Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104809 articles
Browse latest View live

Profesa Kitila: Edward Lowassa na Ukawa Kubalini Yaishe..Kubalini Dk Magufuli Ndio Rais Wenu

$
0
0
Dar es Salaam. Mhadhiri Mwandamizi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), Profesa Kitila Mkumbo amesema aliyekuwa mgombea wa urais wa Chadema, Edward Lowassa, hana budi kukubali matokeo licha ya kupoteza nafasi hiyo.

Pia Profesa Mkumbo alisema mgombea huyo kisheria, hakuwa na haki ya kujitangaza mshindi wa nafasi ya urais katika uchaguzi wa mwaka huu.

Juzi, Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) ilitangaza matokeo ya kura za urais zilipopingwa Jumapili, Oktoba 25 mwaka huu na kumtangaza mgombea wa urais kwa tiketi ya CCM, Dk John Magufuli mshindi, lakini Lowassa siku hiyo pia alisema ameshinda katika uchaguzi kwa kura 10,268,795 sawa na asilimia 62 na kuitaka tume hiyo kumtangaza mshindi.

Profesa Mkumbo ambaye pia alipendekezwa na chama cha ACT- Wazalendo kugombea  nafasi hiyo na kukataa, alisema Lowassa aliingia kwenye kinyang’anyoro hicho akifahamu kuwa tume ndiyo yenye mamlaka ya kumtangaza mshindi.

Alisema licha ya mchuano mkali kati yake na mgombea wa CCM anatakiwa kukubali matokeo.

 “Hivyo Lowassa na  wenzake wa Ukawa hawana msingi wowote wa kisheria au kisiasa kutangaza ushindi wenyewe. Walikubali  kushiriki katika uchaguzi huu wakati wakifahamu kikamilifu kuwa NEC ndiyo yenye  jukumu la  kutangaza mshindi na mshindwa katika uchaguzi.”

Aliongeza: “Zaidi ya hayo, takwimu za uchaguzi zinaeleza pia.”

Hata hivyo alisema katika uchaguzi huu ambao ni wa kihistoria kutokana na upinzania mkali kati ya CCM na upinzani tofauti na miaka ya nyuma, bado upinzani umepoteza nafasi ya ubunge licha ya kujinyakulia viti 76 huku  CCM ikiwa na viti 188.

“Kupoteza viti hivyo ni ishara kwamba ushindi wa Lowassa haukuwa wa uhakika,”alisema Profesa Mkumbo na kuongeza;

“...nawashauri Ukawa kukubali kwamba Dk Magufuli ndiye rais mtaule wa awamu ya tano. Wahakikishe wanashirikiana  na kufanya kazi naye kazi kwa karibu katika kipindi chake cha miaka mitano ya uongozi. Kwa namna hiyo wataweza kuwa chachu ya kupata Katiba Mpya itakayowezesha kubadili mazingira ya kikatiba na kisheria katika uchaguzi ujao.”




Hali ni Tete Zanzibar....Bomu Lategwa Kituo cha Polisi, JWTZ Waliwahi na Kulilipua

$
0
0
Jeshi la Polisi Zanzibar kwa kushirikiana na Jeshi la Wananchi (JWTZ), limefanikiwa kuteguwa bomu lilitegwa eneo la Mkunazini karibu na kituo cha polisi mjini Zanzibar.

Bomu hilo lilitegwa na watu wasiofahamika na jeshi la polisi lilipata taarifa ya kutegwa kwa bomu hilo kutoka kwa wasamaria wema.

Akizungumza na mwandishi wetu, Kamishna wa Jeshi la Polisi Zanzibar, Hamdani Omar Makame, alisema baada ya kupata taarifa kutoka kwa wananchi kuwa eneo hilo kuna kitu kimetegeshwa, jeshi la polisi lilifanya uchunguzi na kubaini kuwa ni bomu na kufanikiwa kulitegua kwa kuliripua ili kuepusha maafa.

“Ni kweli kulikuwa na kishindo kikubwa baada ya jeshi la polisi kuliripua bomu hilo lakini hakuna madhara yoyote yaliotokea,” alisema.

Aidha alisema kuwa jeshi la polisi linaendelea na uchunguzi ili kubaini ni aina gani ya bomu lililotegwa na aliyefanya kitendo hicho.

Kesho ni Siku ya Mwisho ZEC Kumtangaza Rais..Nini Hatima ya Zanzibar Kuanzia Jumatatu

$
0
0
Kwa mujibu wa katiba ya Zanzibar itakapofika November 2 madaraka ya rais aliyepo yatakoma labda baraza la wawakilishi liitishwe kutengua kifungu hicho.

Wakati huo CUF imetoa hadi kesho ZEC wawe wametengua tamko la M/kiti wao na kuendelea kuhakiki majimbo 14 yaliyobaki vinginevyo watawaachia wananchi kudai haki yao wenyewe.

Nini hatima ya Zanzibar kuanzia jumatatu, je Sheni ataendelea kuheshimiwa kama rais au atatafutwa kiongozi wa mpito kipindi cha kusubiri uchaguzi mwingine.

Endapo Dr. Shein ataendelea na madaraka ataaminika vipi kuendelea kupanga uchaguzi wa marudio wakati yeye ni mmoja wa washindani wanaolalamikiwa?

Nawasilisha.

KUKATWA Kwa Mumewe Uchaguzi Mkuu Kwampa Kiwewe JOYCE KIRIA!

$
0
0
Joyce Kiria
‘HOST’ wa Kipindi cha Wanawake Live, Joyce Kiria ameonekana kuwewesekea matokeo ya uchaguzi baada ya mumewe aliyekuwa akigombea Ubunge Jimbo la Mwanga kushindwa. Baada ya matokeo kutangazwa, Joyce alijikuta akiandika waraka mzito kwenye ukurasa wake wa Facebook akieleza jinsi alivyoyapokea matokeo hayo kwa maumivu.
Joyce Kiria na Mumewe

Akizungumza na Ijumaa, Joyce alisema kushindwa si kitu cha ajabu kwani unaangalia umeshindwaje lakini kwa hili la mumewe hakuridhishwa na mchakato.
Nimeumia sana mume wangu kukosa ubunge lakini najiuliza kwa nini walikuwa wakimkatalia kuhesabu kura kwa mara ya pili? Hivi vitu vinaumiza sana, vikitokea lazima upatwe na kiwewe,” alisema Joyce.

Am Not Materialistic But I Still Can't Keep a Man

$
0
0

Am in my late 20s about completing my MMED. Ever since I got out of my first relationship with my first and d only man I have ever loved I have not been able to keep other men coming my way.

Am not really a bad person, am not even materialistic because even as an undergraduate I was working. No man I have ever dated that doesn ’ t not wish to settle down with me but one thing will lead to another and there will be change in plan.

In fact am losing hope of ever getting married may be I should just get pregnant for my first love and be a single mother. Right now am single and I have been for more than a year. Please do u have any advice for me?

Thanks

Yu Wapi Tundu Lissu Wakati Huu wa Madai ya Kuporwa Kura na Kufutwa Uchaguzi Zanzibar?

$
0
0
Nimeshangazwa na ukimya wa yule Mwanasheria nguli wa CHADEMA katika utata mkubwa wa kisheria unaogubika taifa katika suala la uchaguzi Zanzibar na pia madai ya UKAWA kuibiwa kura. Kulikoni kwa mwanasheria huyu nguli? Hata kipindi cha mwisho mwisho cha kampeni za kitaifa UKAWA, hakutokea hadharani kama ilivyokuwa mwanzoni mwa kampeni hizo.
 Je kuna dots za ku-connect?

Breaking News:Ndege ya Urusi Yenye Abiria 200 Yaanguka Sinai

$
0
0

A Russian plane carrying over 220 people from Egypt to Russia disapperaed from radars, according to Russian and Egyptian authorities. It is believed to have crushed in central Sinai.

Kolavia Flight 7K9268, an Airbus A320, went off radar 23 minutes after taking off from Sharm El-Sheikh International Airport, Sergey Izvolskiy told the media citing preliminary data.

The plane was carrying 212 passengers and 7 crewmembers, he added.

Egyptian Prime Minister Sherif Ismail confirmed that the Russian plane did go missing over Sinai and said a cabinet-level crisis committee has been convened to deal with the incident.

The flight was traveling from the Egyptian resort to St. Petersburg, RIA Novosti reported. It belonged to Kogalymavia airline, which also uses the brand name Metrojet.

The plane was supposed to contact air traffic in Turkish Cyprus? Larnaca after leaving Egypt?s airspace, but failed to do so.

A source at Sharm El-Sheikh Airport told RIA Novosti the pilot of the missing plane requested a change of course, saying the jet would have to land in Cairo.

Metrojet had a fatal incident in 2011, when one of its planes caught fire on a runway in Surgut Airport in Russia?s Urals. Three people died and 40 were injured as the plane burned out in just 10 minutes.

The last large-scale Russian airline incident happened in November 2013, when Tatarstan Airlines Flight 363 crashed at Kazan International Airport while attempting to land. Fifty people died in the incident.

Faiza Ally asema huenda ana ujauzito wa mpenzi wake Mmarekani Hivyo Kurudiana na Sugu ni Ndoto

$
0
0
Mzazi mwenzake na mbunge wa Mbeya mjini, Sugu – Faiza Ally, amedai kuwa huenda akawa ni mjamzito.

Akizungumza kwenye kipindi cha Friday Night Live cha EATV, Faiza alisema kutokana na hilo hadhani kama ataweza kurudiana na Sugu tena.

Sasa hivi nipo na mpenzi wangu na pengine naweza kuwa na mimba, not sure kwa sababu sijapima,” alisema. “Kwahiyo kurudiana hiyo ni kwenye ndoto tu siyo kitu hata ambacho unaweza kukizungumzia. Sio mpenzi mpya nimekutana naye baada ya mwaka mmoja kuachana na Sugu, sasa hivi tuna kama mwaka,” aliongeza.

Speed 120 Aliyoihaidi Mh. Lowassa Ingetoka kwa Watu Hawa Kama Angeupata Urais

$
0
0
Edward Lowassa
Ni siku kadhaa zimeshapita ambazo watanzania wengi hasa wale wa mijini waliweka matumaini yao dhidi ya utawala mpya kama nilivyoelezea hapo juu...

Ilikuwa ukipita mitaani utagundua watu wakiwa katika matumaini mapya yenye furaha kuwa hakika yule watakayemchagua ndiye atapita lakini ikawa ndivyo sivyo...

Nilipopita mitaani hasa hapa dar es salaam nilipata nafasi ya kusikia maoni ya watu wengi sana..lakini moja ya maoni ya vijana wengi na wazee wengi pale ubungo kituo cha mabasi yaendayo mikoani ndiyo yaliyonikosha zaidi...

Ni pale niliposikia watu wakidadavua ile ahadi ya lowassa ya speed 120 jinsi ambavyo angetekeleza chini ya baraza hili la mawaziri..kijana mmoja niliyemfahamu kwa jina la yassin alijaribu kuunda baraza la mawaziri chini ya mh. raisi lowassa nalo lilikuwa hivi:::

WAZIRI MKUU----Mh F.A.Mbowe

Waziri wa katiba na sheria---Mh. Tundu lissu.


Waziri wa Maliasili na utalii---Mh. Rev Peter msigwa


Waziri wa wanawake jinsia na watoto---Mh. Halima mdee

Waziri wa ulinzi na usalama---Mh. G.Lema


Waziri wa mambo ya ndani----Mh. J J Mnyika


Waziri wa michezo na sanaa---Mh. Sugu


Waziri wa Waziri wa fedha---mbatia

Waziri wa ardhi----salumu mwalimu


aliendelea kushuka kushuka na akamaliza kwa kusema watanzania mnafikiri chini ya mawaziri hawa kwanini kusiwe na SPEED 120?


SASA: Leo nimepita tena mahali pale Ohooo...ndugu yangu watu kama wamemwagiwa maji....watu wamehuzunika saana watu hawana Amani wamepoteza matumaini hawana hili wala lile....ni sawa na mfungwa aliyewekwa gerezani kwa miaka zaidi ya hamsini baadaya sikuchache akitarajia kufunguliwa halafu siku hiyo anaambiwa ameongezewa miaka mitano tena....ohoooo....piga picha jinsi anatakavyoumia...basi ndivyo hali inavyoendelea huku mitaani....

'Baada ya Watanzania Kudhulumiwa Haki yao ya Kuchagua Nchi Imekuwa Kimya Kama Mkiwa' James Lembeli

$
0
0
 Aliyekuwa Mgombea wa Ubunge Kahama Kwa Kupitia Tiketi ya Chadema Amevunja Ukimya na Kuandika Haya Hapa Chini Katika Page yake ya Facebook:

JOYCE KIRIA...Aibuka na Mpya....Awaponda Wanaume na Wanawake Wenye Hizi Tabia Mbaya...........

$
0
0
Joyce Kiria na Mumewe Henry Kilewo

Joyce Kiria Ameandika Haya Kwenye Ukurasa wake wa Faceook:

'Ukiona Mwanaume anaumia na kupiga makelele ya kukatisha tamaa watu kwenye post zao, hasa pale anapoona mwanamke anamsaidia mume wake kwa hali na mali, ukiona mwanaume anakazana kumkatisha mwanamke wa mwanaume mwenzake tamaa kwa manenomaneno! ukiona Mwanaume wa aina hiyo basi ujue ana mambo mawili!!! Au ana mwanamke mzigo ambae hajawahi kumsaidia hata kwa mawazo ya kumtia moyo katika kazi zake, au mwanaume huyo ni bwabwa! Hahahaha yaani ni Mwanaume/Mwanamke siku hizi mjini wanaongezeka kwa kasi hahaha! Washaingiwa na mawivu ya kike yale ya chuki hahaha

Mwanaume wa kweli Rijali sifa yake anapenda mwanamke anaesaidia familia yake (mwenzi wake) katika shida na raha kwenye gurudumu la maisha, Mwanaume wa kweli anaejiamini hapendi Mwanamke golikipa a.k.a Mwanamke Mzigo!!! Na akiwa na Mwanamke mzigo basi ni wazi hatamshirikisha kamwe katika biashara zake, analiwacha huko ndani kama fanicha ndo maana linakuwa na hasira na bidii za wenzao Hahahaha

Ukiona Mwanamke anapigapiga mayowe kwa post kisa Mwanamke mwenzake anamsaidia mume kwa hali na mali, huyu jua ni wivu wa chuki umemkaba kooni (siyo wivu wa Maendeleo)! Usijisumbie maana wengi wako ivo! Badala ya kutamani nae apate kama mwenzake alivyopata, na kufanya bidii, yeye atawanga mchana kweupe ili ukose! Mawivu ya chuki ndo imewajaa! Yaani hilo si jambo geni kwa wanawake walio wengi Hahaha

Wengi wao wamezoea kuwekwa mjini na wanaume wengi wengi ilimradi waishi mjini hahaha yaani hawana ujasiri wa kuonyesha Waume wao hadharani maana wanao mabuzi kumikumi mjini hahaha... Yaani ili wale, wavae, wamiliki simu, wapige simu, aingie insta ni mpaka watoe dyudyu kwa wanaume mia mia Hahahahaha

Watu wa aina hiyo wana maneno wengi sana ila hayamzuii tembo kunywa maji... Watu waliozoea kuhaso longtime hawaBabaishwi na vimaneno vya watu walioshindwa maisha Hahahaha... watu waliohaso wana misimamo yao miaka 800000000 hawayumbishwi wana Misimamo mupoooo???
Ukitaka kuwajua watu hao pitia coment zao!
(Wanaume wa kweli na Wanawake wa kweli wapo wanatoa sapoti) wewe wafwaaaaaa na wivu wako wa chuki...
Tamani cha mwenzako na huku unaweka bidii ya kutafuta , siyo unaumia kwa sababu mwenzako akipata atakuzidi fyuuuu'

Nimeikumbuka Kauli ya DK SLAA "Chama Changu Chadema Hakiwezi Kushinda Urais Mwaka huu 2015 Kutokana na Kula Matapishi Yetu..."

$
0
0
DK Slaa
"Chadema hakikuwa chama cha kukumbatia ufisadi na mafisadi..hakikuwa chama cha kusomba watu na magari mikutanoni...hakikuwa chama cha kuiba na kununua kura...sasa Chadema hii si ile tulioijenga....
nimeamua kustaafu siasa maana najua chama changu hakiwezi kushinda urais mwaka huu 2015 kutokana na kula matapishi yetu..." Dk Slaa:

Je Slaa ni mkweli??

Watu Sita Wapoteza Maisha Katika Ajali ya Gari Morogoro

$
0
0
Watu sita wamefariki dunia baada ya gari ndogo waliokuwa wakisafiria kugongana uso kwa uso na basi la abiria mali ya kampuni ya Princess Muro, lililokuwa likitokea Dar es salaam kuelekea Tunduma, katika eneo la hifadhi ya taifa ya Mikumi, barabara kuu ya Morogoro-Iringa.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Morogoro Leonard Paulo amethibitisha kutokea kwa ajali hiyo katika eneo la hifadhi ya taifa ya Mikumi, ikihusisha gari ndogo la abiria aina ya Toyota Noah lenye namba za usajili T 359 BBA iliyokuwa imebeba abiria sita wakiwemo wanawake wawili na wanaume wanne ambayo ilipasuka tairi ya Mbele ya kuyumba ovyo barabarani na kugongana na basi hilo la Princess Muro lenye namba T 160 BBC na kusababisha vifo kwa abiria wote wa Noah.

Amesema basi hilo la abiria aina ya Zangton lililoharibika zaidi mbele huku Noah ikiharibika kabisa, likuwa likiendeshwa na Silos Wilfred (55) mkazi wa Mbeya ambaye anahojiwa na polisi kuhusiana na tukio hilo, na kwamba basi alilokuwa akiendesha lilikuwa na abiria 59 ambao hawakupata madhara makubwa, isipokuwa michubuko kidogo kwa baadhi yao na walitafutiwa usafiri kuendelea na safari.

Katika upekuzi wa miili ya abiria waliokuwa kwenye Noah inayodaiwa kuhusika na ubebaji wa magazeti, viligundulika vitambulisho vimne vya Ali Nduti Mohamed (27), mkazi wa Mbeya,Sani Elion Mkwabe (24) mkazi wa Kunduchi, Patrick Mkelegene (43) mkazi wa Buguruni Malapa na Selemani Omary (30) ambaye makazi yake hàyajaweza kujulikana Mara moja.

Miili ya watu hao waliopoteza maisha imehifadhiwa katika chumba cha kuhifadhi maiti cha hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Morogoro.

Matokeo ya Mtihani wa Kitaifa wa Darasa la Saba 2015 Yako Hapa

CCM Washikana 'Uchawi' Baada ya Kulipoteza Jimbo La Bunda

$
0
0
BAADHI ya vijana wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wilayani Bunda wamemtuhumu mwenyekiti wa chama hicho wilayani hapa, Chacha Gimanwa, kwamba alichangia jimbo la Bunda Mjini kuchukuliwa na mgombea wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) katika uchaguzi mkuu uliofanyika Oktoba 25 mwaka huu.

Vijana hao walitoa tuhuma hizo, juzi wakati wakitembea matembezi ya amani ya kushangilia ushindi wa mgombea urais wa CCM, Dk Jonh Magufuli katika mitaa mbalimbali ya mji wa Bunda.
 
Katika uchaguzi mkuu uliopita CCM ilipoteza jimbo hilo, baada ya Stephen Wasira aliyekuwa akitetea kiti hicho kushindwa na mgombea wa Chadema, Ester Bulaya.

Hata hivyo Wasira ambaye pia ni Waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika hivi karibuni akizungumza na waandishi wa habari jijini Mwanza alidai kuwa katika uchaguzi huo kulikuwa na hujuma.

Wanachama hao wa CCM wakiwa wamebeba mabango baadhi yao walisikika wakimtaja moja kwa moja Gimanwa kwamba ndiye alisababisha CCM kushindwa katika jimbo hilo na kuomba uongozi wa juu wa chama hicho umchukulie hatua.

Hata hivyo, Gimanwa akizungumza na mtandao huu kwa njia ya simu jana alisema kuwa tuhuma hizo hazina msingi wowote na kwamba kamwe hawezi kukihujumu chama chake.
 
“Hicho ni kikundi cha watu wachache tu wanaotaka kuniharibia jina.Mimi kura yangu ni moja na wapiga kura ni wengi, sasa iweje mimi nisababishe mgombea wa jimbo la Bunda mjini ashindwe?” Alihoji.

 Alisema yeye kama mwenyekiti wa CCM alikuwa akifanya kampeni pia katika jimbo la Bunda vijijini, na siku tatu kabla ya uchaguzi mkuu alirudi tena Bunda mjini na kuendelea na kampeni.

Butiku: Wazanzibar Msikubali Kurudia Uchaguzi

$
0
0
Taasisi ya mwalimu Nyerere imeitaka tume ya uchaguzi ya Zanzibar ZEC kufanya kazi kwa kuzingatia katiba ya nchi na sheria na sio kutanguliza mbele maslahi binafsi ya kisiasa hatua ambayo inaweza kusababisha machafuko na umwagaji wa damu.
 
Akizungumza na vyombo vya habari mjini Musoma, mkurugenzi mtendaji wa taasisi hiyo mzee Joseph Butiku, amesema amekerwa na tabia ya ZEC kusitisha uchaguzi na kushindwa kuwatangazia wananchi kiongozi wao waliomchagua, huku ikishindwa kuheshimu matakwa ya wananchi waliopiga kura katika visiwa vya Zanzibar.
 
Aidha mzee Butiku amewataka wananchi wa Zanzibar kutokubali tena kurudia upigaji wa kura hadi hapo yatakapotolewa maelezo ya kuridhisha na wahusika waliosababisha uchaguzi huo kufutwa pia waweze kuchukuliwa hatua kali za kisheria
 
Kwa sababu hiyo amewataka viongozi kuheshimu sheria na katiba ya nchi na kwamba chama ambacho kinadhani kimeshindwa katika uchaguzi huo kikubali matokeo badala ya kuifanya zanzibar ni mali ya chama fulani pekeee.

Mwigizaji Aunty Ezekiel Adaiwa Kuhongwa Gari na Kigogo...Mwenyewe Asema Haya

$
0
0
Aunty Ezekiel
BAADA ya kuanika picha za gari lake jipya aina ya Audi A4 kwenye akaunti yake ya mtandao wa kijamii wa Instagram akimshukuru mpenzi wake, Moses Iyobo ‘Mozes’ kwa kumzawadia ‘mkoko’ huo, staa wa sinema za Kibongo, Aunt Ezekiel Grayson ‘Mama Cookie’ anadaiwa kuhongwa gari hilo na kigogo.

Gari analodaiwa kupewa zqawadi Aunt. 
Mara tu baada ya ‘kuposti’ picha za gari hilo, baadhi ya mashabiki wa Aunt ambao ni watu wake wa karibu waligawanyika, wapo waliodai gari hilo lilitokana na kampeni za Chama Cha Mapinduzi (CCM) na wengine walidai amehongwa bila kumtaja mtu aliyemuhonga.

Jamani Aunt si useme tu kuwa gari umehongwa? Usimsingizie Moze Iyobo na kama si hivyo basi ni fedha ulizopata kwenye kampeni si bure,” alisema mmoja wa mashabiki wake hao.

Alipobanwa na mwandishi wetu, Aunt alifunguka kwamba, hana la zaidi kwani ameshaweka wazi gari hilo amelitoa wapi na asiyeamini abaki hivyohivyo. “Nimenunuliwa na baba Cookie, hayo mambo yenu ya kampeni mimi siyajui wala sijahongwa kwani hakuna mwenye ubavu wa kunihonga kwa sasa,” alisema Aunt.
GPL

Oh My God!! Woman Twerking For God in Church Better than VERA and HUDDAH

$
0
0


If you thought tweaking is meant for socialites and wannabes in clubs and in their privacy, think again.

Watch this akorino woman twerking in church way better than socialites like Vera and Huddah.


Jack Wolper Adai Hakika LOWASSA Ni Shupavu na Jasiri Haijawahi Tokea

$
0
0
Jackline Wolper
Msanii wa filamu nchini Tanzania, Jacqueline Wolper, aliyekuwa mstari wa mbele kumsapoti mgombea urais kwa mwavuli wa UKAWA Mhe. Edward Lowassa, amedai kuwa kwake yeye mheshimiwa huyo ndiye kiongozi shupavu na jasiri.

Wolper, amemmwagia sifa lukuki waziri mkuu huyo wa zamani na kuwataka Watanzania kuwa pamoja katika kuijenga nchi na kudai kuwa Mh. Lowassa amekuwa mstari wa mbele kwa kupambana kwa kuleta mabadiliko kwa watanzania.

Amenukuliwa akisema kuwa anaamini kuwa Lowassa, ameleta historia kubwa sana nchini kwasababu haijawahi kutokea Tanzania, kwani ametuma ujumbe kwa viongozi wengine ambao walikua wazembe na waliojisahau na kudai kuwa anaamini wataifanya nchi kuwa mpya.

Ameongeza kuwa yeye bado anaamini Lowassa ni kiongozi shupavu, muelewa na mwenye akili za kupambanua mambo, na kusema kuwa kushindwa kwake haijalishi kwa sababu anaamini watanzania wanamkubali hasa kwenye mabadiliko.

Aidha, amewataka wasanii wenzake ambao wapo CCM wasijengeane chuki kwa yaliyotokea kwani aliamua kutafuta haki yake ya msingi akiwa kama msanii.

Sambamba na hilo amedai kuwa kwa wana mabadiliko wenzake waendelee kupambana na watakao wawakilisha bungeni wafanye kazi ya maana hasa kuwatetea wanyonge.

Dog Finds an Abandoned Baby/Foetus And Takes it to Safety (photos)

$
0
0

This is so amazing but biko, is that a foetus or a fully formed baby? Don't know where this happened but according to reports, this dog found the newly born baby and took it to where people could see it. The dog carried the baby in its mouth and amazingly didn't hurt the baby. See another pic after the cut


Viewing all 104809 articles
Browse latest View live




Latest Images