Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104793 articles
Browse latest View live

Bango la Daladala Lamkuna Lowassa....“Mnashangaa Lowassa Kupanda Daladala, Mbona Hamshangai twiga Kupanda Ndege”.

$
0
0
Mgombea urais wa Chadema na Ukawa, Edward Lowassa alishangaza wapinzani wake wakati alipofanya ziara za kushtukiza jijini Dar es Salaam, ikiwa ni pamoja na kupanda daladala, lakini wananchi mkoani Singida walimsaidia kutoa jibu.

Lowassa, Waziri Mkuu wa kwanza wa Serikali ya Awamu ya Nne aliyejiondoa CCM mwishoni mwa Julai, alikuwa akizungumza na wananchi wa Manyoni mkoani Singida kwenye Uwanja wa Shule ya Msingi ya Tambukareli.

Katika umati wa watu waliofurika kwenye mkutano huo, kulikuwa na mwananchi aliyebeba bango lililoandikwa “mnashangaa Lowassa kupanda daladala, mbona hamshangai twiga kupanda ndege”.

Wakati akimaliza hotuba yake, Lowassa aligeuka upande wa kushoto na akaliona bango hilo likiwa limenyanyuliwa juu. Kabla ya kulisoma alicheka, halafu akalisoma kwa sauti na kuendelea kucheka, kitu kilichowafanya wananchi waungane naye kucheka na baadaye kushangilia.

Kabla ya kuzindua kampeni zake kwenye viwanja vya Jangwani jijini Dar es Salaam mwishoni mwa mwezi Agosti, Lowassa alifanya ziara kadhaa za kustukiza alizozielezea kuwa zililenga kufahamu matatizo ya wananchi.

Alipanda dalkadala kutoka Gongo la Mboto kwenda Chanika wilayani Ilala, kutembelea sokoni Tandale wilayani Kinondoni na Mbagala wilayani Temeke. 
  
Safari zake, ambazo zilipigwa marufuku na taasisi za Serikali, zilimsha mjadala, huku wapinzani wake wakimponda kuwa alikuwa wapi kujua matatizo ya wananchi kabla ya kugombea urais.

Twiga waliopandishwa ndege kutoka Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro na kupelekwa Arabuni waliibwa kwenye moja ya mbuga za mikoa ya kaskazini, na mtuhumiwa katika kesi hiyo alitoweka nchini na kusababisha mdhamini wake kuhukumiwa kwenda jela.

Katika mkutano wa jana, Lowassa pia alikabidhiwa funguo iliyoandikwa “Lowassa ni kiboko cha makufuli mabovu”, ujumbe unaolenga kumrushia kijembe mgombea wa CCM, Dk John Magufuli.

Kwenye mkutano huo, Lowassa alirejea wito wake wa kuwataka wananchi wanaojitokeza kwa wingi kwenye mikutano yake wahakikishe wanajitokeza kumpigia kura ili kuiondoa CCM madarakani.

“Msifurike tu kwenye mikutano, bali mnipigie kura,” alisema Lowassa ambaye alikuwa akishangiliwa wakati wote.

“Nimekuja kuwaombeni kura kila mmoja wenu anipe. Wakatalieni watakaotaka kuchukua shahada zenu. Nataka kura zaidi ya milioni 10. Mwambieni shangazi, mama, baba na hata mshikaji akapige kura na kazi ya pili iwe kuzilinda.” 
  
Mwaka 2010 watu waliojitokeza kupiga kura hawakufika milioni 9, lakini Taasisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) inakadiria watu milioni 24 kujitokeza kujiandikisha kupiga kura mwaka huu. 
  
Hadi sasa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) haijatangaza idadi ya watu waliojiandikisha.

Akizungumzia matatizo ya wananchi, Lowassa alisema kwa miaka 50 Serikali ya CCM imeshindwa kuwapa huduma bora na hivyo kilichobakia ni kuiondoa.

“Hamna maji, hampati huduma bora ya afya, kilimo bora hamna, sasa mna nini bora,” alisema Lowassa na wananchi kumjibu, “hamna kitu tunakutaka wewe utusaidie”.

Lowassa alisema Serikali atakayoiunda itakuwa ya aina yake, na ambaye hataweza kuhimili vishindo vya utendaji kazi, atakaa pembeni.

“Watu wanafurika kwenye mikutano yangu mikoani, hii inaashiria kuwa watu wanataka mabadiliko na hayo yanatakiwa kufanyika katika kura. Kama CCM wameshindwa kufanya mabadiliko kwa miaka 50 wataweza sasa,” alihoji na kuamsha shangwe kutoka kwa maelfu ya wananchi kwenye mkutano huo,

“Muungano huu (Ukawa) utaleta maajabu, wachagueni watu wetu tulete maendeleo.”

Awali, Lowassa alimuita jukwaani mgombea ubunge wa Jimbo la Manyoni Mjini kwa tiketi ya Chadema, Emmanuel Mpandagoya kueleza matatizo yanayowakabili wananchi wa Manyoni.

“Manyoni tuna tatizo kubwa la maji. Wananchi wameahidi kukupa kura, lakini ukiwa Ikulu kumbuka maji ni kero kubwa hapa,” alisema Mpandagoya akizungumzia tatizo hilo linalozungumzwa karibu katika mikutano yote.

“Pia tuna tatizo la huduma za afya, ukiwa rais, mimi mbunge wako nitakupigia simu kukukumbusha kuwa hospitali hazina dawa na baadhi ya vijiji havina zahanati.

“Tuna tatizo kubwa la walimu wa masomo ya sayansi na wengi wanaidai Serikali ya CCM na hawajalipwa madai yao. Hapa Manyoni kila kona watu wanatozwa ushuru wa bidhaa, umeme umekuwa hadithi. Hizo ndizo kero kubwa za watu wa Manyoni.”

Akieleza jinsi atakavyomaliza matatizo hayo Lowassa alisema atashughulikia tatizo la maji hadi suluhisho lipatikane.

“Nawahakikishia wakazi wa Manyoni mkinichagua, kero ya maji itakuwa historia katika wilaya yenu nitalishughulikia tatizo hili mpaka maji yapatikane, haiwezekani tangu uhuru hamna maji sasa mnafaidi nini na haya ndio maisha bora kwa kila Mtanzania?” alihoji.

Kwa mujibu wa takwimu za Taasisi ya Taifa ya Takwimu (NBS), takriban asilimia 80 ya watu wanaoishi mijini wanapata maji ya bomba wakati takriban asilimia 50 ya watu wanaoishi vijijini ndiyo wanaopata maji ya bomba. Inakadiriwa kuwa idadi kubwa ya Watanzania wanaishi vijijini.

Awali, mwanasheria mkuu wa Chadema na mbunge wa Singida Mashariki aliyemaliza muda wake, Tundu Lissu alisema Lowassa analipwa asilimia 80 ya mshahara wa Waziri Mkuu Mizengo Pinda, lakini yeye na wenzake wameamua kujiondoa CCM na kupoteza stahiki zao nyingi kwa ajili ya kuwapigania wananchi.
  
“Sumaye na Lowassa wanahangaika na sisi ili watusaidie kuvuka kipande kidogo kilichobakia. Tunachotakiwa ni kushirikiana ili kuiondoa CCM madarakani,” alisema Lissu.

Lowassa pia alifanya mikutano Singida Mjini, Kondoa mkoani Dodoma na Ikungi ambako aliwataka wananchi kumchagua Lissu kwa mara ya pili kuwa mbunge wa jimbo la Singida Mashariki na kueleza jinsi ilani ya uchaguzi ya Chadema na Ukawa itakavyokuwa na manufaa kwa wananchi kutokana na kuwajali wakulima na wafugaji pamoja na elimu kuwa bure kuanzia darasa la kwanza hadi chuo kikuu.

Mbunge huyo wa zamani wa Monduli leo ataendelea na mikutano mkoani Singida na kesho atakwenda Mkoa wa Shinyanga.

Taarifa kuhusu Watanzania walioko Mecca Saudi Arabia baada ya ajali kutokea Msikiti Mkuu..

$
0
0
Moja ya Habari zilizogusa Vichwa vingi vya Habari Duniani September 12 2015 ilikuwa Breaking News ya kuanguka kwa winch ya kujengea ambayo ilikuwa inatumika kwenye ujenzi wa eneo la pembeni ya Msikiti Mtakatifu wa Mecca, uliopo Saudi Arabia ambako waumini wengi wa Dini ya Kiislamu huwa wanakwenda kwa ajili ya Hijjah.

Taarifa Rasmi kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa imetolewa na inahusu hali ya Watanzania ambao wako Mecca kwa ajili ya Hijjah… Taarifa hiyo inasema hakuna Mtanzania yoyote ambaye amejeruhiwa wala kuumia kutokana na ajali hiyo.
Idadi ya watu waliofariki ni 107 na wengine 200 wamepata majeraha… MUNGU awapumzishe kwa amani wote waliofariki na awape nafuu pia wote waliopata majeraha kwenye ajali hiyo.

Hapa ninazo picha kutoka MICHUZI BLOG ambazo zinaonesha baadhi ya Watanzania walioko Mji wa Mecca, Saudi Arabia… kati yao yumo pia Mchekeshaji na Mwigizaji King Majuto.



Baada ya kushinda pambano la 49, Floyd Mayweather anaachana na mchezo wa Ngumi??

$
0
0
Bondia Floyd Mayweather ni jamaa mwenye rekodi nzuri ambayo ameijenga kwa kipindi chote cha miaka yote 19 aliyoitumia kwenye mchezo wa ngumi..Usiku wa kuamkia leo September 13 2015 kaiendeleza rekodi hiyo kwa kujiandikia ushindi mzuri baada ya kumpiga Bondia Andre Berto… Baada ya hapo kuna kinachofuatia??

Stori ni nyingi kuhusu pambano lake na Manny Pacquiao kurudiwa, kuna stori kuhusu jamaa kuachana na mchezo wa Ngumi >>> ‘Nimekamilisha kila kitu, nimefanya kila kitu kwenye mchezo wangu… Umri wangu unakaribia miaka 40, hakuna nilichobakiza kwenye Ulimwengu wa Ngumi, nahitaji kutumia muda mwingi zaidi na familia yangu‘>> Hii ni moja ya nukuu ya alichokisema Floyd Mayweather baada ya pambano lake na Berto kuisha.

Baba yake Floyd anasema jamaa alilalamika sana maumivu ya mkono wakati akiendelea na pambano na Andre Berto, lakini hakuona kama ni tatizo kwa vile anaelekea kustaafu… Mayweather amemshinda Berto na kuandika headlines za ushindi wa 49 tangu alivyoanza mchezo wa Ngumi mwaka 1996.

Wanawake Wengi Walioolewa ni Wepesi wa Kuchepuka..Yaani Simple Kama Kumsukuma Mlevi

$
0
0
Wanawake wengi walioolewa wamekuwa wepesi (achilia mbali vidada ambavyo havijaolewa, ingawa navyo ni majanga lakini, afadhali mitego yao kidogo ni negotiable).

Wengi wao huwatongozi ila watakutongoza wenyewe! Kundi risky zaidi ni la wamama wa nyumbani au wanawake ambao hawajasoma (I am sorry to say this)!

Unaweza kukuta mme wake ana fedha na kila kitu, lakini kwa sababu jamaa hajaajiriwa serikalini au kwenye taasisi au kampuni (kumbuka tulio wengi tunatamani kujiajiri!), mke wake anamchukulia kama mtu fulani ambaye hana hadhi nzuri ya kuwa mme.

Sumaku kali zaidi ambazo huwavuta wamama wa aina hiyo, ni wale vijana au watu wazima walioajiriwa, wanaotoka asubuhi, wamepiga tai, kiatu kiwi full time, wengine suti, halafu ni watu wa misheni town (wenye magari sijui inakuwaje, mtatuambia), (haata kama kazi zao ni kufagia au kuzunguka na mafile maofisini)!

Wanawake wa aina hiyo huanza kwanza kwa kutafuta ukaribu na mazoea na watu wa aina hiyo kwa udi na uvumba katika harakati za kufanikisha azma zao.

Licha ya uzoefu nilioushuhudia juu ya wamama hapo juu, hivi karibuni nimekumbana na majanga kadhaa yakihusisha wanawake walioolewa kwa ujumla, wengi wao wanaoonekana ni sex hungry moms au gold diggers. Nawapa tu mifano michache kuthibitisha haya ninayoyasema:

1. Mie nakaa mwenyewe mmama from no where akaanza kuniletea chakula (niliogopa sana), akaniambia naona unapata shida unakaa mwenyewe na wewe ni mwanaume huwezi kujipikia.

Siku ya kwanza sikukila (nilikiweka kwenye chombo changu nikampa sahani, baadaye nilikimwaga), maana niliona kama labda kaweka kitu. Siku nyingine akaleta na kuniambia tule wote! Hooooooooo, nikamwambia tutakula wapi?

Akasema kwako, usiogope mme wangu amesafiri! Sasa tukiwa tumekaa, alikuwa amejifunga kanga moja, anatawanya miguu na kuirudisha, nilijikaza sikufanya chochote, vituko anavyonifanyia mpaka sasa ni siri yangu.

2. Mwingine alipata namba yangu kupitia simu ya mmewe ambaye ni rafiki yangu, kila mara hasa usiku ana msgs kama hizi: "shem habari, nahisi wewe ni mcheshi, huna kiburi wala makuu, tena unachat na mimi bila shida, nina hamu siku moja nije Dar nikufahamu, au sio shem?"

Mara nyingi sijibu, akiona hivyo "shem nijibu basi, usiogope maana mme wangu hayupo sasa hivi". Vituko vyake siku hizi havisimuliki!

3. Mwingine, kutwa kulalamika kuhusu maisha yake na ndoa "Yaani shem, we acha tu, maisha magumu, rafiki yako naye kipato hakieleweki na mie sikusoma wala kubahatika kuajiriwa, maisha yanaenda tu kwa nguvu za Mungu, ningekuwa sio mvumilivu sidhani kama hii ndoa ingekwepo, shem unakaa wapi nije kukusalimia au una mke?" Mie najiuliza hivi wakati wa kufunga ndoa hakuapa kuwa na mmewe kwa shida na raha?

4. Mwingine ni mama jirani yangu, tena ni mtu anayejiweza, siku moja akaniita anaomba nimsaidie kurudishia taa imeungua, nilivyopanda juu ya meza alinipa taa - tube light mbovu, kuiweka haiwaki, akaniambia naomba simu yako nimpigie kijana fulani wa mtaani aniletee taa nyingine, nilivyompa kumbe alijipigia, halafiu akaniambia hapatikani, acha.

Tangu awe na namba yangu, utaona mida ya saa 4 usiku anatuma msgs kama vile "Mambo, Jumamosi hii twende tukatembee" au "Nina kitu nataka kukuambia ila tunahitaji faragha", Huwa namjibu, nina mambo mengi, labda siku nyingine.

Ni majanga mengi sana nakutana nayo yanayohusisha akina mama walioolewa. Mliooa kuweni makini na wake zenu, wengi ni washenzi sana na wana sophisticated means za kuwaengage wanaume wengine kwenye mahusaiano na wao! Pia najiuliza tatizo lao la kuzoeana na wanaume wengine na kujifanya wana hamu ya kuchat au kuwa karibu nao na sio waume zao ni nini?

NB: Nawaasa vijana kukaa mbali na mke wa mtu, maana mke wa mtu ni zigo la madawa ya kulevya.

Quote of The Day:
“The sky has never been the limit. We are our own limits. It’s then about breaking our personal limits and outgrowing ourselves to live our best lives.”

Mambo Yaliyombeba Magufuli Mikoa 11 Aliyofanya Kampeni

$
0
0
KAMPENI za mgombea urais wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dk John Magufuli, zimemalizika katika mikoa 11 jana, kwa kumalizia katika Mkoa wa Simiyu, huku ajenda kadhaa na ubora wake wa kutawala jukwaa, vikimng’arisha mgombea huyo na kumfanya kuwa kivutio cha wananchi.

Mpaka sasa Dk Magufuli ameshafanya kampeni katika mikoa ya Katavi, Rukwa, Songwe, Mbeya, Njombe, Ruvuma, Mtwara, Morogoro, Tanga, Mara na jana alifikisha mkoa wa 11 Simiyu.

Kabla ya kufika Mara na Simiyu, takwimu za CCM zilizotolewa na Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi, Abdalah Bulembo, zimeonesha katika mikoa hiyo mingine tisa, Dk Magufuli alikuwa ameshasafiri kwa barabara katika wilaya 42 na kufanya mikutano 48 iliyo katika ratiba na mikutano mingine 260 isiyo rasmi.

Moja ya ajenda kubwa iliyombeba Dk Magufuli katika mikutano hiyo mpaka Simiyu, ilikuwa uadilifu katika utendaji wake wa kazi katika wizara mbalimbali alizofanya kazi katika miaka 20 ya utendaji wake, ikiwemo katika Wizara ya Ujenzi, ambako ametumikia kwa miaka 15.

Uadilifu
Katika mikoa mingi alikopita, uadilifu wake umezungumzwa kwa namna tatu tofauti, ikiwemo mwenendo alioonesha katika nafasi yake ya Waziri katika Wizara ya Ujenzi, iliyokuwa ya kipaumbele kibajeti.

Kwa mfano katika Bajeti ya Serikali kwa mwaka huu wa fedha 2015/2016, Wizara ya Ujenzi imekabidhiwa Sh trilioni 1.2 za wizara, huku Mfuko wa Barabara ulio chini ya wizara hiyo, ukikabidhiwa zaidi ya Sh bilioni 866 na hivyo kwa ujumla kukabidhiwa Sh trilioni mbili, ambazo amepaswa kuzisimamia.

Kwa mujibu wa Dk Magufuli mwenyewe, akipiga hesabu ya fedha za umma alizosimamia kwa ajili ya miradi ya ujenzi wa barabara katika miaka kumi ya uongozi wake, ni zaidi ya Sh trilioni 9.5, lakini hakula hata senti tano, badala yake akajenga mtandao mrefu wa barabara za lami nchi nzima.

Namna ya pili ya kuzungumzia uadilifu wake ni ushirikiano wake na watendaji na wadau wa sekta ya ujenzi, ambao amekuwa akiwapa kazi za mabilioni ya shilingi, katika kuwatumikia Watanzania.

Namna ya tatu iliyotumika kuelezea uadilifu wa Dk Magufuli, imeelezwa na Jaji Joseph Warioba mkoani Mara, ambapo alisema mwaka 1996, aliteuliwa na Rais Benjamini Mkapa, kuongoza Tume ya Kero za Rushwa.

Katika uchunguzi wao, Jaji Warioba alisema walibaini rushwa kubwa na nyingi zilikuwa katika sekta ya ujenzi wa barabara, lakini akafafanua baada ya Dk Magufuli kuanza kufanya kazi katika sekta hiyo, kelele ya rushwa katika sekta hiyo imetoweka.

Uchapakazi
Mbali na uadilifu, ajenda nyingine iliyombeba Dk Magufuli na kusababisha awe kivutio kikubwa kwa maelfu kwa maelfu ya wananchi waliojitokeza katika mikutano yake, ni sifa ya uchapakazi wake ambayo imeendana na matokeo yanayoonekana ya kazi hiyo.

Mbali na watumishi, ukali wake pia umejidhihirisha mara kwa mara alipozungumzia Baraza la Mawaziri atakalounda na hasa Waziri wa Ujenzi, akisema huyo waziri atakayemteua, kama hawezi kazi aseme mwenyewe kabla ya kutimuliwa, kauli ambayo pia imepokewa kwa shangwe na wananchi.

Ubora jukwaani
Dk Magufuli pia katika mikoa hiyo 11, ameonesha umahiri mkubwa wa kutawala majukwaa kwa mbinu mbalimbali, ikiwemo uwezo wa kutoa salamu na vionjo vya makabila zaidi ya kumi jambo lililokuwa likiwavutia wananchi wengi katika mikutano ambayo imekuwa ikifikia mpaka 15 kwa siku.

Akifafanua sababu ya kutumia lugha za makabila mbalimbali, Dk Magufuli amekuwa akisema mwitikio wa salamu hizo, umekuwa ukionesha namna jamii ya Tanzania ilivyo na umoja kwa makabila mbalimbali kukutana katika mikutano yake na kufurahia pamoja.

Mara kadhaa baada ya kutoa salamu hizo, alikuwa akimalizia kwa kusema hiyo ndio Tanzania yenye kila mchanganyiko wa kabila, lakini wanaishi kwa umoja na amani bila aina yoyote ya ubaguzi.

Baada ya kutoa salamu hizo, Dk Magufuli pia amekuwa akiomba kura kutoka kwa vyama vyote, kuanzia CCM, Chadema, CUF, NCCR-Mageuzi, ACT na kwa watu wasio na vyama, huku akiwaambia kuwa kazi yake itakuwa kuwaletea maendeleo na kwa kuwa maendeleo hayabagui, ndio maana anaomba kura za vyama vyote.

Ahadi zake
Dk Magufuli katika mikutano hiyo, amekuwa akiahidi kushusha bei ya vifaa vya ujenzi hasa saruji, mabati na misumari, ili wananchi wanaofanya kazi wajenge nyumba bora.

Katika kuongeza idadi ya Watanzania wanaofanya kazi ili kufikia lengo hilo, Dk Magufuli alisema katika kila mtaa na kijiji, Serikali yake itatoa Sh milioni 50 kwa ajili ya kuanzisha na kukuza biashara ndogo za wanawake na vijana.

Alisema atataka kila anayefanya kazi apate kipato kizuri kitakachomsaidia kukabiliana na mahitaji ya maisha yake, ikiwemo kujenga nyumba bora kutokana na kushushwa kwa bei za bidhaa za ujenzi.

Prof. Mark James Mwandosya Kuhamia Upinzani?

$
0
0
Mark James Mwandosya
Tangu jana kumekuwa na taarifa za moja kati ya makada maarufu na wenye ushawishi ndani ya CCM Prof.Mark Mwandosya kuhamia upinzani, taarifa hizo zimekuwa zikienea kwa kasi sana na kuchagizwa vilivyo na vibaraka wa propaganda za CHADEMA na UKAWA bwana Yeriko Nyerere na wenzake.

Baada ya kuendelea kuzagaa kwa taarifa hizo nimeamua kufanya uchunguzi wangu binafsi dhidi ya madai hayo lakini nilichoambiwa na mmoja kati ya watu wa karibu sana wa Prof.Mwandosya na familia yake ameniambia kuwa PROFESA mara kadhaa amekuwa akihojiwa na watu mbalimbali wakiwemo waandishi wa habari pamoja na baadhi ya wanachama na makada waandamizi wa chama amekuwa akijibu na kusisitiza kuwa HANA MPANGO WA KUHAMA CCM.

Aidha duru za udadisi zinaeleza kuwa PROFESA kwa sasa yupo nchini MAREKANI katika shughuli zake binafsi.
Kwa kuwa wakati ni ukuta nadhani tusubiri tuone ataamua nini, kwenda kujivua nguo upinzani kama SUMAYE na mwenzie LOWASSA au ataendelea kulinda heshima na utu wake akiwa ndani ya CCM.

MUNGU IBARIKI TANZANIA
MUNGU BARIKI UCHAGUZI
MUNGU MUONGEZE PROFESA MWANDOSYA KATIKA KUTOA MAAMUZI YAKE
AMEN.

By Kawakama

Orijino Komedi Wanapo Kashifu Afya ya Lowassa, Wamesahau ya Mwenzao VENGU?

$
0
0
Afya ni majaliwa ya Mungu,leo kundi la OK linasimama majukwaani kwenye kampeni za ccm hata kutoa post mitandaoni za kudhihaki afya ya Lowassa wamesahau yalimpata mwenzao Vengu? mwaka wa nne leo yuko kitandani.ikumbukwe huyu jamaa alikua ni bingwa wa kumuigiza Mrema na maradhi yake kwa bahati mbaya Mungu kampiga kofi leo hii yeye ndio yuko kitandani na Mrema huyoooo yuko mzima kabisa.

Tukumbuke tunayo yafanya Mungu anatuona.kuna Leo na kesho.

Magufuli azidi kuinanga CCM Kwa Kuicha Nchi Katika Dimbwi la Umaskini

$
0
0
MGOMBEA urais kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dk. John Magufuli anaendelea kukosoa Serikali ya CCM inayomaliza muda wake kwa kuiacha nchi katika dimbwi la umasikini.

Akiwa kwenye mkutano wa kampeni Uwanja wa Mkendo, wilayani Musoma, Mkoa wa Mara, amesema yapo mambo mengi hayapendi kwa sababu yanawaumiza wananchi na akichaguliwa kuwa rais atayabadilisha.

Ameutaja mradi wa maji uliopangwa kutekelezwa kupitia ziwa Victoria, aliosema kila siku unatajwa lakini hautekelezwi huku wananchi wa Mkoa wa Mara wakiendelea kupata shida ya maji.
Amesema haina maana kuwa na Waziri wa Maji wakati kunakuwa na mradi usiokwisha, akiwahakikishia wananchi kuwa atakapokuwa Rais, hawezi kushindwa kupata Sh. Bilioni 44 za kutekeleza mradi huo.

Dk. Magufuli ambaye amekuwa waziri katika serikali ya CCM kwa muda mrefu tangu alipoteuliwa kwa mara ya kwanza naibu waziri wa ujenzi mwaka 1995.
Kufufua viwanda vilivyo uliwa na watu kwa makusudi ambako kulikuwa na viwanda vingi ambavyo vimekufa mikononi mwa serikali ya CCM

“Naombeni kura zenu wananchi wa Musoma ili tuwatoe watu waovu kwani Serikali haitoki, watatoka watu wabaya ambao nitawatoa haraka sana,” amesema.

How Does DIAMOND Feel When Eating This, Look at ZARI’s thayos (PHOTOs)

$
0
0


How does DIAMOND feel when eating this, Look at ZARI’s thayos (PHOTOs)

Dr Kessy Anakuletea Dawa za Kutengeneza Hips, Makalio, Nywele na Nguvu za Kiume Kwa Kutumia Dawa za Asili zisizo na Kemikali

$
0
0
PENDEZA NA KESSY PRODUCT.
PATA DAWA ZA ASILI ZISIZO NA MADHARA WALA KEMIKALI YOYOTE,
NA MATOKEO KUANZIA WEEK (2) ADI (4) NAKUENDELEA
1) KUTOA MVI SUGU 70,000/
2) REFUSHA NYWELE NA KUZUIA KUKATIKA 50,000/
3) TENGENEZA SHEP HIPS NA MAKALIO KWA
@ KUPAKA 50,000/
@ DAW YAMAJI 80,000/
@ VIDONGE 100,000
4) PUNGUZA TUMBO NA NYAMA UZEMBE KWA
@ KUPAKA 55,000/
@ KUNYWAA 80,000/
@ MKANDA WENYE DAW 80,000/
@ BELT 150,000/
5)PUNGUZA MWILI MZIMA PAMOJA NA KILO 80,000/
6) ONGEZA UNENE WA MWILI MZIMA NA HAMU YAKULA 80,000/
7) PUNGUZA MAZIWA NA KUYASIMAMISHA 50,000/
8) ONGEZA MAZIWA SAIZ UNAYOTAKA 50,000/
9) ONGEZA NGUVU ZA KIUME KWA DAW
@ JELI YAKUPA 50,000/
@ VIDONGE 70,000/
10) ONGEZA MAUMBILE YA KIUME KWA
@ JELI YAKUPKA 100,000
@ MASHINE YA HUNDSOME UP 170,000/
11) KUWA MWEUPE MWILI MZIMA NA KUWA SOFTI 70,000/
12) TOA CHUNUS,MADOA,MAKOV 45,000/
13) RUDISHA USICHANA (BIKRA) 60,000/
14) TOA MICHIRIZI (STERCH MARKS) 50,000/
15) ONDOA NGIRI ZAAINA YOYOTE 60,000/
16) TUNDISHA NYWELE ZILIZO ISHA (KIPARA) 150,000/
17) TOA MICHUBUKO KWENYE MAPAJA NA SEHEM ZA SIR 60,000/
18) RUDISHA HAMU LA TENDO NA KUFANYA BILA KUCHOKA 60,000/
19) TOA NDEVU KWA WANAWAKE 80,000/
NA HUDUMA NYINGI USISITE  KUSEMA  PIGA SIMU,
TUNAPATIKANA DAR,K-KOO,POSTA NA SINZA.
KWAMIKOWANI UDUMA ITAKUFIKA KWANJIA YA MABASI BILA TATIZO.
CHAKUFANYA PG CIM  0719955528  0756259180  0785371237  Follow
@dr_kessy- product
@dr_kessy -product
@dr_kessy-product
PIA UTALETEWA POPOTE ULIPO

Zitto: Hakika CHADEMA Watamkumbuka Dr. Slaa Baada ya Uchaguzi

$
0
0
Jana katika mahojiano na Tiddo Muhando kwenye kipindi cha Funguka, Zitto Kabwe amewaonya wana CHADEMA wanaomtusi Dr Slaa kwa sababu ya Lowassa kuwa watamkumbuka baada ya uchaguzi. Watu makini kama Dr Slaa na Prof Lipumba wanaondoka na watu eti wanamuona Lowassa leo kawa bora?

Zitto kasema hivi sasa CHADEMA msingi wake umekuwa ni "Lowassa" na si kupambana na ufisadi tena. Baada ya uchaguzi hakutakuwa na CHADEMA ile tuliyoifahamu na ndipo hapo watanzania watakapomkumbuka Dr Slaa.

Tanzania yang'ara kwa Amani! Ya kwanza East Africa...

$
0
0
TANZANIA imeelezwa kuwa nchi yenye amani zaidi na utulivu mkubwa kuliko nchi zote za Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) ikishikilia nafasi ya 55 duniani kati ya nchi 162 ambako utafiti kuhusu hali ya amani na usalama umefanyika.

Utafiti huo unaojulikana kama The 2013 Global Peace Index (GPI) uliofanywa na Taasisi ya Kimataifa ya Uchumi na Amani, ambayo madhumuni yake ni kuchochea maelewano zaidi duniani katika maeneo ya uchumi, biashara na amani, unaonesha kuwa Uganda ni ya pili kwa EAC ikiwa inashikilia nafasi ya 106, Kenya ya 136 na Burundi ni ya 144.

Wakati Tanzania iking’ara kwa mujibu wa ripoti hiyo, Rwanda ni moja ya nchi za mwisho duniani ikionekana kukosa utulivu na amani. Kwa miaka sita iliyopita, Rwanda imewekwa kundi moja na nchi hatari zaidi duniani za Syria na Libya kwa ukosefu wa amani na utulivu.

Kwa kuiweka Rwanda katika nafasi ya 135 miongoni mwa nchi 162 zilizotafitiwa, ripoti hiyo inapingana na msimamo wa Serikali ya nchi hiyo ambayo imekuwa ikisema ni miongoni mwa nchi zenye amani na utulivu zaidi duniani.

Waandishi wa ripoti hiyo wanasema nchi za Ulaya za Nordic ambazo pia zina demokrasia iliyokomaa na kutulia zaidi, ndizo zenye amani na utulivu mkubwa duniani na kuthibitisha uhusiano kati ya utawala wa sheria na ushiriki wa wananchi katika kuwapo ama kutokuwapo kwa amani.

Tanzania imekuwa inapata alama za juu kabisa katika suala la utulivu na amani kwa miaka mingi na zamu hii watafiti wanasema sababu ya kuendelea kwa amani na utulivu huo ni viongozi kuheshimu misingi ya utawala bora likiwamo suala la kuheshimu vipindi viwili vya urais na ukweli, kwamba Tanzania haijapata kukabiliwa na zahama kubwa ya mapambano ya ndani tofauti na nchi jirani.

Ripoti hiyo inasema: “Nchi tatu ambazo zimekuwa na mabadiliko makubwa kwa kuongezeka kwa amani katika miaka sita iliyopita, ni Chad, Georgia na Haiti wakati nchi zilizorudi nyuma kwa haraka na kwa kasi zaidi ni Syria, Libya na Rwanda.”

Lakini hata hivyo, ripoti hiyo imepokewa kwa hisia tofauti nchini Rwanda. Wakati Serikali inaonesha kupingana na matokeo hayo, watu wengine wanayaunga mkono.

Mchambuzi wa masuala ya kisiasa wa chuo kikuu nchini humo, alisema kuna tofauti kati ya amani na usalama, akisisitiza kuwa kutokuwapo vita hakuna maana kuwa wananchi wanaishi kwa amani.

“Amani maana yake ni watu kupata fursa ya maendeleo na kujiendeleza.” Anaongeza: “Watu wanataka kushiriki uendeshaji wa nchi yao. Angalia Bunge letu, si la uwakilishi. Ni jambo la kuchekesha kwamba tuna Rais aliyechaguliwa, lakini si Bunge lililochaguliwa na wananchi.

“Hatuna uhakika na mchakato wa mpito kutoka utawala wa sasa kwenda mwingine. Tunabanwa pia kutokana na uhusiano wetu na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC)…kuweza kutembea usiku bila silaha hakutoshi.”

Aidha, Rwanda inashutumiwa kwa kukandamiza vyombo vya habari na wapinzani wa kisiasa. Inarudi nyuma kwa sababu ya ushiriki wake katika kuchochea uasi ndani ya DRC na ongezeko kubwa la vitendo vya kigaidi na mauaji ndani ya Rwanda yenyewe.

Hivi karibuni, Rwanda imeshuhudia milipuko ya mabomu ambayo Serikali inasema yalilipuliwa na wapinzani wake.

Kuhusu hatua za Serikali ya Rwanda kubana vyombo vya habari na wapinzani wake, maana yake ni kwamba inashuhudia kile kinachoelezwa kwenye Ripoti hiyo kuwa ni ongezeko la kiwango cha vitisho vya kisiasa ikiwa na idadi kubwa ya watu waliofungwa jela, kuyumba kisiasa, kiwango kikubwa cha mauaji na vitendo vya kigaidi.”

Taasisi ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani wa Waandishi Wasio na Mipaka (RWB)inakadiria kuwa uhuru wa vyombo vya habari nchini Rwanda ni mbaya na kuifanya nchi hiyo kuwa moja ya nchi 10 mbaya zaidi duniani ikishikilia nafasi ya 168 kati ya nchi 179 zilizofanyiwa utafiti mwaka jana.

Chanzo: HabariLeo - Juni 25, 2013

Zitto Kabwe Atangaza Nia.. Nitagombea Urais 2020

$
0
0
Taswira na Nuru ya chama,Kiongozi Mkuu wa ACT amekaririwa na Azam TV katika kipindi cha siasa cha Funguka kuwa bado ana ndoto za kuwa rais wa Tanzania.Amesisitiza kuwa 2020 atagombea urais kupitia chama chake.MY TAKE:Kama zigo Mnalo ACT,hivi kweli hiki ni kipindi cha kutangaza nia?

Lowassa Atoa Ujumbe Mzito Usiku wa Kuamkia Leo Kupitia Ukurasa Wake wa Faceook

$
0
0
 Lowassa Atoa Ujumbe Mzito Usiku wa Kuamkia Leo Kupitia Ukurasa Wake wa Faceook
Usome Hapa Chini Nimekuwekea.....

Mgombea Urais Aangua Kilio Jukwaani Kisa Jakaya Kikwete

$
0
0
Jakaya Kikwete
Mgombea urais wa Zanzibar kupitia chama cha Chauma, Mohammed Masod Rashid, amejikuta akiangua kilio jukwaani na kumpigia magoti Rais wa Jamhuri ya Mungano wa Tanzania, Jakaya Kikwete, kumuomba awaachie huru masheikh wa Jumuiya ya Mihadhara ya Dini ya Kiislamu (Uamsho) waliopo gerezani.
Tukio hilo lilitokea katika mkutano wa hadhara wakati akifungua kampeni za chama hicho visiwani hapa.
Mgombea huyo alivuta hisia za wananchi na kila aliyekuwa akipita njia katika eneo hilo la kiwanja cha Komba Wapya kilichopo mjini hapa kusitisha safari yake na kuanza kumsikiliza wakati akiangua kilio.

Mgombea huyo aliacha kunadi sera na kuangua kilio akiwalilia masheikh hao wanaokabiliwa na kesi ya kusaidia ugaidi katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam.

Nakupigia magoti Rais Kikwete naomba uwatoe masheikh wetu kwani unawavunjia haki zao za msingi, alisema mgombea huyo wa urais.
Alisema endapo atapata ridhaa ya Wazanzibari kuwa rais atatoa msamaha kwa wafungwa walioko gerezani ambao wanamakosa madogo madogo.
CHANZO: NIPASHE




Hatimae Mwigizaji Ray Aibuka na Kusema Haya Kuhusu Tetesi za Kuhongwa Mil 50 Aipigie Kampeni CCM

$
0
0
Kufuatia tetesi kuenea mtandaoni kuwa staa wa Bongo Moveis , Vicent Kigosi ‘Ray ‘ amehama UKAWA “team mabadiliko” na kwenda upande wa CCM., Ray amepanga kuvunja ukimya na kutoa tamko lake rasmi juu ya swala hilo.

Kupitia ukursa wake kwenye mtandao  wa  kijamii wa instagram Ray ambaye amekuwa akishambuliwa na baadhi mashakibi wake kwenye mtandao huo wakidai kuwa amenunuliwa , aliandika haya;

Nimeyasikia mengi sana kwenye mitandao ya kijamii ila nasema hivi nitatoa tamko langu soon”.

Nadhani sasa mashabiki wapunguze munkali wasubiri tamko lake.

Unaposema Lowassa mwizi, mwana CCM gani msafi ndani ya CCM?

$
0
0
Ametuibia sisi na tumempenda sisi shida iko wapi? kila siku lowasa mwizi, lowasa mwizi nani msafi ccm? acheni kuhadaa watu, je mkapa msafi? kikwete msafi? kuna kitu mnakijua kuhus lowasa sasa tunamtaka lowasa tuone kwa nini mnamuogopa mtu ambaye kwenu alionekana makapi.

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumatatu ya Septemba 14

$
0
0
Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumatatu ya Septemba 14













Lowassa: Msifanye Kosa Kuichagua CCM Mtakuwa Mmejiangamiza

$
0
0
Mgombea urais iliyesimamishwa na Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa) kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Edward Lowassa,  ametua katika Jimbo Singida Kaskazini la Waziri wa Maliasili na Utalii, Lazoro Nyalandu, huku akiwatahadharisha wananchi wasipompigia kura za kuitosha kuiondoa CCM madarakani watakuwa wamejiangamiza.

Aidha, alimwelezea Nyalandu kuwa anamfahamu mbunge huyo kwa mbwembwe na nguvu ya fedha na kuhoji kama mgombea ubunge kupitia Chadema katika jimbo hilo, David Jumbe atamuweza.

Akizungumza na mamia ya wananchi wa kijiji cha Ilongero, Jimbo la Singida Kaskazini  jana ikiwa ni mfululizo wa ziara zake ya kuomba ridhaa kwa wananchi wamchague awe rais wa awamu ya tano, Lowassa alisema CCM itaondolewa madarakani kama wananchi wengi watajitokeza kupiga kura ya kuikataa.

“Watu wanataka mabadiliko ya maisha yao na sisi tumejitolea kuleta mabadiliko hayo,suala la kura ni muhimu sana mabadiliko yatakuja kwa kupiga kura tusipopata kura za kutosha tumeeangamia,” alisema.

Lowassa ambaye hadi sasa amefanya mikutano ya kampeni zaidi ya  32 katika majimbo ya mikoa 11 aliyotembelea, alisema CCM imeshindwa kuleta mabadiliko ya maendeleo na maisha ya wananchi yameendelea kuwa magumu.

“Wakati wa mchakato wa kumpata mgombea urais ndani ya CCM Nilisema huwezi kuzuia gharika kwa mkono, sasa wameona gharika ya watu, tumekwenda Mpanda, Tabora, Iringa na leo (jana) hapa kwenu hivyo hivyo watu ni wengi,” alisema.

Mgombea huyo wa Ukawa aliwataka  wananchi wasikubali kura ziibwe na kutaka apatiwe kura si chini ya milioni 12 ili awe Rais.

Alisema serikali ya CCM imekuwa ikiahidi mambo mengi lakini haiyatekelezi na kwamba serikali atakayoiunda itakuwa ya vitendo kwa kutekeleza mambo yote.

Lowassa aliahidi akichaguliwa ataanzisha viwanda  vya alizeti na vitunguu ili viwe vinasafirishwa kwenda masoko ya nje.

 Kuhusu Nyalandu                 
Akimzungumzia Mbunge wa Jimbo la Singida Kaskazini, Nyalandu, alisema anamfahamu kwa mbwembwe nyingi.

“Namfahamu Mbunge wenu wa sasa, namfahamu kwa mbwembwe zake sasa namulize Jumbe (mgombea Chadema) utamuweza maana kuna nguvu ya pesa na nguvu ya mtu,” alisema.

Hata hivyo, Jumbe alijibu kuwa tayari ameshamshinda Nyalandu.

Katika hatua nyingine wazee wa mila wa kabila la  kimasai na kinyatulu walimkabidhi Lowassa fimbo na mgolole ili aitumie kwa ajili kuwachapia wezi ili wasimzue kuingia Ikulu na kumtaka asiiache kila aendako.

Mgombea Ubunge CHADEMA
Naye mgombea ubunge wa Chadema Jimbo la Singida Kaskazini, David Jumbe, alimweleza Lowassa kuwa jimbo hilo linakabiliwa na kero za ubovu wa barabara, ukosefu wa soko la kuuzia mazao na hivyo wakulima kulanguliwa na wafanyabiashara.

“Mfano soko la vitunguu ikifika wakati wa mavuno wafanyabiashara kutoka Kenya wanakuja kwa wingi na kununua vitunguu na kwenda kuviuza nje kama bidhaa iliyozalishwa nchini mwao,” alisema.

Alisema kama akichaguliwa, askari wote wa mgambo watapewa majembe wakalime kwa sababu kazi ya kusimama kwenye mageti kwa ajili ya kutoza ushuru haitakuwapo na miti iliyopo katika mageti hayo itageuzwa kuwa kuni.

Tundu Lissu
Kwa upande wake, Mwanasheria Mkuu wa Chadema, Tundu Lissu, alisema CCM haiwezi kuleta mabadiliko yeyote na hata ahadi ya Sh. milioni 50 kwa kila kijiji ni danganya toto.

“ Lowassa ametukanwa na tumemsema sana lakini ukweli wa Mungu hakufanya kosa lolote binafsi na hata wanaomtukana leo ni kwa sababu ameondoka CCM na siyo kwa sababu ya kashfa ya Richmond” alisema.

Laurence Masha
Naye aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Ndani, Laurence Masha, aliwataka  wananchi waiogope CCM, akisema  imesababisha mateso makubwa kwao.

“Mtakayemuona ananunua shahada za kupigia kura katika eneo lenu, makamateni, mshughulikie na mtoweni katika eneo lenu,” alisema.

Mgeja
Kwa upande wake, aliyekuwa Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Shinyanga, Khamis Mgeja, alisema wanaotoka ndani ya CCM ni watu safi na waonang’ang’ania ni wachafu.

“Tunapofanya mabadiliko tujiamini, Ikulu siyo ya Mangula wala Nape, nchi nyingi za Kiafrika zimefanya mabadiliko kwa kuviangusha vyama tawala kwanini isiwezekane Tanzania,” alisema.

Jimbo la Iramba Magharibi
Akihutubia wananchi wa mjini Kiomboi katika  Jimbo la Iramba Magharibi, Lowassa aliahidi kuwa akichaguliwa ataanzisha benki ya bodaboda.

Uwoya Awapa Makavu Wasanii Wasio Jitambua Wasio ona Mchango wa Kikwete na Kuamua Kumsapot Mtu Ambaye Hajawai Watambua

$
0
0
Irene Uwoya 
Staa wa Bongo Movies, Irene Uwoya ambaye ameshapitishwa na hama chake cha CCM kuwania ubunge wa viti maalum amewapa makavu baadhi ya wasanii wenzake wa bongo movies ambao hawakiungio mkono chama cha mapinduzi wakati baadhi yao walikuwa karibu sana na Rais Kikwete anaye maliza muda wake.

Kupitia kurasa wake kwenye mtandao picha wa instagram,  Uwoya awachana wa sanii hao kuwa yule wa nao muunga mkono hakuwahi kuwathamini hata siku moja.

"Sasa narudi kwa wasaniii wasio jitambua!katika tasnia yetu ukweli usio pingika Mh.Kikwete amekuwa karibu Sana na wasaniii na ametufanya tudhaminike.

Lakini chaajabu kunawatu wanajifanya hawajui mchango wake, kiukweli inaumiza sana!

Kunawatu walikuwa wanashinda Ikulu na Mh, anawasaidia sana katika kazi zao lakini leo wamesahau yote na kumsapot mtu ambaye hajawahi hata kuwatambua kwanafasi zao, kama sio ushabiki maandaz niniii? Loooo!!!aibu".Uwoya aliandika.
Viewing all 104793 articles
Browse latest View live




Latest Images