Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104793 articles
Browse latest View live

Sweden Yatinga Robo Fainali Kombe La Dunia

$
0
0
Timu ya taifa ya Sweden imeibuka na ushindi wa bao 1-0, kwenye mchezo wa hatua ya 16 bora Kombe la Dunia dhidi ya Switzerland iliyomalizika jana  usiku  huko Saint Petersburg huko Urusi.

Ushindi huo wa Sweden umeichukua historia ya Kombe la Dunia na kuirudisha nyuma hadi mwaka 1958, ambapo Sweden walikuwa wenyeji na walishinda mechi mbili mfululizo kwa mara ya kwanza robo fainali na nusu fainali na kutinga fainali.

Kabla ya kushinda dhidi ya Switzerland jana, Sweden ilitoka kushinda 3-0 mechi ya mwisho hatua ya makundi kwenye kundi F dhidi ya Mexico, hivyo mechi ya jana imekuwa ya pili mfululizo kwa Sweden kushinda.

Bao la Sweden limefungwa na kiungo Emil Forsberg  ambaye jana ripoti zilieleza kuwa kocha wa Manchester United Jose Mourinho, alitarajiwa kuwepo uwanjani kwaajili ya kumfuatilia nyota huyo ambaye ameibuka kiungo bora wa Sweden katika miaka ya 2014, 2016 na 2017.

Obi Mikel amethibitisha baba yake alitekwa saa nne kabla ya game vs Argentina

$
0
0
Mtandao wa Kwese.ESP.com umethibitisha kupata taarifa kutoka kwa nahodha wa timu ya taifa ya Nigeria John Obi Mikel kuwa baba yake mzazi alitekwa saa nne kabla ya kucheza mchezo muhimu dhidi ya Argentina Jumanne iliyopita.

Obi amethibitisha kuwa alipata taarifa za kutekwa kwa baba yake lakini watekaji walimpa onyo asimwambie mtu yoyote au mamlaka za usalama nchini Nigeria, kwani angefanya hivyo baba yake angeuwawa.



“Waliniambia kwamba wangemuua baba yangu kama ningetoa taarifa kuwa ametekwa kwa mtu yoyote au mamlaka za usalama” Obi Mikel

Watekaji lengo lao kubwa lilikuwa ni kujipatia pesa kutoka kwa staa huyo kwani walimuagiza atoe dola za kimarekani 28000 ambazo ni zaidi ya Tsh milioni 60 za kitanzania  ili wamuachie baba yake akiwa hai bila kumdhulu kwa chochote.

Baba yake Obi na dereva walikuwa safarini kutoka Jos kuelekea sehemu za kusini mwa Nigeria kwa ajili ya mazishi lakini walitekwa na baadae kufanikiwa kuokolewa na Polisi July 2 ikiwa imepita wiki moja toka taarifa za kutekwa kwao ziliripotiwe kwa familia.

Makonda Amwagiwa 'Mijisifa'

$
0
0

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Mhe. Suleiman Jaffo amemwaga sifa kwa Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam, Paul Makonda kwa jitiada binafsi za kuwaboreshea walimu mazingira ya kazi ikiwemo ujenzi wa ofisi 402 za walimu.


Waziri Jaffo ametoa pongezi hizo wakati wa hafla ya uzinduzi wa pikipiki 2,894 zenye thamani ya zaidi ya shilling billion 8.5 zilizotolewa kwa waratibu wa elimu kata ambapo kitaifa zoezi hilo limefanyika Jijini Dar es salaam.

Aidha, Makonda amesema anajivunia kuona Dar es salaam inaendelea kushika kidedea kwenye matokeo ya mitihani ya kitafa kutokana na walimu kuwekewa mazingira bora ya kazi ikiwemo ujenzi wa ofisi 402 za kisasa za walimu, mikopo ya viwanja vya bei nafuu pamoja na kusafiri bure kwenye daladala na treni huku akidai bado ipo mipango mingi ya kuhakikisha walimu wake wanaishi vizuri ili wawe na motisha ya kazi.



Walimu wa Elimu Prof. Ndalichako (kushoto), Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais (TAMISEMI),  Suleiman Jaffo (katikati), Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam, Paul Makonda (Kulia) wakiwa wapo juu ya Pikipiki wakizijaribu.

Vile vile, RC Makonda amesema pikipiki zilizotolewa zitaenda kuongeza nguvu na hari ya kazi kwa waratibu wa elimu Kata ambapo kwa Mkoa wa Dar es salaam umepata pikipiki kwa kila Kata.

Pikipiki 2,894 zilizotolewa kwa waratibu wa elimu Kata nchi nzima zimenunuliwa na Wizara ya Elimu na wafadhili kutoka Global Partnership in education kwa lengo la kuwawezesha kuzitembelea shule kwenye Kata zao ili kuboresha elimu.

EATV

Israel inatuhumiwa Kuiba Mawingu ya Iran

$
0
0
Stori kutoka huko nchini Iran ambapo unaambiwa kuwa Kiongozi mkuu wa idara ya ulinzi nchini Iran Brigadier General Gholam Reza Jalali ameishutumu nchi ya Israel kuiba mawingu ya mvua ya nchi yake na kuisababisha nchi hiyo kukumbwa na ukame.



Kiongozi huyo ameyaeleza hayo alipokuwa akiongea na Waandishi wa habari na kuongeza kuwa nchi ya Israel imekuwa ikiwahujumu kwa kuharibu mawingu ya mvua ya nchi yao katika anga lao na kuwasababishia ukame.

Aidha Kiongozi huyo katika utetezi wa shutuma zake hizo kwa nchi ya Israel ameeleza kuwa milima yote ya Afghanstan na ile ya Mediterranean ina theluji kasoro milima yao kitu anachosema kuwa ni hujuma za taifa la Israel.

Kwa muda mrefu mahusiano kati ya mataifa ya Israel na Iran yamekuwa na utata na shutuma hizi ni kama zinatia chumvi kidonda cha mahusiano ya mataifa hayo mawili.

Download App ya Udaku Special Hapa Kama Bado Hauna Kwenye Simu yako

Mwanamke Mbaroni kwa Wizi Mtoto Mchanga

$
0
0
Mwanamke mbaroni wizi mtoto mchanga Mwanza
Mwanamke  mmoja anashikiliwa na jeshi la polisi kwa tuhuma za kuiba mtoto wa kiume mwenye umri wa wiki tatu.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza, Ahmed Msangi, alisema mwanamke huyo aliyetambulika kwa jina la Paulina Mashiku (27) ni mkazi wa ukijiji cha Mbugani wilayani Sengerema.

Alisema mtuhumiwa huyo aliyekuwa ameolewa na mwanamume anayeishi maeneo ya Bukoba visiwani anakojishughulisha na uvuvi kwa kipindi chote cha ndoa yao hawajawahi kupata mtoto jambo lililosababisha mwanamke huyo kumdanganya mumewe kuwa amepata ujauzito.

Juzi, majira ya saa sita mchana alifanya kitendo hicho lakini siku mbili kabla ya tukio, alipita katika kijiji cha Buliyaheke na kumwona mwanamke akinyonyesha mtoto mchanga ndipo alipochukua jukumu la kumpigia simu mumewe na kuwaaga majirani anakwenda hospitalini kujifungua.

Alisema kesho yake alifika katika nyumba alipo mtoto huyo majira ya 4:00 usiku na kumwona mama wa mtoto akiwa nje akipika wakati huo mtoto akiwa amelala chumbani. Alipita mlango wa uwani na kumwiba mtoto huyo na kurudi naye nyumba kwake huku akiwaeleza majirani kuwa amejifungua salama.

"Jambo hilo liliwapa wasiwasi majirani kwa kuwa walipata taarifa katika kijiji cha Buliyaheke kuna mwanamke ameibiwa mtoto, hivyo wakatoa taarifa kituo cha polisi.

“Baada ya kupokea taarifa, polisi walifanya ufatiliaji wa haraka hadi eneo la tukio kisha mtuhumiwa aliwekwa nguvuni na alipohojiwa alikiri ni kweli alimwiba mtoto," alisema Msangi

Aliongeza kuwa hali ya mtoto ni nzuri na tayari amekabidhiwa kwa mama yake mzazi na polisi wako katika mahojiano na mtuhumiwa. Alisema pindi uchunguzi ukikamilika atafikishwa mahakamani ili hatua za kisheria zichukuliwe dhidi yake.

Kamanda Msangi alitoa wito kwa wakazi wa Mwanza kuwa waangalifu na watoto wao dhidi ya watu wenye nia ovu huku akiwataka waendelee kutoa ushirikiano na jeshi la polisi kwa kutoa taarifa za uhalifu na wahalifu mapema ili wakamatwe na kufikishwa katika vyombo vya sheria.

Merkel Abadilisha Msimamo Kuhusu Uhamiaji

$
0
0
Baada ya vuta nikuvute ya kuda mrefu, Kansela wa Ujerumani, Angela Merkel, na waziri wake wa mambo ya ndani, Horst Zeehofer, wamekubaliana kuondosha tofauti zao kuhusiana na sera ya uhamiaji.

Merkel amesema Ujerumani itawazuia wahamiaji waliosajiliwa katika nchi nyingine wanachama wa Umoja wa Ulaya kwenye vituo maalumu, huku mchakato wa kutafuta njia za kuwarejesha makwao ukiendelea.

Wachambuzi wanasema Merkel amechukua hatua hiyo ili kuunusuru utawala wake.

Baadhi walikuwa wamesema kuwa iwapo Merkel hangechukua uamuzi huo, serikali ya muungano anayoiongoza sasa ingekuwa katika hatari ya kusambaratika na uongozi wake kufika kikomo.

Kiongozi huyo aidha amesifu makubaliano yaliyoafikiwa na washirika wake wa jimbo la Bavaria ambao walikuwa wametishia kujiondoa kutoka serikali yake ya mseto.

Kwendelea kushirikiana kwa vyama vya Christian Social Union, CSU, na Christian Democratic Union, CDU, kumetajwa na wachambuzi kama ambako kutasaidia kulinda kanuni ya uhuru wa watu kutembea katika nchi wanachama wa Umoja wa Ulaya na kuiruhusu Ujerumani kuchukua hatua katika ngazi ya kitaifa kupunguza na kudhibiti idadi ya wakimbizi na wahamiaji wanaowasili kwenye nchi hizo.

Katika kauli ambayo iliwashangaza wengi siku ya Jumatatu, Merkel aliwaambia waandishi wa habari kwamba pamoja na kujenga vituo vya muda vya wahamiaji, Ujerumani pia itatafuta njia za kuwarejesha makwao chini ya makubaliano na nchi wanakotokea waomba hifadhi na ambako tayari wamesajiliwa.

Kwa muda mrefu, Merkel, ambaye, kwa mara ya kwanza aliingiaa mamlakani mwaka wa 2005, amekuwa katika mstari wa mbele kuunga mkono sera ya uhamiaji inayoruhusu wakimbizi na wahamiaji kupata hifadhi katika nchi za bara ulaya, ikiwemo Ujerumani.

Manamo mwaka wa 2015, Merkel alichukua hatua iliyoibua utata, ya kuwaruhusu wahamiaji Zaidi ya milioni moja, kuingia nchini kwake, wengi wao wakitokea nchi kama vile Syria, Iraq na Afghanistan.

VOA imezungumza na mchambuzi wa masuala ya siasa na mwandishi wa habari mstaafu, Ramadhan Ali, akiwa mjini Berlin, Ujerumani, na kwanza ikamuuliza kueleza ni nini ambacho huenda kimepelekea Kansela Merkel kuchukua hatua hiyo ambayo ni tofauti kabisa na sera zake kuhusu uhamiaji, pamoja na masimamo ambao amaekuwa akishikilia kwa muda mrefu.

Nay wa Mitego Awaacha Watu Njia Panda

$
0
0
Nay wa Mitego Awaacha Watu Njia Panda
Hili linaweza likawa la kushangaza kutoka kwa staa wa Bongo Fleva Nay wa Mitego baada ya kuweka wazi kuwa kwa sasa yupo single ikiwa hajawahi kuweka mahusiano yake wazi tokea aachane na mzazi mwenzake Siwema japokuwa aliwahi kuhusishwa kutoka na warembo kadhaa.

Nay wa Mitego aliwahi kuhusishwa kuwa kwenye uhusiano wa kimapenzi na msanii Nini miezi kadhaa iliyopita ingawa wawili hao hawakuwahi kukiri kuwa wapo kwenye mahusiano, ila kwa sasa ameweka wazi kuwa yupo single,

Hiki ni kama kitendawili kutoka kwa Nay wa Mitego, je alikuwa kwenye uhusiano wa kimapenzi na nani? Kupitia instagram account ya Nay wa Mitego aliandika “Usichangie Chochote, Wala Siitaji Comment hata moja , No ushauri wala maoni, yani ni hivyo tu, I’m Single”


Picha ya Jux, Vanessa Yawachefua Serikali

$
0
0
Picha ya Jux, Vanessa Yawachefua Serikali
BAADA ya hivi karibuni kuonyesha mambo ya chumbani jukwaani na picha yao ya mahaba mazito kusambaa mitandaoni, wasanii wa Bongo Fleva ambao ni wapenzi, Juma Khalid ‘Jux’ na Vanessa Mdee ‘V-Money’ wamejikuta wakiuvaa moto wa serikali, Risasi Mchanganyiko linakujuza.

Akizungumza na gazeti hili, Katibu Mtendaji wa Baraza la Sanaa la Taifa (Basata), Godfrey Mngereza alisema wao kama serikali picha hiyo imewachefua na hawajui ni shetani gani amewapata vijana hasa hao wanamuziki kwani kila kukicha wamekuwa wakionyesha vitendo visivyokuwa na maadili kwa jamii.

Mngereza alisema kuwa kutokana na picha hiyo lazima waifanyie kazi kwani kwa sasa hawawafumbii macho wasanii wanaokwenda kinyume na maadili na siku zote moto ni uleule.

“Sijui ni shetani gani amewaingia hawa vijana wanamuziki maana kila siku wanaonyesha vitu vya ajabu vizivyokuwa na maadili wanapokuwa jukwaani kwani hivi karibuni msanii Mbosso naye alifanya shoo na kuonyesha vitendo vilivyo kinyume kabisa na maadili, tukamuita na kumuonya na kumwagiza aombe msamaha kwa mashabiki na alifanya hivyo.

“Sasa huyu Jux na Vanessa hata kama ni wapenzi hawakutakiwa kufanya hayo waliyoonyesha jukwaani kwani kama ni mahaba mnatakiwa muonyeshane mkiwa faragha na siyo hadharani kama walivyofanya tunawafanyia kazi ili kukomesha tabia hizo,” alisema Mngereza.

ATOA TAMKO

Mngereza alitoa tamko kwa kuwataka wasanii kufanya mambo yanayoheshimu maadili na kuachana na tabia ya kuvunja maadili kila kukicha kwa kuonyesha mambo ya chumbani hadharani na wale watakaoendelea na uchafu huo wao kama serikali hawatasita kuwachukulia hatua kali.

Hata hivyo Mngereza aliwataka maafisa utamaduni waliopo katika kila mkoa kuangalia yale wanayoyafanya wasanii wanapokuwa kwenye shoo zao majukwaani na kuwachukulia hatua kuanzia ngazi ya wilaya hadi ngazi za juu na hilo litasaidia kutokomeza tabia hizo chafu zinazoibuka kwa sasa.

TUJIKUMBUSHE

Mwishoni mwa wiki iliyopita Jux na Vanessa wakiwa kwenye shoo jijini Mwanza katika ziara yao ya kimuziki mikoa mbalimbali waliyoipa jina la In love and Money Tour walionyesha mahaba jukwaani kwa kunyonyana ndimi hadharani ambapo picha yao ilikuwa gumzo kila kona baada ya kusambaa mitandaoni.

SIYO HAO TU

Tofauti na Vanessa na Jux hivi karibuni kumeibuka wimbi la wasanii wa muziki wawapo jukwaani wakifanya shoo kuonysha vitendo vilivyo kinyume na maadili akiwemo, Mbwana Kilungi ‘Mbosso’ ambaye aliitwa Basata na kuonywa na mwingine ni Lulu Euggen ‘Amber Lulu’ ambao wote wakiwa jukwaani walionyesha vitendo vya faragha visivyotakiwa kuonyeshwa hadharani

Pretty Kind Ajiweka Alipotoka Wema Sasa Mapenzi MotoMoto na Calisah

$
0
0
Pretty Kind Ajiweka Alipotoka Wema Sasa Mapenzi MotoMoto na Calisah
MSANII wa filamu na muziki Bongo, Suzan Michael ‘Pretty Kind’ anadaiwa kula makom­bo ya msanii mwenzake, Wema Sepetu kwa kutoka kimapenzi na mwanamitindo aliyewa­hi kubanjuka penzini na Wema, Calisah Abdul­hameed.

Kikizungumza na Za Mo­tomoto News, chanzo ma­kini kilieleza kuwa Pretty Kind amekuwa akioneka­na mara kwa mara maeneo ya Sinza, Dar akiwa na Calisah wakionyeshana mahaba niue hivyo ndiye mtu wake kwa sasa.

Za Motomoto News ilimtafuta Pretty Kind akafunguka:“Siyo kweli tupo karibu na Calisah kwa sababu ya kazi na siku ikimalizika mashabiki wataiona.”

Kume Lulu Diva Kahamisha Kambi kwa Bill Nass na Si Rich Mavoko Tena

$
0
0
Kume Lulu Diva Kahamisha Kambi kwa Bill Nass na Si Rich Mavoko Tena
HITMAKER wa Ngoma ya Ona, Lulu Abbas ‘Lulu Diva’ anadaiwa kutoka kimapenzi na msanii mwenzake, William Lyimo ‘Bill Nas’. Kwa mujibu wa ‘source’ wetu, wawili hao wamekuwa karibu kila kona na wala hawaoni aibu kujibebisha hadharani.

“Walianza kama masihara, tukajua labda Rich Mavoko ndiyo anakaa kwa Lulu kumbe ni Bill Nas bwana, juzi walikuwa tena pamoja wakielekea mkoani sijui mkoa gani lakini picha zao za kujibebisha zinamaanisha,” kilisema chanzo.Risasi Vibes halikuacha ishu hiyo iende ‘plain’ , lilimtafuta Lulu na baada ya kupatikana aliwaka;

“Hivi jamani mtu kuongozana na mwanaume ndiyo kutembea naye? Mbona mnataka kuniharibia kwa mtu wangu niliyekuwa naye?“Bill Nas ni mshikaji   wangu wa kawaida tu, juzi (Jumamosi iliyopita) tuliandaliwa shoo ya pamoja huko Iringa, tukiwa njiani tulikuwa tukipiga mapicha picha kama mtu na rafiki yake, nashangaa watu wanageu-zageuza maneno.”
Chanzo: Global Publishers

Thailand Yasaka Njia ya Kuwaokoa Vijana 12 Waliokwama Kwenye Pango

$
0
0
Thailand Yasaka Njia ya Kuwaokoa Vijana 12 Waliokwama Kwenye Pango
Wavulana kumi na wawili pamoja na kocha wao mmoja waliokwama katika pango moja lililojaa maji nchini Thailand wamepokea chakula cha kwanza tangu walipokwama pamoja na dawa kitakachodumu kwa siku kumi.

Wazamiaji saba, pamoja na daktari mmoja na nesi mmoja watakaokuwa wanafuatilia hali za afya zao humo pangoni , wameungana na na kikundi kilichomo pangoni upande wa Kaskazini mwa nchi hiyo baada ya kugundua kuwa timu hiyo iko hai mwanzoni mwa wiki hii.

Wazamiaji kwa sasa wanabangua bongo ni kwa namna gani iliyo bora zaidi watakavyo fanikisha kulitoa kundi hilo pangoni hadi seheme ya usalama.

Mvua nyingi zinazonyesha zinaashiria kiwango cha maji kujaa na kuhatarisha maisha ya watu waliomo pangoni pamoja na mifuko ya hewa waliyonayo mahali waliko kama mateka.

Wavulana hao waligunduliwa siku tisa baada ya kuingia pangoni humo huko katika jimbo la Chiang Rai kufuatia mafunzo ya mpira waliyokuwa wakifanya na kujikuta wakikwama pangoni kutokana na kina cha maji kuongozeka kulikosababisha na mvua nyingi zinazonyesha.

Mapema wiki hii, Maafisa wa serikali nchini Thailand waliwaambia waandishi habari kwamba wakoaji wameanza na zoezi la kuchunguza afya za kundi hilo pamoja na matibabu, na pia kuwaburudisha vijana hao na kuarifu kuwa hakuna hata mmoja mwenye afya mbaya miongoni mwa waliokwama pangoni.

Wavulana hao walipewa chakula chepesi kwa kuanzia ambacho ni rahisi kusagika tumboni, chenye kuongeza nguvu kwa haraka , chenye wingi wa vitamini na madini mwilini. Chini ya uangalizi makini wa madaktari, anaarifu Apagorn Youkonggaew ambaye ni mkuu wa vikosi maalumu vya uokozi nchini Tailand wakati wa mkutano baina yake na waandishi habari.

Wachezaji Nane Waondoka Yanga

$
0
0
Wachezaji Nane Waondoka Yanga
Baada ya kuleta takribani wachezaji 14 kutoka nje ya nchi waliokuja kufanya majaribio na kikosi cha Yanga nchini, jumla ya 8 wameondoka na 6 wakibakia.

Meneja Mkuu wa timu, Hafidh Saleh, amesema kwa sasa wamebaki na wachezaji 6 pekee huku wengine wakifeli mazoezi ambapo sasa watakuwa wanarejea makwao.

Saleh amesema wachezaji waliofeli wameondoka kutokana na mchujo unaoendelea kwa ajili ya kupata wale wanaohitajika kwa ajili ya kukisuka upya kikosi.

Ikumbukwe siku kadhaa zilizopita, Yanga ilitanga kuleta wachezaji 14 wa kimataifa kwa mujibu wa Ofisa Habari wa klabu, Dismas Ten kwa ajili ya kufanya majaribio.

Kikosi hicho kipo kambini kwa ajili ya maandalizi ya mchezo wa Kombe la Shirikisho Afrika dhidi ya Gor Mahia FC ya Kenya na msimu ujao wa Ligi Kuu Bara.

Dawa Bora za Nguvu za Kiume na Kukosa Hamu ya Tendo la Ndoa

$
0
0
Baada ya utafiti wa muda mrefu juu ya matatizo ya upungufu wa nguvu za kiume na ukosaji wa hamu ya tendo la ndoa ama kushindwa kurudia tendo kwa haraka sasa

MWASELE HERBAL CLINIC. inakuletea suluhu juu ya matatizo haya kwa kutumia dawa za

FULL POWER .ni dawa asili ya vidonge inayotibu tatizo la upungufu au ukosefu wa nguvu zakiume. dawa hii ina mchanganyiko wa kutosha kuzalisha vichocheo vingi vya hormone za gestrogen ziwemo vitamin B6&B1, vitamini E pamoja madini aina ya zinc vitakufanya kuwa na nguvu na muzunguko mzuri wa damu na kuongeza hamu na uwezo wa kufanya tendo la ndoa zaidi ya hatua nne au zaidi na kuchelewa kufika kileleni zaidi ya dakika 20-30. ZAT 50 inarudisha maumbile ya uume yaani kurefusha na kunenepesha ulefu nchi 3-7, upana cm, 3-4 standard kiafya haijalishi umri wako hata kwa wazee ukitumia maumbile yatabaki kuwa hivyo siku zote . pia tunatibu matatizo mengine kama presha, kisukari , ngiri ,chango la tumbo,tumbo kujaa gesi, kutokupata choo vizuri,miguu kuwaka moto,matatizo ya uzazi, bawasili namagonjwa yazinaa kama kisonono nakaswende.

Tunapatikana DAR ES SALAAM. SHINYANGA NA ZANZIBAR. kwa wakazi wa dar es salaam utaletewa huduma hii popote ulipo . wa mikoani tunawatumia kwanjia ya mabasi .

Wasiliana nasi kwa sim no 0717702227 au 0754568767.DR . SAGUDA nyote mnakaribishwa

Viongozi Wastaafu Wampa Ushauri Mzito Rais Magufuli

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli tarehe 03 Julai, 2018 amekutana na kufanya mazungumzo na Marais Wastaafu, Makamu wa Rais Mstaafu, Mawaziri Wakuu Wastaafu, Maspika Wastaafu na Majaji Wakuu Wastaafu, Ikulu Jijini Dar es Salaam.

Hii ni mara ya kwanza kwa Mhe. Rais kukutana na viongozi hao wakuu wastaafu na kupokea ushauri na maoni yao juu ya uendeshaji wa Serikali na mustakabali wa Taifa.

Katika mkutano huo viongozi hao wamemshukuru Mhe. Rais Magufuli kwa kuwaita kwa lengo la kusikiliza ushauri na maoni yao, na wamempongeza kwa kazi kubwa iliyofanywa na Serikali ya Awamu ya Tano katika kipindi kifupi cha miaka miwili na nusu tangu ilipoingia madarakani.

Viongozi hao wamemshauri Mhe. Rais Magufuli kuimarisha na kujenga taasisi zinazosimamia uendelevu wa kazi nzuri zinazoendelea kufanywa na Serikali ya Awamu ya Tano zikiwemo utekelezaji wa miradi mikubwa ya maendeleo kama vile ujenzi wa reli, mapambano dhidi ya rushwa, kuimarisha nidhamu kazini, kutilia mkazo watu kuchapa kazi, kuongeza ukusanyaji wa mapato ya Serikali na utoaji wa huduma za jamii.

Viongozi hao wamesisitiza umuhimu wa kudumisha amani kwa kuhakikisha haki inatendeka, kutathmini matatizo ya wananchi na kubuni mbinu za kuyatatua, kusimamia kwa ukaribu shughuli za kilimo na ufugaji ambazo zinaajiri Watanzania wengi na ni muhimu kwa maendeleo ya viwanda na kuboresha kiwango cha elimu.

Kwa upande wake Mhe. Rais Magufuli amewashukuru viongozi hao kwa maoni na ushauri waliompa na amewahakikishia kuwa ataufanyia kazi.

Mhe. Rais Magufuli amewaeleza viongozi hao juhudi mbalimbali zinazofanywa na Serikali hivi sasa ikiwemo kuongeza ukusanyaji wa mapato ya Serikali ambao umeongezeka kutoka Shilingi Bilioni 800 hadi kufikia Shilingi Trilioni 1.3 kwa mwezi, ujenzi wa reli ya kisasa kuanzia Dar es Salaam hadi Dodoma utakaogharimu Shilingi Trilioni 7.26, kujenga mradi wa umeme katika mto Rufiji (Stieglers’ Gorge) utakaozalisha Megawati 2,100 za umeme, kutoa elimu ya msingi na sekondari bila malipo na kuongeza mikopo ya wanafunzi wa elimu ya juu.

Mhe. Rais Magufuli amewahakikishia kuwa Serikali ya Awamu ya Tano inaendelea vizuri na kwamba itaendelea kutatua changamoto ambazo bado zipo kwa juhudi kubwa ili Tanzania iwe nchi nzuri kwa Watanzania wote.

Gerson Msigwa
Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU
Dar es Salaamu

MunaLove "Bila Mwanangu Nisingeokoka Sikuwa Najua Biblia"

$
0
0
Baada ya mfanyabiashara, Muna Love, kuokoka na kuachana na maisha yale ya kidunia aliyokuwa akiishi, amezungumza na Global TV na kufungukia maisha yake ya sasa ndani ya Yesu. Muna amesema kwamba mitihani aliyoipata wakati wa kumuuguza mwanae Patric aliyezaa na mtangazaji wa Clouds TV, Casto Dickson, ndiyo hasa iliyomfanya arudi kwenye mikono ya Mungu, na pengine kama mwanae asingeumwa labda asingeokoka.

Kuhusu sakata lililowahi kuvuma la Muna kuiba nguo ya ndani ya Muigizaji Wema Sepetu ambaye alikuwa shoga ake pete na kiidole, Muna amesema malkia huyo wa Bongo Muvi, alikuwa havai nguo za ndani ila mashabiki wame panic bure na hawakumuelewa dhamira yake. Kuhusu mzazi mwenziye Casto Dickson, Muna amekataa kuzungumzia.

VIDEO:

Mrembo Pretty Kindy Adaiwa Kula Makombo ya Wema Sepetu

$
0
0
MSANII wa filamu na muziki Bongo, Suzan Michael ‘Pretty Kind’ anadaiwa kula makom­bo ya msanii mwenzake, Wema Sepetu kwa kutoka kimapenzi na mwanamitindo aliyewa­hi kubanjuka penzini na Wema, Calisah Abdul­hameed.

Kikizungumza na Za Mo­tomoto News, chanzo ma­kini kilieleza kuwa Pretty Kind amekuwa akioneka­na mara kwa mara maeneo ya Sinza, Dar akiwa na Calisah wakionyeshana mahaba niue hivyo ndiye mtu wake kwa sasa.

Za Motomoto News ilimtafuta Pretty Kind akafunguka:“Siyo kweli tupo karibu na Calisah kwa sababu ya kazi na siku ikimalizika mashabiki wataiona.”

Aliyezaa na Casto! "Tunda Hana Lolote, Casto ni Mchafu Simpendi Tena"

$
0
0
Kufuatia 'Couple' mpya inayotikisa jiji kwa sasa ya mtangazaji wa Clouds, Casto Dickson na Video queen, Tunda, mwanamke mmoja ambaye ni mzazi mwenza wa mtangazaji huyo anayefahamika kwa jina la Don Posh, ameibuka na kuweka bayana kuwa wawili hao hawawezi kuwa na uhusiano kamwe ila ni kiki tu.

Posh amesema kuwa bado anampenda mzazi mwenziye huyo, na kusema kuwa hakuna mwanamke atakayetokea kupendwa na Casto kama yeye kwani alichompatia hawezi kupatiwa na mwanamke mwingine yeyote.

Posh ameongeza kuwa Casto ni mlevi sana, na kuwa hapendi vile ambavyo Casto anashikana shikana na Tunda na kuachia video zao mitandaoni, huku akichanganya maelezo yake baada ya kusema pia kuwa hampendi tena kutokana na uchafu wake wa kutembea na wanawake hovyo hadi mahausigeli. VIDEO

Dimpoz Aweka Hadharani Ugonjwa Unaomsumbua, Tazama Anavyongea Kwa Shida na Mtangazaji

$
0
0
Mwanamuziki wa Bongo Flavour Ommy Dimpoz anabainisha kilichopelekea afanyiwe operesheni ya koo nchini Afrika Kusini. Je anaendeleaje?

Msikilize hapa katika mahojiano maalum na Edo Kumwembe wa Mwananchi Digital akiwa nyumbani kwake Sandton..

VIDEO:

Mwananchi

Kwanini Baadhi ya Wanaume Wana Maumbile Mafupi na Upungufu wa Nguvu za Kiume? Suluhisho Hili Hapa

$
0
0
KWANINI BAADHI YA WANAUME WANA MAUMBILE MAFUPI NA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME DR SITTA NDO SULULISHO LAKO tatiza, hili limekuwa likiwaasili watu wengi,sana kisaikolojia hasa baadhi yao kujiona wako tofauti na wanaume wengine, kwa kawaida, mwanaume anatakiwa awe na uume, usiopungua nchi 6-7au-8 ,vinginevyo mtu huyo anamatatizo zipo , sababu nyingi zinazosababisha, tatizo hilo baadhi ni (i) upungufu wa vichocheo vya HORMONES ZA CETROGEN ambazo mwanaume, anapobarehe vichocheo hivi, HORMONES hizo, husaidia ukuaji wa uume

SUPER MIZIZI, ni dawa inayozalisha HORMONES ZA CETROGEN,na kufanya, uume kukuwa na kuongzeka sazi utakayo na kuzibua mlija iliysinyaa,

NSHOLA ni dawa bora, ya kurudisha nguvu, za, kiume bari inatibu ,kabisa kutoa tatizo hilo, na kukupa , hamu ya , kurudia tendo, la ndoa zaidi, ya mala nne 4 ,bila kuchoka atakama unaumli ,wa mika 80,! pia ana ,dawa za ,kutibu, presha ya kupanda ,na kushuka, kisukari kuondoa, mafuta , mwilini ,na maumivu ya, mgogo kiuno, dawa zipo, matazo, ya hedhi, kwa ,wanawake hedhi, zisizokuwa na, mpangilio, na kasonono, pia , vidonda ,vya, tumbo ,(STOMACHI UCLENS) IHUSHI ndoji lako.

NKANYA ni dwa ya mvuto wa kimapenzi ,mchumba mpenzi ariyekuacha, mke mme, atakuludia kwa, mda, wa msaa3 tu , ukishaitumia atarudi ,mwenyewe bila ,ugovi tena, NKOMA ni dawa kuongeza HIPS na mguu wa bia kwa wadada .

HERBON, ni, dawa, ya kuongeza, CD4, NGAKAMA ,ni dawa ya kutibu ,miguu, kufaganzi, na ,kuwaka moto, huduma zetu ,zipo ,vizuri, popote pale dawa utaletewa! DR SITTA, amebobea, kwa tiba asilia

DAR ANAPATIKANA MBAGALA, ZAKHEM, SONGEA BOMBAMBILI SHINYANGA, KAHAMA MJINI, KWA MAELEZO ZAIDI ,

PIGA SIMU 0763172670 au 0715172670

WOTE MNAKALIBISHWA, KAMA, UTAKUWA NA TATIZOUTAHUDUMIWA
Viewing all 104793 articles
Browse latest View live




Latest Images