Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104808 articles
Browse latest View live

Kajala Masanja Anatoa Wapi Jeuri Hii ya Fedha....?

$
0
0
Imelda mtema
FEDHA inaongea! Ndivyo unavyoweza kusema kufuatia mwigizaji Kajala Masanja kupanga kwenye mjengo mpya wa maana na kuushehenesha samani na ‘vikorombwezo’ kibao hadi kufikia hatua ya watu kuhoji, amepata wapi jeuri hiyo ya fedha? Ijumaa limenasa mchapo kamili.
Mjengo anaoishi mwigizaji Kajala Masanja.
Kajala ambaye awali alikuwa akiishi maeneo ya Sinza-Madukani, kwa sasa amehamia katika mjengo huo mpya uliopo maeneo ya Mwenge jijini Dar.Kwa mujibu wa chanzo, ndani ya mjengo huo, Kajala anaishi na mwanaye Paula huku akiwa amewaajiri wafanyakazi wa ndani watatu na kulindwa na kampuni maalum ya ulinzi.
“Yani Kajala ananuka hela. Mjengo wake mpya una kila kitu ndani. Ukiingia unaweza kupagawa kutokana na vitu vilivyomo ndani. Watu tunajiuliza ni nani anayempa jeuri hii maana filamu pekee haziwezi kufanya matusi haya,” kilisema chanzo hicho.
...Sebuleni.
Baada ya kupenyezewa ‘ubuyu’ huo, mwanahabari wetu alitia timu nyumbani hapo kwa Kajala na kujionea nyumba hiyo ya kifahari aliyopanga sambamba na ‘mazagazaga’ kibao ya thamani yaliyomo ndani.
Alipoulizwa amepata wapi jeuri ya kupanga nyumba hiyo ya gharama ambayo hakutaka kutaja bei ya kodi, kuajiri wafanyakazi watatu na kampuni ya ulinzi, Kajala alidai mambo yote hayo ameyafanikisha kwa kazi ya mikono yake na si vinginevyo.
“Unajua kuna kipindi cha nyuma nilitengeneza filamu zangu kama tano na nilikuwa na maana hata kama nisingepata zile hela kwa wakati ule lakini nilijua baadaye nitapata hela nzuri na nitatengeneza maisha yangu hivyo sasa ndiyo nimevuna matunda ya sinema hizo na kufanya haya unayoyaona,” alisema Kajala licha ya nyuma ya pazia kuwepo na madai kuwa kuna kigogo anamuweka mjini.
Source:GPL

Sugu Mgombea Ubunge CHADEMA (UKAWA) Apigwa Mawe Mbeya MJINI, Aahirisha Mkutano

$
0
0
Mheshimiwa Sugu alipigwa mawe na gari lake kuharibiwa wakati akienda kata ya Iziwaa jiji Mbeya; kutokana na vurugu hizo ; 
Sugu kahairisha kampeni .

Gari la Mgombea Ubunge jimbo la Mbeya Mjini Joseph Mbilinyi Sugu likiwa kituo cha Polisi kati jijini Mbeya mara baada ya kushambuliwa kwa mawe na watu wanaosadikiwa kuwa ni wafuasi wa CCM

UKILAZA Wambikiza Shule Mwigizaji Riyama..Ashindwa Kumaliza Shule Kisa Ugumu wa Maisha

$
0
0
Riyama Ally
KILAZA! Staa wa Filamu Bongo, Riyama Ally ameweka wazi kuwa hakumaliza elimu ya sekondari kutokana na ugumu wa masomo kwani hakuwa akiambulia chochote darasani licha ya walimu kujitahidi kufundisha kwa kiwango cha juu.

Akizungumza na Ijumaa hivi karibuni, Riyama alisema kuwa kutokana na umbumbumbu wake alilazimika kuishia kidato cha pili baada ya masomo kuzidi kuwa magumu.

“Kwa kweli ugumu wa masomo ulinifanya niache shule, niliona kama wazazi wanapoteza pesa yao bure, sikuwa naambulia chochote, walimu walikuwa wakijitahidi sana lakini sikuwa naelewa kitu, kwa hiyo nimekomea kidato cha pili, masomo magumu asikuambie mtu,” alisema Riyama.
Source:Global Publishers

Uwoya Awashangaa Wasanii Wasioisapoti CCM

$
0
0
Mrembo wa filamu za kibongo nchini ambaye ameshapitishwa na Chama Cha Mapinduzi (CCM) kuwania ubunge wa viti maalumu, Irene Uwoya anawashangaa wasanii wenzake ambao hawakiungi mkono chama hicho wakati baadhi yao walikuwa karibu sana na Rais Jakaya Kikwete anayemaliza muda wake.

Kupitia mtandao wake wa kijamii wa Instagram, Uwoya amewachana wasanii ambao wamekuwa wakisema hawaoni sababu ya kumuunga mkono wakati yeye hakuwahi kuwathamini hata siku moja.

Sasa narudi kwa wasaniii wasio jitambua! katika tasnia yetu, ukweli usiopingika Kikwete amekuwa karibu sana na wasanii na ametufanya tuthaminike.

“Lakini chaajabu kunawatu wanajifanya hawajui mchango wake, kiukweli inaumiza sana!

"Kuna watu walikuwa wanashinda Ikulu , anawasaidia sana katika kazi zao lakini leo wamesahau yote na kumsapoti mtu ambaye hajawahi hata kuwatambua kwanafasi zao, kama sio ushabiki maandaz niniii? Loooo!!! aibu”.Uwoya ameandika.

Nawaheshimu Mashabiki Wangu ndio Maana Sishiriki Kwenye Kampeni za Siasa- Joh Makini

$
0
0
Joh Makini
Joh Makini anawaheshimu mashabiki wake kiasi ambacho amekataa mamilioni ya fedha kushiriki kwenye kampeni za siasa zinazoendelea.

joh makini

Hitmaker huyo wa Nusu Nusu amesema ingawa wakiwa kama wasanii wana uhuru na haki ya kufanya hivyo, lakini wao kama Weusi wameona watawachanganya mashabiki wa wao.

Unajua sisi kama wasanii tunaheshimu sana audience yetu, hasa mimi kusema ukweli naheshimu sana audience yangu,” Joh aliiambia Clouds FM.

“Nina mashabiki kutoka vyama vyote, vile vile nina mashabiki kutoka dini zote, kwahiyo najaribu pia kuepuka kuwatenganisha, ingawa sio vibaya kwa mtu yoyote hata msanii kuonesha mimi na-support upande huu, ni haki ya kila mtanzania. Kusema kweli kwa wasanii sidhani kama wanakosea, kwa sababu wanakosea vipi?”

“Kwa sababu mimi kama msanii ni mfanyabiashara end of the day ukinilipa hela yangu, nije ni perfome nyumbani kwako sebuleni au kwenye kampeni yako, mimi nikija pale nitafanya yangu na mwisho wa siku hao wanaopiga kelele, hawajui kwamba hakuna mtu anaweza kukataa kufanya kazi yake akilipwa. Mwisho wa siku kama mtu ameenda kufanya show na amelipwa hela yake hiyo ni haki yake.”

Avril Addresses Lesbianism Allegations That Seriously Maimed Her Reputation

$
0
0
The sultry singer has finally decided to open up about the predicament that earned her unparalleled humiliation!

Sometimes in November 2010, Avril Nyambura was cluttered with lesbianism allegations that gave many, irreversible shocks.

Damning photos popped showing Avril getting seriously cozy with another lady and this was the genesis of the ‘Hallo Baby’ hit maker being labeled a lesbian.

But during an Interview on ‘Zinga La Asubuhi’ with Bonny Msambi and Cynthia Anyango on Radio Taifa, the songstress blatantly denied she has a thing for fellow ladies.

Avril says the whole thing was a malicious scheme intended to dent her well manicured reputation and give some people mileage with their new business.

The soft spoken singer explained she was a victim of character assassination by a new studio that painted her in bad light in order to gain publicity.

“Me personally sijajihusisha na maneno kama hayo. So kuna watu walikua wanataka kuanzisha studio at some point and time na wakaona the easiest way ni wacha tujaribu kuchimbia huyu mwanadada ndo tuweze kunufaisha biashara yetu. And unfortunately me ndo nlikua the person nliend up kuwa hurt.” Explained Avril.

She further disclosed she learnt of the said studio’s ill intention after one of its members came forth and confessed to her.

One thing though, Avril didn’t address the issue of the authenticity of the photos that showed her in a compromising position with another lady.

Those pictured looked real and if they were photoshopped, then the person that created them must be having brains bigger than Albert Einstein’s.

Source:Ghafla

James Mbatia Kuhamia Chadema...NCCR Mageuzi Wadai Amekuwa Msemaji wa Chadema Badala ya Kujenga Chama

$
0
0

Mbatia na Lissu
Kuna kila dalili kuonyesha mbatia atakihama chama chake kwenda Chadema. karibuni akionekana kua msemaji wa mambo ya Chadema hadi kuwashangaza wafuatiliaji wa mambo ya siasa. sasa amejitenga na viongozi wenzake wa NCCR Mageuzi hadi wanatishia kujitoa UKAWA.. ameshindwa kutetea maslahi ya NCCR ndani ya UKAWA na inaekekea amelewa mahaba ya Lowassa mtu anayedaiwa kua tajiri sana. Je Mbatia naye atakua nyumbu kufuata malisho Chadema? si siku nyingi tutapata jibu.
Sumaye ambanae inasemekana amejiunga na NCCR japo hakuna ushahidi wa kukabidhiwa kadi ameoneka na jezi ya CHADEMA kwenye mikutano akipiga debe kwa Lowassa. ni wazi NCCR ni mwathirika wa UKAWA na itabaki na ukiwa. inaelekea nyumbu wote watafuata alipo EL. alipo Edo nyumbu wote wapo. tuombe mungu apishilie mbali UKAWA kutwa uongozi ama sivyo tutaona mparurano wa kugombea vyeo.. Sumaye tayari amapewa uwaziri mkuu mbowe inasemekana atakabidhiwa hazina! mbatia bado haifahamiki etc

By Kmbwembwe

Polisi Wamsaka Mtu Anayejiita 'Daudi Balali' Kwenye Ukurasa wa Twitter....Wakati Daudi Balali ni Marehemu

$
0
0
Jeshi la Polisi nchini linafanya uchunguzi kumbaini mmiliki wa ukurasa wa twitter unaoendeshwa na anayejiita Daudi Balali, aliyewahi kuwa Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT) ili hatua za kisheria zichukuliwe dhidi yake.

Mkurugenzi wa Habari na Mahusiano wa Jeshi la Polisi, Advera Bulimba, aliyasema hayo wakati akizungumza na Gazeti  la  Nipashe ofisini kwake jana.

Bulimba alisema kuwa taarifa za uwapo wa ukurasa huo wa twitter, wamekwishazipata na wanafanya uchunguzi wa kina kumkamata mhusika kisha kumfikisha kwenye vyombo vya sheria.

“Tunazo taarifa juu ya ukurasa huo wenye wafuasi wengi kwa sasa na unaotumika kuwashambulia viongozi wa serikali na wa siasa hasa wale wanaogombea nafasi kubwa za utawala nchini, hivyo Jeshi la Polisi lipo kwenye uchunguzi ili kumbaini mtu huyo haraka iwezekanavyo,” alisisitiza Senso.

Ukurasa huo ulioanza kutumika kabla ya Sheria ya Uhalifu wa Mtandaoni kuanza kutumika, una wafuasi zaidi ya 6,000 kwa sasa na umekuwa ukitumika kuwachafua wagombea urais nchini hasa wa upinzani.

Aidha, umekuwa ukitabiri matokeo ya uchaguzi, kitendo ambacho kimekuwa kikiwachanganya wananchi.

Bulimba alisisitiza kuwa jeshi hilo liko makini na linafuatilia hivyo mtu huyo atasakwa na kukamatwa akiwa mahali popote.

Aliwataka pia wananchi kuripoti katika vituo vya polisi pindi wanapopata vitisho vya aina yoyote, kudhalilishwa ama kufanyiwa kitu chochote kibaya kupitia mitandao ili wahusika wachukuliwe hatua za kisheria.

“Jeshi la polisi linafanya kazi usiku na mchana, hivyo mtu yeyote asijidanganye kwamba atavunja sheria na asikamatwe, maana tuna njia nyingi za kuwabaini watu hao kwa kushirikiana vyema na TCRA pamoja na wananchi, hivyo chanzo chochote kinachohusu uhalifu wa mtandaoni, kitashughulikiwa,” aliongeza.

Aliwaonya pia watu waliokuwa wakitumia kurasa mbalimbali kwenye mitandao ya kijamii kwa kutumia majina ya watu wengine ili kudhalilisha watu na kupotosha umma kwa kutoa taarifa za uongo juu ya masuala mbalimbali kuachana mara moja na tabia hiyo maana wakibainika watachukuliwa hatua kali za kisheria na kuwa mfano kwa wengine wanaojihusisha na vitendo hivyo.

Vera Sidika Responds To Claims She Has Become Broke

$
0
0
News that Vera Sidika was languishing in poverty hit many like a wrecking ball.

A certain blog claimed that the socialite was forced to close shop as she could no longer afford to keep The Vera Sidika Hair Lounge located at Green House Mall afloat.

We reached out to the socialite who refuted claims of going broke. Claiming that the reason why she was out of Green House was because she is moving her hair shop to Westlands as it’s growing into a salon and spa.

Initially it was a hair shop just selling hair extensions but my main goal was to set up a salon so the hair shop was just laying foundation for it” she said.

Before going ahead and adding “It's so lame for them to publish things they don't understand especially when they don't even try to reach out and find out facts! They didn't ask anyone just because I’m moving they assume I'm closing.

“And how lame can one be to even think that moving shop means you're broke?” she asks.

Well there you have it, Vera Sidika has not gone broke, she has just moved shop.


Mke wa LOWASSA Aondolewa Mkutanoni Simiyu na Kupitishwa Mlango wa Nyuma Kisa Hichi Hapa

$
0
0
Mke wa Lowassa Mama Regina Lowassa
MGOGORO wa vyama viwili vya siasa CUF na CHADEMA ambavyo vinaunda Umoja wa Katiba ya Wananchi (UKAWA), katika Wilaya ya Itilima, mkoani Simiyu, juzi ulichukua sura mpya.

Hali hiyo inatokana na  mgombea mmoja wa ubunge wa jimbo hilo kupitia CUF, Martine Makondo na wafuasi wake, kuvamia uzinduzi wa kampeni za mgombea ubunge wa CHADEMA, Martine Magire ambapo mgeni alikuwa Mama Regina Lowassa (mke wa Edward Lowassa).

Mama Lowassa alishindwa kuzindua kampeni hizo kutokana na vurugu kubwa zilizotokea. Awali mkutano ulikuwa ufanyike kwenye Uwanja wa Michezo uliopo katika Sekondari ya Lagangabilili.

Dalili za vurugu zilianza kuonekana mapema baada ya wafuasi wa CHADEMA kudai kuwa, mgombea wa CUF alikuwa amekwenda kwenye mkutano huo na kundi la vijana ili kuvuruga mkutano.

Baada ya Mama Lowassa kuwasili eneo la mkutano akiwa na Naibu Katibu Mkuu Baraza la Wanawake wa CHADEMA Taifa (BAWACHA),Kunti Yusuph, mgombea wa CUF aliwasili eneo hilo akiwa amebebwa na wafuasi wake wakidai mgombea wao amehujumiwa na mgombeawa CHADEMA na kusababisha jina lake likatwe na Kamati Kuu.

Wafuasi wa CUF walimpandisha mgombea wao (Makondo), jukwaani ndipo  vikaanza kutokea vijembe kati yao na wafuasi wa CHADEMA wakiimba, kupiga kelele za kuwataja wagombea wao.

Hali hiyo iliwashangaza viongozi wa CHADEMA na mgeni rasmi (Mama Lowassa) kwa dakika 15 ndipo walinzi wa chama hicho wakamwondoa eneo hilo wakihofia usalama wake katika mkutano huo.

Baada ya Mama Lowassa kuondolewa jukwaani, kupanda gari yake na kuondoka eneo la mkutano, Yusuph alianza kuwatuliza wafuasi wa vyama hivyo bila mafanikio akaamua kuwatuhumu wananchi, lakini wafuasi walimzomea wakitaka Makondo arudishwe.

"Tatizo tunafanya siasa kwa ushabiki na matokeo yake ndiyo haya, mimi sikuja kunadi mahindi kwenye mnada, nimekuja kumwombea kura mgombea urais wa UKAWA (Edward Lowassa), ubunge na udiwani mtajuana wenyewe Oktoba 25, mwaka huu," alisema.

Hata hivyo, Yusuph alishindwa kutuliza vurugu hizo na kulazimika kuondoka eneo hilo chini ya ulinzi wa vijana wa CHADEMA na kuwaacha viongozi wa mkoa, wilaya waendelee na mkutano lakini hata baada ya kuondoka, mkutano huo haukuendelea.

Kamanda wa Polisi mkoani humo, Gemin Mushy, alisema askari wake walitumia busara kutomtoa mgombea wa CUF kutokana na mazingira kutokuruhusu kumkamata.

Chanzo cha mgogoro huo ni Makondo ambaye awali alikuwa CHADEMA, kutimkia CUF baada ya jina lake kukatwa ingawa alishinda kwenye kura za maoni na aliyeshinda nafasi ya pili Magire kupewa nafasi hiyo.

Photos: Zari Shows Off Flat Tummy One Month After Giving Birth To Tiffah Dangotes

$
0
0

Zari is now a mother of four children but she still looks hot just because she is so careful not to lose her stunning shape. two weeks after giving birth to Tiffah Dangote she started hitting the gym and about a month now since the birth of her daughter you can see good results on her body......



Diamond na Zari Wapishana Katika Hili Kuhusiana Binti yao Tiffah

$
0
0
Mara nyingi wazazi hutofautiana katika mambo madogo kuhusu mtoto wao hasa katika upande wa nguo wanazopendelea avae! Diamond na Zari wanakutana na hali hiyo pia.

Kwa mujibu wa Zari, Diamond anapenda kumuona mwanae akivaa nguo za muonekano wa kiume na Zari akiwa na ladha tofauti.


Zari amepost picha ya mwanae huyo na kuandika: My sweet potato….. Her dad loves seeing her looking boyish, mama loves her all dolled up in pink with ribbons. Blame this look on dad… she got a signature lip pause too, my lil diva in the making @princess_tiffah.”

Jumapili wazazi hao wataionesha sura ya Tiffah kwa mara ya kwanza.

Lowassa Atakavyoibuka Kidedea Kwenye Mdahalo wa Urais

$
0
0
Hakuna mtu anayejua kucheza vzr na siasa ya Tanzania. Lowassa ni mastermind anajua watanzania ni washabiki wa matukio.

Anachofanya lowassa na kambi yake nikuwaingiza wapinzani wake kwenye angel kichwa kichwa kana kwamba hataki mdahalo then aibuke kwenye mdahalo na kujibu maswali vzr.

Ni imani yangu mdahalo hauna tofauti na maswali aliyoulizwa Dodoma nyumbani kwake akajibu vzr, kwa uzoefu wake aliokuwa nao kama waziri mkuu mstaafu anazijua vzr sector zote hawezi kushindwa kujibu swali.

Kuhusu ufisadi bado anao wigo mpana wa kulieleza vzr kama alivyokuwa anasema ni mamlaka ya juu imehusika

Binafsi sioni swali litakalimshinda mzee wetu ataibuka kidedea.

CCM yapata pigo wilaya ya Korogwe

$
0
0
Viongozi wote wa CCM wa kata ya mkomazi na pamoja na wapiga kura 1,400 wa eneo hilo wilayani Korogwe wamejiunga na CHADEMA huku baadhi yao wakiamua kugombea nafasi mbali mbali za uongozi kwa tiketi ya chama hicho.

Wakizungumza katika mkutano wa kampeni ulifanyika katika kijiji cha mikocheni kilichopo kata ya mkomazi wilayani Korogwe baadhi ya viongozi hao pamoja na wengine wa CCM katika kata sita waliokatwa majina yao katika zoezi la kura za maoni kwa tiketi ya CCM wamesema wameamua kujiunga na chadema pamoja na wapiga kura wao ili kuongeza nguvu kupata wawakilishi wa wananchi katika baraza la madiwani la halmashauri ya wilaya ya Korogwe.

Kwa upande wake katibu wa CHADEMA jimbo la Korogwe Bwana.Salim Sempoli amemuomba mwenyekiti wa tume ya taifa ya uchaguzi jimbo la Korogwe kuharakisha malalamiko ya wapiga katika baadhi ya vituo ambapo sehemu kubwa ya majina ya wapiga kura katika jimbo la Korogwe vijijini hayaonekani na hadi sasa hakuna utaratibu uliofanywa kusaidia tatizo hilo kwa sababu linaweza kuleta viashiria vya uvunjifu wa amani wakati wa zoezi la kupiga kura.

Kufuatia hatua hiyo mgombea ubunge kwa tiketi ya Chadema Emmanuel Kimea amewataka wananchi kuwachagua viongozi wa chama hicho kuanzia ngazi ya taifa,ubunge na udiwani kwa sababu ndani9 ya chama kikoja changamoto zinazowakabili katika kata ya mkomazi ikiwemo ya migogoro ya ardhi haiwezi kumalizika kama hawatafanya mabadiliko.

Chanzo: ITV

Sumaye : Magufuli Amepoteza Dira......Sasa Anadandia Slogan za CHADEMA

$
0
0
Siku moja baada ya Dk John Magufuli kupachika jina lake kwenye operesheni ya Chadema ya M4C, Waziri Mkuu wa zamani, Frederick Sumaye amemuelezea mgombea huyo urais wa CCM kuwa ni mtu anayedandia hoja baada ya kupoteza dira.

Wakati akipewa majibu hayo, DK Magufuli alikuwa akiendelea na kampeni mkoani Kigoma, ambako ajenda yake kuu ilikuwa ujenzi wa barabara, huku mgombea wa Ukawa, Edward Lowassa akichanja mbuga mkoani Shinyanga.

Akiwa mkoani Kigoma jana, Dk Magufuli aliwaambia wananchi kuwa kirefu cha nembo ya M4C ni Magufuli for Change, badala ya Movement For Change, ambayo imekuwa ikitumiwa na Chadema kwa miaka takriban sita sasa, ikimaanisha “vuguvugu la mabadiliko”.

Dk Magufuli alisema yeye ndiyo mtu sahihi wa kuongoza mabadiliko na hivyo alama hiyo inatakiwa iwe na jina lake.

Lakini jana, Sumaye, ambaye ameingia Ukawa bila ya kujihusisha na chama chochote kati ya vinne vinavyounda umoja huo, jana alisema kauli hiyo ya Magufuli inaonyesha jinsi yeye na chama chake wanavyotapatapa.

“Ni aibu kubwa,” alisema Sumaye ambaye amekuwa mzungumzaji mkuu kwenye mikutano ya kampeni ya Lowassa.

“Yaani ni kama mtu anayezama baharini halafu maji yameanza kumuingia puani na kushindwa kupumua. CCM inazama na sasa inaanza kushika kila mahali kama mtu anayezama katika maji.”

Sumaye alisema hayo jana kabla ya Lowassa kupanda jukwaani kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika Uwanja wa Malambo wilayani Bariadi mkoani Simiyu.

Akimchambua mgombea urais wa CCM, Sumaye alisema kauli yake imeonyesha jinsi asivyokuwa na aibu na imedhihirisha jinsi alivyopoteza dira kwa kudandia hoja na mipango ya wapinzani.

“Sisi tunadai mabadiliko na kama na dawa ya kunguni ni kukitoa kitanda na kukitupa nje wakaozee huko,” alisema Sumaye huku akishangiliwa na wananchi.

Kwenye mkutano huo, Lowassa aliyepokewa na maelfu ya wananchi waliokuwa wakimsubiri, aliahidi kumaliza kero ya maji kwenye wilaya kwa kuendeleza mradi wa kutumia maji ya Ziwa Victoria lililopo umbali wa kilomita 30.

Mbunge huyo wa zamani wa Monduli alifika eneo hilo saa 10:00 jioni na kukimbiliwa na wananchi waliotaka kumshika na kusababisha polisi kutumia nguvu ya ziada kuwazuia.

 Akizungumza na wananchi wa Bariadi, Lowassa alirudia tena ahadi yake ya elimu ya bure akisema kuanzia Januari mwakani hakuna mwanafunzi atakayelipa ada kuanzia darasa la kwanza hadi chuo kikuu.

Pia aliahidi kuboresha kilimo ili kiwe cha kisasa na cha kibiashara, huku akisisitiza msimamo wake kuwa Serikali yake haitamvumilia mtu atakayeshindwa kwenda na kasi yake.

Mgombea huyo pia alifanya mikutano mingine Maswa na Busega.

Mpasuko Familia ya Mwanamuziki Diamond Platnumz....Kisa Hichi Hapa

$
0
0
Breaking news! Saa chache kabla ya ile sherehe ya kukata na shoka ya 40 ya mtoto wa staa wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’, Latifah Nasibu ‘Princess Tiffah’ inayotarajiwa kufanyika mapema kesho, ndani ya familia hiyo kunadaiwa kuibuka bonge la mpasuko.

Habari kutoka kwa chanzo makini ndani ya familia hiyo yenye maskani yake nje kidogo ya Jiji la Dar, maeneo ya Madale-Tegeta zilieleza kuwa, kuna madai mazito ya usengenyaji ambayo yametawala yanayodaiwa kutia doa katika shughuli hiyo ya kesho.


NI MAMA DIAMOND NA ZARI
Habari hizo za kidaku zinadai kwamba, mama mzazi wa Diamond, Sanura Kassim ‘Sandra’ yuko kwenye sintofahamu na mwandani wa mwanaye, Zarinah Hassan ‘Zari The Boss Lady’ kwa kile kilichoelezwa kuwa ni mambo ya umbeya.


KAMERA ZABUMBURUA
Chanzo hicho kimelieleza gazeti hili kuwa, hivi karibuni, Zari, kupitia kamera za ndani ya nyumba hiyo, Close Circuit Television (CCTV), alibaini picha zikimuonesha Mama Diamond na mwanaye wa kike ambaye ni dada wa Diamond aitwaye Esma Platnumz wakiwa kwenye mazungumzo na muonekano wa kumseng’enya, jambo ambalo lilimkera kupitiliza.

ZARI ATAKA KUONDOKA NA TIFFAH
Mpashaji huyo aliendelea ‘kuponyokwa’ na maneno kuwa, baada ya kubaini jambo hilo, Zari amekuwa katika harakati za kutaka kuondoka nchini kwenda kwao kwa kile alichokiita ‘kujiepusha na ya walimwengu’ kabla hata mwanaye, Tiffah hajafanyiwa pati yake ya kutimiza siku 40 tangu kuzaliwa kwake.

“Hapa nyumbani hali si shwari kabisa, Zari hajapendezwa na kitendo hicho, siku zote amekuwa akiishi nao kwa upendo akiamini ni watu wema kwake, sasa anashanga tena kuwepo kwa hali ya majungu na manenomaneno.
“Nasikia amefikia hata hatua ya kulazimisha kuondoka Bongo na mwanaye,” kilisema ‘kikulacho’ hicho.

MPASUKO?
Chanzo hicho kiliendelea kutiririka kuwa, kitendo hicho kimesababisha mpasuko mkubwa kwenye familia ya Diamond kwani kuna baadhi ya wanafamilia wapo upande wa Zari na wengine wapo upande wa Mama Diamond na Esma.

HUYU HAPA MAMA DIAMOND
Baada ya kujazwa ubuyu huo wa motomoto, muda mfupi kabla ya kwenda mitamboni, gazeti hili lilimtafuta Mama Diamond na kumuuliza juu ya ishu hiyo ambapo alikanusha vikali kwa madai kwamba hayo ni maneno ya umbeya kisha akakata simu.

MAMA DIAMOND ADONDOSHA KIMOMBO
Hata hivyo, alipoendelea kupigiwa ili afafanue maswali ya mwandishi, Mama Diamond alituma ujumbe mfupi wa maneno kwa kimombo.
Mama Diamond: Iam driving (naendesha gari).

MAANDALIZI YA SHUGHULI USIPIME
Hata hivyo, wakati hayo yakiendelea, maandalizi ya shughuli ya Tiffah yalikuwa yamekamilika kwa kila kitu huku ndugu wa Zari wakiwa wameshafika nyumbani hapo wakiongozwa na Mama Zari, Halima Hassan.
Hatimaye, Diamond na Zari walifikia makubaliano ya kufanyia shughuli hiyo nyumbani hapo baada ya kuwepo kwa msuguano mkali kufuatia makampuni ya bidhaa za watoto kutaka ifanyikie kwenye ukumbi.

Aunt Ezekiel: Nimeamua Kuhama CHADEMA Na Kurudi CCM Baada ya Kuvutiwa na Sera za Chama........Sijapewa Pesa wala Gari

$
0
0
MWIGIZAJI mahiri wa filamu nchini, Aunt Ezekiel, amedai kutishiwa amani baada ya kufanya maamuzi yake kisiasa ambapo amehamisha ushabiki wake kutoka CHADEMA  na kwenda CCM.

Licha ya mrembo huyo kudai kupokea vitisho mbalimbali, pia alidai amehama chama hicho na kujiunga na CCM kutokana na kukubali sera za chama hicho.

“Sera za chama nilichohamia zimenivutia na wala sikulazimishwa na mtu wala sijapokea fedha wala gari kuhamia huko kama inavyosemekana, bali nafsi na mapenzi pamoja na haki yangu ndiyo yaliyonipeleka huko.

“Nashangaa maamuzi yawe yangu bado watu wanitumie jumbe za vitisho, mimi ni raia kama walivyo wengine, umaarufu wangu usiwe sababu,” alisema Aunt, ambaye awali alikuwa akivaa magwanda  CHADEMA

Davido Atangaza Ujio wa Collabo yake na Joh Makini

$
0
0
Hakuna surprise nzuri kama ile ambayo hukuwahi kuona hata dalili, na kwenye muziki hasa kwa msanii wa Bongo hakuna kitu kizuri kama msanii mkubwa wa nje kuanza kutease ujio wa kazi yenu hata kabla yako.

Ndicho kilichotokea usiku wa Sept 18 pale staa wa Nigeria, Davido alipotweet kuwa kuna collabo yake na Joh Makini inakuja.

Bado haijajulikana kama ni wimbo wa Davido kamshirikisha Joh Makini au Joh kamshirikisha Davido au ni wa wote.

Hii ni hatua nyingine kubwa ya safari ya Joh Makini kwenda kimataifa, baada ya kufanya collabo na AKA na kuwa kwenye matayarisho ya kufanya collabo nyingine na rapper KO wa Afrika Kusini, mashabiki wa rapper huyo wa Weusi watarajie collabo hiyo ya Davido na Mwamba wa Kaskazini.

CHADEMA Kumshitaki Dr. Magufuli.......Yamtuhumu Kuiba na Kutumia Nembo ya M4C

$
0
0
CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kimepanga kumshitaki mgombea wa urais wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dk. John Magufuli kwa madai ya kutumia vibaya nembo za chama hicho.

Ni baada ya Dk. Magufuli kutangaza kuwa nembo ya Movement for Change (M4C) ni  Magufuli  For Change wakati akifanya mkutano wake wa kampeni mkoani Kigoma kwenye Uwanja wa Kawawa uliopo Ujiji.

Katika mkutano huo Dk. Magufuli alisema “hawa jamaa zangu wa Chadema wananipenda, hata ile nembo yao ya M4C ni Magufuli for Change-maana yake Magufuli kwa Mabadiliko.”

Chadema wanaratajia kufungua kesi hiyo Septemba 21 mwaka huu na kwamba, madai hayo yatakwenda sambamba na madai ya kutumia kauli mbiu ya ‘mabadiliko Lowassa’ ambayo kaibadilisha na kuwa‘mabadiliko Magufuli’.

Akizungumza na waandishi wa habari jana jijini Dar es Salaam katika Ukumbi wa Ngome Kawe, Mwanasheria wa Chadema, John Malya alisema “CCM imekuwa ikivunja sheria za uchaguzi kila siku bila kuchukuliwa hatua yoyote na mamlaka husika, wanatumia nembo za Chadema ambazo zimesajiliwa na kujulikana.”

Hata hivyo imeelezwa, baada ya Dk. Magufuli ‘kuiba’ alama hizo za Chadema; wafuasi wake, bodi ya wadhamini na watu wake wa kampeni walianza kusambaza mitandaoni nembo ya M4C huku wakidai ni nembo mpya ya CCM.

Malya alisema mbali na hilo la kuiba nembo ya chama, wamekuwa na tabia ya ‘kukopi’ na ‘kupesti’ kila hatua inayo pigwa na Chadema na kuzitumia katika kampeni zao.

Akivitaja baadhi ya vitu vinavyokopiwa na CCM amesema, Magufuli amesikika mara kadhaa akiwa anatumia sera na Ilani ya Chadema na Ukawa, pia amekuwa akiiba kauli mbiu za Chadema pindi anapokuwa katika kampeni zake.

“Hii ni dalili za kushindwa kwa CCM hana sera wameishiwa na ndio maana wanafuata nyayo zetu kila tunapoenda na kila tunalofanya wanalifuatilia na kuaza kutukopi. Kwa mfano sisi tunatumia Lowassa mabadiliko mabadiliko Lowassa na wao wameshaiga kwa kutumia jina la Magufuli”.

Aidha, Malya alisema Chadema inasikitushwa sana na kitendo cha Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) kwa kuwa kimya huku vitendo vya rushwa vinazidi kukithiri toka kwa CCM.

Malya alitaja baadhi ya matukio yenye viashiria vya rushwa kuwa, Magufuli alionenekana akimpatia mtoto pesa taslimu elfu 30000 katika moja ya kampeni zake, huku Mgombea mwenza wa CCM Samia Suluhu Hassani naye mara kadhaa ameonekana akigawa pesa kwa wananchi wanaohudhulia katika kampeni zake.

“Matukio yote hayo bado tume imekaa kimya japo kuwa tumeshapeleka barua za malalamiko na kutuahidi kulishughulikia kesho. Vivyo hivyo kwa Taasisi ya Kushuhulikia Rushwa Tanzania (TAKUKURU) ambayo tulitegemea itakuwa ya kwanza kukemea hilo lakini ipo kimya na tumeshaandika barua ya malalmiko”.

Alidai, pia CCM wamezidi kukiuka sheria za uchaguzi kwa kuyachana mabango ya Mgombea Urais wa Chadema, Edward Lowassa hadharani na kwamba, wanakiuka sheria

Alisema, matendo hayo yote yanayofanywa na CCM yanakuika sheria za umiliki wa nembo za biashara ya mwaka 1986 na kanuni ya umiliki huo ya 2000 pamoja na taratibu zingine za umiliki.

Credit: Mwanahalisionline

Vurugu ndani ya UKAWA zasambaa mikoa 4 - Mtwara, Tabora, Kilimanjaro na Morogoro...

$
0
0
VURUGU zinazoendelea ndani ya umoja wa vyama vinne vya upinzani (Ukawa), kuhusu kuachiana majimbo na kata baada ya kusambaa katika mikoa ya Mtwara, Tabora na Kilimanjaro, sasa zimegonga hodi mkoani Morogoro.

Hali hiyo ambayo imevuruga hadi majimbo ya wenyeviti wenza wa Ukawa, ni tofauti na mtafaruku mwingine unaoendelea ndani ya chama kimoja katika safu za uongozi wa juu, ambazo zimepewa jina la ‘kushuka njiani wakati safari ikiendelea’.

Mkoa wa Morogoro una majimbo 11 ya uchaguzi, ambapo CUF katika mgawo huo ilipewa majimbo mawili ambayo ni Kilosa na Morogoro Kusini Mashariki na Chadema ikanyakua majimbo tisa.

Morogoro

Akizungumza na gazeti hili mjini Morogoro jana, mgombea wa Ubunge wa Jimbo la Kilosa, Abeid Mlapakolo (CUF), alisema pamoja na kuwa na makubaliano hayo, ameshangazwa kuona Chadema imemsimamisha mgombea ambaye anaendelea kufanya kampeni katika kata mbalimbali zilizomo kwenye jimbo hilo.

Kwa mujibu wa Mlapakolo, mgombea huyo wa ubunge wa Chadema, Rajab Msabaha, tayari ameshasambaza mabango na vipeperushi maeneo mbalimbali ndani ya jimbo hilo na amekuwa akifanya kampeni kinyume na makubaliano yaliyofikiwa na viongozi wa Ukawa.

Mlapakolo alidai mbali na kupiga kampeni, Msabaha pia alishiriki katika mapokezi ya mgombea wa urais wa Chadema anayeungwa mkono na Ukawa, Edward Lowassa alipowasili Kata ya Dumila iliyopo katika Jimbo la Kilosa Septemba 15, mwaka huu na wafuasi wake kadhaa.

“Jimboni ni vurugu tupu, wafuasi wa Chadema wananivurugia shughuli za kampeni...mimi ndiye mgombea halali wa Ukawa Jimbo la Kilosa, lakini ndugu zangu hawa wamemweka mgombea wao wa ubunge,” alisema na kuongeza.

Vurugu hizo zimemkuta pia mgombea wa ubunge wa Jimbo la Morogoro Kusini Mashariki, Salama Omary (CUF) ambaye amesema licha ya jimbo hilo kupewa CUF, Chadema nao wamemsimamisha mgombea wa ubunge kinyume na makubaliano.

Salama alisema bado mgombea wa ubunge wa Chadema, David Lugakingira, anaendelea kufanya kampeni za uchaguzi licha ya viongozi wake kumtaka asifanye hiyo.

Hatua

Kutokana na hali hiyo, Mlapakolo na Salama wameamua kuwasilisha malalamiko kuhusu Chadema kukiuka makubaliano hayo kwa mgombea wa urais wa Jamuhuri wa Muungano wa Tanzania kupitia Chadema, Edward Lowassa, anayeungwa mkono na Ukawa.

Mlapakolo amesema tayari amefikisha suala hilo mbali na litashughulikiwa na viongozi wa Taifa wa Ukawa, ambao wanatarajiwa kwa kupeleka timu ya viongozi kwenda kutatua sakata hilo.

Naye Salama amefikisha sakata hilo kwa Lowassa ambaye alidai kuwa mgombea urais huyo aliahidi kufanyia kazi malalamiko hayo na kufikia uamuzi wa pamoja wa viongozi wa Ukawa.

Mtwara, Makaidi Mkoani Mtwara tangu mwanzoni mwa mwezi huu, mgombea ubunge wa Jimbo la Masasi ambaye pia ni Mwenyekiti Mwenza wa Ukawa, Dk Emmanuel Makaidi (NLD), alijikuta akikataliwa na wananchi katika vijiji mbalimbali vya jimbo hilo kila anapopanda jukwaani, huku wengine wakimzomea wakidai kuwa yeye sio chagua lao.

Dk Makaidi mwenyewe alipoulizwa alikaririwa akisema hawezi kukatishwa tamaa na kikundi cha watu wachache, kinachopiga propaganda zisizo na msingi, huku akiwataka wakazi wa Masasi, kuamini kuwa uteuzi wa majimbo uliofanywa na Ukawa, umezingatia misingi ya makubaliano ya umoja huo.

Akijaribu kuweka mambo sawa, Mwenyekiti wa Chadema Mkoa wa Mtwara, Kassimu Bingwe, alikaririwa akisema mgawanyo wa majimbo uliofanywa na uongozi wa Ukawa Taifa, ulitoa ridhaa kwa NLD kuweka wagombea Masasi, Ndanda na Lulindi na kudai kuwa kinachotokea ni njama za wapinzani.

Hali hiyo ya Masasi, ilisababisha Mgombea Mwenza wa Ukawa, Juma Duni Haji, alipotembelea jimbo hilo kushindwa kuhutubia baada ya wafuasi wa CUF, kupiga kelele za kumkataa Makaidi, huku wakisisitiza kumtaka Ismail Issa Makombe maarufu Kundambanda, ambaye alikuwa mgombea wa CUF kabla ya kuondolewa na Ukawa.

*Kilimanjaro, Mbatia

Katika Mkoa wa Kilimanjaro kwenye Jimbo la Vunjo, wagombea udiwani 16 kutoka Chadema, juzi walitangaza kutomuunga mkono mgombea ubunge wa Vunjo kupitia NCCR-Mageuzi, ambaye pia ni Mwenyekiti Mwenza wa Ukawa, James Mbatia.

Mmoja wa madiwani hao, ambaye ni mgombea wa kata ya Mamba Kusini, Fredy Shayo, alisema hali hiyo imetokea baada ya vyama hivyo kushindwa kuelewana katika makubaliano ya kusimamisha mgombea mmoja, ambapo Chadema na NCCR-Mageuzi vimesimamisha wagombea wao wa udiwani kwenye kata zote 16 za jimbo la Vunjo.

Katibu wa Chadema Jimbo la Vunjo, Emmanuel Mlacky alikiri kuwa mwenendo wa Ukawa katika jimbo hilo haupo vizuri, kwa sababu unahatarisha uhai wa Chadema pamoja na uhai wa Ukawa.

Mlacky alisema maridhiano ya Ukawa yalilenga kumsimamisha mgombea mmoja kuanzia ngazi ya urais, wabunge na madiwani ambapo baada ya makubaliano hayo jina Mbatia liliridhiwa na viongozi wakuu wa umoja wao, huku ngazi ya madiwani ikiachiwa mamlaka ya jimbo kuona namna ya kusimamisha wagombea wa udiwani.

Alisema licha ya kukaa kwenye vikao vya maridhiano zaidi ya mara nane bila mafanikio, lakini viongozi wa NCCR wameona baada ya Mbatia kupitishwa na Makao Makuu kwa makubaliano, wamefikiri ndio inawapa nafasi ya kusimamisha madiwani karibia kata zote, jambo ambalo ni kinyume.

Katibu wa Chadema mkoa wa Kilimanjaro, Basil Lema, alisema haungi mkono madiwani wa chama chake kumsusia Mbatia, pia chama chake hakiungi mkono kubaguliwa kwa wagombea udiwani wa Chadema na mgombea huyo wa ubunge.

Naye Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya NCCR-Mageuzi, Heme Msabaha alisema, mambo yanayoendelea yanawapa ishara kuwa huenda Chadema wakawa wanatumika kwa lengo baya.

Simiyu, Regina

Katika Mkoa wa Simiyu, uzinduzi wa kampeni za mgombea ubunge wa Jimbo la Itilima kupitia Chadema, Martine Magire, uliingia doa baada ya wafuasi wa CUF wakiongozwa na mgombea ubunge wa chama hicho katika jimbo hilo, Martine Makondo, kuvamia na kufanya vurugu katika uzinduzi huo.

Kutokana na vurugu hizo, mke wa mgombea urais wa Chadema, Lowassa ambaye alikuwa mgeni rasmi, Regina Lowassa, aliondolewa jukwaani dakika 15 baada ya kuwasili katika uzinduzi huo.

Chanzo cha vurugu hiyo, ni mgombea huyo wa CUF aliyeingia katika uzinduzi huo akiwa amebebwa na wafuasi wake, kudai kuwa amehujumiwa na mgombea wa Chadema na kusababisha jina lake likatwe na Kamati Kuu ya chama chake.

Kamanda wa Polisi wa Simiyu, Gemin Mushy, alikaririwa akisema askari walitumia busara na kuepuka kumtoa mgombea huyo wa CUF jukwaani, kwa kuwa mazingira hayakuruhusu kumkamata.

Bundi NCCR

Wakati hali ikiwa hivyo majimboni na katika kata, migogoro katika safu za uongozi za vyama hivyo vinavyounda Ukawa, baada ya kutoka Chadema na CUF, sasa imehamia NCCR-Mageuzi.

Tayari aliyekuwa Katibu Mkuu wa Chadema, Dk Willibrod Slaa, ameshaachana na chama hicho katika migogoro hiyo, huku aliyekuwa Mwenyekiti wa Taifa wa CUF, Profesa Ibrahim Lipumba, akijiuzulu nafasi zote ndani ya chama chake na kubakia mwanachama wa kawaida.

Lakini juzi, Makamu Mwenyekiti wa NCCR-Mageuzi, Leticia Mossore akiwa na Katibu Mkuu wa NCCR, Mosena Nyambabe na wajumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa na Kamati Kuu, walimua kupingana na Mwenyekiti wao wa Taifa, Mbatia, mbele ya waandishi wa habari, jijini Dar es Salaam.

Katika mkutano wao na waandishi wa habari, Mossore alilalamika kuwa Ukawa imekuwa ikimshirikisha Mbatia peke yake kutoka NCCR-Mageuzi na kuacha wengine, huku wanachama waliohama CCM, wakipewa umuhimu mkubwa kuliko walioasisi umoja huo.

Makamu Mwenyekiti huyo alisema kinachoonekana ni CUF kuwa Ukawa-Zanzibar, kwa kuwa haijali yanayoendelea Tanzania Bara na Chadema imekuwa ndiyo Ukawa-Tanzania Bara, kwa kuwa haijali yanayoendelea Tanzania Bara, huku NCCR-Mageuzi ikijikuta haipo popote, badala yake ikidhoofika siku hadi siku.

Mossore alifafanua katika taarifa yake kwa waandishi wa habari, jinsi Ukawa ilivyoshindwa kupata muafaka wa kuachiana majimbo.

“Kwa mfano, NCCR-Mageuzi tuliachiwa majimbo 12 tu ya Kasulu Vijijini, Kigoma Kusini, Muhambwe, Kasulu Mjini, Vunjo, Ileje, Mbinga Mjini, Manyovu, Buyungu, Ngara, Nkenge na Korogwe Mjini. Ikumbukwe kwamba mwaka 2010, NCCR-Mageuzi ilisimamisha wagombea katika majimbo 67. Kwa maana hiyo UKAWA umeturudisha nyuma katika kupata wabunge na kuimarisha chama zaidi ya miaka 20 baada ya kuundwa kwake,” ilifafanua taarifa yake hiyo kwa waandishi, aliyoitoa pamoja na Nyambabe.

Taarifa ilisema, “Licha ya kukubaliana kwamba NCCR-Mageuzi iachiwe majimbo 12, wenzetu wa vyama vingine katika UKAWA wamesimamisha wagombea katika majimbo 6 kati ya hayo. Wametuvunja moyo na kutuonesha kwamba hawatujali. Tuna mifano mingi ya kuonesha jinsi wagombea wetu wanavyofanyiwa vurugu. Pia tumeshindwa kupata muafaka wa namna ya kuachiana wagombea udiwani katika kata nyingi”.

Mossore na Nyambabe walimshauri mwenyekiti wao, Mbatia, aitishe vikao vya kikatiba ili waweze kujadiliana kuhusu hatima ya NCCR. Pia, walimshauri Mbatia asiwe msemaji wa Chadema wakati anakiacha chama chake cha NCCR kinadhoofika.

“Kwa mfano, Dk Slaa alipoishambulia Chadema hakuna kiongozi wa Chadema aliyemjibu, isipokuwa Mbatia ndiye aliyeamua kujiingiza kwenye ugomvi ndani ya Chadema.” Ilisema taarifa hiyo. Taarifa ilisema, “Tutachangishana ili tusafiri kwenye majimbo na kata za wagombea wetu na kuwasaidia kwenye kampeni ili wasibaki wapweke kama yatima”.

Taarifa hiyo ya NCCR ilisema, “Tunasisitiza kwamba upinzani wa kweli nchini hauwezi kujengwa kwa njia za hila, kwa kukiuka taratibu za kidemokrasia tulizojiwekea wenyewe, kwa kukiuka misingi muhimu kama uadilifu, kwa kuweka mbele tamaa na maslahi binafsi kuliko taifa, kwa kutegemea propaganda”.

Imeandikwa na John Nditi, Morogoro na Arnold Swai, Vunjo.

HABARI LEO
Viewing all 104808 articles
Browse latest View live




Latest Images

<script src="https://jsc.adskeeper.com/r/s/rssing.com.1596347.js" async> </script>
<script src="https://jsc.adskeeper.com/r/s/rssing.com.1596344.js" async> </script>