Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104789 articles
Browse latest View live

Ghasia ageuka 'Mbogo' bungeni, asema 'hatukubali'

$
0
0

NA FATUMA MUNA
Mbunge wa Mtwara Vijijini, Hawa Ghasia amedai kuwa kuna wabunge wamekaa vikao na kuandaliwa kwenda kuwadhalilisha  wabunge wanaowatetea wakulima katika mabadiliko ya sheria ya zao la korosho.


Mbunge wa Mtwara Vijijini, Hawa Ghasia.

Ghasia ameyasema hayo, katika mjadala wa bajeti ya Serikali mapema leo ambapo ameweka wazi yeye pamoja na na wabunge wengine wa kusini watahakikisha wanapambana kuwapigania wakulima wa zao hilo.

Ghasia amesema kwamba anafahamu vipo vikao vilivyokaliwa kwa ajili ya kuja kuwadhalilisha wabunge watakao watetea wakulima kuhusu suala la kilimo cha korosho kwa ujumla na kuwataka wakulima kufahamu wabunge wao wapo imara na watawatetea kwa kadri itakavyowezekana.

“Wabunge wote tuna haki sawa za kutetea wananchi wetu, anayetoka katika pamba atetee pamba, anayetoka katika madini atatetea madini yake na anayetoka katika korosho atatetea wa korosho. Niwahakikishie wakulima wanaolima korosho wabunge wao tutapambamba na hata haki isipopatikana ila tutawatetea,"Ghasia.

"Tunaambiwa sisi wabinafsi, korosho inalimwa kwa kiwango kikubwa na mikoa miwili au mitatu lakini tulipokaa katika kamati tukakubaliana na kwenda mikoa 17. Leo tunaambiwa sisi wabinafsi, kuna watu wanakuja kusimama wanasema wanaijua korosho kuliko sisi. Mimi utafiti wangu wa shahada ya kwanza na ya pili inahusu korosho. Leo mtu anakuja humu anaijua korosho na ninasema kila mtu atetee lake na wananchi mjiandae kuwasikia.”

Mbali na hayo Mh. Ghasia amesema kwamba kazi ya serikali ni kuwashughulikia waliofanya ubadhirifu, na kwamba hata kama ni "Hawa Ghasia nipelekeni mahakani lakini siyo kusema wabunge wa kusini wabinafsi".

Mbali na hayo, Mbunge amesema kipindi cha gesi aliijua nia ya serikali na ndiyo maana alikuwa mstari wa mbele hali ilimfanya mpaka kumpoteza baba yake mzazi, kuchomewa nyumba na kuharibiwa mali lakini katika suala la korosho  hayupo tayari.

EATV

Casto Kafunguka “Ndoa na Tunda” Asema “Sijachanganyikiwa Tattoo Sifuti” (VIDEO)

$
0
0
Mtangazaji Casto Dickson amezungumza baada ya kuchora Tattoo ya mpenzi wake Tunda ambaye anaishi naye kwa sasa ambapo kasema kuwa amefanya hivyo kutokana na mapenzi aliyonayo na Tunda na si vinginevyo hivyo watu wasimfikirie vibaya.

Casto amesema kwamba hataifuta Tattoo hiyo hata kama wataachana na Tunda pengine watu wategemee ndoa yao kwani mpango wa kuachana haupo. Kuhusu ishu ya kumpa Mimba Tunda na suala la kula hotelini kila wakati Casto ameyajibu yote hapa kwenye hiii

VIDEO:

Rapa Offset Amethibitisha kuwa The Best Hip Hop Female Artist kwa sasa Card B ni Mke wake

$
0
0

Rapa Offset Amethibitisha kuwa The Best Hip Hop Female Artist kwa sasa @iamcardb ni Mke wake, kupitia maneno aliyoyaongea kwenye usiku wa tuzo za Bet zilizofanyika huko Los Angels Marekani Jumapili hii.

Licha ya Maneno ya @offsetyrn , lakini pia Mwanadada huyo anayetarajia kupata mtoto hivi karibuni, alidondosha ujumbe mzito kwenye ukurasa wake wa Twitter ukionesha kuwa hajapata mtoto nje ya ndoa.

Kupitia Mtandao wa TMZ wa Marekani, Cheti walichokiweka katika page zao kinaonesha kuwa wawili hao walifunga ndoa kwa siri tangu tarehe 20 Septemba 2017.

Ukifuatilia Clip mbalimbali Utagundua kuwa wawili hawa walivalishana Pete ya Uchumba hadharani kitambo lakini swala la ndoa hawakulitangaza na kulifanya kama siri.

Card B alivalishwa pete ya Uchumba Miezi 10 Iliyopita na wiki chache baadae akatangaza kuwa ni Mjamzito, kitu kilichonukuliwa kama alifanya hivyo baada ya kuwa Confirmed sasa ni Mke Halali wa Rapa @offsetyrn

Hii Hapa Dawa Bora ya Nguvu za Kiume na Maumbile Madogo ya Uume

$
0
0

Tatizo hili limekuwa likiwaadhiri watu wengi sana kisaikolojia hasa baada ya kujiona wapo tofauti sana na wengine kwa kawaida mwanaume anatakiwa awe na uume kuanzia nchi 6-8 kwanza upungufu wa vichocheo hivi huchochea ukuaji wa uume chongo ambalo hushambulia nerve ambayo uharibu kabisa ukuaji wa uume, ngiri, punyeto, ambayo huathili misuli ya uume, ngiri huleta maumivu, tumbo kuunguruma na kujaa gesi, korodani moja kuvimba, kutopata choo vizuri, sababu hizi hufanya uume kulegea na kusinyaa na kuwa mfupi na mwembamba na mara nyingi hata nguvu za kiume ( hamu ya tendo la ndoa) hupungua na kwisha kabisa

GEMBE :Ni dawa inayozalisha na kukufanya uume kukua na kuongezeka
NGEMO : Ni dawa bora ya kuongeza nguvu za kiume

Hukutia hamu ya kuludia tendo la ndoa zaidi mara4 nne bila kukinai au kuchoka pia itakufanya uchelewe kufika kileleni zaidi ya dk30-45 kwa mtumiaji pia tunatibu kisukari, bp, ngiri, miguu kuwaka moto KAMA HUNAMDA WA KUFIKA OFISINI KWETU UTALETEWA POPOTE TUPO MBAGALA RANGI TATU

 0753471612/ 0715249530
0623 386 305

DR KUZENZA

Mwanaume Afunga Ndoa na Wanawake Wawili kwa Wakati Mmoja

$
0
0
Mwanaume Afunga Ndoa na Wanawake Wawili kwa Wakati Mmoja
Kijana  raia wa Somalia, Bashir Mohamed ameoa wanawake wawili usiku mmoja ameambia BBC kwamba atawashawishi wanaume wengine kufanya hivyo.



Kijana huyo anasema kuwa aliwachumbia wanawake wote kwa takriban miezi minane na kuwashawishi kufunga ndoa naye.

”Nilikuwa nikiwaleta nyumbaji wote pamoja”, aliambia BBC.



”Nilikuwa nikiwaambia wazi wote wawili kwamba nawapenda. Waliridhika” , aliongezea.



”Umuhimu wa kuwaoa wote wawili wakati mmoja ni kwamba hawangekuwa na wivu na kwamba watajua tangu awali kwamba wamekuwa katika ndoa za uke wenza”, alisema bwana Mohammed.



Alioa wanawake wawili kwa sababu alihitaji watoto wengi.
”Nitawashawishi wanaume wengi pia kufuata nyayo zangu iwapo wana uwezo”, alisema Mohamed.



Ndoa za wake wengi ni halali katika utamaduni nchini Somalia lakini sio jambo la kawaida kuoa wanawake wawili wakati mmoja, kulingana na mwandishi wa BBC Mohamed Mohamed.



”Imetokea mara kadhaa katika miaka ya nyuma , ikiashiria kwamba huenda sasa ikawa mtindo mpya”, aliongezea.

Bwana Mohamed aliwaoa wanawake hao wawili , Iqra na Nimo, katika kijiji cha Sinai katika jimbo lililojitenga la Somaliland mnamo tarehe 22 mwezi Juni.

Hamissa Mobetto Aumbuka! Kumbe Daimond Ajamnunulia Ule Mjengo Huu Hapa Ukweli Wote

$
0
0
Hamissa Mobetto Aumbuka! Kumbe Daimond Ajamnunulia Ule Mjengo Huu Hapa Ukweli Wote
Ameumbuka! Ndivyo unavyoweza kusema. Wakati tabia ya mastaa kuanika mijengo yao ya gharama ikizidi kushika kasi, mwanamitindo Hamisa Mobeto amejikuta akiumbuka baada mjengo aliodaiwa kununuliwa na mzazi mwenzie Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’, kubainika kuwa hajanunuliwa kama ambavyo mama yake Mobeto, Shufaa Rutiginga amekuwa akidai.

Nyumba hiyo iliyopo maeneo ya Tegeta-Bahari Beach ilizua gumzo mitandaoni mara baada ya gazeti dugu na hili la Amani, kuichapisha kwa mara ya kwanza hivi karibuni.



GUMZO LENYEWE…

Kufuatia usiri mzito uliokuwepo juu ya makazi hayo ya Mobeto, mara baada ya nyumba hiyo kupamba ukurasa wa mbele wa Amani, gumzo lilikolezwa mitandaoni kwa watu kuhoji kama ni kweli amepangiwa au amenunuliwa na Diamond.

Wale ambao ni mashabiki wa Mobeto walijitapa kuwa mjengo huo ni maalumu kwa mtoto wa Diamond aliyezaa na Mobeto, Prince Dylan lakini wale wasio mashabiki wake, waliponda kwa kusema mjengo huo wamepangiwa tu.

“Mobeto bwana, kila siku tunamuona anaiposti nyumba hiyo kudhihirisha kwamba ni yake wakati si kweli halafu (Mobeto) ukweli anaujua lakini hataki kuanika licha ya sisi kupiga kelele mitandaoni,” aliponda mdau aliyejitambulisha kwa jina la Kikumba katika mtandao wa Instagram.


MAMA’KE ACHOCHEA MOTO

Wakati kitendawili cha amepangiwa au amenunuliwa kikiwa hakijateguka, mama yake Mobeto, Shufaa Rutiginga aliibuka na kudai nyumba hiyo Diamond amemnunulia mtoto aliyezaa na bintiye, Prince Dylan hali iliyoamsha moto zaidi kwa wafuasi wa mitandao.

Kwenye mahojiano hayo, mama Mobeto alisikika akimshukuru Diamond kwa kumnunulia mjengo huo mjukuu wake ndipo watu walipoanza kumshambulia.

“Mh! Mbona jamani tumesikia hii nyumba amepangiwa na si kwamba amenunuliwa? Hivi hizi kiki jamani tutafika kweli? Kwani mtu ukisema ukweli utapungua nini?” alihoji mdau mmoja katika mtandao wa Instagram.



WAUMBUKA

Ili kujiridhisha zaidi na ubuyu huo, Ijumaa Wikienda liliingia mzigoni kuchimbua ukweli wa kauli ya mama pamoja na ukimya wa bintiye katika kusema ukweli, ndipo lilipobaini ukweli kwamba nyumba hiyo Mobeto amepangiwa.

TUMSIKILIZE JIRANI

Jirani mmoja wa Mobeto aliyeomba hifadhi ya jina, alipoibukiwa na wanahabari wetu, aliweka wazi kuwa nyumba hiyo hajanunuliwa na ameshangazwa na habari kwamba amenunuliwa.

“Kwa kweli nimeamini hawa mastaa wanapenda kujikweza, yaani nyumba hii tumeona mchakato wote na mwenye nyumba tunamjua lakini mitandaoni tunaona mama Mobeto anasema Diamond kawanunulia,” alisema jirani huyo huku akitaja jina la mmiliki wa nyumba hiyo (jina tunalihifadhi).



JIRANI AZIDI KUFUNGUKA

Jirani huyo alienda mbali zaidi kwa kutaja siku ambayo mmiliki wa nyumba hiyo huwa anafika kwa ajili ya kushughulikia wateja wake kwani mbali na nyumba hiyo aliyompangisha Mobeto, anazo nyumba nyingi alizopangisha maeneo hayohayo.

“Njooni Jumamosi mara nyingi huwa anakuja na mnaweza kuzungumza naye akawapa ukweli wa mambo wote maana nimesikia pia hakufurahishwa na kitendo cha mitandao kuandika kuwa nyumba imenunuliwa wakati ukweli ni kwamba wamepanga,” alisema jirani huyo.


BALOZI ATHIBITISHA

Balozi wa nyumba kumi, Mtaa wa Fahari, Cloud Kayako alipoulizwa na mwanahabari kama nyumba hiyo amepangishiwa na kwamba mwenye nyumba hakufurahishwa na taarifa za Mobeto kununuliwa nyumba hiyo, alikiri kwamba ni kweli mwenye nyumba hakufurahishwa na habari hiyo.

“Huyu ni kweli amepanga hapa sasa zilipokuja hizo taarifa za kwamba amenunua kwa kweli hata mwenye nyumba kashangaa,” alisema balozi huyo huku akiwataka waandishi kuzungumza na mmliki ili kuweza kupata habari zaidi.



IJUMAA LAIBUKA NYUMBANI

Baada ya kuelezwa kuwa mmiliki huwa anafika kwenye nyumba hizo siku ya Jumamosi, Ijumaa Wikienda lilitinga nyumbani hapo lakini bahati mbaya lilishindwa kuzungumza naye kutokana na ubize aliokuwa nao.


NDUGU WA MMILIKI ANENA

Mara baada ya mmiliki kufika na kuwa bize na wapangaji wake wengine, ndugu wa mmliki aliyeomba hifadhi ya jina alisema kama familia walishangazwa na habari za kwamba Mobeto amenunuliwa nyumba hiyo.

“Mimi mwenyewe niliona kwenye mtandao kwamba wamenunua, nikashtuka sana ikabidi niende kumuonesha babu (mmiliki), akasema si kweli ndipo wakapuuza tu maana,” alidai ndugu huyo.

Hivi karibuni, mastaa wa kike wa Bongo Muvi akiwemo Irene Uwoya, Aunt Ezekiel, Kajala Masanja na Wema Sepetu wamekuwa na kasumba ya kuinadi mijengo yao mtandaoni na kuzua gumzo.


Watu wamekuwa wakiwakosoa kwa kitendo cha kuinadi mijengo hiyo kwani baadhi yao wamekuwa wakiongopa kwamba ni zao kwa maana wamenunua wakati kiuhalisia si kweli. Kama hiyo haitoshi, kuna wengine wamedaiwa kuvumisha kuwa wanamiliki majengo mazima wakati ukichunguza inakuwa ni upande mmoja na si nyumba nzima.

Ijumaa Wikienda limeanza kuifanyia kazi habari hiyo, soon litawaanika mmoja baada ya mwingine.
Chanzo: Global Publishers

Siwezi Kuruhusu Wanangu Wachezwe Unyago- Shilole

$
0
0
Siwezi Kuruhusu Wanangu Wachezwe Unyago- Shilole
Msanii wa Bongo Flava, Shilole amejibu iwapo ataruhusu wanae wa kike kuchezwa unyago.

Muimbaji huyo akipiga stori na Break ya Clouds TV amesema kuwa ingawa katika kabila lao (Wanyamwezi) wana utamaduni huo hawezi kuruhusu kwa wanae.

“Siwezi, sasa hivi hatuna watu wakubwa ambao wapo, sinaunajua zinakuwaga kama familia. Lakini zamani mambo hayo ndio yalikuwepo tofauti na sasa,” amesema Shilole.

Licha ya kufanya muziki na kujiingiza katika biashara mbali mbali hadi kufungua mgahawa wake, Shilole ni mama wa watoto wawili wa kike.

Mahakama Yamng'ang'ania Babu Tale Atakiwa Jumatatu

$
0
0
Mahakama Yamng'ang'ania Babu Tale Atakiwa Jumatatu
Mkurugenzi wa kampuni ya Tip Top Connection, Hamis Shaban Taletale maarufu kama Babu Tale amemchefua Jaji Edson Mkasimongwa wa Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam, baada ya kusafiri nje ya nchi bila taarifa na kushindwa kufika mahakamani

Babu Tale ambaye ni meneja wa mwanamuziki wa kizazi kipya, Naseeb Abdul maarufu Diamond Platnumz, alitakiwa kufika mahakamani jana kusikiliza uamuzi wa shauri lake kuhusiana na uhalali wa amri ya mahakama hiyo kumkamata na kumfunga jela kama mfungwa wa madai.

Hata hivyo hakutokea, badala yake alifika kaka yake Idd Shaban Taletale. Wakili wao, Issa Chondo aliieleza mahakama kuwa Babu Tale hayupo mahakamani kwa kuwa amesafiri nje ya nchi kwa ajili ya matibabu.

Kitendo cha kusafiri nje ya nchi bila kutoa taarifa na hivyo kushindwa kufika mahakamani kilimfanya Jaji Mkasimongwa aseme kuwa alichokifanya Babu Tale si cha kiungwana, kauli aliyoirudia mara tatu kuonyesha kuwa kilimuudhi.

Awali Wakili Chondo alidai kuwa mteja wake amekwenda kutibiwa nchini Afrika Kusini, lakini alipobanwa maswali na jaji alijikuta akibadili kauli yake na kusema hajui amekwenda nchi gani, huku akiiomba Mahakama imruhusu awasiliane naye kumuuliza.

Maelezo ya wakili huyo yalimshangaza jaji na kumhoji wakili huyo kuwa inawezekanaje mteja wake ambaye yuko kwenye amri ya kukamatwa asafiri nje ya nchi bila kumuaga wakati anajua kuwa anatakiwa mahakamani.

“Lakini si anajua yuko under arrest? (chini ya amri ya kukamatwa?) Inawezekanaje amekwenda nje ya nchi bila taarifa, sasa huu si uchokozi?” alihoji Jaji Mkasimongwa baada ya Wakili Chondo kutoa taarifa kuwa mteja wake amesafiri nje.

“Kwanza yuko nchi gani?” alihoji tena jaji na wakili huyo akajibu kuwa naye hajajua kuwa amekwenda nchi gani kwani alimtumia tu taarifa, na akaomba Mahakama imruhusu awasiliane naye kumuuliza.

Wakili wa upande wa pili katika shauri hilo, Mwesigwa Muhingo aliingilia kati na kuieleza Mahakama kuwa Babu Tale yuko nchini Marekani na alipotaka kuendelea kutoa maelezo zaidi jaji a alimtaka asubiri kwanza na akaendelea na mahojiano na wakili wa Babu Tale.

“Sasa si huu si ni uchokozi? Kwa nini hajaja kutoa taarifa?” alizidi kuhoji jaji na Wakili Chondo akajibu kuwa alitarajia kuwa angerudi mapema kabla ya siku ya kesi.

“Au mnajua kinachoendelea mahakamani? Wewe wakili wake hujui yuko nchi gani, ina maana na wewe hajakuaga? Au kwa kuwa anajua kesi iko kwa Mkasimongwa ni muungwana, hivyo akakueleza kuwa wewe nenda utamweleza tu hivi.

“Alichokifanya si cha kiungwana, alichokifanya si cha kiungwana, alichokifanya si cha kiungwana. Kwa kuwa kesho nasafiri na narudi Jumapili naamuru tuonane hapa Jumatatu saa 3:00 asubuhi na yeye (Babu Tale) awepo.”

Mahakama hiyo katika uamuzi wake uliotolewa na naibu msajili, Wilbard Mashauri, Februari 16 iliamuru Babu Tale na nduguye wakamatwe na kupelekwa kifungoni katika Gereza la Ukonga na April 4 akatoa hati ya kuwakamata, kwa kushindwa kutekeleza hukumu ya mahakama hiyo.

Katika hukumu iliyotolewa na Jaji Augustine Shangwa Februari 18, 2016, iliwaamuru ndugu hao kumlipa fidia ya Sh250 milioni, mhadhiri wa Dini la Kiislamu, Sheikh Hashim Mbonde kutokana na makosa ya kutumia mahubiri yake kibiashara bila ridhaa yake.

Kufuatia amri na hati hiyo Babu Tale alitiwa mbaroni na Polisi Mkoa wa Ilala Mei 22, 2018 na kuhidhiwa kituoni hapo kwa siku mbili akimsubiri Naibu Msajili Mashauri kuidhinisha amri ya kumpeleka gerezani kuwa mfungwa wa madai kwa kuwa hakuwepo.

Lakini Mei 24, Jaji Mkasimongwa akikaimu nafasi ya jaji mfawidhi alimuachia huru kwa muda baada ya kubaini kasoro katika amri ya kuwakamata na kuwafunga.

Mei 25 aliwataka mawakili wa pande zote kutoa hoja zao kuhusu hoja iliyoiibua Mahakama hiyo iwapo msajili ana mamlaka ya kutoa na kusaini amri hiyo.

Baada ya kusikiliza hoja za pande zote ndipo Jaji Mkasimongwa aliahirisha shauri hilo hadi jana kwa ajili ya kutoa uamuzi iwapo Naibu Msajili Mashauri ana mamlaka ya kisheria kutoa na kusaini amri ya kumkamata na kumfunga mtu aliyeshindwa kutekeleza hukumu ya Mahakama.
Chanzo :Mwananchi

Baada ya Hoja ya Korosho Kuwavuruga Wabunge Huu Hapa Msimamo wa Wakulima wa Zao Hilo

$
0
0
Baada ya Hoja ya Korosho Kuwavuruga Wabunge Huu Hapa Msimamo wa Wakulima wa Zao Hilo
Chama cha wakulima Tandahimba (Tandahimba Farmers Association -TAFA) walikutana na Waandishi wa habari Dodoma na kutoa msimamo wao juu ya mjadala ulioibuka bungeni kuhusu fedha za ushuru wa mauzo ya korosho ghafi nje (export levies) ambapo wametaka ushuru wa 65% kuendelea kupelekwa kwenye sekta moja kwa moja bila ya kupitia Serikali kuu.

“Hoja kubwa ya wadau ni kwamba fedha hii ikipitia Serikali kuu  mambo mengi hayatatekelezwa lakini pia kwa sababu ya changamoto zilizopo za utekelezaji wa bajeti itakuwa vigumu kusimamia fedha hizo zikiwa kwenye mfuko wa Serikali”-M/Kiti Mohamed Jabuka

Mtu wa Pili Kutembea Kwenye Mwezi Awashtaki Wanawe na Meneja Wake Kisa Hiki Hapa

$
0
0
Mtu wa Pili Kutembea Kwenye Mwezi Awashtaki Wanawe na Meneja Wake Kisa Hiki Hapa
Mwanaanga maarufu kutoka Marekani Buzz Aldrin amewashtaki watoto wake wawili na meneja wa zamani wa biashara zake akidai kwamba waliiba pesa zake.

Aidha, anadai walimharibia sifa ambazo amejizolea katika maisha yake.

Kesi hiyo, ambayo ilifichuliwa Jumatatu, iliwasilishwa katika mahakama moja mjini Florida wiki moja baada ya watoto wake kuwasilisha ombi mahakamani wakitaka waruhusiwe kuchukua udhibiti wa fedha zake.

Jamaa zake walikuwa wamemwambia jaji kwamba anahitaji mlezi wa kumwakilisha kisheria kwa sababu uwezo wake wa "kufikiria umeshuka sana".

Katika mahojiano na gazeti la Wall Street Journal wiki iliyopita, Aldrin ambaye ni kanali mstaafu wa jeshi la wanahewa la Marekani alisema: "Hakuna mtu atakayekaribia kufikiria kwamba ninaweza kuwekwa chini ya mlezi."

Kwenye kesi hiyo, anadai kwmaba mwanawe wa kiume, na binti yake pamoja na meneja wake wa zamani Christina Korp pia walivuruga uhusiano wake wa kimapenzi na watu wengine na kumzuia kuoa tena.

Mzozo unahusu zaidi usimamizi wa kampuni yake ya kibinafsi, Buzz Aldrin Enterprises, na shirika la hisani kwa jina ShareSpace Foundation.

Katika ombi waliloliwasilisha mahakamani, wanawe Andrew Aldrin, 60, na Janice Aldrin, 60, walisema baba yao hivi karibuni ameanza kujihusisha na marafiki wapya ambao wanajaribu kumpotosha na kumtenganisha na familia yake.

Hatima ya Nigeria na Argentina Kujulikana Leo

$
0
0
Hatima ya Nigeria na Argentina Kujulikana Leo
Michuano ya Kombe la Dunia imezidi kuelekea patamu ambapo leo jumla ya mechi nne zitakuwa zinawasha viwanja moto nchini Urusi.

Croatia ambao wanaongoza kundi D wakiwa na alama zao 6 kileleni watakuwa wanacheza dhidi ya Iceland kuanzia saa 3 kamili usiku.

Wakati huo Denmark itakuwa inakipiga na Ufaransa kwenye kundi C na mchezo huo ukianza majira ya saa 11 kamili jioni.

Australia nayo itakuwa inacheza dhidi ya Peru kwenye mchezo wa kundi C ambapo mechi hiyo itaanza kupigwa kuanzia saa 11 jioni.

Mechi ambayo inasubiriwa kwa hamu na Waafrika wengi pamoja na wale mashabiki wa Messi ni Nigeria dhidi ya Argentina itakayoanza saa 3 usiku.

Mechi hii inapewa nafasi kubwa ya Messi kuamua hatima ya taifa hilo kama itaweza kupenya dhidi ya Nigeria ambapo njia pekee ya kusalia kwenye mashindano hayo leo ni kupata matokeo ikipaswa kufunga mabao mengi.

Wakati huo Argentina ikipambana kupata matokeo, maombi yao yatakuwa kwenye mchezo baina ya Iceland na Croatia wakihitaji Iceland iweze kupoteza au kwenda sare na wao wapate matokeo ili waweze kufuzu kuingia 16 bora.

Habari Njema: Tunatibu Busha, Korodani Kuvimba,Ngiri, Miguu Kufa Ganzi Pamoja na Matatizo ya Nguvu za Kiume

$
0
0



Ni dawa ya nguvu za kiume inayorefusha na kunenepesha uume saizi uipendayo (Inch 1-7) kwa muda wa siku 6 tu.Dozi hii itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa muda wa dakika 30, utarudia tendo la ndoa zaidi ya mara 4 bila hamu kuisha bila kujali umri na garantee ni miaka 60 baada ya kutibu tatizo.

Pia tunatibu Busha bila kufanyiwa Oparesheni, korodani moja kuvimba, ngiri, tumbo kujaa gesi na kuunguruma, kutopata choo vizuri, miguu kuwaka moto na kufa ganzi, chango la wanawake, kisukari na kutokwa na kinyama sehemu ya haja kubwa.

MIHAYO:
Inarudisha mke, mchumba, hawara na atakutimizia kila kitu unachotaka kutoka kwake ndani ya  saa 2 tu hata kama yupo mbali. atarudi na kumfunga asiwe na mwingine zaidi yako.

Umefukuzwa kazini? unataka kupandishwa cheo? Umepoteza pesa zako kwenye biashara bila kujua umepandikizwa chuma ulete? Njoo urudishe pesa zako. Unauza mali yako haiendi? Wasiliana na mtaalam Challo kwa; 0714006521

Tupo Mbagala

Rais Museveni Atajwa kuwa Miongoni Mwa Marais Bora Kote Ulimwenguni

$
0
0
- Rais wa Uganda Yoweri Museveni alitajwa kuwa miongoni mwa marais bora kote ulimwenguni
- Museveni anasemekana kuchangia asilimia 2.42% ya kukuza maendeleo na uchumi wa nchi yake tangu alipoingia mamlakani mwaka wa 1986
- Aliwashinda viongozi shupavu akiwemo aliyekuwa waziri mkuu wa Singapore, Lee Kuan Yew Rais wa Uganda Yoweri Kaguta Museveni ametajwa kuwa miongoni mwa marais bora zaidi kote ulimwenguni.

Rais huyo mwenye umri wa miaka 74 na ambaye amekuwa mamlakani kwa zaidi ya miaka 30 alipewa nambari 12 kwenye orodha ya viongozi 24 ulimwengu mzima ambao wamechangia pakubwa katika kukuza uchumi katika mataifa yao. 

Kulingana na takwimu za profesa mmoja wa masuala ya kiuchumi kutoka chuo kikuu cha New York na pia mchumi wa Benki ya Dunia Steven Pennings, Museveni alichangia asilimi 2.42% katika kuendeleza uchumi wa Uganda tangu alipoingia mamlakani.

Udaku iliweza kubaini kuwa, marais wawili pekee kutoka Afrika; Museveni na aliyekuwa rais wa Botswana Seretse Ian Khama ndio waliotajwa kuwa bora kulingana na ripoti ya Pennings. 

Khama alistaafu katika siasa baada ya kutawala Botswana kwa miaka 10 kutoka mwaka wa 2008 hadi 2018. 

Kwa ujumla rais wa Burma, Than Shwe ambaye aliitawala nchi hiyo kutoka mwaka wa 1992 hadi 2011 ndiye aliyetajwa kuwa rais bora zaidi kote ulimwenguni. Wengine waliotajwa kwenye orodha hiyo ya Pennings ni rais wa Ecuado, Guillermo Rodriguez Lara na aliyekuwa waziri wa Malaysia, Najib Razak. 

Jumba La Mobetto Alilozawadiwa na Diamond Lagubikwa na Utata

$
0
0
Wiki iliyopita habari zilienea Kwenye mitandao ya kijamii kuwa Diamond amemnunulia mjengo wa fahari mama mtoto wake na Hamisa Mobetto ambapo Mama Mobetto alithibitisha taarifa hizo.

Lakini hivi sasa Global Publishers wanaripoti kuwa Habari hiyo siyo ya kweli kwani kwa taarifa waliyokuwa nazo ni kuwa nyumba ile haijanunuliwa bali imepangishwa tu kwa muda.


Baada ya Tetesi hizo gazeti hilo lilienda kufanya uchunguzi ambapo Jirani mmoja wa Mobeto aliyeomba hifadhi ya jina, alipoibukiwa na wanahabari wetu, aliweka wazi kuwa nyumba hiyo hajanunuliwa na ameshangazwa na habari kwamba amenunuliwa.

Kwa kweli nimeamini hawa mastaa wanapenda kujikweza, yaani nyumba hii tumeona mchakato wote na mwenye nyumba tunamjua lakini mitandaoni tunaona mama Mobeto anasema Diamond kawanunulia”.

Lakini baada ya taarifa hizo gazeti hilo lilimsaka mmiliki wa mjengo huo ili aweze kuthibitisha taarifa hizo ndipo ndugu wa mmiliki alipofunguka:

Mimi mwenyewe niliona kwenye mtandao kwamba wamenunua, nikashtuka sana ikabidi niende kumuonesha babu (mmiliki), akasema si kweli ndipo wakapuuza tu maana“.

Mama mzazi wa Mobetto anayejulikana kama Shufaa Rutiginga aliweka wazi Kwenye mahojiano na Wasafi Tv kuwa Diamond alinunua mjengo huo maalumu kwa ajili ya mtoto wake Dyalan.

Wakazi Akiri Hakuna Msanii Kama Davido

$
0
0

Msanii wa muziki wa Bongo fleva Wakazi Music amefunguka na kumnyanyulia mikono msanii kutoka Nigeia David Adeleke maarufu kama Davido baadae ya ushindi wake wa tuzo ya BET.

Davido aliibuka mshindi wa tuzo ya BET 2018 katika kipengele cha ‘Best International Act’, tuzo zilizofanyika katika ukumbi wa Microsoft Theater huko mjini Los Angeles, jimboni California, Marekani.

Baada ya ushindi huo Davido alitoa hotuba ambayo ilikuwa imejikita katika kutangaza soko la Muziki wa Africa na kuwataka wasanii wa Marekani kufika Africa Kutembea:

Hotuba hiyo Ikiwa huwa watu wengi na mmoja wao ni Msanii Wakazi ambaye alishindwa kujizuia na kumwagia sifa lukuki Davido kwa hotuba hiyo ambapo kipitia ukurasa wake wa Instagram aliandika:

Hongera nyingi zimwendee Davido kwa ushindi wa “Best International Act” kwenye @betawards huko Marekani. Mwaka huu hakukuwa na mtanzania Ila pia Category ya International iliunganiswa Africa na Europe, so angechukua mwafrika yeyote tungehesabu Ushindi. Ila kikubwa ni kwamba mwaka huu ndio mara ya kwanza Tuzo za International kupokelewa on the Main Stage. Na niseme ukweli Davido hajatuangusha kwenye Speech yake. Ilikuwa Fupi and I understand maana sio mchezo (kutembea tu kwenda pale mbele unamuona kila Star, hatari) lazima utetemeke. Ila Davido alimshukuru D’banj kama Msanii aliyeanza kutufungulia milango african artists upande wa marekani (Collabo na Snoop Dogg, Signed by Kanye West) na pia alichukua Fursa kutoa salamu za rambirambi kwa familia ya D’Banj Maana amefiwa na mwanae (R.I.P Daniel III). Kisha akashukuru Fans, Familia yake, Management yake. Mwisho akawasihi wanyamwezi kuja africa wajionee hali, chakula na kufanya Collabo na Wasanii wetu, pia akasema Album yake inakuja soon. Kiukweli I don’t see any other artist kufanya a better job of representing zaidi ya alivyofanya OBO.
Ila sasa hii iwe changamoto na chachu ya sisi huku kupigania muziki wetu na sisi maybe tuje kushinda na kupata fursa ya kuinadi Tanzania kikamilifu. I know I’m inspired and I’m going to the studio leo. Ikiwezekana tuongeze support ya wenyewe kwa wenyewe kama itasaidia. Tuache UMBEA na kuongelea yasiyotuhusu, Tuache Uvivu… tupige Kazi, uwe underground uwe Legend!! Wote tuna nafasi… peace #AfricaPride

Kutana na Maalim Fadhili Rashid ni Mtaalam Watiba za asili kwa Kutumia Nyota na Kurwani

$
0
0


KUTANA NA MAALIM FADHILI RASHIDI NI MTAALAM WATIBA ZA ASILI JE? UMEACHWA NAMPENZI WAKO? JE? NA HAUJUI NAMNA YA KUMRUSHA?

MAALIM FADHILI RASHIDI HURUDISHA MAHUSINO NA MPENZI WAKO ALIE KUACHA NDANI YA MASAA (72) TU MUONE HARAKA AKUSAIDIE, ACHA KUTESEKA NA MAPENZI

MAALIM FADHILI RASHIDI NI BINGWA WAKUTIBU MARADHI SUGU KAMA VILE MIGUUKUUMA NAKUWAKA MOTO, PRESHA, KISUKARI, VIDONDA VYATUMBO, PUMU,

TEZI NA UVIMBE TUMBONI, ANA UWEZO WAKURUDISHA MTU ALE POTEA KIMAZINGIRA (MSUKURE), KUMFANYA MKE/ MUME/ MPENZI ASIKUSALITI, DAWA YA ( LIMBWATA) KUMTAWALA MPENZI WAKO UNAVYOTAKA,

KUMUONA MBAYAWAKO LIVE KWA SABABU MAALUMU, ANATOWA PETE YA BAHATI NA KUMILIKI MALI ZA MAJINI, DAWA YA UZAZI, KUSHIKA UJAUZITO NDANI YA SIKU (14) TU

DAWA YA KUONGEZA UUME SAIZI UPENDAYO, DAWA YA NGUVU ZA KIUME, PIA ANAYO DAWA YA KUONGEZA HIPSI SHEPU KUWA NA UMBO BOMBA,
KAMA UMEIBIWA AMA KUDHULIMIWA UTARUDISHIWA MALI YAKO NDANI YA MASAA (72) TU, ANAFUNGA KESI NAKUPATA HAKI YAKO, MVUTO WA MAPENZI NA BIASHARA, KUUZA MALIYAKO KWA HARAKA

KUZUIYA CHUMA ULETE KWENYE BIASHARA, KUSAFISHA NYOTA NA KUTOWA MIKOSI, KUPANDISHWA CHEO KAZINI, ACHAKUHANGAIKA MAALIM FADHILI RASHIDI NDIO MKOMBOZI WAKO

CALLING +255 7193628 06/ +255 763276239/
WHATSAPP IMO +255 785786436

Makombe 8 Bandia ya Kombe la Dunia Yakamatwa Yakiwa Yamejazwa Misoko ya Bangi na Cocaine

$
0
0
Makombe 8 Bandia ya Kombe la Dunia Yakamatwa Yakiwa Yamejazwa Misoko ya Bangi na Cocaine
Nchini Argentina yamekamatwa makombe 8 bandia yenye muonekano sawa na ule wa Kombe la Dunia yakiwa yamejazwa misokoto ya bangi na Cocaine.



Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa katika Gazeti la The Sun imesema Makombe hayo 8 yamekamatwa Ijumaa ya wiki iliyopita mjini Isidro Casanova katika jimbo la Greater Buenos Aires.

Jeshi la Polisi mjini Isidro Casanova limethibitisha taarifa hizo na tayari watu nane wanashikiliwa kwa tukio hilo na imekadiriwa kuwa kila kombe lilikuwa na mzigo wa Cocaine wenye thamani ya dola $14,819 sawa na Milioni 33.

Samaki Pia Wana Maumbile Tofauti Kama Binadamu- Msukuma

$
0
0
Samaki Pia Wana Maumbile Tofauti Kama Binadamu- Msukuma
Mbunge wa Geita vijijini (CCM), Joseph Musukuma amesema kuwa samaki wako wa aina tofauti Ziwani na wengine wana tabia kama binadamu kwa kile alichodai wana maumbile madogo lakini wana umri mkubwa.

Musukuma ametoa kauli hiyo bungeni leo, wakati akihoji swali la nyongeza katika kipindi cha maswali na majibu kwa wizara ya mifugo na uvuvi ambapo amesema kuwa suala la kupima kwa rula samaki haliafiki kwa kuwa viumbe hao pia wana maumbile tofauti kama binadamu.

“Dhana ya uvuvi haramu imeenea sana, lakini samaki pia wana maumbile tofauti kama binadamu na mfano ukichukua umri wangu mimi na mheshimiwa Mwalongo tunalingana lakini ukitutazama maumbile tunatofautiana sana, sasa hata samaki wako hivyo, kwahiyo hata samaki wakipimwa kwa rula hawalingani, sheria haijalitazama hilo, Je ni lini sheria itamtazama mvuvi na kumlinda pindi anapokumbana na changamoto hii ya samaki kuwa na maumbile tofauti na umri wake?”, amehoji Musukuma.

Akijibu swali hilo Naibu wa Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Abdallah Ulega amekiri kuwa sheria ina mapungufu na itafanyiwa maboresho ili kuhakikisha inawapa ahueni pia wavuvi katika shughuli zao.

Sanjari na hayo Ulega ameongeza kuwa kumekuwa na malalamiko ya kuteketezwa kwa nyavu bila kufanyiwa uchunguzi na wavuvi wengi wamekuwa wakionewa, na wizara itawachukulia hatua watendaji wote wa sekta hiyo wanaotenda kinyume na taratibu.

Mzee Majuto Azushiwa Tena Kifo Mwanaye Anena Mazito

$
0
0
Baada ya Mzee Majuto  Kuzushiwa Kifo Familia Yaiomba Serikali Kuingilia Kati
Baada ya kusambaa kwa taarifa katika kimtandao ya kijamii kuhusiana na kifo cha Muigizaji Mkongwe nchini, Mzee Amri Majuto, familia yake imeiomba serikali na vyombo husika ikiwemo mamlaka ya mawasiliano, kuwachukulia hatua watu wanaozusha taarifa za kifo kwa madai kuwa sasa ni mara ya 10.

Akikanusha taarifa za kifo cha muigizaji huyo kupitia kipindi cha SUPAMIX kinachorushwa na East Africa Radio, mtoto wa Mzee Majuto, Hamza Majuto amesema kuwa kama familia wameziona taarifa hizo kwenye mitandao ya kijamii na wala hawafahamu nia ya watu hao wanaozusha taarifa za kifo cha baba yake mara kwa mara.

Aidha mtoto huyo wa Mzee Majuto amesema kwamba baba yake kwa sasa anaendelea vizuri tangu aliporudi kutoka nje ya nchi na sasa (Majuto) yupo kwenye mapumziko kama jinsi ambayo inatakiwa.

"Tangu jana nimepokea simu na sms zaidi ya 500 zikitaka nithibitishe kuhusu kifo cha mzee. Kiukweli hii ni mara ya 10 kwa mzee kuzushiwa taarifa ya kifo. Natambua kwamba kuna vyombo vya usalama pamoja na mamlaka inayohusika na makosa ya mitandao hivyo hili la kuzusha kifo ni kosa la jinai naiomba basi TCRA ifuatilie ili kujua dhamira ya huyu mtu ambaye amekuwa akizusha taarifa za kifo" amesema Hamza.

Hata hivyo, Kijana huyo amesema kwamba kwa sasa wapo mapumzikoni lakini hawawezi kusema ni wapi kwa ajili ya kuepusha usumbufu ili kumsaidia mzee Majuto apate mapumziko mazuri.

Tour ya Diamond ‘A Boy From Tandale’ Nchini Marekani na Utofauti Wake

$
0
0
Tour ya Diamond ‘A Boy From Tandale’ Nchini Marekani na Utofauti Wake
Msanii wa muziki Bongo, Diamond Platnumz bado yupo nchini Marekani kwa ajili kumalizia tour ya albamu yake ‘A Boy From Tandale.

Ni mara kadhaa kumekuwepo na stori kuwa wasanii wengi wa Afrika wanapofanya show katika nchi hiyo wengi wanaojitokeza ni wale kutoka Afrika (Africa Community).

Lakini kwa sasa hali inaelezwa kubadilika kidogo ukilinganisha na hapo awali.

Meneja kutokea WCB, Babu Tale ambaye ameongozana na Diamond katika tour hiyo, akipiga stori na JJ wa Jembe FM amesema kuwa show za Diamond zimekuwa ni za watu wote na si wale kutokea Afrika pekee.

“Ukiangalia clip ambayo ameposti Diamond utaona watu weupe kibao, nimeona wazungu kibao, Jamaica walikuwepo,” amesema.

March 13, 2018 ndipo Diamond alizindua albamu hiyo, uzinduzi uliofanyika Nairobi nchini Kenya ambapo star wa muziki kutoka Marekani, Omarion alihudhuria. Hata hivyo hadi sasa tour ya albamu hiyo haijafanyika Tanzania.
Viewing all 104789 articles
Browse latest View live




Latest Images