Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104789 articles
Browse latest View live

Ukweli kuhusu Mo Salah kuivaa Uruguay leo..Jibu Kama Atacheza Lipo Hapa

$
0
0
Kocha mkuu wa Misri Hector Cuper amesema mshambuliaji wa timu hiyo Mohamed Salah yupo kamili kwa asilimia takribani 100 kucheza mechi yao ya kwanza kweney fainali za Kombe la Dunia dhidi ya Uruguay leo.


"Ninaweza kusema karibu asilimia 100 mchezaji Mo Salah yuko vizuri kucheza mchezo wa wetu dhidi ya Uruguay, yeye binafsi yupo tayari kucheza tunachojaribu sisi ni kumpa ujasiri tu'', amesema Cuper.

Mohemed Salah aliumia bega kwenye mchezo wa fainali ya UEFA Mei 26, kufuatia kukumbana na mlinzi wa Real Madrid Sergio Ramos. Awali ilihofiwa kuwa huenda akakosa fainali hizo lakini sasa inaonekana yupo vizuri kuiwakilishi nchi yake.

Misri ambayo ipo Kundi A na timu za Russia, Saudi Arabia na Uruguay leo itaanza rasmi kampeni ya kusaka ubingwa wa dunia ambapo haikupata nafasi ya kucheza fainali hizi tangu mwaka 1990 ambapo Salah alikuwa hajazaliwa.

Mechi hiyo itachezwa majira ya saa 9:00 Mchana kwa saa za Afrika Mashariki, kwenye uwanja wa Yekaterinburg. Uwanja huo una uwezo wa kuingiza mashabiki 35000 lakini utapunguzwa hadi 23000 baada ya fainali za Kombe la Dunia.

Ali Kiba 'Mimi Najivunia Kuwa Mswahili..Asikwambie mtu Acha Uswahili'

$
0
0
"Najivunia sana kuwa mswahili na kuongea Kiswahili na kutumia kiswahil katika kazi yangu ya kunipatia maisha, kwahiyo kila mtanzania ni lazima ajivunie kuwa mswahili, asikwambie mtu acha uswahili"- Alikiba

Nini maoni yako

Zitto Kabwe Ammwagia Sifa Mbunge wa CHADEMA Upendo Peneza Kwa Kupambana Hadi Kodi ya Pedi Ikafutwa

$
0
0
Mbunge wa Kigoma Mjini na Kiongozi wa ACT Wazalendo, Zitto Kabwe amempongeza Mbunge wa Viti Maalumu mkoa wa Kigoma Upendo Peneza (CHADEMA) kuwa amefanikiwa kuacha alama ndani ya bunge la Tanzania akiwa na muda mfupi ndani ya bunge.

Zitto ametoa pongezi hizo ambapo amesema Peneza anaingia katika rekodi za Wabunge waliotumia nafasi yao kushawishi jambo lenye faida kubwa kwa jamii na likafanikiwa ikiwa ni baada ya Serikali kutangaza kuondoa kodi ya VAT kwenye Taulo za Kike zinazotumika na Wanawake kipindi cha hedhi.

Zitto ameandika “Mbunge Upendo Peneza anaingia katika rekodi za Wabunge waliotumia nafasi yao kushawishi jambo lenye faida kubwa kwa jamii na likafanikiwa. Serikali imekubali kuondoa kodi ya VAT kwenye Taulo za Kike zinazotumika na Wanawake kwenye hedhi.”

“Kumekuwa na juhudi za kuleta mabadiliko haya miaka mingi kutokana na kazi za Mashirika kama TGNP Mtandao, SNV, Msichana Initiative nk. Upendo, licha ya kuwa na miaka 2 tu Bungeni aliweza kubeba hoja hii na kuiingiza Bungeni na kuunganisha Wabunge wote kutoka Vyama vyote.” ameandika Zitto

“Licha ya kwamba kampeni yake ilikuwa ni Watoto wa shule wapewe Taulo hizi bure ( litafika tu hilo kupitia mamlaka za Serikali za Mitaa ), amepata mafanikio makubwa kwa uamuzi wa Serikali kuondoa VAT na hivyo kushusha gharama za Taulo hizi. Upendo ameacha alama ( legacy).” Zitto Kabwe

“Mzee William Shelukindo aliwahi kunieleza tofauti ya kuwa Mbunge ( Member of Parliament ) na Mwana Bunge ( a parliamentarian). Kwamba Mwana Bunge ni Mbunge ambaye anaacha alama Katika kazi zake za Bunge na kwamba anaweza kuunganisha wabunge bila kujali Itikadi za Vyama Katika Hoja zenye maslahi ya Umma.”

“Alinieleza haya wakati ananipongeza kuhusu Hoja ya Buzwagi ambayo ndiyo iliyoleta mabadiliko makubwa kwenye sekta ya Madini.”

“Upendo Peneza sasa amepanda daraja kutoka kuwa Mbunge na kuwa Mwana Bunge, a Parliamentarian. Hongera sana Upendo Peneza Mbunge wa Viti Maalumu Mkoa wa Geita ( CHADEMA ) kwa kutendea haki nafasi yako na kufanikisha harakati za wanawake. Umeipa Bajeti ya mwaka 2018/19 taswira ya BAJETI YA KIJINSIA” alimaliza Zitto Kabwe

Maskini..Ommy Dimpoz Afanyiwa Operesheni ya Koo..Je Ataweza Kuimba Tena?

$
0
0
Ommy Dimpoz ni miongoni mwa mastaa ambao wamezoeleka kuonekana kupost picha na videos katika mtandao wa instagram kila mara, lakini kwa wiki kadhaa Ommy Dimpoz ameonekana akiwa kimya katika ukurasa huo na mashabiki kubaki na maswali.

Leo June 15,2018 kupitia ukurasa wa instagram wa Ommy Dimpoz ameelezea chanzo cha ukimya wake na kusema kuwa alikuwa nchini Afrika Kusini ambapo alikuwa katika matibabu ya takribani siku 15 na kufanyiwa opereshani ya koo.

Katika mazungumzo aliyoyafanya na mashabiki zake kupitia ukurasa wake wa instagram hajaelezea sababu ya opereshani hiyo aliyofanyiwa nchini Afrika Kusini na kusema kuwa kwa sasa yupo kwenye mapumziko. VIDEO:

🙏❤️

A post shared by Ommy Dimpoz (@ommydimpoz) on

Viwanja vya makazi: Bunju na MapingaViwanja vipo Kimele, ni km 3 kutoka main road.

$
0
0

Viwanja vya makazi: Bunju na Mapinga
Viwanja vipo Kimele, ni km 3 kutoka main road.
Vipo viwanja size zote kwa bei tofauti: mil 2 for 10/20, mil 4 for 20/20, mil 6 for 20/30, mil 8 for 20/40, mil 12 for 30/40, mil 16 for 40/40 na mil 24 for 40/60. luksa kulipa kwa awamu.
Hakuna dalali, mpigie mhusika: 0757489709

Je Dada Unapenda Kuwa Mrembo na Kaka Kuwa Mtanashati na Kurudisha Heshima ya Ndoa? Soma Hapa

$
0
0

Baada ya kupata cheti cha bidhaa bora 2017-2018, tumeingiza bidhaa zaidi na zenye matokeo ya haraka zaidi bila madhara yoyote.
KWA WANAUME TUNATIBU👇👇
☆Kukosa hamu ya tendo.
☆Kuwahi kufika kileleni na kushindwa kurudia tendo.
☆Maumbile madogo ya uume.
☆Kuchoka sana wakati wa tendo na uume kusinyaa nk.
@markson_beauty_pr tumeandaa tiba bora kabisa kama ifuatavyo:-
1.HANDSOME UP ORIGINAL_ Inaongeza uume kwa size uipendayo na kuimarisha misuli (wiki 2) @250,000/=
2.SHARK POWER GELY_ Inaongeza uume inch 6 (wiki 4) @150,000/=
3VigRX CREAM_ Inaongeza uume inch 6.5 hadi 8 (wiki 2-3) @200,000/=
4.Vidonge maalum vya kuongeza nguvu na hamu ya tendo hata kwa wenye kisukari na BP @150,000/=
5. MAXMAN 2-Hii ni vidonge vinavyoongeza nguvu za kiume pamoja na uume @250,000/=
6.VIGA SPRAY OG_ Inaongeza uwezo ktk tendo na kuchelewesha kufika kileleni @150,000/=
PIA KWA WANAWAKE WANAOPENDA KUWA NA MUONEKANO MZURI ZIPO ZA👇👇👇
1.Kuongeza hips, makalio na mapaja @200,000/=
2.Kushepu mguu (CHUPA YA BIA) @150,000/=
3.Kuwa mweupe mwili mzima bila sugu kwa:-
(a)mafuta @150,000/=
(b) Vidonge @170,000
4.Kurefusha nywele na kutokukatika ovyo @130,000/=
5.Kuongeza hips, makalio na mapaja kwa vidonge (YODI PILLS ORIGINAL) @250,000/=
6.Kupunguza au kuongeza maziwa kuyasimamisha @150,000/=
7.Kubana uke na kuondoa uchafu ukeni @130,000/=
8.Kupunguza unene na manyama uzembe @150,000/=
NB:Hakikisha unapata risiti yenye muhuri halisi na garantii ili kukuhakikishia kufanikiwa kwako

Wasiliana nasi Popote
ulipo duniani kwa (+255)
0767447444
na
0714335378
UTAPATA HUDUMA.
👉🏻OUR WEBSITE:- www.marksnbeuty.org
👉🏻INSTAGRAM PAGE:-
@markson_beauty_pr
#RefushaUume
#OngezaNguvu
#HipsNaMakalio
#BotchoTz
#BidhaaTz

KIVUMBI: Wanawake wagombana Kanisani wakigombea kukaa karibu na Mchungaji

$
0
0
Leo June 15, 2018 kuna hii ya kuifahamu Wanawake wawili nchini Kenya wamewashangaza wengi baada ya kuzozana na kukabana koo kanisani mbele ya Waumini wenzao wakigombania kukaa karibu na Mchungaji wa Kanisa hilo.

Inaelezwa kuwa mwanamke mmoja ambaye alifika kanisani akiwa amechelewa aligundua kuwa Mwanamke mwingine alikuwa ameketi katika kiti alichozoea kukaa ambacho kipo karibu na Mchungaji wa Kanisa lao.

Taarifa zinasema kuwa Mwanamke huyo alimwendea Mwanamke aliyekuwa amekaa karibu na Mchungaji na kumtaka anyanyuke ili akae kitu kilichoamsha mzozo na kuzaa ugomvi mbele ya Waumini wenzao.

Imeelezwa kuwa waumini ambao walibaki wanawashangaa ilibidi waingilie kati kuzima ugomvi huo huku wakidai kuwa waumini hao wanaliaibisha Kanisa lao.

Aidha kwa mujibu wa duru za kuaminika hazijaeleza kama Mchungaji huyo ana mahusiano na Wanawake hao.

Ulikuwa Unajua Rappa French Montana sio Mmarekani?..Hatimaye Apata Uraia wa Marekani

$
0
0
Rapper Maarufu kutokea Marekani French Montana ame-share good news na mashabiki zake kupitia ukurasa wake wa instagram baada ya kupata rasmi uraia wa Marekani na hii ni baada ya kuishi nchini humo kwa muda mrefu na kuomba uraia kwa miaka 20.

French Montana ambaye ni mzaliwa wa Morocco alipata uraia huo na kula kiapo June 14,2018 mjini New Jersey nchini Marekani ambapo unaambiwa utaratibu wa kupata uraia huo ulianza February mwaka 2017.

Rapper huyo alizaliwa na kulelewa nchini Morroco na kuzamia nchini Marekani akiwa na umri wa miaka 13 na kusema kuwa alikuwa hafahamu lugha ya Kingereza lakini alijituma na kuhahakisha anafahamu vizuri lugha hiyo na kwa mafanikio aliyonayo ilikuwa ni kama ndoto kwake.

“AMERICAN DREAM, nchi ambayo ndoto zangu zimetimia, nilitokea Morocco nikiwa na umri wa miaka 13 sikujua hata Kiingereza bali tulikuwa na matumaini na mioyo yenye utajiri . Ilinichukua miaka 20 kufanya hii siku itokee nilijitoa kwa vitu vingi na hata wakati mwingine nilitakiwa kurudisha nyumbani”

Mama Hamisa Mobeto Avujisha Siri Nzito 'Mimi Ndio Huwa Namwambia Hamisa Asitoe Mimba'

$
0
0
Mama mzazi wa Hamisa Mobeto kazungumza kwa mara ya kwanza na Ayo TV na kuelezea baadhi ya mambo kuhusu mwane Hamisa ikiwemo yale yanayotokea kwenye mitandao ya kijamii ambapo kasema kuwa moja ya vitu anavyo mwelezaga Hamisa ni pamoja na swala la kumkatza asitoe mimba huku akitaja sababu za kumwambia hivyo.

Bonyeza PLAY hapa chini kumsikiliza MAMA HAMISA akizungumza.

IGP Mstaafu akamatwa kwa Mauaji ya IGP mwenzie Uganda

$
0
0
Jeshi la Uganda limekamata mkuu wa zamani wa polisi wa nchi hiyo na maafisa wanne wa ngazi za juu kwa madai ya mauaji ya msemaji wa polisi mwaka jana, vyombo vya habari nchini viliripotiwa Alhamisi June 14, 2018.

Kale Kayihura, Mkaguzi Mkuu wa Polisi wa zamani (IGP), na washirika wa karibu walikamatwa kwa sababu ya kushtakiwa kuhusika na mauaji ya Mkaguzi Mkuu wa zamani wa Polisi, Andrew Felix Kaweesi, ambaye pia alikuwa mkurugenzi wa maendeleo ya rasilimali na polisi, kulingana na Daily Vision inayomilikiwa na serikali.

Kaweesi alipigwa risasi na watu wasiojulikana, pamoja na walinzi wake na dereva eneo Kulambiro, kitongoji cha jiji la Kampala, akiwa anaelekea kazini March 17, 2017.

Maiiti mbili zimeokotwa lango la kuingia ofisini Ubungo, Meya amezungumza (Video)

$
0
0
Meya wa Ubungo Boniface Jacob alitoa taarifa katika ukurasa wake wa Twitter June 14, 2018 akiandika hivi nanukuu “Tarehe 07 June 2018 alfajiri na tarehe 12 June 2018 jioni, Siku mbili tofauti, zimeokotwa Maiti mbili za Kiume pembezoni, lango la kuingilia Ofisi za Manispaa ubungo Zikionekana kufungwa kamba na kuteswa kisha kutupwa na ketelekezwa Nje ya ofisi zetu!” mwisho wa kunukuu

VIDEO:

Mobeto kathibitisha ana mimba tena ya Diamond Platnumz

$
0
0

Mobeto kathibitisha ana mimba tena ya Diamond Platnumz..Soma kwenye picha ya juu alichoandika...

TOA MAONI YAKO HAPA TAFADHALI

Tofauti kati ya Eid ul-Fitr na Eid ul-Adha

$
0
0

Waumini wa dini ya Kiislamu kote duniani wanasherehekea sikukuu ya Eid ul-Fitr. Hii ni moja ya sikukuu za idi? Baadhi ya watu, hasa wasio wamini wa dini hiyo wamekuwa wakikanganyikiwa kati ya Eid ul-Fitr na Eid ul-Adha. 

Lakini hizi ni sikukuu tofauti 

Eid ul-Fitr 
Eid ul-Fitr maana yake ni "sikukuu ya kumaliza mfungo" na kutumiwa kuadhimisha mwisho wa mfungo wa mwezi mtukufu wa Ramadhan. 

Siku hii huwa ni siku rasmi ya mapumziko katika mataifa mengi yenye waumini wengi wa Kiislamu. Hata hivyo idadi ya siku za mapumziko huwa tofauti katika nchi mbalimbali. 

Waislamu huanza sherehe hizi kwa kukusanyika kwa maombi ya kila mwaka ambayo hufanyika muda mfupi baada ya macheo. 


Ni kawaida kuwaona Waislamu wakikusanyika katika misikiti na viwanja vya wazi kwa maoni ya pamoja. 

Kabla ya ibada hiyo, huwa wanatoa sadaka kwa maskini (huitwa Zakat) ambayo ni moja ya nguzo kuu katika dini ya Kiislamu. 

Ni kawaida kwa miji mikuu mataifa ya Kiislamu kupambwa sana na sherehe kubwa kuandaliwa, watoto kununuliwa nguo mpya na kupewa zawadi mbalimbali. 

Siku hii huadhimishwa baada ya kuonekana kwa mwezi wa Shawwal, Mwezi huu ulionekana Alhamisi jioni katika baadhi ya mataifa yakiwemo ya Afrika Mashariki na uarabuni. 

Ndio maana sikukuu ya Eid ul-Fitr inaadhimishwa leo Kenya, Uganda na Tanzania nan chi kama vile Qatar, UAE, Saudi Arabia, Indonesia, Uturuki, Morocco, Algeria, Tunisia, Libya na Malaysia wanasherehekea Eid leo. 

Mwezi haukuonekana India na Pakistan Alhamisi hivyo wao watasherehekea Eid ul-Fitr Jumamosi Juni 16 sawa na New Zealand na Australia. 

Eid ul-Adha 
Eid al-Adha ndiyo sikukuu kuu zaidi ya kidini miongoni mwa Waislamu kote duniani na pia huwa ni siku ya mapumziko mataifa mengi yenye Waislamu. 

Nchini Kenya Eid ul-Fitr huwa ni siku ya mapumziko lakini Eid ul-Adha huwa si siku ya mapumziko ya taifa miaka yote. 

Eid al-Adha maana yake ni "sikukuu ya kutoa kafara" kwa Kiarabu na hutumiwa kukumbuka wakati nabii Ibrahimu alipotaka kumtoa kafara mwanawe Ishmael alivyoamriwa na Allah, lakini akapewa kondoo na Mungu amtoe kafara badala yake. 

Sikukuu ya Eid ul-Adha huadhimishwa kuanzia siku ya 10 tangu kuonekana kwa mwezi wa Dhu al-Hijjah. 

Ibada ya Hajj kwenda Mecca huanza siku mbili kabla ya Eid al-Adha na tarehe yake huthibitishwa baada ya kuoenakana kwa mwezi huo wa Dhu al-Hijjah. 

Eid al-Adha ina majina mbalimbali katika mataifa ya Kiislamu: 


Eid el-Kabir nchini Nigeria na MoroccoTabaski nchini Senegal na Gambia.Kurban Bayrami nchini UturukiHari Raya Haji nchini Indonesia, Malaysia na Singapore.Eid è Qurbon, nchini Iran.
Bakr-Id or Qurbani Eid, nchini India, Bangladesh, na kwa Kiurdu pia. 
Waislamu pia huvalia mavazi yao mazuri na ya kupendeza siku hii na huenda msikitini kwa maombi. 

Baadhi humchinja ng'ombe, mbuzi au kondoo kukumbuka kitendo cha imani cha nabii Ibrahimu. 

Hula chakula chenye nyama na huwapa jamaa, majirani na maskini nyama ya mnyama waliyemchinja. 

 Katika baadhi ya mataifa na miji hairuhusiwi watu kuwachinja wanyama kwao nyumbani hivyo vichinjio hutumiwa. Waislamu pia hutoa pesa za hisani kipindi hicho. 

Waislamu hutumia Eid ul-Adha kusherehekea utiifu kamili wa nabii Ibrahimu kwa amri ya Mungu na kuwakumbusha wenyewe kuwa tayari kutoa kafara chochote ili kutimiza maagizo ya Mungu na kumfuata. 

Eid Mubarak 
Eid Mubarak kwa Kiarabu maana yake ni "sherehe au sikukuu njema au yenye Baraka". 

Ni salamu za kawaida wakati wa sikukuu za Eid, Wakati wa Eid ul-Fitr, salamu nyingine maarufu ni 

Ciid wanaagsan - Somalia.Mutlu Bayramlar - Uturuki.Selamat Idul Fitri - Indonesia.Selamat Hari Raya - Malaysia, Brunei, na Singapore.Barka da Sallah - baadhi ya maeneo ya Nigeria.

Master J: Msanii mkubwa hawezi kumlipa Producer

$
0
0

Mtayarishaji mkongwe wa muziki wa Bongo fleva, Joachim Kimario ‘Master J’ amefunguka kuwa wasanii wakubwa huwa hawalipi pesa kubwa kwa watayarishaji wa muziki kwa kigezo kuwa wanatangaza jina la studio. 

Master J amesema hayo wakati kupitia PlanetBongo ya East Africa Radio, ambapo wasanii wakubwa wanatabia za kuchukua ‘beat’ bure anamwambia producer kuwa anakwenda kumtangaza. 

"Mimi nitasema ukweli leo, Msanii mkubwa hawezi kukulipa hela nzuri wewe 'Producer' atakwambia naenda kukutangazia kwa wasanii underground ambao ndio watakao kulipa", amesema Master J. 

Master J ameongeza kuwa kukosekana kwa ushirikiano baina ya watayarishaji wa muziki ndio chanzo cha wasanii kutoheshimu kazi zao na kupelekea wao kubaki katika hali duni.

Afrika Yaanza Vibaya Kombe La Dunia, Misri na Morocco Zatandikwa Bao 1- 0

$
0
0

Dakika 90 zimemalizika kwenye Uwanja wa St, Petersburg kwa Iran kufanikiwa kuibuka na ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Morocco.


Mchezo huo umeshuhudiwa huku milango ikiwa ni migumu zaidi kufungika kama ilivyokuwa kwa Misri dhidi ya Uruguay ambapo bao liliweza kupatikana kuelekea mwishoni mwa mchezo.


Katika dakika ya 90 zikiwa zimeongezwa tano mpira kumalizika, Morocco walijifunga kupitia kwa Aziz na kuweza kuwapa zawadi Iran ambao wameondoka kifua mbele kwa ushindi wa bao hilo pekee.


Morocco imekuwa timu ya pili kutoka Afrika kuweza kupoteza baada ya Misri kufungwa 1-0 na Uruguay kwenye dakika za mwisho za mchezo.

MAAJABU: Anayedaiwa kufariki miaka 18 iliyopita afufuka, ndugu washangaa, wasimulia

$
0
0

Leo June 15, 2018 nakusogezea stori kutoka mkoani Kigoma amabpo Kijana mmoja ambaye katika hali ya kustaajabisha katika mkoa huo, aliyefariki na kuzikwa Miaka 18 iliyopita ameonekana katika Kijiji cha Basanza, akiwa anaongea vizuri na afya yake ikionekana kuwa njema.

Kijana huyO anayeitwa Nicholaus Tahijemaarufu kama Nchaho imeelezwa na wanafamilia kuwa alifariki dunia mnamo mwaka 2000 akiwa na umri wa miaka 16, ambapo sasa ni Miaka 18 baada ya kufanya mazishi ya kijana huyo.

Timu Diamond Mmezidi Mwacheni Basi Hamisa Kidogo Apumue

$
0
0

UHUSIANO wa ki­mapenzi kati ya msanii wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ na mwanadada Hamisa Mobeto ndiyo ishu inayozidi ‘ku-make headlines’ kila kukicha.

Baada ya Diamond kuachana na Zarina Hassan ‘Zari’, Hamisa ndiye anayepewa nafasi kubwa ya kurithi mikoba ya mwanamama huyo mwenye asili ya nchini Uganda lakini mapenzi yake na Diamond yame­kuwa kama mzigo wa miiba kwenye kichwa cha mwanadada huyu, anadhalilishwa sana mpaka anatia huruma. Kwa wafuatiliaji wa mambo, wanaelewa kwamba uhusiano wa Hamisa na Diamond haujaanza jana wala leo, Hamisa amewahi kukiri kwamba alikuwa kwenye uhusiano wa siri na Diamond kwa miaka zaidi ya tisa huko nyuma.

Lakini ishu ilikuja kubumbu­ruka baada ya mwanadada huyo kubeba ujauzito na baadaye kujifungua mtoto wa kiume, Dylan katika kipindi ambacho Diamond alikuwa akiendelea na mapenzi motomoto na mzazi mwenzake, Zari.

Yaliyotokea baada ya hapo wengi watakuwa wanafahamu na kwa faida ya wasioelewa, ni kwamba kitendo cha Diamond kuzaa na Hamisa wakati akiwa na Zari, kilitafsiriwa na mwanamama huyo kama usaliti mkubwa na hiyo ikawa miongoni mwa sababu za ku­sababisha ‘jini mkata kamba’ kulipitia penzi la Zari na Diamond mpaka leo zimebaki stori tu.

Diamond akawa ni kama ‘amem­kunjia’ Hamisa kwa kitendo chake cha kutoa siri kwamba mtoto ni wa Diamond na kumvurugia penzi lake na Zari, wakasumbuana sana mpaka kufikia hatua ya kupelekana mahaka­mani baada ya Diamond kugoma kutoa matunzo ya mtoto.

Baadaye suala hilo lilisuluhishwa mahakamani lakini huo haukuwa mwisho. Hasira za Diamond kumkosa Zari walizokuwa nazo watu wanaojiita Timu Diamond mitandaoni, wakazihamishia kwa kuanza kumtolea maneno yasiyofaa Hamisa na uzao wake.Wale wanaojiita Timu Zari nao wakakasirishwa kwa nini Hamisa aingilie uhusiano wa Diamond na Zari mpaka wakatengana? Nao wakawa wanamsakama mwanadada huyo kila kukicha mitandaoni.

Kundi jingine linalojiita Timu Wema, ambalo lilikuwa na mategemeo makubwa kwamba baada ya Zari kubwaga man­yanga, Wema Sepetu ‘Madam’ atarithi mikoba, nalo likawa na hasira na Mobeto kwa kutibua mi­pango na kuonesha kuwa beneti na Diamond.

Yote tisa, kumi ni familia ya Diamond, akiwemo mama yake mzazi, Sanura Kassim ‘Sandra’ na dada wa Diamond, Esma Platnumz. Kwa nyakati tofauti, tena mara kwa mara, wamekuwa wakip­inga vikali uhusiano wa wawili hao huku wakitoa maneno mengi yasiyo­faa kwa Hamisa.

Ishu mpya ni baada ya juzikati mama wa Hamisa, Shufaa Rutig­inga kuhojiwa na kituo kimoja cha runinga am­bapo amefunguka kwamba Diamond amemnunulia mwanaye nyumba ya ghorofa ambayo ndipo Hamisa, Dylan na mama yake Hamisa wanapoishi hivi sasa.

Matusi anayotukanwa mwan­amke huyu, wengi wakimtuhumu kama amedanganya na matusi anayopewa Hamisa, inafika ma­hali yanakuwa ‘too much’. Una­jiuliza kwa nini watu wanaingilia sana uhusiano huu? Kwa nini Hamisa anaonekana kama adui wa kila anayempenda Diamond? Hamisa akimbilie wapi sasa?

Hamisa ni binadamu kama walivyo binadamu wengine, naye ana moyo na haya ya­nayoendelea yanamuumiza. Hivi watu wanasubiri mpaka ajikute ametopea kwenye dimbwi la matumizi ya madawa yakulevya kwa sababu ya stress ndiyo wamuonee huruma?

Wanasubiri siku wasikie ameamua kuchukua uamuzi wa kuyakatishamaisha yake (hatuombei) kwa sababu ya ku­sakamwa ndipo watu wajifanye walikuwa wanampenda? Ifike mahali huu unafiki wa mitandao­ni ufike mwisho. Hakuna aliyeku­wepo wakati Diamond anaku­tana na Hamisa, hebu waachwe kama ni kuachana waachane wenyewe kwa matatizo yao, siyo kwa sababu ya shinikizo la ndugu au mashabiki.

Sanchi Afungukia ‘Sanchi Feki’ Kuuzwa Dubai

$
0
0

Jane Rimoy ‘Sanchi’
KWA wafua­tiliaji wa mitandao ya kijamii wa­takuwa wameona ile habari iliyotrendi sana inayomhusu staa aliyefungashia Bongo, Jane Rimoy ‘Sanchi’ ya kwamba alipata dili la kwen­da kuhosti shoo huko Dudai huku pia akiongezewa dau kwa ajili ya kwenda kutoa penzi kwa ki­gogo mmoja wa huko.

Kama ni hivyo, basi habari iku­fikie kwamba, mchongo ule ulikuwa ni feki na inaonekana kuna mtu kulicheza dili hilo kwa nia ya kutapeli ama kumcha­fulia jina Sanchi.

Akiizungumzia skendo hiyo iliyowashangaza wengi, Sanchi alisema kuwa, yeye siye aliyehusika kwenye mawa­siliano hayo bali anaamimi kuna watu wamefanya ili kumchafulia jina lake.

“Najua wazi kabisa kuna watu hawapendi maendeleo ya watu wengine hivyo wanatafuta kila namna kuwachafua kwa sababu najua wazi ni vitu vya kutengeneza na ndio maana sijahangaika nao kabisa, naona wanajihangaisha tu.

“Kama kuna Sanchi alitakiwa kwenda Dubai kuhosti shoo na kulala na pedeshee, huyo atakuwa Sanchi feki,” alisema Sanchi.

STORI: IMELDA MTEMA

Kupiga Picha Kuonyesha Nguo za Ndani za Mwanamke Sasa ni Kosa

$
0
0

Tabia hiyo inazidi kukua hasa kutokana na teknolojia inayowezesha mtu kuweka kamera miguuni mwa mwanamke akiwa ameishikilia kwa fimbo maalum.

Tabia ya wanaume kupiga picha maeneo ya kike ya mwanamke kwa kuvizia, maarufu kwa jina la upskirting, huenda ikapigwa marufuku nchini Uingereza, kwa mujibu wa sheria inayojadiliwa bungeni.

Mtu atakayepatikana na hatia ya kupiga picha hizo kwa nia ya kuonyesha nguo za ndani za mwanamke, anaweza kuhukumiwa kifungo cha hadi miaka miwili jela.

"Tabia hii ni uvamizi wa faragha unaomuacha aliyefanyiwa hivyo kujisikia vibaya na amedhalilishwa," waziri mdogo wa sheria, Lucy Frazer alisema, akibainisha msimamo wa serikali kuunga mkono muswada uliowasilishwa na mbunge wa upinzani, Wera Hobhouse.

Watakaopatikana na hatia ya kupiga picha maeneo ya siri ya mwanamke, watachukuliwa wamefanya kosa la shambulizi la kijinsia.

Kwa sasa baadhi ya makosa ya aina hiyo yanashughulikiwa chini ya sheria ya utovu wa heshima, lakini wanaharakati wanasema si matukio yote yanayoweza kushughulikiwa na sheria hiyo.

Mmoja wa wanaharakati hao, Gina Martin alianzisha madai kwa njia ya mtandao baada ya polisi kukataa kumshtaki mtu mmoja aliyemtuhumu kuwa alimpiga picha kwa kutumia simu yake wakati wa tamasha la muziki zikionyesha nguo zake za ndani na baadaye picha hiyo kuchukuliwa kuwa batili.

"Hizi ni habari kubwa," alisema Martin akizungumzia mpango huo wa Serikali ya Uingereza kuharamisha upigaji picha hizo.

"Sasa natumaini tunaweza kuifikia haki kwa waathirika wote kwa sababu wanasiasa wamesikiliza."

Kumchukia Cr7 ni kujitesa, apiga hattrick ya kwanza kombe la dunia

$
0
0

Ilimchukua Cristiano Ronaldo dakika 4 kuiandikia Ureno bao la kwanza kwa mkwaju wa penati, bao hili limemfanya Cr7 kuungana na Pele, Miroslav Klose na Uwe Seeler kama wachezaji waliofunga katika michuano minne tofauti ya kombe la dunia.

Lakini dakika ya 24 Diego Costa alipiga shuti lake la kwanza on target katika kombe la dunia na akafanikiwa kufunga, kabla ya Cr7 dakika ya 44 kufunga bao la pili na kumfanya kufunga mara mbili katika shot on target 3 siku ya leo.

Dakika ya 55 tena Diego Costa aliufanya mchezo kuwa 2-2, lakini Ureno wakiwa bado hawaamini lilipigwa shuti la kushtukiza nje ya box na kuipa Hispania bao la 3, na kuwa mchezaji wa pili kuifungia Hispania goli kwenye kombe la dunia akiwa nje ya box baada ya Fernando Hierro 1998.

Dakika ya 88 wakati mashabiki wa Hispania wakiamini wameshaokota alama 3, Cristiano Ronaldo mchezaji bora wa dunia kwa mara nyingine akaonesha kwamba yeye ndiye bora duniani kwa sasa baada ya kufunga bao la tatu na hii ikiwa hattrick yake ya kwanza katika michuano hii.

Hattrick ya leo inamfanya Cristiano Ronaldo kuwa mchezaji mwenye umri mkubwa zaidi kuwahi kufunga katika kombe la dunia, hii leo Ronaldo alikuwa na miaka 33 na siku 130.
Viewing all 104789 articles
Browse latest View live




Latest Images