Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104795 articles
Browse latest View live

WANA CCM NISIKILIZENI..!! Kama Mlimkata LOWASSA Kwa Maslahi ya Watu Wachache Kwa Kutumia Akili Ndogo Basi Mnalo na Kazi Mnayo

$
0
0
WANA CCM NISIKILIZENI..!!
Nina ushauri kwa wana CCM wenzangu; Lowasa kuhamia CHADEMA msipaniki. Kama kweli tulimaanisha kuwa hafai, ana uchu wa madaraka, alikiuka kanuni na maadili ya chama, ni mwizi na tena ni fisadi basi inabidi tushangilie kuondoka kwake, kwani kuvuja kwa pakacha sio ndio nafuu ya mchukuzi? Ila kama tulimkata kwa maslahi ya watu wachache na ikiwa tulitumia akili ndogo kulikata jina lake basi itabidi tujilaumu wenyewe kwa lolote tusilolitarajia litakalotokea. Na tukiendelea kutumia akili ndogo za kudhani tutashinda kwa "magoli ya mikono", basi tunakwenda na maji mchana kweupe! Tukijidanganya kuwa matusi, kejeli, mipasho, maneno ya kwenye kanga na nyimbo za Komba kwamba zitabadilisha huu upepo, pia tutajikuta tunakuwa chama cha upinzani bila hata kujiandaa kisaikolojia. Mwana CCM utakuwa unajichanganya kuushambulia uamuzi wa Lowasa kuhamia CHADEMA kwa sababu kimsingi CCM yetu ilishabariki vijana kadhaa wamshambulie majukwaani ili aonekane hafai na hao vijana wakazawadiwa vyeo. Mtu tuliemuona hafai kwetu inatuuma nini akiondoka kwetu? Ukioa mke kisha ukamtuhumu mbele za watu kuwa ni mzinzi na mshirikina; kisha mkaachana na akaolewa na mume mwingine, unaanzaje kuhangaika nae tena huko alikoenda? Tuwaache wapiga kura waamue kama ni sisi CCM ama UKAWA. Hata Mh. Mwenyekiti JK alishasema kila mtu ana haki kuongoza hii nchi; tunategemea kushinda lakini haitakuwa ajabu UKAWA wakitwaa madaraka kutokana na makosa yetu kimkakati. Wana CCM tusipaniki, kukomaa kisiasa ni pamoja na kuhimili na kukubali usichotarajia!
Wenu,
Mfurukutwa wa Shina.

BREAKING: Hapa Ndipo Utaipenda Siasa ya Bongo... Unaambiwa Dr. Slaa, Tundu Lissu na John Mnyika hawamtaki Lowassa...Wasusia Mkutano Jana

$
0
0
The fact that Dr. Wilbord Slaa, John Mnyika and Tundu Lissu did not show up on yesterday Lowassa-Ukawa press conference is very crucial… I mean there must be something going on behind the curtains, let’s just wait and see!

KUMEKUCHA: Siasa ni tamuu! Nasikia Dr Wilbroad Slaa amekataa katakata kukubaliana na maamuzi ya kumleta Lowassa Sijui ni kweli Au?!

Anasema bora akae bila Chama kuliko kukaa chama kimoja na Lowassa. Na inaonesha anaungwa Mkono na Lissu, Mnyika na wengine wengi. Utakuwa mchezo wa kupishana huyu anatoka huyo anaingia! Ngoja tusubirie tuone mwisho wake

CCM Kumjibu LOWASSA Leo

$
0
0
Baada ya Mbunge wa Monduli Edward Lowassa kutangaza kuhama Chama Cha Mapinduzi (CCM)  na kuhamia Chadema jana katika ukumbi wa Bahari Beachi jijini Dar es salaam, chama cha Mapinduzi kimetoa taarifa ya kuzungumza na Vyombo vya Habari  leo.

Taarifa hiyo ya chama cha Mapinduzi haijafafanua kuwa ajenda itakuwa nini katika kikao hicho lakini kwa mujibu wa watafiti wa masuala ya kisiasa wanasema kuwa kikao hicho kitakuwa maalumu kwa ajili ya kujibu shutuma zilizotolewa na Lowassa kuhusiana na madai ya kuwepo uonevu wakati akiomba ridhaa ya kupeperusha Bendera ya CCM.

Mtandao huu utakujulisha kitakachojiri katika mkutano huo

Video: Tazama jinsi Kanye West alivyokutana kwa mara ya kwanza na baba mkwe wake tangu ajigeuze kuwa mwanamke

$
0
0
Kanye West amepelekwa na mke wake Kim Kardashian kwa mara ya kwanza kwenda kuonana na baba mkwe wake tangu ajigeuze kuwa mwanamke.


Yote hayo yameonekana kwenye reality show I Am Cait ya Caitlyn Jenner.

“I think this is one of the strongest things that have happened in our existence as human beings, that are so controlled by perception,” anasema Kanye kwenye clip hiyo.

“You couldn’t have been up against more.”

Star wa Empire Trai Byers (Andre Lyon) amvisha pete ya uchumba muigizaji mwenzie Grace Gealey (Anika)

$
0
0
Mastaa wa tamthilia ya Empire, Trai Byers na Grace Gealey sasa ni wachumba.

Chanzo kimeiambia US Weekly kuwa, Trai (32) alim-surprise mchumba wake Grace kwa kumvisha pete ya uchumba kwenye sherehe ya siku yake ya kuzaliwa akiwa amefikisha miaka 31, iliyofanyika Jumapili iliyopita, July 26.


Birthday ya Grace ambayo Trai alimvisha pete

Anika aliyecheza kama mchumba wa Lucious na Andre Lyon aliyecheza kama mtoto wa kwanza wa Lucious, walianza uhusiano wao baada ya kukutana kwenye series hiyo iliyojizolea umaarufu mkubwa ulimwenguni mwaka huu.

Hii Nimeiotoa Kwa Godbless Lema: Kwa nini UKAWA Wamemchukua Lowasa?

$
0
0
KWANINI CHADEMA WAMEMCHUKUA LOWASSA??
(Kama una akili ndogo usisome)
Mnamo mwezi February mwaka huu Umoja wa
Katiba ya Wananchi (UKAWA) waliingia ubia na
kampuni maarufu duniani inayojihusisha na tafiti
za siasa (Political Research) ijulikanayo kama
Greenberg Quinlan Rosner. (
www.gqrr.com/
).
UKAWA walitaka kujua kama wana nafasi ya
kushinda kwenye uchaguzi mkuu mwaka huu.
Kampuni hiyo ilimaliza utafiti wake mwezi May
mwaka huu na haya ndio yalikua majibu;
1. Ikiwa CCM itamsimamisha Lowassa kugombea
Urais, na UKAWA wakamsimamisha Dr.Slaa, CCM
watashinda kwa 58% dhidi ya 42% za UKAWA.
2. Ikiwa CCM itamsimamisha mgombea mwingine
asiye Lowassa kushindana na Dr.Slaa, CCM
itashinda kwa 54% dhidi ya 46% za UKAWA.
3. Ikiwa UKAWA itamsimamisha mgombea
mwingine ambaye si Dr.Slaa na CCM
ikamsimamisha Lowassa, CCM itashinda kwa
68% dhidi ya 32% za UKAWA.
4. Ikiwa UKAWA itamsimamisha mtu mwingine
ambaye sio Dr.Slaa na CCM ikamsimamisha mtu
mwingine ambaye sio Lowassa CCM itashinda
kwa 57% dhidi ya 43% UKAWA.
5. Ikiwa watu wote wa CCM wanaotaka Urais
wakiwekwa Pamoja na wa UKAWA wakawekwa
pamoja kisha wapigiwe kura za Urais kama
wagombea huru, Lowassa ataongoza kwa 14%
kisha Dr.Slaa atafuata kwa 09%, Membe 04% na
wengine chini ya hapo.
6. Ikiwa Lowassa atagombea kupitia UKAWA
atapunguza kura za UKAWA kwa 06% lakini
ataziongeza kwa 24%. Hii ina maana kuwa katika
watu 100 wa CHADEMA watu 6 hawataipigia kura
CHADEMA kwa sababu hawamtaki Lowassa.
Lakini Lowassa ataleta watu wapya 24. Yani
CHADEMA itapoteza kura 6 za wanachama wake
lakini itapata kura mpya 24 mpya.
DATA ANALYSIS
Ukisoma vzr huo utafiti hapo juu utagundua kuwa
Lowassa anaongeza umaarufu wa CCM kwa 18%.
Kwa hiyo kuondoka kwa Lowassa kutaipunguzia
nguvu CCM kwa 18%.
Sasa ikiwa CCM yenye Lowassa ina nguvu 58%
na UKAWA yenye Dr.Slaa ina nguvu 42%, maana
yake ni kwamba kumuondoa Lowassa CCM ni
kupunguza nguvu yao kwa 18% yani (58-18) =
40%.
Na kumleta Lowassa UKAWA ni kupunguza nguvu
ya UKAWA kwa 6% lakini kuongeza kwa 24%. Kwa
hiyo chukua 42 toa 06 kisha jumlisha 24 utapata
60%.
Sasa jumlisha 40% za CCM na 60% za UKAWA
kama haiji 100%??
Kwa hiyo UKAWA yenye Lowassa inashinda
uchaguzi kwa nguvu kubwa zaidi kuliko ambavyo
CCM ingeshinda ikiwa na Lowassa. Na hii ni kwa
sababu ujio wa Lowassa utaivunja CCM vipande
vipande.
Na ili uweze kuishinda CCM lazima uivunje
vipande kwanza. Huwezi kuishinda CCM ikiwa
imesimama imara.
Nchini Kenya KANU ilishindwa kirahisi baada ya
kuvunjwa vipande, Zambia UNIP ilishindwa baada
ya kuvunjwa vipande, na nchi nyingine za Afrika
vivyo hivyo.
Na njia rahisi ya kukivunja chama tawala ni kwa
kuondoa watu wenye ushawishi ktk chama hicho.
Fredrick Chiluba alikua mtu mwenye ushawishi
mkubwa akiwa UNIP lakini alipoondoka kwenda
MMD huo ndio ukawa mwisho wa UNIP maana
alikua na ushawishi na aliondoka na kundi kubwa
la watu.
Nchini Kenya akina Najib Balala, George Saitoti,
Musalia Mudavadi, Raila Odinga, Mwai Kibaki etc
walikua watu wenye ushawishi sana ndani ya
KANU. Lakini walipoondoka kwenda NARC hiyo
ndio ikawa mauti ya KANU.
Hii ni kwa sababu watu hawa walipoondoka,
waliondoka na kundi kubwa la wafuasi. Hivyo
basi hata Lowassa atasaidia kuivunja CCM na
hatimaye kuiwezesha UKAWA kushinda kirahisi.
Ikumbukwe Nyerere aliwahi kusema huwezi
kuishinda CCM imara yenye umoja. Kwa hiyo njia
rahisi ya kuishinda CCM ni kuivunja vunja
vipande. Na tayari kazi hiyo imeanza rasmi.
BAADA YA UTAFITI.
Baada ya ripoti ya utafiti huo wa GNR mnamo
mwezi May, UKAWA walikaa na kutafuta njia ya
kufanya. Walijua wazi CCM ikimpitisha Lowassa
UKAWA itaangushwa hata imsimamishe nani. Na
laiti CCM wangeona ripoti ya utafiti huo
wasingefanya kosa la kumkata Lowassa.
Wangempitisha ili waishinde UKAWA kirahisi.
Kwa hiyo UKAWA walikua wanafuatilia sana
mchakato wa CCM huku wakiomba usiku na
mchana wasimpitishe Lowassa. Na kweli Mungu
akajibu maombi yao.
Lakini UKAWA wakatafakari ikiwa
watamsimamisha Dr.Slaa kushindana na Magufuli
bado UKAWA itashindwa kwa kupata 46% dhidi ya
54% za CCM kama utafiti unavyoonesha.
Kwa hiyo ili kuishinda CCM ni kufanya nini? Ili
kuishinda CCM ni kumshawishi Lowassa ajiunge
na chama kimojawapo kinachounda UKAWA ili
apewe nafasi ya kugombea na kuiwezesha
UKAWA kushinda. Na ndivyo ilivyotokea.
Kwa hiyo kwa mujibu wa utafiti huo UKAWA
itashinda kwa 60% na CCM 40% kwenye uchaguzi
mkuu wa mwaka huu. Sasa nani asiyetaka
ushindi?
Siasa ni hesabu, siasa ni namba, siasa ni sayansi.
Kama hujui hesabu usifanye siasa.
Wavivu wa kufikiri wanaibua hoja uchwara za
ufisadi. Hivi fisadi ndani ya CCM alikua Lowassa
tu? Mbona baada ya kuondoka Lowassa bado
ufisadi umeendelea kushika kasi? Escrow,
Symbion, Meremeta, EPA etc, hivi vyote mbona
vimefanyika bila kuwepo Lowassa?
Acheni akili ndogo, tatizo sio mtu, tatizo ni
mfumo. Tukibadilisha mfumo tumebadilisha kila
kitu. Lowassa hata kama alikua fisadi kitendo cha
kujiunga UKAWA ni rahisi kuacha ufisadi wake
maana amejiondoa kwenye mfumo wa ufisadi.
Lakini kumuweka Magufuli kwny kundi la mafisadi
hata kama yeye sio fisadi lazima alinde mfumo
wa mafisadi uliomuweka.
Ni rahisi kumuokoa mwizi mmoja aliyeingia
kwenye kundi la Watakatifu, kuliko kumuokoa
mtakatifu mmoja aliyeingia kwenye kundi la
makahaba. Mwenye masikio na asikie."
ANGALIZO; Andiko hili nimelicopy na kupaste
kutoka JamiiForums, kwa hiyo unapocomment
hakikisha unazingatia kuwa haya si mawazo
yangu wala msimamo wangu.!
Malisa GJ

Lowassa Ajibu Tuhuma ya Richmond Rasmi, Amtaja Muhusika Hapa

$
0
0
Muda huu katika kukakiribishwa na kukabidhiwa kadi MH.LOWASSA ndani ya CHADEMA ,ameulizwa swali moja kuwa


Swali: Mh. Edward Lowassa unazungumiaje kuhusu kashfa ya Richmond?

Majibu Lowassa: Nipende tu kusema mimi kama waziri mkuu kwa kawaida ya sheria huwa ninaletewa mkataba muda wa mwisho kuupitia na kuupitisha huwa sihusiki na kuandaa mikataba,mwenye mamlaka ni waziri husika,hivyo baada ya kuletewa mkataba husika wa Richmond niliupitia na kiukweli niliuwekea shaka kwa sababu nilishawahi kuwa waziri wizara ya maji nina uzoefu na kuandaa mikataba,nilishauri mkataba huo uvunjwe lakini waziri wa nishati akawasiliana na "NGAZI YA JUU"na kulazimishwa kuupitisha mkataba huo.

Baada ya kugundulika kuwa mkataba huo ulikuwa na mapungufu mengi, "NILICHUKUA MAAMUZI MAGUMU KWA AJILI YA SERIKALI,na kubeba mzigo wote ndio maana hadi leo wanasema mimi ni FISADI WA RICHMOND,nipende kumaliza kwa kusema kwamba MWENYE USHAHIDI WA RICHMOND AENDE MAHAKAMANI AKANISHTAKI.

Mwigulu Ahojiwa Masaa Matatu na TAKUKURU..Kisa Hichi Hapa

$
0
0
Wanajamvi, kale kamchezo ka Mwigulu kujiona yupo juu ya sheria na kutoa rushwa kila kona ya Iramba imemtokea puani baada ya kukamatwa na kuhojiwa na Takukuru kwa muda wa zaidi ya masaa matatu.

Wagombea wenzake walijitoa katika kinyang'anyiro tangu tarehe 25 kwa madai ya kufanyiwa rafu hizo na kutoa malalamiko yao huku wakisubiri suala hilo kushughulikiwa ndipo warejee kwenye kampeni.

===========================

Ofisi ya Takukuru mkoani Singida imemuhoji kwa masaa kadhaa naibu waziri wa fedha na aliye kuwa mbunge wa Iramba Magharibi Mheshimiwa Mwigulu Nchemba, kwa tuhuma za kukiuka sheria ya garama ya uchaguzi na sheria ya kuzui na kupambana na rushwa.

Akiongea na waandishi wa habari mkuu wa Takukuru mkoani Singida Bwana Joshua Msuya amesema Mheshimiwa Mwigulu Nchemba amekiuka sheria ya kuzuia na kupambana na rushwa namba 11/2007 katika zoezi linalo ndelea la kura za maoni ndini ya vyama vya siasa.

Katika hatua nyingine Bwana Msuya amewatahadharisha wagombea wote wa ngaza mbalimbali watakae jihushisha na kutoa rushwa iwe ya fedha au vitu,vifaa vya michezo, madawati watakuwa wamekiuka sheria ya kuzuia na kupambana na rushwa namba 11/2007 na sheria ya uchaguzi cap.343 r.e 2002 na pia sheria ya garama za uchaguzi namba 6/2010.

Katika jimbo la Singida kaskazini wa tia nia saba ambao wanagombea ubunge kwa tiketi ya CCM, wametishia kujitoa katika kinyanganyiri hicho kufuatia msimamizi wa uchaguzi kumwachia mgombea mwenzao ambaye ndiye mbunge wa jimbo hilo kuto kufuata masharati ya sheria za uchaguzi jambo ambalo limekuwa kero hadi kutumia vijana wa shule kuonyesha vipeperushi vyake wakati wa mkutano wa kujinadi.

ITV haikuishi hapa ilifanya juhudi za kumwona kaimu katibu wa CCM mkoa wa Singida ambaye ndiye msimamizi mkuu wa mkoa Bwana Aluu Segamba, amekiri kuwepo kwa matatizo hayo na kuchukuwa jukumu la kumbadilisha msimamizi wa uchaguzi wa jimbo hilo na kumweka mwingine.

Baadhi ya majimbo ya uchaguzi yenye wabunge ambao wameamua kutia nia ya kugombea tena wamekuwa wakioneka wao ni chanzo kimoja wapo kikubwa cha kuvunja mashariti ya uchaguzi na kuwasababishia wenzao kuwa na malalamiko mengi,hadi kufikia hatua ya kuiomba serekali kupeleka maafisa wa takukuru na polisi kwenye mikutano ya kujinadi kugombea ubunge.

Chanzo:ITV

CHADEMA wamsahau Dk.wilbroad Slaa..Kisa LOWASSA

$
0
0
Hili limejitokeza mara baada ya Lowassa kutangaza kuingia UKAWA kupitia CDM, Kufuatia jambo hili upepo wa Dk.Slaa kupendwa na kuaminiwa na wana CHADEMA unaelekea ukingoni kufuatia ingizo jipya, na huenda asisikike tena katika mbio za uchaguzi mkuu akiwa mgombea wa urais wa chama hicho kufuatia wengi kumsahau kuanzia viongozi na wanachama wa chama hicho na sasa ni historia tu!

Dk. Slaa Kwa takribani miaka 10 ya uongozi wake amekuwa muhimili wa CHADEMA na amekua kipenzi cha Wafuasi wa chama hicho hasa vijana kwa ahadi zake na utumishi wake!

Lowassa na Majibu ya Hasira kwa Swali la Msingi

$
0
0
Wadau Habari; jana ilikuwa siku ya kipekee sana kwa historia ya Tanzania ambayo tuliahidiwa na tuliisikia minong'ono mingi na tetesi za kila leo juu ya kuhama chama kwa aliyekuwa mgombea urais kwa tiket ya CCM ndugu, EL.

Binafsi nampongeza kwa kuitumia haki yake ya kidemocrasia na kufanya maamuzi magumu; kama mtanzania nisiyefungamana na upande wowote nimestaajabishwa sana na mambo mawili makubwa.

Mosi ni juu ya umiliki wake wa card ya CCM, EL inasemekana ana miliki card namba 15 ya Uwanachama ndani ya CCM, lakini siku ya jana alijivua uwanachama na kupewa rasmi card ya CDM, sasa bado najiuliza imekuaje kamanda huyu amejiondoa CCM na kwenda CDM lkn bado anamiliki card ya chama hicho? Maana jana sikuona akiirudisha card ya CCM ili ichanwe chanwe pale mbele ya macho yetu.

Lakini kama hiyo haitoshi bado najiuliza inawezekanaje Kiongozi mkubwa kama yeye anathubutu kutoa majibu ya hasira mbele ya Taifa hili juu ya swali la msingi ambalo lilimchafua yeye na baadhi ya Viongozi wa wizara husika.

Kwa kusema kwamba NANUKUU; "Nilipoitisha kikao cha "Government negotiation team" nikawauliza mbona nasikia huu mkataba una matatizo?

mimi nina uzoefu wa kuvunja mikataba na huu tuuvunje! wakaomba ruhusa watoke nje kwa saa moja, baada ya hapo waliporudi wakasema wamepigiwa simu toka mamlaka ya juu mkataba usivunjwe "what else could I have done?"

Mwisho wa KUNUKUU, Sasa najiuliza hapa inawezekanaje PM umeitisha kikao cha subordinates wako alafu anatokea wa kukuambia kuwa et nimewasiliana na wakuu wamekataa hilo, nani basi mwenye kupaswa kufanya consultation na Wakuu wenzake kati ya watu hawa wawili EL kama PM au Subordinates?

Lakini pia napata shaka pale namna ambavyo swali la msingi lilivyojibiwa kwa kusema kwamba, NANUKUU; "Am sick of Richmond, mtu yoyote mwenye ushahidi wa mimi kuhusika na Richmond aende mahakamani, kama huna just shut up. Nilichukua uamuzi kwa niaba ya serikali.

Nimeondoka madarakani miaka nane iliopita, mambo haya yameongezeka yamepungua, mikono yangu ni misafi na mtu mwenye ushahidi acha kupigapiga kelele, peleka mahakamani" mwisho wa KUNUKUU; Kwa uelewa wangu wa kawaida kabisa unyeti wa jambo hili haukutaka jibu la namna hii bali watanzania tungeridhishwa zaidi endapo tungepata majibu mazuri kwa kina na yenye kujitosheleza badala ya kuwa mkali kiasi ambacho inatuacha na maswali mengi kwamba ile ni namna ya kututisha na kutuziba midomo kama ambavyo ilitokea pale kwa wana habari wenzangu au ni nini hasa?

Kama hii haitoshi bado najiuliza, Je na ile hoja ya Dr.Slaa kwamba ushahidi wa jambo hili anao na yupo tayari kwenda kuthibitisha mahakamani leo hii sisi watanzania tunaibebaje hii statement kuwa naye alikuwa anabwabwaja tu au namna gani?

Lakini nathubutu kwenda mbali zaidi kwa kujiuliza Dr.Slaa na wenzake wanasimama vipi Jukwaani kumnadi kwa kumtakasa mtu huyu ambaye wao walikuwa wanachangia kumchafua?

Mambo haya yananipa shida kuyapatia majibu basi nabaki kujiuliza bila mafanikio naombeni wadau mnisaidie kung'amua.
"Majibu ya hasira kwa swali la Msingi"

Wasafi Records yaonesha nia ya kumsaidia Hawa wa 'Nitarejea'

$
0
0
Hayaaa sasa hawa ndo vijana tunaowataka katika kukuza mziki wetu hongera sana Diamond Platnumz kwa hatua uliyofikia kukuza mziki wa vijana na hongera kwa kuonesha nia ya kumsaidia tena msanii HAWA WA NITAREJEA Kwa kusema upo teari kufanya nae kazi wale walokuwa wanasema we sio mzalendo now sijui wataficha wapi sura zao!

Hubagui huchagui yeyote aje a record bure miaka 6 tu lakini umefanya makubwa kuliko wenye miaka 30 katika game.

Mwigizaji Wastara Afurahia Kupigwa Chini Ubunge

$
0
0
Gladness Mallya
BAADA ya kupigwa chini katika kinyang’anyiro cha kuwania Ubunge wa viti maalum kwa tiketi ya CCM Morogoro Vijijini, staa wa filamu Bongo, Wastara Juma ametoa kituko cha mwaka baada ya kusema amejisikia vizuri kwa madai kuwa atapata muda wa kujipanga zaidi.
Akipiga stori na gazeti hili, Wastara ambaye alishika nafasi ya pili katika kinyang’anyiro hicho, alisema amefurahi kwa nafasi hiyo kwani amethubutu na hakuitegemea, hivyo anajipanga kuwa karibu na walengwa wake ambao ni walemavu ili kujua matatizo na malalamiko yao.
“Ukweli nimejitahidi sana maana nimeshindana na mtu aliyekaa madarakani kwa miaka 20 na ni mara yangu ya kwanza kugombea ubunge, nimethubutu, nimepata kura 254 siyo mchezo japo anayetakiwa ni mmoja lakini jina langu litaenda kujadiliwa na nitafikiriwa,” alisema Wastara ambaye alibwagwa na Magreth Mkanga.

Wanaume Wananichukulia Tofauti na Nilivyo...Siko Hivyo Jamani

$
0
0
Naombeni mchango wa mawazo, imetokea wanaume wananiambia ati wananiogopa, mie ni mbabe, najiamini sana na wengine huenda mbali kwa kusema mwanamke wa dizain yako sioi.

Kwakweli sipo hivyo na huwa naumia sana mtu anaponitamkia hayo. Nasikitika mana sielewi ni kitu gani na kutongozwa na waume za watu kumezidi il a sio na singles?

Tafadhalini wanajamii naimani kuna watu wanaofahamu vizuri psychology wanishauri jamani.

Asanteni kwa kunijibu bila kejeli

Edward Lowassa Kesho Anatarajiwa Kuchukua Fomu ya Kuwania Urais Katika Ofisi za Makao Makuu ya Chadema Jijini Dar es Salaam.

$
0
0
Waziri Mkuu Mstaafu Mhe. Edward Lowassa kesho anatarajiwa kuchukua fomu ya kuwania urais katika ofisi za Makao Makuu ya Chadema Jijini Dar es Salaam.

Hatimaye Ngoma Sasa ni Lowassa vs Magufuli....Kura yako Utampa Nani?

$
0
0
Hii ndio nafasi ya kipekee UKAWA kuchukua uongozi Tanzania, inanikumbusha msisimko tuliokua nao mnamo mwaka wa 2002, tulivyoangusha KANU na kuanza kujenga nchi upya. Yaani CCM wakikwepa hii na kuponea, basi ndio kabisa watabaki uongozini. Lazima walijua Lowassa atahamia upinzani na wapo wamejipanga pia. Yetu macho, tujionee siasa ya Bongo.

LOWASSA Vs MAGUFILI......NANI ZAIDI?

WEMA SEPETU Kahamia Chadema ? Hapa Nimekuwekea Ukweli Mzima Kuhusu Habari Hii ya Wema Kuhama Chama na Kumfuata Lowassa

$
0
0
Meneja wa Wema Sepetu Amekanusha taarifa na picha zinazosambaa kwamba Wema Amejiunga na Chama cha Chadema Kumfuata Lowassa.....Hakuna Ukweli wowote.....Mkiona Habari hizo mzipuuzie....

VIDEO:Mheshimiwa Ndugai Amechimbia Kaburi la Kisiasa Baada ya Kumshambulia Mgombea Mwenzake Kwa Gongo Mpaka Kuzimia...

$
0
0
Hatimaye Mheshimiwa Ndugai amechimbia kaburi la kisiasa baada ya kumshambulia Mgombea mwenzake aitwae Dr Joseph Elieza Chilongani kwa gongo katika mkutano wa kuomba kupigiwa kura za maoni CCM Hayo yametokea leo mnamo saa saa 10 jioni katika kitongoji cha ugogoni mjini Kongwa. Katika kile kinachoonekana ni kuishiwa sera na kutumia ubabe na ukorofi ili kutetea nafasi yake ya kugombea ubunge wa Jimbo la Kongwa, Mheshimiwa Naibu Spika wa Bunge La Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mbunge wa Jimbo la Kongwa alipiga kwa gongo ambalo amekuwa akitembea nalo huku wasimamizi wa uchaguzi wakifumbua macho kitendo cha mgombea kutembea na silaha hiyo kwenye kampeni.

 Inadaiwa na mtu aliyefuatilia kwa karibu tukio hilo mkutanoni kuwa Kuna mgombea mmojawapo (mkazi wa Kongwa aitwaye Ngatunga) Alisimama kuuza sera zake na kudai kuwa Kongwa kuna madini jimbo halijafaidika na chochote kutoka kwa wachimbaji wa madini... Mara moja Ndugai alimtishia kuwa anyamaze la sivyo angemuonesha kazi kwa kile anachodai kuwa ni kuongea upuuzi.. Wakati wagombea hao wakiendelea kujibizana suala hilo ndipo ghafla mheshimiwa alipomuona Mmojawapo wa wagombea aitwaye Dr Joseph Chilongani ameshika simu na kutahamaki kuwa alikuwa akimrekodi kwa kuvunja taratibu. Ndipo Job Ndugai alipoamka na kumwambia
"Tena wewe nilikuwa nakutafuta siku nyingi sana, unanirekodi na makamera yako na leo utanitambua mimi ni nani."

 Mara Ndugai akakusanya nguvu na kumpiga Dr Chilongani kwa fimbo hiyo. aidha hata baada ya kuanguka chini Ndugai alimfuata na kumrukia kumkanyaga tumboni akiwa na hasira na nia ovu ya kutaka kumdhuru zaidi.. Baadae wananchi walipata hasira na kutaka kumshughukilia kwa kichapo Mbunge huyo na ndipo alipopanda haraka gari lake haraka na kukimbi Eneo la Tukio...

Inasadikiwa yule mgombea mwingine alijaribu kumnyanyua Dr. Pale chini, jambo ambalo baadhi ya wananchi walilichukulia ni kama kutaka kumdhuru zaidi hivyo walianza kumpa kichapo huyo mgombea mwengine kiasi hadi watu wengine walipoamulia.. Baada ya tukio hilo ovu mkutano ulivurugika. Ndugu zake Dr. Chilongani kwa kusaidiana na watu walimbeba akiwa amezimia na kumkimbiz hospital baada ya kupata PF 3 toka polis

VIDEO HII HAPA:

CCM Wataja Sababu Kadhaa Kwanini Jina la Lowassa Lilikatwa Mchakato wa Mgombea Urais CCM..Nimekuweka Hapa Sababu Hizo

$
0
0
Ndugu wananchama wa Chama cha Mapinduzi-CCM ni wiki mbili tangu tulipo maliza mchakato ndani ya chamakumpata mgombea wa Urais hapo octoba 25,2015. Kwa mara ya kwanza wananchama 41 waliomba kuteuliwa na chama. Hii inaonyesha kwamba demokrasia imekuwa ndani ya chama. Kati ya wanachama wa CCM waliochukua fomu alikuwa ni mheshimiwa waziri mkuu mstaafu Ndugu Edward Lowasa. Utaratibu wa chama ulifuatwa ili kumpata mgombea ikiwa ni pamoja kamati ya maadili, kamati kuu na halmashauri kuu ya taifa na mkutano mkuu. Katika mchakato pia chama kilitumia idara mbalimbali kama usalama wa taifa, takukuru na tume ya maadili ya umma kupata taarifa mbalimbali kuhusu wagombea hasa za uadirifu, usalama wan nchi na kadhalika.

Baada ya mchakato kumalizika baadhi ya wagombea na wanachama hawakuridhika na matokea, katika chama kikubwa kama CCM haiwezekani wanachama wote wakaridhika na maamzi. Ndugu wanachama na watanzania tunaomba kuelewa kuwa kumpata kiongozi mkubwa wa nchi kama Rais siyo kazi rahisi. Baadhi ya wanachama ambao hawakuridhika na maamzi ya chama ni Ndugu Edward Lowasa, amekuwa akizungumza nje ya chama kuhusu kutotendewa haki na baade kuhama chama na kujiunga na chamacha demokrasia na maendeleo-CHADEMA.

Kwa nini Ndugu Lowasa hakuteuliwa kuwa mgombea wa CCM?
Ndugu wanachama na watanzania, Mheshimiwa Lowasa alijenga hisia na kuamini kuwa ndani ya CCM wagombea wote walistahili kuenguliwa isipokuwa yeye. Hii siyo demokrasia, baada ya kupitia repoti mbalimbali Ndugu LOWASA alienguliwa kwa sababu zifuatazo:-

1.Kukiuka taratibu za chama kwaani alionekana kufanya kampeni badala ya kutafuta wadhamini

2.Kutoa rushwa kwa wanachama mbalimbali hivyo kukigawa chama na kama angepishwa kuwa mgombea CCM ilikuwa katika hatari ya kuwekewa pingamizi mahakamani lakini pia angeweka watu wake kwenye utawala kuwalipa fadhira.

3.Edward Lowasa aliwahonga wajumbe katika uchaguzi wa wajumbe NEC uliofanyika miaka iliyopita ili kupata watu wake ndani ya NEC.

4.Kuanza kampeni kabla ya wakati, alikuwa akisafirisha watu mbalimbali na kuwalipa fedha nyingi kisha kutoa taarifa kuwa walikuwa wakimtaka kugombea Urais, hii ni hadaa na hatari kwa chama

5.Kuwa na kashfa nyingi za ufisadi

Tafadhali: MWANAUME Anayeuliza Maswali Haya Mawili ni wa Kumuepuka Kama Ukoma

$
0
0
Kama we mwanamke umekuwa na mwanaume ambaye hamjawahi kusex hata mara moja lakini ndio mnaanza uhusiano then katika chatting za hapa na pale mwanaume akakuuliza haya maswali mawili ujue mbovu wa wabovu, hajui kugegeda na anakibamia. Mkimbie kabisa

MASWALI YENYEWE HAYA HAPA:

1. Huwa unatumia muda gani kufika kileleni?
Ukiona mwanaume kakuuliza swali hilo, ujue yeye ni ''ONE MINUTE MAN'' yaani akiingiza tu kamwaga na mgegedo wake hausimami tena. Sasa anawaza huyu mwanamke kama muziki wake ni wa nusu saa mpaka saa zima nitauweza kweli hivyo anakuuliza mapema ajijue. Ukimtajia dakika nyingi, utaona hana hata nguvu ya kukulazimisha mkagegedane.

2. Huwa unapenda mgegedo wa aina gani?
Hili pia ni moja ya swali ambalo wanaume vibonde huwauliza mademu ambao hawajawahi kusex nao. Mwanaume anayeuliza swali hilo mara nyingi huwa anakuwa ana kibamia hahahaha.

Posted by: MCHUNGUZI HURU (Associate Professor)

Tundu Lissu, Dk. Slaa hawakuwepo Lowassa alivyopokelewa CHADEMA.. Sababu ni hii hapa (Audio)

$
0
0
Waziri Mkuu mstaafu na Mbunge wa Monduli, Edward Lowassa alitambulishwa rasmi kuhamia CHADEMA July 28 2015 Dar es Salaam akiwa ameongozana na mke wake, Regina Lowassa pamoja na watoto wao.

Kwenye list ya Viongozi wa UKAWA ambao walikuwepo kumpokea na kumkabidhi kadi ya CHADEMA, alikuwepo James Mbatia, Prof. Lipumba, Dk. Emmanuel Makaidi, Salum Mwalimu na Freeman Mbowe.

Salum Mwalimu ni Naibu Katibu Mkuu wa CHADEMA Zanzibar, amesema haya kuhusu mapokezi hayo >>> ‘Tunashukuru sana Watanzania, sidhani kama kuna kiongozi wa CHADEMA simu yake iliwahi kuzidiwa kama jana, simu zilizidiwa kwa pongezi… Kila mtu amezungumza kwa sababu ya Historia ya tendo lenyewe‘>>>>


‘Kesho Mheshimiwa Edward Ngoyai Lowassa atachukua fomu ya kugombea Urais wa Tanzania kupitia CHADEMA… pengine kutakuwa na shamrashamra nyingi itategemeana na Mgombea mwenyewe, akiamua kuja na mdundiko haya… lakini tunaamini kutakuwa na shamrashamra nyingi‘ >>>> Salum Mwalimu.

Stori zikaanza kuzushwa kuhusu sababu ya Viongozi wengine wa UKAWA kutokuwepo, majibu kayatoa pia Salum Mwalimu>>> ‘Tuna mambo mengi tuna mikakati mingi, tumegawanyika… sio kila tukio wote tuwe pamoja, jana mliuliza Tundu Lissu yuko wapi na leo huyu hapa hata hamumuulizi… Tuko kwenye kipindi cha Uchaguzi tuna mambo mengi hatuwezi wote kuwa sehemu moja, tunagawanyika kutokana na ratiba tuliyonayo
Viewing all 104795 articles
Browse latest View live




Latest Images