Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104795 articles
Browse latest View live

JACK WOLPER Alia na Soud Brown wa U-Heard..Adai Udaku Wake Usio na Usibitisho Unawakosesha Pesa za Matumizi

$
0
0
Pozi hili limuendee soudbrown popote alipo pale unaposikiliza udaku wake alafu peke yako naunatafakari kwanini kafanya mambo meusi kama haya haha Soud acha mambo meusi uwaga unatupa mtihani tukichepuka kidogo tu habari radion natalaka za week zinatuhusu no busu na call no matumizi sasa bora vyote vifanyike ila swala lamatumizi liwepo lakini vyote vinapotea kwa udaku wako usio nausibitisho soud acha mambo meusi ..maana ukinipgia cm sku hzii na hvi namba zako zote nimezisave ata kma una deal yako unataka msaada wangu sitowaza hvyo nitawaza tuu mambo yako meusi jirekebishe kidogo kua nasubra Soud unatuponza Mimi ajanifanya ktu lkn nameambia tuu mapozi tunayokaaga tena mimi ananistrigi kweli kweli ndo nachompendea


Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumanne ya Tarehe 30 Juni 2015

$
0
0






















Habari  Zilizopo  Katika  Magazeti  ya  Leo  Jumanne  ya  Tarehe 30  Juni 2015

Haya Sasa Hapa Nimekuwekea Video Mpya ya Ali Kiba 'Chekecha' Ambayo Ndio Gumzo Mjini Kwa Sasa

$
0
0
Zilipita pichaz na vipisi tu lakini hii ndio video kamili ya Ali Kiba ‘chekecha‘ ambayo imefanywa South Africa wiki kadhaa zilizopita… ukishaitazama uache maoni yako kwenye comment Ali Kiba na team yake watapita kuona nini mashabiki wanasema.

'Acheni UONGO, Nyerere Hakuwahi Kumkataa Edward Lowassa'

$
0
0
Waziri Mkuu mstaafu, Edward Lowassa, amehitimisha ziara yake ya kutafuta wadhamini katika Mkoa wa Morogoro huku kada mkongwe wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Kanali mstaafu Issack Mwisongo, akisema Baba wa Taifa hayati Mwalimu Julius Nyerere, hakuwahi kutamka kumkataa mbunge huyo wa Monduli kama ambavyo baadhi ya viongozi wanasema.

Katika Mkoa huo ambao ni wa 31, Lowassa alipata wanachama 104,038 waliomdhamini.

Kanali Mwisongo alisema tangu alipojiunga na Tanu mwaka 1967 ambayo sasa ni CCM, hajawahi kumsikia hayati Mwalimu Nyerere akitamka neno la namna hiyo na amekuwa akihudhuria vikao vyote kuanzia Halmashauri Kuu ya CCM (Nec), Kamati Kuu na Mkutano Mkuu.

“Mimi nimekuwa katika vikao hivyo vyote na kama Nyerere ukikosea au hakutaki, alikuwa anakukataa waziwazi na pia unatangazwa kwenye vyombo vya habari. Lowassa ni mtu anayewapenda Watanzania tangu zamani,” alisema Kanali Mwisongo.

Alitolea mfano wa mwekezaji aliyedai kuwa aliletwa na mmoja wa `wakubwa ' ili ajenge hoteli katika chanzo cha gesi, lakini Lowassa aliyekuwa Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kwa wakati huo, alikataa.

“Alikataza hoteli kujengwa katika chanzo cha gesi kwa manufaa ya Watanzania na kila alichoamua aliamua kwa manufaa ya Watanzania,” alisema Kanali Mwisongo.

Aidha, aliwaonya viongozi wa chama hicho kuacha kutoa matamshi kabla ya vikao havijakaa kwani ni makosa makubwa na wanasababisha CCM kuyumba kama hakina mwenyewe.

“CCM kimeyumba kupita kiasi kutokana na hawajui msemaji mkuu ni nani na vikao vikuu vinakaa saa ngapi vya kuamua hayo yanayosemwa ovyo. Viongozi wasifanye makosa katika Kamati Kuu, Kamati ya Maadili ambako kutakuwa na mizengwe, lakini watambue Nec ina nguvu,” alisema Kanali Mwisongo.

Naye Kada mwingine mkongwe, Dk. Juma Ngasongwa, ambaye amewahi kuwa Waziri katika awamu mbalimbali, alisema viongozi wa CCM wameyumba siku za karibuni kutokana na kusemana hadharani wenyewe kwa wenyewe  na Lowassa ndiye dawa ya kuondoa maneno hayo.

“Kuna wanachama wengi wamehamia vyama vingine kutokana na kushindwa kuongoza CCM. Sasa huko katika vyama vingine watawezaje kuviongoza? CCM irudishe wana-CCM imara madarakani ambaye ni Lowassa,” alisema Dk. Ngasongwa.

Kwa upande wake, aliyewahi kuwa Mkuu wa Mkoa wa Morogoro, Steven Mashishanga, alisema vikao vinavyotarajiwa kukaa hivi karibuni vihakikishe vinatenda haki kwa kuangalia ni nani aliye na alama nyingi za vyema mgongoni na anayehitajika na wengi.

Alisema Lowassa ni kiongozi pekee mwenye uwezo na sifa za kuwa Rais kwani amekitumikia chama kwa miaka mingi.

Naye Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Morogoro Mjini, Fikiri Juma, alimtaka Nape Nnauye, kuacha kutoa kauli kuwa wananchi wengi wamepewa fedha kwa ajili ya kumdhamini Lowassa wakati wapo wagombea wengi wamefika kuomba udhamini na kutoa rushwa.

Alisema hakuna mtu aliyepewa fedha kwa ajili ya kumdhamini Lowassa, bali ni wananchi wenyewe ndiyo wana maamuzi ya mwisho ya kumchagua kiongozi wanayemtaka na si Nape.

“Haki isipotendeka katika vikao vya maamuzi sisi bado tupo pamoja na wewe, katika semina ya wenyeviti tuliyopewa tuliambiwa tuchague viongozi wanaokubalika ndani na nje ya Chama ambaye ni wewe,” alisema Juma.

Akizungumza na wanachama CCM, Lowassa aliwashukuru kwa kumdhamini na kwamba Mkoa wa Morogoro amepata watu wengi.

Hata hivyo, alisema licha ya kupata wadhamini wengi, atapeleka wanaotakiwa CCM na wengine atawahifadhi nyumbani kwake kama kumbukumbu yake.

Lowassa amepata jumla ya wadhamini 863,479 katika mikoa 31 aliyoitembelea.

Aidha, alitaja sababu za kugombea urais kuwa ni pamoja na kuchoshwa na hali ya umaskini na pia Rais Jakaya Kikwete, anamaliza muda wake wa uongozi hivyo anatakiwa kukabidhi kijiti kwa mtu mwingine.

"Na anayeweza kukipokea kijiti hicho na kuyaendeleza yale aliyoyaacha Rais Kikwete, ni mimi. Kazi hii haipatikani hivi hivi, naomba dua zenu Waislamu na Wakristo ni muhimu sana,” alisema Lowassa.

Alisema endapo atafanikiwa kupata nafasi anayoiomba, kwanza atahakikisha anafufua viwanda katika mji wa Morogoro.

Aidha, alisema anasononeshwa mno na migogoro ya wakulima na wafugaji kwa hiyo atakapoingia madarakani, ataunda tume ya kusuluhisha migogoro hiyo.

Aliwataka Watanzania wajiandae kuwa na `spidi' ya kuchapa kazi kwani anataka mchakamchaka wa Maendeleo na  atakayeshindwa atalazimika kukaa pembeni.

To all Men, This lady needs your attention, See what she posted

$
0
0
To all Men, This lady needs your attention, See what she posted.

Enough of VERA’s fake assets, BRIDGIT is the real deal, Rate Her (1-10)s

$
0
0



Enough of VERA’s fake assets, BRIDGIT is the real deal, Rate her (1-10)s

US Gay Marriage: Robert Mugabe Asks Obama to Marry Him

$
0
0
Zimbabwean president Robert Mugabe has challenged US President Barack Obama by asking his hand in marriage. His comment comes at the back of the legalization of gay marriage in the US by the Supreme Court.

During Mugabe's weekly radio interview with Zimbabwe’s national radio last Saturday, he said:
“I’ve just concluded since President Obama endorses the same-sex marriage, advocates homosexual people and enjoys an attractive countenance thus if it becomes necessary , I shall travel to Washington, D.C. , get down on my knee and ask Obama’s hand. I can’t understand how these people dare to defy Christ’s explicit orders as our Lord prohibited mankind from sodomy.''
Mugabe said the American Government is run by pervert, Satan-worshipers who insult the Great American nation.
He reportedly added
"That the American tradition and heritage was based on lofty Christian principles, but to the detriment of this great nation, America’s corrupt political elite is acting according to their diabolic whims.
Obama’s endorsement of gay marriage, the first ever from a sitting president, came amid growing pressure for the president to clarify his previously muddled opinion.
Obama’s endorsement of gay marriage, the first ever from a sitting president, came amid growing pressure for the president to clarify his previously muddled opinion, as two senior members of his administration announced personal support for gay marriage and a day after voters in North Carolina approved a state constitutional amendment defining marriage as a union between a man and a woman.

Source: awdnews.com

MWANAMUZIKI Diamond Platnumz Ashikiliwa Airport kwa Saa Mbili Kisa Madawa ya Kulevya..

$
0
0
Musa Mateja

KIBANO! Staa wa Bongo Fleva mwenye jina kubwa Afrika, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’, juzikati alijikuta kwenye wakati mgumu baada ya ‘kutaitiwa’ kwa saa mbili kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA) kisa kikiwa wingi wa mabegi (3) makubwa aliyoshuka nayo akitokea nchini Afrika Kusini ‘Sauzi’, Ijumaa Wikienda linakupa ‘unyunyuz’ kamili.


Tukio hilo lililoshuhudiwa hatua kwa hatua na gazeti hili, lilijiri Juni 26, mwaka huu kwenye eneo la kukagulia mizigo ya abiria uwanjani hapo kitendo kilichosababisha Diamond kutokwa na kijasho chembamba.


TAFSIRI YA MABEGI MAKUBWA

Chanzo chetu kilichokuwa ndani ya jengo la kutokea abiria kililiambia Ijumaa Wikienda kuwa, maafisa ukaguzi wa uwanja huo walimtilia shaka Diamond hivyo ikawalazimu wayakague mabegi hayo hadi ndani lakini pia walimkuta ana upungufu wa stakabadhi za mizigo hiyo.

KUHUSU STAKABADHI

Kuhusu stakabadhi zisizokuwepo, ilibidi Diamond ampigie simu ‘mdogo wake’ (si wa tumbo moja) aliyejulikana kwa jina la Q-Boy ampelekee kwani alitua nazo Bongo siku moja kabla, yaani Juni 25.

NDANI YA MABEGI

Ndani ya mabegi hayo, kulikutwa kamera, maiki na vifaa vya studio.

IMANI YA WAPEKUAJI

Shuhuda mmoja ambaye Ijumaa Wikienda lilimkuta nje ya chumba ambacho Diamond alikuwa akipekuliwa, alisema maafisa hao waliamini msanii huyo alikuwa ameshuka na madawa ya kulevya ‘unga’.“Unajua mastaa siku hizi wanaongoza kwa kubeba unga. Sasa serikali iko makini nao sana. Ndiyo maana wengi wao wakipita hapa wanakaguliwa kuliko abiria wengine,” alisema mtu huyo aliyejitambulisha kuwa ni dereva wa teksi uwanjani hapo.

DIAMOND APIGWA PICHA, AONGEA NA WIKIENDA

Paparazi wetu aliendelea kuganda mlangoni hapo hadi Diamond alipotoka na kumfotoa picha mbalimbali na baadaye alimfuata hadi kwenye gari aina ya Toyota Lexus na kumuuliza kama anajua kisa cha kupekuliwa kwa muda mrefu vile.

“Nilikuwa na mizigo naishughulikia ili itoke hivyo kuna mambo pia tulikuwa tunapishanapishana pale maana walihitaji nilipie ushuru wakati vifaa vya studio tulishaambiwa ni ‘free’ (bure). Pia kulikuwa na risiti za mizigo ambazo zilikuwa hazionekani, kumbe Q-Boy alitangulia nazo jana mimi nikawa nimesahau.

“Ila wao walikuwa wakijiridhisha kwenye mizigo yangu. Walifikiri nimebeba unga,” alisema Diamond.

HALI YA SASA UWANJANI

Mbali na Diamond kupekuliwa kwa muda mrefu, kwa sasa abiria wanaoingia na kutoka kwenye uwanja huo wamekuwa wakikaguliwa kwa umakini ili kubaini uhalali wa mizigo yao lengo kubwa ni kudhibiti uingiaji au utokaji wa madawa ya kulevya ambapo serikali imeweka umakini katika kupambana na biashara hiyo haramu.

CHRISTIAN BELLA

Ukiachana na Diamond, mastaa wengine waliowahi kukumbana na pekuapekua kama hiyo ni Mkurugenzi wa Bendi ya Malaika, Christian Bella na mtangazaji wa Radio Time FM, Hadija Shaibu ‘Dida’.

Bella yeye alikumbwa na adha hiyo, mwaka juzi, usiku wa saa nane akiwa anatokea nchini Uturuki na Ndege ya Shirika la Turkish Airways.

Dida naye ilikuwa mwaka 2012 ambapo alikumbwa na pekuapekua hiyo alipoingia uwanjani hapo kuelekea nchini Thailand kwa shughuli za kibiashara.

Taharuki ya Marehemu Kufufuka Bagamoyo ipo Kwenye Hekaheka ya leo…(Audio)

$
0
0
Jana mji wa Bagamoyo uliingia katika taharuki kubwa baada ya habari kuenea kuwa kuna marehemu kafufuka baada ya kuthibitishwa na madaktari kuwa amefariki.

Timu ya Hekaheka ilifunga safari hadi Bagamoyo na kukuta umati wa watu katika nyumba ambayo marehemu alikua akiishi ikiwa ni muda mchache baada ya mwili wake kurejea kutoka hospitali ya Wilaya ya Bagamoyo ambapo ndipo alipofariki.

Majirani walidai baada ya mwili wa marehemu huyo kurudishwa nyumbani ili kuanza taratibu za mazishi walishangaa kuona bado mwili wa moto na alikua akijitingisha wakati waoshaji wakimuandaa kwa ajili ya kumzika.

Shangazi wa marehemu alisema ni kweli baada ya kumleta walishangaa mwili ukiwa wa moto na mapigo ya moyo yakifanya kazi kama kawaida licha ya madaktari kuthibitisha kuwa amefariki, na wakaamu kusimamisha shughuli za mazishi hadi kesho yake walipoona  amekuwa wa baridi na tayari alishafariki.

Daktari aliyethibitisha kama marehemu amefariki alisema baada ya kumpima marehemu alikua amefariki na kuruhusu taratibu ziendelee, na alisema kuwa mwili wa marehemu kuwa wa moto inategemee na mazingira ya sehemu alipohifadhiwa.

Isikilize stori kamili hapa mtu wangu… Source:Millard Ayo

Davido’s New Video Breaks A Record

$
0
0

On June 9th205, Nigerian artist Davido released his much-anticipated music video called “Fans Mi”, featuring American rapper Meek Mill.

A RECORD BREAKER
15 days after it was released, the video has hit more than a million views on YouTube.  Davido shared his joy on his Instagram account by saying: “RECORD BREAKER!!! 1,000,000 views in days!!!!!!” A few weeks back, Davido did tell his fans that this would be the “biggest video of his career.” 2015 has been a great year for the afrobeats musician: he is in the process of releasing a new album, he recently graduated from university, he had a daughter, he bought a house in Atlanta, and he received three nominations for the 2015 MTV Africa Music Awards. Life is good!

Nimezaa na Mose Iyobo lakini ndoa yangu ipo pale pale – Aunty Ezekiel

$
0
0
Muigizaji wa filamu, Aunty Ezekiel ambaye hivi karibuni alijifungua mtoto wa kike, amedai kuwa licha ya kuzaa nje ya ndoa, bado anaamini ndoa yake ipo pale pale.

Akizungumza na Bongo5 leo, Aunty aka Mama Cookie, amesema aliamua kuzaa na Moses Iyobo, dancer wa Diamond Platnumz kwakuwa muda wa kuwa mama ulikuwa umefika.

Mimi niliamua kupata mtoto baada ya kuona wakati umefika,” amesema.

Kwasababu siku zinaenda pamoja na umri inabidi maisha yaendelee mbele. Ndoa yangu ipo kama ilivyokuwa mwanzo, haijavunjika, sijawahi kuongea kama nimezaa nje ya ndoa au ndani ya ndoa lakini mwisho wa siku ndoa yangu bado ipo,” ameongeza.

Haya ni maisha na vitu vinavyozungumzwa vipo kama vilivyo, lakini familia yangu na watu wa karibu wanaelewa nini kinaendelea ndani yake na watu niliokuwa nao wanaelewa na sidhani kama itakuwa right kuongea kwenye media. Lakini watu wajue baba yake ni Mose,” amesisitiza muigizaji huyo.

Pia Aunty amewatoa hofu mashabiki wa kazi zake kwa kusema kuzaa kwake sio mwisho wa kuigiza.

Kupata mtoto kwenye maisha yangu ni kitu kizuri kwa sababu kuna vitu vingi ambavyo nimepunguza na nimekuwa mama mwenye majukumu, ninapofanya vitu vyangu najua kesho na kesho kutwa kuna mtu ananitegemea. Pia kuzaa kwangu sioo kwamba kutaua sanaa yangu, sanaa yangu ipo pale pale na hata nitakapomaliza kulea nitakuwa na vitu vingi zaidi kwa sababu natumia muda mwingi kulea Kwahiyo nikirudi wategemee vitu vikubwa zaidi ingawa kuna kazi ambazo niliziandaa zitatoka wakati ninalea.


Dotnata Aingilia Ugomvi wa WEMA SEPETU na KAJALA...Amuomba Mungu Haya Yatokee

$
0
0
Mwigizaji mkongwe, Husna Posh ‘Dotnata’ ameengilia kati ugomvi kati ya mastaa wa Bongo Movies, Wema Sepetu na Kajala Masanja kuwataka waachane na hali hiyo kwani bifu lao halina faida kwao na katika jamii.

Akizungumza na Tanuru la Filama hapo jana, Dotnata alisema kuwa  kwa akili ya kibinadamu ugongvi huo hauwezi kuisha  kutokana na kila mmoja kumuona mwenzake ndiyo mbaya.

Namuomba Mungu kila siku ili Wema amsamehe Kajala na Kajala amsamehe Wema ili maisha yaendelee kwani kwa akili za kibinadamu imeshindikana hivyo na nitaonana nao baada ya maombi yaha kwani natambua hakuna jamabo kubwa lisilo na mwisho, hasira zaozina mwisho” alisema Dotnata.

Dotnata pia alimtaka Wema ambaye ni sawa na mwanaye kuwa wa kwanza kumsamehe  Kajala kwani kwenye ugomvi ni vizuri mmoja wapo ajishushe na kujona ni mkosaji kinyume na hapo  hakuna ambacho kinaweza kufanyika.

Zari: My Life Isn't Perfect, But am Thankful For Every Thing I Have

$
0
0

Spent the public holiday literally doing nothing. Happy youth day South Africa. My life isn't perfect, but am thankful for every thing I have 

Maneno Mengine ya OMMY DIMPOZ Kuhusu Waliomtukana Instagram Baada ya Kumposti ALI KIBA Kwenye Page yake ya Instagram

$
0
0
Ommy Dimpoz alipost tangazo la Video mpya ya Ali Kiba lakini baada ya kupost wapo waliopita kwenye post yake @Instagram na kuanza kuandika comments za matusi.

Mwenyewe amesema hakupenda kuona watu wanaandika comments za matusi kila kitu ambacho anapost… Ommy amesema kwenye kurasa za mastaa kama yeye wanaotembelea ni watu wengi kwa hiyo sio kitu kizuri watu kuandika lugha za matusi.

Mitandao huwa inakuwa na story nyingi sana kuhusu mastaa, wakati mwingine utasikia staa huyu na huyu hawapatani, Ommy amesema wakati mwingine watu huwa wanakuza hata beef kati ya mastaa lakini beef nyingine sio za kweli.

Msikilize Gossip Cop na Ommy Dimpoz hapa kwenye U Heard ya leo JUNE 29 2015

Membe Arudisha Fomu Ya Urais......Akana Kuhusika Na Ufisadi Wa Mabilioni Ya Libya.

$
0
0
MAKADA maarufu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wamerejesha fomu na kufafanua mambo kadhaa ambayo yamekuwa yanazungumzwa juu yao kama njia ya kujiweka sawa kabla ya uteuzi kufanywa na vikao vikuu vya chama hicho.

Mmoja wa waliorudisha fomu ni Waziri Mkuu, Mizengo Pinda ambaye wakati akirudisha fomu za kuomba kuteuliwa na kusema kuwa wanaochukulia suala la urais ni la kufa au kupona wana matatizo kwani anayejua Rais wa Tanzania ajaye ni Mungu.

Alisema safari yake ya kutafuta wadhamini ilikuwa na misukosuko mingi ikiwemo kutokea ajali tatu lakini hakuna ambaye alikuwa ameumia sana.

Akiwa ameongozana na mke wake, Tunu Pinda alisema mwana CCM mkomavu ni yule ambaye yuko tayari kukubali matokeo.

Alisema mpaka sasa ni wanachama wa CCM 42 waliojitokeza kugombea lakini katika hatua ya kwanza ni majina matano tu yatakayoteuliwa na kundi kubwa litaondolewa.

“Mimi sitegemei kwenye mchujo wa watu watano watokee watu wa kunung’unika kwani kila mtu aliyefika kuchukua fomu alikuwa anafahamu kuwa kutakuwa na mchujo kama tuko wengi wako watano kisha unakwenda ngazi ya pili, hakuna sababu ya kunung’unika,” alisema.

Alisema baadaye kuna kwenda kwenye Mkutano Mkuu atabaki mmoja. “Utanung’unikia nini? Kuna kushinda na kushindwa na kuna kupata na kukosa na ukisema suala la Urais ni kufa au kupona basi una matatizo, ifike mahali wana CCM wapate mtu ambaye wanadhani anaweza kusaidia kuongoza,” alisema.

Pia alisema waliojitokeza mwaka huu kuchukua fomu ni wengi. “Tuliojitokeza tusinuniane, kwa nini haniungi mimi mkono, na wewe usione jambo hili ni nongwa na usijione mapenzi ya Mungu yako kwako tu,” alisema.

Pia aliwataka viongozi wenzake washirikiane kumuunga mkono mgombea mmoja atakayepeperusha bendera ya CCM. “Anayejua rais wa Tanzania atakuwa nani ni Mungu peke yake,” alisema.

Mwakyembe arudisha fomu
Waziri wa Afrika Mashariki, Dk Harrison Mwakyembe jana alirudisha fomu na kusema CCM itapata ushindi wa kishindo katika uchaguzi mkuu utakaofanyika Oktoba mwaka huu kutokana na kutekeleza ilani yake vizuri na wananchi kuwa na imani kubwa na chama hicho.

Mwakyembe ambaye alirudisha fomu jana mchana alisema katika safari yake ya kutafuta wadhamini mkoani ameweza kuwaona wanachama wengi wa CCM ambao wanaonesha imani kubwa na chama chao.

Alisema kila alipokutana na wana CCM waliojitokeza kumdhamini kwa tathmini aliyofanya tangu kuanza kwa siasa ya vyama vingi nchini CCM, itashinda ushindi wa kimbunga kwani mtaji upo kutokana na kazi kubwa iliyofanya serikali ya awamu ya nne katika utekelezaji wa ilani.

“Tumejipanga kuhakikisha wanaingia kwenye uchaguzi kifua mbele kutokana na kutekeleza ilani,” alisema.

Pia alisema kwa upande wa pili wana kazi ya kuhakikisha yote mazuri yaliyofanywa na CCM yanasemwa.

 “Tuna kazi ya kuhakikisha kuwakumbusha wananchi barabara za lami na mafanikio mengi yamepatikana na serikali ya awamu ya nne ya CCM,” alisema.

Alisema kazi kubwa ni kuhakikisha umma unatambua CCM imefanya mambo mengi kutokana na upotoshaji unaofanywa na wapinzani kuwa CCM haijafanya lolote.

Pia alisema CCM kuwa na wagombea wengi waliojitokeza mwaka huu ni dalili njema za CCM kutoa fursa za kupatikana mmoja ambaye kila moja atamuunga mkono ili kuweza kukivusha chama.

Dk Mwakyembe alisema yuko tayari kumuunga mkono mgombea atakayeteuliwa na chama. Awali alisema amezunguka katika mikoa 15 katika kutafuta wadhamini.

Dk Mwele Malecela
Mwanachama mwingine wa CCM aliyerudisha fomu jana ni Dk Mwele Malecela ambaye alisema pamoja na kazi kubwa iliyofanywa katika uongozi wa awamu nne bado kuna watu wanaoishi kwenye umasikini uliokithiri.

Alitoa kauli hiyo wakati wa mkutano wake na waandishi wa habari. Alisema alifanikiwa kupata wadhamini katika mikoa 20 ikiwemo 17 ya Tanzania bara na mitatu ya Zanzibar.

Alisema wananchi wameonekana kufarijika kuona wanafuatwa kwenye maeneo ya kata walipo. Alisema ameweza kuzunguka mikoa tisa kwa siku nne hali inayoonesha kuwa kazi kubwa imefanyika katika ujenzi wa barabara za lami kuunganisha mikoa.

‘Pamoja na maendeleo na kazi kubwa ya awamu zote bado kuna umasikini uliokithiri lazima kuliangalia suala hilo kama kiongozi na kulitafutia ufumbuzi,” alisema.

Alisema aliguswa sana na wanawake waliojitokeza wakiwemo wazee ambao walikuwa wakitaka kumuona ni mwanamke wa aina gani ambaye anataka kugombea Urais.

“Wanawake wamefurahi sana kuona wanawake tunajitokeza hii ni fursa nzuri ya kuwapa moyo akinamama kugombea nafasi mbalimbali za uongozi katika nchi,” alisema.

Membe Ayakana  Mabilioni  ya  Libya
Membe kwa upande wake wakati anarudisha fomu akijibu swali aliloulizwa kuhusu madai ya kuwa anahusika na ufisadi wa fedha za Libya na kama inavyosambazwa na wapinzani wake, alisema akigundulika kuwa alikula hata dola moja yuko tayari kujiuzulu.

“Uvumi kuwa nahusika na mabilioni ya Libya hauna mashiko kabisa baadhi ya wanasiasa wenzangu wanajua ukweli wote huu lakini kwa makusudi wameamua kuniunganisha na kampuni hiyo na kuwaaminisha watu ni yangu au nina hisa maneno hayo ni ya uongo,” alisema.

Alifafanua kuwa Libya ni moja kati ya nchi wafadhili wa Tanzania ambapo, kama ilivyo wafadhili wengine imekuwa ikiipa Tanzania misaada na mikopo yenye masharti nafuu.

Alisema katika utaratibu huo, Tanzania na Libya zilitia sahihi mkataba wa kubadili madeni na kuyaingiza katika miradi ambao uliweka utaratibu wa matumizi na urejeshaji wa fedha za deni la Libya.

Alisema kumbukumbu alizonazo zinabainisha kuwa kabla ya Serikali ya Libya kuweka saini katika mkataba wa nyongeza iliyotaka fedha hizo zikopeshwe kwa kampuni ya Meis, upembuzi yakinifu wa mradi husika ulifanywa kupitia vyombo vyake, na wao wenyewe kujiridhisha juu ya ubora wa mradi huo.

Sumaye na mahakama ya rushwa
 Naye Waziri Mkuu mstaafu, Frederick Sumaye ambaye naye alirejesha fomu alisema akichagulia kuwa Rais wa nchi ataanzisha mahakama maalumu ya wala rushwa.

Mbali na rushwa pia vipaumbele vyake ni pamoja na ufisadi, uhujumu uchumi na kwamba ataunda chombo cha uchunguzi katika masuala hayo.

Pia alisema wakati akiwa Waziri Mkuu wa Tanzania alifanya mambo makubwa na atahakikisha anaunda serikali inayofahamu kutimiza wajibu wake.

‘Uchumi ninaouzungumzia si wa takwimu ni wa hali halisi, nitaangalia pia maeneo kama viwanda vikubwa na vidogo ili watu wengi waweze kujiajiri na kulinda viwanda vya ndani,” alisema.

Alisema atahakikisha uzalishaji wa viwanda vya ndani unaongezeka na kunakuwa na ongezeko la mauzo ya nje ya nchi. Pia alisema ataimarisha huduma za jamii, ikiwemo elimu, afya upatikanaji wa maji na huduma nyingine muhimu.

Alipohojiwa kama maeneo aliyokwenda kutafuta wadhamini aliombwa rushwa, Sumaye alisema, tangu aanze kazi ya siasa hajawahi kutoa rushwa.

“Hata maeneo ambayo nimekwenda kutafuta wadhamini sijatoa fedha hata zilizodaiwa kwa lugha laini nilikataa kwani nilitaka nidhaminiwe na wale walio na imani na mimi,” alisema.

Alisema wakati akiwa Waziri Mkuu alipambana na wala rushwa ambapo aliweza kuwafukuza kazi watu 3,360 huku wengine 400 walipelekwa mahakamani.

Balozi Mahiga
Balozi Mahiga naye wakati anarejesha fomu alisema ameenda mikoa 15 kwa gari na akawashukuru wana CCM kumlaki na kwamba wamehamasika na wanasubiri kwa hamu uchaguzi.

Alisema kama CCM ikimpitisha kuwa mgombea atahakikisha kuwa anajenga maadili ya uongozi ili kuondokana na vitendo vya rushwa na ufisadi.

Alisema uongozi mzuri ni ule unaojengwa katika misingi ya maadili na atapambana na rushwa ili kukomesha vitendo hivyo ambavyo vimekuwa vikirudisha nyuma wananchi wengi.

“Nitahakikisha ninaimarisha misingi ya umoja na mshikamano katika nchi ikiwa ni pamoja na kudumisha muungano wa Tanzania na Zanzibar,” alisema.

Joseph Chaggama
Mwanachama mwingine wa CCM aliyerudisha fomu jana ni Joseph Chaggama ambaye alisema amezunguka katika mikoa 17 wakati wa kutafuta wadhamini. Alisema anaijua CCM vizuri na jinsi Serikali inavyoendeshwa.

Alisema yeye ni mmoja wa watu wasiofahamika na sababu ya kuchukua fomu ni nia ya dhati kutoka moyoni kuwa anaweza kuongoza nchi.

Pia alisema uwezekano wa yeye kuchaguliwa lazima kutokee muujiza. Alisema yuko tayari kuwatumikia Watanzania ikiwa atapewa ridhaa ya kuwa mgombea wa CCM na akashinda uchaguzi mkuu utakaofanyika Oktoba mwaka huu.

Pia alisema yuko tayari kumuunga mkono mgombea ambaye atateuliwa na chama.

Monica Mbega
Mbunge wa zamani wa Iringa Mjini, Monica Mbega naye alirudisha fomu na kusema kuwa chama kiliweka utaratibu mzuri wakati wakienda mkoani kupata wadhamini katika mikoa 15 ikiwemo mitatu ya Zanzibar.

Alisema amekamilisha kazi yake kwa ukamilifu bila matatizo na kuwashukuru wanawake wengi waliojitokeza kumuunga mkono.

Alisema suala la rushwa linategemea jinsi mtu alivyokwenda wakati akitafuta wadhamini.

Amos akemea matumizi makubwa ya fedha
Mwingine aliyerudisha fomu hizo jana ni Amosi Siyantemi ambaye ni mtumishi wa CCM wakati ambaye alisema kuwa kwenye mchakato wa kutafuta wadhamini baadhi ya wagombea wameonesha matumizi makubwa ya fedha.

“Ni jambo la kujiuliza fedha hizo wamepata wapi na ni kiasi gani ni lazima wachunguzwe na kuchukuliwa hatua,” alisema Siyantemi.

Pia alisema rushwa ni ugonjwa mbaya unaoiangamiza jamii ni lazima zichukuliwe hatua za haraka na makusudi ili kuweza kukomesha suala hilo kabla nchi haijatumbukia kwenye shimo la machafuko.

Alisema CCM ya sasa si kama ile ya Mwalimu Nyerere. “Tunahitaji kurejesha haraka heshima ya CCM machoni mwa Watanzania na kwenye macho ya Jumuiya ya Kimataifa,” alisema.

Alisema akichaguliwa kuwa Rais atahakikisha kunakuwa na huduma bora za matibabu sanjari na bima ya afya kwa kila Mtanzania, kufanya mabadiliko makubwa kwenye mfumo wa elimu kwa kuchukua hatua mbalimbali ikiwemo kupunguza idadi ya masomo.

Pia alisema atapiga marufuku mauzo na manunuzi yanayofanyika nchini kwa malipo ya dola ambapo malipo ya dola yatafanyika kwa kibali maalumu.

Pia alisema atakuwa na jukumu la kuleta mageuzi makubwa katika sekta ya sanaa, michezo na burudani yatakayolenga kuwanufaisha kiuchumi wananchi.

Mfungo Wamuepusha Amanda na Skendo...'Mwezi Huu Nguo Fupi za Kuwatega Wanaume Nimeziweka Pembeni'

$
0
0
Staa wa bongo movies,  Tamrina Posh ‘Amanda’ amesema kuwa  mfungo wa mwezi wa ramadhani umemuweka mbali na skendo ambazo amekuwa akiibuka nazo mara kwa mara  na ikiwezekana huo ndiyo utakuwa mwisho wake kwani kwa sasa yupo katika kipindui cha kuomba toba kwa muumba wake kwa mabaya yote  aliyowahi kufanya siku za nyuma.

Akizungumza na gazeti la Filamu, Amanda  alisema kwa mwezi  huu hatoonekana akikatiza mitaani na nguo zilizobana kiasi cha kuonyesha  maungo yake  ya sehemu za siri bali atakuwa anajisitili ili kujiepusha na kitendo cha kuwaingiza majaribuni wanaume hasa walio kwenye mfungo na mpaka mwezi huu unaisha atakuwa amezoea kuvaa nguo hizo.

“Naweza kusenma kuwa mfungo wa mwezio Ramadhani umeniweka kando na skendo  hasa za kuvaa nguo fupi ambazo huwa zinawaingiza  kwenye mitego  wanaume wasio weza kujizuia wanapoona maungo ya wanawake  hasa waliovaa nguo zenye ushawishi,” alisema Amanda.

Aidha, Amamnda aliwataka hata wasanii wenzake  hasa wa kike kuheshimu kipindi hiki kwani  ni  cha kuvuna neema  kutoka kwa Mungu kutokana na kutibu madhambi  yote yaliyofanyika siku za nyuma  na ikiwezekana na wao uwe mwanzo  wa kubadilishwa huhusu kuachana  na skendo za kujitakia  hasa zile za kutengeneza ili waendelee kusomeka kwenye magazeti

Escrow Yaendelea Kumtesa Tibaijuka..Amshambulia Halima Mdee, Adai Anatumiwa na Wabaya Wake Kumchafua

$
0
0
Mbunge wa Muleba Kusini (CCM), Profesa Anna Tibaijuka amemshambulia Mbunge wa Kawe (Chadema), Halima Mdee pamoja na baadhi ya vyombo vya habari kwamba vinatumiwa na wabaya wake kumkashifu katika utendaji wake.

Profesa Tibaijuka alitoa shutuma hizo wakati akihutubia wananchi wa Kata ya Bureza. Alisema alikumbwa na kashfa ya Escrow, kutokana na kupata fedha kutoka kwa kaka yake Rugemalila (James) alizompa kusaidia shule anayoisimamia.

Alikanusha tuhuma zilizotolewa na Mdee bungeni dhidi yake kwamba alipokuwa Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, kabla ya kuvuliwa wadhifa huo, alikuwa mporaji wa mali za wananchi hasa kumiliki ardhi kubwa.

Alidai kuwa katika kashfa hiyo, kitendo cha kusema fedha aliyoipata ni ya mboga kwa maana ni ndogo imetafsiriwa na kutumiwa na vyombo vya habari, hasa magazeti kumchafua zaidi ndani na nje ya Tanzania.

“Nasema hapa mbele yenu na waandishi wa habari wapo hapa, magazeti yanafanya biashara kupitia kwangu kwani wanapoandika habari zangu magazeti yananunulika kwa haraka siku husika,” alisema Profesa Tibaijuka.

Alilitaja Mwananchi na magazeti mengine pamoja na baadhi yaliyaitwa kuwa ni ya uchwara ambayo alidai kuwa yamenunuliwa na wabaya wake.

Alidai kuwa Mdee alidanganya bungeni kuwa Profesa Tibaijuka ni mporaji ardhi za wananchi kuanzia jimboni na kama isingekuwa ni kinga ya mbunge kutoshtakiwa, angemfungulia mashtaka mahakamani.

Alisema waandishi wa habari wa magazeti hawaandiki mambo mema aliyofanya jimboni badala yake wamesimama kwenye kashfa ya Escrow lakini yeye hafanyi maendeleo yake kwa fedha hizo, bali ana pensheni ya Umoja wa Mataifa (UN).

“Fedha nilizopata Umoja wa Mataifa bado ninazo na Halima Mdee tutakuja kukutana mbele ya safari kama ni pesa ya kula bado ninayo na ile ya Escrow ya Rugemalila ni kuhemea mboga acheni kudanganyika,” alisema Profesa Tibaijuka.

Aliwaomba wananchi wa kata hiyo kumuunga mkono kwani licha ya kudaiwa kuwa ana umri mkubwa hivyo awaachie vijana, bado yumo na atagombea tena kuwaongoza wananchi akiwa mbunge.

Mdee ajibu mapigo

Akijibu shutuma dhidi yake Mdee alisema alichokisema ni cha kweli na kwamba anao ushahidi kuthibitisha madai yake hayo.

“Asiweweseke kwa kuwa hilo suala la uporaji wa ardhi ni la kweli na wala sikumuonea.”

Salama Jabir na Solo Thang wameyasema haya yawafikie mashabiki wa Ali Kiba na Diamond

$
0
0
Upinzani unaokuzwa na mashabiki kati ya Diamond Platnumz na Ali Kiba kwenye mitandao ya kijamii umepelekea Mastaa wa Tanzania kuanza kujitokeza hadharani na kuwaweka mashabiki hawa sawa kwa kuamini wamevuka mipaka kwenye ushabiki.

Mtangazaji wa TV show ya Mkasi Salama Jabir na msanii mkongwe bongoflevani Solo Thang ni miongoni mwa waliozipaza sauti zao June 30 2015.

Kupitia kwenye ukurasa wa twitter Salama Jabir aliandika ‘Wabongo tumekua wakosoaji mpaka wasanii wanajishtukia, hakuna “zuri kabisa” kwenye macho yetu… tuwaache wasanii wawe “Wasanii” nadhani!

Jana tulikua tunaongea na wana job, Ali Kiba hakuwa mtu wa vioo vikali, yeye alikuwa anatoa audio kali na video ya Mwananchi kamaliza, zama zimebadilika mpaka anakwea pipa kwenda kutoa kideo kikaaali tushukuru, kapendeza, rangi nzuri! mengine tuyaache..’  kauli ya Salama Jabiri


Upinzani huo ulioanzishwa na makundi yanayojiita (TeamAliKiba na TeamDiamond) yalimkwaza pia mkongwe wa Hip Hop Solo Thang na kuandika..’Ukiweka habari au picha au muziki wa msanii muyu mashabiki  wa yule wanakutukana!  kwanini? ? hii burudani tu isiwe uhasama, tujivunie sanaa yetu..’

Banza Stone alivyoita Waandishi wa habari kukanusha kifo, kusema anachoumwa na mengine. (video)

$
0
0
Mwimbaji wa longtime kwenye muziki wa dance Tanzania Banza Stone alikutana na Waandishi wa habari wachache kwa ajili ya kukanusha taarifa za kuzushiwa kifo, maisha yake kwa sasa na kilichokua kinamsumbua kiafya.

Muda wa Jakaya Ndio Umeisha, Babu Seya Ndio Basi Tena?

$
0
0
Wanamuziki Nguza Viking na Papii Kocha wanaotumikia kifungo cha maisha jela, wamemuomba Rais Jakaya Kikwete awasamehe kwa makosa waliyofanya.

Nguza na mwanaye Papii walitoa ombi hilo kupitia wimbo wakati wakitumbuiza katika maadhimisho ya Siku ya Magereza yaliyofanyika Chuo cha Magereza Ukonga jijini Dar es Salaam.

Ombi hilo waliliwasilisha kupitia kwa Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mathias Chikawe aliyekuwa mgeni rasmi kwenye sherehe hizo ambapo Nguza maarufu Babu Seya na mwanawe, Johnson Nguza (Papii Kocha), walitumbuiza wakiwa na Bendi ya Wafungwa. Walimwomba Waziri Chikawe kufikisha ombi lao kwa Rais Kikwete.

TAARIFA HII NI YA TEREHE 21/JUNI/2014. Mhe. Rais anamaliza muda na juzi alikuwa kule magereza akitunuku nishani. Alisema akisamehe baada ya muda wanaorudi kifungoni ni zaidi ya aliowasamehe.
Viewing all 104795 articles
Browse latest View live




Latest Images

<script src="https://jsc.adskeeper.com/r/s/rssing.com.1596347.js" async> </script>
<script src="https://jsc.adskeeper.com/r/s/rssing.com.1596344.js" async> </script>