Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104803 articles
Browse latest View live

Lowassa Amtisha Rais Kikwete

$
0
0
EDWARD Lowassa, mmoja wa wanachama wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), waliojiapiza kufia katika urais, amekimega chama hicho vipande viwili. Anaripoti Yusuf Aboud … (endelea).


Lowassa aliyekuwa mmoja wa wanachama sita wa chama hicho walikuwa katika uangalizi, anadaiwa kuwa ameshindikiza kuondolewa mapema adhabu hiyo, vinginevyo angeondoka.

“Ni kweli chama chetu kimemshindwa Lowassa na sasa kimemuondoa kifungoni. Hii maana yeka ni kwamba sasa Lowassa yuko huru kuwa mgombea urais wa chama chetu katika uchaguzi mkuu ujao,” anaeleza mjumbe mmoja wa NEC aliyezungumza kwa sharti la kutotajwa gazetini.

Amesema, “Kwa maoni yangu, hatua hii itakidhoofisha zaidi CCM kuliko kukiimarisha. Kama CCM inajitakia mema, hakiwezi kuruhusu Lowassa kuwa mgombea wake. Huyu mtu amekivuruga chama chetu. Amenunua watu wetu na amekigeuza chama kuwa genge la wanunuzi wa kura.”

Jana Jumatatu, Kamati ya Maadili ya chama hicho iliyodai ilikuwa na “faili la Lowassa na watuhumiwa wengine sita,” imesema kuwa mwanasiasa huyo “hana tena hatia na kwamba adhabu aliyopewa tayari imemalizika.”

Wachambuzi wa mambo ya kisiasa ndani ya chama hicho wanasema, “kuachiwa huru Lowassa” kunathibitisha udhaifu wa mwenyekiti wa chama hicho, katika kusimamia chama chake.

Taarifa zinasema, ikiwa Lowassa atakapitishwa na chama hicho kuwa mgombea wake urais, taifa litaendelea kutumbukia katika visa vya visasi, kutekwa na kuteswa, kumwagiwa tindikali na matukio mengine dhidi ya wananchi na vyombo vya habari.

Aidha, watu kadhaa akiwamo Rais Jakaya Kikwete, Ridhiwani Kikwete, Salma Kikwete, Bernard Membe, George Madafu, Jack Zoka na Othuman Rashid, wataweza kufikishwa mahakamani na kushitakiwa kwa madai ya matumizi mabaya ya madaraka.

Wengine wanaoweza kufikishwa mahakamani, waandishi wa habari na wamiliki wa vyombo vya habari, ambao watatuhumiwa kuandika uchochezi na kudhoofisha serikali.

Jakaya Kikwete ambaye ndiye rais wa Jamhuri, amewahi kunukuliwa na mmoja wa marafiki zake akijiapiza kuwa “Lowassa hawezi hata kufikiriwa kuwa mgombea urais.”

Hivi karibuni, gazeti moja linalotoka mara moja kwa wiki lilichapisha taarifa kuwa Lowassa anaungwa mkono katika mbio zake za kugombea urais na aliyekuwa mbunge wa Igunga (CCM), Rostam Aziz.

Kwa mujibu wa gazeti hilo, Rostam ametajwa kuchukua nafasi ya aliyekuwa mkurugenzi wa usalama wa taifa, Col. Apson Mwang’onda ambaye alitajwa kuwa mwenyekiti wa “kamati ya ushindi ya Lowassa.”

Rostam ambaye amehamishia sehemu kubwa za biashara zake nchini Kenya na Dubai kwa sasa, ndiye aliyekuwa mfadhili mkuu wa Kikwete katika mbio za urais mwaka 2005.

Mfanyabiashara huyo ambaye amewahi kuwa mbunge wa Igunga (CCM), alikuwa miongoni mwa kundi lililohodhi CCM na kufanya maamuzi mengi kwa niaba ya chama na serikali. Katika miaka mitano ya kwanza ya utawala wa Kikwete, Rostam alifanywa mweka hazina wa chama hicho.

Mbali na Rostam Aziz, Lowassa amezunguukwa na watu wengi wanaotiliwa shaka uadilifu wao mbele ya jamii, akiwamo Andrew Chenge na Nazir Karamagi

Source:Mwanahalisionline

Bifu kubwa kati ya Diamond na mbunifu mitindo wa Kimataifa toka Marekani...

$
0
0

Mbunifu wa mavazi toka Marekani anaeitwa Roper amelalamika sana kupitia Instagram kwamba Diamond kamuibia design yake... roper anayewavalisha wasanii wakubwa Marekani kama August Alsina, Future, Meek Mill nk ameandika hivi......


" I usually don't blast people who make or wear fakes of my designs but this person went way to far when they used my logo! diamondplatnumz is wearing fake Roperrope shirt made by a person with bad character and a strong lack or originality! This is not ok! If you steal a design please reframe from using the Designers Logo because it's illegalwww.shoproperrope.com''.


Mimi namshauri Diamond na wasanii wengine wa kitanzania kuwa makini na kila kitu wanachofanya haswa kuhusu product wanazotumia coz muziki wa Tanzania sasa unapaa mpaka mbali tofauti na wana vyofikiria...Hapa kuna ishu za copyright, maana kosa alilofanya ni kupost na kutoa credit kwa Desgner wake Qboymsafi pengine bila kujua stylist wake ambae kiukweli bado ajafikia level za kuitwa dizaina (bongo dizaina hakuna bado) alikopi na kupesti dizaini ya mtu mwingine. Inaweza kuwa hana kosa lakini kikinuka yeye ndio atakuwa responsible.

Niliona Adam Mchomvu amekuja na dizain yake ya mavazi aniita Adamz Apple, kiukweli ukiangalia ile dizaini ni copy and paste sasa na huu utandawazi usishangae tukafirisiwa watu huku.

Tuwe makini sana..Na Diamond kama akiweza kukuafford uyu mchizi aongee nae biashara jamaa amtengenezee kazi zake aigeuze hii ni opportunity.

Mwandamindo wa Marekeani Roper Ajisalimisha kwa Diamond, Afuta Post ya Kwanza Aliyopost Kuponda na Kupost hii Hapa

$
0
0
Waliomchoma chibu ndo wamezidi kumpaisha....
Kijana ni Icon wa ukweli Tanzania...Baada ya wabongo kumkomalia vilivyo mbunifu wa marekani aliyemtuhumu chibu kumuibia kazi zake, sasa ameamua kuifuta ile post yake na kutupia nyingine

Edward Lowassa Aongea na Vyombo vya Habari LEO....... Adai hahusiki na Kashfa ya Richmond, Hana Mpango wa Kuhama CCM na Yupo Tayari Kupima Afya

$
0
0
Waziri Mkuu mstaafu  Edward Lowassa leo amefanya  mkutano maalum nyumbani kwake mjini Dodoma  na  wahariri  wakuu  wa  vyomba  mbalimbali  vya  habari  hapa  nchini. Katika mkutano huo kwa ufupi Lowassa amesema yafuatayo;

1. Amesema Hahusiki lolote na sakata la Richmond na ndio sababu hata kamati ya Mwakyembe haikuona sababu ya kumhoji.

 Amesisitiza kuwa cheo cha uwaziri mkuu ndio ilikuwa lengo la kamati ya mwakyembe na spika wa bunge kipindi hicho Samwel Sitta.

Amesisitiza hicho sio kikwazo kwake katika kuingia Ikulu kwani sakata la Richmond lilipikwa kumchafua. Amechukua muda mrefu kuzungumzia hili la Richmond na amesema atalisema zaidi Arusha wikendi hii.(Jumamosi)

2. Anaamini kila mtangaza nia ana makundi ya kumuunga mkono. Yeye katika mkutano huu na wahariri leo ameambatana na Nazir Karamagi, Peter serukamba, Diana chilolo, Hussein Bashe na wengineo .

Pia aliyekuwa mkurugenzi wa HakiElimu Elizabeti Misoki ametangazwa rasmi kuwa Mkurugenzi wa mahusiano na mawasiliano katika timu ya kampeni ya Lowassa. Amehoji kwani akina Karamagi wana tatizo gani na kwani wao sio binadamu?

3. Lengo kuu atakaloanza nalo ni Elimu na sio Kilimo kwanza . Amesema serikali ya JK ilikosea kuanza na kilimo na kuweka kando elimu. Ametangaza kuwa sera yake ni Elimu Kwanza.

4. Kuhusu pesa anasema anapata michango ya rafiki zake na ataendelea kupokea michango hii wakati wote wa harakati zake na haina madhara yotote.

5. Anasema hatahama CCM na asiyemtaka yeye CCM ndie aondoke ndani ya chama kwani yeye ana uhakika wa kupata nafasi kuwania urais.

6. Amesema hatalipa kisasi kwa lolote lililomtokea katika siasa. Amemwachia Mungu kwani yeye ni mcha Mungu.

7. Amesema Arusha itawaka moto tarehe 30 mwezi huu na kuwataka watanzania kutega sikio kwani ataanika kila jambo kuhusu mustakabali wa nchi hii na mipango yake ya kuiinua nchi kiuchumi katika miaka kumi ijayo.

Bonyeza Hapa Kumsikiliza:

Frola Mbasha Ajiunga Rasmi na Cha cha CHADEMA

$
0
0
MWIMBAJI maarufu wa nyimbo za injili nchini, Frola Mbasha ameijunga na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema).

Akizungumza kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika viwanja vya Tanganyika Packers mjini Dar es Salaam jana, Mbunge wa Kawe, Halima Mdee (Chadema), alisema kuijunga kwa Mbasha katika chama hicho kutasaidia kuhamasisha wasanii wengine ambao wamekuwa wakitumiwa na Chama Chama Mapinduzi (CCM), bila kupata mafanikio.

Idadi kubwa ya wasanii nchini, wanateseka bila ya kujijua, hii inatokana na kutumiwa na CCM bila kupata mafanikio ya aina yoyote…Frola inabidi uwaelimishe ili waweze kujiunga na chama chetu,”alisema Mdee.

Naye Mwenyekiti wa Chadema,Freeman Mbowe alisema siku Serikali itakapowasilisha muswada wa Sheria wa Vyombo vya Habari bungeni, wabunge wa chama hicho na wale wanauounda Umoja wa Katiba ya Wananchi ( Ukawa) watafanya vurugu ili kuhakikisha haupiti.

Alisema baadhi ya vipengele vya muswada huo vinakandamiza waandishi na wananchi kupata habari.

Siku Serikali ikiwasilisha Muswada wa Vyombo vya Habari,mimi na wabunge wangu tutafanya vurugu hadi unaondolewa bungeni,” alisema Mbowe

Naye Naibu Katibu Mkuu- Bara, John Mnyika alisema Jiji la Dar es Salaam lina nafasi kubwa ya kuleta mabadiliko licha ya kuwepo kwa wizi mkubwa kura wakati wa uchaguzi.

Idadi kubwa ya wasanii nchini wanateseka bila ya kujijua, hii inatokana na kutumiwa na CCM Vila ya kupata mafanikio ya aina yoyote, hivyo basi Frola inabidi uwaelimishe ili waweze kujiunga na chama chetu,”alisema Mdee.

Hatimae Mwanamuziki Luteni Karama Amvisha Pete Isabela Mpanda 'Bela'

$
0
0
MWANAMUZIKI Luteni Karama juzi Jumamosi alimmvisha pete ya uchumba mpenzi wake wa siku nyingi ambaye pia ni mwanamuziki, Isabela Mpanda 'Bella'.

Tukio hilo lilifanyika katika Ukumbi wa Klabu Kakala iliyopo Kigamboni jijini Dar es Salaam wakati wa shoo iliyokwenda kwa jina la Swagaz Night ambapo mastaa hao walikuwa wakipiga shoo.

Hawa Ndio Mastaa Vinara wa Kuuza Mechi Sita kwa Sita..Kila Mtoto Ana Mama yake

$
0
0
Watu wengi ambao wamejikuta wakipata watoto wengi kwa wanawake tofauti, wanatafsiriwa tofauti kwenye jamii. Wengine wanaonekana siyo makini katika suala la kujilinda kwa maana ya matumizi ya kinga kwa lugha ya watoto wa mjini hutumia msemo wa ‘kuuza mechi’ bila kujali umuhimu wa afya zao.

Kama hujaelewa, Kuuza mechi ni kushiriki tendo la ndoa bila kinga. Wakati mwingine hutokea kwa bahati mbaya lakini kama itatokea zaidi ya mara moja, lazima watu watakuwa na mtazamo tofauti na wewe, inaonesha ni jinsi gani ni kinara kwenye suala hilo la kuuza mechi.

Uchunguzi unaonesha kuwa kwenye ulimwengu wa mastaa Bongo, kuna wasanii lukuki ambao kwa namna moja au nyingine wameshiriki katika ishu hiyo na matokeo yake ni kuwa na watoto waliozaliwa nje ya ndoa.
Makala haya yanakuletea listi ya vidume mastaa wa Bongo ambao wana watoto waliozaa na wanawake tofauti;

ABDUL SYKES ‘DULLY’ (watoto watatu)
Huyu ni legendary wa Bongo Fleva ambaye hivi karibuni alifikisha miaka 15 katika muziki anaoufanya. Ana watoto watatu ambao anakiri kuzaa na wanawake tofauti ingawa majina ya mama zao huwa ni siri yake.

ALI SALEH KIBA (watoto watatu)
Kiba ni staa mkongwe mwenye mashabiki wengi anayekimbiza na mzigo mpya wa Chekecha Cheketua. Jamaa huyu anaingia katika orodha ya wauza mechi kwa kuwa anakiri kuwa na watoto watatu aliozaa na wanawake tofauti.

Q-Chillah akifikiria jambo wakati akihojiwa na Global TV Online.

ABOUBAKAR KATWILA ‘Q CHILLAH’ (watoto watatu)
Chillah kama ilivyo Dully naye ni legendary wa Bongo Fleva. Jamaa anakiri kuwa na watoto watatu, akiwa amewapata kwa wanawake tofauti ambao siyo mastaa kama alivyo yeye.

KHALEED MOHAMED ‘TID MNYAMA’ (watoto wawili)
Huyu ni mkali wa ngoma kibao kama Zeze, Nyota Yangu, Siku Kama Hizi, Kiuno na nyingine kibao ambazo ziliwahi kuwa nyimbo za taifa. Jamaa ana watoto wawili akiwa amezaa na wanawake tofauti. Mmoja alikuwa maarufu aliyejulikana kwa jina moja la Kinana.


EMMANUEL ELIBARIKI ‘NAY WA MITEGO’ (watoto watatu)
Jamaa anatikisa kwenye Bongo Fleva kwa sasa. Nay anaingia kwenye orodha hii akiwa na watoto watatu, mmoja alizaa na dada wa Kihindi (jina halifahamiki), akazaa na msanii wa Bongo Movies, Skyner Ally na mtoto wa mjini, Siwema Edson.

MACK SEKIMANGA ‘MAKAMUA’ (watoto wawili)
Jamaa ni mmoja wa wakali wa RnB Bongo aliyewahi kutamba na ngoma kama Tell Me Why na nyinginezo. Hakosi kwenye orodha hii kwa sababu ana watoto wawili ambapo kila mmoja ana mama yake.

KULWA KIKUMBA ‘DUDE’ (watoto saba)
Jamaa ‘bana’ ni tishio na  ndiye anaongoza kwa kuwa na watoto wengi kwa wasanii wa Bongo. Dude  ana watoto saba kwa wanawake wanne tofauti. Siku zote amekuwa muwazi kuhusu suala hilo.

(Makala: Gabriel Ng’osha/GPL)

Vita Dhidi ya Diamond ni Kubwa Kuliko Tunavyofikiria

$
0
0
Hakuna ubishi kua kwa sasa diamond platnumz ndie msanii anae ongoza kupigwa vita kuliko msanii yeyote hapa nchini.

Vita hiyo ina ongozwa na baadhi ya walio wahi kuwa wapenzi wake pia na mahasimu wake wa kimuziki (wasanii wengine) kupitia mashabiki zao.

Sawa ni jambo la kawaida kwa wasanii wakubwa duniani na mastar wengine kama wachezaji,maboxer pamoja na waigizaji kuwa na maadui hili linathibitishwa na mfano wasanii kadhaa wa kimarekani walivyo na maadui mpaka inafikia kupigana risasi mfano 2pac,BIG,50cent,mayweather na wengine kibao.

Sababu kubwa za diamond kuanzishiwa vita "maalum" ili ashuke kimuziki na kimafanikio ni kutokana na maneno ya wengi eti kua anaringa,anadharau,ana nyodo,ana mamneno ya shombo,ana ropoka sana,mtoto wa uswahili,hajasoma,mchawi na visababu kedekede.

Wadadisi wa mambo wanasema kua chuki dhidi ya diamond si tu inatokana na sababu zilizo tajwa hapo juu bali inaenda mbali zaidi mapaka kwa team nzima ya diamond hasa mameneja wake.

hapa ni kwamba kwa sasa hakuna asie jua kua unapo ongelea mameneja wakali Tanzania una waongelea Babu tale na Said Fella,Mzozo unakuja pale ambapo kuna watu wanatamani kufika level za wakina Tale but wana chemka ndipo wanapo anzisha kampeni ya kuwaharibia hawa jamaa kwa kisingizio cha kua eti ni wanyonyaji,wana haribu soko la muziki wa bongo fleva na maneno kibao.

kiukweli hawa watu hawajawahi kushindwa kwenye menejimenti yao,kila msanii wanae mmeneji lazma afike mbali wangapi wamejaribu wakaishia njiani? mfano ustadh "juma na musoma", 

Kwa hiyo tunapo itizama vita dhidi ya diamond tusidhani tu kua mashabiki ndio wanao tengeneza hii chuki bali ni mkono wa wadau wakubwa wa muziki hapa nchini wakishirikiana na media kadhaa kuhakikisha wana wapasua mashabiki kwa makusudi tu ili watimize malengo ya kuwamaliza wahasimu wao diamond Fella na babu Tale...!!


Tupingane kwa hoja na sio matusi!!

Desperate Lady Begs Vera Sidika For Her Used Weave

$
0
0
What is the world coming to? I never thought I would see the day when a girl was so desperate for a weave that she literally had to beg for it.

That was the case some time last year when a lady hit Vera Sidika up for one of her used weaves and clothes. The popular socialite is undoubtedly a ‘classy’ lady and she shocked the country when she revealed that one of her weaves cost a whooping Ksh 450,000. We all know that her flashy lifestyle is the envy of many ladies but who knew it could lead to such desperation?!

Below is a screenshot of some of the messages sent to Vera Sidika:



Mchezaji wa Chelsea Didier Drogba Achukua Maamuzi Magumu Kuhusu Kuendelea Kuichezea Chelsea..Soma Hapa

$
0
0
Ligi kuu ya Uingereza leo inafikia ukingoni, huku klabu ya Chelsea wakiwa ndio mabingwa wa ligi hiyo.
Siku ya leo itakuwa ina mchanganyiko wa furaha na huzuni kwa mashabiki wakereketwa wa Chelsea, kwa sababu watakuwa wanakabidhiwa kombe lao rasmi lakini pia itakuwa ndio mwisho wao kumuona gwiji wa klabu hiyo Didier Drogba akiwa anaichezea timu hiyo.
Kupitia akaunti yak rasmi ya mtandao wa kijamii wa Instagram – Drogba ametangaza kwamba leo ndio itakuwa siku yake ya mwisho kuitumikia Chelsea dimbani
Drogba anasema amezungumza na Kocha Jose Mourinho kuhusu hatma yake na amemuelewa kwamba angependa kuendelea kucheza soka japo kwa msimu mmoja. Hivyo ili aendelee kupata nafasi ya kucheza anahitaji kwenda sehemu nyingine.
Drogba amewatakia kila kheri mashabiki wa  Chelsea na ameahidi kurudi kufanya kazi na klabu hiyo huko mbeleni.

Faiza Ally Responds To Her Haters Who Say She Looks Aged And Her Boobs Aren't Saa Sita Kamili

$
0
0
Haters have been haunting Faiza Ally and as we all know Faiza hana simile anapokuwa bullied so she responded to her haters who say she looks aged and her boobs aren't saa sita kamili ya mchana.....Lol. read what Faiza wrote below..........
What do you have to say.......?

Van Vicker Congratulates Wema Sepetu For Her Tuzo Za Watu For Favorite Actress Award

$
0
0
Over the weekend Wema Sepetu won Tanzanian Tuzo Za Watu(People's Choice Awards) 2015 for best actress. Her Day After Death co-star Van Vicker took to instagram to congratulate her. Vicker said.......

"Congrats @wemasepetu on your award for 'Best & Loved' Actress 2015. You deserve it. #DayAfterDeathour movie together should take you another notch higher. Thanks for trusting me. #HatsOff4U#TheYoungGodFather #TheEntrepreneur#TheVanVickerBrand"

DiamondP latnumz "Earlier Yesterday, from Mwanza to Dar...She was in Mwanza tho, ila kisirisiri"

$
0
0

"Lookin good....You guys have many bags though. .@zarithebosslady ....@diamondplatnumz .....Stay safe..stay strong....Stay drunk in love....Blessings blessings upon you....May God purify the hearts of haters..It scares the way the people hate goshhhh! !!

Sikiliza na Download Wimbo Mkali kutoka kwa Mo Music Unaitwa Nitazoea Kupitia Rubega.com

Nampenda sana Wema ila bado ana chuki na mimi – Kajala

$
0
0
Kajala Masanja amesema hadhani kama ni rahisi kuwa karibu tena na Wema Sepetu baada ya kugombana.

Kajala amekiambia kipindi cha The Sporah Show hivi karibuni kuwa bado anampenda Wema na kumheshimu.

“Mimi simchukii Wema, mimi nampenda Wema, kusema ningependa kurudisha urafiki na Wema inakuwa ngumu sana, kwa sababu yeye tayari anachuki na sijui ana chuki kiasi gani? Mimi nataka kusema ni mtu ambaye nampenda na nakaaga nasema namheshimu, ni mtu ambaye alinisaidia,” alisema Kajala.

Pia Kajala amekanusha kutembea na mpenzi wa zamani wa rafiki yake huyo hali iliyozua ugomvi baina yao na kusababisha mpaka sasa kutoelewana.

Mara Nyingine Awashukuru Wema na Petitman na Kufungua Milango ya Urafiki Tena

$
0
0
Binadamu tuliumbwa kuishi katika misingi ya ubinadamu na sio unyama kama waishivyo wanyama wa porini leo naomba kusema kutoka moyoni mwangu.. Najua kabisa nina wazazi wangu ndugu zangu na zaidi sana Mungu wangu ila kuna watu mpaka nakufa kamwe sintowasahau katika kuta za moyo wangu katika kipindi changu kigumu nilichopitia mlikuwa nembo namboni kubwa katika kuokoa maisha yangu...

Napenda kusema kuwa hata kwa haya yote tunayopitia bado ni madogo sana kuficha thamani yenu mliyoijenga juu yangu.

Nakumbuka sana mlipojitoa kwa ajili yangu mlipojinyima kwa ajili yangu mlipopigana kwa ajili yangu,mlivyofedheheka kwa ajili yangu yote hayo nayakumbuka na namshukuruu mungu kwani naona kabisa mliletwa duniani kwa sababu nyingi na moja ya sababu ilikuwa kuniokoa katika kipindi kigumu katika maisha yangu.

Leo hii tarehe 25.5.2015 napenda kusema kwa umma na zaidi kwa Mungu wangu kuwa nawathamini nawapenda na nashukuruuu sana kwa yote mliyofanya juu yangu.

Nawaombea kwa Mungu muendelee na moyo huo huo kwani naamini kuna wengi bado wanawategemea ili kukomboa maisha yao kwa wakati aliyopanga mungu

Hata kitabu cha dini kilisema kuwa "huwezi kumpenda Mungu usiyemuona wakati unamchukia ndugu yako unayemuona" najua siku moja tutaishi kama zamani.. Ahsanteni

Kajala ameandika hayo kwenye ukursa wake kwenye mtandao picha wa Instagram mara baada ya kuweka picha hizo hapo juu ya Wema Sepetu na ya Petitman.

Michango ya wengi kwenye andiko hili, wamewataka Wema na Kajala muda umefika sasa wayamalize.

Mengi akomalia Ikulu Kuhusu Kauli zinazoongeza Hofu ya Usalama wa Maisha yake

$
0
0
MWENYEKITI wa makampuni ya IPP, Regnald Mengi ameendelea kung’ang’ania kuwa, kauli zinazotoka Ofisi ya Rais Ikulu, zinazidi kumpa wasiwasi na hofu kubwa katika maisha yake. Anaandika Sarafina Lidwino

Mengi ameeleza wasiwasi huo leo wakati akizungumza na wanahabari ofisini kwake, na kueleza masikitiko yake juu ya kauli za dharau na dhihaka zilizotolewa na Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais-Ikulu, Salva Rweyemamu.

Mengi amesema kuwa, Aprili 17 mwaka huu, alizungumza na waandishi juu ya hofu yake, baada ya kupata habari kutoka kwenye gazeti la Taifa Imara la Machi 23 mwaka huu.
Habari hiyo iliosema, “Zitto Kabwe amchongea Mengi kwa Kikwete kwamba ndiye kinara wa kuihujumu Serikali yake.”

Mengi ameongeza “habari hiyo iliendelea kusema kwamba, nimeapa kumshuhgulikia Rais Jakaya Kikwete kwa nguvu zangu zote amalizapo muda wake wa urais, na kwamba Rais aliapa kupambana na mimi.

Amesema kauli hizo dhidi yake zilimshtua sana, na kwamba yeye hakuzitoa, hivyo kauli ya Kikwete ya kutaka kupamba naye ilizidi kumpa hofu ya usalama wa maisha yake.
Kutokana na mwingiliano wa kauli hizo, pia nililaumu sana Kurugenzi ya Mawasiliano- Ikulu na Idara ya Habari Maelezo kwa kukaa kimya zaidi ya wiki tatu bila kutoa ufafanuzi wowote katika jambo hili linalomhusu Rais na kuacha habari hizo kusambaa,” ameeleza Mengi.
Amedai kuwa, katika majibu ya Rweyemamu, alisema “Rais hakuwahi kuwa na mawasiliano yoyote na Zitto Kabwe kama ilivyoelezwa.”

“Hivyo, katika majibu yake Rweyemamu, alidai kuwa, hakufanya lolote eti kutokana na kuwa na majukumu mengi na alipuuza habari hizo kwa sababu aliziona ni jambo dogo na ni la upuuzi,” ameeleza Mengi.
Kwamba Rweyemamu kwa jeuri, aliongeza kuwa, alimshangaa sana kwa kutokutoa taarifa latika kituo chochote cha polisi kuhusu hofu ya maisha yake.
Kauli hizo, zinaongeza hofu ya usalama wa maisha yan
gu. Jambo hilo sio dogo la kupuuzwa kama linavyodaiwa. Rweyemamu hakutumia busara katika majibu yake, kutokana na kiti chake na heshima aliyonayo, alipaswa kutoa kauli nzuri na sio kuzidi kunipa hofu.
Na kwa upande wa Rais, mimi sina ugomvi naye na ninaamini yeye pia hana tatizo na mimi ila kauli za huyo mtu ndizo zinanipa shida,” amesema.

BET walitulipa milioni 46 kwa kucheza video ya Diamond kwa siku 4 tu – Babu Tale

$
0
0


Amini usiamini Diamond Platnmuz alifaidika mara mbili baada ya video yake kuchezwa na kituo kikubwa cha runinga cha Marekani, Black Entertainment Television (BET) mwaka jana.

Faida ya kwanza ni yeye kama msanii wa Bongo flevah kupata nafasi ya video yake kuchezwa na kituo hicho kikubwa cha Marekani, na faida ya pili ni kulipwa pesa nyingi kwa video yake kuoneshwa kupitia kituo hicho.

Meneja wa Diamond, Babu Tale amesema kuwa BET iliwalipa shilingi za kitanzania milioni 46 kwa video ya Diamond kuchezwa kwa siku nne tu na kituo hicho.

kwenye siku nne tukalipwa milioni 46, siku nne kwasababu nyimbo yake imeonekana kwenye TV,”. Tale aliiambia Amplifaya ya Clouds FM.

Ameongeza kuwa BET walielekeza jinsi mgao wa pesa hiyo ulivyotakiwa kufanywa kwa wote waliohusika katika kazi hiyo.

lakini walituonesha hii hela inaenda kwa huyu hii hela inaenda kwa huyu, kwa producer, kwa director, kwa editor, ya msanii ilikuwa milioni 19 kitu kama hicho. Hatukua tumeamini, mimi nimetumiwa e-mail ebwana wasije kuwa matapeli wanataka kuhack wale, kuna hela yetu tufanye process watu watuwekee kwenye akaunti…kuchunguza file ya kuonesha ngoma imepigwa BET four days, media za wenzetu zinalipa vizuri.” alimaliza Tale.

Mwaka 2014 Diamond alitajwa kuwania tuzo za BET kwenye kipengele cha ‘Best International Act: Africa’ akiwa msanii pekee wa Afrika Mashariki, lakini hata hivyo Davido ndiye aliibuka mshindi wa kipengele hicho.

Bongo5

Zitto aandika mazito kuhusu CAG katika ukurasa wake wa facebook, soma hapa alichokisema

$
0
0
"Kumbukumbu zangu ( Machi 20, 2015)
"Mjadala mkali ulikuwa kuhusu mtiririko wa fedha kwenda kwa CAG. Sheria ya ukaguzi wa umma kifungu cha 41 na 44 kinataka PAC ikishapitisha Bajeti ya CAG kwa mashauriano na Waziri wa Fedha, Bajeti ile itolewe yote mara moja kwenda mfuko wa Ukaguzi kutoka mfuko Mkuu wa Hazina. Kutokana na upatikanaji wa Mapato ya Serikali PAC ilikubaliana na Serikali kutoa fedha mara 2 kwa mwaka. Nayo ikawa ngumu tukakubaliana mara 4 kwa mwaka. Nayo haikukutekelezwa, fedha zikawa zinatoka kwa wiki mbili mbili. Hali hii imeathiri sana utendaji wa ofisi ya CAG kiasi cha CAG kushindwa hata kununua tairi Mpya za gari yake ya kazi.
Baada ya mjadala mkali na umuhimu wa kutekeleza Sheria, PAC ilikubaliana na Waziri wa Fedha kutoa fedha za Bajeti ya CAG kwa miezi Sita Sita kwa kutoa 50% mwanzo wa mwaka wa Bajeti na 50% nyingine kila mwezi Januari.

Baada ya hapo tukajadiliana kuhusu Bajeti. Waziri wa Fedha aliomba Bajeti ibakie ile ile ya mwaka Jana wakati CAG kaomba nyongeza ya 21%. Waziri alijulisha kamati kuwa Bajeti ya mwaka 2015/16 kila wizara na idara Bajeti imekatwa kwa 19%, hivyo haitakuwa sawa kwa CAG kuongezewa. Waziri aliijulisha kamati kuwa katika Bajeti inayokuja Serikali inataka kujitegemea kwa 100%, bila misaada ya wafadhili. Ndio maana kuna punguzo la Bajeti.

PAC ilijenga hoja kwamba CAG anaanza ukaguzi wa mapato ( revenue audit ) na ukaguzi wa mikataba ya Gesi, Mafuta na Madini hivyo kwa mawanda mapya lazima Bajeti iongezeke. Baada ya mjadala tukakubaliana Bajeti ya CAG kupanda kwa 8% kutoka tshs 86 bilioni mpaka tshs 94 bilioni".
Leo ninasoma vitabu vya Bajeti ya Serikali nakuta Ofisi ya CAG imepunguziwa Bajeti chini ya kiwango cha Bajeti ya Mwaka jana. Kinyume na Sheria. Kinyume standadi za kidunia kuhusu Uhuru wa Ofisi ya Ukaguzi ya Taifa. Kisa? Kuibuliwa kwa hoja za ukaguzi? Impunity? Hili lisikubalike aslani. Mwananchi Communications Ltd The Citizen JamiiForums simamieni hili. Ofisi ya CAG ndio jicho la Watanzania. Hata kama yanayoripotiwa hayafanyiwi kazi, tujue tu. Ipo siku Wananchi wataamka na kufanyia kazi. Cloudsfm Radio EATV EFM"
Zitto Kabwe.

Lowassa “aanza vita” na Kikwete, Adai Sakata la Richmond Lilipikwa Kumchafua

$
0
0
WAZIRI Mkuu aliyejiuzulu kwa kashfa ya Richmond mwaka 2008, Edward Lowassa ameanza safari ya kujiimarisha kisiasa kuelekea mbio za urais kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), akiwashambulia waziwazi viongozi wenzake, akiwemo Mwenyekiti, Jakaya Kikwete…
Lowassa ambaye alikuwa msaidizi wa Rais Kikwete kwa miaka miwili kama msimamizi wa shughuli za Serikali, amepingana na bosi wake akisema alikosea kuanza na kilimo kwanza na kuweka elimu kando.

Kauli ya Lowassa inakinzana na utaratibu wa CCM unaowataka viongozi kupingana au kukosoana kupitia vikao badala ya kufanya hivyo hadharani, hatua inayotafsiriwa kama kudhoofisha chama.
Badala yake, Lowassa ametamba kuwa, akiwa rais ataanza kushughulika na elimu kama lengo kubwa na sio kilimo kwanza cha serikali ya Kikwete.
Vigogo wengine wa CCM aliowashambulia ni aliyekuwa Spika wa Bunge la Tisa, Samuel Sitta na Dk. Harrison Mwakyembe, aliyeongoza Kamati teule, akisema wawili hao walipika ripoti ya kashfa hiyo ili kumdhalilisha.

Lowassa na makada wenzake watano, Fredrick Sumaye, Steven Wassira, Bernard Membe, January Makamba na William Ngeleja, waliondolewa kifungoni Mei 23 mwaka huu, baada ya kufungiwa kwa mwaka mmoja kwa tuhuma za kuanza mchakato mapema ndani ya chama.
Katika kile kilichoonekana kama kujibu mapigo ya tuhuma za ufisadi dhidi yake, Lowassa aliwaalika baadhi ya wahariri wachache kutoka Jukwaa la Wahariri nyumbani kwake mjini Dodoma leo, na kufafanua baadhi ya mambo kadhaa kupitia “wateule wake” hao.
Akizungumzia tuhuma za zabuni tata ya Richmond Development LLC, Lowassa amesema “sihusiki na lolote kuhusu sakata hilo na ndio sababu hata Kamati ya Mwakyembe haikunihoji.”
Amesisitiza kuwa, cheo cha uwaziri mkuu ndicho kilikuwa lengo la kamati ya Dk. Mwakyembe na Spika Sitta kumshughulikia.

“Hicho sio kikwazo kwangu katika kuingia Ikulu, kwani sakata la Richmond lilipikwa kunichafua. Nimechukua muda mrefu kuzungumzia hili la Richmond na nitalisema zaidi Arusha wikendi hii,” amesema Lowassa ambaye atatangaza nia ya kuwania urais siku hiyo.
Kuhusu kutumia makundi ya kumshawishi kutangaza nia, Lowassa amesema “naamini kila mtangaza nia ana makundi ya kumuunga mkono.”
Mkutano wake huo, mbali na wahariri pia ulihudhuriwa na Nazir Karamagi-mmoja wa mawaziri waliojiuzulu pamoja na Lowassa mwaka 2008 kwa kashfa hiyo, wabunge Peter Serukamba, Diana Chilolo.
Walikuwepo pia wafuasi wake wengine, Hussein Bashe, baadhi ya waliokuwa wakuu wa wilaya walioenguliwa kama Elibariki Kingu (Igunga) na aliyekuwa Mkurugenzi wa HakiElimu, Elizabeti Misoki.

Misoki ametangazwa rasmi kuwa mkurugenzi wa mahusiano na mawasiliano katika timu ya kampeni ya Lowassa. Amehoji kwani akina Karamagi wana tatizo gani na kwani wao sio binadamu?
Kuhusu mabilioni ya fedha anazogawa kwa baadhi ya makundi, Lowassa anasema anapata michango ya rafiki zake na kwamba ataendelea kupokea michango hiyo wakati wote wa harakati zake na haina madhara yotote.

“Sitahama CCM. Asiyenitaka ndiye aondoke kwenye chama kwani mimi nina uhakika wa kupata nafasi ya kuwania urais,” amesema.
Lowassa amefafanua kuwa, hatalipa kisasi kwa lolote lililomtokea katika siasa kwani, amemwachia Mungu kwa vile yeye ni mcha Mungu.

Ametamba kuwa Arusha itawaka moto tarehe 30 mwezi huu, na kuwataka Watanzania kutega sikio kwani ataanika kila jambo kuhusu mustakabali wa nchi hii na mipango yake ya kuiinua nchi kiuchumi katika miaka kumi ijayo.
Viewing all 104803 articles
Browse latest View live




Latest Images