Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104809 articles
Browse latest View live

Ushiriki wa Lowassa Vita vya Kumng’oa Nduli Idd Amin wa Uganda Wazua Gumzo Kubwa...Soma Hapa

$
0
0
USHIRIKI wa waziri mkuu wa zamani, Edward Lowassa katika vita vya kumng’oa Nduli Idd Amin wa Uganda mwaka 1978/79 umeibua gumzo kufuatia madai ya katibu mkuu wa zamani wa CCM, Yussuf Makamba kushabihiana na ya Makongoro Nyerere aliyedai kuwa hakuwahi kumwona mstari wa mbele.

Rais wa awamu ya kwanza wa Tanzania, Mwl. J.K Nyerere na makamanda wa Jeshi.
Katika mkutano wa kumnadi mgombea wa chama chake, Makamba alidai kuwa anashangazwa na madai ya Lowassa kuwa alikwenda vitani, wakati aliyeandikisha majina ya askari waliokwenda huko wakati huo alikuwa ni Rais Jakaya Kikwete ambaye hakuwahi kuorodhesha jina hilo.
Wakizungumzia suala hilo, watu mbalimbali waliopiga simu chumba chetu cha habari, walisema ni vyema kama Lowassa angejitokeza na kuthibitisha madai hayo, kwani akikaa kimya, ataonekana ni mwongo, kitu ambacho ni kibaya kwa kiongozi anayeomba kuwa rais wa nchi. 

“Maneno kama haya niliwahi kumsikia akiyasema Makongoro, kwamba hakuwahi kumuona Lowassa mstari wa mbele, leo Makamba anasema jina lake halikuandikwa na Kikwete, ni vizuri akajitokeza ili athibitishe kama kweli alienda au la!” alisema Shauri Shamim, aliyedai kupiga simu akitokea Tanga. 

“Hili ni jambo kubwa, siyo dogo kama inavyoweza kudhaniwa, tunajua kuwa Lowassa aliwahi kuwa askari, ajitokeze na kuzijibu tuhuma hizi za wanajeshi wenzake ili tujue kama ni propaganda za kisiasa au la!” alisema Jane Jarome wa Masasi. 

Mei mwaka huu, wakati wa mkutano wake na wahariri wa vyombo vya habari mjini Dodoma, pamoja na mambo mengine, Lowassa alisema alikuwa miongoni mwa askari wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) walioshiriki vita vya kumng’oa madarakani kiongozi huyo wa Uganda aliyeivamia Tanzania.

Kanisa Katoliki Laja na Mpya..Sasa Kama Upo Kwenye Ndoa Unaweza Mpa Mwenzako Talaka..Kama Wafanyavyo Waislam

$
0
0
KIONGOZI wa Kanisa Katoliki Duniani, Papa Francis jana alieleza mabadiliko mapya yanayolenga kuwarahisishia Wakatoliki kuvunja ndoa zao na kuoa upya.

Dhamira hiyo ni ishara nyingine ya dhamira ya Papa huyo kutaka kulifanya Kanisa Katoliki liwe rafiki zaidi na kuendana matakwa ya walio wengi.

Akizungumza kuhusu mabadiliko hayo, Papa alisema si haki kwa wenzi kuishi muda mrefu ‘wakikandamizwa na wingu la shaka’ kuhusu uhalali wa ndoa zao.

Ikumbukwe kwamba ni msimamo wa Papa kumkatalia Mfalme Henry the VIII wa Uingereza kumtaliki mkewe Catherine wa Aragon katika karne ya 16 uliosababisha England ijitenge na Rome na kushuhudia kuundwa kwa Kanisa la England huku mfalme akiwa mlinzi wa Imani wa kanisa hilo.

Mabadiliko makuu matatu aliyotangaza  Papa jana ni   kuondoa mchakato wa mapitio ya mara ya pili wa uamuzi wa kutoa talaka kupitia mahakama ya kanisa kabla ya ndoa kuvunjwa.

Mengine ni kuwapatia maaskofu uwezo wa kuharakisha na kuvunja ndoa   wenzi wanapoamua wenyewe katika mazingira fulani kama vile ukatili katika ndoa au uasherati na mchakato huo wa talaka kuwa bure, isipokuwa kwa kulipa ada ndogo kwa ajili ya gharama za  utawala.

Kabla ya sheria hiyo, Wakatoliki waliotaka talaka walihitaji kibali kutoka kwa mahakama mbili za kanisa, wakati sheria mpya inabakiza moja ingawa rufaa bado zinaruhusiwa.

Kabla ya sheria hiyo, wanandoa wa Wakatoliki wanaotalikiana bila idhini ya kanisa na kuolewa upya walihesabiwa kama wazinifu na hawakuruhusiwa kupokea komunio.

Lakini kwa mujibu wa  utaratibu mpya, wanaotalikiana wakioa au kuolewa tena watabakia kuwa wafuasi wa kanisa hilo.

Mwaka jana Papa aliunda tume ya wanasheria wa kanisa hilo  kuboresha na kurekebisha taratibu hizo  kurahisisha wanandoa kuachana na kupunguza gharama.

Mageuzi hayo yalikuja katika mfumo wa nyaraka mbili zinazoitwa ‘motu proprio’, neno la kilatini lililobuniwa na Papa mwenyewe.

Taratibu hizo zitakuwa rasmi kama sehemu ya sheria za kanisa (canon law) ifikapo Desemba 8 mwaka huu wakati Papa atakapoanza kutangaza Mwaka wa Jubilee ambao kwa kawaida huhusishwa na msamaha.

Rais Kikwete Ndio Rais Bora Afrika Mashariki..Atunikiwa Tuzo ..Soma Hapa

$
0
0
TANZANIA imetajwa kuwa kinara katika nchi za Afrika Mashariki kwa kutunza amani na utulivu tangu ipate uhuru, huku Rais Jakaya Kikwete akiibuka kiongozi bora katika ukanda huo kwa kujitolea kuleta amani katika Bara la Afrika na kutunza amani hiyo nchini mwake.

Kwa hali hiyo, Rais Kikwete ametunukiwa tuzo mbili na Taasisi ya East Africa Book of Records ya nchini Uganda, moja ikiwa ni kwa ajili ya Tanzania ambayo imefanikiwa kutunza amani pamoja na utulivu tangu uhuru na nyingine ni ya Rais Kikwete mwenyewe kutokana na juhudi zake za kupigania amani nchini mwake na eneo lote la ukanda wa mashariki mwa Afrika.

Kutokana na tuzo hizo, sasa Rais Kikwete ameacha kumbukumbu katika vitabu vya nchi za Afrika Mashariki, kama mtu na kiongozi maarufu aliyetoa mchango mkubwa katika kuleta amani kwenye nchi za ukanda huu.

Akikabidhi tuzo hizo jana Ikulu, Dar es Salaam, Kiongozi wa taasisi hiyo Dk Paul Bamutaze alisema wametoa tuzo hizo baada ya kuangalia mchango wa Rais Kikwete katika kuleta amani katika baadhi ya nchi barani Afrika, akitoa mfano namna kiongozi huyo alivyoleta amani mwaka 2008 nchini Kenya, kufuatia machafuko baada ya kufanyika kwa uchaguzi mkuu.

“Tuzo ya kwanza tunaitoa kwa Tanzania kama nchi kwani ndio nchi pekee katika eneo la Afrika Mashariki ambayo imedumisha amani na utulivu tangu kupata uhuru na ndio imekuwa inasaidia kutatua migogoro mbalimbali kwa majirani zake na inaendeshwa kwa utawala wa sheria,” alisema Dk Bamutaze.

Alisema tuzo ya pili wanamkabidhi Rais Kikwete kutokana na kuwa kiongozi bora, ambaye amedumisha amani nchini mwake, lakini pia ameshiriki kutatua migororo mbalimbali.
  
 Alisema licha ya Kenya, lakini ni Rais Kikwete ambaye ameshiriki kuleta amani nchini Burundi na kurejesha serikali iliyokuwepo madarakani baada ya kuwepo jaribio la uasi.

Rais Kikwete pia amesaidia kuleta amani katika nchi za Sudan Kusini, Comoro, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) baada ya Jeshi la Tanzania kuwasambaratisha kundi la waasi la M23.

Mkuu wa Kitengo cha Utafiti wa taasisi hiyo, Adam Buyinza alisema katika utafiti ambao wameufanya, wamegundua kuwa Tanzania imedumu kuwa na amani kutokana na kuongozwa na CCM ambacho kina sera zinazoeleweka.

Kwa upande wake, Rais Kikwete alisema kwamba misingi ya amani na utulivu uliopo nchini umewekewa misingi yake na Mwalimu Julius Nyerere, ambaye uongozi wake haukubagua watu kwa misingi ya kidini, rangi na kabila au eneo ambako anatoka mtu.

Alisema tuzo hiyo aliyoipokea sio yake peke yake, bali ni ya wananchi wa Tanzania pamoja na wasaidizi wake ambao yeye kama nahodha wa meli wamesaidiana kuhakikisha kuwa meli yao inaenda vizuri hata pale panapotokea mawimbi wanasaidiana kukiendesha chombo hicho.

Rais Kikwete alisema kuwepo kwa amani nchini, kumetokana na watu wake kuamini kwenye majadiliano badala ya kupigana na alisema hata pale ilipotokea tofauti kati ya Serikali na vyama vya upinzani, walikaa meza moja wakazungumza na pale ilipotokea tofauti kati ya Waislamu na Wakristo pia walitatua migogoro yao kwa mazungumzo.

“Kwa mfano kulitokea ugomvi wa nani ana uhalali wa kuchinja, haya mambo walitaka mimi niingilie kati, lakini jamii yenyewe walikaa na kujadiliana kwamba yametoka wapi na nani ameyachochea, walipokaa waligundua kwamba hakuna faida kwani mambo hayo wamejiwekea jamii husika,” alisema Rais Kikwete.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe, alisema kwamba tuzo hizo alizotunukiwa Rais Kikwete ni kitu kikubwa kwa Rais anayeondoka madarakani.

Idara ya Uhamiaji kuhoji Uraia wa Zitto ni Matusi kwa Dola na Watanzania

$
0
0
Habari zilizoripotiwa kwenye vyombo vya habari juu ya Idara ya Uhamiaji kuanza kuchunguza Uraia wa ndugu Zitto Kabwe zinapaswa kuhojiwa kwa kuwa zinazua maswali mengi ya kuudhi

Ni kitu gani hasa kilichoisukuma idara hiyo leo kuanza kufuatilia Uraia wa Zitto?

Turejee historia kwa ufupi:

Mwaka 2010 Mgombea wa Upinzani jimbo la Nyamagana Ezekiel Wenje alitangazwa kuwa si Raia. 

Mwaka huo huot Mgombea wa CCM jimbo la Nzega Hussein Bashe aliyekua kinyume na kambi ya mwenyekiti taifa ambae ni Rais alitangazwa si Raia wa Tanzania

-Baada ya Rais Mkapa kuingia madarakani,alipokosolewa vikali Mwanasiasa na mwanaharakati nguli Jenerali Ulimwengu alitangazwa kuwa si Raia

Je,Hili la ndugu Zitto halina unasaba na siasa za majitaka?

Ni nani mwenyehatimiliki ya nchi kiasi kwamba anaweza kuitumia idara nyeti ya umma kuchokonoa,kutishia haki ya msingi ya mtu kwa sababu za kisiasa?

Zitto amekua Mbunge kwa zaidi ya miaka 10 na Amekua Mwenyekiti wa PAC na Naibu Kiongozi wa Kambi ya Upinzani Bungeni ambazo ni nafasi nyeti. 

Je,Uhamiaji wanataka kutangaza kuwa Idara ya Usalama wa Taifa hawafanyi kazi yao ipasavyo hadi kumuachia mtu ambae hajulikani alipotoka kuwa na access ya nyaraka nyeti za nchi baada ya kuongoza taasisi muhimu?

Niliwahi kuandika kuwa ukitaka kuthibitisha kama wewe ni raia wa nchi hii basi ikosoe serikali ya Tanzania,gombea ubunge au urais halafu uwabane vilivyo watawala.Kama umezaliwa maeneo ya mipakani au kama rangi yako ya ngozi ni ya asili ya nje ya mipaka yetu utakiona

Hii tabia haipaswi kufumbiwa macho hata kidogo. Ni lazima Idara ya Uhamiaji ieleze msingi wa uchunguzi huo unatokana na nini. Tabia ya kuviziana na kutumia dola ikiachwa iendelee hakuna atakaebaki salama

Cha ajabu watu wenye rekodi ya kupambana na ufisadi na kuonyesha uzalendo kwa nchi ndio wanaokua wa kwanza kutiliwa mashaka juu ya Uraia wao.Inachekesha sana

Hakuna mpinzani wa kweli atakayeunga mkono udhalimu huu.Zitto amekua Naibu kiongozi wa Upinzani na kiongozi wa ngazi ya juu kwa vyama vyote viwili vya upinzani alivyowahi kuwa mwanachama.

Kama tunafika Mahali Mwanasheria Mkuu wa Serikali ya Tanzania anamuomba Mkongomani orodha ya walioficha fedha za Tanzania nchini Uswisi basi Mkongomani huyo uzalendo wake ni zaidi ya ule wa viongozi wakuu wa vyombo vya Dola na hata Rais wa nchi.

Usishangae kukuta kuwa suala hili linaibuka kumnusuru Mgombea wa CCM huko Kigoma mjini.Yaani ili kuzua hisia hasi dhidi yake kutoka kwa wapiga kura tu.

Maslahi ya kisiasa yametamalaki kama yalivyotamalaki katikat mradi wa unyanyasaji aliofanyiwa Jenerali Ulimwengu,Hussein Bashe na Ezekiah Wenje mwaka 2010 na hapo kabla

By the way, Katika Kitabu kilichopigwa marufuku cha "The Dark Side of Julius Nyerere " cha Ludovick Mwijage kulikua na tuhuma ambazo hazikuwahi kujibiwa kuhusu uraia wa Mwalimu Nyerere.Au jibu la Serikali ndio kukifungia kitabu kile?

Mch.Christopher Mtikila aliwahi kuibua tuhuma kuhusu Uraia wa Rais Mkapa kuwa sio Mtanzania .Hazijawahi kujibiwa kiufasaha

Serikali ya CCM wana waziri Mwenye tuhuma za kuwa na Uraia wa Marekani na pia chama kilimkabidhi fomu za Urais. Waziri ni mjumbe wa Baraza la Mawaziri la kumshauri Rais wa Nchi. Lazaro Nyalandu hajawahi kukanusha tuhuma hizi na hata idara ya uhamiaji

Ipo siku wanamuziki Alli Kiba,M wasiti na Wengineo kutoka Kigoma au Mipakani watakapotumia nyimbo zao kuelimisha jamii na kugusa maslahi ya watawala wataanza kuonekana kuwa sio watanzania. Tusikubaliane na ujinga huu

Tuhoji ,Tukosoe na kulaani jaribio lolote la kutumia idara nyeti za nchi kutisha sauti kinzani dhidi ya watawala au watu wachache kwa maslahi yao binafsi. 

Tanzania ni yetu sote,Hakuna mwenyehatimiliki ya nchi hii

Mungu Ibariki Tanzania,Mungu Ibariki Afrika...

Aluta Contimua,Victory Ascerta....

Ben Saanane

Wanaharakati, Wasomi Wamshukia Magufuli Kuhusu Kauli yake Mabadiliko

$
0
0


Baadhi ya wasomi na wanaharakati wamekemea kauli ya mgombea urais wa CCM, Dk John Magufuli ambaye amekuwa akiwaonya wanaotaka mabadiliko ya haraka nchini akiwakumbusha yaliyojitokeza nchini Libya.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti leo wasomi hao wameiita kauli hiyo ni ya vitisho kwa wananchi, kwa kuwa mabadiliko wanayotaka ni ya kidemokrasia na siyo vita.

Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Sikika, Irenei Kiria, amesema wananchi wamejiandaa kwa ajili ya kupiga kura na siyo vita kama wachache wanavyofikiri. “Mabadiliko yanayozungumzwa na wengi ni ya kidemokrasia na siyo vita, hivyo Dk Magufuli hapaswi kutolea mfano wa Libya, tumejiandaa tangu 2010” alisema.

Amesisitiza : “ Ukweli ni kwamba kuna watu wamekuwa wanataja vita hapa nchini tangu mwaka 1995 hao wanatamani kuleta machafuko wamethubutu kufananisha na Rwanda au Burundi, wakati nchi hii ni tofauti kwani CCM imekuwa madarakani kwa 50 na amani ipo,” amesema Kiria.

Mkurugenzi wa Kituo Cha Haki za Binadamu (LHRC), Hellen Kijo-Bisimba amesema wakati wa kampeni si wa kutoa kauli za vitisho bali, wananchi wanachohitaji ni kusikiliza sera za vyama husika ambavyo vitawawezesha kufanya uamuzi wa kuvichagua.

Akiwa mikoa ya Morogoro na Tanga, Dk Magufuli amekuwa akitoa kauli za kuwaonya wanaotaka mabadiliko kuwa wakumbuke yaliyotokea Libya ambapo nchi hiyo imezama kwenye machafuko baada ya kuondolewa aliyekuwa kiongozi wan chi hiyo marehemu Muamar Gadhafi.

Kampeni za UKAWA/LOWASSA Zimekwamia Wapi?....Je Minongono Kuwa Lowassa Mgonjwa ni Kweli?

$
0
0
No siku ya pili Leo naona kimya bila Maelezo toka kwa wahusika ni nini kimetokea. Jana walihairisha morogoro bila kutoa sababu na Leo mpaka dakika hivi huku morogoro naona kimya. Wahusika Makene mtujuze tumeshavaa sare teyari tangu juzi.

Diamond apata nomination ya MTV Europe Awards kwa kishindo...Mashabiki wa Ali Kiba Watia Aibu

$
0
0
Msanii na hifadhi ya taifa Diamond Platinumz amepata nomination ya best African act katika tuzo za MTV Europe awards zitakazofanyika Milan Italy.

Diamond amepita bila kupingwa pamoja na Davido, Yemi Alade, na Aka uku imebakia nafasi moja ya nominee ambapo ushindani ni kati ya Casper nyovest, wiz kid, DJ Arafat, K.o na stone boy ambao mshindi atapatikana kutokana na kupata tag nyingi za mashabiki.#inominatecaspernyovest 

Wakati huo huo Katika hali ya kuhuzunisha na kustabisha mashabiki wa kiba wameamua kulilia nomination za MTV Ema kwa kuanzisha tag zao eti nomintee Kiba wakati kiba video ya chekecha haijawahi pigwa MTV

Aunt ezekiel: Nimezaliwa Kisarawe, Siyo CCM

$
0
0
STAA wa Bongo Movies, Aunt Ezekiel ‘mama Cookie’ amewajia juu wanaomsema kuwa amekikacha Chama Cha Mapinduzi (CCM) na kukimbilia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kuwa hajazaliwa na chama hicho bali amezaliwa Kisarawe.

Akiendelea kucharuka mbele ya Amani, Aunt alisema kuwa hata kama huko alipo wakishindwa atakubali matokeo kwa kuwa lazima katika mchezo kuna upande utashinda na mwingine utashindwa hivyo atakubali yote.

“Ninachojua mwisho wa siku lazima kuna mshindi na mshindwa hivyo nakubali yote kwa sababu nampenda Lowassa na sijawahi kutamka kuwa mimi ni CCM kwa kuwa sijazaliwa kwenye chama hicho, nimezaliwa kijijini kwetu Kisarawe alisema Aunt kwa jazba.

Chanzo: GPL

Nuh Mziwanda adai BASATA wamemalizana na Shilole, wao wakanusha

$
0
0
Nuh Mziwanda amedai kuwa kabla Shilole hajaondoka kwenda nchini Marekani walimalizana kila kitu na BASATA.

Nuh amesema vibali alivyochukua Shilole BASATA ndio vilivyomwezesha kuchukua visa ya kusafiria.

Ili upate urahisi wa kupata visa lazima upate vibali vyote vya BASATA,” Nuh aliambia XXL ya Clouds FM. “Kwahiyo ilibidi awe na vibali vyote vya BASATA kwasababu BASATA walizungumza na Msando yakaisha pale pale,” aliongeza.

Hata hivyo Katibu Mtendaji wa baraza hilo Godfrey Mngereza alisisitiza kwa mara nyingine tena kuwa hawajaifuta adhabu kwa Shilole na sasa wanajipanga kumjadili tena baada ya kukiuka adhabu hiyo.

Hakuna mahali ambapo panasema ameondelewa adhabu,” alisema.

Kwa taratibu, baraza linaendeshwa kwa mujibu wa sheria na hii ni sheria ya bunge namba 23 ya mwaka 1984 na kanuni zake za baraza ambazo ni za mwaka 2015. Sasa kikitokea kitu kama hicho tunarudi tena kwa utaratibu ule ule ambao ulikuwa umetumika katika kutoa adhabu ndio mfumo huo huo tena ambao utatumika,” alisema.

Wanataka kuufungia wimbo wangu mpya ‘Viva Roma viva’ kisa tu nimeongea ukweli – Roma

$
0
0
Saa chache baada ya wimbo mpya wa Roma ‘Viva Roma viva’ kutoka September 9, rapper huyo amedai kuwa ametishiwa wimbo huo kufungiwa.
roma new pic
Kupitia Instagram, majira ya saa mbili usiku Roma aliandika;
“WANATAKA KUIFUNGIA NYIMBO YANGU!! KISA TU NIMEONGEA UKWELI!! INANIUMA SANA NATAMANI HATA KULIA NIKIONA UKWELI HAUPEWI NAFASI!! NIOMBEENI NA MNIKUMBUKE KWENYE SALA ZENU NDUGU ZANGU!! Viva Roma viva”
ro
Bado haijafahamika sababu ya wimbo huo kutaka kufungiwa, na Roma hakupatikana kwenye simu yake nilipomtafuta kwaajili ya kuzungumza nae kuhusu swala hilo.
Usikilize hapa kama bado hujausikiliza
Hizi ni baadhi ya comments za mashabiki wake waliotoa maoni yao kwenye post hiyo;
paul2297:
Siku zote ukweli haupendwi na walanguzi na wezi kama ccm, na ninakupongez sana we ni miongoni mwa wasanii wanaojielew, hata kama wakilifungia leo tunashukuru mungu hataa ndege wa angani wameshalidaka nyimbo yako na wataendelea kuimba ukweli daima
stella_njau:
Usjal kaka tutakuombea watu kama nyiny tunawahtaji sana katika kuleta ukomboz najua its not easy kwako coz nchi yetu ni kandamiz but God is dere to protect u from those damb, selfish and lust leaders VIVA ROMA VIVA FOREVER tuko pa1 bro
oscarhimxelf:
Mimi huwa najiuliza ivi ulichoimba wewe na alichoongea slaa au mambo ambayo wanayoongea viongozi kwenye majukwaa ya kampeni mbona hayana tofauti kwann wao huwa hawafungiwi.. mfano juzi slaa akawa anaongea mpaka habar za maaskofu sijui kupewa hela na data nyingine mbalimbali ambazo alisema sikuona ile hutuba imefungiwa bali adi leo inatumika kama kielelezo lkn ww ukiongea kwann waseme ifungiwe …
mikemrossotza:
Hata waufungie kaka mkubwa mzigo tunao wamechelewa
seniorita_tynaalex Roma we ninoma nimeipenda nyimbo yako I salute you dear mpambanaji mwenzangu
galla_bway:
Kila wanachofanya wanachelewa broo ..ucwaze tutasambaza kuhakikisha jamii unaisikia huu wimbo …pamoja
levi_mkushflani:
HAHAHAHA WANAIFUNGIA WAKAT YLTUSHAIDOWNLOAD!? cc tunayo na ujumbe tushaupata
rosewau:
Mi nilijua tu…lazima ifungiwe…so jiandae tu wangu…
shabani_maulidi:
Viva #Roma#viva ukweli unauma wakifungia tutasikiliza hata kwenye simu bodaboda Bajaj daladala na majumbani kwetu message sent #viva#Roma#viva
eetaamajiko:
Usijal @roma2030 kitaa tushaipata na ujumbe umetufikia, hii inanikumbusha wimbo wa @nashMc kaka suma walifungia ukwel uliowazi kama vazi la kahaba,Wenyewe kwenye kampeni zao wanatukana ila hawafungiwi

francy_0903:
Sheria zingine zinavyopitishwa kwa kwel wanabid wàngalie kwa umakin kama mtu akisema ukwel anfungiwa maana matus ndo yamekatazwa sasa hata ukwel hawautaki loh tunapoelekea ni pabaya kwa kwel maana hamna wa kutuongelea juu ya nchi yetu zaid ya sisi wenyewe hawez toka mtu Marekan aje aongee ukwel juu ya Taifa letu coz hana uchungu kama sie wenyewe tuliomo ndan ya Taifa,hongera roma wimbo mzur and u r in my prayers


Bongo5

Video: Kumbe Zari Anaongea Kiswahili Hivi?

$
0
0
Zari the Bosslady anajua kuongea Kiswahili tofauti na unavyoweza kudhani. Video hiyo chini itakuacha mdomo wazi.

Mange Kimambi Aongelea Issue ya Wimbo Mpya wa Roma Kutaka Kufungiwa 'Lini Tanzania Hii Mshawahi Sikia nyimbo ya Propaganda za Kisiasa Inapigwa redioni au TV?'

$
0
0
Issue ya Roma.. Kabla sijaanza wangapi wameiski radioni nyimbo ya Diamond kumsifia Magufuli??? Nyoosheni mikono? Au nyimbo ya Kiba akimsifia Magufuli? Wakangapi mmesikia?? Okay kumbe Jibu mnalo.... Kama kawaida yetu wabongo kudandia Treni kwa mbele. 
Hivi Kweli mlidhani hii nyimbo kuna radio itapiga.? Hata Mengi mwenyewe na uchadema wake hawezi kupiga. Yani Huyu msanii hakuona Muda wa kutoa huu wimbo Hadi kipindi cha Uchaguzi?? ____________________________
Yani maredio wapige nyimbo za kampeni? Yani nyie watu mnachekesha mpaka mnatia huruma. Mnavyojifanya victims of the system sasa , Yani mtu anaweza dhani Tz kuna nini sijui.... Ila mnachokitafuta mtakipata soon. Hivi Kweli nyimbo Kama hii inaweza kupigwa sehemu?? Au sio mnatafuta tu vitu vya kulalamika? Yani mnajitia Kama watu wa South Korea. Maana mnavyojifanya mko oppressed kha!!! Embu msituchafulie uchaguzi na ujinga wenu. Mmeshaanza kutafuta visababu vya kundamana.... Huyu msanii nae alikuwa anatafuta pakutokea tu., Kwenda kutoa nyimbo ya Propaganda za siasa Tena kipindi cha uchaguzi mnadhani alikuwa hajui haitochezwa? Alijua sana. Mie nilikuwa hata sijui Ana exist Ila hii nyimbo Kila mtu atamjua. He is smart aisee. ------------ ___________________________________
Yani mmekuwa wanafki mpaka mnauziii, lini Tanzania hii mshawahi Sikia nyimbo ya Propaganda za kisiasa inapigwa redioni au TV? Mnajua haiwezekani Ila mnatafuta sababu za kuwahamasisha watu kuwa CCM wanawaonea..... Hamumpati mtu...

Source: Mange Kimambi

Dr Kessy Anakuletea Dawa za Kutengeneza Hips, Makalio, Nywele na Nguvu za Kiume Kwa Kutumia Dawa za Asili zisizo na Kemikali

$
0
0
PENDEZA NA KESSY PRODUCT.
PATA DAWA ZA ASILI ZISIZO NA MADHARA WALA KEMIKALI YOYOTE,
NA MATOKEO KUANZIA WEEK (2) ADI (4) NAKUENDELEA
1) KUTOA MVI SUGU 70,000/
2) REFUSHA NYWELE NA KUZUIA KUKATIKA 50,000/
3) TENGENEZA SHEP HIPS NA MAKALIO KWA
@ KUPAKA 50,000/
@ DAW YAMAJI 80,000/
@ VIDONGE 100,000
4) PUNGUZA TUMBO NA NYAMA UZEMBE KWA
@ KUPAKA 55,000/
@ KUNYWAA 80,000/
@ MKANDA WENYE DAW 80,000/
@ BELT 150,000/
5)PUNGUZA MWILI MZIMA PAMOJA NA KILO 80,000/
6) ONGEZA UNENE WA MWILI MZIMA NA HAMU YAKULA 80,000/
7) PUNGUZA MAZIWA NA KUYASIMAMISHA 50,000/
8) ONGEZA MAZIWA SAIZ UNAYOTAKA 50,000/
9) ONGEZA NGUVU ZA KIUME KWA DAW
@ JELI YAKUPA 50,000/
@ VIDONGE 70,000/
10) ONGEZA MAUMBILE YA KIUME KWA
@ JELI YAKUPKA 100,000
@ MASHINE YA HUNDSOME UP 170,000/
11) KUWA MWEUPE MWILI MZIMA NA KUWA SOFTI 70,000/
12) TOA CHUNUS,MADOA,MAKOV 45,000/
13) RUDISHA USICHANA (BIKRA) 60,000/
14) TOA MICHIRIZI (STERCH MARKS) 50,000/
15) ONDOA NGIRI ZAAINA YOYOTE 60,000/
16) TUNDISHA NYWELE ZILIZO ISHA (KIPARA) 150,000/
17) TOA MICHUBUKO KWENYE MAPAJA NA SEHEM ZA SIR 60,000/
18) RUDISHA HAMU LA TENDO NA KUFANYA BILA KUCHOKA 60,000/
19) TOA NDEVU KWA WANAWAKE 80,000/
NA HUDUMA NYINGI USISITE  KUSEMA  PIGA SIMU,
TUNAPATIKANA DAR,K-KOO,POSTA NA SINZA.
KWAMIKOWANI UDUMA ITAKUFIKA KWANJIA YA MABASI BILA TATIZO.
CHAKUFANYA PG CIM  0719955528  0756259180  0785371237  Follow
@dr_kessy- product
@dr_kessy -product
@dr_kessy-product
PIA UTALETEWA POPOTE ULIPO

Maneno ya Diamond Platnumz baada ya kutajwa kuwania tuzo ya MTV Europe Music Awards 2015

$
0
0
Naseeb Abdul aka Diamond Platnumz amepata nafasi ya kuipeperusha bendera ya Tanzania katika tuzo za MTV Europe Music Awards 2015 zitakazotolewa mwezi October 25, 2015 jijini Milani Italy.

Msanii huyo ambaye ametajwa kuwania tuzo ya MTV Europe Music Awards katika kipengele cha Best African Act, akiongea na ripota wa millardayo.com alisema..‘Kiukweli namshukuru sana mwenyezi Mungu kwasababu najua mimi naamini sio mimi tu watanzania wengi ndoto zenu ni kuomba muziki wetu uweze kutambulika kimataifa sio tu kutambulika bali kupewa heshima kwa taifa letu la Tanzania‘ – Diamond Platnumz

Kwasasa mambo yanaenda vizuri kabisa kwa hiyo kuteuliwa katika tuzo za MTV Europe kwangu ndio mara yangu ya kwanza pia hata kwa Tanzania, namshukuru Mwenyezi Mungu nauzuri tuzo hizo haziangalii chochote kwani zinaangalia kura za watu so naamini muda ukifika basi mashabiki tupige sana kura ili tuweze kufanikiwe kuuleta ushindi nyumbani, nakumbuka mwaka jana walishinda Sauti Sol‘ – Diamond Platnumz

Maneno Aliyoandika JB wa CCM Juu Ya Picha Hizi Akiwa na SHAMSA na AUNTY wa UKAWA

$
0
0
Kufuatia tofauti za kimitazamo ya kisiasa baina ya mastaa hawa, ambapo JB akiwa upande wa CCM  wakati Shamsa na Aunt Ezekiel wakiwa UKAWA, JB kiutani kupitia ururasa wake mtandaoni ameibuka na hii kuonyesha kuwa siasa sio vita.

Imenibidi nifute picha hizi (hapo juu)...watu wamepaniki sana...Jamani siasa sio vita nilikuwa nawatania na wao wakacheka na wakati naandika wapo...mashabiki... Daah .. Daah...Jamani Bungeni wanataniana vyama tofauti na sisi pia...Tunashirikiana....Mashabiki mnisamehe kama nimewakosea...Ila ningefurahi siku moja watoto hawa wakirudi kundini pamoja na yule mwingine .....Nawapenda.

Ali Kiba Avuta Mambo Mazito...Yamzidi na Kuzimia

$
0
0
Dustan Shekidele, Moro
KATIKA hali isiyo ya kawaida wananchi mkoani hapa wamejikuta wakipigwa butwaa mara baada ya kumshuhudia staa wa Bongo Fleva, Ali Saleh Kiba akivuta ‘mambo’ (shisha) kisha ‘kuzima gari’ ukumbini.



TUJIUNGE ENEO LA TUKIO
Tukio hilo lililopigwa chabo na mwanahabari wetu lilijiri mishale ya saa 8:00 usiku wa Jumamosi iliyopita katika ukumbi wa kisasa wa burudani wa Samaki Sport mjini hapa ambao kulikuwa na nyomi la kufa mtu.
Awali, baadhi ya wananchi walimpiga chabo Kiba kisha kumtonya paparazi wetu ambaye alifika fasta ndani ya kiwanja hicho na kumshuhudia laivu msanii huyo akiwa na demu mwingine mkali aliyejitambulisha kwa jina la Asia Mujuni na siyo Jokate Mwegelo ‘Kidoti’ ambaye amekuwa akifuatana naye kila sehemu katika siku za hivi karibuni.

JOKATE UPO?
Baadhi ya watu wanajua uhusiano wa Kiba na Jokate walidai kuwa kama mwanadada huyo angekuwepo eneo la tukio pangechimbika.

WAVUTA KWA ‘KUSHEA’
Wawili hao walikuwa wakivuta shisha kwa ‘kushea’ huku Asia akishushia na kinywaji kikali.
Hata hivyo, Kiba awali hakumgundua paparazi wetu hadi alipotonywa na msanii mwenzake, Stanley Yusuf ‘Stan Bakora’ ambaye anamfahamu fika mwandishi wetu.
Kiba aliyeonyesha kama amezidiwa nguvu kwa kilevi hicho, baada ya kutonywa alishtuka kisha akamchukua ‘patna’ wake huyo na kujikokota hadi kwenye gari ambapo walitokomea kusikojulikana.

MASTAA WENGINE WALIOKUWEPO
Kabla ya kutimua, kwenye meza aliyokaa Kiba na mrembo pia kulikuwa na wasanii wengine kama Fareed Kubanda ‘Fid Q’, Esterlina Sanga ‘Linah’ na Kibwana Saleh ‘KB’ ambaye maskani yake ni mjini hapa.

Akizungumza na gazeti hili, KB ambaye pia alikuwa akivuta shisha alimtetea Kiba: “Kiba ni ndugu yangu na haya siyo madawa, ni shisha, Ulaya mastaa wanavuta. Baadhi ya watu humu ukumbini wanadai ni madawa ya kulevya lakini siyo kweli huu ni moshi wa kawaida.”
Naye mmoja wa mashabiki wa Kiba, Jumanne Idd aliyezungumza na gazeti hili kuhusu ishu hiyo alifunguka: ”Kila siku tunakuja kwenye kiwanja hiki cha Samaki, hatujaona watu wakivuta shisha humu ukumbini. Leo ndiyo tumemshuhudia Kiba kufuatia moshi wa kilevi hicho kuwa mkali, ilibidi mimi na demu wangu tuhame meza.”
Kijana mmoja wa mjini aliyefahamika kwa jina la Juma lssa alipoulizwa kuhusiana na tukio hilo alisema: “Ni kweli kifaa kile ni moshi wa kawaida lakini kuna baadhi ya watu wanachanganya na moshi wa bangi.”

KIBA ATAFUTWA
Jitihada za kumtafuta Kiba ili kuzungumzia ishu hiyo ziligonga mwamba na hata alipotafutwa kwa njia ya simu haikuwa hewani.
Shisha ni kiburudisho ambacho kimekuwa maarufu sana miongoni mwa mastaa na vijana wengine wa daraja la kati ambao hukitumia, hasa sehemu za starehe nyakati za usiku na mikusanyiko mingine ya burudani inayojumuisha watu wengi.

Source:Globalpublishers

Lulu Afungukia Siasa na Kura Yake

$
0
0
Okay....nimeulizwa na Wengi na pengine yanasemwa mengi kuhusu ni Chama kipi cha Siasa nina support Kama ilivyoonekana Kwa Wasanii Wenzangu wengine..! Kwa kifupi nitajaribu kufafanua machache Kwa huu uwezo mdogo wa kufikiri nilijaaliwa na Mwenyezi Mungu..!

Kwanza,kila binadamu/mwananchi ana uhuru wa kuchagua na ku support anachokipenda...kwahyo sitangaa wala kuchukia Flani ku support upande flani


Pili,Mimi Kama mm(binafsi)hii ni Mara yangu ya kwanza kupiga kura kwahyo nimeamua kuitumia Kwa busara na kuifanya iwe na kwanza isiyo na majuto Kwa kutofuata mkumbo wowote wa ndugu,jamaa,marafiki au watu walionizunguka..!

Tatu,Nimependa kuitumia NAFASI hii zaidi Kwa UHUSIKA wa ELIZABETH na sio LULU nikimaanisha ikiwa kila kura ya mwananchi wa wakawaida ni ya siri na kuuridhisha moyo wake basi na mm nitakuwa mwananchi wa kawaida kbsa katika hili..!

Nne,natoa pongezi Kwa wasanii wenzangu waloweza kushiriki Kwa namna moja au nyingine ktk ku support upande mmoja au mwingine kwani wameonyesha ujasiri na mapenzi ya kweli Kwa vyama wanavyo support ILA tu mabishano ya HOJA ni mazuri zaidi na yanaweza kuepusha ugomvi au kuvunja mahusiano yetu ambayo yalikuwepo kabla ya UCHAGUZI na yatatakiwa kuendelea kuwepo baada ya UCHAGUZI..!

Tano,Nawatakia Kila La kheri Wagombea wote na Natumaini Uchaguzi utakuwa wa SAWA na HAKI..! Mwisho,mimi nimejiandikisha na nina KIKATIO changu 
tayari,napenda kuwahimiza wananchi/WaTanzania wenzangu kujitokeza katika uchaguzi ili kumchagua yule unayeona anakufaa....tuombe Mungu na Tujitahidi uchaguzi uwe wa Amani na tuepuke maneno au vitu Vyovyote vinavyoweza kuashiria kuleta vurugu katika uchaguzi wetu Mkuu...!

MunguIbarikiTanzania
KuelekeaUchaguziMkuuOctober2015
KuraYanguSiriYangu

Elizabeth Michael ‘Lulu’ “elizabethmichaelofficial” on Instagram

Gwajima Kitanzini. Viongozi wa dini wamshukia kama mwewe

$
0
0
Gazeti la Uhuru Leo Limeandika Hayo Hapo Juu
Gwajima Kitanzini. Viongozi wa dini wamshukia kama mwewe

Tahadhari Kwa Waumini wa Askofu Gwajima !

$
0
0
Ni muda mrefu jamii yetu imekuwa ikiwaheshimu na kuwaamini viongozi wa dini katika masuala mbalimbali ya kiroho na ustawi wa familia.

Ni jambo la kawaida sana kwa waumini wa dini zote kupeleka matatizo yao mbalimbali ya kifamilia kwa viongozi wa dini.

Ni dhahiri kwamba wengi wetu hupeleka masuala mbalimbali hata yale ya unyumba na siri nzito nzito za chumbani na familia kwa ujumla kwa kuwa tuna imani viongozi wa dini wana hulka ya kutunza siri na kusaidia kutatua matatizo yetu ya kiroho au kifamilia.

Hii ni tofauti kwa Gwajima ambaye ni mtomvu wa heshima ya kiongozi wa dini kwa kueleza siri za familia aliyoipa huduma za kiroho kisa tu kachokozwa kisiasa na yeye kajibu kwa kutoa siri za familia ya Slaa.

Angekuwa daktari angeweza kufutiwa cheti na kudaiwa fidia.

Lakini tukumbuke ni Gwajima huyu huyu aliyeshutumiwa kuvuruga ndoa ya Mbasha badala ya kutatua mgogoro wa familia hiyo.

Hii ni trend ya Gwajima anayejiita Bishop ambayo inatakiwa kuangaliwa kwa jicho la Tahadhari hasa hasa na waumini wake wanaompelekea siri za ndani.


KWA HISANI YA MTU WA TANZANI!!

By Jingalao/Jamii Forums

I Hate Kenyans With a Passion & I’ll Deport Them From US - DONALD TRUMP Tells BBC.

$
0
0
US real estate magnate and Republican Presidential candidate, Donald Trump, has again hit out at Kenyans terming them as fraudsters and conmen.

Responding to a Kenyan journalist who works with the BBC, Trump said that he hates Kenyans with a passion because they are opportunists like US President Barrack Obama, who is a Kenyan-American.

“Sir, my name is Gladys, a Kenyan journalist working for BBC; Kenyans have complained that you hate them and that recently you called our athletes that won in Beijing cheap frauds and conmen. Do you still hold that position and if so, why do you hate us so much Mr. Trump?” Gladys asked.

“I hate Kenyans starting with Obama and that is why I promise to deport all of them when I ascend to the helm. You people sneaked into our country and you’ve devalued it greatly. Look at this clown that calls himself POTUS, this one has rendered America to the dogs and it is time we made our beloved country great again. Recently I heard that you people have generated twitter hashtags trying to rebuke me. I am the pillar of America, a true American and any Kenyan that feels irritated can go to hell or call me directly if he has the balls to do so. I will put all of them including you, in their rightful positions” Trump responded.


Gladys went on to ask “But Sir., some say you are a cousin to Adolf Hitler and as we all know, Hitler was a German and not an American, what makes you think you are more of American that other immigrants that came the same way as you?”

Trump responded by saying “You see, these are the kind of questions I dislike answering. Go to Obama and ask him that”

Whether he will keep his promise when he ascends to power is something we will wait and see.

Viewing all 104809 articles
Browse latest View live




Latest Images