Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104809 articles
Browse latest View live

Serikali: “Tutapandisha Mishahara Hali Ikiruhusu”

$
0
0
Serikali Yaahidi Kuongeza Mishahara Hali Ikiruhusu
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Utumishi wa Umma na Utawala Bora, George Mkuchika amesema kuwa serikali itaweza kuboresha maslahi ya watumishi wa umma nchini kwa kuongeza mishahara kulingana na uwezo wa Serikali.


Waziri Mkuchika, amesema hayo leo Juni 8, 2018 Bungeni, Jijini Dodoma akielezea ni kwa namna gani Serikali inawajali watumishi swali lililoulizwa Mbunge wa viti maalumu Catherine Magige na kuongeza kuwa Serikali inafanya jitihada za kuwajali watumishi kwa kuwapa mikopo, mafunzo na kudhamini masomo kwa baadhi ya watumishi wanaosoma taaaluma mbalimbali.

“Kujali mtumishi sio lazima fedha, hata ukimpeleka kwa mafunzo umemjali mtumishi, niseme tu kifupi kwamba tunaendelea kuboresha maslahi ya watumishi wa umma lakini kwa upande wa mishahara, tutaipandisha hali ya nchi ikiruhusu”, amesema Mkuchika.

Waziri huyo ameongeza kuwa Serikali haitasubiri sikukuu ya wafanyakazi (Mei Mosi) ili itangaze kupanda kwa mishahara bali muda wowote amabapo itajiridhisha na hali ya mfuko wa serikali basi itapandisha mishahara.


Baada ya Vifo vya Watu 10 Kigoma..... Serikali Kujenga Vizuizi Kuzuia Magari Kugonga Treni

$
0
0
Baada ya Vifo vya Watu 10 Kigoma..... Serikali Kujenga Vizuizi Kuzuia Magari Kugonga Treni
Katika kudhibiti ajali katika maeneo ambayo barabara imepishana na reli, Serikali imesema itahakikisha inajenga vizuizi katika maeneo hayo ili magari yawe yanasimama wakati treni ikipita.

Hayo yameelezwa leo Ijumaa Juni 8, 2018 na mkuu wa wilaya ya Kigoma, Samson Anga ikiwa zimepita siku mbili tangu kutokea ajali ya basi dogo lililogonga treni eneo la Gungu mkoani Kigoma na kusababisha vifo vya watu 10 na wengine 35 kujeruhiwa.

“Haiwezekani watu wapoteze maisha kwa sababu ya uzembe wa baadhi ya madereva. Tumechoka kuona hali hii ikiendelea na lazima tuchukue hatua kuokoa maisha ya binadamu wenzetu," amesema.

Amesema ujenzi wa vivuko utahusisha wakala wa barabara (Tanroads) na Shirika la Reli Tanzania(TRC) ambao wataratibu na kujenga vizuizi hivyo.

Maeneo ambayo reli imepishana na barabara mkoani Kigoma ni Kibirizi, Gungu, Nyamoli, Kazuramimba, Uvinza, Tubira na Malagalasi.

Nacte Yakifutia Usajili Chuo cha Royal College na Vingine 20

$
0
0
Nacte Yakifutia Usajili Chuo cha Royal College na  Vingine  20
Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi (Nacte) limefuta usajili wa vyuo 20 baada ya kushindwa kufuata sheria zinazoendana na matakwa ya usajili wa vyuo hivyo.

Akizungumza leo Juni 8, Kaimu Katibu Mtendaji wa baraza hilo Dk Adolf Rutayuga amesema uamuzi huo umefikiwa baada ya kufanyika kwa ukaguzi wa vyuo 458 na 32 vilikutwa na mapungufu.

Sanjari na 20 vilivyofungiwa vyuo tisa vimezuiliwa kudahili wanafunzi wapya huku vyuo vitatu vikitakiwa kusitisha baadhi ya kozi walizokuwa wakitoa bila idhini ya baraza.

Dk Rutayuga amesema tayari baraza hilo limeshaviandikia barua vyuo 20 vilivyofungiwa kuvitaka vihakikishe kuwa wanafunzi wanahamia kwenye vyuo vingine.

Vyuo vilivyofutiwa usajili ni Royal College, Covenant College of Business Studies,  Mugerezi Spatial Technology College, Techno Brain, Lisbon Business College, PCTL Training Institute na Mlimani School of Professional Studies vyote vya Dar es Salaam.

Vingine ni Regency School of Hygiene, St Peters College of Health Sciences, Genesis Institute of Social Science, Institute of Management and Information Technology na Boston City Campus of Business College.

Vingine ni Arusha Institute of Technology, East African Institute of Enteprenuership and Financial Management (Arusha) Iringa RETCO Business College (Iringa) na Musoma Utalii College (Musoma).

Vipo pia Highlands Health Institute (Njombe),  Institute of Social Work na Dinobb Institute of Science and Business Technology (Mbeya).

Picha: Ridhiwani Kikwete, Fid Q na Wasanii washiriki Msiba wa Sam wa Ukweli Bagamoyo

$
0
0
Picha: Ridhiwani Kikwete, Fid Q na Wasanii washiriki Msiba wa Sam wa Ukweli Bagamoyo
Leo June 08, 2018 ndipo anapumzishwa katika makazi yake ya milele msanii wa Bongo Flava, Sam wa Uweli ambaye alifariki hapo jana.

Umati wa watu umejitokeza nyumbani kwao Bagamoyo ambapo anazikwa leo, wasanii wenzake nao pia wamehudhuria msiba huo. Picha zaidi na video.

Mwakyembe Aipongeza Simba Kuingia Fainal SportPesa " Kwa Hili Mmethibitisha Hamkubahatisha VPL"

$
0
0
Mwakyembe Aipongeza Simba Kuingia Fainal SportPesa " Kwa Hili Mmethibitisha Hamkubahatisha VPL"
Waziri wa Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo, Harrison Mwakyembe, amewapongeza Simba kufanikiwa kutinga hatua ya fainali ya michuano ya SportPesa Super Cup nchini Kenya.

Simba imefanikiwa kufika hatua hiyo baada ya ushindi wa changamoto ya mikwaju ya penati wa mabao 5-4 dhidi ya Kakamega HomeBoyz FC ikiwa ni baada ya dakika 90 kumalizka kwa sare tasa ya 0-0.

Akizungumza bungeni mjini Dodoma, Mwakyembe amefunguka na kueleza Simba wamethibitisha kuchukua ubingwa wa Ligi Kuu Vodacom si kwa kubahatisha mpaka kufikia hatua hiyo ya kucheza fainali na Gor Mahia.

"Napenda kuchukua fursa hii kuwapongeza Simba kwa kufanikiwa kutinga fainali ya SportPesa Super Kenya, wamethibitisha kuwa walichukua ubingwa wa ligi si kwa kubahatisha kwa soka la kiwango" amesema.

Mchezo wa fainali ya mashindano hayo utachezwa kwenye Uwanja uleule wa Afraha Jumapili ya wiki hii ambapo bingwa wa michuano hiyo atacheza dhidi ya Everton kwenye Uwanja wa Goodison Park nchini England.

Wasiliana na Dr Mabula Anatibu Upungufu wa Nguvu za Kiume, Busha na Matatizo ya Maumbile Madogo kwa Mwanaume

$
0
0
TUNATIBU NA KUPONESHA KABISA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME UUME MDOGO BUSHA BILA KUPASUA PRESHA VIDONDA VYA TUMBO
Asilimia kubwa ya wanadamu wanasumbuliwa na magonjwa mbalimbali na wapo waliongahika sehemu mbalimbali bira MAFANIKIO MABULA CLINIC ni kituo cha tiba asilia kilichopo mbagara zakhemu njia kuu ya JESHINI JE HUNAUPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME AU UUME WAKO MDOGO NA MWEMBAMBA?

MAPRO PAWER NO 2 ndio Tiba kwa sasa utibu matatizo matatu kwa pamoja 1hitakufanya uchelewe kufika kilekeni dikika 15-20 kwa tendo la kwanza 2 uhimalisha misuli iliyoregea na kusinyaa hasa kwa wale walio hasirika na upigaji punyeto 3 itakufanya upate amu ya kurudia tendo zaidi ya Mara tatu

KWA NINI UJIONE MPWEKE PALE UKUTANAPO NA MPENZI AU MKE WAKO kisa unawai kukojoa au unakomea bao moja tu na huku dawa zipo MAKAKANUA mix ni dawa iliyochanganywa na miti Shamba 9 na Kuwa na uwezo wa kuongeza uume saizi upendayo inchi 5-8 Kwa Urefu na unene sentimita 1-5 dawa hizi hazina madhara yoyote kwa mtumiaji ata wazee wenye umri mkubwa wanapona? zipo dawa za mvuto wa mpenzi mme au mke Kwa masaa matatu tu na kukupigia simu yeye mwenyewe mvuto wa biashara kutengeneza mwonekano mzuri wa mwili kwa wanawake yani shepu tunatibu ngiri miguu mgongo na kiuno kuumwa kupunguza kitambi minyama uzembe matiti na mwili mkubwa

TIBA NA USHAULI MUONE DR MABULA AU PIGA SIMU NO 0752348593 UDUMA ZANGU UTAZIPATA POPOTE ULIPO KAMA UWEZI KUFIKA OFISINI

Mjengo Uliomponza Hamisa Mobetto Wanaswa

$
0
0
UMENASWA! Ndivyo unavyoweza kusema kwani kila mtu alikuwa na hamu ya kuuona mjengo unaodaiwa kusababisha ugomvi kati ya familia ya Nasibu Abdul ‘Diamond’ na Hamisa Mobeto.

Baada ya wenye ubuyu wao hivi karibuni kueneza taarifa kwamba mama wa mwanamuziki huyo, Sanura Kasim ‘Bi Sandra’ na wanafamilia wengine wanaomuunga mkono wamenunia kile kinachohisiwa kuwa Diamond amempangia Mobeto mjengo wa gharama, ambapo OFM juzikati waliamua kuufungia kazi na kuusaka.

Sakasaka kila kona ya Jiji la Dar, mara paaa; timu ya wanasa vya mafichoni ya Amani ilitinga eneo la Bahari Beach, Tegeta ambako inadaiwa mwanadada huyo mwenye fani ya mitindo nchini amepangishiwa nyumba ya ghorofa na mzazi mwenzake ikimaanishwa Diamond.



KWA NINI WAMENUNA?

Sosi alidai kuwa familia ya Diamond hasa mama yake hawapendi wanawake wanaopenda kitumia ‘kitonga’ kwa kumchuna pesa mwanamuziki huyo.

“Zari hatoki midomoni mwao kwa kuwa ni mwanamke anayejiweza, lakini hawa wenzangu na mimi akina Mobeto hata kama wanatumia fedha zao kufanya vitu, familia inajua wamepewa na Diamond.

“Ndicho kilichomponza Mobeto, hizi chokochoko nyingine zote ni za nyongeza tu, lakini nyumba hiyo ndiyo mchawi mwenyewe,” sosi alidai.


OFM KAZINI TEGETA

Kuna maeneo hapa Dar ukiyaingia inabidi kichwa kinase vizuri netiweki vinginevyo unaweza kugeuka kioja watu wakakucheka, walipoibukia OFM hapo Bahari Beach si pa kitoto, ilikuwa ni kujiuliza; “ni ipi sasa kati ya hizi?”

Baada ya ukaguzi ulioenda shule wa OFM, kikosi kazi makini kilibaini kuwa moja kati ya majumba mazuri yaliyokuwa mbele yao ni mjengo anaoishi Mobeto, macho yalikula nakshi si za kitoto kwenye nyumba hiyo.



Mjengo huo ni balaa, kwanza mtaa wenyewe ni uzunguni hasa maana hauna kelele na nyumba zote zilizopo eneo hilo ni za hadhi ya wenye nazo, angalia hata picha ukurasa wa mbele unadhani kwa akina Kayumba utaziona nyumba kama hizo?

Hata hivyo, wazee wa kazi zao walifika hadi kwenye geti la nyumba hiyo inayodaiwa anaishi Mobeto kisha kugonga geti lakini wenyeji hawakuitikia.

Ndani ya mjengo huo zilisikika sauti za watu zikiongea, hapo ndipo OFM ilipoingia shaka kidogo kwamba huenda si kwa Mobeto, maana ni vipi asiitikie hodi za wageni, anaringia kitu gani?



UAMUZI WA KUHAKIKISHA

Kwa wachunguzi wetu suala la kubahatisha halitakiwi kupewa nafasi, baada ya wasiwasi ambao siku zote ndiyo akili kuibuka ikabidi makamanda washauriane kufanya uhakiki wa anayeishi kwenye nyumba hiyo.

Mtu wa kwanza kufika katika akili za mmoja wa makamanda wa OFM alikuwa ni Balozi wa Shina Namba 6, aitwaye Claud Andrew Kayako wa Mtaa huo anaoishi Mobeto kwamba angetegua haraka kitendawili cha uhakika uliohitajika.


MSIKIE BALOZI

Balozi huyo alieleza kuwa anao uhakika kuwa Hamisa anaishi mtaani pale na kuonesha jengo husika (Picha ukurasa wa mbele) na kwamba anaishi na ndugu zake.

“Kweli alihamia hapa ila tarehe siikumbuki, ni siku za hivi karibuni.

“Yupo hapa na anaishi yeye pamoja na mama yake na watoto zake wawili, na ndugu yake mwingine anaitwa Mwajuma na mwingine wa kiume lakini simjui jina.

“Mama yake na ndugu zake huwa wanatusalimia kutujulia hali, na yeye huwa tunamuona akitoka na gari la rangi ya bluu bahari na kwenda kwenye shughuli zake. Mama yake huwa anatoka na gari nyeupe,’’alisema Claud akiziacha kwatu roho za makamanda wa OFM.”



HADHI YA NYUMBA

Kama ilivyoelezwa, mjengo anaoishi Mobeto si wa kitoto, kwa muonekano wa macho tu lakini hata hadhi yake ukiutazama unaupa thamani ya mamilioni.

“Ni nyumba ya gharama sana, hata kodi yake inaweza kufikia milioni 3 kwa mwezi, maana ile pale (anaonesha nyumba nyingine jirani) rafiki yangu amepanga kila mwezi analipa milioni mbili na nusu, ndani kaweka hadi ofisi,” kijana mmoja anayeishi eneo hilo ambaye hakutaka kutaja jina aliliambia Amani kujaribu kusaidia ukadiriaji wa kodi ya pango.



MOBETO NA KODI YA MIL. 3?

Hivi huyu dada huwa anafanya kazi gani zaidi ya huo uanamitindo wake?

Ina maana ana hela za kuweza kupanga nyumba ya milioni 3 kwa mwezi kwa usawa huu?

Kama anahongwa ndiyo ahongwe milioni 3 za nyumba tu; hizo ni mbali na za mavazi, chakula, mapambo na mambo mengine, ama kweli huyo anayemhonga atakuwa na ‘mihela’.


UNAJIULIZA PAMOJA NASI

Kama ambavyo ulikuwa ukisisimka ulipokuwa ukisoma viulizo hapo juu, wengi katika mijadala wamekuwa wakiuliza ughali wa maisha ya mastaa wa kike Bongo ukilinganishwa na kipato chao na si kwa Mobeto tu.



Hata hivyo uchunguzi uliofanywa na Amani mara kadhaa umekuwa ukibaini kuwa, kazi za wazi wanazozifanya mastaa wa kike hapa Bongo ni muziki, uigizaji, uanamitindo na sanaa nyingine ambazo kwa namna moja ama nyingine haziwawezeshi kuishi maisha ya anasa.

Pengine maswali ya wengi katika maisha ya mastaa wetu ni ‘wapi wanapata hizo fedha za ziada’, wapo watu wamekuwa wakiwahukumu kuwa huenda wanafanya biashara ya ukahaba, jambo ambalo Amani haliwezi kuliamini hata kama itakuwa kweli kwa sababu haijapata hoja za kuweka mkononi.



NI LAZIMA MOBETO APANGISHIWE?

Pamoja na kwamba Mobeto amekuwa mgumu kupokea simu lakini bado haiwezi kuwa sawa kumtuhumu kuwa amepangishiwa nyumba na Diamond kwa sababu hana ulazima.

Inawezekana katika kipato na jasho lake anaweza kuwa na huo uwezo wa kufanya ‘fujo mjini’ ili kufurahia maisha na familia yake kama waswahili wasemavyo; ukipata tumia, ukikosa jutia.

Maana ubuyu mwingine uliopo mjini ni kwamba mwanamitindo huyo anamiliki duka kubwa la nguo maeneo ya Kijitonyama, duka ambalo nalo wambeya wa mjini wamekuwa wakisema amefunguliwa na Diamond bila kuweka ushahidi mezani.



PICHA BADO LINAENDELEA

Picha la familia ya Diamond na Mobeto bado linaendelea mpaka hapo kitakapoeleweka kati ya Zari na Mobeto atakayekuwa mkwe halali wa familia hiyo kwani pande bado zinavutana, wapo wanaomtaka Zari lakini wapo wanaomtaka Mobeto.



NENO LA MHARIRI

Gazeti hili linamsihi Diamond kuangalia furaha yake kwani mwisho wa yote yeye ndiye atakayeingia kwenye ndoa na kuishi maisha ya kindoa, ausikilize moyo wake, iwapo utaangukia kwa Hamisa basi heri lakini kama moyo utaangukia kwa Zari nayo ni heri kwani wote ni wazazi wenzake au ikiwezekana afunge nao ndoa wote wawili kwani dini yake inamruhusu.

Hali si Shwari Yanga..Yaamua Kujitoa Kombe la Kagame

$
0
0
Uongozi wa klabu ya Yanga umeandika barua kwenda TFF kuiomba kujitoa katika mashindano ya Kagame Cup yanayotarajiwa kuanza Juni 29 mpaka Julai 13, 2018 jijini Dar es Salaam

 Sababu za msingi za kujitoa Kagame Cup ni kufanya maandalizi kwa ajili ya michunao ya Kombe la Shirikisho Afrika ambapo watacheza na Gor Mahia FC ya Kenya, Julai 18, 2018 jijini Nairobi

 Kutokana na muingiliano wa ratiba ya Kagame Cup na Michuano ya Shirikisho, Yanga imeona ni vema kuwapatia wachezaji wao mapumziko ili kuwapa fursa ya kujiandaa vizuri

 Katika ratiba ya michuano hiyo ya Kagame, Simba na Yanga zimepangwa pamoja kwenye kundi C ambapo kuna timu zingine ambazo ni Dakadaha ya Somalia pamoja na St. George kutoka Ethiopia

Binti wa Kazi Amuua Bosi Wake Pamoja na Mwanae

$
0
0

Jeshi la Polisi katika eneo la Kisumu, nchini Kenya, linamtafuta msichana ambaye ni msaidizi wa kazi za nyumbani kwa tuhuma za kumuuwa muajiri wake na mtoto wa miezi mitatu ambaye ni wa muajiri huyo.

Kwa mujibu Citizen Kenya imeripoti leo Juni 8, 2018 na mashahidi katika eneo hilo, wamedai kwamba tukio hilo limetokea usiku wa kuamkia Alhamisi, Juni 7, 2018 na ilipofika saa 2:00 usiku waliamua kuvunja mlango wa nyumba ambao ulikuwa umefungwa kwa siku nzima ya jana jambo ambalo halikuwa la kawaida

Mwili wa marehemu aliyejulikana kwa jina la Elizabeth Ojwang, ulikutwa umeviringishwa mfuko wa plastiki shingoni, kando na mwili wa mtoto wake uliokutwa na majeraha mbalimbali katika mwili yaliyosababishwa na kuchomwa na kitu chenye ncha kali.

Akithibitisha tukio hilo kamanda Jeshi la Polisi, kaunti ya Muhoroni, John Kamau amesema kwamba Jeshi hilo linaendelea kumtafuta binti wa kazi kwa mahojiano ambaye alitoweka baada tukio hilo na kuongeza kuwa msichana huyo anaweza kuwa mtuhumiwa wa kwanza wa mauji hayo.

Sababu kubwa ya mauaji hayo bado haijajulikana, Jeshi la Polisi ilichukua miili ya marehemu hao na kupelekwa katika chumba cha kuhifadhia maiti Hospitali ya Kisumu kwa uchunguzi zaidi

Menejiment BOT Yahojiwa na PAC....Ripoti Kukabidhiwa kwa Spika Jumatatu

$
0
0


Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC) imemaliza kazi ya kuwahoji Bodi na Menejimenti ya Benki Kuu ya Tanzania (BoT) juu ya tuhuma zinazowakabili za kutumia bima binafsi ya afya badala ya Bima ya Taifa ya Afya (NHIF).

Bodi na Menejimenti ya BoT wamefika mbele ya kamati ya PAC kujibu tuhuma hizo ambazo ziliibuliwa bungeni Juni 4 na Mbunge wa Ulanga (CCM), Goodluck Mlinga.

Mwenyekiti wa PAC, Naghenjwa Kaboyoka amesema, wameshazungumza na Bodi na Menejimenti ya BoT pamoja na NHIF.

“Kwa kuwa ni agizo la Mheshimiwa Spika (Job Ndugai), tunakamilisha kuandaa taarifa na Jumatatu (Juni 11, 2018) tutamkabidhi,” ameongeza Kaboyoka ambaye pia ni Mbunge wa Same Mashariki (Chadema).

Bodi na Menejimenti ya BoT ikiongozwa na Gavana wa Benki hiyo, Profesa Florens Luoga pia wamehudhuria kikao cha 47, Mkutano wa 11 leo na kutambulishwa na Mwenyekiti wa Bunge, Andrew Chenge.

Ni Nani Aliyekutuma Kuoa Mwanamke Flat Screen?

$
0
0
Naongea na wanaume wenzangu wale walio owa wanawake wenye makalio madogo halafu wakiona wa wenzao wenye makalio makubwa wanaanza kupiga mikelele.

Utakuta uko na mkeo matembezini uku kafungashia kidogo basi mijanaume isiyokuwa na akili inaanza kupiga mayowe oh wakubwa wanafaidi ohh marshallah.


Kwanini na wewe usioe au kutafuta mwanamke mwenye makalio na ukaacha kutamani vya wenzao. Kwanza unamkosea adabu mwanaume mwenzio kupiga miyowe utadhani umeona utupu wa mzazi wako.

Acheni ujinga tuacheni tuenjoy na wake zetu maana hatukuwatuma kuoa flat screen.

By Nitonye

Masunzu Power Mix Dawa Bora ya Nguvu za Kiume na Maumbile Madogo

$
0
0

MASUNZU POWER MIX DAWA BORA YA NGUVU ZA KIUME NA MAUMBILE MADOGO

🌸MASUNZU POWER MIX ni dawa ya asilia yenye mchanganyiko wa mitishamba 7 yenye maajabu yafuatayo (1) inatibu upungufu wa nguvu za kiume Mara dufu na kuimalisha uume uliolegea wakati wa tendo la ndoa (2) kurefusha uume uliorudi ndani nchi 5-8 (3) kunenepesha uume sm4 ya upana itakufanya uchelewe kufika kileleni dk (15-20) kwa tendo la kwanza na utakuwa nauwezo wa kurudia tendo la ndoa Mara (2-4) bila hamu kuisha nainatibu kabisa. Dawa hii haina madhara yoyote kwa mtumiaji huanza kufanya kazi baada ya dk 50 tu 🌾🌾🌾🌾🌾🌾🌾🌾

MATATIZO HAYA HUSABABISHWA NA ngiri. au umejichua kwa muda mrefu. Punyeto kisukari. Presha. Tumbo kujaa gesi na kuunguruma chini ya Kitovu. Kutopata choo vizuri. Msongo wa mawazo. Kaswende. Gono. Haya yote husababisha kuwa na maubile madogo na kukosa nguvu za kiume

🌸SOSOMA DX. ni dawa ya kumvuta mme au mke au mpenzi wako arudi haraka na kuanza mapenzi mapya kama mlivyo anza mwanzo baada ya masaa 2 atarudi na kutulia ndani ya nyumba na kutimiza ahadi yako

🌸GINDU EXTRA ni dawa ya kutibu kisukari siku 14 unapona kabisa hata kama imepanda itashuka haraka Sana. Tunatibu busha bila upasuaji nk. Dar es salaam tunapatikana buguruni chama au unaweza kuletewa popote ulipo

Wasiliana na tabibu ATHUMAN SIMU +255673552294 / +255784552299

Mtoto Afariki Akiombewa na Mchungaji

$
0
0
Mtoto Afariki Akiombewa na Mchungaji
Nakusogezea stori kumhusu Mtoto ambaye ni mgonjwa ambapo amefariki baada ya wazazi wake kumpeleka kuombewa na Mchungaji wa kanisa la ‘Kanitha Ya Ngai’ ambaye haruhusu waumini wake kutumia tiba za kisasa.

Wazazi hao kwa sasa wamekamatwa na Polisi katika kijiji cha Kinungi kaunti ya Nakuru nchini Kenya huku Mchungaji huyo akitokomea kusikojulikana.

Katika eneo la Kinungi kunatajwa kuwa na waumini wengi wa kanisa hilo ambao hawaamini katika tiba za kisasa.

Mzazi wa kwanza kukamatwa alikuwa ni mzazi wa kike ambaye alikamatwa baada ya kwenda kuomba kibali cha kumzika mtoto wake kwa Chifu wa eneo hilo.

Kwa mujibu wa Chifu, visa vingi vya waumini hao vimeongezeka sana kwa siku za hivi karibuni na amesema kuwa kwa sasa wanamtafuta mchungaji huyo ambaye amekimbia baada ya kusikia anatafutwa ili ahojiwe.

Shaaban Chilunda Amechaguliwa Kuwa Mchezaji Bora VPL

$
0
0
Shaaban Chilunda Amechaguliwa Kuwa Mchezaji Bora VPL
Mchezaji wa Klabu Bingwa ya Afrika Mashariki na Kati Azam FC, Shaaban Idd Chilunda amechaguliwa kuwa mchezaji bora wa ligi kuu soka Tanzania Bara (VPL) kwa mwezi Mei.


Hayo yamebainishwa na taarifa zilizotolewa na uongozi wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) alasiri ya leo Juni 08, 2018 na kusema Chilunda alitwaa tuzo hiyo baada ya kuwashinda wenzake wawili, Jacob Massawe wa Ndanda na Edward Shija wa Kagera Sugar katika uchambuzi uliofanywa wiki hii na kamati ya tuzo hizo.

Chilunda aliisaidia Azam FC akifunga mabao 6 kwa mwezi huo, ambapo kati ya mabao hayo matatu 'hat trick' alifunga katika mchezo mmoja.

Kwa mwezi huo Azam ilicheza michezo minne na kupata pointi tisa, baada ya kushinda michezo mitatu na kufungwa mmoja ikibaki katika nafasi yake ya pili na hakuwa na kadi yoyote. Kwa upande wa Shija aliisaidia Kagera Sugar kupata pointi 10, akifunga mabao matatu katika michezo minne iliyocheza timu yake, ikishinda mitatu na kutoka sare mmoja na kupanda kutoka nafasi ya 12 iliyokuwepo mwezi Aprili hadi ya tisa.

Massawe alitoa mchango mkubwa katika kufanikisha timu yake kuepuka kushuka daraja ikiwa ni pamoja na kufunga mabao matatu, akiisaidia kushinda mechi mbili kati ya nne walizocheza na hivyo kupanda katika msimamo wa ligi kutoka nafasi ya 15 hadi ya 14 katika timu 16 zilizoshiriki ligi hiyo.

Kutokana na ushindi huo, Chilunda atazawadiwa tuzo, fedha taslimu sh. 1,000,000 (milioni moja) pamoja na zawadi mbalimbali kutoka kwa wadhamini wa michuano hiyo.

Polepole Aisifu Barua ya Maaskofu, Serikali Yaikana

$
0
0
Polepole Aisifu Barua ya Maaskofu, Serikali Yaikana
Wakati Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Humphrey Polepole akiisifu barua waliyoandikiwa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri (KKKT) na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi wakitakiwa kuufuta waraka wa Pasaka ndani ya siku kumi, Serikali imesema barua hiyo ni batili.

Ufafanuzi wa Serikali kuhusu barua hiyo umetolewa leo Ijumaa Juni 8, 2018 na waziri wa wizara hiyo, Dk Mwigulu Nchemba katika mkutano wake na waandishi wa habari.

Wakati leo Mwigulu akieleza kuwa taarifa zilizosambaa kwenye mitandao ya kijamii ni batili na sio maelekezo ya serikali au wizara, Polepole kupitia ukurasa wake wa mtandao wa kijamii wa Twitter alionekana kuunga mkono tamko la Serikali lililokanushwa na Dk Mwigulu.

Hata hivyo, baada ya barua ya msajili kusambaa katika mitandao ya kijamii, Polepole kupitia ukurasa wake wa Twitter aliandika ujumbe wenye tafsiri ya kukubaliana na kilichoandikwa.

“Serikali makini ina wajibu wa kukumbusha, kuelekeza, kuonya au kuchukua hatua kwa mtu au taasisi yoyote inayokwenda kinyume na taratibu za nchi ambazo tumejiwekea,” ameeleza Polepole aliyekuwa katika majibizano na mbunge wa Kigoma Mjini (ACT-Wazalendo), Zitto Kabwe.

Dk Mwigulu amesema waraka wa viongozi wa dini uliotolewa miezi iliyopita ni jambo lililopita na hivyo akawataka viongozi wa dini waendelee na kazi zao.

Kufuatia tamko hilo batili, waziri huyo amemsimamisha kazi Mkurugenzi wa Idara ya Sheria na Usajili wa Jumuiya za Kidini na Vyama vya Kiraia, Merlin Komba.

Waziri Mwigulu amesema serikali ikiwabaini waliotengeneza barua hiyo feki itawachukulia hatua za kisheria huku akionya watu wanaotaka kucheza na amani na nchi.

Pia, jana Juni 7, 2018 baada ya kusambaa kwa barua ya KKKT kwenda kwa msajili wa vyama, ikieleza ufafanuzi wa mambo waliyotakiwa kutekeleza, Polepole aliandika tena katika ukurasa wake wa Twitter;

“Kama hii ni kweli, ni ukomavu wa juu kabisa kiuongozi. Kwa awali kuwapongeza KKKT, niliumia moyo ibilisi alitaka kutumia pungufu hili kuleta mfarakano usiokuwepo, tumemshinda. Wale walifanya press conference (mkutano na waandishi wa habari) kwa barua hii waitishe press nyingine. Mzee wa kujichomeka hapa imekwama,” ameandika.


Selikali Kumchukulia Hatua Kali Mwalimu wa Mt Florence Anayewanajisi Wanafunzi

$
0
0
Selikali Kumchukulia Hatua Kali Mwalimu wa Mt Florence Anayewanajisi Wanafunzi
Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Joyce Ndalichako Ndalichako ameweka wazi kwamba serikali haiwezi kuvumilia vitendo vya udhalilishaji  ambavyo vimeonekana kufanywa na mwalimu wa shule St. Florence iliyopo jijini Dar es salaam.


Waziri Ndalichakoameyasema hayo  wakati akikabidhi zawadi kwa shule na wanafunzi wa darasa la saba, kidato cha nne na sita jijini Dodoma  baada ya kufanya vizuri kwenye matokeo ya mwisho ya mitihani yao.

Akizungumzia suala hilo Ndalichako amewahakikishia wananchi kuwa mwalimu aliyewafanyia udhalilishaji wanafunzi wa kike wa shule ya Mt. Florence vyombo vya dola vinaendelea na uchunguzi lakini watahakikisha serikali inawamchukulia hatua kali.

Pamoja na hayo Waziri Ndalichako ameshauri walimu wa kike kusafiri na wanafunzi wa jinsia ya kike katika ziara mbalimbali za kishule badala ya wanaume ili kuepukana na vitendo vya unyanyasaji wa kijinsia kama ilivyowatokea wanafunzi wa shule St. Florence.

Hivi karibuni kuliibuka sintofahamu ndani ya jiji la Dar es salaam na Tanzania kwa ujumla baada ya kuwepo na taarifa kwamba katika shule ya St. Florence mwalimu mmoja aliyetajwa kwa jina la Ayubu kudaiwa kuwanajisi watoto wanne wa darasa la saba.

Hata hivyo tukio hilo bado lipo chini ya vyombo vya sheria linafanyiwa uchunguzi.

JE, Dada Unapenda Shepu Bomba na ya Kuvutia, Weupe Bila Doa Wala Sugu?

$
0
0

Baada ya utafiti wa miaka 18 sasa kampuni ya MARKSON BEAUTY imeingiza bidhaa bora kabisa zenye matokeo ya haraka zaidi BILA madhara yoyote:

TUNAZO ZA👇👇👇
1.Kuongeza hips, makalio na mapaja kwa:-
(a)Botcho multi plus ya kunywa @250,000/=
(b)Botcho multi function ya kupaka @200,000/=
(c)Vidonge (YODDI PILLS ORIGINAL) @250,000/=
2.Kushepu mguu (CHUPA YA BIA) @150,000/=
3.Kuwa mweupe bila sugu kwa:-
(a)mafuta @150,000/=
(b) Vidonge @170,000
4.Kurefusha nywele na kutokukatika ovyo @150,000/=
5.Kuongeza urefu na upana wa uume pamoja na nguvu kwa:-
(a)Gely ya kupaka @150,000/=
(b)Vidonge maalumu kwa ajili ya nguvu na hamu ya tendo @150,000/=
(c)Max man 2plus ya kuongeza uume na nguvu pamoja na kuimarisha misuli @250,000/=
6Kupunguza au kuongeza maziwa kuyasimamisha @150,000/=
7.Kubana uke na kuondoa uchafu ukeni @130,000/=
8.Kupunguza unene na manyama uzembe @150,000/=
9.Kupunguza tumbo (kitambi) na nyama za pembeni @150,000/=
NB:Hakikisha unapata risiti yenye muhuri halisi na garantii ili kukuhakikishia kufanikiwa kwako.

Wasiliana nasi Popote
ulipo duniani kwa (+255)
0767447444
na
0714335378
UTAPATA HUDUMA.
👉🏻OUR WEBSITE:- www.marksnbeuty.org
👉🏻INSTAGRAM PAGE:-
@markson_beauty_pr
#HipsNaMakalio
#BidhaaTz
#YodiPillsTz
#BotchoOg
#CosmeticsTz
#WeupeBilaDoa

Kimenuka..Vyuo Ishirini Vyafutiwa Usajili..List ipo Hapa

$
0
0

Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi(NACTE) limefuta usajili wa vyuo 20 kwa sababu mbalimbali ikiwemo kushindwa kufuata utaratibu wa usajili wa vyuo vya ufundi na upungufu wa rasilimali za kufundishia.
-
Pia, jumla ya vyuo 9 vimesitishiwa kudahili wanafunzi wapya kuanzia mwaka wa masomo 2018/2019 kwa kuzingatia kifungu cha 22(1) cha usajili wa vyuo vya ufundi
-
Aidha, NACTE imetoa agizo kwamba kabla ya kuanza kuendesha mafunzo ya kozi yoyete chuo kinatakiwa kihakikishe kuwa mtaala wa mafunzo hayo umepitishwa na Baraza na idara itakayosimamia mafunzo hayo
-
Kaimu Katibu Mtendaji wa NACTE, Dkt. Adolf Rutayuga amesema "Kuna vyuo ambavyo mapungufu yake yalikuwa ni makubwa kiasi kwamba tumevisitishia kutoa mafunzo na vyenyewe hivi ni vyuo 20, lakini kuna vyuo vingine ambavyo tumekuta vinaendesha Program ambazo hazina idhini ya Baraza"

Waraka wa KKKT....Mkurugenzi wa Idara ya Sheria na Usajili wa Jumuiya za Kidini Asimamishwa Kazi.

$
0
0

DAR: Waziri wa Mambo ya Ndani, Mwigulu Nchemba amemsimamisha kazi Mkurugenzi wa Idara ya Sheria na Usajili wa Jumuiya za Kidini na Vyama vya Kijamii, Merlin Komba

Bi. Merlin amesimamishwa leo Juni 08 ili kupisha uchunguzi wa barua iliyoandikwa kwa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania(KKKT)

Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania(KKKT) liliandikiwa barua kutoka kwa Wizara ya Mambo ya Ndani kupitia kwa Msajili wa Vyama na kupewa siku 10 kufuta Waraka wake

Haji Manara "Mimi Ndio Msemaji Bora Kuwahi Kutokea Tanzania

$
0
0

"Sisubiri nife ili mnisifu, najijua 'my self' kuwa mimi ni msemaji wa klabu wa muda wote ndani ya nchi hii ya Tanzania kwa vigezo vyovyote vile hakuna hata wa kukaribia robo. Ukibisha lazima wewe ni mwanga"Maneno ya Haji Manara Msemaji wa Simba
Viewing all 104809 articles
Browse latest View live




Latest Images