Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104795 articles
Browse latest View live

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa Afungua Mashindano Ya Umisseta Na Umitashumta- Mwanza

$
0
0

WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amewataka Maafisa Elimu wahakikishe wanafunzi wanaoshiriki mashindano hayo ni wale waliovuka katika ngazi ya shule, kata, wilaya na mkoa, ambao wote ni wanafunzi halali wa shule na marufuku kuchezesha mamluki.


“Endapo itabainika yupo mchezaji aliyeletwa kushiriki michezo hii ambaye si mwanafunzi (yaani mamluki) naagiza hatua kali zichukuliwe dhidi ya wahusika kwa kuzingatia kanuni na sheria za mashindano haya,” amesisitiza.


Waziri Mkuu ambaye ameambatana na mkewe Mama Mary Majaliwa ametoa agizo hilo jana (Jumamosi, Juni 9, 2018) wakati akifunguaMashindano ya Umoja wa Michezo na Taaluma kwa Shule za Msingi na Sekondari Tanzania yanayofanyika kwenye Uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza.


Pia, Waziri Mkuu amewataka viongozi wa mikoa na wilaya zote nchini wahakikishe kuwa masomo ya haiba, michezo na stadi za kazi yanafundishwa kikamilifu kwenye shule zote za msingi.


Hata hivyo, Waziri Mkuu amesema somo la elimu ya michezo kwa Shule za Sekondari nalo lifundishwe kikamilifu na vyuo vya michezo kama Malya viendelee kuwaendeleza walimu wa michezo.


Amesema utafiti na ubunifu wa kuendeleza michezo nchini ni jambo linalohitaji kupewa msukumo wa pekee, ambapo ameviasa vyama vya michezo na asasi za sanaa zijihusishe na ukuzaji wa michezo shuleni, bila kuathiri taratibu za shule.


Katika hatua nyingine, Waziri Mkuu amewaagiza Maafisa Elimu wa Mikoa na Wilaya wahakikishe maeneo ya michezo na burudani yanapimwa na yasiingiliwe, pia vitengo vya michezo kwenye ofisi za Halmashauri na Mikoa vitengewe fedha za kuendeshea michezo.


Amesema pamoja na manufaa yatokanayo na michezo, kiwango cha michezo  nchini si cha kuridhisha, hivyo  ni vema kujenga msingi wa kupata matokeo mazuri kwa kuwa na viwanja vyenye viwango vinavyokubalika, walimu wenye utaalamu wa michezo na vifaa.


“Inawezekana kuna sababu za msingi, lakini ni lazima tuhakikishe kuwa vijana kuanzia Shule za Awali, Msingi, Sekondari na Vyuo wanatengenezewa mazingira mazuri ikiwa ni pamoja na kupewa fursa za kucheza na kushindana miongoni mwao,” amesema.


Amesema kutokana na hali hiyo, Serikali ya Awamu ya Tano inayoongozwa na Rais Dkt. John Magufuli kupitia shule za msingi na sekondari, itahakikisha walimu waliosomea michezo wanapata ajira ili waendeleze vipaji vya vijana nchini.


Waziri Mkuu amesema vipaji vya michezo na sanaa vitaitangaza nchi kimataifa na kuongeza fursa ya ajira kwa Watanzania. Amesema kauli mbiu ya michezo ya UMISSETA na UMITASHUMTA ya mwaka  huu ni “michezo, sanaa na taaluma ni msingi wa maendeleo ya mwanafunzi  katika Taifa letu”.


Amesema kauli mbiu hiyo inawataka wanafunzi wajihusishe na michezo na sanaa kama sehemu ya taaluma, ambapo wataweza kuonesha vipaji vyao ambavyo vikiendelezwa vema vitawapatia manufaa ikiwemo afya, matokeo mazuri ya kitaaluma na ajira.


Pia amempongeza Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Bw. John Mongella na wananchi wote kwa kukubali kuwa wenyeji wa mashindano hayo kwa mara ya tatu mfululizo, pamoja na  kampuni ya COCA COLA kwa kudhamini michezo ya mpira wa miguu na kikapu kwa Shule za Sekondari na kampuni ya AZAM kwa kujitolea kuonesha michezo hiyo kwa mwaka huu.


Aidha, amewataka wanafunzi wanaoshiriki mashindano hayo watumie ushiriki wao kwa kuuthibitishia umma dhamira waliyonayo ya kuonesha kuwa, zipo fursa nyingi za ajira endapo vipaji vya michezo na sanaa vitatumika kikamilifu.


Amesema mashindano kama hayo yanatoa fursa kwao kuonesha uwezo wao na kuonekana kwa wadau mbalimbali  wanaoweza kuwaendeleza.  “Si hivyo tu, uwepo wenu hapa unawapa fursa ya kutambua uwezo mlionao pamoja na kujiwekea malengo na mwelekeo wa maisha yenu ya baadaye,”.


Amesema uhalali wa michezo na mashindano shuleni unatajwa katika Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya 2015-2020, Sera ya Maendeleo ya Michezo ya mwaka 1995,  Sera ya Elimu ya mwaka 2014 ambazo kwa pamoja zinaelekeza kutambua na kuendeleza vipaji vya wanafunzi shuleni kufikia malengo ya maendeleo endelevu.


Mashindano hayo yamehudhuriwa na Naibu Waziri waNchi, OR – TAMISEMI, Joseph Kakunda, Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Juliana Shonza, Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, John Mongella pamoja na viongozi mbalimbali wa Serikali, Wadhamini wa Mashindano hayo, Wadau wa michezo na baadhi ya wananchi wa mkoa wa Mwanza.


IMETOLEWA NA:

OFISI YA WAZIRI MKUU,

Video: Alikiba alianza kwa mbwembwe, mwisho ametoka kichwa chini – Samatta

$
0
0
Mchezaji wa Taifa Star na klabu ya Genk ya Ubelgiji, Mbwana Samatta ameeleza mbinu za kimchezo alizotumia kumsambaratisha muimbaji Alikiba katika mechi yao ya hisani iliyochezeka Uwanja wa Taifa na kuhudhuriwa na maelfu ya watu. Mapato ya mchezo huo yatapelekwa kuchangia elimu nchini Tanzania.

VIDEO:

Akilimali wa Yanga Anyoosha Mikono na Kukubali Mabadiliko Yanga Aliyokuwa Akiyakataaa

$
0
0
Kuelekea Mkutano Mkuu wa Yanga unaofanyika Jumapili ya leo katika ukumbi wa Police Officers Mess jijini Dar es Salaam, Katibu wa Baraza la Wazee wa klabu hiyo, Ibrahim Akilimali ametoa neno lake.

Mzee huyo ambaye awali alionekana kupinga mabadiliko hayo amesema kuwa kwa sasa anayaunga mkono kwa asilimia zote.

Akilimali ameeleza kuwa mabadiliko Yanga kwa sasa hayakwepeki kutokana na timu yao ilipofikia hivi sasa mpaka kwa mwenendo ilionao kuwa si mzuri.

Kiongozi huyo amesema yeye hajawahi kupinga mabadiliko bali alikataa mfumo ambao alikuja nao Yusuph Manji hapo awali akitaka kukodisha timu na nembo jambo ambalo amefunguka kwa kueleza halikuwa sahihi kwake hata kidogo.

Ikumbukwe wakati Manji akiwa Mwenyekiti Yanga, alikuja na ombi la kutaka Yanga aikodishe akihitaji timu na nembo na baadhi ya wanachama ikiwemo Akilimali na wengine kuibuka na kupinga kwa nguvu suala hilo.

Mkutanoo Mkuu wa Yanga unatarajia kuanza leo majira ya saa 4 kamili za asubuhi ambapo Waziri mwenye dhamana ya michezo, Harrison Mkwayembe anatarajiwa kuwa mgeni rasmi.

Wimbo wa Iyena Umechangia Asilimia 98 Kumrudisha Zari Kwa Diamond....Soma Hapa

$
0
0
MWENYE nyumba kafufuka na nyumba ya mirathi haiuzwi tena, pole Hamisa Mobeto! Waswahili bhana, wao wape kichwa cha habari na habari yote watakuandikia…Ha! Ha! Haaa!

 Kama ninawaona vile wanavyocheka kwa ‘dharaaau’ pale mrembo Zarinah Hassan ‘Zari The Boss Lady’ mzazi mwenza na mwanamuziki, Naseeb Abdul ‘Diamond Platnumz’, atakapotua Madale, kwenye makazi ya mwanamuziki huyo.

 Halafu pia ninajiuliza mwanamitindo, Hamisa Mobeto, mzazi mwenza pia na Diamond, ambaye hivi karibuni alionekana kufurahia penzi la mwanamuziki huyo atazungumza nini juu ya suala hili.
Mengi ninajiuliza. Lakini nikuhakikishie mpenzi msomaji, maneno yale ya kwanza kabisa juu si yangu. Ni ya mashabiki wa Diamond ambao wanapenda kumuona akiwa kwenye uhusiano na Zari.

 Maneno hayo yameibuka baada ya kuonekana kuwa kuna kila dalili za wawili hao ambao walikuwa wamepigana chini kurudiana, baada ya meneja wa Diamond na familia ya mwanamuziki huyo kufanya jitihada za kumrudisha Zari kwenye familia hiyo.

Hata hivyo pamoja na yote yanayoendelea na hatua zinazochukuliwa kumrudisha Zari kwenye ‘White House’ ya Diamond huko Madale, niamini mimi Wimbo wa Iyena wa Diamond umechangia kwa asilimia 98 kumrudisha Zari kwa Diamond.

KIVIPI?
Hili ndilo swali la msingi unaloweza kujiuliza, si ndiyo? Sasa ipo hivi; Baada ya wimbo ambao Diamond kamshirikisha Rayvanny, kutoka na Zari kuonekana kashiriki kwa asilimia kubwa kwenye upande wa video, mashabiki wengi walianza kukomenti kwenye ukurasa wa Diamond, Instagram na meneja wake Babu Tale kwamba wanamtaka Zari, Madale.

BABU TALE ACHUKUA HATUA
Baada ya komenti kuwa nyingi Instagram, hiki ndicho Babu Tale aliandika; “Naona watu mnania-ndikia niwarudishe Mr and Mrs Dangote, hili kwangu ni kama kumsukuma mlevi yaani ni kazi ndogo sana.
“Ila Niliwaacha tu kwanza kila mtu sumu na hasira za mioyo yao ziwaishe ili wakirudiana akili iwakae sawa, sasa naona muda muafaka wa kulitumia jina langu ipasavyo, kama ambavyo mama Tee ananiita “Godfather”, siendi na magoti wala kutambaa nitapanda ndege kwenda hadi SA (Afrika Kusini) kuongea na mtu mzima mwenzangu na ninaamini yataisha kwa asilimia 100, wananzengo niende nisiende?”


Baada ya posti hiyo Instagram, Juni 2, Babu Tale aliposti picha akiwa uwanja wa ndege na kuweka wazi kwamba safari ya Sauz ilikuwa imewiva. Baadaye aliposti picha akiwa na Zari, Sauz. Nguvu ya Iyena inafanya kazi!

 MAMA DIAMOND NAYE HAYUPO NYUMA!
Mama wa mwanamziki huyo si habari ya kukushangaza kwamba anampenda Zari. Ni jambo ambalo linajulikana kwa wengi na hafichi mapenzi yake kwa mrembo huyo mwenye asili ya Uganda.

 Baada tu ya Wimbo wa Iyena kutoka, mama Diamond amekuwa akitupia picha mbalimbali kutoka kwenye video ya wimbo huo pamoja na vipande vya video huku akiandika maneno ya kumsifu Zari. Picha ya kwanza ya Zari aliyoposti baada ya Iyena kutoka aliambatanisha na maneno yaliyosomeka hivi; “#Mama Latiffa mwenye IYENA yake, mwanamke usafi gaga kulisugua mume akirudi sharti viatu kumvua.

 NDUGU WA DIAMOND WENGINE VIPI?
Kwa upande wa ndugu wengine wa Diamond, akiwemo dada yake Esma, Wimbo wa Iyena pamoja na komenti za mashabiki za kuwataka wawili hao kurudiana ni kama zimechochea nao wazidi kuonesha waziwazi mapenzi yao kwa Zari.

 Kwenye akaunti ya Instagram ya Esma, Zari hakauki, mara kwa mara anamposti huku akiambatanisha kepsheni fupifupi zinazoonesha mahaba yake kwa Zari. Ni nguvu ya Iyena inafanya kazi!

HITIMISHO
Baada ya nguvu kubwa ya Wimbo wa Iyena kuenezwa na familia ya Diamond, kwenye mitandao taarifa zimeshaanza kuzagaa kuwa, Zari ametia mguu ndani ya Dar huku nyingine (sio rasmi) zikiwaonesha Diamond na Zari wapo chumbani.

MAKALA NA BONIFACE NGUMIJE

Dawa Bora za Nguvu za Kiume na Kukosa Hamu ya Tendo la Ndoa

$
0
0
Baada ya utafiti wa muda mrefu juu ya matatizo ya upungufu wa nguvu za kiume na ukosaji wa hamu ya tendo la ndoa ama kushindwa kurudia tendo kwa haraka sasa

MWASELE HERBAL CLINIC. inakuletea suluhu juu ya matatizo haya kwa kutumia dawa za

FULL POWER .ni dawa asili ya vidonge inayotibu tatizo la upungufu au ukosefu wa nguvu zakiume. dawa hii ina mchanganyiko wa kutosha kuzalisha vichocheo vingi vya hormone za gestrogen ziwemo vitamin B6&B1, vitamini E pamoja madini aina ya zinc vitakufanya kuwa na nguvu na muzunguko mzuri wa damu na kuongeza hamu na uwezo wa kufanya tendo la ndoa zaidi ya hatua nne au zaidi na kuchelewa kufika kileleni zaidi ya dakika 20-30. ZAT 50 inarudisha maumbile ya uume yaani kurefusha na kunenepesha ulefu nchi 3-7, upana cm, 3-4 standard kiafya haijalishi umri wako hata kwa wazee ukitumia maumbile yatabaki kuwa hivyo siku zote . pia tunatibu matatizo mengine kama presha, kisukari , ngiri ,chango la tumbo,tumbo kujaa gesi, kutokupata choo vizuri,miguu kuwaka moto,matatizo ya uzazi, bawasili namagonjwa yazinaa kama kisonono nakaswende.

Tunapatikana DAR ES SALAAM. SHINYANGA NA ZANZIBAR. kwa wakazi wa dar es salaam utaletewa huduma hii popote ulipo . wa mikoani tunawatumia kwanjia ya mabasi .

Wasiliana nasi kwa sim no 0717702227 au 0754568767.DR . SAGUDA nyote mnakaribishwa

Vera Sidika Amwagiwa Mahaba Matamu Hadharani

$
0
0
MWANAMITINDO maarufu nchini Kenya, Vera Sidika ‘Vee Beiby’ amemwagiwa mahaba hadharani na mpenzi wake ambaye ni mwanamuziki, Otile Brown.
Kwa muda mrefu mapenzi ya wawili hao yamekuwa ya siri lakini juzikati Otile aliingia kwenye ukurasa wake wa Instagram na kumwagia Vera mahaba hadharani.

 “Nakupenda sana wewe mwanamke (Vera)… wewe ni kila kitu kwangu… na kinachonivutia zaidi kwako ni jinsi ulivyoumbika… niamini, nimewaona wanawake wengi lakini upo tofauti nao sana, wewe mvumilivu, una busara na mtu spesho,” aliandika Otile.

VIDEO:

Dogo Janja "Young Dee na Young Killer Madogo Sana Kwangu Hawaoni Ndani, Niko Juu Sana'

$
0
0
Na James Timber, Mwanza
Msanii wa kizazi kipya nchini Abdulaziz Chende maarufu Dogo Janja anayetamba  kwa kibao cha "wayu wayu" amesema bado yupo juu hashindanishwi na young D wala young Killer.

Akipiga story na Muungwana Blog baada kumaliza show kwenye uzinduzi wa UMISSETA Kitaifa mkoani Mwanza ameshukuru kwa kupokelewa vizuri na wananfunzi wanaoshiriki mashindano hayo ambapo amesema kuwa uwezo na kipaji alichonacho ndio kimeleta shangwe hizo.

"Bado mie ni mkali ndio maana na najua mashabiki wanataka nini hicho ni moja ya kitu kinachonifanya niendelee kuwa bora, amesema.

Aidha amewaomba mashabiki wa Mwanza na wadau mbalimbali wa burudani  waendelee kumsapot kwa ngoma kali anazotoa.

Nini na Nay wa Mitego wazidi kuacha alama ya viulizo

$
0
0

Ikiwa leo June 9,2018 ni siku ambayo watu wengi husherekea siku zao za kuzaliwa basi katika list hiyo huwezi kuacha kumtaja mkali katika bongo Fleva Nay wa mitego ambaye na yeye amezaliwa siku kama ya leo.

Msanii Nini amehusika kumu-wish Nay wa Mitego kupitia account yake ya instagram lakini maswali yamekuja baada ya kupost picha ya Nay Wa Mitego na kuandika caption ambayo imezua alama za kuuliza hii ni kutokana tu na wawili hao kuhusishwa kwenye mahusiano ya kimapenzi.

Nini ameandika
“Hey Handsome!Happy Birthday my ❤, My Chaga Boss, My Never Gonna Billnass and Nandy me (Kidding😂)..Ukawe mwaka wa mafanikio mengi katika maisha yako!I love you extra much BOJ❤😗🎉 @naytrueboytz @naytrueboytz”


Masunzu Power Mix Dawa Bora ya Nguvu za Kiume na Maumbile Madogo

$
0
0
MASUNZU POWER MIX DAWA BORA YA NGUVU ZA KIUME NA MAUMBILE MADOGO

🌸MASUNZU POWER MIX ni dawa ya asilia yenye mchanganyiko wa mitishamba 7 yenye maajabu yafuatayo (1) inatibu upungufu wa nguvu za kiume Mara dufu na kuimalisha uume uliolegea wakati wa tendo la ndoa (2) kurefusha uume uliorudi ndani nchi 5-8 (3) kunenepesha uume sm4 ya upana itakufanya uchelewe kufika kileleni dk (15-20) kwa tendo la kwanza na utakuwa nauwezo wa kurudia tendo la ndoa Mara (2-4) bila hamu kuisha nainatibu kabisa. Dawa hii haina madhara yoyote kwa mtumiaji huanza kufanya kazi baada ya dk 50 tu 🌾🌾🌾🌾🌾🌾🌾🌾

MATATIZO HAYA HUSABABISHWA NA ngiri. au umejichua kwa muda mrefu. Punyeto kisukari. Presha. Tumbo kujaa gesi na kuunguruma chini ya Kitovu. Kutopata choo vizuri. Msongo wa mawazo. Kaswende. Gono. Haya yote husababisha kuwa na maubile madogo na kukosa nguvu za kiume

🌸SOSOMA DX. ni dawa ya kumvuta mme au mke au mpenzi wako arudi haraka na kuanza mapenzi mapya kama mlivyo anza mwanzo baada ya masaa 2 atarudi na kutulia ndani ya nyumba na kutimiza ahadi yako

🌸GINDU EXTRA ni dawa ya kutibu kisukari siku 14 unapona kabisa hata kama imepanda itashuka haraka Sana. Tunatibu busha bila upasuaji nk. Dar es salaam tunapatikana buguruni chama au unaweza kuletewa popote ulipo

Wasiliana na tabibu ATHUMAN SIMU +255673552294 / +255784552299

Davido A-Sign Dili Nono na Manager wa Justin Bieber

$
0
0
Kumekuwa na tetesi kuwa staa maarufu kutokea Nigeria Davido ambaye kwa sasa anafanya vizuri kimataifa kuwa amesaini dili nono lenye mkwanja mrefu na Manager wa Justin Bieber ambaye ni Scooter Braun

Tetesi hizo zimezuka baada ya wawili hao kuonekana wakiwa pamoja na kufanya mazungumzo katika mkutano wa kibiashara  huko Marekani , Scooter Braun kwa sasa anasimamia kazi za wasanii maarufu ikiwemo Ariana Grande, Justin Bieber , Tori Kelly, Martin Garrix na wengine wengi akiwa chini ya kampuni yake ya SB projects.

Hii inaweza ikawa ni good news kwa mashabiki wa Davido ambapo inawezekana ngoma kali ikaja soon ikiwa imewashirikisha baadhi ya wasanii wanaosimamiwa na kampuni hiyo ya SB projects.

Bonyeza PLAY hapa chini kuangalia Davido akiwa na Manger huyo.

Mwanaume Usimwachie Mkeo Hela Chumbani, Mwachie Mbele ya Watoto Wakiona

$
0
0
MWACHIE MBELE YA WATOTO NA UMWAMBIE NA MATUMIZI YAKE, NA WATOTO WASIKIE USIJE KUISHI MAISHA YA UPWEKE UZEENI

MWANAUME
Unamwachia mkeo hela ya Chakula Chumbani, Mke Anatoka na Kapu anaenda kununua Chakula, Anapika, Anawaambia watoto, Njooni Wanangu Mle Nimewapikia Chakula Kitamu, Watoto wakishakula Wanasema Asante Mama.

MWANAUME
Unamwachia Mkeo hela ya Nguo za Sikukuu Chumbani,
Kesho Yake mkeo Anatoka kwenda Kununua Nguo, Akirudi Anawaambia Wanangu Nimewanunulia Nguo za Sikukuu Njooni Mjipimie, Watoto Wakishajipima, Anawaambia Wanangu Mmependeza Eeee, Simnaona Ninavyowapenda
Watoto wanafurahi na Kusema Asante Mama,

MWANAUME
Kila Aina ya Pesa ya Matumizi Unamwachia Mkeo Hela Chumbani,

MWANANUME
Ukifika muda wa kutoa Ada Unamkabidhi Mkeo Hela Chumbani,
Kesho yake Mkeo Anawaambia Watoto kuwa Anaenda kuwalipia Ada ya Shule, Akirudi Anawaambia Wananhu nimeshawalipia Ada, Na gari za Shule Zitakua Zinawapitia, Nataka Msome Wanangu ili Baadae Mje Mnitunze, Watoto Wanasema Asante Mama.

KIBAYA ZAIDI
Ukifika muda wa kutoa Adhabu, Mkeo yeye hatoi Adhabu, Anawaambia Watoto, Ngoja Babayenu Arudi, Nawewe Ukirudi Unaelezwa na Mkeo matatizo ya Wanao, Unachukua Bakora Unawaadhibu Watoto, Bila kujua kuwa Unazidi Kujenga Uhusiano M'BAYA na Wanao.

NGUMU KUMEZA
Ukifika Uzeeni, Watoto wako Hawana KUMBUKUMBU Yoyote Ya Mema Uliyowafanyia.

NA
UKUMBUKE KUWA-->>
MTOTO ANAANZA KULISHWA SUMU YA MANENO KUTOKA KWA MAMAYAKE KUANZIA UMRI WA MIAKA 9 --- 15

MWANAUME KUWA MAKINI SANA

ZINGATIA HAYO KWA MAISHA YA UZEENI

Jambazi maarufu kwa jina la Rambo auawa na wananchi

$
0
0
Mtuhumiwa wa ujambazi anayedaiwa kuteka magari na kunyang'anya mali za watu wanaotumia barabara ya Kisili - Buhigwe mkoani Kigoma maarufu kwa jina la ‘Rambo’ ameuawa.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kigoma, Martin Ottieno amethibitisha kutokea kwa tukio hilo ambapo mtuhumiwa huyo ameuawa akiwa njiani kupelekwa Hospitali ya Wilaya Kasulu kutokana na kipigo alichopata kutoka kwa wananchi wenye hasira.

Ottieno amesema Rambo alikamatwa katika Kijiji cha Bukuba, Kata ya Janda wilayani Buhigwe akiwa katika harakati ya kuteka magari na watu wanaopita barabarani.

"Kwa kuwa tumehamasisha jamii kumkabili huyo Rambo kwa vile anatumia bunduki za bandia, watu walipomuona waliamua kumkabili na wakamdhibiti kikamilifu kabla ya kutupigia simu (Polisi)," amesema.

Rambo alikuwa raia wa Burundi anayetoka jimbo la Makamba, lakini aliingia Kigoma kwa njia za panya kinyume cha sheria na alikuwa akitumia bunduki bandia zilizochongwa kwa ustadi akitumia mbao na kuviringisha vitambaa ili kuwahadaa watu anaowateka alikuwa tishio kutokana na kuwakwepa polisi mara mbili.

Credit: Mwananchi

Mama Amuua Mtoto Wake Kwa Kumkaba Shingoni na Kisha Kumtupa Mtoni

$
0
0
Polisi Kirinyaga nchini Kenya wamemkamata Mwanamke mmoja kwa tuhuma za kumkaba shingoni mtoto wake wa miaka 5 na kisha kumtupa katika mto Rutui.

Kwa mujibu wa wakazi wa eneo hilo wamesema kuwa Mwanamke huyo mwenye miaka 23 ambaye anaishi peke yake, baada ya kutenda tukio hilo alimtupa mwanae kwenye mto na kukaa kimya akiamini kuwa maiti ya mtoto wake itachukuliwa na maji na kupelekewa sehemu isiyojulikana.

Duru za kuaminika zinasema kuwa ndugu wa mtuhumiwa huyo walianza kumuulizia mtoto  na mtuhumiwa akawa anawajibu  kuwa na  yeye anashangaa kutoweka kwa mwanae.

Aidha mwili wa mtoto huyo ulionekana ukielea katika mto Rutui asubuhi ya June 9 na ndipo wakazi wa eneo hilo ikiwemo mtuhumiwa waliwaita Polisi na kuutoa mwili wa mtoto huyo kisha wakamkamata mtuhumiwa.

Kwa mujibu wa Polisi wa kituo cha Kirinyaga Yaya Chome amesema kuwa mwanamke huyo amefunguliwa mashitaka ya kusudio la kutaka kuua katika mahakama ya Kerugoya.

Chanzo cha mama huyo kutenda tukio hilo la kinyama bado hakijawekwa wazi.

Wasiliana na Dr Mabula Anatibu Upungufu wa Nguvu za Kiume, Busha na Matatizo ya Maumbile Madogo kwa Mwanaume

$
0
0

TUNATIBU NA KUPONESHA KABISA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME UUME MDOGO BUSHA BILA KUPASUA PRESHA VIDONDA VYA TUMBO
Asilimia kubwa ya wanadamu wanasumbuliwa na magonjwa mbalimbali na wapo waliongahika sehemu mbalimbali bira MAFANIKIO MABULA CLINIC ni kituo cha tiba asilia kilichopo mbagara zakhemu njia kuu ya JESHINI JE HUNAUPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME AU UUME WAKO MDOGO NA MWEMBAMBA?

MAPRO PAWER NO 2 ndio Tiba kwa sasa utibu matatizo matatu kwa pamoja 1hitakufanya uchelewe kufika kilekeni dikika 15-20 kwa tendo la kwanza 2 uhimalisha misuli iliyoregea na kusinyaa hasa kwa wale walio hasirika na upigaji punyeto 3 itakufanya upate amu ya kurudia tendo zaidi ya Mara tatu

KWA NINI UJIONE MPWEKE PALE UKUTANAPO NA MPENZI AU MKE WAKO kisa unawai kukojoa au unakomea bao moja tu na huku dawa zipo MAKAKANUA mix ni dawa iliyochanganywa na miti Shamba 9 na Kuwa na uwezo wa kuongeza uume saizi upendayo inchi 5-8 Kwa Urefu na unene sentimita 1-5 dawa hizi hazina madhara yoyote kwa mtumiaji ata wazee wenye umri mkubwa wanapona? zipo dawa za mvuto wa mpenzi mme au mke Kwa masaa matatu tu na kukupigia simu yeye mwenyewe mvuto wa biashara kutengeneza mwonekano mzuri wa mwili kwa wanawake yani shepu tunatibu ngiri miguu mgongo na kiuno kuumwa kupunguza kitambi minyama uzembe matiti na mwili mkubwa

TIBA NA USHAULI MUONE DR MABULA AU PIGA SIMU NO 0752348593 UDUMA ZANGU UTAZIPATA POPOTE ULIPO KAMA UWEZI KUFIKA OFISINI

Kenya waanza mchakato wa kumtafuta Rais wa Kwanza Mwanamke

$
0
0
Huku juhudi za kisiasa pamoja na zile za kisheria kuleta usawa wa kijinsia kupitia kuwa na wanawake wengi katika nyadhfa za juu zikiendelea duniani, kipindi kimoja cha runinga kimeanza nchini Kenya kikiwa na lengo la kuendeleza mjadala huo mbele, kupitia ajenda ya 'wanawake kama viongozi' kwa lengo la kukuza usawa wa kijinsia na viongozi wanawake.

Kipindi hicho kwa jina Bi rais chenye sehemu 26 kinatokana na msururu wa kipindi kama hicho nchini Palestina kwa jina Rais ambacho kilikuwa kikishirikisha kumchagua kijana mmoja wa Palestina kuongoza taifa hilo.

Kitatayarishwa na Media Focus on Africa kupitia ufadhili wa Muungano wa Ulaya na kitashirikisha wanawake wenye vipaji vya uongozi kwa lengo la kuongeza uwezo wao kuchukua nyadhfa mbalimbali za uongozi nchini humo.
''Hatutafuti malkia wa urembo, tunatafuta wanawake ambao ni viongozi''. Sio kuwaleta wanawake katika runinga bali kuwafunza na kuwashauri'', alisema afisa wa mradi huo katika Media Focus on Africa Frenny Jowi.

Watakaofuzu watapewa mafunzi ya uongoizi na ushauri ikiwa ni pamoja na mpango wa kuleta amani utakaoonyesha kwamba wanawake wanaweza kuchukua jukumu la kuzuia kuenea kwa uchochezi wa ghasia.

Wanawake walio kati ya umri wa miaka 20 hadi 70 waliomaliza kidato cha nne , wana hadi mwezi Julai 27 kutuma maombi yao ambayo yatatamatishwa kupitia kupatikana kwa Bi Rais wa Kenya.
''Mwanamke atakayefaulu kushiriki katika kipindi hiki atakuwa mfano wetu sote.Tungependa kufanya kazi na wanawake wote watakaotuma maombi yao katika kipindi hicho kama wizara ya Jinsia'', alisema Lydia Mathia mshauri wa waziri wa Huduma kwa umma ,vijana na Jinsia.
Licha ya kuwa na sheria nzuri zinazotoa fursa ya usawa wa uwakilishi wa wanawake, vijana, walemavu na walio wachache, Kenya bado imesalia nyuma ikilinganishwa na mataifa mengine ya bara Afrika katika kuwa na wanawake katika nyadhfa mbali mbali za uongozi.

Donald Trump Ataka Urusi irejeshwe Kundi la G8

$
0
0
Rais wa Marekani Donald Trump ametoa wito mpya wa kuirudhisha Urusi katika kundi la mataifa yaliostawi zaidi kiviwanda duniani, licha ya kukumbana na upinzani mkali kwa pendekezo lake kutoka kwa wenzake nchini Canada.

"Nadhani ingekuwa jambo la manufaa kuirejsha Urusi," Trump aliwaambia waandishi habari kabla ya kuondoka kwenye mkutano wa kilele wa kundi la mataifa saba yalioendelea zaidi kiviwanda.
"Nadhani ingekuwa vizuri kwa Urusi, Nadhani lingekuwa jambo zuri kwa Marekani, nadhani ingekuwa vizuri kwa mataifa yote ya kundi la sasa la G7. Nadhani G8 ingekuwa bora. Nadhani kuirudisha Urusi lingekuwa jambo zuri. Tunatafuta amani duniani. Hatutafuti kucheza michezo."

Pendekezo la Trump la kuirejesha Urusi ndani ya kundi -- ambalo alilitolea mjini Washington muda mfupi kabla ya kuondoka kwenda Canada -- lilikataliwa mara moja na wanachama wa G7 kutoka barani Ulaya, zikiwemo Uingereza, Ufaransa na Ujerumani katika siku ya kwanza ya mkutano huo.

Urusi ilitimuliwa katika kundi lililokuwa wakati huo G8 baada ya hatua yake ya kulitwaa kimabavu eneo la Crimea mwaka 2014, hatua iliolaaniwa pakubwa kama shambulizi dhidi ya mamlaka ya kujitawala ya Ukraine.

Ushamba na Ulimbukeni wa watanzania kuhusu Zari na Hamisa Mobetto

$
0
0

Watanzania wengi washamba sana.. Baba Nyerere angefufuka leo nadhani angewatia mboko asilimia 80 ya watanzania wote kwa akili zenu zilizojaa upupu. Mzee nyerere hakuacha taifa la majitu majinga hivi. Leo watanzania wamekuwa watu wa kumthamini mgeni kuliko mtanzania mwenzao. Au hutotuvingereza mkimsikia huyo zari basi mnashoboka ebu usee nyinyi. Unamtukana bint wa watu kosa lake nini. Diamond yupo na zari amekwenda kutembea na huyo Hamisa, Kosa la Hamisa ni nini.. Kutembea na Diamond au. Acheni ulimbukeni nyinyi,. Eti timu Zari..hamna za kufanya nyinyi.

Huyu binti Hamisa bado mdogo sana hana hata 25..Kila siku mnamtukana kisa huyo bibi wa Kiganda. Eti timu Zari badala muwe timu kilimo au timu biashara..mnakaa siku nzima mnashinda kwenye mitandao badala ya kufanya Kazi. Taifa la watu wambeya na usengenyaji. Mnatukana binti wa watu eti kaingilia mapenzi. Diamond i support mziki wako..lakini drama zako unafanya huyu Binti anatukanwa sana, Kumbuka unamtoto naye..sidhan km mtoto atafurahi akikuwa Mkubwa aone jinsi Mama yake alivyokuwa anatukanwa kisa wewe. Sikuchagulii mtu wa kumuoa but udhalilishaji huu kwa Hamisa uliusababisha interview yako ya Clouds fm.

Eti Hamisa malaya..nani siyo malaya Tanzania..huyo Zari kwani siyo malaya..si mdangaji tu.. ..Eti Zari ana pesa sana Tununu hana pesa..Pesa za Zari zinakuhusu..Acheni usee nyinyi. Na hii Tabia kubwa ya Midada ya kitanzania hata ikiwa nje ya Nchi kushoboka na wageni..ushamba mzigo sana.

Watanzania nawasihi sana acheni kushoboka na wageni, wapambane mastar wenu, Zari hana mashabiki sehemu yeyote zaidi ya Tz. Kabinti kadogo mnakachukia kwa ulimbukeni tu. Mishamba na miseee sana nyie.

Mdogo wangu wewe ni mzuri sana unayofanyiwa Mungu anaona. Nakushauri move on na endelea kuwa strong. Matusi ya watz yasikuondoe kwenye malengo yako. Diamond we msanii Mkubwa acha drama za kipuuzi.

By Blindspot/JF

Ofa Kubwa ya EID, Pata Bidhaa za Urembo na Kukufanya Mwanaume Kuwa Rijali Kutoka Natural Beauty

$
0
0

OFA KUBWA YA EID

NATURAL BEAUTY PROD
Ni kampuni inayotoa bidhaa ORIGINAL na zilizothibitishwa kiafya.
Sasa inatoa ofa ya punguzo la bei la 10% kwa kila bidhaa wahi sasa upatne tiba za uhakika na uweze kufulahia matokeo mazuri kwa haraka.

🥑🍇🍋🍓 🍒🌱

1.HANDSOME UP ORIGINAL_ Inaongeza uume kwa size uipendayo na kuimarisha misuli (wiki 2) @240,000/=
2.SHARK POWER GELY_ Inaongeza uume inch 6 (wiki 4) @170,000/=
3VigRX CREAM_ Inaongeza uume inch 7.5 hadi 8 (wiki 2-3) @200,000/=
4.Vidonge maalum vya kuongeza nguvu na hamu ya tendo hata kwa wenye kisukari na BP @150,000/=
5. MAXMAN 2-Hii ni vidonge vinavyoongeza nguvu za kiume pamoja na uume @230,000/=
6.VIGA SPRAY OG_ Inaongeza uwezo ktk tendo na kuchelewesha kufika kileleni @150,000/
7.BOTCHO MULT PLUS_Hii ni dawa ya kunywa ya kuongeza ( Hips mapaja na makalio) inapatikana kwa @170,000/=
8.BOTCHO CREAM HOLOGRAM_ Hii ni yakupaka ya kuongeza (HIPS na MAKALIO) @150,000/=
9.LEG BOOSTER_Ni dawa ya kuongeza miguu (CHUPA YA BIA) @150,000/=
10.BODY BOOSTER_ Hii ni yakuongeza mwili pamoja na hamu ya kula vizuri @140,000/= N.K

NB:Hakikisha unapata risiti yenye muhuri halisi wa NATURAL BEAUTY PROD ili kuthibitisha ubora wa bidhaa zetu.
Wasiliana nasi Popote ulipo duniani kwa no÷

(+255) 659618585
au
0759029968
Follow us instagram-
Google
@natural_beauty_prod
@natural_beauty_prod
@natural_beauty_prod
@natural_beauty_prod

Download Hapa Application Mpya ya Udaku Special Uweze Soma Vimbwanga na Udaku Mtaani Kila Siku

Ripoti yawagusa Ngoma na Wenzake Wanne

$
0
0

NA ELBOGAST MYALUKO
Klabu ya soka ya Azam FC kupitia kwa daktari wake Mwanandi Mwankemwa, imetoa ripoti ya wachezaji wake watano ambao ni majeruhi, juu ya hali zao zinavyoendelea na kueleza kuwa mshambuliaji mpya wa timu hiyo Donald Ngoma atarejea dimbani  Agosti 11.


Daktari Mwanandi amesema kuwa wachezaji Yakubu Mohamed, Daniel Amoah, Ladislaus Stanslaus, Waziri Junior na Donald Ngoma wanaendelea na matibabu na wengine wameshapona na kuanza mazoezi mepesi.

Amesema Yakubu Mohamed ambaye alivunjika mguu kwenye mechi ya kirafiki dhidi ya Polisi Combine mwezi Februari, alitibiwa nchini Afrika Kusini na ameshapona akiwa ameanza mazoezi tangu Juni 1.

Kwa upande wake mlinzi Daniel Amoah ambaye aliumia goti kwenye mechi dhidi ya Simba, anaendelea na matibabu na sasa yupo kwenye hatua ya kuanza mazoezi taratibu lakini itamchukua miezi 9 kurejea uwanjani.

Wachezaji Waziri Junior na Ladislaus Stanslaus ambaye alikuwa Costal Union kwa mkopo wanaendelea na matibabu ambapo hivi karibuni watapelekwa Afrika Kusini kwaajili ya matibabu zaidi.

Mshamabuliaji Mzimbabwe Donald Ngoma aliyesajiliwa kutoka Yanga, amefanyiwa vipimo na matibabu nchini Afrika Kusini na ameambiwa ataanza kucheza mwezi Agosti. Aidha Azam FC wameweka wazi kuwa walikuwa wanasubiri ripoti ya vipimo ili waweze kuona kama watamsajili.
Viewing all 104795 articles
Browse latest View live




Latest Images