Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104809 articles
Browse latest View live

KENYATTA APOZA HASIRA ZA JAKAYA KIKWETE

$
0
0
Baada ya malalamiko ya Rais Jakaya Kikwete, ushirikiano wa nchi tatu unaojulikana kama Umoja wa Walio Tayari, umeivuta Tanzania katika mradi wa reli.

Akizungumza jana wakati wa uzinduzi wa mradi wa reli wa kuanzia Mombasa hadi Kigali, Rwanda, Rais Uhuru Kenyatta wa Kenya alisema mradi wa ujenzi huo pia utaijumuisha Tanzania.

Umoja wa Walio Tayari unaundwa na Kenya, Rwanda na Uganda ambazo pia ni wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC).

Katika siku za karibuni, nchi hizo zimekuwa zikilaumiwa kwa kuzitenga nchi nyingine wanachama wa EAC za Tanzania na Burundi.

Akizungumzia madai hayo, Rais Kenyatta alisema nchi zinazounda Umoja wa Walio Tayari hazikuwa na mpango wa kuitenga Tanzania.

Hatua hiyo inakuja huku wakuu wa nchi tano za EAC wakitarajiwa kukutana kesho huko Kampala, Uganda.

Rais Kenyatta alisema reli hiyo inayotoka Mombasa, Kampala hadi Kigali itakuwa na tawi la kupitia Voi hadi Taveta kabla ya kuingia Tanzania ikianzia Moshi hadi Arusha.

Alisema reli hiyo inajengwa ili kurahisisha usafirishwaji wa mizigo kutoka bandari ya Mombasa kwenda katika nchi za jirani.

Alisema ujenzi wa reli hiyo haukufanywa nje ya jumuiya na nchi hizo tatu, bali ulipitia katika kamati ya EAC kwa kufuata taratibu zilizowekwa.

Akilihutubia Bunge mjini Dodoma Novemba 7, mwaka huu, Rais Kikwete alisema mradi huo wa reli haumo EAC na hawakuwa na tatizo nao ila alishangazwa na kutengwa kwenye mpango wa awali wa nchi hizo akiamini Tanzania ni mshirika muhimu wa kibiashara katika eneo hili.

Pamoja na hayo, Rais Kenyatta alisema Tanzania itahusishwa pia katika mradi wa ujenzi wa barabara.

“Mwezi ujao tutakuwa kule Voi kuzindua barabara itakaokwenda Taveta na kutuunganisha na majirani zetu Tanzania, pia tunataka turekebishe hii barabara ya Lungalunga ya kupitia mpaka wa Horohoro ili ituunganishe na majirani zetu wa Tanzania sasa jamani wale ambao wanasema tunavunja.... tunavunja nini wakati sisi tunaunganisha,” alisema Rais Kenyatta.

Hata hivyo, Rais Kenyatta alisema Umoja wa Walio Tayari hauwezi kuvunja EAC kwa kuwa nchi zote ziko pamoja katika kutekeleza majukumu ya jumuiya hiyo.

Alisema wanaodai kuwa umoja huo unaleta matatizo hawajui wanachokisema kwa kuwa hakuna nchi yoyote inayoachwa nyuma katika mambo hayo muhimu.

Marais Kenyatta, Paul Kagame wa Rwanda na Yoweri Museveni wamefanya vikao vitatu kujadili ushirikiano miongoni mwa nchi zao.

Viongozi hao wamefanya mikutano mitatu mwaka huu, Juni 24-25 Mjini Entebbe, Uganda; Agosti 28 Mjini Mombasa, Kenya na Oktoba 28, Mjini Kigali, Rwanda.

Katika vikao hivyo, iliamuliwa kuwa nchi hizo zishirikiane katika kuboresha miundombinu, uanzishwaji wa himaya moja ya ushuru wa forodha, uhamiaji na kuundwa kwa shirikisho kisiasa.

MASOGANGE YUPO DAR..AJIFICHA KUKWEPA MAPAPARAZI

$
0
0
Stori: Gladness Mallya
VIDEO Queen wa Bongo, Agnes Gerald Waya ‘Masogange’ ambaye alipata soo la kukamatwa na malighafi haramu aina ya Ephedrine Julai 5, mwaka huu nchini Afrika Kusini amejaa tele jijini Dar es Salaam, Ijumaa limethibitisha.
Masogange akipozi na Jack Patrick.
Masogange ambaye siku ya tukio alikuwa na nduguye, Melisa Edward baada ya kunaswa na madawa hayo kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Oliver Tambo uliopo Kempton Park jijini Johannesburg nchini humo alihukumiwa kwenda jela miezi 32 au kulipa faini ya shilinghi milioni 4.8 ambapo aliweza kulipa na kuwa huru.
Tangu aachiwe huru, Septemba mwaka huu, msanii huyo akawa hajulikani alipo huku baadhi ya ‘posti’ zake kwenye mtandao wa kijamii wa Instagram zikionesha yupo Tanzania au Afrika Kusini.
Masogange akipozi dukani Bongo.
Jumatatu iliyopita, mida ya saa kumi jioni, paparazi wetu alipigiwa simu na msomaji wa gazeti hili (jina tunalo) akisema amemwona Masogange akiingia kwenye duka la nguo lililopo Sinza Kamanyola, Dar akiwa peke yake.
Paparazi wetu alijipanga kwa kamera na kutia timu kwenye duka hilo ambapo hata hivyo muuzaji alisema aliondoka baada ya kufanya manunuzi ya kawaida.
Jumatano, Masogange alitumbukiza picha kwenye mtandao wake akiwa ndani ya duka hilo na modo maarufu nchini, Jacqueline Patrick.
Jack alipigiwa simu ambapo alikiri kuwa na Masogange siku ya Jumanne kwenye duka hilo. Akasema: “Mimi nilimkuta pale, tukapiga picha tukaachana, basi.”
Kwa kutumia namba yake ya simu ya mkononi, Masogange alipatikana na kukiri yupo Dar lakini akasema hakutaka kuweka wazi kwa sababu anawaogopa sana mapaparazi.
-Global Publishers

MWANAFUNZI ATEKWA HUKO MOSHI NA KUFANYISHWA NGONO KWA SIKU NNE..SOMA ZAIDI HAPA

$
0
0
MWANAFUNZI wa kidato cha kwanza katika shule ya sekondari Marangu inayomilikiwa na kanisa Katoliki jimbo la Moshi, (jina limehifadhiwa) alitekwa na kukufungiwa kwenye hoteli moja ya kitalii mjini hapa na kufanyiwa vitendo vya ngono kwa muda wa siku nne mfululizo.
Mwanafunzi huyo anadaiwa kutekwa Agosti 6 mwaka huu na kijana mmoja (jina linahifadhiwa) mfanyakazi wa kampuni ya simu za mikononi (Airtel) mjini Dodoma.

Akizungumza jana na Tanzania Daima Jumatano, kaka wa mwanafunzi huyo, Joseph Temba, alidai mdogo wake alitekwa na mtu huyo na tayari mtuhumiwa ameshakamatwa.
  
Alisema walifanikiwa kumkamata mtuhumiwa huyo Agosti 10, mwaka huu, katika baa moja akiwa na mdogo wake baada ya raia wema kutoa taarifa za kuonekana kwake.
  
Kwa mujibu wa kaka wa mwanfunzi huyo siku ya tukio alipokea simu kutoka kwa mwangalizi wa wanafunzi (matroni) akimjulisha kutokuwapo bwenini kwa mdogo wake na ndipo walipoanza kufuatilia na kutoa taarifa kituo kikuu cha polisi mjini Moshi na kupewa namba Mos/RB/9196/2013.

Alisema siku iliyofuata ya Agosti saba jioni walipokea simu kutoka kwa watu wa karibu wakiwataarifu kuwapo katika hoteli hiyo mdogo wake lakini baada ya kufika walinyimwa kuona kitabu cha wageni ili kuangalia orodha ya majina ya wageni waliofikia hapo ili kujiridhisha kama mtuhumiwa huyo alikuwapo mahali hapo.
  
Hata hivyo alisema jioni ya Agosti 10 walipokea taarifa za kuonekana kwenye baa hiyo mtuhumiwa akiwa na mdogo wake na kuwajulisha polisi na hatimaye kufanikiwa kumtia mbaroni ambapo hadi sasa bado anahojiwa na jeshi la polisi.
  
Chanzo cha kutekwa kwa mwanafunzi huyo ni mawasiliano ya simu baina ya mtekaji na mwanafunzi huyo ambapo inadaiwa mtuhumiwa huyo alimrubuni mwafunzi huyo kuacha masomo na kwamba angemtafutia nafasi kwenye shule kubwa za kimataifa.

Inadaiwa kwamba mwanfunzi huyo alikubaliana na propaganda hiyo na kutoka shuleni jioni ya Agosti 6 na kumfuata mtuhumiwa kwenye gari lake na kwenda naye hadi Moshi mjini umbali wa kilomteta 50 kutoka shule ya sekondari Marangu.
Kamanda wa polisi mkoa wa Kilimanjaro, Robert Boaz, alisema hana taarifa za kutekwa kwa mwanafunzi huyo kwa kile alichodai alikuwa ametingwa na majukumu ya kikazi mjini Arusha na kuahidi kulifuatilia baadaye

HIZI NDIZO SABABU 10 ZA WANAWAKE KUTOKUOLEWA NA KUISHIIA KUSAGANA TU

$
0
0

Pamoja na kuwa kuna wanawake husita kuolewa, lakini jambo hili si kubwa sana kwa wanawake kama ilivyo kwa wanaume.


 Kwa kiasi kikubwa katika suala la kutaka kuingia ndani ya ndoa, wanawake ni wengi ambao hutaka kufunga ndoa kuliko ilivyo kwa wanaume. Hilo tunaliona wazi tokana na shamra shamra awazo nazo mwanamke wakati wa maandalizi ya shughuli za Ndoa na Harusi.


Hata hivyo, kwa wale wanawake wachache ambao husuasua kuolewa hizi ni baadhi ya sababu zinazopelekea kusuasua huko. (Izingatiwe hii ni kwa wanawake ambao hawajawahi kuolewa kabisa)

 

Vigezo vilivyopitiliza viwango (hasa kwa muonekano)

 

Wanawake wengi hasa wa umri mdogo (lakini unatosha kuolewa) hutumia muda mwingi katika kuchagua aina ya mwanaume ambaye angependa awe mume wake.Wanawake hawa hujiamini zaidi na kusimamia sifa zile ambazo huamini ni muhimu mwanaume wa kumuoa awe nazo.  


Vigezo hivyo huwa hata kwa misingi ya muonekano wa mwanaume huyo – kuna wale ambao hutaka mwanaume huyo wa kumuoa awe na sifa kama vile, mrefu, aliyejazia kifua, mtanashati, sauti nzuri n.k. 


Inaweza kuwa kama mzaha na ikaonekana ni kipengele kidogo sana lakini bado kuna wale ambao anaweza kuwa tayari kuolewa ila hataki sababu tu huyo mwanaume hafananii vile ambavyo yeye anataka mumewe awe.

 

Kutaka mwanaume tajiri

 

Kuna wanawake ambao tayari wameshajiwekea akilini kuwa hatakubali kuolewa na mwanaume yeyote yule ambaye hana pesa nyingi.


 Yupo tayari kuolewa ila si kwa mwanaume mwenye uwezo wa kawaida – hata ikitokea mwanaume ana uwezo kidogo wa kuweza kujitosheleza, yeye bado huona huyo mwanaume hamfai hadi pale tu atakapo pata yule ambaye anahisi ataishi maisha ya kifahari.


 Hivyo hukazana kusubiri na kujitahidi kuwinda aina ya mwanaume ambaye atakuwa na uwezo mkubwa, bila kujalisha kama huyo mwanaume kampita sana umri.


 

Kutompata Mwanaume Ampendae

 

Hili ni kama tu vile ilivyo kwa wanaume ambao huamini ndoa haiwezekani na haifai bali tu hadi pale umpatapo yule ambaye unampenda na unaamini anakupenda pia.  


Wengi katika kundi hili huamini kuwa mafanikio ya ndoa kigezo kikubwa ni kupendana tu na mengine hufuata kwenye sababu ya upendo. Kunawanawake vigezo vya mwanamme awe vipi havina umuhimu kabisa katika kutaka kuamua kuolewa.


 Yeye kikubwa anataka ampate mume ambaye atampenda kwa dhati na huku akiwa na matumaini kuwa huyo mume atampenda na yeye pia kwa dhati.  Huyu mwanamke anaamini msingi bora wa ndoa ni mapenzi ya dhati kati ya yeye na mmewe basi! Hana haraka hadi pale atakapompata mwanaume akampenda ndipo atakapokuwa tayari kuolewa.  

 

Kuchagua mno Wanaume wa Kumuoa (SO SELECTIVE)

 

Kuna wale wachache ambao akili hubadilika kama kinyonga; wasioridhika wala kujitambua ni nini wanataka ama mwanaume wa aina ipi wanataka. 


Akija wa mwenye uwezo atasema nataka wa kuchuma nae, akija asiye na uwezo atatoa sababu tu hata kama kumlaumu kuwa inaonyesha hajitumi kutafuta maendeleo. 


Akija wa kabila hii, atasema hapana hao wana tabia hii mimi siitaki! Yaani kwa ufupi ni mtu asiyeisha kutoa kasoro za wale ambao wanajitokeza kutaka kumuoa.


 Hatimaye inaweza tokea muda wa kuolewa ukapita na akaishia kupunguza uchunguzaji lakini ikiwa hata wanaume wa umri wa kufaa kumuoa kutokuwepo tena katika soko.

 

Kujiona ni mzuri sana

 

Kuna wanawake ambao ni kweli Mwenyezi Mungu kawajaalia uzuri hasa (uzuri wa muonekano), anakuwa ni mzuri kiasi kwamba wake kwa waume wote wanamkubali kwa uzuri huo na hata wote kumtamani.


 Hata hivyo hapo hapo kuna wale ambao huwa ni wazuri kawaida – ila kwa mtazamowake hujiona ni mzuri mno hakuna mfano kama yeye; kitendo ambacho kwa wachache kwenye kundi hili hufanya kujiona yeye ni yeye na kuwa kwa yeyote kuwa na yeye huyo mtu anatakiwa atambue kuwa ana bahati sana. 


Kitendo hiki hukuza nyodo za hali ya juu ya mwanamke mwenye mtazamo huu, kiasi kwamba wanapojitokeza wanaume kutaka kuoa – anaweza onyesha tabia kama maringo, dharau na kiburi.

 

Kujiona ana Umri mdogo

 

Binti yeyote wa miaka 18 na kuendelea anaruhusiwa kuolewa endapo tu karidhia kuolewa.


 Wanawake wametofautiana mipangilio yao ya kimaisha, kuna wale akiwa katika umri wa kuolewa hutamani sana kuolewa na kuna wale ambao hupenda kuolewa wakiwa wakubwa zaidi.


 Katika kundi hili umri kuwa mdogo hutegemeana, kuna mwingine anakuwa na umri wa miaka 25 na bado akajiona mdogo na hali kuna mwingine anakuwa na miaka 20 na akajiona ni mkubwa na anafaa kuolewa. 


Hii pia ni kwa wanawake wale ambao huwa na malengo ya kutotaka kuharakisha katika ndoa.


 Anapokuwa na umri ambao anaweza kuolewa lakini yeye hayupo tayari kwa muda huo, huwa ni kikwazo kwake kuingia katika ndoa.

 

Maradhi hasa UKIMWI

 

Hili kama lilivyo kwa wanaume -  Pamoja na kuhamasishwa kwingi na wataalamu wa maradhi ya HIV/AIDS kuwa mtu hata ukiwa umeathirika unaweza kuwa na mahusiano na hata kuoa na kuwa na watoto; bado haisaidii sana kwa vijana wanaojitambua kuwa ni waathirika wakiwa bado ni wadogo, hawajaoa/olewa ama kuwahi kuwa na mtoto. 


 Wengi sana hukata tamaa na huona ni kheri kubaki walivyo kuliko kuingia katika ndoa, hasa tokana na imani kuwa wanawake wakizaa wakati ni waathirika; afya hudhoofika zaidi.

 

Kutaka maisha ya Tamthilia (Ndoa za kuishi kwa furaha milele)

 

Kutokana na kukua kwa idadi ya tamthilia nyingi ambazo huonyesha maisha ya kimagharibi zaidi; kumekuwa na dhana kwa baadhi ya wanawake kutaka hayo maisha ya tamthilia yawe na kwao pia.


Hilo linafanya vigezo ambavyo mwanamke huyo anatumia kuchagua ama kukubali mwanaume kumuoa kutotimiza yale ambayo yeye binafsi anatarajia.  


Wengi hushindwa kutambua kuwa hakuna maisha ya furaha milele, na hasa kuwa maisha ya maigizo yapaswa kuchanganya na zako kuweza kufanya maamuzi ya kipi kiigwe na kipi kiachwe kama kilivyo.

 

Kuona taasisi ya Ndoa kama Utumwa

Mtazamo huu kwa wanawake wenye msimamo huu, huchangiwa na baadhi kama haya:

 

Usomi: Aina ya usomi ambao hupelekea kwa baadhi kuwa na tafsiri tofauti juu ya ndoa, haki, majukumu na mengine mengi.

 

Kushuhudia ndoa mbovu: Hii inaweza kuwa ya wazazi/walezi wake wenyewe (pengine mama aliteswa sana), na hata ndugu wa karibu kama vile kushuhudia kila ndoa ya ndugu yake anayoijua mwanamke huishi kwa mateso, manyanyaso na maisha ya taabu na kuonewa.

 

- Kuwa na uwezo sana wa kujitosheleza ambao unaweza kumtimizia na kufanya lolote lile ambalo anataka katika maisha. Kwake kuwa na mwanaume kama mume kwake anaona kama ni utumwa.

 

Kutokuwa kabisa na mshipa wa hisia za kufanya mapenzi

 

Kuna wanawake wale wachache waliozaliwa hivyo. Hawana hisia yoyote ile ya kimwili ya kuweza kupata hisia za kuweza kujisikia ama kutamani kufanya mapenzi. 


Wengi wa aina hii ya wanawake huwa ni waoga sana wa kuwa karibu na mwanaume, na kwa wale ambao wamewahi hata jaribu baadhi huona kama kitendo cha ndoa ni kero, unyanyasaji na uchafu.  


 Hivyo wazo la kuwa akiolewa anatarajia kufanya kitendo cha ndoa mara kwa mara kinamvunja kabisa hamu ya kutaka kuolewa.

DIRECTOR WA ENDLESS FAME AJIBU TUHUMU ZA KUKUTWA AKIFANYA UFUSKA NA GARI YA WEMA SEPETU

$
0
0
Baada ya juzi kati kuripotiwa habari ya aliyekuwa producer ama mtengenezaji wa vipindi vya Wema Sepetu Chidi Mohamed kufukuzwa kazi kutokana na kulitumia gari la kampuni kama sehemu yake ya kuvunjia amri ya sita na wadada wa mjini, hatimaye katika pitapita zetu za mtandaoni tuliweza kukutana na kauli ya producer huyo akizungumzia habari hiyo ya yeye kufukuzwa kazi kwenye kampuni ya Endless Fame ya wema sepetu.
Chidi mwenyewe anasema kuwa habari hizo si za kwel na ni kwamba wote walioandika wamepanga kumchafua tuu kwa kuogopa kuwa anaweza kuyaniika mambo mazito yanayoendelea huko endless Fame
Kwa mujibu wa chidi anasema kuwa yeye ameondoka kwenye Kampuni hiyo siyo kwa sababu ya uzinzi ngani ya gari kama ilivyoripotiwa bali ni kutokana na sababu hizi kuu mbili.
1. Ameona hamna jipya na wala hamna maendeleo yoyote ndani ya Kampuni hiyo ndio maana ameamua kuondoka
2. Wafanyakazi wa Endless Fame hawalipwi kabisa ndio maana yeye akaamua kujitoa kwani anafanya kazi bure na pia sio yeye peke yake aliyeondoka bali kuna wafanyakazi zaidi ya watatu walioondoka kwenye kampuni hiyo ila nashangaa ni kwanini wameamua kumchafua yeye?
Bado tunafanya mawasiliano na Endless Fame ili tujue kama daia haya ni ya kweli au la

HATIMAYE MWANA FA, AY NA HERMY B WAMALIZA BIFU LEO LA MIAKA MINGI

$
0
0
‘Friends again’, ni maneno yaliyoandikwa na Amani Joachim (Chief Operations Officers wa B’Hits), kwenye ukurasa wake wa facebook na kupost link yenye picha inayowaonesha AY, Mwana FA, na Hermy B wakiwa kwenye picha moja.

Wengine kwenye picha hiyo ni Fid Q, Carol Ndosi na Arthur.
Picha hiyo imepigwa usiku wa kuamkia leo (November 29) inamuonesha Producer wa ‘Habari Ndiyo Hiyo’ Hermy B baada ya kumwagia ndoo ya maji katika kusherehekea siku yake ya kuzaliwa.
Leo mchana Hermy B amepost picha akiwa na FA uwanja wa ndege wa J.K na kuandika ‘Bday continues’.

MWANAMKE MMOJA AISHI NA WANAUME WAWILI NDANI YA CHUMBA KIMOJA WOTE NI WAUME ZAKE

$
0
0
DUNIA ina kila kituko, kama hujawahi kukisikia omba Mungu akupe uzima!  Mama mmoja, aitwae  Elizabeth Selestine, mkazi wa Kigogo-Mburahati, Dar hivi karibuni alizua timbwili nyumbani kwake baada ya majirani, wajumbe na ndugu zake kumjia juu kwa kitendo chake cha kuishi na wanaume wawili kwenye chumba kimoja, Ijumaa lina mkasa kamili. 
Elizabeth Selestine anayeishi na wanaume wawili.


Ndani ya timbwili hilo, watu kibao walikuwepo, lakini muhimu sana ni mdogo wa mwanamke huyo, Oscar Selestine (17) ambaye alianika kila kitu.
Oscar alisema shemejiye anaitwa Benedicto Ludovic na dada yake huyo walipanga kwenye nyumba ya akina Juma Ngulumo ambaye ndiye mwanaume wa pili, yaani hawara.

 
Mume wa ndoa.


“Baada ya kuanzisha uhusiano na Juma, mwenye nyumba (baba wa Juma) aliwafukuza akiogopa kuwa kwa tabia ya dada lisije likatokea balaa kubwa. Hata mimi na mdogo wangu tuliishi kwa dada na shemeji.
“Dada na shemeji  wakahamia kwenye chumba kimoja nyumba ya jirani, dada akaniambia mimi na mdogo wangu mwingine tuishi nao huku tukitafuta pa kulala kwa sababu wao walipata chumba kimoja ambacho tulikuwa tunalala wote, mimi, mdogo wangu, dada, shemeji na watoto wao wawili.

Lakini siku moja nilishangaa kumwona Juma akija na godoro hapo hapo kwenye chumba kimoja huku shemeji akiwemo,” alisema Oscar na kuwashangaza hata mapaparazi. Dunia ina mambo mengi.
 
Mama mwenye nyumba.


 “Nilishtuka sana! Kulala kwenyewe, shemeji  na dada kitandani, Juma akawa analala chini wakati na yeye ni mtu mzima tena ana watoto,” alisema Oscar.
Oscar aliendelea kusema kuwa, siku moja alishangaa kumwona Juma akimpiga dada yake, alipojaribu kuuliza dada huyo  akamjibu: “We mtoto, hayakuhusu.” Mwisho yeye na mdogo wake wakafukuzwa na kuambiwa wasifike  nyumbani hapo.
Oscar hakuona sababu ya kufunga kinywa bila kumalizia kusema yote, akaanika kwamba ilifika mahali Juma alianza kumpiga shemeji yao kisa eti amekuwa na wivu kwa mke wake. Makubwa hayo!

Kumbe mtoto mmoja wa dada alikuwa akiona kila kitu, siku moja akaanika siri kwamba, Juma huwa anampiga shemeji usiku na ili amuache dada alale naye chini,” alisema Oscar.
 
Ndugu wa mke.


Oscar akasema hakuna siri ya watu wawili, baadaye habari zilizagaa kwa ndugu wote kuwa dada yao anaishi na wanaume wawili, ndipo mama mwenye nyumba alimuita na kumkanya lakini hakusikia.
Mwenye nyumba alipoona jeuri hiyo alimuita tena na kumpa siku saba aondoke ndani ya nyumba yake lakini bado Elizabeth hakufanya hivyo.
Oscar tena: “Huwezi amini ilifika wakati shemeji akileta chakula kinapikwa halafu yeye hatengewi, anatengewa Juma, shemeji akiuliza anaambiwa akale na watoto. Sisi hatumuelewi shemeji, kama ni madawa basi yamemkolea sana.

Ikadokezwa kwamba tukio hilo lilifika mbali, hadi kwa  wazazi wa mwanaume, Kilosa, Morogoro ambao walifunga safari mpaka Dar lengo lilikuwa kuwachukua wajukuu na mtoto wao Benedicto, lakini ilishindikana kwani waliambulia kutukanwa na mwanamke huyo, wakaondoka wakiacha laana nyuma.
Vituko viliendelea siku hadi siku, siku moja Benedicto au maarufu kwa jina la ‘baba Gire’ alikwenda kwa mjumbe wa eneo hilo, Maua Thabiti  huku akilia na kuapa ipo siku atafanya kitu kibaya ambacho mkewe na Juma hawatakaa wakisahau.
Mjumbe huyo ambaye ni wa shina namba 48, mtaa wa National Housing Mburahati, Dar alikiri kupokea malalamiko hayo lakini akasema mwanaume huyo anaogopa kuweka wazi kwa sababu atapigwa, hivyo anamuachia Mungu.

Mwenye nyumba wanayoishi watu hao, Flora Mtumbati alipoulizwa naye alikiri kuwa, Eliza anaishi na wanaume wawili.
“Baada ya kubaini hilo, Eliza aliitwa na Jumuiya ya Katoliki anakosali na kuonywa. Mimi nilimpa siku saba za kumtoa Juma na kubaki na mumewe, aliniahidi lakini hakufanya hivyo, bora watu wa magazeti mmekuja mnaweza kunisaidia,” alisema Flora.
Baada ya kuongea na vyanzo vyote, gazeti lilimtafuta Elizabeth:

Huyu bwana (Juma) alikuja kwangu kwa matatizo, alikaribishwa na mume wangu, nilimkaribisha chumbani kwangu kwa sababu ndiyo chumba hichohicho. Hata hivyo, leo (Ijumaa iliyopita) anahama.”
Baada ya waandishi kuondoka, mwanamke huyo alitishia kujiua. Siku ya pili, waandishi waliambiwa kuwa mwanamke huyo alikimbilia Kimara  kwa wifi yake ambaye ni ndugu wa Juma.

Benedicto alipopatikana alisema: “Sikuamini kama mke wangu anatembea na Juma ingawa niliwahi kusikia. Kuhusu kupigwa ni kweli hasa akilewa pombe. Baada ya sakata hili mke wangu amesema kwa watu kuwa hata mtoto wa mwisho si wangu, ni wa Juma. Inauma sana.”
Baada ya waandishi kuibua ishu na watu kujaa, inadaiwa  Juma alitafuta vijana na kumpa kichapo cha nguvu baba Gire ambapo ameshonwa nyuzi kumi na mbili mdomoni na jichoni.
Kesi hii ilifikishwa Kituo cha Polisi Mburahati na kufunguliwa jalada namba MBR/RB/1204/13  KUJERUHI.

SIKU HIZI UOVU HAUCHAGUI PA KUTUA-MCHUNGAJI GWAJIMA ALISHWA SUMU

$
0
0
Stori: Chande Abdallah na Jelard Lucas
SIKU hizi uovu hauchagui pa kutua, Mchungaji wa Kanisa la Ufufuo na Uzima, Josephat Gwajima amejikuta katika hali mbaya baada ya kulishwa sumu na mtu mwenye nia mbaya, Risasi Jumamosi lina kisa hicho.
Akizungumza na mapaparazi wetu kanisani kwake, Kawe, Dar es Salaam hivi karibuni, Gwajima aliweka wazi kwamba, tukio hilo lilimtokea mwanzoni mwa mwezi huu.

MCHEZO ULIVYOANZA
Mchungaji Gwajima ambaye anasifika kwa kuwarejesha katika hali ya ubinadamu watu waliodhaniwa wamekufa (misukule) alisema kuwa sumu hiyo aliwekewa kwenye soda aliyokaribishwa na askofu mmoja mkuu wa kanisa kubwa nchini Tanzania (jina kapuni). 
“Siku hiyo, huyo askofu aliniita nyumbani kwake (hakupataja jina), nikaenda nikiongozana na askofu mwingine ambaye ni rafiki yangu.

MAONGEZI KUHUSU MUNGU NA SODA JUU
“Tulipofika, tuliongea  mambo mengi ya kiroho. Baadaye akatupa soda lakini nilipoinywa nilihisi kuna kitu ndani yake. Roho wa Mungu pia akasema nami kuhusu hilo, palepale nilimwambia yule askofu kwamba amenipa  soda yenye sumu ndani yake,” anafunguka Gwajima kwa mara ya kwanza kwenye gazeti hili.
“Yeye alikuwa akikataa kwamba hajaniwekea sumu kwenye kinywaji hicho lakini cha kushangaza alionekana kutetemeka sana.”

AISHIWA NGUVU, AAGA
Gwajina alisema filamu ya sumu hiyo haikuishia hapo kwani ghafla alianza kuhisi kuishiwa nguvu jambo ambalo lilimshtua na kuanza kubabaika.
Gwajima: “Niliondoka haraka sana huku nikimhakikishia yule askofu kwamba sitakufa bali nitaishi kama maandiko yanavyosema kwa kuwa naamini katika ufufuo na uzima.

MKEWE AMTAKA AENDE HOSPITALI
Akaongeza: “Wakati huo nilikuwa nikitakiwa kuja kwenye huduma hapa kanisani, nikaingia huku tumbo likiwa linakata sana. Cha kushangaza nikafanya maombi kama kawaida. 
“Nilipomaliza huduma nilirudi nyumbani na kumwambia mke wangu. Yeye akanisihi niende hospitali lakini nilikataa.” 

AENDA KUONANA NA DAKTARI WAKE
Gwajima anaendelea: “Katikati ya usiku mnene, nilisikia kitu kimelipuka tumboni na maumivu makali yakafuatia, nilimwomba Mungu anifikishe hadi asubuhi. Ilipofika nilikwenda kwa daktari wangu ambaye baada ya kunichunguza aliniambia nilipewa sumu ya kuniharibu akili na si ya kufa kama nilivyodhani.”
Mchungaji huyo aliendelea kusema kwamba, daktari wake huyo alimwambia kwa vile sumu hiyo aliinywa kidogo dawa yake ni kunywa maji mengi ili kuimaliza kabisa, akamtahadharisha kuwa angeinywa kwa kiwango kikubwa na kuchelewa tiba angechanganyikiwa akili kiasi cha kushindwa kuwa na mawasiliano mema na binadamu wenzake.

ASKOFU ALISHALIPWA FEDHA ILI AMDHURU GWAJIMA
Gwajina alisema katika utafiti wake, aligundua kuwa askofu huyo alilipwa shilingi milioni 300 na wabaya wake ili wamdhuru kwa sumu hiyo, lengo ni kumfanya ashindwe kutoa huduma ya kiroho katika kanisa lake ambalo linakua siku hadi siku.

AMPIGIA SIMU ASKOFU MBAYA WAKE
“Asubuhi ya siku iliyofuata nikiwa nimepata nafuu nilimpigia simu yule askofu nikamwambia kwa kumtania kwamba anigawie pesa kidogo katika hizo alizolipwa,” alisema Gwajima.

AMWACHIA MUNGU
Gwajima alisema alikuwa na uwezo wa kumpeleka mbele ya sheria askofu huyo lakini kwa vile yeye ni mtumishi wa Mungu alitakiwa aoneshe mfano wa kusamehe kama maandiko yanavyotaka.
Hata hivyo, alisema kama angeamua kumwanika askofu huyo ana uhakika waumini wake wangetimka kanisani kwake na kubaki yeye na familia yake tu.
Imeandikwa na Global Publishers

WANANCHI WA JIMBO LA ARUSHA MJINI[CHADEMA] WAMPINGA HADHARANI KWA MABANGO MBUNGE WAO, GODBLESS LEMA

$
0
0
Soma Bango hilo, wafuasi wa CHADEMA jijini Arusha ,walioambatana na Mwenyekiti wa CHADEMA wilaya ya Monduli Bw. Amani Salenga wakionyesha bango hilo kwa waandishi wa Habari (hawapo pichani) ,wakidai kuwa Mbunge Lema ndie chanzo cha vurugu kwenye Chama kwa kuanzisha kikundi cha vijana ambacho kimekuwa tishio kwa wale wanaojaribu kupingana na sera za Mbunge huyo. pia wamedai kuwa Arusha kwa sasa CHADEMA imegawanyika katika makundi mawili, amabyo ni CHADEMA ASILI na CHADEMA FAMILY.

PENNY MCHUMBA WA DIAMOND AZIDI KUKONDA

$
0
0
Stori: Imelda Mtema
MTANGAZAJI wa Runinga ya DTV, Penniel Mungilwa ‘Penny’ ameamua kujikondesha mwili ambapo amefanikiwa kupoteze uzito usiopungua kilo  18 mwilini.

Akizungumza na Weekly Star Exclusive, Penny alifunguka kuwa, kutokana na kuona mwili wake unavimbiana, aliamua kufanya mazoezi maalum ya kupunguza mwili sambamba na kufanya ‘dayati’ ambayo imembadilisha muonekano wake (tazama picha ndogo).
“Nimeamua tu kuubadilisha muonekano wangu wa unene kwani nilikuwa ninazidi kuwa bonge, kweli nimefanikiwa maana hata uzito nimepungua kwa sasa.
“Kabla sijaanza kufanya mazoezi nilikuwa na kilo 85 lakini sasa nimepungua hadi kufikia kilo 67, ni mafanikio makubwa ambayo nimeyapata katika zoezi langu la kupunguza uzito,” alisema Penny ambaye ni ‘ubavu’ wa Mbongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond’.
Kuhusu msosi, kwa sasa Penny asubuhi anakula ‘ma-apple’ mawili au kipande cha papai, mchana anakunywa juisi na usiku anamalizia na saladi ya samaki au kuku, analala.
Global Publishers

JACKLINE WOLPER 'FILAMU NILIYOTOA KUMUENZI STEVE KANUMBA ILINIPA HASARA YA MAMILIONI YA SHILINGI"

$
0
0
NYOTA wa filamu Bongo, Jacqueline Wolper amefunguka kuwa filamu yake aliyoitoa kumuenzi marehemu Steven Kanumba iitwayo After Death ilimlostisha kwa kuwa ilimpatia hasara kubwa.

“Nilitengeneza ile filamu kwa hela nyingi kidogo, kama milioni 35 au 40, nikafanya na uzinduzi pale Leaders Club uliogharimu kama milioni 13 hivi, lakini nilipokwenda kwa Wahindi wakanipa shilingi milioni 25, yaani inakatisha sana tamaa,” alisema muigizaji huyo wakati alipofanya mahojiano maalum na waandishi wetu.

Alisema hasara aliyoipata na ambayo hata wasanii wenzake huipata inatokana na uwepo wa wasambazaji wachache wa kazi za wasanii, kitu kinachowafanya watu hao kujipangia bei bila kujali gharama ambazo wameingia katika utengenezaji wake. 

Chanzo: GPL

BAADA YA KUGOMA KUFUNGUA MADUKA WAKIGOMEA MASHINE ZA TRA..WAFANYABIASHARA WA KARIAKOO WAGOMEA SEMINA YA TRA

$
0
0
Dar es Salaam. Baadhi ya wafanyabiashara walio katika maeneo ya Kariakoo wamegoma kushiriki semina ya  uelimishaji iliyokuwa itolewe na  Mamlaka ya Mapato nchini (TRA) katika kile walichokiita kupuuza madai yao na kutaka kufanya vile wanavyotaka wao kuhusiana na  sakata la mashine za kielektroniki za kukusanyia mapato.
Mamlaka hiyo iliitisha mkutano katika Hoteli ya Starlight ikilenga kuwaelimisha wafanyabiashara hao juu ya matumizi ya mashine za kielektroniki, jambo ambalo lilizua zogo miongoni mwa  wafanyabiashara waliokuwepo katika eneo hilo.
Akizungumza na gazeti hili, mmoja wa wafanyabiashara wa nguo eneo la Kariakoo aliyekuwepo hotelini hapo, akijitambulisha kwa jina moja tu la Mwanahamisi alisema siku ya Jumatano gari la matangazo lilipita baadhi ya mitaa ya Kariakoo likiwataka wafanyabiashara hao wafike kwenye mkutano uliopangwa kufanyika.
“Kutokana na taarifa hiyo kuletwa kienyeji, baadhi ya wafanyabiashara wachache tumefika  tukijua tutapata ufumbuzi juu ya kilio  cha muda mrefu kuhusiana na malalamiko waliyopeleka kwenye mamlaka hiyo, a alisema.
Matokeo yake watu kutoka mamlaka hiyo waliofika kwenye mkutano, walianza kutoa utambulisho juu ya kile walichotarajia kukifanya ikiwa ni kutoa elimu juu ya matumizi ya mashine hizo.

Gazeti la Mwananchi

USHAHIDI WA UMILIKI WA ZIWA NYASA WATOLEWA

$
0
0
Dar es Salaam. Malawi na Tanzania zimewasilisha ushahidi na majibu ya maswali kuhusu umiliki wa maeneo kwenye Ziwa Nyasa, kwa jopo la wasuluhishi linaloongozwa na Rais mstaafu wa Msumbiji Joachim Chissano.

Wasuluhishi hao walizitaka Malawi na Tanzania kutoa majibu ya maswali manne muhimu, wakati wakiwasilisha ushahidi wao kuhusu umiliki wa ziwa hilo wenye mgogoro.

Mgogoro huo uliibuka baada ya Serikali ya Malawi bila kushauriana na Tanzania kutoa leseni kwa kampuni mbili za kigeni, kutafuta mafuta katika eneo la ziwa ambalo linamilikiwa na Tanzania.

Kwa mujibu wa gazeti la mtandaoni la Malawi la  Nyasa Times, msemaji wa Waziri wa Mambo ya Nje na Uhusiano wa Kimataifa wa Malawi, Quent Kalichero alithibitisha Jumatano wiki hii kwamba nchi hiyo imewasilisha majibu ya maswali hayo na ushahidi uliohitajika.

“Waziri wetu amewasilisha taarifa maalumu ya maandishi kwa wasuluhishi na kwa sasa yuko nchini Msumbiji, kwa ajili ya suala hilo,” alisema Kalichero juzi.

Makabidhiano hayo yalifanyika mjini Maputo, Msumbiji ikiwa ni siku chache baada ya Rais Jakaya Kikwete kufanya mazungumzo na wasuluhishi, marais wa zamani wa Msumbiji, Joachim Chissano na wa Botswana, Festus Mogae jijini Dar es Salaam.

Akizungumza baada ya mkutano huo wa Jumatatu mjini Dar es Salaam, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa wa Tanzania, Bernard Membe aliwaeleza wanahabari kwamba mazungumzo baina ya Rais Kikwete na wasuluhishi hao yalihusu zaidi ushahidi wa Tanzania katika suala la umiliki wa Ziwa Nyasa.

Pia alithibitisha kwamba Tanzania ilikuwa tayari  kuwasilisha ushahidi wake kwa sekretarieti ya ofisi ya waliokuwa wakuu wa nchi za Jumuiya ya Maendeleo ya Kusini mwa Afrika (Sadc) inayoongozwa na Chissano, Jumatano iliyopita.

Baada ya mkutano huo wa Jumatatu, Membe alieleza kwamba nchi zote husika, yaani Tanzania na Malawi zinatakiwa kuheshimu maagizo na kuwasilisha ushahidi huo kwa wakati, na kuwaachia wasuluhishi kazi ya kupitia na kutekeleza wajibu wao wakiwa wamepewa muda unaofikia mwaka mmoja kupata suluhu.

Wasuluhishi hao wa Sadc, Chissano na Mogae waliwasili jijini Dar es Salaam Jumapili iliyopita kwa ajili ya mazungumzo kuhusu mgogoro huo, kama walivyofanya kwa Malawi Julai mwaka huu.

Julai mwaka huu, Rais Joyce Banda wa Malawi alinukuliwa akisema kuwa nchi yake haina nia ya kulegeza kamba katika mgogoro wa mpaka wa Ziwa Nyasa na Tanzania.

 Alitoa msimamo huo baada ya kukutana na Chissano wa Msumbiji na Thabo Mbeki wa Afrika Kusini ambao ni wajumbe maalumu wa Jumuiya ya Sadc katika mgogoro huo.

Alisema kwamba madai ya Tanzania kuwa inamiliki sehemu ya Ziwa Nyasa, siyo ya kweli na kwamba mpaka uko ufukweni mwa ziwa hilo upande wa Tanzania.

Rais Banda alidai kuwa nchi yake inafuatilia kwa karibu upatanishi wa SADC na kwamba isiporidhishwa na uamuzi ya jumuiya hiyo italiwasilisha suala hilo Mahakama ya Kimataifa ya Uadilifu (ICJ).

Kabla ya hatua hiyo ya Malawi,  Aprili mwaka huu Serikali ya Tanzania iliitaka nchi hiyo kuacha kutapatapa na kuonya kuwa kamwe isithubutu kugusa eneo hilo la mpaka.

Akitoa kauli ya Serikali ya Tanzania Membe alisema: “Nadhani watasikia na kuelewa, Serikali ya Malawi iache kutapatapa, nchi zote ilikoenda kulalamika kuhusu mgogoro huu, Tanzania tumekuwa tukielezwa na hata hao wanaotueleza wanaishangaa sana Malawi.” Kauli hiyo ya Serikali ilifuatia Rais Banda kusema kuwa mgogoro huo sasa utapelekwa katika Mahakama ya Kimataifa ya Haki (ICJ), kwa madai kwamba juhudi za usuluhishi wa kidiplomasia zimeshindikana.

Hata hivyo, uamuzi huo wa Malawi ni kinyume na makubaliano baina ya nchi hizo mbili yaliyofanyika Novemba 7 mwaka jana, jijini Dar es Salaam ambapo zilikubaliana kwamba jopo hilo ndiyo sehemu ya mwisho ya makubaliano.

Katika maelezo yake, Rais Banda alisema nchi yake imejitoa katika mazungumzo ya usuluhishi kwa madai ya kuhujumiwa na katibu wa jopo hilo ambaye ni Mtanzania, John Tesha kwa maelezo kuwa anavujisha taarifa muhimu za Malawi kwa Tanzania kabla ya Tanzania haijawasilisha taarifa zake kwa jopo hilo. Alisema kuwa tangu kuibuka kwa mgogoro huo, Malawi imekwenda kulalamika katika nchi za Uingereza, Marekani, Umoja wa Afrika (AU) na katika Jumuiya ya Maendeleo ya Nchi za Kusini mwa Afrika (Sadc).

Hata hivyo, baadaye Julai mwaka huu, Serikali ya Malawi ilitangaza kuwa itaendelea na mazungumzo na Tanzania kuhusu mpaka huku ikieleza kuwa viongozi wa Tanzania hawaelewi mipaka ndiyo maana wanapigania kuwa wao ni sehemu ya ziwa.

Waziri wa Habari wa Malawi, Moses Kunkuyu aliliambia Shirika la Utangazaji la Malawi (MBC) kuwa viongozi wote wa Tanzania wanadhani wanamiliki Ziwa Malawi (Nyasa) lakini watakuja kubaini baadaye kuwa hawana hata tone la umiliki.

TANZANIA YAPANDA KIWANGO CHA SOKA KATIKA VIWANGO VYA FIFA

$
0
0
Tanzania imepanda nafasi tano zaidi katika viwango vya Fifa, hivyo sasa kuwa ya 124, huku Zimbabwe ambayo ilitoka sare tasa na Taifa Stars katika mechi ya kirafiki iliyopigwa Uwanja wa Taifa mwezi huu, ikishuka kwa nafasi nne na sasa kuwa ya 106.

Zambia ambayo jana ilitoka sare ya bao 1-1 dhidi ya Kilimanjaro Stars ikiwa kama timu alikwa kwenye michuano ya Kombe la Chalenji iliyoanza juzi jijini Nairobi, Kenya, imeshuka nafasi tano na sasa ni ya 72 katika viwango hivyo.

Katika nchi za Ukanda huu wa Afrika Mashariki na Kati (Cecafa), Uganda ndiyo inayoshika nafasi ya juu ikiwa ya 86 duniani licha ya kushuka kwa nafasi moja mwezi huu.

Burundi ambayo imepanda kwa nafasi tisa, inashika nafasi ya pili kwa upande wa Cecafa ikiwa nafasi ya 112 duniani, ikifuatiwa na Kenya iliyopanda kwa nafasi moja na kuwa ya 117 duniani, huku Rwanda iliyopanda kwa nafasi mbili na kuwa ya 127, ikiburuza mkia kwa nchi za Afrika Mashariki na Kati.

Jirani zetu  DR Congo wanashika nafasi ya 84    baada ya kupanda kwa nafasi saba zaidi mwezi huu, huku kwa upande wa Afrika Ivory Coast ikiongoza na kwa dunia ikishika nafasi ya 17.

Ghana iliyoshuka kwa nafasi moja, inashika nafasi ya pili kwa Afrika huku kwa dunia ikiwa ya 24 na kwa bara hili ikifuatiwa na Algeria iliyopo nafasi ya 26 duniani baada ya kupanda nafasi sita. 

Hispania ndiyo kinara katika vingo hivyo ikifuatiwa na Ujerumani, Argentina, Colombia, Ureno, Uruguay, Italia, Switzerland    , Uholanzi, Brazil, Ubelgiji, Ugiriki na England     ikiwa ya 13 baada ya kushuka kwa nafasi tatu mwezi huu.

DIAMOND PLATINUMZ APIGWA MADONGO VIBAYA NA BABY MADAHA!

$
0
0
MSANII filamu na muziki wa kizazi kipya wa Tanzania Baby Joseph Madaha maarufu kwa jina la (Baby Madaha) amesema kwamba msanii mwenzake wa muziki nchini,Naseeb Abdul maarufu kwa jina la Diamond Platinumz si msanii bali ni mfanyabiashara.
Madaha amesema kwamba Diamond si mwanamuziki na kwamwe huwezi kumlinganisha na msanii kama Barnaba Boy, anayefanya muziki kama sanaa na kazi kulingana na kipaji chake na kwamba Diamond si msanii wa muziki bali ni msanii ngono anayefanya biashara ya muziki kupitia mapenzi.


Baby madaha ambaye hivi sasa yuko nchini Kenya kwa shuguli za muziki amesema kwamba, Diamond hajui kuimba na ndiyo maana amekuwa msanii wa matukio huku nyota yake ikiegemea kwenye mapenzi na wasichana wenye majina makubwa hususn wasanii.
Akizungumza na kandili yetu katika mahojiano maalum leo baby Madaha alisema kwamba, “Binafsi niliposikia kwamba Diamond anaumiza kichwa kunasa penzi la msanii Elizabeth Michael maarufu kwa jina la (Lulu) sikushangaa hata kidogo. kwa sababu nilitambua kwamba soko lake la muziki limeanza kushuka hivyo lazima atafute eneo lingine la kujiimarisha kibiashara, ili jina lake liendelee kuwika”.

“Siku wanawake maarufu nchini Tanzania watakapo jitambua na kuacha kulewa penzi la Diamond ndiyo itakayokuwa mwisho wa maisha yake kimuziki,kwa sababu hatakuwa na jipya na hivyo soko lake litaanza kuporomoka”alifafanua Baby Madaha.

JK AMUWEKA KITANZINI PROFESA KAPUYA

$
0
0
RAIS Jakaya Kikwete ameviagiza vyombo vya dola kuhakikisha vinamkamata mtu yeyote bila kujali cheo, atakayebainika kumbaka au kumuoa mwanafunzi wa shule.

Ametoa kauli hiyo huku aliyekuwa waziri wa wizara tofauti katika awamu mbalimbali za uongozi, Profesa Juma Kapuya, akiandamwa na tuhuma za kumbaka na kutishia kumuua binti, mwanafunzi mwenye umri wa miaka 16.

Ingawa Rais Kikwete hakutaja jina, lakini ni dhahiri kuwa kauli hiyo inamgusa pia Profesa Kapuya, Mbunge wa Urambo Magharibi (CCM).

Akizungumza kwa nyakati tofauti kwenye mikutano ya hadhara kwenye wilaya za Itilima, Meatu na Maswa mkoani Simiyu, Rais Kikwete alisema mtu anayefanya mapenzi na wanafunzi lazima akamatwe, ahojiwe na kufunguliwa mashitaka ya ubakaji na si vinginevyo.

“Kuna watu wanafanya mapenzi hadi na wanafunzi wakati sote tunajua ukimwi upo na hauna dawa na unaua. Kwa hiyo kila mmoja wetu awe makini kujikinga nao na tuepuke kuwaambukiza wengine,” alisisitiza Rais Kikwete.

Wakati Rais Kikwete akisisitiza wahalifu wa makosa ya kubaka na kuoa wanafunzi wachukuliwe hatua, polisi jijini Dar es Salaam wamekuwa wakisuasua kumchukulia hatua Profesa Kapuya licha ya binti anayedaiwa kumbaka, kufungua jalada namba OB/RB/21124/13 katika kituo cha Polisi Oysterbay, jijini Dar es Salaam, akidai kutishiwa kuuawa na mbunge huyo.

Kauli ya Rais Kikwete imeonyesha dhahiri kukerwa na moja ya ujumbe mfupi wa maneno wa simu ya mkononi kutoka kwenye simu inayodaiwa kumilikiwa na Profesa Kapuya kwenda kwa binti aliyebakwa, ambapo mbunge huyo alijigamba kwamba serikali haiwezi kumfanya chochote.

Ujumbe huo unasomeka hivi: “Mkiuawa itakuwa vizuri…itawapunguzia gharama za kuishi, usitake kugombana na serikali mtoto mdogo kama wewe, sisi ndiyo wenye nchi yetu, mwenye hilo gazeti ni Mbowe, sasa mwambieni nyumba ya kuishi si mmemuingizia hela leo?
 Mnatumika tu bure watu wanaingiza hela nyingi, ila mmenitibua lazima niwaue, wiki hii haitaisha, nitapiga kambi kote, jana si wamekuficha, tuone utalindwa milele, maana washatengeneza hela, lazima mvae sanda tu, hilo sio ombi ni wajibu wenu, mnajitia na nyie mafia watoto siyo, watoto wetu wanauza unga nani anawakamata? Nani atapingana  nasi.”

Habari kutoka Ikulu ya Rais Kikwete zinaeleza kuwa kiongozi huyo wa nchi amekerwa na kauli ya mbunge huyo wa Urambo Magharibi kwamba serikali haiwezi kumfanya jambo lolote.

Ni kutokana na kauli hiyo, mtoa taarifa wetu alisema rais aliagiza vyombo vya dola kufuatilia kwa karibu sakata hilo na kuhakikisha sheria inachukua mkondo wake.

Pamoja na msimamo wa Rais Kikwete na binti anayedaiwa kubakwa kuripoti polisi, Profesa Kapuya alifanikiwa kusafiri nje ya nchi huku polisi wakimshuhudia bila kumtia mbaroni.

Akiwa nje ya nchi, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kinondoni, Camilius Wambura, alikaririwa mara kadhaa akijigamba kuwa polisi inamsaka mbunge huyo na itamtia mbaroni mahala popote alipo.

Hata hivyo, Profesa Kapuya alirejea nchini juzi huku polisi wakimshuhudia bila kuchufkua hatua zozote.

Mwanafunzi huyo anadai kubakwa na Profesa Kapuya kwenye moja ya hoteli ya kitalii iliyoko jijini Dar es Salaam mwaka 2011, na kurudia tena kitendo hicho ndani ya ofisi yake katika Jengo la Biashara Complex lililoko Mwananyamala Juni 3, 2012 alipomuita kwenda kuchukua ada.

Source: Tanzania Daima

SABABU ZA KWANINI WABUNIFU WENGI WA KIUME WA MITINDO NI MASHOGA

$
0
0
Dolce-Gabbana-13
Bila shaka umeshajiuliza sana kwanini wabunifu wengi wa nguo wa kiume duniani ni mashoga. Haya ndio majibu:
Kwanza, tasnia ya mitindo (fashion industry) kiutamaduni imekuwa ikiwakubali zaidi mashoga wanaojulikana wazi (openly gay men) tofauti na fani zingine. Hata leo, ni changamoto kubwa kwa shoga kufikia level ya kuwa CEO ama Mkurugenzi kuliko wanaume wa kawaida.
Tofauti ni kwamba shoga kwenye fashion anaweza kuheshimika na kuenziwa kwenye fani hiyo na kufanikiwa binafsi na kifedha bila kudhihakiwa kama ambavyo anaweza kujikuta akifanyiwa kwenye fani zingine kama upolisi, jeshi na kwenye michezo.

Mifano mizuri inaweza kuwa kwa manguli wa fashion duniani kama Valentino Garavani, Yves Saint Laurent, Perry Ellis, Karl Lagerfeld, Alexander McQueen, Gianni Versace, Alexander Wang, Giorgio Armani, Marc Jacobs (Louis Vuitton) Domenico Dolce na Stefano Gabbana, Tom Ford na wengine. Na hata kwa Tanzania wapo wengi wanaofahamika wazi.
Karl Lagerfeld
Japokuwa mambo yanabadilika na hasa kwa nchi za wenzetu na kukubalika kwa watu wanaojihusisha na mapenzi ya jinsia moja, kumefanya mashoga nao wafanikiwe kwenye fani zinazotawaliwa na wanaume wa kawaida, lakini mifano ya dunia halisi inabaki michache na hasa tu kwenye majiji ama nchi ambazo mashoga na wasagaji wanapewa heshima sawa na wengine.

Pia kihistoria mashoga kwenye fashion walikuwa wakipewa kipaumbele zaidi kuliko wanawake. Ni Coco Chanel pekee ndio alikuwa miongoni mwa wanawake wachache waliofanikiwa kwenye kiwanda hicho kilichokuwa kikitawaliwa zaidi na mashoga Christian Dior na Cristobal Balenciaga. 
dolce-and-gabbanaDolce & Gabbana
Pili, inasemekana kuwa utamaduni wa ushoga huwapa nafasi watu hao uwezo wa ubunifu. Mashujaa kwenye jumuiya ya mashoga sio wachezaji wa soka ama wanajeshi- japo wapo. Lakini zaidi wapo kwenye muziki, uigizaji, utengezaji wa filamu, uandishi na sanaa zingine.
Hii ni kwasababu ya ukweli kwamba hizi ndio zilikuwa kazi ambazo mashoga waliweza kufanikiwa na kuendelea kuwa walivyo na kujivunia wanachokifanya. Uwezo wao wa ubinifu huongezeka na ile sense ya upekee ambayo mashoga huikuza ndani ya ulimwengu wa mapenzi ya jinsia mbili (heterosexual world).
1_(1)-7Tom Ford
Pointi ya msingi: Upenzi wa mashoga katika urembo, utanashati hauwezi kuelezeka. Inasemekana kuwa mwanaume anayebuni nguo nzuri kwa mwanamke aidha hutaka kuwa na mwanamke ama hutaka kuwa mwanamke’

Credit: Bongo 5

BREAKING NEWS:MSANII TID ATUPWA MAHABUSU KWA KOSA LA KUMPIGA DEMU WAKE

$
0
0
Msanii mahiri wa muziki wa kizazi kipya, Khaleed Mohamed 'TID' yupo mahabusu katika Kituo cha Polisi Oysterbay tangu jana usiku baada ya kukamatwa na polisi kwa tuhuma za kumpiga na kumjeruhi msichana anayedaiwa kuwa ni mpenzi wake,  Mariam Nnauye.

ALI KIBA "NI WAKATI WANGU WA KUAMKA KATIKA USINGIZII ULIYOJAA MAUMIVU NA DRAMA"

$
0
0
Hitmaker wa Cinderela na Dushelele, Ali Kiba ambaye leo anasherehekea birthday yake ya kutimiza umri wa miaka 27, amefunguka kwa kusema alikuwa kimya kutokana maisha ya muziki anayosema yamejaa drama, mateso na mambo mengi.
Akizungumza na Bongo5 leo, Ali Kiba amesema muziki wa Tanzania umejaa drama zilizomfanya atulie kidogo kutafakari na ili kusudi ajue jinsi ya kukabiliana na changamoto zake.
“Nashukuru Mungu nimetiza miaka 27, ni wakati wangu wa kuamka katika usingizi uliyojaa maumivu,drama na mambo mengi ambayo yameweza kunikalisha kimya. Sitaki kusema moja kwa moja kwamba nilikuwa kimya kwasababu maalum ambayo hata ingemkuta mwingine lazima angetulia,” Ali Kiba ameiambia Bongo5.
“Namalizia audio na video ambavo ni kali sana. Unajua nimekuwa nikipokea maoni mengi kwenye Twitter,Instagram na baadhi ya rafiki zangu wakinitaka niamke nifanye mambo. Kwahiyo nadhani muda wangu umefika wa kuamka na kufanya yale mambo ambayo nilikuwa nayafanya. Huu ni muda wa kutoka kutoka nilipokuwa.”
Happy Birthday Ali K and welcome back.
Credit-BONGO5.COM

MSHINDI WA EBSS ATAYETANGAZWA LEO..KAA TAYARI

$
0
0
Shindano la Epiq Bongo Star Search 2013 linafikia ukingoni leo usiku (November 30), ambapo mmoja kati ya washiriki watano walioingia fainali atatangazwa kuwa mshindi.
Kila mshiriki ana sifa za pekee ambazo zinamtofautisha na washiriki wengine na huenda ikamsaidia kuibuka mshindi.
Jina moja kati ya majina haya litapamba vichwa vya habari kesho.
Emmanuel Msuya:     
 Ni mshiriki namba 21 anaewakilisha kanda ya ziwa. Ndiye mshiriki pekee wa kiume ambaye ameingia fainali akiwa na uwezo mkubwa wa kuimba, lakini kitu kikubwa kinachomtofautisha na wenzake ni uwezo mkubwa alionao wa kupiga vyombo vya muziki kama kinanda na gitaa.
Msuya amerekodi wimbo unaoitwa ‘Leo Leo’ ambao ameufanya na Producer Sheddy Clever.
Elizabeth Mwakijambile:
Sifa moja kubwa aliyonayo inayomtofautisha na wenzake ni uwezo wake mkubwa wa kubadili sauti nakuimba vizuri sauti ya base (ya kiume), mbali na vocal ya nguvu ya kike aliyonayo.
Mara kwa mara anapoimba unaweza kuifananisha sauti yake na ya mwanamuziki mkongwe Stara Thomas.
Elizabeth amerekodi wimbo unaoitwa ‘Nifanyeje’ uliotayarishwa na producer Lamar wa Fish Crab.
Maina Thadei:
Uwezo mkubwa alionao wa kuimba nyimbo za taarab na miduara umemfanya kuwa na ladha tofauti na wenzake na kujikombea fans wengi wanaopenda aiana hiyo ya muziki.
Sio tu aina ya muziki anaochagua, lakini performance yake awapo jukwaani na mbwembwe za aina yake ni kitu ambacho kitakufanya umuangalie hadi anaposhuka jukwaani.
Maina amefanya wimbo wa mduara unaitwa ‘Panya Buku’, na ukisikiliza utahisi unasikiliza wimbo wa msanii mzoefu kwenye miondoko hiyo.
Viewing all 104809 articles
Browse latest View live




Latest Images