Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104799 articles
Browse latest View live

Download Hapa Application ya Udaku Special Kwenye Simu Yako Kushuhudia Vimbwanga Mtaani na Stori za Mapenzi


Steve Nyerere Awacharukia Wanaombeza Kukosa Ukuu wa Wilaya

$
0
0
Baada ya mwanamitindo Jokate Mwegelo pamoja na aliyekuwa msemaji wa Yanga Jerry Murro kuteuliwa na Rais Magufuli kuwa Wakuu wa Wilaya, mashabiki na wadau katika mitandao ya kijamii wanambeza Steve Nyerere kwa kuwa amekosa kuteuliwa.


Muigizaji huyo amekuwa akionekana katika matukio mengi akitetea utendaji wa Rais Magufuli hali ambayo iliwajenga picha mashabiki hao kwamba anataka nafasi ya uongozi..

Steve baada ya kupokea meseji nyingi za kubezwa, amedai yeye hamsupport Rais Magufuli ili apewe nafasi ya uongozi anafanya hivyo kwaajili ya kusaidia na kuunga mkono harakati zeke.



“Mnao nitumia meseji za pole naomba iwe mwisho sasa. Sipo kwa ajili ya cheo nipo kwa ajili ya Watanzania kwanza mengine no, msinilishe maneno,” aliandika Steve Nyerere kupitia Instagram yake.

Muigizaji huyo alikuwa mmoja kati ya wasanii ambao walimpigania Rais Magufuli katika uchaguzi mkuu uliopita.

Kutana na Sharifu Seif Mohammed Mtaalam wa Tiba za Asili Tanzania

$
0
0

Wasiliana na Mtaalam Huyu Kwani yeye hufaulu Pale wote waliko Shindwa na Pia Humaliza kazi zilizo Shindikana ama Zilizo Achwa ndani ya Siku Moja 1. 



Sharifu seif Mohammed ANAWASHUKURU WALE WOTE WANAOPIGA SIMU ZA SHUKRANI NA KUTOA SHUHUDA JINSI TIBA ZAKE ZINAVYO SAIDIA(Rudisha Mahusiano yako Ndani ya Saa 12 tu) 



Sharifu seif Mohammed ni Mtabibu wa Nyota za Binadamu na Dawa za Asili Mwenye Uwezo wa Kubaini Tatizo lako tu Pindi Utakapo Fanya Mawasiliano Kupitia Wasaa Husika. 

(NA ANATIBU KWA NJIA YA SIMU UKIWA NCHI YOYOTE MKOA WOWOTE ENDAPO UTAFATA MAELEKEZO YAKE..) Je Unasumbuliwa na Mapenzi..? 

Umeachwa na UMPENDAE Awe Mume/Mke na Bado Unampenda Je Umejaribu Sehemu Nyingi Bila Mafanikio? Mpigie Simu sasa Hivi Ujionee Muujiza wa Papo kwa Papo.. Anauwezo wa Kurudisha Mahusiano yako na Kuimarisha NDOA Ndani ya saa 12 tu. 

Je Umekimbiwa na Mumeo/Mkeo au Mpenzi na Anaishi na Mtu Mwingine..? 

Muone akutatulie Anauwezo wa Hali ya Juu wa Kusambalatisha Mahusiano yao (Mfarakano/Kimavi) Endapo Utafata Atakacho Kuelekeza. 

Je Una Mpenzi wako ana Pesa na unataka Kumkamata? Muone Maalim khatibu Atamfanya Atimize Ahadi zote Ndani ya Muda Mfupi.. Sharifu seif Mohammed Anatumia Jina La Muhusika au Picha Kumaliza Tatizo.. 

Anatibu Kutumia QUR_AN DAWA ZA ASILI YA AFRICA, Dawa za KIARABU NA MAJINI.. 

ANATAFSIRI NDOTO. ANAPANDIKIZA NYOTA YA KUSHINDA BAHATI NASIBU, KUSAFISHA NYOTA NA KUKUPA MVUTO WA AJABU, KUTOA NUSKI NA VIFUNGO MBALIMBALI. 

ZINDIKO ZA NYUMBA NA BIASHARA.. PETE ZA BAHATI.. HUMALIZA KABISA TATIZO LA NGUVU ZA KIUME NA KUREFUSHA UUME KWA SAIZI UNAYOTAKA. HUZUIA CHUMA ULETE KWENYE BIASHARA. HURUDISHA MALI ZILIZOPOTEA.. 

MAGONJWA SUGU, MIGUU KUWAKA MOTO AU KUFA GANZI, HUTIBU BUSHA BILA KUPASUA..ANAO UWEZO WA KUMRUDISHA  ALIE MBALI AU ALIECHUKULIWA MSUKULE.. 

Humaliza Kesi ya Aina Yoyote Ndani ya Siku 7 tu.. 

Hutoa Jini la MALI kwa wale Wanao Hitaji Utajiri Bila Masharti.. Kwa mawasiliano na ushauri zaidi 



Mobile + 255 654 836970 

WhatsApp +255 756 033670 

NB: Ni vyema kupiga simu kuliko kutuma sms ili upate huduma kwa haraka

Jokate Afunguka Kwa Mara ya Kwanza Baada ya Kuteuliwa na Rais Kuwa Mkuu wa Wilaya

$
0
0

From Jokate - Amini Mungu ni mwingi wa rehema kamwe hamtupi amtumainiye yeye!! Ahsante Mungu Wangu.

Labda ni-share kitu kidogo, kuna muda mwaka jana mwishoni nilikuwa so down nilitamani kukata tamaa na kila kitu kwenye maisha nilikuwa pia sijaelewa vizuri hatma yangu kwenye siasa. Nilikuwa kwenye mkutano mkuu wa chama kuna mdada mmoja kutoka Arusha akanikimbilia na kunikumbatia kwa nguvu sana alikuwa na mama mmoja hivi walikuwa wamekuja kupiga picha namimi. Huyo dada mdogo hivi akasema ananipenda sana sana na mimi ndio nilimfanya aingie kwenye siasa na akagombea nafasi kupitia mkoa wa Arusha akashinda!! Nikabaki natabasamu. Ikanipa nguvu kubwa ya kupiga moyo konde na kusonga mbele. Nilifurahi kuona kuna mdada nimeweza kumhamasisha na kumpa ujasiri wa kugombea. Unaweza ukawa unapitia mitihani migumu sana kwenye maisha yako lakini inakubidi usikate tamaa saa zingine kwasababu tu ya wale wanaokutegemea, wanaokuangalia na kuvutiwa nawe na kujifunza kupitia maisha yako. Lakini zaidi kwasababu safari ya mafanikio ina milima na mabonde, inabidi upambane na kiukweli hakuna mafanikio yasiokuwa na changamoto. Na kuna muda changamoto ndio haswa zinatengeneza “character” zetu. .

Kikubwa zaidi wakati wa changamoto tukumbuke kuwa wanyenyekevu, wenye kujishusha na kumuomba Mungu aendelee kutupa imani, hekima na busara ya kusubiri wakati wake. Tukumbuke Mungu hamtupi mja wake. Nawatakia Jumapili Njema. Nawapenda Sana. Ahsanteni

Aliyeachiwa Huru Kesi ya mauaji ya bilionea Msuya Asimulia Mambo Mazito Aliyokutana Nayo Gerezani

$
0
0

Wakati Shwaibu Jumanne akitafakari jinsi ya kuanza tena maisha uraiani, mambo mawili bado yanamtesa baada ya kukaa mahabusu kwa miaka mitano.


Jumanne, maarufu kwa jina la Mredii, ndiye pekee aliyeepuka hukumu ya kifo wakati Mahakama Kuu ilipotoa hukumu dhidi ya watu sita walioshtakiwa kwa kosa la kumuua mfanyabiashara maarufu wa Mirerani mkoani Manyara, Erasto Msuya.


Washtakiwa wenzake watano wamehukumiwa kunyongwa hadi kufa, lakini Mredii amerudi uraiani akitafakari maisha mapya baada ya kusimama kazi yake ya uchimbaji madini kwa miaka mitano.


Hata hivyo, tafakuri hiyo inakabiliwa na kumbukumbu mbaya ya tukio lake; kuanzia alipokamatwa hadi maisha ya mahabusu.


“Moja ya mambo ambayo sitakaa niyasahau ni maumivu niliyoyapata wakati nilipokamatwa,” anasema Mrediii katika mahojiano maalumu na Mwananchi baada ya kuachiwa huru.


“Kipigo nilichokipata mikononi mwa polisi kimemsababishia kilema na maumivu.”


Pamoja na kwamba hakusema bayana katika mazungumzo na Mwananchi, Mredii aliiambia mahakama wakati wa utetezi kuwa aliteswa na polisi hadi kupewa ulemavu, ikiwamo kuhasiwa.


Kutokana na kuhasiwa, Mredii alidai aliamua kumpa talaka mmoja ya wake zake, aliyemtaja kuwa ni Zuhura Hassan kwa vile alikuwa hana uwezo tena kama mwanamume. Amebakiwa na mkewe anayeitwa Adile Juma.


Akiongozwa na wakili wake Majura Magafu kutoa utetezi wake, Mredii alidai mbali na kuhasiwa, polisi walimvunja mara mbili mguu wa kushoto na mara moja mguu wa kulia.


Alisema wakati fulani walimfunga kamba na kumning’iniza kama mbuzi aliyebanikwa.


“Kwa hayo mateso niliyopata hapo kituoni nimekuwa mlemavu. Niliwekwa staili ya mbuzi anayechomwa nikiwa sina nguo,” alidai mahakamani.


Katika mahojiano maalumu na Mwananchi, Mredii alisema hakupata matibabu mazuri kutokana na kipigo hicho na kwamba kwa vile sasa yuko huru, moja ya vipaumbele vyake ni kupata matibabu sahihi ya afya yake.


Anasema jambo jingine ambalo hatalisahau ni kulazimishwa kulala saa 9:00 alasiri na kufungiwa vyumbani hata kama huna usingizi. “Wakati mwingine watu wako nje kwenye shughuli zao, lakini sisi tunalazimishwa kulala,” alisema Mredii.


“Hili jambo haliwezi kutoka kwenye akili yangu kwa haraka na litanisumbua kwa muda mrefu sana.


“Kuanzia saa 9:00 (alasiri) mtu unafungiwa ndani, unaambiwa ulale. Kwa kweli yale yalikuwa mateso makubwa kwangu. Halafu chumba kimoja tunalala watu 18 hadi 27. Kwa kweli sitakaa niyasahau maisha haya.”


Hali hiyo ndiyo inamfanya ashauri vijana na watu wengine kutojihusisha na mambo ambayo yanaweza kusababisha wapelekwee gerezani.


“Waepuke kufanya jambo lolote litakalowafanya wapelekwe gerezani kwa kuwa kule ni mahali pa kudhalilisha sana,” anasema.


“Mtu unapokuwa gerezani unakuchukuliwa kama mhalifu na unapokuwa kwenye lile karandinga watu wanaona wewe ni mhalifu na wengine wanakuita mwizi bila kujua ni kosa gani limekupeleka gerezani.


“Lipo suala la matitabu. Mtu anapewa matibabu ya kawaida bila kujali tatizo linalomkabili na ikitokea wakaamua kukupeleka Hospitali za Rufaa nje ya magereza ni kwamba mtu utakuwa umezidiwa.


“Mimi mwenyewe nimetoa matatizo yangu ikiwemo tatizo la vidonda vya tumbo, lakini sijawahi kupimwa licha ya kuomba sana nipelekwe kwenye vipimo ili kujua vidonda vimefikia hatua gani.


“Nimekuwa nikitumia dawa bila kujua (kama) ndizo zinatibu. Sasa natakiwa kwenda kwenye vipimo kwa kuwa kipindi cha miaka mitano nimekaa gerezani (vidonda vya tumbo vimekuwa sugu hasa (kwa kuwa) kule mlo ni mmoja.”


Hukumu ya Mredii na wenzake; Sharifu Mohamed, aliyekuwa mshtakiwa wa kwanza, Musa Mangu (wa tatu), Karim Kuhundwa (wa tano), Sadik Mohamed (wa sita) na Ally Mussa (wa saba), ilitolewa Julai 23 na Jaji Salma Maghimbi.


Walishtakiwa kwa mauaji ya Msuya, maarufu kwa jina la Bilionea Msuya, aliyeuawa Agosti 7, 2013 kwa kupigwa risasi eneo la Mijohoroni wilayani Hai.


Lakini wakati Jaji Maghimbi aliwapa adhabu ya kifo washtakiwa watano, alimuachia huru Mredii baada ya kutoridhika na hoja za kutaka atiwe hatiani.


Jaji Maghimbi alisema ushahidi wa mashahidi wa upande wa mashitaka haukuweza kuthibitisha shitaka dhidi ya Mredii, hivyo kuamua kumuachia huru.


‘Sikuhusika kupanga wala kushiriki mauaji ya Erasto Msuya na naomba jamii inipokee” alisema Mredii katika mahojiano na Mwananchi.


Anasema uhusiano wake na baadhi ya watu umekuwa ukimtia matatizoni na vyombo vya dola.


“Mwaka 2000 niliwahi kutuhumiwa kwa kosa la mauaji porini Mirerani lakini baada ya upelelezi, nilionekana sikuhusika na kuachiliwa baada ya kukaa mahabusu miezi sita,” alisema Mredii.


“Na hii naona inaweza kusababishwa na hisia kwa kuwa hata tukio linalonikabili naona linaweza kuwa watu wanaangalia ukaribu wangu na watu kwa kuwa Mjeshi ni shemeji yangu.


“Sharifu ni mfanyabiashara ambaye nimekuwa nikimpelekea mawe na hii inaweza kuwa ndiyo iliyosababisha nikahusishwa na matatizo hayo. Lakini namshukuru Mungu na jaji.


“Hakika nilifurahi sana sana kuachiwa na naamini jaji alitumia waledi wake wa kazi kwa kuona kuwa mimi sihusiki na tukio lile, na ukweli ni kwamba mimi sihusiki.” Anasema sasa ana amani kwa kuwa yuko huru.


“Unapokuwa huru, hata kama huna chochote unakuwa na amani. Sitamani kurudi gerezani kwa sababu maisha kule ni magumu sana,” anasema Mredii mwenye watato wanne.

Chanzo: Mwananchi

Rais Magufuli Atoa Pole Kwa Mwanahabari Eric Shigongo Kwa Kufiwa Na Mama Yake Mzazi Jijini Dar Es Salaam Leo

$
0
0

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli na mkewe Mama Janeth Magufuli wakitoa heshima za mwisho wakiwa na  Mkurugenzi Mkuu wa Makampuni ya Global Group Eric Shigongo ambaye amefiwa na mama yake Mzazi Bi Asteria Kahabi Kapela walipofika kuwafariji msibani Mikocheni B jijini Dar es salaam leo Julai 29, 2018


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiweka saini kwenye kitabu cha maombolezo wakati yeye na  mkewe Mama Janeth Magufuli walipofika  msibani Mikocheni B jijini Dar es salaam leo Julai 29, 2018  kutoa   pole kwa Mkurugenzi Mkuu wa Makampuni ya Global Group Eric Shigongo ambaye amefiwa na mama yake Mzazi Bi Asteria Kahabi Kapela

Polisi Kilimanjaro yaanzisha msako wa mashine feki

$
0
0

Bodi ya michezo ya kubahatisha imetekeza kwa moto mashine feki 12 za mchezo huo ambazo zimekamatwa katika wilaya za rombo, moshi vijijini na manspaa ya moshi mkoani kilimanjaro baada ya kuiangizwa nchini visivyo halali. 

Meneja wa Ukaguzi na Udhibiti wa Bodi hiyo Sadiki  Elimsu amesema, wamiliki  wa mashine hizo zenye thamani ya shs. 24mil/=  ambazo pia hazina viwango  wametoroka  na juhudi zinafanywa na jeshi la polisi mkoani kilimanjaro za  kuwatia mbaroni. 

Elimsu amesema, wamiliki wa mashine hizo pia  walikuwa wakiichezesha mchezo huo bila kulipia kodi na kuikosesha serikali mapato ya zaidi ya shs. 100mil/= kwa mwaka mmoja uliopita. 

Kamanda wa polisi mkoani kilimanjaro kamishna msaidizi wa polisi Hamisi Issa amesema, jeshi la polisi limeanzisha msako mkali wa kuwatafuta wamiliki hao ambao wanafahamika ili wafikishwe mahakamani kwa kuingiza mashine hizo kinyemela na kuikosesha mapato serikali.

Niyonzima aiacha Simba njia panda, viongozi wamtafuta bila mafanikio

$
0
0

KIUNGO mchezeshaji wa Simba Mnyarwanda, Haruna Niyonzima ni kama ameikacha kiaina kambi ya timu hiyo ni baada ya viongozi kulalamika kutopokea simu kila wakimtafuta hewani. 

Kiungo huyo alitakiwa kuwepo kwenye msafara wa wachezaji wanne waliosafiri juzi kuelekea Uturuki kujiunga na wenzao lakini hakuwepo huku wenzake, Said Ndemla, Hassani Dilunga, Meddie Kagere na Erasto Nyoni wakiwa wametua na kuanza kujifua. 

Mnyarwanda huyo alijiunga na Simba kwenye msimu uliopita wa Ligi Kuu Bara akitokea Yanga baada ya mkataba wake kumalizika wa miaka miwili. 

Kwa mujibu wa taarifa ambazo imezipata Championi Jumamosi, kiungo huyo bado yupo nyumbani kwao Rwanda alipokwenda kwenye mapumziko, hivyo bado hajajiunga na kambi ya Uturuki kama inavyoelezwa. 

Mtoa taarifa huyo alisema, kiungo huyo alitakiwa kuripoti Dar wiki moja iliyopita kabla ya timu kuelekea Uturuki, lakini alikaidi agizo alilopewa na uongozi na sababu ni kibali chake cha kuisafiria ‘paspoti’ kumalizika. 

“Awali, Niyonzima alituambia kuwa paspoti yake imemalizika tukamuambia atutumie kwa ajili ya kumtengezea mpya akatutumia, lakini tangu alipotutumia ikawa kimya. 

“Tumejaribu kumtafuta mara kwa njia ya simu kwa kumpigia wakati mwingine simu inaiita lakini haipokelewi, tukimtafuta wakati mwingine simu yenyewe haipatikani, hivyo tunashindwa kumuelewa. 

“Inavyoonekana kama hataki kujiunga na kambi ya Uturuki, hivyo kama uongozi tumeona tuachane naye atakapojisikia kujiunga na timu atakuja kwa sababu yeye anafahamu kabisa timu ipo kwenye ‘pre season’ alitakiwa kuwa na timu pamoja,” alisema mtoa taarifa huyo. 

Alipotafutwa Niyonzima kuzungumzia hilo simu yake mkononi ilikuwa haipatikani na alipotafutwa kwa njia ya mtandao wa kijamii wa ‘WhatsAp’ meseji yake haikufika kujibu hilo.

Chadema ni Kampuni ya Watu Binafsi, Mwita Waitara Atoboa Siri

$
0
0

Mwita Waitara anasema bado Chadema sio taasisi bali ni kampuni ya watu binafsi, kuna shida nyingi ndani ya chama wabunge na wanachama wake hawasemi" .
***Aliyasema hayo Mwita Waitara Jana katika press conference na waandishi wa habari

Hii Hapa Dawa Bora ya Nguvu za Kiume na Maumbile Madogo ya Uume

$
0
0

Tatizo hili limekuwa likiwaadhiri watu wengi sana kisaikolojia hasa baada ya kujiona wapo tofauti sana na wengine kwa kawaida mwanaume anatakiwa awe na uume kuanzia nchi 6-8 kwanza upungufu wa vichocheo hivi huchochea ukuaji wa uume chongo ambalo hushambulia nerve ambayo uharibu kabisa ukuaji wa uume, ngiri, punyeto, ambayo huathili misuli ya uume, ngiri huleta maumivu, tumbo kuunguruma na kujaa gesi, korodani moja kuvimba, kutopata choo vizuri, sababu hizi hufanya uume kulegea na kusinyaa na kuwa mfupi na mwembamba na mara nyingi hata nguvu za kiume ( hamu ya tendo la ndoa) hupungua na kwisha kabisa 

GEMBE :Ni dawa inayozalisha na kukufanya uume kukua na kuongezeka 
NGEMO : Ni dawa bora ya kuongeza nguvu za kiume 

Hukutia hamu ya kuludia tendo la ndoa zaidi mara4 nne bila kukinai au kuchoka pia itakufanya uchelewe kufika kileleni zaidi ya dk30-45 kwa mtumiaji pia tunatibu kisukari, bp, ngiri, miguu kuwaka moto KAMA HUNAMDA WA KUFIKA OFISINI KWETU UTALETEWA POPOTE TUPO MBAGALA RANGI TATU 

 0753471612/ 0715249530 
0623 386 305 

DR KUZENZA

Simba ya Mwaka Huu si Mchezo, Lazima Wachukue Kombe Tena

$
0
0

Wakati kikosi cha Simba kikiwa katika programu ya mazoezi nchini Uturuki kwa takribani wiki moja sasa, uongozi wa klabu hiyo kupitia kwa Kocha Msaidizi, Masoud Djuma, umesema timu hiyo haitoshikika msimu ujao. 

Simba ipo Instabul katika Milima ya Kartepe ikijifua kwa maandalizi ya tamasha la Simba Day ambalo khufanyika Agosti 8 kila mwaka pamoja na msimu mpya ujao wa Ligi Kuu Bara. 

Taarifa zimeeleza Djuma amesema kila mchezaji ameahidi makubwa kuelekea pazia la ligi kufunguliwa ambapo Simba itaanza kucheza dhidi ya Tanzania Prisons kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam. 

Aidha, Kocha huyo amefunguka na kusema uwepo wa Kocha Mbelgiji, Patrick Aussems umechangia kwa wachezaji wote kujituma zaidi mazoezini ili kumuonesha uwezo walionao. 

Mbali na programu za mazoezi, kikosi cha Simba kimekuwa kikiingia darasani kupewa mafunzo mbalimbali ili kuwaongezea uelewa wachezaji wake ikiwemo elimu ya saikolojia. 

Baada ya kambi hiyo kumalizika, SImba wataanza kurejea jijini Dar es Salaam Agosti 4 tayari kwa maandalizi ya Simba Day na mchezo wa Ngao ya Hisani dhidi ya Mtibwa Suhar utakaopigwa Agosti 12 Uwanja wa CCM Kirumba.

Haya Hapa Madhara Makubwa yanayowapata Wanaokula Mirungi

$
0
0

AFYA: Je, unayajua madhara ya kiafya anayoyapata mtumiaji wa Mirungi

Mirungi ni mmea ambao una majina mengi kulingana na eneo. Mfano; gomba, miraa nakadhalika

Ulaji wa mirungi unadaiwa kuanzia nchini Ethiopia, ukaenea hadi nchi za Afrika Mashariki, Yemen, Zimbabwe, Zambia, Malawi na hata Afrika kusini

Mirungi ilionekana kuwa ni moja ya madawa ya kulevya hivyo ikakatangazwa na umoja wa mataifa UN na kupigwa marufuku mwaka 1971 kwasababu ya ufanano wa kemikali iitwayo amphetamine

Yafuatayo ni madhara ya kiafya ya mirungi kama ilivyofanywa na shirika la afya duniani kama ifuatavyo;

1. Mtumiaji wa mirungi yupo katika hatari ya kupata vidonda vya tumbo
-l
2. Kupungukiwa msukumo wa kufanya tendo la ndoa(low sex drive) na pia kuwahi kumaliza haraka na kutoweza kudumu kwenye tendo la ndoa kwa muda mrefu

3. Ukosefu wa haja kubwa(constipation)

4. Utumiaji wa muda mrefu husababisha ini kushindwa kufanya kazi na pia meno kubadilika rangi, kudhoofika, fizi kuuma na harufu mbaya mdomoni

5. Upungufu wa usingizi

6. Madhara ambayo bado kinamama walaji Mirungi hawajagundua ni kwamba mtoto anayezaliwa na mama mlaji Mirungi mara nyingi hukataa kunyonya titi la mama yake kwa sababu ladha ya maziwa inabadilika kwa ajili ya utumiaji wa madawa(pesticides) unaotumiwa na wakulima wa Mirungi kama inavyoeleza utafiti uliofanyika na Chuo Kikuu Cha Aden(Aden University)

Aidha,Utafiti mwengine kule Ethiopia unaeleza kuwa mtoto wa mama mwenye kula Mirungi kwa wingi huwa hana uzito wa kawaida wakati wa kuzaliwa

7. Ukosefu wa hamu ya kula chakula

Hayo ndio madhara yanayoelezwa kutokana na utumiaji wa mirungi

Anne Kilango, Ajiteua kuwa Mbunge wa Jimbo la Moshi mjini

$
0
0

Mbunge wa kuteuliwa, Anne Kilango Malecela amejiteua kuwa mbunge wa Jimbo la Moshi mjini ili kukamilisha muundo wa uongozi aliouita wa mafiga matatu katika kushughulikia kero za wananchi. 

Kilango ambaye ni miongoni mwa wabunge wa kuteuliwa na Rais John Magufuli, ametengaza uamuzi huo katika mkutano wa hadhara wa kumnadi mgombea udiwani kata ya Mawenzi kwa tiketi ya (CCM) Apaikunda Naburi. 

"Mafiga matatu ndiyo yanayopika ngoja niwaambie leo watu wa Mawenzi, na asiwadanganye mtu, tupeni diwani wa CCM ili kukamilisha mafiga matatu,mtauliza mbunge ni nani? mbunge ndio mimi hapa”, amesema Kilango. 

Kilango amesema mafiga matatu ndio yanayopika chakula akitaka kuwepo na sare ya kuwepo Rais anayetokana na CCM, mbunge anayetokana na chama hicho sambamba na diwani. 

Akiomba kura katika mkutano huo, Apaikunda amesema yeye ndio anazifahamu vizuri kero za wananchi wa kata hiyo likiwamo tatizo la taa za barabarani na maeneo ya kufanyia biashara kwa machinga, hivyo akaomba wamchague ili kuzipatia majawabu kero hizo. 

Jimbo la Moshi mjini linaongozwa na mbunge kutoka upinzani, Jafary Michael ambaye ni kutoka Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA).

Muone na Wasiliana na Dr Kanengo Bingwa wa Tiba Asili, Hutibu Magonjwa Haya

$
0
0

NKURURU:-ni dawa inayotibu miguu kuwaka moto, kiuno tumbo     kupooza/kuparalazi  kupoteza  fahamu  MALABALA  hutibu  kisukari , uti  wa  mgogo,  Change, pumu, busha, kaswende, kifua  kikuu, muwasho  sehemu  ya siri

POWER :-ni dawa ya kuongeza nguvu za kiume ni vidonge  20

MPERAMPERA:- ni dawa ya kurudisha Mke, mme, mpenzi,mchumba aliyekuacha /kuteseka, ni kwa mda wa siku 2 tu kusafisha, pia kunakuna dawa za kupunguza vitambi(nyama uzembe),  maziwa makubwa,michirizi, mikovu makubwa, chunusi sugu.

SIX POWER:-inatibu upungufu wa nguvu za kiume kwa wasio weza kumudu tendo la ndoa itakufanya uwe na hamu ya kurudia tendo la ndoa zaidi ya Mara 4 bila hamu Keisha, inaboresha maumbile madogo na inaimarisha misuri iliyo regea na kusinyaa una pona kabisa, ndani ya siku 4 tu 

GASELA:-ni dawa ya maajabu (9) yaliyoshindikana.    (1)-Kisukari, vidonda vya tumbo, tezi dume,walioshindikanika kupata watoto(ugumba),busha bila oparesheni, (2)zindiko Kali Katika biashara yako (chuma ulete)  ndo kiboko yao kumkamata mwizi aliye kuibia vitu vyako pikipiki, gari, n, k( 2)zindiko la nyumba, mashamba, viwanja,. ( 3 ) kurudisha mtu aliye kufa kiutatanishi (msukule) (4)kukutolea sumu uliyo ikanyaga (Mtego) (5)ujiamini kutumia dawa ya maajabu Saba (6)kutoa mikafara mfano ugomvi ndani ya nyumba kufukuzwa kazini bila sababu (7)kutabiri nyota na kung'arisha (8)kurudisha Mali iliyo potea mazingira ya kutatanisha, kushinda kesi uliyo sumbuka nayo mda mrefu. (9)kufukuza majini wa  chafu ndani ya mji,.Haya yote yana wezekana kwa DR KANENGO popote ulipo ukiniitaji nafika napatikana buguruni chama, mbagala zakhiem karibia na uwanja wa mkutano, na wilaya ya bunda musoma : mawasiliano  ni simu namba :-0767-17-17-73 na  0716-60-89-59   

NI  KWA  WALIO  TUMIA  DAWA  ZA MATATIZO  MBALIMBLI  BILA  MAFANIKIO   uwezo  WA  kurudisha  mali  iliyopotea  au  kudhulumiwa    muda  mfupi  tu,  Na natoa  dawa  ya  utajiri  kwa  wafanya  biashara     wachimbaji  madini, wafaryakazi,  wakulima, wafugaji na  kwa yeyote  anayetaka  kuwa  na  pesa   nyingi  katika   maisha  yake,  Na  pia  anaunganisha  utajiri    kwa muda  mfupi  sana  pamoja  na  kuboresha  akili  kwa  wanafunzi  na  kumfanya  afaulu  mitihani  yote  au  intaview  yeyote  na  ana  uwezo  mkubwa  wa  kutibu  ugonjwa  wa  Uvimbe tumboni .  pia anarudisha  Mke, mme, mchumba,    hawara, kwa  muda  wa  saa  3  na  anatimiza mahitaji  yote  hata  kama  upo  mbali   kiasi  gani,  ahadi  zote  atatimiza  kwa  muda  mfupi  tu  Na  kumfunga  asiwe  na mtu  mwingine  kwa  nini  unaumiza  kichwa ? 

Muone  ( DR  )KANENGO,anatibu  nguvu  za  kiume  anarefusha  na  kunenepesha  uume  kwa  saizi  uipendayo  kwa  muda  mfupi   sana, pamoja  na  kuwa  na  hamu  ya  kurudia  tendo  la  ndoa  mara  4  bila  hamu  kuisha   Na  utachelewa   kufika  kileleni  kwa  muda  wa  dakika   40  bila  kuchoka  hata  kama  una umri  mkubwa  kiasi  gani   Gerentii  miaka /=60    ukisha  pona  bila tatizo   kurudia  pia ana  uwezo  mkubwa  wa  kuongeza  hips na  makalio,  pia   anatibu  magonjwa  sugu  ya  zinaa  tumbo  kujaa  gesi,  kuuma  chini  ya  kitovu,vidonda vya tumbo,   kiuno,  miguu    kuwaka  moto  miguu,  kuvimba..Nk..Angalizo usitume meseji wala kubipu..
You can get it in   all East African countries, our service is fast and easy... contact Whatsapp 0767171773.Dar es salaam Tanzania. ..Dr. KANENGO 0716608959...You are welcome.

Chadema yajibu mapigo, yadai Waitara ni Muongo

$
0
0

Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), kimedai sababu kubwa ya kuondoka aliyekuwa Mbunge wa Ukonga na mwanachama wa chama hicho, Mwita Waitara ni kutokana na hofu ya kukosa Ubunge mwaka 2020 kutoka na safu yake ya viongozi kushindwa kupata nafasi.


Hayo yamebainishwa na Mkurugenzi wa Itifaki na Mawasiliano ya Mambo ya Nje wa Chadema, John Mrema ikiwa imepita siku moja tokea Mbunge huyo kutangaza hadharani kujivua uanachama wake na kujiunga na Chama Cha Mapinduzi (CCM), huku kudai sababu kubwa ya yeye kuchukua maamuzi hayo ni kutokana na ugomvi wake na Mwenyekiti wa CHADEMA Freeman Mbowe ndani ya chama.


Sababu nyingine za Mwita Waitara kuondoka CHADEMA amedai kwamba ndani ya chama hicho hakuna ruhusa ya Mbunge kusema lolote, hakuna uchaguzi wa haki bali kuna pachika pachika pamoja na Mbowe kutotaka kushauriwa.


"Anaposema hakuna uchaguzi ndani ya chama ni muongo, jimbo la Ukonga tulifanya uchaguzi kuanzia ngazi ya chini kabisa ya misingi, tukaenda matawi, kata na hatimaye Wilaya. Mwita alikuwa amepanga safu yake ya viongozi ambayo imeshindwa na kulalamika sana kwanini safu yake ilishindwa..


"Walishindwa kutokana na wapiga kura waliamua kuchagua viongozi wengine na hicho ndicho kilimfaya Mwita kuwa na hofu ya kukosa Ubunge katika chaguzi zijazo na amelalamika kwa maandishi", amesema Mrema.


Mbali na hilo, Mrema amemtaka Mwita Waitara kutoa sababu za msingi za kuondoka ndani ya chama hicho nasio kufanya siasa nyepesi za kuchafuana.


Mwita Waitara amekuwa Mbunge wa pili kutoka CHADEMA kujivua Ubunge, ambapo Mbunge wa kwanza alikuwa Dkt. Godwin Oloyce Mollel mnamo Disemba 14, 2017 alitangaza kujivua rasmi uanachama wa chama hicho na kujiunga na CCM kwa madai ya kuunga mkono utendaji ya Rais Magufuli.

Wabunge Wa Kigoma Waridhishwa Na Utendaji Wa Serikali .

$
0
0

WABUNGE wa mkoa wa Kigoma wameipongeza Serikali ya Awamu ya Tano inayoongozwa na Rais Dkt. John Magufuli kwa kuanzisha kampeni ya kuhamasisha kilimo cha zao la michikichi kwa sababu litasaidia kuondoa umasiki kwa wananchi wa mkoa huo.


Wamesema kwa muda mrefu wamekuwa wakiiomba Serikali kulifufua zao hilo kwa kuwa ndilo zao kubwa la biashara linalotegemewa na wananchi wengi wa mkoa huo, hivyo kitendo cha kuanzisha kampeni hiyo kinaonesha dhamira ya dhati ya Serikali ya kuwakwamua wananchi.


Wakizungumza kwa jana (Jumamosi, Julai 28, 2018) wabunge hao waliahidi kushirikiana na Serikali bega kwa bega kuhakikisha kampeni ya kuhamasisha kilimo cha zao la michikichi linafanikiwa kama ilivyokusudiwa na Serikali.


Wabunge hao waliyasema hayo  baada ya Waziri Mkuu Kassim Majaliwa kuzindua kampeni ya kuhamasisha kilimo cha zao la michikichi katika mkutano uliofanyika kwenye ukumbi wa NSSF mkoani Kigoma. Mkutano huo ulihudhuriwa na wadau wa zao hilo.


Miongoni mwa wabunge hao ni mbunge wa Kigoma Mjini, Zitto Kabwe ambaye aliipongeza Serikali kwa kusikia kilio cha muda mrfu cha wananchi wa mkoa huo cha kufufuliwa kwa zao la michikichi kwa kuwa litakwenda kuchochea ukuaji wa uchumi wa wananchi wa Kigoma.


“Nakupongeza Mheshimiwa Waziri Mkuu pamoja na Serikali kwa kitendo hiki cha kufufua zao la michikichi kwani hiki ndicho kilio cha muda mrefu cha wananchi wa Kigoma kwa hatu hii naamini kuwa leo hata waliotangulia mbele ya haki watakuwa wanatabasamu huko waliko,”.


Pia mbunge huyo alitumia fursa hiyo kuwasisitiza wananchi na viongozi wa mkoa wa Kigoma kuwa ni vema wakashirikiana kwa pamoja katika kuhakikisha zao hilo linafufuliwa kwa watu kuchangamkia fursa ya kupanda michikichi kwenye mashamba yao.


Mbunge mwingine wa jimbo la Kigoma Kaskazini, Peter Serukamba alisema changamoto kubwa inayowakabili wananchi wa mkoa huo ni upatikanaji wa mbegu bora za michikichi, hivyo ameiomba Serikali kuwasaidia katika upatikanaji wa mbegu.


Kwa upande wake,Mkurugenzi Mtendaji wa Trade Mark Bw. John Luaga alisema walifanya utafiti kuhusu zao la michikichi na walibaini kuwa kuna soko kubwa la mafuta ya mawese ndani ya nchi yetu, pamoja na nchi za jirani ila uzalishaji wa mafuta hayo ndani ya nchi bado ni mdogo sana.


Alisema hali inachangiwa na kuwepo kwavikwazo vichache vinavyokwamisha ongezeko la uzalishaji wa ndani, ambavyo ni matumizi ya teknologia hafifu katika kilimo cha mchikichi, na ukamuaji  wa mafuta ya mawese.


Pia ukosefu wa miundombinu na usafiri, ukosefu wa maghala ya kukusanyia matunda ngazi ya wilaya, na badala yake mkulima mmoja mmoja anahangaika kupeleka kwa mteja hivyo kumuongezea gharama, ukubwa wa gharama za usafiri kutoka shambani mpaka sokoni.


Naye, Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania (TADB), Bw. Josephat Faustine alisema kilimo cha zao la michikichi kina faida kubwa na kinawekezeka, hivyo wao wataanisha maeneo yote yanayofaa kuwekeza.


Pia Mkurugenzi huyo wa TADB alisema benki yao inauwezo wa kutoa mikopo ya mitaji kwa vituo vya uzalishaji mbegu za zao la michikichi na kumaliza changamoto ya upatikanaji wa mbegu, hivyo ni muhimu kwa wakala wa mbegu kuchangamkia fursa hiyo.


Kwa upande wake, Waziri Mkuu alisema Serikali imedhamiria kufufua zao hilo na kwamba changamoto zinazowakabili wakulima wa zao la michikichi ikiwemoya upatikanaji wa mitaji na mikopo kwa ajili ya kununua mbegu au miche mipya zinafanyiwa kazi.


Waziri Mkuu alisema Serikali itahakikisha zao hilo linafufuliwa na kulimwa kwa wingi mkoani Kigoma pamoja na mikoa mingine inayolima michikichi nchini, ambapo amewata Maafisa Kilimo katika ngazi zote waanzishe mashamba ya michikichi.


Pia amewaagiza Wakurugenzi wa halmashauri zote nchi kuhakikisha mashamba ya wananchi yanapimwa na wahusika kupewa hati ili ziwaweze kupata dhamana ya mikopo kwenye taasisi mbalimbali za kifedha na kuwekeza kwenye kilimo.


Waziri Mkuu alisema halmashauri zinazolima michikichi viongozi wake wantakiwa kuanzisha vitalu vya miche ya zao hilo na watakaoshindwa kuanzisha vitalu hivyo pamoja na kuhamasisha kilimo cha michikichi kwenye maeneo yao wajitathimini mwenyewe.


Aliongeza kuwa kuanzia sasa mkoa huo uhakikishe miche ya michikichi inapandwa katika maeneo yote yakiwemo ya pembezoni mwa barabara, katika mashamba ya shule za msingi na sekondari, kambi ya JKT na kwenye magereza na kwenye makazi ya wananchi.


Hata hivyo Waziri Mkuu alitoa angalizo kwa wawekezaji watakaowekeza katika kilimo cha michikichi kutoanzisha migogoro na wananchi watakaowakuta katika maeneo yao na badala yake washirikiane nao vizuri kwa sababu migogoro haina tija kwao na kwa wananchi.


IMETOLEWA NA:

OFISI YA WAZIRI MKUU,

Mambo Yatayomfanya Mumeo Akupende zaidi

$
0
0

Wapo baadhi ya wanawake hudiliki hata kutumia dumba hii yote ikiwa kuwafanya wanaume zao wawapende, lakini wengi wao wamesahau ya kwamba kufanya hivo sio chachu ya kufanya mahusiano hayo yakue bali ni kuyadidimiza. 

Lakini ukweli kwamba mambo ya libwata yamepitwa na wakati katika karne hii hivyo ili mumeo akupende zaidi katika mahusiano yenu unatakiwa kufanya yafautayo; 

1. Muamini mmeo au mchumba wako. 
2. Usimkatishe tamaa katika maono yake. 
3. Usimlazimishe kupenda mambo unayoyapenda. 
4. Kila wakati kila unapo tatizo ni vyema ukamwambia kuliko kusema kwa wengine. 
5. Usidhani kwamba hawezi kutambua uwepo na uzuri wa wanawake wengine hivyo mfanye awe karibu nawe ilia one thamani yaw ewe pekeee.. 
6. Usilazimishe kuwajibika juu ya mambo yako: 

Kama vile kwenda saluni, umeme, vocha na mambo mengine hasa kama bado mko katika mchakato wa uchumba, kama atafanya hivyo mwache afanye mwenyewe msimlazimishe eti kwa sababu shosti wako huwa anafanyiwa hivyo na wewe unataka, ladies huo ni utoto. 

Endelea kutembelea  Muungwana Blog kila wakati 

Vanessa Mdee Afunguka Show yake ya Arusha Kupigwa Vita..Haamini Kama Imefanyika

$
0
0

From @vanessamdee - Nipo hapa leo sababu ya kumtumaini Mungu na kumuamini yeye tu. Maana hii show ya Arusha ndugu zangu ilikuwa inapigwa vita zaidi ya kawaida. Nikisema kwamba asubuhi ya kuamkia jana yaani siku ya show nilishajianda kurudi Dar sababu mambo yalikwamaaaaa, would you believe me? Lakini Mungu ana malaika wake wanawapigania wanyonge. Let me start by thanking my hometown ARUSHA

Pata Super Mkuyati Mpya Orjinal Inayo Imarisha Heshima ya Ndoa

$
0
0

SUPER MKUYATI MPYA ORJINAL INAYO IMARISHA HESHIMA YA NDOA 

SUPER MKUYATI NI DAWA ILIYO KATIKA MFUMO WAJIDONGE NA UNGA IMETENGENEZWA KWA TEKNOLOJIA YA KISASA ILIYOFANYIWA UTAFITI WA KINA NA KUNDULIKA INAPAMBANA NA MAGONJWA SUGU YA KINA BABA DAWA HII INA GUVU (3)NA INAFANYA KAZI KWA PAMOJA (1) INAONGEZA NGUVU ZA KIUME 2 KWA UCHELEWE KUFIKA KILELEI KWA KWA WA DK 10-20 (3) INAZALISHA HOMONI KWA WINGI NA KUKUFANYA UWE NA MBEGU NYINGI ZENYE VIMELEO NYA UZAZI VILIVOKOMAA 

MDINGO MIX NI DAWA INAYO LEFUSHA NA KUNENEPESHA MAUMBILE MADOGO YALIYOSINYAA KUNZIA NCHI 
6-8 UPANA 3-4 INAZIBUA MILIJA YA UZAZI DAW HIZI HAZINA MADHARA KWA MTUMIAJI HATA KWA WAZEE WALIO NA UMRI WAMIKA 68-82 TUMIA LEO UONE MAJABU YAKE TIBA HIZI NIZAKUDUMU 

DR GATUNDU ANAZO DAW ZAKISUKALI PRESHA HENIA NGILI YAKUSHUKA BILA UPADUJI VIDONDA VATUMBO KUPUNGUZA UNENE UZITO TEZI DUME NA KUPONA KABISA DAWA ZASILI 

OFISI ZETU ZINA PATIKANA DR ZAKHEM KWA WALE WAMIKOANIi WATA TUMIWA KWA NJIA YA MABASI PASIPO NA MASHAKA 


Piga Simu Namba 0768 408 794

Ndege ya Boeing 787-8 Dreamliner yatua Mwanza kwa mara ya kwanza, viongozi wa dini wamshushia dua Rais Magufuli

$
0
0

Kwa mara ya kwanza ndege kubwa ya Boeing 787-8 Dreamliner yenye uwezo wa kubeba watu 262 imewasili majira ya saa 5:00 asubuhi ikitokea Kilimanajro.


Hii ni safari yake ya kwanza kuzinduliwa tangu ndege hiyo ilivyowasili nchini Tanzania mapema mwezi huu ikitokea Marekani.

Baada ya kuwasili katika Uwanja wa ndege wa Mwanza Viongozi mbalimbali wa kidini walitoa dua zao kwa Rais Magufuli kwa kutimiza ahadi yake.
Viewing all 104799 articles
Browse latest View live




Latest Images