Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104808 articles
Browse latest View live

Leo Ndo Mwisho wa Gwajima Kusali Kawe.....NHC Wanadai Lile ni Eneo Lao, Kanisa La Gwajima Lipo Pale Kimakosa

$
0
0
Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) limemtaka Mkuu wa Kanisa la Ufufuo na Uzima, Askofu Josephat Gwajima, kuhamisha makazi ya kanisa lake lililopo katika  viwanja vya Tanganyika Packers, Kawe, jijini Dar es Salaam leo.

Meneja Uhusiano wa NHC, Yahya Charahani amelieleza Gazeti  la Nipashe kuwa, walimpatia notisi Askofu Gwajima ya kuhama eneo hilo mwezi mmoja uliopita, lakini hakutekeleza badala yake ameendelea kulitumia eneo hilo kuendesha shughuli za kanisa lake, zikiwamo ibada.

Charahani alisema eneo hilo ni mali ya NHC na ni maalum kwa ajili ya ujenzi wa mji wa kisasa na wakazi waliokuwa wanaishi eneo hilo walishalipwa fidia muda mrefu uliopita ili kuondoka.

Lile eneo ni la NHC kwa muda mrefu na kabla ya hapo kulikuwa na nyumba nyingi sana na zilibomolewa, hizo zilizobaki zimebaki tu kimakosa,” alisema Charahani.

Aliongeza kuwa, hiyo siyo mara ya kwanza  kwa NHC kumpatia notisi Askofu kiongozi huyo kulihamisha kanisa lake.

Kwa mujibu wa Charahani,  NHC walimpatia notisi Askofu Gwajima ya mwezi mmoja kuondoka katika makazi hayo na kwamba notisi hiyo ilimalizika Machi 9, mwaka huu.

Alisema baada ya kumalizika kwa notisi hiyo, NHC lilimpatia muda zaidi Askofu huyo ambao unamalizika leo.

Juhusi za kumpata Askofu Gwajima kuthibitisha kama amepokea notisi hiyo zilishindikana kutoka na simu yake ya mkononi kutopatikana kila alipopigiwa tangu Alhamisi iliyopita.

Hata hivyo, jana alipotafutwa Mwanasheria wa Askofu Gwajima, Paul Mallya kuelezea hatua ya NHC ya kumpa mteja wake notisi ya kuhamisha makao ya kanisa lake, alisema bado hajapata notisi hiyo.

Sijapata taarifa hiyo, ndiyo kwanza nasikia kwako, ngoja nifuatilie nije nikupe majibu yaliyokamilika,” alisema Mallya.

Zitto Kabwe na Chama Chake cha ACT Wajigamba Kunyakua Majimbo Manne ya Ubunge Uchanguzi 2015

$
0
0
Chama cha Alliance for Change and Transparency (ACT), kimesema kinatarajia kunyakuwa majimbo manne ya ubunge katika Uchaguzi Mkuu utakaofanyika Oktoba, mwaka huu.

Kimetaja majimbo hayo kuwa ni Ubungo, ambalo linaongozwa na John Mnyika (Chadema), Kawe linaloshikiliwa na Halima Mdee (Chadema), Segerea ambalo Mbunge wake ni Makongoro Mahanga (CCM) na Kahama la James Lembeli (CCM).

Kiongozi  Mkuu wa Chama hicho, Zitto Kabwe, alisema hayo katika kipindi cha Hot Mix kinachorushwa na kituo cha EATV.

Zitto aliendeleza msimamo wake wa kutogombea ubunge kwenye jimbo lake la awali la Kigoma Kaskazini.

Nina maombi jimbo la Kahama, Kawe, Ubungo na Segerea lakini kwa kuwa ACT kinaongozwa kizalendo, tutaweka utaratibu mzuri wa kuweka wagombea kila eneo, binafsi kwa sasa siwezi kusema wapi nitagombea,” alisema.

Alipoulizwa ni eneo gani kati ya hayo aliyoyataja huduma yake inahitajika, alijibu kwa kifupi kuwa, nchi nzima ina muhitaji.

Kabla ya kampeni kuanza wagombea wakirudisha fomu ndipo mtajua Zitto anagombea jimbo gani, lakini lazima niongozwe na chama nikagombee wapi , wanaweza kusema Zitto kagombee jimbo A,” alisema.

Aliongeza kuwa, ACT kinahitaji kujipanga kuingia kwenye mapambano ya kufyeka msitu wa siasa kwa kuwa ndani yake kuna vyama zaidi 22 na vingine vikiwa na uzoefu mkubwa kutokana na kudumu zaidi ya miaka 23.

Alisema kazi kubwa walionayo ni kukijenga chama ili kiweze kulirudisha taifa kwenye misingi ya waasisi waliyoiacha.

Aliongeza kuwa, baadhi ya watu wanamuona kama anaanza upya kwa sababu wapo wachache waliwahi kujaribu na kuishia njiani.

Alipoulizwa kuhusu wachambuzi wa siasa wanavyomchukulia hivi sasa, Zitto alisema wapo wenye mtazamo hasi na wengine chanya.

Alisema kwa wale wanaomchukulia kwa mtazamo  hasi anaendelea kuwafundisha na kuwaonyesha kwamba muono wao ni tofauti wakati wale wa chanya anaendelea kuwasikiliza ili kupata muongozo zaidi kutoka kwao.

Tukumbuke hii nchi watu wamezoea kuchukia mabadiliko angalia kwenye sanaa wakimuona Diamond amefanikiwa waanza kutoa maneno ambayo siyo, watu wanachukia mabadiliko,” alisema.

Udaku Specially Blog


Wagombea urais CCM wafungukakia Kauli ya Rais Kikwete Aliyosema Urais ni Kazi Ngumu na ya Kadhia

$
0
0
Siku chache baada ya Rais Jakaya Kikwete kusema kuwa nafasi hiyo ni kadhia na kazi ngumu, baadhi ya wanasiasa waliotangaza nia ya kuwania nafasi hiyo wamesema wanafahamu changamoto hizo na kwamba kauli hiyo inazidi kuwapa nguvu na hamasa ya kuendelea na mchakato huo.

Wiki iliyopita, Rais Kikwete akiwa Marekani, wakati akihutubia kwenye taasisi ya Wood Wilson International Center for Scholars alielezea mafanikio na changamoto alizokumbana nazo wakati wa uongozi wake wa miaka 10 unaomalizika Oktoba, mwaka huu na kusema:

“Wakati unaingia Ikulu unakuwa na shauku kubwa sana pamoja na furaha ya ushindi, lakini hakika urais ni kadhia kubwa. Ukipata fursa ya kuwa rais kwa awamu mbili kama mimi nadhani zinatosha kabisa. Nimefanya mengi kwa nchi yangu atakayekuja ataendeleza nilipoishia.”

Kauli hiyo ya Rais Kikwete imekuja wakati makada wa CCM wakipigana vikumbo kuwania urais.

January Makamba:
"Nilitangaza nia hiyo huku nikiwa nafahamu kwa asilimia 100 uzito wa jambo hilo... kufahamu changamoto hizo ndiyo moja ya vitu vilivyonisukuma kuchukua uamuzi huo,” alisema.

Sumaye:
“Kama mtu ameamua kuwania nafasi hiyo ina maana anafahamu anachokitaka. Tunajua ziko changamoto na namna ya kukabiliana nazo kwa hiyo hakuna sababu ya kuwa na wasiwasi.”

Dk Kigwangalla alisema:
“Kauli kama hiyo haiwezi kumvunja mtu moyo, ari itabaki palepale tu kwa aliyetangaza nia. Aliyetangaza nia anataka kutoa utumishi wake kwa nchi yake kama mimi.”

Udaku Specially Blog
Maoni yako

Watu Sita Wakamatwa Na Jeshi La Polisi Kwa Tuhuma Za Kumbaka Mwanamke Mmoja Kwa Zamu

$
0
0
Watu sita wamekamatwa na Polisi kwa tuhuma za kumbaka mwanamke mmoja mwenye umri wa miaka 40.

Kamanda wa Polisi mkoa wa Kusini Unguja Juma Saad Khamis, alisema hilo ni moja ya matukio mabaya kuripotiwa kufanywa katika kipindi cha maadhimisho ya sikukuu ya Pasaka.

Watu hao walikamatwa Jumapili saa 2 usiku wakihusishwa kuhusika na tukio hilo,” alisema.

Uchunguzi wa awali unaonesha kuwa siku ya tukio watuhumiwa walionekana wakinywa na mwanamke huyo na baadaye walianza kumpiga na kumchukua hadi maeneo ya Bwejuu.

Hata hivyo Kamanda Khamis alikataa kutoa maelezo ya kina kuhusiana na watuhumiwa hao kwa maelezo kuwa yanaweza kuvuruga upelelezi wa tukio hilo ambao unaendelea kufanywa na mamlaka husika.

Alisema ukiacha tukio hilo baya, wananchi walisherehekea kwa amani sikukuu ya Pasaka.

Kulikuwa na amani, nawashukuru polisi wa doria kwa kazi yao nzuri na kusababisha wananchi kusherehekea sikukuu kwa amani,” alisema Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Mjini Mkadam Khamis Mkadam.

Kamishna Msaidizi (ACP) Mkadam alisema kulikuwa na matukio madogo ya ajali za barabarani, naye Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Kaskazini Unguja Mohamed Msangi alisema katika mkoa wake hakukuwa na matukio mabaya

Gwajima: Siwezi kuwasahau Dr. Slaa na Edward Lowassa

$
0
0
Dar es Salaam.-Askofu wa Kanisa la Ufufuo na Uzima, Josephat Gwajima jana alihubiri akiwa katika kiti cha magurudumu na kusema hawezi kuwatupa Mbunge wa Monduli (CCM), Edward Lowassa na Katibu Mkuu wa Chadema, Dk Willibrod Slaa kwa kuwa ni marafiki zake wa siku nyingi.

Pia askofu huyo, amewataka waumini wote wa kanisa hilo kufika katika Kituo Kikuu cha Polisi, Alhamisi ijayo siku ambayo atakwenda kukamilisha mahojiano dhidi ya tuhuma za kumtukana Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu la Dar es Salaam, Polycarp Kardinali Pengo.

Akihubiri mamia ya waumini waliofika kanisani hapo kwa ajili ya ibada ya Pasaka jana, Gwajima alisema kumekuwa uvumi kwamba kuhojiwa kwake na polisi kulitokana na kuwakaribisha wanasiasa hao kanisani kwake kwa nyakati tofauti na kuzungumza na waumini wake.

Alisema alifahamiana na Lowassa tangu mwaka 1996 wakati huo mbunge huyo akiwa Waziri wa Ardhi na tangu kipindi hicho amekuwa mtu wake wa karibu.

Alisema alifahamiana na Dk Slaa tangu mwaka 1994 kabla hajagombea nafasi ya urais kupitia Chadema na kwamba tangu wakati huo amekuwa rafiki wa familia.

“Hawawezi kunichagulia marafiki, hawa ni watu wangu wa karibu hata kabla hawajawa na ndoto za kugombea urais, nitaendelea kuwa nao karibu,” alisema.

Asimulia mahojiano
Akizungumzia mahojiano yake na polisi, Gwajima aliwaeleza waumini wake kwamba mambo mengi aliyohojiwa hayakuhusiana na suala la kumkashifu Kardinali Pengo.

“Polisi walinihoji mambo mengi binafsi yanayonihusu mimi na hayakuhusiana kabisa na Pengo, maswali ya Pengo yalikuwa machache sana,” alisema.

Hata hivyo, Gwajima alisema hana ugomvi na polisi wala Serikali kwa kuwa amekuwa akitoa ushirikiano kwa vyombo hivyo. Akitoa mfano, alisema Februari mwaka huu alipeleka barua polisi kueleza anataka kudhamini kampeni kwa ajili ya kupinga mauaji ya albino kwa kushirikiana na jeshi hilo.

“Niliwaeleza kwamba tungezunguka na polisi mikoa yote Tanzania na wamenijibu kwamba nipeleke ratiba ya shughuli hiyo ili tuanze,” alisema.

Alisema pia alidhamini mafunzo ya ulinzi shirikishi kwa vijana 400 kwa kushirikiana na polisi... “Shughuli hizi zinaonyesha kwamba sina ugomvi na polisi, bali nimekuwa rafiki kwa kushiriki katika shughuli zenye masilahi kwa Taifa.”

Viongozi wamiminika
Alisema pia hana ugomvi na Serikali na kwamba viongozi wake wamekuwa wakimiminika katika kanisa lake.

Aliwataja viongozi hao kuwa ni Waziri Mkuu mstaafu, Frederick Sumaye, Waziri wa Uchukuzi, Samuel Sitta, Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Lukuvi na Waziri wa Jumuiya ya Afrika Mashariki, Dk Harrison Mwakyembe.

Viongozi wengine, alisema ni Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Nape Nauye, Mbunge wa Kawe (Chadema), Halima Mdee na wabunge wa Viti Maalumu, Dk Mary Mwanjelwa na Vicky Kamata wote wa CCM “Kama ningekuwa na ugomvi na Serikali viongozi hawa wasingekuja katika kanisa langu kwa nyakati tofauti. Hii inaonyesha nilivyo na uhusiano mzuri na Serikali,” alisema.

Alhamisi ijayo
Askofu Gwajima amewataka waumini wake kumsindikiza katika Kituo cha Polisi siku ambayo atahojiwa kwa mara nyingine. “Nitakwenda Central Police Alhamisi saa moja asubuhi, nawaomba waumini wote mfike katika eneo hilo lakini msilete fujo wala kumtukana mtu, kuweni watulivu wakati wote nitakapokuwa nahojiwa,” alisema.

Askofu huyo alitakiwa kuhojiwa Alhamisi iliyopita lakini polisi waliahirisha kutokana na hali yake kutokuwa ya kuridhisha.

Hata hivyo, Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Suleiman Kova alisema Jeshi la Polisi halitaruhusu mkusanyiko wa watu katika eneo hilo wakati Askofu Gwajima atakapohojiwa.

“Atatakiwa kufika na wakili wake na mtu mmoja ambaye ataona anafaa kuingia naye kwenye mahojiano. Kama kuna waumini wanajiandaa kukusanyika katika ofisi zetu hapa Central Polisi, wafahamu kwamba haturuhusu na wakikaidi tutachukua hatua.”

Ilivyokuwa kanisani
Gwajima alifika katika kanisa hilo lililopo kwenye viwanja vya Tanganyika Packers Kawe saa 5.00 asubuhi na kupokewa kwa shangwe na waumini walioanza kufika tangu saa 2.00 asubuhi.

Msafara wa magari matatu; Toyota Land Cruiser mbili na Hammer, yaliwasili kwenye viwanja vya kanisa hilo na kulakiwa na waumini walioyazingira kwa shangwe na vigelegele wakitaka kumwona Askofu Gwajima.

Waumini hao walikuwa na shauku ya kumwona Gwajima na walionekana wakisukumana ovyo kila mmoja akitaka kumwona.

Akiwa amevaa suti ya rangi ya kijivu na shati jekundu, Gwajima aliteremka katika Hammer akishikiliwa na wasaidizi wake na kukalishwa katika kiti cha magurudumu mawili kilichokuwa kikisukumwa na wasaidizi hao kuelekea kwenye jukwaa la kanisa hilo.

Baada ya kufika, vikundi vya kwaya viliendelea kuimba na kucheza nyimbo mbalimbali za kumtukuza Mungu.

Gwajima alizungumza na waumini wake kuanzia saa 5.30 hadi saa 6.45, akiwaeleza kilichotokea kuanzia siku alipofika polisi kwa mara kwanza, mahojiano hadi alipotoka hospitali.

Katika mahubiri yake, Gwajima alisema ataendelea kuwaonya viongozi wa Serikali na wa dini watakaokosea masuala mbalimbali. “Sitajali ni kiongozi wa aina gani amekosea nitawakemea. Rais akikosea nitamkemea. Waziri akikosea nitamkemea na viongozi wa dini wakikosea nitaendelea kuwakemea,” alisema.

Chanzo: Mwananchi

Comments

Dr Slaa Atoa Madai Mapya Ya Kuongezwa Mshahara - CHADEMA

$
0
0
Katibu mkuu wa CHADEMA, Dr Slaa, ametoa madai mapya ya kuongezewa mshahara na stahiki zake kufuatia mafanikio aliyoyapata ya kuongezewa mshahara katika madai yake yaliyopita ambayo yalikuwa ni ongezeko la asilimia 40 tu ya kile kiwango alichokitaka!

Mchanganuo sahihi wa mshahara wa katibu mkuu wa CHADEMA na stahiki zake:

Mshahara anaolipwa Dr Slaa kwa sasa ni Tshs. 9,300,000 kwa mwezi wakati kabla ya madai yake ya mara ya mwisho alikuwa akilipwa Tshs. 6,600,000. Ambalo ni ongezeko la 40%.

Stahiki za Dr Slaa kama Katibu Mkuu:

Dr Slaa anawekewa kiasi cha lita 1000 za mafuta ya Petrol kila mwezi ambayo kwa wastani ni Tshs milioni 2,000,000 katika gari lake alilokabidhiwa na chama ambalo pia ulitumia kwa shughuli zake binafsi na za chama. Ifahamike, hii ni nje ya mshahara!

Haijaishia hapo, Dr Slaa pia anapewa pesa kiasi cha Tshs 2,500,000 kama fedha ya matumizi ya ofisi ya katibu mkuu wa chama kila mwezi. Hii pia ipo nje ya mshahara wake na matumizi yake hayaeleweki.

Kama hiyo haitoshi, Dr Slaa kila afanyapo vikao vya chama vya ngazi mbalimbali uinuka na wastani wa Tshs. 1,500,000 kwa kikao kimoja.

Madai Mapya:

Mshahara: Dr Slaa kwa sasa ameitaarifu CHADEMA kuwa wakati wa kukamilisha asilimia 60 zilizobaki za madai yake ya awali ya mshahara wake umewadia. "Hii ni kutokana na ongezeko la gharama za maisha na pia kuongezwa mkataba wa kutumikia chama kwa nafasi ya ukatibu mkuu" alieleza Dr Slaa.

Hivyo basi, kama CHADEMA itaridhia madai hayo mapya na kumuongeza Dr Slaa kiasi cha asilimia 60 kilichobaki, Dr Slaa ndiye atakuwa katibu mkuu wa chama cha siasa anayelipwa pesa nyingi kuliko wote katika nchi za ukanda wa Afrika mashariki! Kiasi hicho kitafikia Tshs. 13,200,000 kwa mwezi huku kikienda sambamba na kuongezeka kwa posho na stahiki zingine.
By PATIENT ZERO-JF

Udaku Specially Blog

Tetesi:Mgogoro ACT-Wazalendo: Mwenyekiti Taifa Atishia Kuachia Ngazi

$
0
0
By G Sam -JF
Mgogoro wa kimajukumu umeanza kuibuka ndani ya chama kipya cha ACT-Wazalendo ambapo mwenyekiti wa taifa wa chama hicho bi Anastazia Mghwira jana alitishia kuachia ngazi.

Habari zilizopatikana kutoka ndani ya chama hicho zinadai kuwa kiongozi mkuu wa chama Kabwe @ Zitto alimuonya mwenyekiti huyo kuwa anaingilia majukumu ya kukieneza chama ambayo kimsingi si yake.

Kwa mujibu wa katiba ya ACT-Wazalendo, kazi ya kukieneza chama ni ya kiongozi mkuu ambapo mwenyekiti kazi yake ni kuongoza vikao vya chama na kusimamia maadili ya wanachama.

Kufuatia mgogoro huo mwenyekiti huyo alitishia kujiondoa ndani ya uongozi wa chama hicho kutokana na mkanganyiko wa kimajukumu kati ya mwenyekiti na kiongozi mkuu.


My take!
Muda si mrefu Zitto atajihalalishia uenyekiti wake ndani ya ACT ambao umo chini ya kivuli cha Anastazia Mghwira na kuitimiza rasmi azma yake ya muda mrefu!

Udaku Specially Blog

Mwigizaji Shamsa Ford, Ney wa Mitego Ndani ya "PENZI ZITO"

$
0
0
Baada ya ivi karibuni staa aliyefanya vizuri kwenye movie ya CHAUSIKU, shamsa ford kutangaza rasmi kuachana na aliyekuwa mume wake, kwa kigezo kuwa mwanaume huyo alikuwa akimtesa na kumpiga kwa muda mrefu, uku akimshutumu mwanaume huyo kutoijali familia yake zaidi ya marafiki na starehe, kitu ambacho kimemfanya staa huyo ajiweke pembeni kuepusha msongamano.

Siku chache baada ya staa huyo kutangaza rasmi kuachana na zilipendwa wake huyo anayefahamika kwa jina moja la dickson, ivi sasa staa huyo yupo kwenye mahaba mazito na mwana hip hop maarufu nchini, ney wa mitego, ambapo kwa nyakati tofauti wameonekana wakiwa wote zero distance , uku wakijiachia na mapicha kama ilivyo kawaida ya mastaa watafuta kick.

Kitendo hicho kimewashtua kama sio kuwapandisha presha wapenda ubuyu wa mujini.

Udaku Specially Blog

Dr Kessy Anakuletea Dawa za Kutengeneza Hips, Makalio, Nywele na Nguvu za Kiume Kwa Kutumia Dawa za Asili zisizo na Kemikali

$
0
0


Kifaa cha Kurefusha uume Kinachouzwa 160,000
Pendeza na Dr Kessy Products 
Ni dawa za Asili zisizo na Kemikali wala madhara yoyote kwa Binadamu, zimetengenezwa kwa kutumia mimea na matunda mbali mbali kukupa matokeo ya Haraka

1.Refusha Nywele na zisikatike  45,000/
2.Ondoa Mvi Sugu kichwani  45,000/
3.Toa Michirizi Mapajani, Chunusi na Madoa mwilini 40,000/
4.Punguza tumbo na Manyama uzembe 45,000/
5.Mkanda wa Kufunga Kupunguza tumbo 70,000/
6.Tengeneza Shepu Hips na Makalio  45,000/ ,Vidonge 80,000/
7.Ongeza Nguvu za Kiume  Jelly 45,000/ , Vidonge 60,000/
8.Ongeza Ukubwa wa Maumbile ya kiume Jelly 80,000/ , Mashine 160,000/
9.Kuongeza Mwili Mzima 40,000/
10.Kupunguza Mwili 45,000/
11.Kupunguza Maziwa na Kuyasimamisha 40,000/
12.Ongeza Mguu uwe wa Kupendeza 45,000/
13.Rudisha usichana ama Bikira 55,000/
14.Ongeza Hamu ya Kula 40,000/
15.Ongeza Hamu ya Kufanya Mapenzi 55,000/
16. Fanya mwili Kuwa Soft 60,000/
17. Dawa ya kutoa Michububuko kwenye mapaja 45,000/
18. Dawa ya kutoa maji maji sehemu ya siri na kukuacha mkavu 55,000/

TUNAPATIKANA DAR NA MIKOA YOTE, HUDUMA ZINAFIKA POPOTE ULIPO , 
DAR TUPO KARIAKOO MSIMBAZI NA POSTA  MPYA

PIGA SIMU: 0719955528, 0756259180 au 0785371237

Tanesco Kuja na Mfumo Mpya wa Kulipia LUKU Mwezi Ujao..Sasa Kupata LUKU itakuwa Ndani ya Sekunde Tatu

$
0
0
Shirika la Umeme nchini (TANESCO) linatarajia kubadilisha mfumo wa huduma ya Lipia Umeme Kadri Utumiavyo (Luku) na kuuweka wa kisasa ili kuwaondolea usumbufu wateja wake.

Imeelezwa kuwa mfumo unaotumika sasa ni tatizo kutokana na mabadiliko hayo, mfumo mpya huenda ukaanza kutumika mwezi ujao. Hayo yalisemwa jana na Meneja Uhusiano wa Tanesco, Adrian Severin.

Alisema mfumo utakaowekwa, utakuwa wa kisasa na kwamba utawasaidia watumiaji kupata haraka huduma ya Luku. Alisema mfumo huo ni wa kompyuta, wa kisasa na wa haraka, utakaotibu kero wanayoipata watumiaji wa huduma ya Luku.

‘’Mfumo huo utakuwa una uwezo wa kuhudumia wateja wengi zaidi na kwa haraka ndani ya sekunde tatu, ikilinganishwa na mfumo wa zamani ambao ulikuwa unatumia zaidi ya dakika moja au sekunde 30,’’ alisema Severin.

Aliongeza maandalizi ya mfumo huo, yamekamilika na kwamba watakaokuwa wanatumia simu za mikononi na mawakala wanaouza Luku, wataendelea kutoa huduma hiyo.

‘’Mawakala wa MaxMalipo na simu zote za mikononi kama Tigo, Airtel, Zantel na Vodacom wataendelea kutoa huduma hiyo, lakini itakuwa kwa haraka na kwamba hakutakuwa na shida ya mitandao,’’ alisema.

Akizungumzia suala la kutopatikana kwa huduma ya Luku tangu juzi jioni, Severin alisema huduma hiyo haikupatikana, kutokana na tatizo la mtandao.

‘’Wakati mwingine simu za mikononi zinakuwa hazina tatizo la mitandao, lakini unakuta Tanesco mitandao yao ipo chini, vivyo hivyo na kwamba Tanesco inakuwa ipo sawa kwa mtandao, lakini simu zinasumbua,’’ alisema Severin.

Alisisitiza kuwa ili kupatikana haraka kwa huduma ya Luku, inatakiwa Tanesco na simu zote zinazotoa huduma hiyo kuwa na mitandao iliyo sawa. Hata hivyo, alisema huduma hiyo inapatikana kwa sasa.

Kwa muda mrefu, watumiaji wa huduma ya Luku, wamekuwa wakilalamikia uduni wa huduma, kiasi cha kuwafanya wateja wake kushindwa kuwa na umeme kwa siku kadhaa, kutokana na tatizo la kimfumo katika mitambo ya huduma za Luku.

Toa Maoni yako Hapa Chini (Matusi Hapana)

Lulu: Nilishalia Sana, Nishaumia Sana Lakini Kwasasa.....

$
0
0
Staa mrembo kutoka Bongo Movies Elizabeth Michael ‘Lulu’ ameamua kutoboa kile alichokiita kama faraja yake kwa hivi sasa.

Faraja YANGU...Nishalia sana,nishaumia sana lakini kwa sasa nikiona mmoja kati ya hawa analia au kuumia ndo kitu kinachoweza kuniumiza zaidi...!MUNGU awatunzeeee”-Lulu aliandika hayo jana usiku kwenye ukursa wake mtandaoni mara baada ya kuweka picha ya mama yake na mdogo wake.

Kufuatia andiko hilo komenti za mashabiki wengi zilielekea zaidi kumzungumzia kifo cha Steven Kanumba kwani leo tarehe 7  mwezi huu ni siku ya kumbukumbu cha kifo cha staa huyo wa Bongo Movies ambae alikuwa na mahusiano ya kimapenzi na Lulu.

Japo kuna baadhi ya watu amabo sio wastaarabu wamekua wakimshabuliaLulu kwa maneno makali, lakini kwa maneneo hayo ya Lulu nadhani wenye busara wamekuelewa.

Toa Maoni yako Hapa Chini

Zari Aendelea Kuionyesha Dunia Kuwa Ana ujauzito wa Mwanamuziki Diamond Platnumz

$
0
0
"When you keep that ambition high amazing things will happen for you. Trust me. If you woke up with no vision or ambition go back to sleep. Seriously!!"-ZARI  captioned this photo


Makadirio ya Mapato ya Askofu Ngwajima kutoka Kwenye Sadaka za Waumini

$
0
0
Kama ni kweli Ngwajima ana waumini wasiopungua elfu sabini na wanaenda kanisani mara mbili kwa wiki basi Ngwajima anaingiza zaidi ya bilioni tatu kwa mwaka (makadirio ya chini kabisa)

NI HIVI:
Tufanye kila muumini wake hutoa sadaka ya sh. 500 tu-hiyo ni flat rate, ina include waliotoa elfu kumi, waliotoa sh mia na wasio toa kabisa.

Hivyo basi kwa siku moja kwa waumini 70,000 wakitoa sh 500 ni sawa na sh milioni 35. Kwa wiki wanaenda mara mbili hivyo ni sawa na sh milioni 70.

Kama kwa wiki anaingiza milioni 70, je kwa mwezi anaingiza kiasi gani? Uki cross multiplication utapata milioni 280 

Kama kwa mwezi anaingiza milioni 280, je kwa mwaka anaingiza kiasi gani? uki cross tena multiplication utapata bilioni 3 na milioni 360. Sasa piga hesabu kwa miaka yote aliyotoa huduma ameingiza sh ngapi?

Kwa mantiki hiyo pesa aliyonunulia Hummer aliipata ndani ya mwezi mmoja tu.

Achilia mbali fungu la kumi na pesa mbali mbali anazopewa kama zawadi, hapo tumepiga hesabu ya sadaka tu.

NAMALIZIA, Biblia inasema "vya madhabahuni vitaliwa na wamadhabahuni" full stop.

Udaku Specially Blog


Waislamu Watoa Tamko, Kusomwa kila Msikiti Ijumaa kuhusu Tamko la Maaskofu, Kunyimwa Dhamana Kwa Mashehe na Issue ya Madrassa

$
0
0
SIKU chache kupita baada ya Mkutano wa 19 wa Bunge kumalizika,na serikali kuutupia mbali mswaada wa sheria ambao unaruhusu kuwepo makakama ya Kadhi nchini kutajadiliwa kwenye mkutano huo.

Nayo Jumuiya na Taasisi za Kiislam nchini wameibuka na kutoa tamko zito kwa kuwataka waislam wote nchini kutoshiriki kwenye kura ya maoni ya kupitisha katiba pendekezwa Bunge Maalum la Katiba,kwa madai kwamba serikali haina nia nzuri na waislam nchini kwa kitendo chake cha kukataa kuwepo mahakama ya Kadhi nchini.

Vilevile Taasisi hiyo imewataka pia waislam wote kujitokeza kujiandikisha kwenye Daftari la wapiga kura na kujiandaa kufanya uamuzi mgumu ambao wanasema hajawai fanywa na waislam nchini tangu taifa kupata Uhuru.

Akisoma Tamko hilo lenye kura sita jana jioni kwenye msikiti wa Kichangani uliopo Magomeni Jijini Dar es Salaam ,Naibu Katibu Mkuu wa Jumuiya na Taasisi ya Kiislam nchini Sheikh Mussa Kundesha kwa niaba ya asasi za kiislam 11 zinazounda umoja huo na kushuhudiwa na Mamia ya waumini wa dini hiyo pamoja waandishi wa Habari ambapo Sheikh Kundesha alisema-

Waislam wote nchini wamechoka na uonevu wanaodai kufanyiwa na Serikali iliyoko madarakani kwa kitendo cha kuondo Mswaada wa Mahakama ya kadhi Bungeni ambapo alisema ni kuendelea kuchochea vita ya kidini nchini.

“Kuna kila sababu ya kuamini kuwa Serikali ya CCM imeshindwa kulishughulikia suala la mahakama ya Kadhi katika uhalisia wake kama ilivyoahidi kupitia ilani yake kwenye uchaguzi ibara ya 108 (b) mwaka 2005 na sasa inafanya hadaa za kisiasa kuwadanganya waislam ili waonekane inalishughulikia suala la mahakama ya Kadhi kama walivyoahidi”

“Kwa ubabe huu wanaotufanyia waislam sasa tunawaomba waumini wote wa kiislam nchini kutoipigia kura katiba pendekezwa kwasababu sio katiba nzuri kwa waislam harafu tunawataka kila mmoja aliyetimiza miaka 18 ajiandikishe kwenye Daftari wa wapiga kura kujiandaa kufanya uamuzi mgumu ambapo utalitikisa nchi”alisema Sheikh Kundesha.

Alisema kuwa kitendo cha Serikali kuwatambua Makadhi wa Bakwata pamoja wanachosema ni ‘Mahakama hewa ya Kadhi’ chini ya Bakwata ni kinyume na Katiba ya nchini ibara 19(1) na (20) kwa kuwalazimisha waislam wawe chini ya Bakwata ambapo wanasema hawatakubaliana nalo.

KUHUSU TAMKO LA MAASKOFU.
Pia katika Tamko la Taasisi hiyo kiislam ambapo litasomwa kila msikiti Ijumaa wiki hii nchi nzima pia wamezungumzia Matamko mawili yaliyotolewa Jukwaa la kikiristo nchini ambapo Taasisi hiyo ya Kiislam wameonyesha masikitiko yao kwa kusema ni dhahili hapa nchini kuna serikali dhaifu kwa kuwaacha maaskofu kutoa matamko ambayo wanadai ni ya kichochezi.

“Ushahidi kwamba ni chuki tu husda ni pale ambapo hata waislam tuliopendekeza mahakama ya Kadi iwekwe kwenye Katiba pendekezwa,lakini tunashangaa hawa maaskofu wamekuwa wakiipinga Mahakama hii wakati hii dini tofauti na y a kwao na sisi waislam tumewavumilia lakini tunahoji hawa maaskofu wanataka nini”

KUHUSU KESI ZA MASHEIKH NA KUNYIMWA DHAMANA.
Pia Taasisi ya Kiislam wameonyesha kuchukizwa kwa kitendo cha Masheikh mbalimbali akiwemo shehe Ponda ambao wapo mahabusu na kunyimwa Dhamana na Serikali ila wanashangaa kitendo cha Serikali kuwamwachia Askofu wa Kanisa la Ufufuo na Uzima Askofu Josephat Gwajima wanadai kitendo hicho kinaonesha Serikali kuwapendelea wakristo.

“Masheikh mbalimbali wako mahabusu wakinyimwa Dhamana bila sababu za msingi kwa kesi za uchochezi au kwa kisingizio cha Ugaidi wakati huo huo tumeshuhudia Maaskofu wakitoa kauli za uchochezi pasina kuchukuliwa hatua yeyote ikiwemo sakata la Askofu Gwajima”

KAMPENI WANAO DAI KUUA MADRASA.
Pia Taasisi hiyo wamezungumia kitendo cha Serikali kuwakamata wa Mashehe mbalimbali wanaowafundisha watoto majumbani kwa madai ya serikali kutofuata taratibu za mafunzo likiwemo matukioa tofauti yaliyotokea mkoani arusha-

Kwa kusema ni wazi serikali imejitosa kuua madrasa nchini.

“Lakini Takriban mwezi mmoja sasa,njama hizi za kuua madrasa zetu zimeibuka kwa kasi kubwa na nguvu kwa kuendesha kamatakamata ya waalimu wa madrasa zao katika hali duni majumbani mwao wakifundisha Quran na mafunzo mengine ya Uislam kama tulivyoshudia huko mkoan Moshi na Arusha”

“Tunataka Serikali itusaidie kufundisha Elimu ya dini ya Kiislam kwa mujibu wa sheria ndiyo ipi,sheria hiyo ilipitishwa lini na Bunge lipi?kwa mujibu wa Katiba ya nchi ibara 20 (1) kazi ya kutangaza dini ni suala binafsi,iweje sasa Serikali inakuja na madai haya ya kufundisha dini kinyume na Sheria kwa walimu wetu wa madrasa”

Chanzo: FullHabari Blog

Mrembo Mtanzania Afia China Baada ya Kuugua Kwa Muda Mrefu

$
0
0
Mrembo Mtanzania aliyejulikana kwa jina la Rehema Mohamed (30), anadaiwa kufia katika Mji wa Shanghai nchini China wiki mbili zilizopita baada ya kuugua kwa muda mrefu hadi mauti yalipomfika huku ndugu zake wakichanganyikiwa kutokana na taarifa za kifo hicho.

Habari zaidi kutoka kwa aliyekuwa rafiki wa karibu wa Rehema nchini China, (jina lake linahifadhiwa) zinasema kuwa wamekuwa wakihangaika ili kupata fedha za kusafirisha mwili huo lakini imekuwa ngumu kupatikana.

Chanzo hicho kilisema kuwa kimefanya mawasiliano na baadhi ya ndugu wa marehemu ambao nao wanajikusanya kwa ajili ya kupata fedha hizo ili kuurudisha mwili nyumbani Dar kwa mazishi.

“Yaani huku tunapata tabu sana na tuna uchungu kwa kuwa fedha zilikuwa zikihitajika nyingi sana lakini tunashukuru taratibu zinaenda sawa karibu tutaleta mwili nyumbani,” alisema rafiki huyo.

Mmoja wa ndugu wa marehemu ambaye hakupenda jina lake liandikwe gazetini, alisema kuwa kifo cha ndugu yao ni pigo kubwa ukizingatia amefia ughaibuni na fedha za kumleta zinahitajika nyingi hivyo wamekaa na kumuomba Mungu ili mwili ufike Bongo waupumzishe.

“Msiba wa mdogo wetu umetupa wakati mgumu sana jamani, ukizingatia amefia mbali sana na kumleta huku ni fedha nyingi mno, hivyo tunamuomba Mungu tu ili mwili ufike na tuupumzishe katika makaburi ya nyumbani,” alisema ndugu huyo.

Toa Maoni Yako Hapa Chini

Shahidi Aeleza Kisa cha Al Shabaab Kuuwa Wasichana Wengi Katika Shambulio la Kigaidi Chuo cha Garissa Kenya

$
0
0
A survivor of the deadly terror attack in Garissa University has told the media how the Al Shabaab tricked female students to draw them out in the open and kill them like insects.

Narrating his story, Francis Gicobi, a second year Bachelor of Education student, said many female students fell for Al Shabaab’s lies and that’s why they were killed in large numbers compared to male students.

Gicobi noted that when Al Shabaab stormed the women’s hostel, they tricked them to comply with their orders to come out because they would not be killed since Islam does not permit them to kill women.

Many females students fell for this lie and came out and the Al Shabaab sprayed them with bullets indiscriminately killing them like insects

The Al-Shabaab shouted 

Kama hamtaki kufa, tokeni hapa nje nyote kwani kulingana na dini yetu, hatuui wasichana na kwa hivyo mtoke taratibu kwa gorofa hadi hapa chini, au mpigie baba zenu simu waje wakuokoe. (If you don’t want to die, come outside. According to our religion, we do not kill girls. Walk down the stairs to the ground level, or alternatively call your fathers to come and save you),” narrated Gicobi.

Female students walked to the ground floor of the storied building in droves only for the attackers to indiscriminately spray them with bullets,” he added.

However, he thanked God for keeping him alive to tell Kenyans what he witnessed on that fateful day.

I thank God for saving me to be able to tell Kenyans what I witnessed as my innocent colleagues were riddled with bullets like animals,’’ he said.


Toa Maoni Yako Hapa chini

Askofu Gwajima Aligomea Shirika la Nyumba la Taifa (NHC), Mpaka Jana Kanisa Hilo Lilikuwa Bado Lipo katika viwanja vya Tanganyika Packers, Kawe jijini Dar es Salaam

$
0
0
Licha ya Shirika la Nyumba la Taifa (NHC), kumtaka Mkuu wa Kanisa la Ufufuo na Uzima, Askofu Josephat Gwajima, kuhamisha makazi ya kanisa lake lililopo katika viwanja vya Tanganyika Packers, Kawe jijini Dar es Salaam, bado hajatekeleza.

Wiki iliyopita, Meneja Uhusiano wa NHC, Yahya Charahani, akizungumza na Gazeti la Nipashe alisema kuwa walimpatia notisi Askofu Gwajima ya kuhama eneo hilo mwezi mmoja uliopita, muda ambao ulimalizika jana.

Jana mwandishi wetu alitembelea  katika viwanja lililopo kanisa hilo saa 5:00 asubuhi na kukuta shughuli za kiibada zikiendelea kama kawaida.

Katika viwanja hivyo, kulikuwapo na mahema madogo madogo yaliyokuwa na waumini wa Kanisa la Ufufuo na Uzima linaloongozwa na Askofu Gwajima wakifundishana Neno la Mungu.

Kadhalika, mbele ya uwanja huo, kulikuwapo na jukwaa kubwa lililopambwa kwa vitambaa na hakukuwa na dalili zozote za kuhamisha vifaa vikiwamo vya muziki na spika kubwa.

Hata mwandishi alipoingia katika viwanja hivyo, alipokelewa na baadhi ya watumishi wa kanisa hilo na kuulizwa kama amekuja katika maombi au anahitaji huduma ya kiroho.

“Majeshi Majeshi, karibu tukuhudumie mpendwa, umekuja kwenye maombi au unahitaji huduma yoyote kutoka katika kanisa letu?,” mmoja wa wahudumu ambaye hakufahamika jina lake alimhoji.

Hata hivyo, Askofu Gwajima mwenyewe hakuwapo na hata alipotafutwa kupitia simu yake ya mkononi, iliita bila majibu na  alipotumiwa ujumbe mfupi wa mkononi, pia hakujibu.

Kwa mujibu wa Charahani,  NHC walimpatia notisi Askofu Gwajima ya mwezi mmoja kuondoka katika viwanja hivyo na kwamba notisi hiyo ilimalizika tangu Machi 9, mwaka huu.

Alisema baada ya kumalizika kwa notisi hiyo, NHC lilimpatia muda zaidi Askofu huyo ambao ulimalizika jana.

Hata hivyo, jana alipotafuwa Mkuu wa Kitengo cha Huduma na Mawasiliano wa NHC, Suzan Omary, kuelezea hatua gani zitafuata endapo Askofu Gwajima hatahamisha huduma za kanisa lake baada ya notisi kuisha, alieleza kuwa atafutwe leo kwa kuwa hakuwa ofisini wakati huo.

“Sipo ofisini leo (jana), nitafute kesho (leo), nitakupa ufafanuzi zaidi, na hata nikikuelekeza kwa mtu mwingine hatakusaidia kwa kuwa leo hakuna mtu ofisini,” alieleza Omary.

Toa Maoni Yako Hapa Chini

Kakobe Amshukia Lowassa, Awataka Watanzania Kususia Kura Ya Maoni Kwa Madai Kuwa Katiba hiyo ni ya Kishetani na Mwandishi Wake Ni "Nyoka Wa Makengeza" ( Shetani)

$
0
0
Akihubiri siku ya Pasaka katika Kanisa la Full Gospel Bible Fellowship lililopo Mwenge katika Jiji la Dar-Es-Salaam, Askofu Mkuu Zachary Kakobe alisema kwamba, inajulikana wazi kwamba Lowassa amekuwa anautaka Urais kwa udi na uvumba kwa miaka mingi, hata mwaka 1995 alijitosa hadharani kuuwania, sasa anapodai kwamba hivi sasa kuna makundi yanayokwenda kwake kumshawishi agombee Urais, kana kwamba yeye hataki Urais, anakuwa anamdanganya nani?


Ingawa katika mahubiri hayo ya saa mbili, Kakobe hakumtaja Lowassa kwa jina, hata hivyo Kakobe alisema, "Wako watu wengine ambao inajulikana wazi kwamba wamekuwa wakiutaka Urais kwa udi na uvumba, kwa miaka mingi, lakini hivi sasa wanasema kuna makundi ya watu yanawafuata nyumbani, kuwashawishi kugombea Urais; kama vile hawautaki Urais, hivi watu hawa wanamdanganya nani?

"Na wale wanaokwenda kumshawishi mtu ambaye kwa miaka mingi, anajulikana kwamba anautaka Urais, hawajui kwamba nao wanafanywa kuwa wajinga? Mtu anayejulikana kwa muda mrefu kwamba anautaka Urais, ni vema akatangaza tu moja kwa moja nia yake, bila haja ya ghiliba."

Katika mahubiri yake yenye kichwa, "UPOTOSHAJI WA UKWELI", Kakobe alieleza jinsi Gavana wa Kirumi, au liwali Pontio Pilato, alivyojiunga na Viongozi wengine kupotosha ukweli wa kufufuka kwa Yesu, na kusema kwamba wanafunzi wake waliuiba mwili wake, wakati askari walinzi walipokuwa wamelala, na kuwadanganya watu, ingawa wao wenyewe waliujua ukweli.

"Pilato aliwadanganya watu hao kwa muda tu, lakini hatimaye ukweli ulikuwa dhahiri, walipomwona Yesu kati yao kwa muda wa siku 40. Unaweza kuwadanganya watu kwa muda tu, lakini hatimaye ukweli hudhihirika, na kumfedhehesha yule aliyeupotosha ukweli huo", alisema.

Aliendelea kusema kuwa, hata leo kuna upotoshaji wa kweli mbalimbali za kiroho na kimwili. Baada ya kuelezea juu ya baadhi ya kweli za kiroho zilizopotoshwa, aliwageukia wanasiasa waongo, akianza kwa kutoa mfano wa Waziri wa Habari wa Iraq, wakati wa vita ya mwaka 2003, Muhammad Saeed al-Sahhaf, aliyekuwa akipotosha ukweli kuhusu jinsi Iraq ilivyokuwa inapigwa vibaya katika vita hivyo, na akaendelea kusema;

"Kabla sijaendelea, nifafanue kwanza juu ya watu wanaopotosha ukweli, kwa kusema kwamba eti Wachungaji hawapaswi kuwakemea wanasiasa wananapopotoka. Watu hawa hawajui Biblia. Katika MAMBO YA WALAWI 4:22-23, Biblia inasema, Mtawala akifanya dhambi, inampasa Kuhani yaani Mchungaji, kumjulisha dhambi yake."

Kakobe aliendelea kusema kwamba huu ni mwaka wa Uchaguzi, hivyo Watanzania wawe makini na wanasiasa waongo wanaofanya uongo kuwa sehemu ya siasa zao.

"Siasa, ni Sayansi, inaitwa POLITICAL SCIENCE, na "any kind of science only deals with facts". Wanasiasa hawana budi kuwa wakweli kwa kuwa siasa ni sayansi.

"Siasa siyo mchezo mchafu, bali baadhi ya wanasiasa ndiyo wachafu. Msidanganywe tena na wanasiasa ambao watakuja kwenu mwaka huu na ahadi za uongo za kuibadili miji na kuifanya kuwa kama New York, kwa miaka mitano; na wengine hawana AIBU, wanaweza hata kuwaambia wakazi wa Dodoma kwamba watawaletea meli! Hamna budi kuyachunguza kwa makini maneno yao, na kuona kama ni ya kweli."

Kuhusu Katiba, Kakobe aliwaunga mkono Maaskofu waliowapa Wakristo maelekezo ya kuikataa Katiba Pendekezwa, katika Kura ya Maoni, na kusema kwamba hiyo ndiyo kazi ya Mchungaji.

"Mchungaji, pia ni Mwalimu, kazi yake ni kuchunga na pia kulisha kondoo (YOHANA 21:15-17), na Biblia inafafanua juu ya kazi ya Mwalimu katika ISAYA 30:20-21, ikieleza kwamba Mwalimu anatakiwa kuwaambia anaowaongoza, "Njia ni hii ifuateni, wageukapo kwenda kulia au kushoto".

Aliendelea kusema, "Kumekuwa na udanganyifu au upotoshaji wa ukweli kuhusu Katiba, tangu katika hatua za mwanzo kabisa za mchakato wa Katiba, ambapo Chama kimoja cha siasa, kiliwapachika makada wake katika vikundi mbalimbali, ili kiwe na wajumbe wengi.

"Kwa mfano Kingunge Ngombale Mwiru aliwawakilisha waganga wa kienyeji, lakini cha ajabu, ukienda kwake hata leo, hakuna kibao kwake kinachozitambulisha kazi zake za uganga wa kienyeji, kama ilivyo kwa waganga wengine! Siyo hilo tu, kote duniani, Katiba yoyote ya nchi, lazima itokane na muafaka wa Kitaifa, ili Katiba hiyo iwe na sifa ya kusomeka katika Utangulizi wake, "SISI WANANCHI".

"Hapa kwetu, watawala hawakutaka kabisa muafaka katika kutengeneza Katiba yetu, lakini wanadai eti, Katiba Pendekezwa, ni bora kuliko zote Afrika! Huu ni upotoshaji wa ukweli, wa hali ya juu sana."

Aliendelea kusema kwamba, Sheria ya Mabadiliko ya Katiba na Sheria ya Kura ya Maoni, hazikuzingatiwa kikamilifu katika mchakato huo uliojaa udanganyifu.

"Sheria ya Kura ya Maoni, Ibara ya 5(3), inasema kwamba kungetakiwa kuwepo na elimu kwa wapiga kura, kwa siku 60, mara tu baada ya Tangazo la Katiba Pendekezwa katika Gazeti la Serikali Na. 382 lililotolewa tarehe 10.10.2014, lakini elimu hiyo iliyopaswa kutolewa na Tume ya Uchaguzi, haijafanyika hadi hivi leo!

V"ilevile, Sheria ya Kura ya Maoni Ibara ya 4(3) na 4(4), inasema kwamba kungetakiwa kutangazwa katika Gazeti la Serikali, SWALI LA KURA YA MAONI, ambalo wananchi wangelijibu kwa jibu la NDIYO au HAPANA, na pia Sheria ya Kura ya Maoni Ibara ya 12(1) na 12(2) na Ibara ya 16(1) inasema kwamba, kungetakiwa kuwepo na Kamati mbili za Kura ya Maoni, Kamati moja ya NDIYO, na nyingine ya HAPANA, ambazo zingejumuisha wananchi wenye misimamo tofauti kutoka katika makundi mbalimbali katika jamii, na Kamati hizo zingepiga kampeni kwa siku 30.

"Yote haya hayakuzingatiwa, lakini kinyume chake, Watawala hadi hivi leo, hawataki hata kusikia watu wakisema HAPANA kwa Kura ya Maoni, na wakati huohuo, wengine bado wanataka Kura ya Maoni ifanyike Aprili 30, pamoja na kwamba imetangazwa na Tume ya Uchaguzi, kwamba imeahirishwa!

"Wachungaji wengine wenye njaa, wanathubutu kusema kwamba eti kwa sababu kwenye Katiba Pendekezwa kuna Uhuru wa kuabudu, basi sisi Wachungaji tukae kimya, mengine hayatuhusu, hawa wana njaa kali, na upeo mdogo wa uelewa wa mambo haya.

"Mimi sina njaa, na ninasema kwa msisitizo, Katiba ni zaidi ya Uhuru wa kuabudu. Ilikuwa rahisi kwa Pilato kuwadanganya watu wa nyakati hizo, lakini leo ni kazi sana kuwadanganya watu wanaopata maarifa na habari juu ya yote yanayofanyika kote duniani, kwa TV, Redio, Magazeti, Intaneti na Mitandao ya kijamii.

"Watu wanajua kwamba kote ulimwenguni, Katiba ya Wananchi hutokana na muafaka, na Kura ya Maoni, hufanyika baada ya Kampeni ya NDIYO na HAPANA, kama ilivyofanyika Kenya ambako waliosema NDIYO waliitwa kundi la NDIZI, na waliosema HAPANA waliitwa kundi la CHUNGWA.

"Waliowaambia Wakristo wapige kura ya HAPANA kwenye Kura ya Maoni, ninawapa asilimia 90, hata hivyo kwa unyenyekevu, mimi ninaomba kuhitilafiana nao, kwa kuongeza kwamba Kura ya Maoni inapaswa kususiwa kabisa, kwa sababu kushiriki katika Kura hiyo, ni kuuhalalisha udanganyifu wa Watawala hawa, na kujifedhehesha mwishoni.

"Tangu mwanzo, watu hawa walitumia ubabe na wizi wa kura wa dhahiri katika Bunge la Katiba, na kutangaza kura feki za NDIYO za mahujaji na wajumbe wengine ambao hawakuwepo ukumbini wakati wa kupiga kura, na pia kura za Wazanzibari feki, na hivyo kupitisha kwa lazima, Katiba Pendekezwa.

"Wamedhamiria kufanya hivyohivyo hata katika Kura ya Maoni, ili kuipitisha kwa lazima Katiba yao Pendekezwa; ukizingatia kwamba, ili kutimiza kusudi hilo, wameweka sheria mbaya kwa makusudi ya kuhalalisha udanganyifu.

"Kwa mfano Sheria ya Kura ya Maoni Ibara ya 34(2), inahalalisha wapiga kura walioandikishwa Tanzania Bara, kwenda kupiga kupiga Kura ya Maoni, huko Zanzibar. Katika mazingira haya, Kura za HAPANA zitasaidia nini? Ni kuhalalisha tu udanganyifu wao, na kujifedhehesha.

"Mwandishi Mkuu wa Katiba Pendekezwa, yeye mwenyewe amesema anapenda aitwe JOKA LA MAKENGEZA! Niliposikia juu ya Jina lake hili, nilipigwa na butwaa!

Katika Biblia, Joka ni Ibilisi au Shetani (UFUNUO 12:7-9; 20:1-2), maana yake ni kwamba Mwandishi Mkuu wa Katiba Pendekezwa, ni Joka yaani Shetani, na hivyo tunaweza kusema Katiba hiyo ni ya Kishetani, maana imetokana na Shetani ambaye ni Joka lililoko kuzimu!

"Kumbe basi, siyo tu kwamba Katiba Pendekezwa imeahirishwa, ila ni kwamba Mungu ameikataa tangu siku ya kwanza ya mchakato wake!

"Kwa sasa tuwaze tu kujiandikisha kwa wingi katika Uandikishaji wa Wapiga Kura, kwa BVR, na kuwa tayari tu kwa Uchaguzi Mkuu, na kuisahau kabisa Kura ya Maoni."

(SOURCE:  Tanzania Daima 7/4/2015; na CD ya Neno la Pasaka la Kakobe.)

Ushahidi wa Laivu Kuwa na Nay wa Mitego na Shamsa Ford Wanapika na Kupakua Huu Hapa

$
0
0
Staa mrembo kutoka Bongo Movies, Shamsa Ford ambae hivi majuzi aliweka wazi kuachana na mume wake ambae wamezaanae mtoto mmoja, imebainika kuwa kwasasa yupo kwenye mahusino ya kimapenzi na Staa wa Bongo Fleva, Nay Wamitego.

Hivi sasa wawili hao wanaonekana sehemu mablimbali wakiwa wapo close na kutupia mapicha mtandaoni kitu kinachompa presha mwadada Siwema ambae hivi majuzi alinyang’anywa mototo na Nay Wa Mitego na hiyo kuamua kurusha madogo mtandaoni.

Japo kuwa Nay wa Mitego yupo mstari wa mbele kuwapondea wadada wa Bongo Movies kwenye nyimbo zake, lakini kwenye maisha halisi anaonekana kuwzimia sana kwani alishakuwa na mahusia yo kimapenzi na wadadawa bongo movies kadhaa kabla ya Shamsa wakiwemo  Nisha na Bozi.

Hapo juu ni picha ya Nay na Shamsa Wakilana Denda kwa Raha zao......
Toa Maoni Yako Hapa Chini Matusi Hayarusiwi

Shilole Awatega Midume Coco Beach Awaonyesha Laivu Kazi ya Kiuno Chake Chumbani

$
0
0
Staa wa muziki wa kizazi kipya Bongo, Zuwena Mohamed 'Shilole' juzikati aliwatega vidume baada ya kufanya utundu wa aina yake kwa kuwaita jukwaani na kucheza nao wakati akipafomu kwenye shoo maalum ya Pasaka iliyodhaminiwa na Vodacom mwishoni mwa wiki.

Tukio hilo lilinaswa sawia na mwandishi wetu maeneo ya Coco Beach jijini Dar es Salaam baada ya Shilole kupandwa na ‘mzuka’ wakati akicheza na madensa wake waliovaa vibukta vifupi ambapo aliwaomba wanaume kadhaa wapande jukwaani wacheze naye kwa staili za ‘hatari’ kwani yeye alilala chini na mwanaume akaja kwa juu, hali iliyozua miguno kwa umati uliohudhuria

Viewing all 104808 articles
Browse latest View live




Latest Images