Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104799 articles
Browse latest View live

“Ubelgiji ilistahili kucheza fainali kombe la dunia 2018 kuliko Ufaransa”-Shaffih Dauda

$
0
0
Jana Ubelgiji walifanikiwa kuwa washindi wa tatu wa fainali za kombe la dunia 2018 baada ya kuifunga England kwa magoli 2-0.

Ubelgiji imetoa meseji kwa dunia kwamba ilijiandaa kwa ajili ya kufanya vizuri kwenye fainali za kombe la dunia mwaka huu ukiangalia namna walivyocheza na kiwango walichoonesha katika mechi zote kuanzia hatua ya makundi.



Huku na huko Shaffih Dauda huyu hapa, yeye kwa upande wake anasema Ubelgiji hawakustahili kucheza mechi ya mshindi wa tatu, yeye anasema walistahili kucheza fainali na kuwa mabingwa au washindi wa pili.

“Ubelgiji ni kikosi ambacho sio kimekuja tu Urusi kushiriki kombe la dunia ni timu ambayo imeandaliwa (project). Wakati wanaanza kuunganishwa pamoja ilikuwa ni mpango wa taifa la Ubelgiji pamoja na chama cha soka wakiwa wameweka mpango wa muda mrefu ili kufanya vizuri kwenye mashindano.



“Walianza kutengeneza academies ili kuzalisha vipaji vingi kama akina De Bruyne, Courtois, Kompany, Naigollani na wengine ambao wote ni kizazi kimoja.

“Ubelgiji ilikuwa inatarajiwa kufanya vizuri na kila mtu ameona ni timu ambayo haikustahili hata kumaliza katika nafasi ya tatu kwa mtazamo wangu. Ni timu ambayo ilistahili kucheza fainali, kwa upande wangu naona Ubelgiji walistahili kucheza fainali kuliko Ufaransa kutokana na project yao ilivyokwenda na timu yao inavyocheza.

“Wameonesha kiwango cha juu na matokeo waliyokuwa wakipata walistahili. Kwangu Ubelgiji ni moja kati ya timu bora ambazo zimenifurahisha kwenye mashindano ya mwaka huu (2018).

“Watu wengi wanaweza kusema walistahili kumaliza katika nafasi ya tatu lakini mimi siwezi kusema wamestahili kuwa washindi wa tatu, walistahili kushika nafasi mbili za juu kuwa mabingwa au nafasi ya pili kwa maana ya kucheza mechi ya fainali.



Jambo la kujifunza

Watu wengi walitarajia kuona mabadiliko makubwa kwenye vikosi vyote katika mechi hii ya mshindi wa tatu, waliamini wachezaji ambao hawakupata nafasi kwenye mechi zilizopita ndio ingekuwa mechi yao lakini ilikuwa tofauti kabisa.

Makocha wote waliitolea macho mechi hiyo, kwa kuonesha umuhimu wake walipanga wachezaji wengi waliocheza kikosi cha kwanza mechi zilizopita hata mabadiliko yaliyokuwepo likuwa ya kiufundi hayakuwa ilimradi tu mchezaji fulani nae acheze mechi ya kombe la duni.

“Level ya professionalism kwa wenzetu ipo juu sana, kuna baadhi ya watu mechi ya mshindi wa watatu wanaichukulia poa. Hii ni mechi ambayo ipo kwenye utaratibu kama mechi nyingine zote, mshindi wa tatu anapata sifa na ‘insentives’.

“Pia Fifa wana sisitiza kuupa heshima mchezo wa mpira wa miguu na wenzetu ambao wameendelea katika level za juu wanaelewa hilo.

“Hakuna mechi ambayo ya kuchukulia poa, hivi karibuni tuliona mechi ya EPL Stoke City wakiwa tayari wameshuka daraja walicheza mechi yao ya mwisho kwa nguvu zote kutafuta ushindi hii ndio inaonesha level ya professionalism hivi ni vitu vya kujifunza sisi ambao tunakua.”

Shafih

Rekodi zinasemaje kuhusu Ufaransa vs Croatia? Wote wana nafasi

$
0
0
 
Wakati watu wengi wakiwaza ni ajabu kwa Croatia kwenda fainali na huku wana watu milioni 4.17 tu nchini mwao, wanasahu mwaka 1930 ambapo Uruguay walikwenda fainali huku taifa lao likiwa na watu milioni 1.7 na wakabeba ubingwa.

Mwaka 1991 ndipo taifa hili lilipata uhuru wake kamili, na raia wa Croatia wanaamini kuingia katika fainali za mwaka huu ni kama ndoto kwao ambayo imetimia wakiwa na imani wanaweza fanya lolote dhidi ya Ufaransa.

Kuna wazee wanaoamini kuhusu data na rekodi na wanaoamini hivyo wanawapa Croatia nafasi kubeba kombe hii leo kwani mara mbili zilizopita ambazo taifa lilicheza fainali ya kombe la dunia ya kwanza kama ilivyo Croatia walibeba kombe hilo(Ufaransa 1998 na Hispania 2010).

Lakini Croatia wakiwaza hivyo, kwa Ufaransa mawazo yao ni tofauti na matumaini yao ni makubwa sana hii leo kwani hawa Wacroatia wameshawafunga katika mara zote tano ambazo timu hizi zimekutana.

Mwaka 1998 ngoja nkukumbushe, Croatia walikutana na Ufaransa katika mchezo wa nusu fainali kombe la duniana Croatia wakaanza kufunga wao lakini baadae Ufaransa walisawazisha na wakapata goli la ushindi mechi ikaisha 2-1.

Endapo Ufaransa watafanikiwa kubeba kombe hii leo baasi Didier Dechamps atakuwa kocha wa tatu kuwahi kuchukua kombe hilo kama mchezaji na pia kocha baada ya Mario Zagallo na Franz Bckenbauer.

Kylian Mbappe atavunja rekodi nyingine ya Pele hii leo kama atafanikiwa kufunga goli kwani atakuwa kinda wa pili kuwahi kufunga katika fainali za kombe la dunia tangu baada ya Pele kufunga mwaka 1958.

Ufaransa pia wanatafuta nafasi hii leo ya kuingia kwenye kundi la mataifa ambayo yamebeba kombe hili zaidi ya mara moja wakiungana na Brazil, Ujerumani, Italia na Argentina.

Shafih Dauda

Naibu Spika wa Bunge Dk. Tulia Ackson Kugombea Ubunge 2020

$
0
0
Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Tulia Ackson, amekiri kuwa na matarajio ya kugombea nafasi ya ubunge katika moja ya majimbo ya Mkoa wa Mbeya.

Ingawa hakutaja jimbo ambalo atagombea, watu ambao wamekuwa wakifuatilia mwenendo wake wanasema huenda akagombea Jimbo la Mbeya Mjini linaloongozwa na Mbunge wa Chadema, Joseph Mbilinyi (Sugu) au Jimbo la Rungwe linaloongozwa na Sauli Amon wa CCM kutokana na miradi mingi inayotekelezwa na taasisi yake inayofahamika kama Tulia Trust kuelekezwa katika maeneo hayo.

Akizungumza na waandishi wa habari jana katika viwanja vilivyopo nyumbani kwake eneo la uzunguni jijini hapa, Naibu Spika huyo alisema ingawa anatambua ya kwamba dhamana ya uwakilishi ipo mikononi mwa wananchi, lakini ndani ya chama chake upo utaratibu hivyo wakati utakapofika ataamua.

“Wengi wamekuwa wakihoji kwamba je, nina nia ya kugombea? Na hata hapa kuna baadhi yenu mmeniuliza, ngoja niondoe sintofahamu hii, ni kweli nia yangu ya kugombea ubunge ipo lakini bado sijajua nitagombea wapi,” alisema.

Alisema CCM imeweka utaratibu mzuri kwa wanachama wake wenye nia ya kugombea nafasi mbalimbali na wale wanaotaka kuwawakilisha wananchi bungeni, hivyo haitakuwa busara kwake kuvunja kanuni, taratibu na sheria za chama.

Alisema kwa sasa anatekeleza majukumu ya Serikali ya kuhakikisha wananchi wa Mkoa wa Mbeya na nchi kwa ujumla wanapata maendeleo.

Kuhusu taasisi yake ya Tulia Trust, alisema imejipanga vema kuleta ukombozi wa Mtanzania kupitia sekta ya elimu.

Aidha, akizungumzia siasa zinavyokwamisha maendeleo ya Mkoa wa Mbeya, Dk. Tulia aliwaasa watendaji na wanasiasa kuondoa siasa kwenye masuala muhimu ya maendeleo na kwamba atahakikisha anawasilisha changamoto hizo kwenye vyombo husika ili hatua kwa wahusika zichukuliwe.

“Waandishi mmeeleza mengi lakini kubwa ninaloliona ni changamoto za siasa kuingizwa kwenye utendaji kazi hasa kwenye mambo muhimu ya maendeleo, hili nitalifanyia kazi na kuangalia uwezekano wa kulikomesha kwani Mbeya itajengwa na Wanambeya wenyewe,” alisema.


OFA!OFA!OFA Je Umepungukiwa Nguvu za Kiume na Umetumia Dawa Bila Mafanikio?

$
0
0
OFA!OFA!OFA je umepungukiwa nguvu za kiume na umetumia dawa bila mafanikio? sasa utapona kwa sh 15000 tu ofa ni kwa watu kumi wakwanza kila siku ofa hii itadumu ndani ya wiki 2 baada ya hapo bei itakuwa nyingine na kama hujapona tunakurudishia hera yako !

Dawa hii ni dawa ya maajabu huwezi kuamini Ila wengi wameiamini, inatibu tatizo la upungufu wa nguvu za kiume na utapewa garantee ya mwezi mmoja dawa hii inapatikana hapo hapo ulipo nyumbani kwako na tutakupatia maelezo ya namna ya kuiandaa wewe mwenyewe na baada ya kuiandaa utakunywa Mara moja tu,na hautatumia dawa yoyote ya nguvu za kiume dawa hii inawafaaa watu kuanzia miaka 18 mpaka miaka 70 zaidi ya miaka hyo haitakusaidia ni dawa ya asilia haina madhara yoyote.

Watafiti na waganga wameikubali pia hii dawa inawafaa hata wanawake wasiopata hisia za mapenzi pia tunaweza kukutumia dawa popote ulipo lakini c kwa bei ya ofa ukiitumia dawa hii unakuwa na uwezo wa kurudia tendo la ndoa zaidi ya Mara 3 bila hamu kuisha na itakufanya uwe na uwezo wa kufanya tendo la ndoa muda wowote imesaidia watu zaidi yawatu 148 ndani ya mwakammoja tangu igunduliwe Dr kiboko mganga wa tiba za jadi toka kisiwani mafia pia tunatibu magonjwa mbalimbali kurudisha mpenzi aliye kuacha,biashara iliyoyumba, kuondoa mikosi, nyota na nk maelezo zaidi

Wasiliana na Dr kiboko 0679923297

Maagizo 10 Aliyopewa Mkuu wa Mpya wa Jeshi laagereza na Rais Magufuli

$
0
0


Rais  Dk. John Magufuli, amempa maagizo 10 Kamishna Jenerali mpya wa Magereza, Phaustine Kasike, huku akimwonya kuwa asipochukua hatua atamchukia.

Maagizo hayo aliyatoa jana Ikulu, Dar es Salaam, wakati akiwaapisha Kamishna Jenerali Kasike na Balozi Joseph Sokoine ambaye anakuwa Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira.

Kamishna Jenerali Kasike ametakiwa kushughulikia promosheni za askari wa jeshi hilo, kuhakikisha mashine ya ukaguzi inafungwa, wafungwa wanajilisha wenyewe, wanafanya kazi ikiwamo ujenzi, kufanya ufugaji na kujenga nyumba za askari.

Pia alimtaka kuhakikisha mfungwa hafanyi mambo asiyotakiwa kama simu, bangi, kujamiiana lakini pia mfungwa kuhukumiwa kisha anakutwa na hatia nje ya gereza.

Akifafanua agizo moja baada ya jingine, Rais Dk. Magufuli ambaye alianza kwa kutoa pole nyingi kwa Kamishna Jenerali Kasike kuliko pongezi, alisema askari wako nyuma katika kupandishwa vyeo.

“Naanza kwa kukupongeza na kukupa pole. Mategemeo yangu nataka yakawe makubwa ya kuleta mabadiliko magerezani. Sio siri Jeshi la Magereza na maaskari wenyewe wamekaa kama wameachwa hivi, hata katika promosheni zao imekuwa ni tatizo.

“Wakati nampromoti Kamishna Jenerali aliyestaafu, palikuwa na makamishna wawili tu, si kwamba hawana sifa, waliachwa aidha kwa makusudi au kuhofia waliojuu,” alisema Rais Magufuli.

Alisema hadi Kamishna Kasike anashika kijiti hicho mtangulizi wake alikuwa ameanza kutekeleza agizo la Rais na kufanikiwa kuwapandisha Makamishna na Manaibu Kamishna zaidi ya 10, hivyo aendeleze hilo hadi kwa askari wa chini waliokaa muda mrefu.

Mbali na hilo, Rais Dk. Magufuli alirudia kauli yake aliyopata kuizungumza siku za nyuma kwamba ni jambo la aibu kwa nchi kulisha wafungwa kwa kuwa mashamba yapo.

Alisema wafungwa wanapaswa kufanya kazi na si kuomba msaada wa tofali wala chakula.

“Maeneo ya Magereza ni mengi, ukienda Mbeya eneo linalolimwa ni robo tu. Kila mwaka kuna maombi ya bajeti kulisha wafungwa, kufungwa maana yake ni ukamenyeke kwa kazi,” alisema Rais Magufuli.

Alisema si sahihi watumishi wa magereza kukosa nyumba za kuishi na kuomba fedha serikalini wakati wafungwa wanaweza kufyatua tofali na kuzichoma.

Mbali na hilo, Rais Dk. Magufuli, alisema hataki kuona mtu akipangiwa majukumu kutokana na kufahamiana na mtu fulani.

“Sitaki niyasikie yale ya Mbeya, mfungwa amehukumiwa kufungwa ni jambazi halafu baadaye anashikwa akishirikiana kuwinda tembo porini na anakamatiwa huko wakati huku amehukumiwa kufungwa, sitaki nisikie mfungwa aliyeacha familia yake kule nyumbani anakuja mke wake gerezani, anakaribishwa na askari wa magereza akafanye yule mfungwa mambo ambayo hakutakiwa kuyafanya akiwa gerezani,” alisema Rais Magufuli.

Alisema hataki kusikia wafungwa wakiwasiliana na familia au jamaa zao kupitia simu ambazo zimejaa magerezani na kusababisha kuwa kitu cha kawaida.

Katika hilo, Rais alikwenda mbali na kusema kuwa jambo hilo linafanyika hata katika magereza ya Dar es Salaam ambako wapo wanaopiga simu hadi nje ya nchi wakiwa gerezani.

“Sitaki kwenye magereza wafungwa wakapate nguvu ya kuvuta bangi na saa nyingine kujamiiana, kwa sababu hawafanyishwi kazi za kutosha. Sitaki mfungwa akafungwe, baadaye akiwa huko akaanze kufuga mbuzi na ng’ombe anapeleka hadi mnadani, anakuwa tajiri hata kuliko askari. Nina mifano ya kila gereza,” alisema Rais Magufuli.

Akisisitiza Rais Magufuli alisema: “Nakupongeza kidogo, pole ndio nyingi. Najua wapo maaskari watakaochukia kwa hatua utakazochukua na usipozichukua mimi utanichukia, nataka magereza ikafanye kazi askari wafaidike.”

Rais Magufuli pia alisema haoni sababu ya Jeshi la Magereza kukosa vitendea kazi kama trekta wakati Jeshi la Kujenga Taifa liliwahi kukopesha vitu hivyo.

Changamoto nyingine aliyotakiwa kuishughulikia ni fedha alizotoa kiasi cha takribani Sh bilioni 10 ili kukamilisha ujenzi wa nyumba za maaskari katika eneo ya Ukonga ambazo hazijakamilika.

“Kama malori yamepungua, nitayatoa mengine yaliyokuwa ya polisi, nitawapa ninyi. Serikali ni moja, fedha ni za wananchi, kaeni mjadili namna mtakavyogawana. Ni wizara moja. Nataka Jeshi la Magereza likawe mfano,” alisema Rais Magufuli.

Alimtaka Kamishna huyo kupanga vizuri safu yake ikiwamo kushirikiana na makamishna wenzake katika kufanya kazi ili kupata mwelekeo.

“Kuna watu wana rekodi nzuri, mfano Mwakijungu alipelekwa Makete kila mtu alikuwa akipakataa, akapelekwa Iringa akafanya vizuri, mtu wa operesheni kama huyo mnampeleka akawe store keeper? (mtunza stoo), sina hakika kama wamepangwa vizuri. Sikufundishi kazi,” alisema Rais Magufuli.

Ili kukabiliana na tatizo la kupitisha simu kwa wafungwa, Rais Magufuli alishauri kifungwe kifaa cha utambuzi ili kuwabaini wahusika.

Zaidi alimtaka Kamishna huyo kutembelea magereza pamoja na kukutana na majeshi mengine nchini ili kupata mikakati ya kujiimarisha.

Awali Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola, ambaye alianza kwa kumwamkia Rais Magufuli kwa kusema; “Shikamoo Mheshimiwa Rais,” alisema mambo ambayo alimwagiza wakati akimwapisha alikwishaanza kuyafanyia kazi likiwamo suala la ajali za barabarani pamoja na mikataba.

Alisema baada ya kuingia kuongoza Wizara hiyo aliitisha mkutano na wakuu wa vyombo vilivyo chini yake kujitafakari huku akitoa siku 21 kila chombo kuwasilisha kwake taarifa ya mwelekeo.

“Zimebaki siku saba, hakika tutachukuwa hatua bila kutazama usoni,” alisema Lugola.

Alisema kwa sasa wanaelekea kufanya mikakati ya maandalizi ya uchaguzi wa Serikali za Mitaa ambao utafanyika mwakani ili kuweka hali ya utulivu na usalama.

Naye Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais, Mazingira na Muungano, January Makamba, akizungumza katika hafla hiyo alisema walipata maelekezo ya Rais kuhusu ucheleweshaji wa vyeti vya tathmini ya athari kwa mazingira kwenye ujenzi wa viwanda.

“Wiki mbili zijazo nitasaini kanuni mpya za kufanya tathmini ya athari kwa mazingira ambazo zitawezesha ndani ya siku tatu tangu mtu atakapoleta ombi la kujenga kiwanda tutakuwa tumetazama na tutatoa ruhusa ya awali ili aanze kujenga halafu mchakato mwingine uendelee,” alisema January.

Gabo atwaa Tuzo nyingine

$
0
0

Muigizaji nguli wa filamu Tanzania Gabo Zigamba ametunukiwa tuzo ya ushindi katika kipengele cha muigizaji bora wa kiume kupitia filamu aliyoigiza ya ‘SUMU’ kwenye tamasha la ZIFF lililofanyika visiwani Zanzibar.

Akizungumza na www.eatv.tv, Gabo ameweka wazi juu ya hatua zinazofanyika mpaka yeye kushinda tuzo hiyo licha ya filamu kuwa haijaangaliwa na watazamaji wengi na kusema hilo ni jambo la kawaida kufanyika kwa majaji duniani kote kupitisha filamu ambayo haijatazamwa na mashabiki.

"Tuzo zilivyo duniani zipo za aina mbili, zile za ‘Choice Awards’ kwa maana ya tuzo zinazopatikana kwa Kura za mashabiki kwa filamu walizoziona, na kuna tuzo zinazotolewa kwa kufanyiwa ‘judgement’ na watengenezaji filamu ambazo huchujwa hata kabla watazamaji hawajaziona kwa mara ya kwanza kwenye ‘Movie Premiers’. Mfumo huo hutumika duniani kote na ndio tuzo yenye hela sana na kubwa duniani ukiachana na tuzo zinazopatikana kwa kura za mashabiki, sababu kura wanazopiga mashabiki ni kipimo cha kujua watu wanakupenda kias gani", amesema Gabo.

Hii ni tuzo ya pili kwa muigizaji Gabo kutunukiwa katika rekodi za utolewaji wa tuzo za ZIFF ikiwemo tuzo ya muigizaji bora wa kiume kupitia filamu ya ‘SAFARI YA GWALU’ aliyoshinda mwaka 2016.

Hata hivyo mshindi mwingine katika tamasha hilo kutoka Tanzania ni muigizaji Catherine Credo mwenye umri wa miaka 21, ambaye amefanikiwa kutwaa tuzo ya muigizaji bora wa kike kupitia filamu ya Fatuma.

Rais Magufuli atengua uteuzi wa Mkuu wa Wilaya ya Kahama

$
0
0
Kuanzia leo July 15, 2018 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli ametengua uteuzi wa Mkuu wa Wilaya ya Kahama Mkoani Shinyanga Fadhili Nkurlu kuanzia.

Kufuatia hatua hiyo, Rais Magufuli amemteua Anamringi Macha kuwa Mkuu wa Wilaya ya Kahama.
Anamringi Macha ametakiwa kuripoti katika kituo chake cha kazi mara moja.

Hii ni Habari Njema Kwa Wale Wote Waliohangaika na Matatizo ya Magonjwa Sugu Yaliyokosa Tiba

$
0
0

"HII NI HABARI NJEMA KWA WALE WOTE WALIOHANGAIKA NA MATATIZO YA MAGONJWA SUGU NA YALIYOKOSA TIBA" sasa usikate tamaa tiba imepatikanika kwa DK. ABDALA MUSSA anatibu matatizo kama yafuatayo:

Nguvu za kiume, uzazi, kisukari, tezi dume, vidoda vya tumbo, mgongo kuuma, miguu kuwaka moto na mataizo uliyonayo

1/ITAGULA- ni dawa ya mkosi kuosha nyota, kumvuta mpenzi, mke, mume, kuua kesi na kupata kazi haraka kama umeomba maombi serikalini au kampuni binafisi unaitwa ndani ya siku mbili 2/

NINJIWE- ni dawa inayomaliza matatizo ya wanaume heshima ndani ya ndoa, kuwa na nguvu za kiume milele na kukomaza mbegu na kuwa na uwezo kufanya tendo la ndoa zaidi ya mara 5 bila kuchoka kama umezaraulika na kufanya tendo na kusinyaa uume dawa ipo dozi yake siku sita vidoge 12 pia kuna na unga inayokomaza uume ndani ya siku 7 unapona kabisa.

3/MPALALA- ni dawa ya kutibu busha miguu kuwaka moto, kiuno, kisukari.

4/NGEKEWA- ni dawa ya kuvuta wateja kwenye biashara yoyote kuwa na wateja wengi katika biashara na kuzuia chuma ulete. 4/LINGWATA- ni dawa ya punguza unene, mafuta tumbo, matiti, miguu, hipsi na kutengeneza shepu dawa hii ni ya unga ukitumia utaona mabadiliko baada ya siku 3.

5/DUBISHO- ni dawa zindiko la mwili, majumba, gari, biashara, mteja wangu huduma utaipata mahali popote ulipo kuna wanasaplai mahali ulipo kama huna muda wa kufika osifini mkoa wa dar-es-salaam, iringa, kanda ya ziwa wilaya ya bunda. angalizo kwa wateja usitume sms wala kubipu huduma yangu ni kuanzia saa 12 asubui hadi saa 12 jioni kwa wateja wa dar-es-salaam ofisi ipo buguruni na mbagala zakhem na kwa wale walio nje ya mkoa dawa hizi mtazipata kwa njia za mabasi. punguzo la bei kwa wateja 5 wa kisukari na nguvu za kiume

KWA MAWASILIANAO ZAIDI WASILIANA NA DK. ABDALA MUSSA KWA SIM NAMBA 0767-171773/ 0716-608959 WOTE MNAKARIBISHWA:

Asilimia 66 ya Wanaume wakubali kuachia wake zao waolewe na Dangote

$
0
0
Stori kuhusiana ishu ya Tajiri namba moja Afrika Aliko Dangote kutangaza kuwa yupo single na akitokea Mwanamke yupo tayari kumuoa zinaendele kushika headlines ambapo asilimia 66 ya wanaume wamekubali kuachia wake zao waolewe na Dangote iwapo tu wataingiziwa fedha katika akaunti zao.

Wanaume hao walipiga kura katika swali lililoulizwa katika akaunti ya Twitter iwapo wako tayari uwaachia wachumba zao ikiwa Dangote ataingiza Mamilioni ya fedha ili aoe wachumba zao.

Katika kura hiyo asilimia 34 ya wanaume walisema hapana hawatakubali kupokea fedha hizo kwani fedha sio kila kitu katika mapenzi.

Juzi iliripotiwa kuwa Wanawake zaidi 800 wakiwamo wa hapa nchini wametuma maombi ya kutaka kuolewa na tajiri huyo.

PICHA: Mtazame Rais Mstaafu Jakaya Kikwete Akiwa Shambani Kwake Kijijini Msoga

$
0
0

Rais Mstaafu Dkt Jakaya Kikwete akikagua shamba lake la majaribio ya kilimo cha mapapai kijijini kwake Msoga, Pwani. 

Bwege: Katika kiongozi ambaye mimi nina mpenda ni Rais Magufuli

$
0
0

Mbunge wa jimbo la Kilwa Kusini (CUF), Selemani Bungara maarufu kama 'Bwege' amefunguka na kudai katika viongozi ambao anawapenda katika nchi hii ni Rais Dkt. John Magufuli huku akimuomba asimamie haki za wananchi kwani akifanya hivyo ataweza kushinda hata miaka 100. 

Bwege ametoa kauli hiyo wakati akizungumza kwenye kipindi cha KIKAANGONI  kinachorushwa mubashara kwenye ukurasa wa facebook wa EATV kila siku ya Jumatano kuanzia saa nane mchana hadi saa 10 alasiri na kusema hilo ndio jambo kubwa ambalo alitaka kulisema ili kusudi liweze kumfikia Rais Magufuli kwa kuwa ameweza kurejesha heshima katika baadhi ya maeneo ambayo hapo awali yalikuwa ya hovyo. 

"Katika kiongozi ambaye mimi nina mpenda ni Rais Magufuli maana ameweza kurejesha nidhamu katika ofisi za Utumishi wa Umma. Hilo amefanikiwa sana lakini bado naendelea kumuomba sana asimamie utawala wa sheria. Watanzania wote wanamuamini Dkt. Magufuli yeye ni kichwa", amesema Bwege. 

Pamoja na hayo, Bwege ameendelea kwa kusema "akifanya hivyo tu ataendelea kushinda hata miaka 100, lakini yote mazuri ambayo ameyafanya kama hatosimamia haki za wananchi hali haitokuwa nzuri". 

Itakavyokuwa kama Croatia wataifunga Ufaransa leo…

$
0
0

1 min ago Comments Off on Itakavyokuwa kama Croatia wataifunga Ufaransa leo…

‘Leo ni leo’, utakaposhuhudiwa mtanange mkubwa zaidi kwenye maisha ya soka duniani kwa mwaka 2018, pale Croatia itakapominyana na Ufaransa kuwa bingwa wa Kombe la Dunia mwaka huu kutokea uwanja wa Luzhniki jijini Moscow,  nchini Ufaransa.

Ingawa Ufaransa ni kisu kikali kinachokata kote, ni kosa la karne kuwachukulia poa Croatia ambao wameshaonesha maajabu katika njia finyu walizopitia kwa kasi.

Tunaitaja zaidi Croatia kwani wao ni mara yao ya kwanza kufikia katika hatua hii kwenye historia ya Fainali za Kombe la Dunia, ingawa awali iliwahi kushiriki mara nne (1998, 2002, 2006 na 2014). Ilizaliwa baada ya kujitenga na Yugoslavia mwaka 1991.

Tofauti na wepinzani wao Ufaransa ambao wamewahi kushinda kombe hilo mara moja huku ikiwa mara yao ya tatu kucheza fainali, kati ya mara sita ilizowahi kushiriki.

Hivyo, endapo Croatia itashinda leo, itaweka historia ya kushinda kombe hilo kwa mara ya kwanza.

Pia, kocha wa kikosi hicho, Zlatko Dalic atakuwa ameweka historia ya mafanikio akikinoa kikosi hicho kwa muda mfupi, miezi tisa tu akichukua kijiti kutoka kwa mtangulizi wake. Dalic alianza kukinoa kikosi hicho Oktoba 7, 2017, baada ya Shirikisho la Soka la Croatia kumtimua Ante Cacic.


Kocha Dalic atakoreza wino wa rekodi itakayobaki kwenye historia ya vitabu vya soka, kwa uamuzi wake wa kumrejesha nyumbani mshambuaji nyota na tegemezi, Nikola Kalinić wakati timu hiyo ikiingia kwenye mzunguko wa 16 bora, baada ya mchezaji huyo kuonesha ukaidi na visingizio akikataa kucheza dakika za mwisho za mechi dhidi ya Nigeri

Hivyo, itakuwa Dalic amechukua uamuzi kama meneja na kufanikisha bila Nikola Kalinić, ingawa hata akiishia nafasi ya pili sifa hiyo itabaki. Nikola Kalinić anatajwa kugoma kwa visingizio vilevile wakati wa mechi ya kirafiki dhidi ya Brazil na pia katika nyakati tofauti mazoezini.

Kadhalika, Croatia itaweka historia ya kuwa timu ya pili kushinda kombe la dunia ikiwa na idadi ndogo zaidi ya watu (Milioni 4.17). Idadi hiyo inakaribiana na wakaazi wa Jiji la Dar es Salaam, ambao ni Milioni 4.4 kwa mujibu wa Sensa ya Watu na Makazi ya mwaka 2012.

Nchi itakayoendelea kuwa na historia ya kushinda kombe la dunia ikiwa na idadi ndogo zaidi ya watu ni Uruguay ambayo ilishinda kombe hilo ikiwa na watu takribani milioni 1.7 tu.

Lakini kwa upande wa Ufaransa, ushindi wa leo utaikata kiu ya miaka 20 ya kusubiri kutwaa tena kombe hili, tangu ilipoivuruga Brazil 3-0 mwaka 1998, Ufaransa wakiwa wenyeji.

Hii ni fainali ya tatu kwa Ufaransa, mwaka 1998, 2006 na leo.

Kylian Mbappé anapewa nafasi zaidi ya kung’ara kwenye mashindano haya, kwa kuzingatia kuwa wale mafahari watatu Lionel Messi, Cristiano Ronaldo na Neymar Jr. walishatupwa nje ya mashindano

Said Fella aanika mshahara anaolipwa na Diamond

$
0
0

Meneja nguli wa muziki wa kizazi kipya ambaye hivi sasa anasimamia biashara ya muziki wa Diamond Platnumz, Said Fella ameweka wazi kiasi cha mshahara anaolipwa na Bosi huyo wa WCB, kwa asilimia.

Fella ambaye pia ni diwani, amesema kuwa hupokea asilimia 30 ya pato lote lililoingia kutokana na muziki wa Diamond kila mwezi bila kujali mamilioni yatakayokuwa yamepatikana.

“Mshahara wangu ni asilimia 30 ya pato la kila mwezi analoingiza Diamond kwa muziki wake. Haijalishi ameingiza shilingi ngapi, hata kama ni milioni 800,” alisema Fella.

Akizungumzia hatua ya mameneja wa Diamond kuanza kuweka wazi mishahara wanayolipwa, alisema kuwa hii inatokana na kufuata sera ya Rais John Magufuli ya kuwa wazi.

“Mheshimiwa Rais Magufuli sasa hivi amesema ni lazima tuwe wazi. Kama unachosema unacho, kama hauna sema hauna. Usilazimishe kuwa hauna useme unacho au unacho useme hauna. Kwahiyo, naona kuweka wazi inakuwa sawa kwasababu mwisho wa siku hata yule mtu anayedhani kuwa uko pale afahamu kuwa sio hivyo uko hapa,” aliongeza.

Mkubwa Fella ana historia kubwa kwenye muziki wa kizazi kipya, akiwa ndiye meneja wa kwanza wa Juma Nature aliyesaidia mafanikio makubwa ya kimuziki katika safari ya mwimbaji huyo.


Fella anaendelea kushika historia ya kuyapa mafanikio makubwa makundi ya Wanaume Family, Yamoto Band na mengine huku akiwaibua na kuwaweka kwenye kilele cha muziki wasanii tangu wakiwa na umri mdogo kama ilivyokuwa kwa Aslay.

Tunatibu Na Kuponesha Kabisa Upugufu wa Nguvu za Kiume, Busha, Kisukari na Vidonda vya Tumbo

$
0
0

TUNATIBU NA KUPONESHA KABISA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME UUME MDOGO? BUSHA BILA KUPASUA KISUKALI NA VIDONDA VYA TUMBO? asilimia kubwa ya wanaume wanaupungufu wa nguvu za kiume NA maumbile madogo NI NINI KINACHOSABABISHA UUME KUZIDI KUWA MDOGO NA WEMBAMBA 1 kuugua chango LA uzazi 2 unene kupita kiasi 3 kuvaa nguo au chupi za kubana 4 kupiga punyeto kwa mda mrfu ,NI NINI TIBA YAKE MAKAKANUA MIX nidawa ya mitishamba iliyochanganywa NA mizizi kumi NA mbili urfusha NA kunenepesha UUME saizi upendayo ich 5,6,7, NA 8 kwa urfu NA sentimita 3,4, na 5 ipo dawa ya kunywa na kupaka NI NINI KINASABABISHA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME 1 kupungukiwa kwa homoni ya testerone 2 kuhudhurika kwa Neva au uti wa mgongo 3 utumiaji holela wa madawa ya kizungu 4 usongo wa mawazo na asira 5 utumiaji wa vyakula vya mafuta mengi NI NINI TIBA YAKE MAPRO POWER NO 2 NDIO tiba tosha kwa sasa kwani utibu matatizo matatu kwa pamoja 1 itakufanya uchelewe kufika kileleni dk 15 adi 20 ,2 itakufanya urudie tendo zaidi Mara tatu 3 uhimalisha uume uliolegea na kusinyaa OKOA NDOA YAKO SASA ujihepusha na lawama ndani ya ndoa yako au pale ukutanapo na mpezi dawa hii itamfanya mpenzi wako hakueshimu na hasitoke nnje ya ndoa na ata wazee wenye umri mkubwa wanapona zipo dawa za kupunguza kitambi,minyama uzembe, presha ,kisukar mvuto wa mpezi au biashara FIKA OFISINI KWETU MBAGALA ZAKHEMU na wateja wa kanda ya ziwa yupo wakala wetu mwanza mjini au piga simu 0752348593

DR MABULA na utaletewa popote ulipo uduma hizi

Kiongozi wa Mbio za Mwenge akataa kuzindua mradi wa Kituo cha Afya Ikwiriri

$
0
0

KIONGOZI wa mbio za mwenge mwaka huu, Charles Kabeho ,amekataa kuzindua mradi wa upanuzi wa kituo cha afya cha Ikwiriri wilaya ya Rufiji mkoa wa Pwani. 

Hali hiyo imezua sintofahamu mara baada ya kusomwa ripoti ya matumizi ya fedha ambazo hazijaeleweka zimetumikaje huku serikali ikiwa imechangia kiasi cha sh.milioni 400. 

Aidha kwa mujibu wa taarifa ya wilaya imedaiwa wananchi wamechangia milioni tatu wakati taarifa ya mkoa inaonyesha ilichangia milioni moja.Akizungumza kwenye kituo hicho cha afya, Kabeho alishtushwa na kuhoji kutokea kwa hali hiyo. 

Alimtaka mkuu wa wilaya atoe kauli yake na kukataa kuuzindua mradi mpaka watakapotoa taarifa ya uhakika.Kabeho aliasa halmashauri na wilaya mbalimbali ,kusimamia miradi ya maendeleo ili iendane na thamani halisi ya fedha . 

Nae mkuu wa wilaya ya Rufiji,Juma Njwayo aliviagiza vyombo vya ulinzi na usalama hususani taasisi ya kupambana na rushwa (TAKUKURU) kufuatilia suala hilo.Kati ya miradi tisa ambayo ilipaswa kukaguliwa,kuwekwa jiwe la msingi na kuzinduliwa wilayani Rufiji ,iliyogharimu bilioni 2.654.40 mradi huo mmoja ulikwama kuzinduliwa . 

July 13 mwenge huo ulikuwa Rufiji na July 14 umetembelea miradi ya maendeleo katika wilaya ya Kibiti. 

Mtibwa Sugar yafunguka baada ya Simba kumchukua Hassan Dilunga

$
0
0

Baada ya kuondokewa na wachezaji wake tegemeo, uongozi wa klabu ya mtibwa Sugar umefunguka na kueleza kuwa sasa watakiboresha upya kikosi chao kwa kuwatumia vijana walionao. 

Kupitia Msemaji wa timu hiyo, Thobias Kifaru, amesema kuwa wao ni chuo cha soka hivyo  hawana wasiwasi wowote juu ya kuondoka kwa wachezaji wao wawili kuelekea klabu kongwe za Kariakoo. 

Kifaru ameeleza Mtibwa itawapasa kuandaa vijana wengine kama ilivyo sera yao ya kuwafua vijana na baadaye wanaimarika kisha kufanua vizuri kama ilivyokuwa kwa Shiza Kichuya, Mohammed Ibrahim na wengineo. 

"Tutatumia vijana tulionao kutokana na utamaduni wetu wa kuwafua vijana ambao huwa wanakuja kuwa na vipaji vizuri, kuondoka kwa Dilunga na Banka kwetu wala haitupi shida kubwa" alisema. 

Mtibwa imeondokewa na wachezaji Mohammed Issa Banka pamoja na Hassan Dilunga ambao wote wanacheza nafasi ya kiungo. 

Banka amefanikiwa kunaswa na Yanga na kusainishwa mkataba wa miaka miwili pia Dilunga akitia kandarasi ya miaka miwili na Simba. 

Huna Sababu ya Kuaibika Tena, Jipatie Dawa Bora ya Tatizo la Nguvu za Kiume na Maumbile Madogo

$
0
0

HUNA SABABU YA KUAIBIKA TENA........ JIPATIE DAWA BORA YA TATIZO LA NGUVU ZA KIUME NA MAUMBILE MADOGO

Matatizo ya nguvu za kiume yamekua yakiathiri watu wengi sana kisaikologia hasa baada ya kujiona wakotofauti sana na wengine, kawaida mwanaume anatakiwa awe na uume kuanzia nchi (6-8) vinginevyo mtuhuyo anamatatizo. 

Zipo sababu nyingi zinazosababisha tatizo hili, chango :- hushambulia never ambayo huasili misuli ya uume, Ngiri :- hii huleta maumivu ya tumbo chini ya kitovu na kufanya tumbo kuunguluma na kujaa gesi, kolodani moja kuvimba au kuingia ndani pamoja na kutopata choo vizuli Sababuhizi na nyingine hufanya uume kulegea na kusinyaa na kuwa mfupi na mwembamba namarakwamara husababisha kukosa hamu ya kuludia tendo la ndoa na baadae kukosa kabisa 

MIFINI:- Nidawa ya vidonge iliyotengenezwa kwa mitishamba, huongeza nguvu za kiume maradufu kuanzia umri wa miaka (15-80) inakomaza mbegu zisizo na viini vya uzazi (manii) ,inaimalisha mishipa iliyolegea wakati wa tendo la ndoa, itakufanya uwe na hamu ya kuludia tendo la ndoa zaidi ya maratatu bilahamu kuisha wara kuhisi kuchoka na itakufanya uchelewe kufika kilelen Kwa mda wa dk (18-25). 

SUPER MORISIS :- hurefusha na kunenepesha maumbile madogo ya uume uliosinyaa inchi 6-8 na unene wa sm 3-4 kwamda mfupi sana , ni Dr CHILAMBO mtatuzi wa matatizo yako kunadawa ya kupunguza unene, kitambi (nyamazembe),matiti makubwa kuwa madogo, uzazi, kuludisha mali iliyopotea, kuuzavitu bila kununuliwa, biashara, wachimba madini kusafisha nyota, kuludishwa kazini mvuto wa mapenzi nk. 

KWAUSHAURI NA TIBA WASILIANA NA DR CHILAMBO ATAKUSAIDIA MATATIZO YAKO, NIPO DAR ES SALAAM PIA HUDUMAHII ITAKUFIKIA POPOTE ULIPO NYOTE MNAKARIBISHWA. 

0744 391 089 / 0622344969

Walichokubaliana Waziri Mwakyembe na Wasanii juu ya Tozo ya Milioni

$
0
0

Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dkt. Harrison Mwakyembe amezungumza na wadau wa sanaa wakiwemo wasanii wa muziki kujadili kuhusu tozo ambayo imeanzishwa na Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA).

Waziri Mwakyembe amewataka wasanii wachache pamoja na wadau wa sanaa wakae na BASATA kujadili namna kubadili huo mfumo.

Njia za Kushinda Hofu Pale Unapozungumza Mbele za Watu

$
0
0

Fikiria bosi wako amekupa taarifa kuwa kesho asubuhi utatoa mada kwenye mkutano wa wafanyakazi wote ofisini.

Je, ungesisimka kwa kupata fursa hii adhimu au ungejawa na wasiwasi?

Kwa wengi wetu, inawezekana kabisa usingizi ukapaa usiku. Wazo kwamba utazungumza mbele ya watu muhimu wenye uelewa mkubwa kuliko wewe linaweza kukunyima amani.

Ukweli ni kwamba watu wengi, kwa viwango tofauti, hupata wasiwasi wanapokaribishwa kuzungumza mbele ya watu.

Hata watu wanaoonekana jasiri huweza kutokwa na jasho wanapojiandaa kuzungumza mbele ya watu.

Lakini pia ni kweli kuwa, kama mfanyakazi, wakati mwingine utalazimika kusimama mbele ya watu kuzungumza.

Inaweza kuwa kutangaza bidhaa au huduma, kufundisha na hata kuwasilisha andiko la mradi kwa wafadhili.

Hiyo ina maana kuwa uwezo wa kuzungumza mbele ya watu ni raslimali muhimu kwa mfanyakazi.

Ili kukuwezesha kukabiliana na hofu, hapa inapendekewza kanuni kadhaa rahisi za kukuwezesha kufanya hivyo mosi;

Siri kubwa ya kuondoa wasiwasi ni maandalizi. Jiandae kwa kujiuliza matokeo gani unataka kuyapata baada ya mazungumzo yako?

Je, una hoja zipi mbili kubwa unazotaka wasikilizaji wako waondoke nazo? Je, unataka wajisikieje na wafanye nini baada ya kukusikiliza?

Maana yake ni kwamba, kama sehemu ya maandalizi yako, unahitaji kufikiria mwisho wa mazungumzo yako utakuwaje kabla hata hujaanza kuzungumza.

Pia, unapojiandaa unahitaji kuoanisha dhima ya mazungumzo yako na mahitaji ya watu watakaokusikiliza.

Utafiti wa kujua changamoto za watu unaotarajia kuzungumza nao ili mazungumzo yako yajikite kwenye ufumbuzi wa vikwazo vinavyowakabili.

Lakini pia, mahitaji ya wasikilizaji wako yanaweza kuwa matamanio waliyonayo.

Ukiweza kujua matamanio ya watu unaotaka kuongea nao, itakuwa rahisi kuyafanya mazungumzo yako yatakayojenga hamasa ya kuwawezesha kufikia kule wanakokutamani.

Baadhi ya wahubiri, wanasiasa na waganga wa kienyeji wanaijua siri hii.

Watu hawa wana uwezo wa kutumia matamanio ya watu na kuyageuza kuwa mtaji wa shughuli zao.

Hivyo nawae tumia udhaifu huu wa kibinadamu kuyafanya mazungumzo yako yasikilizwe.

Hofu ya kuzungumza mbele ya watu inaweza kukufanya ukataka kukariri kile utakachokisema.

Kukariri maana yake ni kujaribu kukumbuka kila neno utakalolizungumza.

Mtindo huu unaweza kukuletea matatizo makubwa mawili.

Kwanza, ili usisahau utalazimika kuzungumza kwa mtiririko fulani wa bandia na hivyo wasikilizaji wako wanaweza kuhisi huamini unachokisema.

Bila shaka umewahi kuwasikiliza watu wanaozungumza mambo mazito kwa kutumia maneno mazito, lakini hujisikii kuwaamini kwa sababu wanaonekana kukariri.

Pili, unapokariri unajiweka kwenye hatari ya kusahau. Ile hofu ya kukosea inaweza kukuchanganya ukajikuta umesahau maneno fulani uliyotamani kuyatumia.

Hilo likitokea, ujasiri wako unaweza kupeperuka.

Kuna nyakati utalazimika kukumbuka maneno fulani ya muhimu. Lakini haifai kuyafanya maneno hayo kuwa msaafu, bali dira ya jumla ya kuongoza mwelekeo wa mazungumzo yako.

Nikitumia mfano wangu, binafsi ninapojiandaa kuzungumza huwa ninajitahidi kuufanya ujumbe utoke moyoni mwangu.

Hiyo ina maana kwamba, ninapojifunza jambo nitalifuatilia kwa undani wake na kulihusisha na mifano halisi niliyowahi kukutana nayo katika maisha yangu ya kila siku.

Kwa kufanya hivyo, inakuwa rahisi kuzungumza kwa ujasiri kwa sababu silazimiki kukumbuka kila neno nitakalolitumia wakati ninazungumza.

Gusa hisia za wasikilizaji

Namna unavyozungumza inaweza kuwa muhimu kuliko hata ujumbe ulionao.

Katika kufikisha ujumbe wako, swali unalohitaji kulijibu ni, namna gani unafikisha ujumbe wako? Je, unatumia mbinu gani kugusa hisia za wasikilizaji wako?

Uamuzi mwingi unaongozwa na hisia za watu. Tafiti nyingi za kisaikolojia zinaonyesha watu hawavutiwi na hoja kuliko hisia zinazozunguka hoja.

Unafahamu, kwa mfano, kuna vitu vingi tunavipinga sio kwa sababu haviko sahihi, lakini ile tu kujua kuwa vinachokoza hisia zakufanya kupinga.

Kwa hiyo, mbali na kiini cha ujumbe wa muwakilisha hoja, bado anayo kazi kubwa ya kuhakikisha anaupamba ujumbe wake kwa kuzingatia hisia za msikilizaji wake.

Namna moja wapo ya kufanya hivyo ni kutia moyo, kuleta matumaini, kuonyesha inawezekana.

Utakubaliana na mimi kuwa mtu akizungumza na wewe akakufanya uone haiwezekani, hakuna tumaini, itakuwa vigumu kwako kumpa nafasi kubwa ya kukushawishi.

Ni hivyo kwa sababu tunapenda watu wenye ujumbe wenye faraja na matumaini kuliko wale wanaotukatisha tamaa.

Ukitaka kusikilizwa na watu tembea kwenye udhaifu wa watu kupenda kusikia mambo yanayotia moyo si kukatisha tamaa.

Boresha uwasilishaji wako

Mtindo wa uwasilishaji wako unaweza kuathiri ubora wa mazungumzo yako.

Kumbuka kutumia nyenzo zitakazofanya ujumbe wako ufikike kirahisi mfano picha, vielelezo, vitu halisi pamoja na simulizi halisi.

Siku hizi kuna matumizi ya teknolojia kama ‘slides za powerpoint’ kuweka dondoo za ujumbe wako. Vyote hivi vinafahisisha uwasilishaji wako.

Siku ya kuzungumza, jitahidi kuanza vizuri. Namna unavyofungua mazungumzo yako itaamua kwa kiwango gani wasikilizaji wako watakuchukulia kwa uzito unaostahili.

Dakika za mwanzo, zitumie kuvuta usikivu wa hadhira yako.

Ukitumia dakika za mwanzo vibaya, unajiweka kwenye hatari ya kupoteza asilimia zaidi ya 50 ya wasikilizaji wako.

Mahali pa kuanzia ni kubainisha tatizo liko wapi na kisha taratibu waonyeshe ufumbuzi.

Mazungumzo yasiyoeleweka yanatatua shida gani hayawezi kupata usikivu.

Ungana na wasikilizaji wako kwa kutumia vichekesho vinavyoendana na mahitaji yao.

Lugha ya mwili iende sambamba na maneno unayotamka.

Kama unazungumzia jambo lenye huzuni, onekana kweli una huzuni.

Pia, usiwe na papara hata kama unakimbizana na muda. Zungumza taratibu kwa ufasaha.

Unapozungumza taratibu, unajipa muda wa kutafakari kabla hujasema na hiyo itakuongezea ujasiri.

Ikiwa unasikia hofu wakati unazungumza, unaweza kuvuta pumzi kubwa ya taratibu, kuruhusu hewa iingie tumboni. Ishikilie kwa muda kwa kutumia misuli ya tumbo, kisha zungumza wakati ukipumua hewa hiyo taratibu.

Pumzi kubwa husaidia kupunguza wasiwasi.

Christian Bwaya ni Mhadhiri wa Saikolojia, Chuo Kikuu cha Kikatoliki Mwenge (MWECAU).

Tanzanite yaendelea kutoroshwa licha ya ukuta kujengwa

$
0
0

Tume ya Madini inayoongozwa na Mwenyekiti Profesa Idris Kikula imesema imebaini kuendelea kwa vitendo vya  utoroshaji wa madini ya Tanzanite katika mgodi wa Mererani licha ya kukamilika kwa ujenzi wa ukuta mkubwa ulioligharimu taifa kiasi kikubwa cha fedha . 

Akitoa taarifa ya ziara ya Tume hiyo  katika migodi ya madini iliyopo mikoa ya Manyara, aliyeambatana na Kamishna wa Tume  Profesa Abdulkarim Mruma na Mwanasheria wa Tume , anasema utoroshaji huo wa madini unachangiwa na mfumo duni wa ulinzi katika lango kuu. 

Ni kutokana na upotevu huo wa madini ambao Profesa Kikula anasema umesababisha kushuka kwa mrahaba uliokuwa ukipokelewa na serikali ambao ulikuwa umepanda kwa kasi mara  baada tu  ya ukuta kukamilika ,tume ikatoa maelekezo yake. 

Tume hiyo imesisitiza pia umuhimu wa wawekezaji kutii na kufuata kanuni na maelekezo yote ya leseni wanazopewa likiwemo suala la mahusiano na  uongozi wa serikali kuanzia ngazi za vijiji na jamii inayoishi jirani ikishauri kuigwa kwa mfano wa mwekezaji wa mgodi wa madini ya Rubi wa Mundarara  uliopo wilayani Longido.
Viewing all 104799 articles
Browse latest View live




Latest Images