Tofauti ya Askari Wetu na Wenzetu..Katika Majanga ya Mafuriko
Hapa Nimeweka Taarifa ya Wizara ya Mawasiliano Kuhusu Sheria Ya Makosa ya Mitandao kuanza Kutumika
Ndugu Wananchi,
Ndugu Waandishi wa Habari,
Kukua kwa kasi kwa matumizi ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA) kumeleta mafanikio mengi katika nyanja mbalimbali za maisha ya kila siku. Mafanikio haya yanathibitika kwa kuongezeka kwa huduma za mawasiliano, huduma za kifedha na matumizi ya mitandao ya kijamii.
Aidha, mafanikio hayo yameleta changamoto nyingi katika jamii. Changamoto hizo ni pamoja na kuibuka kwa makosa mapya ya jinai na pia mbinu mpya za kutenda makosa ya zamani.
Ndugu Wananchi,
Makosa hayo hujumuisha uhalifu wa Mitandao ambao simu za mkononi, kompyuta au mifumo ya kompyuta hutumika kama nyenzo za kutenda uhalifu huo.
Mifano ya makosa hayo ni kama ifuatavyo:
1. Kumekuwepo na wizi wa fedha kwa njia ya mtandao,
2. Kumekuwepo na ugaidi kupitia kwenye mitandao,
4. Kuwepo na mmomonyoko mkubwa wa maadili,
3. Kumekuwepo na uharibifu wa miundombinu muhimu ya Taifa kwa makusudi, Kwa mfano kukatwa kwa makusudi Mkongo wa Taifa wa Mawasiliano. [Hii imepelekea kuisababishia Serikali na Sekta binafsi hasara na kusababisha kukosekana kwa huduma mbalimbali za kiuchumi na za kijamii].
Ndugu Wananchi,
Kama mnavyofahamu kwenye kikao cha Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania lililopita, Serikali ilipeleka Mswada wa kutunga sheria ya uhalifu wa mtandao (Cyber Crimes) na Sheria hiyo ilipitishwa na Bunge.
Madhumuni ya kutunga sheria hii kama sheria nyingine zilizotungwa na Bunge hapa nchini ni kutatua changamoto mbalimbali zinazoikabili jamii hasa kwenye matumizi ya TEHAMA.
Ndugu Wananchi,
Ndugu Wandishi wa Habari,
Tanzania siyo nchi ya kwanza kutunga sheria kama hii. Kuna nchi mbalimbali duniani zimetunga sheria kama hii, kwa mfano nchi ya Uingereza (UK Computer Misuse Act, 1990), India (IT Act, 2000), Malaysia (Computer Crime Act 2. ) Uganda (Computer Misuse Act, 2010), Korea ya Kusini (Information and Communications Network Act na Information and Communication Infrastructure Protection Act), Singapore (The Computer Misuse and Cybersecurity Act), Maturities (Computer Misuse and Cybercrime Act, 2003), Afrika ya Kusini, Marekani (Computer Fraud and Abuse Act, 1984) na nyingi nyinginezo.
Ndugu Wananchi sasa mmepata pahala pa kukimbilia, kwani mukitendewa uhalifu kupitia mitando sheria hii itawasaidia kupata haki zenu. Ninawashangaa sana wale wanaopinga kutungwa kwa sheria hii hapa Tanzania.
Haikubaliki hata kidogo kuona Wantanzania wengine wanakumbana na uhalifu kupitia Kwenye mtandao na wachache kwa faida zao binafsi wanataka Serikali ikae kimya.
Sheria hii haina tofauti na sheria za nchi nyingine nilizozitaja hapo awali. Sheria hii imetungwa kwa mazingira ya nchi yetu ya Tanzania.
Ndugu Wananchi,
Sheria hii sasa imeshasainiwa na Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete baada ya kupitia hatua zote za kuiboresha.
Hatua ya MWISHO ilikuwa ni ile ya marekebisho yaliyofanywa na Bunge ambapo baadhi ya vifungu vilivyolalamikiwa viliboreshwa.
Kwa hivyo wananchi sasa tuipokee sheria hii na kuitumia. Sheria hii ni nzuri na itasaidia sana kuwalinda wananchi, mitandao na miundombinu yetu muhimu ya kitaifa.
Katika kuitumia sheria hii na kama ilivyo kwa sheria nyingine yoyote, patakapoonekana kuna mapungufu, marekebisho yatafanyika. Kwa hivyo kama kuna mtu yeyote mwenye maoni ya kuiboresha sheria hii anaweza kuleta maoni Serikalini hapa Wizarani.
Ninarejea tena: Waheshimiwa Wabunge, Waheshimiwa Mabalozi, wadau mbalimbali wa Sekta ya Mawasiliano, waandishi wa habari, wana-bloggers, na wananchi kwa ujumla kama kuna yeyote mwenye maoni ya kuboresha kifungu chochote cha sheria hii alate maoni hayo hapa Wizarani.
Serikali kupitia Wizara yangu itapokea maoni au ushauri huo, tutayatafakari na kuyafanyia kazi kwa kina. Haitosaidia sana kusema huko pembeni, jukwaa zuri la kuleta maoni ni kupitia Wizara yangu.
Ndugu Wananchi, na
Ndugu Waandishi wa Habari,
Hii haitokuwa sheria ya kwanza kufanyiwa marekebisho kama itaonekana kuna umuhimu wa kufanya hivyo.
Ahsanteni na Ninawashukuru sana kwa kunisikiliza.
Watu Watano Wathibitishwa Kufariki Dunia Jijini Dar es Salaam Kutokana na Mafuriko
JAMHURI YA MUUNGANO WATANZANIA
WIZARA YA MAMBO YANDANI YA NCHI
JESHI LA POLISI TANZANIA
PRESS RELEASE
08/05/2015
WATU WATANO WATHIBITISHWA KUFARIKI DUNIA JIJINI DAR ES SALAAM KUTOKANA NA MAFURIKO
Watu watano wameripotiwa kupoteza maisha jijini Dar es Salaam kutokana na athari za mafuriko kufuatia mvua zinazoendelea kunyesha jiji. Mvua hizo zinazonyesha kwa siku tatu mfululizo zimesababisha vifo vya watanzania hawa katika maeneo tofauti ya jiji la Dar es Salaam kama ifuatavyo:
Mnamo tarehe 06/05/2015 majira ya saa moja kamili usiku huko maeneo ya Magomeni Kinondoni jijini Dar es Salaam mtu mmoja jina SHABAN S/O IDD, Miaka 73, Mkazi wa Manzese alisombwa na maji ya mto ng’ombe alipokuwa akijaribu kuvuka mto huo. Mwili wake ulipatikana siku iliyofuata 07/05/2015 akiwatayari amekwishafariki dunia na umehifadhiwa katika hospitali ya Mwananyamala.
Kifo kingine kilitokea tarehe 07/05/2015majira ya saa sita kamili mchana huko maeneo ya Mwananyamala Mbuyuni Kata ya Mwananyamala, OysterBay, Kinondoni jijini Dar es Salaam ambapo mtu mmoja aitwaye MASUMBUKO S/O DOUGLASS @ LIMAMU, Miaka kati ya 50-55, mkazi wa Mwananyamala Mbuyuni, alianguka na kufariki dunia ghafla wakati anatoa maji yaliyoingia nyumbani kwake. Uchunguzi wa awali umebaini kuwa marehemu alikuwa na tatizo la ugonjwa wa kifafa hivyo wakati akihangaika kutoa maji, ugonjwa huo ulimpata na kuanguka kwenye maji na kufariki dunia baada ya kukosa msaada wa haraka. Mwili wa marehemu umehifadhiwa Hospitali ya Mwananyamala kwa uchunguzi.
Mtu mwingine mwanaume RASHIDI S/O HASSAN, Miaka 36, Mkazi wa maeneo ya Mvuruhani Pemba Mnazi Kigamboni jijini Dar es Salaam alizama katika mkondo wa maji unaoelekea baharini tarehe 06/05/2015. Mwili wake ulipatikana tarehe 07/05/2015 ukiwa unaelea majini umbali wa mita 500 toka eneo alilozama.
Kifo kingine kimetokea tarehe 06/05/2015 huko Yombo Makangarawe ambapo mtoto aitwaye GLORIA D/O MREMA, mwaka mmoja na miezi mitatu alipotea baada ya watoto wenzake kumuacha wakati wakicheza pamoja. Juhudi za kumtafuta zilifanyika bila mafanikio hadi mwili wake ulipopatikana ukiwa unaelea majini katima mto mzinga akiwa tayari ameshapoteza maisha. Mwili umehifadhiwa katika Hospitali ya Temeke
Kifo kingine kimetokea tarehe 08/05/2015 saa moja kamili asubuhi huko maeneo ya Kinondoni Mkwajuni, Kata ya Mkwajuni Wilaya ya Kinondoni ambapo mtu mmoja mwanaume ambaye jina lake halikufahamika mara moja anayekadiriwa kuwa na umri kati ya miaka (40-45) mkazi wa Kinondoni Mkwajuni, alikutwa amefariki dunia. Mwili umehifadhiwa Hospitali ya Taifa Muhimbili kwa uchunguzi.
Pamoja na vifo hivyo kuripotiwa, pia mtu mmoja ajulikanae kwa jina la MABULA S/O MOSSES, Miaka 65, Mkulima, Mkazi wa Vingunguti, Buguruni wilaya Ilala amevunjika mguu wake wa kulia sehemu ya chini ya goti baada ya kuangukiwa na ukuta wa Godown la FIDA S/O HUSSEIN lililopakana na nyumba yake. Pia ukuta huo umesababisha uharibifu wa vitu mbalimbali. Majeruhi amepekwa Hospitali ya Amana kwa matibabu.
Katika kata ya Mchikichini, taarifa ya mafuriko inaonyesha takribani nyumba 60 hadi 70 zimefunikwa na maji hadi juu ya mapaa ambapo wakazi wake tayari walikuwa wamehama kufuatia agizo la Serikali kuwa wahame maeneo hayo. Pia takribani watu 30 hadi 35 wamejihifadhi katika shule ya Srkondari Mchikichini.
Katika Kata ya Jangwani, zipo nyumba zinazokadiriwa kufikia 90-100 zimefunikwa na maji hadi juu ya paa. Wakazi takribani 250-300 walihama mapema kufuatia taarifa hiyo ya Serikali. Aidha watu wanaokadiriwa kati ya 25-30 nao wamejihifadhi katika Shule ya Sekondari Mchikichini.
Aidha, maeneo yaliyoathirika zaidi kutokana na mvua zinazoendelea kunyesha ni Keko, Chang’ombe maduka mawili, Yombo Vituka, Vingunguti, Africana, Msasani Bonde la Mpunga, Eneo la Jangwani, Manzese, Kigogo, Mburahati, Boko Basihaya, na maeneo mengine ambayo taarifa zake bado hazijapokelewa
Barabara zinazounganisha katikati ya Jiji na pembezoni zimeharibika na hivyo kusababisha kutolewa maelekezo barabara hizo kufungwa ili kupunguza madhara ambayo yangeweza kutokea.
Aidha, madaraja mbalimbali yameharibika h
ivyo kukata mawasiliano kutoka upande mmoja kwenda upande mwingine. Kwa mfano daraja la linalounganisha Mbagala na Mtoni Kijichi maarufu kama njia ya ng’ombe. Daraja lingine ni lile la Kinyerezi ambalo halipitiki baada ya kusombwa na maji.
Jeshi la Polisi kwa kushirikiana na Serikali limejiandaa kwa hali ya dharura itakayojitokeza. Pia Jeshi la Polisi limejipanga kukabili foleni kwa kuhusisha askari wa vikosi mbalimbali ili kukwamua tatizo hilo ambalo limesababishwa na uharibifu wa miundombinu.
Aidha nawataka wananchi wote kuchukua tahadhari ya hali ya juu hasa wale waishio maeneo ambayo ni mikondo ya maji au watumiaji barabara zinazopitiwa na mikondo hiyo. Wananchi wanaombwa kutoa taarifa za mapema na haraka pindi wanapoona au kugundua kuna maeneo au jambo linalohatarisha maisha yao na ya watu wengine.
NB: Wakati huo huo zimepokelewa taarifa za kupatikana kwa miili ya watu watatu waliofariki ambayo inafanyiwa uchunguzi katika hospitali mbalimbali jiji Dar es Salaam ili kujua kama vifo hivyo vimetokana na mafuriko yaliyosababishwa na mvua zinazoendelea kunyesha jiji. Taarifa kamili zitatolewa kuhusu wajihi wa watu hao na wako katika hospitali gani
S. H. KOVA
KAMISHNA WA POLISI KANDA MAALUM
DAR ES SALAAM
Kajala Aapa Kutousahau Msaada wa Wema Sepetu
Kajala amesema hafikirii kuzirudisha fedha hizo kwa Wema ambaye amekuwa akieleza kujuta kuutoa msaada huo.
“Sio kwamba natamani kumrudishia milioni 13, kwa sababu mimi najua yeye alinisaidia kipindi mimi naHitaji na hakuna mtu yoyote alitokea kunisaidia kipindi hicho,” Kajala aliiambia Global TV.
“Kweli nashukuru mpaka kesho kwa sababu alitoa msaada ambao siwezi kuusahau hata kama tuna ugomvi kiasi gani. Sasa kwa sababu yeye alisaidia kwa moyo mmoja na akikaa akiongea anajuta kwanini alinisaidia kumlipia Kajala inakuwa inamfutia hata zile baraka alizozipata.”
Hii ndiyo Sababu ya Mwigizaji Ray Kutooa Hadi Sasa..Japo Umri Unazidi Kumtupa Mkono
Akizungumza na gazeti la Ijumaa katika mahojiano maalum, Ray alisema amekuwa akipangua mawazo ya kuoa kila wakati kutokana na ugumu wa kumpata mwanamke ambaye hatampa stress kama zinazowapata baadhi ya watu.
Alisema, kwa kuwa suala la kuoa ni jambo nyeti, halihitaji kukurupuka na hicho ndicho kimemfanya mpaka leo asiingie kwenye maisha ya ndoa.
“Unajua hili suala la ndoa ni sensitive ‘nyeti’ sana, halihitaji kukurupuka, linakutaka ukiingia kwenye uhusiano umchunguze vizuri huyo uliyempata ili kujiaminisha kwamba, hatakusumbua.
“Hilo ndilo linalonifanya niwe singo mpaka leo, najua wengi wananishangaa lakini kwa kifupi ugumu wa kumpata mweza sahihi ndiyo sababu ya kutooa mpaka leo,” alisema Ray.
Alipoulizwa kwamba, ina maana kwa wapenzi wake waliopita wakiwemo Ruth Suka ‘Mainda’, Blandina Chagula ‘Johari na Hans Chuchu hakuna aliyeona anafaa kuwa mke, msanii huyo alicheka sana kisha akasema: “Wewee, acha mambo yako.”
Sakata la Escrow: IKULU Yasema Katibu Mkuu, Wizara ya Nishati na Madini Ndugu Eliakim C. Maswi Hana HATIA
SAKATA LA OPARESHENI TOKOMEZA: Ikulu Yasema Mawaziri WOTE Waliofukuzwa Kwa Kashfa Hiyo Hawana HATIA
- Wanakijiji hawakupewa taarifa ya kutosha kuhamisha mali zao kabla ya kuchoma nyumba zao;
- Baadhi ya wanakijiji walipoteza vyakula na mali zao katika zoezi hilo la uchomaji moto;
- Kuna vijiji vilivyosajiliwa lakini sehemu ya vitongoji vyake viko ndani ya Hifadhi za Taifa;
- Kuna maeneo ya hifadhi au ushoroba (buffer zone) ambayo hayana alama za mipaka kati ya hifadhi au ushoroba na vijiji husika;
- Kuna nyumba ambazo hazikuwa kwenye eneo la hifadhi au ushoroba na hivyo zilichomwa moto kinyume cha sheria.
- Baadhi ya matukio na malalamiko ya kuchomewa moto nyumba yalitokea kabla ya Operesheni.
Kioja..Aunty Lulu Adai Makalio Yake Makubwa Yanamtesa Sana..Wavulana Wanamfuata Kutaka Kamchezo Kabaya
Akipiga stori na Risasi Jumamosi, Aunty Lulu alisema wanaume wengi wamekuwa wakimiminika kutaka baada ya kusambaziana kuwa mwigizaji huyo analitumia umbo lake ndivyo sivyo.
“Nawaomba wanaume waache kunifatafata jamani wananikosesha amani kwani mimi nimefundwa najua madhara ya hako kamchezo kabaya, siwezi kuthubutu hata mara moja,” alisema Aunty Lulu
~Global Publishers
Despite Being The No.1 Victim, Wema Sepetu Criticizes And Rejects Cyber Bullying/Crime Law Just For Freedom of Speech To Tanzanians
However, Wema seems to get influency from Mange Kimambi to reject the bill because Mange posted nice article on her blog rejecting the bill and reasons why it should not pass as law, Mange and Wema are like sisters because Mange is the one who discovered Wema through Miss Dar Indian Occean in 2006 and eventually Wema Became Miss Tanzania the same year.
Anyhow, this law is not good, it will not be appropriate to a country which prioritize good and transparent governance
Photo: A Glimpse of Jacqueline Wolper's Closet Which Looks Like a Boutique At Her Home !
"Good morning farm, am getting ready to go to work...as always the hardest part of starting my day is finding what to wear...look at me"
Pamoja na Kukanusha Mara Nyingi ..Watu Wadai Wema Sepetu Anatumia Madawa ya Kulevya "Unga"
UBUYU WAVUJISHWA
Kwa mujibu wa chanzo makini, Wema amekuwa akitumia kilevi hicho kwa muda mrefu huku akifanya jambo hilo kwa siri kubwa.“Hivi hamna habari ya Wema kubwia unga? Mbona kila mtu anajua, watu wengi tu wanafahamu lakini wanashindwa namna tu ya kumueleza mwenyewe ili aache maana kila mtu anamhofia si unamjua naye Madam mtu wa kumaindimaindi,” kilisema chanzo hicho.
MITANDAO YAKAZIA MADAI
Kama hiyo haitoshi, kwa nyakati tofauti, watumiaji mbalimbali wa mitandao ya kijamii wamekuwa wakidai kuwa staa huyo anabwia unga licha ya kuwa hawana ushahidi wa moja kwa moja.“Mimi sijawahi kumuona lakini kuna watu wake wa karibu tu wananihakikishia kwamba Wema anatumia madawa ya kulevya, ila naamini mwenyewe anaujua ukweli wote wa haya yanayosemwa,” ilisomeka sehemu ya maoni mtandaoni.
RISASI LAMFUNGIA KAZI
Baada ya kupata madai hayo, Risasi Jumamosi lilimfungia kazi Madam ili kuweza kumsikia anazungumziaje tuhuma hizo nzito.
Jumatano iliyopita, mwanahabari wetu alikwenda nyumbani kwa mwigizaji huyo mwenye mvuto wa kipekee, Mtaa wa Bwawani-Kijitonyama lakini bahati mbaya alikuwa ametoka kwenda kurekodi na hata alipofanya subira hadi jioni, bado hakurejea huku simu yake ikiita bila kupokelewa.
JITIHADA ZAIDI
Siku iliyofuata, mwanahabari wetu aliyeambatana na mmoja wa wahariri wa Global Publishers, walitia timu kwa mara nyingine nyumbani kwa Madam lakini pia mwigizaji huyo alikuwa ametoka lakini bahati nzuri alipopigiwa simu alipokea, mambo yalikuwa hivi:Risasi: Wema tumekutafuta sana hapa nyumbani kwako bila mafanikio tuna ishu ya msingi kweli tunataka kujua kutoka kwako?
Wema: Poleni, ishu gani?
Risasi: Tumepokea habari kuwa wewe unatumia madawa ya kulevya, umewahi kusikia hizi habari?
Wema: Ndiyo hizo habari nimewahi kuzisikia. Nakumbuka nilianza kuzisikia tangu kipindi kile mimi natembea na CK (yule kigogo wake), walivumisha sana lakini hakuna ukweli wowote.
ADAI WAMEMPONZA
“Tena imefika wakati wananikosesha hadi amani, imenifanya hadi niwe nakaguliwa kupindukia bila sababu za msingi, juzi hapa wakati naenda Mwanza (kwenye shoo ya Instagram), walinibana sana pale Air Port hadi nikataka kuachwa na ndege.
AISHI KWA TAHADHARI
“Yaani kwa sasa nimelazimika kuweka hadi ulinzi mkali pale nyumbani, maana huwezi jua watu wasionipenda wanaweza kuja wakanibambikia nikaonekana natumia kumbe sijui hata ukoje. Sasa hivi kila atakayeingia lazima akaguliwe, ahojiwe ndipo aingie.
ATAJA KUHUSISHWA NA ROMMY
“Kuna wakati walinitaja kuwa natumia kwa kuwa nina ukaribu na Rommy Johnson (binamu yake msanii Diamond) kitu ambacho nilikikanusha na ninaendelea kusema hakuna ukweli wowote.
MAMA’KE ARIPOTI POLISI
“Ili kuwataka watu wasinihusishe kwa namna yoyote na kujihadhari, tuliongea na mama, akaenda kutoa taarifa polisi Mabatini ili nisije kupata tatizo lolote linalohusishwa na madawa ya kulevya.”
RAFIKI ZAKE WANENA
Mwanahabari wetu aliwavutia waya marafiki wa Wema, Aunt Ezekiel na Martin Kadinda ambaye ni meneja wa mwigizaji huyo ambao kwa pamoja walidai hawajawahi kumuona Madam hata siku moja akibwia unga achilia mbali kukaa karibu na wabwiaji.
“Sijawahi kumuona Wema hata siku moja anatumia hivyo vitu (unga), watakuwa wanamzushia ili watimize azma yao ya kumchafua si unajua si wote wanampenda?,” alisema Aunt huku Martin akikazia:“Hakuna kitu kama hicho, Madam hatumii bwana, sisi tupo naye, tunafanya naye kazi siku zote, hatujawahi kumuona, huo ni uzushi tu.”
~Global Publishers
Askofu Gwajima Asimamisha Mvua Dar "Mvua imekoma kuanzia sasa na haitaharibu tena, na ninaiamuru ardhi imeze maji yote yaliyojaa juu ya nchi".
Katika mahubiri yake jana jioni tarehe 08/05/2015 siku ya Ijumaa, Askofu Mkuu wa Makanisa ya Ufufuo na Uzima alifundisha juu ya somo liitwalo "VITA VYA HALI".
Katika somo hilo Askofu Gwajima alibainisha wazi ya kuwa sio kila mabadiliko ya hali ya hewa yanayotokea duniani ni matokea ya nguvu za kiasilia za dunia yaani Nature au ni mabadiliko ya majira ya mwaka bali wapo watu pia wenye uwezo wa kubadili hali ya hewa kwa njia za kichawi na kusababisha mafuriko makubwa, vifo, uharibifu Wa mali na hasara zinazoweza kuwarudisha watu nyuma.
Katika kudhihirisha mambo hayo Askofu Gwajima alitolea mfano mtu mmoja aliyewahi kuishi duniani aitwaye Nicolas Tesla ambaye alikua na uwezo mkubwa juu ya kubadili na kutawala(control) hali ya hewa.
Baadaye nikaunganisha ujumbe wa Askofu Gwajima na nikagundua jambo hili ni kweli kabisa baada ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Bw. Sadick kutangaza kuwa MVUA HIZI ZINASAIDIA SANA KUWAONDOA WATU MABONDENI pasipo kuwaza kuwa watu hawa ndio walipa kodi wake na ndio wanaomlipa mshahara wake!
Kwa maneno yale sasa tunaamini ya kuwa Sio kila mvua, mafuriko, ajali za moto, ajali za magari au kiangazi ni mambo ya asili bali mengi hutengenezwa na wanadamu(wachawi) na mashetani ili kuwaangamiza wengine.
Kabla ya kumaliza Ibada hiyo jana jioni majira ya saa moja na nusu, Askofu Gwajima ambaye ni Amiri Jeshi Mkuu wa Jeshi la Bwana la Ufufuo na Uzima aliyaongoza majeshi yote kwenye maombi ya kusambaratisha mvua na mafuriko yote na hali kuwa ya kawaida.
Maarifa makubwa aliyonayo Askofu Gwajima juu ya mambo ya rohoni na mwilini umefanya watu kuzijua hila za wachawi na mashetani wenye nia ya kuangamiza watu na kuwafanya masikini kwa njia ya maji..
"Mvua imekoma kuanzia sasa na haitaharibu tena, na ninaiamuru ardhi imeze maji yote yaliyojaa juu ya nchi"... alisema Askofu Gwajima katika kumalizia ibada.
JE Thamani ya Yamoto Band ni Nyumba na Gari ?
Kilichonifanya niandike huu uzi ni Tukio ambalo limetokea jana ikiwa ni siku ya kuzaliwa ya kiongozi wa band hiyo Aslay, katika siku hiyo ndugu Fella alitoa zawadi ya gari dogo kwa kijana wake. Sambamba na hili Fella ameshatangazia uma kuwa Nyumba za hawa vijana watakabidhiwa mwezi wa saba na pengine Rais akawa mgeni rasmi. Nimpongeze tena Fella kwa hatua hii nzuri
Ninachojiuliza hapa na kilichopelekea kuandika huu uzi ni Je nini thamani ya mziki wa hawa vijana? Mimi sio mtaalam wa kutathimini mziki ila kitu kimoja ambacho nina uhakika ni kuwa hawa vijana wana kipaji kikubwa chenye thamani zaidi ya hili gari na hizo Nyumba watakazopewa. Najua utajiuliza iweje niseme hivi Wakati hizo Nyumba sijaziona, naongea haya kwa uzoefu wa Fella kwani amekuwa akiwanunulia Nyumba wasanii wake Temba na Chege,
Mara ya mwisho nilimuona Fella akimkabidhi Temba Nyumba aliyomnunulia nje ya mji. Kimsingi ile Nyumba ilikuwa ni ya kawaida sana na ni Nyumba ambayo ilikuwa chakavu kwa kiasi fulani. Thamani ya Temba na Chege Sidhani kama ni sawa na Nyumba ya namna ile. Kutokana na hilo ndio maana naamini hata hawa vijana wa Yamoto nao watapewa Nyumba za ubora wa kawaida ambayo si linganifu na thamani ya vipaji vyao.
Kwanini Fella uwanunulie Au kuwajengea Nyumba wasanii wako? Kwanini usiwape hela zao wafanye yao wewe ubaki kuwasimamia na kuwakumbusha umuhimu wa kufanya maendeleo. Wasanii wako sio Watoto kiasi kwamba washindwe kusimamia ujenzi Au ununuzi wa Nyumba zao. Kitendo hiki cha kuwajengea Au kuwanunulia Nyumba kinaficha Mengi juu ya gharama halisi za manunuzi.
Mbona dimond Nyumba yake hamjamjengea Au kumnunulia? Hili ni swali ambalo nawaachia Yamoto band,Chege na Temba. Ifike mahali msanii awe mwajiri wa manager na sio kinyume chake, ndio maana Diamond anafanikiwa sababu yeye kawaajiri Fela na Babu Tale japo mbele ya Jamii huwa anajishusha ili ionekane kama Hao wawili ni maboss zake
By xfactor
New Couple Alert? Alikiba & Jokate Mwegelo (Details)
Tetesi hizo zimekuwepo kwa muda sasa japo wawili hao bado hawajaweza kuthibitisha muungano wao.
Mtangazaji namba moja kwa udaku nchini, Soudy Brown wa Clouds FM alijaribu kumtafuta Jokate kutaka kutegua kitendawili hicho lakini kama ilivyotarajiwa, Jokate aliishia kuangua kicheko tu na kutotoa jibu.
Wafuatiliaji wa mambo wameenda mbali zaidi na kudai kuwa wawili hao wamekuwa wakionekana pamoja kwenye sehemu kadhaa ikiwemo nyumbani kwa Alikiba.
Wengine wamefuatilia baadhi ya picha zao mitandao ya kijamii na kugundua kuwa Jokate amewahi kuivaa kofia ya mkeka ya Alikiba!
Bongo5 binafsi haijaweza kuthibitisha uwepo wa uhusiano huo.
Shilole Posted Her Video On Instagram Talking Broken English..Seriously !
MKE Alininyanyasa Sana Nilipofukuzwa Kazi, MUNGU Ameniona, Sasa Yamegeuka
Hiyo ilikua ni baada ya uchunguzi wa miezi kdhaa wa kosa nililokua nimelifanya bahati mbaya. Miezi mitatu nyuma nilimuingizia pesa mteja kimakosa kwenye akaunti yake kiasi cha million mia tatu na hamsini ambazo alitakiwa kuwekewa Mteja mwingine halali kupata pesa hizo.
Kama humu ndani Kuna banker ataelewa nachokisema, kwamba makosa kama haya benki ni kawaida sana. Ukigundua kosa kama hili unawahi una reverse hiyo entry una m-credit anaetakiwa shida ni kama uliemwekea kimakosa akawahi kuzichukua ndipo yanakukuta yaliyonikuta mimi.
Baada ya kufukuzwa kazi mke wangu alibadilika kabisa
Nilishuhudia yafuatayo:-
(1) Alitamka mimi ni mjinga ndio maana nimefukuzwa kazi.
(2) Chake kikawa chake tu.
(3) Akawa anawaambia wazi watoto kuwa kitu fulani kimenunuliwa na yeye na sio mimi.
(4) Muda wa kurudi home ukabadilika sasa anarudi usiku mwingi, nampa kipigo cha nguvu anazira na kukimbilia kwao, kwenye usuluhishi anawaambia wasuluhishi kwamba mimi namuonea wivu kwa kuwa ana kazi mimi sina.
(5) Niliuza Gari zangu mbili ili nipate mtaji wa kufanya biashara hivyo nikawa sina Gari nilijua maadam wife ana Gari tutatumia wote maana hata yeye wakati hana Gari alikua akitumia magari yangu.
Kinyume na matarajio hakutaka kabisa niguse Gari lake mimi nikawa mtu wa miguu.Majirani wakawa wanashangaa mfumo wetu wa maisha.
(6) Life yetu ya bedroom ikawa imekufa no intimacy no love making nothing. Alianza kidogo kidogo leo mara aseme anaumwa, kesho kachoka, hadi mwezi unaisha. Nikaamua isiwe tabu nikaacha kuulizia tena, nae akawa amepotezea moja kwa moja.
Hata wazazi wangu aliwa mistreat sana wakawa hawaji tena kwangu, mama yangu akawa ananitumia vitu kwa njia basi kutoka nyumbani kama mchele, maharage, unga na kadhalika ili na mm nionekane nachangia.Wakuu siku ya kufa nyani miti yote huteleza. Kila nilichojaribu kukifanya ili nijinasue kinakwama, nakuta mtaji wote unakata naanza moja.Ilikatika miaka minne nikiwa kwenye hali hii maana nilipata matatizo 2010. Mwaka Jana kuna Dada mmoja tulisoma wote primary school akaamua kunisaidia, huyu dada tulikutana Posta accidentally tukapeana contact
mimi nilishamsahau ila yeye alinikumbuka.
Baadae akaniunganisha na mumewe ambae ni HR manager kwenye shirika fulani, nikamwelezea ukweli wote na akaniingiza kaziniWife sikumwambia kuwa nimepata kazi akaanza kuona nakuja na mahitaji ndani, nikawa naondoka zangu alfajiri narudi usiku mwingi. Nikaita mafundi wakabomoa ukuta wote wa fensi uliokua umeoza waliiba sana cement wakati wa ujenzi ukajengwa upya, vitu vyote vilivyochoka ndani nikabadilisha. Wife alishangaa sana ila akashindwa kuniuliza maana hadi hapo tulikua hatuongeleshani zaidi ya salam za asubuhi na jioni tu basi.
Wana jf siwezi kuwaficha sehemu niliyopata naingiza hela Mara kumi ya ile kazi yangu ya benki, hii sikutokana na mshahara bali njia mbali mbali katikati ya mwezi kitengo chetu tupo wanne,hali ikiwa nzuri huwa tunagawana hadi laki mbili kila siku, kama hali ni mbaya tunagawana laki moja kwa siku hii ni mbali na ile tunayogawana mwisho wa mwezi kama million 3 each person mshahara ni mdogo tu ni laki saba tu kwa mwezi.Maana mshikaji alisema anaweza kuniingiza kazini ila kama mfanyakazi wa kawaida kwa kuwa benki nilifukuzwa hakukua na reference wala background check so nikaamua kufuta kwenye CV kuwa nilifanya bank.
Nimeanza mchakato wa talaka kupitia mwanasheria mmoja rafiki yangu, mwezi January mwaka huu amemwandikia barua ya kumtaarifu uamuzi huo na copy Ustawi wa jamii pia, baadae tutafungua shauri la talaka.Kinyume na matarajio yangu wife kwa kuwa alishañichoka na hakuna kinachoendelea kati yetu nilijua angekubali tu. Cha ajabu hivi sasa kupitia wazee wake wameniita kikao zaidi ya Mara 6 sasa ili tusuluhishe tofauti zetuKawa mpole sana, alidhan nitaendelea kuteseka milele
Wakuu sasa sipo nyumbani kwa hasira ya mambo aliyonitendea hivi sasa sipo nyumbani nimepanga upande wa nyumba nimeanza ujenzi ili nihamie. Kila siku lazima nipite kwa watoto niwaone ndo niondoke. Nimesimama njia panda, mm binafsi nilishaamua simtaki tena huyu mwanamke ila wazee na viongozi wa dini tunakoabudu wanasema turudiane juzi mke wangu alinipigia magoti tukiwa kikaoni kwamba nimsamehe, nifute kusudio la kuomba talaka mahakamani. Wazazi wangu hawataki kusikia kabisa neno msamahakwa matendo aliyotufanyia.
NB: Nimetaja kipato ili kuwapa mwanga na uelewa wa tatizo isichukuliwe vinginevyo
Nimesikia amepata matatizo kazini ila sina uhakika na taarifa hizo
Naomba ushauri wenu
By Christo devries/Jamii Forums
Wema Sepetu: Ray, Steve Nyerere Wanafiki Wakubwa
Akizungumza na paparazi wa GPL, Wema alisema alikubaliana na mastaa hao kutoenda kwenye Shoo ya Zari All White Party iliyofanyika Mlimani City jijini Dar badala yake waongozane naye jijini Mwanza lakini wakamgeuka.
“Sitaki kabisa nisikie mtu ananiambia habari ya Steve Nyerere au Ray maana ni wanafiki wakubwa, hawawezi kuniahidi kutokwenda pati ya Zari lakini wakaenda na wasije Mwanza kama walivyoniahidi,” alisema Wema.Paparazi wetu baada ya kupata malalamiko ya Wema, alimsaka Steve ili aweze kuzungumzia unafiki wao, akafunguka:
“Kweli mimi na Ray tuliahidi kuungana na Wema kwenye shoo yake ya Mwanza ila siku ya mwisho tulikwama baada ya kupungukiwa fedha ya nauli, hivyo tukashindwa kabisa na tusingeweza sisi kwenda huko kwa kumtegemea yeye atulipie kila kitu.Tukaona twende kwa Diamond ambaye naye alitualika.”
Ray hakuweza kupatikana mara moja kuzungumzia tuhuma hizo.
Globalpublishers
Mchumba wa Shilole Nuhu Mziwanda Atoa Kali Nyingine ya Mwaka...Hii Sasa Kutafuta Kick
tueleweshane wapendwa
Nuhu Ameandika Hivi kwenye caption ya hiyo picha hapo Juu : She is my angel to me and inside my heart is draw she is name by natural ink from the God , love of me mziwanda to she is so not aproched with others girls
Baada ya Wema Kupromote Watu Wampigie Kura Ali Kiba Kill Awards, Diamond Aibuka na Kuziponda Vibaya Tuzo Hizo ya Kill Awards
Embu ona hiii : Wema Sasa amekuja na nguvu zote ana mtangaza Ali Kiba Kwenye Instagram yake na Kuomba watu wampigie kura kushinda Kill Music Awards wakati akijua kabisa Ali Kiba na Diamond haziivi ...
Baada ya Muda Diamond Anaibuka na Kuziponda Vibaya Tuzo za Kill Awards Kama Univyosomeka Hapa Chini:
Mwigizaji Lulu Michael Amganda Van Vicker!
Habari kutoka chanzo makini ambacho ni mtu wa karibu wa Lulu kilidai kwamba, mwanadada huyo amekuwa na mawasiliano ya karibu na Van Vicker tangu walipokutana Septemba, 2013 kwenye Jengo la Akade, Posta jijini Dar ambapo jamaa huyo alitua nchini kurekodi filamu na mastaa wa Bongo.
“Kwa taarifa yenu Lulu sasa hivi mambo yake na Van Vicker ni bambam na wanawasiliana usiku na mchana, nadhani kuna kitu kikubwa kinakuja. Yaani Lulu amemganda jamaa japokuwa sijajua kamili kama wana project gani.
“Kama mtakumbuka kipindi kile Van Vicker alikuja Bongo kucheza filamu ya Hashim Kambi (mwigizaji wa Bongo) ndiyo walifahamiana.
“Inawezekana anataka kufanya naye kazi kama Wema (Sepetu) ambaye hivi karibuni alikwenda Ghana na picha zikasambaa wakifanya yao,” alisema mtu huyo kwa sharti la kutochorwa jina gazetini.
Baada ya kumwagiwa ‘ubuyu’ huo, gazeti hilo lilizungumza na Lulu juu ya ishu hiyo ambapo alikiri kuwa ni mtu wake wa karibu na kwamba ni kweli amekuwa akiwasiliana naye.“Van Vicker ni mtu wangu, nimekuwa nikiwasiliana naye, kusalimiana na kuulizana maendeleo ya kazi zetu za sanaa,” alisema Lulu.