Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104809 articles
Browse latest View live

Wema Sepetu, Adai Lowassa Angeshinda Urais wa Tanzania Ingebidi Ahame Nchi

$
0
0
Maneno kuntu! Staa mwenye nyota ya kipekee Bongo, Wema Isaac Sepetu amefungua kinywa chake na kusema kuwa endapo Mgombea wa Urais wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Edward Lowassa angeshinda kuwa Rais wa Tanzania katika uchaguzi uliopita, bila hiyana yeye angehama nchi.

Akizungumza na Ijumaa Wikienda, Wema alisema kuwa anamshukuru Mungu kuwa anasubiri kwa hamu kuapishwa kwa mshindi wa nafasi hiyo, Dk. John Magufuli ambaye anamuamini ni mchapakazi asiyekuwa na urafiki na mtu mzembe.

“Sifichi, kweli kabisa Lowassa angeshinda, bila ubishi ningehama nchi yangu niipendayo,” alisema Wema.
GPL

Baraza Jipya la Mawaziri la Rais Mteuliwa John Pombe Magufuli

$
0
0
TAIFA liko katika mkao wa kusubiri kuapishwa kwa Rais Mteule wa Awamu ya Tano, Dk. John Pombe Magufuli ambaye Alhamisi iliyopita alitangazwa kuwa mshindi wa kinyang’anyiro cha urais dhidi ya wenzake saba lakini tayari Wabongo wanaumiza vichwa kuhusu Baraza Jipya la Mawaziri la Magufuli.

Tume ya Taifa ya Uchaguzi Tanzania (Nec), ilimtangaza Dk. Magufuli kuwa mshindi mbele ya wagombea wengine ambao ni Anna Elisha Mghwira (ACT-Wazalendo), Hashim Rungwe Spunda (Chaumma), John Pombe Magufuli (CCM) na Edward Nyoyai Lowassa (Chadema akiungwa mkono na Umoja wa Katiba ya Wananchi, Ukawa ambao ni Cuf, NCCR-Mageuzi na NLD).

Wengine ni Macmillan Lyimo Elifatio (TLP), Chief Lutasola Yemba (ADC), Malick Jankin Kasambala (NRA) na Fahim Dovutwa Nassoro (UPDP).

WIKIENDA LAINGIA MTAANI
Mwishoni mwa wiki iliyopita, gazeti hili lilizunguka katika Jiji la Dar kwa lengo la kuzungumza na wasomaji wake kuhusu mitazamo yao ya wana-CCM waliopata nafasi ya ubunge ambao wanaweza kuitwa kwenye baraza la mawaziri la Dk. Magufuli ambaye ataapishwa Alhamisi wiki hii.

Kila msomaji alikuwa na mawazo yake, lakini wengi mawazo yao yaliangukia sehemu moja kwa kuzingatia mikoa, kanda na imani za kidini na hivyo kutoa picha ya baraza hilo.
“Kwanza kabisa ijulikane kwamba, Magufuli hataweza kufanya kazi na mawaziri wazembe. Yeye ni mchapa kazi, lazima atachagua wenye uwezo lakini pia uteuzi wake lazima ataangalia haki, kila mkoa atatoa waziri, pia ataangalia kanda na kubalansi dini.

“Hii inanipa picha kwamba, pia anaweza kuwateua wabunge kupitia zile nafasi zake kumi kama ataona kuna mtu anamtaka afanye naye kazi lakini hakuupata ubunge. Si unajua katiba inasema ili uwe waziri lazima uwe mbunge,” alisema msomaji mmoja aliyejitambulisha kwa jina la Fime, mkazi wa Mwananyama A,

WAZIRI MKUU
Kwa mujibu wa wasomaji hao, nafasi ya uwaziri mkuu wengi wameipeleka kwa Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Vangimembe Lukuvi (Mkoa wa Iringa).

“Huyu bwana ni mwenye subira, mstahimilivu, mvumilivu na mtulivu lakini pia ni mchapa kazi. Tumeona alivyoinyoosha wizara yake ya ardhi. Hata alipokuwa Mkuu wa Mkoa wa Dar, alifanya vizuri. Anaweza kumsaidia rais katika ubora wake,” alisema msomaji mwingine akisema anaitwa Bakar Omar, mkazi wa Tabata Matumbi.

NISHATI NA MADINI

“Mimi naamini Wizara ya Nishati na Madini atarudishwa Sospeter Augustino Muhongo (Mkoa wa Mara). Huyu alijiuzulu uwaziri kwa kashfa ya Akaunti ya Tegeta Escrow, lakini baadaye alisafishwa kwamba hakuhusika. Akiwa kwenye wizara ile aliiweza kwa kipindi kifupi tuliona mabadiliko. Msaidizi wake awe Charles Mwijage (Mkoa wa Kagera),” alisema mama Mapunda, mkazi wa Kigogo Luhanga.

MAMBO YA NJE NA USHIRIKIANO WA KIMATAIFA
“Mimi mawazo yangu lazima Magufuli atamrejesha Benard Kamilius Membe (Mkoa wa Lindi) au atamuweka mama Asha-rose Mtengeti Migiro (atamteua) kwa sababu, Magufuli kimataifa hajulikani sana. Kwa hiyo ili mambo yake yaende vizuri, lazima atawategemea hawa kwa vile wana uzoefu na nje kwa muda mrefu.
“Migiro alishakaa Umoja wa Mataifa akimsaidia Katibu Mkuu, Ban Ki-moon. Membe yeye alikuwa waziri wa wizara hiyo kwa miaka kumi,” alisema Celina Samson, mkazi wa Ilala Boma.

WIZARA YA AFYA 

“Naamini Hussein Ally Mwinyi (Zanzibar) anaiweza. Arudishwe pale kwani hata alipokuwa awali aliiweza. Lakini naibu wake anafaa sana kuwa Mbunge wa Kigamboni, Faustine Ndungulile (Mkoa wa Dar es Salaam). Huyu jamaa kwenye afya ni mkali,” alisema Joseph Hamisi, mkazi wa Temeke Sokota.

WIZARA YA UJENZI

“Hii wizara ndiyo ya Magufuli mwenyewe. Kwanza naamini ataipeleka kwenye ofisi yake. Waziri wake ataitwa waziri wa nchi ofisi ya rais, ujenzi, uchukuzi na miundombinu. Atampa Harrison Mwakyembe (Mkoa wa Mbeya). Asaidiwe na Gerson Lwenge ( mpya Mkoa wa Njombe), hawa jamaa wataiweza kwani na wao ni mchakachaka kama Magufuli mwenyewe,” alisema Kidawa Halfan, mkazi wa Kigamboni, Tungi, Dar.

MAWASILIANO SAYANSI NA TEKNOLOJIA
Mzee Salimu Jenda, mkazi wa Mikocheni: “January Makamba (Mkoa wa Tanga), naamini atarudi kuwa waziri kabisa. Lakini huyu anatakiwa kusaidiana na Hamis Kigwangala (Mkoa wa Tabora). Hii timu ikiwa pamoja mambo yataiva.”

WIZARA YA FEDHA
“Kwanza hii wizara naamini itaunganishwa na Mipango. Mwigulu Lameck Nchemba (Mkoa wa Singida) ni sahihi kwake kuwa waziri kamili badala ya unaibu kama alivyokuwa mwanzo. Asaidiwe na yule mama Angelina Mabula (mpya Mkoa wa Mwanza) ni mzuri sana. Ni mchumi na mbobezi wa mambo ya uhasibu. Wataiweza hii wizara ikiwa moja,” alisema Maua Jumanne, mkazi wa Kibamba.

WIZARA YA ULINZI
Sakina Ngalawa, mkazi wa Vingunguti: “Kwanza hii wizara iungwe na wizara ya mambo ya ndani, iwe moja tu. Magufuli alishasema ataunda baraza dogo. Anayeimudu ni Kangi Lugola (mpya Mkoa wa Mara) ni mpiganaji mzuri sana. awe waziri kamili akisaidiwa na Injinia Stella Manyanya (Mkoa wa Ruvuma)

WIZARA YA SHERIA

“Anayefaa ni Job Ndugai (mpya Mkoa wa Dodoma). Unajua yule bwana yupo vizuri sana kwenye sheria na ana misimamo. Wanasheria wote wako vile,” alisema Roman Joseph, mkazi wa Mbagala Kuu.

OFISI YA WAZIRI MKUU, SERA NA URATIBU WA BUNGE
“Jamani mimi naona Nape Nnauye (mpya Mkoa wa Lindi) ndiyo anaiweza. Tumeona alivyopigania chama chake mpaka kubaki madarakani. Ni mzuri kwenye kuratibu na kusimamia sera,” alisema Anna Mmakonde, mkazi wa Msasani.

WIZARA YA ELIMU

“Jenista Joachim Mhagama (Mkoa wa Ruvuma), angetolewa kwenye sera na uratibu wa bunge awe waziri kamili wa elimu. Huyu mama ataiweza, ni mpiga kazi mzuri sana,” alisema Saimen Kimari, mkazi wa Buguruni.
Hata hivyo, haya yanabaki kuwa maoni na mtazamo wa wasomaji wetu, nafasi hizo za utumishi, zinabaki kuwa maamuzi ya rais mwenyewe kulingana na sifa zao.

Source: Global Publishers

SHAMEFUL ACT! Bride Raises Wedding Gown to Twerk with Bare As$ [Video]

$
0
0

The bride in the video below raises her wedding gown to twerk with her bare bu*tt. Is she under the influence of alcohol? Find out. A young lady raises up her already transparent wedding gown and twerks with her n@ked b*utt during what looks like an after wedding party. The video which has gone viral shows her twerking around a pole on a platform that looks like one set up for Stripers

Dr. Magufuli Ashauriwa Kutofanya Uteuzi Wa Baraza la Mawaziri Kwa Kulipa FADHILA

$
0
0
RAIS Mteule wa awamu ya tano katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Dkt.John Pombe Magufuli, ameshauriwa kuwa makini katika uundaji wa Baraza lake la Mawaziri kwa kuepuka masuala ya kujuana au kuteua kwa shinikizo la baadhi ya wanasiasa wenye masilahi binafsi.

Akizungumza na m,wandishi wetu jana jijini Dar es Salaam, Mhadhiri mstaafu wa masuala ya Uongozi katika Chuo Kikuu cha Mzumbe, Morogoro Dkt. Alfred Chimage, alisema tatizo kubwa la viongozi wa Tanzania ni kutokuwa na uwezo wa kutambua watu wanaofaa, wanaopaswa kuwateua ili kuwasaidia kuongoza nchi.

Aliongeza kwamba viongozi wengi waliofanikiwa ni wale wenye uwezo mkubwa wa kupanga timu sahihi ya wasaidizi katika masuala ya uongozi.

Dkt. Chimage alisema Dkt. Magufuli anaweza kuwa kiongozi mzuri lakini hofu iliyopo anaonekana kuzungukwa na kundi kubwa la wanasiasa hususan wanaoamini kwamba wametoa mchango mkubwa kwake kumfikisha hapo alipo; hivyo kutaka kupata fadhila za nafasi za juu za uongozi kwa ajili ya ndugu zao wa karibu na hata watoto wao.

"Inawezekana Magufuli ni kiongozi mzuri, lakini ukiangalia anavyoonekana ni kama tayari amemezwa na baadhi ya wanasiasa wanaojinasibu na kujiona kana kwamba amefikia hatua hiyo kwa nguvu yao.

"Mbali na hilo, ukiangalia mazingira ya siasa zinazomzunguka ni kama kwamba kuna kundi la wanasiasa wakongwe ndani ya CCM linaloamini kwamba litaendelea kumpa maelekezo kwa hatua mbalimbali ikiwemo ya kuteua baraza la mawaziri.

"Akinaswa kwenye mtego huo atakuwa amefanya kosa kubwa la kwanza kwenye uongozi wake," alisema mtaalamu huyo na kuongeza;

"Kuna wanasiasa wengi ambao unawaona moja kwa moja wanajisogeza kwa nguvu sana kwa Magufuli si kwa kumsaidia kuongoza nchi peke yake, bali wana malengo maalumu kuhakikisha wananufaika kwenye uongozi wake kwa ndugu, jamaa na hata watoto wao kupewa madaraka ya juu".

Alisema katika kipindi hiki, Dkt. Magufuli anapaswa kuwa makini zaidi ili kuepusha Serikali yake kupoteza imani mbele ya Watanzania kwa kuendekeza kile kinachofahamika kama siasa za kujuana na kubebana kama njia ya kulipa fadhila.

Alisema Dkt. Magufuli anapaswa kutambua kwamba yeye ni rais wa Watanzania wote na si rais wala rafiki ya familia au kundi fulani la watu, hivyo anapaswa kuteua mawaziri na watendaji wengine kwa kigezo cha uwezo.
 
"Magufuli asipokuwa makini malalamiko ya kwanza ya wananchi yatakuja baada tu ya kutangaza Baraza lake la Mawaziri, kama litaonekana kubeba watu kwa misingi ya kujuana. Anachopaswa kufanya ni kuacha mamlaka husika zifanye proper vetting (Uhakiki wa kina) wa sifa za kila anayeona anafaa".

"Asiteue baraza kwa misingi ya huyu ni rafiki yangu au ni ndugu au mtoto wa mtu fulani, hapana atajiharibia kabisa," alisema.

Ameshauri pia kuwa makini kuepuka watendaji wote ambao kwa njia moja ama nyingine walihusishwa na kashfa mbalimbali kwenye serikali iliyopita.

"Wakati wa kampeni Magufuli ameimba sana neno mabadiliko, mabadiliko haya yasiwe ya kusema tu. Wananchi wanasubiri waone mabadiliko hayo kuanzia timu ya watu atakaowateua kufanya nao kazi. Watu wanatarajia kuona mawaziri safi wasio na 'makandokando'.

"Anapaswa kuwa makini na kila mtu. Atumie ile falsafa ya mke wa Kaisari. Aachane na wote waliosemwa vibaya kwenye serikali iliyopita hata kama wanaonekana kuchapa kazi. Mifano ipo mingi, waliochafuka kwa Escrow, kwa uozo wa bandari, ununuzi wa mabehewa mabovu. Ili aingie kama kiongozi safi na mtu wa mabadiliko ya kweli azibe mapema mianya kama hii. Watanzania watapata imani na atafanikiwa," alisema.

Alisisitiza kwamba Magufuli anapaswa kuwa makini kuepuka mitego ya kindugu, urafiki na kifamilia ambayo alisema imeonekana kuwa tatizo kubwa katika masuala ya uongozi hapa nchini.

Alisema kigezo pekee cha mtu kuteuliwa kuwa waziri au kiongozi wa nafasi yoyote ile ni kuchapa kazi.

MREMA Afunguka: Sijakata Tamaa, Nitaendelea Kuwania Nafasi Mbalimbali za Kisiasa

$
0
0
Mwenyekiti wa Taifa wa Tanzania Labour Party (TLP), Augustine Mrema, amesema hata kama vyama vinavyounda Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa) vimefanikiwa kumwangusha kwenye kinyang’anyiro cha ubunge katika Jimbo la Vunjo mkoani Kilimanjaro, bado ana nguvu ya kuendelea kuwania nafasi mbalimbali za kisiasa na wala hajakata tamaa ya kukisuka upya chama chake.

Mrema aliangushwa katika kiti hicho na hasimu wake kisiasa, James Mbatia, ambaye pia ni Mwenyekiti wa Taifa wa Chama cha NCCR-Mageuzi, aliyevunja rekodi ya kupata kura nyingi kwa upande wa wabunge wa upinzani, baada ya kuibuka na ushindi mnono wa  kura 60,187 dhidi ya 6,416 alizoambulia Mrema (TLP) aliyekuwa akishikilia jimbo hilo huku mgombea wa CCM, Innocent Shirima, akipata kura 16,097.

Alikuwa akihojiwa jana na kituo kimoja cha redio mkoani Kilimanjaro kuhusu majaliwa yake kisiasa, baada ya yeye na chama chake kukosa uwakilishi kwenye Bunge na Halmashauri za Wilaya. Mbali ya kupoteza kiti cha ubunge, TLP haikuambulia   hata kiti kimoja cha udiwani.

“Chama changu hakifi na wala sijakata tamaa, tutaanza moja na ninawaomba wanachama wa TLP watulie…Nitashirikiana na Rais ajaye aliyetangazwa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi (Nec), na tutakijenga chama chetu…Hata Dk. John Magufuli, anajua mimi ni mchapakazi na alinipigia debe na wananchi wakapuuza,” alisema Mrema.

Katika Mkoa wa Kilimanjaro wenye majimbo tisa ya uchaguzi, viti saba vya ubunge vimenyakuliwa na baadhi ya vyama vinavyounda Ukawa vya Chadema na NCCR-Mageuzi, huku majimbo mawili ya Mwanga na Same Magharibi, yakiangukia CCM.

Kwa mujibu wa matokeo hayo, Chadema iliyovuna wabunge sita na NCCR-Mageuzi yenye mbunge mmoja mkoani  Kilimanjaro, sasa zitaunda halmashauri tano za wilaya ambazo ni Moshi Mjini, Hai, Siha, Rombo, Moshi Vijijini na Vunjo; wakati CCM ikiwa imeambulia Halmashauri mbili za Mwanga na Same.

Majimbo hayo na idadi ya kata ambazo Chadema na NCCR-Mageuzi zitaunda halmashauri zake ni kama ifuatavyo;
Moshi Mjini, Chadema imeshinda Kata 19 kati ya 21 na CCM imepata Kata mbili za Bondeni na Kilimanjaro, wakati Jimbo la Hai, Chadema imeshinda kata 16 kati ya 17, ambapo Kata moja ya Bomang’ombe ndio pekee haijafanya uchaguzi kutokana na mgombea wa CCM kufariki dunia wakati wa kampeni za uchaguzi mkuu.

Aidha, Chadema iliyoshinda kata 27 kati ya 28 za Wilaya ya Rombo, ndiyo itakayounda halmashauri ya wilaya hiyo, huku NCCR-Mageuzi iliyoshinda kata nane, kati ya 16 na Chadema iliyoshinda viti 15 vya udiwani katika Jimbo la Moshi Vijijini, sasa zitaunda Halmashauri moja ya Wilaya ya Moshi.

Katika Jimbo la Moshi Vijijini, CCM imeshinda kata moja tu.

Jeshi la Polisi Lapiga Stop Maandamano ya Chadema Kupinga Matokeo ya Uchaguzi Mkuu, Chadema Yasema Maandamano yapo Pale Pale

$
0
0
Taarifa ya jeshi la polisi mkoa wa Shinyanga kwa vyombo vya habari
Jeshi la polisi mkoa wa Shinyanga limezuia maandamano ya Chama Cha Demokrasia na Maendeleo(Chadema) yaliyopangwa kufanyika Kesho Novemba 03,2015 katika mji wa Shinyanga kwa lengo la kupinga matokeo yaliyotangazwa na tume ya taifa ya uchaguzi katika uchaguzi mkuu uliofanyika Oktoba 25,2015.

Akizungumza na waandishi wa habari leo asubuhi kamanda wa polisi mkoa wa Shinyanga SACP Justus Kamugisha amesema wamezuia maandamano yaliyopangwa na Chadema kufanyika Novemba 03,2015 asubuhi akidai kuwa katika kipindi hiki hawaruhusu kufanyika kwa maandamano na mikutano kwa sababu jeshi la polisi limejikita katika kuangalia hali ya usalama utawale ili kusubiria kuapishwa kwa rais mteule na wabunge.
Amesema pia wamezuia mikusanyiko yoyote isiyo rasmi ambayo inaweza kuleta uchochezi na uvunjifu wa amani kwani kufanya hivyo ni kinyume cha sheria na watakaokiuka watachukuliwa hatua za kisheria.

Kamanda Kamugisha amesema Chadema wametoa taarifa kuwa Kesho wanataka kuandamana kupinga matokeo ya uchaguzi yaliyotangazwa na tume ya taifa ya uchaguzi uliofanyika Oktoba 25,2015 na baada ya kufanya maandamaano hayo wanataka kutoa ujumbe kwa serikali.
Amewashauri wananchi wote wa mkoa wa Shinyanga wasishawishiwe na viongozi wa vyama vya siasa,na kuwaomba wabaki majumbani,waendelee na shughuli zao na kutokubali kurubuniwa au kushawishiwa kuandamana kwani wanaowashawishi hawatakuwa mbele .

Katibu wa Chadema wilaya ya Shinyanga mjini George Kitalama amesema hawajapata taarifa wala maelekezo yoyote kuhusu kuzuiwa kwa maandamano yao na wanaendelea kujiandaa na wanachama wao kwa maandamano kama walivyopewa maagizo na viongozi wao wa kitaifa.
Amesema kesho 03.11.2015,watafanya maandamano ya amani kuanzia ofisi za Chadema wilaya kisha kuzunguka mji mzima wa Shinyanga kuanzia saa tatu asubuhi kupinga matokeo ya uchaguzi yaliyotangazwa na tume,na kwamba ni maandamano ya nchi nzima siyo Shinyanga pekee.

Ukomo wa Urais wa Dk Shein Zanzibar Utata Mtupu

$
0
0
Ukomo wa madaraka wa Rais wa Zanzibar, Dk Ali Mohamed Shein umeibua utata na kusababisha wanasheria na polisi kutoa tafsiri zinazokinzana.

Wakati Chama cha Wanasheria wa Zanzibar (ZLS) kikisema kwa mujibu wa Katiba ya Zanzibar tarehe ya mwisho ya Dk Shein kuingia ofisini ni leo Novemba 2, polisi kwa upande wao wanasema Rais huyo anatakiwa kushika madaraka hayo hadi pale rais mpya atakapoapishwa.

Rais wa ZLS, Awadh Ali Said alisema mwishoni mwa wiki kuwa moja ya athari za tamko la Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC) kufuta uchaguzi wa Zanzibar ni kusababisha mgogoro wa kikatiba hasa katika muda wa rais kushika madaraka.

Said alisema Ibara ya 28 (2) ya Katiba ya Zanzibar ya 1984 inaeleza kuwa Rais ataacha madaraka yake baada ya kumalizika miaka mitano kuanzia tarehe alipokula kiapo cha uaminifu na kiapo cha kuwa Rais.

Alisema tafsiri yake ni kuwa tangu Dk Shein alipokula kiapo cha uaminifu na kiapo cha kuwa rais Novemba 3, 2010 atakuwa ametimiza miaka mitano Novemba 2, 2015.

“Hivyo akiendelea kushikilia madaraka ya urais zaidi ya tarehe hiyo itakuwa kinyume na Katiba ya nchi,” alisema.

Kutokana na madai hayo, Jeshi la Polisi Zanzibar limewatahadharisha wananchi kutojihusisha na vitendo vya fujo kwa madai kwamba kuanzia leo hakutakuwa na Serikali.



Walichosema ZLS

Kwa mujibu wa Rais wa ZLS, maudhui ya Ibara 28 (1) hiyo ni kumpa uwezo wa kikatiba Rais kuendelea ili kutoa nafasi ya maandalizi ya kula kiapo kwa Rais anayefuata tu na si kuendelea kukaa madarakani bila ya kufanyika kwa uchaguzi au kwa sababu ya Uchaguzi kufutwa.

Hata hivyo Said alisema nchi kuendeshwa muda mrefu bila ya Baraza la Wawakilishi (MBW) kama mazingira yaliyopo yanavyoonyesha ni tatizo.

Alisema Katiba ya Zanzibar imeruhusu hali ya kuendesha nchi bila ya BLW kwa muda usiozidi siku tisini (90) tu kuanzia siku Baraza lilipovunjwa.

“Kwa mazingira tuliyonayo, siku tisini (90) zinazokubalika kikatiba zinaishia Novemba 12, 2015 kwa kuwa BLW lilivunjwa Agosti 13, 2015,” alisema.

Rais huyo wa TLS alionyesha pia hatari ya kuwa na rais ambaye yuko juu ya Sheria na Katiba, akibainisha Ibara ya 37 ya Katiba ya Zanzibar ya 1984 inayoipa Mamlaka Baraza la Wawakilishi kuondoa kinga ya Rais kutoshtakiwa anapokuwa madarakani kama inavyotolewa na Ibara ya 36 ya Katiba.

Alisema katika mazingira yaliyopo hivi sasa ambapo ifikapo tarehe 12 Novemba, 2015, Baraza la Wawakilishi halitakuwapo na haliwezi kuitishwa kikatiba, ni wazi kuwa ikiwa Rais atafanya matendo yoyote yenye kuvunja katiba ya nchi na kukiuka kiapo chake, hakutakuwa na mamlaka nyingine yoyote yenye uwezo wa kuhoji matendo ya Rais.

Alidai hii inatoa fursa na inatengeneza hatari ya kuwa na Serikali inayoongozwa na ‘dikteta’.


Kauli ya Polisi

Kamishna wa Polisi Zanzibar, Hamdan Omar Makame alisema jana kuwa kutokana na taarifa hizo za wanasiasa na watu wengine, huenda wananchi watakuwa huru kufanya watakavyo na hivyo kuvunja sheria.

“Tunawaomba wananchi kuacha ushabiki na jazba ili kuwaepusha na gharama za matatizo, wao wenyewe na familia zao. Waswahili wanasema ‘vyako ni vyako, likikupata ni la kwako na kila mchumia janga hula na mwanawe’,’’ alisema Kamishna Makame.

Makame alisema ni vyema kipindi hiki kuhubiri amani na kuwa na subira kuiachia ZEC ambayo ndiyo yenye dhamana na mamlaka ya kutangaza tarehe ya kurejewa kwa uchaguzi na si mtu mwingine.

Kamishna Makame alinukuu kifungu cha 28 (1) cha Katiba ambacho pia wanasheria wa ZLS walikitoa na kumwomba Rais wa Zanzibar kuchukua tahadhari ili asiwe wa kwanza kuvunja Katiba ya Zanzibar kwa kuvuka terehe ya mwisho kuwapo madarakani.

Kifungu cha 28 (1) cha Katiba kinasema, “Kufuatana na Katiba hii mtu ataendelea kuwa Rais mpaka (a) Rais anayefuata ale kiapo cha kuwa Rais, au (b)afariki wakati akiwa Rais, au (c) hapo atakapojiuzulu; au (d) iwapo amechaguliwa kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ; au (e) kwa sababu yoyote nyingine ameacha kuwa kiongozi kwa mujibu wa vifungu vingine vya katiba hii.

“Ikumbukwe kuwa kutokuwapo Rais wa nchi kama inavyodaiwa, haimaanishi sheria hazipo na watu wafanye watakavyo. Kuna makosa ukiyafanya moja kwa moja sheria itachukua mkondo wake ikiwamo kufanya kitendo cha uvunjifu wa amani, kufanya maandamano au mikusanyiko ya watu isiyo halali,” alisema kamishna huyo.

 Lipumba: Ni jukumu la JK

Sakata hilo la Zanzibar kwa mara ya pili lilimwibua mwenyekiti wa zamani wa Chama cha Wananchi (CUF), Profesa Ibrahim Lipumba akimtaka Rais Jakaya Kikwete kumaliza tatizo la Zanzibar kwa kuiamuru ZEC kumtangaza mshindi wa uchaguzi mkuu wa Oktoba 25 ili kuliepusha Taifa lisiingie kwenye machafuko.

Akizungumza na waandishi wa habari jana, Lipumba alisema ni muhimu Kikwete akahakikisha anatekeleza hilo kabla ya kumaliza muda wake, badala ya kumwongezea matatizo na mzigo rais mpya, Dk John Magufuli anayetarajiwa kuapishwa Novemba 5.

“Alhamisi ijayo Dk John Magufuli ataapishwa kuwa Rais na Amiri Jeshi Mkuu wa Vikosi vya Ulinzi na Usalama vya Tanzania, Kikwete usimwongezee Magufuli matatizo, yaliyopo yanamtosha,” alisema Lipumba ambaye wiki iliyopita akizungumzia pia mgogoro huo akiitaka ZEC imtangaze mshindi.

Lipumba aliyepokewa na wafuasi zaidi ya 100 kwenye ofisi za makao makuu ya chama hicho, Buguruni , Dar es Salaam, alisema amelazimika kutoa ushauri huo baada ya kuona hatari iliyo mbele, iwapo wananchi wa Zanzibar watanyang’anywa haki yao.

“Vigogo wa Tanzania na Zanzibar wasisubiri hadi maafa yatokee ndipo waanze kuchukua hatua, watumie muda huu kuyazuia,” alisema na kuonya:

“Nayakumbuka mauaji ya wafuasi wa CUF yaliyotokea mwaka 2001 na wengine kukimbilia uhamishoni Shimoni nchini Kenya, nimeona kukaa kimya kutaleta madhara katika nchi hii,” alisema.

Mmoja wa wanachama wa chama hicho, tawi la Buguruni, Ashura Mohammed alisema ni muhimu Wazanzibari wapewe haki yao kwa matokeo ya uchaguzi walioufanya kutangazwa.

 ADC : Jecha, ZEC wamekosa sifa

Wakati huohuo, Mwenyekiti wa chama cha ADC, Said Miraaj Abdulla amesema ZEC chini ya Jecha Salim Jecha haiwezi kusimamia tena uchaguzi wa Zanzibar baada ya siku 90 kwa sababu ina mapungufu mengi kama ilivyoyaainisha yenyewe.

Abdulla alisema sababu zilizotolewa na Jecha kufuta matokeo hazina mashiko, zimelenga kuficha ukweli na kutetea maslahi ya upande mmoja. Alisema chama chake kitasimamia haki na ukweli kuhakikisha kwamba matakwa ya wananchi yanasikilizwa.

“Kwanini Jecha aje leo kutueleza kuwa tume yake iliingiliwa na wanasiasa? Siku zote alikuwa wapi na alichukua hatua gani katika kuhakikisha tume yake inakuwa huru,” alihoji mwenyekiti huyo na kusisitiza kuwa kuna ajenda inafichwa na Jecha.

Mwenyekiti huyo aliendelea kusema, Jecha alisisitiza katika matamshi kwamba wajumbe wa ZEC walikuwa wamegawanyika kwa misingi ya vyama vyao lakini hakueleza ni kwa namna gani mgogoro wa wajumbe hao umeathiri kura zilizopigwa.

Aliwataka viongozi kuwa makini na matamshi yao ili yasije kusababisha migogoro na kuvunja amani ya nchi na vyama vyote kuwa na sauti moja ili viweze kutetea haki za wananchi wa Zanzibar ambao wamechagua viongozi wao kwa misingi ya kidemokrasia.

“Viongozi wa CUF na CCM waache kuangalia maslahi ya vyama vyao bali waangalie maslahi mapana ya umma. Chama changu kiko tayari kushirikiana na chama chochote katika kuhakikisha kwamba suluhu ya mgogoro huo inapatikana,” alisema.

Imeandikwa na Salma Said, Raymond Kaminyoge na Peter Elias

Mkanda wa Ngono wa DJ Anayeheshimika zaidi Kenya, Crème De La Crème Wavuja Mtandaoni,

$
0
0
DJ Crème De La Crème, DJ anayeshimika zaidi nchini Kenya amekutana na skendo kubwa kuwahi kutokea kwenye maisha yake baada ya mkanda wa ngono akiwa na mwanamke mwingine zaidi ya mke wake kusambaa mtandaoni.

Pamoja na kuwa DJ anayeheshimika, Creme amekuwa mfano bora wa jinsi anavyoishi na mke wake pamoja na familia na hivyo mkanda huu umewashangaza wengi.



Mkanda huo wenye dakika tano, uliovunja mtandaoni kupitia tovuti ya ‘Indulge Kenya’, unamuonesha DJ huyo huyo akila uroda na msichana ambaye hajulikani.

Msichana kwenye video hiyo anaonekana kama alivyozaliwa.

Wengi wanahisi mkanda huo utasababisha mpasuko mkubwa kwenye uhusiano wake na mkewe Denise. Hata hivyo habari hiyo inaweza kuwa na faida kwake kutokana na kupata attention kubwa duniani ikiwa ni pamoja na mtandao wa Uingereza, Daily Mirror kuandika.

Creme ana watoto wawili, Jamari na Zawadi. Bado DJ huyo hajatoa maelezo yoyote.

Hivi karibuni DJ huyo ataachia collabo yake aliowashirikisha AY, Prezzo, Big Pin, Ulopa Ngoma, Nameless na wasanii wengine.

Bonyeza Hapa Kuangalia Huo Mkanda >>>VIDEO

Collabo ya Wizkid na Diamond Haiepukiki

$
0
0
Diamond Platnumz amefanya collabo na kila msanii mkubwa wa Nigeria.

Ameshafanya ngoma au kushiriki kwenye ngoma na P-Square, Davido, D’Banj, Tiwa Savage, Iyanya, Waje, Kcee, Bracket, Flavour na wengine lakini ni msanii mmoja tu mkubwa hajakutana naye kwenye wimbo wowote – Wizkid.

Wawili hao walikutana mwishoni mwa wiki iliyopita kwenye show ya Leaders Club jijini Dar es Salaam, na picha zinaonesha kuwa tayari zimeiva, licha ya ukweli kuwa huenda wamewahi kuwasiliana kabla ya hapo.

Baada tu ya show yao ya Leaders wawili hao hawakuwa wachoyo kwa mashabiki wao kuwaonesha kuwa mazungumzo ya kazi za baadaye yameanza.

Wikzid alipost picha akiwa na hitmaker huyo wa Nana na kuandika, “Big up to @diamondplatnumz for the love!! We link up soon!! #OneAfrica.”

Naye Diamond alipost picha akiwa na hitmaker huyo wa Ojuelegba na kuandika, “When they ask you, what was the name of the food you ate in Tanzania… tell them “Ubwabwa na Kuku” @wizkidayo.”

Wizkid atarejea tena December kwenye Fiesta na huenda kile mashabiki wamekililia kwa muda mrefu kati ya mastaa hawa kitakamilika.

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Nov. 3 Ikiwemo Vihunzi Nane Kwa Rais John Pombe Magufuli

$
0
0
Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Nov. 3 Ikiwemo Vihunzi Nane Kwa Rais John Pombe Magufuli


Polisi Kanda ya Pwani (Pwani, Dar es Salaam, Morogoro) Yapiga Marufuku Maandamano Novemba 3 Kumpinga Magufuli

$
0
0
Kamanda Kova
POLISI Kanda Maalumu ya Dar es Salaam imepiga marufuku maandamano ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), yaliyopangwa kufanyika bila ukomo kutokana na kile kilichoelezwa kuwa ni kinyume cha sheria.

Kamanda wa Kanda hiyo, Suleiman Kova aliwaambia waandishi wa habari jana ofisini kwake, jijini Dar es Salaam, kwamba maandamano hayo yana viashiria vya uvunjifu wa amani.

Maandamano hayo yaliyotajwa kuwa hayana kikomo, yalipangwa kufanyika katika maeneo yote ya jiji la Dar es Salaam. Kova alisema kama yakiruhusiwa, yatakuwa chanzo cha mfarakano mkubwa nchini, jambo ambalo litaathiri amani na maisha ya Watanzania.

Alisema maandamano hayo ni jambo ambalo haliwezekani, kwani pia yatasababisha msongamano mkubwa kwa wakazi wa jiji hilo na watapata usumbufu kwa kushindwa kufanya shughuli zao kwa ufasaha.

Alisema walipokea barua yenye Kumbukumbu namba CDM/PW/ GEN/042/2015 iliyoandikwa Oktoba 31, lakini iliwasilishwa ofisini kwake jana, ikitoa taarifa ya kufanya maandamano leo.

“Katika barua hiyo, Chadema Kanda ya Pwani walitoa taarifa ya kufanya maandamano ya amani yasiyo na kikomo kuanzia kesho (leo) katika maeneo yote ya jiji la Dar es Salaam kupinga kile walichodai ni uporwaji wa demokrasia dhidi ya mgombea wao wa urais Edward Lowassa ambaye wamedai ndiye mshindi,” alisema Kova.

Alisema baada ya kusoma barua hiyo kwa makini na kutafakari, amebaini kuwa kutokana na Sheria ya Polisi na Polisi Wasaidizi Sura ya 322 Kifungu cha 43 (1) kama ilivyorekebishwa mwaka 2002, taarifa ya maandamano inatakaiwa itolewe saa 48 kabla ya muda wa kuanza maandamano, kitu ambacho kimekiukwa, kwani barua hiyo ilipelekwa ofisini kwake jana.

“Kwa mujibu wa sheria hii, Chadema hawataruhusiwa kufanya maandamano hayo kutokana na kuchelewa kutoa taarifa kwa wakati. Wamemtaja Lowassa kuwa ndiyo mshindi, lakini kwa mujibu wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano ya Mwaka 1977, Tume ya Taifa ya Uchaguzi ndiyo ina mamlaka ya kumtangaza mshindi,” alisema.

Alisema maandamano hayo ni batili na ni kinyume cha Sheria. Alisema kama hawakuridhika na uamuzi huo wa polisi, wanaruhusiwa kukata rufaa kwa Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi chini ya Kifungu Namba 43 (6) ya Sheria za Polisi na Polisi Wasaidizi Sura ya 322.

Hata hivyo, Kova alisema barua hiyo iliyowasilishwa na Chadema imeandikwa huku ikitawaliwa na shari; na pia inaonekana taarifa hiyo lengo lake ni kuvuruga amani.

“Nawaomba viongozi wa Chadema watumie busara, wasitake kuiingiza hii nchi katika matatizo na umwagaji damu, Watanzania sisi ni watu wa amani, hatujazoea haya mambo. Kuna taratibu na sheria wazifuate hizo,” alisema.

Alisema polisi wamejipanga vizuri kuhakikisha nchi inakuwa salama na atakayekaidi agizo hilo, atachukuliwa hatua kali za kisheria. Pia, alitaka vijana wasikubali kutumiwa katika kuvuruga amani

Yericko Nyerere Apandishwa Kizimbani kwa Kutoa Taarifa za Uongo Facebook

$
0
0
Mfanyabiashara Yericko Nyerere amepandishwa kizimbani katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, akikabiliwa na mashitaka matano ya kutoa taarifa za uongo kupitia mtandao wa kijamii wa Facebook.

Nyerere alifikishwa mahakamani hapo jana na kusomewa mashitaka na mawakili wa Serikali, Simon Wankyo na Paul Kadushi mbele ya Hakimu Mfawidhi, Cyprian Mkeha.

Anashitakiwa chini ya Kifungu cha 16 cha Sheria ya Mtandao Namba 14 ya 2015. Nyerere anadaiwa Oktoba 25, mwaka huu katika eneo lisilojulikana, alichapisha taarifa za upotoshaji kupitia mtandao wa Facebook, akidai kuwa “Piga kura leo huku ukikumbuka kifo cha Mwangosi, Mateso ya Ulimboka na Kibanda, mateso ya vijana wetu wa JKT, ukikumbuka hayo fanya uamuzi sahihi bila ushabiki”.

Wanyo alidai kuwa Oktoba 24, mwaka huu jijini Dar es Salaam, Nyerere alichapisha taarifa za upotoshaji kupitia mtandao wa Facebook kuwa Taifa la Tanzania kuanzia leo halihitaji amani, linahitaji haki tu.

Inadaiwa, alichapisha taarifa za uongo kupitia mtandao huo kuwa, “siku ya leo mpaka siku ya kuapishwa Lowassa, taifa halihitaji amani, bali taifa hili linahitaji haki tu, amani ilishatoweka siku nyingi, kilichobaki ni uvumilivu tu…, njia sahihi ya kulitibu taifa hili ni kwa dola dhalimu kutenda haki hata kama itawauma”.

Inadaiwa Nyerere aliendelea kudai kuwa “Uchaguzi huu ni vita, anayedhani ni demokrasia apimwe akili…hii ni vita kati ya umma na dola, ni vita kati ya wema na ubaya, kati ya shibe na njaa, kati ya masikini na matajiri… umma umekosa amani na furaha, fursa pekee waliyoipata watanzania wanamjua rais wao wanayekwenda kumchagua kesho, jaribio lolote litakalofanywa na CCM na vibaraka wao la kukwamisha matakwa ya umma, litaondoa hata ule uvumilivu kidogo walionao watanzania na kisha vitazaliwa vichaa chongo ambavyo hata risasi na mabomu hayatakizima”.

Aidha, anadaiwa siku hiyo hiyo alichapisha taarifa nyingine ya upotoshaji kupitia mtandao ikisema “mipango ya hujuma ya JK toka Ngurdoto Arusha muda huu…Kikwete yupo Ngurdoto Arusha na wakuu wote wa mikoa na wilaya Tanzania nzima pia wakuu wa vyombo vya dola na wanadhimu mbalimbali… wakuu wa mkoa wanaelezwa kuwa NEC kwa kushirikiana na CCM tayari wameshatengeneza kura bandia kwa kutumia mfumo wa kalamu za kichina… pia wanaamuliwa kuhakikisha wanahujumu kampeni za Ukawa kwa kutumia vyombo vya dola, wanaagizwa kuhakikisha kamatakamata ya vijana bodaboda wiki moja kabla ya uchaguzi na zaidi wanaagizwa wakawaagize maDC kote nchini kuhakikisha wanalinda maslahi ya CCM siku yaUchaguzi."

Katika mashitaka mengine, Nyerere anadaiwa Septemba 3, mwakahuu katika eneo lisilojulikana alichapisha taarifa za uongo kuhusu uwepo wa akaunti ya benki ya kughushi inayomilikiwa na mtanzania katika benki ya HSBC Tawi la North London, ikionesha CCM imemwekea Dk Wilbrod Slaa Euro milioni 1.5 kupitia kwa mchumba wake, Josephine Mshumbusi ikiwa ni rushwa ili kushinda uchaguzi mwaka huu.

Nyerere anadaiwa alichapisha na kusambaza taarifa hizo za uongo kupitia mtandao wa Facebook kwa lengo la kupotosha umma katika Uchaguzi mkuu wa mwaka huu. Mshitakiwa alikana mashitaka na upande wa jamhuri ulidai upelelezi wa kesi hiyo bado haujakamilika, pia hawana pingamizi la dhamana kwa mshitakiwa huyo.

Nyerere aliachiwa kwa dhamana baada ya kutimiza masharti ya kuwa na mdhamini mmoja, aliyesaini hati ya Sh milioni tano. Kesi itatajwa tena Desemba Mosi mwaka huu.

Mafuriko ya maji ya mvua yaua wawili Mwanza ....Uwanja wa Ndege Wafungwa Kwa Muda

$
0
0
MVUA kubwa imenyesha mkoani Mwanza na kusababisha maafa, ikiwemo vifo vya watu wawili na familia kadhaa kukosa makazi kutokana na nyumba kubomoka.

Aidha, mvua hiyo imesababisha kufungwa kwa muda uwanja wa ndege wa Mwanza kutokana na kujaa maji.

Mvua hiyo inasadikiwa ndiyo mwanzo wa El-Nino kutokana na taarifa ya Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) kueleza jana kwamba, kutakuwa na mvua za El-Nino, kama ilivyokuwa imeelezwa katika taarifa yake ya Septemba mwaka huu.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza, Charles Mkumbo katika mkutano wake na waandishi wa habari, alisema mmoja wa waliopoteza maisha, ni mwendesha bodaboda wa Kirumba aliyekuwa amepakiza wanafunzi wawili akiwapeleka shuleni.

Kuhusu wanafunzi hao, Kamanda alisema, taarifa zake hazijathibitishwa kama pia wao wamepoteza maisha, ingawa tukio hilo limo katika orodha ya athari za mvua hizo.
 
Alisema mtu mwingine alionekana akiwa anaelea katika maji eneo la Mabatini, lakini baadaye mwili wake haukuonekana kutokana na mafuriko hayo.

“Tumepokea taarifa juu ya mvua hizi kutoka maeneo mbalimbali ya jiji la Mwanza na tunaendelea kukusanya taarifa na kuchukua hatua stahiki,” alisema Kamanda Mkumbo.

Kuhusu uwanja wa ndege, mvua hizo zilisababisha kufungwa kwa saa tano kwa uwanja wa ndege wa Mwanza baada ya kujaa maji. Meneja wa uwanja wa Ndege wa Mwanza, Esther Madale alimwambia mwandishi wa habari  kwamba uwanja huo ulilazimika kufungwa kwa saa tano kwa ajili ya kuwezesha wahandisi, kufanya uchunguzi wa miundombinu yake.

Hakuna ndege iliyoruhusiwa kutua katika muda huo. “Ni kweli tulikumbwa na mkasa huo wa mvua ambazo zilinyesha mfululizo na kusababisha kufungwa kwa uwanja kwa muda…kwa sasa tunavyoongea tayari huduma zimerejea katika hali yake ya kawaida,” alisema Madale.

Uwanja huo wa ndege upo katika matengenezo makubwa, ikiwamo mnara wa kuongozea ndege, njia za kurukia ndege ambazo sasa ni meta 2000 na zinaongezwa hadi kufikia meta 3300. Ukarabati huo ulianza mwaka 2012 na ulitarajiwa kumalizika Oktoba mwaka huu.

El-Nino imeanza
Katika taarifa ya TMA kwa vyombo vya habari jana, ilisema kuendelea kuongezeka kwa joto katika maeneo ya Bahari ya Pasifiki kunaonesha kuimarika kwa mvua za El-Nino kama ilivyoelezwa katika taarifa iliyotolewa Septemba, mwaka huu.

Taarifa hiyo iliyosainiwa na Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa TMA, imesema mvua zimeshaanza kunyesha katika maeneo mbalimbali nchini hususani Ukanda wa Ziwa Viktoria, Kanda ya Magharibi na Nyanda za Juu, Kaskazini Mashariki na zinataraji kuwa za juu ya wastani.

“Hata hivyo, mifumo mingine ya hali ya hewa ikiwemo mwitikio wa mfumo ya hali ya hewa katika Bahari ya Hindi imekuwa na mchango hasi kinyume na ilivyotarajiwa katika mwenendo wa mvua za Vuli nchini katika kipindi cha mwezi Oktoba, 2015 na kusababisha vipindi virefu vya upungufu wa mvua katika mikoa ya Morogoro, Pwani na Dar es Salaam,” ilisema sehemu ya taarifa hiyo.

Aidha taarifa hiyo ya Dk Chang’a ilisema maeneo yanayopata mvua mara moja kwa mwaka mikoa ya Dodoma, Singinda, Ruvuma, Lindi, Mtwara, Songea, Mbeya, Iringa, Njombe, Tabora, Kigoma Rukwa na Katavi mvua zinatarajiwa kuanza kati ya wiki ya pili na ya nne ya Novemba, 2015.

Alisema mvua hizo zimeanza kujiimarisha katika mikoa ya Kigoma, Tabora na Katavi na zinatarajiwa kusambaa katika maeneo mengine mwezi huu. Hata hivyo, wilaya za Kondoa, Kongwa na Singida Vijijini katika mikoa ya Dodoma na Singida, zinatarajiwa pia kupata vipindi vya mvua mwanzoni mwa mwezi huu.

Mamlaka hiyo imeshauri wananchi, hususani wafugaji, Mamlaka za Wanyamapori, Mamlaka za Maji na Afya waendelee kutafuta, kupata na kufuata ushauri wa wataalamu katika sekta husika katika kutekeleza mipango inayoweza kuathiriwa na mwelekeo wa hali ya hewa iliyotabiriwa. Aidha mamlaka imetaka wananchi na wadau kwa ujumla kuzingatia hadhari mbalimbali zilizokwisha kutolewa.

Taarifa hiyo imesema mwelekeo wa mvua uliotolewa umezingatia zaidi viashiria vya mvua katika kipindi cha msimu (miezi mitatu) na hali ya mvua katika maeneo makubwa.

Hivyo, viashiria vinavyochangia mwenendo wa mifumo ya mvua na mabadiliko ya muda mfupi katika maeneo madogo utazingatiwa katika uchambuzi wa utabiri wa muda wa kati na mfupi.

TMA imeahidi kuendelea kufuatilia mwenendo wa mifumo ya hali ya hewa na kutoa taarifa za mwelekeo wa mvua nchini.

Mbwana Samatta katangazwa kuingia katika Top 10 ya wanaowania Tuzo ya mchezaji bora Afrika 2015, hii ni list kamili

$
0
0

Shirikisho la mpira wa miguu barani Afrika CAF huwa linautamaduni wa kutoa Tuzo ya mchezaji bora wa Afrika kila mwaka, kama ambavyo Shirirkisho la mpira wa miguu barani Ulaya UEFA wanavyokuwa wanaandaa Tuzo ya mchezaji bora Ulaya, basi Afrika huwa wanaandaa Tuzo hizo kwa wachezaji wanaocheza ndani ya Afrika na nje ya Afrika

November 2 wametangaza Top 10 ya majina yaliofanikiwa kuingia katika Top 10 hiyo kwa wachezaji wa ndani na nje ya Afrika. Good news ni kuwa mtanzania Mbwana Samatta ambaye anakipiga katika klabu ya TP Mazembe ndio mchezaji pekee kutoka Afrika Mashariki aliyekuwemo katika list hiyo, Hii ni List ya majina 20 ya wachezaji waliochaguliwa kuingia katika Top 10 ya wachezaji wanaocheza ndani ya Afrika na Top 10 ya wachezaji wanaocheza nje ya Afrika.


Hii ni Top 10 ya wachezaji wanaowania tuzo ya mchezaji bora Afrika kwa wanaocheza ndani ya Afrika

Abdeladim Khadrouf (Morocco & Moghreb Tetouan)
Baghdad Bounedjah ( Algeria & Etoile du Sahel)
Felipe Ovono (Equatorial Guinea & Orlando Pirates)
Kermit Erasmus (South Africa & Orlando Pirates)
Mbwana Aly Samatta (Tanzania & TP Mazembe)
Mohamed Meftah ( Algeria & USM Alger)
Mudather Eltaib Ibrahim ‘Karika’ (Sudan & El Hilal)
Robert Kidiaba Muteba ( DR Congo & TP Mazembe)
Roger Assalé (Cote d’Ivoire & TP Mazembe)
Zineddine Ferhat (Algeria & USM Alger)

Top 10 ya wachezaji wanaocheza nje ya Afrika

André Ayew (Ghana & Swansea)
Aymen Abdennour (Tunisia & Valencia)
Mudather Eltaib Ibrahim ‘Karika’ (Sudan & El Hilal)
Mohamed Salah (Egypt & Roma)
Pierre-Emerick Aubameyang (Gabon & Borussia Dortmund)
Sadio Mané (Senegal & Southampton)
Serge Aurier (Cote d’Ivoire & Paris Saint Germain)
Sofiane Feghouli (Algeria & Valencia)
Yacine Brahimi ( Algeria & Porto)
Yaya Touré (Cote d’Ivoire & Manchester City)

Namna ya kumpata mshindi wa tuzo hiyo ni kwa njia ya kupiga kura kwa makocha wa timu za taifa au wakurugenzi wa ufundi wa mashirikisho wanachama wa CAF. Tuzo hizo za mchezaji bora wa Afrika kwa 2015 zitatolewa Alhamisi ya January 7 2016 Abuja Nigeria.

Legal Battle Now Looms Over Uchumi Super Makert Closure

$
0
0

 About 460 workers of Uchumi Supermarket are collecting their particulars to support them in claiming their legal and contractual rights.

The move comes after Uchumi management through its contracted Mawalla Advocate law chamber reported that the company was set for liquidation so that all obligations are settled.

Tanzania Union of Industrial and Commercial Workers (Tuico) Kinondoni District secretary, Mansoor Ramadhan told The Citizen that workers will each need to fill a form detailing his or her names, employment history, place of work, leaves that are for payment and other important information.

We had a meeting this morning with advocates from Mawalla law firm where we discussed the fate of the employees after the employer announced to end operations in Tanzania,” he said.

In its letter to Dar es Salaam Stock Exchange (DSE), Uchumi company secretary John Wambugu said the board was cognizant of the responsibilities in respect of the obligations of two subsidiaries to various stakeholders.

Uchumi is pursuing various avenues of raising funds to meet these obligations as well as to finance its activities over the coming Christmas and New Year period which is typically a busy one for the retail sector,” he said is a statement published on DSE website.

He said the company was already in the process of engaging all stakeholders including suppliers, employees, financiers and regulators in the jurisdiction in which it operates.

Mr Ramadhan met with Uchumi staff to give them the updates with regard to the fate of their employment. Some workers seemed to be over ambitious about their benefits during the meeting.

But they were cautioned that some particulars for submission will only hold water if attached with evidences like leaves that were not granted when sought.

“It is unfortunate that most of us do not keep records when at work which makes you risk losing your rights,” he said.

They also wanted to know which specific benefits are they entitled to given the employers’ decision to end the contract. He told them that benefits might differ due to a number of factors like a number of years they been at work.

Asked about the October salary as it was agreed, Mr madhan said the employer did not pay as it was agreed but promised to pay this week. “I have written a letter to the management and copied to the law firm, asking how the company will handle employees’ benefits,” he said.

and more importantly pay the October salary as it was agreed when we met last month,” he said.

According to him, Tuico is currently collecting evidences that will support employees when the issue is forced to go to Commission for Mediation and Arbitration (CMA) in case the Uchumi is not compliant.

Mr Ramadhan said the meeting also leant that there were some staff who were assisted by Uchumi to secure loans from some banks like Equity and Kenya Commercial Bank (KCB) and they were still paying.

We will also see how to handle this issue in the process of resolving the matter. I have leant that Uchumi will also involve the bank. That is why I tell you to be patient,” he said.





CCM Yafuta Ushindi wa Mtoto wa Dk Abdallah Kigoda

$
0
0
Kamati Kuu ya CCM imefuta matokeo ya kura za maoni katika Jimbo la Handeni, mkoani Tanga ambako Omar Abdallah Kigoda ambaye ni mtoto wa mbunge wa zamani, marehemu Abdallah Kigoda alikuwa ameshinda.

Akizungumza jana, Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Nape Nnauye alisema jana kuwa kutokana na kufutwa kwa matokeo hayo, uchaguzi wa kura maoni katika jimbo hilo unarudiwa leo.

Alifafanua kuwa wagombea 11 waliwania nafasi hiyo lakini wawili kati yao, Kigoda na Hamis Amad Mnondwa walipata kura zaidi kuwashinda wenzao.

Mkutano mkuu wa jimbo la Handeni, ulimchangua Omari Kigoda kwa kura 296 akiwashinda wenzake wawili Hamisi Mnondwa na Athumani Lukoya waliokuwa wamechujwa kutoka miongoni mwa wanachama 11 walioomba nafasi hiyo.

“Lakini matokeo yanaonyesha hakuna mshindi aliyepata kura za kuridhisha kuingia katika ushindani na vyama vingine, ndiyo maana Kamati Kuu imeamua urudiwe,” alisema bila kutaja idadi ya kura walizopata wagombea hao.

Mchakato huo wa kupata mgombea unafanyika kutokana na kifo cha aliyekuwa mgombea ubunge wa jimbo hilo, Dk Abdallah Kigoda kilichotokea Oktoba 12, mwaka huu nchini India.

Nape alisema marudio hayo ya kura za maoni yatasimamiwa na makada watatu wa CCM, Dk Maua Daftari, Dk Emmanuel Nchimbi na Abdallah Bulembo.

Nape alisema Kamati Kuu inaendelea na kikao chake cha siku moja ambacho kina ajenda ambazo hakutaka kuzitaja. Kamati Kuu imefanya uamuzi huo huku kukiwa na sintofahamu juu ya chama hicho kuanza ‘utaratibu mpya’ wa kuwateua watoto wa vigogo wa chama hicho wanaofariki dunia wakiwa wabunge au wagombea, kuwania nafasi iliyoachwa na wazazi wao.

Mbali na Omary, Goodluck Mtinga, mtoto wa aliyekuwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Utumishi) Celina Kombani naye amepitishwa na chama hicho kugombea ubunge katika jimbo la Ulanga.

Utaratibu kama huo ulitumika katika Jimbo la Kalenga mwaka 2014, CCM ilipomsimamisha Godfrey Mgimwa, mtoto wa marehemu Dk William Mgimwa, kugombea ubunge katika jimbo hilo lililokuwa likishikiliwa na baba yake.

Mwaka 2012, CCM pia ilimteua Sioyi Sumari kugombea ubunge katika Jimbo la Arumeru Mashariki kuziba nafasi iliyoachwa na baba yake, marehemu Jeremiah Sumari.

CCM Watuhumiana kwa Unafiki Kila Kona Kwa Kushindwa Ubunge na Udiwani Baadhi ya Majimbo

$
0
0
Baada ya upepo wa Uchaguzi Mkuu kuanza kutulia, baadhi ya makada wa CCM wameanza kutuhumiana kuwa unafiki na hujuma zilizofanywa na baadhi ya wanancha wa chama hicho zimesababisha kishindwe kufanya vizuri katika baadhi ya maeneo kwa ngazi za udiwani na ubunge.

Baadhi ya makada hao kwa nyakati tofauti wamekuwa wakieleza kuwa CCM ina ‘wanafiki’ wengi ambao wanaangalia zaidi masilahi yao kuliko chama.

Hata Rais mteule, Dk John Magufuli amekuwa akizungumzia suala hilo tangu kipindi cha kampeni, akilalamika kuwa kuna watu waliokuwa naye mchana lakini usiku wanahamia Ukawa.

Dk Magufuli alipigilia msumari suala hilo alipozungumza na wafuasi waliojitokeza kumpokea katika ofisi ndogo za CCM, Lumumba baada ya kupatiwa cheti cha ushindi wa urais na Tume ya Uchaguzi ya Taifa (NEC), akisema kuna haja ya kukijenga upya chama hicho kwa kuwaondoa wanafiki wote.

Dk Magufuli alimweleza mwenyekiti wa chama hicho, Rais Jakaya Kikwete huku akimuomba radhi kwa maneno aliyoyazungumza kuwa akiona mnafiki amfukuze mara moja kwa kuwa hakuna sababu ya kuwa na makada wengi ambao ni wanafiki, ni bora kubaki na wachache waaminifu.

Nisiposema nitakuwa mnafiki, msema kweli ni mpenzi wa Mungu. Watubu wajirekebishe. Ni heri mara kumi kuwa na mpinzani kutoka nje kuliko ndani ya chama. Mipango yenu mtaipanga mchana usiku wataitoa nje, ni afadhali uwe na mchawi atakuroga ufe kuliko mtu mnafiki,” alisema Dk Magufuli.

Tuhuma za unafiki zimeendelea kutawala ndani ya chama hicho, aliyekuwa mgombea ubunge wa CCM Jimbo la Moshi Mjini, Davis Mosha juzi alitangaza kuachana na siasa akidai kuwa chama hicho kimejaa wanafiki waliochangia kuanguka kwake.

Mosha, ambaye alisema ataendelea na biashara zake badala ya kufanya siasa, alisema kushindwa kwake kulisababishwa na viongozi wa CCM kuanzia Serikali za Mitaa, kata, wilaya hadi mkoa ambao alidai kuwa waliweka mbele masilahi yao binafsi.

“Viongozi wa CCM Mkoa wa Kilimanjaro ni ndumilakuwili na nia yao si ushindi kwa chama, bali wapo kimasilahi zaidi na hawana nia njema, ndio maana chama kinashindwa,” alisema Mosha alipokuwa akiwashukuru wakazi wa Moshi Mjini baada ya kumalizika kwa uchaguzi.

Mfululizo wa tuhuma za hujuma umeendelea katika maeneo mbalimbali nchini, huku baadhi ya wanachama wa chama hicho katika Jimbo la Iringa Mjini, wakimtuhumu Mwenyekiti wa chama hicho mkoani Iringa, Jesca Msambatavangu na viongozi wengine kwa kukihujumu chama hicho.

Wanachama hao, walishinikiza Msambatavangu, Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana Iringa Mjini (UVCCM), Kaunda Mwaipyana na Mwenyekiti wa UVCCM Kata ya Mkwawa, Salum Keita waachie ngazi au wachukuliwe hatua na chama kwa kusababisha kupoteza jimbo na kata 14.

Hata hivyo, Msambatavangu alikana tuhuma hizo na kuanisha kuwa kuna mambo mengi yaliyofanyika kinyume na utaratibu na kusababisha jimbo hilo kupotea kwa mara nyingine na kata 14.

Hali hiyo imejitokeza pia wilayani Kilombero ambako baadhi ya wanachama wa CCM wamewataka viongozi wao wa wilaya kung’atuka ndani ya siku 21 kuanzia jana, wakiwatuhumu kusababisha kupoteza majimbo mawili ya Mlimba na Kilombero ambayo yamechukuliwa na Chadema.

Wanachama hao 16 walioongozwa na Dismas Lyassa, walisema dalili za kuanguka kwa chama hicho zilianza kuonekana mapema wakati wa uchaguzi wa Serikali za Mitaa Desemba, mwaka jana, lakini hakuna hatua za dhati zilizochukuliwa.

Jambo hilo limezidi kuwakera wengi kiasi cha kuwafanya wanachama wasiopungua 400 wa UVCCM Jimbo la Babati Mjini mkoani Manyara, kufanya maandamano juzi hadi ofisi ya CCM mkoa wakiwatuhumu baadhi ya viongozi wa wilaya kuhujumu uchaguzi na kusababisha jimbo hilo kuchukuliwa na Chadema.

Vijana hao wakiwa na mabango yaliyokuwa na maandishi yaliyokuwa yakiwatuhumu viongozi wanane wa juu wa chama hicho, waliandamana na kupokelewa na Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Manyara, Lucas Ole Mukus.

Miongoni mwa waandamanaji hao, Steven Kairo alisema madai hayo yakithibitishwa, watuhumiwa wote wafukuzwe uanachama.

Alisema kama viongozi hawatayafanyia kazi madai yao, wao watakuwa wa kwanza kurudisha kadi.

Tumehangaika kuusaka ushindi wa CCM Babati Mjini, lakini ndumilakuwili wakatuangusha, tunaomba mbariki ombi letu la kuwawajibisha viongozi hao, watupishe, hata sisi tunaweza kuongoza,” alisema Kairo.

Kuepusha Balaa, ZEC itangaze Matokeo ya Uchaguzi Zanzibar

$
0
0
By Ibrahim Haruna Lipumba
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ikiwamo Zanzibar ilifanya Uchaguzi Mkuu Oktoba 25, 2015. Kwa upande wa Visiwani, Wazanzibari walipiga kura kumchagua diwani, mwakilishi, Rais wa Zanzibar, mbunge wa Jamhuri ya Muungano na Rais wa Jamhuri ya Muungano kwa kutumia Daftari la Wapigakura la ZEC.

Tume ya Uchaguzi ya Taifa (NEC) imetumia matokeo ya kura za Rais katika majimbo ya Zanzibar kujumlisha na matokeo ya majimbo ya Bara na hatimaye kumtangaza Dk John Magufuli kuwa mshindi wa kiti cha Rais katika Uchaguzi Mkuu wa Jamhuri ya Muungano. Kwa uamuzi huo wa kuchukua matokeo ya majimbo ya Zanzibar yaliyotumia Daftari la Wapigakura la ZEC na kupiga kura kwenye vituo vilivyoandaliwa na ZEC, Tume ya Uchaguzi ya Taifa inatambua kuwa uchaguzi uliofanyika Zanzibar chini ya usimamizi wa ZEC ni halali na matokeo yake ni halali.

Oktoba 28, siku tatu baada ya uchaguzi, Mwenyekiti wa ZEC, Jecha Salim Jecha alitangaza kuwa uchaguzi wa Zanzibar umefutwa. Alipokuwa anatangaza alikuwa peke yake. Makamu Mwenyekiti hakuwepo. Mkurugenzi wa ZEC hakuwepo. Wajumbe wengine wa Tume hawakuwepo. Wajumbe wa ZEC walikuwa Bwawani wakimsubiri Mwenyekiti wao. Walijaribu kuendelea na kazi ya kuhakiki matokeo chini ya uongozi wa Makamu Mwenyekiti. Hawakuweza kuendelea na kazi hiyo baada ya Makamu Mwenyekiti kuondolewa na vyombo vya dola.

Sababu ambazo Mwenyekiti ametoa za kufuta uchaguzi ni pamoja na eti makamishna wa uchaguzi katika Tume hiyo walidundana kutokana na tofauti zao. Makamishna walikuwa wanapendelea vyama vyao. Katika vituo vingine, hasa Pemba, kura zilizopigwa zilikuwa zaidi ya zilizosajiliwa. Masanduku ya kupigia kura hayakupewa ulinzi wa kutosha na mawakala pamoja na maofisa wa uchaguzi. Mawakala wa vyama walifukuzwa katika vituo kadhaa. Vijana walivamia vituo vya kupigia kura wakiwa na lengo la kuzua ghasia na kadhalika.

Sababu za Mwenyekiti hazina mashiko. Malalamiko haya yalipaswa kutolewa na mawakala wa vyama mapema. Vituo vya kupigia kura vilikuwa na ulinzi wa kutosha wa vyombo vya dola. Watazamaji wa ndani na nje walisifia namna upigaji wa kura Zanzibar ulivyokuwa wa amani na utulivu.

Jecha alieleza kwamba, “Kwa kuzingatia hayo na mengine mengi ambayo sijayaeleza, Mimi Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar, nimeridhika kwamba uchaguzi huu haukuwa wa haki na kuna ukiukwaji mkubwa wa sheria na taratibu za uchaguzi. Hivyo kwa uwezo nilionao natangaza rasmi uchaguzi huu na matokeo yake yote yamefutwa na kwamba kuna haja ya kurudia uchaguzi huu.” Mwenyekiti Jecha hakuvitaja vifungu vya Katiba na sheria vinavyompa mamlaka ya kufuta uchaguzi.

Sura ya tisa ya Katiba ya Zanzibar inaelezea pamoja na mambo mengine uundwaji, mamlaka na taratibu za uamuzi wa Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar. Hakuna kifungu chochote cha Katiba kinachoipa tume au mwenyekiti wake maamlaka ya kufuta uchaguzi. Katiba inaeleza bayana kuwa uamuzi wa masuala yote unafanywa na tume kwa pamoja. Kifungu cha 119(10) kinaeleza kuwa “Kiwango cha mikutano ya Tume ya Uchaguzi ni Mwenyekiti au Makamu Mwenyekiti na wajumbe wanne na kila uamuzi wa tume ni lazima uungwe mkono na wajumbe walio wengi.” Mwenyekiti Jecha hakueleza kikao gani cha Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar kilichokaa na kufikia uamuzi aliotangaza. Ukweli ni kwamba Jecha amevunja Katiba ya Zanzibar kwa kutoa uamuzi mzito bila kufuata taratibu zilizowekwa na Katiba ya Zanzibar. Uamuzi wake ni batili na hauna nguvu ya kisheria. Katiba na sheria ya Zanzibar hazijampa mamlaka mwenyekiti na hata tume yote kufuta uchaguzi. Kufanya hivyo ni kuvunja Katiba ya Zanzibar.

Inaelekea mwenyekiti amepewa shinikizo na ndiyo maana hakuwashirikisha wajumbe wengine wa ZEC. Bila shaka waliomshinikiza Mwenyekiti wa ZEC kuvunja Katiba watawashinikiza wajumbe wengine wa ZEC kuunga mkono uvunjaji wa Katiba uliofanywa na mwenyekiti wao.

Athari za kufuta uchaguzi ni kuleta vurugu za kisiasa na maafa Zanzibar na Tanzania kwa ujumla. Kwa kuwa matokeo ya kura za Zanzibar kwa uchaguzi wa Rais wa Jamhuri ya Muungano hayaathiri ushindi wa mgombea wa CCM, matokeo hayo yamekubaliwa. Matokeo ya kura za uchaguzi wa Rais wa Zanzibar uliofanyika katika mazingira yaleyale na kutumia Daftari la Wapigakura la ZEC yanakataliwa kwa sababu mgombea wa CCM ameshindwa. Mwenyekiti wa ZEC ameshinikizwa kufuta uchaguzi wote wa Zanzibar.

Ni wazi wananchi wengi wa Zanzibar hawawezi kukubali kurudia uchaguzi kwa sababu wenye vyombo vya dola wameamua lazima CCM ishinde ndiyo matokeo ya uchaguzi yakubaliwe. CCM inawaeleza Wazanzibari mabadiliko ya Serikali hayawezi kuletwa na vikaratasi vya kura. Mapinduzi daima maana yake lazima CCM itawale Wazanzibari wakitaka au wasitake. CCM inawaeleza Wazanzibari na Watanzania kwa ujumla kama wanataka mabadiliko aslani hawatayapata kupitia visanduku vya kura. Watafute njia nyingine. Hili ni jambo la hatari.

Nilidhani CCM imejifunza tangu matukio ya 2001 baada ya uchaguzi wa 2000, uchaguzi wa majimbo 16 ulifutwa na kurudiwa.

CUF ilipotoa taarifa ya kufanya maandamano ya amani nchi nzima kudai tume huru ya uchaguzi, Katiba Mpya yenye misingi ya demokrasia, utawala bora na kurudiwa kwa uchaguzi wote wa Zanzibar kama ilivyopendekezwa na watazamaji wa uchaguzi wa ndani na wa nje, mimi binafsi nilikamatwa nikapigwa na kuvunjwa mkono na kutupwa jela. Dhahama hiyo iliwakuta wanachama na viongozi wengine wa CUF. Wananchi wa Zanzibar walipojaribu kuandamana Januari 27, zaidi ya watu 60 waliuawa na kwa mara ya kwanza Watanzania zaidi ya 2000 walikimbia nchi yao kwenda Kenya kunusuru maisha yao. Watanzania tusikubali wanaoishinikiza ZEC kuturudisha huko.

Rais mteule wa Jamhuri ya Muungano, Dk John Magufuli ataapishwa Novemba 5, 2015 na ndiye atakayekuwa Amiri Jeshi Mkuu. Rais Jakaya Kikwete hatamtendea haki Rais Magufuli kumwachia mgogoro wa Zanzibar ambao anaweza kuutatua.

Uchaguzi umefanyika Zanzibar na kwa kuzingatia matokeo kwenye vituo vyote vya wapigakura yaliyotiwa saini na wasimamizi wa vituo na mawakala wa vyama, mgombea wa urais wa Zanzibar kwa tiketi ya CUF, Maalim Seif Sharif Hamad ameshinda uchaguzi huo. Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar ikamilishe uhakiki wa matokeo na kumtangaza mshindi.

Tangu mwaka 1995 sera ya CUF ni kuunda serikali ya umoja wa kitaifa Zanzibar. Katiba ya Zanzibar ya 2010 imeingiza serikali ya umoja wa kitaifa kuwa sharti la kikatiba. CCM watakuwa sehemu ya serikali ya umoja wa kitaifa. Nina uhakika kwa uzalendo wa Kizanzibari wa Maalim Seif, ataunda Serikali ya Umoja wa Kitaifa itakayowaunganisha Wazanzibari.

Propaganda kubwa dhidi ya CUF ni kwamba ikipewa fursa ya kuongoza Zanzibar, itavunja Muungano. Msimamo rasmi wa CUF ni mfumo wa muungano wa shirikisho lenye serikali tatu ya Zanzibar, Tanganyika na Muungano kama uliopendekezwa na Tume ya Jaji Warioba. Huu ndiyo msimamo wa CUF tangu mwaka 1995 wakati wa uchaguzi mkuu wa kwanza wa vyama vingi. Msimamo huu ulifanana na mapendekezo ya Tume ya Jaji Nyalali. CUF inaheshimu sheria mama ya Jamhuri ya Muungano ambayo ni Makubaliano ya Muungano.

Tume ya Jaji Warioba ilitoa uhuru kwa Watanzania kutoa maoni kuhusu Katiba wanayoitaka. Mjadala huu ulitoa mapendekezo mengi likiwamo la Muungano wa mkataba. Baada ya kuchambua mapendekezo yote, Tume ya Jaji Warioba iliandaa Rasimu ya Katiba yenye mfumo wa Muungano wa serikali tatu. Chama cha CUF na Katibu Mkuu wake waliunga mkono mapendekezo ya Tume ya Jaji Warioba na ndiyo sababu ya kuanzisha Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa) katika Bunge Maalumu la Katiba. Wazanzibari wengi wanaoishi Tanzania Bara wanaunga mkono CUF, lakini pia wanaelewa umuhimu na faida za Muungano. CUF haitavunja muungano bali itauimarisha kwa kutumia njia za demokrasia na sheria kutatua kero za Muungano.

Kufuta uchaguzi wa Zanzibar ni kuwanyima Wazanzibari haki ya kuchagua viongozi wanaowataka. Nikuwaeleza hawawezi kupata mabadiliko kupitia visanduku vya kura. Watafute njia nyingine. Wanaowanyima Wazanzibari haki ya kuchagua viongozi wao kwa utaratibu wa kupiga kura ndiyo wanaoandaa mazingira ya kuvunja Muungano. Rais Kikwete na Rais Ali Mohammed Shein malizeni tatizo msiliingize taifa kwenye balaa na kumuachia Rais mteule mgogoro utakaomzuiwa kusimamia ajenda ya maendeleo ya nchi yetu.

Mwandishi wa makala haya, Profesa Ibrahim Lipumba alikuwa Mwenyekiti wa CUF

     

Mhubiri Maarufu Duniani TB Joshua Atua Tanzania, Apokelewa na Rais Kikwete Ikulu ...

$
0
0
Mhubiri maarufu duniani TB Joshua wa kanisa la Church of All Nations nchini Nigeria ametua jijini Dar es salaam leo tayari kwa kushuhudia kuapishwa kwa Rais wa Awamu ya Tano Dkt. John Pombe Magufuli siku ya Alhamisi.

Mara tu baada ya kutua uwanja wa Ndeghe wa Kimataifa wa Julius Nyerere, TB Joshua alikwenda Ikulu moja kwa moja kumsalimia Rais Jakaya Mrisho Kikwete kumsabahi na kumpongeza kwa kufanikisha uchaguzi mkuu kwa uhuru na amani, huku akiondoka madarakani akiwa mtu mwenye furaha. TB Joshua amepongeza Rais Kikwete pia kwa kupata Dkt Magufuli kama mrithi wake, akimtaja Rais huyo mpya mteule kama Rais wa Tanzania wa Baraka na Fanaka tele katika awamu hii mpya.

WEMA SEPETU: Nasib Abdul Angekuwa Mume Wangu wa Maisha!

$
0
0
Nasib Abdul ni jina halisi la Diamond Platnumz. 
Miss Tanzania huyo wa mwaka 2006 na muigizaji wa filamu alikuwa akijibu swali kwenye kipindi cha Hitzone kupitia kituo cha redio cha Jembe FM cha jijini Mwanza alipoulizwa ni mwanaume gani ambaye alitamani awe mume wake wa ndoa. 

“Ni yupi ambaye niliwahi kusema huyu anaweza kuwa wa maisha,” alisema Wema. “Kiukweli alikuwa anaitwa Nasib Abdul,nilishawahi kusema hivyo,” alisisitiza.
Hata hivyo ndoto hiyo iliyeyuka baada ya wawili hao kuachana mwaka jana na Diamond kuhamisha mahaba yake kwa Zari the Bosslady ambaye tayari wana mtoto wa kike, Tiffah. 
Viewing all 104809 articles
Browse latest View live




Latest Images