Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104796 articles
Browse latest View live

MTANDAO WA UNGA WA JACK PATRICK UNATISHA

$
0
0
Na Mwandishi Wetu
BADO habari ya mjini ni skendo ya kunaswa na madawa ya kulevya ‘unga’ inayomtafuna Video Queen wa Bongo, Jacqueline Clifford Fitzpatrick ‘Jack Patrick’ ambaye inadaiwa kuwa mtandao wake wa biashara hiyo ni wa kutisha, Ijumaa limetonywa.

Habari kutoka kwa rafiki wa karibu wa Jack ambaye aliomba chondechonde asitajwe, alidai kwa sasa vigogo wanaojihusisha na biashara hiyo haramu wamekuwa wakihaha kwa hofu kuwa modo huyo anaweza kuwataja hivyo wanafanya kila linalowezekana ili wamnusuru kama ilivyokuwa kwa Agnes Gerald ‘Masogange’.

Ilisemekana kuwa katika mtandao huo, vigogo hao wenye maskani jijini Dar, Rwanda, Uganda, Kenya, Dubai, Thailand, Italia na Hong Kong wamekuwa wakihaha kumuokoa Jack bila mafanikio.
“Unajua China siyo rahisi kumchomoa kama ilivyokuwa kwa Masogange (Agness Gerald) aliyenaswa Sauz (Afrika Kusini) kwa sababu wale (China) Tanzania haikuwasaidia kupata uhuru kama ilivyokuwa kwa Sauz.

“Ile ngoma ni mbichi, hakuna upenyo wa rushwa pale. Ngojeni tusubiri hukumu maana itakuwa kali sana, nazijua vizuri sheria za China juu ya madawa ya kulevya,” alisema rafiki huyo wa Jack na kuongeza:

“Hakuna ishu iliyoniuma kama ya Jack kwa mwaka uliomalizika.”
Katika nusanusa za gazeti hili, ilidaiwa kuwa bosi aliyemtuma Jack ni mwanamke mmoja tajiri aishie jijini Dar ambaye ana mtandao mkubwa wa biashara hiyo duniani.

Ili kuthibitisha kuwa mtandao uliodaiwa kumtuma Jack unatisha na una watu wazito, ilielezwa kwamba mrembo huyo hakuwa peke yake kwani alifuatana na warembo wawili, mmoja Mtanzania na mwingine raia wa Rwanda ambao wao walifanikiwa kuwatoroka polisi wa China.

Mbali na timu hiyo ya watu watatu waliokuwa na mzigo mwilini, pia kulikuwa na mtu mwingine aliyekuwa akiwasindikiza.

WARIOBA"KATIBA YA TANGANYIKA INAWEZA KUANDALIWA NDANI YA MIEZI MITATU"

$
0
0
Dar es Salaam. Mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Jaji Joseph Warioba amesema Katiba ya Tanganyika inaweza kuandikwa ndani ya miezi mitatu tu kwa kuwa maoni mengi yaliyomo katika Rasimu ya Katiba iliyozinduliwa Jumatatu, kwa kiwango kikubwa yametoka kwa wananchi wa upande huo wa Muungano.

Warioba alisema hayo jana wakati akizungumza na Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF), kwenye Ukumbi wa Karimjee, jijini Dar es Salaam.

“Kutunga Katiba ya Tanganyika siyo kazi ngumu, ukisoma rasimu hii sura ya kwanza mpaka ya tano, sioni kama Katiba ya Tanganyika itakuwa tofauti na maoni yaliyomo katika sura hizo,” alisema na kuongeza:

“Misingi iliyopo katika utangulizi wa rasimu hii imetokana na maoni ya wananchi hao. Wakati wa kukusanya maoni, Zanzibar walijikita zaidi kwenye Muungano, maoni mengine kwa kiwango kikubwa yametoka kwa Watanzania Bara na katika kuandika Katiba ya Tanganyika sioni kama watabadilisha chochote kuhusu misingi hii ambayo ni; tunu za taifa, maadili, malengo na haki za binadamu.”

Alisema kuhusu kubadilishwa kwa mihimili ya Serikali na vyombo vingine vya kitaifa, kikubwa kinachoweza kuguswa ni muundo wa Bunge la Tanganyika, Baraza la Wawakilishi Zanzibar na Baraza la Mawaziri.

“Kuhusu taratibu za kufanya kazi; iwe ni madaraka ya Rais, utaratibu wa kufanya kazi katika Bunge, Mahakama na Serikali sioni kama litakuja suala jipya kwa sababu mambo hayo yameshatolewa maoni. “Kilichobaki ni madaraka kwa umma tu, kwa maana ya Local Government (Serikali za Mitaa). Hata hili la madaraka kwa umma watakaolishughulikia watumie taarifa za wananchi waliotoa maoni yao kuhusu Katiba Mpya. Wananchi walitoa maoni kuhusu jambo hili ambayo yapo wazi kabisa.”

Uchaguzi Mkuu 2015

Kuhusu uwezekano wa Katiba Mpya kutumika katika Uchaguzi Mkuu 2015, Jaji Warioba alisema Tume hiyo ilipewa muda mfupi wa kuandaa Rasimu ya Katiba kwa sababu ilielezwa kuwa uchaguzi wa mwaka 2015, utafanyika kwa kutumia Katiba Mpya.

“Katiba hii ilitakiwa iwe imekamilika Aprili mwaka huu, maana yake tungekuwa na mwaka mmoja na nusu wa kufanya mambo mengine ya kuwezesha itumike kwenye uchaguzi wa mwaka 2015,” alisema.

Alisema ndiyo maana katika rasimu hiyo, Tume imeweka masharti ya mpito ya miaka minne, kuanzia siku inapopatikana Katiba Mpya hadi Desemba 28, 2018.

Alisema rasimu hiyo imefafanua Baraza la Mawaziri na Bunge vitakuwaje… “Sasa hivi tuna Serikali na Bunge. Katiba Mpya itapatikana mwaka huu, lakini Bunge letu litaendelea kuwapo kwa msingi wa Katiba ya sasa mpaka ufike wakati wa uchaguzi, hiyo inafanyika kwa ajili ya kulinda uongozi wa Bunge na Serikali.”

Alisema ili kuwepo na Uchaguzi Mkuu kwa Katiba Mpya ni lazima itungwe Katiba ya Tanganyika, kwamba wamependekeza miaka minne ya mpito ili kutoa nafasi ya kubadilishwa kwa mambo kadhaa, ikiwa ni pamoja na kuundwa upya Tume ya Uchaguzi itakayoendesha uchaguzi kwa msingi wa Katiba Mpya.

KAULI YA ZITTO KABWE BAADA YA MAHAKAMA KUMPA USHINDI DHIDI YA CHADEMA

$
0
0
Mbunge wa Kigoma Kaskazini Zitto Kabwe jana alitinga  mahakama kuu  kupinga kujadiliwa kwenye kikao cha kamati kuu ya Chadema,Kikao ambacho kilikuwa kikutane leo.

Hii  ni  kauli  yake  baada  ya  mahakama  kumpa  ushindi;
"Jana tulikwenda mahakamani kwa ajili ya jambo moja tu kutaka haki itendeke kwa sababu mahakaama ndiyo chombo cha juu kabisa kwenye nchi yetu cha kuweza kutenda haki mara baada ya kamati kuu ya chama changu kufanya maamuzi ya  kunivua nafasi zangu ambayo niliandikiwa makosa 11

"Nilikata rufaa kwenye baraza kuu la chama ili baraza kuu liweze kuona kama kamati kuu ilifuata taratibu za chama kufikia maamuzi yale japo mimi naamini haijafuata taratibu za chama lakini kwa bahati mbaya viongozi wangu wa chama changu wameamua kuendelea na kikao cha kamati kuu.

"Hawajajibu barua yangu ya nia ya kukata rufaa na kuweza kupatiwa taarifa na mwenendo wa kikao ili niweze kukata rufaa kwa mujibu wa chama. Kwa hiyo nimekwenda mahakani ili mahakama iweze kutoa maamuzi ya mimi kuweza kupata nafasi ya kusikilizwa na kujadiliwa.

"Nashukuru Jaji John Utamwa ametoa amri ya muda ya kuzuia kamati kuu ya chama kunijadili mpaka hapo Chadema watakapoweza kujibu hoja zilizotolewa na mwanasheria wangu Albert Msando.

"Leo tunarudi mahakamani kwa ajili ya kuendelea na kuweza kupokea majibu kutoka Chadema lakini kikao cha leo kamati kuu imezuiliwa na mahakama kujadili hoja yoyote inayonihusu,lakini pia mapingamizi yote mwanasheria wa Chadema Tundu Lissu aliyokua ameyaweka dhidi ya mwanasheria wangu Jaji ameyatupilia mbali kwa hiyo kesi inaendelea.

"Muhimu katika hili ni haki na mimi kama mtu ambaye siku zote natetea haki sasa ni fursa yangu kutetea haki yangu mwenyewe ya kuweza kusikilizwa  ya kutumia taratibu zote za chama katika hali ya kawaida baraza kuu la chama liitwe kwanza  lijadili jambo hili kabla ya kikao cha kamati kuu kuitwa".

TUSIMLAUMU JACKIE CLIFF...TUMLAUMU ALIYE MFUNDISHA KUVUA SAMAKI

$
0
0
Jackie Cliff… mrembo wa haja niliyeanza kumfahamu kwenye video ya She Got A Gwan ya Ngwair. Ni msichana aliyeenda hewani na Mungu kampelea haswaa. Ukikutana naye huwezi kumwangalia mara moja ukaridhika, lazima ugeukE kumwangalia tena.

Nilipata bahati ya kumhoji mwezi September mwaka jana kwenye fashion show ya Ally Rehmtullah iliyofanyika kwenye hoteli ya Serena, jijini Dar es Salaam na katika maongezi yetu kuhusu Ngwair na kazi yake kama mrembo wa video nikagundua kuwa, Jackie ni msichana mpiganaji asiyejali kitu.

Jackie The Boss Lady, ni msichana anayejulikana kwa kuishi maisha ya kifahari yakiwemo kuendesha magari ya gharama ambayo wengi yaliwapa maswali mengi, ni wapi anapata fedha hizo? Ni kweli fani ya urembo inalipa hivyo? Sijasahau pia kuwa aliyekuwa mume wake, ni miongoni mwa madon wa Dar na ambaye alifungwa kwa miaka kadhaa kwa shutuma zile zile za sembe.

Huenda fedha alizokuwa akizitumia na kuziumiza roho za watu wengi zilikuwa za mume wake ama tayari alikuwa ameshaanza kufanya biashara hiyo haramu na ya hatari kabisa duniani.

Ni ngumu kujua nani aliyemuingiza Jackie kwenye biashara hiyo lakini uhakika mkubwa ni kuwa aliingizwa na mtu wake wa karibu, mume ama mpenzi wake. Kwa lugha nyingine ni kwamba, nyuma ya wasichana wengi wanaofanya biashara hii, wapo wanaume, madon wenye nguvu, madaraka, connection na fedha nyingi ambao si rahisi kuwafahamu. Hata wale wanaofahamika, ni nguvu kuthibitisha tuhuma hizo kwakuwa si wao wanaosafiri.

Kwa mtu kama Ray C, ambaye kukamatwa kwa Jackie hakumshtui hata kidogo kutokana na jinsi anavyowachukia wafanya biashara wa sembe, naamini anapata hasira kufahamu ukweli huu kwamba, wasichana hawa wanatumiwa tu.

Kuna watu wakubwa nyuma yao. Matajiri wakubwa katika nchi hii ambao ukitaka kuwajua, unaweza kujikuta pabaya hasa kama unaishi kwenye nchi kama Tanzania ambayo fedha inaongea kuliko haki na rushwa imetawala. Ni rahisi kudeal na majambazi kuliko kudeal na wazee wa unga. Wale waliojaribu wanajua vitisho walivyovipata. Biashara ya unga ni hatari kwa vijana wengi wa Tanzania na wauzaji wanajua hilo, lakini kamwe hawawezi kukubali kuona unawaharibia ugali wao.

Akina Jackie, Agnes na wengine, ni mfano tu wa wasichana wengi warembo na mastaa wa Tanzania wanaotumiwa kwenye biashara hii haramu. Wapo wengi, wanaume na wanawake, wenye majina na wanaofanya kazi hii. Naamini siku moja atakuja kukamatwa mtu asiyetegemewa kabisa na kila mmoja atabaki mdomo wazi.

Pengine kinachowaponza wasichana wengi, ni kutaka kuishi maisha yasiyo yao. Hupenda kuishi maisha ya anasa na starehe. Kwa mji kama Dar es Salaam na maisha fake ya Instagram yanayooneshwa na wasichana wengi wa Kibongo, inahitaji moyo kwa msichana mrembo kuvumilia kuishi maisha ya kawaida.

Na ndio maana, wengi hujikuta kwenye himaya za wauza unga ambao pamoja na kuwageuza chombo cha starehe zao za kimwili, huwaingia kwenye biashara hizo hatari na hata kama uhusiano ukiisha, wengi hushindwa kujitoa.

Wakati ambapo kila mtu anamsema vibaya Jackie na kumkejeli kwa kila neno, tujikumbushe kuwa, nyuma yake wapo watu wazito na hatari zaidi. Jackie kafundishwa tu kuvua samaki na aliyemfundisha haoni shida kutafuta msichana mwingine wa kuziba pengo hilo na biashara itaendelea.

Kama ilivyo kwa Jackie na hata kwa Agnes Masongange, ukifanikiwa kuufuatilia mlolongo wa wahusika, ni lazima ukufikishe kwa mtu mzito anayewapa kazi hizo. Kwakuwa safari moja tu ya kupeleka ama kuleta madawa nchini na iliyofanikiwa inaweza kubadilisha maisha yao kabisa, wasichana wengi warembo wameshindwa kukataa ofa hizo.
Hujiulizi kwanini wanaotumiwa kwenye safari hizi karibu wote ni wasichana warembo?

Kwa muda mrefu, kumekuwepo uhusiano mkubwa kati ya urembo na biashara hiyo. Si Tanzania tu, bali ni duniani kote.
Hii ni kwasababu ni ngumu kuhisi ‘uharamu’ wowote kwenye sura nzuri ya msichana na tena anayejulikana kwa kazi nyingine tofauti. Kama ya ulimbwende.

Swali la kujiuliza, ni kwanini madon hawa huwatumia zaidi warembo wa video ama Mamiss? Hadi sasa watatu wanafahamika kunaswa na mtego. Binti Kiziwi ambaye amefungwa nchini China, Jackie Cliff ambaye naye kifungo kinamngojea na Agnes Masogange ambaye kesi yake iligeuka kuwa nyepesi na kuhukumiwa kulipa faini tu.

MMH HAPA YALIKUWEPO MAPENZI KWELI?

$
0
0
Heri ya mwaka mpya wanajamvi!!!!! 
Mwenzenu nilikuwa kwenye mahusiano na mwanaume mmoja hivi, nilichoexperience ndio utata mtupu!!!!!!! 
From the second date hata sijasema ndio, anawaza tu when are we going to sex!!!! 
Nikaona duh!!! Sijui itakuwaje coz mi Nataka nimsome kwanza nimuelewe kabla ya mambo mengine.
Then came the third date hapo nimeshakubali, baby can i pay for a room!!!!"haaaa!!!!!!! hapana its too soon hata mwezi haujaisha!!!!
Kilichofuata tukawa hatuwasiliani for a week,solutions aliponitafuta tu anauliza when are we going to do it!!!!! Mh nikamzingua ,mawasiliano yakawa yakusuasua sana ila nikawa nimeshamsoma yuko selfish mno.
Katika kipindi hicho sijawahi kutaka chochote kutoka kwake in terms of cash mwisho nikaona what am i waiting for,mapenzi siyaoni kisa nimegoma kutanguliza sex. 
Nikamwacha tu aende atakutana na wanaotaka pesa in exchange for sex hatakama mapenzi hayapo. 
Mtizamo wenu ukoje great thinkers!!!! Nilikuwa sahihi kuona he was only after sex!!!!!!!
By  afrique 

NAPE:LOWASA KAPOTEZA SIFA YA KUGOMBEA URAIS

$
0
0
Sakata la Nape na lowasa limeendelea baada ya Nape jana kumwambia kwa kutangaza nia kabla ya wakati wake amepoteza sifa ya kuteuliwa kupitia chama cha mapibduzi.
maoni yangu: Nabe acha kushindana na Lowasa au umesahau ulivyobanwa kule dodoma ukitakiwa kupeleka ushahidi wa ufisadi wa lowasa vinginevyo umuombe msamaha, ukakomea kumpigia magoti, umesahau ulishatangaza siku 90 vinginevyo ungemg'o mpaka leo Siku 90 imegeuka miaka 90..

Source: Mwananchi/rfa

SHOGA WA KIUME ANATAKA KUNIHARIBIA NDOA..MSAADA JAMANI

$
0
0
Mwanzoni sikujua kama huyu jamaa anatabia ya ushoga nilipojaribu kumchunguza vizuri nikagundua jamaa si riziki.

Alianza kunitumia sms za mapenzi huku akinitakia magudinight kila siku
Nimejaribu kumkanya ila naona hasikii hadi wife ameshtukia nakuanza kugomba.

Ameniambia hata nifanye nini lazima nimlale mimi huo mchezo si uwezi kabisa


Msaada please nimuepuke huyu jamaa

DIAMOND AISIFIA NGOZI YA WEMA SEPETU ASEMA INA MVUTO NA MNG'ARO ZAIDI YA KITU CHOCHOTE

$
0
0
Umemwona Wema, kwa sasa ana ngozi nzuri yenye afya na iliyo na mng’aro kama alivyokuwa awali,ni nzuri sana yani,  ameacha kabisa kutumia dawa za kung’arisha ngozi hilo ndilo lililonivutia zaidi kwani alisikiliza ushauri niliompa kabla.



Hiyo ni kauli ya staa aliyetikisa mwaka 2013 bwana Diamond Platnumz aliyoitoa hivi karibuni alipokuwa akizungumza na gazeti maarufu la michezo nchini hivi karibuni.



 Diamond amesema Wema ndiye mwanamke anayetamani kuwa naye katika maisha yake, hivyo kauli yake aliyoitoa mwanzo kuhusu kuzaa na Wema ipo mbioni kutimia.



Miezi kadhaa nyuma niliongea kuhusu nia yangu ya kuzaa na Wema, wakati huo nilikuwa bado na Penny, siwezi kukimbia kivuli changu kwani ukweli unabaki palepale nampenda yule binti, japokuwa wapo wanaosema kwamba sijatulia au natafuta ‘kiki’ kupitia warembo hawa, si kweli, Wema nilikuwa naye kabla ya Penny na vigezo vyangu ni mchumba anayejali kazi yangu na kujua kwamba mimi ni staa nahitajika sehemu yoyote, muda wowote, Wema ni mwelewa.” Alisisitiza Diamond

MHUBIRI AFA MAJI BAADA YA KUJARIBU KUTEMBEA JUU YA MAJI KAMA YESU

$
0
0
NIGERIA. Ilikuwa sikitisho kubwa kwa waumini baada ya mchungaji wao kusombwa na maji baada ya kujaribu kutembea juu ya maji kama vile masihi Yesu alivyofanya wakati wake alipokuwa duniani.

Pastor Frank Kabele mwenye umri wa miaka 35, aliwaambia waumini wake kuwa mtu mwenye imani anaweza kufanya miujiza yeyote ila tu uwe na imani. Aliwaahidi wafuasi wake kuwa atatembea juu ya maji pindi tu atakapomaliza maombi yake.

Lakini mambo yalienda ndivyo sivyo baada ya pastor huyo kujaribu kutembea katika mto mkubwa, alididimia mtoni humo na ilikuwa vigumu kwa waumini wake kumsaidia kwani maji yalikuwa na nguvu nyingi.

NIMESIKITISHWA NA CHADEMA KUKODI VIJANA WA KUMZOMEA ZITTO LEO MAHAKAMANI

$
0
0
Nimehuzunishwa sana na nimesikitika chadema kukodi vijana ambao wamekiri wazi kulipwa ili kwenda kumzomea mh zito, hili bila kukemewa ni hatari kwani inajenga chuki kubwa baina ya wapenzi wa chadema. kama staili ya kuwalipa vijana ili washushe reputation ya mtu ni sawa basi ipo siku huu ushetani utawarudia wenyewe time will tell
wapenzi wote wa mh zito j3 tujitose mahakamani kusikiliza shauri la kiongzi wetu 
cc team zito

ISAYA 54:14 Utathibitika katika haki utakua mbali na kuonewa, kwa maana hutoogopa, na mbali na hofu, kwa maana haitakukaribia.Tazama, yamkini watakusanyana , lakini si kwa shauri langu watu wowote watakaokusanyana juu yako wataanguka kwa ajili yako.
Jamii Forums

HILI NDILO VURUMAI KAMA SIO VIMBWANGA VILIVYO TOKEA MAHAKAMANI WAKATI WA HUKUMU YA ZITTO KABWE

$
0
0
Dar es Salaam,Tanzania
MAHAKAMA Kuu Kanda ya Dar es Salaam, imeahirisha kutoa hukumu ya kesi iliyofunguliwa jana na Mbunge wa Kigoma Kaskazini Zitto Zuberi Kabwe (Chadema), kuhusu ombi la kuitaka Mahakama hiyo kuizuia Kamati Kuu ya Chama hicho, kutomjadili katika kikao ambacho kilipangwa kufanyika leo jijini Dar es Salaam.
Wanachama wa Chadema, wakitwangana nje ya Mahakama Kuu, jijini Dar es Salaam. 
Jaji John Utumwa alisitisha kutoa hukumu hiyo mpaka siku ya Jumatatu saa 4:00 asubuhi.Hata hiyo baada ya Jaji huyo kuahirisha kesi hiyo, nje ya Mahakama hiyo kulikuwa na vurugu kubwa baada ya kundi linalo unga mkono maamuzi ya Chadema kutwangana na kundi linalo muunga Zitto Kabwe.

Mwanachama wa Chadema, anayepinga hoja za Zitto Kabwe, akimtwanga mfuasi wa Zitto Kabwe. 
Hatua hiyo ilisababisha Askari wa Jeshi la Polisi kuingilia kati, huku wakiungana na upande wa Chadema na kuwatwanga marundi wafuasi wa Zitto waliokuwa na mambango kama ilivyokuwa kwa wenzao wa Chadema.
Kesi hiyo ilifunguliwa jana na wakili wa Mbunge huyo Albert Msando huku wakili wa Chadema Tundu Lissu akiweka pingamizi,hata hivyo Jaji John Utumwa wa Mahakama hiyo alitupilia mbali mapingamizi yote yaliyowekwa na Tundu Lissu,

MFANYABIASHARA WA KIKE APIGWA RISASI USONI NA KUPORWA MABEGI MAWILI YA HELA KARIAKOO

$
0
0
Damu ya Mfanyabiashara huyo ikiwa imetapakaa katika gari lake baada ya kupigwa risasi na majambazi waliompora kiasi kikubwa cha fedha na kutoweka.
Mfanyabiashara mmoja (Jina Halikufahamika) Mwenye asili ya Asia ameshambuliwa na majabazi (majira ya saa 12 Kasoro jioni )kwa kupigwa risasi katika paji la uso wake na kisha majambazi hao kutoweka na mabegi mawili yaliyoojaa fedha.
Hata hivyo haikujulikana kwa haraka ni kiasi gani cha fedha ambacho kilikuwemo katika mabegi hayo. Wakiongea na mwandishi wetu baadhi ya mashuhuda wa tukio walidai kuwa majambazi hao walikuwa  watatu na mmoja alikuwa na bunduki aina ya SMG

Wakielezea tukio hilo baadhi ya wafanyabiashara wengine katika maeneo hayo ya mtaa wa Lindi na Kongo (Kariakoo) walidai kwamba Mfanyabiashara huyo alitoka na kufunga duka lake huku akiwa na mabegi mawili na Mashine ya kutolea Risiti ya EFD na kuelekea katika gari lake dogo aina ya Suzuki Carry na Ghafla walitokea watu wawili waliokuwa katika pikipiki na mmoja wa tatu alikuwa amesimama pembeni kidogo na gari hiyo na kisha kuelekea moja kwa moja katika gari hiyo na kumpiga risasi mfanya biashara huyo aliyekuwa akijiandaa kuondosha gari lake.


Hata hivyo baadhi ya watu wamelaumu utaratibu wa wafanya biashara wengi wa kariakoo kuhifadhi fedha nyingi katika maduka na badala yake wamewataka wafanya biashara hao kutafuta mbinu mbadala itakayowaezesha kuweka fedha na mali zao salama kabisa ikiwa ni pamoja na kutumia huduma za kuhamisha fedha kwa kutumia mitandao, cheque, na hata credit card kuliko Cash kwani imekuwa kawaida kwa mtukio haya kujirudia eleo hili la Kariakoo.

KIGOGO WA WEMA ATANGAZA VITA NA DIAMOND

$
0
0
Stori: Shakoor Jongo
Yule kigogo au taita aliyekuwa akimpa jeuri ya fedha Wema Isaac Sepetu ajulikanaye kwa jina moja la Clement anadaiwa kutangaza vita na staa wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul Jumaa ‘Diamond Platnumz’.
Habari ‘hoti’ zinadai kuwa Clement anataka Diamond arudishe gharama alizomgharamia Wema ndipo waendeleze mapenzi yao.

Kwa mujibu wa mtu wa karibu wa kigogo huo, Clement anadai kwamba gharama alizotumia kwa Wema ni kubwa mno lakini bidada hakujali chochote na kuukabidhi moyo wake kwa ‘Mtoto wa Tandale’ ambaye ndiye barafu wa moyo wake.

Stori: Shakoor Jongo
Yule kigogo au taita aliyekuwa akimpa jeuri ya fedha Wema Isaac Sepetu ajulikanaye kwa jina moja la Clement anadaiwa kutangaza vita na staa wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul Jumaa ‘Diamond Platnumz’.
Habari ‘hoti’ zinadai kuwa Clement anataka Diamond arudishe gharama alizomgharamia Wema ndipo waendeleze mapenzi yao.

“CK (Clement) anaumia sana kuona kuwa ameteketeza fedha nyingi kwa Wema lakini bila hiyana, mrembo huyo akabwaga manyanga kisha akarudisha mpira kwa kipa na kuanza moja huku kaka mkubwa akiachwa kwenye mataa,” alitonya mnyetishaji huyo bila kufafanua kama Clement aliachwa mataa ya eneo gani.

Akiendelea kutiririka bila kuweka nukta au ya mkato, mtu huyo alisema kuwa kiasi ambacho kinadaiwa kuteketea kwa Wema kinakaribia Sh. milioni 279.6 ambazo gharama hizo zinahusisha vitu kadhaa alivyowekeza kwa Wema.
“Kuna gharama za utengenezaji wa Filamu ya The Super Star ambayo haijulikani kilichotokea kwani hadi leo haionekani sokoni.

“Kama hiyo haitoshi kwenye uzinduzi wa filamu hiyo akamleta staa wa filamu wa Nollywood, Nigeria, Omotola Jalade Ekeinde na sherehe mbili za uzinduzi zilifanyika katika hoteli kubwa mbili tofauti, ikasemekana milioni arobaini na nane ziliteketea.
“Kuna kodi ya pango la ofisi ya Wema ya Endless Fame iliyopo Mwananyamala Koma-koma, Dar, jamaa alilipa milioni nane na laki nne kodi ya miaka miwili ambayo kwa mwezi ni laki tatu na nusu.

“Ukiachana na gharama za nyumba na ofisi, kuna gari aina ya Audi Q7, inadaiwa kanunua Clement kwa Sh. milioni 98, Toyota  Harrier Lexusya Sh. milioni 48 na Toyota Mark X iliyomtoa Sh. milioni 25.
“Usisahau hata lile Toyota Noah ‘kitimoto’ la ofisi alinunua Clement kwa Sh. milioni 10, faini aliyolipiwa

Kajala Masanja mahakamani Sh. milioni 13, gharama za kuirekebisha ngozi yake alipoenda nchini China iligharimu Sh. milioni 14, yaani jumla ni kama Sh. milioni 279 na ushee. Na hiyo ni kwa vitu vinavyojulikana ukiachia mbali shopping za Dubai,” alitiririka kikulacho huyo.

Baada ya kujazwa data, Risasi Jumamosi lilijaribu kumtafuta kigogo huyo lakini licha ya juhudi zote hizo hakuweza kupatikana ndipo alipogeukiwa Diamond:
 “Sitishiki kwa lolote lile kwani huko nyuma kabla sijawa maarufu kivile enzi ya Nenda Kamwambie (wimbo) niliwahi kukaa mahabusu kwa siku kadhaa na sababu ilikuwa mapenzi kwa hiyo kwa hili siogopi kitu kwanza mimi ndiyo alinichukulia na mwana mpotevu amerudi kundini,” alisema Diamond anayekimbiza na Ngoma ya Number One.
Chanzo:Global Publishers

DALILI KUU MBILI ZA MWANAMKE ANAPOKARIBIA KUFIKA KILELENI

$
0
0
- Siku zote katika mapenzi hakuna kitu kizuri kama kuridhishana hususan katika tendo la ndoa, ukweli uliopo ni rahisi sana kwa mwanaume kuwahi kufika kileleni kuliko 

mwanamke hii inatokana na sababu nyingi kwa upande wa mwanaume suala la kuwahi kumaliza mapema linaweza kusababishwa na tatizo la nguvu za kiume na kukurupuka 

katika tendo kwa maana ya kuwahi kumuingilia mwanamke bila kufanya Romans/maandalizi ya kwanza kabla ya tendo na kwa upande wa wanawake suala la 

kuchelewa kufika kileleni ni asili yao kutokana na jinsi walivyoumbwa ila napenda ifahamike kuwa pamoja na wanawake kuumbwa hivi ila unauwezo wa kumfanya afike 

kileleni mapema kwa kuzingatia maandalizi ya awali kabla ya tendo inabidi utumie muda mwingi katika kumuandaa mpenzi wako kwa kumtomasa sehemu husika ili iwe njia rahisi ya wewe kumridhisha na kumfanya afike katika kilele cha raha. 

ZIFUATAZO NI DALILI KUU ZA MWANAMKE ANAPOKARIBIA KUFIKA KILELENI:

1. Dalili ya kwanza inayomuashiria mwanamke anapotaka kufika kileleni ni ya kupiga mayowe/kelele, hii ni dalili kubwa kwa wanawake wengi napozungumzia dalili hii sina maana kwamba ya kupiga kelele za fujo ila kelele zinazopigwa ni zile za raha 

zilizoambatana na Miguno ya kimahaba kama alikuwa anatoa sauti ya chini ghafla utaanza kuona anapandisha na kuikuza sauti. Pia kuna wanawake wengine hujikuta wakiropokwa maneno pindi raha zinapozidi,

2. Dalili nyingine ya pili inayoweza kukusaidia kumtambua mwanamke anapotaka kufika kileleni ni hii wanawake wengi hubainika kufika kileleni pindi raha zinapo 

wazidia na wanapo kojoa (Bao) huwakumbatia wapenzi wao kwanguvu na kuwavuta hutumia nguvu nyingi kuwakumbalia wapenzi wao mpaka wanapomaliza kukidhi haja 

yao katika hili pia unaweza kumuona mwanamke mwingine anafikia mpaka hatua ya kukung'ata meno ila fahamu zote zinakuwa ni raha anajikuta anafanya vitu bila kutarajia. 

- Naamini somo limeeleweka na kwa hizi dalili chache sidhani kama ikitokea mwanamke wako akifanya moja wapo kati ya hili kwako itakuwa kama suprise ni vitu 

vya kawaida katika mapenzi na jinsia zote mbili zina haki ya kuridhika katika sehemu ya kusex. Ushauri wangu mkubwa ni kuzingatia maandalizi mazuri kabla ya tendo 

kwani siku zote huwezi kuplan kujenga nyumba bila kuwa na msingi na kwenye mapenzi pia huwezi kufanikiwa kumridhisha mwenza wako bila kumuandaa.

CCM WAAMUA KUMTELEA UVIVU LOWASSA MBIO ZA URAIS 2015

$
0
0
Unaweza kusema sasa Chama Cha Mapinduzi (CCM) kimeamua kumfungia kazi Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa baada ya jana Makamu Mwenyekiti wake (Bara), Phillip Mangula kusema kuwa wanachama wake walioanza mbio za kuwania urais mwaka 2015 watachukuliwa hatua kali za kinidhamu.

Mangula alisema kama wanachama hao wasipochukuliwa hatua watakifanya chama hicho kupoteza mvuto katika medani ya kisiasa nchini;

“Wapo watu wanataka waichanechane CCM kwa sababu ya uroho wao wa madaraka, uroho wa udiwani, ubunge na hata urais. Kuna makundi ndani ya chama kazi yake ni kuwabomoa wenzao, kamwe hatuwezi kuyafumbia macho.”

Akifafanua hilo Mangula alisema: “Tutawaita wote walioonyesha nia ya kuutaka urais 2015 na kuwahoji kwanini wanafanya hivyo wakati muda bado haujafika. Tumeshawachunguza katika mikutano wanayoifanya, tumebaini kuwa wanatoa misaada na kusafirisha watu, tunajua dhamira yao ni nini.”

Mangula ametoa kauli hiyo ikiwa imepita siku moja tangu Katibu wa Itikadi na Uenezi wa chama hicho, Nape Nnauye kusema mwanachama yeyote wa CCM anayetangaza nia ya kuwania urais kabla ya muda mwafaka kutangazwa atapoteza sifa za kugombea.

Nape alitoa kauli hiyo baada ya Lowassa siku mbili zilizopita, kutangaza nia ‘kimtindo’ akisema anaanza rasmi safari aliyoiita ya matumaini ya ndoto zake, ambayo pia itatimiza ndoto za Watanzania za kupata elimu bure, maji safi na maendeleo ya uhakika.

Lowassa ambaye amekuwa akitajwa kuwa mmoja wa wagombea wa nafasi ya urais kupitia CCM katika Uchaguzi Mkuu wa 2015, alitoa kauli hiyo katika ibada ya shukrani ya kuupokea mwaka mpya, katika Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Usharika wa Monduli.

Mangula aliwashukia vigogo wa chama hicho wanaoutaka urais jana katika Kikao cha Halmashauri Kuu ya Kamati ya Siasa tawi la Ofisi ndogo za chama hicho Lumumba, wakati akitoa salamu za mwaka mpya kwa wanachama wote wa CCM nchini.

Ataja kanuni za uongozi

Katika mkutano huo Mangula alisaidiwa kusoma kanuni za uongozi na maadili ya chama hicho, kutolea ufafanuzi mambo mbalimbali na Katibu Tume ya Udhibiti wa Nidhamu ya Viongozi wa CCM na wanachama taifa, Masoud Mbengula.

Moja ya kanuni hizo inasema “Ni mwiko kwa kiongozi wa CCM kutumia dini yake au kabila au rangi au jinsia au eneo analotoka, kama sifa ya kushawishi wapiga kura wamchague ama yeye mwenyewe ama mgombea anayemuunga mkono.”

Mangula alisema kwa mujibu wa kanuni za chama hicho, mwanachama anayefanya mambo kinyume na kanuni huitwa msaliti na hafai kuendelea kufumbiwa macho kwani anaweza kukiangamiza chama wakati wowote.

MCHINA ASHITAKIWA KWA KUCHANA NOTI YA SHILINGI ELFU 10

$
0
0
Raia wa China ambaye ni meneja uzalishaji katika kampuni ya ujenzi  Shen Hai,46, amepandishwa kizimbani kwa kosa la kuchana noti ya shilingi 10,000 ambayo ni mali ya Serikali ya Tanzania.

Akisomewa mashtaka hayo mbele ya Hakimu Mfawidhi wa mkoa Janeth Masesa, Mwendesha Mashtaka wa Serikali,   Castus Ndamugobas alidai kuwa Mchina huyo alitenda kosa hilo mnamo Desemba 3 mwaka jana katika maeneo ya uwanja wa ndege Wilaya ya Ilemela majira ya saa 10:30 jioni ambapo kwa makusudi aliichana noti hiyo  yenye namba AY3748043, ambayo  thamani yake ni Sh10,000 mali ya Serikali ya Tanzania.

Mshtakiwa huyo ambaye ni meneja mzalishaji aliyeajiriwa na Serikali ya Tanzania ili kufanya ukarabati katika Uwanja wa Ndege wa Mwanza, alikana mashtaka yote na alirudishwa rumande baada ya kutokidhi masharti ya dhamana na hakimu Masesa aliahirisha kesi hiyo hadi Januari 8 mwaka huu ambapo itafikishwa mahakamani hapo kwa ajili ya kutajwa tena.

Kitendo  hicho cha raia huyo wa China kuchana noti kilionyesha dharau kwa nchi ya Tanzania na raia wake.

MAN GIVES BIRTH TO BABY GIRL, HIS WIFE IS THE FATHER

$
0
0
The first baby to be born to transgender parents in Argentina was delivered via C-section in the province of Entre Ríos.

The proud parents are 26-year-old Alexis Taborda and 28-year-old Karen Bruselario.

Alexis was born a woman, but lives as a man and Karen was born a man, but lives as a woman. Because of Argentina’s Gender Identity Law passed in May of 2012, the couple have both been able to legally change their genders without gender reassignment surgery, which meant that when they got pregnant via natural means, it was the man, Alexis, who carried the baby.

The baby was due on December 22 via scheduled C-section, but couldn’t wait. Alexis started having contractions the weekend before the scheduled birth, and the  baby was born ”early” weighing 9.37 pounds at Hospital Fermín Salaberry in Victoriain.

The couple named their baby girl Génesis Evangelina.

Alexis and Karen do not only hold the distinction of being the first transgender couple to give birth in Argentina they are also the first transgender couple to have gotten married while the groom was pregnant.

They officially tied the knot in November. 


BONGO MOVIES WAPATA VIONGOZI WAPYA-STEVE NYERERE ALA SHAVU KUBWA

$
0
0
Kundi la Bongo movie unity limepata  uongozi mpya wa club hapa nchini hapo jana baada ya kufanyika kwa uchaguzi wake kwenye viwanja vya leaders kinondoni jijini Dar es Salaam.

Katika uchaguzi huo viongozi wapya walichaguliwa ni;

Mwenyekiti.  Steven Nyerere.

Makamu mwenyekiti : Mahsein awadhi "Dr cheni"

Katibu mkuu:  William Mtitu

Katibu mkuu msaidizi : Devotha mbaga 

Mtunza hazina: Issa musa “cloud"

 Msaidizi wake ni:  Cathy rupia

GIZA NENE LATANDA NDANI YA CHAMA CHA CHADEMA

$
0
0
Giza nene limeendelea kutanda ndani ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), baada ya juzi kulazimika kuongeza muda wa kikao cha Kamati Kuu kusubiri uamuzi wa Mahakama Kuu kuhusu aliyekuwa Naibu Katibu Mkuu wake Zitto Kabwe.

Kikao hicho kiliendelea jana kikimhoji aliyekuwa Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya chama hicho, Dk Kitila Mkumbo, huku taarifa nyingine zikieleza kuwa Zitto Kabwe ameendelea na msimamo wake akituhumu chama hicho kuongozwa kwa ubabe.

Habari kutoka ndani ya kikao hicho kinachofanyika Hoteli ya Mbezi Garden jijini Dar es Salaam zinaeleza kuwa mkutano huo ulianza saa 4:00 asubuhi kwa kujadili ajenda zilizoshindwa kujadiliwa juzi, ambapo Dk Kitila alianza kuhojiwa saa 7:00 mchana.

Hata hivyo, taarifa hizo zinaeleza kuwa baada ya Dk Kitila kuingia kuhojiwa, aliwaomba  wajumbe amwite mwanasheria wake, ambaye anazifahamu vyema taratibu na sheria za chama ili amsaidie kujibu hoja.

Kazi hiyo ya Dk Kitila kutafuta mwanasheria ilichukua muda mrefu na akapatikana saa 11;00 jioni ndipo kikao kilipoanza.

Hata hivyo, kabla ya kuingia katika ukumbi huo wa mkutano, Dk Kitila aliliambia gazeti hili kuwa atatoa ufafanuzi wa msimamo wake baada ya kutoka ndani ya kikao hicho.

Hata hivyo, hadi saa 1:00 jioni jana alikuwa bado ndani ya chumba cha mkutano akihojiwa, huku taarifa zaidi zikieleza kuwa wajumbe wengi walikuwa wakimsihi Dk Kitila aombe radhi ili asamehewe, yaishe.

Baada ya kumaliza kuhojiwa saa 1:40 usiku, Dk Kitila alimwambia mwandishi  amemaliza kazi yake na anauachia uongozi kutoa uamuzi wake.

Mnyika

Awali akitoa taarifa ya kikao hicho, Mkurugenzi wa Mawasiliano na Uenezi wa chama hicho, John Mnyika alisema kuwa Kamati Kuu ilishindwa kuwahoji Dk Kitila na aliyekuwa mwenyekiti wa chama hicho Mkoa wa Arusha, Samson Mwigamba baada ya kuondoka mapema eneo la mkutano bila ya kuaga na kuzima simu zao. Alisema kwa sababu Chadema ni chama kinachoamini katika demokrasia, waliamua kuwatafuta kwa namna nyingine na kufanikiwa kuwapata jana asubuhi.

Mnyika alisema kuwa kama mmoja wa watu hao hatafika kuhojiwa mbele ya Kamati Kuu, basi chama kitachukua uamuzi kitakachoona unafaa dhidi yake.

Mjumbe wa Kamati Kuu apigwa

Katika hali isiyokuwa ya kawaida, Mjumbe wa Kamati Kuu ya Chadema, Shaaban Mwamba, juzi usiku alipata kipigo kutoka kwa maofisa wa  kikundi cha ulinzi cha chama hicho waliokuwa katika eneo ambalo mkutano wa Kamati Kuu ulifanyika, baada ya kutuhumiwa alikuwa akiwasiliana na wafuasi wa Zitto.

Taarifa kutoka kwa mjumbe mmoja ambaye hakupenda jina lake litajwe gazetini, ilisema kuwa mtu huyo alikuwa akichunguzwa na maofisa wa ulinzi wa chama hicho muda mrefu, kutokana na nyendo alizokuwa akizionyesha zilizotia shaka.

Mwandishi wa habari hizi ambaye alikuwa katika eneo hilo, alishuhudia kiongozi huyo akibebwa juu juu na maofisa hao, huku akiulizwa aliyekuwa akiwasiliana naye ni nani, kabla ya vijana wengine wa chama kumkamata na kumweka chini ya ulinzi, wakimtaka atoe ufafanuzi wa alichokuwa anakifanya.

Baada ya mahojiano ya muda mfupi, kiongozi huyo alionekana akiinuka na kwenda  kunawa kwenye bomba la maji, huku akitokwa damu mdomoni.

Taarifa zilizopatikana baadaye zilidai kuwa kiongozi huyo alikuwa akiwasiliana na mama yake Zitto na Katibu wa Zitto, Dk Alex na kwamba pia simu yake ilikutwa na ujumbe mfupi aliokuwa amewaandikia watu hao.

Gazeti hili lilijaribu kumtafuta kiongozi huyo ili kueleza sababu ya kupigwa kwake, lakini hakupatikana eneo la mkutano kwa madai kuwa alikwenda hospitali kupata huduma ya kwanza, lakini hakurudi.

Wakati suala la Mbunge wa Kigoma Kaskazini Zitto Kabwe na uongozi wa chama chake likiendelea kuwasumbua vichwa wapenzi wa chama hicho, inadaiwa kuwa baadhi wa wabunge, viongozi na wazee wa Chadema, wanataka suala hilo liishe mapema.

Habari ambazo gazeti hili lilizipata jana, zilisema kuwa baadhi ya viongozi hao walitaka Zitto aende Halmashauri Kuu ya Chadema na kuomba msamaha ili mambo yaishe.

“Walimfuata Kitila (Dk Kitila Mkumbo) wakamwambia amshawishi Zitto ili mambo yaishe nje ya mahakama, wanataka aende kwenye Halmashauri Kuu kuomba radhi. Kitila akawaambia kuomba radhi kwa kosa gani?” kiilisema chanzo hicho.

Zitto azungumza

Hata hivyo, Zitto aliliambia gazeti hili jana kuwa kumekuwa na jitihada  mbalimbali za wazee kutaka kukiepusha chama hicho na migogoro na kuwa amekuwa tayari kwa suala hilo. “Wazee walikuwa na wajibu wa kuhakikisha hatufiki hapa tulipofika. Sijui kama fursa hiyo bado ipo,” alisema Zitto.

Kuhusu uamuzi wake wa kwenda mahakamani alisema: “Nimekwenda mahakamani kutaka haki itendeke. Chama cha kidemokrasia kinanyima vipi mwanachama fursa ya kukata rufaa?

“Nisingekwenda mahakamani kama ningeona haki ikitendeka. Tatizo kubwa la chama chetu sasa kinaongozwa na mawazo ya kihuni na yeyote mwenye mawazo ya kujenga anaonekana msaliti.

UAMUZI WA YANGU KUJITOA KOMBE LA MAPINDUZI HAUKUWA WA BUSARA

$
0
0
Klabu ya Yanga ya Dar es Salaam imechukua hatua ya kushangaza ya kujitoa kwenye michuano ya Kombe la Mapinduzi inayoendelea Zanzibar katika dakika za mwisho.

Uongozi wa Yanga ulichukua hatua hiyo siku moja kabla ya mashindano hayo yanayoshirikisha timu 12 kutoka Kenya, Uganda na wenyeji Tanzania kuanza.

Kwa kweli hatua hii ilikuwa ya ghafla mno na tunaamini imewakwaza na kuwapa mtihani  mkubwa waandaaji wa mashindano hayo.

Itiliwe maanani kwamba mashindano hayo ya mwaka huu ni makubwa zaidi na yamepewa uzito mkubwa kwa vile yanafanyika wakati Zanzibar inasherehekea miaka 50 ya Mapinduzi. Kitendo cha Yanga kujiondoa kwenye mashindano hayo tena dakika za mwiso kimeshangaza hasa kwa kuzingatia uhusiano wa klabu ya Yanga na Mapinduzi ya Zanzibar.

Historia inaonyesha kuwa aliyekuwa Rais wa kwanza wa Zanzibar, Abeid Amani  Karume aliwahi kutumia fedha za wananchi wa Zanzibar katika kusaidia kujenga makao makuu ya klabu ya Yanga yaliyopo Jangwani, Dar es Salaam.

Sasa inashangaza kwa uongozi wa Yanga kusahau  historia hiyo na kujitoa katika mashindano yanayotukuza Mapinduzi hayo ya mwaka 1964.

Ukiacha suala hilo la kihistoria, mashindano hayo ya Zanzibar yalikuwa muhimu mno kwa Yanga katika maandalizi yake ya mzunguko wa pili wa Ligi Kuu Bara na michuano ya kimataifa ya Ligi ya Mabingwa Afrika ambayo wanashiriki mwaka huu.

Yanga ingeshiriki  mashindano hayo timu yake ingepata nafasi ya kujua upungufu na udhaifu wake kwani katika hatua za awali ingepambana na Azam ya Dar es Salaam na Tusker ya Kenya ambazo ni timu kubwa na ngumu.

Kuondoa benchi la ufundi na kuitumia kama ndiyo sababu ya kujitoa kwenye mashindano hayo hakutoshi kwani klabu kadhaa zimekuwa zikifukuza makocha lakini zinaendelea na mechi zinazowakabili.

Kama uongozi wa Yanga ungekuwa umejipanga vizuri ungekuwa tayari na kocha mpya ambaye angeitumia michuano ya Kombe la Mapinduzi kuona na kufahamu aina ya wachezaji alionao. Yanga ni lazima ijifahamu kuwa ni klabu kubwa na yenye mashabiki wengi nchini kwa hiyo inatakiwa kutafakari kwa makini kabla ya kuchukua uamuzi wowote ule.

Ni dhahiri kwamba kujitoa kwa Yanga kwenye mashindano hayo kutawaathiri sana waandaaji hasa kwenye mapato kwani mechi za Yanga zilitarajiwa kuwavutia mashabiki wengi.

Lakini, kama Yanga ingejitoa mapema katika mashindano hayo na kuukataa mwaliko wa kushiriki kungewapa nafasi waandaaji kualika timu kubwa kwenye mashindano hayo na ambayo ingepata nafasi ya kujiandaa kabla ya kwenda kwenye mashindano.
Viewing all 104796 articles
Browse latest View live




Latest Images