Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104789 articles
Browse latest View live

Ni kweli Clouds Media ndo Referee wa Game ya Muziki hapa Tanzania? DJ Choka Afunguka

$
0
0
Kumekuwa na malalamiko ya muda mrefu dhidi ya Clouds Media..Wasanii na watu mbalimbali wamekuwa wakiwatuhumu hawa jamaa kwa unyonyaji,ukandamizaji,uonezi n.k

Hata tumewahi kumsikia P funk kwa kauli yake akisema Clouds fm ndo chanzo cha marehemu Albert Mangwea kujiingiza kwenye matumizi ya madawa ya kulevya..
Ukiachia malalamiko mengi ya baadhi ya watu..Pia tumeshashuhudia Ugomvi mkubwa(ambao hata baadhi ya watu walidiriki kusema ulibeba sura ya kitaifa) kati ya clouds Fm na Mh. Sugu na hata ule wa Jay dee na Clouds Fm..Tuhuma zikiwa ni zilezile za uonezi,dhuluma,Ukandamizaji nk

Jana nilikuwa naangalia kipindi cha Mkasi..Dj Choka akiwa ndo mgeni mwalikwa...Ikumbukwe wakati wa ugomvi wa Clouds na Jay Dee..Dj Choka alikuwa anamsapoti Lady Jay dee...Moja ya swali aliloulizwa kwenye kipindi ni kuwa ule ugomvi ulimuathiri vipi...Dj Choka alisema moja ya athari aliyoipata ni Nyimbo zake alizokuwa akitengeneza(Megamix) kutopigwa katika radio hiyo..

KITU KILICHONISHANGAZA
Dj choka alienda mbali zaidi na kusema kitendo cha kazi zake kutopigwa katika radio hiyo kilimfanya ASITISHE KUTENGENEZA KAZI mpaka hapo atakapoweka mambo sawa..

Kauli hii ya dj choka na baadhi ya malalamiko ya muda mrefu ya baadhi ya watu na wasanii yakanipa shauku ya kutaka kujua kama kweli Clouds media ndo referee wa hii industry bongo..

Na mengine ninayojiuliza ni pamoja na
1-Tz kuna zaidi ya vituo 50 vya radio..kwann clouds?
2-Clouds media wana nguvu kiasi gani inayowafanya wasanii wengi waamini kuwa clouds ndo wameibeba future yao?
3-Hiyo nguvu hawa jamaa wanaitoa wapi?

By Kaboom-JF

Nay wa Mitego Afunguka 'Nina Mashaka Yule Sio Demu wa Ommy Dimpoz ni Gelesha tu'

$
0
0
Baada ya Ommy Dimpoz leo Kumuonyesha demu wake laivu kwenye mtandao wa Instagram kupangua dongo alilopigwa na Nay wa mitego kuwa yeye ni Shoga, Nay wa Mitego amerudi tena na kuandika haya hapa:

Breaking News: Lori la Mizigo Laangukia Dala Dala Barabara ya Mandela Maeneo ya Tabata..Angalia Picha

$
0
0

Lori la Mizigo lenye namba za usalili T 493 DBR limepiga mweleka na kuangukia basi la abiria aina ya Toyota DCM lenye namba za usajili T 104 BCT lifanyalo safari zake kati ya Gongo la Mboto mpaka Simu 200 mapema leo asubuhi katika ma kutano ya barabara ya Tabara na Mandela, jijini Dar es salaam. Hakuna aliepoteza maisha kwenye ajali hii ila kuna watu kadhaa wamejeruhiwa na kukimbizwa hospitali kwa matibabu.




Baada ya Ney wa Mitego Kuachia Wimbo Wake wa 'Shika Adabu yako', BASATA Imesema Wimbo Huo Haufai Katika Jamii

$
0
0
BASATA imetoa kauli hiyo kupitia Katibu mkuu mtendaji wa baraza hilo Godfrey Lebejo, alipokuwa akiongea katika kipindi cha Planet Bongo kinachorushwa na East Africa Radio, na kusema kwamba anaamini hata kwenye media wimbo huo hautapigwa.

“Ni wimbo ambao haufai na ni msanii ambaye I dont know hata unashindwa kumpima ana akli ya namna gani, au kwa nini ameamua kufanya hivyo, lakini watu kama hao kwenye jamii wapo, ni kazi ambayo haifai katika jamii kwa hiyo kwa mujibu wa sheria na kanuni zake, kitu ambacho hakifai kwenye jamii sio mpaka litolewe tamko kwamba wimbo umefungiwa, ni wimbo ambao haufai hata wanajamii wameona haufai, nadhani mtu mwenye akili timamu kiujumla anajua, najua kwenye media hauwezi kupigwa”, alisema Godfrey.

Katibu huyo wa BASATA amesema kinachotakiwa kwa Ney ni kujitambua kama yeye ni kioo cha jamii, na kwa kufanya vitendo kama hivyo si sahihi kwake kwani jamii inamtazama yeye.

“Anachofanya afikirie yeye ni nani na ana nafasi gani kwenye jamii, kwa sababu mtu anayefanya namna hii asidhani kama anamdhalilisha mtu, anajidhalilisha yeye mwenyewe kwa sababu mtu yeyote ambaye anatoa lugha chafu, anafanya vitendo vya aibu, asidhani kama anamdhalilisha mtu, kwa hiyo yeye mwenyewe ni kama hayawani fulani tu”, alisema Godfrey Lebejo.

Wanafunzi 21 Wafukuzwa Shule Kwa Muda Usiojulikana.......Kosa Lao Ni Kuvaa "YeboYebo", Mwalimu Wa Zamu Alizichukua na Kuzichoma Moto

$
0
0
Wanafunzi wapatao 21 wanaosoma Shule ya Msingi Kilambo cha Mkolechi, Kata ya Kala mwambao mwa Ziwa Tanganyika wilayani Nkasi, wamefukuzwa shule kwa muda usiojulikana kwa kuvaa viatu maarufu yeboyebo.

Imeelezwa kwamba yeboyebo hizo zilikusanywa na kuchomwa kwa kile kilichoelezwa kwamba ni kunatokana na waraka uliotolewa na Ofisa Elimu Halmashauri ya Nkasi (Msingi) ukipiga marufuku wanafunzi kuvaa aina hiyo ya viatu shuleni.

Hata hivyo,jana  Ofisa Elimu Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi (Msingi), Misana Kwangula, alikanusha kutoa waraka huo kwa shule hiyo.

“Sina taarifa rasmi ila jana jioni (Jumatatu) alinipigia simu mkazi mmoja akinitaarifu kwamba kuna mwalimu wa shule ya msingi Kilambo cha Mkolechi amechoma moto viatu vya wanafunzi kwa madai kuwa ofisa elimu (msingi) ametoa waraka kwamba wanafunzi hawatakiwi kuvaa yeboyebo shuleni…

“Hakuna waraka wala marufuku yoyote iliyotolewa, isitoshe sio sahihi hata kidogo wala sio kitu kizuri kuchoma vifaa walivyonavyo wanafunzi…. Sasa kama amewachomea wanafunzi hao viatu hivyo vya yeboyebo basi awanunulie viatu vya ngozi,” alisema Kwangula.

Mkasa huo wa wanafunzi hao kufukuzwa shule na kuchomewa yeboyebo walizovaa ulitokea juzi wakati wanafunzi hao walipofika shuleni wakiwa wamevaa viatu hivyo.

Inaelezwa kwamba mwalimu wa zamu, Baraka Mwakasege aliwazuia kuingia darasani, badala yake akawaamuru wavue viatu vyao.

Taarifa kutoka shuleni hapo zinaeleza kuwa, baada ya hatua hiyo, mwalimu huyo wa zamu alizikusanya yeboyebo na kuzitia kiberiti kisha akawafukuza wanafunzi hao kwa muda usiojulikana hadi wazazi na walezi watakapowanunulia viatu vya ngozi.

Mwalimu Mkuu wa shule hiyo, Posian Ally alikanusha kumtuma mwalimu wa zamu kuwafukuza wanafunzi hao shule kwa muda usiojulikana wala kuteketeza kwa moto yeboyebo zao.

 Alisema ataitisha kikao ili kujadili suala hilo na kwamba mwalimu huyo akibainika kutenda kosa hilo ataamriwa kuwanunulia watoto hao viatu vingine.

Wema Sepetu Afunguka Kuhusu ‘Range’ Yake, Aeleza Kilichotokea

$
0
0
Baada ya kuzagaa kwa taarifa katika mitandao ya kijamii pamoja na baadhi ya magazeti kuwa ile ‘Range Rover Evogue’ ya staa wa filamu, Wema Sepetu aliyojizawadi katika siku yake ya kuzaliwa imekamatwa na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), kwa madai alikwepa kulipa kodi, Wema amesema gari yake ipo nyumbani kwake.
Akizungumza na 255 katika kipindi cha XXL cha Clouds FM, Jumatatu hii, Wema alisema baada ya kukamatwa na (TRA) aliwaonyesha document za umiliki wa gari hiyo na baadae kumuachia.

“Gari ni langu, nimelinunua na kitu kilichobaki sasa hivi ni kulisajili tu, lipate namba za Tanzania,” alisema.
“Sasa hivi TRA wapo kila sehemu hata sasa hivi ninapoongea rafiki yangu amekamatwa na gari ina namba za Afrika Kusini. Kwahiyo sasa hivi TRA wanafanya kazi, jamani Magufuli sasa hivi ana Magufulika, kwahiyo tuache wafanye kazi zao. Yeah walinifuatilia, kwahiyo wanafuatilia kila gari ambalo lina namba ngeni. Kwahiyo ukiwa na document za kumiliki hawakusumbui, hapa tunapo ongea gari yangu ipo nyumbani kwangu, walihitaji document nimewapatia ndiyo maana wameniachia.,” alieleza Wema.

Dk Phillip Mpango Akataa Kuwa Waziri OmbaOmba......Asema Serikali Haipo Tayari Kukubali Ndoa Za Mashoga Kisa Misaada Ya Wahisani

$
0
0
WAZIRI wa Fedha na Mipango, Dk Phillip Mpango amesema hatua ya Serikali ya kukusanya kodi kwa nguvu kwa baadhi ya wafanyabiashara waliotorosha makontena bila kulipiwa ushuru, haikuwa lengo la kumkomoa mtu, bali ililenga kukusanya fedha za Serikali yenye lengo la kuifanya nchi iache utegemezi wa wahisani.

Waziri huyo ambaye jana alikutana na makundi mbalimbali ya wafanyabiashara ofisini kwake Dar es Salaam, alisema yeye kama waziri wa fedha asingependa kuwa waziri ombaomba kwa wahisani, ambao alidai baadhi yao wana masharti magumu, ambayo hayatekelezeki kwa maadili ya Watanzania.

“Nimewasindikiza wenzangu huko nje kuomba fedha sasa nimechoka, nataka kutembea kifua mbele, maana wana masharti magumu, wengine wanataka turuhusu homosexual (ndoa za jinsia moja), masharti haya kwa kweli yanakera sana,” alisema Dk Mpango ambaye katika serikali iliyopita alikuwa Katibu Mtendaji wa Tume ya Mipango.

Dk Mpango aliongeza kuwa ili nchi isonge mbele, ni lazima ikusanye kodi ya kutosha; na jana aliahidi kuchukua hatua kadhaa, zitakazoiwezesha sekta binafsi kuwa mhimili wa kuimarisha uchumi wa nchi ili kufikia malengo ya kuifanya Tanzania kuwa nchi yenye kipato cha kati.

Alisema Rais John Magufuli ni kiongozi ambaye akilala na kuamka, anawaza namna ambavyo atawahudumia wananchi wake, ambao wengi wako kwenye dimbwi la umaskini.

Alisema Rais atafanikiwa tu, pale Serikali yake itakusanya kodi ya kutosha na kuwahudumia wananchi hao.

“Kuna minong’ono kwamba eti Serikali ya Awamu ya Tano inawanyanyasa wafanyabiashara wakubwa na kwamba hatua tulizochukua kukusanya kodi, ililenga kuwadhalilisha baadhi ya wafanyabiashara, hii sio kweli kabisa,” alisema Dk Mpango.

Dk Mpango alisema Serikali ya Awamu ya Tano, inatambua umuhimu wa wafanyabiashara, hivyo wizara yake itakuwa ya mwisho kuchukua hatua za kuwanyanyasa.

“Nawahakikishia kwamba nina dhamira ya dhati ya kufanya kazi kwa kushirikiana na ninyi wafanyabiashara wakubwa na wadogo ili tutimize ndoto ya Rais,” alisema.

Alisema serikali yoyote duniani ni lazima ikusanye kodi, hivyo aliwahakikishia wafanyabiashara hao kuwa kama bado kuna wafanyabiashara wanaokwepa au hawataki kulipa kodi kwa mujibu wa sheria, serikali haitakuwa tayari kuwavumilia.

Dk Mpango alisema idadi ya watu wanaolipa kodi kwa sasa nchini bado wachache, hivyo aliwaagiza wafanyabiashara wote kujisajili wapatiwe Namba ya Utambulisho wa Mlipa Kodi (TIN).

Pia, aliwataka waache tabia ya kufanya udanganyifu kwa kuwa na vitabu vingi vya utunzaji wa kumbukumbu za biashara. Aliwaagiza kuhakikisha wanatoa stakabadhi na suala hilo lisiwe hiyari.

“Tunajua kwamba mnatoa vitisho kwa wanunuzi kuwa kama wanataka risiti bei ni ya juu, hiki mnachofanya ni hatari kwa nchi,” alisema na kuwataka wote watumie mashine za EFD na serikali inaendelea na mpango wa kununua zingine ili wagawiwe bure.

Aliwataka kutoa taarifa kwa Kamishna Mkuu wa TRA, kama kuna mfanyakazi wa Mamlaka ya Mapato (TRA) au wa Halmashauri ya Wilaya, ambaye atadai hongo au atawanyanyasa wakati wa kudai kodi.

Katika kutekeleza hilo, aliwapatia namba zake pamoja na za Kamishna na kuwataka waache tabia ya kutoa rushwa ili wasilipe kodi.

 Dk Mpango alisema baada ya wafanyabiashara kufanya kikao na Rais Magufuli, Serikali imeunda kikosi kazi kushughulikia kero zote, zilizotolewa na Baraza la Biashara na mojawapo ni kufuta utiriri wa kodi ili kuwapa wepesi wawekezaji kufanya biashara nchini na kumpungumzia mzigo mkulima.

Wengi hawajui, Diamond ni rapper – Producer Hermy B

$
0
0
Producer na CEO wa Bhitz Music Group, Hermy B amewataja wasanii anaotamani kufanya nao kazi, akiwemo Diamond.

Akizungumza na 255 katika kipindi cha XXL cha Clouds FM Jumatatu hii, Hermy B alisema Maua Sama, Ben Pol pamoja na Diamond ni miongoni mwa wasanii anaotamani kufanya nao kazi.

“Sijawahi kufanya kazi na Maua Sama, lakini natamani kufanya kazi na Maua Sama kutokana na ubora wa sauti yake. Kwahiyo Maua Sama ni mmoja kati ya wasanii ambao naimani naye. Pia natamani kufanya kazi na Ben Pol, sijawahi kufanya kazi na Ben Pol.,” alisema Hermy B

Aliongeza, “Pia natamani kufanya kazi na Diamond kutokana na sauti yake na jinsi ambavyo anavyoweza kuitwist. Halafu one thing ni kwamba Diamond ana element ambayo watu wengi hawaijui, Diamond ni rapper.”

UFISADI ATCL: Mkurugenzi wa Fedha, Steven Kasubi Asimamishwa Kazi

$
0
0
SERIKANI imebaini wizi wa takribani shilingi Milioni 715 katika Shirika la Ndege Tanzania (ATCL) kupitia kampuni ya Wakala wa ukatishaji tiketi ya Salama World Travel iliyopo visiwa vya Komoro.

Akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam ,Waziri wa Ujenzi,Uchukuzi na Mawasiliano Prof.Makame Mbarawa ameeleza kuwa wizi huo umefanywa kwa kushirikiana na wafanyakazi wa shirika hilo.

“Kufuatia upotevu huo Serikali imechukua hatua thabiti ikiwemo kumsimamisha kazi Mkurugenzi wa Fedha wa ATCL Bw.Steven Kasubi ili kupisha uchunguzi utakaofanywa na kikosi cha polisi kitengo cha usalama mtandaoni ili kubaini mtandao mzima uliohusika ” alisema Prof.Mbarawa.

Aidha aliongeza kuwa kwa utaratibu wa kawaida wa shirika hilo wakala anapewa ruhusa ya kuuza tiketi za ndege kuanzia kiasi cha shilingi milioni 15 tu na pale anapomaliza mauzo anarudisha fedha kwa shirika na baadaye kupewa ruhusa tena.

Prof.Mbarawa anasema kwa sasa wameanza na shirika la Ndege la Tanzania kwa kwa lengo la kulifufua kwa kununua ndege mpya na kuwa na wafanyakazi wachapakazi na waadilifu.

“Siku mbili zilizopita nilifanikiwa kukutana na menejimenti ya ATCL na kubaini mapungufu mengi na hivyo kuamua kuyafanyia kazi kwa kuhakikisha shirika hii linarudi kutenda kazi kwa udhabiti kwa kuwashughuikia wale wote wanaoenda kinyume na maadili ya utumishi wa umma” alisema Prof.Mbarawa.

Vilevile aliongeza kuwa Serikali imemuagiza Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali(CAG) kufanya uchunguzi kwa mawakala wengine wote wa Shirika hilo kubaini kama fedha za uuzaji wa tiketi hizo zinarudishwa kama inavyotakiwa.

Makampuni 210 ya Clearing & Forwarding yasimamishwa kutoa huduma na TPA

$
0
0
Makampuni yafuatayo ya kupitisha mizigo bandarini (Clearing and Forwarding Agents) yamezuiwa kufanya kazi katika bandari zote zinazomilikiwa na TPA pamoja na washirika wake (ICS’s, CF’s na TICTS) tangu 9 Februari 2016. Uamuzi huo umechukuliwa kwa sababu ya kushindwa kuwasilisha vielelezo vya malipo, kama walivyotakiwa na mamlaka ya bandari. Pia wameshindwa kufika bandarini kupokea nyaraka kadhaa kuhusiana na madeni wanayodaiwa na TPA.

Orodha ya Mawakala wa kupitisha Mizigo bandarini (CLEARING & FORWARDING), Waliosimamishwa kutoa huduma katika Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA) Kuanzia Februari 9, 2016 ni;

1. 21st Century Freight Forwarders
2. Aristepro Investment Co. Ltd
3. Ace Exim
4. Ally Vay C & F Agency
5. A & D Holdings Ltd
6 A & G Holdings Ltd
7.ACW Investment Ltd
8.Afro Centre (T) Ltd
9.Allmol trading
10.Amico Trading Ltd
11.Avow Holding (T) Ltd
12.Afritel Systems Ltd
13.Afrovision International Co. Ltd
14.Arusha Cargo Clearing & Forwarding Ltd
15.Arusha Freight Transport Agency
16.Bakhresa Food Products Ltd
17.Boston Forwarders Ltd
18.Babylon Freight Ltd
19.Beam Tanzania Ltd
20.Best Ocean Air Ltd
21.Break Through Holdings Ltd
22.Business Service Promotion Ltd
23.B & J Co. Ltd
24.BNM Co. Ltd
25.Boneste General Enterprises Ltd
26.Blue Light Investment Ltd
27.BN Metro ( E.A) Ltd
28.Cad Mulungu Co. Ltd
29.Capital Cargo Removers Ltd
30.Cargo Stars Ltd
31.Car Freight Station ICDV
32.Clear Services Tanzania Ltd
33.Clampek (T) Ltd
34.Classic Choices Investment Ltd
35.Continetal Reliable Clearing Ltd
36.Conanza Express Ltd
37.Cos Africa Logistics Ltd
38.Cosmos Haulage Co. Ltd
39.Chissel C & F Ltd
40.Cusna Investment Ltd
41.Daffor Enterprises Ltd
42.Dynamic Freight Forwarders Ltd
43.Datar & Co. Ltd
44.Dar Es Salaam Global Access Ltd
45.Dar Coast Enterprises Ltd
46.Denilo Freight Ltd
47.Destination Tanzania Cargo Logistics
48.Divine Cargo Services Ltd
49.Dow Elef Ltd
50.Dolusi (T) Ltd
51.Dolphin Sea And Air Ltd
52.E-3 Freight Co. Ltd
53.Eagle Tallons (T) Ltd
54.Econ Consult & Trading Co. Ltd
55.Eltex Investment Ltd
56.Edams Holdings Ltd
57.Efficient Freighters (T) Ltd
58.Equity Agencies
59.Expro Freight Services Ltd
60.Evergreen General Logistics (T) Ltd
61.Enterprises Logistics Ltd
62.East African Fossils Fossils Ltd
63.Fedrol Cargo Ltd
64.Full Cargo Support Ltd
65.Freight 24/7 Ltd
66.Favre Freight Forwarders Ltd
67.Freight Forwarders (T) Ltd
68.Freedom Freight Forwarders Ltd
69.Fifa & Flow Co. Ltd
70.F.K. Farms & Co. Ltd
71.First Choice Clearing & Forwarding Ltd
72.Freight Works Ltd
73.Frafza Freight Forwarders Ltd
74.General Envirocare (T) Ltd
75.General Shami Investment Co. Ltd
76.Glory Freight Ltd
77.Grand Movers Co. Ltd
78.Gwiholoto Impex Ltd
79.GS InterTrade Co. Ltd
80.Hamymack Trading Co. Ltd
81.Hadolin (T) Ltd
82.Hasa Customs Agency (T) Ltd
83.Horizon Freight Forwarders Ltd
84.Hodari Freight Ltd
85.Hardmark Logistics Ltd
86.HK Freight Forwarders Ltd
87.Hotreef Trading Ltd
88.Home Base Tanzania Ltd
89.Ilemela Investment Ltd
90.Impact Trading And Investment Co. Ltd
91.Jambo Freight Ltd
92.Jas Express Ltd
93.Jamaap Co. Ltd
94.Joe Ocean C & F Ltd
95.Juhudi Clearing And Forwarding
96.Juni Trust Freight Tz Ltd
97.Kas Freight Ltd
98.Kahe International Ltd
99.Kassam freight Ltd
100.Kiwaepa International Co. Ltd
101.Khan's C & F Ltd
102.Kams Trading Ltd
103.Kings Freight (T) Ltd
104.K & K Cargo Logistics
105.K&K Company Ltd
106.Kadengere Traders Ltd
107.Korufreight (T) Ltd
108.Lawia (T) Ltd
109.Laz ltd
110.Lesidi General Cargo Ltd
111.Liberal International Ltd
112.LCR Limited
113.LDV Macro Investment Ltd
114.Logistics Efficiency Co. Ltd
115.Lesheti Trading Ltd
116.Lichinga (T) Ltd
117.Mambona freight Ltd
118.Mamba Enterprises Ltd
119.Maxima C & F Ltd
120.Mwaya C & F
121.Marine Air Freight Ltd
122.Maritime Shipping Consultants
123.Mechanised Cargo Systems
124.METL
125.Metrologic C &f F Ltd
126.Minex Logistics Ltd
127.Mpepa Traders Co. Ltd
128.Mogo Forwarders Ltd
129.Mokha Agency Co. Ltd
130.Mwagy Investment Ltd
131.Naito General Supplies Ltd
132.Nal Business Co. Ltd
133.Nemarts Limited
134.Neighbour Trading Co . Ltd
135.Ngaramau Contractors Ltd
136.Nutricare (T) Ltd
137.Nkira Trading Ltd
138.NM Freight Ltd
139.Overseas Hi-Tech Industrial Ltd
140.Orbit Freight Ltd
141.Pasiwa Cargo Ltd
142.P & D Freight Forwarders Ltd
143.Platinum Trading Co. Ltd
144.Palm Swift Tz Ltd
145.Quality Logistics Ltd
146.Runner Co. Ltd
147.Rungwe Trading Ltd
148.Reindeer Investment Ltd
149.Regent (T) Ltd
150.Rukwi Holdings Ltd
151.Royal Freight Ltd
152.Ruma International Ltd
153.R.H.G General Traders Ltd
154.Sky Land Across Freight
155.Sai C & F Ltd
156.Shift Cargo Ltd
157.Sachsen Spedition Ltd
158.Sahara Desert Freighters
159.Sahuse Services & Supplies Ltd
160.Selwek & Solar Forwarders Ltd
161.Sami Agency Ltd
162.Sahe C & F Ltd
163.Sangare Express Ltd
164.Sea Bridge Co. Ltd
165.Sea Air Forwarders Ltd
166.Sea Africa Cargo Freight Ltd
167.Scol (T) Ltd
168.Shakura Trading Services
169.Space Land Logistics
170.Senkondos Import & Export Ltd
171.Smith Freight Forwarders Ltd
172.Sino Logistics Ltd
173.Scanland Shipping Consultants Ltd
174.SpacelandLogistics Ltd
175.Sachsen Spedition Ltd
176.Swiftways International Ltd
177.Stepio Freight Ltd
178.Switch Trade Ltd
179.Sun Fresh Co .Ltd
180.StarVision International Ltd
181.Tanga Cargo & Trust Ltd
182.Trade Waves Investment Co. Ltd
183.Transit Ltd
184.Trident Clearing Ltd
185.Team Freight
186.Trans Net Freighters
187.Three way Shipping Service Ltd
188.Trans Pack Tanzania Ltd
189.Trans African Forwarders Ltd
190.TransBarriers Freight Ltd
191.Transit Ltd
192.Tripple D
193.Twende Freight Forwarders Ltd
194.Ujiji C & F Ltd
195.United Youth Shipping Co. Ltd
196.United family Co. Ltd
197.Uwanji General Tradersb Ltd
198.Uprising C & F Ltd
199.Upland Freight Ltd
200.Vigu Trading Ltd
201.Vamwe Investment Co. Ltd
202.Viccom resources co ltd
203.Way Logistics Ltd
204.West Freight Forwarders
205.Wings Wheels Co. Ltd
206.Walmax Freight Forwarders Co. Ltd
207.Xpress Maritime Agency Co. Ltd
208.Zappex International Ltd
209.Zaihuse C & F Ltd
210.Zzoikos (T) Ltd

F.J. Liundi
For : Port Manager
Dar es Port.

Ikulu yatoa Sababu ya Rais Kutohudhuria Sherehe ya Mabalozi

$
0
0
Akiongea na gazeti la Mtanzania, Kaimu Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais Ikulu, bwana Gerson Msigwa amesema rais hakuhudhuria sherehe hiyo kwasababu alikuwa nje ya Dar-es-salaam.

Hapa nanukuu baadhi tu ya maneno machache aliyoyasema: "Rais alikuwa nje ya Dar-es-salaam na ndio maana akawakilishwa na Waziri wa Mambo ya Nje na sherry Party ni hafla tu ya kutakiana heri ya mwaka mpya.....".

========

Sababu za Magufuli kutohudhuria sherehe ya mabalozi

HATUA ya kutoonekana kwa Rais Dk. John Magufuli katika sherehe ya kutakiana heri ya mwaka mpya na wanadiplomasia (Sherry Party), imezua mjadala mzito miongoni mwa Watanzania.

Kutokana na kutokuwapo kwa rais katika sherehe hiyo iliyofanyika juzi Ikulu jijini Dar es Salaam, Waziri wa Mambo ya Nje, Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Kikanda na Kimataifa, Balozi Dk. Augustine Mahiga, alimwakilisha na alisoma hotuba kwa niaba yake.

Akizungumza na MTANZANIA Dar es Salaam jana, Kaimu Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais Ikulu, Gerson Msigwa, alisema ilikuwa ni sahihi kwa Rais Magufuli kuwakilishwa na Waziri Mahiga katika sherehe hiyo.

Alisema hatua hiyo ilitokana na Rais Magufuli kuwa nje ya Dar es Salaam, ambapo asipokuwapo huwakilishwa na Makamu wa Rais, Waziri Mkuu au Waziri wa Mambo ya Nje.

“Rais alikuwa nje ya Dar es Salaam ndiyo maana akawakilishwa na Waziri wa Mambo ya Nje na ‘Sherry Party’ ni hafla ya kutakiana heri ya mwaka mpya na wanadiplomasia.

“Na Cocktail (mchapalo) hufanyika kila mwaka na huwa ya muda mfupi ambao wanadiplomasia husikiliza hotuba ya rais kuhusu sera yake ya mambo ya nje. Hivyo kwa kuwa Rais Magufuli hakuwepo, hotuba yake ilisomwa na Waziri Mahiga jambo ambalo ni sahihi na hakuna kosa lolote,” alisema Msigwa.

Akizungumza suala la mabalozi hao kuwekewa makatarasi chini, alisema si karatasi za kawaida, huwa zimeandikwa jina la balozi au nchi anayowakilisha ambapo hutakiwa kusimama katika eneo lake husika alilopangiwa.

“Suala la kuwekewa karatasi mbele si geni, huwa linafanyika kila mwaka na pindi zinapowekwa huandikwa jina na cheo cha mwanadiplomasia anayewakilisha nchi husika, na baada ya kusomwa hotuba hupita mbele na kumpa mkono kiongozi.

“Na kwa jana (juzi), aliyesimama mbele alikuwa ni Mheshimiwa Waziri Dk. Mahiga, naibu waziri pamoja na mkuu wa itifaki, na walifanya hivyo kwa sababu walikuwa wakimwakilisha Rais Magufuli katika hafla,” alisema.

Balozi Cisco atoa maoni

Aliyewahi kuwa Balozi wa Tanzania katika nchi za Falme za Kiarabu, Abdul Cisco Mtiro, alisema alichofanya Rais Magufuli kutuma mwakilishi katika hafla hiyo haijawahi kutokea tangu Serikali ya awamu ya kwanza hadi ya nne.

“Ni kweli Rais Magufuli ndiye kwa mara ya kwanza amefanya kitu tofauti na marais wote waliomtangulia kutuma mtu kwa niaba yake, hiyo haijawahi kutokea,” alisema Balozi Mtiro.

Balozi Mtiro ambaye ni mwanadipomasia aliyebobea, alisema hafla hizo ambazo hufanyika kila mwaka humwezesha rais husika kutoa mwelekeo wa nchi yake katika sera ya Serikali kuhusu mambo ya nje.

“Sherry Party ni Standard Party na kwa kawaida huchukua dakika zisizozidi 30 ambapo rais hutoa ‘speech’ (hotuba) ya dakika tano kuelezea mwelekeo wa sera ya nchi yake kuhusu mambo ya nje na baadaye hupeana mkono na mabalozi na kuondoka.

“Sherry Party ni hafla ambazo hufanyika kila mwaka ambapo ambapo rais anakutana na mabalozi, hakuna viti, ndiyo maana uliona vile vikaratasi vya majina ya mabalozi kuwekwa pale ingawa utaratibu ni kwamba mabalozi wenyewe wanajua utaratibu kwamba nani alitangulia kutoa hati za utambulisho katika lile kundi, ndiyo wanafuata wengine kadiri walivyoingia nchini.

“Ni utamaduni wa nchi za Jumuiya ya Madola, na Uingereza ambako ndiko tulichukua utamaduni huo, zamani ilitumika soda na maji, lakini miaka ya karibuni vinawekwa pia vinywaji vikali,” alisema.

PROFESA LIPUMBA

Akizungumza hali hiyo katika moja za makala zake, Mwenyekiti mstaafu wa Chama cha Wananchi (CUF), Profesa Ibrahim Lipumba, alisema mabalozi wengi waliopo hapa nchini na ambao nchi zao zinaisaidia Tanzania wameomba fursa ya kukutana na Rais Magufuli lakini wamekwama.

Kutokana na hali hiyo alisema kiongozi huyo wa nchi ameendelea kuwabeza mabalozi waliopo hapa nchini kwa kutohudhuria sherehe maalumu ‘Sherry Party’ ambayo rais huwaandalia mabalozi na kuwaeleza sera na malengo yake ya kuboresha uhusiano wa Tanzania na mataifa ya nje.

“Katika Sherry Party ya mwaka huu, rais kawakilishwa na Dk. Mahiga, Waziri wa Mambo ya Nje. Kwa kuwa Rais Magufuli ndiyo kaingia madarakani, mabalozi wengi walikuwa na shauku ya kumuona na kumsikiliza,” alisema.

HOTUBA YA MAGUFULI

Katika hotuba yake kwa wanadiplomasia hao iliyosomwa na Waziri Mahiga juzi, Rais Magufuli alisema hatua ya kurudia uchaguzi Zanzibar ndiyo njia sahihi ya kutatua mgogoro wa kisiasa visiwani humo.

Alisema kufanyika uchaguzi huo wa marudio kutasaidia kuondoa mvutano wa kisiasa uliopo na kusisitiza kuwa mazungumzo kati ya vyama vya siasa yaliyoanza Novemba mwaka jana, hayakufikia mwafaka wa namna ya kutatua tatizo hilo.

“Zanzibar ina mfumo wake wa siasa, ina Katiba na ina Tume Huru ya Uchaguzi. Hatua ya kufanya uchaguzi ndiyo njia sahihi katika hali ya sasa katika kumaliza tatizo hilo.

“Chama kikuu cha upinzani (CUF) wanadai wameshinda, lakini chama tawala na vyama vingine vinaona haja ya kufanya uchaguzi wa marudio ili kuondoa kasoro,” alisema Dk. Magufuli.

Alisema mlango wa mazungumzo juu ya namna ya kufanya uchaguzi wa marudio kuwa huru na haki na kufuata taratibu za kimataifa uko wazi na kuwa ni imani yake nchi marafiki wa Zanzibar na Tanzania wataunga mkono juhudi hizo.

“Kama ilivyo kwa Watanzania wengi wanavyoona, njia ya kuthibitisha ushindi ni boksi la kura na kukataa kushiriki ni kukataa kufikia mwafaka na Serikali na kujinyima haki ya miaka mitano ijayo,” alisema Rais Magufuli.

Alisema bado kuna siku 40 ambazo zinatosha kuwa na mazungumzo ya kuja na suluhisho la tatizo hilo.

Zanzibar inatarajia kufanya uchaguzi wa marudio Machi 20 kutokana na uliofanyika Oktoba 25, mwaka jana kufutwa na Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC).

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa mabalozi waliopo nchini, ambaye pia ni Balozi wa Zimbabwe, Edzai Chimonyo, alisema mgogoro wa Zanzibar unaweza kumalizwa kwa mazungumzo ya pamoja visiwani humo.

Alisema wananchi wa Zanzibar wanapaswa kuweka tofauti zao pembeni na kujali masilahi ya nchi kwa masilahi yao na taifa lao.

Chanzo: Mtanzania

Muhimbuli Hali Bado Tata Wagonjwa Wanalala Chini Japo Tuliambiwa Vitanda Vimenunuliwa...Nini Tatizo?

$
0
0
Picha ya Ziara ya Kwanza
Leo ukifuatilia taarifa ya habari Magufuli katembelea tena Muhimbili kwa kustukiza
kakuta matatizo tele hasa amewakuta wamama waki share vitanda hadi watu watano
na wengine wakilala chini.....

Utakumbuka few months ago tulitangaziwa kuwa baada ya Magufuli kwenda Muhimbili
vitanda vilipelekwa hadi vikakosa wagonjwa
kuna picha zilisambazwa paka kalalia kitanda kipya Muhimbili
na kwamba sasa mambo ni tofauti kabisa...vitanda tele na kila kitu saafi

Sasa binafsi siamini kabisa Muhimbili imewahi kuwa safi na matatizo yakaisha
ambacho najiuliza why 'maigizo yale ya kuwa mambo ni saafi' yaliruhusiwa
kuendelea ?

why sisi wananchi na waandishi wa habari hatukupinga kabisa habari za kuwa
mambo ni saafi muhimbili?
why habari ya leo iwe kama habari mpya
while in reality watu wameendelea kulala chini tu kama zamani?

Inawezekana kabisa tatizo haliko kwa wanasiasa?

tatizo liko kwetu wananchi na hasa media?
tumeletewa 'sanaa tukaishangilia huku ukweli tunaujua'?
sababu muhimbili hali yake sio siri
lakini tulipoambiwa mambo sasa ni saafi tuliruka ruka na kushangilia...
huku kiukweli hali ni ile ile tu.....

Na leo tena wananchi wamemlilia tena Magufuli bila kujiuliza
ni kweli Magufuli hali iliyopo haijui?si alikwenda juzi tu hapo hapo Muhimbili?
au haya matatizo ni mapya kabisa?

Rais Magufuli akumbana na kero lukuki Muhimbili. Zisome kero hizo hapa

$
0
0
Rais Magufuli ametembelea kwa ghafla wodi ya Wazazi katika Hospitali ya Taifa Muhimbili Jijini Dar es salaam, na kujionea hali ya msongamano mkubwa wa wazazi uliosababishwa na uhaba wa vitanda na nafasi finyu katika wodi hiyo.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli ametembelea kwa ghafla wodi ya Wazazi katika Hospitali ya Taifa Muhimbili Jijini Dar es salaam, na kujionea hali ya msongamano mkubwa wa wazazi uliosababishwa na uhaba wa vitanda na nafasi finyu katika wodi hiyo.

Rais Magufuli aliyekuwa akitoka katika Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete alikokwenda kumuona na kumjulia hali Mufti wa Tanzania Sheikh Abubakar Zubery Bin Ally, amelazimika kwenda katika wodi hiyo baada ya msafara wake kusimamishwa na kundi la akina mama, waliomtaka kwenda katika wodi ya wazazi ili akajionee jinsi wazazi wanavyokabiliwa na kero mbalimbali ikiwemo ya kulala chini kutokana na kukosa vitanda.

Baada ya kujionea mwenyewe kero ya msongamano na kuzungumza baadhi wazazi waliojifungua, Rais Magufuli amewaahidi wazazi hao kuwa atashughulikia kero alizozishuhudia.
"Nimeiona hali halisi mimi mwenyewe, watu wanapata shida, watu wana mateso, na ndio maana nimeamua kuja kwa makusudi, sikuomba ruhusa ili nijionee hali ilivyo, nimejifunza mengi, ninayabeba na nitajua namna ya kuyatatua" Alisema Rais Magufuli.
Kabla ya kutembelea wodi ya wazazi, Dkt. Magufuli amemjulia hali Mufti wa Tanzania Sheikh Abubakar Zubery Ally aliyelazwa katika Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete ambapo amempa pole na kumuombea apone haraka.

Pamoja na kupokea pole ya Rais, Mufti wa Tanzania ameongoza dua ya kumuombea heri Rais Magufuli ili aweze kutekeleza vyema majukumu yake katika kuwahudumia watanzania.
Dua kama hiyo pia imefanywa na wananchi wengine waliokuwa wakimsubiri nje ya majengo ya Hospitali ya Taifa Muhimbili ambapo katika dua hiyo wamemuomba Mwenyezi Mungu kumlinda na kumuongoza katika majukumu yake ya kuiongoza nchi.

"Mwenyezi Mungu mbariki Rais wetu, mpe hekima, busara na upendo katika kazi zake za kuiongoza nchi hii ili watanzania wote wanufaike" ilisema sehemu ya dua hiyo iliyoongozwa na mmoja wa akina Mama.

FAMILIA ya Mwanamuziki Diamond Platnumz ilivyotengeneza Mamilion ya Pesa Kutoka Vodacom

$
0
0
FAMILIA ya mkali wa Muziki wa Kizazi Kipya Bongo, Nasibu Abdul ‘Diamond Platinumz’ imelamba mamilioni ya shilingi kufuatia mkataba walioingia hivi majuzi na kampuni ya simu ya mkononi ya Vodacom, Risasi Mchanganyiko lina ripoti kamili.

Kwa mujibu wa chanzo kilicho ndani ya kampuni hiyo yenye mtandao mkubwa zaidi wa simu nchini, Diamond na familia yake inayowahusisha mama yake mzazi, mzazi mwenzake Zarinah Hassan na mtoto wao Tiffah, wamepewa kiasi cha shilingi milioni 700.

“Mimi nipo hapa, mkataba umefanywa kwa usiri mkubwa na unajua haya mambo yanakuwaga kisheria zaidi, lakini dogo (Diamond) kalamba siyo chini ya milioni 700, nadhani ndiyo msanii wa kwanza Bongo kupata mkwanja wa maana kwenye haya matangazo ya biashara,” kilisema chanzo hicho.

Wakati chanzo hicho kikitoa madai hayo, katika baadhi ya mitandao ya kijamii, kiasi cha fedha kinachotajwa kutolewa katika mkataba huo ni kiasi cha dola 650,000.
Gazeti hili lilimtafuta Meneja Uhusiano wa Vodacom Tanzania, Matina Nkurlu ili azungumzie madai hayo ikiwemo kiasi halisi ambacho Diamond alipewa.

“Ni kweli kuwa ni jambo jema kama wasanii wachanga na wengine wakijua kiasi halisi cha fedha ambacho Diamond amepewa, ila suala hili lipo kisheria, nitakuwa nimevunja sheria endapo nitasema, kifupi ni kwamba amesaini mkataba mnono na kama Vodacom, tutaendelea kuwasapoti wasanii wetu wa ndani na maisha yao yataendelea kuwa murua.
“Tunachoomba ni kwa wasanii wetu kujituma zaidi na kuwa kioo cha jamii kwa kuwawakilisha Watanzania kwa uweledi,” alisema.

Alisema Vodacom imeingia mkataba wa mwaka mmoja na Diamond, lakini milango ipo wazi kwake kuweza kusaini upya baada ya huu kumalizika. Aidha, alisema msanii huyo ndiye pekee aliyesainishwa na kampuni yao, lakini Aprili mwaka huu, ambao ni mwezi wa kuanza kwa bajeti yao mpya, wanategemea kuwasainisha wasanii zaidi wa Bongo Fleva.

Kwa upande wake, mmoja wa mameneja wa Diamond, Babu Tale, alikiri msanii wake kupata mkataba mnono kuliko aliowahi kupata msanii yeyote kabla, lakini hata hivyo hana mamlaka ya kutaja kiasi, kwani ni suala binafsi la Diamond.

“Kwanza nikusaidie, hakuna kampuni ya ndani hivi sasa inayoruhusiwa kutoa malipo kwa dola, fedha zote zinatolewa kwa shilingi, lakini kwamba ni kiasi gani kwa kweli siwezi kusema, ila mkataba wake ni mnono kuliko msanii yeyote Bongo kwa sasa.”

Juhudi za kumtafuta mkali huyo anayetamba barani Afrika kwa sasa zilishindikana kwani hadi gazeti hili linakwenda mitamboni, taarifa zilisema alikuwa Afrika Kusini.

Chanzo:GPL

Majangili 9 Wanaotuhumiwa Kutungua Helkopta Wafikishwa Mahakamani

$
0
0
Watu tisa wamefikishwa mahakamani wakituhumiwa kutungua helikopta iliyokuwa ikifanya doria kwenye Pori la Akiba la Maswa wilayani Meatu, Simiyu na na kumuua rubani wake.

Mbali na kutungua chopa na kumuua rubani wake, Rogers Gower, raia wa Uingereza, watu hao pia wameshtakiwa kwa kukutwa na nyara za Serikali, kuuza na kumiliki silaha kinyume cha sheria.

Washtakiwa hao walifikishwa mbele ya Mahakama ya Mkoa wa Simiyu jana wakiwa chini ya ulinzi mkali wa polisi, huku umati wa wananchi wakifurika na kusababisha hekaheka mahakamani hapo.

Yamiko Mlekano, ambaye ni wakili mwandamizi wa Serikali, alidai kuwa washtakiwa wote kwa pamoja wanakabiliwa na kesi tatu; uhujumu uchumi, mauaji na umiliki wa silaha bila ya kibali.

Katika kesi namba mbili ya mauaji, Wakili Yamiko alidai kuwa Shija Mjika (38), Njile Gunga (28), Dotto Pangali (42) na Moses Mandagu walitungua helikopta hiyo Januari 29 kwenye Hifadhi ya Mwiba iliyoko Kijiji cha Makao wilayani Meatu na kumuua rubani Gower.

Mlekano alidai kuwa katika kesi ya uhujumu, mshtakiwa namba moja Iddy Mashaka (49) anadaiwa kujihusisha na kuratibu tukio la uhujumu uchumi kinyume na sheria.

Mbele ya Hakimu Mkazi Mfawidhi Mwandamizi, John Nkwabi, wakili huyo alida kuwa mshtakiwa alitenda kosa hilo Januari 6 na Februari Mosi wilayani Meatu kwa kumshauri mshtakiwa namba mbili, Shija Mjika (38) kuua wanyama wasioruhusiwa.

Katika shtaka la pili, watu saba; Njile Gunga (28), Dotto Pangali (42), Moses Mandagu (48), Dotto Huya (45), Mwigulu Kanga (40), Mapolu Njige (50) na Mange Barumu (47) pia wanashtakiwa kwa kuhujumu uchumi.

Aliieleza mahakama kuwa kati ya Januari 21 na 29 katika wilayani Meatu, washtakiwa walipanga na kuratibu tukio la kuwinda wanyama aina ya tembo bila ya kibali cha Serikali.

Wakili Mlekano alidai kuwa shtaka la tatu la uwindaji wanyama wasioruhusiwa linawakabili mshtakiwa wa pili hadi tisa na wanadaiwa kutenda Januari 26 na 29 kwenye Hifadhi ya Mwiba Kijiji cha Makao wilayani Meatu wa kumuua tembo mwenye thamani ya Sh32,891,100 bila ya kibali.

Katika shtaka la nne, mshtakiwa namba mbili na tisa wanatuhumiwa kumiliki nyara za Serikali kinyume na sheria.

Washtakiwa wanadaiwa kutenda kosa hilo Januari 29 na Februari Mosi wilayani Meatu ambako walikamatwa na meno ya tembo yenye uzito wa kilo 31 na thamani ya Sh32,891,100.

Katika shtaka namba tano, Mashaka na Mjika wanashtakiwa kwa kuuzaji nyara za Serikali kinyume na sheria na kwamba walitenda kosa hilo kati ya Januari 6 na Februari Mosi wilayani Meatu.

Hakimu Nkwabi alisema washtakiwa hawatakiwi kujibu chochote kutokana na mahakama hiyo kutokuwa na uwezo wa kusikiliza kesi hiyo na aliahirisha hadi Februari 24 zitakapotajwa tena.

Katika kesi ya tatu ambayo ni kukutwa na silaha kinyume cha sheria iliyosomwa mbele ya Hakimu Mfawidhi wa Wilaya, Mary Mrio, washtakiwa wanakabiliwa na mashtaka matano.

Washtakiwa hao ni Buluma, Mjika, Pangani, Ngunga, Mandagu, Huya na Kanga ambao baadhi yao walikiri kumiliki silaha na risasi kinyume cha sheria akiwamo Njile anayedaiwa kutungua helikopta hiyo.

Washtakiwa hao walikiri mashtaka mawili ambayo ni kukutwa na bunduki aina ya Riffle 303, wakati Ngunga na Mandagu walikiri shtaka la tatu, nne na tano la kukutwa na silaha na risasi bila ya kibali.

Hata hivyo, Hakimu Mrio alishindwa kutoa hukumu kwa washtakiwa waliokiri kosa kutokana na kutokuwapo kwa vielelezo mahakamani hapo, hivyo kesi hiyo iliahirishwa hadi leo.


Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Alhamisi Ya Februari 11, Ikiwemo ya Sumaye Kumpinga Magufuli..

$
0
0
Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Alhamisi Ya Februari 11, Ikiwemo ya Sumaye Kumpinga Magufuli..

Mchumba wa Riyama Ally Afunguka 'Ukipata Mtu kama Riyama Usichelewe Kumuoa'

$
0
0
Leo Mysterio amesema hayo kupitia kipindi cha Planet Bongo ya East Africa Radio na kusema kwa sasa tayari yeye amefanya maamuzi ya kuishi na Riyama na muda wowote kuanzia sasa wanaweza kufunga ndoa kwani hatua za awali tayari wameanza kuzifanya.

"Unajua Riyana ni mtu ambaye ana huruma sana, ana akili pia ana mapenzi ya kweli kwangu na amekuwa akinisaidia katika kazi zangu hivyo nimefikia wakati nimeona ni bora nimuweke ndani kwani nimeridhika na yeye kwa kila kitu, ndiyo maana sijataka kuchelewesha kwa sababu yeye ndiye mwenye sifa kwangu" Alisema Leo Mysterio

Mbali na hilo Leo Mystereo amesema hajakurupuka katika maamuzi sababu yeye tayari alishafahamiana na Riyama Ally kwa zaidi ya miaka kumi uliyopita, lakini pia hajawahi kumuweka wazi mpenzi wake yeyote yule kipindi cha nyuma lakini mpaka amefikia hatua hii amejiridhisha na kuona kuwa Riwaya ndiye chaguo lake la kweli.

Sio Dimpoz tu, Wema, Shetta, Choka, Ray, Shilole, BASATA nao ni wahanga wa ngoma mpya ya Nay wa Mitego

$
0
0
Nay wa Mitego amechafua hali ya hewa tayari.

Wimbo wake mpya Shika Adabu Yako umejaa controversy kibao.

Ommy Dimpoz amejibu tayari kwa kile alichoambiwa. Soma hapa.

Lakini kuna wahanga zaidi ya Ommy. Wapo pia Wema Sepetu, Shetta, DJ Choka, Ray, Shilole na hata BASATA. Hii ni baadhi ya mistari yenye utata:

Bongo Movie imekufa wamebaki kuuza sura
Wote wanataka kuimba ka Shilole na Snura
Ray Kigosi kawa mkongo hadi leo anaishi kwao
Hela za kuuza movie zote ananunua mkorogo
Kama ni umri umeshaenda, au bado anajiona dogo?

Kama ni vumbi litaruka na mikia watafyata
Hizi taarifa zangu na ziwafikie BASATA
Nyie ni kuku au bata? Msumeno usiokata
Kazi kufungia nyimbo, mnajua shida tunazopata?
Hamjui wajibu wenu, mngekuwa watoto nshawachapa

Na wasanii wadananda, ila Shetta kazidi
Huyo ndo baba Qaila (okay!)
Gari kapewa na Chief Kiumbe utasikia, “my new ride!”

Huyu jamaa anajiita Dimpoz, Poz kwa Poz
Wanae wanalalamika hawamjui shemeji
Kitaani kuna tetesi mwana hapigi mechi
Mara oh jogoo hawiki, huwa haonyeshi shemeji

DJ Choka daily bata, hivi hauna familia?
Nasikia hata nyumbani huna godoro la kulalia

Wema Sepetu una mimba kweli, au ndo kiki za msimu?
Miezi tisa sio mingi, isije ikakugharimu
Na siku hazigandi tayari ushakuwa bibi
Na unakoelekea utatafuta kiki hadi kwa Fid

Breaking News: Ajali Nyingine Tanga..Basi la Simba Mtoto Limegongana Uso kwa Uso na Semi Trella

$
0
0

Nduguzangu inavyosemekana Tanga kumetokea ajali kubwa ya bus la Simba Mtoto ya saa kumi na mbili inayondoka tanga kuja dar na imekutana na Semi Trella uso kwa uso kwenye maeneo ya panda mlima jirani na hale majeraha wako muheza teule na maiti bado zimebanwa kwenye bus subhaana llah eemungu tustiri wajawako na utujaalie mwisho mwema inshallah



Yatokea Sitofahamu katika Pantoni La Kigamboni baada Ya Kugoma Leo Asubuhi

$
0
0
 Hatari....Nimetumiwa picha hizi hapa na wadau wa Udaku Special Blog zikionyesha hali ilivyokuwa katika kivuko cha Kigamboni leo asubuhi , Bado sijapata nini kilisababisha hatari hiyo nitawajuza nitakapopata habari kamili baadae

Viewing all 104789 articles
Browse latest View live




Latest Images