Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104803 articles
Browse latest View live

Roma Asema Hapendi Kumpost Mpenzi Wake Kwenye Mitandao ya Kijamii..Sababu Hii Hapa..

$
0
0
Msanii wa Hip Hop Tanzania,Roma amefunguka kuwa huwa hapendi kumpost mpenzi wake kwenye mitandao ya kijamii kwa kuhofia kuwa inaweza kumharibia biashara yake muziki.

Roma anaamini kuwa kuna mashabiki wengi na kila mtu anapenda kitu fulani kutoka kwa msanii sio nyimbo tu,wengine hata kukupenda kimapenzi kwa hiyo kumpost mpenzi wako kila mara inaweza kuwafukuza mashabiki wa namna hiyo.

“Sometimes kumpost sana unaharibu biashara yako hasa hii ya sanaa yetu,mashabiki wanakuja kwenye show yako sio tu kwa sababu ya ngoma zako,kila mtu anachokipenda kwako...” alisema Roma ambaye amewahi kumpost mpenzi wake mara moja toka ajiunge instagram.

Source:Fredrick Bundala,conversation with Roma.

Jamii Forums Wafungua Kesi Ya Kikatiba Mahakamani Kupinga Baadhi ya Vifungu vya Sheria ya Makosa ya Mtandao.

$
0
0
Septemba Mosi, 2015 Tanzania ilianza kutumia sheria ya Makosa ya Mtandao licha ya kuwepo kwa mvutano na malalamiko kutoka kwa wananchi wanaotumia mitandao hiyo kwamba hawakushirikishwa kuijadili na kuichambua.

Leo March 4 2016 Kampuni ya Jamii Media inayoendesha JamiiForums.com na Fikrapevu.com imejitosa kutetea kile inachokiita ni kunyimwa haki ya wananchi kupata taarifa na kulindwa kwa uhuru wao wa maoni na kujieleza unaolindwa kwa mujibu wa katiba ya Nchi.

Jamii Media wameamua kufungua shauri Mahakama kuu kutaka kifungu cha 32 na 38 cha sheria ya Makosa ya Mtandao viangaliwe upya. Akizungumza kwa niaba ya Jamii Media,wakili Shukuru Mlwafu ameeleza…

"Baadhi ya vifungu vya sheria ya kimtandao vinakiuka masharti ambayo yamewekwa na katiba hasahasa vinaingilia haki ya faragha ambayo wateja wetu wanayo kikatiba.

"Njia pekee ni kufungua shauri la kikatiba kupinga vifungu hivyo na kuiomba mahakama ibatilishe na itamke kuwa vifungu hivyo ni batili kwa kuwa vinaenda kinyume na ibara 16 na 18 ya katiba" Amesema Shukuru Mlwafu

Hatua hiyo ya kufungua shauri Mahakamani imekuja baada ya kuwepo  na shinikizo kutoka Jeshi la polisi kuwataka Jamii Forum kutoa taarifa za baadhi ya wateja wake. Mkurugenzi Mtendaji wa Jamii Maxence Melo amesema..

"Kuanzia uchaguzi october 2015 kumekuwa na barua kadha wa kadha zinazotaka kupata taarifa za siri za wanachama wa mtandao wa  jamii forum kitu ambacho tunahisi hata mitandao mingine ya kijamii wanafanyiwa na kumekuwa na mashinikizo kadha wakadha wakitaka tutoe IP Address za wateja, majina halisi na hata maeneo waliopo.Sasa tunaona hii itapekea kuvunjwa kwa  haki ya watumiaji wa Jamii forum":-Amesema Maxence Melo

Flora Mbasha Akimbilia Kenya.......

$
0
0
MWIMBAJI wa nyimbo za injili nchini, Flora Mbasha, amekimbilia nchini Kenya kurekodi albamu yake mpya anayotarajia kuipa jina tofauti na nyimbo zitakazokuwa katika albamu hiyo.
Mwimbaji huyo ambaye kwa sasa amefungua darasa la kufundisha uimbaji wenye mafanikio, alisema albamu hiyo inayotarajiwa kuingia sokoni mwishoni mwa Machi, imerekodiwa nchini humo kwa lengo la kubadili ladha ya muziki tofauti na ule anaorekodia hapa nchini.


“Nyimbo tatu kati ya nane zilizomo kwenye albamu hiyo ndizo nimezirekodia hapa nchini, nyingine zote nimerekodi nchini Kenya na lengo langu ni kupata ladha tofauti,’’ alieleza.
Flora alizitaja nyimbo zitakazokuwa katika albamu hiyo kuwa ni ‘Rafiki wa Kweli’, ‘Nakupenda Yesu’, H’akuna Kama Yesu’, ‘Nikuone Mungu Wangu’, ‘Sema Zaidi’, ‘Jipe Moyo (remix)’, ‘Mungu Umenivusha’ na ‘Kwa Yesu Nasimama’.

Mtanzania

Steve R&B Ataja Hiki Kama Kikwazo cha Bongo Fleva Kuwika Kimataifa...Kipi Hicho?

$
0
0
Msanii wa bongo fleva toka Tanzania Steve RnB ametaja uchache wa wasanii wa bongo fleva wanaopeperusha bendera ya Tanzania kimataifa ndio sababu kubwa inayofanya muziki huo usitambe sana nje ya mipaka.

Steve amesema kuwa ametembelea nchi kadhaa ambapo amegundua watu wanasikiliza sana wanaigeria kuliko mziki wetu kwa kuwa wao wana wasanii wengi wa kimataifa na kuongeza wengi hudhani hata Diamond ni Mnigeria.

“Naona muziki wetu kama bado,ila nigeria wamejitahidi..nilikuwa Jamaica wanasikiliza sana wanaigeria .may be wakiwepo watu watano kama Diamond,tunaweza kupiga hatua,kwa sababu tatizo la muziki wetu hatuna watu wengi ambao wanapeperusha bendera..wakati mwingine watu hudhani Diamond ni mnigeria” alisema Steve RnB.

Source: Clouds

Nay wa Mitego Adai Baada ya Mwaka 1 Anaweza Akawa Tajiri Mkubwa Kuliko mtu yoyote Tanzania

$
0
0
Msanii wa muziki wa Hip Hop, Nay wa Mitego baada ya kudai kuwa utajiri wake kwa sasa ni zaidi ya bilioni 1, amedai baada ya mwaka mmoja atakuwa tajiri mkubwa kuliko mtu yoyote Tanzania.
nay new2

Akizungumza katika kipindi cha Weekend Chart cha Clouds TV hivi karibuni, Nay amesema kwa sasa tayari ameshaingia kwa miguu miwili katika biashara ya kilimo.

“Mimi ni mtu ambaye naishi maisha ya ukweli na sijawai kufake, kuanzia mwezi wa sita nimeshaanza kuwekeza, nafikiri hii inaweza ikawa surprise kwa mashabiki wangu. Nimeshaanza kuwekeza katika kilimo, mimi nimeshaanza kununua eka kadhaa pengine panapo majaliwa ikifika mwakani kuna uwezokano wa kuwa tajiri mkubwa kuliko mtu yoyote,” alisema Nay.

Nay alidai kwa sasa nje ya muziki anaingiza pesa kupitia biashara ya daladala.

Magufuli: Afrika Mashariki Haipaswi Kuwa Maskini

$
0
0
Mwenyekiti wa Jumuiya ya Afrika ya Mashariki, Rais John Magufuli jana alizindua barabara ya Afrika Mashariki akibainisha kuwa wananchi wa nchi za jumuiya hiyo hawapaswi kuwa maskini kwa kuwa mradi huo na mingine itakayotekelezwa itasaidia kuinua hali ya maisha.

Akizungumza katika hafla ya uzinduzi wa barabara hiyo ya Arusha - Holili/Taveta - Voi yenye urefu wa kilomita 234.3, Rais Magufuli alisema watu wa Afrika Mashariki hawana shida na vyama, bali wanataka maendeleo.

Katika hafla hiyo ambayo pia ilihudhuriwa na Rais Yoweri Museveni (Uganda), Rais Uhuru Kenyatta (Kenya) na wawakilishi wa marais wa Rwanda, Burundi na Sudan Kusini, Dk Magufuli alisema watu wa Afrika Mashariki wanataka ajira hivyo mambo ya kuwafanya wachache kuwa na mali nyingi na wengi kuwa maskini lazima yaishe.

“Sisi kama marais wa Afrika ya Mashariki tumejipanga kuhakikisha tunabadilisha maisha ya wananchi,” alisema Rais huyo aliyekabidhiwa uenyekiti wa jumuiya hiyo juzi.

Alisema anataka kuona Afrika ya Mashariki yenye viwanda ambavyo vitasaidia kupatikana ajira kwa vijana na kukuza uchumi.

Alisema ni lazima nchi za Tanzania, Kenya, Uganda, Rwanda, Burundi na Sudan Kusini zinazounda jumuiya hiyo ziondokane na tabia ya kuombaomba wakati zina rasilimali za kutosha.

Alisema asilimia 63 ya vijana katika nchi za Afrika ya Mashariki, hawana ajira ndiyo sababu juzi wakuu wa nchi hizo wamefikia makubaliano ya kuhakikisha wanafufua na kujenga viwanda katika nchi zao.

“Hakuna sababu ya pamba inayolimwa Jinja (Uganda), iende Ulaya kutengeneza nguo na ajira kwa vijana wao na nguo ambazo wanavaa Wazungu wakizichoka wanazirejesha kwetu kama mitumba,” alisema.

Alisema lengo la sasa la Jumuiya ya Afrika Mashariki ni kuona pamba inalimwa na inatengeza nguo ambazo zinavaliwa hapa na nyingine kuuzwa nje.

Rais Magufuli alisema wanataka kuona madini ya chuma ambayo yanapatikana Afrika ya Mashariki yanatumika kutengeneza magari na kuuza nchi za Ulaya.

“Tanzania tuna ng’ombe zaidi ya milioni 22, lakini tunauza ngozi nje ambayo haijaongezewa thamani na wao wanatengeneza viatu bora wanavaa, sisi huku wanatuletea viatu vya magome ya miti ambavyo havidumu, tunataka kuondoka katika hali hii,” alisema.

Aliwataka wananchi kuwaamini na kuwasaidia viongozi wao akisema wanaweza kuleta mabadiliko katika jumuiya hiyo ambayo ina watu zaidi ya milioni 160 baada ya Sudan Kusini kujiunga.

Alisema kimsingi nchi za Afrika ya Mashariki si maskini kwa kuwa zimejaaliwa rasilimali nyingi ambazo zingeweza kutumika vyema kuwasaidia wananchi.

“Tumeambiwa Sudan Kusini kuna madini ya aina 22, hapa Tanzania tuna madini mengi, yakiwamo tanzanite lakini ukienda Mererani maisha wanayoishi watu wa eneo hilo huwezi kuamini,” alisema.

Rais Museveni alisema nchi za Afrika si maskini, bali kuna tatizo la kukosa maendeleo.

Alisema ili nchi za Afrika Mashariki ziendelee, zinahitaji vitu vitatu, kilimo cha kisasa, viwanda na matumizi ya teknolojia ya kompyuta.

Rais Kenyatta alisema kuwa nyuma kwa nchi za Afrika ya Mashariki kumetokana na Serikali husika kuwa nyuma katika kuwasaidia wananchi kufanya biashara na hivyo kupata usumbufu kutokana na kujali mipaka ya kila nchi.

“Haitawezekana kupata maendeleo tukiendelea na hii mipaka iliyowekwa na Wazungu, mipaka ya nchi ilichorwa na Mjerumani ambaye hakuwahi hata kufika katika nchi hizi,” alisema akimaanisha kuwa biashara inatakiwa kuvuka mipaka. Makamu wa Pili wa Rais wa Sudan Kusini, James Wani Igga aliwataka wakazi wa Afrika ya Mashariki kutoiona nchi yake kama mzigo kwao baada ya kuwa mwanachama juzi akisema ina ardhi kubwa yenye rutuba, madini na hivyo ni moja ya maeneo ambayo wananchi wa nchi hizo wanaweza kwenda kuwekeza.

Barabara yenyewe

Akizungumzia barabara hiyo, alisema kwa upande wa Tanzania, Sh209.3 bilioni zitatumika katika ujenzi wa barabara ya kilomita 14.1 ya njia nne ya Arusha - Tengeru na fedha nyingine zitatumika kwa barabara ya nje ya mji wa Arusha yenye urefu wa kilomita 42.3.

Alisema kati ya fedha hizo, Sh109 bilioni zimetolewa na Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) kwa kushirikiana na Shirika la Maendeleo la Kimataifa la Japan (Jaica) na Sh19.4 bilioni zimetolewa na Serikali ya Tanzania na Jumuiya ya Afrika ya Mashariki.  

Chanzo Rasmi Cha Kifo Cha Mtoto wa Whitney Houston Bobbi Kristina Chafahamika...

$
0
0
Chanzo rasmi cha kifo cha Bobbi Kristina Brown kinakaribiana na kile cha mama yake, Whitney Houston – kuzama kwenye maji baada ya kutumia madawa ya kulevya Bobbi Kristina alikufa kutokana na kuzama kichwa chake kwenye maji baada ya kuwa ametumia mchanganyiko wa madawa.

Umebaini vitu alivyokuwa ametumia ni bangi, pombe, madawa yenye uhusiano na cocaine, benzoylecgonine, benzodiazepines na morphine. Ripoti imedai kuwa alifariki kutokana na kupata The pneumonia na encephalopathy – kwamba mapafu yake yalijaa maji na ubongo wake ulijeruhiwa.

Kifo cha Whitney kilitokana na kuzama kwenye bafu katika hoteli ya Beverly Hilton, kulikochangiwa na cocaine na ugonjwa moyo. Bobbi Kristina alifariki July 26 baada ya kukaa miezi kadhaa mahututi. Alikuwa na miaka 22.

Waziri Mkuu Asema Mtu Akiharibu Kazi Asitarajie Uhamisho.

$
0
0
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa(Pichani) amesema watumishi wa umma wako huru kuhamia kokote wapendako lakini wahakikishe wanaenda huko wakiwa safi na kamwe mtu asiharibu kazi kazi akitarajia kuwa atahamishiwa sehemu nyingine.

"Serikali hii haina utumishi kwa mtu aliyeharibu kazi,usije ukaharibu hapa Itilima ukadhani utaenda Bunda kuendelea na kazi. Serikali ya awamu hii haina nafasi na  watumishi wa aina hiyo," amesema.

Waziri Mkuu ametoa onyo hilo leo (Ijumaa, Machi 4, 2016) wakati akizungumza na watumishi wa wilaya ya Itilima kwenye ukumbi wa Halmashauri ya wilaya hiyo ambao ameuzindua leo hii wilayani Itilima, mkoani Simiyu.

"Watumishi wenzangu huu ni wakati wa kubadilika na kuona mwelekeo wa Serikali hii ya awamu ya tano ukoje. Jukumu letu ni kuwatumikia Watanzania wote bila kujali itikadi zao, rangi wala dini zao," alisisitiza.

Waziri Mkuu aliwahakikishia watumishi hao kwamba Serikali inatambua changamoto walizonazo kutokana na upya wa wilaya hiyo na mkoa huo na akawaahidi kuwa itaboresha mazingira yenu.

"Msiwaadhibu wananchi kwa kisingizio cha mazingira magumu ya kazi zenu, tunajua mnayo madai ya nauli, posho za mafunzo, kupandishwa madaraja na malimbikizo ya likizo," alisema huku akishangiliwa.

Alisema Serikali itayalipa madeni hayo japo haitamaliza yote kwa wakati mmoja ila ana uhakika wa kukamilisha walau kwa asilimia 80.

Mapema, akitoa taarifa ya wilaya hiyo, Mkuu wa wilaya hiyo, Bibi Georgina Bundala alisema wilaya hiyo iliyoanzishwa Machi 2012 na kupata Halmashauri Julai 2013 haina kituo cha polisi cha wilaya, haina gereza, Ofisi za TAKUKURU, mahakama ya wilaya wala benki.

Alisema wilaya hiyo haina hospitali ya wilaya ila akabainisha kuwa wamekwishatenga eneo la ekari 30 kwa ajili ya ujenzi huo.

 "Pia tumekwishapima viwanja 123 na eneo la kujenga  taasisi lenye ekari 143.8 limefanyiwa uthamini na fidia kukamilika," alisema.

IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,
IJUMAA, MACHI 4, 2016.

Paul Makonda Atinga Kortini, Amkataa Hakimu

$
0
0
Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Paul Makonda jana alitinga mahakamani na kumkataa hakimu aliyekuwa akisikiliza kesi iliyofunguliwa dhidi yake na makada wawili wa zamani wa CCM wanaodai aliwakashifu.

Kesi dhidi ya Makonda, ambayo awali ilikuwa inasikilizwa na Hakimu Hellen Liwa wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, ilishafikia hatua ya utetezi na Makonda alitakiwa kuanza kujitetea jana, baada ya mahakama hiyo kumuona kuwa ana kesi ya kujibu.

Hata hivyo, jana Makonda ambaye ilifika mahakamani kwa mara ya kwanza tangu kesi hiyo ilipofunguliwa, alishikilia msimamo wa kutokuwa na imani na hakimu huyo na hivyo kuomba apangiwe hakimu mwingine.

Makonda alifikia msimamo huo kutokana na maneno aliyoelezwa na wakili wake, ambayo kwa mtazamo yalionyesha kuwa hakimu atakuwa anawapendelea wadai na hivyo asingemtendea haki.

Kutokana na madai ya Makonda, Hakimu Liwa amejitoa kwenye kesi hiyo na amepanga ianze kusikiliza upande wa mashtaka Machi 23.

Kesi dhidi ya Kubenea

Wakati Makonda akimkataa hakimu, mbunge wa Ubungo kwa tiketi ya Chadema, Saed Kubenea ameonekana ana kesi ya kujibu katika kesi inayomkabili ya tuhuma za kumtukana mkuu huyo wa wilaya. Uamuzi huo ulitolewa jana na Hakimu Thomas Simba wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu anayesikiliza kesi hiyo, ikiwa ni siku chache baada ya upande wa mashtaka kufunga ushahidi wake.

Akitoa uamuzi huo jana, Hakimu Simba alisema kuwa baada ya kupitia ushahidi wa upande wa mashtaka uliotolewa na mashahidi watatu, aridhika kuwa mshtakiwa ana kesi ya kujibu.

Baada ya uamuzi huo wakili wa Kubenea, Peter Kibatala aliieleza mahakama kuwa mteja wake atajitetea kwa kiapo na kwamba watakuwa na mashahidi wanne na wanakusudia kuwaita wote mahakamani siku ya kujitetea.

Hakimu Simba alipanga mshtakiwa huyo aanze kujitetea Machi 7, mwaka huu.

Kubenea, ambaye alipandishwa kizimbani, mahakamani hapo Desemba 15, mwaka jana, anadaiwa kumtolea DC huyo lugha ya matusi Desemba 14 mwaka jana wakati wakiwa kiwanda cha Tooku Garments kilichoko Mabibo External, Kinondoni, jambo ambalo lingeweza kusababisha uvunjifu wa amani.

Anadaiwa kuwa siku  hiyo  alimuita Makonda kuwa ni “kibaka, mpumbavu na mjinga” na kwamba cheo chenyewe cha ukuu wa wilaya ni cha kupewa.

Wakati wa ushahidi wake, Makonda aliieleza mahakama kuwa alitumia nafasi yake ya ukuu wa wilaya kwenda kiwandani kwa lengo la kuzungumza na wafanyakazi waliokuwa wamegoma.

Mashahidi wengine wa upande wa mashtaka walikuwa ni maofisa wa polisi waliokuwapo eneo la tukio siku hiyo.

Alisema alipomaliza kuzungumza na wafanyakazi hao na kufunga kikao hicho, wakati anageuka alishangaa kumsikia mshtakiwa akimtukana.    


SOMA Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumamosi ya March 5, Ikiwemo ya CCM Yanukia Madeni...

$
0
0
SOMA Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumamosi ya March 5, Ikiwemo ya CCM Yanukia Madeni...

CCM Chawafukuza Uanachama Wananchama 25 Kwa Madai ya Kukisaliti Chama Kipindi Cha Uchaguzi Mkuu 2015.

$
0
0
Chama cha Mapinduzi(CCM) Kigoma, chawafukuza uanachama wananchama 25 kwa madai ya kukisaliti chama kipindi cha Uchaguzi mkuu 2015.

Uamuzi huo wa kuwafuta uanachama ulitolewa na kikao cha halmashauri kuu cha Mkoa kilichofanyika tarehe 2 Machi mwaka huu.

Madiwani wa UKAWA Wavamia Ofisi ya Halmashauri ya Jiji La Dar Wakitaka Kuelezwa ni Lini Uchaguzi wa Meya Utafanyika

$
0
0
Zaidi ya madiwani 20 wanaotokana na vyama vinavyounda Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa), jana walivamia ofisi za Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam kumshinikiza Kaimu Mkurugenzi wake, Sarah Yohana kuitisha Baraza la madiwani kwa ajili ya kufanya uchaguzi wa meya na naibu wake.

Madiwani hao waliovamia ofisi hiyo jana, walisema kikao hicho kinatakiwa kuitishwa ndani ya siku saba kikiwa na ajenda moja ambayo ni uchaguzi wa meya na naibu wake, ambao umekwama mara kadhaa kwa kile walichodai kuwa ni hila na hujuma.

Uchaguzi huo umeahirishwa mara tatu kwa sababu mbalimbali, Januari 23 uliahirishwa kutokana na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Tamisemi), George Simbachawene kutoa muda kwa mameya wa manispaa zinazounda Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam; Kinondoni, Temeke na Ilala kuandaa mfumo bora wa kuwapata wajumbe watatu watakaounda Baraza la Jiji.

Februari 8, uliahirishwa kutokana na kubainika kwa nyongeza ya majina 14 yaliyopenyezwa kutoka halmashauri za Kinondoni na Ilala ambao hawakustahili kushiriki kikao hicho, pia Februari 27 uliahirishwa kutokana na zuio feki la mahakama.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti jana baada ya kukaa zaidi ya saa tatu bila kuonana na Yohana, madiwani hao na wabunge walisema wamechoshwa na uongozi wa jiji kuwahadaa kama watoto wadogo.

Mbunge wa Kawe (Chadema), Halima Mdee alisema wamechoka kupigwa danadana na kwamba wanachohitaji ni uchaguzi wa Meya wa Dar es Salaam kufanyika ndani ya siku saba siyo vinginevyo.

“Tumekaa zaidi ya saa tatu wametwambia Yohana hayupo, sasa akija mfikishieni taarifa kuwa Ukawa hatuna maelezo na Jumatatu tutatia timu tena hapa ofisini kwake,” alisema Mdee akimpa maagizo Ofisa Utawala wa Dar es Salaam, Iman Kasagara.

“Narudi tena, mfikishieni salamu, Jumatatu hatutaki kusikia longolongo za aina yoyote kutoka kwake. Tunataka majibu ya kueleweka vinginevyo hatutamuelewa,” alisema Mdee ambaye pia ni Mwenyekiti wa Baraza la Wanawake Chadema (Bawacha).

Kasagara aliahidi kufikisha ujumbe huo kwa mhusika ambaye ilidaiwa alikuwa nje ya ofisi kikazi.

Mwenyekiti wa Madiwani wa Ukawa Dar es Salaam, Manase Mjema alisema uvumilivu umewashinda kutokana na figufigisu zinazofanywa na Jiji la Dar es Salaam kuhusu uchaguzi huo.

Mbunge wa Ukonga (Chadema), Mwita Waitara alisema ajenda kuu ya Ukawa ni uchaguzi wa meya na wameacha shughuli zote hadi suala hilo lipatiwe ufumbuzi.

“Sasa hivi wakurugenzi akiwamo wa Dar es Salaam, wamepeleka bajeti zao hazina bila kushirikiana na meya kwa sababu hajapatikana, hivi hapo kuna maendeleo kweli?” alihoji Waitara.

“Kimsingi utaratibu wa kisheria ulishapita, sasa tunaelekea siku 90 bila meya tumechoka na hali hii,” alisema Waitara.

Mbowe Kuzungumza na Taifa Kupitia Waandishi wa Habari Makao Makuu CHADEMA Leo

$
0
0
Mwenyekiti wa CHADEMA Taifa Freeman Mbowe leo atazungumza na Taifa kupitia mkutano wa waandishi wa Habari.

Mkutano huo wa waandishi utafanyika saa 6 mchana makao makuu Kinondoni Ufipa.

Kiongozi huyo mkuu wa upinzani nchini anatarajiwa kutoa tamko rasmi la maazimio ya Kamati kuu ya chama iliyokutana Machi 1

Tayari vyombo vya ndani na nje ya nchi vimealikwa kwenye mkutano huo na imetakiwa ifikapo saa 5 asubuhi waandishi wote wawe wamekaa kwenye nafasi zao.

Mwenyekiti huyo anabashiriwa mbali na mambo kadhaa lakini atatoa msimamo rasmi wa chama kuhusiana na hujuma ya watawala dhidi ya uchaguzi wa meya wa DSM

Maalim Seif Arejea Zanzibar Akitokea India Kwenye Matibabu......Mamia ya Wafuasi wake Wampokea, Asema Polisi Imegeuka tawi la CCM

$
0
0
Katibu Mkuu wa CUF, Maalim Seif Sharif Hamad jana aliwasili Zanzibar kutoka ughaibuni na kulilaumu Jeshi la Polisi nchini akisema, “hapana shaka yoyote sasa limegeuka tawi la CCM.”

Maalim Seif alisema hayo jana jioni wakati akizungumza na wafuasi wake waliofika kumpokea katika Uwanja wa Ndege wa Abeid Amani Karume na baadaye kumsindikiza hadi nyumbani kwake Mbweni mjini hapa.

Baadhi ya viongozi wa CUF waliohudhuria mapokezi hayo ni pamoja na Mansour Yussuf Himid, Nassor Ahmed Mazrui, Fatma Abdulhabibi Ferej na aliyekuwa mgombea mwenza wa Chadema chini ya mwavuliwa wa Ukawa katika urais wa Muungano, Juma Duni Haji.

Maalim Seif aliyetokea India kupitia Falme za Kiarabu, alisema anaunga mkono kauli za Mazrui ambaye ni Naibu Katibu Mkuu wake, zilizosababisha ahojiwe na polisi juzi, kuwa “sasa CUF wamechoka na uhuni dhidi ya mali na ofisi zao.”

“Nasikitika kuona hujuma, watu wakipigwa na kujeruhiwa na mazombi kila kukicha, polisi wapo wanayaona na hakuna aliyeitwa kuhojiwa kwa uchochezi. Sasa haitawezekana na haitakubalika tena...” alisema.

Alipoulizwa kuhusu madai hayo jana, Inspekta Jenerali wa Polisi, Ernest Mangu alimtaka mwandishi kuzungumza na msemaji wa jeshi hilo, Advera Bulimba ambaye simu yake haikupatikana.

Hata hivyo, akizungumzia suala la mazombi hivi karibuni, Mkurugenzi wa Upelelezi Zanzibar, Salum Msangi alisema taswira ya haraka wanayoipata ni kwamba inawezekana wanaotendewa vitendo hivyo ni wahalifu ambao wamekutana na wahalifu wenzao hivyo kuhofia kutoa taarifa ili uhalifu wao usibainike hali inayosababisha kunung’unika pembeni bila ya kufikisha taarifa maeneo sahihi ili zifanyiwe kazi.

“Kwa mujibu wa taratibu zilizopo ni kwamba mtu yeyote anayefanyiwa kitendo cha kihalifu anapaswa kutoa taarifa kwenye kituo cha polisi ili hatua za uchunguzi au upelelezi zifanyike ili kubaini wahalifu hao,” alisema Msangi.

Katika hatua nyingine, Maalim Seif alimlaumu, Dk Ali Mohamed Shein kuwa si muungwana akidai kuwa amekataa kuondoka madarakani.

Alisema la kushangaza zaidi ni kuona aking’ang’ania uchaguzi wa marudio, ilihali hakuna mantiki wala kifungu chochote cha sheria kinachohalalisha hatua hiyo.

“Nasema sisi hatutambui uchaguzi huo wa marudio maana wameshindwa kututhibitishia ni wapi zilipo hizo dosari za uchaguzi uliokwishafanyika,” alisema.

Katika salamu hizo za takriban dakika 10, Maalim Seif alimtahadharisha Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar (ZEC), Jecha Salim Jecha asijaribu kulazimisha chama hicho kushiriki uchaguzi ‘batili’ wa marudio.

Mrembo Gigy Money Ajirekodi Video ya Utupu

$
0
0
Video Queen anayezitendea haki video za wasanii mbalimbali hapa Bongo, Gift Stanford ‘Gigy Money’ ameambulia matusi na maneno ya dhihaka kutoka kwa mashabiki wake mbalimbali baada ya juzikati kutupia video ya utupu katika akaunti yake katika Mtandao wa Kijamii wa Instagram.
gigy

Wakionesha kukerwa na kitendo hicho, mashabiki hao walionekana kuchukizwa na kitendo hicho hivyo kumjia juu mrembo huyo ambaye ameuza nyago katika video mbalimbali ikiwemo ya Shika Adabu Yako ya Emmanuel Elibariki ‘Nay wa Mitego’.

Mara baada ya kuyasoma matusi hayo, Gigy aliamua kuitoa video hiyo haraka kwani kadiri muda ulivyozidi kwenda mbele, ndivyo watu walivyozidi kumtukana, hali iliyoonekana kumvuruga.

“Huyu dada ni jipu na anahitaji kutumbuliwa. Haiwezekani afanye vitu kama hivi. Hii si video ya kuweka katika mtandao wa kijamii ambayo inafunguliwa hadi na watoto. Angalia hata picha zake nyingine zimejaa utata, nadhani TCRA inatakiwa kumtumbua japo kidogo,” alisema mdau mmoja mara baada ya kuiona video hiyo na picha kibao za mrembo huyo.

Mara baada ya kuinyaka video hiyo kwa ‘kui-screenshot’, gazeti hili lilijaribu kumtafuta Gigy ili aizungumzie video hiyo na kutoa sababu ya kuiweka lakini hakupokea simu.

Chanzo:GPL

Lady Jaydee Kufunga Ndoa Tena Baada ya Kupewa Talaka na Gadner

$
0
0
Siku chache baada ya kupewa talaka na aliyekuwa mumewe, mtangazaji Gardner G. Habash ‘Captain’, mkongwe wa muziki wa Bongo Fleva anayekuja na ujio mpya alioubatiza jina la Naamka Tena, Judith Wambura ‘Lady Jaydee’ au Jide amedaiwa kupata mwanaume mwingine ambaye yupo kwenye mikakati kabambe ya kumuoa, Risasi Jumamosi lina ubuyu kamili.

Jide ambaye amekuwa kimya kimuziki kwa zaidi ya miaka miwili, Februari mwaka huu alipewa talaka katika Mahakama ya Manzese-Sinza jijini Dar baada ya mvutano uliodumu kwa muda mrefu tangu wawili hao washindwe kuishi pamoja.

Kwa mujibu wa chanzo makini, Jide alimpata mwenza muda mrefu tangu walipomwagana na Gardner lakini mipango ya ndoa ikashindwa kwenda haraka kwa sababu hakuwa amepewa talaka hiyo aliyoidai mahakamani.

“Mbona Jide kitambo tu alishapata mtu sema alikuwa hawezi kufanya mambo ya ndoa kwani hakuwa amepewa talaka na Gardner ila sasa hivi yupo huru na mwaka huuhuu huenda kikaeleweka,” kilisema chanzo hicho na kuongeza:

“Sema Jide kama unavyomjua, mtu wa usiri sana. Anatumia nguvu nyingi kweli kumficha mchumba wake wa sasa. Hataki watu wamjue.”

Mwanahabari wetu alijaribu kumvutia waya Jide kupitia simu yake ya mkononi ambapo alipopatikana aliomba  asizungumzie mambo ya uhusiano na badala yake akadai aulizwe kuhusu ujio wake mpya.

“Niulize kuhusu program yangu ya Naamka Tena, nipo bize kuandaa ngoma hiyo na kama unavyoona siku chache zijazo natarajia kuiachia, inanifanya niwe bize sana please niache kwanza,” alisema Jide.

Hata hivyo, mmoja wa mameneja wa msanii huyo ambaye aliomba hifadhi ya jina lake kwa kile alichoeleza kuwa hapaswi kumsemea Jide katika masuala ya uhusiano, alikiri Jide kuwa na mchumba ambaye wapo katika hatua nzuri ya kuyaanza maisha ya ndoa.

Chanzo:Risasi

Diamond Platnumz akutana na Kanye West, Los Angeles

$
0
0
Diamond Platnumz amekutana na rapper ambaye watu wengi wangependa kukutana naye na kuongea mawili matatu kutokana na heshima yake, Kanye West.

Najua kuwa Diamond na Kanye wana kitu kimoja wanachofanana – wote wanapenda fashion kwahiyo kwa hitmaker huyo wa ‘Make Me Sing’ kukutana na Yeezy hata kwa dakika chache tu ni kitu alichokipokea kwa heshima kubwa.

Bila shaka Diamond alikutana na rapper huyo aliyeachia album mpya The Life of Pablo hivi karibuni kwenye uwanja wa ndege wa kimataifa wa Los Angeles, LAX.

“LA am in Town Baby!!!….. With my bro #WEST,” aliandika Diamond kwenye picha aliyopost Instagram.

Hata hivyo mwisho wa safari yake ni Las Vegas.

“Duh tangu jana saa 10 jioni nipo kwa mandege tu [disappointed_relieved] ….What a Long a** flight!…. Still gat 28 mints to land in LA, then wait for 4 hrs transit….then connect from LA to Las Vegas,” aliandika kwenye picha hiyo chini.

Jibu la Vanessa Mdee Kwa Shabiki Aliyemdiss Juma Jux.....Ilikuaje?

$
0
0
Kupitia akaunti yake ya instagram Vanessa amepost picha ya promo ya Jux na cyril ya kwa ajili ya show ya Morogoro na Dodoma na kuandika maneno haya..

 “Moro na Dodoma sio kwa kunichukulia mtu wangu weekend nzimaaaa dahhhhh!!! Freshi lakini nendeni mkashow love basi. @cyrill_kamikaze @juma_jux @bdozen”

Katika hali isiyo ya kawaida shabiki mmoja alijitokeza na kuandika comment inayoonekana kumdiss mpenzi wa msanii huyo,Jux iliyosomeka ifuatavyo..
”Afu Vanessa mwambie msela wako aache tabia ya kuingia chumvini!!!”

Vanessa alionekana kutopendezwa na comment hiyo na kumjibu kama ifuatavyo..
“@d.magezi kwaresma yote hii usije ukanishindisha nja mwananangu naona kuna mengi yanakustress kama vipi Pita LEFT arif isiwe tabu.” kama inavyoonekana kwenye picha chini..

Waziri wa Magufuli, January Makamba Katika Kashfa Nzito ya Kifisadi..Mange Kimambi Afichua...

$
0
0
Katika hali isiyo ya kawaida, Mwanadada anayejulikana katika Mitandao ya Kijamii, Mange Kimambi, amewachana January Makamba na Mwamvita katika Instagram page yake kwa kuweka sauti zilizorekodiwa wakipanga deal na mfanyabiashara wa kiitaliano ambaye amelizwa dola milion 100 ili apewe deal la kujenga port Bagamaoyo.

Jaribu kupitia Instagram yake Kusikiliza Sauti zao:

Chanzo:Mange Kimambi Insta Page

Mr Nice Afunguka Kuhusu Picha yake Akiwa Amekonda Iliyoshtua Watu...Adai Alilishwa Sumu

$
0
0
SIKU chache baada ya kusambaa kwa picha yake inayomuonesha akiwa amepungua mwili na kuzua mjadala mitandaoni huku wengi wakimuonea huruma, mkongwe wa Muziki wa Takeu, Lucas Mkenda ‘Mr. Nice’ ameibuka na kufungukia afya yake.

Picha inayomuonesha Nice akiwa amepungua mwili ilizagaa mapema wiki hii kwenye mitandao ya kijamii ambapo wengi waliochangia mjadala wa picha hiyo, walisema staa huyo aliyetikisa kwa utajiri enzi hizo, kwa sasa atakuwa anaumwa sana huku mjadala mkubwa ukawa ni ya lini?

Baada ya Ijumaa kuinasa picha hiyo, lilifanya jitihada za kumpata msanii huyo kwa kumvutia waya alipopatikana, alifunguka kwa kirefu kuhusu afya yake:

“Kwanza hiyo picha ni ya kitambo sana. Si unakumbua lile sakata langu la mimi kulishwa sumu kwenye chakula? Basi ndiyo kipindi kile.

“Namshukuru Mungu niliiwahi ile sumu na kupewa dawa ambazo natumia mpaka sasa. Kweli nilipungua lakini ni wakati huo, kwa sasa sipo hivyo kama kwenye hiyo picha inayosambazwa mitandaoni,” alisema Mr. Nice.

Akaongeza kuwa ni kweli afya yake haiko poa sana kwa kuwa bado anaendelea kutumia dawa za kuimaliza sumu ile lakini siyo kama vile anavyoonekana kwenye picha hiyo.

Chanzo: GPL
Viewing all 104803 articles
Browse latest View live




Latest Images