Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104795 articles
Browse latest View live

Zitto Kabwe, Polepole, Dr Mashinji Wafunguka Mazito Sakata la Waraka KKKT

$
0
0
Zitto Kabwe, Polepole, Dr Mashinji Wafunguka Mazito Sakata la Waraka KKKT
Lile sakata la serikali kuliandikia barua Kanisa la Kiinjili la Kilutheri, (KKKT) limezua mjadala kwenye twitter za viongozi mbalimbali wa kisiasa.

Jana Juni 6, mara baada ya kusambaa kwa barua hiyo inayodaiwa kuandikwa Mei 30 na Wizara ya Mambo ya Ndani ikilitaka KKKT kuufuta waraka wa maaskofu, viongozi wa kisiasa walianza kutuma ujumbe kwenye akaunti zao za twitter.

Mbunge wa Kigoma Mjini (ACT-Wazalendo) Zitto Kabwe ameandika katika ukurasa wake akisema: “Tishio la serikali kwa kanisa la KKKT linapaswa kupingwa na kila mtanzania. Tukiruhusu KKKT kuingiliwa, hakuna atakayepona.”

Jana jioni, Zitto aliandika tena na safari hii alipeleka ujumbe moja kwa moja kwenda kwa Katibu wa Itikadi na Uenezi, wa CCM, Humphrey Polepole akisema:

“Nimeambiwa kuwa TEC ya Kanisa Katoliki pia imepewa barua kama ya KKKT. Serikali ya CCM ya awamu ya Tano imeamua kupambana na makanisa 2 makuu nchini ...”

Baada ya kutumwa kwa ujumbe huo na Zitto, Polepole amejibu akisema:

“Serikali makini ina wajibu wa kukumbusha, kuelekeza, kuonya au kuchukua hatua kwa mtu/taasisi yoyote inayokwenda kinyume na taratibu za nchi ambazo tumejiwekea. Nimeisoma barua ya Msajili anazo hoja za msingi. Usijichomeke hapa kutafuta huruma na umaarufu hewa. Soma Warumi 13:1-5.”

Kwa upande wake, Katibu Mkuu wa Chadema, Vincent Mashinji yeye ameandika akisema:

“Nimeona barua hii kwa masikitiko na majonzi makubwa. Naweza sema tu kwamba: “hakuna mtu mwenye akili timamu aliyewahi kuvunja kioo kilichomwonyesha uchafu wake.”

Wanaopiga Simu za Uongo Fire Kukiona

$
0
0
Wanaopiga Simu za Uongo Fire Kukiona
Kamanda wa Jeshi la Zimamoto mkoa wa Arusha Kennedy Komba ametoa angalizo kwa wateja wanaopiga simu za bure katika jeshi hilo wakiwa hawana tatizo lolote kuwa wataanza kuchukuliwa hatua ikiwemo kupelekwa mahakamani kwa kuwa wanatenda kosa la jinai.

Komba pamoja na mambo mengine amesema wajenzi waa majengo katika maeneo mbalimbali wanatakiwa kuwasiliana na jeshi hilo ili kupata ushauri wa jinsi gani wanaweza kutengeneza miundombinu imara ya kukabiliana na majanga ya moto.

Jay Moe Atabiri Wasanii Watakaopotea Kwenye Muziki

$
0
0
 Jay Moe Atabiri Wasanii Watakaopotea Kwenye Muziki
Mkongwe wa hip hop Bongo, Jay Moe amefunguka na kudai nidhamu ndio kitu kikubwa kilichosababisha wasanii wengi kupoteza kwenye 'game' wakiwemo wakongwe hata wa sasa wanaojiita kizazi kipya.


Jay Moe ametoa kauli hiyo wakati alipokuwa anazungumza kwenye kipindi cha 5SELEKT kilichorushwa mubashara Juni 06, 2018 na kusema kilichomsababisha yeye kudumu katika muziki mpaka hii leo licha ya kuwa mkongwe ni nidhamu yake ambayo anaionesha kwa kila mtu ambaye anamzunguka kwa kuwa alishawahi kuona madhara yake.

"kwenye kila kitu unachotaka kidumu kwa muda mrefu ni lazima uwe na nidhamu, katika 'game' yangu walikuwa wasanii wengi ambao walikuja kwenye zama zangu na wakapata umaarufu mkubwa kuliko mimi lakini labda nidhamu yao na kile wanachokifanya ndicho kilichowaangusha", amesema Jay Moe.

Pamoja na hayo, Jay Moe ameenedelea kwa kusema "ninachoshukuru nipo na mahusiano mazuri na watu ambao ninawahitaji kama 'media', mashabiki pamoja na watu wa kwenye muziki 'industry' na hicho ndio kitu kikubwa kwasababu unaweza leo ukawa maarufu halafu ukawa ulishawahi kuwadharau watu wengine hata ikitokea ukawa na shida hawataweza kukusaidia".

Kwa upande mwingine, Jay Moe amesema jambo jingine linalowatesa wasanii wengi wakongwe ni kutotaka kukubali mabadiliko ya muziki ili waweze kuendana na soko jinsi linavyotaka kwa sasa nasio kuendelea kufanya kazi kizamani.

Madaktari Wasema Puto la Seth Limeisha Muda Linatakiwa Kuondolewa

$
0
0
Madaktari Wasema Puto la Seth Limeisha Muda Linatakiwa Kuondolewa
Jopo la madaktari lililomfanyia uchunguzi, Mmiliki wa kampuni ya kufua umeme ya IPTL, Habinder Seth, limebaini kuwa, puto lililopo tumboni mwa mshtakiwa huyo, linatakiwa kuondolewa.

Wakili kutoka Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) Leonard Swai ameieleza mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, leo Juni 7, 2018, wakati shauri hilo lilipokuja kwa ajili ya kutajwa.

Swai amedai mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu wa Mahakama hiyo, Huruma Shahidi, kuwa wamepokea ripoti ya jopo la madaktari kutoka Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH), ambayo imeeleza kuwa Seth hasumbuliwi na tatizo lolote, isipokuwa anatakiwa kutolewa puto lililo tumboni, alilowekewa kwa sababu za kiafya na sasa limeisha muda wake.

"Katika taarifa ya uchunguzi niliyopewa na jopo hilo, wameeleza kuwa wanamsubiri daktari wa Seth kutoka Afrika Kusini ndio wamfanyie upasuaji wa kuliondoa puto hilo, kwa sababu mshtakiwa aliomba, wakati anafanyiwa upasuaji, daktari wake awepo," alidai Swai.

Awali, Swai alidai kuwa kesi hiyo ilikuja kwa ajili ya kutajwa na upelelezi wa ndani umekamilika na kwamba  upande wa mashtaka wanaendelea na mawasiliano na nchi husika ili kupata nyaraka muhimu kwa ajili ya kukamilisha upelelezi.

Katika hatua nyingine, Mahakama hiyo imemruhusu Mke wa Seth kwenda kumuona Mume gerezani.

Uamuzi huo umetolewa na Hakimu Shahidi, baada ya Wakili wa Seth, Dora Maraba kuiomba mahakama kibali kwa ajili ya mke wa Seth, kwenda kumuona mumewe gerezani.

"Tuliandika barua kwa mkuu  wa Gereza la Ukonga, tukiomba  mke wa Seth, aweze kuruhusiwa kumuona mumewe lakini imeshindikana, hivyo tunaomba  Mahakama yako, itupatie kibali ili Seth aweze kuonana na mke wake," alidai Maraba na kuongeza

"Mwezi uliopita, mke wa Seth alifiwa na mama yake mzazi, hivyo tangu kutokee kwa msiba huo, mkewe hajapata nafasi ya kuonana na mume wake, gerezani" alidai Wakili Maraba.

Hakimu Shahidi, baada ya kusikiliza maelezo ya pande zote, amesema mshtakiwa ana haki ya kupewa nafasi ya kuonana na kuongea na mke wake kwa sababu bado hajatiwa hatiani.

“Japokuwa hatupaswi kuingilia taratibu za magereza, lakini mshtakiwa ana haki ya kupewa nafasi ya kuongea na mke wake, hivyo naomba aruhusiwe kuongea na mke wake," amesema Hakimu Shahidi.

Kesi hiyo imeahirishwa hadi Juni 21, 2018, itakapotajwa.

Sethi na Rugemarila wanakabiliwa na mashtaka  12 ya  uhujumu uchumi  kwa kula njama, kujihusisha mtandao wa uhalifu , kughushi,  kutoa nyaraka za kughushi.

Pia wanadaiwa kujipatia fedha kwa njia za udanganyifu,  kutakatisha fedha  na kusababisha hasara ya Dola za Marekani 22,198,544.60 na Sh 309,461,300,158.27.

Wema Sepetu Afanyiwa Oparesheni Arejea Nchini.... Meneja Wake Atoboa Siri ya Ugonjwa Unaomsumbua

$
0
0
Wema SepetuAfanyiwa Oparesheni Arejea Nchini.... Meneja Wake Atoboa Siri ya Ugonjwa Unaomsumbua
Mwigizaji Wema Sepetu, amerejea kutoka nchini India ambapo alienda kwa matibabu.

Meneja wa mlimbwende huyo ambaye amewahi kutwaa taji la  Miss Tanzania 2006, Martin Kadinda amesema amerejea juzi, baada ya kufanyiwa upasuaji mdogo.

“Wema amerejea lakini kwa sasa hawezi kuzungumza kwenye simu anahitaji kupumzika, amefanyiwa upasuaji mdogo na anaendelea vizuri,” amesema Kadinda.

Alipoulizwa kuhusu upasuaji huo, hakuwa tayari kuzungumzia kwa kina badala yake alijibu ni mambo ya wanawake.

“ Ninachoweza kukwamba ni kwamba ni upasuaji mdogo, ndiyo maana alikwenda pekee yake, tena natumia nafasi hii kuwajulisha mashabiki wake kuwa Wema anaendelea vizuri kiafya,” amesema Kadinda.

Habari kuhusu matibabu ya Wema anayekabiliwa na kesi ya kutumia dawa za kulevya, zilibainishwa wiki iliyopita baada ya kushindwa kufika mahakamani  Mei 29 ili kuendelea kusikiliza kesi yake.

Mama mzazi wa mwigizaji huyo, Mariamu Sepetu  alifika mahakamani hapo na kuijulisha kuwa mwanaye anaumwa yupo India kwa ajili ya matibabu.

 Mama huyo alilazimika kuwasilisha  nyaraka za kusafiria na kuzionyesha  kwenye Mahakama hiyo badala ya za matibabu.

Hatimaye Simba Yatafuna Mfupa Uliomshinda Yanga Yatinga Fainali ya SpotPesa Super Cup

$
0
0
Hatimaye Simba Yatinga Fainali ya SpotPesa Supa Cup
Mabingwa wa soka Tanzania, Simba wamefuzu kucheza fainali ya SportPesa Super Cup baada ya kuichapa Kakamega Homeboyz kwa mikwaju 5-4.

Mechi hiyo iliisha kwa sare ya bao 0-0 katika hatua ya dakika 90 za kawaida.

Baada ya hapo ikawa ni mikwaju ya penalti na wachezaji wote watano wa Simba walifunga wakiongozwa na Jonas Mkude ambaye alifunga penalti ya mwisho.



WALIOPATA PENALTI SIMBA;
Niyonzima PATA
Nyoni PATA
Kapombe PATA
Kichuya PATA

Hotel yaamuriwa kumlipa zaidi ya Milioni 68 Mwanamke waliyemuita ‘Kahaba’

$
0
0
Leo June 7, 2018 Mahakama Kuu imeamuru mwanamke aliyetimuliwa katika hoteli moja ya kifahari kwa kudaiwa kuwa kahaba alipwe fidia ya dola 30,000 za Marekani ambazo ni zaidi Milioni 68 za Kitanzania katika Mahakama kuu ya Kenya iliyopo Nairobi.

Jaji Msagha aliitaka hoteli ya Intercontinental kulipa fidia ya milioni 2 na mwanasheria mkuu wa serikali milioni 1 kwa Winfred Clarke kwa kumdunisha na kumharibia jina.

Tukio hilo lilitokea miongo miwili iliyopita mwanamke huyo alipofika hotelini kwa nia ya kufurahia kinywaji akiwa na rafiki yake kabla ya kusimamishwa na mlinzi wa hoteli kwa sababu hakuwa ameandamana na mwanaume.

Clarke hata hivyo, alienda hadi eneo la kuuzia vileo ambapo aliagiza bia mbili kabla ya kulazimishwa kulipa “ada ya kujisitiri” ambayo hakuelewa ni kwa nini alitakiwa kulipa.

Baadaye, alitolewa kwa nguvu kutoka hotelini humo na kuzuiwa kukaa eneo ambalo wageni wanakaa wanapongojea teksi, kabla ya polisi kuitwa na kumkamata ambapo alizuiliwa kwa siku mbili.

Wasiliana na Dr Mabula Anatibu Upungufu wa Nguvu za Kiume, Busha na Matatizo ya Maumbile Madogo kwa Mwanaume

$
0
0
TUNATIBU NA KUPONESHA KABISA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME UUME MDOGO BUSHA BILA KUPASUA PRESHA VIDONDA VYA TUMBO
Asilimia kubwa ya wanadamu wanasumbuliwa na magonjwa mbalimbali na wapo waliongahika sehemu mbalimbali bira MAFANIKIO MABULA CLINIC ni kituo cha tiba asilia kilichopo mbagara zakhemu njia kuu ya JESHINI JE HUNAUPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME AU UUME WAKO MDOGO NA MWEMBAMBA?

MAPRO PAWER NO 2 ndio Tiba kwa sasa utibu matatizo matatu kwa pamoja 1hitakufanya uchelewe kufika kilekeni dikika 15-20 kwa tendo la kwanza 2 uhimalisha misuli iliyoregea na kusinyaa hasa kwa wale walio hasirika na upigaji punyeto 3 itakufanya upate amu ya kurudia tendo zaidi ya Mara tatu

KWA NINI UJIONE MPWEKE PALE UKUTANAPO NA MPENZI AU MKE WAKO kisa unawai kukojoa au unakomea bao moja tu na huku dawa zipo MAKAKANUA mix ni dawa iliyochanganywa na miti Shamba 9 na Kuwa na uwezo wa kuongeza uume saizi upendayo inchi 5-8 Kwa Urefu na unene sentimita 1-5 dawa hizi hazina madhara yoyote kwa mtumiaji ata wazee wenye umri mkubwa wanapona? zipo dawa za mvuto wa mpenzi mme au mke Kwa masaa matatu tu na kukupigia simu yeye mwenyewe mvuto wa biashara kutengeneza mwonekano mzuri wa mwili kwa wanawake yani shepu tunatibu ngiri miguu mgongo na kiuno kuumwa kupunguza kitambi minyama uzembe matiti na mwili mkubwa

TIBA NA USHAULI MUONE DR MABULA AU PIGA SIMU NO 0752348593 UDUMA ZANGU UTAZIPATA POPOTE ULIPO KAMA UWEZI KUFIKA OFISINI

Mpaka Mwanamke Anaamua Kuchepuka Ujue Kuna Shida kwa Mumewe

$
0
0

Katika Utafiti wangu imegundua kuna tatizo kubwa katika mahusiano aidha ya kimapenzi au ya ndoa.Uaminifu umekuwa tatizo kubwa miongoni mwa jamii ya kizazi hiki! Kutoridhika imekuwa sehemu ya maisha ya sasa si kwa mwanaume au mwanamke kuchepuka ndiyo habari ya mujini kwa sasa hadi wale walioaminika kuwa viongozi wa dini maana hakuna mwenye kinga ya kutotenda dhambi hivyo imekuwa kujitwalia kadri tupendavyo nani atakuwa kiini cha mabadiliko katika wimbi hili linaoelekea kupoteza wengi.

Tatizo ni nini hasa kwa uzoefu wangu wa kuishi katika dunia hii na katika ndoa kwa muongo zaidi ya mmoja nimegundua mwanamke anaweza akatulizwa (walioko ndoani) tu endapo mume atakidhi mahitaji yote ya kiuchumi,zaidi kuwa na muda wa kutosha na mkewe bila kusahau kusaidiana kufikishana katika kilele cha maraha ambacho.Mungu aliona ni vema atupe wanadamu kama kitulizo ktk maisha yetu haya yenye adha nyingi.

Sasa cha ajabu kuna baadhi ya wanaume wamekuwa busy wakiamini magari,pesa na fahari ndiyo vitaziba uhitaji wa mke katika kukidhi haja ya upendo ndiyo maaana lawama haziishi watu wanachapiwa na kuishia kulalama eti wanawake hawaridhiki hata uwape nini mwanamke haswa alilyelewa vyema akihudumiwa bed na akapata mahitaji ya kiuchumi sina cha kufata nje hata kidogo.

Nina zaidi ya miaka 13 ya ndoa hivyo najua nisemacho sioni fahari wala sijawahi kufikiria kutoka na mtu nje ya mume wangu kwa muda wote huo ila kuna mazingira baadhi wanaume wanasababisha hadi mke unajiona mhitaji,mume hashikiki ndani kila siku kuja home late mvivu kitandani hayuko romantic nk unategemea mke afanyeje?

Ilihali naye ana damu inachemka(hapa siharalishi kuchepuka ila mke anakuwa katika upweke mkuu nani ampe faraja mpaka mke anaamua kutoka nje kuna tatizo kubwa hivyo chukueni tahadhari waume wenye tabia hizi zinajeruhi sana mioyo yetu (nasi tunapendwa sana huko nje uwezo wa kutoka kama mnavyotoka tunao sana..ila ni staha tu na hofu kwa Mungu muumbaji.Wanaume many sehemu yenu na wanawake pia ili tuishi kwa raha bila kuumizana.

Naibu Spika alivyomkataza Waziri Mkuu kujibu swali linalohusu Waraka KKKT

$
0
0
Leo June 7, 2018 Naibu Spika wa Bunge, Tulia Ackson amemzuia Waziri Mkuu wa Tanzania, Kassim Majaliwa kujibu swali aliloulizwa na Mbunge Vunjo, James Mbatia kuhusu agizo la Serikali kwa Kanisa la Kilutheri kufuta waraka wake

Naibu Spika alitoa zuio hilo kwa Waziri Mkuu huku akitumia mfano kuwa Spika wa Bunge alishawahi kumzuia Mbunge Saed Kubenea kujibiwa maswali yake yanayohusu dini.

Mbunge wa Vunjo, James Mbatia alitaka kujua Serikali inatoa tamko gani juu ya nyaraka hizo ambazo zimezua taharuki kwa jamii hasa ukizingatia Makanisa ni wadau wakubwa wa amani na maendeleo katika jamii. VIDEO:

Kauli ya 'Hatuna Pesa' Inavyoimaliza Timu ya Yanga

$
0
0
YANGA imeondolewa kwenye michuano ya Sportpesa Super Cup ambayo inaendelea nchini Kenya.

Awali moja ya timu ambazo zilikuwa zinapewa nafasi kubwa na mashabiki ya kufanya vizuri kwenye michuano hiyo, Yanga ilikuwepo.



Ni ngumu kushindwa kuitaja Yanga kwenye michuano kama hii kwa kuwa ni kati ya timu kubwa hapa nchini na Afrika Mashariki kwa ujumla.



Yanga ina heshima yake, Yanga ni timu kubwa ndiyo maana ipo kwenye michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika hatua ya makundi, huwezi kuepuka kuipa sifa yake.

Lakini kinachotokea Yanga sasa kinaonekana kuanza kuzoeleka, imeshakuwa kawaida kwa Yanga kufungwa sasa, mashabiki nao wameonyesha kama vile wameanza kuzoea hali hiyo.



Kama Yanga ikishinda mchezo kila mmoja anashangaa na atakuuliza imekuwaje wakashinda? Hii ni kwa kuwa imekuwa ni kawaida kwao kufungwa.

Siku chache kabla ya kwenda Kenya, Yanga walichapwa mabao 3-1 na Azam, juzi tena wamechapwa mabao 3-1 na Kakamega, timu ambayo ilikuwa haipewi nafasi kubwa ya kufanya vizuri kwenye michuano hiyo.

Lakini ukiitazama Yanga uwanjani, mashabiki jukwaani utakubaliana nami kwamba walikuwa wanasubiri kufungwa tu na siyo jambo lingine.



Yanga wakifungwa bao moja wanasubiri kufungwa lingine, hawana wachezaji wanaojali, lakini hata wale ambao wapo uwanjani wanaona kawaida hata kama wakipoteza kwa kuwa naamini hata kocha huwaambia tumefungwa kwa kuwa hatuna fedha.

Hii ni kauli mbaya sana, kwa Yanga na itawatafuna kwa muda mrefu sana, kauli yao wanatembea nayo kwa sasa ni kuwa “Sisi ni maskini, Yanga haina hela”.



Sasa Yanga wanafungwa hata na Mbeya City wanasema hawana hela, ni kweli kuwa Yanga na Mbeya City kigezo kinakuwa na fedha? Siyo kweli.



Yanga ukiwatazama uwanjani unamuona mchezaji mmoja tu anayejituma, Papy Tshishimbi, je huyu ana fedha? Au analipwa mshahara na TP Mazembe? Hapana analipwa na Yanga, lakini anajituma mpaka wakati mwingine unaweza

kufikiri anafanya mazoezi na timu nyingine.

Hakuna sura ambayo inaonekana kukasirika kutokana na matokeo wanayopata Yanga kwa sasa, kila mmoja anaona kawaida tu.



Hii inaonyesha kuwa kupoteza mchezo kwao ni jambo la kawaida kabisa ndiyo maana hata ukimsikia kocha wao, Shadrack Nsajigwa na Noel Mwandila wakiwa wanazungumza kuhusu kupoteza mchezo wanaongea kawaida kwa kuwa wameshaaminishwa kuwa Yanga haina hela hivyo haiwezi kushinda, upuuzi.



Kwenye mchezo wa juzi dhidi ya Kakamega jukwaani walikuwa wanaonekana baadhi ya mashabiki ambao wametoka Tanzania kwenda kuishabikia timu yao wakiwa wanalia baada ya dakika tisini kumalizika na Yanga kuchapapwa mabao 3-1, hii inaonyesha kuwa wenyewe wanaumizwa na kile kinachotokea sasa kwenye timu hiyo, lakini ni kweli kuwa makocha na wachezaji wanalia kama hawa mashabiki, sidhani naona kwao ni kawaida kufungwa kwa kuwa wana kauli yao “Hatuna fedha”.



Nani anaweza kuwafuta machozi hawa mashabiki waliotumia fedha zao kuifuta timu nchini Kenya halafu ndani ya dakika 45 tu, Yanga ilishaondolewa kwenye michuano hii tena kwa aibu.

Wengine wameacha familia zao bila chakula cha kutosha kuifuta Yanga, watalipwa na nani, wameacha watoto wao hawajamaliza kulipa ada nani atawalipa na bado wanatoa machozi jukwaani.



Kuna kiongozi au mchezaji wa Yanga ambaye alilia baada ya kuona timu hiyo imepoteza mchezo wa juzi kama wale mashabiki jukwaani au walienda kwenye vyumba wakasema Yanga haina fedha?

Mashabiki wapo na Yanga sasa, wale wanaotaka kuwa viongozi kwenye timu hiyo nao wapo wapi, wale wanaotaka kugombea uenyekiti kwenye timu hiyo wapo wapi, mbona hawafanyi kazi sasa?

Kama kuna kipindi ambacho Yanga wanahitaji kufarijiwa ni sasa, kama kuna kipindi ambacho Yanga wanahitaji msaada ni sasa ambapo wanategeneza timu yao, lakini kama kuna kipindi ambacho mtu angepata uongozi bila jasho kubwa ni sasa.



Mashabiki wa Yanga sasa ndiyo wanatakiwa kufahamu nani ndugu yao, nani anaweza kuwasaidia, nani siyo ndugu yao, wale mashabiki wanafaa kuwa viongozi Yanga kuliko bosi anayetoka ofisini amevaa suti.

Yanga sasa wanatakiwa kushikamana na kuonyesha kuwa wanaweza wakati mwingine kung’ang’ania madaraka kama mambo hayaendi ni jambo baya, kama viongozi wa Yanga wanaona hakuna mwanga mbele ni vyema wakajiuzulu na kuwapa nafasi wengine, labda watawafuta machozi mashabiki wao waliokwenda Kenya.



Kwa mwenendo wa Yanga kwa sasa ni hakika inahitajika akili mpya, inahitaji watu ambao wanaweza kulia baada ya kupoteza mchezo na siyo wanaokwenda vyumbani wakisema hatuna fedha.

Hii Hapa Dawa Bora ya Nguvu za Kiume na Maumbile Madogo ya Uume

$
0
0

Tatizo hili limekuwa likiwaadhiri watu wengi sana kisaikolojia hasa baada ya kujiona wapo tofauti sana na wengine kwa kawaida mwanaume anatakiwa awe na uume kuanzia nchi 6-8 kwanza upungufu wa vichocheo hivi huchochea ukuaji wa uume chongo ambalo hushambulia nerve ambayo uharibu kabisa ukuaji wa uume, ngiri, punyeto, ambayo huathili misuli ya uume, ngiri huleta maumivu, tumbo kuunguruma na kujaa gesi, korodani moja kuvimba, kutopata choo vizuri, sababu hizi hufanya uume kulegea na kusinyaa na kuwa mfupi na mwembamba na mara nyingi hata nguvu za kiume ( hamu ya tendo la ndoa) hupungua na kwisha kabisa

GEMBE :Ni dawa inayozalisha na kukufanya uume kukua na kuongezeka
NGEMO : Ni dawa bora ya kuongeza nguvu za kiume

Hukutia hamu ya kuludia tendo la ndoa zaidi mara4 nne bila kukinai au kuchoka pia itakufanya uchelewe kufika kileleni zaidi ya dk30-45 kwa mtumiaji pia tunatibu kisukari, bp, ngiri, miguu kuwaka moto KAMA HUNAMDA WA KUFIKA OFISINI KWETU UTALETEWA POPOTE TUPO MBAGALA RANGI TATU

 0753471612/ 0715249530
0623 386 305

DR KUZENZA

Jay Z na Beyonce Wazindua Ziara Yao ya 'On The Run II...... Waanza kwq Kuwaonyesha Mapacha wao

$
0
0
Jay Z na Beyonce Wazindua Ziara Yao ya 'On The Run II......  Waanza kwq Kuwaonyesha Mapacha wao
Mastaa maarufu kutokea Marekani “The Carters” Beyonce na Jay Z wamezindua rasmi ziara yao ya muziki ‘On The Run II’ huko Cardiff, Wales Marekani, Jumatanao ya June 6,2018 ambayo itahusisha nchi mbalimbali mpaka October 4,2018.

Katika uzinduzi huo Beyonce na Jay Z walionyesha picha ya watoto wao mapacha Sir Carter na Rummy wakiwa wamewabeba na ujumbe ulioandikwa “Love is Universal” na picha hizo zimetumika kama zawadi kwa mashabiki wao.



Sir Carter na Rummy walizaliwa June 13,2017 na hivyo Beyonce aliwahi kuwapost watoto hao mara moja kwenye account yake ya instagram na hakuwahi kuwaonyesha tena katika mitandao ya kijamii.

Tanzania Yatajwa Kuwa Nchi Iliyofanikiwa

$
0
0
Tanzania Yatajwa Kuwa Nchi Iliyofanikiwa
Tanzania imetajwa kuwa nchi iliyofanikiwa kuwa na mifumo bora ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA) inayolenga kuchochea ustawi wa maisha ya wananchi hasa wanaoishi katika maeneo ya vijijini.


Akizungumza katika mahojiano maalum yaliyofanyika Jijini Mbeya leo, Mkuu wa Timu ya Mifumo ya Mawasiliano wa Mradi wa Kuimarisha Mifumo ya Sekta za Umma (PS3) Bw. Desderi Wengaa, amesema kuwa hivi sasa Tanzania ni nchi ya kupigiwa mfano kwa kuwa na mifumo bora na inayoongea, hali inayosaidia kuimarisha huduma kwa wananchi hasa wanyonge.

"Mifumo hii inalenga kuwawezesha watoa huduma katika ngazi ya vituo vyao kama Zahanati, Shule na Vituo vya Afya kutoa huduma kulingana na mahitaji ya wananchi na vipaumbele vya Serikali ambavyo kimsingi vinalenga kuwaletea wananchi maendeleo endelevu", amesema Wengaa.

Wengaa ameendelea kufafanua kwa kusema "mfumo kama wa Epicor 10.2 utasaidia Serikali kujua mapato na matumizi ya fedha za umma katika sekta za kipaumbele kama Afya na Elimu, ikiwa ni dhamira ya serikali kuhakikisha kuwa rasilimali zote, ikiwemo fedha zinatumika kuboresha maisha ya wananchi".

Aidha, Wengaa ameongeza kuwa kwa kutumia mifumo hiyo, thamani halisi ya fedha zitakazotumika katika miradi ya maendeleo itaonekana na pia itaongeza muda wa kuwahudumia wananchi katika vituo vya kutolea huduma, kwakuwa muda utakaotumika kwa kila anayehitaji huduma kuwa mchache.

PS3 ni mradi unaofadhiliwa na Serikali ya Marekani kupitia Shirika la Maendeleo ya Kimataifa la Marekani (USAID).  Mradi huo wa miaka mitano unatekelezwa katika mikoa 13 ya Tanzania bara

Kampuni ya Ndege ya Emirates Yazindua Ndege Isiyo na Madirisha

$
0
0
Kampuni ya ndege ya Emirates Yazindua Ndege Isiyo na Madirisha
Kampuni ya ndege ya Emirates imezindua ndege ambayo imetengezwa na madirisha bandia

Badala ya abiria kuweza kuona nje moja kwa moja, sasa watalazimika kutazama picha kutoka nje wakiwa ndani kwa kutumia kamera za fibre-optic

Emirates inasema kuwa hatua hiyo inatoa fursa ya kuondoa madirisha yote katika ndege za siku zijazo, swala litakalozifanya kuwa nyepesi na kuongeza kasi yake.

Rais wa Emirates Sir Tim Clark amesema kuwa picha hizo ni nzuri sana ikilinganishwa na picha zinazotazamwa kwa macho.

Wafanyikazi wa ndege wanatakiwa kuona nje ya ndege iwapo kuna dharura, mtaalam wa usalama wa angani Profesa Graham Braithwaite wa chuo kikuu cha Cranfield University alisema.

"Kuweza kuona nje ya ndege katika dharura ni muhimu, hususan wakati ambapo dharura ya uokoaji inafaa kutekelezwa'', alisema.

"Wahudumu wa ndege watalazimika kuona nje katika dharura , kwa mfano wakati wa moto, kabla ya kufungua mlango na kuanza uokoaji- na kitu chochote ambacho kitahitaji nguvu kufanya hivyo haitakuwa rahisi kuidhinishwa na afisa wa usalama wa angani''.

Hatahivyo maafisa wa usalama wa angani kutoka mamlak ya kudhitibi anga barani Ulaya European Aviation Safety Agency alisema: Hatuoni changamoto yoyote ambayo haiwezi kukabiliwa ili kuhakikisha kuwa kiwango cha usalama sawasawa na kile cha ndege ambayo ina madirisha ya wahudumu wa ndege.

Profesa Braithwaite alisema kwamba kizuizi kikuu katika ndege isiyo na madirisha itakuwa abiria wanavyohisi kuhusu teknolojia hiyo.

Maneno ya Jux Kwenye Birthday ya Vanessa Mdee "Swala la Kukupa Furaha Mimi Mwenyewe Nalimaliza Nakupenda Sana"

$
0
0
Maneno ya Jux Kwenye Birthday ya Vanessa Mdee "Swala la Kukupa Furaha Mimi Mwenyewe Nalimaliza Nakupenda Sana"
Kila mwaka ifikapo June 7 huwa ni siku muhimu kwa staa wa kike katika game ya muziki wa Bongofleva Vanessa Mdee, kwani huwa ni kumbukumbu ya siku yake ya kuzaliwa (Birthday).

Leo June 7,2018 Vanessa Mdee anasherehekea  siku yake ya kuzaliwa akiwa Gabon Brazzavile, Vanessa amepostiwa na watu mbalimbali katika mitandoa ya kijamii kumtakia kheri ya kumbukumbu ya siku ya kuzaliwa.

Jux ameamua kumpost Vanessa na kuandika maneno yanayodhihirisha upendo wake kwa mpenzi wake Vanessa ambaye anasherehekea Birthday yake ya kutimiza miaka 30.

Jux ameandika “Sijui niseme nini kitachoweza kubeba uzito wa thamani yako kwenye maisha yangu @vanessamdee Nitaendelea kumuomba mungu kila siku 🙏🙏 Akupe maisha marefu na afya bora.

“Swala la kukupa furahaa mimi mwenyewe nalimaliza vizuri kabisa Nakupenda sana my love #happybirthday KHAUSA bado naendelea sijamaliza  🎉🎉🎉🎉🎉🎉”

Pierre Nkurunziza Atangaza Kuachia Madaraka 2020 Burundi

$
0
0
Pierre Nkurunziza Kuachia Madaraka 2020 Burundi
Rais wa Burundi Pierre Nkurunziza amesema kwamba hataomba kuchaguliwa tena baada ya muhula wake wa sasa kumalizika mwaka 2020.

Ametoa tangazo hilo akiwa eneo la Bugendana, Gitega ambapo alikuwa anaidhinisha katiba mpya ya nchi hiyo.

Mwezi uliopita, raia nchini humo walipiga kura na kuunga mkono kwa wingi marekebisho ya katiba ambayo yalifanyia marekebisho katiba ya nchi hiyo kubadilisha muhula wa rais kutoka miaka mitano kuwa saba.

Mwandishi wa BBC Bujumbura Ismail Misigaro amesema kwa sasa wengi wanatarajiwa kutakuwa na mabadiliko katika baraza la mawaziri karibuni.

Wapiga kura waidhinisha marekebisho ya katiba Burundi
Wengi waliamini Bw Nkurunziza ndiye aliyeshinikiza kufanyika kwa kura hiyo ya maoni ili kumpa fursa ya kuongoza taifa hilo hadi mwaka 2034.

Matokeo yaliyotolewa na tume hiyo yalionesha waliokuwa wanaunga mkono marekebisho hayo walikuwa 73.6%.

Waliokuwa wanapinga walikuwa19.3% ilhali kura 4.1% ziliharibika.

Asilimia 3.2 ya wapiga kura hawakuunga mkono upande wowote.

Wapiga kura zaidi ya 98% ya waliojiandikisha kuwa wapiga kura nchini humo hawakushiriki shughuli hiyo.

Rais wa Burundi walikuwa wanaamua iwapo muda wa muhula wa rais uongezwe kutoka miaka mitano hadi miaka saba, yenye kikomo cha mihula miwili.

Marekebisho hayo ya katiba yanamruhusu Nkurunziza kuwania uchaguzi wa mwaka 2020 na angeweza kuwania kwa mihula mingine miwili chini ya katiba mpya, kwani kuhesabiwa kwa mihula kungeanza tena baada ya mwaka huo.

Burundi ina historia ya machafuko tangu miaka ya 60, mabaya zaidi yakiwa ya miaka ya 90 ambapo vita vya wenyewe kwa wenyewe vilisababisha vifo vya zaidi ya watu 300,000.

Mkataba wa Amani uliotiwa sahihi Arusha ndio ulimaliza vita hivyo na kumwezesha Pierre Nkurunziza kuwa rais.

Alitarajiwa kuondoka madarakani mwaka 2015 lakini akaamua kuwania kwa muhula mwingine.

Muziki wa Diamond unakosha roho hata kwa sisi wazee – Mrema

$
0
0
Muziki wa Diamond unakosha roho hata kwa sisi wazee – Mrema
Mwenyekiti wa Bodi ya Taifa ya Parole, Augustino Mrema amesema msanii wa Bongo Flava anayemfuatilia kwa sana ni Diamond Platnumz.

Ameeleza sababu ya kumfuatilia muimbaji huyo ni kutokana na kujituma kwake na muziki wake unavutia.

“Namfuatilia sana Diamond, ni kijana mdogo, muimbaji mahiri, yaani Diamond asaidiwe naona hatima yake katika maisha yake na nchi yetu atatufikisha mahali pazuri. Kwa muziki wake unakosha roho, hata sisi wazee, mimi naridhika sana,” Mrema ameiambia Times FM.

Katika hatua nyingine ametoa wito kwa serikali kuwa karibu zaidi na wasanii, hata hivyo amesema anaziona jitihada za Waziri wa Habari, Utamaduni Sanaa na Michezo, Dk. Harrison Mwakyembe za kukutana na wasanii kila mara hasa pale wanapopata matatizo na kuwasaidia.

Ilivyokuwa studio Sam wa Ukweli akirekodi wimbo wake kabla ya kifo

$
0
0
Msanii wa Bongo Fleva, Salum Mohamed maarufu ‘Sam wa Ukweli’ amefariki dunia usiku wa kuamkia leo June 7, 2018  katika hospitali ya Palestina, Sinza baada ya kuugua.

Huu hapa ni wimbo ambao ulimfanya alale studio siku nne akiusubiri umalizike mpaka alipozidiwa na umauti kumkuta unaitwa ‘Walimwengu’

Bonyeza PLAY hapa chini kuutazama.

Ongeza Nguvu za Kiume na Hamu ya Tendo Hata Kwa Wenye Kisukari na BP

$
0
0

👇👇
Tatizo la upungufu wa nguvu za kiume au ukosefu wa hamu ya tendo la ndoa limezidi kuongezeka kwa kasi duniani kote na limekuwa chanzo kikubwa cha ndoa nyingi na mahusiano kukosa uaminifu kutokana na wengi kutoka nje ya ndoa ili kupata mtu atakayemtosheleza na kumfikisha kileleni. Pia udogo wa maumbile ni tatizo kubwa na limekuwa likiwakosesha wanaume wengi uwezo wa kujiamini katika tendo na kusababisha tendo hilo kutokufanyika kwa usahihi. Hili pia huchangia kwa kiasi kikubwa wanawake wengi kwenda nje ya ndoa ( MAHUSIANO) kutafuta mbadala wake.
BAADHI YA DALILI ZA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME NI KAMA:-
☆Kukosa hamu ya tendo la ndoa
☆Uume kusimama kwa ulegevu
☆Kuwahi kufika kileleni
☆Uume kusinyaa katikati ya tendo
☆Kushindwa kurudia tendo kwa wakati
☆Kuchoka sana baada ya round ya kwanza na hata kukinai kabisa.

Kwa kutumia mimea tiba na matunda bila kemikali sasa
@markson_beauty_pr Tunakuletea suluhisho la matatizo hayo hata kwa wenye "KISUKARI NA PRESSURE" kwa:-
1.HANDSOME UP ORIGINAL:- kifaa chenye uwezo wa 99% kuongeza uume kwa size uipendayo na kuimarisha misuli ya uume iliyolegea @250,000/=
2.SHARK POWER ni gely ya kupaka inayoongeza uume kwa wastani wa inch 5.5 hadi 6 @150,000/=
3.VigRX CREAM:- ni gely iliyoboreshwa mahususi kwa ajili ya kuongeza maumbile kwa wastani wa inch 6.5 hadi 8 na kuimarisha misuli ya uume iliyolegea @200,000/=
4.Vidonge maalum kwa ajili ya kuongeza nguvu na hamu ya tendo la ndoa hata kwa wenye kisukari @150,000/=
5.Spray ya kuchelewesha kufika kileleni na kuweza kurudia tendo ×3. @150,000/=
BIDHAA HIZI HAZINA MADHARA KIAFYA NA ZIMETHIBITISHWA
NA SHIRIKA LA AFYA DUNIANI (WHO).
KWA BIDHAA HIZI NA NYINGINE NYINGI TEMBELEA UKURASA WETU WA INSTAGRAM :-
@markson_beauty_pr
@markson_beauty_pr
@markson_beauty_pr
WEB:www.markbeauty.org
Wasiliana nasi Popote
ulipo duniani kwa (+255)
0767447444 na
0714335378
UTAPATA HUDUMA
NB:Matokeo ni uhakika na garantii na hakikisha unapata risiti yenye muhuri halisi wa MARKSON CO pamoja na garantii ili kukuhakikishia kufanikiwa kwako.
#OngezaUume
#NguvuZaKiume
#HandsomeUpOg
#BidhaaTz
Viewing all 104795 articles
Browse latest View live




Latest Images