Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104789 articles
Browse latest View live

Mama Diamond Amkimbia Zari Boss Lady Kisa Chote Kipo Hapa

$
0
0
MAMA DIAMOND AMKIMBIA ZARI BOSS LADY KISA CHOTE KIPO HAPA

Mama wa Mbongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond’, Sanura Kasim. KWELI maisha si popote! Msemo huu wenye kinyume na ule usemao maisha ni popote umedhihirika baada ya hivi karibuni mapaparazi wetu kutonywa kuwa, mama wa Mbongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond’, Sanura Kasim amekuwa akimkimbia mkaza mwanaye, Zarinah Hassan ‘mama Tiffah’ ndani na kwenda kukaa nje kutokana na Zari kujikita sana kwenye mitandao ya kijamii hivyo kutokuwa na mawasiliano.


Zarinah Hassan ‘mama Tiffah’. “Mnajua mama Diamond hana neno. Anaweza kukaa na Zari wakaongea, tatizo Zari. Muda mwingi yupo kwenye Instagram, mara WhatsApp, ukiangalia mama yeye na mambo hayo si sana. Anajikuta yuko mwenyewe tu.
“Ndiyo maana inafika wakati inabidi mwanamke huyo atoke ndani na kwenda kushinda nje. Zari mara nyingi yeye yupo na simu kwenye eneo la bwawa la kuogelea,” kilisema chanzo.


Mama wa Mbongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond’, Sanura Kasim. UZUNGU KWA SANA
Chanzo kiliendelea kueleza kuwa, maisha ya mama Diamond na Zari ndani ya mjengo huo ni ya watu wawili tofauti.
“Zari anapenda sana mambo ya uzunguni. Si unajua maisha yake ya kitajiri halafu amezoea sana Afrika Kusini, akienda Uganda kwao ni mara mojamoja.


Mama Tiffah akifanya yake. “Sasa mama Diamond yeye kazoea maisha ya ‘uswahilini’. Kujiachia kwa sana. Akiamua leo anataka kula ugali na bamia, Zari anataka kukaangiza sana. mara asubuhi chai na tambi, wakati mama mkwe wake anataka chai na vitumbua au mihogo yenye kachumbari. Si unaona wasivyo kopu”
NI KWELI HAWAENDANI?
Kwa mujibu wa chanzo, mama Diamond na Zari hawaendani kwa maana ya kila mmoja anapenda kitu ambacho mwenzake hakipendi au hajakizoea kukifanya katika maisha yake. Hata nyie waandishi semeni, mama Diamond na Zari wanaendana wapi!

“Lakini si kwamba ni wagomvi, hapana! Wako vizuri sana ila maisha tu. Zari ni ‘mzungu’ mama Diamond ni ‘mswahili’ sasa wapi kwa wapi!” kilisema chanzo.
MAMA DIAMOND ANASWA
Mwanzoni mwa wiki hii, mapaparazi wetu walifunga safari hadi Madale jijini Dar nyumbani kwa Diamond ili kuona kama kweli mwanamke huyo humkimbia mkaza mwanaye huyo ambaye ana kichanga na kwenda kukaa nje muda mwingi.
NI KWELI
Katika hali ya kushangaza, mapaparazi wetu walimkuta mama huyo akiwa amekaa kwenye kibaraza cha nyumba ya jirani eneo ambalo lina akina dada wanachoma maandazi ya kuuza na wateja wanafika wakifuata mahitaji ya vitafunwa hivyo.
Mama Diamond alionekana hana wasiwasi na alikuwa akitumia muda mwingi kuzungumza na wakaanga maandazi hao.
APIGA STORI NA WAPITA NJIA
Mbali na kuzungumza muda mwingi na wakaanga maandazi, pia mama Diamond alikuwa akizungumza na wapita njia ambao walikuwa wakitoka sehemu moja kwenda nyingine.
MAJIRANI WAMCHAMBUA
Baadaye, mapaparazi wetu walipata nafasi ya kuzungumza na majirani wa mama Diamond ambapo wengi walimchambua vilivyo.
“Sisi hatukutegemea kama angekuwa ni mwanamke wa kuja kukaa nje na majirani zake. Mama Diamond ni wa ajabu sana. uwezo wa mwanaye, angekuwa mwanamke mwingine hata salamu tusingepata.
“Yeye amekuwa mtu wa watu. Akiwa na nafasi atatoka nje kama unavyomwona pale, anaongea baadaye anarudi ndani kwake,” alisema jirani mmoja mwanamke akikataa kutaja jina lake.
“Mimi sina la zaidi, ila nasema Mungu ambariki mama Diamond. Ni mwanamke asiyejionesha kwamba ana mtoto mwenye jina kubwa hapa Tanzania na Afrika kwa ujumla. Anajibeba yeye kama yeye. Sasa kama ndani anakimbia kukaa na mkewe Zari sisi hatujui,” alisema mwanamke mwingine.
MAMA DIAMOND
Alipofuatwa mama Diamond ili azungumzie madai ya kumkimbia Zari ndani, alikuwa ameshazama ndani ya geti na mlinzi alikuwa mkali kutoa ushirikiano.
Simu yake ya mkononi iliita bila kupokelewa huku ikielezwa kuwa, namba asizozijua ni mgumu wa kupokea simu.
CREDIT : GLOBAL PUBLISHER 

Nimeupenda Ukauzu wa Dr. Maghufuli Kutokumshirikisha Mkewe Katika Kampeni za Kusaka Urais

$
0
0
Magufuli
Tumlizoea, kwenye chaguzi nyingi, wagombea kuambatana na wenza wao, kwenye campaign, hii hali imezusha maswali kibao, hasa kwa marafiki zangu wa UKAWA, wamediriki hadi kunitania wakisema Magufuli hana mke, hatutaki Rais bachelor, lakini niliwajibu kuwa ana mke na watoto, ikumbukwe magufuli sio mtu wa kujivuna, Mungu amsaidie, pia anajua anachofanya ni kwa manufaa ya taifa, hata watoto wake wanasoma shule hizi hizi za St Kayumba, hivyo sio mtu wa kujiweka matawi ya juu, Magufuli ana hofu ya mungu kama hutaki kajinyonge. Dkt. Magufuli ni mmoja ya mawaziri wanaoogopwa sana kwa misimamo hata na Rais mwenyewe kwa jambo analoliamini analifanya kwa mujibu wa sheria,kanuni na taratibu.

Amemuekeza Kanali Kinana kuwa moja hatapenda kuiona familia yake ikishiriki katika kampeni za urais kwani sitaki familia yangu kujihusisha au kujinasibisha na urais wa nchi.

Nataka nikapambane kufuta hili lililojengeka kwa watoto wa vigogo kubebwa kwenye nafasi za uongozi hata ajira na kuwaacha watoto wa watanzania maskini wakiwa mitaani eti kwa sababu hawana wa kuwashika mikono haki ya Mungu hili nitapambana nalo ili chama hiki kiwe cha wote na nchi hii iwe ya wote.

Hivyo mke wangu naomba aachwe akafundishe,wanangu waendelee na mambo yao na hata ndugu zangu. Jukumu lao kubwa ni kuniombea kwa Mungu ili nikawatumikie watanzania kwa moyo wa dhati bila kiburi na majivuno.

#hapakazitu.

Haya ni Majimbo 11 Ambayo UKAWA Wasipoteze Fedha Washapita

$
0
0
1. Ubungo,
2.Kibamba,
3.Bariadi,
4.Arusha,
5.Busanda,
6.Dodoma,
7.Maswa,
8.Tarime,
9.Mikumi .
10.Arumeru,
11.ilemela
Haya ni majimbo ambayo kwa asilimia mia moja yashachukuluwa na Ukawa.
Ebu kama una mengine yenye uhakika yatupie hapa Magamba yajifiche.

UTAFITI: Umaarufu wa Wasanii Wanaoishabikia CCM Umengua Ghafla!!

$
0
0
Tangu kuanza kwa kampeni za uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika Oct - 2015, wasanii mbali mbali walijitokeza kuunga aidha UKAWA au CCM. Ni ukweli usiopingia CCM imekusanya kundi kubwa la wasanii kama akina Wema Sepetu, Diaomond Platinumz, Ali Kiba, Peter Msechu, JB, na wengine wengi kama Original Komed.

Katika hao wapo waliokuwa wanajihusisha na kampeni zaidi mtandao, kwa maana ya live politics na wapo ambao walikuwa wanasoma alama za nyakati yaani ni kama wapo hawapo.

Katika group ambao walikuwa wanafanya kampeni kwenye mitandao kama INSTAGRAM, FB, Twitter kwa ujumla umaarufu wao umeshuka tofauti na awali. Katika kuthibitisha hili, unaweza kukuta post zao zinaweza kuwa na likes kama 500 hivi licha ya masaa mengi kupita jambo ambalo halikuwa kawaida. Mfano ni Blogger Mange Kimambi, Wema Sepetu, Diamond Platinumz na wengine wengi katika post zao kisiasa wemekuwa wakipata likes chache na maoni hasi kuwa wamepotea.

Hali ni tofauti kabisa kwa wasanii waliojitokeza UKAWA kama akina Aunt Ezekiel, Shamsa Ford na wenzake, clips na picha zao Instagram, Facebook, Whatsupp zimekuwa lulu. Watu wanaonyesha kuzipokea kwa shangwe kwa kupata malikes ya kutosha licha na comments za kuwatia moyo.

Huo ni uthibitisho tosha kwamba tusiishi kwa mazoea, wasanii wanatakiwa wasome alama za nyakati na hata ni maslahi basi usijiingize katika live politics kwa maana zinaua umaarufu na kukushusha labda kama uwe UMEAMUA SIASA KUWA KAZI YAKO.

Na mwisho hii, ni kama utabiri wa upande ambao unakubalika sana ambao unaweza kuwa mshindi.

Nawasilisha

Vurugu Mara: Msafara wa Heche wavamiwa, Mwanachama mmoja wa CHADEMA Afariki

$
0
0

Kwa namna hii nishaona kila dalili za ICC..... Too sad
" Msafara wangu umevamiwa na wanaccm wakati nikitoka kijiji cha mangucha kwenda kegonga watu wetu wameumizwa na mmoja amefariki dunia" Msg ya Heche kanithibitishia sasa hivi....
Source: Jamii Forums

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Ijumaa Ya Tarehe 11 Septemba

$
0
0
Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Ijumaa Ya Tarehe 11 Septemba



















Abubakary Zubeiry Achaguliwa Rasmi Mufti Mkuu wa Tanzania

$
0
0
Abubakary Zubeiry
Baraza Kuu la Waislamu Tanzania (Bakwata) jana limemchagua Sheikh Abubakary Zubeiry bin Ally kuwa Mufti Mkuu wa Tanzania.

Katika uchaguzi huo uliofanyika jana kwenye Ukumbi wa Africa Dream mjini Dodoma, Tume ya Dini ya Kiislamu imemchagua Sheikh Zubeiry kwa kura 310 za ndiyo baada ya kuingia kwenye uchaguzi huo akiwa mgombea pekee.

Akitangaza matokeo hayo, Mwenyekiti mstaafu wa Halmashauri Kuu ya Bakwata, Alhaji Habib Ndassiwa alisema majina mawili yaliyotoka kwenye Baraza la Ulamaa yalikuwa ni ya Sheikh Ally Muhidini Mkoyogole na Sheikh Zubeiry.

Hata hivyo Sheikh Mkoyogole alijitoa na hivyo kumuacha Sheikh Zebeiry kuwa mgombea pekee.

Mufti Zubeiry aliteuliwa kukaimu nafasi hiyo ya juu katika dini ya Kiislamu mnamo Juni 22 mwaka huu baada ya kifo cha Mufti Issa Shaaban Simba kilichotokea katika Hospitali ya TMJ jijini Dar es Salaam alikokuwa amelazwa kwa matibabu.

Alitakiwa kushikilia nafasi hiyo kwa muda wa miezi mitatu (Siku Tisini) hadi Septemba mwaka huu kabla ya kufanyika kwa uchaguzi mkuu wa kujaza nafasi hiyo.

Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu Chamtaka Dkt. Magufuli Kufuta Kauli zake za Vitisho

$
0
0
Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu kimekemea kauli zenye kuwajengea hofu wananchi kushiriki kikamilifu katika mchakato wa kidemokrasia unaoendelea kwa kutoa mifano isiyoshabihiana na hali iliyopo nchini ikiwemo kufananisha na nchi zenye machafuko

Katika taarifa yake iliyotolewa kwa vyombo vya habari imemtaka mgombea urais kupitia Chama cha Mapinduzi CCM, Mh. John Magufuli kufuta kauli zake ikiwemo ya kufanisha mchakato wa uchaguzi na vuguvugu la mabadiliko ya Libya pamoja na serikali yake kuwapiga risasi wahalifu wa kutumia silaha.

Mh. Magufuli mnamo tar 28 Agost akiwahutubia wakazi wa Mbalizi Mbeya vijijini alisema “Msitoe hukumu ya jumla zipo nchi zilifanya hivyo zilijuta,Libya ya Gadafi ilikuwa ukioa unapewa nyumba, unatafutiwa mtaji ,elimu na umeme bure lakini wananchi walichoka raha.....wakasema wanaondoka lakini wale vijana waliosema wanataka raha na wale vijana waliosema wanataka ukombozi wa haraka ndio wa kwanza kuvuka bahari ya Mediteranian kwenda Ulaya."

Kituo hicho kimesema kauli hizo zinatoa vitisho kwa wapiga kura kinyume na demokrasia kwa kuwa huwezi kufananisha mabadiliko ya kimapinduzi ya Libya na umwagaji damu uliotokea huko na mabadiliko ya amani kwa kupitia mchakato wa uchaguzi za kidemokrasia.

Taarifa hiyo imeogeza kuwa kauli hizo za mgombea huyo ni za kukemewa kwa kuzingatia nchi na chaguzi zinaongozwa kikatiba na Katiba inakinzana kabisa na kauli zilizotolewa na kiongozi huyo

Mwigizaji wa Filamu Diana Kimari Akiri Kuanza Mapenzi ‘Utotoni'

$
0
0
CONFESSION! Msanii wa filamu Bongo, Diana Kimari ameanika ukweli wa moyoni kuwa, alianza kujihusisha na mambo ya mapenzi akiwa anasoma shule ya msingi.

Akipiga stori na Amani, Diana alisema alianza kuwa na uhusiano wa kimapenzi akiwa darasa la saba na hii ni baada ya kuingia kwenye utu uzima ‘kuvunja ungo’ kitu ambacho huona kwamba zile zilikuwa akili za kitoto na kwamba hakukuwa na ‘ladha ya mapenzi’ hivyo huwa hataki kukumbuka kabisa nyakati hizo.

“Ni kweli mimi si mgeni wa mapenzi, niliwahi kuwa na mpenzi tangu nikiwa shule ya msingi, japo hayakuwa na ladha maana si unajua mapenzi ya utotoni tena? Kwa sasa sina tena hamu na wanaume, nimeshaumizwa sana na mapenzi, sasa mimi na shule tu,” alisema Diana anayesomea biashara katika chuo kimoja kilichoko mkoani Kilimanjaro.

Chanzo: GPL

Corazon Kwamboka Leaves Men Salivating After Her Bubble Butt Hits The Gym

$
0
0
Corazon Kwamboka is known for having a behind so huge and corpulent that it looks like she is smuggling watermelons under her clothing.

And she put her rotund derriere in full display as she hit the gym to lose some new pounds.

But it was not the workout that caught the attention of male admires but the plump behind that kept going up and down, awakening some wild feelings in those that beheld the sight.

"That ass is a national treasure. Stay blessed. Sheeesh." one man wrote with another adding "Now thats a pretty sight"

She had promised to quit the entertainment industry so feast your eyes because these may be the last derriere videos we will get to see of the "promising lawyer.



Picha 6 za Mafuriko ya Lowassa Kibaigwa Mkoani Dodoma Jana

$
0
0


Tangu tarehe 29 August ulipofanyika uzinduzi wa kampeni  za Ukawa,Lowassa  ameendelea kuwa gumzo  sehemu mbali mbali anapofanya  mikutano   ya  kampeni  zake.
 
Jana Sept 10,Lowassa alikuwa Mkoani Dodoma katika wilaya ya Kongwa mji mdogo Kibaigwa katika uwanja wa Amani 

Mbunge wa CCM Aibuka Katika Mkutano wa ACT-Wazalendo.....Polisi Wamwondoa Kuepusha Vurugu

$
0
0
Mbunge wa Nkasi Kaskazini (CCM), aliyemaliza muda wake, Ally Keissy jana aliibuka kwenye mkutano wa kampeni wa chama cha ACT-Wazalendo na kupinga maelezo kwamba mshahara wake wa ubunge ni zaidi ya Sh10 milioni.

Keissy aliwasili kwenye mkutano huo uliokuwa wa mgombea urais wa ACT-Wazalendo, Anna Mghwira na mgombea mwenza wake, Hamad Yusuph Mussa uliofanyika Kijiji cha Namanyere, akiwa kwenye gari lake aina ya Toyota Land Cruiser.

Mgombea mwenza, Mussa alipopanda jukwaani, alianza kuhutubia kwa kuwaeleza wananchi kwamba mbunge wao, Keissy anayemaliza muda wake ameshindwa kuwaletea maendeleo, hivyo mwaka huu wasimpe kura zao.

“Niwaambie kitu, wabunge wenu akiwamo Keissy wanapata mshahara wa zaidi Sh10 milioni ndiyo maana akiwa bungeni kazi yake ni kupiga makofi kwa kushangalia kupitisha kwa bajeti ambayo haina masilahi kwa wananchi wa jimbo lenu,” alisema Mussa na kushangiliwa na umati ambao mmoja alisikika akisema:

“Sema baba sema, ujumbe umefika na mwenyewe yupo hapa.”

Kauli hiyo ilionekana kumkera Keissy, ambaye alinyanyuka alipokuwa ameketi na kwenda kwenye gari lake kuchukua ‘salary slip’ iliyogongwa muhuri wa Ofisi ya Bunge, ikionyesha kwa mwezi anapokea mshahara Sh3 milioni.

Akionyesha kukerwa na alichoeleza kuwa ni upotoshaji wa mgombea mwenza, Keissy alikwenda karibu na meza kuu na kumwita Ofisa Habari wa ACT-Wazalendo, Abdallah Khamis na kumkabidhi nyaraka hiyo ili aipeleke jukwaani kwa mgombea mwenza aliyekuwa akiendelea kuhutubia.

Hata hivyo, Mussa alipopelekewa nyaraka hiyo aliwaambia wananchi: “Keissy anasema nimpige kidogo kidogo maana yamemchoma.” 
  
Keissy hakuonyesha kuridhika na majibu hayo na alionyesha ishara za kutaka kulazimisha nyaraka hiyo isomwe, kitendo kilichozuiwa na askari waliokuwa eneo hilo na kumtaka aondoke kwa kuwa mkutano huo ulikuwa haumhusu.

Awali, Keissy aliwaambia waandishi wa habari kuwa: “Uchaguzi wa mwaka huu ni mgumu kwa vyama vyote kutokana na uelewa na mwamko wa wananchi, hivyo siyo vibaya hata mimi kuhudhuria mkutano huu.

“Hakatazwi mtu kuhudhuria mikutano kama hii maana uchaguzi wa mwaka huu ni tofauti na miaka mingine na ACT-Wazalendo wana siasa nzuri na kitakuwa chama cha pili cha upinzani.”

Katika mkutano huo, Mghwira aliwaambia wananchi waliohudhuria kwamba viongozi waliopewa dhamana ya kuongoza nchi hawana cha kujitetea kuhusu kusuasua kwa maendeleo nchini.

Alisema katika mikoa aliyotembelea, ameona jinsi gani Watanzania walivyopigika na ugumu wa maisha na hali hiyo inasababishwa na viongozi waliowapa dhamana ya kuwaongoza kutojali maendeleo yao. 

“Suluhisho pekee la hali hii ni ACT-Wazalendo. Tumejipanga ipasavyo kuwatumikia na endapo nikifanikiwa kuingia madarakani uchumi wa Taifa hili na thamani ya shilingi haitoshuka ili kuleta maendeleo kwenu,” alisema Mghwira.

Pia, aliwaahidi wakazi wa Katavi kubadilisha mfumo wao wa kilimo na kuwa kilimo cha biashara ili vijana wake wapate ajira na kuachana na kilimo cha kizamani na kuweka mfumo bora wa usambazaji wa pembejeo za kilimo.

Sauti Sol wamerudi tena kwenye headlines za burudani na single yao mpya ‘Isabella’..(Audio)

$
0
0
Kundi la Sauti Sol kutoka Kenya inazidi kufanya vizuri kwenye industry ya burudani ..wamerudi tena kwenye headlines za burudani baada ya kuachia single yao mpya inaitwa ‘Isabella’.

Sauti Sol wanatamba na ngoma zao kama ‘Narea’, ‘Sura yako’ na ‘Shake Yo Bam Bam’

Isikilize hapa mtu wangu…

Utata Nyumba Aliyojenga Mwigizaji Lulu Michael

$
0
0
HALI si shwari! Mjengo wa staa wa filamu Bongo, Elizabeth Michael ‘Lulu’ uliopo Kimara Saranga, Dar ambao alisema amemzawadia mama yake mzazi, Lucresia Karugila, umezua utata baada ya madai kwamba eti umeshauzwa.

Kwa mujibu wa chanzo ambacho ni jirani mmoja wa eneo hilo, mjengo huo umeuzwa kutokana na uamuzi wa Lulu mwenyewe bila kujulikana sababu licha ya manenomaneno kwamba, mama Lulu alikuwa hataki kuhamia hapo akitaka mjengo mkubwa zaidi kama wa Mbongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond’ uliopo Madale, Dar.

Jirani huyo alisema kuwa, ni muda mrefu hajamwona Lulu wala mama yake licha ya kwamba kuna mlinzi wa kulinda nyumba hiyo lakini anaishi nyumba nyingine ya jirani.

“Watu wanasema umeshauzwa, lakini mnunuzi hajajulikana. Ila mtu ambaye anaweza kuwaambia kwa undani zaidi ni Lulu mwenyewe. Yule mlinzi hayuko wazi sana. Ila nyumba imeisha kwa sasa,” alisema jirani huyo akiomba jina lake liingizwe kwenye ghala.

Baada ya kupata ubuyu huo bila kupoteza muda mapaparazi wetu walifunga safari mpaka Saranga kwenda kujiridhisha na kile walichoelezwa na sosi huyo na kushuhudia mjengo huo wa maana ukionekana upo tayari mtu kuweza kuishi lakini kukiwa hakuna mtu ndani.

Wakazi wa eneo hilo walihoji siku ambayo mama huyo atahamia kwenye mjengo wake huo aliozawadiwa na mwanaye huku wengine wakidai walipata fununu nyumba hiyo imeshapigwa bei.

“Hakuna kitu cha kumkwamisha kuhamia kwa sababu bado madirisha tu ndiyo hayajakamilika japo tayari kuna magrili, sasa nashangaa mbona hawahamii na isitoshe hakuna hata mlinzi. Mtu si anaweza kuingia akawa analala bila ridhaa yao!



“Kuna kipindi Lulu alikuwa anakuja hapa na mama yake kuitazama lakini baadaye akawa anakuja mama yake tu japo kipindi hiki cha karibuni tangu nyumba ifikie hatua hiyo ya kuisha sijawaona wote,” alisema mmoja wa majirani zake.

Baada ya hapo, mapaparazi wetu walimvutia ‘waya’ mama Lulu na kumsomea madai yote ambapo alijibu kwa kifupi:

“Jamani naomba mniache kwanza, si mnajua nimetoka kufiwa siku si nyingi. Hivyo bado akili yangu haijakaa sawa kwa pigo nililolipata. Hayo mambo siwezi kuyaongelea kwa sasa.”

Baada ya hapo, mapaparazi walimsaka Lulu kwa njia ya simu na alipopatikana alikuwa na haya ya kusema:

“Hizo ni ishu binafsi za kifamilia, siwezi kuzizungumzia sana kama nikitaka kumkabidhi mama nitamuita ndani na kumkabidhi, nikitaka kuanika kwenye vyombo vya habari nitasema, ila mengine hayo siyajui.”

Chanzo: GPL

Nyaraka Feki ya TCRA Yasambaa Mitandaoni..TCRA Watangaza Kiama Kwa Wahusika

$
0
0
Mamlaka ya mawasiliano TCRA imekanusha taarifa inayosambazwa mitandaoni hivi sasa kuwa imetuma waraka kwa jeshi la polisi kuishughulikia akaunti moja inayohusika na makosa ya mitandaoni


Taarifa hito iliyosambazwa mitandaoni ni ambayo haioneshi anuani ya aliyetuma wala aliyetumiwa, tarehe, wala kumbukumbu namba, lakini pia taarifa hiyo inaonesha kusainiwa na Mkurugenzi mkuu Prof John Nkoma ambaye alishastaafu kwa mujibu wa sheria toka Juni 30 mwaka huu, na kwa sasa TCRA ina mkurugenzi mpya aitwaye Dkt Ally Simba

Taarifa hiyo Feki iliyosambazwa mitandaoni
Kufuatia usambaaji huo wa taarifa hiyo feki, mamlaka hiyo imelazimika kukanusha taarifa hiyo na kusema ni ya uongo na wametangaza kuwa watamshughulikia muhusika kwa mujibu wa sheria ya makosa ya mtandao ya mwaka 2015, na kanusho hilo limetolewa kupitia ukurasa wa twitter wa TCRA


Wanachama wa Chadema Feki Wakamatwa Makao Makuu ya Chadema..Mwandishi wa Gazeti la Uhuru Ndani

$
0
0

Mwandishi wa gazeti la UHURU CRISTOPHER LISSA katikati  ya maafisa ya CHADEMA baada ya kujaribu kiukimbia kwa kuruka ukuta wa chama hicho na kuambulia kukatwa na chupa zilizokuwa ukutani na kumsababishia kutoka na damu maeneo kadhaa ya mwili wake.
 Katika hali ya kushangaza leo makao makuu ya chama cha democrasia na maendeleo CHADEMA kimetokea kihoja cha karne baada ya watu wanaodhaniwa kuwa wanachama wa chama cha mapinduzi kufanya maandamano ambayo hayakufanikiwa na badala yake kusababisha mwandishi wa gazeti la UHURU kuingia matatani baada ya kuonekana kuambatana na vijana hao waliokuwa wanataka kuandamana kutokumtaka Edward lowasa.

Majira ya saa nne asubuhi vijana kadhaa ambao walikuwa wamevalia sare za chama cha CHADEMA na mabango kadhaa walionekana wakikatiza makao makuu ya chama hicho kwa mithili ya maandamano huku wakiwa wanachukuliwa picha na mwandishi wa gazeti la UHURU pamoja na mpiga picha wa Television ya STAR TV ambapo baada ya kufika makao makuu ya chama hicho walinzi pamoja na maafisa wa cham hicho walijipanga na kuwazunguka vijana hao ambao baadhi walikuwa na boda boda hali iliyowafanya vijana hao kutawanyika kwa kukimbia na kuvua t shirt za chama hicho ambazo walikuwa wamevalia juu ya nguo nyingine.
Baadhi ya kadi ambazo inadaiwa kukutwa nazo mwandhishi huyo
Katika purukushani hizo waandishi waliokuwa wanawasindikiza waandamanaji hao akiwemo mwandishi wa gazeti la uhuru CHRISTOPHER LISSA pamoja na mpiga picha wa STAR TV waliwekwa chini ya ulinzi wa makamanda wa chama hicho kuwa kuhusishwa na kupanga tukio hilo ili wapate habari kuwa kuna maandamano lengo likiwa ni kukichafua chama hicho.

Mara baada ya kuwekwa chini ya ulinzi akiwemo mmoja kati ya vijana ambao alionekana kuchoka (TEJA) naye alikamatwa ambapo katika maelezo yake alikiri kupokea shilingi elfu kumi pamoja na T-SHIRT ya CHADEMA kutoka kwa vijana hao kwa lengo la kuambatana nao katika maandamano hayo ambayo hayakuwa halali.
Mwandishi wa gazeti la uhuru CHRISPHER LISSA wakati akitoa maelezo kwa maafisa wa chadema alisema kuwa yeye alipokea ujumbe mfupi wa maelezo kuwa kutakuwa na maandamano kuelekea CHADEMA kupinga alichofanyiwa DK SLAA ambapo kwa mujibu wa mwandishi huyo aliamua kufikisha ofisini na kupangiwa kazi hiyo ya kufanya coverage katika maandamano hayo ya leo.

Kwa mujibu wake anasema kuwa leo aliamua kufikia kinondoni kituo cha manyanya kutafuta hao waandamaji  na ndipo alipokutana na wenzake wa STAR TV na kisha watu ambao walikuwa wamepanga kuandamana kwalifika wakiwa na gari na kushuka na kuanza kupeana T-SHIRT za CHADEMA huku wakiwa ni kama wageni wa eneo hilo wakiulizia makao makuu ya chama kwa watu wengine.



Anasema kuwa baada ya kugawiana nguo za chadema huku wakiwa hawasemi wao ni kina nani na wametumwa na nani walianza kusogea makao makuu ya chama hicho huku wakiimba na kushiria kuwa kua kitu wanakidai,ambapo ndipo maafisa wa chama waliamua kuwaweka kati na kufanikiwa kuzima tukio hilo.

Akizngumza na wanahabari afisa wa chama hicho BONIFACE JACOB amesema kuwa chama kilipata taarifa siku tatu nyuma kuwa kuna vikao vinakaa chini ya viongozi wawili wa CCM avikao ambavyo vilifanyika kurasini na ndipo chama kilijipanga kwa tukio hilo la leo.

Kwa mujibu wa afisa huyo anasema kuwa mwandishi huyo wa UHURU anahisiwa kushiriki kupanga maandamano hayo kutokana na kukutwa na kadi zaidi ya 20 feki za chama hicho ambazo walijipanga kujifanya kama zimerudishwa na wanachama hao kadi ambazo mwandishi huyo amekana kuhusika nazo

Lusinde Amshambulia Lowassa.....Asema Kichwani Hayuko Sawasawa Maana Kichwa Kimejaa UJI Badala ya Ubongo

$
0
0
Mgombea Ubunge Jimbo la Mtera, kupitia Chama cha Mapinduzi,Livingstone Lusinde,amesema mawaziri wakuu wastaafu Fredrick Sumaye na Edward Lowassa hawapo sawa sawa  kichwani  kwa  kuwa  vichwa  vyao  vimejaa  UJI  Badala  ya  Ubongo.

Lusinde amesema anamshangaa Sumaye kwani amepata maisha mazuri akiwa CCM,amesomesha watoto wake akiwa CCM,na kwamba Sumaye hana sifa za kuitukana CCM.

Msikilize hapo  chini.

Lowassa Azidi Kushangaza Watu, Maelfu Wajitokeza Dodoma, Hapa Angalia Picha Sita za Mafuriko Hayo Dodoma

$
0
0




Lowassa Azidi Kushangaza Watu, Maelfu Wajitokeza Dodoma, Hapa Angalia Picha Sita za Mafuriko Hayo Dodoma

Picha Za Wasanii Maarufu Wa Bongo Movie Wakiwa Katika Msafara Wa Kampeni Za Magufuli

$
0
0
Baadhi ya nyota wa Bongo Movie wakiwa katika basi lao kwenye msafara wa kampeni za mgombea Urais kwa tiketi ya CCM Dkt. John Pombe Magufuli.

 Wasanii hawa na wengine wengi wa kiume na fani ya muziki wanamunga mkono mgombea wa CCM 

KIMENUKA..TCRA Waanza Kazi, Wahusika wa Website Feki za Utapeli Wakamatwa..Vicoba Tanzania, Alikiba Saccos, Zitto Kabwe Foundation, Ridhiwan Foundation

$
0
0
Maxmillian Rafael Msacky (wapili kushoto) na Patrick James Natala (wa tatu kulia)  wakiwa mahakama ya kisutu jana Ijumaa.

Watu wawili, Patrick Natala na Maxmillian Msacky wamepandishwa kizimbani katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu wakikabiliwa na mashtaka 10 yakiwamo ya kughushi, kutengeneza tovuti feki na mifumo ya mtandao kwa kutumia majina ya Taasisi, viongozi na wanasiasa.

Akiwasomea hati ya mashtaka jana Wakili wa Serikali, Theophil Mutakyawa akishirikiana na Wakili Mwandamizi Mkuu wa TCRA, Johannes Kalungura walidai kuwa washtakiwa hao walitengeneza tovuti feki kwa kutumia majina ya Taasisi ya Jakaya Kikwete Foundation (Ikulu), TCRA Foundation, Akiba Saccos Social Company, Social Credit and Loans Company, Ridhiwani Social Company, Hisa Tanzania, Zitto Kabwe Foundation, Vicoba Tanzania na Wekeza Fund.

Mutakyawa alidai kuwa washtakiwa hao wametengeneza tovuti hizo feki kati ya Januari na Aprili 2014 jijini Dar es Salaam kinyume na kifungu cha 122 (b) cha sheria ya Kielektoliniki na Mawasiliano ya Posta namba 3 ya 2010.

Mbali na mashtaka hayo, Mshtakiwa Msacky yeye anadaiwa kuwa kati ya 2006 na 2024 kwa njia ya udanganyifu alighushi cheti cha Sekondari namba 0421130 chenye indexi namba S 0260-0001.

Iliendelea kudaiwa kuwa kati ya 2005 na 2014 mshtakiwa huyo alighushi cheti kingine cha Sekondari namba 0217951 chenye indexi namba S 0310-0532,akionyesha ni halali na kwamba vimetolewa na Baraza la Mitihani Tanzania wakati akijua kuwa ni uongo.

Washtakiwa hao walikana mashtaka na upande wa mashtaka ulidai kuwa upelelezi bado haujakamilika na washtakiwa walipelekwa rumande hadi Septemba 28, 2015 itakapotajwa.

Akizungumzia tukio hilo, Mkurugenzi wa Sheria wa TCRA, Elizabeth Nzage alisema kati ya Aprili na Juni katika mwaka wa fedha wa 2014/2015 walipata malalamiko toka kwa wananchi kuhusu kuwepo kwa makampuni feki yaliyokuwa yakidai kuwa yanatoa mikopo kwa muda mfupi.

Nzage alidai kuwa wahusika hao walitumia majina ya wanasiasa na pia kujifanya ni viongozi na wamiliki wa taasisi hizo na kwamba makumpuni hayo yanaandaa shughuli za kuchangisha fedha.
Viewing all 104789 articles
Browse latest View live




Latest Images