliwa," Melissa Ohden, sasa ana miaka 41 anasema.

"Kitu ambacho sikujuwa ni kwamba kulikuwana siri kubwa. Kwamba nilitakiwa nife, na badala yake nilizaliwa nikiwa hai."

Mnamo 1977, katika hospitali moja nchini Marekani katika jimbo la Iowa, Mamake Melissa aliyekuwa na umri wamiaka 19 aliavya mimba kwa kutumia kemikali kwa zaidi ya siku tano.


Melissa - ambaye ameandika vitabu kuhadithia maisha yake- anasema aligundua kwamba aliasiliwa wakati alipogombana na dadake kutoka familia iliomuasili.

Kwa mara ya kwanza Melissa alichanganyikiwa, lakini wakati fahamu ilipomuingia na alipokaa kuzungumzana wazazi waliomlea hapo ndipo athari ikamjia kwa kuugua matatizo ya kiakili.

Uchungu uliendelea kuongezeka, mpaka miaka mitano baadaye - akiwa na miaka 19 - alichukuwa uamuzi wa kijasiri kumsaka mamake aliyetaka kumtoa uhai.

Ni shughuli iliyomchukua muda wa karibu muongo mmoja, lakini hatimaye alimpata - na akagundua ukweli ulimshutusha.
Melissa akiwa na miaka 14 ndiyo alitambua kwa mara ya kwanza kuwa mamake alijaribu kumuavya
"Siri kubwa kweli ni kuwa mamangu alikaa miaka 30 akiamini kwamba nilifariki hospitalini.

"Hakuambiwa kwamba nilipona, ilikuwa siri aliofichwa," anasema.

Na ndio kwa sababu hiyo walipokutana ana kwa ana miaka mitatau baada ya kutumiana barua pepe , Melissa aliguswa na kwamba mamake alijutia kitendo hicho, kilichomsumbua roho kwa miaka mingi..

Mamake mzazi, Ruth, alimuambia kwamba hakutaka kuitoa mimba , na kwamba aliwekwa katika hali ambayo ni kama alilazimishwa kuitoa mimba hiyo.

"Nilichokuja kujua ni kwamba bibi yangu - mamake mamangu - alikuwa mhudumu maarufu wa afya katika jamii, na mtu anayefanya kazi ya kutoa mimba alikuwana rafiki yake.

Melissa Ohden amekutana na mamake kwa mara ya kwanza akiwa na miaka 30
Melissa anasema yeye ni "mojawapo ya watu wenye bahati duniani", kwanza kwamba aliweza kupona mkasa huo, na pia kubarikiwa na kuwa na wazazi waliomuasili na mamake mzazi katika maisha yake.

Kwa bahati tu, Melissa na mamake mzazi sasa wanaishi mjini Kansas pamoja na mojawapo wa dada zake wa kambo.

Kwanini Baadhi ya Wanaume Wana Maumbile Madogo na Mafupi ya Kiume na Hawana Nguvu ?

$
0
0

KWA NINI BAADHI YA WANAUME WANA MAUMBILE MADOGO NA MAFUPI YA KIUME NA HAWANA NGUVU ZA KIUME NINI HUCHANGIA?


Kama una Ngiri, au umejichua kwa muda mrefu, punyeto, una stres nyingi Sana, lishe duni, kisukari, presha, kutopata choo vizuri, tumbo kujaa gesi, na kuunguruma chini ya kitovu, kaswende, gono,haya yote husababisha kuwa na maumbile madogo na mafupi ya kiume na kukosa nguvu za kiume.MATIBABU

Tumia dawa ya asili itwayo (MASUNZU POWER MIX) inatibu tatizo la nguvu za kiume maradufu inatibu uume mdogo na mfupi na kuimalisha mishipa iliyolegea inarefusha Nchi(4-8) na kunenepesha maumbile na upana (cm3-4) dawa hii haina madhala hata kwa wazee walio na umri wa miaka (70-85) pia inaongea hamu ya kufanya tendo la ndoa Mara (3-5) bila hamu kuisha dawa hii inatibu siku 6 na kupona kabisa

MASUNZU POWER MIX. ni dawa ya asilia yenye mchanganyiko wa mitishamba 7 yenye maajabu yafuatayo kunyoosha mishipa ya askari aliyesinyaa kutokana na kujichua kwa muda mrefu au Ngiri, nk 🌸pia tuna dawa ya kutibu busha bila opresheni
SOSOMA DX ni dawa ya kumvuta mme au mke mpenzi wako arudi haraka na kuanza mapenzi mapya kama mlivyoanza mwanzo baada ya Masaa 2 atarudi na kutulia ndani ya nyumba
GINDU EXTRA ni dawa ya kutibu kisukari siku 14 unapona kabisa hata kama imepanda 350 itashuka haraka tunatibu presha, vidonda vya tumbo nk:

OFISI IPO DAR ES SALAAM BUGURUNI CHAMA UNAWEZA KULETEWA POPOTE ULIPO AU SIMU 0673552294 / +255784552299 TABIBU ATHUMAN.

Askofu Afunguka Kuhusu Kifo cha Mapacha Maria na Consolata

$
0
0

Askofu Afunguka Kuhusu Kifo cha Mapacha Maria na Consolata
Askofu Jimbo Katoliki Njombe, Alfred Maluma amesema vifo vya pacha walioungana,  Maria na Consolata Mwakikuti kinapaswa kuenziwa na Watanzania kukumbushana  wajibu wao kwa watu wenye ulemavu.

"Wameacha somo hilo, tuwajali watu wenye ulemavu hilo ndilo somo walilotuachia Maria na Cobsolata," amesema Akofu Maluma leo Jumatano Juni 6, 2018 katika ibada ya kuaga miili ya pacha hao.

Amesema Mungu aliwaumba pacha hao kwa mfano wa sura yake na akawapa uhai kwa kipindi walichokuwa duniani.

Amebainisha kuwa masista wa shirika la Maria Consolata wameonyesha mfano wa kuigwa kwa kuwaleta pacha hao waliofariki dunia katika hospitali ya Mkoa wa Iringa.

Rais wa TFF Atuma Salamu za Rambirambi Kufuatia Kifo cha Mchezaji wa Zamani wa Taifa Stars

$
0
0
Rais wa TFF Atuma Salamu za Rambirambi Kufuatia Kifo cha Mchezaji wa Zamani wa Taifa Stars
Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania TFF Ndugu Wallace Karia ametuma salamu za rambirambi kwa aliyekuwa mchezaji wa zamani wa timu ya Taifa ya Tanzania "Taifa Stars" Rajabu Digongwa aliyefariki huko mkoani Tanga.

Rais wa TFF Ndugu Karia amepokea kwa huzuni na mshtuko mkubwa taarifa za kifo cha mchezaji huyo wa zamani aliyefariki baada ya kuugua.

Kwa niaba ya TFF Rais wa TFF Ndugu Karia ametoa pole kwa familia ya mchezaji huyo ,wanafamilia wa Mpira wa Miguu,ndugu ,jamaa na marafiki.

“Marehemu Digongwa namfahamu vizuri toka enzi akicheza na kifo chake kimenishtua na kunihuzunisha kwa niaba ya TFF natoa pole kwa wafiwa" alisema Karia.

Enzi za uhai wake marehemu Digongwa alicheza timu za Wananchi FC, African Sports, pia alipata kuitwa kwenye timu ya mkoa wa Tanga na pia timu ya Taifa ya Tanzania.

 Mazishi ya marehemu Digongwa yamefanyika leo saa 4 asubuhi mkoani Tanga

Wakati huohuo Rais Karia pia ametuma salamu za rambirambi kwa mchezaji wa zamani Khalid Bitebo aliyefiwa na mkewe.

Ametoa pole kwa Bitebo na familia kiujumla akiwataka kuwa na subira katika kipindi hiki cha majonzi.

Watanzania Washauliwa Kukatia Bima Nyumba Zao

$
0
0
Watanzania Washauliwa Kukatia Bima Nyumba Zao
WATANZANIA wametakiwa kuzikatia bima nyumba zao ili wanufaike na fidia pindi nyumba hizo zikipatwa na majanga ya aina mbalimbali kama vile kuungua, kuharibiwa na mafuriko au majanga yoyote yale.

Mwito huo umetolewa na Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Bima ya Resolution, Maryanne Mugo wakati akizungumzia bima ya nyumba itolewayo na kampuni hiyo.

Alisema, jamii inatakiwa kuwa na mwamko katika kujiunga na bima hiyo ambapo malipo yake sio makubwa ikilinganishwa hasara inayoweza kutokea pindi nyumba ikikutwa na majanga mbalimbali.

Alisema,“ jamii inapaswa kutambua kuwa kuna amani na faida kubwa iwapo wakizikatia bima nyumba zao na hiyo inajidhihirisha pindi pale ambapo nyumba zikipatwa majanga iwe kuungua moto, kuvunjwa, kuharibiwa na mafuriko au majanga yoyote yale huwa bima inalipa”

Akizungumzia kuhusiana na mwamko wa watu kutumia huduma ya bima ya kampuni hiyo, alisema mpaka sasa wanao wateja 210 ambapo kati yao ni wawili tu ndo wamepatwa na majanga, mmoja ameshalipwa na mwingine anakaribia kulipwa.

Aliongeza, kuwa kuna dhana kati ya watu mbalimbali wakifikiria kuwa inachukua muda mrefu sana tangia nyumba ikipatwa majanga na kulipwa fidia ambapo alisema kwa kampuni hiyo huchukua muda mchache tu iwapo taratibu za malipo zikishakamilishwa.

Alisema, mteja hulipwa iwapo tu atakamilisha nakala muhimu kama vile ripoti ya Polisi, Makadirio ya vitu vilivyopotea au kuharibiwa ambavyo vinatokana na ripoti ya mpimaji au mkadiriaji wa bima.

“Hivi ni vitu muhimu na vya haraka vinavyotakiwa kuwakilishwa na mteja pindi nyumba yake itakapopatwa na majanga ya aina yoyote ile na kampuni za bima zinashughulikia kwa wakati”alisema.

Muone Ustadhi Ashrafu Atimize ndoto yako..Anatumia Nyota na Nguvu za Asili Kutibu

$
0
0

Muone Ustadhi Ashrafu Atimize ndoto yako. yawezekana ulizaliwa nanyota yakitajiri ila watu wabaya wameikalia mpaka sasa ikawa hufahamu chochote. Mtafute ust Ashrafu Airudishe nyota yako yakitajiri kwakupitia pete inayoendana na nyota yako. Ust Ashrafu Ananguvu zamajini katika utendaji wake.

Anauwezo wakutoa Mali kwakupitia pete nakwakupitia majini wake. Na anauwezo wakuzirudisha Mali zilizopotea kwanjia zakichawi kwakupitia Pete yakifalme Ambayo inayong'aa muda wowote nakubadilikabadilika rangi. Ust Ashrafu Ametembea baadhi ya nchi kwakuwapatia watu huduma mbalimbali. Kama vile maradhi yakisukari, presha, ukimwi, bawasiri, tezidume, mwiliwote kupooza nakutetemeka, NK. Navilevile Amewapatia wengi huduma yamvuto wa kibiashara, nayamvuto wakimapenzi.

Nawengi wametoa shukrani zao kwa ust Ashrafu namna Alivyozirudisha Ndoa zao zilizo sambaratika kwamuda mrefu. Mtafute ust Ashrafu ili akusaidie juu yamambo yako. Nahuyu ust anasaidia matatizo yauzazi, nguvu zakiume, kuwashwa mwilini, kutokwa namapere usoni nasehemu za siri, NK. Na anadawa yakumtuliza mume asiesikia nakutulia inayoitwa limbwata. Na anadawa yakumrudisha mpenzi ktk mahusiano kwamda mchache.

Na amezipatanisha familia nyingi zilizogombana. Na anauwezo wakufarakanisha maadui waliokua pamoja.

Mtafute Ustadhi Ashrafu kwa no. 0768486717-0627423037 Au Mtafute kwa whasapp 0659438578

Hizi ndio namba zake mpigie muda wowote usiogope yupo kwaajili yako. Mpigie hupate muongozo wa bure naushri. Ustadhi Ashrafu huduma zake hupatikana mahala popote utakapo muhitaji, ila sehemu kuu anapatikana Bagamoyo.


“UDF ni zaidi ya vyama vya siasa” - Zitto

$
0
0

Kiongozi wa Chama cha ACT-Wazalendo Zitto Kabwe Akizungumzia ushirikiano huo wa kidemokrasia (DeFront), Zitto anasema hilo ni vuguvugu litakalohusisha si vyama vya siasa tu, bali makundi mbalimbali katika jamii.


Akizungumza na eatv.tv Zitto amefunguka kuwa Chama cha ACT Wazalendo Katika kikao chake cha Kamati Kuu cha Januari Mwaka 2018 kiliazimia kuwa ni muhimu kujenga mashirikiano na vyama vingine na makundi mengine ya kijamii.

“Tunataka kujenga ‘The Democratic Front’ kwa kuhusisha wana Demokrasia nchini kwa madhumuni ya  kutetea, kuimarisha na kulinda demokrasia yetu ya vyama vingi pia kujenga Uchumi shirikishi wa Wananchi”, amesema Zitto

Zitto anafafanua kuwa tayari chama chake kimeanza mazungumzo na vyama vya siasa, asasi za kiraia na vyama vya wafanyakazi ili kufikia azma hiyo.

BAVICHA waitaka serikali kujifunza kupitia Mapacha

$
0
0

Baraza la Vijana wa  Chama cha Demokrasia na Maendeleo (BAVICHA), limeitaka serikali kujifunza kupitia kifo cha mapacha walioungana, Maria na Consolata ambao wamefariki Jumamosi Usiku wakati wakipatiwa matibabu katika hospitali ya Rufaa Iringa.


Kupitia tarifa ya salamu za rambi rambi iliyotolewa na Mwenyekiti wa BAVICHA, Patrick Ole Sosopi, amesema kuwa kama taifa inabidi kukubaliana na ukweli kuwa sekta ya afya ina changamoto nyingi ikiwepo huduma za Afya na uduni wa mazingira hivyo viongozi wanapaswa kushughulikia matatizo hayo na siyo kuwa mbele katika kushiriki misiba.

Aidha Mwenyekiti wa Baraza hilo amesema kwamba Taifa limepoteza nguvu kazi ambao walikuwa na malengo pamoja na ndoto kubwa katika taifa pindi watakapokuwa wamemaliza masomo yao.

Pamoja na hayo BAVICHA wametoa shukrani na pongezi kwa kanisa Katoliki kwa kuwalea mapacha hao ambao wanatambulika kama mashujaa kwa taifa katika kipindi chote cha uhai wao.

Maria na Consolata walizaliwa Novemba 19, 1997 na wamefariki  Juni 2, 2018 ambapo enzi za uhai wao walikataa kutenganishwa miili yao na waliishi kwa miaka 21 wakiwa wameunga hivyo hivyo.

Septemba mwaka jana, baada ya kufaulu mtihani wa kidato cha sita, Maria na Consolata walijiunga na Chuo Kikuu cha Kikatoliki cha Ruaha, Iringa. Walianza kuugua maradhi ya moyo na Desemba mwaka jana, wakahamishiwa taasisi ya maradhi ya moyo ya Jakaya Kikwete katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili, Dar es Salaam ambako walilazwa kwa miezi miwili.

Leo hii Maria na Consolata watazikwa kwenye kaburi moja litakalokuwa na misalaba miwili katika makaburi ya viongozi wa dini yaliyopo Tosamaganga mkoani Iringa

Kisa Mume, Mwanamke Ajifungulia Polisi

$
0
0
Mwanamke mmoja Amina  Rafael Mbunda (26) mkazi wa Kiswanya,kijiji cha Mgudeni,kata ya mwaya,Tarafa ya Mang'ula wilayani kilombero mkoani Morogoro,anadaiwa kujifungua nje ya kituo cha polisi baada ya kutolewa mahabusu alikokuwa akishikiliwa kwa tuhuma zilizomhusu mumewe aliyedaiwa kuhusika na ununuzi wa kitanda cha wizi.

Mwanamke huyo aliyelazwa kituo cha afya mang'ula alikopelekwa na kulazwa baada ya kujifungua,amedai alikamatwa Juni mosi na polisi,Mwenyekiti wa kitongoji na mwanaume mmoja waliofika nyumbani kwake,saa chache baada ya kuondoka mgambo waliokuwa wakimtafuta mumewe kwa tuhuma za ununuzi wa kitanda cha wizi,ambapo akiwa mahabusu licha ya kulalamika kuumwa uchungu,askari wa zamu alimpuuza hadi alipoona amezidiwa na kumtoa nje alipojifungulia kwenye nyasi bila msaada.

Mganga wa kituo cha afya Mang'ula,aliyetajwa kwa jina moja la Msomba ametafutwa kwa njia ya simu ili afafanue kuhusu afya ya mwanamke huyo na kichanga cha kike kilichozaliwa kikiwa na uzito wa kilo 3.5 kwa mujibu wa kadi yake ya kliniki iliyoonesha pia amejifungua kwa msaada wa ndugu,lakini simu yake iliita bila majibu.

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Alhamisi ya June 7

$
0
0


 Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Alhamisi ya June 7

Pata Tiba ya Tatizo la Nguvu Za Kiume, Inasaidia Kukufanya Urudie Mara 5 na kuchelewa kwa Dakika 20

$
0
0
TATIZO LA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME NA MAUMBILE MADOGO LINATIBIKA.Baada ya utafiti wa mda mrefu juu ya matatizo ya upungufu wa nguvu za kiume na ukosaji wa hamu ya tendo la ndoa ama kushindwa kurudia tendo kwa haraka DR Magise imekuletea tiba ya matatizo hayo kwa kutumia dawa za:

GUMBA POWER:Ni dawa asili ya vidonge inayotibu tatizo la upungufu au ukosefu wa nguvu za kiume,dawa hii inamchanganyiko wakutosha wenyekuzalisha vichocheo vingi vya Hemone za Gestrogen vikiwemo vitamin B6&B1,vitamini E,pamoja na madini aina ya zinc vitakufanya kuwa na nguvu na mzunguko mzuri wa damu na kuongeza hamu na uwezo wa kufanya tendo la ndoa zaidi ya hatua nne au zaidi,na kuchelewa kufika kileleni zaidi dakka 20-30.

NTINJE:Inarutubisha maumbile ya uume yani kurefusha na kunenepesha nchi 4-7 upana cm3-4 standard kiafya haijalishi umri wako hata kwa wazee ukiitumia maumbile yako yatabaki kuwa hivyo siku zote,Pia tunatibu Presha,kisukari siku7,ngiri,chango la tumbo tumbo kujaa gesi,kutopata choo vizuri

 TUPO TZ DAR ES SALAAM   MBAGALA RANGI TATU.HUDUMA HII UTALETEWA POPOTE ULIPO .WASILIANA NAMI 0754741788, 0715741788, 0783741788

-DR MAGESA
Viewing all 104795 articles
Browse latest View live




Latest Images