Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104803 articles
Browse latest View live

Diamond Platnumz Kuingia Kwenye Jumba la BBA Hotshots leo (Nov 27) Kupiga Story na Washiriki

$
0
0
Diamond Platnumz tayari ametua jijini Johannesburg, Afrika Kusini toka jana, tayari kuhudhuria tuzo za Channel O (CHOAMVA) zinazotarajiwa kutolewa siku ya Jumamosi Nov.29 akiwa anawania vipengele vinne.

Staa huyo ambaye ameachia ngoma mpya siku chache zilizopita ‘Ntampata wapi’, ameandika kupitia akaunti zake za mitandao ya kijamaii kuwa pia leo Alhamisi Nov.27 atapata nafasi ya kuingia kwenye jumba la Big Brother kubadilishana mawazo na washiriki.

“Tafadhali usikose kuangalia Big Brother Afrika kuanzia saa tano Asubuhi kesho (leo), kijana wako Platnumz ntakuwa ndani ya nyumba nikizoza mawili matatu na washiriki….” aliandika Diamond.

Baada ya ishu ya Escrow, Haya ni Majibu Mawili ya Waziri Mkuu Pinda ikiwemo Kujiuzulu

$
0
0
Kikao cha Bunge leo Novemba 27 kimeanza kwa maswali mawili kuulizwa na Kiongozi wa Kambi ya Upinzani Bungeni Freeman Mbowe kwa Waziri Mkuu Mizengo Pinda
.
“…Chini ya uongozi wako kama Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na ukiwa kiongozi wa shughuli za Kiserikali Bungen, tumeiona Serikali ikikumbana na matatizo na vikwazo vingi ikiwemo ‘Operesheni Tokomeza’ ambayo ilipelekea wananchi wengi kupoteza maisha na wengine kupata vilema…“– Mbowe.

Tumeona mauaji ya raia yakiendelea Kiteto, kashfa kubwa ambayo iko current sasa hivi ikiwa ni pamoja na kauli zako ulizowahi kuzisema kwamba fedha zilizopotea za akaunti ya Escrow hazikuwa fedha za umma bali zilikuwa fedha za watu binafsi…“– Mbowe.

Baada ya Ripoti ya CAG kutolewa hadharani kuhusiana na fedha za Escrow na baada ya Ripoti ya PCCB kutolewa na hatimaye jana hapa Bungeni kusomwa taarifa ya Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali, nini msimamo wako kuhusu kauli yako ya awali kwamba fedha zile zilikuwa ni za watu binafsi na sio fedha za umma?“– Mbowe.
Kwa uzito huo ukichanganya na matukio mengine mbalimbali ambayo yamepelekea fedheha kubwa kwa taifa letu, huoni kama ingekuwa muafaka kwako binafsi na taifa kupumzika kidogo ili kupisha nafasi kwa watu wengine kuweza kumalizia ngwe hii ya utawala wenu?”– Mbowe.
Akijibu maswali hayo, Waziri Mkuu Mizengo Pinda amesema; “…Inawezekana Mheshimiwa Mbowe una shauku ya kutaka litokee hilo lakini mambo haya yanategemea kama ndivyo Mungu kapanga au hapana…“

Ningeweza nikajaribu kukujibu lakini sina sababu ya kufanya hivyo, sina sababu ya kufanya hivyo kwa sababu suala lenyewe ndiyo subject ya mjadala hapa Bungeni ambao unaanza leo.. Tusubiri mjadala utakavyokwenda naamini na mimi nitapata nafasi ya kusema mawili matatu, kwa hiyo nadhani mwisho wa yote Bunge litakuwa limefikia mahali ambapo tunaweza tukasema kwa uhakika ni hatua stahiki namna gani inaweza kuchukuliwa…” Waziri Mkuu Mizengo Pinda.

Baada ya majibu hayo, Mbowe alipata nafasi ya kuuliza swali la nyongeza kwa Waziri Mkuu; “…Pamoja na kwamba jambo hili litajitokeza baadaye katika mijadala ya leo, bado haiondoi ukweli kwamba una wajibu wa kulijibu swali langu. Naomba kwa heshima sana nikuulize tena kwa mara nyingine, taifa limepata fedheha kubwa sana kutokana na sakata hili, nchi nzima inasikiliza tatizo hili…“– Mbowe.

“…Una heshima kama kiongozi wa Serikali lakini heshima ambayo itakuwa imethibitishwa zaidi kama utaamua kujiwajibisha mwenyewe ili kuweka heshima yako na heshima ya Serikali, je kwa mara nyingine huoni ingekuwa vema kama basi utujibu kama unafikiri bado zile fedha ni za umma kama hutaki ku-declare kujiuzulu katika hatua ya sasa?”– Mbowe.

Nimekurekodia sauti ya wakati maswali hayo yakiulizwa na kujibiwa Bungeni leo Dodoma, unaweza kusikiliza kwa kubonyeza play.

The Nyama Choma Festival Dar 6 Desemba – Jipatie tiketi yako kwa shilingi 7,000 tu

$
0
0
Tembelea vituo vya mauzo ujipatie tiketi yako Sasa.

1.Samaki Samaki-Mlimani City Na Posta

2.Tripple 7 Kawe

3.Didis Oysterbay

4.Born 2 Shine Mwenge

Mwanamke ni Kiumbe katili Kuliko Hata Unavyofikiria

$
0
0
Mara nyingi sana watu wamekuwa wakiwasifu wanawake kwamba ni watu wapole lakini ukweli haupo hivyo.

Mwanamke ni mtu wa maamuzi ya haraka na pengine anapotaka kufanya jambo huwa hafikiri madhara yake huwa anakuja kutafakari wakati nambo yamesha haribika.

Mwanamke akiwa na hasira anakutoa roho muda wowote na anabadilika tabia muda wowote. Ukitaka kuamini embu siku moja muulize mkeo kwamba hivi nikizaa nje mtoto upo tayari kuishi naye halafu usikie majibu atakayokupa. Niliwahi kumueleza mke wangu nataka kuoa mke wa pili jibu alilonipa kwamba nisimtafutie mada kesi tafadhari , jibu ambalo mpaka leo huwa najiuliza alikusudia nini.

Mwanamke si mtu wa kumsaidia kwa sababu hawana shukrani na wepesi mno kusahau fadhira walizo tendewa. Unaweza kuwa na mke ukampa kila kitu lakini siku moja akimpata wa nje utapata tabu.

Wanawake ni wepesi sana kudanganyika hata asome vipi ni wachache mno unao weza kuwakuta na misimamo imara.


Au siku moja partner wako akiwa na mimba jaribu kumwambia mimba hii nina mashaka si yangu halafu uone response ya kikatili utakakuta katoto kenyewe kametupwa jalalani huko .

Asali Asili (Nature Honey) Inapatikana Kwa Bei Poa Kabisa

$
0
0


Ngase Company Limited Inakuletea Asali Asili Kabisa ikiwa imepakiwa Kwenye Chupa kwa usafi wa hali ya juu, 

PACKAGES & PRICE
Carton of 12 Jars of 500g Each, Price is 96000/= Per Carton

Wanapatikana Tegeta Wazo Hill
Wasiliana Nao Kwa Number zifuatazo:

TEL: 0737 209890
MOB:0756669494
0655418466
0777418466

E –mail: sales@ngasecompanyltd.com
ngamanya.kitangalala@ngasecompanyltd.com



ESCROW:Majibu ya PROF MUHONGO ni Aibu ya Mwaka kwa PAC na Wasaka Tonge

$
0
0
Kwa aliyefatilia majibu ya waziri wa nishati na madini profesa Sospeter Muhongo leo bungeni akijibu hoja za kamati ya PAC atakubali kuwa kamati ya ZITTO KABWE imewadanganya watanzania. Muhongo ambaye amejibu hoja moja baada ya nyingine kwa kutoa ushahidi wa viambatanisho muhimu amedhihirishia bunge kuwa kamati ya bunge imetoa taarifa ya uongo. 

Katika majibu yake, profesa Muhongo amedhihirisha kwa ushahidi kuwa pesa za ESCROW hazikua za serikali. Pesa hizo ni za IPTL na kwamba serikali bado inadaiwa kiasi cha shilingi bilioni 94 na IPTL kama malipo ya kufua umeme. 
Aidha, Muhongo amemlipua mwanasheria Mkono ambaye aliingia mkataba na TANESCO wa kuwa mwanasheria wao na alidai na kulipwa kiasi cha bilioni 62 (robo ya pesa za ESCROW) kama malipo ya uanasheria. Mkataba huu ulivunjwa na TANESCO chini ya uongozi wa waziri Muhongo. 

Majibu haya ya Muhongo yameivua nguo kamati ya PAC na kuzua maswali mengi yasiyo na majibu. 
Kwanini PAC ilidanganya bunge? 
Kwanini PAC haikuonesha vielelezo hivyo? 
Nani yako nyuma ya PAC? 
Kwanini PAC haikutaja ufisadi huu wa Mkono? 
Taarifa kuwa wasaka Urais wa CCM ndio waliopika uongo huu tuziamini? 

Mahakama Kuu Yamwachia Huru Sheikh Ponda Leo

$
0
0
MAHAKAMA  Kuu ya Tanzania imemuachia huru aliyekuwa Katibu wa Taasisi za Kiislam, Sheikh Ponda Issa Ponda baada ya kuona hana hatia dhidi ya Kesi ya madai ya Ardhi ya Agrekanza inayomilikiwa na Afidhi Self  iliyokuwa inamkabili.

Akisoma Mashtaka hayo Mwanasheria wa Serikali, Tumaini Kweka mbele ya Jaji, Augustino Shangwe alisema baada ya kupitia vifungu vyote mahakama imejiridhisha na kuona Sheikh Ponda hana hatia yoyote na kumuachia huru tangu leo lakini katika hali ya kushangaza Sheikh Ponda amerudishwa rumande akisubiri kesi nyingine ya madai ya uchochezi,  Mkoani Morogoro inayomkabili.

Diamond Platnumz na Zari the Lady Boss Waumbuka Vibaya

$
0
0
Stori: Imelda mtema
Licha ya madai wanayoyatoa mastaa wawili hot kwa sasa, Nasibu Abdul ‘Diamond’ na Zarinah Hassan a.k.a Zari au The Boss Lady kuwa si wapenzi bali kuna project wanaifanya, wawili hao wameumbuka.
Kuumbuka huko kumekuja kufuatia kuvuja kwa picha inayowaonesha mastaa hao wakidendeka huku wakiwa kwenye hisia kali.

Katika picha hizo ambazo kwa sasa zinapatikana mtandaoni, Zari anaonekana akiwa amevaa kofia ya Diamond wakionekana wenye furaha na baadaye wakahamia kwenye kupeana mahaba.
Aidha, picha ambayo inawaumbua ni ile ya kudendeka ambapo baadhi ya wadau walioiona walisema, inavyoonekana projecti wanayoifanya imevuka mipaka.

“Wasitutanie bwana, hivi kweli kwa picha hii watasema ni projekti? Hawa ni wapenzi ila hawataki tu watu wajue,” alisema mdau mmoja aliyejitambulisha kwa jina la John baada ya kuona moja ya picha hizo.

Awali, Diamond ambaye hivi karibuni alimwagana na mpenzi wake Wema Sepetu alinukuliwa akisema kuwa, watu wasidhani yeye na Zari ni wapenzi bali kuna projecti wanayoifanya.

Licha ya madai hayo, wengi wamekuwa hawaamini kutokana na ukaribu uliopitiliza na picha zinazoendelea kuvuja huku wakisema, kama ni wapenzi bora waseme kwani wote wako singo kwa sasa.

Mwigizaji Johari Adaiwa Kunaswa Kwa Mganga wa Kienyeji Akifanya Mambo

$
0
0
Stori: Hamida hassan na Gladness Mallya
STAA wa filamu za Kibongo, Blandina Chagula (pichani) maarufu kama Johari, hivi karibuni alidaiwa kuonekana akiingia nyumbani kwa mganga wa kienyeji (jina linahifadhiwa) katika Kijiji cha Kibeta, mjini Bukoba mkoani Kagera.

Chanzo chetu cha habari kimedai kuwa Johari akiwa katika bodaboda, aliingia kwa mganga huyo wa kike anayefahamika sana eneo hilo.

“Sijui nilikuwa namfananisha? Nimemuona msanii wenu hapa Kibeta akiingia kwa mganga ila nimeshindwa kumpiga picha maana kasimu kangu ni ka’ tochi, labda kaja kuweka mambo yake sawa,” kilidai chanzo hicho.

Baada ya kunyetishiwa habari hizi, mwandishi wetu fasta alibonyeza namba za Johari katika simu yake ambaye alikiri kuwepo Bukoba kwa siku mbili kwa shughuli zake.

“Jamani siyo kila kitu muandike, mmejuaje mimi nilienda Bukoba, naomba hii isiwe habari tafadhali si ulimwengu mzima ujue mimi nimefanya nini,” alisema Johari, mmoja wa waigizaji nyota na mkurugenzi mwenza wa RJ Company.

Katika kujitetea zaidi, Johari alisema alikwenda Bukoba kwa mama yake mkubwa, (jina linahifadhiwa) ambaye hakujua kama anajishughulisha na mambo ya uganga kwani hakuwahi kusikia.

“Sikupenda hii habari kabisa, lakini kiukweli nilienda kumuona mama yangu mkubwa nikiwa na ndugu zangu wengine, kwani alikuwa akiumwa,  sikukaa sana, nilikaa siku mbili tu na kugeuza kwani nilikuwa nikitokea Shinyanga kwenye msiba kama ulisikia nilifiwa,” alisema na kuongeza kuwa hajawahi kupanda pikipiki kwani magari yapo tena kwa bei rahisi.

Irene Uwoya Amfuata Mumewe Ndikumana Nchini Rwanda

$
0
0


Star wa filamu Tanzania Irene Uwoya ambaye ndoa yake na Ndikumana Katauti wa Rwanda iliingia katika gogoro zito na kila mtu kuishi peke yake wanataka kuishi tena pamoja !.....Picha mpya za Irene Uwoya akiwa na Ndikumana zimetoka. Inadaiwa kuwa Uwoya alienda Rwanda kumtembelea Ndikumana ambaye wamezaa mtoto mmoja. Hizi picha zinaonyesha kama vile Uwoya alikuwa akiagwa na Ndiku kurudi Tanzania ingawa Uwoya anaonekana hana raha na sababu bado haijulikani.

Je kwakwuangalia picha hizo, unamzungumziaje Irene?

Lowassa Afunguka 'Sakata la Richmond Hakuna Aliyesimama Kunitetea Leo Wanasimama Kutetea Wizi wa Wazi'

$
0
0
Haya ndio Maneno aliyoyasema Lowassa Kupitia Account yake ya Twitter kuhusu Sakata la Wizi wa Pesa za IPTL:

 


Baba Askofu Kilaini Akiri Kupokea Milioni 80.5 Kutoka kwa Rugeemanila

$
0
0
Askofu msaidizi wa jimbo la Bukoba Methodius Kilaini amekiri kupokea milioni 80.5 kutoka kwa James Rugemalira na akisema hii si mara yake ya kwanza kupokea fedha toka kwa mfanyabiashara huyo kwakuwa mara nyingi huwa anachangia kwa uwazi miradi ya jamiii. Na michango amesema michango inayopelekwa kwake haina siri hivyo washikwe wezi halisi sio yeye

Lemutuz:Waliopokea Pesa za Escrow ni Wezi kama Wezi Wengine wa Kuku na Mbuzi Warudishe Haraka Sana

$
0
0
Well, mwisho wa yote kuna Viongozi wengi wametajwa kuhusika na kupewa pesa za Escrow na hakuna aliyetajwa kuzikataa na so far sijaona popote inaposemwa kwamba kazi waliyoifanya ili kupewa na kupokea pesa hizo, na naomba niwe mkweli kati ya wote walioatajwa kupokea pesa hizo nimeshitushwa sana na Wawili, yaani Waziri Mama Tibaijuka na Askofu Kilaini I mean wengine sikushitushwa sana maana some of them tumewazoea na habari za rushwa all the times.

Mama Tibaijuka, hivi kweli anaweza kusimama mbele ya umma na kusema pesa alizopewa sio chafu? Hivi ni kweli alipokuwa UN aliwahi kupokea pesa za namna hiyo? Sasa kwa nini anakuja kupokea akiwa Waziri wa CCM? Askofu Kilaini hata na yeye naye anaweza kweli kukubali kupokea Shillingi Millioni 80 bila ya kuzifanyia kazi inawezekana vipi? Hizi pesa walipewa za Rushwa nia na madhumuni ilikuwa kuwanunua their influence, wamekamatwa red handed tunapoteza muda kujadili bungeni kujadili nini na ukweli upo wazi kuwa wamepewa pesa na wamezipokea!

- Kwanza warudishe hizo pesa kwa waliowapa, and then hatua za kinidhamu zichukuliwe na hasa kutoka kwa Chama cha Mapinduzi, wale wote walio wanachama wa CCM waliopokea hizo pesa chafu wachukuliwe hatua na ikibidi waende Mahakamani kwa kupokea Rushwa, huyo Askofu watajijua wenyewe huko Kanisani kwake ila I hope hatahubiri tena ila ndio maana sijawahi hata kumsikiliza nilishamshitukia siku nyingi kuwa hayupo kwenye mstari na Mungu, wanajifanya kupiga piga kelele za siasa kumbe wanatafuta mlo tu na hizi siasa za kuwachanganya Maaskofu sijui tumezianza lini Tanzania.

- Warudishe Pesa chafu ni za Rushwa na halafu waadhibiwe na CCM and then Sheria ichukue mkondo wake si kuna Rushwa hapo!!

Le Mutuz

CCM yabariki wizi wa ESCROW, UKAWA pekee tegemeo la wananchi

$
0
0
Ripoti ya BUNGE kupitia Kamati ya PAC sasa inakataliwa kutokana na maslahi ya CHAMA, Chama kimekuwa pango kuu la wezi na hivyo kwa maneno ya Warioba CCM Maslahi. CCM imani imebaki kwa Butiku na wenzake pekee.

Kitendo cha Nagu kusema kuita watu wezi sio vizuri bila kusema kama kuiba ni vizuri ni dhahiri kuwa CCM haina kinyaa tena na wezi, mafisadi wala watu wenye tabia za kutowajibika ktk kazi kama Pinda.

CCM imeshindwa kutetea umma na hivyo kutetea maslahi yake na wanachama wake viongozi pekee huku wanachama wadogo wakiachwa kuishi kwa bahatisha za maisha.

Maneno ya Kibajaji kuwa kumpatia mtu hela haliwezi kuwa kosa, ni kuthibitisha kukosa kwa maadili ndani ya chama mchana kweupe, mtumishi wa umma anapatiwa fedha na mtoa huduma za jamii kwa mikataba ambayo kila siku inabishaniwa kuwa ni ya wiz wizi. Haingii akili mwa mtanzania isipokuwa mwanaccm tu kuwa waziri wa nishati wastaafu na aliopo wapate chochote, ag mstaafu na aliyepo atape chochote, mawaziri kama tibaijuka apate chochote, watumishi wa umma na wengine wa TRA wapate chochote kutoka kwa mtu mmoja bila kujua hela hiyo ni hongo kwa namna fulani. mbona hajagawia watu tu mitaaani? ni wazi wamepewa hela kwa nyazifa zao. na ni rushwa.

Rais yuko kimya, na uozo huu. Serrikali inadai hela ni za mtu binafsi, je iweje ag na cag watoe maelekezo ya kutoa na kukagua fedha za mtu binafsi??? JK tujibu hilo.

Tukishindwa kwa hili basi jamii ya tanzania bila kujali hasara na mwelekeo wa mbele, inapaswa tukatae kwa nguvu zote watu wa namna hii wizi wa namna hii, na matumizi mabaya ya ofisi.

Nawasilisha

Audio: Msikilize Jide Akithibitisha Rasmi kuwa Amemuacha Gadner

$
0
0
Hatimaye Lady Jaydee amethibitisha kwa kauli yake mwenyewe
kuwa ndoa yake na mtangazaji mkongwe wa redio, Gadner G
Habash imevunjika.
Akiongea leo kwenye Exclusive Friday ya kipindi cha Sunrise cha
Times FM, Jaydee amesema ni yeye ndiye aliyeamuacha Gadner.
Kwenye mahojiano hayo, Jide alizungumzia kuwa kwenye
uhusiano na mtu aliyekuwa akimpiga mara kwa mara licha ya
kutomtaja moja kwa moja kuwa ni Gadner lakini alisema alikuwa
akiteswa.
Kabla ya kuamua kuusema ukweli huo, Jide aliweka wazi kuwa
siku zote amekuwa akiepuka kuongea masuala yake binafsi
kwenye vyombo vya habari.
“Kitu kimoja ambacho ningependa watu wafahamu, mimi sio mtu
ambaye huwa napenda kuongea maisha maisha yangu kwenye
media, kwenye magazeti au wapi,” alisema. “Na ndio maana lolote
ambalo linaendelea ndani ya nyumba yangu au kwenye maisha
yangu, sijawahi kulitoa nje. Ni watu wanaongea chochote
wanachohisi, chochote wanachotaka kusema. Ninavyofikiria mtu
anayenipenda mimi alinijua sababu ya muziki na waendelee
kuliheshimu hilo, kwasababu kila mtu ana haki ya kuwa na
privacy. Ingekuwa kila mmoja angekuwa anatoka kwake anaanza
kuelezea mambo yake, mama yake jana walishinda njaa, au
mume wake alimfanya hivi, sidhani kama kuna mtu yeyote
anapenda kuelezea maisha yake, hata matatizo yake mbele za
watu.”
“Kwahiyo mpenzi wako Gadner bado mko naye,” aliuliza mmoja
wa watangazaji wa kipindi hicho na mchekeshaji, MC Pilipili.
“Swali nafikiri hujalijibu, umemtosa, hujamtosa?,” aliuliza Fadhil
Haule, mtangazaji mwingine wa show hiyo.
“Nimemuacha,” alijibu Jide. “Huyu (Gadner) tumeshamalizana.”
Isikilize interview hiyo hapo chini.

Diamond Azidi Kuchanja Mbuga achaguliwa Kwenye 'We Are The world Africa'

$
0
0
Hahaha muzeee wa project a.k.a msaniii bora East africa A.k.a ngazi ya waliopotea amechaguliwa kwenye Le project mpya ya We are the world africa

Project hiyo imewashirikisha wasanii wote bora kutoka Afrika ,kwa kutambua uwezo nafasi ya Dai hawakusita kumchagua.....

Tokea kuisha kwa fiesta haya ndio matukio makubwa aliyofanya Dai huku wale wasanii wa fiesta wakisubiri mwakani msimu wa fiesta uanze..

1. Kupiga shoo zaidi ya 15 hapa tz na nje

2. Kuperfom kwenye Big brother

3. Kutoa nyimbo mpya yenye Video kali saana

4. Kuvunja rekodi za youtube, mkito.com na Mziiki.com

5. Kutoa nyimbo na msanii kitoka Nigeria "Waje"

6. Kuujaza uwanja(stadium) Iringa yeye mwenyewe

7. Kuchaguliwa kwenye Project ya We are te world Afrika

8. Jana Kuingia Kwenye Jumba la Big Brother Kupiga Mastori na Washiriki

9. Stil counting



Utaipendraaaaaaaaaaaa

Mkombozi Bank: Hatujihusishi na Hatutajihusisha na Utakatishaji wa Fedha Chafu

$
0
0
Utangulizi
Taarifa hii inatolewa kwa umma kutokana na ripoti mbalimbali zilizotolewa na baadhi ya vyombo vya habari mitandao ya kijamii na taarifa iliyotolewa kwenye mjadala katika Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

1. Ufunguzi wa akaunti ya VIP engineering and Marketing (VIP)


Kampuni ya VIP engineering and Marketing ni kampuni ambayo imesajiliwa kwa mujibu wa sheria za Tanzania. Kampuni hii ilifungua akaunti katika benki ya biashara ya Mkombozi na hivyo kuwa moja kati ya wateja wa benki. Benki ilijiridhisha na ilizingatia taratibu zote za ufunguzi wa akaunti husika kwa kuzingatia sheria za nchi na kanuni zinazozitaka benki kupata nyaraka muhimu kutoka kwa mteja wakati wa ufunguzi wa akaunti hiyo. 

Nyaraka hizo ni pamoja na kuwepo kwa cheti cha usajili wa kampuni, kanuni za kampuni, idhinisho la kampuni kumruhusu moja kati ya wanahisa wake kuendesha akaunti pamoja na picha na hati ya kusafiria ya mhusika wa kuendesha akaunti hiyo.

2.0 Mauzo ya hisa za VIP

Kampuni ya VIP ilileta mkataba kwenye benki ya Mkombozi wa mauziano ya hisa za asilimia 30 baina ya VIP na kampuni ya Pan Africa Power Solutions (PAP) ambazo inamiliki katika kampuni ya IPTL. Mkataba huo ulisainiwa tarehe 19 Ogasti, 2013. Bei ya asilimia 30 ya hisa hizo ilikuwa ni dola za Marekani milioni 75. Katika kifungu namba 2.4 cha mkataba wao kinaelekeza fedha za mauzo ya hisa zilipwe kwenye akaunti ya VIP iliyopo benki ya Mkombozi. Mkataba huo wa mauziano ya hisa baina ya kampuni hizi mbili ulitambuliwa na hukumu ya Mahakama Kuu ya Tanzania iliyotolewa na Jaji J.H.K Utamwa tarehe 5 Septemba, 2013.

3. Mchakato wa kulipa kodi ya serikali


Benki ilitambua kwamba katika mauziano hayo ya hisa ni lazima kodi ya Serikali ilipwe na hivyo iliizishauri pande zote mbili kupeleka mkataba husika katika ofisi za Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) ili kufanyiwa makadirio ya kodi husika. Tarehe 20 Januari, 2014 TRA iliiandikia barua kampuni ya VIP na nakala ya barua hiyo kuletwa kwenye benki ya Mkombozi. Katika barua hiyo TRA iliitaarifu kampuni ya VIP kuwa makadirio ya kodi yatokanayo na mauzo ya hisa ni shilingi 38,186,584,322.00 ikiwa ni kodi ya mauzo ya hisa ya asilimia 30 za mauzo ya hisa kutoka VIP kwenda kwa PAP.(Capital gains and stamp duty). 

TRA pia iliiagiza benki ya Mkombozi kuhakikisha kuwa inalipa kodi hiyo kwa niaba ya VIP mara tu fedha zitakapoingia kwenye akaunti yake.

Malipo ya kodi ya shilingi 38,186,584,322.00 yalilipwa TRA kwenye akaunti 11120100 iliyopo katika Benki Kuu ya Tanzania na TRA ilikiri kupokea kodi hiyo kwa barua yake yenye kumbukumbu namba 3-4/100/100/223/4 ya tarehe 24 Januari, 2014.

4. Ufafanuzi wa mambo mbalimbali


4.1 Benki ya mkombozi kuhusika katika kusafisha fedha chafu

Fedha zote zilizoingizwa kwenye akaunti ya VIP iliyopo kwenye benki ya Mkombozi zilitokana na mauziano ya hisa kati ya VIP na PAP kwa mkataba uliotambuliwa na Mahakama Kuu ya Tanzania. Chanzo cha malipo hayo ni kuhamisha fedha kutoka kwenye akaunti ya PAP iliyopo katika benki ya Stanbic na kuingizwa kwenye akaunti ya VIP iliyopo katika benki ya Mkombozi. 

Fedha hizo zilihamishwa katika mafungu mawili. Fungu la kwanza ilikuwa ni shilingi 73,573,500,000.00 zilihamishwa kwa njia ya TISS kwa kumbukumbu namba 000000050720 ya tarehe 23 Januari, 2014 na fungu la pili ni dola za Kimarekani 22,000,000.00 zilihamishwa kwa TISS kwa kumbukumbu namba 000000050812 ya tarehe 23 Januari, 2014. Malipo mengine ya asilimia kumi ya mauzo ya hisa yalilipwa kwenye akaunti ya Mkombozi iliyopo Benki Kuu ya Tanzania. Kutokana na mchakato huo benki ya Mkombozi ilijiridhisha kuwa fedha hizo ni malipo halali na siyo fedha chafu. 

Benki ya Mkombozi haijihusishi na utakasishaji wa fedha chafu na haramu katika uchumi wa Tanzania.

4.2 Malipo yatokanayo na akaunti ya VIP

Malipo toka kwenye akaunti ya mteja hufanywa kutokana na maelekezo ya mteja. Benki ikishajiridhisha kuwa fedha ya mteja ni halali na ipo kwa mujibu wa sheria na hamna zuio lolote toka katika mahakama hapa nchini hutekeleza malipo kwenye akaunti ya mteja kutokana na maelekezo yake. 

Benki ilijiridhisha kuwa malipo yote yaliyofanywa kutoka kwenye akaunti ya VIP ni halali kwa kuwa chanzo cha pesa hizo ilikuwa ni halali kutokana na mauzo ya hisa na ulipwaji wa kodi ya Serikali kama ilinyoelezwa hapo juu. Kutokana na sababu hiyo benki haikuwa na shaka juu ya malipo hayo.

4.3 Malipo taslimu kwa wateja na kubeba fedha kwenye viroba, mifuko ya rambo na magunia

Benki inatoa tamko kuwa malipo yote yaliyofanywa katika akaunti ya VIP yalilipwa kupitia akaunti za walipwaji. Hakuna fedha zilizolipwa taslimu kwa wateja na kubebwa kwenye viroba au magunia kama ilivyoripotiwa Bungeni. Pesa iliyotoka kwenye akaunti ya VIP tarehe 6 Februari, 2014 kiasi cha shilingi 3,314,850,000.00 ililipwa kwenye akaunti nane za wateja tofauti na siyo kubebwa kwenye viroba au magunia. 

Na zile zilizotoka toka benki ya Stanbic zilizotajwa hapo juu zilitumwa kwa njia ya TISS na siyo kubeba kwenye magunia au viroba.

4.4 Malipo kwa mfanyakazi wa benki ya Mkombozi

Gazeti la Mawio la tarehe 20-26, Novemba, 2014 tolea namba 0122 liliandika kuwa mwanasheria wa benki ya Mkombozi ajulikanaye kwa jina la Rweyengeza Alfred alipokea malipo toka akaunti ya VIP ya shilingi milioni 40.2. 

Benki inatoa tamko kuwa haina mfanyakazi anayetambuliwa kwa jina hilo na wala hakuna mfanyakazi yeyote wa benki aliyelipwa fedha toka kwenye akaunti ya VIP.

Wito kwa umma

Benki ya Mkombozi inachukua fursa hii kuwatarifu wateja wake na umma kutopotoshwa na taarifa au tuhumma zilizofafanuliwa hapo juu na kuwataka wateja wake wote kutokuwa na hofu yeyote kwani benki ipo imara na inafanya kazi kwa kufuata misingi ya sheria, taratibu na kanuni zilizowekwa na Benki Kuu ya Tanzania. Benki inawataarifu wateja wake na Watanzania kwa ujumla kutoyumbishwa na tuhumma hizo ambazo hazina ukweli ndani yake na badala yake waitumie benki yao kwa shughuli za maendeleo ya nchi yetu.

Pamoja tunajenga nchi na uchumi wa nchi yetu.

Hitimisho

Benki ya biashara ya Mkombozi haijihusishi na haitajihusisha na utakasishaji wa fedha chafu.

Imetolewa na:

MKURUGENZI MTENDAJI BENKI YA BIASHARA YA MKOMBOZI

Hakika Wasomi Ndio Wanao Itafuna Hii Nchi

$
0
0
Makala: Sifael Paul
Hatuwezi kunyamaza! Kuhusu uchotwaji wa fedha nyingi za umma, za wavuja jasho Watanzania kiasi cha Sh. bilioni 306 zilizopotea katika Akaunti ya Tegeta Escrow kwenye Benki Kuu ya Tanzania kwa ajili ya kununulia umeme wa Kampuni ya IPTL, pasi na shaka utakubaliana nami kuwa wasomi ndiyo wanaoitafuna nchi hii.

Hii ni kashfa kubwa hasa inapoonekana wajanja wachache ambao ni wezi wanaojulikana kwa majina ndiyo wanaohusika. Tukubaliane kuwa si kweli Tanzania haina wasomi, wataalam na wazoefu katika nyanja mbalimbali kiasi cha kushindwa kung’amua wizi huo uliopitia kwenye mikono ya wasomi waliobobea serikalini. Nitawagusa watajwa wachache.

Kuanzia kwenye Wizara ya Nishati na Madini, waziri wake, Profesa Sospeter Muhongo ni msomi wa ngazi ya uprofesa aliyebobea katika masuala ya ‘jiolojia’ hivyo si kweli kwamba hakujua kikamilifu kazi yake katika masuala ya nishati ya umeme. Pia naibu wake, Stephen Masele naye ni msomi.

Wakati Eliakim Maswi anachukua nafasi ya ukatibu mkuu wa wizara hiyo baada ya David Jairo kukumbwa na kashfa, tuliamini kwamba mambo yatakuwa shwari kwa kuwa alionekana msomi mzuri. 
Hata hivyo, fedha ni shetani na la kuvunda halina ubani kwani ndiye anayetajwa kuratibu kila kitu kwenye sakata la wizi huo. Hapa nimegusa watu watatu tu wizarani hapo.

Huwezi kuamini wizara hiyo imejaa wasomi wa ngazi za udaktari (PHD), mainjia na wataalam lukuki. Inashangaza kuona tukiibiwa na wenyewe wapo maofisini wanapigwa kiyoyozi na kufurahia maisha na familia zao huku Watanzania wakitaabika.

Kuhusu Tanesco ndiyo usiseme, mkurugenzi wake, Mhandisi Felchesmi Mramba na bodi ya Tanesco imejaa wasomi. Nani kawaloga hata washindwe kuona tatizo katika mkataba wa IPTL hadi kuwe na wizi wa fedha za kutosha kujenga hospitali za hadhi ya Muhimbili zaidi ya kumi?

Kwa upande wake, Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Jaji Feredrick Werema ni msomi wa sheria kwa ngazi ya juu kabisa.Werema amepitia vyuo vikuu vikubwa duniani vikiwemo Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na Chuo Kikuu cha American Graduate School (Marekani).

Pia amepitia vyuo vingine huko Italia, Uingereza na Bolivia. Huko kote, Werema alibobea kwenye masomo ya mikataba ya ubinafsishaji wa makampuni ya umeme hivyo hakuwa mgeni kwenye sakata hili la IPTL na Tegeta Escrow kiasi cha kupoteza Sh. bilioni 306 kirahisi kiasi hicho. Labda kama alifumbwa macho asione.

Kwa upande wa Benki Kuu ya Tanzania, gavana wake, Profesa Benno Ndulu ni msomi mkubwa kwa ngazi ya uprofesa wa masuala ya uchumi akipitia na kufundisha vyuo vikuu kikiwemo North-Western huko Evanston, Illinois, Marekani. Pia amefanya kazi kwenye Benki ya Dunia hivyo anajua vizuri majukumu yake. Mbali na kichwa chake, pale Benki Kuu ya Tanzania anafanya kazi na wasomi wa kila namna kwenye nyanja ya uchumi.

Swali ni je, ilikuwaje fedha ikayeyuka kwenye akaunti hiyo ndani ya Benki Kuu? Ina maana wote walipigwa ganzi wasing’amue mchezo au nao walishiriki?

Huku akipachikwa jina la Mtoto wa Mkulima, akikalia kiti kilichoachwa na Edward Lowassa aliyejiuzulu Februari 7, 2008, Waziri Mkuu Mizengo Pinda, anayeaminika kwa uadilifu amejikuta akiingia kwenye kashfa hii kwa kuwa tu ni mtendani mkuu wa serikali.

Kinachotokea kwa Pinda ni kuwaamini hao tunaowaita wasomi bila kuthibitisha na kujikuta akitoa kauli ambazo Kamati ya Bunge ya Kudumu ya Hesabu za Serikali (PAC) imethibitisha kwamba fedha zilizopotea ni za umma na siyo za IPTL kama yeye alivyonukuliwa.

Ukiufuatilia mjadala huu utagundua kuwa hata watuhumiwa wa uchotaji wa fedha hizo si watu mambumbumbu bali ni wasomi, tena wa ngazi za juu wanaoitafuna nchi hii kama wanavyotaka.
Kati ya wanaotajwa wapo wasomi kama Profesa Anne Tibaijuka, mwanasheria Andrew Chenge na wengine wengi.

Nihitimishe kwa kuwahakikishia kuwa wasomi wengi nchi hii si wazalendo, waadilifu, waaminifu, wawajibikaji. Ni wala rushwa, wameoza na wamepumbazwa. Wanajali zaidi matumbo yao. Hawatufai na kwa sasa ni aibu kusimama mbele za watu na kujiita msomi.

Niamini mimi, wapo watu wasio na uprofesa wala udaktari lakini ni wazalendo wa taifa hili. Hao ndiyo tuwape nafasi ya kusimamia kwa dhati rasilimali zetu.

Mtekaji na Muuaji wa Watoto Ifakara Akamatwa na Polisi, Wananchi Wachoma Nyumba Yake

$
0
0
Polisi hapa mjini Ifakara wamepata wakati mgumu kumwokoa bwana mmoja aliyefahamika kwa jina la Nurdin Mangula, baada RAIA wenye hasira Kali kutaka kumuua wakimtuhumu kuiba watoto na kuwaua kisha kuchukua baadhi ya viungo na kuviuza kwa baadhi ya wafanyabiashara.

Jamaa huyo ambaye mke wake ni hakimu wa mahakama ya mwanzo aliokolewa na polisi waliotumia nguvu kubwa kumnusuru asiuawe na RAIA wenye hasira Kali.

Tukio hilo lililotokea jana saa 10 jioni, lilivuta watu wengi na kuifanya polisi kutumia mabomu ya machozi na risasi za moto kuwatawanya watu hao. 

Wiki mbili zilizopita kuna watoto wawili walipotea katika mazingira ya kutatanisha na mmoja kupatikana akiwa tayari ameshakufa na baadhi ya viungo akielwa hana. 

Mtuhumiwa huyo ambaye ana undugu na makamu mwenyekiti wa CCM Philip Mangula amekutwa na watoto watatu kwenye gari aina ya Noah na mmoja akiwa tayari amekufa.

Pamoj na kuokolewa na polisi watu wamefanikiwa kuichoma moto nyumba yake na magari mawili. kuchukua kila kitu ndani ya nyumba.

Mfanyakazi wa Ndani Aliye Mtesa Mtoto Afunguka' Kumbe Nae Alikuwa Akiteswa na Maboss Wake'

$
0
0
The nanny who beat an 18 months old to near death has explained why she did it. Jolly Tumuhiirwe who is presently awaiting trial in Luzira prison,told Ugandaonline.net

“My dad in Kabale was very sick and my mom did not have any money. I asked my bosses for some money to send to my dad but they told me that I hadn’t made a month yet and my father was dying, so it kept on haunting me. That is the
more reason I referred the anger to the baby but I’m sorry.

But that madam (Arnella’s mom) is not easy. She used to say that I steal money from the clothes and Eric’s wallet, I eat the babies food…and yet I can’t eat the food, I’m not a baby, those were all lies, so, I was also not happy from my heart.I feel guilty..ok when I was doing it I thought I was disciplining the baby because also the mother sometimes slaps her, I also saw from the mom. The torch I used was small and it’s not hard. I think, I will never do it again”
Viewing all 104803 articles
Browse latest View live




Latest Images