Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104809 articles
Browse latest View live

Timu ya Simba Kuweka Kambi Italia

$
0
0
Timu ya Simba Kuweka Kambi Italia
Imeelezwa kuwa kikosi cha Simba kitasafiri kuweka kambi nchini Italia endapo kitafanikiwa kutwaa ubingwa wa Sportpesa Super Cup nchini Kenya.

Taarifa kutoka ndani kutoka klabu hiyo zimeeleza mabingwa hao wa Ligi Kuu Bara msimu wa 2017/18 wataelekea nchini Italia kwa ajili ya kambi ya maandalizi ya msimu ujao wa ligi.

Kikosi hicho kesho Jumapili kitakuwa kinashuka Uwanja wa Afraha mjini Nakuru, Kenya kucheza fainali ya SportPesa Super Cup dhidi ya Gor Mahia FC.

Simba walitinga hatua huyo baada ya kuwaondosha Kakamega HomeBoyz kutoka Kenya na Gor Mahia wakiiondoa Singida United ya Tanzania.

Fainali ya mchezo huo unaosubiriwa kwa hamu na wadau wengi wa soka la Tanzania na Kenya utaanza majira ya saa 9:00 alasiri.

Zari Amtolea Povu Hamisa Mobetto "Hata Akitaka Kuzaa Watoto Kumi na Diamond Azae Tu”

$
0
0
Zari Amtolea Povu Hamisa Mobetto "Hata Akitaka Kuzaa Watoto Kumi na Diamond Azae Tu”
Mfanyabiashara maarufu na mama watoto wa Staa wa Bongo fleva Diamond Platnumz, Zarinah Hassan amemwaga povu na kusema Hamisa hata akitaka kumzalia watoto kumi Diamond yeye kwake ruksa.

Zari ametoa kauli hiyo jana baada ya kuweka posti yake aliyokuwa anasherehekea kufikisha followers milioni 4 Kwenye mtandao wa Instagram ambapo shabiki alimtahadharisha kuwa kuna tetesi Hamisa ana ujauzito mwingine.

"Zari kuwa makini kuna tetesi huku mtaani kwetu kuwa Hamisa kashanasa mimba nyingine ila lisemwalo lipo kama halipo laja”.Aliandika shabiki huyo

Baada ya kupewa maneno hayo Zari alimjibu hata wangezaa watoto kumi yeye hana habari kwani hayumo.

Zari alijibu kwa kuandika:" Azae hata kumi mimi simo!”.

Huu ni muendelezo tu wa drama iliyoanza mwaka jana baada ya Hamisa kubeba mimba ya  Diamond

Kumekuwa na tetesi  kuwa Diamond amerudisha majeshi kwa mama watoto wake Zari baada ya kuachana na  kutoonana kwa muda mrefu

Makonda Alichowaomba Viongozi wa Dini Baada ya Kuftarisha

$
0
0
Makonda Alichowaomba Viongozi wa Dini Baada ya Kuftarisha
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda amewaomba viongozi wa dini kuendelea kumuombea Rais Dk.John Magufuli kwani anafanya kazi ngumu na kitu pekee ni kuendelea kumuombea.

Amesema kwa nafasi ya Rais wapo ambao wanampenda na wapo ambao wanakasirishwa lakini cha msingi ni kuongeza maombi na Dia kwa Rais wetu huku akihimiza umoja na mshikamano. Makonda ametoa kauli hiyo leo jioni hii katika ukumbi wa Mliman City jijini Dar es Salaam kabla ya futari maalum ambayo ameiandaa kwa mamia ya wakazi wa Mkoa huo.



Amesema viongozi wa dini wana nguvu kubwa na ndio maana watu wanakwenda Kanisani, watu wanakwenda Msikiti na kueleza nguvu hiyo itumike kushirikiana na Serikali. Hivyo ameomba viongozi wa dini kuendelea kumuombea Rais Dk.John Magufuli ili aweze kulitumikia Taifa na kusisitiza nafasi anayoitumikia Rais ni kubwa na inahitaji maombi.

"Rais wetu anafanya kazi kubwa, na dua za viongozi wa dini ni muhimu ili aweze kulitumikia vema taifa letu. Kama mimi kwa nafasi yangu napigwa mawe hivi je kwenye nafasi ya Rais itakuaje? "Rais wetu anapongezwa na mataifa mengi kwa kazi nzuri anayoifanya na kwa hapa nchini wapo wanaopongeza kwa nguvu zao zote na wapo wanaomkasirikia.

"Sishangai wakitokea wa kubeza na ukwel ni kwamba wabadharifu wa fedha za umma hawawezi kufurahia, "amesema Makonda. Akizungumza siku ya leo kutokana na kuandaa futari hiyo Makonda amesema wapo viongozi wa dini mbalimbali, viongozi wa vyama vya siasa na makundi mbalimbali.



 Amesema anamshukuru Mungu kwa wananchi wote bila kujali dini zao wanaungana katika mwezi wa Ramadhan kuuheshimu.Amesema hakuna imani ya dini ambayo ameihasau kwani wote wamejumuika kwenye futar hiyo na kubwa zaidi ni kwamba hiyo inaonesha umoja na mshikamano Katika Mkoa wa Dar es Salaam.

Amefafanua ktika futari hiyo kuna makundi mbalimbali wakiwamo wacheza mpira,wasanii wa Bongo Fleva, watu mashuhuri, na kila aina ya makundi ya wananchi. Makonda amesema kumewepo na tofauti katika baadhi ya watu ambapo amefafanua jambo kubwa kwa Mkoa wa Dar es Salaam viongozi wa dini zote na waumini wote wamebaki kuwa wamoja.

Amesema wakazi wa Dar es Salaam hawana muda wa kulumbana katika mambo ya kidini kwasababu wameamua kuwa wamoja.Ameongeza katika kuhakikisha watoto waishio kwenye mazingira magumu nao kupata futari ameamua kuwapelekea huko huko wanakolelewa.

"Leo hii kwenye futar hii wote tumependeza kutokana na mavazi nadhifu na kwa umoja uliopo huwezi kujua kati ya Sheikh na ambaye si Sheikh. Hili ni jambo jema na kwangu linanifariji. Ameeleza Mkoa wa Dar es Salaam kwa sasa umefikia watu milioni sita na Wilaya ya Temeke ndio inaongoza kwa idadi ya watu.

Amefafanua idadi ya watu iliyopo inachangamoto zake kwani ongezeko la watu linachangia kuibuka kwa changamoto nyingine za kijamii.

Mbunge Aliyekuwa Mstari wa Mbele Kushinikiza Katiba Mpya Apigwa Risasi

$
0
0

UGANDA: Mbunge Ibrahim Abiringa ambaye ni miongoni mwa viongozi waliokuwa mstari wa mbele kushinikiza mabadiliko ya Katiba, ameuawa kwa kupigwa risasi na #WatuWasiojulikana usiku wa kuamkia jana

Mwanasiasa huyo wa chama tawala cha NRM na mlinzi wake waliuawa karibu na makazi yake huko jijini Kampala

Jeshi la Polisi nchini humo limeagizwa na Rais Yoweri Museveni kuwasaka waliomuua Mbunge huyo na kuwafikisha mbele ya sheria

JE, Una Upungufu wa Nguvu za Kiume, Hamu ya Tendo la Ndoa au Maumbile Madogo? Soma Hapa

$
0
0

Tatizo la upungufu wa nguvu za kiume au ukosefu wa hamu ya tendo la ndoa limezidi kuongezeka kwa kasi duniani kote na limekuwa chanzo kikubwa cha ndoa nyingi na mahusiano kukosa uaminifu kutokana na wengi kutoka nje ya ndoa ili kupata mtu atakayemtosheleza na kumfikisha kileleni. Pia udogo wa maumbile ni tatizo kubwa na limekuwa likiwakosesha wanaume wengi uwezo wa kujiamini katika tendo na kusababisha tendo hilo kutokufanyika kwa usahihi. Hili pia huchangia kwa kiasi kikubwa wanawake wengi kwenda nje ya ndoa ( MAHUSIANO) kutafuta mbadala wake.
BAADHI YA DALILI ZA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME NI KAMA:-
☆Kukosa hamu ya tendo la ndoa
☆Uume kusimama kwa ulegevu
☆Kuwahi kufika kileleni
☆Uume kusinyaa katikati ya tendo
☆Kushindwa kurudia tendo kwa wakati
☆Kuchoka sana baada ya round ya kwanza na hata kukinai kabisa.

Kwa kutumia mimea na matunda bila kemikali 🍇🍍🍓🌿🍉🍒🍎🍑 @markson_beauty_pr Tunakuletea suluhisho la matatizo hayo hata kwa wenye "KISUKARI NA PRESSURE" kwa:-
1.HANDSOME UP ORIGINAL:- kifaa chenye uwezo wa 99% kuongeza uume kwa size uipendayo na kuimarisha misuli ya uume iliyolegea @250,000/=
2.SHARK POWER ni gely ya kupaka inayoongeza uume kwa wastani wa inch 5.5 hadi 6 @150,000/=
3.VigRX CREAM:- ni gely iliyoboreshwa mahususi kwa ajili ya kuongeza maumbile kwa wastani wa inch 6.5 hadi 8 na kuimarisha misuli ya uume iliyolegea @200,000/=
4.Vidonge maalum kwa ajili ya kuongeza nguvu na hamu ya tendo la ndoa hata kwa wenye kisukari @150,000/=
5.Spray ya kuchelewesha kufika kileleni na kuweza kurudia tendo ×3. @150,000/=
BIDHAA HIZI HAZINA MADHARA KIAFYA NA ZIMETHIBITISHWA
NA SHIRIKA LA AFYA DUNIANI (WHO).
KWA BIDHAA HIZI NA NYINGINE NYINGI TEMBELEA UKURASA WETU WA INSTAGRAM :-
@markson_beauty_pr
@markson_beauty_pr
@markson_beauty_pr
WEB:www.markbeauty.org
Wasiliana nasi Popote
ulipo duniani kwa (+255)
0767447444 na
0714335378
UTAPATA HUDUMA
NB:Matokeo ni uhakika na garantii na hakikisha unapata risiti yenye muhuri halisi wa MARKSON CO pamoja na garantii ili kukuhakikishia kufanikiwa kwako.

Sakata la Trillion 1.5, Serikali yafunguka Zilipo Billion 204 Sehemu ya Hela Hizo

$
0
0

SAKATA LA TRILIONI 1.5, Serikali yafunguka kuhusu Tsh. Bilioni 204 ambazo ni sehemu ya sakata la Tsh. Trilioni 1.5 zinazodaiwa kutopelekwa Zanzibar na kusema kuwa ziliingizwa moja kwa moja kwenye akaunti ya Mlipaji Mkuu wa Serikali ya Zanzibar

Kwa mujibu wa Mhe. Zitto Kabwe(ACT-Wazalendo), Ufafanuzi huo ulitolewa Bungeni jana Juni 08, na Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Ashatu Kijaji, alipokuwa akijibu swali la Mbunge wa Konde(CUF), Khatib Said Haji

Mbunge Konde alihoji kuwa Serikali wakati ikitoa ufafanuzi kuhusu suala la kutoonekana Tsh. Trilioni 1.5, ilieleza kwamba kati ya fedha hizo Tsh. Bilioni 204 ni makusanyo ya Zanzibar. “Sasa Waziri kabla hazijatumbukia kuwa kwenye kero ya Muungano ni lini fedha hizi zitafika Zanzibar?”

Dkt. Kijaji alipokuwa anajibu alisema “Fedha hizi hukusanywa na TRA inayofanya kazi Zanzibar na zinapokusanywa fedha hizo zinasomeka kwenye taarifa za fedha TRA kwasababu zinakusanywa na TRA,”

Aidha, Dkt. Kijaji aliongeza kuwa fedha hizo hazivuki maji kuja Tanzania bara bali zinaingia moja kwa moja kwenye akaunti ya mlipaji mkuu wa serikali ya Zanzibar

Ishu ya umri katika mapenzi yamshangaza Zari, ‘Watu na vibabu vyenu

$
0
0

Mzazi mwenza wa Diamond Platnumz, Zari The Boss Lady ameelezwa kushangazwa na jinsi jamii inavyomchukulia mwanamke mwenye umri mkubwa kuwa na mahusiano na kijana mdogo wa kiume.

Zari amesema lakini jamii haishangai pindi mwanamke mdogo anapokuwa na mahusiano na mtu mzima zaidi. Kupitia mtandao wa Snapchart ameandika;

Sitting here and thinking. Society is so quick to judge an older woman dating a young guy, but not a 40+ guy dating a 19 yr old. so tyical! Watu na vibabu vyenu.

Utambuka Zari na Diamond wamewahi kuwa katika mahusiano na kujaliwa kupata watoto wawili na inafahamika Zari ni mkubwa kwa Diamond. Baada ya kuachana kwao hivi karibuni kumekuwa na taarifa zinadai kuwa wamerudiana ila hakuna kati yao aliyethibitisha hilo.

Simba Kumleta Mfaransa Mwingine Atakayerithi Mikoba ya Lechantre

$
0
0
Simba Kumleta Mfaransa Mwingine Atakayerithi Mikoba ya Lechantre
Inaelezwa kuwa mabosi wa klabu ya Simba wameanza mazungumzo na Mfaransa mwingine atakayerithi kiti cha Pierre Lechantre ambaye amenyimwa mkataba wa kuendelea kuitumikia klabu hiyo.

Taarifa za ndani zinasema Hubert Velud ni jina la kocha ambaye anahusishwa kuja kuinoa timu hiyo yenye maskani yake maeneo ya Kariakoo jijini Dar es Salaam.

Velud amewahi kuzinoa klabu kubwa barani Afrika ikiwemo Etoile du Sahel, ES Setif, TP Mazembe pia timu ya taifa ya Togo.

Mfaransa huyo anaweza kuja nchini kuchukua nafasi ya Mfaransa mwenzake ambaye mkataba wake umeshamalizika baada ya kusaini miezi 6 inayomalizika siku chache zilizosalia.

Na taarifa zilizopo kwa wekendu hao wa Msimbazi ni kuwa tayari wameshaachana na Lechantre kutokana na kutorodhishwa na kiwango chake ndani ya timu na sasa wameanza mazungumzo na makocha wengine ikiwemo Velud anayehusishwa.

Kisa Paka Kuingia Uwanjani, Timu Yatozwa Faini

$
0
0
Kisa Paka Kuingia Uwanjani, Timu Yatozwa Faini
Klabu ya Besiktas imetozwa faini na Uefa baada ya Paka kujitosa uwanjani wakati wa mchezo wa ligi ya mabingwa dhidi ya Bayern Munich mwezi Machi mwaka huu.

Mwamuzi Michael Oliver alisimamisha mchezo katika kipindi cha pili cha mchezo uliochezwa Vodafone Park mpaka mnyama huyo alipoondoka katika dimba hilo.

Klabu hiyo ya Uturuki wameshutumiwa kwa uratibu usiokidhi viwango na wamepigwa faini kutokana na vitendo vya mashabiki kurusha vitu uwanjani na kufunga njia za kwenye ngazi, na kusababisha kutozwa faini ya pauni (£29,880).

Besiktas ilimaliza kwa ushindi wa 8-1 kwa wingi wa magoli ya kufunga kisha kusonga mbele kwenye hatua ya robo fainali, huku mashabiki wa klabu hiyo ya Ujerumani ikipiga kura kuwa Paka ni mchezaji bora wa mchezo huo.

Picha: Dkt. Shein Akutana na Kufanya Mazungumzo na Vyama vya Upinzani

$
0
0
Picha: Dkt. Shein Akutana na Kufanya Mazungumzo na Vyama vya Upinzani
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (katikati) akizungumza na viongozi wa Vyama vya Upinzani katika mkutano wa ushauriano uliofanyika leo katika ukumbi wa Ikulu Mjini Zanzibar(wa nne kushoto) Mwenyekiti wa CUF Taifa Mhe.Ibrahim Haruna Lipumba

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (katikati) katika  picha ya pamoja na  Vyama vya Upinzani baada ya  mkutano wa pamoja wa ushauriano uliofanyika leo katika ukumbi wa Ikulu Mjini Zanzibar

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (kulia) akisalimiana na  Mwenyekiti wa CUF Taifa Mhe.Ibrahim Haruna Lipumba,  wakati wa  Mkutano wa kushauriana na Vyama vya Upinzani  uliofanyika leo  katika Ukumbi wa Ikulu Mjini Zanzibar. 

Rais Kim Jong Un Atangulia Singapore Kumsubiri Trump

$
0
0
Rais Kim Jong Un Atangulia Singapore Kumsubiri Trump
Kiongozi mkuu wa Korea Kaskazini Kim Jong Un anatarajiwa kuwasili leo nchini Singapore kwa ajili ya mkutano wa kihistoria kati yake na Rais Donald Trump wa Marekani uliopangwa kufanyika Jumanne, vyombo vya habari vimesema.

Shirika la habari la Reuters lilinukuu chanzo kimoja kikisema kuwa Kim anatarajiwa kusafiri hadi katika uwanja wa ndege wa Changi, Singapore leo Jumapili.

Juhudi za Reuters kutaka kupata uhakika kutoka mamlaka za usafiri wa anga Singapore ziligonga mwamba baada ya kukataa kuzumgumzia safari hiyo ya Kim.

Kim na Trump pamoja na mambo mengine watajadili ajenda ya kuondoa silaha za nyuklia katika Rasi ya Korea na kwamba rais huyo wa Marekani anatarajiwa kumtaka Kim kuachana na uundaji wa silaha hizo.

Wakati Kim akijiandaa kuwasili leo kwa ajili ya mkutano huo wa kihistoria, viongozi wakuu wa nchi zilizoendelea zaidi kiviwanda duniani (G7) Ijumaa walianza mkutano wa siku mbili nchini Canada ambao mada kuu ni biashara duniani na Korea Kaskazini.

Mkutano huo ulifanyika Charlevoix katika jimbo la Quebec lililopo mashariki mwa Canada.

Biashara huru na uchumi wa dunia ilikuwa mada kuu katika siku ya kwanza. Mkutano huo unafuatia hatua ya Rais Donald Trump kuendelea na msimamo wake wa kulinda masoko ya ndani,ushuru wa forodha katika bidhaa za chuma cha pua na alumini uliowekwa na utawala wa Trump umeifanya Marekani kutofautiana na mataifa mengine ya G7.

Katika kikao cha jana Ijumaa, vyanzo vya habari vilisema kuwa Waziri Mkuu wa Japan Shinzo Abe aliwaambia viongozi wenzake kuwa majibizano ya vikwazo vya kibiashara ya papo kwa papo yataathiri uchumi wa dunia kwa kiwango kikubwa na hayatamnufaisha mtu yeyote.

Ofa Kubwa ya EID, Pata Bidhaa za Urembo na Kukufanya Mwanaume Kuwa Rijali Kutoka Natural Beauty

$
0
0

OFA KUBWA YA EID

NATURAL BEAUTY PROD
Ni kampuni inayotoa bidhaa ORIGINAL na zilizothibitishwa kiafya.
Sasa inatoa ofa ya punguzo la bei la 10% kwa kila bidhaa wahi sasa upatne tiba za uhakika na uweze kufulahia matokeo mazuri kwa haraka.

🥑🍇🍋🍓 🍒🌱

1.HANDSOME UP ORIGINAL_ Inaongeza uume kwa size uipendayo na kuimarisha misuli (wiki 2) @240,000/=
2.SHARK POWER GELY_ Inaongeza uume inch 6 (wiki 4) @170,000/=
3VigRX CREAM_ Inaongeza uume inch 7.5 hadi 8 (wiki 2-3) @200,000/=
4.Vidonge maalum vya kuongeza nguvu na hamu ya tendo hata kwa wenye kisukari na BP @150,000/=
5. MAXMAN 2-Hii ni vidonge vinavyoongeza nguvu za kiume pamoja na uume @230,000/=
6.VIGA SPRAY OG_ Inaongeza uwezo ktk tendo na kuchelewesha kufika kileleni @150,000/
7.BOTCHO MULT PLUS_Hii ni dawa ya kunywa ya kuongeza ( Hips mapaja na makalio) inapatikana kwa @170,000/=
8.BOTCHO CREAM HOLOGRAM_ Hii ni yakupaka ya kuongeza (HIPS na MAKALIO) @150,000/=
9.LEG BOOSTER_Ni dawa ya kuongeza miguu (CHUPA YA BIA) @150,000/=
10.BODY BOOSTER_ Hii ni yakuongeza mwili pamoja na hamu ya kula vizuri @140,000/= N.K

NB:Hakikisha unapata risiti yenye muhuri halisi wa NATURAL BEAUTY PROD ili kuthibitisha ubora wa bidhaa zetu.
Wasiliana nasi Popote ulipo duniani kwa no÷

(+255) 659618585
au
0759029968
Follow us instagram-
Google
@natural_beauty_prod
@natural_beauty_prod
@natural_beauty_prod
@natural_beauty_prod

Polisi, TRA wakamata kiwanda bubu

$
0
0

Polisi Mkoani Kilimanjaro kwa kushirikiana na Mamlaka ya Mapato Tanzania mkoani humo, wamekamata kiwanda bubu kinachotengeneza vinywaji vikali ambavyo vimepigwa marufuku hapa nchini. 

Kamanda wa Polisi Mkoani Kilimanjaro, Bwana HAMISI ISSA amethibitisha kukamatwa kwa vifaa mbalimbali vya kutengenezea pombe hizo katika nyumba  moja ya kuishi maeneo ya Msaranga Manispaa ya Moshi. 

Amesema vifaa mbalimbali vya kutengeneza pombe hizo vimekamatwa zikiwemo chupa 1,600 na stika 800 zenye nembo feki za Mamlaka ya Mapato nchini pamoja na watu wawili waliokuwa wanatengeneza pombe hizo. 

Naye Afisa Mwandamizi wa Kodi, Mamlaka ya Mapato Tanzania Mkoani Kilimanjaro, Bwana TILSONI KABUJE amesema bidha hizo hazina ubora kutokana na kutengenezwa katika mazingura ambayo siyo salama pamoja na kuziingiza sokoni bila kulipa kodi. 

Hizi Hapa Timu 6 ambazo zinawachezaji wengi kwenye Michuano ya Kombe la Dunia

$
0
0

KUELEKEA KOMBE LA DUNIA, URUSI 2018: Ikiwa zimebaki siku 6 kuanza kwa Michuano hiyo. Je, unafahamu ni Klabu gani ambazo wachezaji wake wengi wameenda kwenye michuano hiyo?

Mara nyingi baada ya msimu kuisha kukiwa na michuano ya kimataifa klabu nyingi zinaanza kujiandaa kwa ajili ya msimu unaofuata(Pre-season) bila wachezaji wao kadhaa
-
Kwa mfano Liverpool itakuwa bila wachezaji wake 8 wakati wa kujiandaa kwa msimu ujao wakati klabu ya Juventus itakuwa bila wachezaji wake 11 japokuwa timu ya taifa ya Italy haijafuzu katika michuano hiyo
-
Vilabu 6 ambavyo vinawachezaji wengi kwenye Michuano ya Kombe la Dunia msimu huu ni;
1. Manchester City ya Uingereza - Wachezaji 16
2. Real Madrid ya Uhispania - Wachezaji 15
3. Barcelona ya Uhispania - Wachezaji 14
4. Chelsea ya Uingereza - Wachezaji 14
5. Paris Saint-Germain ya Ufaransa - Wachezaji 12
6. Tottenham ya Uingereza - Wachezaji 12

Je, unadhani wachezaji kutoka katika ligi ya nchi gani watafanya vizuri zaidi kwenye michuano hiyo?

Team Kiba kukubali Kichapo cha 4-2 dhidi ya Team Samatta

$
0
0

Kikosi cha TeamKiba kimekubali kichapo cha mabao 4-2 dhidi ya TeamSamatta katika mchezo maalum wa kuchangia fedha kwa ajili ya vifaa vya kujifunzia wanafunzi uliopigwa Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Mechi hiyo ilianza kwa kasi ambapo TeamKiba walianza na kasi kubwa mshambuliaji Ibrahim Ajibu alitikisha nyavu mara mbili ndani ya kipindi cha kwanza.

Mohammed Samatta aliipatia TeamSamatta alisawazishia  bao la kwanza na kuweza kufanya dakika 45 za kwanza kumalizika kwa TeamKiba ikiwa mbele kwa mabao 2-1.

Kipindi cha pili kilianza kwa TeamSamatta kuja juu zaidi ikilishambulia lango la TeamKiba na kuweza kujipatia mabao matatu kupitia kwa Haruna Moshi 'Boban', Jamhuri Julio na Mbwana Samatta.

Mpaka dakika 90 zinamalizika, TeamSamatta ilikuwa 4, TeamKiba 2.

Wanaotumia Namba za Polisi na zimamoto Vibaya Kuchukuliwa Hatua - Majaliwa

$
0
0

WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa ameliagiza Jeshi la Zimamoto na Uokoaji kwa kushirikiana na Jeshi la Polisi wawachukulie hatua kali wananchi wote wanaotumia vibaya namba za mawasiliano za jeshi hilo kwa kutoa taarifa za uongo kuhusu matukio ya majanga ya moto. 


Hata hivyo, Waziri Mkuu ameliagiza Jeshi la Zimamoto na Uokoaji nchini kuendelea kutoa mafunzo kwa wananchi juu ya namna ya kujikinga na kupambana na majanga ya moto pindi yanapotokea katika maeneo yao. Pia ameziagiza Halmashauri zote nchini kuwa na magari ya zimamoto pamoja na magari ya kubeba wagonjwa kwenye vituo vyote vya Zimamoto na Uokoaji katika maeneo yao.


Waziri Mkuu ametoa agizo hilo leo (Ijumaa, Juni 8, 2018) wakati alipofanya ziara katika Kituo cha Operesheni na Mawasiliano ya Dharura ya Maafa pamoja na Kituo cha Zimamoto na Uokoaji cha mkoa wa Ilala. Amesema ili kudhibiti wananchi wanaopiga simu za kuomba msaada wa kutaka kuokolewa, huku kukiwa hakuna tukio lolote la janga la moto lililotokea kwenye maeneo yao, ni vema watu hao wachukuliwe hatua kali ili iwe fundisho kwa wengine wenye tabia kama hiyo.


Waziri Mkuu ametoa agizo hilo baada ya Kamishna Jenerali wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji,  Thobias Andengenye kumweleza baadhi ya changamoto zinazolikabili jeshi hilo kuwa ni pamoja na wananchi kupiga simu wakidai kuna ajali ya moto imetokea katika maeneo yao na baada watu wa uokoaji kufika wanabaini ni uongo.


Hata hivyo, Waziri Mkuu aziagiza Halmashauri zote nchini kuwa na magari ya zimamoto pamoja na ya kubebea wagonjwa kwa ajili ya kutoa huduma pindi majanga yanapotokea kwenye maeneo yao ili kuharakisha utoaji wa huduma za dharura.


Pia amelitaka Jeshi la Zimamoto na Uokoaji kuendelea kutoa elimu kwa wananchi ili kila Mtanzania aweze kuwa na uelewa wa kutoa huduma za awali pindi majanga ya moto yanapotokea katika maeneo yao ikiwa ni pamoja na kutumia vifaa vya kuzima moto.

Waziri Mkuu ambaye alitembelea kituo cha Jeshi la Zimamoto cha Ilala amejionea magari ya kuzimia moto likiwemo la aina ya Bronto Sky Lift lenye uwezo wa kufika futi 54 na kuzunguka nyuzi 360. Alielezwa kuwa katika Bara la Afrika, magari ya aina hiyo yapo matatu tu, ambayo yapo nchini Tanzania, Misri na Afrika Kusini. Kwa upande wa Tanzania, gari hilo lilinunuliwa miaka 10 iliyopita kwa sh. bilioni 1.5.  


Katika hatua nyingine, Waziri Mkuu alitembelea Kituo cha Operesheni na Mawasiliano ya Dharura ya Maafa, ambapo aliwasisitiza viongozi wa kituo hicho kutoa elimu kwa wananchi juu ya madhara yatokanayo na kuishi kwenye maeneo hatarishi hususan mabondeni.


Waziri Mkuu alisema licha ya kuwapa elimu, pia wanatakiwa kuwashawishi wakazi wa maeneo hayo kuondoka kabla ya kutokea kwa maafa badala ya kusubiri majanga yatokee. Pia aliwataka wawe na mpango wa kuonesha eneo lenye maafa na kuujulisha umma. Pia aliwataka watendaji wanaohusika na kamati za maafa waimarishe mawasiliano katika ngazi zote kuanzia ya kijiji hadi Taifa na wafanye kazi kwa ushirikiano ili kurahisisha utoaji wa huduma kwa wananchi pindi maafa yanapotokea.


Awali, Waziri Mkuualitembelea Ofisi za Mpiga Chapa wa Serikali jijini Dar es salaam ambapo mbali na mambo mengine alijionea moja kati ya mitambo ya kwanza ya Mpiga  Chapa wa Serikali uitwao  Original Heidelberg wenye zaidi ya miaka 100 ambao bado unafanya kazi vizuri.

Trump agoma Kushawishika Mkutano wa G-7

$
0
0

Hisia mbalimbali zilijitokeza wakati Rais Donald Trump alipokutana na viongozi wa mataifa ya G 7 yenye uchumi mkubwa duniani katika mkutano wao wa kila mwaka huko Canada Ijumaa, lakini mazungumzo yao yalikuwa yakistaarabu, kidiplomasia kwa mujibu wa vyanzo vya habari.

Trump alichukua msimamo kwa kuweka wazi kuwa Marekani inakandamizwa inapofanya biashara na washirika wake wa Ulaya.

“Viongozi wengine walitoa hisabu zao na Trump alitoa zake,” afisa moja wa G-7 ambaye alizungumza kwa sharti la jina lake kutotajwa ameliambia shirika la habari la Reuters.

“Kama ilivyokuwa imetarajiwa hakubadilisha msimamo. Hii pengine siyo kwa sababu hafahamu hali halisi, lakini ni kwa sababu ya siasa za nyumbani.”

Baadae katika mkutano wa ushirikiano kati ya pande mbili na mwenyeji wa mkutano huo Justin Trudeau, Rais wa Marekani alifanya mashara kuwa waziri mkuu wa Canadaalikuwa amekubali “kupunguza ushuru wote.”

Pamoja na viongozi wa pande mbili hizo kukosoana juu ya sera za biashara za kila upande siku iliyopita, Trump alieleza mahusiano ya mipakani mwao yalikuwa mazuri, akisema “kwa kweli tunashirikiana kupunguza kodi na kufanya hilo litoe haki kwa nchi zote mbili. Na kwa kweli tumepiga hatua kubwa hivi leo. Tutaona vipi yote haya yatatekelezeka.”

Katika mikutano iliyofuatia kati yake na Rais wa Ufaransa Emmanuel Macron, Trump amesema “ Marekani imekuwa na pengo kubwa la kibiashara kwa miaka mingi kati yake na nchi za Umoja wa Ulaya na tunalifanyia kazi suala hili. Na Emmanuel amekuwa na msaada mkubwa sana juu ya hili.”

Kwa upande wake Macron alijibu kuwa alikuwa “na mazungumzo ya wazi na moja kwa moja” na Trump na kuwa “hali ni ngumu lakini kwa ujumla hiyo ndio njia ya kupiga hatua .”

Kwanini Baadhi ya Wanaume Wana Maumbile Mafupi na Upungufu wa Nguvu za Kiume? Suluhisho Hili Hapa

$
0
0

KWANINI BAADHI YA WANAUME WANA MAUMBILE MAFUPI NA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME DR SITTA NDO SULULISHO LAKO tatiza, hili limekuwa likiwaasili watu wengi,sana kisaikolojia hasa baadhi yao kujiona wako tofauti na wanaume wengine, kwa kawaida, mwanaume anatakiwa awe na uume, usiopungua nchi 6-7au-8 ,vinginevyo mtu huyo anamatatizo zipo , sababu nyingi zinazosababisha, tatizo hilo baadhi ni (i) upungufu wa vichocheo vya HORMONES ZA CETROGEN ambazo mwanaume, anapobarehe vichocheo hivi, HORMONES hizo, husaidia ukuaji wa uume 

SUPER MIZIZI, ni dawa inayozalisha HORMONES ZA CETROGEN,na kufanya, uume kukuwa na kuongzeka sazi utakayo na kuzibua mlija iliysinyaa, 

NSHOLA ni dawa bora, ya kurudisha nguvu, za, kiume bari inatibu ,kabisa kutoa tatizo hilo, na kukupa , hamu ya , kurudia tendo, la ndoa zaidi, ya mala nne 4 ,bila kuchoka atakama unaumli ,wa mika 80,! pia ana ,dawa za ,kutibu, presha ya kupanda ,na kushuka, kisukari kuondoa, mafuta , mwilini ,na maumivu ya, mgogo kiuno, dawa zipo, matazo, ya hedhi, kwa ,wanawake hedhi, zisizokuwa na, mpangilio, na kasonono, pia , vidonda ,vya, tumbo ,(STOMACHI UCLENS) IHUSHI ndoji lako. 

NKANYA ni dwa ya mvuto wa kimapenzi ,mchumba mpenzi ariyekuacha, mke mme, atakuludia kwa, mda, wa msaa3 tu , ukishaitumia atarudi ,mwenyewe bila ,ugovi tena, NKOMA ni dawa kuongeza HIPS na mguu wa bia kwa wadada . 

HERBON, ni, dawa, ya kuongeza, CD4, NGAKAMA ,ni dawa ya kutibu ,miguu, kufaganzi, na ,kuwaka moto, huduma zetu ,zipo ,vizuri, popote pale dawa utaletewa! DR SITTA, amebobea, kwa tiba asilia 

DAR ANAPATIKANA MBAGALA, ZAKHEM, SONGEA BOMBAMBILI SHINYANGA, KAHAMA MJINI, KWA MAELEZO ZAIDI , PIGA SIMU 0763172670 au 0715172670 

WOTE MNAKALIBISHWA, KAMA, UTAKUWA NA TATIZOUTAHUDUMIWA,

Mwakyembe aifagilia Simba

$
0
0

Waziri wa Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo, Dk. Harrison Mwakyembe, amesema ushiriki wa Simba katika Michuano ya Sportpesa ni alama kwa Taifa.


Akizungumza na waandishi wa habari mjini Morogoro leo, Dk. Mwakyembe amesema hatua ya Simba kushiriki fainali ya michuano hiyo sasa inakwenda kuitangaza Tanzania kwenye medani za kimataifa.


“Ushiriki wa Simba kwenye michuano ya Sportpesa ni alama kwa nchi yetu, kwa sababu akishinda anakwenda kucheza na Everton ya Uingereza.


“Nami nilikuwa nafikiria kwenda kushuhudia fainali hizi nchini Kenya, lakini acha tuone kwanza. Hapa lazima tuweke uzalendo mbele kwa Simba ambayo inawakilisha Tanzania kwenye michuano hii, ” amesema Dk. Mwakyembe.

Waziri Tizeba Aagiza Kukamatwa Kiongozi Wa AMKOS Aliyefuja Milioni 23

$
0
0

Na Mathias Canal-WK, Singida

Waziri wa Kilimo Mhe. Dkt Charles Tizeba amemuagiza Mrakibu wa polisi Wilaya ya Iramba ASP Magoma Mtani kumkamata aliyekuwa mwenyekiti wa Bodi ya Chama cha ushirika (AMKOS) Msai.


Waziri Tizeba ametoa agizo hilo jana 9 June 2018 Mara baada ya kutembelea kitongoji cha Kati, Msai na Mtoa akiwa katika ziara ya kikazi ya Siku mbili kwa ajili ya kutembelea vituo vya ununuzi wa pamba na kujionea msimu wa ununuzi wa zao hilo katika vijiji hivyo.


Dkt Tizeba amelaani vikali ufujaji huo wa fedha za wakulima huku akimtaja Paul Ramadhan Kurwa kuhusika na ufujaji huo wa shilingi milioni 23 huku akiendelea kuonekana mtaani pasina kuchukuliwa hatua za kisheria.


"Wakati muelekeo wa serikali yetu inayoongozwa na Rais wetu Dkt John Pombe Magufuli ukijipambanua kutaka kuboresha maisha ya watanzania kupitia Kilimo lakini kuna watu wanataka kurudisha nyuma juhudi hizo, hakika tutawapa kibano kweli kweli hakuna utani kwenye fedha za wananchi" Alikaririwa Dkt Tizeba


Mhe Tizeba ametoa siku moja kukamatwa kwa mwizi huyo na kufikishwa mahakamani ili awe mfano kwa wezi wengine wasio kuwa na haya wala soni.


Aidha, amewataka wananchi katika msimu huu wa uuzaji na ununuzi wa Pamba kutouza Pamba zenye uchafu wakidhani wataongeza idadi ya kilo kwani kufanya hivyo ni kufifihisha juhudi zao wenyewe jambo ambalo halina tija.


Sambamba na hayo pia amewaondoa hofu wakulima kote nchini kuwa serikali ya awamu ya tano inatekeleza kwa vitendo ilani ya uchaguzi ya Chama Cha Mapinduzi yenye mkataba na wananchi katika kipindi cha miaka mitano 2015-2020.


Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Iramba Mhe Emmanuely Lwehahula amempongeza Waziri Tizeba kwa kutembelea maeneo mbalimbali ili kujionea ununuzi wa Pamba huku akiwasihi wananchi wilayani humo kulima kiasi kikubwa cha Pamba msimu ujao kwani mbegu na madawa ya kuulia wadudu vitatolewa bure kuanzia msimu ujao wa mwaka 2018/2019.
Viewing all 104809 articles
Browse latest View live


Latest Images

<script src="https://jsc.adskeeper.com/r/s/rssing.com.1596347.js" async> </script>
<script src="https://jsc.adskeeper.com/r/s/rssing.com.1596344.js" async> </script>