Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104809 articles
Browse latest View live

Rais Magufuli atangaza neema kwa wafanyabishara wa Mbezi Jijini Dar es Salaam

$
0
0

Rais Dkt. John Magufuli ametangaza neema kwa wafanyabiashara wadogo wadogo wa eneo la Mbezi Jijini Dar es Salaam kuendelea kufanya biashara zao pembezoni mwa barabara huku akizitaka mamlaka husika zisiwanyanyase wafanyabiashara hao wanaotafuta kipato . 


Dkt. Magufuli ameeleza hayo jana Julai 16, 2018 wakati akiwa njiani kuelekea Ikulu akiwa anatokea Mkoa wa Pwani, Kibaha kuweka jiwe la msingi la Chuo cha Uongozi cha Julius Nyerere na kusema wafanyabiashara hawawezi kunyanyaswa katika kipindi chake ambacho atakuwa madarakani huku akiwataka wafanyabiashara hao nao pia kuacha tabia ya kuinyanyasa serikali.


"Biashara haifanywi porini, biashara inafanywa mahali pa watu. Kama mnaviongozi wenu mkae nao na muambizane msisogee barabarani kufanya biashara zenu, kwasababu kwa amri hii niliyoitoa ikitokea watu wakafa kesho kwa kugongwa na gari watasema Magufuli aliamrisha watu wagongwe, maana nitakuwa nina deni kubwa la kulipa kwa Mwenyezi Mungu", amesema Rais Magufuli.


Pamoja na hayo, Magufuli ameendelea kwa kusema "sitaki nikalipe hiyo dhambi kwa hiyo nawaomba sana ndugu zangu wa Mbezi na TANROADS wameshanisikia. 


"Kuanzia leo wasiwanyanyase watu wa pembeni lakini na nyinyi msifanyie biashara barabarani maana TANROADS watawashika na Jeshi la Polisi litashughulika. Kama kuna wafanyabiashara wowote wameshikiliwa bidhaa zao warudishiwe".


Kwa upande mwingine, Rais Magufuli amemtaka Mkuu wa Wilaya ya Ubungo na Mkurugenzi kutenga eneo kwaajili ya wafanyabiashara hao waliopo katika eneo la Mbezi mwisho jijini Dar es Salaam ili kusudi wawe na eneo maalum la kufanyia kazi zao.

Watu Sita Watiwa mbaroni kwa uchochezi Tarime

$
0
0

Watu sita wanashikiliwa na Jeshi la Polisi kituo cha Sirari wilayani hapa Mkoa wa Mara kwa tuhuma za kula njama ya kuanzisha mapigano baina ya koo mbili za Wakira na Wanyabasi katika vijiji vya Kebweye na Kyoruba.


Akizungumza leo Jumatatu Julai 16, 2018 Kamanda wa polisi Tarime/Rorya,  Henry Mwaibambe amesema watu hao walikamatwa kwa tuhuma za uchochezi wa koo wakigombea mipaka ya vijiji hivyo.


Amesema walipanga kuanzisha vurugu lakini polisi walipata taarifa na kufanikiwa kuizima.


Mwenyekiti wa kijiji cha Kebweye, Marwa Nyasoko amesema vurugu hizo ziliibuka Julai 13, 2018 baada ya wananchi wa kijiji cha Kyoruba kuvamia miji iliyopo mpakani na kuchoma nyumba moto.


"Saa tatu usiku walivamia miji mitatu ya mpakani wakachoma nyumba mbili za nyasi na kukatakata bati zilizokuwa zimeezeka nyumba moja lakini polisi wakawa wamefika na kuwatawanya,” amesema  Nyasoko.

Majaliwa amuagiza RPC Shinyanga kukamata viongozi tisa

$
0
0

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amemwagiza Kamanda wa Polisi Mkoa wa Shinyanga, Simon Haule awakamate viongozi wa Chama cha Msingi cha Mkombozi kwa upotevu wa dola za Kimarekani elfu 21 za chama hicho sawa na takribani milioni 47.8 za kitanzania. 

Waziri Mkuu ametoa agizo hilo leo Julai 16, 2018 wakati akizungumza na mamia ya wananchi wa kijiji cha Kangeme, kata ya Ulowa katika Halmashauri ya Ushetu wilayani Kahama ambapo alienda kuzindua mpango wa Ushirika Afya na 
NHIF. 

"Wabebe hawa watu, wahoji waseme hiyo fedha iko wapi na jambo la kwanza wailete hiyo fedha ya wakulima. wakishindwa kurejesha fedha, wawekwe ndani",amesema Majaliwa. 

Waziri Mkuu amefikia uamuzi huo baada ya kuwaita viongozi wa chama cha Mkombozi watoke hadharani na kubaini kuwa hakuwepo hata mmoja. huku ikidaiwa kwamba walitoroka baada ya wananchi kuanza kuzomea. 

Kwa upande wake, Kamanda Haule amewataja watuhumiwa hao kuwa ni Mwenyekiti, Bw. Shilinde Abdallah na mhasibu wa AMCOS hiyo, Bw. Kulwa Shinzi pamoja na wajumbe saba wa bodi ya chama hicho.

Pasta wa Kanisa Amshukuru Mkewe Kwa Kumpa Vizuri Mambo Kitandani

$
0
0

Wauton Knight, mhubiri maarufu kutoka taifa la Nigeria alizua joto na ucheshi mitandaoni alipotoa ujumbe wake wa kimapenzi katika kusherehekea siku yake ya kuzaliwa.

Pasta huyo aliamua kumsifu mkewe kwa weledi wake wa kusakata ngoma ya kitandani kati ya mambo mengi humfanyia, katika mtandao wa kijamii.

Kupitia kwa mtandao wa Facebook, Knight alifichua kuwa mkewe ni wa maana sana kwa jinsi humshughulikia kila upande.

Moja wapo ya hulka za mkewe ni pamoja na kuwa mwanamke asiyemnyika haki ya ndoa hata siku moja tangu waoane.

"Mwanamke ambaye hajawahi kataa kunitimizia matakwa yangu ya kimapenzi tangu kuoana," Alisema Knight.

Kulingana na Knight, mkewe ni kama dhahabu ifaayo kutunzwa na kutuzwa.

Kupoteza World Cup 2018 hakujawafanya Croatia wasipokelewe kishujaa

$
0
0

Timu ya taifa ya Croatia baada ya kupoteza katika mchezo wa fainali ya Kombe la Dunia 2018 imewasili kwao katika mji wa Zagreb na kupokelewa na mashabiki mbalimbali wa soka wa nchi hiyo, kwani ndio mara ya kwanza kwa taifa lao kufika fainali ya World Cup.



DJ Maphorisa, Wizkid uso kwa uso na Chris Brown

$
0
0

Staa maarufu kutokea Nigeria Wizkid pamoja na Dj Maphorisa kutokea Afrika kusini wamekutana na mkali wa RnB kutokea Marekani Chris Brown hivi karibuni kitendo ambacho kimewafurahisha mashabiki na wengi kuhisi ni ujio wa kazi mpya.

Kupitia ukurasa wa instagram wa Dj Maphorisaamepost picha hiyo na mashabiki kuona  ni fursa nzuri kwa wawili hao ambayo itazidi kulitambulisha vizuri bara la Afrika katika kitengo cha muziki ikiwa wakishirikiana na kufanya collaboration.

Dj Maphorisa pamoja na Wizkid waliwahi pia kushirikiana katika ngoma ya Soweto babyambayo ilifanya vizuri ndani na nje ya bara la Afrika, picha hii inaweza pia ikawa ni dalili tosha ya kazi mpya kutoka kwa Chris Brownpamoja na Dj Maphorisa.

Mbunge azuiwa kuingia hotelini bila cheti cha Ndoa

$
0
0

Mwakilishi wa wanawake wa kaunti ya Laikipia, jimbo linalopatikana takriban 250km kaskazini mwa jiji la Nairobi, Catherine Waruguru anasema haki zake za kimsingi zilikiukwa baada ya yeye na mumewe kuzuiwa kuingia katika hoteli moja nchini humo kwa kukosa cheti cha ndoa. 

Mbunge huyo ametishia kuishtaki hoteli hiyo ya mjini Kericho, eneo la Bonde la Ufa akisema alidhalilishwa. 

Hoteli hiyo imeweka ilani kwamba mwanamume na mwanamke hawawezi kuruhusiwa katika chumba kimoja iwapo hawajaoana. 

Lakini mbunge huyo anasema wanandoa wengine waliruhusiwa kuingia bila kuitishwa cheti cha ndoa, na kwamba walifanya kila juhudi kuthibitisha kwamba walikuwa mume na mke ingawa hawakuwa na cheti cha ndoa.

Hii Hapa Dawa Bora ya Nguvu za Kiume na Maumbile Madogo ya Uume

$
0
0
Tatizo hili limekuwa likiwaadhiri watu wengi sana kisaikolojia hasa baada ya kujiona wapo tofauti sana na wengine kwa kawaida mwanaume anatakiwa awe na uume kuanzia nchi 6-8 kwanza upungufu wa vichocheo hivi huchochea ukuaji wa uume chongo ambalo hushambulia nerve ambayo uharibu kabisa ukuaji wa uume, ngiri, punyeto, ambayo huathili misuli ya uume, ngiri huleta maumivu, tumbo kuunguruma na kujaa gesi, korodani moja kuvimba, kutopata choo vizuri, sababu hizi hufanya uume kulegea na kusinyaa na kuwa mfupi na mwembamba na mara nyingi hata nguvu za kiume ( hamu ya tendo la ndoa) hupungua na kwisha kabisa

GEMBE :Ni dawa inayozalisha na kukufanya uume kukua na kuongezeka
NGEMO : Ni dawa bora ya kuongeza nguvu za kiume

Hukutia hamu ya kuludia tendo la ndoa zaidi mara4 nne bila kukinai au kuchoka pia itakufanya uchelewe kufika kileleni zaidi ya dk30-45 kwa mtumiaji pia tunatibu kisukari, bp, ngiri, miguu kuwaka moto KAMA HUNAMDA WA KUFIKA OFISINI KWETU UTALETEWA POPOTE TUPO MBAGALA RANGI TATU

 0753471612/ 0715249530
0623 386 305

DR KUZENZA

Enyi Wadada wa Mjini Maisha yamebadilika Mwenye Masikio na Asikie

$
0
0

Maisha yamebadilika, nyakati zimebadilika ela za mchezo hazipo tena kila senti inakazi ya kufanya. Enyi wadada mliozoea mizinga jifungeni Mikanda mwafwaaa. Ile ya baby naomba unitumie elfu 30 kwenye MPESA hizo zama zimepita, hyo ela ukiihitaji itabidi uje uifanyie kazi haswa, itabidi ufue, Utandike kitanda, upike na game uperform Vizuri. Maisha ya ujanja ujanja yamepita nasema na mwenye masikio asikie

Ushauri wa Bure Kwa 'Rockstar' Ali Kiba, Kaka Siku Hazigandi

$
0
0
Awali ya yote naomba nitangaze "mahaba" yangu (decralation of interest) kwa mwanamuziki nyota nchini Ali Kiba, kwamba mimi ni mshabiki wako wa kutupwa. una sauti nzuri, una kipaji cha hali ya juu, una jina Tanzania, Afika Mashariki, Afrika na duniani kote. Hiyo haina ubishi. Hivyo nisemayo hapa hayahusiani na hujuma ama ushabiki wa aina yoyote. Bali ni hasira tu. Naomba unisamehe kama nitakukwaza. Cos I feel you buddy!

Nimesukumwa kusema haya baada ya kuperuzi mtandaoni na kukuta picha yako hii Ali Kiba ukiwa na Diamond. Nikasema woow! (japo body language haisemi hivyo) na kufurahi kwamba kumbe mmeshawahi kukutana. Nilifurahi sana.

Hata hivyo, furaha yangu hiyo ikawa fupi (short lived) nikivuta kumbukumbu ya mambo kibao katika fani yenu nyie wawili (ninayoifananisha kama Yanga na Simba vile - najua Diamond ni Simba kindakindaki, hivyo bila shaka we Ali ni wa mitaa ya Twiga na Jangwani - aka Kaunda Stadium) maana mpo kama hampo vile.

Kama hizo kumbukumbu zangu haziko mbumbumbu kama nilivyo, hadi naandika haya nadhani kama ni mechi mabao ni 6-0, na Diamond ndiye mshindi. Yaani kila niamkapo nategemea Ali unafanya mashambulizi dhidi ya mpinzani wako Diamond, nakuta patupu. Yaani wewe umekuwa adimu mno katika tasnia wakati mwenzako kila uchao anakuja na ngoma mpya, tena sio ngoma tu bali NGOMA KALI.

Kumbukumbu zangu mbumbumbu zinaniambia kwamba umewahi kunukuliwa ukisema ukimya huamsha hisia. Yaani unajifanya Michael Jackson kwa kutoa kibao kimoja baada ya kingine kwa msimu, na kwamba kutoa vibao kila mara sio dili. Kaka Ali nakupa point blank kwamba hapo umenoa. Yaani ukisubiri siku kibao ndio utoe kitu kwa kujiamini utakubalika kwa mgongo wa kuwa wewe ni "Rockstar" kaa ukijua unakosea. Unatukosea mashabiki wako KAKA!! Tunahitaji vitu kila mara ili tujue ukio hai na fiti. Hayo mambo ya kuiga kina Beyonce na Jay Z (yaani hata kwenye insta huja-follow mtu kwa staili yao hao ni ujuha). Siku hazigandi KAKA ALI. Umwinyi, Ujuaji na kujiona uko juu vitakuzamisha! Piga kazi baba! Sie mashabiki zako tunategemea ukija kwenye show uje na jioya sio na ma "dusherere" na kubweka kama mbweha kila uchao.

Ona mwenzio Diamond anavyowika. Yeye ni mega star kama wewe lakini hategemei kubebwa na historia ya "ALIKUWA" (has been) kwa kutegemea nyota zilipendwa. Ona sasa ngoma yako latest ya "Mvumo wa Radi" ilivyododa. Hiyo ni bonge moja la ngoma lakini imepitwa na wakati. Najua una producer kabambe nchini (Man Water) lakini maudhui ya ngoma hiyo ni two years old! Wakati mwenzio Diamond kaibuka na vitu vya moto kibao ikiwemo hii ya "Baila" aliyo-shoot London, wakati wewe una ngoma kali kuliko hiyo/hizo ambazo hutaki kuzitoa eti kisa hutaki kumwaga lazi kila mara, Ujuha huo Ali Kiba! AMKA!

Sie mashabiki wako tumeshachoka na masebene yako ya "Dusherere" na tunataka utoke upya kila mara udhihirishe u "Rockstar" wako bhana! Hayo mapicha kwenye insta ya kuonesha fashion za mkeo na kujirusha na meneja wako Seven havisaidii kitu. Unatakiwa baada ya ndoa yako hata wakwezo wa Mombasa wajue kweli wana mkwe Star na sio bishoo wa kuishia kwenye Insta kuonesha leo umeenda wapi na mkeo kavaa nini. Huo ni UJUHA kaka. Piga kazi utuliwaze mashabiki zako!!!!!

Naomba nimalizie kwa kukupa ushauri wa bure: Acha nyodo, siku hazigandi, piga kazi, lete mambo mapya ili tujue kuwa naam! tunayemshabikia ana uwezo. Sio kuuza sura na makanzu yako (yanaboa!) huku ukitembelea nyota yako zilipendwa. Yaani unatakiwa utengeneze vitu na kuvimwaga hapo hapo. Kama ushauri huu utaupuuza basi jiandae kuanguka maana kila mtu nchini na nje anakuona wewe ni mtu wa makidai, mtu wa nyodo, usieambilika na juu ya yote unadhani yale ya kale yaliyokupaisha yatadumu. Acha ujuha wa Kiswahili, PIGA KAZI ionekane. Kazi mpya kaka tunataka kila uchao.

By Tarishi

Diva The Bawse amtumia meseji za mahaba Aliko Dangote, asema yupo amejaa tele

$
0
0
Mara baada ya tajiri Aliko Dangote kutangaza kuwa umefika muda wa yeye kupata mpenzi hatimaye awe mke wake wa ndoa , wadada na mastaa wengi wa kike hapa nchini na duniani kwa ujumla wamejikuta akili zimewaruka na wengi wameshaanza kuwasahau wapenzi wao na kujaribu bahati yao kwa Dangote.

Mwanadada Diva the Bawse ameshindwa kuvumilia kabisa hatimaye amekuwa akisumbuka bila mafanikio kujaribu bahati yake kwa Aliko Dangote kwa kumtumia meseji mbalimbali za mapenzi na kumuahidi yupo tayari kumpa chochote anachokitaka ili tu ile ndoto yake ya kuolewa na tajiri iweze kutimia.

Bila kusahau hapo awali Diva alikuwa akilisumbukia penzi la msakata kabumbu kutoka Brazil Neymar na kudai kuwa uzuri wa Neymar unamzuzua sana kumfanya awe chizi juu yake ,lakini kutokana na hili la Dangote, Diva ameamua kumuweka kando kwanza Neymar ili kuangalia maslahi zaidi.

Hii ni Habari Njema Kwa Wale Wote Waliohangaika na Matatizo ya Magonjwa Sugu Yaliyokosa Tib

$
0
0
"HII NI HABARI NJEMA KWA WALE WOTE WALIOHANGAIKA NA MATATIZO YA MAGONJWA SUGU NA YALIYOKOSA TIBA" sasa usikate tamaa tiba imepatikanika kwa DK. ABDALA MUSSA anatibu matatizo kama yafuatayo:

Nguvu za kiume, uzazi, kisukari, tezi dume, vidoda vya tumbo, mgongo kuuma, miguu kuwaka moto na mataizo uliyonayo

1/ITAGULA- ni dawa ya mkosi kuosha nyota, kumvuta mpenzi, mke, mume, kuua kesi na kupata kazi haraka kama umeomba maombi serikalini au kampuni binafisi unaitwa ndani ya siku mbili 2/

NINJIWE- ni dawa inayomaliza matatizo ya wanaume heshima ndani ya ndoa, kuwa na nguvu za kiume milele na kukomaza mbegu na kuwa na uwezo kufanya tendo la ndoa zaidi ya mara 5 bila kuchoka kama umezaraulika na kufanya tendo na kusinyaa uume dawa ipo dozi yake siku sita vidoge 12 pia kuna na unga inayokomaza uume ndani ya siku 7 unapona kabisa.

3/MPALALA- ni dawa ya kutibu busha miguu kuwaka moto, kiuno, kisukari.

4/NGEKEWA- ni dawa ya kuvuta wateja kwenye biashara yoyote kuwa na wateja wengi katika biashara na kuzuia chuma ulete. 4/LINGWATA- ni dawa ya punguza unene, mafuta tumbo, matiti, miguu, hipsi na kutengeneza shepu dawa hii ni ya unga ukitumia utaona mabadiliko baada ya siku 3.

5/DUBISHO- ni dawa zindiko la mwili, majumba, gari, biashara, mteja wangu huduma utaipata mahali popote ulipo kuna wanasaplai mahali ulipo kama huna muda wa kufika osifini mkoa wa dar-es-salaam, iringa, kanda ya ziwa wilaya ya bunda. angalizo kwa wateja usitume sms wala kubipu huduma yangu ni kuanzia saa 12 asubui hadi saa 12 jioni kwa wateja wa dar-es-salaam ofisi ipo buguruni na mbagala zakhem na kwa wale walio nje ya mkoa dawa hizi mtazipata kwa njia za mabasi. punguzo la bei kwa wateja 5 wa kisukari na nguvu za kiume

KWA MAWASILIANAO ZAIDI WASILIANA NA DK. ABDALA MUSSA KWA SIM NAMBA 0767-171773/ 0716-608959 WOTE MNAKARIBISHWA:

Kijana wa Miaka 24 Mbaroni kwa Kifo cha Mama Yake

$
0
0
Kijana wa Miaka 24 Mbaroni kwa Kifo cha Mama Yake
Kijana Ngassa Mathias (24), mkazi wa Kitongoji cha Kiloleli, Kijiji cha Ilebelebe, Kata ya Itilima, Wilaya ya Kishapu amekamatwa na jeshi la polisi baada ya mama yake mzazi, Nyawamba Dohoi kuuawa kwa kuchomwa na kitu chenye ncha kali maeneo ya kichwani na mikononi na watu wasiojulikana.

Kutokea kwa mauaji hayo na kukamatwa kwa kijana huyo kumethibitishwa na Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Shinyanga, ACP Simon Haule. Akizungumza na mwandishi wa Uwazi kwa njia ya simu, Mwenyekiti wa Kijiji cha Ilebelebe, Thomas Nkindo alisema kuwa inashangaza mauaji hayo yanayolenga wanawake kutokea, kwani mwaka jana mwezi kama huu kulitokea mauaji ya mwanamke mmoja aliyeuawa kikatili kama huyu.

Nkindo alisema kuwa wananchi wengi wamekimbia kijiji baada kutokea mauaji ya marehemu Nyawamba yaliyofanywa na watu ambao mpaka sasa hawajafahamika.

“Nitaitisha mkutano wa hadhara wa wananchi ili kubaini tatizo hili kwani msiba huu ni mkubwa, watu wasiwe wanaingia kijijini kwetu kufanya mauaji ya kinyama, hatuwezi kusema marehemu alikuwa na ugomvi na nani bali tuangalie ni akina nani waliotenda haya. “Kutokana na mauaji haya, watu wanaogopa kuja msibani kwa hofu na wengine wamekimbia kijiji kwa hofu ya kukamatwa na polisi,” alisema mwenyekiti huyo wa kijiji.

Wifi wa marehemu, Sia Shija alisema kuwa waligundua kuuawa kwa marehemu saa tatu asubuhi baada ya jirani mmoja kwenda nyumbani kwake kuchukua ndoo yake aliyokuwa ameiazima marehemu.

Kamanda wa Jeshi la Polisi mkoani hapa, ACP Simon Haule amethibitisha kutokea kwa tukio hilo mwishoni mwa wiki iliyopita huku akieleza kuwa mauaji hayo chanzo chake ni ni mali alizoachiwa marehemu na mume wake ambaye naye ni marehemu. “Hivi sasa tunamshikilia mtoto wa marehemu, Ngassa Mathias kwa uchunguzi zaidi wa tukio hilo,” alisema Kamanda Haule.

Vanessa Mdee Amchimba Biti Jux Kuvaa Kikuku

$
0
0
Vanessa Mdee Amchimba Biti Jux Kuvaa Kikuku
Je wewe unaweza mruhusu mpenzi wako wa kiume avae kikuku?. Muimbaji Vanessa Mdee amemchimba biti mpenzi wake Jux kuingia kwenye anga hizo.


Vee amedai uvaaji wa vikuku sio utamaduni wa wanaume wa Kitanzania hivyo hawezi pendezwa na utamaduni huo kwa madai umamshushia heshima mwanaume.

“Kusema kweli Jux hawezi kuvaa kikuku ,” Vanessa aliiambia Wasafi TV. “Sidhani kama inaendana na tamaduni zetu. Vikuku ni kwaajili ya wasichana, sipendi japo naona kuna watu wengi wanavaa,”

Aliongeza, “Kiukweli kuna msanii wa Marekani anampenda Jux anaitwa Fabulous, na yeye nahisi anavaa kikuku, nikasema nini hiki, nikamwambia ole wako na wewe uvae.,”

Wawili hao kwa sasa wanafanya vizuri na tour yao ya muziki iitwao ‘In Love and Money’.

Katika hatua nyingine, mapema leo muimbaji Diamond Platnumz amepokea madongo kutoka kwa mashabiki wake mtandaoni baada ya kuonekana amevaa kitu ambacho kinaonekana kama ni kikuku.

Mapenzi Kiboko Baraka The Prince Abadili Dini ya Mpenzi Wake Naj

$
0
0
Mapenzi Kiboko Baraka The Prince Abadili Dini ya Mpenzi Wake Naj
Kwa kitambo sasa hivi tunafahamu kwamba Mwimbaji wa Bongofleva Baraka The Prince amekua mapenzini na Mrembo Naj ambae ni Mwigizaji/Msanii ila hili la kubadili dini hatukua tunalifahamu.

Kwenye EXCLUSIVE Baraka amethibitisha kwa kusema ni kweli amebadili dini ambapo namnukuu akianza kwa kusema “Ujue mambo ya dini bro ni imani, sio rahisi kama wengine wanavyochukulia hivyo mpaka unaikana imani unakua umeamua sana, umefatilia umejua faida na hasara zake“



Wanawake Wawapiga Marufuku Wanaume Kuzika Kisa Hiki Hapa

$
0
0
Wanawake Wawapiga Marufuku Wanaume Kuzika Kisa Hiki Hapa
Taarifa kutoka katika kata ya mto wa Mbu, Arusha leo July 17, 2018 ni hii ya wanawake kukataa wanaume wasishiriki kwenye mazishi ya mama anayejulikana kwa jina la Ruth kutokana nakudaiwa kuuawa kisha kubakwa na watu wasiojulikana huku wakiwatuhumu wanaume wa eneo hilo kuhusika na matukio hayo.

Wakati jeshi la polisi Arusha likithibitisha kutokea kwa tukio hilo, Mbunge wa jimbo hilo la Monduli Julius Kalanga amesema wanawake hao wamefikia uamuzi huo baada ya matukio hayo kukithiri huku akilitaka jeshi la polisi kuchunguza na kuchukua hatua.

“Pamoja na kuwa ni mtu wa nane kuuawa wanawake wameonyesha hisia zao kwa kudhani kwamba wanaume ndio wanaowauwa kwani tangu matukio haya yatokee haijawahi kutokea mtu aliyehukumiwa kutokana na matukio haya” -Mbunge Kalanga

Watu Wamvaa Daimond Baada ya Kuvaa Kikuku

$
0
0
Watu Wamvaa Daimond Baada ya Kuvaa Kikuku
Mashabiki katika mtandao wa Instagram wamecharuka baada ya kuona picha inayomuonyesha muimbaji maarufu nchini Tanzania, Diamond Platnumz akiwa amevaa cheni mguuni (kikuku).


Mapema leo muimbaji huyo ambaye yupo nchini Marekani kwenye tour ya ABoy From Tandale, alipost picha zake mpya kupitia mtandao huo huku moja katika mguu wake wa kushoto akionekana kama amevaa kitu kinachohisiwa ni cheni.


Baada ya kuona picha hiyo mashabiki wengi kupitia instagram wamekasirishwa na kitendo hicho kwa madai hakiendani na tamaduni za Kitanzania.

Haya hapa chini ni maoni ya mashabiki hao, hata wewe unaweza kutoa maoni yako kupitia kurasa zetu za mitandao ya kijamii.

Makerahabiba
Mm mmmm hadi kikuku huko sio kabisa jaribu kumtafakari na mwenyez mungu juu ya ukuu wale Leo ni raha kuvaa herein .kikuku je je ukirejea kweke mungu utamjibu kitu gani … CIO poa.

diamondpletnumz
Kwani kikuku maana yake nin? Mimi kwa mtazamo wangu nipambo kama pambo jingine tu , then kuhusu maana ya kitu hua inatengenezwa na mtu mweenyewe nikama vile kisu unaweza kukitumia kukatia nyanya na vitunguu au ukaamua kumdunga mtu

lemon_spiceup

Man_ada sio uteam..kwani huyo Si MTU mzima mtampangiaje maisha…kaamua ni yeye..who are u kumwambia what to do…tatizo wabongo chokochoko nyingi…jifunzeni kwa wazungu wenzenu kila MTU ana maisha take…who are u to judge someone wewe mangapi unafanya ambayo sio sahihi..eti?.

ishamwinyi2454.

Heee!!!😨😨😨 kikuku tenaaa!😭😭😭 innaalillah wainnaailah rajiun yaaAllah tujaaliye mwisho mwema waja wako kwan ss ni wadhalimu kwako na kwako tutarejea.


WAnaxhangaaa

Kikukuu wakat shanga unazo kiunon hawajui bila kumkatikia mzee baba pesa aziingiii😂😂😂👌👌 waambie saiv utuumii nguvu kubwa kujikaza toilet 😁😁🙌.


uwalymussa
Wachokozi Na vikuku haya sindio Mwenenu kazi kwenu Wazee wa Modo zakubana cjui vikondomu Mama yenu Ameanza watoto mutafata Sio wakwetu huyo Kiumeni hatuna Tamaduni hizi

Trump Shutumani kwa Kuitetea Urusi Kuhusu Tuhuma za Udukuzi

$
0
0
Rais wa Marekani Donald Trump ameitetea Urusi na tuhuma kwamba ziliingilia uchaguzi wa Rais nchini mwake mwaka 2016.

Baada ya mazungumzo yao, ya ana kwa ana na Rais wa Urusi Vladmir Putin, Rais Trump ameyapinga mashirika ya ujasusi ya Marekani na kusema hakukua na sababu yoyote ya Urusi kuingilia uchaguzi huo.

Kwa upande wake Rais Putin amesisitiza kwamba kamwe nchi yake haijawahi kuingilia mahusiano na Marekani.

Aidha kuhusiana na mkutano wa Helsinki, Kwa upande wake Rais Putin ameuelezea mkutano huo kama uliokuwa wazi bila ya kupangwa na wenye manufaa.

Mazungumzo hayo ya faragha ya viongozi hao, yalichukua karibu saa mbili katika mji mkuu wa Finland Helsinki hapo jana.

Katika mkutano na Waandishi wa Habari, baada ya mkutano huo, Rais Trump aliulizwa kama anayaamini mashirika yake ya ujasusi ama Rais wa Urusi, zinapokuja tuhuma za udukuzi katika uchaguzi.

Koffi Olomide Azuiwa Kuingia Zambia Kisa Hiki Hapa

$
0
0
Koff Olomide Azuiwa Kuingia Zambia Kisa Hiki Hapa
Mwanamziki maarufu wa rhumba Koffi Olomide amenyimwa kuingia nchini Zambia kutokana na makosa mengi yanayomkabili katika taifa hilo la kusini mwa Afrika na Ufaransa ikiwemo madai ya kumshambulia mpiga picha katika hafla moja ya mziki alipokuwa ziarani nchini humo.

Pia, anakabiliwa na madai ya kuwanyanyasa kingono wachezaji wake wa densi, kuwateka nyara pamoja na kuwaajiri kwa njia ya udanganyifu kutumia vibali ghushi.

Kabla ya ziara hiyo yake iliyopigwa marufuku kwa sasa, Olomide - anayeishi Jamhuri ya kidemokrasia ya Kongo, ameitaja Zambia kuwa "makazi yake ya pili" na kuongeza kuwa angependa kupiga shoo nchini humo "kabla afe."

Taarifa ya kuomba msamaha kutoka msanii huyo wa miaka 62 imepeperushwa kwenye kituo kimoja cha radio nchini Zambia. Amefunguka kuwa anawapenda wanawake wa Zambia huku akikwepa madai dhidi yake bila kuyaangazia.

Olomide, majina kamili Antoine Christophe Agbepa Mumba, alitarajiwa kuandaa burudani katika maonyesho mawili nchini Zambia mwezi huu, lakini serikali imetishia kuwa itamtia pingu pindi atakapotua taifa hilo.

Mwanamuziki Koffi Olomide amealikwa tena nchini Kenya
Ubalozi wa Ufaransa nchini Zambia imejiunga na juhudi za kumkamata msanii huyo huku ikiitisha kukamatwa kwake siku ya Jumamosi wiki hii.

Balozi wa Ufaransa nchini humo, Sylvain Berger, ametishia kuwashirikisha maafisa wa usalama wa Interpol kumkamata Olomide, aliyesema kuwa bado mashataka dhidi yake nchini Ufaransa hayajafutiliwa mbali.

Mnamo 2016, alinaswa kwenye Kamera akimlisha teke mmoja wapiga densi wake alipowasili nchini Kenya. Alitolewa taifa hilo kwa haraka.

Mwaka wa 2012, alipatikana na hatia ya kumshambulia msimamizi wake Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo.

Mnamo mwaka wa 2008, alidaiwa kumpiga mpiga picha wa Shirika la habari la kibinafsi la RTGA na kuvunja kamera yake baada ya kumvamia katika sehemu moja ya burudani mji mkuu wa Kinshasa, baada ya kutofautiana kuhusu vibali vya kupiga picha.

Mwishowe, spika wa bunge la kitaifa aliingilia kati na kusuluhisha mtafaruku huo huku akituliza uhasama kati ya mwimbaji huyo na mmiliki wa runinga hiyo.

Lugola: Sitaki Kusikia Habari za Wafungwa Kula Bure

$
0
0
Lugola: Sitaki Kusikia Habari za Wafungwa Kula Bure
Waziri wa Mambo ya Ndani, Kangi Lugola amesema hataki kuona wafungwa nchini wanaishi kama ndege wa angani.

Amesema hayo akimaanisha kuwa hawalimi ila wanakula bure, badala yake wanatakiwa wafanye kazi na kujitafutia chakula wao wenyewe badala ya kusubiri kupewa chakula na Serikali.

Lugola ameyasema hayo jana Julai 16 wakati akihojiwa katika kipindi cha Tuambie kilichorushwa na kituo cha televisheni cha TBC1 Jumatatu usiku, na kubainisha kuwa amewaagiza wasaidizi wake kupitia sheria vizuri na kumpelekea mpango mzuri wa utekelezaji wa agizo la Rais, la kuwatumia wafungwa kufanya kazi za kilimo na ufugaji na kujitafutia chakula wao wenyewe.

“Hata kama ni meno, lazima walimie meno, watatumia meno yao kulima mahindi, kulima maharage ili wajilishe, na nimemwambia Inspekta Jenerali wa Magereza, katika hili sitaki kisingizio cha aina yoyote".

Lugola amesema kuwa amemueleza Inspekta Jenerali wa Magereza kutumia Shirika la Uzalishaji Mali, Benki ya Kilimo na TIB kuchukua mikopo katika kutekeleza agizo hilo la Rais.

Waziri Lugola amesema utoaji wa chakula bure gerezani umepelekea baadhi ya wafungwa kuona gerezani kama ndiyo sehemu ya kupumzika na kula bure bila kufanya kazi, na kusababisha baadhi yao kila wanapobakisha mwezi mmoja kumaliza vifungo au wakimaliza vifungo na kuachiwa huru, wamekuwa wakifanya makosa mengine kwa makusudi ili warudi tena gerezani.

"Wanajitafutia makosa na kuendelea kukaa bure na kula chakula bure bila kufanya kazi,"amesema.
Viewing all 104809 articles
Browse latest View live


Latest Images