Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104796 articles
Browse latest View live

MARKSON BEAUTY PRODUCTS Inakuletea Dawa za Kurefusha Nywele, Kukuza Makalio, Kupunguza Tumbo, Kung'arisha Ngozi na Zingine Nyingi

$
0
0


MARKSON BEAUTY PRODUCTS 2015
Je Unapenda Kuongeza Hips, Makalio, Urefu na Unene wa uume na Nguvu za Kiume bila Madhara? Markson Beuty tunakupatia hizo na Zingine nyingi zenye matokeo ya haraka na uhakika zisizo na kemikali wala madhara ..Tuna uzoefu wa Miaka 15 na Bidhaa zetu ni za mimea na Matunda na zimethibitishwa

1.Kurefusha nywele na kuzuia kukatika ovyo @80,000/=
2.Kutengeneza shepu (hips na makalio) @100,000/=. 
3.Kuwa mweupe na softi mwili mzima @80,000/=. 
4.Kuondoa mvi milele zisirudi @90,000/=. 
5.Kuongeza maumbile na nguvu za kiume kwa:-(1)Gely ya kupaka @80,000/=  (11)Vidonge maalum@90,000/=      (111)Mashine original ya Handsome up@200,000@/=     
6.Kupunguza unene na uzito wa mwili mzima @90,000/=.  
7.Kushepu maziwa na kuyasimamisha @70,000/=   
8.Kuongeza unene na uzito wa mwili mzima @80,000/=  
9.Kupunguza tumbo na nyama za pembeni kwa:- (1)Dawa @80,000/=  (11)Mkanda wa kawaida @80,000/= (111)Mkanda wa umeme (Micro computer belt) @200,000/=   
10.Kushepu miguu na kuwa minene (Chupa ya bia) @70,000/=    
11.Kuondoa mipasuko (Michirizi) mwilini @70,000/=                                
12.Kubana Uke na Kuongeza Hamu ya Tendo la Ndoa kwa Mwanamke @80,000/=

 

Wasiliana nasi kwa no (+255 ) 0767-447444 na 0714335378.


NB: Hakikisha unapata Risiti yenye muhuri halisi wa Markson Beauty na Garantii ili kuhakikisha kufanikiwa Kwako.



Mchezaji Lionel Messi Amulikwa na Kitu cha Hatari Akiwa Uwanjani..Check Picha za Tukio zima Hapa

$
0
0
Messi na timu yake ya taifa wamefanikiwa kuingia nusu fainali ya Copa America hayo tuliyajua baada ya mechi kuisha, tuliyoyajua leo ni kuhusu Messi kumulikwa na kitu cha kijani ambacho kitajwa kama “green laser” ambapo miale hiyo ilipiga sehemu ya mbele ya kichwa chake.

Wachambuzi wanasema hiyo miale inaweza kutoka kwenye kitu kinaitwa laser pen ambapo lengo lao ni kumulika usoni Messi na kumtoa kwenye mchezo au kumzozoa tu usoni. Kwenye historia inasemekana sio mara ya kwanza kwa Messi kufanyiwa hivyo, hata Ulaya kuna wahuni wanaofanyaga hivyo.

Umbo la laser pen ni kama peni ya kawaida kwa hiyo hata sehemu ya kusachiwa sio rahisi kujua ukubwa wa matumizi zaidi ya pen hiyo. Ushahidi wa miale hiyo umeonekana kwenye picha zilitoka mtandao hivi sasa

Kauli ya Mwigizaji Steve Nyerere Baada ya Wadau Kudai Amekurupuka Kufuata Mkumbo Kutangaza Kugombea UBUNGE Kinondoni

$
0
0
Staa wa Bongo Movies na aliyekuwa mwenyekiti wa Bongo Movie Unit, Steve Mengere ‘Steve Nyerere’ ambaye wiki iliyopita alitangaza niua yake ya kugombe ubunge mwaka huu wa uchaguzi amedai kua hajakurupuka kuutaka ubunge kupitia jimbo la Kinondoni na kuwa ataendeleza sanaa hata akiwa mbunge.

Steve Nyerere Amesema Haya.’Kwanza ninataka kuwahakikishia watanzania sijakurupuka, nimekuwa  mwanachama wa chama cha Mapinduzi  umoja wa vijana almost miaka 25 na sasa hivi nina miaka 29 naelekea 30 lakini vilevile nimekuwa kamanda wa vijana miaka 10 tawi la bwani kinondoni, nimekuwa mwamasishaji  wa chama cha mapinduzi kitaifa kwa muda wa miaka 10

Kwa hiyo nataka kusema sijakurupuka na wala sijatamkia sifa kwasababu labda nimeona mtu Fulani amegombea na mimi basi tu  nigombee hapana  nimeona  katika wilaya yangu ya  kinondoni kuna matatizo kadhaa  nani anaweza kuyatetea hayo matatiizo  basi mimi ndio nitakuwa mtetezi wa wilaya wa Kinondoni pamoja na matatizo ya wasanii wetu, kuhusu kazi zangu za filamu nitakuwa nafanya kama kawaida huku nikiwa natumikia kazi za Bungeni’alisema

Hii Hapa Taarifa Kamili ya ‘Magaidi’ Morogoro na Picha za Vitu Walivyokamatwa Navyo

$
0
0
Ripoti hii ni ya ITV June 27 2015 kutoka Morogoro inahusu watu watatu kufariki katika mapambano na Polisi, huku wawili kati yao wakihisiwa kuwa na uhusiano na kundi la kigaidi la Al Shabaab.

Breaking News nyingine kuhusu tukio hilihili iliyoripotiwa na Gazeti la Mwananchi inahusu watu sita kukamatwa na wengine 50 wanatafutwa, walikutwa wakiwa na sare za majeshi pamoja na silaha kama majambia kwenye msitu Mvomero.

Kwenye taarifa iliyofatia kutoka Mwananchi, imesema Mkulima Cassian Peter amefariki mchana wa June 27 2015 kwenye Hospitali ya Bwagala ambapo Polisi mmoja amelazwa na hii ni baada ya kujeruhiwa na hao watuhumiwa wa Ugaidi kabla hawajakamatwa


Mtangazaji na Mwandishi wa habari wa Radio One Maulid Kambaya kwenye page yake ya Facebook alipost picha za walivyokamatwa navyo ‘Magaidi’ hawa



Mafuriko Ya Lowassa Yatua Jijini Dar......Kingunge Amwaga Wino Hadharani Kumdhamini, WanaCCM 212,150 Wajitokeza Kumdhamini

$
0
0
WAZIRI  Mkuu wa zamani, Edward Ngoyai Lowassa amepata udhamini wa kishindo katika mkutano uliofanyika jana  katika ofisi kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Kinondoni.

Lowassa alipata udhamini huo baada ya wanachama kujitokeza katika ofisi za Makao Makuu ya CCM ya Wilaya ya Kinondoni, Mkwajuni, Dar, ambapo alipata zaidi ya wadhamini  212,150 huku akisema Dar  imevunja  rekodi  ya mikoa yote ya Tanzania.

Akizungumza na maelfu ya wananchi waliofika katika mkutano huo Lowassa alisema kuwa amefurahishwa na watu waliojitokeza kumdhamini kwa kishindo kikubwa na hivyo hatavunjwa moyo  na maneno ya watu yanayovumishwa  kuwa anawapatia fedha ili wafike kwenye mkutano wake .

Lowassa aliongeza kuwa anawaomba Watanzania wampe ridhaa ya kuwa rais wao kwani atahakikisha mianya yote ya rushwa na utendaji mbovu  wa kusuasua anausimamia kwa haki na weredi na ndani ya miezi sita tayari matokeo yatakuwa yameonekana.

“Nawaombeni wananchi mnipeni ridhaa ya kuingia ikulu yaani nitahakikisha mianya yote ya rushwa na ufisadi nautokomeza, muyapuuze maneno na minong’ono ya watu kutaka kunichafua,” alisema.

Mwanasiasa Mkongwe hapa nchini, Mzee Kingunge Ngombale Mwiru akisani fomu ya udhamini mbele ya Mtangaza nia ya kuwania Urais wa Tanzania, Mh. Edward Lowassa ikiwa ni ishara ya kumuunga mkono mgombea huyo.

Zoezi hili lilifanyika jana jioni ya Juni 27, 2015 kwenye Ofisi za CCM Wilaya ya Kinondoni, Mkwajuni Jijini Dar ambapo Lowassa  alipata  jumla  ya  Wadhamni 212, 150 na kuifanya Dar es salaam kuwa Mkoa wa kwanza kuwa na idadi kubwa ya WanaCCM waliomdhamini .

Matokeo ya Mechi ya YANGA na Timu ya SPORTS CLUB VILLA Haya Hapa ....

$
0
0
Mabingwa wa ligi kuu Tanzania bara timu ya Yanga wameshindwa kutamba mbele mabingwa wa kombe la FA nchini Uganda timu ya Sports Club Villa baada ya mabingwa hao kulazimishwa sare ya bila kufungana kwenye mchezo wa kirafiki wa kimataifa wa hisani ulioandaliwa na taasisi ya Numbani Kwanza kwa ajili ya kuchangia watoto wanaoishi kwenye mazingira hatarishi uliomalizika muda mfupi kwenye uwanja wa Taifa.

Winga wa Yanga na timu ya Taifa Simon Msuva alikosa penati baada ya yeye mwenyewe Msuva kufanyiwa madhambi na golikipa wa Sports Club Villa wakati alipopata nafasi ya kwenda kufunga na mwamuzi wa mchezo huo kuamuru ipigwe penati lakini penati hiyo iliota mbawa baada ya Msuva kuipaisha juu.

Mchezo huo kwa upande wa Yanga ulikuwa ni sehehemu ya maandalizi kwa ajili ya michuano ya Kagame ambayo inatarajia kuanza kutimua umbi mapema mwa mwezi Julai ikishirikisha vilabu bingwa vya Afrika Mashariki na Kati.

Kipindi cha kwanza kilishuhudiwa kikiwa na upinzani mkali kwa timu zote mbili kufanya mashambulizi kadhaa kwa kupokezana lakini hakuna timu iliyoweza kuweka mpira wavuni kutokana na washambuliaji wa timu zote mbili kushindwa kuzitumia vyema nafasi chache zilizopatikana.

Kipindi cha pili Yanga walifanya mabadiliko kwa kumtoa Malimi Busungu na nafai yake kuchukuliwa na Kpah Sherman wakati Pato Ngonyani aliingia kuchukua nafasi ya Nadir Haroub ‘Cannavaro’ na Msuva akaingia kumpokea Amis Tambwe lakini mabadiliko hayo hayakuisaidia Yanga kuweza kupata bao.

Wachezaji wapya waliosajiliwa na Yanga Deus Kaseke akitokea Mbeya City, Geofrey Mwashiuya aliyekuwa akikipiga Kimondo, na Malimi Busungu kutoka timu ya Mgambo JKT walipata nafasi ya kucheza kwenye mchezo huo na kuonesha viwango vizuri lakini Geofrey Mwashiuya alionekana kukonga nyoyo za mashabiki wengi Yanga waliojitokeza kushuhudia pambano hilo.

Wema Sepetu Kubadili Wanaume Kila Mara Chanzo ni Hichi Hapa

$
0
0
IMEBAINIKA! Kufuatia tabia yake ya kubadili wanaume, mrembo asiyeishiwa matukio Bongo, Wema Isaac Sepetu imefahamika kuwa chanzo cha yote ni kusumbuliwa na ugonjwa ujulikanao kitaalamu kwa jina la Sex Maniac.

Wema Sepetu na Diamond.

Akizungumza na gazeti hili, mtaalam wa masuala ya utabiri na nyota, Maalim Hassan Yahya alisema kwamba suala la Wema kubadili wanaume kila mara si kulogwa bali anasumbuliwa na ugonjwa huo ambao mtu akiwa nao kila wakati anawaza mapenzi na raha yake ni kufanya tendo la ndoa.

Wema Sepetu na Chaz Baba.

Maalim alidadavua kwamba, ugonjwa huo hautibiwa na dawa za hospitali kama magonjwa mengine ila kama mtu anahitaji kuondokana na tatizo hilo anatakiwa kumtafuta mwanasaikolojia ambaye mara kwa mara atakuwa anamjenga kwa ushauri hadi atakapoona amekuwa sawa kwa kuacha kuwaza mambo hayo.

KanumbaWema Sepetu na Steven Kanumba.

“Watu wanashindwa kuelewa, unakuta mtu anakuwa na wanaume wengi, anabadili kila mara alafu watu wanamsema bila kujua kwamba ni ugonjwa ambao mtu anajikuta akipenda ngono kila wakati na kwenye mawazo yake anatawaliwa na kutamani tendo la ndoa tu.

Wema Sepetu  na Bob Juniour.

“Lakini wapo wengine wanabadili mabwana maarufu ili nao wawe maarufu,” alisema Maalim.

Wema Sepetu na Jumbe.

Wema aliwahi kutoka kimapenzi na wanaume tofauti akiwemo, Herry Samir ‘Mr. Blue’, Khaleed Mohamed ‘TID’, marehemu Steven Kanumba, Yusuf Jumbe, Tuesday Kihangala ‘Mr Chuz’, Charles Gabriel ‘Chaz Baba’, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’, CK na Nagari Kombo.

Jitihada za kumpata Wema ili kuzungumzia hali hiyo ziligonga mwamba baada ya simu yake kutokuwa hewani na kukosekana nyumbani kwake hivyo jitihada zinaendelea.

Source:GPL

Faiza Ally: Mimi ni wa Nusu Uchi Toka Nizaliwe

$
0
0
Imelda Mtema
MREMBO aliyewahi kuwa na uhusiano na Mbunge wa Mbeya Mjini, Joseph Mbilinyi ‘Sugu’, Faiza Ally, mwanzoni mwa wiki hii aliamriwa na Mahakama ya Manzese/Sinza, amkabidhi mtoto kwa baba yake (Sugu) ambaye aliiomba mahakama hiyo imruhusu apewe mtoto huyo kwa madai kuwa mama yake huyo anamlea kinyume na maadili.



Sugu aliileza mahakama kuwa mrembo huyo hana maadili kwani amekuwa akijipiga na kumpiga picha za nusu utupu mtoto na kuziweka mitandaoni kitu ambacho aliamini kitamsababishia akose maadili.

Mara baada ya hukumu hiyo kutolewa, Mikito Nusunusu ilimtafuta Faiza na kutaka kujua ameipokeaje pamoja na historia nzima ya yeye kukutana na mzazi mwenzake huyo, shuka na mtiririko wa maswali na majibu:

Alianza lini kuvaa mavazi ya nusu utupu?

“Jamani haya mavazi wanayosema navaa uchi sijaanza kuvaa leo ni tangu utotoni, hakuna ambaye hajui kitu hicho kwa kuwa hata mama yangu alikuwa akinishonea sketi ya shule ndefu mimi naenda kwa fundi kuikata.”

Alikutana vipi na Sugu?

“Nilikutana naye kwenye Mtandao wa Facebook na alikuwa akiniona nikiwa katika mavazi hayohayo ambayo yeye anadai ni ya kuvunja maadili na alinitongoza nakumbuka nilikuwa Zanzibar kwenye hoteli moja inaitwa Lagema, ambapo nilitupia picha zangu zilezile ndipo alipovutiwa nazo akarusha nyavu.”


Hakumpa masharti ya nguo anazopenda?

“Yeye aliniambia kuwa kama ‘package’ amepata iliyokamilika kuanzia mavazi yangu ninayovaa mpaka ‘tatoo’ nilizochora hivyo alinikubali kwa jinsi nilivyo.”

Anazungumziaje kuvaa nguo fupi?

“Jamani ninachoamini mimi nguo siyo kila kitu katika maisha ya mtu, mimi ni mama wa tofauti kwa mtoto wangu hilo hata Sugu mwenyewe analijua kabisa, nimeanza kumfundisha mtoto wangu kusoma kabla hata hajaanza shule na si mtu wa kujirusha kama wanavyofikiria.”


Kumbe vimini vilianzia kwenye filamu

“Kabla sijawa na Sugu, nilikuwa na filamu yangu inaitwa Jesca, nafikiri ndiyo muigizaji wa kwanza kuvaa bikini na kutembea hadharani lakini yote hiyo ni kutokana na mazoea, hata Sugu aliiona filamu hiyo, hakuona kama ni ukosefu wa maadili.”

Alitinga ‘swimming’ akiwa na mama mkwe

“Nakumbuka mimi na mama yake Sugu tulishawahi kwenda ufukweni nikiwa na mtoto wangu na nilikuwa nimevaa nguo za kuogelea na wala haikuwa tatizo na siyo mama hata nikiwa naye mara nyingi navaa hivyo, nashangaa sasa anasema navunja maadili.”

Sugu alimkuta akiwa na maisha mazuri?


“Wakati nimeanza kuwa na Sugu hakuwa hata na kibanda alikuwa amepanga na nilimuambia kuwa hadhi yake hapaswi kuwa hivyo, tulinunua kiwanja na tukajenga nyumba Mbeya tena kwa kuisimamia huku akikiri kuwa alimshukuru Mungu kunikutanisha naye.”

Unawaambia nini Watanzania?

“Nawaomba sana Watanzania wasitumie nguo niliyovaa siku ile (kwenye Tuzo za Kili 2015) iliyoniacha wazi kwa bahati mbaya kuwa fimbo ya kunichapia, nina vitu vingi sana nimefanya kwa jamii yangu, kama kuwatembelea wagonjwa, kufanya usafi mahospitalini na hata kutembelea watoto yatima mbona hivyo havionekani?”

Vipi maisha yake bila Sasha?


“Bila Sasha kwangu hakuna maisha kabisa ni bora kufa kuliko kukaa mbali na mtoto wangu kwa kuwa ndiye kila kitu kwangu na wala siwezi kupata usingizi mpaka mtoto wangu atakaporudi mikononi mwangu, nimeshaanza process za kukata rufaa.”

Kumbe sugu alimtambulisha Bilicanas

“Sugu alinitambulisha katika Ukumbi wa Bilicanas tena mbele ya kadamnasi kuwa mimi ni mchumba wake tena nikiwa nimevaa nguo fupi kabisa, hapo pia hakuniona?”

Nini chanzo cha kugombana?

“Wala hakuna ugomvi mkubwa, nafikiri tu upendo ulianza kupungua kwa kuwa niliondoka Mbeya kwenda kumsaidia mama yangu kuhama, yeye alikuwa hataki niondoke hiyo ndiyo sababu kubwa.”

TB Joshua reacts to gay law in USA

$
0
0
Various reactions have come in the wake of America formally legalising gay marriage across the entirety of its borders but one of the most unusual has sprung from a popular Nigerian cleric.

After the historic announcement, T.B. Joshua tweeted a YouTube video showing a young man allegedly receiving ‘deliverance’ from a ‘homosexual demon’.


The clip titled, ‘Deliverance From Homosexual Demon’ shows a Nigerian from Imo State who identified himself as ‘Tedus’ receiving prayer at the church of T.B. Joshua in Lagos, Nigeria.
“I made him gay; I made him love men,” the young man says after being questioned by one of Joshua’s ministers, the clip clarifying that it was an ‘evil spirit’ speaking, which was allegedly behind his homosexual tendencies. Tedus is subsequently ‘delivered’ and later shares his experiences about how the ‘devil’ of homosexuality had possessed him.

He narrated how, upon his return from a business trip in Asia, he had lodged in a hotel in Kenya where he met some male friends who suggested they go for a swim in the hotel pool. “After swimming, I went back to my room and had a dream,” Tedus recounted. “I dreamt where I saw myself swimming in the same pool with naked men.

When I woke up, I felt as if something entered into me. I started having passion for men.” Upon returning to Cameroon where he was based, Tedus ‘sacked’ his fiancé without any explanation. “I had no passion for her anymore – no more affection. She was astonished and asked so many questions which I couldn’t abswered. On the internet, I discovered so many things on gay websites and began downloading gay pornography. That’s how it started.”

According to Tedus, he saw his newfound homosexual lifestyle as ‘normal’ until his pastor in the church where he worked as a translator called him aside privately. “He told me that I had to go to Nigeria to The SCOAN and that I needed deliverance.” Tedus reluctantly agreed. After making the journey in December 2013, when the time arrived for people to receive prayer in the church service, he described a sense of anger welling within him as one of Joshua’s pastors approached. “When he prayed for me, I lost control,” he described.

“I knew I was talking but I never knew what I was saying.” Since receiving prayer, Tedus testified that all homosexual feelings have left him. “Those feelings for men are no longer there; I have real passion for the opposite sex. I couldn’t control the former passion.” The clip then jumps to almost one year later where Tedus returns, this time with a young lady whom he introduced as his fiancé. “The Bible says that a man ought to be with a woman.

After my deliverance, I travelled to Imo State and there I met this wonderful lady and proposed to her,” he said, with a large smile, testifying that is life has changed ‘tremendously’ since receiving prayer. “My advice is that if you come across somebody that may be having the same problem, you shouldn’t criticise them but rather pray for them,” he said. “People just believe it’s a normal thing; it’s not just ordinary. There is a force or spirit behind it. The only way out of this is deliverance. It is like a virus. Once it gets into you, it is only deliverance from Jesus Christ that can get you out of it.” In his comments, T.B. Joshua quoted Matthew 7:1, stating that Christians should ‘talk salvation, not condemnation’. “God hates sin, not sinners,” he insisted.

“When I say, 'Do not judge so that you will not be judged', I mean we should hate sin, not the sinner because sinners can change. If you have killed a sinner by judging him, there will be no opportunity for change. Sinners can be delivered. We should hate the act, not the people because our battle is not against flesh and blood but against the 'spirit beings' that cause all these acts.”

He then went further to clarify his stance: “The Bible is my standard. If my parents were one, I would not have been given birth to.”

Article by Ihechukwu Njoku

Kumbe Zari Anajua Kiswahili ..Mambo Yamfika Shingoni Soma Alivyoamua Kuwapa VIDONGE Wanaomsema Vibaya.....

$
0
0
Shemeji yetu Zari ambaye ni mrembo kutoka Uganda ambaye toka amekua mapenzini na Mtanzania staa wa bongofleva Diamond amekua akipokea comments tofautitofauti kwenye page yake ya Instagram, June 28 2015 ameamua kuyaandika haya tena mengine kwa kutumia lugha ya kiswahili baada ya kushindwa kuvumilia.

Waliomkasirisha ni wale wanaokosoa uvaaji wake na kuendelea kumfatilia ambapo alianza kwa kuandika >>>’Mnikome, maisha yangu yanakuhusu nini wewe, nayako hayanihusu mimi kabisa ata kidogo….oh sijui high heels, mara nguo imembana, sijui anapikia heels,pili pili hujakula wewe inaakuwashia nini? Mvae madera zenu mfunge mkanda mpite kimya kimya. Kwanini unastress????‘


Ameendelea kwa kuandika mengine kwa kiingereza na nitatafsiri kwa wino mwekundu>>> ‘HAYA NI MAISHA YANGU na sasa your all Gods’ judges now…. how many people do we know that wear hijab but have very dirty ugly hearts? (ni watu wangapi tunawajua wanavaa Hijab lakini mioyo yao sio misafi? ni wangapi wenu mnaigiza kuwa wasafi kwenye hizi siku 30 lakini miezi 11 iliyobaki ni waovu? )How many of you act so straight for these 30 days but the last 11 months your the worst monsters this world has ever seen’


Kwenye sentensi nyingine kaandika>>> ‘Now u wana come here and judge my faith by the dress???? (sasa mnakuja kujudge imani yangu kutokana na nguo? Allah bless all of you….atleast I ain’t acting snitchy, am being ME. And oh🙋, if you happen not to like what you see in ur news feed (my page) U always have 3 options, Block yourself, unfollow ama fast forward coz if your still following na you exercise your fingers kuwakya matusi page yangu, babe your just an obsessed fan if not a confused admirer dah majirani Habari nakazi mnayo……like I always say, no bad vibes from me. So stay blessed

Kingunge: Hatutakubali Jina la Lowassa likatwe CCM ‪Urais2015‬ - Adai Likikatwa "Patachimbika"

$
0
0
Kada maarufu wa CCM,mzee Kingunge, amesema hawatakubali kuona jina la Lowassa linakatwa.

-Atahadharisha uteuzi wagombea Urais CCM

-Si mchezo wa kuchezwa na kila mtu

-Lowassa atikisa Dar na kusema: Nikiteuliwa nitaunda serikali rafiki kwa masikini na matajiri

Mwanasiasa Mkongwe nchini, Kingunge Ngombale Mwiru akizungumza machache na WanaCCM wa Wilaya ya Kinondoni.

Wakati Chama Cha Mapinduzi (CCM), kikielekea katika hatua ya kuteua mgombea urais wa chama hicho, mwanasiasa mkongwe nchini, Kingunge Ngombale-Mwiru, amefyatuka na kusema urais ni hatima ya Watanzania hivyo lisifanywe mchezo kuwa mtu yeyote anaweza kuucheza.

Amesema si vizuri watu waliopewa vyeo ndani ya CCM kuendelea kukitumia chama kwa mambo yao binafsi.

"Kama wana mashaka chama hiki kina historia, vyema wakatutafuta watu ambao tupo, watu tunaojua mambo ya chama," alisema.

Alisema wanaofanya jitihada za kuunda mazingira ya kukitafutia chama kushindwa, wanataka historia ya CCM iishie katika awamu ya nne.

Kingunge ambaye alikuwa miongoni mwa wanachama waliomdhamini Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa, katika Wilaya ya Kinondoni, alisema yupo ndani ya chama hicho kwa miaka 60 sasa, ameona mengi ya mkoloni na Tanzania.

"Asilimia kubwa ya Watanzania ni maskini na chama chetu tangu mwanzo tulisema tutapambana na umasikini...Pamoja na mambo mazuri yaliyofanywa lakini sio mwisho, tunahitaji uongozi utakaotutoa katika umaskini na linawezekana hilo," alisema Kingunge.

Alisema ni mwiko kumhukumu mtu kabla ya vikao kwani haijawahi kufanywa hivyo mwaka 1995 na 2005, na hawatafanya hivyo mwaka huu
"Wakifanya hivyo tutakataa, tunataka mchakato ufuate taratibu zilizowekwa, nimemsikia kiongozi wetu mmoja alizungumzia katika Tv kuwa mtu hawezi kwenda kujinadi yeye binafsi bali chama ndio kinamnadi...Mimi nataka niseme kuna ngazi mbili; mwanachama anatakiwa kujinadi ndani ya chama na ndiyo tumefanya hivyo miaka yote kwa mujibu wa taratibu na ndivyo wanavyofanya kina Lowassa, anajinadi kwa wanachama," alisema.

Alisema baada ya mkutano mkuu wa kumpata mgombea, atanadiwa na chama hivyo si vizuri watu waliopewa vyeo kutumia chama kwa mambo yao binafsi.

"Katika utaratibu wetu tuna misingi ya kuamua na mwenyekiti wa chama chetu, Jakaya Kikwete, alitangaza yeye mwenyewe kwamba tutafute mgombea anayekubalika ndani na nje ya chama na ndio msimamo wa chama...CCM inamtafuta mtu anayekubalika ili kuleta ushindi ndani ya chama, wale wanaojitahidi kufanya hivyo kukitafutia chama kushindwa wanataka historia ya Chama Cha Mapinduzi iishie katika awamu ya nne," alitahadharisha.

Alisema suala la urais lisifanyiwe mizengwe, watu waulizwe wanamtaka nani na nani atakayewatatulia changamoto zao.

"Watu wenye busara wanafuatilia mambo yanavyoenda na wameona, wagombea wapo wengi, wenye macho wapo wengi na wanaona, hivyo watu watulize vichwa na kuamua ni nani watamchagua," alisema Kingunge.

Naye Mwenyekiti mstaafu wa CCM mkoa huo, Hemed Mkali, alisema Lowassa ndiyo Rais kwani anakubalika na wananchi wengi hivyo ni vyema viongozi wakaliangalia hilo.

"Kama wakipeleka kiatu cha polisi hawatakichagua hivyo CCM ikipeleka kiongozi ambaye hakubaliki watambue wananchi watamkataa,"alisema Mkali.

LOWASSA: NITAUNDA SERIKALI RAFIKI
Akizungumza baada ya kudhaminiwa na wanaCCM 212,150, jijini Dar es Salaam, Lowassa alisema endapo atateuliwa kuwa rais ataunda serikali ambayo ni rafiki kwa masikini na matajiri.

Alisema yeye ni rafiki wa wanyonge na anachukizwa na vitendo vya wamachinga na mama ntilie kufukuzwa ovyo.

"Siruhusiwi kusema maneno mengi lakini nawashukuru sana kwa kunidhamini hapa Dar es Salaam, udhamini wenu nyie ndio mnaoongoza katika nchi nzima kwa kunipatia wadhamini wengi, heshima mlionipa nitaitunza na kuienzi katika maisha yangu," alisema Lowassa.

"Tunaheshimu kazi zilizofanywa na waliotutangulia sisi tunachukua kijiti tu cha kuboresha nina uwezo na nia ya kubadilisha nchi hii...mwaka 1995 Mwalimu aliwaambia Watanzania wananchi wanayataka mabadiliko wakiyakosa ndani ya CCM watayatafuta nje ya CCM, mimi naamini ndani ya CCM tunaweza kuleta mabadiliko haya na mimi ndio nitakayeyaleta," alisema.

Alisema endapo atafanikiwa katika safari yake ya kusaka urais, moja ya ajenda itakuwa ni kuboresha miundombinu ya jiji hilo ndani ya miezi sita.

Alisema wakati akiwa Waziri Mkuu alijaribu kutafuta ufumbuzi wa suala hilo na kuongeza kuwa miundombinu hiyo itaenda sambamba na ujenzi wa nyumba milioni moja kila mwaka ili Dar es Salaam iwe ya kisasa.

Aidha, alisema akifanikiwa atahakikisha inatungwa sera kwa ajili ya ujenzi wa nyumba hizo ili jiji liwe na hadhi ya kipekee.

Alisema kutakuwapo na Waziri wa Dar es Salaam atakayeshughulikia matatizo ya jiji hilo ambapo akilala akiamka anawashughuliki bila kusubiri maamuzi yakatolewe Dodoma.

Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Ilala, Asaa Simba, alisema kudhaminiwa kwa Lowassa na wanachama wengi kunatokana na kukubalika kwa matendo na utendaji wake.

" WanaCCM Ilala wamefurahia sana kitendo cha wewe kutangaza kugombea na wamejitokeza wengi kukudhamini mpaka sasa wamekudhamini 44,799 hapa Ilala," alisema Simba.

Aidha alisema ishara ya wananchi ni kwamba CCM na wananchi wanamtaka Lowassa na tayari viongozi walishasema achaguliwe mtu anayekubalika na kwa sasa yeye ndiyo anayeonekana.

Naye Mbunge wa jimbo la Ilala, Mussa Zungu alisema Lowassa ndio mwarobaini wa matatizo ya wamachinga, mama ntilie na Bodaboda.

Naye Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Dar es Salaam alhaji Ramadhani Madabida, alisema ameonesha dhamira ya kutaka kuwatumikia Watanzania na moja ya sifa za kiongozi ni kuwa mstahimilivu na kuhilimili mikikimikiki.

Aidha alimfananisha Lowassa na Mtume Muhammad kwamba ni kiongozi mvumilivu.

Alipowasili Dar es Salaam, baadhi ya barabara zilifungwa ikiwamo barabara ya Nyerere kutokana na msafara mkubwa.

Mkeo/Girlfriend Katuma Picha zake za Uchi kwa Mwanaume

$
0
0
Wakuu naombeni ushauri... nimeishi na mke wangu wa ndoa kwa miaka kama 10 hivi sasa. Ila ndani ya muda huo ndani kumekuwa na migogoro ya hapa na pale ya kutoaminiana. Ila katika hali hiyo yeye ndiyo alikuwa ananishutumu mimi kuwa nina michepuko na yeye kujiona yupo innocent kama malaika. Lakini juzi kati hivi, katika pita pita yangu nikgundakuna mwanaume yupo nae busy ofisi kwake.

Nilipomuuliza akaribu kutoa utetezi ambao sikuridhika nao, nikaanza kumfutilia kimyakimya kenye simu zake n email zake. Siku ya siku nikkutana na chats kwenye whatsap baina yake na uyo mwanaume.. na mke wangu kimtumia huyo mwanume picha zake akiwa mtupu kigia kwenye kitanda chetu...

Hebu nipeni ushauri, maana hatua ya kwanza niliyoichukua ni kumrudisha kwa wakati natafakari maamuzi ya kudumu. Mpaka sasa yupo kwa mjomba wake..

Advice please guys!!!

Unaikumbuka Hii.....Barua ya Mfungwa Papii Kocha kwa Rais JK.

$
0
0
BARUA YA PAPII KOCHA
KWA RAIS
JAKAYA KIKWETE... KWA
WALE
AMBAO HAMJAISOMA HÍI
HAPA.
MF/NA: 836'04
Johnson Nguza
(Papii Kocha)
Gereza Kuu Ukonga
S.L.P 9091
Dar es Salaam
Mh. Rais Jamuhuri ya
Muungano
Tanzania
YAH: MAOMBI YA
KUPEWA MSAADA
(MSAMAHA) WA
KUFUTIWA ADHABU
YA KIFUNGO NILIYOPEWA
NA
MAHAKAMA YA HAKIMU
MKAZI
KISUTU.
Husika na somo hilo hapo
juu.
Mimi ni mfungwa katika
gereza
kuu Ukonga. Kwa heshma
na
taadhima na kwa
kutambua utu
na huruma yako ya
kiMUNGU
ulionayo dhidi ya
binadamu
wenzako pamoja na
mamlaka
uliokabidhiwa na Jamuhuri
ya
Muungano wa Tanzania.
Naanguka na kushika
miguu yako
mitukufu muheshimiwa
rais.
Nakuomba msaada
(msamaha)
kwako muheshimiwa
rais, kwa
njia hii ya maandishi
kusudi
niweze kuondolewa
adhabu ya
kifungo cha maisha
gerezani,niliyohukumiwa
na
mahakama tajwa hapo
juu.
Mh.Rais mimi
nimefungwa nikiwa
bado kijana mwenye umri
mdogo,
na ukweli kutoka moyoni
sikufanya kosa hilo. Si
mimi, baba
yangu Nguza wala ndugu
yangu
yeyote aliyefanya
kitendo kile.
Lakini wenye mamlaka
wakatuona tuna hatia na
kuamua
kuteketeza kizazi chetu
gerezani.
Natamani kiama ifike ili
mwenyezi
Mungu aweke wazi
ukweli wote
uliojificha nyuma ya pazia.
Mpaka
sasa natambua wazi
hatima
pamoja na dhamana ya
maisha
yangu ipo katika mikono
yako
mitukufu Mh. Rais
Naomba huruma yako
muheshimiwa Rais
maana mimi ni
mtoto wako ninaehitaji
huruma
yako wewe mzazi. Lakini
pia sisi
ni binadamu wenye nafsi
na miili
kama wengine.
Waliotumia mamlaka yao
kutuweka gerezani nao ni
binadamu pia, wenye miili
na
nafsi. Ipo siku nafsi zetu
zitapaswa kutoa hesabu
ya
tuliyoyafanya hapa
duniani.
wakati huo miili yetu
tunayoitumia
kunyanyasa
wanyonge itakuwa
imeoza
mavumbini.
Natumaini kauli yako ya
mwisho
ndio itakayoleta pumzi ya
uhai
nafsini mwangu.
Nakutakia kazi
njema, afya njema na
maisha
marefu.
Mungu akubariki.
Wako mtiifu
Mfungwa NO:836'04
JOHNSON
NGUZA (PAPII KOCHA)

Things That You Must Do on a First Date

$
0
0
 We all want our first dates to be perfect. But do you really how to impress a girl on a date without overdoing it?
When you hook up on a first date with a gorgeous girl, it is understandable that you want to go all out and please her, maybe by showing her that you’re manly and in command, or by behaving like a doormat.
But there may be a few things that could be overdone and you might just blow any opportunity of getting to the next date.
The Huggable Understanding Guy tells you where to draw the line between doing the right things, and overdoing them. Here are 8 tips for first dates that every man should know to have a successful first date

#1 ARE YOU IN CONTROL?
It’ss important to be in control and make those tough decisions, like calling the waiter, deciding where to go, etc. when you’re with your date.
It’s not easy when you get all groggy and drool while staring at this beautiful woman beside you.
But there may be times when your behavior borders rudeness and arrogance. Swearing, snapping your fingers to call waiters and bad behavior is just unacceptable. So if you want to hold on to the hope of getting a second date, then learn to be courteous and gentle, not just with her, but with everyone around.

#2 TRYING TOO HARD
You may have waited since you were in first grade before the both of you got together for this date. You may have marked this moment in your secret diary and stored it as one of the best moments of your life. But you know what? She doesn’t have to know that!
She’ss still contemplating and figuring is she’s having a good date. Don’t ruin the moment by droning on about how happy you are.
She knows that you’re happy, but don’t blow it all out, all through the date. Make her wonder if you’re having a great time. Don’t give in to the chase even before it begins!

#3 DON’T SHOW OFF YOUR INDEPENDENCE
You love hanging out and bonding with your guy friends, and every Friday in your calendar might be allotted for hanging out with the boys. But saying that out aloud on your first date could actually turn out bad for you.
You might think that it shows your independence and confidence, and that you also respect her space and are not going to be a clingy boyfriend, but it actually works otherwise. She might think that your life is just too rigid.
Or worse, it may seem like you’re trying to set boundary rules even before both of you get steady.It’ss almost like you’re already imposing a rule on her. What did you think, that she would like it?!

#4 ANSWERING PHONE CALLS
Now no one’s telling you not to pick up calls or that you have to leave your cell phone at home, but you should know how to use it well.
Make sure your calls are short, even if you have to answer them. Don’t cut her in mid sentence to answer the call. Wait until she’s done with her sentence, and then excuse yourself, if only for a moment.
Another way you can actually make her feel more special is by answering the call, only to tell the person that you’re with someone who’s very important to you, and whatever it is, you could talk about it the next day! You could also add a cheeky grin to stop you from appearing pompous.
Now why wouldn’t that make just about anyone beam with happiness?
To top that, you could hang up, and then say, ‘Sorry, that was Bill Gates and he’s just so annoying.’ You could just laugh off that little joke of yours, and show her that you can be humorous at the same time!

#5 BE TOO CONCERNED
Remember, you’re out with someone who’s matured enough to think and take care of herself. You can ask her occasionally ifshe’ss comfortable, or if she requires something.
But don’t keep popping the same question to her again and again. It can get really annoying. Just enjoy the conversation and relax. Don’t push your protective and concerned act too far.
And if you find yourself running out of things to talk about, stop asking her ifshe’ss having fun. Instead, be comfortable and speak about something else. Usually the four magic words – music, work, movies, and shopping, will take the conversation really far and you can also have a great time getting to know each other.
You could also use the awesome six conversation starters on a date to start great conversations. And another thing, if you both have something in common in these four words, then you can go ahead and book your next date’s dinner reservation.

#6 REVEAL TOO MUCH
It’s fun to be with this girl who’s so much fun to hang out with. And you want to prove that you’re a great guy to hang out with to her. So what do you do? You tell her about all your brave, silly and hilarious encounters.
You start off right from the first time you ripped your pants in first grade, and go on all the way to the latest incident. Stop! First of all, she doesn’t want to know all of that, even if she seems like she loves hearing all of that. And secondly, spare some loving and exploring for later.
You don’t want her to know everything about you on the first date itself, do you? Give her a chance to learn more about you by herself. Let there by mystery in your togetherness, and let her wonder what else you have in store for her, the next time you meet up.

#7 YOUR VIEW AND HERS
This is a very touchy situation to handle.It’ss obvious that both of you have different views about different things. Arguing about anything is a big turn off for a girl.
Anything about religion, politics, or moral issues should be avoided at any cost. And even if this does crop up, don’t tell her outright that you don’t want to talk about it, instead try sweeping the topic under the carpet without a big fuss.
Just answer the question in a vague and abrupt manner, and bring up something more exciting to talk about.
Do not be dominating about any of your views, or be very boisterous about voicing your opinions.
Even if she supports something you’re firmly against, just give a small laugh, and tell her ‘Well, that’s one thing that i’m not too sure of, because I’ve always felt the other way about that’ and complete the sentence saying, ‘but I obviously respect your view, and our difference in opinions.’ Anyways tell me about the last time you’ And change the topic as subtly as you can.

#8 GETTING DISTRACTED!
Well, this is really easy to fall for, and one of the things you have to pay the most attention to. When you’re out with a lady, she expects to be treated like one.
Don’t sit across the table and dream or doze off. Worse, don’t squint your eyes so that you can focus one eye on her, while the other eye ogles that girl with those never ending legs walking past you in short skirts. Pay a lot attention to her, and listen to what she has to say.
And for crying out loud, is she’s wearing something with a deep neckline, stop staring at her bosoms and trying to judge how much more cleavage is concealed! This is not the time, and definitely not the place either.

Concentrate on her face, and have a great conversation. Be attentive to her needs. If you see her glass of water half empty, have a waiter refill it. If she wonders what ‘a-la-carte’ means and if you can’t figure it out, then let the waiter help you with that. Basically don’t distract yourself with things that can be put on hold, and pay a lot of attention to her needs.
Staring at a girl’s cleavage is a big no-no too, unless, of course, you know the art of staring at a girl’s cleavage like a gentleman.

If you can pay attention to these little details, it’s more than definite that your first date would only take you further into the next, and then the next.
Every date has a potential to be a great one just as long as you remember the things you need to avoid on a first date, and remember the things you need to do. So go on, enjoy yourself. Have a perfect first date!

UWOYA: Aonya Wauza Sura Bongo Movie

$
0
0
Baada ya  kuwa  mrembo asiye  kifani  aliyefanikiwa  Zaidi kwenye  fani , Irene  Uwoya  ameonya  wasanii wa kike  wa  Filamu wanaochipukia  kutonaswa  na mtego wa kutumia uzuri wa Sura na Maumbo yao kujimaliza  kisanii.
Akizungumza na  gazeti la Nipashe Uwoya   alisema  wasanii  wengi  wa  sasa  wanashindwa kufanya  kazi  kwa  sababu  wanaona  kazi  hiyo  ni  sehemu  ya  kupatia  wapenzi  wa  kiume.


Alisema  wacheza  Filamu wa  kike  huwa  wanapenda  kujirahisisha  kwa  Wanaume  na  matokeo  yake  kushindwa  kutoka  kama ilivyo kwa  wengi  wa  waanzilishi wa  sanaaa ya  uigizaji  Filamu  nchini.
Hivyo  amewataka  wasanii wa  aina  hiyo  kuacha  tabia  ya  kujilengesha  kwa  Wanaume  na  badala  yake  wajione  wapo  kazini  muda  wote.

ZITTO KABWE na Prof MARK MWANDOSYA Wapeana za Uso laivu Bila Chenga...Zitto Aanza na Mwondosya Akajibu..Soma Hapa

$
0
0
Majibu ya Prof. Mwandosya kwa Mhe. Zitto Kabwe kwenye post yake Instagram

ZITTOKABWE: Prof. Mark Mwandosya aliwahi kuwa Waziri wa Mawasiliano na Uchukuzi wakati wa uongozi wa Rais Benjamin Mkapa. Mashirika yote ya Umma , takribani, katika Wizara hii yaliyobinafsishwa zoezi la ubinafsishaji liligubikwa na tuhuma za ufisadi na hata kuchukuliwa upya na Serikali. Shirika la Ndege la Taifa lilibinafsishwa chini ya Mwandosya na likafa. Kitengo cha makontena katika Bandari ya Dar Es Salaam kilibinafsishwa kipindi hiki na kuleta maneno mengi sana. Mchakato wa kubinafsisha Shirika la Reli pia ulianza kipindi hiki. Ubinafsishaji ulioleta maneno mengi zaidi ulikuwa ni wa Kampuni ya simu (TTCL) kwa MSI detecon na Celtel International. Prof. Mwandosya binafsi alipata tuhuma na mtoto wake kusomeshwa na watu waliouziwa kampuni hii kwa bei ya chee. Masuala haya yaliandikwa na vyombo vya habari miaka ya kati ya 2001 na 2005. Prof. Hana budi kufafanua haya mbele ya umma ili kujiridhisha na uwezo wake wa kupambana na rushwa na ufisadi.

MARKMWANDOSYA: Zitto, salaam. Hongera pia kwa kuwa kiongozi wa ACT na hongera kwa kazi kubwa unayoifanya kueneza itikadi ya chama chako. Ni jambo zuri katika kukuza demokrasia ya nchi yetu na hasa kukuza uzalendo. Siku zote nimekuelezea kama kijana ambaye hakika utakuwa tegemeo la Taifa letu, na hili nimekuambia mara nyingi. Nimeona vema nifafanue yale ambayo umeyataja katika post yako. Niliyatolea maelezo ya kina miaka mingi iliyopita lakini nadhani utafiti sio moja ya maeneo tuliyo na nguvu nayo kwa hiyo umeyafufua bila kuyafanyia utafiti au kutaka upate ufafanuzi kutoka kwa mhusika. Nianze na hili suala la ubinafsishaji kwa ujumla wake. Inawezekana wakati huo ulikuwa bado shule ukiwa mwanafunzi. Pamoja na nia njema ya kuanzisha mashirika ya umma, hatimaye yalikuja kuwa mzigo mkubwa kwa hazina yetu, maana yake kwa wananchi.

Asilimia kubwa yalitegemea ruzuku ya serikali na baadhi yalikuwa mufilisi. Teknolojia ilikuwa imebadilika sana na ili kuyafufua ingeigharimu serikali na umma wa Tanzania kiasi kikubwa sana. Uchumi wa nchi wakati ule usingeweza kubeba mzigo huo. Ndipo Chama, wakati ule kiliporidhia serikali ibakie na shughuli zake za msingi za Utawala, Ulinzi na Usalama, na Usimamizi wa ujumla wa uchumi. Maamuzi yafuatayo yakachukuliwa: Kwa upande wa shughuli za serikali zenye sura ya kibiashara, idara husika zikageuzwa kuwa wakala wa serikali, zikifanya kazi kwa uhuru zaidi chini ya Bodi zao. Kuhusu mashirika na kampuni za umma zenye mwelekeo wa kiniashara, ilikubalika zirekebishwe na hatimaye zibinafsishwe. Ndipo kilipoundwa chombo maalum kisheria kilichokuwa na mamlaka kamili ya kubinafsisha mashirika ya umma. Chombo hiki, Tume ya Kurekebisha Mashirika ya Umma(Parastatal Sector Reform Commission, PSRC), kilikuwa chombo huru kikiwa chini ya Ofisi ya Rais, Mipango. Kiliwekwa hapo kwa sababu mamlaka yake yalikuwa Mtambuka, na vyombo husika vilikuwa kwenye sekta mbalimbali. Kwa hiyo sekta husika na Wizara husika, pamoja na kuitwa PSRC wakatii wa majadiliano yaliyohusu mashirika yake, hazikuwa na mamlaka ya kisheria kuhusu ubinafsishaji. Kwa mujibu wa Sheria ya Kurekebishaashirika ya Umma,mara shiriks lilipoorodheshwa na PSRC, liliwekwa chini ya PSRC ili kurekebishwa na hatimaye kubinafsishwa. Ni vema suala uuuhili likaeleweka.

Pamoja na hayo, nirudie ufafanuzi kuhusu ubinafsishaji wa TTCL, nafanya hivyo kutokana na dhana ya uwajibikaji wa pamoja, ikumbukwe kwamba maamuzi ya ubinafsishaji wa TTCL yalifikiwa na PSRC mwaka mmoja kabla Waziri Mwandosya hajaingia siasa! Hata hivyo suala kubwa ni mabadiliko ya teknolojia tu. TTCL ilikuwa imejikita zaidi kimfumo na kiteknolojia katika teknolojia ya analogue na land lines na simu za mezani ambazo zilikuwa na hata sasa zimepitwa na wakati. Mfumo wake, kiutawala na kiteknolojia ulikuwa katika msingi huo. Teknolojia ya simu za mkononi, na ushindani uliojitokeza ndio hasa umekuwa changamoto kubwa ya TTCL. Hata hivyo mabadiliko makubwa na maendeleo makubwa katika TEHAMA na mfumo mpya wa utoaji leseni katika huduma za mawasiliano umepelekea Tanzania kuwa mbali na kuwa mfano wa kuigwa na nchi nyingi za Afrika.

Katika mawasiliano, Tanzania imekuwa 'Mecca' na wengi wamekuja kujifunza tumewezaje kufanikiwa. Namshukuru Rabuka kwa kuniwezesha kutoa mchango wangu katika maendeleo ya sekta hii. Na ili kuhakikisha kwamba mlaji au mtumiaji wa huduma za kiuchumi hahujumiwi na wakati huo huo mtoa huduma au mwekezaji ana uhakika wa kufaidika na kuweza kutoa huduma endelevu, ndipo vilipoanzishwa vyombo vya udhibiti wa huduma za kiuchumi, (Regulatory Bodies). Nimebahatika kuwa Waziri pekee mwanzilishi na msimamizi wa TCRA, SUMATRA, TCAA, na EWURA. Nimeelezea kuhusu mfumo wa ubinafsishaji hivyo basi ninachoweza kufafanua ni kwamba nilipomaliza muda wangu kama Waziri wa Mawasiliano na Uchukuzi, niliacha Shirika la Reli likisafirisha tani laki tisa za shehena kwa mwaka, safari za abiria kwenda Tabora kutoka Dar zilikuwa kila siku, na ATC ilikuwa na ndege mbili aina ya Boeing 737 na mbili aina ya Fokker Friendship.

Tuhuma za mtoto wa Profesa kulipiwa na kampuni moja ya simu hazina chembe yoyote ya ukweli Bwana Zitto. Mtoto ambaye alifuzu uhandisi wa mawasiliano ya simu aliomba kazi ya muda na akapewa.

MARKMWANDOSYA: Kampuni husika ilikanusha tuhuma hizo ambazo zilitolewa wakati wa mchakato wa kugombea uteuzi katika CCM kwa nafasi ya kuwa mgombea wa Urais mwaka 2005. Sasa zinafufuliwa tena na Bwana Zitto wakati wa mchakato huo huo mwaka 2015! Inaeleweka.

MARKMWANDOSYA: Na kwa taarifa kwako Bwana Zitto, kwa kuwa bandari ni kitovu cha mapato ya serikali, ubinafsishaji wa Container Terminal ya Bandari ya Dar es Salaam ulifanywa na PSRC kwa kushirikiana na Wizara ya Fedha, na siyo Wizara ya Mawasiliano na Uchukuzi.

Namalizia kama nilivyoanza, Zitto ni mwanasiasa ninayemheshimu sana. Mara nyingi naye amenitambua na kunielezea mimi kama mwanasiasa wa kuigwa (role model). Lakini katika siasa tunasema saa 24 ni kipindi kirefu sana, na huwa tunabadilika! Ushauri wangu kwake ni kwamba siku zote kabla hujahukumu sikiliza upande wa pili, kwa kilatini hii ni dhana muhimu inayojulikana kama AUDI ALTERAM PARTEM. Pili ni vema ukazingatia zaidi mambo chanya ya mipango, mkakati, msimamo na itikadi ya ACT. Siasa za majitaka hazimuachi mtu bila doa! Lakini katika kushauri hivyo natambua kwamba "akili ni nywele, kila mtu ana zake" Ramadhan Kareem. Wakatabahu, Mwandosya.

Majibu ya Zari kwa wanaomshutumu kutoheshimu Mwezi wa Ramadhan yanashtua

$
0
0
Zari the Bosslady amejikuta kwenye kitimoto kutokana na mashabiki kumshambulia mtandaoni kwa mavazi yake katika mwezi mtukufu wa Ramadhan.

Mama huyo mtarajiwa wa mtoto wa Diamond amelazimika kutumia Kiswahili kuwajibu wale wanaomshambulia kwa mavazi yake katika kipindi hiki ambacho waislamu duniani kote wapo kwenye mfungo wa mwezi mtukufu wa Ramadhan.

Mnikome, maisha yangu yanakuhusu nini wewe, na yako hayanihusu mimi kabisa ata kidogo,” ameandika Zari kwenye Instagram.

“Oh sijui high heels, mara nguo imembana, sijui anapikia heels,pili pili hujakula wewe inaakuwashia nini? Mvae madera zenu mfunge mkanda mpite kimya kimya. Kwanini unastress???? HAYA NI MAISHA YANGU,”ameongeza.

“Na sasa your all Gods’ judges now…. how many people do we know that wear hijab but have very dirty ugly hearts? Huh? How many of you act so straight for these 30 days but the last 11 months you’re the worst monsters this world has ever seen. Now u wana come here and judge my faith by the dress?”


“Allah bless all of you….atleast I ain’t acting snitchy, am being ME. And oh, if you happen not to like what you see in ur news feed (my page) U always have 3 options, Block yourself, unfollow ama fast forward coz if your still following na you exercise your fingers kuwakya matusi page yangu, babe your just an obsessed fan if not a confused admirer dah majirani. Habari nakazi mnayo……like I always say, no bad vibes from me. So stay blessed.

Walimu Wabakwa na Kunyolewa Sehemu za Siri Usiku Kishirikina

$
0
0
WALIMU katika shule ya msingi  Nambaza Kata ya Nansimo wilayani Bunda,    wamesema watahama shule hiyo endapo serikali ya wilaya hiyo haitachukua hatua madhubuti kukomesha ushirikina shuleni hapo.

Mwalimu Mkuu wa shule hiyo, Sospiter Mafuru,  alisema walimu wake wanafanyiwa vitendo vya ushirikina ikiwa  ni pamoja na kusumbuliwa   usiku  na kunyolewa  nywele   sehemu za siri.

Alitaja vitendo vingine kuwa ni kuvuruga vyombo vya ndani wakati wa usiku, kumwaga michuzi na damu kwenye mashuka na nguo za walimu hao.

“ Vitendo hivi vimetishia usalama wa walimu hadi sasa walimu watatu wa kike wamehama shule hii kwa hiyo tunaomba jamii ya Nambaza wachukue hatua,”alisema.

Alisema awali   ushirikiana huo ulianza kwa wanafunzi  kuugua na kuanguka ovyo na baadaye kwa walimu na aliomba Serikali   kuchukua hatua na kukaa na wananchi wao.

Mafuru alisema hadi sasa ana    walimu tisa,wa kike watano na wa kiume wanne.

 Mkuu wa wilaya ya Bunda, Joshua Mirumbe, alisema  tayari ameviagiza vyombo vya dola kwenda kijijini hapo kufanya utafiti kuwabaini watuhumiwa hao.

Trace TV kuionesha video ya Chekecha ya Alikiba mara ya kwanza leo

$
0
0
Video ya wimbo wa Alikiba ‘Chekecha Cheketua’, itaoneshwa kwa mara ya kwanza kwenye kituo cha runinga cha Ufaransa, Trace TV Jumatatu hii.

Video hiyo imeongezwa na muongozaji wa video za muziki wa Nigeria, Meji Alabi. Itaoneshwa saa tatu na dakika 32 asubuhi kwa saa za Afrika Mashariki.


Jiunge na Bongo5.com sasa

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook, Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Bongo5!

Millem Magese atunukiwa tuzo ya heshima ya Global Good ya BET Awards 2015

$
0
0
Miss Tanzania, 2001, Happiness Millen Magese, hatimaye ametunukiwa tuzo ya kwanza ya heshima ya Global Good ya BET Awards 2015.

Millen amepewa tuzo hiyo kutokana na jitihada zake za kampeni ya ugonjwa wa endometriosis ambao pia amekuwa nao katika maisha yake yote tangu awe msichana. Tatizo hilo limempelekea kuwa mgumba.

Pamoja na hivyo Millen amekuwa mstari wa mbele kutoa misaada mbalimbali kwa wasiojiweza.
Viewing all 104796 articles
Browse latest View live




Latest Images