Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104793 articles
Browse latest View live

JPM 'Sio kweli kwamba watanzania wanashindwa kuwekeza'

$
0
0
"Sio kweli kwamba watanzania wanashindwa kuwekeza, lakini pia sio kweli kwamba Tanzania hatuna wazalendo wakufanya mageuzi makubwa ya kiuchumi katika nchi hii mimi ninaamini wapo"- Rais Magufuli

Nini maoni yako


Mwakyembe 'Kuruhusu Uraia Pacha sio Sababu ya Taifa Star Kuja Kufanya Vizuri'

$
0
0
Waziri Mwakyembe asema kwamba uraia pacha hauwezi kuwa sababu ya Taifa Stars kuja kufanya vizuri ikiwa itategemea wachezaji wawili watatu wanaoishi nje ya nchi.

Nini maoni yako?

Siwezi Kwenda Kula Chakula kwa Shishi Food;-Mziwanda

$
0
0

Mwanamuziki Nuh Mziwanda amefunguka na kusema kuwa kamwe katika maisha yake hawezi kwenda kula chakula kwa shiloleh mwanamke ambae aliwahi kuwa nae katika mahusiano hapo awali lakini baadae kutengana na shiloleh kuolewa na mwanaume mwingine.

Nuh anasema kuwa hata kama kuna chakula cha aia gani lakini hatokaa hata siku moja kukanyaga pale kwa sababu wameshagombana na aatakuwa anaenda pale kufanya nini .

Siwezi kwenda kula chakula kwa kwake,siwezi hata kukanyaga mguu wangu pale  siwezi tu.naendaje mii kula pale na wala haitatokea mimi kwenda kula pale hata kama kuna msosi mtamu lakini pia hata mama yangu anajua sana kupika.

Nuh na shiloleh waliwahi kuwa wapenzi kwa muda mrefu  kipindi cha nyuma lakini walikuja kushindwana kwa tetesi kuwa Nuh alikuwa akiteswa sana na Shiloleh na kupigwa  sana shiloleh.

Serikili yanuia kufungua fursa za kibiashara katika Kimondo cha songwe

$
0
0

Wawekezaji na wafanyabiashara wametakiwa kujikita kwenye uwekezaji wa kimondo kilichopo mkoani songwe eneo ambalo linafanyiwa marekebisho hivi sasa ambapo itaandaliwa  hafla kubwa  itakayofanyika siku ya maadhimisho ya kimondo duniani ambayo hufanyika kila mwaka juni 30, ikiambatana  na ugawaji wa maeneo ya uwekezaji wa miradi mikubwa ikiwemo hotel, viwanja vya kisasa vya michezo, kumbi za starehe, pamoja na fursa mbalimbali za uchumi.

Muungwana blog imetembelea kimondo hicho na kuzungumza na baadhi ya watalii waliofika eneo hilo ambao  mbali ya kuona kama ni nafasi ya kipekee kukiona kimondo hicho pia wameahidi kuwa mabalozi huko wanakokwenda, lakini wametaja dosari ya miundombinu ya mradi huo.

Zainabu Vullu ni mmoja wa watalii waliofika eneo la kimondo amesem kuwa licha ya kuwa ni mara yake ya kwanza kufika kujionea kivutio hicho lakini ameomba watanzania kujifunza kuthamini wao kwanza kuliko wageni wanakuja kufaidi kuona na kujua historia ya kimondo huku wenyeji wakishindwa kutumia fursa hiyo huku Jasmine Tisekwa akisema kuwa kuanzia sasa baada ya kufika eneo la kimondo cha mbozi watakuwa mabalozi wazuri kwa watanzania wengine.

Mkuu wa mkoa wa songwe bi. CHIKU GALLAWA amesema ni wakati mwafaka sasa  wawekezaji kujitokeza na kuwahi nafasi za kuwekeza kwenye eneo la kimondo kwa kuwa maboresho ya sasa yataibua fursa mbalimbali za kiuchumi na biashara na kuongeza  mahitaji ya huduma za jamii.

 Aidha  mkuu wa mkoa amewataka wakurugenzi wa halmashauri zote za mkoa wa songwe  kuhakikisha wanaungana  na kufanya maboresho ya miundombinu ya eneo la kimondo kilichopo katika kijiji cha ndolezi kata ya mlangali wilayani mbozi lengo ni kupanua fursa za uwekezaji kupitia kimondo hicho

Bocco atwaa Tuzo ya Mchezaji bora wa Ligi kuu bara

$
0
0
Mshambuliaji wa klabu ya Simba, John Bocco, ameibuka mshindi wa Tuzo ya Mchezaji Bora wa Ligi Kuu Tanzania Bara msimu wa 2017/18.

Bocco ametwaa tuzo hiyo huku akiwapiku wachezaji wenzake beki Erasto Nyoni na Emmanuel Okwi ambao pia walikuwa kwenye kinyang'anyiro.

Ukiachana na tuzo ya mchezaji bora VPL, Bocco ambaye ni Nahodha wa kikosi cha Simba amekuwa na msimu mzuri kwa kufanikiwa kubeba pia tuzo ya Mo akiwa mchezaji bora ndani ya timu hiyo.

Vodacom ambao ni wadhamini wakuu wa ligi wamempatia kitita sha shilingi milioni 12 Bocco kama zawadi kutokana na kitengo cha kinyang'anyiro alichokuwa amewekwa.

Okwi ambaye ameshindwa katika kitengo hicho, ametwaa tuzo ya mchezaji bora wa ligi kwa kufikisha idadi ya mabao 17 aliyofunga sambamba na zawadi ya shilingi milioni 3.

Aidha, timu bingwa ambayo ni Simba imepokea kitita cha fedha, shilingi milioni 96 huku Azam ambao ni washindi wa pili wakibeba milioni 48 na Yanga waliomaliza msimu wakiwa namba 3 wakijinyakulia milioni 27.

Kikosi bora cha Wachezaji Ligi kuu bara 2017/18 Simba yaongoza

$
0
0
Kikosi bora cha Wachezaji Ligi kuu bara 2017/18 Simba yaongoza
 Muungwana Blog 5  Sunday, June 24, 2018


Wachezaji waliounda kikosi bora cha msimu wa 2017/18 katika Ligi Kuu Vodacom Tanzania Bara.

1. Aishi Manula
2. Hassan Kessy
3. Shafiq Batambuzi
4. Erasto Nyoni
5. Kelvin Yondani
6. Patrick Tshishimbi
7. Shiza Kichuya
8. Tafadzwa kotinyu
9. John Bocco
10. Emanuel Okwi
11. Marcel Kaheza

Download Hapa Application ya Udaku Special Kwenye Simu Yako Kushuhudia Vimbwanga Mtaani na Stori za Mapenzi

Miujiza ya Maalim Khatibu Kutoka Bagamoyo Pwani

$
0
0
MAALIM KHATIBU anawashukuru wale wote wanaopiga simu za shukrani, na wale ambao bado wanamatatizo musikate tamaa kwa kuchelewa kupokelewa simu zenu,

(Rudisha mahusiano yako ndani ya masaa 72 tu)

MAALIM KHATIBU Ni  mtaalam na mnajimu maarufu wa nyota na kubashiri mambo yanayo watesa binadamu duniani kote na kupata ufumbuzi, Anatumia kitabu cha QUR'AN dawa za asili ya afrika na njiwa,

Je Umeachwa na UMPENDAE awe Mme/Mke na bado unampenda? Je Umekimbiwa na Mmeo/ Mkeo n anaishi na mtu mwingine? Je Umejaribu sehemu nyingi bila mafanikio? Mpigie simu MAALIM KHATIBU sasa hivi ujionee Muujiza wa Papo kwa Papo, Anauwezo wa hali ya juu wa kusambaratisha mahusiano yao na kumrejesha kwako haraka sana na Kumfanya Atimize Ahadi zote Ndani ya Muda Mfupi Endapo Utafwata maelekezo yake,

 ZINDIKO LA NYUMBA NA BIASHARA, PETE ZA BAHATI, HUMALIZA KABISA TATIZO   HUZUIA CHUMA ULETE KWENYE BIASHARA, HURUDISHA MALI ZILIZOPOTEA, NA KUPONYA MAGONJWA SUGU, ANAO UWEZO WA KUMRUDISHA ALIE MBALI AU ALIECHUKULIWA MSUKULE, KUPANDISHA NYOTA NA KUSHINDA BAHATI NA SIBU, KASAFISHA NYOTA NA KUKUPA MVUTO WA AJABU, KUTOA NUKSI NA VIFUNGO MBALIMBALI,  MAFANIKIO YA MAISHA NA UTAJIRI BILA MASHARI, NA MENGINE MENGI YA SIRI,

JE UMAHANGAIKA KUPATA MTOTO BILA MAFANIKIO? WASILIANA NA MTAALAMU HUYU KWANI YEYE HUFAULU PALE WOTE WALIPOSHINDWA, PIA UMALIZA KAZI ZILIZO SHINDIKANA NA WATAALAM WENGINE NDANI YA MASAA 24 TU,

(NA ANATIBU KWA NJIA YA SIMU UKIWA NCHI YOYOTE AU MKOA WOWOTE ENDAPO UTAFWATA MAELEKEZO YAKE)

Kwa ushauri na mawasiliano  zaidi Piga SIMU No:

Mobile +255 710-332103
WhatsApp +255 766-705404
Instagram: Follow@maalim_khatibu

USHAURI: Ni vyema kupiga simu kuliko kutuma sms ili upate msaada kwa wakati.

Mnyeti Afungua Kiwanda Kilichofungwa na Mkea Mkuu wa Serikali, Ataka Akamatwe Yeye Badala ya Mmiliki

$
0
0
Mkuu wa Mkoa wa Manyara, Alexander Mnyeti amekifungua kiwanda cha pombe kali cha Mati Super Brand cha mjini Babati kilichofungwa na Mkemia Mkuu wa Serikali huku akitaka akamatwe yeye, badala ya wamiliki wa kiwanda hicho.

Mnyeti ameyasema hayo juzi wakati akichukua uamuzi huo ambapo amefafanua kwamba hakubaliani na sababu zilizotolewa mpaka kiwanda hicho kufungwa

Akitoa maelezo Mnyeti amesema mwekezaji huyo amefunga mitambo yake na kutoa ajira kwa wananchi, badala ya kupewa ushirikiano watendaji wanaohusika, wao ndiyo  wanamkwamisha kwa kukifunga kiwanda, ikiwa ni takribani miezi mitatu sasa.

"Bado kuna watu wanaandaa mazingira ya rushwa, yaani badala watumie hata siku tatu za kumshauri kitaalamu wanakimbilia kufunga kiwanda. Kuna baadhi ya watumishi wa Serikali wana ukiritimba mno, sasa mimi nakifungua kiwanda hiki halafu wakija wanikamate mimi," alisema.

Mkemia Mkuu wa Serikali alikifunga kiwanda hicho kwa maelezo kuwa kimekosa kibali cha kuidhinisha matumizi ya kemikali za kuzalisha pombe hizo Machi, 2018

Balozi wa Syria aiomba radhi Serikali ya Tanzania

$
0
0
Balozi wa Syira nchini Abdulmonem Annan ameiomba radhi serikali ya Tanzania baada ya kusambaa kwa video iliyomuonyesha akisema atahamasisha raia wa Syria, wasiwekeze nchini kwa kile alichodai polisi hawalifanyii kazi suala la kuporwa fedha kwa Ofisa Ubalozi wa Syria.

 Machi 20, Ofisa Ubalozi huyo, Hassan Alfaouri alishambuliwa na watu wasiojulikana na kuporwa zaidi ya euro 9300(zaidi ya Sh 25 milioni).

Baada ya tukio hilo, Balozi huyo alisema  alitoa taarifa kwenye mitandao ya kijamii  kwa njia ya video akisema kuna ufuatiliaji hafifu wa suala hilo na hivyo atahamasisha raia wa Syria wasije kuwekeza nchini.

Akizungumza na waandishi wa habari jana Mkurugenzi wa Idara ya Mashariki, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Suleman Salehe alisema maneno aliyosema balozi Annam yalikuwa ni ya uchochezi hivyo waliamua kufanya nae mikutano minne.

Alisema wao kama Wizara walifanya jitihada na kuhakikisha jeshi la polisi linafanya uchunguzi na kuhusiana na tukio hilo na kuwakamata watu wawili ambao ni dereva na katibu wake.

“Wizara inamshukuru Balozi kufunguka na kutoa taarifa muhimu kuwa ametaarifiwa na jeshi la polisi kuwa watuhumiwa wawili wamekamatwa na sehemu ya kiasii cha fedha kimepatikana”amesema Salehe

Amesema kwa kuwa balozi amebakiza miezi michache  amalize muda wake hapa nchini, Wizara itaanda taarifa ili aweze kukutana na Mkuu wa jeshi la polisi na washughulikie suala hilo.

Godbless Lema Aguswa Na Hali za Vigogo wa Escrow Wanaosota Mahabusu

$
0
0
Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema amekiri kuwaone huruma watuhumiwa wa makosa ya uhujumu uchumi, wafanyabiashara Harbinder Seth  pamoja na James Rugemalila kwa kuitaka serikali ikamilishe upelelezi kwani watu hao wanapitia mateso kwa kukaa mahabusu.

Lema ameonyesha kuguswa na watu hao baada ya picha zao kusambaa siku ya Jumatano hii walipokuwa wamekwenda kusikiliza kesi yao huku upande wa mashtaka wakidai kuwa bado upelelezi haujakamilika.

"Ninaona huruma juu yenu. Serikali kamilisheni upelelezi juu ya watu hawa kama wanastahili adhabu walipe walichopanda, kuwa mahabusu bila kesi yako kusikilizwa ni mateso kuliko mnavyoweza kufikiri".

Ameongeza Pengine wanastahili adhabu lakini ni vyema Mahakama ifanye maamuzi.

Seth na Rugemarila wanakabiliwa na mashtaka 12 ya uhujumu uchumi kwa kula njama, kujihusisha mtandao wa uhalifu, kughushi na kutoa nyaraka za kughushi.

Pia, wanadaiwa kujipatia fedha kwa njia za udanganyifu, kutakatisha fedha na kusababisha hasara ya Dola 22 milioni za Marekani na Sh309.46 bilioni

Afande Sele Apigwa Onyo Kali

$
0
0

Msanii mkongwe wa BongoFleva nchini Afande sele ameonywa na rapa Zaiid kuacha kubishana na umma walioupitisha wimbo wake wa 'wowowo' mpaka kufikia hatua ya kutambulika kila mahali kwasababu zake binafsi zisizokuwa na tija.

 Hayo yameelezwa na Zaiid wakati alipokuwa anazungumza kwenye kipindi cha 'FNL' inayorushwa mubashara kupitia EATV kila siku ya Ijumaa baada ya mkongwe huyo ku-dis ngoma kuwa sio nzuri na hata Marehemu Baba wa Taifa Julius Nyerere angeamka kutoka kaburini kwake akiikuta inafanya vizuri katika nchi ya Tanzania na mipaka yake basi angesononeshwa na tasnia hiyo nzima.

"Nina muheshimu sana bwana Afande Sele kwasababu ametukuza lakini sasa ajaribu kubishana na wabongo nasio uuma. Umma ndio umeamua kuupitisha huo muziki hata hivyo afande kabla ya wowowo alishasema mimi hanijui kwenye group za hip hop", amesema Zaiid.

Pamoja na hayo, Zaiid ameendelea kwa kusema "najua ni utu uzima nao unamchangia lakini mimi nina muheshimu, ukiachilia Afande kuwa ni msanii pia yeye ni shabiki wa nyimbo zangu maana hata washkaji zangu nilivyotoa wowowo walisema ni wimbo mbaya".

Zaiid aliishia wimbo wa Wowowo mwaka 2017 na kushika kasi na kupendwa na watu wengi mpaka kufikia hatua ya usumbufu kuongezeka kwa msanii huyo baada ya mashabiki wengi na marafiki zake kuomba namba wakihitaji mawowowo yaliyomo kwenye wimbo wake.

Ruby kuhusu Kukonda na kutumia dawa za kulevya

$
0
0
Msanii wa muziki wa kizazi kipya Ruby, amekanusha picha zilizokuwa zinasambaa kwenye mitandao ya kijamii zikimuonesha akiwa amekonda mpaka mbavu kuonekana kuwa sio zake, huku akidai maishani mwake hajawahi kunenepa mpaka awe amekonda kiasi hicho.


Rubby ametoa kauli hiyo wakati alipokuwa anazungumza kwenye kipindi cha 'FRIDAY NIGHT LIVE' inayorushwa mubashara kupitia EATV kila siku ya Ijumaa baada ya kuzagaa picha hizo na kuzua gumzo na kupelekea baadhi ya watu kumuhusisha mwanadada huyo na utumiaji wa vilevi vikali pamoja na matumizi ya dawa za kulevya ikiwemo bangi.

"Ile ni picha nasio Rubby halafu mnasema nimekonda kwani mlishawahi kuniona nimenenepa ?, haingii akilini kama vitu ambavyo vya negative wanavyoongea wakati mimi kazi ninafanya, ninaangalia mbele kwenye kazi zangu. Kazi yangu ndio inaongea lakini sio maneno ya watu. Mnaongelea mimi kuonekana mbavu zangu kwanini hamzungumzii kuonekana nina makalio makubwa", amesema Rubby.

Pamoja na hayo, Rubby ameendelea kwa kusema "ile picha ili kuwa imepigwa kwa pembeni angalieni video yangu niwaze ndio mtamuona Rubby nasio katika hizo picha, wawe wanaleta 'show' ili tunenepe".

Kwa upande mwingine, Rubby amesema kukaa kwake kimya kwa kipindi kirefu katika muziki alikuwa anataka kuja kivingine ili aweze kuwapa radha tofauti mashabiki zake wanaomfuatilia na kusikiliza kazi zake kila uchao.

EATV

Muimbaji Papii Kocha Mamoja na Binti yake Aliyempata Kabla ya Kuingia Jela

$
0
0

Muimbaji wa Muziki wa Dance Papii Kocha katika picha ya pamoja na Binti yake ambaye Alimuacha na umri mdogo sana Kipindi Anahukumiwa kwenda jela na sasa Amekuwa Mtu mzima kabisa. ..Mungu Ni Mwema Sana.

Sallam SK Amshutumu Diamond Platnumz Kwenda Makao Makuu ya YouTube Kununua Viewers

$
0
0

Mzee Baba Diamond week hii Platnumz ameonekana Ofisini Makao makuu ya Yotube alipoenda kuwatembelea...Baada ya Diamond Kupost picha akiwa katika ofisi hiyo Meneja wake Salam SK alicoment akimshutuma Kuwa ameenda kununua viewers na Diamond Bila kusita alimjibu kama inavyoonyesha hapo juu kwenye picha

Dawa Bora za Nguvu za Kiume na Kukosa Hamu ya Tendo la Ndoa

$
0
0

Baada ya utafiti wa muda mrefu juu ya matatizo ya upungufu wa nguvu za kiume na ukosaji wa hamu ya tendo la ndoa ama kushindwa kurudia tendo kwa haraka sasa

MWASELE HERBAL CLINIC. inakuletea suluhu juu ya matatizo haya kwa kutumia dawa za 

FULL POWER .ni dawa asili ya vidonge inayotibu tatizo la upungufu au ukosefu wa nguvu zakiume. dawa hii ina mchanganyiko wa kutosha kuzalisha vichocheo vingi vya hormone za gestrogen ziwemo vitamin B6&B1, vitamini E pamoja madini aina ya zinc vitakufanya kuwa na nguvu na muzunguko mzuri wa damu na kuongeza hamu na uwezo wa kufanya tendo la ndoa zaidi ya hatua nne au zaidi na kuchelewa kufika kileleni zaidi ya dakika 20-30. ZAT 50 inarudisha maumbile ya uume yaani kurefusha na kunenepesha ulefu nchi 3-7, upana cm, 3-4 standard kiafya haijalishi umri wako hata kwa wazee ukitumia maumbile yatabaki kuwa hivyo siku zote . pia tunatibu matatizo mengine kama presha, kisukari , ngiri ,chango la tumbo,tumbo kujaa gesi, kutokupata choo vizuri,miguu kuwaka moto,matatizo ya uzazi, bawasili namagonjwa yazinaa kama kisonono nakaswende. 

Tunapatikana DAR ES SALAAM. SHINYANGA NA ZANZIBAR. kwa wakazi wa dar es salaam utaletewa huduma hii popote ulipo . wa mikoani tunawatumia kwanjia ya mabasi . 

Wasiliana nasi kwa sim no 0717702227 au 0754568767.DR . SAGUDA nyote mnakaribishwa

Wanawake wa Saudi Arabia rasmi waanza kuendesha magari

$
0
0

Wanawake nchni Saudi Arabia rasmi sasa wameruhusiwa kukaa kwenye usukani, baa ya miongo kadhaa kutopata ruhusa hiyo 

Mabadiliko haya yalitangazwa mwezi Septemba mwaka jana na Saudi Arabia ikatoa leseni za kwanza kwa wanawake mwanzoni mwa mwezi huu. 

Ilikuwa nchi pekee iliyobaki duniani ambapo wanawake walikuwa hawaendeshi magari na familia zao zilikuwa zinakodisha dereva kwa ajili ya wanawake. 

Hata hivyo, hatua hii imefikiwa wakati kukiwa na Kampeni ya kuwakamata wanaharakati ambao wamekuwa wakipaza sauti wapatiwe haki ya kuendesha magari. 

Takriban wanaharakati wa haki za wanawake wanane wanashikiliwa na huenda wakafikishwa mahakamani na kupatiwa kifungo kwa uanaharakati wao, Shirika la kutetea haki za binaadamu, Amnesty International limeeleza. 

Miongoni mwa wanaoshikiliwa ni pamoja na Loujain al-Hathloul, mwanaharakati kinara katika kampeni hiyo. 
Amnesty pia imetaka kufanyiwa mabadiliko makubwa nchini Saudi Arabia, ambapo wanawake bado wameendelea kukandamizwa na sheria zinazowapa mamlaka zaidi wanaume. 

Kundi hilo la haki za binaadamu limefanya kampeni kwa miaka mingi kuhakikisha wanawake wanaendesha magari. 

Wanawake kadhaa walikamatwa mjini Riyadh mwaka 1990 na baadhi walianza kutuma picha za video wakiwa wamekaa nyuma ya usukani mwaka 2008 na kati ya mwaka 2011 na 2014, Maelfu ta wanawake sasa wataingia barabarani. 

Mtangazaji wa televisheni Sabika al-Dosari ameliambia shirika la habari la Ufaransa, AFP kuwa ''ni tukio la kihistoria kwa kila mwanamke wa Saudi Arabia''. 

Amesema alikuwa kwenye usukani mara tu muda wa ukomo wa marufuku ulipotimia. 

Hata hivyo, baadhi ya wanaume nchini humo wameelezwa kutoridhishwa kwao na mabadiliko hayo, wakitumia hashtag ya kiarabu ikimaanisha ''Hamtaendesha''. 

Kuondolewa kwa marufuku hiyo ni sehemu ya mpango wa Mwanamfalme wa nchini humo,Mohammed bin Salman kubadili mtazamo wa jamii ya Saudi 

Hata hivyo bado kuna mambo ambayo wanawake wa Saudi Arabia hawaruhusiwi kufanya, 
Wanawake wanapaswa kufuata sheria za nguo wanazopaswa kuvaa, na kutojihusisha na wanaume wasio ndugu zao.Ikiwa wanataka kusafiri, kupata huduma ya kiafya au kufanya kazi, wanapaswa kuongozana mwanaume ambaye ni kiongozi kwenye familia au kuwa na ruhusa yake. 

Mwenyekiti wa Chadema avamiwa na kuporwa fedha

$
0
0

Na Timothy Itembe Tarime, 
MWENYEKITI wa mtaa wa Bugosi kata ya Turuwa ndani ya halmashauri ya Mji wa Tarime mkioani Mara,Zacharia Chacha Ghati (CHADEMA) juzi majira ya saa 04 usiku alivamiwa na kundi la watu sita wanaodhaniwa kuwa ni majambazi wakati njiani akielekea Nyumbani kwake 

Kundi hilo la Watu  walimvamia na kumpiga  pamoja na kumjeruhi sehemu mbalimbali za mwili wake wakati ambapo walimteka huku wakimpiga kwa kutumia  silaha mbalimbali za jadi marungu,mapanga mishale pamoja na nondo hadi kusababisha kupelekwas kualzwa katika hospitali ya Wilaya inayomilikiwa na halmashauri ya Mji wa Tarime. 

Akionglelea tukio hilo,Bashiri Abdala jina maarufu Sauti ambaye ni  diwani kata ya Nyamisangura pia makamu mwenyekiti wa halmashauri ya Mji wa Tarime alisema kuwa tukio hilo halihuisiani na maswala ya kisiasa isipokuwa ni tukio la kiujambazi. 

Sauti alitumia nafasi hiyo kulitaka jaeshi la polisi mkoa wa kipolisiTarime Na Rorya  kutumia taaluma yao kukomesha vitendo vya kuhalifu pamoja na kuwahi eneo la tukiop pindi wanapokuwa wamepewa taarifa na wananchi kuwa kuna tukio la kuihalifu ili kukabiliana na majambazi. 

Sauti ametumia nafasi hiyo pia kuwataka wanachi na jamii kwa ujumla kutoa taarifa sehemu husika pindi wanapokuwa wanamashaka na makundi ambayo wanayahisi kuwa niyakiuhalifu pamoja na kuongeza kuwa hali ya majeruhi huyo inaendelea vizuri. 

"Tukio la kuvamiwa mwenyekiti wangu was mtaa wa  Bugosi alihusiani na maswala ya kisiasa isipokua ni tukio la kiujambazi natumia nafasi hii kulitaka jeshi la polisi mkoa wa kipolis Tarime/Rorya kuacha visingizio vya kusema kuwa hawana mafuta,kwenye magari wako mbali na tukio magari yameharibika pale ambapo kuna tukio linapokuwa limetokea na wananchi wakawa wametoa taarifa ili kuomba masaada"alisema Sauti. 

Akiwa anapati matibabu wodini namba Tatu ya wanaume ndani ya hospitali ya wilaya inayomilikiwa na halmashauri ya Mji wa TYarime mwenyekiti huyo,Zacharia Chacha Gahati  alisema kuwa alivamiwa majira ya saa 04 usiku wakati alipokuwa njiani akitoka  kumsindikiza rafiki yake sherehe huku Bisalwi ambapo majambazi hao walimvamia na kumpiga huku wakimjeruhi sehemu mbalimbami za mwili pamoja na kumpora shilingi laki tatu na alfu ishirini. 

"Nikiwa njiani baada ya kuachana na rafiki yangu ambaye nilikuwa nimempeleka ugeni wa kumchinjia Mama mkwe wake Bisalwi nilivamiwa na kundi la watu sita ambao wanadhaniwa kuwa majambazi na kunipiga sehemu mbaimbali za mwili wangu huku wakiwa na silaha za jadi ikiwemo nondo wamenipiga mgongono,magotini,kichwani na machoni pamoja na kunipora shilingi 300,000"alisema Ghati. 

Kwa upasnde wake kamanda mkoa wa kipolisi Tarime/Rorya,Henry Mwaibambe aliwaambia waandhishi wa habari kuwa tukio hilo hajalipata ofisini kwake na kuwa anafuatilia ili kujua na atakapolipata atatoa taarifa kwa waandishi wa habari. 

Waziri Ummy: Nitakuwa Mkali Kwa Yeyote Atakayekwamisha Huduma za Afya Nchini

$
0
0

SERIKALI imesema itaongeza nguvu kuhakikisha wagonjwa wa figo, moyo na saratani wanapata huduma za kibingwa katika hospitali za hapa nchini.


Pia imesema haitamvumilia mtu yeyote ambaye atasababisha kudorora kwa mkakati huo wa serikali wa kuwezesha huduma za magonjwa yasiyoambukiza nchini ambayo yamekuwa yakiongezeka kwa kasi.


Kauli hiyo ilitolewa na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu wakati wa uzinduzi wa Bodi ya Wadhamini wa Hospitali ya Benjamin Mkapa jijini hapa. Bodi hiyo inaongozwa na Dk Deodatus Mtasiwa.


“Mimi nitaendelea kuwa mkali sana kwa mtumishi yeyote atakayesababisha kudorora au kukwama kwa huduma za afya katika hospitali zetu,” alisema Ummy na kuitaka bodi hiyo kuwa makini na kuhakikisha hakuna uzembe unaofanyika katika uendeshaji wa hospitali hiyo nyeti.


Alisisitiza kuwa usimamizi makini utawezesha lengo la kuanzishwa kwa hospitali hiyo la kutoa huduma za afya maalumu za kibingwa, huduma za uchunguzi na tiba kwa magonjwa yote huku ikijikita zaidi kwenye magonjwa yasiyo ya kuambukiza kama figo, moyo, macho, damu na saratani kufikiwa kwa ufanisi uliotarajiwa.


Huduma nyingine zilizopangwa kutolewa ni pamoja na kutoa huduma za endoscope, kufundisha wataalamu wa kada za afya na kufanya tafiti mbalimbali ili kuboresha afya ya jamii ya Watanzania na hivyo kuipunguzia serikali mzigo wa gharama za matibabu nje ya nchi.


Akizungumzia umuhimu wa hospitali hiyo, alisema kuna ongezeko kubwa la magonjwa yasiyo ya kuambukiza duniani kwani Shirika la Afya Duniani (WHO) limesema wagonjwa 100, kati ya hao, 47 huugua magonjwa yasiyo ya kuambukiza, na vifo 100, kati yake, 60 hutokana na magonjwa hayo.


“Kama tusipochukua hatua za kudhibiti takwimu hizo zitaongezeka mara mbili zaidi na serikali itaongeza nguvu kusaidia magonjwa ya figo, moyo na saratani,” alisema Ummy.


Alisema kwa mwaka 2013 hadi 2016, serikali ilipeleka wagonjwa 590 kwenda kutibiwa nje ya nchi, ambao wagonjwa 430 kati yao, walikuwa wa moyo na 160 wa kupandikizwa figo.


“Kwa takwimu za kuanzia Julai 2013 hadi Juni 2016, magonjwa ya moyo na figo ndiyo yalikuwa yakiongoza kwa idadi kubwa ya wagonjwa kutibiwa nje ya nchi na kuigharimu serikali kiasi cha shilingi bilioni 36.6,” aliongeza waziri.


Alisema, kati ya wagonjwa 590 waliosafirishwa na serikali, 430 walienda kutibiwa moyo na 160 walienda kupandikizwa figo.


Alisisitiza kuwa kwa kuanzishwa huduma hizo katika hospitali mbalimbali nchini ikiwemo ya Benjamin Mkapa, kutaokoa kiasi kikubwa cha fedha na kuipunguzia serikali mzigo wa gharama.


Aliiagiza Bodi ya Hospitali ya Benjamin Mkapa kuwa kwa kuwa imeanza upandikizaji wa figo kuhakikisha inaweka malengo ya kupandikiza idadi maalumu ya wagonjwa itakayosaidia kukuza uwezo na taaluma.


Awali, Mkurugenzi Mtendaji wa hospitali hiyo iliyopo katika Chuo Kikuu cha Dodoma (Udom), Alphonce Chandika alimweleza waziri kwamba baada ya mafanikio ya upandikizaji wa figo wakisaidiana na wadau wa Tokushukai kutoka Japan, Machi 22, mwaka huu, wagonjwa wengine watafanyiwa upandikizaji huo Agosti mwaka huu.


Alisema mwezi ujao wataanzisha upasuaji wa kutumia matundu madogo kwa kushirikiana na wadau kutoka Marekani baada ya madaktari bingwa wa magonjwa ya wanawake, koo, pua na masikio kurejea nyumbani wakitokea India walikonoa bongo zao kuhusu tiba hiyo.


Pamoja na kutaka usimamizi makini ili kuokoa maisha ya Watanzania na fedha zinazotumika kupeleka wagonjwa nje, Ummy alitaka bodi kuhakikisha fedha za mkopo Sh bilioni 119 kutoka Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) zilizokopwa kujenga hospitali zinalipwa.


Akizungumzia masuala ya utafiti, pamoja na kulazwa kwa wagonjwa, alisema ndani ya mwezi moja wagonjwa wataanza kulazwa katika hospitali hiyo na anatarajia watakaofika kulazwa ni wale wanaohitaji huduma za kibingwa.


“Ndugu Mwenyekiti wa Bodi, tafiti ni eneo nyeti na muhimu sana katika kukuza na kuendeleza weledi, ujuzi na maarifa katika taaluma mbalimbali, hivyo ni lazima hospitali ijikite katika kufanya tafiti mbalimbali ili kugundua matatizo/changamoto na kuyapatia majawabu kwa maendeleo ya hospitali na Taifa kwa ujumla,” alisema Ummy.


Aliongeza kuwa ni matumaini yake bodi hiyo kwa kushirikiana na uongozi wa hospitali itahakikisha shughuli za utafiti zinaendelea kufanyika kikamilifu na matokeo ya utafiti yatumike kubaini na kutatua changamoto ili kuboresha utoaji wa huduma ya matibabu nchini.


Alisema uanzishwaji wa hospitali hiyo ya kibingwa ni utekelezaji wa mikakati ya serikali ya kupambana na magonjwa ya kuambukiza na yasiyo ya kuambukiza.

“Kwenye Vitu Vingi Tumeshika Mkia Dunia Lakini Kwenye hili Tupo Kwenye 10 Bora

$
0
0

Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Harrison Mwakyembe amesema kuwa Lugha ya Kiswahili ni moja ya lugha 10 duniani zinazotumiwa na watu wengi kati ya lugha 6000.

“Kwenye vitu vingi tumeshika mkia dunia lakini kwenye hili tupo kwenye 10 bora katika ya lugha 6000,” alisema Waziri Mwakyembe.

Waziri Mwakyembe ameyasema hayo kwenye uzinduzi wa kumbukizi ya Shaaban Robert na Tamasha la Ustaarabu wa Mswahili uliofanyika katika ukumbi wa Baraza la Chuo cha Mt. John jijini Dodoma.

Shaaban Robert alikuwa ni mwandishi nguli wa vitabu vyenye maudhui mbalimbali vikiwemo vya Kusadikika, Kufikirika pamoja na Adili na Nduguze, alizaliwa Januari Mosi, 1909 na kufariki June 22,1962.
Viewing all 104793 articles
Browse latest View live




Latest Images