Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104809 articles
Browse latest View live

Rais Bora Africa Apatikana...Huwezi Amani Anatoka Afrika Mashariki.....

$
0
0
Muungano wa Wanavyuo Barani Africa AASU umemchagua Rais Uhuru Kenyatta wa Kenya Kuwa Rais Bora wa Bara la Afrika 2014/2015 ...
Kabla yake alikuwa Rais Paul Kagame wa Rwanda...

Davido atoa uthibitisho mwingine kuwa hakuna ‘beef’ kati yake na Diamond

$
0
0
Bado una wasiwasi juu ya maelewano kati ya muimbaji wa Nigeria, Davido na Diamond? Pamoja na Diamond kujibu kwenye Interview mbalimbali kuwa hawana tatizo, Davido naye ametoa uthibitisho mwingine kuwa hakuna ‘beef’ kati yao.

Ni jambo gumu kupost kitu kinachomhusu mtu ambaye hamna maelewano, ndio maana kwa post hii ya Davido watu wanapaswa kufahamu kuwa jamaa hawa wawili wanaiva chungu kimoja, na tutarajie kuwaona wakitumbuiza tena pamoja kwenye tuzo za MTV mwezi huu.

Baada ya MTV kutaja majina ya wasanii wa Afrika watakaotumbuiza wakati wa utolewaji wa tuzo za MAMA akiwemo Davido na Diamond, Davido alipost picha ya performance aliyofanya na Diamond mwaka jana kwenye tuzo hizo.

Katika picha hiyo ameandika:

“PERFORMING AGAIN LIKE THIS AT ‪#‎MTVMAMA2015‬ !! TOO MUCH BLESSINGS…”

Diamond Azidi Kumpa Machungu ALI KIBA Amevunja record kashika No.1 kwenye Top 10 ya Afrika

$
0
0

Kwenye Top 10 ya muziki mkali wa Afrika ambayo hufanyika kila Alhamisi kwenye kituo cha TV cha Ufaransa ambacho kina mamilioni ya Watazamaji Afrika (TRACE TV Urban) July 2, 2015 single ya ‘Nana’ Diamond ft Mr Flavour imeshika nafasi ya kwanza

Eti Wachezaji wa Taifa Stars Walikuwa Hawakuelewa Kingereza?, Cannavaro Atoboa Siri

$
0
0
Kumekuwa na headlines tofauti tofauti katika mitandao zikiwahukumu wachezaji wa timu ya ‘Taifa Stars’  kutojua lugha ya kingereza ndio chanzo iliyopelekea kutofanya vizuri uwanja na kutoelewana na aliyekuwa kocha mkuu wa timu ya taifa ya Tanzania ‘Taifa Stars’  Mart Nooi.


Sasa leo July 2, 2015 Nadir Haroub a.k.a  Cannavaro amefunguka na kuelezea hujuma hizo…‘Sisi wachezaji tunaumia zaidi kuliko mashabiki kwasababu maisha yetu tunategemea mpira tunapopata matokeo mabaya familia zetu zinakaa na njaa, kwanza tunakosa fedha tunazoahidiwa, tunakosa pia kuthaminiwa na watu nje unajua unapofanya vibaya watu hawawezi kukusapoti sisi tunaumia zaidi.

Kwa suala la mwalimu kusema kuwa watu hawajui kingereza sio kweli, kwani suala la mpira ni vitendo mwalimu anakuambia fanya hivi hivi na mchezaji unaelewa nini cha kufanya, matokeo yanatokea kwenye mpira unaweza ukashindwa au ukafungwa, sisi tunaumia sana na tunataka matokea mazuri ili tupate kuheshimika kwenye vilabu vyetu. Tutajitaidi na nitawaambia wenzangu to force kila game ambayo itakuwa mbele yetu tuweze kupata matokeo mazuri, sisi kwanza tunatarajia kuanzia mechi na Uganda tukishinda moja tukishinda mbili ilimradi turudishe imani kwa watanzania…’alisema.

MAUAJI ya Kusikitisha Mwanaume Amuuwa Mwenzake Kwa Kutumia KISU Wakigombea Mwanamke

$
0
0
WATU watatu wamekufa katika matukio matatu tofauti katika Wilaya za Tarime na Rorya akiwemo mtu aliyeuawa wakati wanagombania mwanamke.

Waliokufa ni Chacha Mwita (24) aliyechomwa kisu kifuani na mwenzake wakigombea mwanamke wa baa huko Sirari.

Wengine ni Juma Nguka (25) aliyeuawa na watu wenye hasira baada ya kutuhumiwa kupora pikipiki yenye namba za usajili MC 936 ACA, mali ya Erick Jumanne mkazi wa Kijiji cha Mkoma.

Tukio lingine ni kufa maji kwa mvuvi aliyefahamika kwa jina la Wambura Maregeri (30) mkazi wa kijiji cha Muhundwe aliyekufa maji baada ya Boya kutoboka.

Kaimu Kamanda wa Polisi Tarime Rorya ACP Swetbert Njewike alisema kuwa matukio hayo matatu ya vifo yalitokea Julai mosi mwaka huu katika Wilaya za Rorya na Tarime.

Akielezea tukio la baa ambalo Mwita aliuawa, alisema siku hiyo marehemu akiwa baa moja katika mji wa Sirari, Tarime, nyakati za saa moja jioni kulitokea ugomvi kati ya marehemu na mtu mwingine ambaye hajafahamika jina lake wakigombania mwanamke aliyetajwa kwa jina moja la Dina.

Alisema wakati wa ugomvi huo, Mwita alichomwa kisu kifuani na aliyefanya kitendo hicho alitoroka ambapo majeruhi huyo alitokwa damu nyingi na alipofikishwa Hospitali ya Wilaya Tarime alifariki dunia.

Alisema Nguka yeye alipoteza maisha baada ya kushambuliwa na wananchi wenye hasira baada ya kudaiwa kuiba pikipiki.
 
Akasema Maregesi alikufa maji baada ya boya lililotengenezwa kienyeji alilokuwa anatumia katika uvuvi kutoboka na kuzama majini hali iliyopelekea kifo chake.

“Jeshi la Polisi linafanya msako wa watuhumiwa wa mauaji Chacha Mwita na watuhumiwa waliohusika katika mauaji ya Nguka ili waweze kufikishwa katika vyombo vya Sheria,” alisema.

Aliwaonya wananchi kutojichukulia sheria mikononi ya kuwauawa watu wengine badala yake wawafikishe katika vyombo husika vikiwemo vya Dola.
 
 Aliwaomba raia wema kutoa taarifa mara watakapowaona watuhumiwa hao wa mauaji hayo ii wakamatwe.

Wazazi wa Mwigizaji ROSE NDAUKA Wacharuka....Hawamwelewi Mtoto Wao Kuhusu Wanaume..Wampa Onyo

$
0
0
Staa wa filamu Bongo, Rose Ndauka hivi karibuni amewekwa chini na familia yake na kupewa onyo kuhusu wanaume pamoja na maadili.

Kwa mujibu wa chanzo, Rose aliambiwa maneno mengi na familia yake ikimtaka ajirekebishe na haswa ajitume zaidi katika kazi zake anazofanya.

“Familia yake imeamua kumuweka chini na kumwambia mengi kuhusu maisha haswa ikimtaka ajirekebishe tabia yake kwa ujumla,” kilisema chanzo.

Rose alipotafutwa kuweka wazi juu ya hili, alifunguka;
“Kila familia ina utaratibu wake, kwahiyo mimi kuwekwa na familia na kupewa onyo wala siyo suala la ajabu.”

Mwanamuziki AFANDE SELE Ajigamba..Adai yeye Akiingia Bungeni Atakuwa Tofauti Sana...Atafanya Haya Mambo Kujitofautisha na Wengine

$
0
0
Afande Sele amesema akiingia bungeni hawezi kuwasahau wasanii wenzake kama walivyosahauliwa na wasanii wabunge waliotangulia kuingia mjengoni.

Rapper huyo  atawania kiti cha ubunge wa jimbo la Morogoro Mjini kwa tiketi cha ya chama cha ACT na amesemakuwa akiingia bungeni wasanii watarajie mambo makubwa kutoka kwake.

“Lengo langu kubwa kwa wasanii ni kupigania haki za wasanii,” Amesema  Afande Sele

“Nimegundua tukizungumzia haki za wasanii kwenye muziki kwa kuimba tu, hakuna kitachofanyika. Viongozi hawana shinikizo la kutekeleza, wanazungumzia tu kidogo halafu wanaacha.

 "Lakini nimeona ukiingia bungeni wasanii tutashiriki moja kwa moja kwenye utungaji sheria za nchi.

 "Suala la haki za wasanii nitakuwa niko nalo karibu sana na nitalipigania kwa namna yoyote kwa sababu nipo kwenye chombo cha maamuzi na nina rungu mkononi,” ameongeza msanii huyo.

“Lakini leo hii hata nikiwa nazungumza sina silaha yoyote, lakini tukiingia bungeni tunaweza kupaza sauti na zikasikika kwa sababu tupo kwenye chombo cha sheria na kina mamlaka na uwezo.

"Unajua kila anayeingia bungeni unakuta baadaye anabadilika, mimi nina upeo mkubwa tofauti na wabunge wanaomaliza muda wao. Inaonyesha waliingia kwenye siasa kwaajili ya kutafuta maslahi. Kwahiyo wasanii watarajie kuona sheria za haki miliki zikipatikana au zile zilizopo zikifanyiwa marekebisho,” amesisitiza.

“Kwa sasa hivi bungeni hakuna mtu mwenye uchungu na sanaa, wasanii ambao walibahatika kuwa wabunge wameingia bungeni nao wamegeuka mafisadi vilevile.

"Wamekuwa wawekezaji wa biashara, wamedharau shida za wasanii. KwaHiyo mimi nafikiri bungeni kulikuwa hakuna wasanii ambao wanatuwakilisha, wasanii tunaotaka kuingia bungeni sasa hivi tuna wito. Kwahiyo watu wategemee kuona mabadiliko makubwa sana kwenye sanaa.”

Katika hatua nyingine, Afande amesema kwa sasa hatoweza kutoa wimbo wowote mpaka uchaguzi utakapopita.

“Ningependa sana mashabiki wa muziki wangu wasubiri uchaguzi upite ndio wasikie kazi mpya kwa sababu tayari akili na mawazo na malengo yangu yapo kwenye uchaguzi. Mimi nimeona nisiwa-disturb kwa kitu chochote mpaka uchaguzi upite.
 
"Kwa sababu hili ni jambo muhimu sana linatokea kwenye taifa na ni maisha yao. Kwahiyo watu wajitokeze kujiandikisha pamoja na kupiga kura ili kuwachagua viongozi wanaowataka.”

Vibinti vyakosa Haya...Mzee MAJUTO Atoa Shutuma Kali..Adai Vibinti Vinamtongoza Bila Aibu

$
0
0
Staa mkongwe kunako filamu Bongo, Amri Athuman ‘Mzee Majuto’ amefungukia shutuma anazopewa na mashabiki wake kwa kupenda kuonekana na ‘vibinti’ kuwa wanamshobokea mwenyewe.

Mzee Majuto ambaye kifani ni bingwa wa komedi amesema, kutokana na kazi yake ya uigizaji imemfanya kuzimikiwa haswa na mabinti.

“Sijawahi kumshobokea binti yoyote ila wenyewe ndiyo huwa wananishobokea kutokana na uigizaji wangu,” amesema Mzee Majuto.

Hivi karibuni, Mzee Majuto alidaiwa kuoa binti mdogo ambaye ni sawa na mjukuu wake mwenye umri wa miaka 18 akidai kuwa sheria ya dini inamruhusu kufunga ndoa na wake wanne.

Huku Akidaiwa Siku Hizi ni Tajiri..LULU MICHAEL Amwaga Minoti Ukumbini Kwenye Pati..Noti zatolewa Kwenye Maboksi..Ushahidi wa Picha Upo Hapa

$
0
0
Lulu Akijiandaa kumwaga minoti iliyopo kwenye box
ULE msemo wa ‘pata pesa tuone tabia yako’ huenda ni kweli, kufuatia staa wa sinema za Kibongo, Elizabeth Michael Kimemeta ‘Lulu’ ambaye siku hizi anaitwa ‘tajiri mtoto’ kutokana na kuwa na fedha na kumwaga ‘minoti’ (pesa) kwenye pati, Ijumaa ‘Kubwa’ lilikuwepo.

Kwa mujibu wa shushushu wetu, ishu nzima ilijiri usiku wa Ijumaa iliyopita kwenye pati ya ‘bethidei’ ya mwanamuziki wa Bendi ya The African Stars ‘Twanga Pepeta’, Kalala Hamza ‘Kalala Junior’ iliyofanyika ndani ya ukumbi wa hoteli moja yenye hadhi ya nyota tano iliyopo Masaki jijini Dar ambapo mastaa na mapedeshee kibao wa ‘mujini’ walihudhuria.

LULU AMWAGA MINOTI
Ilielezwa kwamba, Lulu alifanya ‘kufuru’ hiyo baada ya waalikwa wa pati hiyo kumaliza kula na kunywa ambapo ikafika wakati ratiba ikaelekeza watu kutoa zawadi kwa kadiri watakavyojisikia au kujaliwa nacho.

Ndipo Lulu ambaye siku hizi amekuwa hapendi kujitokeza kwenye shughuli, alipita mbele na kuanza kumpa noti nyekundu ‘Msimbazi’ aliyekuwa akizikusanya kwa niaba ya Kalala Junior kwa staili ya moja-moja.


Shuhuda wetu alidadavua kuwa, kila aliponyoosha mkono kutoa Msimbazi mmoja, watu walimkodolea macho wakiamini hawezi kufika ‘kilo moja’ (Sh. 100,000).

MANENO YA WATU
“Lulu bwana, anajitutumua tu. Hawezi kumpa laki moja Kalala Junior. Kwanza sidhani kama siku hizi ana pesa za kufanyia fujo,” alisema mwalikwa mmoja, mwenzake akampinga.“Wee! Lulu siku hizi ana pesa. Wenzake wanamuita tajiri mtoto. Ndiyo maana ana jeuri ile,” alisema mwingine miongoni mwa waalikwa hao.

Hata hivyo, Ijumaa halikuweza kufuatilia noti hizo katika mtiririko wa kutoka ili kujua ni shilingi ngapi bali baada ya kumaliza, lilimfuata Lulu ili kumuuliza ambapo hakuwa tayari kutoa ushirikiano.

Mtu wa karibu na Lulu ambaye aliomba jina lihifadhiwe, aliliambia Ijumaa kuwa, Lulu siku hiyo alitenga shilingi milioni moja na laki nne (1,400,000) kwa ajili ya kumtuza Kalala Junior tu.“Hawezi kusema, lakini mimi ninavyojua alitenga milioni moja na laki nne. Lulu kwa sasa yuko vizuri kipesa,” alisema mtu huyo na kuachana na Ijumaa.

KWA NINI LULU ALITOA KIASI HICHO CHA PESA KWA KALALA JUNIOR?
Habari za ndani zinasema kuwa, Lulu aliamua kumwaga mkwanja huo kwa vile, mwanamuziki huyo kwa sasa ni mpenzi wa shoga kipenzi wa Lulu, Rose Alphonce ‘Muna’.

Wakati wa matatizo ya Lulu kuswekwa Magereza ya Segerea, Dar kwa madai ya kumuua bila kukusudia aliyekuwa staa wa filamu Bongo, marehemu Steven Kanumba, Muna ndiye aliyebeba jukumu la kumpelekea chakula mahabusu huyo kila siku.

Lakini pia, Lulu alipotoka gerezani kwa dhamana, alikwenda kuishi kwa muda nyumbani kwa Muna, Mwananyamala jijini Dar.

MAPEDESHEE NAO
Baada ya Lulu kumaliza kutuza minoti yake, mapedeshee waliokuwa ukumbini humo nao walicharuka ambapo walichomoa minoti yao na kuimwaga kwenye maboksi mawili na kutolewa ukumbini hapo na wapambe.

KUMBE KALALA ALIFANYIWA SAPRAIZI
Kwa mujibu wa chanzo chetu ndani ya ukumbi huo, Kalala Junior akiwa hajui chochote, mpenzi wake huyo ambaye pia ni msanii wa filamu, alimtaka watoke kwa ajili ya kupata chakula cha jioni ambapo walikwenda kwenye hoteli hiyo.


Baada ya kufika, Kalala alipokelewa na watu waliokuwa ukumbini hapo huku wakimmwagia maji, bia na soda hadi akawa chapachapa huku wakimwimbia nyimbo za ‘hepi bethidei tu yuuu…’ jambo ambalo hakulitegemea.
Kutokana na kulowa chapachapa, Muna  alimchukua hadi kwenye chumba alichochukua mapema ndani ya hoteli hiyo ambapo alimbadilisha nguo.

Muna alimvalisha Kalala suti yenye gharama ya shilingi 2,800,000, viatu vya shilingi 800,000 (inadaiwa ni vya kutoka Italia), vyote hivyo alivinunua mwanadada huyo ikiwa ni zawadi kwa mpenzi wake.
Wawili hao walirudi ukumbini ambako walipokelewa kwa shangwe huku mtangazaji maarufu Bongo, Maimartha Jesse ‘Mai’ akiwa ni mshehereshaji (MC) wa shughuli hiyo ambayo kwa kuangalia tu iligharimu mamilioni ya shilingi.

KALALA AMFUNGUKIA MUNA
Kufuatia mbwembwe hizo za Muna, Kalala alitumia nafasi hiyo kumtambulisha rasmi kwamba ndiye mchumba’ke wa sasa na kumshukuru kwa kumwandalia sherehe kubwa na ya gharama kwani hakuwahi kufanyiwa hapo awali.

MAIMARTHA ATIA NENO
Naye mshereheshaji wa shughuli hiyo, Maimatha aliliambia gazeti hili kwamba, sherehe hiyo ilikuwa ya aina yake na yeye alilipwa zaidi ya shilingi milioni moja.

Source:GPL

Wagombea Urais Wanne (4) CCM washindwa kurejesha Fomu Dodoma...

$
0
0
Wagombea 38 kati ya 42 wanaoomba kuteuliwa na CCM kugombea Urais,wamerejesha fomu hadi saa 10:30 jioni julai 2,2015.Kati ya hao Wagombea wanne waeshindwa kurejesha fomu.

Hapa chini ni majina ya wagombea urais ambao wameshindwa kurejesha fomu hizi.

Wagombea ambao hawajarejesha fomu ni pamoja na Dr Kalokola, Hellena Dina Elinawinga, Anthony Chalamila na Peter Nyalali

Baada ya kukamilika kwa kazi ya urejeshaji wa fomu, makada hao 38 watasubiri kufanyika kwa vikao vya juu vya maamuzi.

Vikao hivyo ni pamoja na Sekretarieti ya Halmashauri Kuu ya Taifa itakayokutana Julai 7 na Kamati Kuu (CC) itakayokutana Julai 8, chini ya Mwenyekiti wa CCM Taifa, Rais Jakaya Kikwete, ikifuatiwa na kikao cha Nec Julai 9, mwaka huu.

Mchakato wa kumpata mgombea urais atakayepeperusha bendera ya CCM katika uchaguzi mkuu wa mwaka huu, utahitimishwa Julai 11, mwaka huu na Mkutano Mkuu wa Taifa CCM ambao ni maalum kwa ajili kulipigia kura jina la mgombea mmoja kati ya watatu.

Mwanaume: OA Mwanamke Anayekupenda, Sio Uliyemtengenezea Mazingira Akupende..Utajuta Mbeleni...

$
0
0
Habari za wakati huu, Muwazima?..

Baada ya salamu, mimi mwaka huu nimedhamiria kuwakomboa wanaume wenzangu kwenye majanga ya mapenzi, maana wengi katika wao, wanasumbuka mno! Naomba nianze kuifafanua hiyo heading hapo juu. Juzi kati hapa nilileta tofauti kati ya kupendwa na kuonyeshwa mapenzi, wengi walielewa, lakini wengine bado wanaendelea kuwang'ang'ania waonyeshaji mapenzi, but that'z none of my business! Cha msingi mimi nimewazindua.

Leo, tuje hapa, kwa mara nyingine tena! Ewe ndugu yangu, mwanaume mwenzangu, kwanini uoe mtu asiyekupenda? Mtu uliyemtengenezea mazingira akupende kwanini? Unaoaje mwanamke uliyemtongoza miezi sita? Mwaka mmoja? Miaka miwili? Mwanamke mwenye mapenzi na anayejua haswa thamani ya mapenzi hatongozwi miezi 6 au mwaka mzima banaa. Mimi hata mwezi kwanza siwezi naanzaje kukuchombeza mwezi mzima? Unataka usome nini kutoka kwangu?

Hawa wanawake wa kutongozwa muda mrefu hawajatoa majibu ni wanawake wanaokuchunguza na kukulinganisha na watongozaji wengine na wewe bado unang'ang'ania tu kutongoza.

Hapa kuna matokeo mawili muhimu sana:
1. Kuna uwezekano mkubwa akakukubalia baadae kwa moyo mmoja tu, tena kwa nia njema. Hii ni kwa sababu umemtengenezea mazingira, amekuona unafaa, na katika kipindi hicho kirefu cha kumbembeleza na kumuomba majibu kuna mengi umemtendea.

Ameyakubali, umenunua sana vocha, out sana umemtoa, umejali na kuzitambua sana baadhi (kama si zote) ya shida zake, sasa asikupende kwanini?! Na principle ni kuwa Moyo umeumbwa kumpenda anayeufanyia wema na kumchukia anayeutendea mabaya.Sasa unataka ufanye mazuri halafu moyo usikupende?! Utakupenda tu. Lakini Je, unadhani wewe ndo mfanyaji mazuri peke yako? Mazuri uyafanyayo wewe unahisi ndo yanayomtosheleza?! Be careful!

2. Kwa kipindi chote hicho unachong'ang'ana kutongoza, labda miezi 6 yako au mwaka, atakuelewa na kuusoma udhaifu wako wootee.Halafu atakukubalia! Ataishi na wewe kimjinimjini na kukufanya zoba huku akiendelea na vidume vingine kimyakimya bila wewe kushtukia! Utashtukia vipi sasa wakati ulipokuwa unabembeleza ukubaliwe ulijisahau na kuanza kujionyesha jinsi ulivyo na udhaifu wako wote! Umshtukie? Wapi.

Hivi hujui kuwa wakati wa kutongoza ndo mwanaume anaposema vingi vya ukweli kumuhusu yeye? Hata kama wewe ni mdanganyaji mzuri, jichunguze ukiwa unatongoza, unavyofunguka. Sasa unaanzaje kutongoza miezi sita? Ili ufunguke vyote kuhusu wewe na ukoo wako? Au unataka ugundue nini. Hayo 1 & 2 hapo juu yote hayapo upande wako mwanaume mwenzangu, kwahyo jiongeze baba.

Nahitimisha sasa;

Dalili kuu ya kwanza ya mwanamke wa maslahi/asiye na mapenzi ya kweli ni kutongozwa muda mrefu! Chunguza vizuri utajijibu.Yaani ukiona unabembeleza wee ujue utkubaliwa, maana wakibembelezwa sana hawakatai hao, anaweza akakukubalia kwa sababu ya kukuonea huruma tu ili uridhike, au kwa ushauri tu wa mashoga zake baada ya kuwaelezea jinsi unavyopata tabu kuwa makini sana.

Hii statement ya kizungu niliiokota sehemu, nadhani inaweza kukufungua akili kidogo:
Decision Making is easier when there is no Contradictions into your value system .
Kwahiyo ukiona decision making yake ni ngumu, ujue hapo kuna kinyume na hiyo statement hapo, Contradictions zimetawala. Angalia sana kijana mimi ushauri wangu, please.

Usijiendekeze bana, tongoza, bembeleza, onyesha nia ya dhati. Kama kweli maneno yanatoka moyoni, yataingia tu kwenye moyo wake tena kirahisi.Kama atashawishika atarespond mapema tu na kama hataki na anajitambua atakwambia "Mi nina mpenzi/occupied" usilazimishee. Utakua unamtengenezea mazingira tutarudi kulekule! Kwani wewe ukiwa na msichana ungependa atoke na msela mwingine? Sasa kwanini wewe unataka kutoka na mademu wa wenzio?

Akikwambia haiwezekani au nina mpenzi, geuka kulia na kushoto vuka barabara hamia upande wa pili huko, wapo kibao. Wanaume sisi ni wachache kuliko wanawake, sasa unaanzaje kubembeleza mtu miezi au miaka, ili? Akutangaze au?! Wengine wanabembeleza sana eti wanaogopa kuonekana wamekataliwa!

Wee ni bora ukataliwe kuliko kujifanya kidume halafu ukaanza kutengeneza mazingira upendwe usipopendwa madhara yake ni makubwa. Nimeeleza hapo juu!.Kwanza ukweli ni kuwa watoto wa mjini ndo wanaogongwa na magari, wale wa kijijini wanachukua tahadhari sana kwenye kuvuka, lazima waangalie kushoto, mara kulia ndo avuke. Sasa wewe wa mjini gani unaogopa kutoswa bana?! Ngoja nkale daku nilale, nikimaliza UE nitarudi hapa kuwapa trick jinsi ya kutokea siku ya kwanza ya kutongoza.

Rafiki wa Mke Wangu Alitaka Kunifitinisha na Mke wangu, ila Nimemuweza

$
0
0
Salam zenu wakuu,

Siku mbili kabla ya ramadhan kuanza nilikua na mihadi na binti mmoja ili tuvunje jungu kupisha mwezi mtukufu wa Ramadhan ili mwenzangu aweze kufunga kwa amani, yeye ni muslim mimi ni christian tukasema tuonane Sugar ray bar and guest house Temeke, mimi nilitokea kazini kwenda hapo, yeye alitokea Keko Magurumbasi.

Siku hizi nimeamua nitoke na watoto wa kiswahili maana hawana gharama ukimpa elfu tano tu anaenda kuhadithia ukoo mzima, na atayarudi mayenu hadi utakimbia na boxer kichwani. Tukiwa hapo sugar ray, tukiwa tumechangamka mno, na mziki mzito ukiporomoshwa na bendi ya nyimbo za copy huku yule binti akinibusu na kunikumbatia, akiwa ameniwekea miguu juu ya mapaja yangu huku akideka kike, ahamadi nageuza shingo kwa nyuma ilibaki kidogo nianguke nakutana uso kwa usona rafiki kipenzi wa mke wangu akiwa na kampani ya wanawake wenzie wakionekana kunisonta kwa vidole.

Nikamwambia yule mwanamke wangu disco limeingiliwa na mmasai tuondoke haraka.Tukaenda kuvunjia jungu Lelo guest house unubini, baadae saa tano usiku nikarudi kwangu.Nimepiga honi zaidi ya dakika ishirini hakuna aliefungua, nastukia sauti ya wife kwa ndani ya Geti ikisema Rudi huko huko sugar ray ukalale.Nikajua tu Rafiki mtu alipiga simu zamani kusema umbea.Hivi mtu unapotoa taarifa kama hiyo unategemea nini? Ndoa ya watu ife au? Nashukuru mungu wife alinielewa, maana nilisema rafiki ananihitaji siku nyingi mimi ndo namchenga, nashangaa unasikiliza taarifa zake wakati ananitaka.

Vita niliyowaachia huko ile ya Idd Amin haifai

Muziki wa Tanzania umepenya vipi wakati tunawakilishwa na msanii mmoja tu? – Dudu Baya

$
0
0
Dudu Baya anapingana na kauli kuwa muziki wa Tanzania umepenya Afrika.

Akiongea kwenye kipindi cha Siz Kitaa cha Clouds TV, rapper huyo amesema muziki wa Tanzania haujapenya kwakuwa anayeiwakilisha Tanzania ni mmoja tu – Diamond.

Amesema ili muziki wa Tanzania uweze kusemwa umepenya kimataifa ni lazima kuwepo na wasanii wengi wanaofanya vizuri kama ukubwa wa Diamond kwa sasa.

Amedai kuwa muziki wa Nigeria ndio uliopenya zaidi kwakuwa kuna wasanii wengi wanaofanya vizuri na wenye ukubwa sawa tofauti na Tanzania.

Rapper huyo amezitaja chuki, wivu na kubaniana ndio sababu kubwa za muziki wa Tanzania kushindwa kupenya.

Ali Kiba Kataja Sababu za Kwanini Hamfollow mtu Hata Mmoja Instagram

$
0
0
Ali Kiba 
Ali Kiba ni staa kwenye muziki wa Bongo Fleva.. kama wewe ni mtumiaji wa Instagram utakuwa umeona kwamba Ali Kiba haja-follow mtu yoyote ukitembelea mitandao ya kijamii ya Ali Kiba utaona ya kuwa ana mashabiki wengi wanaomfuatilia kupitia mitandao hiyo.

Katika post ya Instagram kwenye page ya Mseto East Africa ambao walikaa na kuongea na Ali Kiba na kumuuliza swali hilo, majibu yake ni haya hapa


  • “Yea si follow mtu kwasababu, kwanza kabisa nafanya kazi na watu wengi kuna akina TUVA kuna watu kibao lakini watu wa Media ndio tuko nao karibu,sasa wengine walikua waki complain nikawa naogopa zile lawama nilichoshauriwa na hao wenyewe kwamba ni heri ni si follow mtu na vile vile nilipenda ivyo kutokana na promotion ya ujio wangu ambao ulikuwa unakuja ili niweze ku concetrate na account yangu nijue mafans wangu wanataka kitu gani wanani advice kitu gani na pia imesaidia naona jinsi gani wako serious namimi kwasababu naongea nao,kuna wengine wananipa challenge kuna matusi uhmm ni vitu vya kawaida na vile vile wanapokuwa wananisema wananijenga wananitengeneza kiasi fulani,wananibadilisha ni wapi nimekosea naweza kubadilisha”

Diamond Platnumz Akiri Kumpenda Omotola wa Nigeria

$
0
0
Omotola
KING wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ ametengeneza kichwa cha habari nchini Nigeria baada ya kufunguka kuwa anampenda ‘vibaya’ staa wa filamu nchini humo, Omotola Jalade Ekeinde

Kwa mujibu wa chanzo kilichoambatana na Diamond katika ziara ya kimuziki iitwayo ‘Nana Tour’ nchini humo, staa huyo ambaye kwa sasa ni mpenzi wa mjasiamali maarufu, Zarinah Hassan ‘Zari The Boss Lady’ amekuwa akiumizwa na penzi la Omotola kitambo sana lakini hakuwahi kuzungumza katika vyombo vya habari.

Diamond Platnumz

  • “Diamond ana maumbo yake flani hivi amazing ambayo huwa anayapenda, siku nyingi sana kabla hata hajakutana na Zari, alikuwa akituambia watu wake wa karibu kwamba miongoni mwa wanawake mastaa ambao anawatamani awaweke kwenye himaya ya penzi lake ni Omotola.



  • “Alisema anampenda kwa kila kitu kuanzia ufanyaji kazi wake, umbo lake na hata umaarufu mkubwa alionao ndani na nje ya Bara la Afrika,” kilisema chanzo hicho.


Baada ya chanzo hicho kueleza habari hiyo, mapema wiki hii, mtandao wa nigeriafilms.com ulithibitisha maneno hayo kwa kuposti habari iliyobainisha Diamond anampenda Omotola sanjari na mastaa wengine wawili wa Nigeria anaovutiwa nao kimapenzi.

Akiwa hewani alipokuwa akihojiwa na redio moja jijini Lagos, Diamond aliweka bayana kuwa anateswa na penzi la mastaa watatu Nigeria, Omotola, Tonto Dikeh na Genevieve Nnaji.


  • “Jamaa kitambo sana anateswa na penzi la Omotola sasa leo kaongeza na wengine wawili na ninavyomjua hashindwi kufanya kweli ingawa nina wasiwasi kwa Omotola na Tonto maana wana waume zao labda ajiweke kwa Genevieve ambaye hajaolewa,” kilikazia chanzo chetu.


Diamond hakupatikana ili kusikia kauli yake juu ya ishu hiyo.

Chanzo: GPL

Je Unajua nini Kinaendelea Kuhusu ile Kesi ya Mchungaji Gwajima Kumtukana Askofu Pengo? Nimekuwekea Hapa Kinachoendelea

$
0
0
Askofu Gwajima
MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu jana imeshindwa kumsomea maelezo ya awali Askofu wa Kanisa la Ufufuo na Uzima, Josephat Gwajima na wenzake wanaokabiliwa na kesi ya kutumia lugha ya matusi na kushindwa kuhifadhi silaha.

Kesi hiyo ilitajwa jana kwa ajili ya washitakiwa kusomewa maelezo ya awali lakini iliahirishwa kwa kuwa Hakimu Mkazi Wilfred Dyansobera anayesikiliza kesi hiyo hakuwepo mahakamani.

Hakimu Mkazi, Thomas Simba aliahirisha kesi hiyo hiyo Julai 20, mwaka huu kwa ajili ya washitakiwa hao kusomewa maelezo ya awali mbele ya Hakimu Dyansobera.

Mbali na Gwajima washitakiwa wengine, ni Mlinzi wake, George Mzava, Msaidizi wake, Yekonia Bihagaze (39) na Mchungaji Georgey Milulu (31) wanakabiliwa na shitaka la kukutwa na silaha pamoja na risasi kinyume cha sheria.

 Katika kesi ya kwanza namba 85, Gwajima anadaiwa kati ya Machi16 na 25, mwaka huu katika Viwanja vya Tanganyika Packers Wilaya ya Kinondoni Dar es Salaam alitoa lugha ya matusi dhidi ya Askofu wa Kanisa Katoliki Mwadhama Polycarp Kardinali Pengo akimueleza Askofu kwamba ni mtoto, mpuuzi asiye na akili katika namna ya kwamba ingeleta uvunjifu wa amani.

Katika kesi nyingine namba 84 , Gwajima anakabiliwa na mashitaka ya kushindwa kuhifadhi silaha na risasi jambo ambalo ni kinyume cha sheria ya uhifadhi wa silaha za moto.

Anadaiwa kati ya Machi 27 na 29, mwaka huu, ndani ya Jiji na Mkoa wa Dar es Salaam, alishindwa kuhifadhi silaha aina ya Beretta namba CAT 5802, risasi 3 za pisto na risasi 17 za shotgun.

Katika mashitaka mengine yanayowakabili washitakiwa wengine, inadaiwa Machi 29, mwaka huu katika Hospitali ya TMJ Mikocheni ‘A’ walikutwa wakimiliki silaha na risasi hizo bila ruhusa kutoka mamlaka husika.

Duuh huyu Mrembo ni sheedah..Mapozi yake yanaweza Mtoa Nyoka Pangoni

Hapa Ndio Chumbani Kwa Diamond Platnumz..Zari Anaonekana Amepozi Pale Kati Akimsubiri Diamond..Video

$
0
0
Nimekuwekea Video Hapa Ikionyesha chumba cha Gharama Kubwa cha Mwanamuziki  Diamond Platnumz katika Nyumba yake mpya iliyokotegetea...
Video Hii Hapa:

Kama Msichana Ushavuka Miaka 30 Bado Hujaolewa Jua Una Hali Mbaya

$
0
0
Kama wewe ni msichana na umeshavuka miaka 30 bado hujaolewa na wala huna mtu wa kueleweka ambaye amejitambulisha kwenu tambua kwamba una hali mbaya.

Wasichana wengi siku hizi wamekua na tabia ya kupenda vitu vya anasa hali inayopelekea sisi wanaume kuwaogopa kama ukoma.Mfano kutaka kufanyiwa shopping za bei mbaya,kumiliki simu za gharama zinazoanzia milioni moja na kuendelea,kupenda kuwa na mwanaume mwenye mshahara unaoanzia milioni tatu kwa mwezi na kuendelea n.k

Hali hii inasababisha hata sisi wenye kipata cha laki saba kushuka chini tuwaogope kwa kuamimini kwamba hatuna uwezo wa kukidhi mahitaji yenu hatimaye mnajikuta mnazeekea nyumbani kutaamakitaamaki miaka 45 hii hapa ambapo ndo kipindi cha menopause kwa mwanamke yeyote.

Msipende mteremko sababu hata huyo mwenye magari,majumba na kipato kikubwa hujui ametumia njia gani mpaka kupata hivyo vitu.Starehe hazina mwisho hivyo unapobweteka na starehe fahamu kwamba fainali uzeeni muda ndio refa.

Aliesikia na asikie na alieamua kupuuzia na apuuzie

Linnah Kama Shilole,Achorwa ‘Tattoo’ na Mpenzi wake Mpya.

$
0
0
Baada ya kuachana na aliyekuwa mpenzi wake wa siku nyingi aitwaye,Nagari,Staa wa Bongo Fleva,Linnah Sanga amepata mpenzi mpya aitwaye Williams Bugeme’Boss Mutoto’raia wa Uganda,ambaye hivi karibuni amechora ‘tattoo’ kwenye mwili wake yenye jina la msanii huyo.

Akizungumza na Clouds FM,Linnah alisema ilikuwa ni kit cha kushtukiza sana kwani mpenzi wake alimtumia sms kuwa anataka kumfanyia ‘surprise’ na afikirie ni kitu gani anataka kumfanyia alimjibu kuwa hajui ila amwambie tu.

‘’Alinitumia sms akaniambia ni ‘guess’ ni kitu gani anataka kunifanyia ‘surprise’ nikwambia mimi sijui basi akaniambia amechora tattoo yenye jina langu daah! Nilishtuka sana na pia nilikuwa na furaha sana,’’alisema Linnah.

‘’Unajua ni maamuzi magumu sana mtu kukuchora tattoo na mpaka anakuchora ujue basi ana mapenzi ya kweli na kama ni shabiki basi ni shabiki kwelikweli amezama kabisa,’’aliongeza Linnah.

Msanii mwingine aliyeweka rekodi ya kuchora tattoo ya jina la mpenzi wake na sura yake ni msanii wa Bongo Fleva,Nuh Mziwanda aliyechora tattoo ya mpenzi wake Shilole.
Viewing all 104809 articles
Browse latest View live




Latest Images