Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104796 articles
Browse latest View live

CHADEMA Wamtaka Polepole Ajifunze Kupitia Kwa Mwigulu Nchemba

$
0
0

Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kimemtaka Katibu Mwenezi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Humphrey Polepole kuwa makini na kauli zake anazozitoa kuhusu mikutano ya hadhara lasivyo itakuja kumtokea kama Mwigulu Nchemba alivyofanyiwa.

Hayo yameelezwa na Mkurugenzi wa Itifaki na Mawasiliano ya Mambo ya Nje wa Chadema, John Mrema baada ya kupita siku kadhaa tokea Polepole alivyotoa kauli yake kuwa 'mikutano ya hadhara haijapigwa marufuku ila imewekewa utaratibu mzuri zaidi wa namna ambavyo wanapaswa kufanya siasa katika nchi huku akidai tatizo kubwa sio mikutano hiyo kutofanyika bali ni viongozi wa upinzani kuishi nje ya majimbo yao'.

"Hicho anachokifanya Polepole ni propaganda nyepesi tu na nimshauri kwamba kwa sasa ajifunze kupitia Mwigulu Nchemba maana naye alikuwa anasema hivyo hivyo kuwa mikutano haijazuiliwa lakini yeye mwenyewe ni juzi tu wamemzuia kufanya mikutano jimboni kwake kabla ya kumruhusu.

"Anavyosema mikutano haijazuiliwa yeye ndio anakuwa kinara sasa wa kupotosha umma juu ya suala hilo na wala sio sisi", amesema Mrema.

Pamoja na hayo, Mrema ameendelea kwa kusema "hoja yake ambayo anasema Wabunge wetu hawaishi katika majimbo yao ni dhaifu na mufilisi kwasababu Wabunge wetu ndio wanaongoza kukaa katika maeneo yao kuliko wowote wale na pia Wabunge wetu wamezuiliwa kufanya mikutano yao katika baadhi ya maeneo na tuna barua rasmi ya kuzuiliwa".

ACT- Wazalendo Wataja Sababu Chama Chao Kutokukubalika kwa Wanawake

$
0
0
Katibu wa Itikadi na Uenezi Chama cha ACT - Wazalendo, Ndg. Ado Shaibu amedai sababu kubwa ya  chama chao kuonekana hakikubaliki na wanawake wengi ni kutokana na mazingira yasiyo rafiki ya kufanya siasa za upinzani yalivyo nchini na kwamba hayavutii wanawake.

Shaibu amesema kwamba uwezo wa kuvutia wanawake kujiunga na vyama vya upinzani ni changamoto kwa kuwa siasa hizo ni za mikiki mikiki na hiyo imepelekea kuwa tatizo la ki-nchi na siyo la ACT tuu.

Kiongozi huyo ameongeza kwamba licha ya kwamba mazingira kuwa ni magumu, wao ACT wamechukua takwimu hizo za Taasisi ya TWAWEZA kama changamoto na wataangalia mbinu zinazofaa ili kushawishi wanawake wengi kujiunga na vyama vya upinzani.

"Takwimu za TWAWEZA hatupingani nazo japokuwa zina changamoto, kwa hili la kukubalika na wanaume zaidi ya wanawake tumelichukua kama changamoto.

"Tunatafuta mbinu za kuweza kushawishi wanawake wengi kujiunga. Unajua uwezo wa kuvutia wanawake wakaja kwenye siasa za upinzani ni changamoto sana.

"Siasa za upinzani ni mikiki mikiki, mabavu, vitisho, mahakamani na kiuhalisia wanawake wana majukumu mengi sana ikiwepo kulea familia hivyo inakuwa changamoto kwao," amesema Shaibu.

"Lakini ukienda hata kwenye vyama vingine huwezi kukuta wanawake wengi kuliko wanaume, hata ukienda Kamati Kuu ya CHADEMA, hii ni kutokana na mazingira ya siasa zetu yalivyo, hii ni changamoto kwetu sote". Aliongeza

Pamoja na hayo Shaibu amevitaka vyama vingine kutopuuza utafiti huo wa TWAWEZA unapotolewa na badala yake waufanyie kazi na hata kama kuna mapungufu wajitahidi kutoa maoni ya maboresho na siyo kubeza.

Katika takwimu zilizotolewa na TWAWEZA wiki iliyopita zinaonyesha kuwa Chama cha ACT- Wazalendo kinakubalika na asilimia 24 ya wanawake huku wanaume wakiwa ni asilimia 40 tu.

Kauli ya Jeshi la Polisi Baada ya Basi la Dar Express Kuteketea Kwa Moto

$
0
0
Baada ya basi la abiria  la Dar Express linalofanya safari zake Arusha - Dar es salaam kuteketea kwa moto  maeneo ya Tegeta,  Mkuu wa Kikosi cha Usalama Barabarani Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Marison Mwakyoma amesema bado wanamsaka dereva wa basi hilo ili kuweza kutoa maelezo ya kina juu ya ajali hiyo.

Kamanda Mwakyoma amesema kwamba ingawa taarifa za awali zinadai kwamba ni kufeli kwa breki ya nyuma, lakini zipo sababu za msingi ambazo zinaweza kutolewa na dereva huyo kwani tukio lililopelekea gari hilo kulipuka halikuwa la ghafla.

Akizungumzia ajali hiyo iliyotokea Tegeta  usiku wa kuamkia jana, Kamanda Mwakyoma amesema kwamba basi hilo lilitokea Arusha likuwa na abiria 42, ambapo 22 walishukia Bagamoyo na wengine waliosalia walifikia maamuzi  ya kushuka baada ya kuona gari linazidi kutoa harufu na ndipo dereva alipoamua kulitelekeza.

Aidha Mwakyoma ameongeza kwamba siyo kila ajali husababishwa na uzembe wa dereva kwani yapo mambo mengi ikiwepo nyaya za umeme kugusana, ku-jam kwa breki ya gari hivyo wamiliki wa magari wanapaswa kuwa makini wanapofanya 'service' ya magari ikiwa ni pamoja na kutazama mfumo mzima wa umeme na siyo kumwaga 'oil'.

Pamoja na hayo Mwakyoma amesema uchunguzi wa kina wa kuhusu ajali hiyo bado unaendelea kufanyika na sasa wanasubiria hati ya ukaguzi wa gari hilo kutokea Arusha kabla ya safari.

Nisha apost video mtandaoni inayomuonyesha Akibadilishana Ulimi na Mzungu

$
0
0
Msanii wa filamu Salma Jabu aka Nisha amewaacha mdomo wazi mashabiki wake wa filamu baada ya kupost video mtandaoni ambayo inamuonyesha akiliwa denda na mpenzi wake mpya mzungu.

Muigizaji huyo amedai hawezi kukaa kimya bila kumuonyesha mpenzi wake huyo licha ya mashabiki wengi mtandaoni kumdhihaki.

“Ni ngumu sana kuficha hisia zangu kwa mtu nnayempenda, nimeshakuwa na m-black, Mwarabu ila kote niliambulia usaliti na uongo wa mapenzi, niliwahi sikia Wazungu wana mapenzi ya kweli kuliko Waafrica, kujaribu si mbaya.

“Me ni msafiri sijafika bado, na Mwenyezi Mungu anajua kama hapa ndo mwisho wa safari yangu au inaendelea, kikubwa nimeshampata na maneno sijali,’ amesema Nisha.

Katika post nyingine Nisha amesema;“Walimwengu sijui mna nini, nikiibiwa bwana mnanyamaza kimya, nikiwa na wa rika langu ben 10, akinizidi umri kizee, au mlikuwa mnafurahia kujiita bachelor? Sasa nimeshampata bado maneno kedekede. Yeye na mimi kwani tuna kasoro gani? Au mimi nimezaliwa niliye tu na kuibiwa?”

A post shared by Salma Jabu Nisha (@nishabebee) on
.

Lugola: Bodaboda dawa yenu inachemka, aja na mwarobaini kupunguza ajali

$
0
0

Kufuatia kuvuliwa cheo kwa aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Ndani, Mwigulu Nchemba kutokana na ongezeko kubwa la ajali nchini na kuteuliwa kwa Kangi Lugola ambaye sasa anashika nafasi hiyo, Waziri huyo mpya tayari ameanza kazi kwa kasi hasa katika kutafuta suluhu za ajali ambazo zimekuwa zikitokea mara kwa mara.

Ambapo amesema Serikali inajipanga kuja na mbinu mpya ya kudhibiti na kupunguza ajali zinazosababishwa na pikipiki.

Lugola amesema Serikali itaanzisha utaratibu wa kufunga tela katika pikipiki kwamba abiria wataweza kupanda kati ya mmoja hadi wanne na kuketi katika tela hilo.

Kwa kufanya hivyo amesema ajali za pikipiki zitapungua kwa kiasi kikubwa sana kwani pikipiki zikishafungwa tela zitashindwa kutembea kwa mwendokasi mkubwa kutokana na uzito lakini pia zitashindwa kupenya penya barabarani na kufanya vurugu.

”Tutawafungia matela ya kubeba abiria na nyie mkae kwenye foleni kama bajaji na magari mengine. Matela haya yataleta utulivu barabarani lakini pia yatawaongezea tija kwani badala ya kubeba abiria mmoja sasa mtapakia zaidi” amesema Lugola

Ameongezea kuwa ufungwaji huo wa matela utahusisha zaidi pikipiki za biashara na hautazihusu pikipiki binafsi.

”Bodaboda dawa yenu inachemka Serikali inakuja na mpango madhubuti wa kupunguza kama si kumaliza kabisa ajali za barabarani zinazosababishwa na madereva pikipiki,” amesema Lugola.

Hii Hapa Dawa Bora ya Nguvu za Kiume na Maumbile Madogo ya Uume

$
0
0
Tatizo hili limekuwa likiwaadhiri watu wengi sana kisaikolojia hasa baada ya kujiona wapo tofauti sana na wengine kwa kawaida mwanaume anatakiwa awe na uume kuanzia nchi 6-8 kwanza upungufu wa vichocheo hivi huchochea ukuaji wa uume chongo ambalo hushambulia nerve ambayo uharibu kabisa ukuaji wa uume, ngiri, punyeto, ambayo huathili misuli ya uume, ngiri huleta maumivu, tumbo kuunguruma na kujaa gesi, korodani moja kuvimba, kutopata choo vizuri, sababu hizi hufanya uume kulegea na kusinyaa na kuwa mfupi na mwembamba na mara nyingi hata nguvu za kiume ( hamu ya tendo la ndoa) hupungua na kwisha kabisa

GEMBE :Ni dawa inayozalisha na kukufanya uume kukua na kuongezeka
NGEMO : Ni dawa bora ya kuongeza nguvu za kiume

Hukutia hamu ya kuludia tendo la ndoa zaidi mara4 nne bila kukinai au kuchoka pia itakufanya uchelewe kufika kileleni zaidi ya dk30-45 kwa mtumiaji pia tunatibu kisukari, bp, ngiri, miguu kuwaka moto KAMA HUNAMDA WA KUFIKA OFISINI KWETU UTALETEWA POPOTE TUPO MBAGALA RANGI TATU

 0753471612/ 0715249530
0623 386 305

DR KUZENZA

MAMBO 10 ya Kufanya Kabla Hujafikia Miaka 28..!!!

$
0
0
1. Jifunze kuweka akiba ya fedha

2.Tafuta mpenzi sahihi na tulia nae

3. Acha kuishi na wazazi au kupanga nyumba na washikaji

4. Achana na starehe zisizo na maana

5. Jali sana afya yako

6. Kuwa na marafiki wenye changamoto za maendeleo

7. Anza kununua asset kama vile ardhi, kitanda, vyombo vya nyumbani na n.k

8. Jifunze kuvaa kwa heshima na si tu suala la kupendeza

9. Acha mambo ya kitoto jisikie umekua mkubwa na mambo unayoyafanya yawe ya kiutu uzima

10. Zingatia sana muda wako.

HIVI Ndivyo Ubongo wa Mwanamke Unavyofanya Kazi kwa Haraka Zaidi Kuliko wa Mwanaume.!!!

$
0
0
Ubongo wa mwanamke ni mdogo kwa 8% kuliko wa mwanaume, lakini unamuungano wa mawasiliano (interconnections) nzuri sana kuliko wa mwanaume, na ndio mana mwanamke
anaweza kufanya kazi nyingi kwa wakati mmoja bila kukosea (multi-tasking).

Itakua umeshaona: kwa wakati huohuo, mwanamke anapika, anaangalia tamthilia kwenye TV, anasuka nywele n.k. na vyote hufanya kwa ufanisi, lakini mwanaume amalize kimoja kwanza ndio ahamie kingine.

Ubongo wa mwanamke unauwezo wa kufanya mawasiliano ya haraka sana (fast data transfer) kuliko wa mwanaume, hivyo mwanamke anao uwezo mkubwa wa kuwasiliana (communication), kusoma lugha za maumbile (body languages), kufikiri na kutabiri yajayo (situational thinking) kwa urahisi na haraka zaidi, yani mara 10 zaidi ya mwanaume. Ndio mana, mwanamke anauwezo wa kujenga mahusiano ya kijami kirahisi (social thinking and interaction) zaidi ya mwanaume.

Umeshawahi gundua: upo na mwanamke (dating with a lady) labda mpo beach au kwenye gari (private driving), alafu ukataka umbusu (kiss) kwa kumstukiza (obvious no one seeks lady's attention for kissing, it is done in surprise). Sasa kile kitendo cha wewe kuwaza kumbusu, utakuta yeye alishagundua dakika chache zilizopita kabla yako, kupitia mihemko ya mwili wako. Na kama hayupo tayari (ready for kissing), anao uwezo wa kukwepesha mdomo wake haraka zaidi kabla ya wewe kumfikia, bila kujali alikua ktk mazingira gani au akifanya nini.

Fahamu jinsi Damu ya Hedhi ya Mwanamke Ilivyo na Nguvu Katika Imani za Kishirikina..!!!

$
0
0

Nitangulie kuomba radhi kwa wale watakaokereka na hii mada..Nina heshima kubwa kwa akina mama wote na privacy yao..naomba tuichukulie hii kwa muktadha wa maarifa, elimu na ufunuo wa dunia ya upande wa imani

Makuzi yetu yametulea kutufundisha kwamba damu husika ni uchafu na jambo la Siri sana... Wahusika kwenye hili hufanya ni jambo la siri huku wengine wakijichukia kabisa

Kwa dhima ya udugu wa kishetani damu ya hedhi ni kitu cha thamani kubwa kwakuwa imebeba uhai nguvu na kiwakilishi cha maisha marefu, ikijulikana kama nyota ya moto kiashiria cha mungu mwezi...kwenye ibada za kishetani alama nyekundu ni kiwakilishi cha hiyo damu na hata wale ANNUNAKI(malaika walioanguka) wanaichukulia kama dhahabu ya miungu kwa imani yao
Hedhi mzunguko wake unatawaliwa na mizunguko ya mwezi na kuna mahusiano ya moja kwa moja kati ya damu ya hedhi mzunguko wa mwezi na mwanamke!

Kwa wenzetu wahindi hii wanaita SOMA na Greece ikijulikana kama AMBROSIA...Tafsiri kwa muktadha wao ikiwa asali ya miungu. ...

Mwezi ni alama ya makazi ya mungu na malaika wa kike. Hivyo basi ibada yoyote inayouhusika na kunywa damu ya hedhi, hiyo ni ibada ya kuabudu mwezi kwa maana ya kumuabudu mwanamke
Hapa kuna mifakarano kwa baadhi ya wayahudi kwakuwa baadhi yao hupenda kufuata kalenda ya mwezi na hata miungu yao mingi ikiwa ni masanamu ya kike lakini wale wanaojiita Israeties wakipinga hilo kwakuwa wanaamini anayepaswa kuabudiwa ni mungu jua hivyo kuabudu mwezi ni kuruhusu kutawaliwa na mwanamke....

Tukiachana na hao hapa kwetu damu ya hedhi hutumika kutengeneza dawa za mvuto wa kimapenzi na ishu za kishirikina kufarakanisha ama hata kupatanisha...!

Vyovyote iwavyo hiki tunachodhani ni uchafu kina siri yenye nguvu kubwa kwenye ulimwengu wa roho

FA!OFA!OFA je umepungukiwa nguvu za kiume na umetumia dawa bila mafanikio?

$
0
0

OFA!OFA!OFA je umepungukiwa nguvu za kiume na umetumia dawa bila mafanikio? sasa utapona kwa sh 15000 tu ofa ni kwa watu kumi wakwanza kila siku ofa hii itadumu ndani ya wiki 2 baada ya hapo bei itakuwa nyingine na kama hujapona tunakurudishia hera yako !

Dawa hii ni dawa ya maajabu huwezi kuamini Ila wengi wameiamini, inatibu tatizo la upungufu wa nguvu za kiume na utapewa garantee ya mwezi mmoja dawa hii inapatikana hapo hapo ulipo nyumbani kwako na tutakupatia maelezo ya namna ya kuiandaa wewe mwenyewe na baada ya kuiandaa utakunywa Mara moja tu,na hautatumia dawa yoyote ya nguvu za kiume dawa hii inawafaaa watu kuanzia miaka 18 mpaka miaka 70 zaidi ya miaka hyo haitakusaidia ni dawa ya asilia haina madhara yoyote.

Watafiti na waganga wameikubali pia hii dawa inawafaa hata wanawake wasiopata hisia za mapenzi pia tunaweza kukutumia dawa popote ulipo lakini c kwa bei ya ofa ukiitumia dawa hii unakuwa na uwezo wa kurudia tendo la ndoa zaidi ya Mara 3 bila hamu kuisha na itakufanya uwe na uwezo wa kufanya tendo la ndoa muda wowote imesaidia watu zaidi yawatu 148 ndani ya mwakammoja tangu igunduliwe Dr kiboko mganga wa tiba za jadi toka kisiwani mafia pia tunatibu magonjwa mbalimbali kurudisha mpenzi aliye kuacha,biashara iliyoyumba, kuondoa mikosi, nyota na nk maelezo zaidi Wasiliana na Dr kiboko 0679923297

Watu Wamtolea Povu Lulu Kushindwa Kumzika Patrick

$
0
0
BAADA ya mazishi ya mtoto wa muigizaji Rose Alphonce ‘Muna’, Patrick kufanyika kisha rafiki yake kipenzi, muigizaji Elizabeth Michael ‘Lulu’ kushindwa kuhudhuria, siri ya mrembo huyo kutoonekana msibani imefichuka!

Marehemu Patrick alizikwa juzi kwenye Makaburi ya Kinondoni jijini Dar baada ya kuagwa katika Viwanja vya Leaders Club. Gumzo la Lulu kutoonekaa liliibuka kwenye Viwanja vya Leaders wakati watu walipoanza zoezi la kuaga huku mastaa karibu wote wakiwa wameshaaga na Lulu kutoonekana.

“Mh! Mbona sielewi, naangalia mastaa wote wanaaga lakini Lulu sijamuona hapa kulikoni? Ana shida gani huyu mtoto,” alisikika mmoja wa waombolezaji anayeonekana kuwa na jicho la kidaku.

Kama hiyo haitoshi, mdaku mwingine aliyekuwepo msibani hapo, alinaswa na kinasa sauti cha Ijumaa Wikienda akienda mbali zaidi kwa kusema haiwezekani Lulu akashindwa kumzika Patrick ambaye alikuwa kipenzi chake na ukizingatia ni rafiki mkubwa wa Muna.“Haiingii akilini, kuna kitu tu lazima. Yaani mastaa karibu wote waje hapa halafu yeye ashindwe kufika, ni kitu cha kushangaza sana kwani yeye ni mtu wa karibu sana na familia ya Muna.”

MAPAPARAZI WAJIRIDHISHA

Mara baada ya mapaparazi wetu kujiridhisha kwamba Lulu hajakanyaga msibani kuanzia pale nyumbani kwa baba wa marehemu, Peter Zakaria Mwananyamala- Kisiwani, Leaders na hata makaburini ndipo walipochimba na kunasa mambo kibao yaliyofichika.

Ijumaa Wikienda lilianza kuzungumza na watu wa karibu na familia ya Peter ambao waliweka wazi kuwa wamesikitishwa na kitendo cha Lulu kushindwa kufika msibani, achilia hata kutoa pole.

“Lulu tumemshangaa sana, kweli kabisa unashindwa kutoa hata pole? Yaani Peter huyu ambaye alijitoa kwa hali na mali wakati wa kesi yake ya kuua bila kukusudia kweli anashindwa hata kumpigia simu kumpa pole? “Lulu ni wa kushindwa hata kufika hapa kwenye mazishi kweli? Yeye ni nani haswa hata ashindwe hata kuona ubinadamu katika jambo kama hili?” alihoji mwanafamilia huyo wa Peter.

SIRI YAFICHUKA

Mmoja wa wasanii ambao walikuwa upande wa Peter ambaye pia alikuwa akisimamia mambo mbalimbali katika msiba huo aliyeomba jina lake lisiandikwe gazetini, alivujisha siku kuwa kilichomfanya Lulu ashindwe kuhudhuria ni aibu.

“Ni aibu tu maana kama ulivyojua yeye alikuwa upande ule wa Muna, alionekana siku ya kwanza akiwa anaratibu msiba na yeye ndiye miongoni mwa wasanii waliokuwa wanamuunga mkono Muna kukataa baba yake marehemu asimzike mwanaye hivyo aliona akijitokeza pale wapambe wanaweza hata kumzomea kwa jinsi hali ya hewa ilivyokuwa imechafuka,” alidai mtu huyo.

NI MAMBO YA KISHERIA?

Baadhi ya waombolezaji walikwenda mbele zaidi na kudai kuwa, yawezekana Lulu kutomzika Patrick kumetokana na masuala ya kisheria kwamba haruhusiwi kwenda kwenye mijumuiko ya watu kama vile msibani, harusini na kwingineko lakini mmoja wa wanasheria alisema Lulu anaweza kwenda popote hata kuolewa anaruhusiwa.

PETER AFUNGUKA

Katika mahojiano maalum na Ijumaa Wikienda, baba wa marehemu Patrick alieleza kuwa amesikitishwa na kitendo cha Lulu kushindwa kumpa pole kwa msiba huo mzito wakati alijitoa kwa hali na mali kumsaidia alipopata matatizo ya kimahakama. Alisema, wakati Lulu alipokuwa akikabiliwa na kesi ya kumuua bila kukusudia muigizaji Steven Kanumba, alipokuwa mahabusu kabla ya kuhukumiwa, alimsaidia sana.

“Nilimsaidia sana kwa kumtumia pikipiki iliyokuwa inabeba chakula kila siku kwa muda mrefu, nilitoa hadi gari langu kwa ajili ya kumpeleka mahakamani lakini leo hii nashangaa sana anashindwa, hata kunipa pole?” alihoji Peter kwa uchungu.

MAMIA WAMUAGA

Katika safari yake ya mwisho Patrick ambaye alikuwa kipenzi cha watu wengi mtandaoni kutokana na muonekano wake, mamia ya watu walijitokeza kumuaga wakiwemo wasanii mbalimbali. Wakati Peter alipokuwa akitoa neno la shukurani, aliwataka watu waliokuwa wanamsema vibaya mitandaoni kuhusu yeye na Muna waache maana ni mke wake halali.

Alisema, alimtolea mahari na mama yake Muna akamkabidhi hivyo asingependa kuona suala hilo linajadiliwa zaidi kwenye mitandao ya kijamii. Lakini wakati akiyasema hayo, Muna alionekana kutikisa kichwa kuashiria kutokubaliana naye pamoja na kwamba walikuwa wameshapatanishwa, kitendo kilichozua minong’ono kwa watu waliokuwa karibu na mapaparazi wetu.

Kwa upande wake muigizaji Wema Sepetu alipopewa kipaza sauti, alisema anaelewa maumivu anayopitia Muna na kwamba anamuombea kwa Mungu aweze kusimama imara. Mrembo huyo ambaye aliwahi kuwa shosti wa karibu na Muna kisha kugombana, alitumia fursa hiyo kumaliza tofauti zake na kusema yaliyopita si ndwele, wagange yajayo.


Kwenye tukio hilo, baadhi ya wanaume ambao walitajwa kutembea na Muna kwa nyakati tofauti kama Casto Dickson na Joel Luaga ambaye ndiye anatajwa kuwa na uhusiano na Muna kwa sasa, walishindwa kuhudhuria mazishi hayo.

Wasanii waliojitokeza kumuaga katika Viwanja vya Leaders juzi licha ya Wema Sepetu ni Steven Mengere ‘Steve Nyerere’, Khadija Shaban ‘Keisha’, Halima Yahya ‘Davina’, Emmanuel Mgaya ‘Masanja’, Jimmy Mafufu, Zuwena Mohamed ‘Shilole’ na wengine wengi.

TUJIKUMBUSHE

Patrick alipatwa na umauti Julai 3, mwaka huu nchini Kenya baada ya kuugua na kulazwa kwa takriban siku sita. Mara baada ya kufariki dunia, uliibuka mvutano mkali kati ya Muna na mumewe juu ya suala zima la nani baba halali wa mtoto huyo. Peter alisema yeye ni baba halali kwani alimuoa Muna kwa ndoa takatifu na mtoto ni wake licha ya kumuoa akiwa na ujauzito wa miezi mitatu.

Baada ya kuyasema hayo, Muna aligeuza upepo kwa kusema baba wa mtoto ni Casto na kwamba shughuli za msiba zitafanyika nyumbani kwake Mbezi na si kwa mumewe huyo, Mwananyamala- Kisiwani. Kutokana na mvutano huo, Steve Nyerere alilazimika kuingilia kati na kutokana na busara zake alifanikiwa kuweka mambo sawa kwa kuzungumza na wanandoa hao ambapo Muna aliridhia msiba kufanyika nyumbani kwa mumewe.

Mtoto wa Miaka Miwili Afariki Baada ya Kujipiga Risasi

$
0
0
Mtoto wa miaka miwili afariki baada ya kujipiga risasi
Mtoto wa umri wa miaka miwili nchini Marekani amefariki baada ya kujipiga risasi kichwani kwa bunduki ambayo imekuwa ikihifadhiwa na wazazi wake nyumbani kwao.

Polisi wa Houston, Texas wanasema wazazi wa mtoto huyo - Christopher Williams Jr - walikuwa nyumbani wakati wa kutokea kwa kisa hicho.

Polisi wanasema bunduki hiyo ambayo hutumia risasi za ukubwa wa 9mm ilipatikana eneo la tukio na kwamba ilikuwa inamilikiwa na babake.

Mganga aliyedai kuwa na nguvu za kuzuia risasi afariki kwa kupigwa risasi
Mtoto wa miaka 9 amuua nduguye kwa risasi Marekani
Watoto kadha wamekuwa wakijipiga risasi na kujiua kimakosa nchini Marekani miaka ya karibuni.

Polisi wa Houston wamesema wanajaribu kubaini ni vipi mtoto huyo aliyepewa jina la utani "Junior" aliweza kuifikia bunduki hiyo.

Mkuu wa kitengo cha waathiriwa maalum katika idara ya polisi ya Houston David Angelo ametoa wito kwa wazazi walio na bunduki kuchukua tahadhari zaidi.

"Ni lazima uweke salama silaha, iwe ni kwa kuhakikisha kifaa cha kufyatulia risasi kimewekwa salama au kuiweka salama silaha kwa njia nyingine kuhakikisha matukio kama haya hayatokei tena siku za usoni," alisema.


Binamu yake marehemu Suzzane Alvarado ameambia ABC 13 kwamba marehemu "hakustahili yaliyomkuta. Alikuwa mtoto mdogo na mwenye matumaini makubwa maishani."

Kwa mujibu wa gazeti la Houston Chronicle, babake marehemu Christopher Charles Williams, alipatikana na hatia ya kuwa na bastola kinyume cha sheria mwaka 2009.
.

"Saa 24 kwa siku, alikuwa na mwanawe. Alikuwa akifanya zaidi ya kina baba wengine."

Jumatatu, polisi Houston walimshtaki baba mwingine kutokana na kujipiga risasi kimakosa kwa mwanawe wa kiume mwezi Mei.

Ali Parvez Masoom, 32, anadaiwa kuiacha bunduki yake aina ya .308 mezani ambapo mwanawe aliweza kuifikia na kujipiga risasi usoni.

Bw Massom aliachuliwa huru baada ya kulipa dhamana ya $1,000 (£750) na kwa sasa anakabiliwa na kosa la kutowajibika na kumuwezesha mtoto kuifikia silaha.

Jumamosi, mtoto mwingine wa miaka miwili alifariki Fresno, California katika kisa karibu sawa na hicho.

Wazazi wa mtoto huyo walikuwa nyumbani alipoifikia bastola hiyo na kujipiga risasi kichwani.

Idadi ya Vijana Waliookolewa Kutoka Pangoni Yafikia Nane

$
0
0

Idadi ya Vijana Waliookolewa Kutoka Pangoni Yafikia Nane
Shughuli ya kuwaokoa vijana 12 wa timu ya soka na kocha wao waliokwama kwenye pango kwa zaidi wa wiki mbili imechukuliwa kama mchezo wa sinema.

Ilihitajii ujasiri na weledi kutokana na mazingira magumu ya tukio hilo. Timu ya waokoaji ililazimika kunoa bongo na kuweka michoro kufanikisha kazi ya uokoaji bila ya kuathiri maisha yao na ya vijana wenyewe.

Ugumu wa kazi hiyo uliongezeka zaidi baada ya mwogeleaji mmoja kuzama maji na kufariki dunia wakati akirejea toka walikonasa vijana hao.

Uokoaji huo ambao pia unawahusisha waogeleaji wa kimataifa umefanywa kwa tahadhari kubwa hasa wakati huu ambapo mamlaka ya hali ya hewa ikionywa uwezekano wa kutokea mvua na kutatiza kazi ya uokoaji.

Tayari zaidi ya nusu ya vijana hao wameokolewa, wanne wa kwanza waliokolewa Jumapili asubuhi na baadaye kijana mwingine kuokolewa jana kabla ya idadi yao kuongezeka tena jana hiyo hiyo jioni kwa watu kuokolewa na kufikia wanane na hivyo hadi sasa pangoni wamebaki watu watano.

Maofisa wanaosimamia kazi hiyo wameanza kutoka taarifa zenye matarajio chanya kuhusiana na shughuli hiyo ya uokozi ambayo kwa kipindi kirefu imekabiliwa na vikwazo, ambavyo ni pamoja na mvua kubwa iliyosababisha mafuriko.

Mapema jana kamanda wa kikosi cha uokozi, Narongsak Osottanakorn alisema awamu ya pili ya uokozi ilishaanza na kuna matarajio makubwa ya vijana hao kuokolewa wakiwa salama.

Waziri wa Mambo ya Nje wa Australia, Julie Bishop ameelezea kuridhishwa na hatua iliyofikiwa hadi sasa hususan baada ya vijana hao kuokolewa.

Australia imetuma wataalamu 19, ikiwa ni pamoja na daktari ambaye amekuwa akijihusisha zaidi na kuwapima wavulana hao, na kutoa kibali cha kuwaondoa kwa kuzingatia hali yao kiafya.

Vijana hao waliookolewa wanapatiwa matibabu na familia zao bado hazijaanza kuwaona, hadi baada ya kuruhusiwa na madaktari

Ingawa walikuwa na afya njema, lakini walikuwa na njaa kali. Maofisa wamesema, vijana hao hata hivyo, wametengwa na wazazi wao kwa sasa ili kuepusha hatari ya magonjwa ya kuambukiza.

Kamanda Narungsok, amewaambia waandishi wa habari kwamba, hali ya hewa ni nzuri na kiwango cha maji ni kidogo na hivyo waliamua kuanza mapema shughuli hiyo kuliko ilivyotarajiwa.

Lakini kwa upande mwingine kamanda huyo ameelezea wasiwasi kuhusu mabadiliko ya hali ya hewa, baada ya mamlaka ya hali ya hewa kutangaza mvua kubwa itakayonyesha eneo hilo kuanzia jana mchana na kuendelea kwa wiki nzima, hatua inayoweza kusababisha ugumu kwenye kazi hiyo.

Operesheni hiyo ngumu ya uokozi ambayo inawashirikisha wapigambizi mahiri kutoka Thailand na nchi nyingine kadhaa za kigeni imekuwa ikifanywa kwa uangalifu mkubwa.

Kulingana na mipango ya uokozi, kila kijana alikuwa akisindikizwa na wapigambizi wawili wenye uzoefu, na walikuwa wakitolewa mmoja baada ya mwingine.

Kila kijana anavishwa kifaa maalumu cha kumsaidia kupumua ndani ya maji, huku akiongozwa kwa kamba na wapigambizi mahiri, mmoja mbele, mwingine nyuma.Baada ya kuvuka vyumba vitatu vya pango hilo, vijana hao hutembea sehemu iliyobaki ya mwendo wa takriban kilomita mbili.

Kwa ujumla wapo wapigambizi wazoefu wapatao 90 watakaohusika katika operesheni hii ya uokozi, 40 miongoni mwao wakiwa ni kutoka nchi za kigeni.

Gavana Osotthanakorn amesema baadhi ya sehemu za pango zimejaa maji hadi juu, ikimaanisha kuwa njia pekee za kuzivuka ni kupita ndani ya maji hayo ukiwa na vifaa vya hewa ya oksijeni.

Lakini kwa ujumla kiwango cha maji ndani ya pango hilo kimepungua kutokana na juhudi zilizofanywa kuyavuta nje.

Madaktari kutoka Australia waliingia katika pango hilo jana asubuhi kutathmini afya ya wavulana hao, na kutoa ripoti kwamba wanao uwezo wa kuanza safari ngumu ya kutoka nje.

Hospitali ya Chiangrai Prachunakroh iliyo umbali wa km 60 kutoka kwenye pango hilo, imejiweka tayari kuwapokea mara tu watakapofanikiwa kutoka nje.

Vijana hao waliingia katika pango hilo Juni 23 wakiwa na kocha wao mwenye umri wa miaka 25, lakini baada ya kuingia wakazingirwa na maji yaliyojazwa na mvua iliyonyesha ghafla. Wavulana hao 12 wana umri wa kati ya miaka 11 na 16. Ilichukua muda wa siku tisa kuwasaka kabla ya kugundulika kuwa walikuwa wamenasa pangoni.

Hii Hapa Ratiba ya Nusu Fainali Kombe la Dunia

$
0
0
Hii Hapa Ratiba ya Nusu Fainali Kombe la Dunia
HAPA nimekuwekea ratiba ya mechi zote za Nusu Fainali michuanpo ya Fainali za Kombe la Dunia 2018  nchini Urusi, kuanzia kuanzia leo Julai 10, 2018.

Semi-finals
Tuesday 10 July
France vs Belgium  – St Petersburg, 7pm (Match 61) – Saa 3:00 Usiku

Wednesday 11 July
England vs Croatia – Moscow (Luzhniki), 7pm (Match 62) – Saa 3:00 Usiku

Third place play-off
Saturday 14 July

Loser match 61 vs Loser match 62 – St Petersburg, 3pm

World Cup 2018 final
Sunday 15 July

Moscow (Luzhniki), 4pm

Straika wa Croatia Amwaga Pombe za Bure kwa Mashabiki wa Timu Hiyo

$
0
0
Straika wa Croatia Amwaga Pombe za Bure kwa Mashabiki wa Timu Hiyo
Straika wa Croatia, Mario Mandzukic ametumia jumla ya pauni 3,000 kuwanunulia pombe mashabiki wa timu hiyo ambayo ipo kwenye michuano ya kombe la dunia.

Croatia fans in Slavonski Brod enjoyed free beers thanks to star striker Mario Mandzukic

Mandzukic alitumia kiasi hicho cha fedha kuwanunulia pombe mashabiki wa Croatia ambao wapo kwenye mji aliyotoka mchezaji huyo wakati wa mechi yao ya robo fainali dhidi ya Urusi na kushinda kwa mikwaju ya penati.

The forward accumulated a bar bill of £3,000 so fans in his home town could enjoy free beers

Kwa mujibu wa chombo cha Croatia news site 24Sata kimesema kuwa nyota huyo mwenye umri wa miaka 32 anayekipiga kwenye klabu ya Juventus amewalipia zaidi ya maelfu ya mashabiki pombe kushudia mchezo huo kupitia Tv kubwa inayopatikana Brod Fortress.

Mandzukic and Co fought hard against Russia to earn a semi-final date with England next


Wanafunzi Kenya Wanachoma Shule kwa Kuogopa Mitihani

$
0
0
Wanafunzi Kenya wanachoma shule kwa kuogopa mitihani
Zaidi ya shule 10 zimefungwa nchini Kenya kufuatia kinachotajwa kuwa ni utovu wa nidhamu na uharibifu wa mali.

Shule 7 kati ya 10 zilizofungwa zimeteketezwa moto inatuhumiwa na wanafunzi.

Mabweni katika shule hizo yaliteketezwa moto wakati wanafunzi walipokuwa darasani wakidurusu jioni.

Wizara ya elimu nchini inasema huenda ghasia hizo zinatokana na uoga walio nao wanafunzi wa mtihani.

Je kuna ukweli gani katika hili?
Dickson Bandika, mwanafunzi wa zamani katika shule ya upili ya Kenyatta Mwatate pwani ya Kenya anasema kwamba wanafunzi wanaona ghasia na maandamano ndio njia pekee ya kuwasilisha malalamiko yao bila ya kutambuliwa, kulengwa na kuonewa kwa malalamiko wanayoyawasilisha.

Ameeleza kwamba katika kuepuka aibu ya matokeo duni ya mitihani, wanafunzi huzusha ghasia katika kutaka kukwepa mitihani hiyo.

'Watu wanaogopa kuonekana mumeshindwa na shule fulani'.

kitabu kimeteketezwa
'Tulikuwa hatuna shida na mitihani ya ndani ya shule, tatizo linazuka inapokuwa mitihani ya kieneo ambapo matokeo huziorodhesha shule kwa ubora wake. Hiyo aibu ndiyo watu waliokuwa wanaiogopa'. Amesema Dickson.

Wizara ya Elimu inasema nini?
Amina Mohammed waziri wa elimu Kenya anasema wanafunzi walizusha ghasia kupinga hatua kali zilizoidhinishwa hivi karibuni na wizara kuzuia udanganyifu katika mitihani.

Ameeleza kuwa katika shuel mbili, wanafunzi waliokuwa wanagoma walitaka mwalimu mkuu awaahidi kuwa atawasaidia kudanganya katika mtihani mkuu wa mwisho wa kufuzu kuingia vyuo vikuu.

'Kwa zaidi ya miaka miwili wizara ya elimu imekaa ngumu sana na baadhi ya wanafunzi wa shule ya upili wana shinikizo kubwa sana la kutaka kupita mtihani, na sababu nyingine ni kesi za kawaida za utovu wa nidhamu tu' amesema waziri wa elimu Kenya, Amina Mohammed.

Tarimba Ajitoa Katika Kamati ya Kuisaidia Yanga .... Afunguka Mazito

$
0
0
Tarimba Ajitoa Katika Kamati ya Kuisaidia Yanga .... Afunguka Mazito
Aliyekuwa Mwenyekiti wa Kamati Maalum ya kuivusha Yanga wakati wa mpito, Abbas Tarimba, ametangaza kuachana rasmi na wadhifa huo.


Kwa mujibu wa Radio Uhuru, Tarimba amefunguka na kueleza kuwa kumekuwa hakuna maelewano baina yake na Makamu Mwenyikiti wa Yanga, Clement Sanga, ambaye ameivunja kimyakimya kamati hiyo ambayo ilipitishwa katika mkutano mkuu.

Kufuatia tukio la kuvunjwa kwa kamati, Tarimba amesema hawezi akawa na muda wa kuonana na Sanga kwasababu ameivunja kamati, na hata kama asingefanya hivyo asingekuwa tayari kutekeleza majukumu ya kamati hiyo.

"Waachane na mimi , mimi sina muda wa kuonana na Sanga waachane na mimi, yeye kwanza kamati kaisha ivunja na hata kama wasinge vunja mimi nisingeweza kufanya kazi nao" alisema Tarimba.

Mbali na kauli hiyo, Tarimba amekanusha uwepo wa taarifa zilizokuwa zimeripotiwa kuwa kamati yake imelipa madeni ya fedha zote zilizokuwa ni malimbikizo ya madeni kwa wachezaji.

Tarimba ameeleza kuwa hakuna ukweli kuhusiana na hilo akiwahusisha viongozi wa Yanga kuwa wamekuwa waongo hivyo na kuwaomba waache masuala ya usanii kwa kuwa klabu hiyo ni taasisi kubwa.

"Wanayanga mnadanganywa Yaani wanayanga mnadanganywa mchana kweupe, Yanga tuna tamaduni zetu sio hizi, viongozi ni waongo ,nawaomba watulize akili zao wasaidie timu ,wengine ni wakubwa wanaongoza mpaka bodi ya ligi ,sasa watumie ukubwa huo kuipeleka Yanga mbele waache uongo uongo" alisema.

Hivi Ndivyo Kifuu cha Nazi Kinavyosababisha Mabusha

$
0
0
Hivi Ndivyo Kifuu cha Nazi Kinavyosababisha Mabusha
Inakadiriwa kuwa karibu asilimia moja ya wanaume wote kote duniani huathiriwa na ugonjwa wa mabusha, kwa hapa nchini, tatizo hili ni maarufu sana maeneo ya mwambao wa Pwani ya Bahari ya Hindi, mikoa ya Pwani, Tanga na Dar es salaam.

Tofauti na wengi wanavyodhani kuwa mabusha huwapata wanaume tu, wataalamu wanasema ni ugonjwa wa jinsia zote haubagui kwakuwa mbu anayeeneza ugonjwa huo hachagui kwani hata wanawake huambukizwa ugonjwa huo.

Www.eatv.tv imefanya mahojiano na Daktari kutoka Mpango wa taifa wa kudhibiti magonjwa yaliyokuwa hayapewi kipaumbele, Dkt. Oscar Kaitaba ambapo amesema kuwa ugonjwa wa mabusha umekuwa ukienezwa na mbua ambao chanzo chake kikuu ni vifuu vya nazi na madafu baada ya kutumika na kutupwa ovyo mvua zinaponyesha maji hutuama na kugeuka mazalia ya mbu wanao ambukiza ugonjwa huo.

“Wengi wetu tukimaliza kutumia vifuu vya nazi hatufahamu kama vina madhara matokeo yake vinazagaa na kuzalisha mbu, kifuu kinazalisha mbu anaye ambukiza matende na mabusha kutokana na kugeuka mazalia ya mbu pindi mvua zinapoanza kunyesha”, amesema Dkt. Kaitaba.

Daktari ameongeza kuwa, “Busha linawapata pia wanawake lakini wengi huwa hawajitokezi na nadhani kwa sababu zamani kwa mfano walikuwa wakijifungua kwa wakunga wa jadi ilikuwa rahisi kwao kujificha,  kwa wanawake huwa mashavu ya uke yanavimba kiasi cha kuziba kabisa eneo lote la uke na wakati mwingine uvimbe unapozidi huweza kuziba ile njia ya mkojo na hivyo kusababisha kupata mkojo kwa kiwango kidogo mno”.

Dkt. Kaitaba ameongeza kuwa, dhana iliyojengeka kwa jamii kwamba ulaji wa madafu unasababisha mabusha si kweli bali ugonjwa huo unazalishwa na mbu anayezaliwa kutokana na vifuu vya nazi kutupwa ovyo na kuhifadhi maji, lakini wengi huhusisha ugonjwa huo na imani za kishirikina jamboa ambalo wataalamu wa afya wanalipiga vita.

Mabusha ni uvimbe kwenye korodani ambao unasababishwa na kujaa kwa maji kwenye moja ya sehemu zinazounda korodani na hutokea pale maji yanayotengenezwa kwenye korodani kua mengi sana kuliko yale yanayo ondolewa.

Kwanini Baadhi ya Wanaume Wana Maumbile Mafupi na Upungufu wa Nguvu za Kiume? Suluhisho Hili Hapa

$
0
0
KWANINI BAADHI YA WANAUME WANA MAUMBILE MAFUPI NA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME DR SITTA NDO SULULISHO LAKO tatiza, hili limekuwa likiwaasili watu wengi,sana kisaikolojia hasa baadhi yao kujiona wako tofauti na wanaume wengine, kwa kawaida, mwanaume anatakiwa awe na uume, usiopungua nchi 6-7au-8 ,vinginevyo mtu huyo anamatatizo zipo , sababu nyingi zinazosababisha, tatizo hilo baadhi ni (i) upungufu wa vichocheo vya HORMONES ZA CETROGEN ambazo mwanaume, anapobarehe vichocheo hivi, HORMONES hizo, husaidia ukuaji wa uume

SUPER MIZIZI, ni dawa inayozalisha HORMONES ZA CETROGEN,na kufanya, uume kukuwa na kuongzeka sazi utakayo na kuzibua mlija iliysinyaa,

NSHOLA ni dawa bora, ya kurudisha nguvu, za, kiume bari inatibu ,kabisa kutoa tatizo hilo, na kukupa , hamu ya , kurudia tendo, la ndoa zaidi, ya mala nne 4 ,bila kuchoka atakama unaumli ,wa mika 80,! pia ana ,dawa za ,kutibu, presha ya kupanda ,na kushuka, kisukari kuondoa, mafuta , mwilini ,na maumivu ya, mgogo kiuno, dawa zipo, matazo, ya hedhi, kwa ,wanawake hedhi, zisizokuwa na, mpangilio, na kasonono, pia , vidonda ,vya, tumbo ,(STOMACHI UCLENS) IHUSHI ndoji lako.

NKANYA ni dwa ya mvuto wa kimapenzi ,mchumba mpenzi ariyekuacha, mke mme, atakuludia kwa, mda, wa msaa3 tu , ukishaitumia atarudi ,mwenyewe bila ,ugovi tena, NKOMA ni dawa kuongeza HIPS na mguu wa bia kwa wadada .

HERBON, ni, dawa, ya kuongeza, CD4, NGAKAMA ,ni dawa ya kutibu ,miguu, kufaganzi, na ,kuwaka moto, huduma zetu ,zipo ,vizuri, popote pale dawa utaletewa! DR SITTA, amebobea, kwa tiba asilia

DAR ANAPATIKANA MBAGALA, ZAKHEM, SONGEA BOMBAMBILI SHINYANGA, KAHAMA MJINI, KWA MAELEZO ZAIDI ,

PIGA SIMU 0763172670 au 0715172670

WOTE MNAKALIBISHWA, KAMA, UTAKUWA NA TATIZOUTAHUDUMIWA

Kila Mwanamke Kabla Hatujavurugwa na Dunia, Matamanio yetu ni Kuolewa na Mwanaume Amazing..Ila...

$
0
0
Kuna hili jambo ningependa tujadiliane ama tushirikishane kidogo.

Hakuna asiejua kuwa kila mwanamke kabla hatujavurugwa na dunia huwa matamanio yetu ni siku moja kuolewa na kutengeneza familia na mwanaume fulani hivi amazing(fantancy vs reality).

Sasa tatizo linakuja kuwa huwa wanawake wengi wana mentality kuwa maandalizi ya familia ya baadae haswa kwa mambo yanayohusu assets na gharama zingine ni majukumu ya mwanaume na sio mwanamke.
Hivyo unaweza kukuta binti ana kazi nzuri tu ila hata kujiwekeza kununua hata kiwanja walaaa hawazi au hata kufungua biashara. Anawekeza kwenye mikoba,mawigi,simu za bei ghali,viatu nk. Vitu ambavyo ukivipigia mahesabu unakuta ana viwanja vitano vikubwa tu huku kijijini kwetu.

Hebu fikiria unaolewa ukiwa angalau umejiwekeza kiasi fulani hivyo mkiunganisha nguvu na mwenza wako angalau mnapiga hatua kadhaa kwa haraka kuliko kusubiria mwanaume afanye kila kitu.

Wakati mwingine unakuta binti anadate mwanaume mwenye expossure ya kutosha na mfanyabiashara mzuri, hata kuomba basi hata aelekezwe abc's za biashara, hata kuunganishwa kibiashara nehiiii.

Au unadate mwanaume mwenye uwezo mkubwa kifedha hivyo kazi yake ni kuomba kununuliwa simu ya milioni 2 nk, vitu vya anasa ambavyo kwa kiasi kikubwa havikuongezei lolote la maana zaidi ya sifa za kijinga. Ni kwanini usimuombe mtu wa aina hiyo hata business idea, au angalau uanze jambo lako ie biashara,ujenzi nk kisha umuombe akuongezee kiasi fulani cha pesa? Kwa mwanaume mwenye upeo atakuona una akili na anaweza kukusogeza mahali pazuri.

Mwingine unakuta ni mama kabisa ila hata haiwazii kesho ya mtoto wake ambae anamlea peke yake, yuko busy na starehe na kutumbua pesa za child support, kesho na keshokutwa baba hayupo mtu anaanza kuhaha wakati nafasi ilikuwepo akaichezea

Maisha yamebadilika sana jamani basi nasi wanawake tubadilike in a positive way, tuyaishi maisha halisi na sio ya kuigiza ili angalau tunapoingia kwenye maisha ya ndoa angalau tuwe na cha kuongeza sio ndio ukiolewa umtwishe mwanaume majukumu ya familia mnayoijenga,familia ya kwao na ya kwenu pia. No wonder wanakufa mapema hawa watu.

Tuzitumie fursa vizuri pale zinapopatikana kabla haijawa too late.

Jamani hapa simchagulii mtu maisha ila hakikisha hautokuwa na majuto baadae kuwa "laiti ningejua"!!! Maana hakuna anaependa kesho yake iwe ya kuunga unga.

Nawasilisha.
Viewing all 104796 articles
Browse latest View live




Latest Images