Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104795 articles
Browse latest View live

Jinsi ya Kuishi na Mwanamke Asikuloge au Kukupa Limbwata..!!!

$
0
0

Nipo tena kwa Mara nyingine katika kubadilishana uzoefu juu ya mambo mbalimbali yanayohusu mahusiano,kuna jambo limekuwa likiniumiza kichwa sana ni swala zima la kulogwa au kupewa limbwata na mwanamke.

Nidhahiri kabisa mambo haya katika jamii yetu yanafanyika kwa baadhi ya wanawake huwa wanawafanyia wanaume,na tatizo hilo limezidi kushamiri zaidi kutokana na ongezeko kubwa la waganga wa kienyeji.

Nimefanya research kwa baadhi ya waganga wameniambia wateja wao wakubwa ni wanawake na shida kubwa wanayokuwa wanahitaji ni kuolewa au kuwadhibiti wanaume zao.

Nami mekuja kugundua wanaume wengi huwa wanafanyiwa madawa ila wakati mwengine mungu huwalinda hawazuriki bila ya wao kujua na wanaume wengi ambao wapo katika hatari hiyo ni wale wenye kipato kidogo ambacho kinarizisha.

Sasa basi nimejaribu kutafuta prevention za ki psychology, ambanzo hazihusiani na mambo ya kishirikina ambazo zinaweza kukusaidia uepukane na janga hilo nimejaribu kutumia experience yangu ni kama zifuatazo:

Kwanza kabisa kama mwanaume unapoanza mahusiano ya kimapenzi na mwanamke unatakiwa umwambie mwanamke vitu ambavyo huvipendi na moja katika ya vitu ambavyo utamwambia hupendi ni mambo ya kishirikina na unatakiwa umsisitizie kwamba endapo kama wewe utagundua yeye anapenda mambo ya kwenda kwa waganga umwambie siku hiyo ndio itakuwa mwisho wa mapenzi yenu.

Jambo la pili ukiwa unaishi na mwanamke ndani usipende kula chakula peke yako hata kama umechelewa kurudi umerudi labda saa sita usiku mwambie mke wako mle wote chakula cause peke yako hujazoea kula au kama mna mtoto wenu ama ndugu wa mwanamke kula nae chakula.

Kwa kufanya hivyo mwanamke atajua hupendi kula peke yako na unampenda yeye na ndugu zake kumbe unalako moyoni unajilinda na limbwata,jambo la tatu pendelea kufanya ibada ukitaka kula na ukitaka kulala na mshirikishe mkeo katika ibada na wakati mwingine msomee maandiko ya vitabu vya mungu ambayo yanakataza ushirikina na adhabu zake watakazo zipata wanaofanya mambo hayo,mengine mnaweza mkaongezea.

Note:Mwanamke anaweza akawa sio mshirikina lakini akashawishiwa na marafiki zake akufanyie hivyo,kwa hiyo kama mwanaume ni bora ukachukua tahadhari mapema.

Muone Ustadhi Ashrafu Atimize ndoto yako..Anatumia Nyota na Nguvu za Asili Kutibu

$
0
0
Muone Ustadhi Ashrafu Atimize ndoto yako. yawezekana ulizaliwa nanyota yakitajiri ila watu wabaya wameikalia mpaka sasa ikawa hufahamu chochote. Mtafute ust Ashrafu Airudishe nyota yako yakitajiri kwakupitia pete inayoendana na nyota yako. Ust Ashrafu Ananguvu zamajini katika utendaji wake. 

Anauwezo wakutoa Mali kwakupitia pete nakwakupitia majini wake. Na anauwezo wakuzirudisha Mali zilizopotea kwanjia zakichawi kwakupitia Pete yakifalme Ambayo inayong'aa muda wowote nakubadilikabadilika rangi. Ust Ashrafu Ametembea baadhi ya nchi kwakuwapatia watu huduma mbalimbali. Kama vile maradhi yakisukari, presha, ukimwi, bawasiri, tezidume, mwiliwote kupooza nakutetemeka, NK. Navilevile Amewapatia wengi huduma yamvuto wa kibiashara, nayamvuto wakimapenzi. 

Nawengi wametoa shukrani zao kwa ust Ashrafu namna Alivyozirudisha Ndoa zao zilizo sambaratika kwamuda mrefu. Mtafute ust Ashrafu ili akusaidie juu yamambo yako. Nahuyu ust anasaidia matatizo yauzazi, nguvu zakiume, kuwashwa mwilini, kutokwa namapere usoni nasehemu za siri, NK. Na anadawa yakumtuliza mume asiesikia nakutulia inayoitwa limbwata. Na anadawa yakumrudisha mpenzi ktk mahusiano kwamda mchache. 

Na amezipatanisha familia nyingi zilizogombana. Na anauwezo wakufarakanisha maadui waliokua pamoja.

Mtafute Ustadhi Ashrafu kwa no. 0768486717-0627423037 Au Mtafute kwa whasapp 0659438578 

Hizi ndio namba zake mpigie muda wowote usiogope yupo kwaajili yako. Mpigie hupate muongozo wa bure naushri. Ustadhi Ashrafu huduma zake hupatikana mahala popote utakapo muhitaji, ila sehemu kuu anapatikana Bagamoyo.

Tazama Hapa Kuona Majina Ya Walimu Wa Ajira Mpya Waliopangwa Katika Vituo Vya Kazi Kwenye Shule Za Msingi Na Sekondari Julai, 2018

$
0
0
TAARIFA KWA UMMA KUHUSU AJIRA YA WALIMU WA SHULE ZA MSINGI NA SEKONDARI JULAI, 2018

Ofisi ya Rais – TAMISEMI inapenda kuutarifu Umma kuwa, jumla ya Walimu 4,840 wamepangiwa vituo vya kazi kwenye Shule mbalimbali za Msingi na baadhi kwenye Shule za Sekondari nchini.

Walimu hao waliopangiwa vituo vya kazi wanatakiwa kuripoti katika Ofisi za Wakurugenzi wa Halmashauri zilipo shule walizopangiwa na baadaye kuripoti kwenye Shule walizopangiwa.

Walimu wote wanatakiwa kuripoti kwenye vituo vyao vya kazi kuanzia tarehe 23 Julai, 2018 hadi tarehe 7 Agosti, 2018 wakiwa na mahitaji yafuatayo:
Vyeti halisi vya taaluma vya Kidato cha Nne na/au Kidato cha Sita;
Vyeti halisi vya kitaaluma vya mafunzo ya Ualimu katika ngazi husika; na
Cheti halisi cha kuzaliwa.
Walimu wote waliopangiwa vituo vya kazi wanaelekezwa kuwa:
Vituo vyao vya kazi ni Shule ya Msingi au Sekondari alizopangiwa na sio Makao Makuu ya Halmashauri;
Mwajiriwa atakayeripoti na kuchukua posho ya kujikimu kisha akaondoka katika kituo chake cha kazi alichopangiwa Serikali itamchukulia hatua kali kwa mujibu wa sheria na taratibu zilizopo; na
Hakuna Mwalimu atakayekubaliwa kubadilisha kituo kwa sababu yoyote ile. Kila mwajiriwa mpya anapaswa kuripoti katika kituo chake alichopangiwa na si vinginevyo. Waajiriwa wapya ambao watashindwa kuripoti katika vituo walivyopangiwa nafasi zao zitachukuliwa na Walimu wengine 5,220 wenye sifa waliokosa nafasi.
Wakurugenzi wa Halmashauri husika wawapokee Walimu waliopangwa kwenye Halmashauri zao kwa kuzingatia taratibu na kanuni zote za utumishi wa Umma, ikiwa ni pamoja na kutoa taarifa ya kuripoti kwao. Taarifa ya kuripoti waajiriwa hao itumwe Ofisi ya Rais- TAMISEMI ifikapo au kabla ya tarehe 10.08.2018 baada ya tarehe ya mwisho ya kuripoti.

Majina ya Walimu waliopangiwa vituo yanapatikana katika tovuti ya Ofisi ya Rais – TAMISEMI ya www.tamisemi.go.tz

Imetolewa na:
KATIBU MKUU OFISI YA RAIS – TAMISEMI

BOFYA  HAPA  KUONA  MAJINA  YA WALIMU WA AJIRA MPYA WALIOPANGWA KATIKA VITUO VYA KAZI KWENYE SHULE ZA MSINGI NA SEKONDARI JULAI, 2018

Wapinzani Walia Mchezo Mchafu CCM, Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumatano ya July 18

$
0
0

Wapinzani Walia Mchezo Mchafu CCM, Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumatano ya July 18

Hawa "Pombe Nayo ni Madawa ya Kulevya, Mimi ni Muathirika wa Pombe za Kienyeji'

$
0
0
Mwanadada Hawa ambae aliwahi kuwika sana kipindi cha nyuma kutokana na kushirikishwa katika wimbo wa Diamond amefunguka na kusema kuwa watu wamekuwa hawajui kama hata pombe pia  inaweza kumfanya mtu kuharibikiwa kama madawa ya kulevya.

Hawa ambae alikuwa muathiika wa pombe zakienyeji kwa muda mrefu na kuuua kabisa kipaji chake cha muziki mpaka pale alipopata watu wa kumsaidia anasema kuwa haikuwa rahisi kwake kutoka huko kama asingepatiwa msaada kama wanavyowatokea waathirika wa madawa ya kulevya.

"Pombe pia ni miongoni mwa madawa ya kulevya sema tu watu wamekuwa hawalijui hilo,maana mimi pia ni muathurika wa pombe"

Hata hivyo mwanadada huyo ambae kwa sasa hali yake imeanza kuimarika, anasema kuwa anajipanga upya na kuja kivingine ili kuendeleza kipaji chake cha muziki kwa kuwa anaamini kipaji anacho.

Barnaba 'Nina Mashabiki Wengi wa Kike ila Naogopa Kupiga Nao Picha...Kwasababu....

$
0
0
Msanii wa muziki wa Bongo fleva anayefanya vizuri na kibao chake cha ‘Chausiku’ Barnaba Boy amefunguka na kuweka wazi kuwa hivi sasa anahofia sana kupiga picha na wasichana kwa kuhofia uzushi.

Barnaba amefunguka hayo baada ya kuulizwa kuhusu picha zake na wasichana kadhaa ambazo zimekuwa zikionekana Kwenye mitandao ya kijamii na kudaiwa kubadilisha badilisha wasichana.

Kwenye mahojiano na Enews ya East Africa Tv, Barnaba ameweka wazi kuwa wasichana wengine ni mashabiki zake akikutana nao wanaomba picha lakini baadae anasingiziwa ni wanawake wake:

Sio siri siku hizi nimekuwa muoga wa kupiga picha na watoto wa kike na Kuposti Kwenye mitandao ya kijamii naona kama itAleta maneno maneno kuwa ni wapenzi wangu wakati wengi ni mashabiki tu”.

Lakini pia Barnaba alikataa taarifa kuwa tangu ameachana na mama watoto wake MAma Steve amekuwa na wanawake wengi:

Mimi sina mahusiano na wasichana wengi ila nina mashabiki wa kike wengi sana na hata marafiki zangu wengi ni wa kike sio wanaume halafu watoto wa kike wananipenda sana kwa sababu mimi ni mtu ambaye ni mcheshi mtani na mtu wa stori.

Billnass "Wanawake Wanaojichubua Kwangu ni Sumu, Siwezi Ku.......

$
0
0
Staa wa muziki wa Bongo fleva anayefanya miondoko ya kuchana BillNas ameibuka na kuweka wazi kuwa hawezi kuwa kwenye mahusiano ya Kimapenzi na mwanamke anayejichubua.

Billnas ameweka wazi kuwa Kitendo Cha mwanamke kubadilisha rangi yake ya mwili kutoka Kwenye weusi asilia kuwa mweupe anakuwa kama amejikataa mwenyewe.

Kwenye mahojiano na kipindi cha Refresh cha Wasafi Tv, Billnas amekataa uhusiano na wanawake wanaotumia kitaulo (mkorogo):

Kujichubua au kubadilisha rangi ya mwili sio pia kabisa mimi mwanamke anayejichubua siwezi kuwa naye kimapenzi uaani sijui iweje.

Kujichubua ni kitu ambacho mimi niko tofauti nacho sana kwa sababu kwanza unakataa uhalisia wako vile ambavyo mwenyezi Mungu amekubariki na hii rangi yetu nyeusi ipo very unique.

Lakini pia kuna vitu vingi vinavyomfanya mtu kuwa mzuri na viko ndani yako na sio muonekano wako wa nje Fanya matendo mema mazuri watu watakupenda”.

Baada ya kuachia kibao chake kipya ‘Labda’ Bill Nas alitangaza kuwa video hiyo ilidukuliwa katika mtandao wa Youtube na kufutwa.

Peter Zakaria aanza kurudisha mali zote alizonunua yeye na mkewe serikalini

$
0
0
Mfanyabiashara Peter Zakaria (58), amerejesha mali zote alizonunua kutoka Chama Kikuu cha Ushirika Nyanza (NCU), akiamini kwa kufanya hivyo ataondoa ‘nuksi’ ya kuandamwa na Serikali. Tajiri huyo mkazi wa Tarime mkoani Mara, anayemiliki vitegauchumi mbalimbali yakiwamo mabasi ya Zakaria, amekabidhi nyaraka za umiliki wa mali hizo serikalini, wiki iliyopita. Zakaria anashikiliwa rumande akituhumiwa kuwajeruhi kwa risasi maofisa usalama wawili waliomfuata kwenye ofisi zake usiku, kwa kile kinachoelezwa kuwa ni ‘kumteka’ na kumpeleka kusikojulikana. Kwa miezi saba sasa, mkewe yuko mahabusu akishitakiwa kwa uhujumu uchumi kutokana na kuwa kwenye nyaraka za ununuzi wa mali za Chama cha Ushirika Nyanza. Mkuu wa Mkoa (RC) wa Mara, Adam Malima, amethibitisha kuwa waliojeruhiwa kwenye tukio hilo la Juni 29, mwaka huu ni maofisa wa Usalama wa Taifa. Chanzo cha habari kutoka ndani ya familia ya Zakaria kimesema wanaamini misukosuko mingi inayoiandama familia hiyo, inasababishwa na mambo kadhaa, moja likiwa hilo la ununuzi wa mali za NCU.

Mke wa Zakaria, Anthonio Zakaria, amefunguliwa kesi ya uhujumu uchumi akihusishwa na ununuzi wa mali za chama hicho cha ushirika. Tangu alipokamatwa mwaka jana, ameendelea kuwa rumande. Msemaji wa ukoo wa Zakaria, Samuel Chomete (65), amethibitisha urejeshaji wa nyaraka na mali zote za NCU ambazo zinamilikiwa na familia ya Zakaria. Chomete ameliambia JAMHURI mjini Tarime kwamba mali hizo zimerejeshwa rasmi serikalini kuanzia Julai 3, mwaka huu. Hata hivyo, hakueleza makabidhiano hayo yamewahusisha viongozi gani wa Serikali au NCU. Mali zinazotajwa ni nyumba ya NCU ambayo kwa sasa kuna Benki ya CBA (Commercial Bank of Africa), na kituo cha mafuta cha Zakaria kinachotazamana na Jengo la Kitegauchumi la Mfuko wa Hifadhi ya Jamii (NSSF), Barabara ya Kenyatta jijini Mwanza. Familia ya Zakaria inasema ilinunua mali hizo kihalali mwaka 2002.

Kurejeshwa kwake kunatokana na msimamo wa Serikali ya Awamu ya Tano wa kuhakikisha wale wote walioshiriki ‘kufilisi’ ushirika maeneo mbalimbali nchini wanashitakiwa. Chomete amekataa kutaja kiasi cha fedha kilichotumika kununua mali za ushirika huo. Uamuzi wa familia na
ukoo wa Zakaria unalenga kulinda usalama wa mfanyabiashara huyo na familia yake. “Tumeonana na yeye Zakaria, ameshauri mali hizo zirudishwe, asije akafa bure. Na mama mkurugenzi (Anthonio) amesaini nyaraka za makabidhiano Jumanne (iliyopita). “Vyote tumerudisha serikalini ili vikabidhiwe Nyanza Co-operative Union,” Chomete ameliambia JAMHURI. Anthonio Zakaria, ambaye ndiye anayeonekana kwenye nyaraka za ununuzi tangu Januari, mwaka huu, amezuiwa katika Gereza la Butimba jijini Mwanza, akikabiliwa na kesi ya uhujumu uchumi. Meneja wa NCU, Juma Mokili, ameulizwa kama ameshapokea mali za chama hicho kutoka kwa familia ya Zakaria, na amesema hawajakabidhiwa. Licha ya kukiri kuwa familia hiyo inamiliki mali zinazotajwa, amesema asingependa kuingia kwenye undani wa suala hilo kwa kuwa lipo mahakamani. Mkuu wa Wilaya ya Nyamagana, mahali ambako kuna mali hizo, Marry Tesha, ameulizwa na kujibu kuwa kazi ya urejeshaji mali hizo inasimamiwa na mkoa. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, John Mongella, amezungumza na JAMHURI na kuomba apewe muda ili apate ukweli juu ya kurejeshwa kwa mali hizo.

“Hiyo taarifa ndiyo naisikia kwako… Ngoja nifuatilie Jumatatu au Jumanne (jana au leo) nitakuwa na jibu,” amesema Mongella.
UPEKUZI NYUMBANI KWA ZAKARIA Julai 5, 2018 Polisi walimchukua Zakaria kutoka Musoma na kwenda kufanya upekuzi nyumbani kwake Tarime. Magari kadhaa, yakiwamo mawili yaliyojaa polisi wa Kikosi cha Kutuliza Ghasia (FFU) wenye silaha, yalifika kwenye makazi ya mfanyabiashara huyo na kufanya upekuzi. Mamia ya wananchi walikaribia eneo la tukio. Katika upekuzi huo unaodaiwa kuwa na baraka za Mahakama, inaarifiwa kuwa bunduki mbili aina ya shotgun na rifle pamoja na vibali vya umiliki vilichukuliwa na polisi. Baadaye walirejea Musoma. Wananchi kadhaa mjini Tarime bado wanajadili tukio la kuvamiwa Zakaria. Mwananchi mmoja, Heche Chacha, amehoji, “Kama kweli hawa watu walikuwa na nia njema ilikuwaje wabandike namba kwenye gari lao (T 245 CTW) wakati siyo yao? “Yawezekana pengine hawa watu walitaka kumchonganisha Zakaria na Ndesi Mbusiro, anayemiliki gari lenye namba hiyo T 245 CTW,” amesema Heche ambaye ni Katibu wa Chadema Mkoa wa Mara.

Zakaria mahakamani Julai 5, mwaka huu Zakaria alifikishwa mahakamani mjini Musoma akikabiliwa na mashitaka ya kujaribu kuua. Alikanusha tuhuma hizo. Katika kesi hiyo Na. 3/2018 iliyopo Mahakama ya Hakimu Mkazi Mkoa wa Mara, mfanyabiashara huyo anatetewa na mawakili wawili – Onyango Otieno na Kassim Gilla. Upande wa mashitaka yupo Wakili Lukelo Samuel. Wakili Samuel amedai kuwa mshitakiwa anakabiliwa na makosa mawili ya kujaribu kuua. “Mshitakiwa alitenda kosa hilo Juni 29, 2018 katika Mtaa wa Anglikana wilayani Tarime. Ametenda kosa hilo kinyume cha Kifungu cha Sheria cha Kanuni ya Adhabu, Sura Na 16 Kifungu cha 211 (a) kilichofanyiwa marejeo mwaka 2006,” amedai Wakili huyo wa Serikali. Inadaiwa kuwa mshitakiwa alitenda makosa hayo kwa watu wawili waliotajwa kwa majina ya Ahmad Segure na Isack Bwire.

Wakili huyo wa Serikali hakutaja kazi zao wala mahali wanapoishi. Alisema majeruhi hao wanatibiwa katika Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) jijini Dar es Salaam. Akaiomba Mahakama kutompa dhamana mtuhumiwa huyo, akidai hiyo ni kwa ajili ya usalama wa mshitakiwa na pia hali za kiafya za majeruhi si nzuri. Wakili Gilla akaiomba Mahakama impatie mteja wake dhamana kwa kuwa shitaka linalomkabili linadhaminika kisheria. “Vifungu vya Sheria Na 148 Kifungu kidogo cha 5 (a) Na ( i-v) pamoja na Kifungu cha Sheria Na 148 Kifungu cha 6-7, vinaainisha juu ya uwepo wa dhamana. “Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ibara ya 13 (6) inazungumzia suala zima la upatikanaji wa dhamana kwa mtuhumiwa,” alisema Wakili Gilla. Akadai kwamba upande wa Serikali umeshindwa kutoa nyaraka zinaoonesha kuwa majeruhi wapo hospitalini wakitibiwa. Pia hakuna kiapo cha daktari kinachothibitisha yote hayo. “Mwanasheria wa Serikali ameshindwa kutoa pia ushahidi unaothibitisha moja kwa moja kuwa kuna viashiria vya kuhatarisha maisha ya Zakaria, iwapo atapatiwa dhamana.” Akijibu hoja hizo, Mwanasheria wa Serikali, Samuel, alidai kuwa wanajua kuwa mshitakiwa ana haki ya kupewa dhamana, lakini Jamhuri imeona kuna haja ya kuzuia dhamana, kwani kesi hiyo haijaanza kusikilizwa. Kutokana na majibizano hayo ya kisheria, Hakimu Mfawidhi wa Mkoa, Hashim Mushi, akasema: “Nimesikiliza hoja za pande zote mbili na nimeona nikae nizipitie kwanza, ili kujiridhisha. Hivyo, naahirisha kesi hii hadi tarehe 10/7/2018, Mahakama itakapotoa uamuzi kuhusu dhamana kwa mshitakiwa.”

Download Hapa Application ya Udaku Special Kwenye Simu Yako Kushuhudia Vimbwanga Mtaani na Stori za Mapenzi

Michepuko Tuweni na Huruma Kidogo Jamani....Ona Huyu Dada Anachofanyiwa na Mchepuko wa Mmewe

$
0
0

Kuna wanawake wengine ni mashetani, hata kama unatembea na mme wake ndo ufanye hivyo jamani

Dada angu anapitia wakati mgumu anahitaji ushauri baada ya kushika simu ya Mme wake wakati ameacha chaji hapo jana jioni na akakuta meseji za hivi kutoka kwa mchepuko

Dada aliolewa na Mme wake mwaka mmoja na nusu na ana mtoto kichanga cha miezi 6

Anatamani amuulize Mme wake kulikoni anaogopa

Nimeshindwa nimwambieje mie

Kwanini Baadhi ya Wanaume Wana Maumbile Mafupi na Upungufu wa Nguvu za Kiume? Suluhisho Hili Hapa

$
0
0
KWANINI BAADHI YA WANAUME WANA MAUMBILE MAFUPI NA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME DR SITTA NDO SULULISHO LAKO tatiza, hili limekuwa likiwaasili watu wengi,sana kisaikolojia hasa baadhi yao kujiona wako tofauti na wanaume wengine, kwa kawaida, mwanaume anatakiwa awe na uume, usiopungua nchi 6-7au-8 ,vinginevyo mtu huyo anamatatizo zipo , sababu nyingi zinazosababisha, tatizo hilo baadhi ni (i) upungufu wa vichocheo vya HORMONES ZA CETROGEN ambazo mwanaume, anapobarehe vichocheo hivi, HORMONES hizo, husaidia ukuaji wa uume

SUPER MIZIZI, ni dawa inayozalisha HORMONES ZA CETROGEN,na kufanya, uume kukuwa na kuongzeka sazi utakayo na kuzibua mlija iliysinyaa,

NSHOLA ni dawa bora, ya kurudisha nguvu, za, kiume bari inatibu ,kabisa kutoa tatizo hilo, na kukupa , hamu ya , kurudia tendo, la ndoa zaidi, ya mala nne 4 ,bila kuchoka atakama unaumli ,wa mika 80,! pia ana ,dawa za ,kutibu, presha ya kupanda ,na kushuka, kisukari kuondoa, mafuta , mwilini ,na maumivu ya, mgogo kiuno, dawa zipo, matazo, ya hedhi, kwa ,wanawake hedhi, zisizokuwa na, mpangilio, na kasonono, pia , vidonda ,vya, tumbo ,(STOMACHI UCLENS) IHUSHI ndoji lako.

NKANYA ni dwa ya mvuto wa kimapenzi ,mchumba mpenzi ariyekuacha, mke mme, atakuludia kwa, mda, wa msaa3 tu , ukishaitumia atarudi ,mwenyewe bila ,ugovi tena, NKOMA ni dawa kuongeza HIPS na mguu wa bia kwa wadada .

HERBON, ni, dawa, ya kuongeza, CD4, NGAKAMA ,ni dawa ya kutibu ,miguu, kufaganzi, na ,kuwaka moto, huduma zetu ,zipo ,vizuri, popote pale dawa utaletewa! DR SITTA, amebobea, kwa tiba asilia

DAR ANAPATIKANA MBAGALA, ZAKHEM, SONGEA BOMBAMBILI SHINYANGA, KAHAMA MJINI, KWA MAELEZO ZAIDI ,

PIGA SIMU 0763172670 au 0715172670

Arsene Wenger Ajutia Kukaa Miaka 22 Arsenal

$
0
0
Aliyekuwa meneja wa klabu ya Arsenal, Arsene Wenger amesema kuwa makosa makubwa anayojutia kwenye taaluma yake ya ufundishaji soka ni kukaa kwa miaka 22 ndani ya timu hiyo.

Former Arsenal manager Arsene Wenger was interviewed by Christine Kelly on RTL

Wenger ameyasema hayo wakati alipokuwa akifanya mahojiano na chombo cha habari cha RTL hali iliyoshangaza watu wengi waliyokuwepo mahala hapo.

Wenger stepped down as Arsenal manager earlier this summer after 22 years at the helm

Mfaransa huyo mwenye umri wa miaka 68 ameeleza kuwa hajatambua bado atakwenda kufundisha klabu gani huku akisisitiza kamwe hatotumia muda mrefu kwenye kazi atakayofanya.

Alipoulizwa na Christine Kelly anadhani ni kosa gani kubwa alishawahi kufanya ndipo akajibu kuwa ni kukaa kwenye klabu moja kwa muda wa miaka 22.

”Kukaa ndani ya Gunners kwa muda wa miaka 22 ni kosa kubwa sana kwangu. Mimi ni mtu ambaye napenda kutoka sehemu moja kwenda nyingine lakini pia kukutana na changamoto,” amesema Wenger.

Arsene Wenger ameongeza ”Nilikuwa mfungwa wa changamoto zangu mwenyewe kwa wakati huo. Niliamua kuachana na Arsenal baada ya kujua kuwa kuna watu wengi wanao nizunguka wanaumia myoyo yao pamoja na familia yangu.”

Wenger ameipatia Arsenal mataji matatu ya ligi kuu ya Uingereza, saba ya FA Cup na kujenga historia iliyotukuka msimu wa mwaka 2003-04 kumaliza ligi bila kufungwa.

Trump Ajichanganya na Kauli Yake Kuhusu Urusi

$
0
0
Rais wa Marekani Donald Trump amesema anakubaliana na hitimisho lililotolewa na Taasisi za Ujasusi za nchi yake kwamba Urusi iliingilia kati uchaguzi mkuu wa nchi hiyo wa mwaka 2016.

Akikanusha kauli yake aliyoitoa siku moja iliyopita baada ya mkutano wake na Rais Vladmir Putin wa Urusi.

Amesema alieleweka vibaya siku ya Jumatatu na kwamba alikuwa akimaanisha kwamba hakuona sababu kwanini isiwe Urusi ambayo ilifanya udukuzi katika uchaguzi huo.

Obama aonya dhidi ya viongozi wababe, azungumzia Ufaransa

Kamera zinazotambua iwapo una raha ama wewe ni tishio

Ni Rais Trump akiitolea ufafanuzi na kuikanusha kauli yake ya awali, ambayo imezua sintofahamu na kukosolewa vikali. Hata kwa baadhi ya washirika wake wakitaka ufafanuzi zaidi na kusafisha kauli hiyo.

Amedai kuwa katika mkutano huo wa Helsinki alimaanisha kusema kwamba hakuna sababu ya kufikiria kuwa Moscow haiwezi kuingilia kati uchaguzi wa Marekani.

Amesema ana imani na kuunga mkono taasisi za usalama za nchi yake.

Ajali: Hiace Yawaka Moto Barabarani Mbeya

$
0
0
Ajali Nyingine Yatokea Mbeya
Ajali nyingine yatokea mbeya ambapo gari aina ya Toyota Hiace iliwaka moto ikiwa barabarani, ndani yake kulikua na Konda na Dereva ambao wote wamenusurika.

Mkoa wa Mbeya umekumbwa na ajali mfululizo hivi karibuni mpaka kupelekea Viongozi wa dini na Wazee wa kimila kufanya maombi kulikemea zimwi hilo ambapo ikiwa ni siku chache baada ya maombi hayo, ajali nyingine zimetokea usiku wa kuamkia leo.

Usiku wa kuamkia leo gari aina ya Land Cruiser limeigonga Bajaji na kusababisha vifo vya watu watatu kwenye eneo la Kadege usiku wa kuamkia leo ambapo usiku huohuo gari aina ya Toyota Hiace imewaka moto ikiwa barabarani katika eneo la Mbembela ambapo Dereva na Kondakta waliokuwemo ndani yake wamenusurika.



Ikumbukwe kuwa baada ya ajali iliyotokea katika mteremko wa Mbalizi, Waziri Mpya wa Mambo ya Ndani, Kangi Lugola alitangaza kuyavunja mabaraza ya Usalama Barabarani ya Mikoa na Wilaya zote nchini.

Waziri huyo pia alimshusha cheo aliyekuwa Kamanda wa Kikosi cha Usalama Barabarani (RTO) wa Jiji la Mbeya, Leopold Fungu hadi kubaki na nyota 3 ambapo baada ya hatua hizo, ajali nyingine ilitokea katika mteremko wa Igawalo na kuua watu watano na kujeruhi mmoja.

Hivi Ndivyo Wema, Daimond na Mastaa Wengine Walivyompongeza Makonda Baada ya Kupata Mtoto

$
0
0
Hivi Ndivyo Wema, Daimond na Mastaa Wengine Walivyompongeza Makonda Baada ya Kupata Mtoto
STAA wa Bongo Fleva Diamond Platinumz na aliyewahi kuwa mpenzi wake ambaye pia ni Malkia wa Bongo movies, Wema Sepetu wametoa neno la pongezi kwa Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda na mkewe kwa kufanikiwa kupata mtoto wa kiume waliyompa jina la Keagan.


Kupitia kurasa zao za Instagram, Wema ameandika maneno haya kwa Makonda;

“Hakika kuna Mungu, wakati wa Mungu ndo wakati sahihi, hongera sana kaka yangu na wifi yangu, kama nawaona, mtoto raha jamani, congratulations once again. All these testimonies are giving me sooo much hope. Tuseme Inshallah, congrats Baba na Mama Keagan.

“Keagan ni mtoto atakaependwa sana wallahy, yaani uwiiii simpatii picha, Keagan you are a blessing to your Mummy and Daddy, and with parents like yours I guarantee you are going to be a good Boy, a blessed child,” ameandika Wema.


Diamond naye akafunguka;

“Congrats, Paul Makonda, Mwenyezi Mungu amkuze mtoto vyema na kumkinga na mabaya ya walimwengu.


Ambwene Yessaya “AY” hakuwa nyuma, naye ametupia ujumbe huu kwa Makonda na mkewe;

“Hongereni sana Familia ya Paul Makonda kwa kupata mtoto. Mungu awajaalie Baraka na Upendo na awasimamie katika malezi ya mtoto.”


Ratiba ya Ligi Kuu Msimu Ujao Kutolewa Leo

$
0
0
Ratiba ya Ligi Kuu Msimu Ujao Kutolewa Leo
Wakati msimu wa Ligi Kuu Bara 2018/19 ukisubiriwa kwa hamu na wadau wengi wa soka hapa nchini, Mkurungenzi wa Bodi ya Ligi, Boniface Wambura, amesema ratiba ya mechi zote inatoka leo.

Wambura amesema ratiba hiyo imezingatia kila kitu ikiwemo uwepo wa michuano ya CAF pamoja na mingine ambayo inakuwa inafanyika nchini ili kuondoa muingiliano wa ratiba.

Mkurugenzi huyo ameeleza awamu hii wamejitahidi kuiweka ratiba katika mpangilio mzuri tofauti na misimu ambayo imepita ili kuepuka uvunjaji na kupunguza malalamiko kwa baadhi ya klabu.

Kikao na Waandishi wa Habari kitafanyika leo kwa ajili ya kuiweka hadharani ratiba hiyo ili klabu zote ziweze kuiona tayari kujipanga kwa mechi za msimu mpya.

Ikumbukwe Ligi Kuu itaanza mwezi ujao wa Agosti ambapo jumla ya timu 20 zitakuwa zinawania kikombe cha ligi tofauti na 16 zilizokuwepo awali.

Whatsapp Yawaponza Shule ya Jangwani Hadi Kushika Mkia

$
0
0
 Whatsapp Yawaponza Shule ya Jangwani  Hadi Kushika Mkia
Waziri wa nchi Ofisi ya Rais Tamisemi, Selemani Jafo amefunguka na kudai chanzo kikubwa kilichopelekea shule ya sekondari Jangwani kushika mkia kwenye matokeo ya kidato cha sita ni kutokana na wanafunzi hao kujihusisha na uhasherati pamoja na matumizi ya Whatsapp.


Mrembo Jokate akiwa na baadhi ya wanafunzi wa Jangwani katika project zake za Netball. Picha hii sio ya tukio la hivi karibuni

Waziri Jafo ametoa kauli hiyo leo Julai 17, 2018 wakati alipokuwa shuleni hapo na kumuagiza Katibu Tawala Mkoa wa Dar es Salaam kufanya mabadiliko katika safu ya uongozi wa shule hiyo kwa kuwa hajaridhishwa na ufaulu wa wanafunzi kwa sababu Jangwani ndio shule ya ndoto ya wasichana wengi wa kitanzania.

“Shule ya Jangwani ni shule ambayo yenye upako maalum, sifa na tunu kwa nchi yetu lakini shule hii sasa imekuwa ya tatu kutoka mwisho. Hii ni fedheha ambayo haijawahi kutokea katika shule ya Jangwani. Wanafunzi mmekuja hapa kwaajili ya kusoma sio kwa sketi zenu za rangi ya chungwa, tunataka msome…..

Kwa taarifa nilizozipata wanafunzi wanatumia simu hizi za Whatsapp na muda mwingi wanaangalia picha zilizokuwa mbovu badala ya kusoma huku wengine wakikalia ku-chat na kuangalia vitu ambavyo sio sawa sawa”, amesema Jafo.

Pamoja na hayo, Jafo ameendelea kwa kusema “kwa taarifa nilizozipata hapa za kiuchunguzi ni kwamba wanafunzi wengi wanajihusisha na mambo ya uhasharati, naomba niwaambie endapo mtajihusisha na mambo hayo, elimu haitaweza kuwa rafiki yenu na hilo jambo hata wakubwa wazima linawashughulisha sembuse nyie wanafunzi, nasema kuanzia leo hilo suala lishindwe na ndio maana ufaulu wenu unakuwa mbovu”.

Shule hiyo kongwe iliyopo eneo la Jangwani Jijini Dar es Salaam imeingia kwenye nafasi ya 10 shule zilizoweza kufanya vibaya katika matokeo yaliyotangazwa Julai 13, 2018 na Baraza la Mitihani la Tanzania (Necta).

Shule 10 za mwisho kitaifa ni Jangwani ya mkoani Dar es Salaam, Jang’ombe (Mjini Magharibi), Forest Hill (Morogoro), St James Kilolo (Iringa), Aggrey (Mbeya), Nyailigamba (Kagera), White Lake (Dar es Salaam), Musoma Utalii (Mara), Golden Ridge (Geita) na Ben Bella (Mjini Magharibi).

Huku shule 10 zilizoweza kufanya vizuri zaidi zikiwa ni Kibaha ya Mkoani Pwani, Kisimiri (Arusha), Kemebos (Kagera), Mzumbe (Morogoro), Feza Boys’ (Dar es Salaam), Marian Boys (Pwani), Ahmes (Pwani), St, Mary’s Mazinde Juu (Tanga), Marian Girls (Pwani) pamoja na Feza Girls ya Dar es Salaam.

Gigy Money Awapa Makavu Wanawake Wanaotembea na Wanaume za Watu

$
0
0
MWANAMUZIKI wa Bongo Fleva, Model na mtangazi, Gift Stanford ‘Gigy Money’ amewageuka wanawake wanaotembea na waume za watu huku akionyeshwa kusikitishwa kwake na kitendo hicho na kuwashauri waache tabia hiyo.



Kupitia Ukurasa wake wa instagram, Gigy ameandika waraka mrefu akiwatuhumu wanawake wa aina hiyo.



“Kama unatembea na mume wa mtu na upo huru kumpigia simu wakati wowote, anaweza hata kulala kwako na asiulizwe chochote, anaishi na wewe kama vile hana mke basi jua kuna mwanamke mwenzako anateseka na kulia kila siku. Unaweza kudhani kua huyo mwanaume ana upendo lakini ukweli nikuwa ni aina ya mwanaume ambaye ni mshenzi na mnyama kupita kiasi.



“Usidhani kwamba labda mke wake ni mjinga kwakua anavumilia, wala usije kudhani kua mke wake anamng’ang’ania huyo mwanaume. Kuna mara nyingi sana mke wake alihajaribu kuondoka lakini huyo mwanaume akamtishia, labda alishamuambia “Ukiondoka niachie wanangu, ukiondoka nakuua,



“Najua unadhani kwamba anakupenda labda ukimpindua huyo mke wake basi wewe utakua na furaha! Hapana hata akikuoa leo jua kua mwanaume kama huyo ashakua teja wa kunyanyasa, mkewe akiondoka akabaki na wewe basi jua kuwa wewe ndiyo utakua mtu wake wa kunyanyasa na atatafuta mwanamke mwingine kama wewe ili kula naye raha. Ndiyo mwanaume kama huyo anachukulia mke wake kama choo.



“Kwamba anakula raha kwengine lakini takataka zake anaenda kuweka kwa mkewe. Kwa maana hiyo akikuoa wewe basi jua ataendelea kula raha kwengine na wewe utakua ndiyo choo chake. Huna ujanja wowote, huna uzuri wowote wala hivyo viuno au mganga uloenda havijamchanganya, hiyo ni tabia yake hivyo wakati ukifurahia mwanamke mwenzako analia na kumuita mshamba usilogwe ukachukua nafasi ya mkewe kuna mwingine nawe atakuita mshamba.”

Soma Nafasi za Ajira Zilizotangazwa Leo

$
0
0

OFA!OFA!OFA Je Umepungukiwa Nguvu za Kiume na Umetumia Dawa Bila Mafanikio?

$
0
0
OFA!OFA!OFA je umepungukiwa nguvu za kiume na umetumia dawa bila mafanikio? sasa utapona kwa sh 15000 tu ofa ni kwa watu kumi wakwanza kila siku ofa hii itadumu ndani ya wiki 2 baada ya hapo bei itakuwa nyingine na kama hujapona tunakurudishia hera yako !

Dawa hii ni dawa ya maajabu huwezi kuamini Ila wengi wameiamini, inatibu tatizo la upungufu wa nguvu za kiume na utapewa garantee ya mwezi mmoja dawa hii inapatikana hapo hapo ulipo nyumbani kwako na tutakupatia maelezo ya namna ya kuiandaa wewe mwenyewe na baada ya kuiandaa utakunywa Mara moja tu,na hautatumia dawa yoyote ya nguvu za kiume dawa hii inawafaaa watu kuanzia miaka 18 mpaka miaka 70 zaidi ya miaka hyo haitakusaidia ni dawa ya asilia haina madhara yoyote.

Watafiti na waganga wameikubali pia hii dawa inawafaa hata wanawake wasiopata hisia za mapenzi pia tunaweza kukutumia dawa popote ulipo lakini c kwa bei ya ofa ukiitumia dawa hii unakuwa na uwezo wa kurudia tendo la ndoa zaidi ya Mara 3 bila hamu kuisha na itakufanya uwe na uwezo wa kufanya tendo la ndoa muda wowote imesaidia watu zaidi yawatu 148 ndani ya mwakammoja tangu igunduliwe Dr kiboko mganga wa tiba za jadi toka kisiwani mafia pia tunatibu magonjwa mbalimbali kurudisha mpenzi aliye kuacha,biashara iliyoyumba, kuondoa mikosi, nyota na nk maelezo zaidi

Wasiliana na Dr kiboko 0679923297
Viewing all 104795 articles
Browse latest View live




Latest Images