Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104809 articles
Browse latest View live

Hii ni Habari Njema Kwa Wale Wote Waliohangaika na Matatizo ya Magonjwa Sugu Yaliyokosa Tiba

$
0
0

"HII NI HABARI NJEMA KWA WALE WOTE WALIOHANGAIKA NA MATATIZO YA MAGONJWA SUGU NA YALIYOKOSA TIBA" sasa usikate tamaa tiba imepatikanika kwa DK. ABDALA MUSSA anatibu matatizo kama yafuatayo:

Nguvu za kiume, uzazi, kisukari, tezi dume, vidoda vya tumbo, mgongo kuuma, miguu kuwaka moto na mataizo uliyonayo

1/ITAGULA- ni dawa ya mkosi kuosha nyota, kumvuta mpenzi, mke, mume, kuua kesi na kupata kazi haraka kama umeomba maombi serikalini au kampuni binafisi unaitwa ndani ya siku mbili 2/

NINJIWE- ni dawa inayomaliza matatizo ya wanaume heshima ndani ya ndoa, kuwa na nguvu za kiume milele na kukomaza mbegu na kuwa na uwezo kufanya tendo la ndoa zaidi ya mara 5 bila kuchoka kama umezaraulika na kufanya tendo na kusinyaa uume dawa ipo dozi yake siku sita vidoge 12 pia kuna na unga inayokomaza uume ndani ya siku 7 unapona kabisa.

3/MPALALA- ni dawa ya kutibu busha miguu kuwaka moto, kiuno, kisukari.

4/NGEKEWA- ni dawa ya kuvuta wateja kwenye biashara yoyote kuwa na wateja wengi katika biashara na kuzuia chuma ulete. 4/LINGWATA- ni dawa ya punguza unene, mafuta tumbo, matiti, miguu, hipsi na kutengeneza shepu dawa hii ni ya unga ukitumia utaona mabadiliko baada ya siku 3.

5/DUBISHO- ni dawa zindiko la mwili, majumba, gari, biashara, mteja wangu huduma utaipata mahali popote ulipo kuna wanasaplai mahali ulipo kama huna muda wa kufika osifini mkoa wa dar-es-salaam, iringa, kanda ya ziwa wilaya ya bunda. angalizo kwa wateja usitume sms wala kubipu huduma yangu ni kuanzia saa 12 asubui hadi saa 12 jioni kwa wateja wa dar-es-salaam ofisi ipo buguruni na mbagala zakhem na kwa wale walio nje ya mkoa dawa hizi mtazipata kwa njia za mabasi. punguzo la bei kwa wateja 5 wa kisukari na nguvu za kiume

KWA MAWASILIANAO ZAIDI WASILIANA NA DK. ABDALA MUSSA KWA SIM NAMBA 0767-171773/ 0716-608959 WOTE MNAKARIBISHWA:

Ratiba ya Ligi Kuu Yatoka Simba na Yanga Kukutana na Yanga

$
0
0
Ratiba ya Ligi Kuu Yatoka Simba na Yanga Kukutana na Yanga
Pazia la ligi kuu ya soka Tanzania bara msimu wa 2018/19 litafunguliwa rasmi Agosti 22 kwa jumla ya timu 12 kushuka dimbani kukamilisha mechi 6 za ufunguzi ambapo mabingwa watetezi Simba watacheza na Tanzania Prison kwenye uwanja wa taifa.


Yanga itaanzia ugenini huko Morogoro Agosti 23 kucheza na timu ya Mtibwa Sugar huku Azam FC wakianza nyumbani kukipiga na Mbeya City.  Ratiba hiyo inaonesha pambano la watani wa jadi litapigwa Septemba 20 kwenye uwanja wa taifa na Simba watakuwa wenyeji wa Yanga.

Kwa upande wa timu zilizopanda ligi kuu msimu huu Alliance watacheza na Mbao FC, Biashara United wakianza na Singida United. JKT Tanzania watakipiga na KMC, African Lyon watacheza na Stand United huku Coastal Union wakicheza na Lipuli FC.

Aidha Afisa mtendaji mkuu wa bodi ya ligi, Boniface Wambura amesema mechi ya Ngao ya Jamii kati ya bingwa Simba na bingwa wa kombe la shirikisho Mtibwa Sugar itapigwa Agosti 18 kwenye uwanja wa CCM Kriumba Mwanza.

Msimu huu utashirikisha jumla ya timu 20 kutoka 16 zilizoshiriki msimu uliopita. Timu tatu zitakazoshika nafasi za chini moja itashuka moja kwa moja huku mbili zikicheza mechi na washindi wa pili na tatu wa ligi daraja la kwanza na wakifungwa wanashuka ila wakishinda wanabaki ligi kuu.

Waziri Awapiga Marufuku Wanaume Kutoa Talaka kwa Simu

$
0
0
Waziri Awapiga Marufuku Wanaume Kutoa Talaka kwa Simu
Waziri  wa Kazi, Uwezeshaji, Wazee, Wanawake na Watoto, Moudline Castico, amekemea tabia ya baadhi ya wanaume kuwataliki wake zao kupitia ujumbe wa simu.

Akizungumza na wanachama wa Jumuiya ya Wanawake wa Chama Cha Mapinduzi (UWT) katika Tawi la Kiembesamaki Unguja, Waziri Castico alisema kitendo cha kutaliki mke kwa ujumbe wa simu (SMS) ni dharau na udhalilishaji.

Waziri huyo alieleza masikitiko yake kwamba baadhi ya wanaume wanaofanya hivyo ni wale waliowezeshwa na wake zao wanaojituma, ambapo hali za waume hao zilikuwa duni wakati wakioana.

Alisema wapo wanaume wanaosaidiwa kujenga nyumba na hata kununuliwa magari na wake zao, lakini hatimaye wanawatoa thamani na kuwanyanyasa baada ya kupata wanawake wanaowaona ni wazuri zaidi.

Alieleza kuwa jambo baya zaidi ni kuacha kuwashughulikia watoto kwa kuwanyima huduma na matunzo hali inayowasukuma kuzurura mitaani na kuingia katika ajira mbaya na kusababisha wafanyiwe vitendo vya udhalilishaji.

“Dini zote zinaitambua ndoa kuwa ni kitu cha heshima na ina maadili yanayopaswa kufuatwa na watu wanaoamua kushirikiana kimaisha.

“Hata hivyo, iwapo kunatokezea sababu ya wanandoa kutengana, lazima waachane kwa wema, heshima na mafahamiano ili ihsani waliyokuwa nayo wakati wakiwa pamoja iendelee na hasa wanapokuwa wamejaaliwa kupata watoto.

“Kuacha kuna taratibu zake, akina baba mnapowapenda wake zenu muwe na busara, mnapoanza pamoja lazima muende pamoja kama unavyombembeleza siku ya kwanza.

“Sio kashakuchumia mali zako, ushakuwa na uwezo, kakununulia kigari unampelekea talaka kwenye simu,” alisisitiza waziri Castico.

Katika hotuba hiyo pia Castico aliwanasihi wanawake kuwa waaminifu kwenye ndoa zao hata pale waume zao wanapokengeuka, badala ya kutaka kulipa kisasi.

Kundi la Waasi la MRDC Latuhumu Kupambana na Jeshi la Rwanda

$
0
0
Kundi la waasi la MRDC latuhumu kupambana na jeshi la Rwanda
Mamlaka nchini Rwanda zimetupilia mbali uvumi kuhusu kuwepo ukosefu wa usalama maeneo yanayozunguka msitu wa Nyungwe, ambapo kundi jipya la waasi wa MRCD linalodai kuwa linataka kuangusha uongozi wa Rais Paul Kageme linasemekana kuwa na ngome yake.

Akiongea na wenyeji wa wilaya wa Nyaruguru, inspekta mkuu wa polisi Emmanuel Gasana alisema kuwa licha ya majambazi wachache kuvuka na kuingia Rwanda na kuwapora watu eneo moja la Nyaruguru hali hiyo ilikuwa imeshughulikiwa vilivyo na vikosi vya usalama na majambazi hao kukimbilia eneo walitoka.

Wanawake wanaotamani kugawanya uongozi
Kundi la MRCD (Rwanda Democratic Movement for Change) limetangaza rasmi uasi dhidi ya serikali ya Rwanda. Msemaji wa kundi hilo meja Callixte Sankara ameiambia BBC kwamba ni mwezi mzima sasa tangu majeshi ya kundi lake yakipigana na majeshi ya Rwanda katika msitu wa Nyungwe kusini mwa nchi hiyo ,na kwamba majeshi yao yamehusika katika mashambulizi ya mwezi uliopita katika kijiji cha Nyabimata karibu na msitu huo.

Ni machache yanayojulikana kuhusu Callixte Sankara, mtu aliyejitangaza kama naibu kamanda na msemaji wa kundi jipya la waasi la Rwanda Movement for Democratic Change.

Kenya, Rwanda zang'ara kwenye viwango vya uvumbuzi duniani
Meja Callixte Sankara, kama avyojitambulisha kwa vyombo vya habari, ni mwanajeshi aliyekuwa mshirika wa karibu wa rais Paul kagame kwenye kundi la Rwanda Patriotic Front (RPF) katika harakati za kupigania ukombozi.

Alikuwa askari mwenye cheo cha chini baada ya RPF kushinda vita vya msituni na kuchukuwa hatamu za uongozi kufuatia baada ya kifo cha rais Juvenal Hybiamamana kwenye shambulzi la ndege.

Haijulikani kwanini Meja Sankara alikosana na utawala wa kagame, lakini alifungwa jela na mahakama ya kijeshi kwa kipindi kisichojulikana kutokana na kile kilichotajwa kama utovu wa nidhamu.

Mahakama kuamua Hatima ya CUF

$
0
0
Mahakama kuamua matumaini ya CUF
Mbunge wa Temeke, Abdallah Mtolea ameweka wazi kwamba anaamini chama chao kitasimama tena upya licha ya changamoto na migogoro inayoendelea ambayo kwa kiasi kikubwa imeleta mpasuko mkubwa ndani ya chama.


Akizungumza na www.eatv.tv, Mtolea amesema kwamba bado anaamini meza ya mahakama inaweza kuwa suluhisho la migogoro ya Chama chao ambayo imedumu kwa takribani miaka mitatu sasa.

Mtolea ambaye ni Mbunge asiyemuunga mkono Prof. Ibrahim Lipumba amesema kwamba, anaamini vyama vingi vina migogoro, na kwamba  hakuna chama kisicho na migogoro kwa kuwa wanasiasa wanakuwa na mitazamo tofauti.

"Sisi tusiomtambua Prof. Lipumba kama Mwenyekiti wa CUF, tunaaamini zaidi kwenye utawala wa sheria tunaamini kwamba mahakama itatusaidia kumaliza mgogoro wetu na tutasimama kuwa wapya na  imara zaidi kama awali. Kwa sasa siwezi kutoa maamuzi ya kwamba upande flani utashinda au utashindwa ila kesi zilizopo mahakamani ndizo zitakazoamua hatima ya chama chetu. Matatizo ni sehemu ya changamoto kwenye siasa Chama kisicho na migogoro kinaweza kuwa na watu wa ajabu sana. Tupo kwenye siasa kwa kuwa tunaamini tuna mawazo tofauti na maoni tofauti, hivyo kutofautina kwa mawazo hakujawahi kuwa mgogoro wa kudumu." Mtolea

Akizungumzia kuhusu mtu mmoja (Naibu Katibu Mkuu, Magdalena Sakaya) kuonekana kuwa na mamlaka ndani ya chama chao, Mtolea amesema hayo yote yanasababishwa na udhaifu wa serikali ndiyo maana mwanamama huyo anaonekana na nguvu.

"Siyo kwamba Sakaya ananguvu ya kukiendesha chama lakini serikali kwa kuwa ni dhaifu ndiyo maana inaonekana hivyo, kwa mfanoo kitendo cha Mkurugenzi kukubali kuvuliwa uanachama kwa madiwani wetu Tanga ni udhaifu kwani fika ilikuwa inafahamika kuwa chama kina matatizo na kesi takribani 13 zipo mahakamani" Mtolea

Chama cha CUF kilianza kuwa na mgogoro mwaka 2016 baada ya Mwenyekiti wao Prof. Ibrahim Lipumba kutangaza kurejea kwenye nafasi yake ya uongozi ambayo alijiuzulu wakati wa uchaguzi mkuu wa mwaka 2015.

ESma: Naumia Sana Mama Yangu Akitukanwa Mitandaoni

$
0
0
Mwanadada Esma Platinumz, dada wa msanii mkubwa wa bongo fleva Diamond Platinumz,ameongea na waandishi wa habari wa wasafi tv na kufunguka ya moyoni kuhusu  jinsi anavyojisikia anapoona matusi katika mitandao ya kijamii kuhusu matusi yanayomuendea mama yake mzazi.

Esma anasema kuwa mara nyingi amekuwa akikaa kimya lakini kuna muda inamuumiza sana mpaka kuamua kuwajibu wanaomtukana kwa sababu hata yeye anajisikia vibaya.

Esma anasema kuwa pamoja na  yote lakini wanaona saa zingine hakuna cha kufanya kutokana na kuwa tayari wameshaingia katika mitandao ya kijamii na kujulikana hivyo wanavumilia hivyo hivyo  na hakuna jinsi ya kufanya kwa yanayotokea.

Najiskia vibaya sana na unajua mimi huwa sipendagi sana kuingilia katika maswala kama hayo,ila kuna wakati ukisoma unajikuta unashindwa kuvumilia hasira zako kwaio unajikuta unasoma na wewe unajibu pale pale.ila ni kitu ambacho kinauma sana lakini hakikwepeki kwa sababu tayari tulishaingia katika ulimwengu wa kujulikana, watu wanakujua na kukufatilia.

Takukuru Yachunguza Miradi ya Bilioni 15 Rukwa

$
0
0
Takukuru Yachunguza Miradi ya Bilioni 15 Rukwa
TAASISI ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) mkoani Rukwa, inaifanyia uchunguzi miradi minne yenye thamani ya Sh. bilioni 15.3 iliyotekelezwa kwa kukiuka sheria ya manunuzi na kuisababishia hasara serikali.

Akitoa taarifa ya utendaji kazi jana ofisini kwake mbele ya waandishi wa habari ya kipindi cha miezi mitatu kuanzia Aprili hadi Juni mwaka huu, Mkuu wa Takukuru mkoani humo, Hamza Mwenda, alisema uchunguzi huo upo katika hatua za mwisho kukamilika ili watuhumiwa waweze kufikishwa mahakamani.

Alisema uchunguzi uliofanywa mpaka sasa, umebaini kuwapo kwa upungufu mkubwa unaojirudia katika mchakato wa manunuzi, usimamizi wa mikataba na malipo kwa miradi ya umma ambayo yameilazimisha taasisi hiyo kuchukua hatua.

Mwenda aliyataja baadhi ya upungufu uliosababisha taasisi hiyo kuchukua ni pamoja na kutoandaliwa kwa ukamilifu vitabu vya zabuni wakati zabuni husika ikitangazwa.

Alisema baadhi ya zabuni zimekuwa zikitangazwa katika magazeti yasiyo na mzunguko mkubwa ama wasomaji wengi au kutangazwa katika magazeti yanayotoka mwisho wa wiki ambayo hayawafikii wasomaji ipasavyo.

Mkuu huyo wa Takukuru, alitaja upungufu mwingine kuwa ni kutofautisha kurasa yenye maelezo ya msingi ya mkataba ikiwamo bei kutofautishwa na kurasa inayotiwa saini, hali inayosababisha uwezekano wa kubadilishwa kwa taarifa za mkataba bila watia saini kuhusishwa.

Alisema taasisi hiyo imebaini kuwa baadhi ya kazi zimeanza kutekelezwa kabla hata ya mkataba husika kusainiwa kitendo kinacho kinaashiria kuna kupeana kazi kienyeji bila kufuata sheria inavyotaka.

Mwenda alisema hizo ni sababu chache miongoni mwa nyingi zinazo sababisha Takukuru kufanya uchunguzi katika miradi hiyo minne kwa kuwa kuna kila dalili ya ukiukwaji wa sheria na rushwa hali ambayo haiwezi kufumbiwa macho kutokana na kuitia serikali hasara kubwa.

Hata hivyo, aliwataka watumishi wa umma bila kujali nafasi zao, pamoja na wazabuni kuwa waadilifu na kuzingatia sheria mbalimbali  tofauti na hivyo wengi wao watafikishwa mbele ya sheria.

CUF Yaiweka Njia Panda Yanga

$
0
0
CUF Yaiweka Njia Panda Yanga
Uongozi wa klabu ya Yanga umesema hautaweza kuwatumia wachezaji wake wapya waliowasajili hivi karibuni kwenye mechi yake ya leo dhidi ya Gor Mahia ya nchini Kenya kutokana na kutokamilisha usajili wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Afrika (CAF).


Hayo yamebainishwa na Afisa habari wa Yanga, Dismas Ten na kuwataja wachezaji hao kuwa ni Deus Kaseke, Mrisho Ngasa pamoja na Mohamed Banka huku akifafanua zaidi kuwa sababu kubwa ni kutokamilika kwa baadhi ya vitu kwenye usajili wao.

"Kulitokea changamoto kwenye mfumo wa usajili hivyo hatutaweza kuwatumia wachezaji hao licha ya kuwa walitakiwa kujumuishwa kwenye mashindano ya kimataifa", amesema Dismas.

Pamoja na hayo, Dismas ameendelea kwa kusema "kucheza na Gor Mahia ni changamoto kwa maana kwamba Gor ni timu nzuri na yenye matokeo mazuri wakati wote. kwenye michezo kadhaa waliowahi kucheza hivi karibuni tumeona jinsi wanavyocheza, nasi pia tumefanya mazoezi ya kutosha lengo ni kuona timu inakaa sawa sawa kwaajili ya huu mchezo wa leo ambao unapopata matokeo unaweza kujitengenezea nafasi nzuri kwenye msimamo wa kundi kabla ya kwenda kwenye hatua nyingine".

Yanga itashuka dimbani majira ya saa 1:00 usiku kuvaana na Gor Mahia ambapo baada ya mchezo wa leo timu hizo mbili zinatarajiwa kurudiana tena Jijini Dar es Salaam Julai 19 mwaka huu kwenye uwanja wa Taifa.


Muna Akomalia Kuwa Patrick ni Mtoto wa Castro "Peter Anajua Mtoto si Wake"

$
0
0
Muna Asisi Tiza Kuwa Patrick ni Mtoto wa Castro "Peter Anajua Mtoto si Wake"
Muigiza Maarufu Bongo, Muna Love, amezungumza na waandishi wa habari leo nyumbani kwake maeneo ya Mbezi jijini Dar es Salaam na kuweka wazi jinsi ambavyo alikutana na Peter Zakaria Komu, mwanaume ambaye hivi karibuni ilisemekana kuwa ndiye baba wa mtoto wake Marehemu Patrick.



“Nilikutana na Peter jijini Mbeya tukiwa tunafanya kazi Safari Pool Table, tulikaa kwenye mahusiano kwa miezi miwili tukaingia kwenye ndoa, lakini kuna vitu nilivyokutana navyo kwenye ndoa hiyo nikaamua kuachika.



“Wakati naingia kwenye mahusiano na Peter nilikuwa nina mimba ya Casto ya miezi miwili, Casto aliikana mimba hiyo. Baadaye alirudi wakati mtoto Patrick akiwa na miaka mitatu. Kwa sababu nilizaa nikiwa kwenye ndoa na Peter ndiye alisimamia hata ubatizo ndizo picha zilizosabaa, lakini hata yeye Peter anaujua ukweli kuhusu mtoto huyo.



“Tulifanya taratubu na Casto za kubadilisha jina la mtoto pale RITA lakini kuna ugumu uliotokea, lakini tulikuwa tunaendelea kufuatilia,” amesema Muna.

Hizi Hapa Dalili za Kuwa Mtoto Wako ana Akili Kuliko za Kawaida "Genius"

$
0
0

Wazazi wengi hujivunia watoto wao walio werevu kutokana na sifa wanazopata kwa sababu ya weledi wao. Hii ni kutokana kuwa Wengi hupenda watoto wawe werevu na wako radhi kufanya chochote kuimarisha kitu kizuri katika maisha ya watoto wao.

Werevu wa mtoto unaweza kutambuliwa akiwa mdogo kisha kukuzwa kwa b; ya kumfaidi atakapokuwa mtu mzima.

Udaku Special Blog imekuorodheshea ishara, vidokezo na vitendo vitakavyokuonyesha kuwa mtoto wako ni mwerevu sana na hizi hapa ni njia 11 za kutambua iwapo mtoto wako ni ‘Genius’.

1. Kutambua Muundo na Fomu Akiwa Mchanga

Kuna watoto ambao huwa na uwezo wa kutambua muundo na fomu wakiwa wachanga. Hali hiyo inaweza kugunduliwa kutokana na jinsi mtoto anavyotumia vifaa vya michezo vya watoto, kadi, kifaa cha michezo cha ‘brick’ miongoni mwa michezo mingine.

Ikiwa mtoto anaweza kutambua na kuambatanisha muundo na fomu, basi hiyo ni ishara tosha kuwa mtoto huyo ni mwerevu sana. Kumbuka, kuna watu wazima ambao wanatatizwa sana kuambatanisha miundo na fomu!!.

2. Ari Ya Kujua Mengi Duniani

Umewahi kuulizwa na mtoto akiwa mdogo, Mfano swali kwamba “Watoto hutokea wapi?”

Kuna watoto wanaouliza na kukata kujua mambo yanayowazingira, kwa mfano chakula chao, vitu vyao vya kucheza na kadhalika, lakini mtoto mwerevu hutaka kujua jinsi kila kitu kinavyotokea na kwa nini.

Watoto werevu huwazonga wazazi wao na maswali mengi ambayo watu hudhani ni rahisi kujibu mpaka pale wanaposhindwa kupata majibu sahihi. Mtoto ambaye hutaka kujua mambo kwa kina anaonyesha kuwa yeye ni mwerevu.

03. Kujua Lugha Mapema

Watoto wanaopata maendeleo makubwa wakiwa wachanga kama kuweza kuzungumza lugha ya mama au Kiswahili vizuri ni ishara kuwa ni werevu.

Watoto hao huwa na ujuzi mkubwa wa lugha unaozidi ule wa umri wao na wanaweza kubuni sentensi zilizoboreka. Kwenye masomo ya isimu, weledi wa lugha humsaidia mtu kuwa na mawazo pana, hali inayodhibitisha kuwa ikiwa mtoto wako ameimarika kwa lugha akiwa mchanga, basi yeye ni mwerevu.

04. Kujua Maswali Ya Kitu Fulani Kwa Undani

Watoto wanaojua mambo kuhusu mada fulani kwa undani wanaonyesha kuwa ni werevu, kwa mfano mtoto mdogo kwa jina Aithamu Masoud kutoka Bukoba, aliyesisimua mitandao kwa jinsi alivyowajua marais wote wa bara la Afrika na Mawaziri ni ishara kuwa ni mwerevu.

Pia mtoto ambaye hajatimiza umri wa miaka 11 ambaye ana weledi wa mada zinazosomwa na kuangaziwa na watu wazima ni ishara kuwa yeye ni mwerevu.

05. Sifa za Uongozi

Mzazi anaweza kugundua sifa za uongozi kwa mtoto wake kutokana na jinsi anavyowapanga watoto wenzake wanapocheza au wakiwa mahali, kuandaa vitu vyake kama vitabu kwa utaratibu na ujasiri wake kwa yale anayoyafanya.

Watoto ambao huonekana wakiwa na sifa za uongozi wana nafasi ya kuwa viongozi siku za usoni na bila shaka sifa hizo ni ishara ya mtoto mwerevu.

06. Wana malengo, Uamuzi na Misimamo Dhabiti

Watoto wadogo wanaweza kushawishiwa kwa urahisi kufanya lolote, lakini mtoto asiyekubali kitu chochote anachoambiwa kwa kuamini kuwa sio nzuri kwake ni mwerevu, kwa mfano wao hukataa kushawishiwa kufanya makosa shuleni.

Watoto wanaoonyesha kufuata na kutimiza malengo na uamuzi wao bila ya kubabaika ni watoto werevu.

07. Wanapendelea Kukaa na Watu Wazima Zaidi Ya Watoto wa Umri Wao

Kuna watoto ambao utawapata kwenye vikao vya watu wazima kila mara. Wakati mwingine, wazazi wao hulazimika kuwafukuza ili waweze kusemezana mambo ya watu wazima. Hii ni ishara kuwa mtoto huyo ni mwerevu na utamwona akiendeleza mazungumzo na mtu mzima katika hali ya wastani.

Mtoto kama huyo anastahili kusaidiwa kuwapata marafiki wa umri tofauti ili kuimarisha hali yake kimawazo. Watoto hao wakati mwingi hawafurahishwi na kazi zao za darasani kwa kuwa kwao ni rahisi sana.

08. Hufanya Vizuri Masomoni

Wataalamu wa teknolojia mpya za kimatibabu zinazoangazia jeni wamedhibitisha kuwa ikiwa mtoto anafanya vizuri kwenye masomo yake, basi huenda mtoto huyo ni mwerevu sana. Uwezo wa mtoto wa kufanya vizuri katika somo la hesabu na somo la lugha ni ishara tosha kuwa yeye ni mwerevu.

9. Wana Uhalisia Wao

Watoto werevu wanakubali mawazo ya watu wengine, lakini wana mbinu na mawazo yao kuhusu jambo fulani au kuhusu jinsi ya kukifanya kitu fulani.

Watoto werevu huwa na ari na bidii ya kutafuta njia nyingine ya kutatua jambo fulani. Utamsikia mtoto akimuuliza mwalimu au wazazi wake, “Ni njia nyingine ipi tunayoweza kutumia kutatua jambo hiyo/hesabu hiyo?” Hiyo ni ishara kuwa mtoto huyo ni mwerevu.

10. Wana Udhaifu Kama Binadamu Wengine

Mtoto mwerevu atakuwa na udhaifu kwa sababu kadhaa. Anaweza kuwa na udhaifu kwa jambo fulani kwa kuwa yeye ni mtoto na kuna mambo ambayo atakosea.

Yawezekana kuwa mwanao ni gwiji kwenye somo la hesabu, lakini somo la sayansi linamtatiza. Watoto werevu wanaweza kuwa udhaifu wa kutojali, kutatizika kiakili na kukosa ujuzi wa kawaida.

11. Wanapenda Kusoma

Watoto werevu hupenda kusoma na hujifunza kusoma haraka kuwalika wenzao walio na umri sawa.

Kimenuka..Lugola Amvaa Kamanda Sirro, Ampa Wiki Mbili

$
0
0

WAZIRI wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola, amempa wiki mbili Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini (IGP) Simon Sirro, amweleze kama Jeshi la Polisi limenyoosha mikono kwa majambazi.

WAZIRI wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola, akisalimiana na Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini (IGP) Simon Sirro.

Lugola alitoa kauli hiyo jana jijini Dar es Salaam, wakati akiwa katika ziara ya kikazi Makao Makuu ya Kikosi cha Kutuliza Ghasia (FFU), kilichopo Ukonga ambako pia aliongea na askari wa kikosi hicho.

“Ninamwagiza Mkuu wa Jeshi la Polisi ndani ya wiki mbili afike ofisini kwangu na timu ya makamishna alionao Makao Makuu ya Polisi, aniambie huu uchumi wa kati ambao Rais amelenga tuufikie, mahusiano yake na Jeshi la Polisi:

“Aniambie Watanzania tunataka wafanye shughuli za kiuchumi saa 24, hatuwezi kufikia malengo ya uchumi wa kati kama Watanzania watafanya kazi saa 12 au nane,” alisema.

Alimtaka IGP pia amweleze iwapo hatua ya mabasi kutokutembea usiku imewashinda na kunyoosha mikono kwa majambazi.

“Biashara zinafungwa saa 12 jioni ukiuliza wanasema ni kwa sababu ya usalama, IGP aje aniambie Jeshi la Polisi limenyoosha mikono kwa majambazi?” Alihoji.

Waziri Lugola aliongeza “Hatuwezi tukakubali kupewa amri na majambazi wakatupangia ni saa ngapi tufanye shughuli za kiuchumi au ni maeneo gani twende au tusiende,” alisisitiza.

Nipashe ilipomtafuta kwa njia ya simu IGP Sirro, kuhusu kupokea agizo hilo, simu yake iliita bila kupokelewa.

Muna: Wakati naingia kwenye mahusiano na Peter nilikuwa nina mimba ya Casto

$
0
0

Muigiza Maarufu Bongo, Muna Love, amezungumza na waandishi wa habari leo nyumbani kwake maeneo ya Mbezi jijini Dar es Salaam na kuweka wazi jinsi ambavyo alikutana na Peter Zakaria Komu, mwanaume ambaye hivi karibuni ilisemekana kuwa ndiye baba wa mtoto wake Marehemu Patrick. 

“Nilikutana na Peter jijini Mbeya tukiwa tunafanya kazi Safari Pool Table, tulikaa kwenye mahusiano kwa miezi miwili tukaingia kwenye ndoa, lakini kuna vitu nilivyokutana navyo kwenye ndoa hiyo nikaamua kuachika. 

“Wakati naingia kwenye mahusiano na Peter nilikuwa nina mimba ya Casto ya miezi miwili, Casto aliikana mimba hiyo. Baadaye alirudi wakati mtoto Patrick akiwa na miaka mitatu. Kwa sababu nilizaa nikiwa kwenye ndoa na Peter ndiye alisimamia hata ubatizo ndizo picha zilizosabaa, lakini hata yeye Peter anaujua ukweli kuhusu mtoto huyo. 

“Tulifanya taratubu na Casto za kubadilisha jina la mtoto pale RITA lakini kuna ugumu uliotokea, lakini tulikuwa tunaendelea kufuatilia,” amesema Muna. 

Hii Hapa Dawa Bora ya Nguvu za Kiume na Maumbile Madogo ya Uume

$
0
0
Tatizo hili limekuwa likiwaadhiri watu wengi sana kisaikolojia hasa baada ya kujiona wapo tofauti sana na wengine kwa kawaida mwanaume anatakiwa awe na uume kuanzia nchi 6-8 kwanza upungufu wa vichocheo hivi huchochea ukuaji wa uume chongo ambalo hushambulia nerve ambayo uharibu kabisa ukuaji wa uume, ngiri, punyeto, ambayo huathili misuli ya uume, ngiri huleta maumivu, tumbo kuunguruma na kujaa gesi, korodani moja kuvimba, kutopata choo vizuri, sababu hizi hufanya uume kulegea na kusinyaa na kuwa mfupi na mwembamba na mara nyingi hata nguvu za kiume ( hamu ya tendo la ndoa) hupungua na kwisha kabisa

GEMBE :Ni dawa inayozalisha na kukufanya uume kukua na kuongezeka
NGEMO : Ni dawa bora ya kuongeza nguvu za kiume

Hukutia hamu ya kuludia tendo la ndoa zaidi mara4 nne bila kukinai au kuchoka pia itakufanya uchelewe kufika kileleni zaidi ya dk30-45 kwa mtumiaji pia tunatibu kisukari, bp, ngiri, miguu kuwaka moto KAMA HUNAMDA WA KUFIKA OFISINI KWETU UTALETEWA POPOTE TUPO MBAGALA RANGI TATU

 0753471612/ 0715249530
0623 386 305

DR KUZENZA

Shilole Aingilia Sakata la MunaLove "Sijawahi Kuona Mwanamke Mwenye Roho Ngumu Kama Muna”

$
0
0
Wiki mbili zimepita tokea muigizaji Munalove ampumzishe mwanae  Patrick katika nyumba yake ya milele na hivyo leo July 18,2018 kwa mara ya kwanza amezungumza na waandishi wa habari kuhusiana na ugonjwa uliokuwa ukimsumbua mwanae pamoja na baba mzazi wa Marehemu Patrick.

Kupitia ukurasa wa instagram wa Shilole ameonyeshwa kuchukizwa na kitendo alichokifanya Munalove cha kuita na kuzungumza na waandishi wa habari na kusema kuwa hajawahi kuona mwanamke kama Muna

“Hakuna siku nimevurugwa kama Leo, hakuna mwanamke wa namna hii kwenye hii Dunia!!! Sijawahi kuona mwanamke mwenye roho ngumu kwenye hii Dunia kama munah!!..😢😢😢😢#YouGirlUtapataTabuSanaaaa!!!”

Sakata la Mchezaji wa Yanga Kelvin Yondani Lamfungua Mdomo Haji Manara

$
0
0
Moja kati ya stories zinazochukua headlines kwa sasa katika soka la bongo ni ishu ya usajili wa wachezaji kutoka club moja kwenda nyingine, imekuwa kawaida duniani kote mchezaji fulani kuhusishwa kwenda club fulani.

Kwa sasa kwa Tanzania moja kati ya wachezaji wanaohusishwa kuhama vilabu vyao ni beki wa Yanga aliyemaliza mkataba wake Kelvin Yondani ambaye anahusishwa kwenda Simba SC, baada ya tetesi kuwa nyingi afisa habari wa Simba Haji Manara ameandika maneno haya kupitia ukurasa wake wa instagram kwa wanaomuuliza kuhusiana na ishu hiyo.

“Shida yangu mimi ni moja tu…jambo linazushwa halafu napigiwa eti nithibitishe!! Kawaulizeni waliotoa taarifa hii..Simba haipo na mimi ndio spokesman wa klabu”>>> Haji 

Muna: Wakati Naingia Kwenye Mahusiano na Peter Nilikuwa Nina Mimba ya Casto

$
0
0
Muna: Wakati naingia kwenye mahusiano na Peter nilikuwa nina mimba ya Casto
Muigiza Maarufu Bongo, Muna Love, amezungumza na waandishi wa habari leo nyumbani kwake maeneo ya Mbezi jijini Dar es Salaam na kuweka wazi jinsi ambavyo alikutana na Peter Zakaria Komu, mwanaume ambaye hivi karibuni ilisemekana kuwa ndiye baba wa mtoto wake Marehemu Patrick.

“Nilikutana na Peter jijini Mbeya tukiwa tunafanya kazi Safari Pool Table, tulikaa kwenye mahusiano kwa miezi miwili tukaingia kwenye ndoa, lakini kuna vitu nilivyokutana navyo kwenye ndoa hiyo nikaamua kuachika.

“Wakati naingia kwenye mahusiano na Peter nilikuwa nina mimba ya Casto ya miezi miwili, Casto aliikana mimba hiyo. Baadaye alirudi wakati mtoto Patrick akiwa na miaka mitatu. Kwa sababu nilizaa nikiwa kwenye ndoa na Peter ndiye alisimamia hata ubatizo ndizo picha zilizosabaa, lakini hata yeye Peter anaujua ukweli kuhusu mtoto huyo.

“Tulifanya taratubu na Casto za kubadilisha jina la mtoto pale RITA lakini kuna ugumu uliotokea, lakini tulikuwa tunaendelea kufuatilia,” amesema Muna.

Pata Tiba ya Tatizo la Nguvu Za Kiume, nasaidia Kukufanya Urudie Mara 5 na kuchelewa kwa Dakika 20

$
0
0
TATIZO LA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME NA MAUMBILE MADOGO LINATIBIKA.Baada ya utafiti wa mda mrefu juu ya matatizo ya upungufu wa nguvu za kiume na ukosaji wa hamu ya tendo la ndoa ama kushindwa kurudia tendo kwa haraka DR Magise imekuletea tiba ya matatizo hayo kwa kutumia dawa za:

GUMBA POWER:Ni dawa asili ya vidonge inayotibu tatizo la upungufu au ukosefu wa nguvu za kiume,dawa hii inamchanganyiko wakutosha wenyekuzalisha vichocheo vingi vya Hemone za Gestrogen vikiwemo vitamin B6&B1,vitamini E,pamoja na madini aina ya zinc vitakufanya kuwa na nguvu na mzunguko mzuri wa damu na kuongeza hamu na uwezo wa kufanya tendo la ndoa zaidi ya hatua nne au zaidi,na kuchelewa kufika kileleni zaidi dakka 20-30.

NTINJE:Inarutubisha maumbile ya uume yani kurefusha na kunenepesha nchi 4-7 upana cm3-4 standard kiafya haijalishi umri wako hata kwa wazee ukiitumia maumbile yako yatabaki kuwa hivyo siku zote,Pia tunatibu Presha,kisukari siku7,ngiri,chango la tumbo tumbo kujaa gesi,kutopata choo vizuri

 TUPO TZ DAR ES SALAAM   MBAGALA RANGI TATU.HUDUMA HII UTALETEWA POPOTE ULIPO .WASILIANA NAMI 0754741788, 0715741788, 0783741788

-DR MAGISE

Muna Love Amruka Steve Nyerere Aanika Sauti Zake " Sijamkubalia Steve Msiba Ufanyike kwa Peter"

$
0
0
Kimenuka Muna Love Amruka Steve Nyerere Aanika Sauti Zake " Sijamkubalia Steve Msiba Ufanyike kwa Peter"
Muigizaji maarufu Bongo, Muna Love ameanika wazi maongezi yake aliyozungumza na muigizaji mwenzake, Steve Nyerere wakati alipokuwa Kenya akishughulika kusafirisha mwili wa mwanaye, marehemu Patrick.



Kufuatia sauti hiyo Muna amekanusha taarifa iliyotolewa na Steve Nyerere akisema kwamba amekubali msiba ufanyike Mwananyamala katika nyumba anayoishi Peter Zacharia Komu.

Kimenuka Yanga Mkwasa Ajiuzuru Nafasi ya Ukatibu Mkuu

$
0
0
Inaelezwa kuwa Katibu Mkuu wa mabingwa wa kihistoria wa ligi kuu soka Tanzania Bara klabu ya Yanga, Charles Boniface Mkwasa ameamua kujiuzuru nafasi yake ndani ya timu hiyo kongwe nchini.



Mkwasa ametangazwa kuwa Katibu Mkuu wa klabu hiyo mnamo Februari 1 mwaka 2017 na kujaza nafasi iliyoachwa wazi kwa muda mrefu iliyokuwa ikikaimiwa na Baraka Deusdedith baada ya kuondoka kwa Dkt. Jonas Tiboroha.

Charles Boniface Mkwasa aliwahi kuwa kocha wa klabu hiyo kabla ya kuwa kocha wa Taifa Stars.

Na Klabu ya Yanga imemuita beki wake wake, Kelvin Yondani pamoja na Hassan Kessy kwaajili ya mazungumzo baada ya kuwepo na uvumi wa wachezaji hao huenda wakajiunga na mabingwa wa ligi kuu soka Tanzania Bara msimu 2017/18.



Habari zisizo rasmi zinaeleza kuwa Yondani alishamalizana na Simba kilichobaki ni kukabidhiwa kitita cha fedha tu ili kusaini mkataba lakini uongozi wa Yanga wanapambana kufa na kupona ili kuhakikisha dili hilo halikamiliki.

Ikumbukwe kuwa wachezaji hawa wote wawili wanao husishwa na kutimkia Simba hawajasafiri kwenda nchini Kenya kuikabili Gor Mahia kwenye mchezo wa kombe la shirikisho.

Haji Afunguka Kuhusu Simba Kumsajili Kelvin Yondani

$
0
0
Haji Afunguka Kuhusu Simba Kumsajili Kelvin Yondani
Moja kati ya stories zinazochukua headlines kwa sasa katika soka la bongo ni ishu ya usajili wa wachezaji kutoka club moja kwenda nyingine, imekuwa kawaida duniani kote mchezaji fulani kuhusishwa kwenda club fulani.

Kwa sasa kwa Tanzania moja kati ya wachezaji wanaohusishwa kuhama vilabu vyao ni beki wa Yanga aliyemaliza mkataba wake Kelvin Yondani ambaye anahusishwa kwenda Simba SC, baada ya tetesi kuwa nyingi afisa habari wa Simba Haji Manara ameandika maneno haya kupitia ukurasa wake wa instagram kwa wanaomuuliza kuhusiana na ishu hiyo.



“Shida yangu mimi ni moja tu…jambo linazushwa halafu napigiwa eti nithibitishe!! Kawaulizeni waliotoa taarifa hii..Simba haipo na mimi ndio spokesman wa klabu”>>> Haji Manara

Viewing all 104809 articles
Browse latest View live




Latest Images

<script src="https://jsc.adskeeper.com/r/s/rssing.com.1596347.js" async> </script>
<script src="https://jsc.adskeeper.com/r/s/rssing.com.1596344.js" async> </script>