Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104799 articles
Browse latest View live

Wafuasi wa CCM na CUF Watwangana Makonde Live Live Wakigombea Uwanja

$
0
0
Wafuasi wa CCM na CUF jana walitwangana makonde wakigombea Uwanja wa Buguruni Chama ili kufanya mkutano wa hadhara.

Mvutano huo ulisababisha Polisi kuingilia kati na kuwatawanya wafuasi hao kisha kuwaruhusu CUF wafanye mkutano wao kwa kuwa ndiyo waliokuwa na kibali halali.

Kamanda wa Mkoa wa Ilala, Mary Nzuki alisema vurugu hizo zilidhibitiwa na Polisi waliowaondoa wafuasi wa CCM ambao hawakuwa na kibali halali.

Mashuhuda walisema ilikuwa vurugu kwa wafuasi wa CCM na CUF baada ya kupigana kwa kutumia viti na mawe na kwamba polisi walizuia vurugu hizo kwa mabomu ya machozi.

Mmoja wa viongozi wa CUF, Mohamed Mluya alisema walipewa kibali cha kufanya mkutano huo jana.

Alisema waliwaonyesha kibali chao lakini wafuasi wa CCM walionyesha kibali kilichoonyesha kuwa walipaswa kufanya mkutano Ijumaa.

Mbunge Kessy Asipigwe, Ajibiwe Hoja Zake Kwani Anayosema Ni Baadhi ya Kero za Muungano

$
0
0
Mbunge wa Nkasi (CCM),  Ally Kessy wiki iliyopita  alilazimika kusindikizwa na askari wa Bunge la Jamhuri kuondoka katika viwanja vya eneo hilo kumnusuru na hasira za wajumbe kutoka Zanzibar waliokerwa na mchango wake kuhusu masuala ya Muungano.

Kessy alisimama bungeni hapo kutoa mchango wake kuhusu Katiba ya Jamhuri akijikita zaidi katika suala la muundo wa Muungano na kusema kwamba Zanzibar inabebwa na Tanganyika.
Nimnukuu, alisema: “Mheshimiwa Mwenyekiti, Tanganyika inabeba mzigo mkubwa ambao haubebeki, hapa tunahudumia wabunge 83 kutoka Zanzibar ambao wanatibiwa wao na wake zao na watoto kwa gharama za Tanganyika wakati hawachangii.”


Aliongeza kuwa haiwezekani kwa Tanganyika kubeba mzigo mkubwa kama huo wakati katika Jimbo lake la Nkasi wananchi wanalia na shida ya maji.Alisema katika kamati yao Namba Moja, Gavana wa Benki Kuu, Profesa Benno Ndulu alitoa semina iliyoonyesha kuwa Zanzibar haichangii chochote kwenye Serikali ya Muungano na kuwa hata mishahara wakati mwingine wanategemea Tanganyika.
Kessy alisema wananchi wakilijua jambo hilo, wataikataa katiba inayopendekezwa na kuitupilia mbali kwa kuwa inatoa upendeleo kwa Wazanzibari na kuikandamiza Tanganyika.

“Mimi naweza kuwa na wanawake sita, nikazaa nao lakini kila mtoto anaendelea kutunzwa na baba yangu, jambo kama hili halivumiliki hata kidogo japo najua kuwa ukweli unawauma,” alisema huku baadhi ya wajumbe wakipaza sauti wengine kumpinga na wengine kuomba mwongozo wa mwenyekiti.

Lakini ninachotaka kusema hapa ni kwamba wananchi wengi wa Tanganyika niliozungumza nao katika utafiti wangu usio rasmi wanaungana na mbunge huyo.

Hapa Dar es Salaam baadhi ya wakazi wanasema iweje Zanzibar yenye watu milioni moja na ushee wawe na wabunge 83 wakati jiji lao lina wakazi zaidi ya milioni nne na lina wabunge wasiozidi kumi?
Alipinga suala la Rais wa Zanzibar kuwa makamu wa rais wa Muungano kwa maelezo kuwa katika mfumo wa vyama vingi jambo kama hilo haliwezekani na kuhoji itakuwaje awe makamu wa kwanza wa rais wakati hajachaguliwa na wananchi wa Tanzania Bara?

Baada ya kauli hiyo, kelele za wajumbe kutoka Zanzibar ziliongezeka baadhi wakisimama na kuwasha vipaza sauti kumshambulia Kessy hivi: “Chizi huyo, chizi huyo, hafai kwanza ni Mwarabu,” zilisikika sauti huku nyingine zikimtaka aombe radhi.

Ukweli ni kwamba alichokizungumza Kessy ndizo kero za muungano kwa upande wa Tanganyika. Kati ya watu 50  niliowauliza jijini Dar kuhusiana na kauli hizo, ni wawili tu waliopingana naye, hivyo ni dhahiri kwamba kauli yake inapaswa kutazamwa.

Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere aliwahi kusema kwamba wachache wakitokea na kutoa wazo ambalo baadaye linaweza kuleta vurugu, ni bora likakubaliwa kama halina madhara. Hivyo hayo ya Kessy yatazamwe na yasipelekwe kisiasa.

Sikuona sababu za wajumbe kutoka Zanzibar kumshambulia Kessy wakati aliyesema hayo ni Gavana wa Benki Kuu, Bwana Ndulu yeye alikuwa akirudia na ndiyo maana akasema hayupo tayari kuomba radhi.
Alidai Ndulu alikuja katika kamati na akasema kwamba tangu kifo cha Abeid Karume (rais wa kwanza wa Zanzibar), Zanzibar hawajawahi kuchangia muungano, hili lilikuwa ndilo la msingi la kulijadili kama ni kweli au ni uzushi na siyo kuzomea na kutaka kumpiga mtoa hoja.

Hatari:Wachungaji Mbaroni kwa Ulawiti wa watoto Kanisani, Wadaiwa Kuwarubuni Kwa Sh 2000

$
0
0
WATOTO sita, wakiwemo wawili wa kiume wenye umri wa miaka 8 hadi 14 wameharibiwa vibaya sehemu zao za siri baada ya kubakwa kanisani na watu wanaodaiwa ni wachungaji.

Wakiwa katika Hospitali ya Mkoa wa Arusha, Mount Meru walikopelekwa kwa matibabu na kuangaliwa maambukizi ya magonjwa ya zinaa, watoto hao walidai kufanyiwa mchezo huo kwa nyakati tofauti  na wachungaji watatu wa kanisa hilo lililopo eneo la  Feed Force, Kwamorombo jijini Arusha.

Mmoja wa watoto hao anayesoma darasa la 4 katika shule ya msingi alieleza kuwa yeye na wenzake wamekuwa wakifanyiwa mchezo mchafu katika kanisa hilo baada ya wachungaji hao kuwapatia shilingi 2,000 za kufungia mdomo.

“Siku moja nilipofika shuleni wenzangu wakaniambia niende pale kanisani tukapewe hela, nilipofika niliwaona wenzangu wengine wakifanyiwa mchezo mchafu na mimi mchungaji aliniambia niiname akanifanyia kitendo kibaya na kunipa shilingi 2,000, niliumia sana,’’ alisema mwanafunzi mmoja.
Mwanafunzi mwingine alisema amekuwa akitoroka shuleni na wenzake na kwenda kwa watumishi hao ambapo huwaingiza katika kanisa hilo na kujifanya wanawaombea baadaye huwafanyia mchezo mbaya.

“Tukifika huwa wanatufungia ndani na kutuambia tuwanyonye, baadaye wanatubaka  na wakimaliza wanatuambia tukisema kwa mtu yeyote watatuchinja na kutuzika ndani ya kanisa lao,” alisema denti huyo.

Wanafunzi hao walieleza kuwa watumishi hao huwarubuni kwa kuwaeleza kuwa watawasaidia kuwasomesha iwapo watakuwa wakienda kwenye kanisa hilo na kuwaingilia.
Mzazi mmoja wa watoto hao, Julius, mkazi wa Kwamorombo alisema mtoto wake alimweleza kwamba amekuwa akifanyiwa mchezo mbaya na watumishi hao baada ya kupewa shilingi 2,000.
Alisema aligundua hilo kufuatia tabia ya mtoto wake kuchelewa kurudi nyumbani.

Naye Mbunge wa Arusha Mjini kwa tiketi ya Chadema, Godbless Lema ambaye alifika hospitalini kuwajulia hali watoto hao alisikitishwa na kitendo hicho na kulitaka jeshi la polisi lifanye uchunguzi wa kina kwa kushirikiana na vipimo vya kidaktari ili kupata ukweli wa tukio hilo.

“Nimeongea na mkuu wa mkoa, Magesa Mulongo ambaye ameahidi kulifuatilia kwa kina suala hili na kujua undani wake,’’ alisema Lema.

Hata hivyo, watoto hao baadaye walihamishiwa katika Hospitali ya Seliani kwa ajili ya vipimo zaidi huku taarifa za awali zikithibitishwa na daktari wa hospitali hiyo kuwa, baadhi yao walikutwa na michubuko na kupanuka sehemu za siri hali inayooneshwa kuingiliwa.

Watuhumiwa wa tukio hilo wanashikiliwa katika Kituo Kikuu cha Polisi jijini hapa  kwa uchunguzi zaidi na Kamanda wa Polisi Arusha, Leberatus Sabas amethibitisha kutokea kwa tukio hilo.

Usikubali Kuogopa Kumuonyesha Mke au Girlfriend Wako Unampenda Kisa Unaogopa Washkaji Watakuona Bwege

$
0
0
Usikubali kuogopa kumuonyesha mke wako au girlfriend wako unampenda kisa unaogopa washkaji au ndugu watakusema umekaliwa naye. Ni tabia mbaya sana unakuta mtu mzima eti anajitamba mbele za wanaume eti "mimi bwana mwanamke hawezi niuliza niko wapi" sasa ndugu yangu wewe ndio ulimtongoza mwenyewe tena ulimsumbua hasa msichana wa watu leo hii anakupigia simu anakuuliza uko wapi unaanza kupanic. Tusifanye vitu ili kuwaridhisha washkaji huko viringeni...tufanye vitu kuwaridhisha wake zetu.... imefikia wakati mwanaume usipokaa bar mpaka saa nane au saa saba usiku unaonekana bwege na ukiangalia ligi ya ulaya sebleni kwako na mke wako unaonekana bwege pia...au usipokua na demu wa nje eti wewe sio mjanja. huu ni upuuzu tubadilikeni jamani. ndio sikatai usikae na washkaji lakini usipitilize sasa. Naona huruma sana unakuta mtu kavaa lipete likuuubwa la ndoa amekaa bar kwenye kiti anasinzia..jamani ?

Follow Udaku Specially Blog on Instagram Kupata Udaku wa Chini ya Kapeti

$
0
0
Usipitwe na Stori Kubwa za Kimjini Mjini na Udaku wa Chini ya Kapeti , Tufuate INSTAGRAM Kwa Kubonyeza Link Ifuatayo na Ikifunguka Bonyeza Kitufye cha Follow chini ya Profile Picha:
>>>>> @Udakuspecially

Justin Bieber Aacha Pombe, Atanganza Maisha Mapya na Selena Gomez

$
0
0
Mwimbaji Justin Bieber ameamua kuyaanza maisha mapya kwa kuacha kutumia vilevi na vyakula visivyoshauriwa kiafya ili kuinusuru zaidi kazi yake ya sanaa.

Kwa mujibu wa chanzo cha gazeti la The Sun, Justin Bieber amekuwa akijigamba mbele ya marafiki zake kuhusu maisha mapya ya afya bora.

“Hanywi tena pombe na ameacha kula vyakula visivyoshauriwa kiafya pia. Alikuwa katika wakati mgumu miezi michache iliyopita na anatumaini hii itampa mwanzo mzuri.” Kimeeleza chanzo hicho.

Mwimbaji huyo ambaye amekuwa katika matatizo ya kisheria hivi karibuni, anaonekana kuyaanza maisha mapya katika uhusiano wake pia baada ya kutangaza kuwa yuko tayari kuwa baba na anataka kumuoa mpenzi wake Selena Gomez.

Kupitia Instagram, Bieber amepost picha inayooashiria hatua yake hiyo na kuandika, “To start something new you have to stop something old.What are you living for? What is your calling? Set standards and boundaries #begreat.”

Exclusive: Babu Tale Azungumzia Ujio Mpya wa Diamond, Kazi Zote Zimetayarishwa Nje

$
0
0
Wakati wimbo wa MdogoMdogo ukiwa bado unasumbua kwenye media, Diamond Platinumz anatarajia kurusha mawe mengine mazito zaidi kwa ajili ya kuwaburudisha mashabiki wake.

Akiongea na tovuti ya Times Fm, Babu Tale ambaye ni meneja wa Diamond amesema mkali huyo anatarajia kuachia nyimbo mbili kwa mpigo na kwamba zote zimetayarishwa nje.

“Tusubirie kidogo, baada ya miezi miwili mitatu tutaongea kwa sababu kuna kazi zinakuja, Diamond anarelease ngoma mbili mfululizo na zote zimetoka nje. Lakini hatuwezi kueongea sasa hivi hadi muda ufike.” Babu Tale ameiambia tovuti ya Times Fm.

Inaonekana Diamond hataki kuacha gap, anakandamizia palepale azidi kwenda juu na kutwaa tuzo nyingi za kimataifa kama alivyofanya mwaka huu.

Endelea kusubiri, tutakujuza hapa hapa. 

Utata Watawala Taarifa za Kuuawa Kiongozi wa Boko Haram

$
0
0
Taarifa zilizosambazwa na baadhi ya vyombo vya habari nchini Nigeria zinadai kuwa kiongozi wa kundi la kigaidi la Boko Haram, Abubakar Shekau ameuwa na majeshi ya Nigeria.

Tetesi hizo zilianza kusambaa Alhamisi iliyopita baada ya jeshi la Nigeria kutoa taarifa kupitia Twitter kuwa wamemjeruhi vibaya kiongozi wa ngazi za juu wa Boko Haram katika eneo la Konduga, Borno.

Wikendi iliyopita taarifa hizo zilianza kuaminika zaidi baada ya picha zinazoonesha mwili wa mtu anaeaminika kuwa Abubakar Shekau kusambaa kwenye mitandao ya kijamii na tovuti mbalimbali.

Hata hivyo, msemaji wa jeshi la Nigeria amekataa kuthibitisha taarifa hizo wala kuzikanusha akidai kuwa bado uchunguzi unaendelea.

“Katika point hii, sitaweza kuthibitisha au kukanusha taarifa hizi. Major General Chris Olukolade (Msemaji wa jeshi la Ulinzi) ataweza kutoa taarifa kuhusu hali hiyo hivi punde. Endeleeni kusubiri.” Msemaji wa jeshi la Nigeria, General Olajide Olaleye aliiambia AFP jana.

Jeshi la Nigeria linapata kigugumizi kuhusu taarifa hizo kwa kuwa miaka iliyopita waliwahi kutangaza kumuua Shekau na baadae akatokea na kutangaza uwepo wake kupitia kipande cha video.

 July 30, 2009, kitengo cha ulinzi cha jiji la Maiduguri walieleza kuwa wamemuua Abubakar Shekau aliyekuwa msaidizi wa mwanzilishi wa Boko Haram, Mohammed Yusuf katika shambulizi lililosababisha vifo vya wapiganaji 200 wa kundi hilo.

Lakini kabla mwaka haujaisha, Shekau alijitokeza kupitia kipande cha video na kukanusha taarifa hizo.

June 30 mwaka jana, vyombo vya usalama vilieleza kuwa Abubakar Shekau anahofiwa kufa katika mapigano makali yaliyotokea kaskazini mwa Nigeria.

Wiki kadhaa baadae alijitokeza tena na kukanusha habari hizo kupiti mkanda wa video.

Here is Shekau, Shekau, Shekau, Shekau, original... I want the whole world to know that I'm alive by the grace of Alla.”

Wanamgambo wa Islamic State Wametoa Video Nyingine inayomuonyesha Mwandishi wa Wingereza Waliomteka

$
0
0
Wanamgambo wa islamic state wametoa video nyingine inayomuonyesha mwandishi wa uingereza John Cantlie aliyekuwa ametekwa nyara.

Cantlie akiongea katika video hiyo ya dakika sita amesema alikuwa ametelekezwa na serikali yake na kwamba nchi za Magharibi zilikuwa zimepuuza uwezo wa wanamgambo wa IS.
Cantlie alitekwa huko syria mwaka 2012 ,na video yake inafanana na ile iliyotolewa wiki chache zilizopita ambapo alisema alikuwa ni mmoja wa wafungwa katika kundi.
IS tayari imeua mateka watatu wa nchi za magharibi na wamenuia kuua waingereza wanaofanya kazi ya kutoa misaada wanaowashikilia mateka.

Nataka Kuzamia Nje ya Nchi, Nishaurini Wakuu Niende Nchi Ipi?

$
0
0
Nimepambana sana hapa nyumbani lakini sioni dalili yoyote ya kufanikiwa nikiwa hapa.

Kama kusoma nimesoma, kazi nimefanya japo sio za kunilipa , nimejaribu ujasiriamali mdogo na vitu vingine vingi lakini sioni nikisogea.

Wataalamu wanasema ukiishi maisha yale yale uku unafanya mambo yale yale na hauoni mabadiriko lakini umeyangangania ujue kufeli kunakusubiri.

Kwa hiyo naomba mnisaidie mawazo ndugu zangu ni nchi gani ninaweza kwenda dunia hii nikafanikiwa.

Naomba mnishauri nchi ya kwenda na kazi zake uko za kufanya au biashara.

Na njia zipi nitumie kufika huko maana pesa yangu ni ya kuungaunga tu sipo safi.


NB: Usiangaike kunishauri juu ya nibaki bongo nifanye nini, sababu sitokusikiliza 
By Stivii

Wasira Aamua Kufungu 'Urais si Mama Mkwe wa Kuonea Haya Wakati Ukifika Nitasema Tu'

$
0
0
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Uhusiano na Uratibu), Steven Wasira amesema hana sababu ya kuona haya kutangaza kuutaka urais kwa kuwa urais si ukwe ila anasubiri wakati mwafaka.

Wasira alitoa kauli hiyo hivi karibuni alipokuwa akizungumza katika mahojiano maalumu na gazeti hili mjini Dodoma.

“Watakaposema ruksa, nitasema na wala kugombea urais si suala la kuonea haya. Ni kutoa huduma kwa Watanzania. Unalionea haya la nini? Kwani kugombea urais ni ukwe?” alihoji Wasira na kuendelea;

“Urais ni mama mkwe wako, hapana. Wakati ukifika nitasema tu. Na mradi kuna wananchi wanasemasema na wananitia moyo, ukifika wakati nitasema.”

Ajabu: Anamkodisha Mpenzi wake kwa Yeyote Apate Pesa ya Kununua iPhone 6

$
0
0
Mwanafunzi wa Chuo kikuu kimoja cha China ambaye jina lake halikutambulika kwa haraka ameamua kufanya ‘uchizi’ ili mradi tu aipate pesa ya kununua aina mpya ya iPhone iliyoingia sokoni, iPhone6.

Kijana huyo wa alionekana akiwa nje ya chuo kikuu cha Songijiang akiwa na bango kubwa lililoandikwa kwa kichina na kutafsiriwa ‘Girlfriend Sharing’.

 Katika tangazo hilo kijana huyo anaeleza kuwa yuko tayari kumkodisha mpenzi wake kwa mtu yeyote atakayeweza kutoa pesa ili jamaa apate kiasi cha kutosha kuinunua iPhone 6 yenye screen kubwa.

Picha ya kijana huyo imesambaa kwa kasi katika mtandao wa kijamii unaotumiwa na wachina uitwao ‘Weibo’ ambao ni kama Twitter.

Tangazo hilo limeambatana na picha za mpenzi wake na amewatoa hofu wateja wanaosita kuingia nae mkataba kuwa hata mpenzi wake ameridhia na yuko tayari kudate na mtu yeyote atakaejitokeza.

Muda wa kuwa na msichana huyo baada ya kumkodi umebainishwa kutokana na malipo yatakayofanywa na mteja. Viwango ni vya saa 1 (10 yuan), siku 1 (50 yuan) au mwezi mmoja (500 yuan).

Hata hivyo, wapenzi hawa sio wa kwanza kujiweka sokoni ili wapate bidhaa ya kampuni ya Apple. Mwaka jana katika uzinduzi wa iPhone 5, wanandoa wa Shaghai waliwaweka sokoni watoto wao watatu ili wapate pesa ya kununua computer na simu za iphones lakini walikamatwa na kufunguliwa mashitaka.

Lakini pia kijana mdogo wa Hunan alijitolea kuuza figo lake ili apate pesa ya kununua iPad na iPhone.

Siyo hayo tu, hivi karibuni mwanaume mmoja wa Saudi Arabia ametaka kupewa iPhone 6 kama mahari ya dada yake hata kabla aina hiyo ya simu haijazinduliwa Bahrain.

Maajabu: Kutana na Mwanaume Anayefika Kileleni Mara Mia Kwa Siku

$
0
0

37 year old Dale Decker (pictured above with his wife) says his life is being ruined by having 100 orgasms a day. Speaking for the first time about his near-constant erection which he says he doesn't enjoy and says has cost him friends and destroyed his family, Dave says he hardly goes out because of the embarrassment he feels when the orgasms start coming in public places...

According to the UK Mirror, Dave's condition is called Persistent Genital Arousal Syndrome which he developed in September 2012 when he slipped a disk in his back while getting out of a chair.
"Imagine being on your knees at your father's funeral beside his casket - saying goodbye to him and then you have nine orgasms right there, while your whole family is standing behind you. It makes you never want to have another orgasm for as long as you live. There's nothing pleasurable about it because even though it might feel physically good - you're completely disgusted by what's going on.” Dave said..

 "If you're in public, if you're in front of kids - it's disgusting and it can break you real fast. It happened to me at the grocery store and when it was over there were around 150 people looking straight at me - why would I leave the house when something like this can happen.”
Dale lives in Two Rivers, Wisconsin with his wife April and two sons Christian, 12, and Tayten, 11.
While she does everything she can to support him, April, 33, is finding Dale's condition just as hard to live with as he is. She said:
“We really struggle right now as he is unable to work and supply for his family and I feel like all the strain is on me. It's really upsetting, we don't do things that man and wife should do and we argue over things that should not be affecting us. Because he sometimes has episodes at night we took the decision to sleep in separate beds. That can be very frustrating. You want the comfort from another person, particularly your husband but we don't have that. I really miss the old Dale, we used to have a lot of fun and one day I pray that he will come back to me. Maybe the doctors will find a cure for this - I don't know - I just really hope that they do.”
Despite suffering from a near constant erection Dale and April rarely have sex. Dale said;
“Occasionally we will but it's very frustrating for both of us as this condition has left me unable to finish. I've tried reading about it, tried going to doctors but nobody can help me - I don't know what I'm going to do. I just want to get my old life back - I just want to get back what this condition has taken from me.”

Angalia Video Jinsi Wanigeria Wanavyokufa Kwa Njaa na Kiu Wakizamia Ulaya Kupitia Jangwa la Sahara

$
0
0
Samahani Kwa Video Hii Inatisha , ila Hali ndo ilivyo huko Nigeria Kwa wale wanaozamania ulaya kupitia jangwa la Sahara, Ukiangalia ramani ya Dunia Utaoni Nigeria Imepakana na nchi za ulaya ila hapo katikati kuna jangwa kubwa la sahara sasa baadhi ya Wanaigeria Hujaribu kukatiza Jangwa hilo kwa kutembea kwa Miguu ambapo wengine uishiwa na chakula na maji na kuishia kufa.. Angalia video Hapa chini:

Mkurugenzi wa Manispaa ya Mtwara Amewalazimisha Waalimu Kuchangia Jumla ya Shilingi 48,000/= Bila idhini yao

$
0
0
Katika hali isiyo ya kawaida, mkurugenzi wa Manispaa ya Mtwara/Mikindani Bwana Limbakisye Shimwela amewalazimisha waalimu wa manispaa hiyo kuchangia jumla ya Shilingi 48,000/= bila idhini yao kwaajili ya
1. Fulana alizowagawia kipindi cha mwenge, ambazo hata hivyo hawakuambiwa wala kukubaliana kuwa zitalipiwa.
2. Mchango wa elimu ambapo hakutoa mrejesho wa mapato na matumizi kwa mchango wa mwaka jana.
3. Mchango wa ujenzi wa maabara ambapo hakuwashirikisha katika kupanga kiwango
cha kuchangia.
Aidha ufafanuzi wa michango hiyo ni kwamba 13,000/= Ni fedha kwaajili ya fulana na kofia, 5,000/= mchango wa maendeleo ya elimu na 30,000/= kama mchango wa ujenzi wa maabara katika shule za sekondari. Suala hilo limeibua maswali mengi kwani walengwa hawakuitwa ili kukubaliana kwa pamoja kuhusu michango hiyo.
Ikumbukwe kuwa miezi michache iliyopita mkurugenzi huyu alitoa barua zilizojaa vitisho kwa waalimu ambao hawakwenda kukesha katika viwanja vya shule ya sekondari Umoja na waliokesha hawakulipwa chochote kama sheria inavyotaka kwamaana tukio hilo lilifanyika muda ambao si wakazi.
Waalimu wengi wamevunjika moyo kutokana na vitisho na matamko ya mara kwa mara ya mkurugenzi huyo hasa yale yanayohusu michango ambayo hata hivyo hawahusishwi katika makubaliano.
Licha ya barua za kuwataka waalimu wasiolala kwenye mwenge kutoa maelezo, Mkurugenzi huyo amewaandikia barua walimu ambao hawajatoa mchango wa fulana na kofia kuwa wanatakiwa kufanya hivyo mapema kwani walikopeshwa fulana hizo japo hakuna vielelezo vinavyo thibitisha hayo.

Facebook Kuanza Kuwachaji Dola 2.99 Watumiaji wa Mtandao Huo Kila Mwezi Kuanzia Mwezi wa Kumi na Moja

$
0
0
At a press conference this morning, Facebook rolled out their new monthly service plan. Beginning November 1st of this year, the social media giant will start charging members $2.99/mo to use services which users currently enjoy for free.
“After thinking long and hard about this decision, at the end of the day, we were forced to add this monthly fee,” Facebook founder and CEO Mark Zuckerberg told reporters. “If we don’t do something about our rising costs now, Facebook could face an unrecoverable financial burden and become obsolete.”

Mwigizaji Yusuph Mlela Ampiga Dongo Nora Amwita Kibibi

$
0
0
KUFUATIA madai ya hivi karibuni ya mkongwe wa filamu Bongo, Nuru Nassoro ‘Nora’ kuwa baadhi ya waigizaji hawana sifa za kuwa wacheza sinema zaidi ya kuuza sura, msanii Yusuph Mlela amempa dongo zito akisema licha ya umri kuwa mkubwa, pia ana matatizo flani yanayomsumbua.

“Nora naona siyo kosa lake kwani alishaugua yule,  isitoshe ameshakuwa bibi hivyo nimemsamehe na sina tatizo naye kwani najua, lingekuwa jambo la maana kama angetufuata na kutushauri kama mkongwe lakini si kwa njia aliyofanya,” alisema Mlela.

Hivi karibuni Nora aliwataja mastaa wenzake wa filamu akiwemo Mlela, Chuchu Hans, Steve Nyerere, Kajala na Batuli akisema hawawezi kazi zaidi ya kuuza sura tu.

Mpambano Unaendelea Wema Sepetu Awatunza Fedha Chafu Yamoto Band

$
0
0
“MADAM…Madam…Madam…” ndizo kelele zilizosikika wakati Beutiful Onyinye, Wema Sepetu ‘Madam’ alipokuwa akimtunza fedha nyingi dogo machachari wa Bendi ya Yamoto, Asilahi Isiyaka ‘Dogo Aslay’.

Tukio hilo limetokea ndani ya ukumbi wa Dar Live uliopo Mbagala-Zakhem na kuweka historia kwa Wema kuwa staa wa kwanza ‘kumwaga’ fedha wakati wa uzinduzi wa bendi ya Yamoto.

MAMBO YALIVYOANZA
Awali, wakati bendi ya Yamoto ilipokuwa ikitumbuiza, ulifika wakati kiongozi wa bendi hiyo, Said Fella alitambulisha uwepo wa Wema kwa kudai amemuwakilisha bebi wake, Nasibu Abdul ‘Diamond’ hivyo apande jukwaani na kusema chochote lakini mrembo huyo akasema kilichompeleka ukumbini hapo ni uzinduzi wa Yamoto Band.

“Jamani nimekuja hapa kwenye uzinduzi wa Bendi ya Yamoto na siyo kumuwakilisha Diamond, ya huku hayamuhusu kabisa sasa semeni niwaimbie wimbo gani,” alisikika Wema Sepetu na kuanza kuimba wimbo wa Niseme ambao mashabiki waliupendekeza.

AMWAGA FEDHA
Mrembo huyo asiyechuja tangu alipotwaa taji la u-miss Tanzania (2006), akiwa na wapambe wake, baada ya kuimba kidogo, alichukua pochi yake na kuanza kummwagia fedha mfululizo Dogo Aslay huku akiwa anamzunguka kwa kucheza.

ASLAY APAGAWA
Kwa fedha hizo zilizokadiriwa kuzidi milioni moja alizotunzwa Aslay, ilifika wakati dogo huyo akawa anaziangalia tu kama bubu na kupigwa butwaa huku akiishia kuzitazama bila kuimba chochote.

BAUNSA AMZUIA WEMA
Katika hali iliyowashangaza wengi, baunsa mmoja aliyekuwa akimlinda Wema alimzuia staa huyo kuendelea kutoa fedha zaidi akidai zimetosha ndipo akaacha na kushuka jukwaani.

KWA NINI ASLAY TU?
Wakati zoezi hilo likiendelea, kuna baadhi ya mashabiki waliibua minong’ono wakihoji kwa nini atunzwe Aslay peke yake wakati bendi hiyo ina wakali wengine watatu, Malomboso, Enock na Beka?
“Mbona kama anampendelea Aslay tu  wengine hawatunzi ona hela zote ameshikilia yeye tu kweli, inaonekana anamzimia sana Aslay, si bure, haikatazwi lakini,” alihoji shabiki mmoja aliyekuwa akifuatilia shoo hiyo.

MPAMBANO UNAENDELEA!
Wema ameonekana kuja juu kwa sasa kifedha, wiki iliyopita alifanya tukio kama hilo katika Ukumbi wa Thai Village Masaki kwa kumtunza ‘pesa ndefu’ mwanamuziki wa Bendi ya Skylight, Sam Mapenzi huku ikidaiwa ni mwendelezo wa kampeni ya kumziba mdomo aliyekuwa shosti wake, Kajala Masanja ambaye inadaiwa kwa sasa yuko ‘vizuri’ kifedha.

Aliyeua Mke Kwa Wivu wa Mapenzi Naye Auawa na Wananchi Wenye Hasira Kali

$
0
0
WATU wenye hasira wamempiga hadi kumuua mwanamume, aliyemuua mke wake kwa kumpiga rungu tumboni.

Kamanda wa Polisi mkoani hapa, David Misime, alisema tukio hilo la Septemba 20, mwaka huu katika Kijiji cha Mzogole wilayani Mpwapwa, ambapo mtu mmoja, Mwajuma Chomola (48) aliuawa kwa kupigwa na rungu tumboni upande wa kushoto na mume wake, Richard Kodi (55).

Hata hivyo, alisema Kodi naye aliuawa Septemba 21, mwaka huu baada ya kushambuliwa na wananchi waliojichukulia sheria mkononi. Alifariki dunia akiwa anaendelea na matibabu katika Hospitali ya Wilaya ya Mpwapwa.

Aliuawa baada ya wananchi hao kupata taarifa kuwa mwanamke huyo, amekufa baada ya kupigwa na mtu huyo.

Misime alisema uchunguzi wa awali, unaonesha kuwa chanzo cha mauaji hayo ni wivu wa mapenzi.

Kamanda huyo alisema Kodi alimuua mkewe huyo, aliyekuwa akiishi naye baada ya kuchelewa kurudi kutoka kwenye sherehe, iliyokuwa kijijini hapo, akidhani kuwa alikuwa ameenda kwenye masuala mengine.

Samwel Sitta Amwaga Sifa Kede Kede Kwa Chama Kipya ACT-Tanzania Ndani ya Bunge

$
0
0
Mwenyekiti wa Bunge la katiba ndugu Samwel Sitta ameendelea kudhihirisha kwa umma wa watanzania juu ya uwepo wa chama cha siasa kilichopata usajili ndani ya muda mfupi sana cha ACT-Tanzania.

Huku akionekana kufurahishwa na ujio wa chama hiki Samwel Sitta anasema..."Wageni wengine ni Katibu wa ACT-Tanzania Jimbo la UBUNGO, chama hiki ni kipya ila kinakuwa kwa kasi sana...mwisho wa kunukuu" Hapa alikuwa anafanya utambulisho kwa wageni wawili wa chama hiki cha ACT-TANZANIA toka jimbo la UBUNGO waliofika kusikiliza uwasilishaji wa katiba mpya inayopendekezwa.

My Take:
Kwanini ACT-Tanzania inapata publicity kubwa sana toka kwa vyombo vya habari vya CCM au wanachama wake. Mfano UHURU, MZALENDO, STAR TV, TBC1, JAMBO LEO, nk. Na makada wengi wa CCM wanafurahia ujio wa chama hiki?
Hawa viongozi wa ACT-TANZANIA walikwenda kufanya nini bungeni kama sio wanaungana na ujinga unaoendelea bungeni?
Viewing all 104799 articles
Browse latest View live




Latest Images