Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104809 articles
Browse latest View live

Picha: Mapokezi ya Diamond, Familia yake na Team yake Mjini KISUMU

$
0
0
Mkali wa Bongo Fleva, Diamond Platinum siku ya jana akiwa na Zari  na Tiffah pamoja na team yake ya wasafi walitua mjini Kisumu nchini Kenya, na hizi ni baadhi ya picha za mapokezi yake hapo jana pamoja na ‘sound check’ aliyoifanya mapema leo kwa ajili ya show itakayofanyika leo mjini humo.



Mgombea wa Urais Marekani Donald Trump Aitukana Tena Africa..Adai lazima Itawaliwe Tena na Mkoloni...

$
0
0
Donald Trump: “There Is No Shortcut To Maturity, Africa Should Be Recolonized”

American business mogul Donald Trump has said that Africa needs to be recolonized. This time around he has directed his anger to African leaders who according to Trump, have failed to exercise leadership and are keeping their people in worse conditions.

Speaking yesterday in Nebraska, Trump said that Africans are slaves living like slaves in their own land yet they claim they are independent.

Trump was responding to a question by a South African journalist on whether he thinks African leaders were right to seek mass withdrawal from the Hague based International Criminal Court.

“It is shameful for African leaders to seek exit from ICC. In my view, these leaders want to have all the freedom to oppress their poor people without anyone asking them a question. I think there is no shortcut to maturity and in my view, Africa should be recolonized because Africans are still under slavery. Look at how those African leaders change constitutions in their favour so that they can be live presidents.

They are all greedy and do not care about the common people” Said Trump
“When I saw them gang up against ICC yet they can’t even find an amicable solution for the ongoing quandary in Burundi, I thought to myself these people lack discipline and humane heart. They can’t lead by example. The only thing they are interested in is accumulating wealth from poor tax payers. Before they think of exiting from ICC, they should first restore peace in Burundi and other war-tone countries rather than gathering like hyenas with the aim of finishing the poor people” Added Trump.

Serikali Yafunguka Kuhusu Rais Magufuli Kukandamiza Uhuru wa Habari Nchini Kwa Kulifuta Gazeti la Mawio.

$
0
0
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Serikali imepokea kwa masikitiko makubwa taarifa iliyotolewa na Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binadamu (THRDC) na kusambazwa kwenye vyombo mbalimbali vya habari kuhusu siku 100 za utawala wa Rais Magufuli kuwa zimekandamiza Uhuru wa Habari nchini kwa kulifuta Gazeti la Mawio.

Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo inasisisitiza kwamba hatua iliyochukuliwa dhidi ya gazeti la Mawio ni Sahihi na lilistahili adhabu hiyo. Aidha, taratibu zote za kulifuta Gazeti hilo zilifuatwa ikiwa ni pamoja na Mhariri Mtendaji wa Gazeti hilo kupewa nafasi ya kujitetea.
Hatua ya Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binadamu (THRCD) kutaka kujenga taswira kwamba Gazeti la MAWIO lilionewa na kwamba halikupewa nafasi ya kujieleza na kujitetea si sahihi na ni kuupotosha umma.

Serikali inazitaka taasisi zinazo jishughulisha na Utetezi wa Haki za Binadamu kuacha kufanya tafsiri potofu kwa Sheria ya Magazeti ya Mwaka 1976 na Sheria nyingine za nchi. Hakuna Uhuru usio na Mipaka na Staha.

Serikali inautaarifu Umma kuwa hatua ya kutunga Sheria ya Huduma za Habari (Media Service Bill) na Haki ya kupata tarifa inaendelea vizuri na Wizara zinaendelea kupokea maoni ya kuboresha Miswaada hiyo.

Muswaada wa Haki ya Kupata Taarifa unasimaiwa na Wizara ya Katiba na Sheria, Muswaada huo unawahusu watu wote. Muswaada wa Huduma za Habari ni mahsusi kwa Wadau wote wa tasnia ya Habari.

Serikali inatoa wito kwa wadau wote wa sekta ya habari kuchangia kuboresha miswaada hiyo. Aidha, inawataka Wanahabari wawe mstari wa mbele katika kuchangia uboreshaji wa Muswaada wa Huduma za Habari badala ya kuwaachia wanataaluma nyingine kutoa maoni na maelekezo katika muswaada huo.

Serikali inawakumbusha wananchi kwamba Sheria ya Magazeti ya mwaka 1976 itaendelea kutumika mpaka pale Sheria mpya itakapopitishwa na Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Katika hatua nyingine Serikali inapenda kuwataarifu wananchi kuwa suala la urushaji wa matangazo ya “live” kupitia Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC) lilisha tolewa ufafanuzi na Viongozi Wakuu wa Serikali. Hivyo mjadala huo ulihitimishwa.

IMETOLEWA NA IDARA YA HABARI (MAELEZO)

Mtandao wa Uhalifu Bandarini Uanikwe..Kuna Uhalifu wa Kitaasisi na si Wanjanja Wachache Kama Inavyodhwaniwa

$
0
0
Jumatano Waziri Mkuu Kassim Majaliwa alitembelea tena Bandari ya Dar es Salaam kufuatilia utendaji kwenye eneo hilo muhimu katika kuendesha nchi.

Kwa mara nyingine, Waziri Mkuu alishuhudia mambo yanavyoendesha kwa jinsi ambayo inatia shaka baada ya kukuta bomba lililojengwa kutoka bandarini hadi eneo la kampuni ya Tipper, ambayo inafanya shughuli za uagizaji mafuta.

Eneo ambalo bomba hilo linaelekeza mafuta, limezungushiwa uzio na hivyo haliwezi kufikiwa na wafanyakazi wa Mamlaka ya Bandari (TPA) na hivyo usimamizi wa kinachoendelea humo ndani ni mgumu hata kama kuna wizi mkubwa wa mafuta.

Waziri Mkuu hakuweza kupata maelezo ya kutosha kuhusu bomba hilo na kuagiza uongozi wa Tipper, kampuni inayoendeshwa kwa ubia baina ya Serikali na Oryx Energy na uzio unaozuinguka eneo la Tipper uvunjwe ili Mamlaka ya Bandari iweze kuratibu uingizaji mafuta.

Tukio hilo limetokea wakati Waziri Majaliwa akiibua kashfa za ufisadi bandarini, zikiwamo za ukwepaji kodi kwa kupitisha makontena kinyemela na kutolipa ushuru. Imebainika kuwa zaidi ya makontena 11,000 yalipitishwa kinyemelea bila ya kulipiwa ushuru na hayo ndiyo maisha ya bandarini kwa miaka mingi sasa.

Tukio hilo la Jumatano limeibua maswali mengi kuhusu usimamizi wa bidhaa zinazoingia bandarini, na hasa mafuta ambayo kwa sasa ndiyo yanayotegemewa sana kuendesha uchumi kutokana na kutegemewa na sekta zote. Haiingii akilini kwamba bomba linalochepusha mafuta linajengwa mchana bila ya viongozi wahusika kuhoji sababu za ujenzi huo na linaanza kutumika bila ya wahusika kuhoji.

Haiingii akilini kwamba ujenzi wa bomba hilo pia ulihusisha ujenzi wa mabomba mengine ya kuchepusha mafuta na yakaanza kufanya kazi kwa muda wote bila ya wahusika kuhoji.

Kwa maana nyingine kama wizi huo uchunguzi utabaini wizi huo, ni dhahiri kuwa utakuwa ni uhalifu wa kitaasisi na si wa wajanja wachache kama inavyotokea kwenye maeneo mengine, kitu ambacho ni hatari. Wakati hayo yakitokea, Wakala wa Vipimo (WMA) nao waliamua kuzima mita za kupima mafuta na badala yake kufanya kazi hiyo kwa kutumia miti, uamuzi ambao pia unatia shaka kuhusu usimamizi wa mali za umma.

Katika hali inayotia shaka, mita iliwashwa saa chache kabla ya Waziri Mkuu kutembelea na alipouliza sababu za kuwasha mita siku hiyo, aliambiwa ni maagizo kutoka kwa kigogo.

Kuhusu mita kuzimwa, Waziri Mkuu aliambiwa kuwa hilo lilifanyika kwa hisia kuwa wafanyabiashara walikuwa wanapunjwa ndiyo maana mita zikazimwa. Hivi bidhaa nyeti kwa uchumi kama hiyo inafanyiwa maamuzi kwa hisia?

Ni lazima kuna uhalifu wa kitaasisi unafanyika katika uingizaji mafuta na ndiyo maana mambo ambayo yalikuwa yakifanyika kweupe, lakini yakafumbiwa macho na viongozi.

Tunashauri kuwa uchunguzi wa kina ufanyike ili kubaini mtandao wote wa uhalifu huo kwenye nishati hiyo nyeti kwa uchumi wa Taifa.

Uchunguzi huo uwe wa kina ambao utalenga kubaini watu wote walioko kwenye mtandao huo unaojihusisha na vitendo vya upitishaji bidhaa bila ya kulipia ushuru na kodi husika kwa kuwa ndio wanaopunguza uwezo wa Serikali kuwahudumia wananchi wake.

Na kwa kuwa bandarini kunaonekana kuwa kumekithiri kwa vitendo vya wizi na hujuma, Serikali iendelee kuweka jicho kali eneo hilo ili kukomesha wizi unaotesa wananchi huku ukinufaisha kikundi cha wachache wanaoishi maisha ya kifahari kwenye nchi maskini.

Hatimaye Rommy (DJ wa Diamond) Arejea Kazini Baada ya Kusemekana Wametofautiana na Diamond Platnumz

$
0
0
Sina uhakika kama Diamond na Rommy waligombana lakini kwa habari za chini chini inasemekana kuwa Rommy na Diamond walitofautiana ingawa wao hawakuthibitisha hilo!

Taarifa za chini chini zinasema kuwa Rommy na Diamond walitofautiana baada ya Rommy kuambiwa ajitegemee! Ndipo Rommy alipo kaa mbali na WCB na kuamua kuanza kurusha Matangazo katika Ukurasa wake wa Insta! matangazo yalio kuwa yana muhusu diamond alikuwa anatoa kwa kuibia ibia sana

Ikumbukwe kuwa show za Diamond zote Rommy alikuwa ndio Dj lakini baada ya kutofautiana kwao hakuonekana tena kwenye show hadi Usiku wa Mkesha wa Valentines day ambapo Diamond Alifanya Show kubwa Kisumu Kenya

Wakiwa na Crew ya WCB kenya Rommy ameonekana kwenye picha ya pamoja jambo ambalo watu wamesema ni kutokana na kumaliza tofauti zao na hivyo ataendelea kuwa Dj wa Diamond katika show zake zote

Juzi Rommy alipost videos mbili zikionesha akiwa kwenye Ndege kuelekea kenya ingawa yeye hakusema kama anaende kenya ndipo Esmaplatnumz alipo comment na kusema nakuona Rommy Nairobi Moja!

Diamond nae alipost video akionesha anatoka SA kwenda Kenya kwenye show!

Ule usemi wa kuwa Ndugu wakigombana Shika Jembe ukalime ni dhahiri kuwa umetimia!

Sasa Diamond + Rommy wapo pamoja tena na Kazi zinaendelea! kama ni kweli waligombana Hongera kwa alie wapatanisha!

Kauli ya Diamond Platnumz yamfanya Mrisho Mpoto asitishe kuachilia video ya 'Sizonje

$
0
0
Kauli ya staa wa muziki Diamond Platnumz ‘Kuna kushoot video na kurekodiwa’ imemfanya msanii wa muziki wa asili Mrisho Mpoto kuitia kapuni kwanza video yake mpya ya wimbo ‘Sizonje’ ili aichunguze kwanza kama inafaa.

Kupitia ukurasa wa instagram, Mpoto ameandika "Diamondplatnumz post yako ya leo imenifanya nisile Siku nzima. Nikiitafakari na sasa nimeamua kusitisha kutoa video yangu mpya ya #SIZONJE maana sina uhakika kama nime shoot au nimerecord. Ukimkimbiza sana mjusi anageuka kuwa nyoka"

Ijumaa hii Diamond aliachia video mpya ya wimbo ‘Make Me Sing’ akiwa na AKA wa Africa kusini na kutwitter.

Nimegundua Mimi na Baba Yangu Mzazi Tunashare Msichana Mmoja Bila Kujua...

$
0
0
Ni wiki ya tatu sasa tangu mama asafiri kwenda kwenye msiba huko nyumbani kwao, nyumbani tumebaki mimi, baba na mfanyakazi wetu wa ndani.

Kwa vile mimi nimeshamaliza chuo na muda mwingi huwa nashinda nyumbani (sina kazi) nimejikuta nikiingia katika mahusiano ya mapenzi na huyu msichana waa kazi.

Juzi usiku kama kawaidayangu nilienda chumbani kwake ila sikumkuta ikabidi nitege mingo ili nijue huyu msichana kaenda wapi, baada ya kama lisaa 1 nilishtuka kuona mlango wa kwa baba unafunguliwa na yule msichana wa kazi kakatoka na kwenda chumbani kwake.

Niliumia sana kuona kile kitendo si kwa wivu wa mapenzi bali kwa kile kitendo alichofanya baba na ukizingatia anamke wa ndoa (mama yangu).

Wadau naombeni busara zenu kuwa anachokifanya sio kizuri au nimwambie na bi mkubwa?

Waafrika Wanaosoma India Waitwa Nyani, Sokwe

$
0
0
Wanafunzi wa Tanzania wanaosoma India wamefunguka na kueleza unyanyasaji na ubaguzi wanaoupata wanapokuwa masomoni nchini humo.

Ikiwa ni siku chache baada ya mwenzao kupigwa na mwingine kuvuliwa nguo huku akilazimishwa kutembea uchi, wanafunzi hao wamesema unyanyasaji wanaofanyiwa hauelezeki.

Inaelezwa kuwa karibu wanafunzi 400 hadi 500 Afrika wanasoma nchini humo, wengi wanatoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC), Nigeria, Tanzania, Sudan na Rwanda.

New Delhi

Mhariri wa Habari wa Kampuni ya Sahara, Jennifer Sumi ambaye alisoma Shahada ya Uzamili katika Chuo Kikuu cha ICFAI, New Delhi, alisema Waafrika wanaoishi nchini humo huitwa majina ya kashfa kama mbwa weusi na wakati mwingine wahindi huhama eneo ambalo Mwafrika anaishi.

“Unyanyasaji wao upo wazi, wanadharau sababu upo nchini kwao. Wakati mwingine unashindwa kuvumilia na kujikuta unajibu mashambulizi,” alisema.

Aliutaja udhalilishaji mwingine kwa Waafrika ni pamoja na baadhi ya raia wa nchi hiyo kugusa ngozi kisha kuangalia vidole kama vimebakia na rangi nyeusi.

“Wanaweza kukuuliza wewe ni mweusi kwa sababu ya jua? Au ukachekwa tu bila sababu na kwa kuwa huelewi lugha yao,” alisema.

Sumi ambaye pia alikuwa Mwenyekiti wa Wanafunzi wa Kitanzania wanaosoma India, alisema ni vigumu kuishi nchini humo, lakini walivumilia mengi kwa ajili ya kufuata elimu.

Sumi anasimulia zaidi kuwa wanafunzi wanawake wanaonekana ni watu waliokwenda India kufanya biashara ya ukahaba.

“Sijui kwa nini wana mtazamo huo, Wahindi wanaamini kuwa wasichana wa Kiafrika wanaoishi India wanafanya biashara ya ukahaba, ndiyo maana kuna ubakaji mkubwa,” alisema.

Sumi alisema wakati anasoma India wanafunzi wengi walikuwa wanaogopa kupanda daladala za bei nafuu kuepuka ubaguzi, kuchekwa na matusi.

Alitoa mfano wa wakati wa kuadhimisha mila za kurushiana rangi, (Walid), baadhi ya raia wa nchi hiyo waliwarushia pia Waafrika na kuanza kuwacheka.

Mbunge wa Viti Maalum CUF, Riziki Lulida ambaye pia amesoma India, alisema alikumbana na ubaguzi na udhalilishaji akiwa masomoni.

Acharya, Bangalore

Mwanafunzi mwingine anayesoma Chuo Kikuu cha Acharya, Bangalore, Dawson Kimenya anasema ubaguzi huo huwezi kuuona kama utaishi kwenye miji mikubwa au hoteli za kitalii au hospitali bali mitaani.

Alisema Waafrika wanalazimika kupanga vyumba uswahilini kwa sababu ya gharama za malazi na chakula vyuoni kuwa juu.

Anasema ni kawaida kwa Waafrika kuitwa ‘kalu’ (nyani) au absiii (sokwe) mitaani na wakati wakipanda daladala.

“Wakati mwingine mtoto ambaye yupo na wazazi wake anakuita hivyo na huwezi kumfanya kitu,” anasema.

Changamoto nyingine aliyoitaja Kimenya ni kukosa siku maalum ya Watanzania kukutana ubalozi wa Tanzania nchini humo.

“Kufika ubalozini hadi unapopatwa na tatizo tu, hakuna siku maalum ya Watanzania kukutana kueleza changamoto,” alisema.

Kifo cha Yannik huko Punjab

Mtanzania, anayesoma Chuo Kikuu cha TGC, New Delhi, Pius Mmasy alishuhudia Aprili 22, 2012 mwanafunzi raia wa Burundi, Yannik Nihangaza akishambuliwa na vijana wa Kihindi na kusababisha kifo chake.

Tukio hilo lilitokea Kaskazini mwa India, eneo la Punjab. Yannik alikuwa akisoma Shahada ya Sayansi ya Kompyuta katika Chuo Kikuu cha Lovely Professional.

Mmasy alisema vijana hao walikuwa nje ya nyumba ambayo Watanzania walikuwa wakifanya sherehe siku hiyo.

Vijana hao walikuwa wakilazimisha kuingia kwenye sherehe bila ya kualikwa. “Yannik alichukua pikipiki ili arudi bwenini kwake kwa kuwa alisahau kitu, alipotoka nje alivamia na kuanza kupigwa, ” alisema.

Baada ya kupigwa na kujeruhiwa vibaya, Yannik alilazwa katika hospitali ya Patlala kitengo cha wagonjwa mahututi kwa miaka miwili akipumulia mashine na kufariki dunia Julai 1 , 2014.

Hakuna mtuhumiwa aliyekamatwa kuhusiana na mauaji hayo na kwa mujibu wa vyombo vya habari vya nchini humo, wengi wa watuhumiwa walitoroshwa kupelekwa nje ya nchi. “Katika kipindi hicho, Waafrika tuliishi kwa hofu, wasichana walibakwa na kupigwa hovyo, kibaya ni kuwa hatuna pa kuripoti,” alisema Mmasy.

Agra

Mtanzania aliyesoma Chuo Kikuu cha Agra, India, Jane Balama, alisema maisha nchini humo ni magumu kutokana na kukithiri kwa ubaguzi.

Mkenya kuvuliwa nguo

Balama anaeleza mwaka 2013 wakati na Waafrika wenzake wanatoka kufanya manunuzi, walikutana na kundi la Wahindi wakiadhimisha moja ya sikukuu zao za kimila eneo la Agra (ilipo Taj Mahal)

Wahindi hao walianza kumrushia chakula msichana wa Kenya aliyekuwa ameongozana na Balama kisha wakamvua nguo zote.

“Ilibidi wanaume tuliokuwa tumeongozana nao wavue mashati wamsitiri,” alisema.

Balama alieleza alivyoporwa pochi yake yenye fedha na mali zake, lakini polisi aliyekuwa karibu akikataa kumsaidia. “Niliripoti polisi lakini sikusaidiwa,” alisema.

Mwanafunzi anayesoma Chuo Kikuu cha Ambedkar, New Delhi, Richard Msuya alisema ameshuhudia kuitwa majina yanayoashiria ubaguzi kama nyani au nigga. “Kiwango cha unyanyasaji kinatofautiana na mazingira, nipo mji mkuu, New Delhi ni Diplomatic City” alisema.

Balozi mdogo wa ubalozi wa India nchini, Robert Shetkntong anasema hajawahi kupokea malalamiko kuhusu ubaguzi huo.

Hata hivyo, anasema haoni kama kuna ubaguzi wa rangi katika mashambulizi hayo zaidi ya ugomvi wa kawaida wa mitaani.

Kuhusu Waafrika kuitwa nyani na kuvuliwa nguo, alikataa kuzungumzia.

Balozi Kijazi

Balozi wa Tanzania, India, John Kijazi alisema ubalozi upo kwenye mchakato wa kuunda kamati zitakazohusisha wanafunzi, polisi, uongozi wa wenyeji, uongozi wa chuo na Serikali ya jimbo kushughulikia tatizo hilo .

Alisema baada ya kudhalilishwa kwa Mtanzania huyo Januari 31, polisi watano na raia wengine 11 waliofanya tukio hilo wamekamatwa.

Alisema ubalozi ulikwenda kuzungumza na wanafunzi wanaoishi Bangalore na kukubaliana kuunda kamati hizo.

“Nia yetu kurudisha amani wanafunzi wasome kwa amani na utulivu na zisiwepo fujo nyingine,” alisema.



Breaking News:Mbunge wa Zamani wa Nyamagana Ezekiel Wenje Apata Ajali ya Gari

$
0
0
Gari lililokuwa likiendeshwa na aliyekuwa Mbunge wa Nyamagana, Ezekiel Wenje limepata ajali maeneo ya Magereza Bariadi mkoani Simiyu mchaba wa leo baada ya kuacha njia na kugonga mtaro na kisha kuanguka. Ndani ya gari hilo alikuwepo pia Mbunge wa VIti Maalumu (Chadema), Gimbi Masaba na Mwandishi wa habati wa Tanzania Daima, Sitta Tuma ambao wamepata michubuko kidogo.

Wanamuziki Deo Mwanambilimbi, Allain Mulumba Kashama Mbaroni Kwa Uhamiaji Haramu

$
0
0
IDARA ya Uhamiaji imewatia mbaroni wanamuziki mashuhuri Deogratius ‘Deo’ Mwanambilimbi, rapa maarufu Alain Mulumba Kashama na Mwenabantu Kibyabya Michel wakihusishwa na uhamiaji haramu katika kutekeleza kauli mbiu ya Rais John Magufuli ya ‘Hapa Kazi Tu’.

Mbali ya kuwakamata wanamuziki hao, Uhamiaji pia imemtia mbaroni Abdulahi Suleiman Mberwa kwa kosa la kujihusisha na biashara haramu ya kusafirisha binadamu kuwapeleka nje ya Tanzania.


Naibu Kamishna wa Uhamiaji nchini, John Mfumule, amewaambia waandishi wa habari leo kwamba, Mwanambilimbi anakabiliwa na kosa la kuajiri na kuwafanyisha kazi wageni – Alain Mulumba (39) na Mwenabantu Michel (35) wote raia wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo – katika bendi yake ya Kalunde huku akijua wanamuziki hao hawana vibali vya kazi na ukaazi.

Mwanambilimbi (43), mkazi wa Goba-Kinondoni jijini Dar es Salaam, ndiye mmiliki wa bendi ya Kalunde ambayo ina mkataba wa kutumbuiza kwenye hoteli ya Giraffe ya jijini humo.

“Kashama na Michel wote kwa pamoja wanakabiliwa na kosa la kuishi nchini na kufanya kazi bila kuwa na vibali,” alisema Naibu Kamishna Mfumule.

Inaelezwa kwamba, Kashama anamiliki hati ya kusafiria ya DR Congo yenye Namba OBO782268 iliyotolewa Aprili 21, 2015 itakayomalizika muda wake Aprili 20, 2020. Hati yake ya zamani ya kusafiria ni Namba C0172419 iliyotolewa Juni 12, 2008 na ilimalizika muda wake Juni 11, 2011.

Mwenabantu Michel ana hati Namba OBO487018 iliyotolewa Machi 29, 2008.

Hata hivyo, Kashamba ni miongoni mwa wanamuziki wakongwe kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo aliyeingia nchini Tanzania mwishoni mwa miaka ya 1990 na mwanzilishi wa bendi ya Diamond Sound ‘Wana Dar es Salaam Ikibinda Nkoi’ iliyokuwa ikilimikiwa na mfanyabiashara Fred Rwegasira ikiwa na makao yake makuu Silent Inn, Mwenge, ingawa kwa sasa haipo kwenye ulimwengu wa muziki.

Baada ya kusambaratika, wanamuziki wa bendi hiyo wakaanzisha bendi nyingine iliyojulikana kama Diamond Musica International.

Ni miongoni mwa wanamuziki walioleta mabadiliko ya muziki nchini kwa kuingiza rap, ghani ambazo zimeteka bendi nyingi za muziki wa dansi kwa sasa na kuvutia mashabiki wengi.

Baadhi ya wanamuziki waliokuwa wakiunda bendi hiyo kabla ya kusambaratika ni Hassan Liver, Richard Mangustino, Wayne Zola Ndonga na aliyekuwa kiongozi wa bendi hiyo, Ibonga Katumbi ‘Jesus’.

Kwa upande mwingine, Abdulahi Mberwa (37), mkazi wa Kisauni, Zanzibar ambaye kwa sasa anaishi Magomeni Mapipa jijini Dar es Salaam, yeye anakabiliwa na makosa ya kuwasafirisha wasichana wa Kitanzania kwenda Arabuni, kosa ambalo ni la usafirishaji haramu wa binadamu.

Lakini pia anakabiliwa na kosa la kutoa nyaraka za uongo za wasichana ili kuwapatia hati za kusafiria na kuwapeleka huko Arabuni.

Mberwa alikamatwa pamoja na wasichana wawili ambao alitaka kuwasafirisha ambao ni Asma Halfe Mkeyenge (26), mkazi wa Tandika Davis Corner jijini Dar es Salaam na Nyamizi Halfa Kambunga (31), mzaliwa wa Urambo mkoani Tabora na mkazi wa Mbagala Misheni (KTM) jijini Dar es Salaam.

Naibu Kamishna Mfumule alisema kwamba, Asma aliwasilisha nyaraka za uongo ili kujipatia hati ya kusafiria yenye namba AB 402133 iliyotolewa Februari 9, 2026 ambayo inakwisha muda wake Februari 8, 2016, wakati Nyamizi naye aliwasilisha nyaraka za uongo na kujipatia hati ya kusafiria namba AB 402592 iliyotolewa Februari 10, 2016 na matumizi yake yanakwisha Februari 9, 2026.

Watu hao wote sita tayari wamekwishafikishwa mahakamani.

Unaambiwa Tukiacha Ufisadi Bandari zetu...Tanzania Haitahitaji Misaada ya Wahisani Kutoka nje

$
0
0
Kufichuka kwa kashfa za ufisadi katika Bandari kumedhihirisha namna serikali inavyopoteza mabilioni ya shilingi kupita Bandari ya Dar es Salaam pekee kutokana na uzembe na ufisadi wa watendaji.

Mapato yanayopatikana katika Bandari ya Dar es Salaam ni mengi mno kiasi kwamba kama serikali inakusanya na kusimamia kwa makini, hata maendeleo yanaweza kuonekana na hakutakuwa na haja ya kutegemea misaada ya wahisani ambayo mara nyingi ni ya kujidhalilisha.

Lakini bandari ya Dar es Salaam ni miongoni mwa bandari karibu 10 muhimu zilizopo nchini Tanzania, ambazo ‘zimetelekezwa’ na serikali na hivyo kuikosesha mapato mengi.

Kabati la Nguo la Mmiliki wa Facebook Lashangaza Wengi....

$
0
0
Nilikuwa napita huku na huko katika mitandao,hatimaye nikakutana na maisha ya uvaaji wa nguo za mmiliki wa mtandao wa facebook MARK ZUCKEBERG.Huyu jamaa ametoa picha ya kabati la nguo zake,na kuelezea kuwa ndio kabati la nguo zake za kila siku azivaazo.

Mark anasema ili asipoteze akili nyingi kwa mkewe na kwake juu ya nini avae na ni nmana gani anatakiwa kuvaa,ameamua kuwa na nguo za aina moja katika kabati yake na kutoa "tender"(zabuni) kwa kampuni kumtengenezea aina hiyo ya nguo,pia ameamua kununua nyumba iliyo karibu kabisa na Makao Makuu ya Facebook ili asiwe anatumia usafiri wa aina yoyote zaidi ya kutembea toka nyumbani mpaka ofisini.

Ukifuatilia hata katika makongamano yake na mihadhara ya kitaaluma ktk vyuo na maeneo mbalimbali unaweza dhania kuwa Mark huwa habadilishi nguo,kumbe ana kabati lililojaa nguo za aina moja

Baba Diamond Platnumz Ataka Kufia Studio Kwa Mwanaye!

$
0
0
Abdul Juma ambaye ni baba mzazi wa staa wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond’ amenaswa akiwa katika studio ya mwanaye iliyopo Sinza Mapambano jijini Dar akidaiwa kusaka suluhu ya ugomvi wake na mwanaye, Risasi Jumamosi lina habari kamili.


Katika kusaka suluhu ya ugomvi wao huo wa muda mrefu, chanzo kilieleza kuwa, mzazi huyo hakujali ugonjwa wa miguu unaomsumbua kwa muda mrefu, kwani alikuwa tayari hata kufia studioni hapo ilimradi afanikiwe kuonana na Diamond, wamalize tofauti zao.
diamond-platnumzDiamond

TUJIUNGE NA CHANZO
Februari 10, mwaka huu, mwanahabari wetu alipokea simu iliyoeleza kuwa mzazi huyo alikuwa akimsaka Diamond ambapo alilazimika kuweka makazi ya muda kwenye jengo lililo studio hiyo huku akiwa mgonjwa, akiwa na lengo moja tu, kumaliza tofauti zao.
baba diamond (3)Akitafta mahala pa kukaa ili amsubiri Diamond
“Njooni hapa Mapambano kwenye studio ya Diamond, baba Diamond amefika hapa, anaonekana mgonjwa hata tembea yake anazunguka hapa mara atoke geti hili, mara aende lingine maana nyumba hii ya studio ina mageti mawili.
“Anasema bora afie hapa lakini lazima leo aonane na Diamond ili moyo wake uridhike. Ameongozana na mwanaume mmoja nafikiri ndiye anayempa msaada wa karibu,” kilisema chanzo hicho.

RISASI MZIGONI
Baada ya kupata maelezo hayo kutoka kwa chanzo, mwanahabari wetu kwa kutumia usafiri wa bodaboda, alifika fasta katika studio ya Diamond na kumkuta mzee huyo aliyeonekana kuumwa miguu iliyokuwa imevimba, akihaha kugonga geti la nyumba hiyo ya studio.
Kwa kutumia kamera za kidaku zaidi, mwanahabari wetu alikita kambi maeneo ya jirani na studio hiyo tangu saa 5 asubuhi hadi jioni akisubiri kuona namna itakavyokuwa wawili hao watakapoonana, huku akimfotoa picha tofauti mzazi huyo na mpambe aliyeongozana naye.

WACHOKA, WAKAA
Kuna wakati mwanahabari wetu alimshuhudia baba Diamond na mwenzake wakiwa wamechoka kugonga mageti ya nyumba hiyo na kuamua kukaa chini katika mawe yaliyokuwa jirani.
“Mzee anaonekana anaumwa yule, ona anavyokaa pale anaonekana ana maumivu mwilini ila atakuwa anajikaza tu, si bora angepumzika tu nyumbani akatafuta njia mbadala ya kuonana na Diamond,” alisikika shuhuda mmoja.

RISASI LAMVAA BABA DIAMOND
Baada ya kumfotoa picha za kutosha, Risasi Jumamosi lilimfuata mzazi huyo na kumuuliza kulikoni afike studio hapo angali mgonjwa na kwa nini asiwasiliane na mwanaye kwenye simu? Mzee huyo alifunguka:
“Yametokea mengi huko nyuma, lakini nahisi ni muda muafaka wa kumaliza hizi tofauti zetu. Katika pitapita zangu maeneo haya, nikaoneshwa hapa ndiyo studio kwake, nikaona bora nishinde hapa kutwa nzima nikiamini lazima atafika tu japo naumwa lakini sikuona haja ya kuondoka ni bora nifie hapa lakini leo hadi nionane naye.
“Nimegundua Diamond hana makosa. Mimi ndiyo kuna maeneo nilikuwa siko sahihi. Mama yake tulishamaliza tofauti zetu, tuko vizuri na ndiyo maana nikaona nimsake Diamond kwa udi na uvumba.”

AAMBULIA PATUPU
Licha ya kushinda kwa matumaini studio hapo hadi jioni, Risasi Jumamosi lilimshuhudia mzazi huyo akiondoka bila mafanikio kwani licha ya wasanii wa Diamond kudaiwa huwa wanafanya mazoezi karibu kila siku kwenye nyumba hiyo, siku hiyo geti halikufunguliwa hadi mzazi huyo alipokata tamaa na kuamua kuondoka zake.

DIAMOND HAPATIKANI
Gazeti hili lilifanya juhudi za kuwasiliana na Diamond kuhusu suala hilo lakini halikuweza kupata mawasiliano yake ya moja kwa moja baada ya marafiki zake kudai kuwa yupo nchini Afrika Kusini kwa ajili ya shughuli zake za kimuziki.

TUMEFIKAJE HAPA?
Diamond na baba yake waliingia kwenye bifu zito baada ya mzazi huyo kumtuhumu mwanaye kuwa hamjali kwa sababu tu ana ugomvi na mama yake mzazi, Sanura Kassim ‘Sandra’.

Source:Global Publishers

Waziri wa Afya Ummy Mwalimu Atembelea Hospital ya Muhimbili Kukagua Utekelezaji wa Agizo la Rais Magufuli

$
0
0
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu ametembelea hospitali ya Taifa Muhimbili kukagua utekelezaji wa agizo la Rais John Magufuli la kuwataka watumishi wa wizara hiyo waliokuwa wakilitumia jengo la Kitengo cha Afya ya Uzazi na Mtoto kuhamisha ofisi zao na kuliacha kwa ajili ya matumizi ya wodi ya wazazi.
Akizungumza na waandishi wa habari, Dar es Salaam leo katika hospitali hiyo, Waziri Ummy amesema kuwa mpaka kufikia kesho tayari jengo hilo litakuwa limeanza kutumika kwa kuwa watafanya kazi ya kuhamisha makabrasha ya watumishi hao usiku kucha kuhakikisha agizo la Rais John Magufuli linatekelezwa mara moja.

Picha mbalimbali zinaonesha Waziri Ummy Mwalimu akikagua utekelezaji wa agizo la Rais John Magufuli pamoja na watumishi na vibarua wakihamisha nyaraka na makabrasha mbalimbali kutoka kwenye jengo lililokuwa likitumiwa kama ofisi na watumishi wa wizara hiyo katika Hospitali ya Taifa Muhimbili, Dar es Salaam.






Msiwalaumu Wadada wa Mjini Kutembea na Wazee

$
0
0
Nimepanda lift kwenye moja ya jengo maarufu na refu hapa mjinikati karibu na Ohio st. Niko ndani ya lift mzee mmoja smart anongea na simu kwa sauti ya maringo , upole na yenye kujiamini, kulikua kimya hivyo unasikia kabisa upande wa pili ni sauti ya kasichana mazungumzo yalikua hivi.

Mzee - What do you mean..I've told you before not to worry it is within my capability usichukue gari ya chini, chagua landcruiser au yoyote ya juu.

Mdada.- '............. .... ....... ..... ........ ........ .... ............

Mzee. - Ok no problem, njoo sasa hivi uchukue cheque kwa ajili ya kuwalipa NSSF niliongea na mkurugenzi wake akanipromse a nice location for your appartment.

Anyway we njoo ukifika go to reception I have already reserve a place, just wait me in the room nina kikao na waziri nikimaliza nakuja. 

Niliwai kufika nikatoka liftini nikamuacha bado anaongea.

Kwa kweli niliona hamna sababu ya kuwasema wadada wanaotembea na wazee this dudes knows how to care jamani......

Vijana Siku hizi Hawajui Kuhonga zaidi ya Kuchafuana tu hata hela ya kununua sababu ni kujisafishia hupati

Nina Miaka Minne Kwenye Ndoa ila Mume Wangu Hajawahi Kunifikisha Kileleni..

$
0
0

Mimi ni msichana wa miaka 27 nimeolewa miaka minne iliyopita na nina watoto wawili wote wa kike. Mwanzoni mwa mahusiano yetu na mume wangu (wakati tukiwa wachumba) na hata kama mwaka mmoja na nusu hivi kwenye ndoa yetu, baba watoto alikuwa ananiweza kweli….yaani nikikutana nae…aaah, allahmdullillah, nilikuwa naiona anga kwa uhalisia kabisa….na akiwa amechoka sana, basi hata mbili nitapata na kweli nilikuwa najisikia nime…..! Na kwa wiki nilikuwa napata kama siku nne hivi, yale mapigo ya sawa sawa.

Sasa kwa kipindi kama cha mwaka mmoja hivi…da, baba watoto kwa kweli ana underperform kabisa….wakati mwingine inapita wiki nzima, sionji na mimi mwanamke huwa nahitaji…nikimwambia anasema nimechoka sana kazini. Kwa heshima niliyo nayo kwa mume wangu, huwa namwambia sawa, lakini moyoni huwa nabaki na maswali mengi kuliko majibu. Huwa nahisi moja kati ya mambno haya:



1. Huenda mume wangu ameanza mambo ya nyumba ndogo, so akitoka kazini huenda anamalizia huko huko then akirudi nyumbani anakuwa hoi


2. Labda umbile langu limemchosha, coz kabla hatujaoana nilikuwa na bambataa ya wastani na kiuno chembamba, lakini now sio utani, nyonga imebaki vile vile lakini makalio yameongezeka mara-dufu, so huwa hafikii pale “Dar es Salaam“ kisawasawa kama tunado ile style ya chuma mboga.


Haya yoye ni mawazo yangu ambayo ninayo moyoni. Sasa sijajua kama nimuulize au na mimi nianze kupiga show za nje kwani wanaonitongoza nikiwapanga kuanzia Dar, basi watafika hadi morogoro……tatizo nampenda baba watoto na nimempa muda wa kama miezi 6 hivi, kama hatobadilika, basi nita-confirm namba (1) ya hapo juu….so na mimi nitaanzia  kutafuta wa kurusha nae roho.

Naomba mnisadies what to do at the moment!

By Koleta

Kuna Wakati Nauchukia Umaarufu – Shamsa Ford

$
0
0
Staa mrembo wa Bongo Movies, Shamsa Ford amefunguka kwa kusema kuwa wakati mwingine anajuta kuwa maarufu.

Kupiti instagram, Shamsa ameandika.

"Umaarufu una raha lakini ubaya wake ukiwa maarufu ni ngumu kumjua mtu anayekupenda kwa dhati kwa sababu wengine wanaweza wakawa wanakufwata kwa ajili ya jina lako ili mradi awe karibu tu na wewe. Umaarufu Ubaya wake unakuwa Huna uhuru wa maisha yako.yaani tena ukiwaendekeza hao binadamu unaweza ukajikuta unaishi kwa matakwa yao which is not good coz mwisho wa siku kila mtu ataiaga dunia na kila nafsi itajitetea kivyake . .kitu kidogo akifanya mtu maarufu kinaweza kikawa kikubwa kuliko akifanya mtu wa kawaida wakati wote ni binadamu. Loh muda mwingine nauchukia umaarufu"

Diamond Azungumzia Collabo Mpya na Yemi Alade na Jinsi Zari Alivyobadilisha Maisha yake

$
0
0
Diamond Platnumz na Yemi Alade wanatarajia kuja na collabo mpya.
Taarifa hiyo imetolewa na muimbaji huyo wa ‘Make Me Sing’ alipokuwa akiongea na na D’Mike wa kipindi cha Mseto cha Radio Citizen. Amesema yeye na Yemi tangu wakutane kwenye kipindi cha Coke Studio Africa, wameendelea kuwa washkaji wa karibu.

“Wiki mbili zilizopita amenitumia nyimbo yake mpya ambayo tutafanya, na ukiisikiliza hiyo nyimbo ina mahadhi ya kinyumbani East Africa kabisa, siwezi kusema jina inaitwaje japokuwa jina pia ni la Kiswahili,” alisema Diamond.

Katika hatua nyingine, Diamond alieleza jinsi ambavyo Zari amebadilisha maisha yake.

“Kwenye siku hii nzuri maalum ya Valentine’s kitu kikubwa nitakachoweza kumwambia [Zari] ni kwamba nampenda sana na kiukweli amecheza part kubwa sana katika maisha yangu mpaka hapa nilipo,” amesema.
“Amenizalia mtoto ambaye nilikuwa na ndoto hiyo siku zote na kila siku amekuwa akinifanya napevuka kwasababu nakuwa na akili za kimaisha natoka katika utoto nakuwa katika utu uzima ambao unanifanya niweze kutengeneza hata misingi mizuri ya kazi yangu pia. Ukisikiliza nyimbo zangu, strategy zangu za kimuziki zinazidi kupevuka. Ananitunzia moyo wangu vizuri sababu nina mapenzi naye mazito.”

Msikilize zaidi hapo chini.

CUF: Maalim Seif Sharif Hamad Akishinda Uchaguzi wa Marudio Zanzibar Hatakubaliana Na Matokeo

$
0
0
Chama cha Wananchi (CUF) kimesema ikitokea Makamu wa Kwanza wa Rais wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Maalim Seif Sharrif Hamad ameshinda kwa kupigiwa kura na akaibuka mshindi wa kiti cha urais katika uchaguzi wa marudio utakaofanyika Machi 20, hatakwenda kuapishwa.

Kimesema kuna uwezekano mkubwa Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC), ikaweka jina la Maalim, wawakilishi na madiwani katika karatasi za kupigia kura na kusisitiza, ikitokea hivyo na wagombea hao wakapigiwa kura, wote hawataenda kuapa.

“Kama wagombea wetu wakichaguliwa na ZEC ikawatangaza washindi itakuwa ni kazi bure. Pia, CUF hatutakwenda mahakamani kufungua kesi ya kikatiba kupinga hatua ya mwenyekiti wa ZEC kufuta matokeo ya Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 25,” Kaimu Katibu Mkuu wa CUF, Nassor Ahmed Mazrui aliwaambia waandishi wa habari jana.

Oktoba 28, mwaka jana mwenyekiti wa ZEC, Jecha Salim Jecha alifuta matokeo ya uchaguzi wa rais, wawakili shi na madiwani kwa maelezo kuwa sheria na kanuni zilikiukwa na baadaye kutangaza Machi 20 kuwa siku ya kupiga kura upya.

Mazrui alisema licha ya CUF kuiandikia barua ZEC, ikitaka wagombea wake wote kuondolewa katika orodha ya karatasi ya kupigia kura, kuna uwezekano mkubwa wa majina hayo kutoondolewa.

“... Sisi tumeshaipelekea ZEC barua 54 za wawakilishi na madiwani walioshindwa au kushinda katika uchaguzi wa Oktoba 25 na kuwaeleza kuwa wawaondoe katika karatasi za uchaguzi wa marudio.

"Hata kama wananchi watamchagua Maalim Seif kwa asilimia 90 hawezi kwenda kuapishwa. Kufanya hivyo ni sawa na kukataa kula nyama ya nguruwe lakini mchuzi wa nyama hiyo unaunywa.”

Mazrui ambaye alitangazwa mshindi wa uwakilishi wa jimbo la Mtopepo, kabla ya kufutwa kwa matokeo hayo alisema, “Hatuna shida na uchaguzi wao, tumekosa nini mpaka tuwe na shida nao?”

Alisema CCM inadhani kwamba CUF itajitosa kushiriki uchaguzi huo wa marudio katika dakika za mwisho; “wanachotakiwa kujua ni kwamba hatuingii katika uchaguzi wao wawe na amani yote.”

Akizungumzia kauli ya Jaji Mkuu wa Zanzibar, Omar Othman Makungu kwamba CUF walipaswa kupinga kufutwa kwa matokeo ya uchaguzi, siku 14 baada ya kutangazwa, Mazrui alisema kauli hiyo imedhihirisha kuwa hata wakienda mahakamani hakuna haki itakayotendeka.

“Ameshatoa hukumu kabla hata kesi haijafunguliwa. Muda wa siku 14 aliousema unahusu ukomo wa kupeleka kesi ya uchaguzi Mahakama Kuu. Kesi ya uchaguzi msingi wake mkubwa ni uamuzi wa msimamizi wa uchaguzi ambao CUF na wajumbe wateule hatuna tatizo nao,” alisema.

“Hakuna anayetaka atangazwe mshindi kati ya wagombea wote wa CUF kwa kuwa walitangazwa kihalali na wasimamizi wa uchaguzi na kupewa vyeti.

"Aliyehujumu uchaguzi si ZEC ni Jecha. Sisi kesi tunayoweza kufungua ni ya kikatiba si kupinga matokeo na kesi ya kikatiba haina muda wa kufungua kwa mujibu wa Katiba ya Zanzibar.”

Alisema kutokana na kauli ya Makungu, CUF imewashauri wajumbe wa Baraza la Wawakilishi waliokuwa na nia ya kupeleka shauri mahakamani kuachana na wazo hilo kwa maelezo kuwa Jaji Makungu ameshaandaa hukumu na kuisoma hadharani.

ACT-Wazalendo Wapinga Uchaguzi wa Marudio Zanzibar........Wamtaka Rais Magufuli Afute Posho za Makalio Na Matumizi Ya Magari Ya Anasa

$
0
0
Maazimio Ya Kamati Kuu Ya ACT-Wazalendo Kufuatia Kikao Chake Kilichofanyika Jumamosi 13 Februari 2016 Katika Hoteli Ya Kagame Jijini Dar Es Salaam

Kamati Kuu ya Chama cha Wazalendo (ACT-Wazalendo) ilifanya kikao chake cha kawaida siku ya Jumamosi tarehe 13 Februari 2016 katika Ukumbi wa Hoteli ya Kagame Jijini Dar es Salaam.

Pamoja na mambo mengine, Kamati Kuu ilijadili, kutolea maoni na kuazimia mambo yafuatayo yanayohusu chama na Taifa kwa ujumla.

1. Kamati Kuu ilijadili na kuzingatia hali ya kisiasa nchini na kutolea maoni mambo yafuatayo:

a. Kamati Kuu iliwapongeza wananchi na Tume ya Taifa Uchaguzi (NEC) kwa kufanikisha uchaguzi mkuu kwa amani kwa upande wa Jamhuri Muungano wa Tanzania. Hata hivyo, Kamati Kuu inalaani kitendo cha Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi wa Zanzibar za kuvuruga zoezi la kukamilisha kujumlisha matokeo ya kura zilizopigwa katika uchaguzi huo.

b. Kamati Kuu ilipokea na kujadili utendaji wa serikali ya awamu ya tano ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inayoongozwa na Rais John Pombe Joseph Magufuli na kuzingatia yafuatayo:

i. Kamati Kuu imetambua jitihada za serikali ya Dk Magufuli katika kupambana na rushwa na ufisadi nchini kupitia dhana ya kile anachokiita ‘kutumbua majipu’. Hata hivyo, Kamati Kuu imezingatia kuwa bado hali ya maisha ya wananchi imeendelea kuwa ngumu kama inavyothibitishwa na kuendelea kupanda kwa bei ya bidhaa muhimu kwa maisha ya binadamu kama vile sukari, mchele, na mafuta ya kula. Aidha, pamoja na bei ya mafuta kuendelea kushuka kwa kasi katika soko la mafuta duniani, bei ya mafuta hapa nchini imeshuka kwa kiwango kidogo kisicholingana na kiwango cha kushuka katika soko la dunia.

ii. Pamoja na kwamba chama chetu kinaunga mkono juhudi za kuwachukukia hatua za kinidhamu watumishi wa umma wenye tuhuma za rushwa na ubadhirifu wa mali za umma, tunasisitiza kwamba juhudi hizo lazima zifanywe kwa kuzingatia misingi ya utawala wa sheria, utawala bora na utu.

Aidha, serikali ya Rais Magufuli haijajikita katika kuleta mabadiliko ya kimfumo, ikiwemo: kubadili mikataba ya kinyonyaji ya raslimali kama vile madini na mafuta; kufuta posho za makalio katika mfumo wa utumishi wa umma ikiwemo Bunge; kuachana na matumizi ya magari ya anasa (mashangingi); tunaendelea kuagizi sukari nje; hakuna mpango wa kuifanyia mabadiliko TAKUKURU; na serikali haielekei kama itashughulikia suala la Katiba Mpya ambayo ndiyo ajenda kubwa kwa miaka mingi sasa.

2. Kamati Kuu imepokea na kujadili hali ya kisiasa katika visiwa vya Zanzibar na kuzingatia na kuazimia yafuatayo:

a. Kamati Kuu imeendelea kusisitiza kuwa Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi Zanzibar, Ndugu Jecha Salumu Jecha, hakuwa na uhalali wa kisiasa, kikatiba na kisheria kufuta zoezi lililokuwa linaendelea la kuhesabu kura mnamo tarehe 28 Oktoba 2015.

Dalili zote za kisiasa zinaonyesha kwamba Ndugu Jecha alichukua hatua alizochukua kwa shinikizo na/au mapenzi ya kisiasa kwa lengo la kuzuia ushindi wa chama kimojawapo ulioelekea kuwa dhahiri.

Kamati Kuu imezingatia pia kuwa, mbali na Chama cha Mapinduzi, waangalizi wote wa uchaguzi wa ndani na nje, pamoja na Jumuiya ya Kimataifa, ikiwemo Jumuiya ya Afrika Mashariki, wametamka bayana kwamba uchaguzi wa Zanzibar ulifanyika katika mazingira ya haki, huru na demokrasia na matokeo ya uchaguzi huo yalizingatia utashi na matakwa ya wapiga kura wa Zanzibar.

Kwa kuzingatia haya, Kamati Kuu imeazimia yafuatayo:

i. Kupinga marudio ya uchaguzi uliopangwa kufanyika tarehe 20 Machi 2016 na kwamba Chama chetu cha ACT-Wazalendo hakitashiriki katika uchaguzi huo

ii. Kutoa wito maalumu kwa Rais wa Jamhuri wa Muungano wa Tanzania kuchukua hatua stahiki kwa mamlaka aliyepewa kikatiba kuhakikisha kwamba Umoja na Amani ya Taifa inaendelea kuimarika nchini kwa kuzingatia misingi ya demokrasia, utawala wa sheria na utawala bora.

iii. Kamati kuu ya ACT-Wazalendo,inataka madiwani na wawakilishi walioshinda na kutangazwa rasmi na ZEC katika uchaguzi uliofanyika Oktoba 25/2015 watambuliwe na waanze kuwatumikia wananchi.

Kwa sababu wawakilishi na madiwani waliotangazwa na ZEC ni halali kwa mujibu wa katiba, sheria na kanuni za Uchaguzi wa Zanzibar

iv. Kamati Kuu inaamini kwamba suluhu ya mkwamo wa kisiasa Zanzibar ni kufanya mazungumzo yatakayojumuisha wadau wote muhimu katika mchakato wa uchaguzi wa Zanzibar. Hatuamini kwamba mkwamo huu utatuliwa kwa vitisho vya kidola.

3. Kamati Kuu imepokea, kujadili na kupitisha taarifa ya uchaguzi wa chama na kuzingatia yafuatayo:

a. Kamati Kuu imewapongeza na kuwashukuru wananchi waliojitokeza kupiga kura na kukiunga mkono chama na hata kufanikiwa kumpata mbunge mmoja, madiwani 41 katika mikoa mbalimbali, na kuongoza Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji

b. Kamati Kuu imepitisha taarifa ya mapato na matumizi katika uchaguzi mkuu ambapo chama kilipokea na kutumia shilingi 656,625,000/=.Taarifa hii inawekwa wazi kwa umma kama tulivyoahidi kwa kuzingatia tunu yetu ya uwazi

c. Kamati Kuu imevipongeza vyombo vya habari kwa kazi kubwa waliofanya katika kuwaelimisha wananchi kuhusu uchaguzi mkuu na kwa kufanya kazi kwa weledi na bila ubaguzi

4. Kamati Kuu imejadili na kupitisha Mkakati wa Chama kwa kipindi cha miaka mitano 2016-2020.

Mkakati huu unalenga kukiimarisha chama katika maeneo matano yafuatayo:

i) Kuimarisha safu ya uongozi na watendaji katika ngazi zote
ii) Kuimarisha mfumo wa mawasiliano ya ndani na kwa umma
iii) Kuibua na kushiriki katika miradi mbalimbali ya maendeleo ya wananchi kwa kuwashirikishi wananchi
iv) Kuimarisha mahusiano na vyombo vya habari
v) Kujiandaa kikamilifu na kimkakati kwa chaguzi za serikali za mitaa wa mwaka 2019 na uchaguzi mkuu wa mwaka 2020, na chaguzi ndogo zitakazojitokeza.

5. Ili kutekeleza kikamilifu Mkakati wa Chama, pamoja na hatua zingine, Kamati Kuu imeziunda upya Kamati za chama makao makuu kama ifuatavyo:

i) Kamati ya Fedha na Miradi ya Kujetegemea
ii) Kamati ya Utafiti, Sera na Mipango
iii) Kamati ya Uadilifu, Ulinzi na Usalama wa Chama
iv) Kamati ya Katiba, Sheria na Mambo ya Nje
v) Kamati ya Itikadi, Mawasiliano na Uenezi
vi) Kamati ya Maendeleo ya Jamii
vii) Kamati ya Mafunzo na Chaguzi
viii) Kamati ya Wabunge na Uendeshaji wa Serikali za Mitaa

Kamati kuu imeiagiza sekretariet ya chama kuanza utekelezaji wa mpango mkakati, ili kukiandaa chama kwa Uchaguzi ujao na uchaguzi mbali mbali

Pia kamati kuu inawahimiza wanachama waendelee na juhudi za ujenzi wa Chama na kutunza amani ya nchi.

Zitto Ruyagwa Kabwe
Kiongozi wa Chama
14/02/2016
Viewing all 104809 articles
Browse latest View live




Latest Images